Wakati Herode anaua watoto kule Bethlehemu baada ya kuzaliwa YESU je roho iliyokuwa ndani yake ilikuwa inatoka wapi?.. Kama ni shetani, je shetani hakujua kama Yusufu na Mariamu wametoka na wameelekea Misri?.
Jibu: Awali ya yote ni muhimu kujua kuwa roho iliyokuwa ndani ya Herode ni ya “shetani” na wala hazikuwa akili zake Herode..Kwasababu kitabu cha Ufunuo kinaonyesha wazi kuwa ni Joka (yaani shetani mwenyewe) ndiye alikuwa anatafuta kumwangamiza Bwana YESU wakati anazaliwa na si Herode (Herode alitumika tu kama chombo)
Ufunuo 12:3 “Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba.
4 Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka AKASIMAMA MBELE YA YULE MWANAMKE ALIYE TAYARI KUZAA, ILI AZAAPO, AMLE MTOTO WAKE.
5 Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi”.
Sasa swali kwanini shetani asiahirishe ajenda yake ya kuua watoto Bethlehemu baada ya kujua kuwa mtoto hayupo tena Bethlehemu?..
Kikawaida uwezo wa shetani si kama wa MUNGU.. MUNGU anaweza kufanya pasipo ushirika na yoyote, na anaweza kufanya jambo likabadilika kwa muda mfupi, lakini si shetani..
shetani anaposhindwa kufanikisha jambo lake lolote baya kupitia mapepo wake, huwa anatumia wanadamu.. kwamfano akishindwa kumuua amtu kimazingara, basi anaweza kutumia mtu/watu kufanikisha adhimio lake hilo, hivyo anaweza kuweka wazo ndani ya mtu la kuua, na huyo mtu akaanza maandalizi ya mauaji (jambo ambalo linaweza kuchukua muda mrefu) tofauti na hiyo njia ya kwanza ya kimiujiza-ujiza ambayo ni ya haraka tu ikiwa mtu huyo hana ulinzi wowote wa kiMungu.
Lakini njia ya kumtumia mtu kuua inachangamoto kubwa kwa shetani, Kwasababu ni lazima kwanza amwandae huyo mtu (atakayemtumia kuua), pengine amwekee wivu ndani yake au hasira, na pia amshawishi vya kutosha na kumfundisha njia, sasa mpaka yule mtu aelewe na kutenda kama shetani anavyotaka inaweza kuchukua muda,
Na vile vile si rahisi kulitoa wazo ndani ya mtu (alilokwisha kumwekea), na kubadilisha mpango kwa haraka, kwamfano kama alikuwa amemfundisha mtu aue kwa sumu, na akataka ambadilishie wazo hilo amwekee lingine la kumuua kwa kumchoma kisu, haiwezi kuwa ni jambo la haraka, itamgharimu shetani muda mwingine wa kutosha kufuta wazo la kwanza na kupandikiza wazo la pili ndani ya mtu.
Ndio maana utaona baada ya mtoto kukimbizwa Misri, bado wazo lile la ibilisi ndani ya Herode la kumuua mtoto halikutoka, matokeo yake Herode aliendelea na mauaji….hivyo kubadilisha mpango kwa haraka ilikuwa ni ngumu, zilihitajika taarifa zimfikie Herode kwamba mtoto hayupo kakimbilia Misri, na Herode aamini, na kuahirisha wazo lile.
Kwahiyo shetani alishajua mtoto kakimbilia Misri, lakini kulibadilisha wazo kwenye kichwa cha Herode halikuwa jambo jepesi la dakika moja.
Hiyo pia ikifunua kuwa dhambi ndani ya mtu inayo maandalizi, huwa haiji ghafla, ni lazima kwanza shetani apandikize magugu ndani ya mtu ndipo mwisho aitekeleze, Hivyo ni lazima tuikatae dhambi katika msingi wake, Laiti Herode angeikataa dhambi katika msingi wake pale wivu ulipoingia ndani yake, bila shaka asingeendelea na hatua zinazofuta za mauaji, lakini aliporuhusu wazo la ibilisi lichipue ndani yake ndipo akawa kifaa tosha cha ibilisi.
Vile vile Kaini alionywa na MUNGU, juu ya dhambi ya wivu inayochipuka ndani yake, laiti kama angemsikiliza MUNGU asingefikia hatua ya mauaji, lakini alidharau maonyo ya MUNGU na mwisho akawa kifaa cha ibilisi cha mauaji.
Mwanzo 4:6 “Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?
7 Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.
8 Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani]Ikawa walipokuwapo uwandani,Kaini akamwinukia Habili nduguye, akamwua”.
Vile vile na sisi ni lazima tuikatae dhambi katika uchanga wake, mawazo mabaya yajapo ni wakati wa kuyakataa kabla hayajatupeleka katika matendo, fikra mbaya zijapo ni wakati wa kuzikataa katika uchanga wake, hasira ijapo, chuki zijapo, uchungu ujapo na mambo mengine yote mabaya ni wakati wa kukataa, kama hayajafikia kukomaa..
Vile vile dhambi ikiisha kukomaa ni ngumu kuiacha, ndio maana ilikuwa ni ngumu shetani kumbadilishia Herode mpango kwa haraka, kwasababu tayari ile dhambi imeshikamana naye.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)
CHACHU YA MAFARISAYO NA CHACHU YA HERODE.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mithali 29:9 Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.
Mstari huo kwa lugha rahisi tunaweza kuuweka kwa namna hii. “Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu, akijibu kwa kicheko au kwa hasira, matokeo ni yaleyale tu hakuna amani au suluhisho”
Unafunua sifa za mpumbavu, kwamba sikuzote mwitikio wake wowote hauwezi kuleta mabadiliko. Kwamfano labda hoja imetolewa na ikamuumiza kiasi cha kumfanya ajibu kwa hasira. Sasa wewe waweza tarajia pengine jambo hilo limemgusa kweli moyo, litambadilisha lakini matokeo yake ni kwamba anakuwa vilevile, Halikadhalika waweza kutoa hoja ikamfanya acheke ukitarajia kitaambatana na badiliko lolote ndani yake lakini hakuna.
Maana yake mpumbavu, haguswi kwa ukali au kwa wepesi wa maneno ya aina yoyote…Na hivyo ni kuachana naye Tu.
Tukiachia wapumbavu wa kawaida tunaowafahamu..Mpumbavu hasaa ni yule mtu anayeikataa kweli ya Mungu mfano wa wale waandishi na mafarisayo wakati wa Bwana Yesu (Mathayo 23:17), mtu wa namna hii unapomuhubiri injili, hata imchomeje au imchekesheje hawezi kufikiri hata chembe kubadilika, kinyume Chake ni mapambano tu.
Bwana Yesu alitufundisha na kutuambia kuwa si kila mtu ni wa kumtupia lulu zetu, maana yake wanaweza kutugeukia na Kuturarua. Ukiona mtu anaishia kwenye ubishi tu na mashindano, ni kuachana naye na kugeukia waliotayari kupokea.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)
Elewa tafsiri ya Mithali 27:22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni.
Theolojia ni elimu ya kujifunza sifa za Mungu na mapenzi yake na jinsi anavyohusiana na wanadamu na ulimwengu kwa ujumla.
Neno Theolojia limezaliwa kutoka katika maneno mawili ya kigiriki ‘theos’, na ‘logos’
Theos likiwa na maana ya Mungu, na logos ni neno/wazo/elimu/maarifa.
Hivyo tukiunganisha maneno hayo, ni sawa kusema theolojia ni mafundisho au maarifa au elimu kuhusu Mungu.
Ni utafiti kuhusu Mungu katika mpangilio na mtiririko maalumu. Ukweli ni kwamba theolojia haiwezi kumfafanua Mungu katika ufasaha wote, ikiwa mtu ataitegemea theolojia tu kumjua Mungu, ukweli ni kwamba amepotea, lakini ikiwa itasomwa vema (si kwa lengo la kitaaluma), bali kwa lengo la kupanua upana wa fikra kuhusu Mungu na maandiko, inafaa sana katika uelewa wa nyanja mbalimbali, hususani kwa wale viongozi na waangalizi kama vile wachungaji, na wahubiri. Si lazima isomwe kwenye vyuo maalumu, mtu yeyote akitia nia kujifunza theolojia anaweza jifunza, kwa kupitia mafundisho mengi, majadiliano na waalimu walio na upeo mpana wa biblia, semina, na kujisomea mwenyewe n.k.
Na Haya ni matawi makuu ya theolojia katika kuichambua biblia.
Imejikita katika kutafiti Maudhui au fundisho kuu la biblia, inaangazia jinsi gani vitabu mbalimbali kwenye biblia, vinavyoelezea mpango wa Mungu katika nyakati tofauti tofauti tangu mwanzo hadi mwisho. Mfano kujifunza MAAGANO, katika agano la kale na jipya yalivyotenda kazi na jinsi Yesu alivyoanza kutambulishwa tangu Edeni kama mzao wa mwanamke, hadi nyakati za manabii Isaya 53, hadi wakati wa kutokea kwake duniani Luka 24:27.
Upo umuhimu wa kuijua hii theolojia kwasababu itakupa kujua kiini cha biblia ni nini? Zipo habari nyingi, hadithi nyingi, nyimbo nyingi, mifano mingi, lakini ni vema ujue maudhui zao ni zipi ili usijikute unatoka nje ya shabaha ya imani.
Inaegemea kujifunza biblia katika migawanyo maalumu ya mada, kwa mfano,
Fundisho la Mungu (theolojia),
Fundisho La Yesu Kristo (Kristolojia),
Fundisho La Roho Mtakatifu (niumatolojia),
Fundisho La wokovu (Soteriolojia),
Fundisho La kanisa,(Ekleziolojia)
La Siku za mwisho.(Esokatolojia)
La mwanadamu (Anthropolojia)
La malaika (Angeolojia)
Inajikita kujifunza jinsi maagizo ya kibiblia yanavyoweza kutendewa kazi katika,, huduma kwa mfano kuhubiri na kufundisha , katika uangalizi wa kichungaji, katika umisheni, na katika taratibu za kiibada, na katika kutoa mashauri ya kikristo kama vile kuwaonya wenye matatizo ya kiroho, kifikra, vifungo n.k.
Inaangazia jinsi gani imani ya kikristo imekuwa ikipiga hatua katika vipindi mbalimbali vya kihistoria, inaangazia mabaraza mbalimbali ya makanisa yaliyokaa katika kujadili fundisho na misingi ya imani. Kwamfano lile baraza la Nikea (325WK). Mpaka nyakati za matengenezo mfano akina Martin Luther, calvin, na wengine.
Hii inakusaidia kujua historia na chimbuko la imani yetu, na sababu ya ukristo kuonekana katika muundo huu leo.
Hii inaegemea katika ukristo na jamii, kwamfano mtazamo wa ukristo katika maeneo ya kijamii mfano ndoa, biashara, taratibu za kijamii, haki za kibinadamu, vita,
Zipo theolojia nyingine kama vile theolojia za tafsiri, za kulinganisha, za utetezi, za kifalsafa. n.k. Kwasababu ya upana wa theolojia, haya ni matawi baadhi tu, kati ya mengi. Hivyo, kama watu wa Mungu, pamoja na kutegemea Bwana kutufunulia mwenyewe maandiko, upo pia wakati ambao hatuna budi kuyamulika maandiko kiundani (Kitheolojia), tukiwa na lengo la kumjua Mungu kwa upana na sio kuwa wasomi, au wanataaluma.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Matendo 17:28 Kwa maana ndani yake yeye tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu. Kama vile mmoja wenu, mtunga mashairi alivyosema, Maana sisi sote tu wazao wake.
29 Basi, kwa kuwa sisi tu wazao wa Mungu, haitupasi kudhani ya kuwa Uungu ni mfano wa dhahabu au fedha au jiwe, vitu vilivyochongwa kwa ustadi na akili za wanadamu.
JIBU: Paulo alipofika Athene, na kuona jinsi mji ule ulivyojaa sanamu nyingi, maandiko yanatuambia moyo wake ulichukizwa sana, hivyo kama ilivyo desturi yake kuhubiri injili, alijua njia mojawapo ya kuwavuta watu ni “kujiungamanisha nao”, kwa kuwagusia kwanza yale mambo mema waliyoyafikiri au kuyatenda.
Ndio maana utaona kabla ya kuwagusia kuhusu huyo mtunga mashairi, aliwaambia kuhusu madhabahu waliyoijenga, ambayo waliipa jina la “MUNGU ASIYEJULIKANA”
Matendo 17:23 Kwa sababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, naliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, KWA MUNGU ASIYEJULIKANA. Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua.
Paulo akaanza kuwahubiria Kristo kwa kupitia huyo wanayemwabudu kimakosa, Lakini tunajua Paulo, hakuwa na ushirika wowote na mifumo yao ya kipagani, wala hakuwahimiza waendelee kumwabudu Kristo kwa njia yao hiyo hiyo.
Tunaona katika kuendelea kujiungamanisha zaidi ya wenyeji wale wa Athene, Paulo akagusia tena habari nyingine za mtunga mashairi, ambaye alikuwa maarifu katikati yao, nyimbo zake zilivuma na kila mmoja alikuwa anazijua, na ndani ya mashairi yake, aliweka vina vinavyoeleza kuwa sisi sote ni wazao wake, au kusema sisi sote ni watoto wa Mungu.
Hivyo akatumia tena fursa hiyo, kuwaeleza uhai wa Mungu, ikiwa sisi tumezaliwa na yeye, basi haiwezekani Baba yetu akawa mfano wa sanamu, ni lazima tu atakuwa mwenye akili, ufahamu, na uelewa kama sisi na zaidi, na sio kama kipande cha mti.
Kwa njia hiyo Paulo akawapata watu wengi, kwa Kristo.
Lakini hatuoni mahali popote akiwaambia wawe wafuatiliaji au mashabiki, wa nyimbo za kidunia.Hiyo ilikuwa njia ya kuwapata wapagani, wamjue Kristo.
Kinyume chake Paulo katika nyaraka zake, anahimiza, waamini kutofuatisha namna ya dunia hii (Warumi 12:1). Na kuhimiza uimbaji unaomtukuza Mungu na kutujenga sisi nafsi zetu kwake ndio unaopaswa kwa wakristo.
Waefeso 5:19 mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;
20 na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;
Wakolosai 3:16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.
17 Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.
Hivyo hatuoni mahali popote Paulo akikubaliana na usikilizaji wa nyimbo za kidunia, wala sisi kama wakristo, hatupaswi kujikita huko, kwasababu tumeshajua ni nani hasaa wa kumwimbia na kumsifu, na wa kumburudikia.
Mungu akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kuharimishwa ni nini, na kwanini Paulo aombe hivyo?(Warumi 9:2).
Ni kwa namna gani Bwana YESU alikula Siagi na Maziwa? (Isaya 7:15)
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine: