SWALI: Nini maana ya Mithali 21:3
[3]Kutenda haki na hukumu Humpendeza BWANA kuliko kutoa sadaka.
JIBU:
Mstari huo unatufundisha mambo ambayo Mungu huvutiwa nayo zaidi…
Mungu hupendezwa zaidi na sisi tunapoishi maisha ya haki, tunatenda mema, tunawajali wengine, tunaishi sawasawa ni viwango vyake vya kiroho hapa duniani..kwake hiyo ni bora zaidi ya sadaka zetu tumtoleazo.
Sadaka huwakilisha mambo yote Ya kidini tunayoweza kumfanyia Mungu, mfano ibada, fedha, mifungo, maombi, kuhubiri, kuimba n.k
Bwana huvutiwa zaidi na mioyo na tabia zetu, na sio zile Ibada za nje tu..
Haimaanishi kuwa hapendezwi na hivyo vitu hapana…bali hivyo vifanywe baada ya kutii kwanza..
Tunaona jambo kama hilo amelisisitiza sehemu nyingi kwenye maandiko; Tukianzia kwa Sauli alimwambia, hivyo;
1 Samweli 15:22
[22]Naye Samweli akasema, je! BWANA huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya BWANA? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya beberu.
Mika 6:6-8 inasema;
[6]Nimkaribie BWANA na kitu gani, na kuinama mbele za Mungu aliye juu? Je! Nimkaribie na sadaka za kuteketezwa, na ndama za umri wa mwaka mmoja?
[7]Je! BWANA atapendezwa na elfu za kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je! Nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa kosa langu, mzao wa mwili wangu kwa dhambi ya roho yangu?
[8]Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na BWANA anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!
Soma pia..
Isaya 1:11-17 – Inasema…Bwana huchukizwa na sadaka za watu wanaishi katika dhambi
Hivyo ni lazima tujiulize Je! tunatenda haki kwa wengine?
Je! Tunatembea kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wetu?
Je! tunamtii Mungu, kuliko vitu vingine vyovyote?
Je tunawahurumia wengine…?
Mambo kama haya ndio yenye uzito zaidi kwa Mungu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Maana ya 2Wakorintho 9:11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote
katika agano jipya wapo watu wanne ambao wametajwa kwa jina la Yohana.. Wawili kati ya hao ndio hujulikana sana…ambao ni Yohana mbatizaji na Yohana mtume wa Yesu ..hawa wametajwa Sehemu nyingi katika agano jipya..
Mfano vifungu ambavyo utamsoma Yohana mbatizaji ni kama vifuatavyo:
Hivi ni vifungu vinavyomtaja Yohana Mtume;
Na ndiye mwandishi wa injili ya Yohana, pia na nyaraka zote tatu (1,2, 3 Yohana, ) pamoja na kitabu cha Ufunuo.
Yohana mwingine ni Marko, ndiye mwandishi wa kitabu cha Marko,..anatajwa katika kitabu cha Matendo 12:12, 13:5, Wakolosai 4:10
Na ndiye aliyekuwa Msaidizi wa Paulo na Barnaba katika ziara zao za kupeleka injili kwa mataifa.
Yohana mwingine ni Baba wa Simoni Petro anatajwa katika;
Yohana 1:42
[42]Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe).
Soma pia Yohana 21:15-27
Hivyo jumla Yao ni wanne…
Je ungependa kufahamu Zaidi watu wengine Katika biblia? Kama ni ndio basi jiunge tazama chini kwa makala nyingine..
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Maherodi walikuwa ni akina nani, Na kazi yao ilikuwa ni ipi?
Kwanini nguo za waliomwua Stefano ziwekwe miguuni mwa Sauli?.
Biblia haitoi umri fulani maalumu kwamba mtu akiufikia huo basi ndio huitwa kijana.. Japokuwa ni mtu ambaye yupo umri wa hapo katikati yaani utoto na utu uzima, lakini hutambulika kwa kuangalia vitu kama hatua za ukuaji wake, uwajibikaji wake na uzoefu wake wa kimaisha.
Kwamfano katika biblia watu hawa walitajwa kama vijana.
Na wengine kadha wa kadha..
Yafuatayo ni Mambo ambayo kijana yeyote anatarajiwa awe nayo kibiblia.
Mhubiri 12:1
[1]Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo.
Zaburi 119:9
[9]Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.
1 Timotheo 4:12
[12]Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.
Mithali 20:29
[29]Fahari ya vijana ni nguvu zao,..
1 Yohana 2:14
[14]Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.
Lakini pia kijana anakabiliwa na tamaa za ujanani kama vile uzinzi, anasa,starehe..hivyo Anatarajiwa azikimbie wakati wote.
2 Timotheo 2:22
[22]Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.
Kutokana na vigezo hivyo tunaweza Kuona ujana pengine huanzia umri wa kubalehe, mpaka wakati mtu anapungua Nguvu zake mwilini.. labda Miaka 12-45…japo yaweza kupungua au kuzidi..
Ikiwa wewe ni kijana, hakikisha maonyo hayo unayatendea kazi mapema…
Lakini ikiwa wewe ni mzazi na una mtoto, fahamu kuwa siku moja atakuwa kijana,hivyo kabla adui hajamtumia, anza kumjengea misingi mizuri ya kutembea katika Imani ya wokovu, naye hataicha njia hiyo mpaka atakapokuwa mtu mzima
Mithali 22:6
[6]Mlee mtoto katika njia impasayo,
Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je Bwana YESU alikuwa na amri ya kumwingiza mtu katika ufalme wa MUNGU au hakuwa nayo?
Fahamu maana ya Mithali 10:5 Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima;
Kuseta kama ilivyotumika kwenye maandiko maana yake ni kukiharibu kitu, aidha kwa kukiponda, kukikanyaga, au Kukivunja vipande vipande.
Kwamfano kwenye maandiko kama haya tunaweza kuona neno hilo..
Warumi 16:19-20
[19]Maana utii wenu umewafikilia watu wote; basi nafurahi kwa ajili yenu, lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya.
[20]Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi.
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. [Amina.]
Hapa Mungu anaonyesha kwamba pale tunapokuwa mbali na mambo mabaya ndivyo anavyomponda shetani chini ya miguu yetu..
Kuonyesha kuwa njia kuu ya kumshinda shetani sio kumkemea bali ni kujitenga na mambo maovu.
Vifungu vingine ni kama hivi..
Zaburi 110:5
[5]Bwana yu mkono wako wa kuume; Ataseta wafalme, Siku ya ghadhabu yake.
Hapa Mungu anaonyesha ukali wa ghadhabu yake juu ya watu waovu..hata wale wanaoonekana ni wakuu, hawataikwepa hasira yake atawaharibu kwa kuwaponda- ponda.
kwa hitimisho ni kuwa kuseta ni kuharibu kabisa Kabisa ..Na Mungu amekusudia kufanya hivyo sio kwetu bali kwa shetani… Ni sisi tu kuishi maisha yanayomlingana yeye ikiwa tayari tumeshaokoka…Lakini ikiwa ni kinyume na hapo tutaingia katika mkondo huo huo wa shetani, wa kuharibiwa endapo hatutamwamini Yesu Kristo leo.
Je upo tayari kumpokea Yesu leo? Kama ni ndio basi bofya hapa >> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Yapo mavazi ya nje na yapo mavazi ya ndani… Mfano wa mavazi ya nje ni haya tunayoyavika juu ya miili yetu (kanzu, suruali, kitani n.k) haya kazi yake ni kuusitiri mwili katika heshima, na ni lazima tuvae mavazi ya kujisitiri..
Lakini pamoja na hayo yapo mavazi ya ndani, ambayo ni ya muhimu sana, na yanamaana kubwa sana zaidi hata ya nje, na haya ni lazima tujivike, kwamaana kama tukijivika vizuri mavazi ya nje, halafu ya ndani tukayakosa, tutakuwa tuna kasoro kubwa sana.
Sasa hetu tujifunze mavazi hayo ya ndani ni yapi…
Wakolosai 3:12 “Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa REHEMA, UTU WEMA, UNYENYEKEVU, UPOLE, UVUMILIVU,
13 mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.
14 Zaidi ya hayo yote JIVIKENI UPENDO, ndio kifungo cha ukamilifu”.
Hapo Biblia inatumia neno “JIVIKENI” Ikiwa na maana kuwa mambo yafuatayo yanafananishwa na mavazi.. na anayataja pale kuwa ni moyo wa Rehema, Utu wema, Unyenyekevu, Upole, Uvumilivu na mwisho anamaliza na Upendo, tutazame moyo baada ya lingine.
1. REHEMA.
Hapo anataja moyo wa rehema, Mtu mwenye moyo wa rehema wakati wote atajishusha mbele za Mungu, na kujitakasa, kamwe hawezi kujiona ni bora mbele za Mungu, na pia mtu mwenye rehema siku zote atakuwa ni mtu wa kuwarehemu wengine, kuwasamehe na kuachia, kwahiyo nasi hatuna budi kujivika moyo huo wa rehema kila siku.
2. UTU WEMA.
Hapa anasema “Utu” maana yake ni “jambo la ndani” sio nje. Mfano wa Utu ulio mwema ni ule aliokuwa nao Yule Msamaria, ambaye alimwona mtu Yule kaangukia mikononi mwa wanyang’anyi akaenda kumsaidia kwa moyo wote Luka 10:30-37. Nasi lazima tulivae hili vazi la Utu wema (2Wakorintho 6:6)
3. UNYENYEKEVU.
Unyenyekevu ni hali ya kujishusha, na kinyume cha unyenyekevu ni kiburi na majivuno, ili tuhesabike tumesitirika kiroho ni lazima tujivike vazi hili la unyenyekevu 1Petro 5:5.
4. UPOLE.
Anasema “Upole” na si “Unyonge”.. Unyonge ni ile hali ya kuwa mtulivu kwasababu ya hofu, au hali Fulani..lakini upole ni hali ya kuwa mtulivu si kwasababu unashindwa kurudisha majibu au kufanya jambo..uwezo wote unakuwa unao lakini hufanyi hivyo, kama alivyokuwa Bwana wetu Yesu, yeye alikuwa na uwezo wa kushusha moto kwa wasamaria lakini hakufanya hivyo.. nasi ni lazima tujivike hili vazi. (Mathayo 11:29)
5. UVUMILIVU.
Uvumilivu ni uwezo wa ndani wa kustahimili jambo baya, laweza kuwa shutuma, mapigo, au jambo jingine lolote, uwezo huo ni muhimu sana sisi wakristo kuwa nao.
Yakobo 5:10 “Ndugu, watwaeni manabii walionena kwa jina la Bwana, wawe mfano wa kustahimili mabaya, na wa uvumilivu.
11 Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma”.
6. UPENDO.
Hapa anasema kuwa hiki ndicho kifungo cha ukamilifu.. Maana yake tukiwa na upendo ni sawa na mtu aliyevaa shati sasa anamalizia kuvaa koti juu yake na kufunga vifungo vyake, na tena Biblia inasema pasipo upendo sisi si kitu haijalishi tunanena kwa lugha au tunafanya ishara (1Wakorintho 13:1).
Kwahiyo hayo ndio mavazi tunayopaswa kuyavaa katika utu wetu wa ndani kila siku, na utaona pia yamerudiwa katika Wagalatia 5:22 kama matunda ya roho, na mengine baadhi kuongezeka.
Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
TUNZA MAVAZI YAKO NA FUA NGUO ZAKO!
USIYAACHE MAVAZI YAKO NA KWENDA UCHI!
WALIYATWAA MAVAZI YAKE, WAKAFANYA MAFUNGU MANNE,
JINSI MATENDO YA IMANI YANAVYOWEZA KULETA UTAMBULISHO MPYA KWA MTU.
Musa (Mgongo)
Kristo (kioo)
Mbinguni (Dhahiri)
Ilikuwa ni shauku ya Musa kutaka Kuuona uso wa Mungu baada ya muda mrefu kukaa bila kumwona Mungu..
Lakini tukirudi kwenye maandiko yanasema, Mungu alizungumza na Musa uso kwa uso kama mtu anavyozungumza na rafiki yake.
Kutoka 33:11 Naye Bwana akasema na Musa uso kwa uso, kama vile mtu asemavyo na rafiki yake. Kisha akageuka akarejea hata maragoni; bali mtumishi wake Yoshua, mwana wa Nuni, naye ni kijana, hakutoka mle hemani.
Lakini iweje tena, aombe kuuona uso wa Mungu, na Mungu kumwambia huwezi kuuona uso wangu ukaishi?
Kutoka 33:20 Kisha akasema, Huwezi kuniona uso wangu, maana mwanadamu hataniona akaishi.
21 Bwana akasema, Tazama, hapa pana mahali karibu nami, nawe utasimama juu ya mwamba;
22 kisha itakuwa wakati unapopita utukufu wangu, nitakutia katika ufa wa ule mwamba, na kukufunika kwa
mkono wangu hata nitakapokuwa nimekwisha kupita;
23 nami nitaondoa mkono wangu, nawe utaniona nyuma yangu, bali uso wangu hautaonekana
Ukweli ni kwamba kuuona uso wa Mungu, sio kuona mwonekano Fulani, au umbo Fulani la Mungu. Hapana, bali ni kumjua yeye ndani ni nani.. Tangu zamani Mungu alikuwa akijifunua kwa wanadamu kupitia maumbile mbalimbali, ambayo yanaweza kuchukua taswira ya vitu, wanadamu au malaika(huitwa Theofania),. Hivyo kwa namna yoyote ile Mungu anapomtokea mtu kwa namna mojawapo ya hizo na kuisikia sauti yake kama vile mwanadamu mwenzako anavyozungumza na wewe, ni sawa na kusema Mungu amesema nawe uso kwa uso. Lakini haimaanishi kuwa umeouna uso wake. Kuuona uso wake ni kumjua yeye ni nani.
Sasa Mungu akamwambia, Musa, huwezi kuniona ukaishi, Kwanini amwambie vile, Je! Mungu ni kifo? Hapana, Mungu ni uzima, lakini Musa alikuwa bado hajakamilika kwasababu ya dhambi, hivyo utukufu wa Mungu asingeweza kuustahimili, kwasababu wakati wa kuustahimili ulikuwa bado, kwani ulihitaji kwanza ondoleo la dhambi kabisa.
Hivyo Mungu akamwonyesha sehemu yake ya nyuma (Mgongo). Lakini Uso hakuuona.. Ndipo akamjua Mungu kwa sehemu yeye ni nani..
Alipomwona alishangaa sana, kwa zile tabia na sifa, Mungu alizokuwa nazo, jinsi zilivyo tofauti na mawazo ya wanadamu.. Pengine alijua ataona mafunuo makubwa ya nguvu na uweza, na mamlaka, ya ukuu, na utukufu usioelezeka kibinadamu, lakini alipomwona Mungu alimwona ni mwenye huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema, mwenye hukumu za haki.
Kutoka 34:5-7
5 Bwana akashuka ndani ya lile wingu, akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina la Bwana.
6 Bwana akapita mbele yake, akatangaza, Bwana, Bwana, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si
mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli;
7 mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba
zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne.
Hata sasa, mtu anayemtambua Mungu kwa namna hii, basi ameuona mgongo wa Mungu.. Na pale mtu anapoiga tabia hizo basi, amemkaribia Mungu sana.
Lakini safari ya kuuona Uso wa Mungu, ilikuwa bado haijakamilika..
Hivyo wakati ulipofika, Mungu akamtuma mwanawe duniani, (Yesu Kristo), kutuonyesha sasa uso wa Mungu ulivyo..Maandiko yanasema hivyo;
Yohana 1:18 Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua.
Umeona kumbe, hakukuwahi kutokea mtu duniani aliyeuona uso wa Mungu, na moja ya kazi kubwa aliyokuja kuifanya Yesu duniani ni kumfunua Mungu(uso wake) ni nani?
Na kwasababu hakuna mtu mwenye dhambi anayeweza kumwona Mungu akaishi, ilimbidi yeye mwenyewe awe fidia ya dhambi zetu, kwa kufa kwake pale msalabani, ili sisi tuhesabiwe kuwa hatuna dhambi (kwa neema), na ndipo sasa tustahimili kuuona utukufu wa Uso wa Mungu.
Na alipotukamilisha kwa namna hiyo, basi, akatuwezesha pia kumkaribia Mungu tumwone.
Yesu akatufunulia uso wa Mungu, kuwa yeye ni UPENDO. Na upendo wake si ule wa kibinadamu, , kwamba nakupenda kwasababu umenipenda, au umenitendea jambo zuri.. Hapana, bali ni ule usio na sharti wa kuonyesha fadhili hata kwa wanautuchukia..
Musa, aliishia kujua huruma tu za Mungu juu juu (kibinadamu), lakini hakujua kuwa hata jino kwa jino, ilikuwa ni makosa, kumwonea mwenzako hasira, au hata kumfolea ilikuwa ni makosa, yanayostahili hukumu, talaka Mungu hapendezwi nazo.. Musa hakujua kuwa Mungu anataka tumwone yeye kama BABA, ambaye ni ‘ABA’ yaani Baba mwenye mahusiano ya karibu na mwanawe, kama ilivyokuwa kwa Yesu na Mungu,yeye alidhani Mungu ni wa kutoa tu amri, sheria na hukumu, Musa hakujua kuwa mwenye dhambi (mfano wa mzinzi, mwanamke mchawi) hapaswi kutupiwa mawe, bali kuhubiriwa injili ili atubu.. Yote hayo Yesu alikuja kutufunulia, kiufasaha kabisa wala hakutuficha chochote..
Kwa jinsi nyingine ni kuwa sisi tumemwona Mungu kupitia Kristo, na kwa kupitia uhalisia wa maisha yake. Tukiyaishi maneno ya Kristo, basi tumemjua Mungu uso wake, kiufasaha kabisa..
Lakini Safari bado inaendelea… Uso wa Mungu katika kilele chake, bado hatujaufikia…
Utauliza kwa namna gani?
Ni kwamba kwasasa tunaouona kwa njia ya KIOO, bado hatujauona kiuhalisia kabisa kwa macho, japo tunaweza kusema kuona kwenye kioo hakuna tofauti na kuona kabisa kwa macho, lakini ladha huwa zinatofautiana, kumwona Raisi kwenye Tv, ni Yule Yule utakayemwona kwa macho, lakini ladha ni tofauti..
Hivyo Kristo alikuwa kama chapa (kioo) ya Mungu yenyewe, duniani..Yaani sisi tayari tumemwona Mungu kupitia Kristo Yesu..
Waebrania 1:3 Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu;
Ndio maana maandiko bado yanasema, kwasasa tunaona kwa kioo, lakini wakati ule tumjua sana yeye alivyo..
1Wakorintho 13:12 Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana.
Wakati wa kuona dhahiri, wema wote wa Mungu, itakuwa ni mbinguni.
Tutamjua katika eneo gani?
Katika eneo lilelile la upendo, (sawasawa na ile 1Wakorintho 13 ilivyokuwa inaeleza habari hiyo tangu juu)
Hapo ndipo tutaufurahia upendo wa Mungu katika namna ambayo hatujawahi kuijua, kwa vile vitu tulivyoandaliwa na yeye mbinguni, milele…
Hivyo, hatuna budi sasa kutembea katika upendo wa Mungu kwasababu yeye ndio huo..
1Yohana 4:16 Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.
Hitimisho:
Hatua za kuuona Uso wa Mungu, zilianza, na Musa, (kwa mgongo), zikaja kwa Kristo (kwa kioo), na mwisho mbinguni, (dhahiri).
Je! Umempokea Kristo? Ikiwa bado, fahamu kuwa huwezi kamwe kumwona Mungu, hata iweje, mpokee leo, akuoshe dhambi zako, kwasababu kumbuka pia alimwambia Musa, hatamwesabia mtu mwovu kuwa hana hatia, yaani kila mmoja atapewa anachostahili. Ukifa katika dhambi zako, hakuna upendo huko kuzimu,hutatolewa huko na kuletwa mbinguni.. kwasababu umechagua mwenyewe giza. Yesu alisema Jehanamu ya moto ipo, na mtu asipomwamini yeye, atakufa katika dhambi zake. Hivyo ndugu, Ingia ndani ya Yesu leo upokee neema, hujui ni lini utaondoka duniani, usiishi tu kama mnyama, tubu dhambi mkimbilie Yesu, akuponye.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Wakolosai 1:9
[9]Kwa sababu hiyo sisi nasi, tangu siku ile tuliposikia, hatuachi kufanya maombi na dua kwa ajili yenu, ili mjazwe maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa rohoni;
JIBU:
Vifungu hivyo vinaonyesha kiu ya mtume Paulo juu ya watakatifu wa kanisa la Kolosai, Kwamba wajawe kuyajua mapenzi ya Mungu katika hekima yote na ufahamu wa rohoni.
Alijua ili kanisa liweze kumpendeza Mungu na kusimama ni lazima lijue mapenzi ya Mungu makamilifu.. Hivyo Ikawa shauku yake tangu zamani lijazwe kujua mapenzi hayo.
Kuna makundi mawili (2), ya mapenzi ya Mungu.
1)Mapenzi Ya daima
2) Mapenzi Ya wakati
Mapenzi ya daima: Ni yale ambayo yapo wakati wote, na kwa wote kwamba kila mwamini lazima ayatimize..mfano wa haya ni..ni kama utakatifu (1Wathesalonike 4:3), kuhubiri Injili, kuishi kwa upendo, kukusanyika pamoja, kudumu katika maombi, kumwabudu Mungu.
Lakini mapenzi ya wakati: Ni yale ambayo Mungu anakusudia uyafanye katika kipindi fulani tu, ni mapenzi yasiyo na mfanano, au mwendelezo fulani.. Kwamfano Mungu anakutaka leo usihubiri, bali uende kumtembelea yatima mmoja kijijini. Mfano wa kama alivyoambiwa Filipo awaache makutano aende jangwani kwa ajili ya yule mtu mmoja mkushi.(matendo Matendo 8:26)
Au wakati mwingine unapitishwa katika jaribu fulani, halafu pasipo kujua kuwa hilo ni darasa la Mungu ili kutumiza kusudi fulani, unajikuta unakemea na kushindana nayo…Ndio maana Bwana Yesu alipoomba juu ya kuondolewa kikombe cha mateso, alimalizia kwa kusema Baba mapenzi yako yatimizwe.
Sasa yote haya yanahitaji hekima na maarifa kuyatambua na kuyatimiliza. Si rahisi kuyatambua kwa akili za kibinadamu au kuyatimiliza.
Jambo la kwanza Paulo analitaja ni kuomba, aliwaombea watakatifu Wa Kolosai kwasababu alijua uwezekano wa kupokea Maarifa hayo upo katika maombi.
Yakobo 1:5
[5]Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.
Maombi hufungua mlango wa Mungu kuyaingilia maisha yetu na kututia katika kusudi Lake kamilifu. Mungu anafanya kazi ndani yetu kupitia maombi…Bila uombaji haiwezekani kutembea ndani ya mapenzi yote ya Mungu.
Kwa kusoma Neno ndipo unapojua Tabia za Mungu, nini anataka na nini hataki. Sauti ya Mungu, maagizo ya Mungu ya moja kwa moja yasiyohitaji usaidizi ni biblia takatifu.
Zaburi 119:105
[105]Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.
Mtu ajijengeaye tabia ya kusoma biblia, si rahisi kuanguka au kutoka nje ya mpango wa Mungu. Kwasababu lile neno linakaa ndani yake kama mafuta kumfundisha.
Bwana anafunua mapenzi yake tuwapo katika mabaraza yetu kutafakari maneno yake.. alisema wawili watatu kwa jina lake yupo hapo hapo katikati yao…Wale watu wawili waliokuwa wanakwenda Emau, tunaona walikuwa zaidi ya mmoja, ndipo wakiwa katika kutafakari habari za Kristo, Aliungana nao bila hata wao kujua akaanza kuwafundisha, na mwisho wote kujua mapenzi makamilifu ya Mungu ni nini..(Luka 24)
Na ndio maana hatupaswi kulikwepa kanisa kwasababu huko tunaungana na viungo vingi katika Mwili wa Kristo, na hivyo kujengana na kuonyana. Hatimaye mapenzi ya Mungu yanafunuliwa kwetu.
Hata wakati ule kulipotokea sintofahamu ndani ya kanisa kuhusu vyakula na sheria..baraza lilikalishwa kule Yerusalemu kisha mahojiana mengi yakaendelea …lakini mwishoni Mungu alitoa maarifa kwa kusema wajiepushe.na damu na uasherati lakini sio mataifa watwikwe tena kongwa la torati lililowashinda wao.(Matendo 15 )
Hivyo ni vema kumshirikisha pia mpendwa mwenzako/ kanisa mpango wako, yapo mashauri ya ki-Mungu ndani yao yaliyojaa hekima yatakusaidia.
Huu ni uwezo wa Mungu ambao mtu humwingia kutokana na kiwango chake cha juu cha ukuaji wa kiroho (Waebrania 5:14).. Bila kutegemea kuomba au kumuuliza Mungu mtu hutambua lililo la kweli na lililo la uongo.. lililosahihi na lisilosahihi, la rohoni au la mwilini, lenye Mwongozo wa ki- Mungu au kibinadamu. Tunaweza kujua mapenzi ya Mungu kwa ujuzi huu, unaozalika kutokana na ukomavu wetu wa kiroho.
Hivyo wewe kama mwana wa Mungu, kumbuka ni sharti kutembea ndani ya mapenzi yake…madhara ya kutembea nje ya hayo ndio kama yale aliyoyasema Bwana kwenye Mathayo Mathayo 7:21..
[21]Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Petro.(1Petro)
SWALI: Je ni kitu gani hasaa kilikuwa kinatokea mpaka wafikie hatua kama ile, je! Ni utahira ulikuwa unawapata au ni nini hasaa?
JIBU: Silaha mojawapo ambayo tuona Mungu alikuwa akiitumia kuwashindania watu wake mara myingi wawapo vitani, Ni hii ya “machafuko” yaani Ni kuwavuraga maadui washindwe kuelewana na hatimaye kuanza kushambuliana wao kwa wao.
Kwamfano wa matukio kama hayo tunaweza kuyathibitisha katika habari hizi;
Wana wa Israeli Walipoizunguka Yeriko.
Waamuzi 7:22
[22]Wakazipiga zile tarumbeta mia tatu, naye BWANA akaufanya upanga wa kila mtu uwe juu ya mwenziwe, na juu ya jeshi lote, jeshi likakimbia mpaka Bethshita, kuendelea Serera, hata mpaka wa Abel-Mehola, karibu na Tabathi.
Sasa tuone ni njia zipi alikuwa anazitumia Mungu mpaka wauane wao kwa wao, watu ambao walikuwa wamekubaliana kabisa kwenda vitani?
Hii ni hali ya kutoweza fikiri vema, kuwa kama mtu fulani nusu aliyerukwa na akili.
Kumbukumbu la Torati 28:28
[28]BWANA atakupiga kwa wazimu, na kwa upofu, na kwa bumbuazi la moyoni;
Hii ni hali yakutokuwa sawa katika ufahamu, unamwona mwenzako kuwa ndiye adui, na hatimaye vita vinaanza kabla hata ya maadui wenyewe kufika..hili ndio yamkini Bwana alilowapiga watu wa Yeriko.
Kama tu vile Mungu alivyowapiga upofu watu wa Sodoma na Gomora wasione mlango wa Lutu, vivyo hivyo hawa wanapigwa katika eneo la fikra wasifiri vema wauane, wao kwa wao.
Hii ni namna ambayo mnapisha usemi. Kiasi kwamba hakuna mtu wa kumsikiliza mwenzake, huyu anataka hili, Yule hili, kila mmoja haafikiani na mwenzake hatimaye chuki inatokea, matengano na mwisho kuanza kupigana wao kwa wao.
Watu wa Babeli walipigwa ‘usemi’ isipokuwa tu wao hawakufikia hatua ya kuuana, lakini ni namna tu hii hii .(Mwanzo 10)
Hii ni hali ya kuwashuku wenzako kuwa ni wasaliti, hivyo ghafla kupoteza imani nao, na kuanzisha vita ili kujilinda…mfano wa hili tunaliona kwenye ile vita ya Yuda na majeshi ya wamoabu, waamoni na wameuni walipokutanika kupigana na taifa la Mungu..ghafla moabu Na amoni wakaipiga Seiri, halafu baadaye wakarudiana Wao kwa wao.
2 Mambo ya Nyakati 20:22-23
[22]Nao walipoanza kuimba na kusifu, BWANA akaweka waviziao juu ya wana wa Amoni, na Moabu, na wa mlima Seiri, waliokuja juu ya Yuda; nao wakapigwa.
[23]Kwani wana wa Amoni na wa Moabu waliwaondokea wenyeji wa mlima Seiri kuwaulia mbali na kuwaharibu; nao walipokwisha kuwakomesha hao wakaao Seiri, wakajitia kuharibu kila mtu mwenziwe.
Hii ya visasi inatokeaje?
Labda mmoja alikuwa na chuki na mwenzake, hivyo unamlipizia kisasi, na huyu naye kaona ndugu yake kauliwa anaamka kumtetea, mara kabila hili na hili hatimaye taifa zima linaiingia katika kujiharibu.
Hivyo Mungu anapotaka kutupigania, silaha hii huwa anaitumia hata katika agano jipya hususani hapo kwenye kugonganisha ndimi.
Kwamfano mtume Paulo alipokamatwa awekwe barazani ili ahukumiwe…kwa hekima ya Roho alipewa kujua kuwa katikati ya baraza wapo mafarisayo na masadukayo. Hivyo alilolifanya ni kuwachonganisha ndimi, badala ya kumshambulia yeye..wakaanza kushambuliana wao kwa wao…hiyo ni silaha ya Bwana ambayo kwa hekima ya Roho aliitamka..
Matendo ya Mitume 23:6-7
[6]Paulo alipotambua ya kuwa sehemu moja ni Masadukayo, na sehemu ya pili ni Mafarisayo, akapaza sauti yake katika ile baraza, Ndugu zangu, mimi ni Farisayo mwana wa Farisayo; mimi ninahukumiwa kwa ajili ya tumaini la ufufuo wa wafu.
[7]Alipokwisha kunena hayo palikuwa na mashindano baina ya Mafarisayo na Masadukayo, mkutano ukafarakana.
Ni vema kufahamu aina hii ya silaha ni mbaya kuliko ile ya kushindana na adui yako.
Lakini ni vema kufahamu kuwa hata shetani hutumia silaha hii, pale tunapotoka nje ya mpango wa Mungu.
Israeli iliingia kwenye vita vya wao kwa wao, na kupelekea mauaji mengi sana…
Ni nini kilitokea?
Baadhi ya wana wa Benyamini waliendekeza dhambi ya uasherati mpaka ikafikia hatua inayokaribia ile ya sodoma Na Gomora na Israeli yote ilipopata taarifa, wakataka wawatoe hao watu wauliwe, lakini wabenyamini wakawaficha kwasababu ni watu wa kabila lao. Machafuko yakaanzia hapo, hatimaye wakauana Sana. (Waamuzi 19-21)
Hata sasa silaha hii shetani hupenda kuirusha kwenye kanisa la Mungu, watu wapoteze upendo na utakatifu ili waanze kulana na kung’atana..kwasababu ya wivu, visasi na vinyongo.
Wagalatia 5:14-15
[14]Maana torati yote imetimilika katika neno moja, nalo ni hili, Umpende jirani yako kama nafsi yako.
[15]Lakini mkiumana na kulana, angalieni msije mkaangamizana.
Lazima tuijue hila hii ya shetani na kukataa kuipa nafasi.. Na Bwana atatuhifadhi, na matokeo itakuwa ni yeye kuleta machafuko kwa maadui zetu wanaposimama Kinyume na sisi.
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, tunashindanaje vita vya kiroho?
Jibu: Tuanzie ule mstari wa kwanza..
2Timotheo 4:1 “Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake;
2 lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, KARIPIA, KEMEA, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho”.
“Kukaripia” ni kulaani au kukosoa kosa lilolofanyika… Kwamfano mama anaweza kumkaripia mwanae kwa tabia ya Uvivu, kwamba aiache hiyo tabia, kwani ni mbaya na itamletea madhara huko mbeleni..na kukaripia mara nyingi kunaambatana na kutoa elimu,ushauri au darasa juu ya hilo kosa..
Lakini “Kukemea” inaenda mbali zaidi, kwani kunahusisha kulaani kitendo kibaya na kutoa amri ya zuio ya jambo hilo lisiendelee kutokea… Kwamfano Mama anaweza kumkemea mwanae kwa kosa la Wizi, Kwamba tendo hilo ni kosa na lisirudiwe tena! (hiyo inakuwa ni amri, sio ombi tena wala ushauri).
Serikali inaweza kukemea vitendo vya mauaji, ubakaji au rushwa.. kwamba vitendo hivyo ni vibaya na havipaswi kutendeka kwani ni uvunjifu wa sheria, hivyo kutofanya hayo ni amri na sio ombi wala ushauri..
Na katika Biblia, Neno la Mungu linatuagiza “Kukaripia” na “Kukemea”
2Timotheo 4:2 “lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, KARIPIA, KEMEA, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho”.
Zipo tabia au mienendo iliyopo kati ya watu ambayo kiuhalisia inahitaji “kukaripiwa” na mingine “kukemewa” na Neno la Mungu linatufundisha kufanya hivyo bila kuogopa pale inapobidi. (hususani ndani ya kanisa)
Kwamfano vitendo vya wivu, uvivu, uzembe, utegeaji ndani ya kanisa, (hivyo katika hali ya uchanga vinaweza kukaripiwa tu na vikaisha), lakini vinapozidi mipaka vinapaswa vikemewe!.
Lakini vitendo vingine kama vya Ulevi, Uchawi, uzinzi, uasherati, wizi, utukanaji, fitina na vingine vinavyofanana na hivyo, havihitaji kukaripiwa bali KUKEMEWA, kwamba visiendelee kufanyanyika na hiyo inakuwa ni “Amri” na sio “Ombi wala ushauri”, maana yake mtu akiendelea kufanya hayo makusudi baada ya kuonywa mara nyingi, ni haki yake kutengwa kwa muda mpaka atakapojirekebisha ili asilichafue kanisa la Kristo.
1Wakorintho 5:11 “Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.
12 Maana yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani?
13 Lakini hao walio nje Mungu atawahukumu. Ninyi mwondoeni yule mbaya miongoni mwenu”.
Hapo anaposema “ndugu” anamaanisha Ndugu katika Imani (mkristo), hususani Yule ambaye tayari analijua Neno la Mungu, lakini hataki kubadilika yuko vile vile ndani ya kanisa ni mlevi, au mzinzi, au mwizi, huyo kama amekemewa na hakubali kubadilika, Biblia imetoa ruhusa ya kumtenga kwa muda, ili asilichafue kanisa..
Lengo la kumtenga ni ili atafakari na asione kanisani ni mahali pa kufanyia mchezo, au pango la wanyang’anyi.. Akifanyiwa hivyo itampa muda wa kutafakari na kama ni mtu wa kujali basi atatambua makosa yake na kujirekebisha na hivyo atarudishwa kanisani… Lakini kwa wale wengine walioingia kwenye wokovu hivi karibuni (ambao bado ni wachanga) hao hawawezi kutengwa wanapofanya makosa yale yale waliotokea nayo duniani kwani bado ni wachanga wanahitaji kufundishwa zaidi..Lakini kwa wale wengine waliokaa miaka na hawabadiliki, Neno limeruhusu kuwatenga kwa muda.
Hivyo kwa hitimisho ni lazima kukaripia mabaya, lakini pia kukeme na kuonya pia..Kwani hata Bwana Yesu Kristo huwa anatukemea pale tunapoondoka kwenye njia (Ufunuo 3:19)
Neno hilo “Kukemea” linaweza kutumika pia katika kutoa pepo, kwasababu pepo anapokuwa ndani ya mtu, huwa anamtesa Yule mtu, na si haki yake kumtesa.. hivyo tunapoamuru pepo atoke ndani ya mtu maana yake tunatoa “AMRI” sio “Ombi”.. kwamba hizo shughuli zake anazozifanya ndani ya mtu, zisimame na amtoke Yule mtu, Pepo hatulikaripii bali tunalikemea (Luka 9:42)
Bwana atubariki na kutusaidia sote.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MAMBO MANNE(4) YAFANYAYO NENO LA MUNGU.
Vita vya kiroho, na mwamini Mpya.
Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote (Yohana 16:23)
NAYE ALIKUWA HANA BUDI KUPITA KATIKATI YA SAMARIA.
Kumwambia mtu mwenye dhambi kuwa atakwenda kuzimu asipotubu Je! ni kuhukumu?
Ahadi mojawapo ya Roho Mtakatifu Kwa wote waliompokea ni kupewa uwezo wa kuzungumza “ufahamu wa Mungu”, kwa vinywa vyao.
Ufahamu huu unaweza kujifunua katika maumbile mbalimbali aidha kwa kueleza habari zilizopita, au habari zijazo, au zinazoendelea sasa hivi, au kutoa maelekezo, au faraja, au neno la hekima, au maarifa, au uponyaji au baraka..Namna zote hizi kwa lugha rahisi kuitwa utabiri/ unabii.
Ukiwa kama mwamini ni vema kufahamu sehemu kubwa sana ambayo Roho Mtakatifu anaitumia kuhudumu ni katika vinywa vyetu. Ndio maana siku ile ya kwanza ya pentekoste aliposhuka, alikaa juu ya wale watu kama “ndimi za moto”. Maana yake ni kuwa huduma yake hasaa hujidhihirisha katika ndimi…ndio maana akaweka moto wake juu ya ndimi zao, lugha zao zikabadilishwa wakaanza kunena kwa lugha mpya.
Kwahiyo kinywa cha mtu aliyeokoka, ni kinywa cha Mungu duniani. Usipojifunza kukifungua kinywa chako kiufasaha, ujue hiyo ni namna mojawapo ya kumzimisha Roho Mtakatifu ndani yako.
Watu wengi hawajui kuwa kila mmoja amepewa uwezo wa kutabiri/ kuhutubu na sio suala la huduma fulani ya kinabii tu, hapana utauliza hilo lipo wapi kwenye maandiko? Soma..
Matendo 2:17 wana wenu na binti zenu watatabiri..
Lakini pia 1 Wakorintho 14:31. Inasema..
[31]Kwa maana ninyi nyote mwaweza kuhutubu mmoja mmoja, ili wote wapate kujifunza, na wote wafarijiwe.
Kuhutubu kama ilivyotumika hapo, ni kutabiri/ kusema ufahamu wa Mungu. Jambo ambalo ni la wote sio baadhi.
Usisubiri mpaka karama fulani ije juu yako, yaani kuonyeshwa/kufunuliwa.. hapana…kwasababu tayari una Roho Mtakatifu ndani yako anza kusema maneno yanayolanda na ahadi za Neno la Mungu, bila kufikiri- fikiri
Kwamfano…
Umepelekwa kwenye mashtaka fulani kwa ajili ya Neno. Au unatakiwa uwasilishe hoja, au ufundishe Neno, au uhubiri, au umekwenda mtaaani kushuhudia.. usianze kusema mimi nitawezaje kuhubiri, au kujieleza, sijui sheria, sijui vizuri biblia, sijui kupangilia maneno…hupaswi kufikiri hivyo. bali ukumbuke ulishapewa kinywa cha moto, tangu siku ulipoamini, wewe nenda kisha anza kuzungumza huko huko katikati ya maneno yako Roho Mtakatifu ataunganika na wewe.
Mathayo 10:18-20
[18]nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa.
[19]Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.
[20]Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu.
Mwingine atakuambia mimi siwezi kuomba masafa marefu ninaishiwa na maneno…ndugu hupaswi kukatisha maneno na kuacha Kuomba, ukaenda kulala.. endelea kutafakari huku ukizunguza na Mungu wako Habari mbalimbali za kwenye maandiko, na ghafla tu baada ya muda kidogo utaona unaingia kwenye mkondo fulani wa kimaombi, linatoka neno hili kwenye ufahamu linakuja neno hili la kuombea…ulikuwa umepanga uombe Saa 1, unajikuta unaomba matatu.hapo ni Roho Mtakatifu amekupa Kinywa cha kuomba..na ndani ya maombi hayo ni utabiri tosha, kwasababu sio ufahamu wako, bali ni wa Mungu ndani yako.
Vilevile jifunze kutoa sauti katika uombaji wako wa mara kwa mara..ndio tunafahamu Maombi sio sauti, hata kimoyo- moyo Mungu anasikia, lakini usimzimishe Roho..
Watu wengi wanatamani kunena kwa lugha lakini, wanazuia vinywa vyao kutoa sauti.. wanategemea vipi wanene kwa lugha mpya..unapojiachia Kwenye maombi huku unatoa sauti ni rahisi sana kujazwa Roho Na kuomba kwa lugha.
Eneo lingine labda mtu ni mgonjwa..anahitaji maombi…Fungua kinywa chako kwa ujasiri mtamkie uponyaji…unaweza kudhani ni maneno yako, hujui kumbe Ni Roho Mtakatifu Ameyaingilia na kulifanya tayari kuwa Neno la kinabii la uponyaji, na hatimaye anapokea uponyaji wake saa hiyo hiyo.
Uwapo na Watoto wako, Acha kuzungumza nao, habari za kidunia dunia tu..wawekee mikono wabariki kwa Imani kama vile Isaka alivyowabariki Yakobo na Esau na maneno yale yakawa kweli. Vivyo hivyo na wewe tabiri juu ya watoto wako unataka wawe nani wawapo watu wazima.
Uwapo kazini na marafiki zako, penda kuzungumza maneno ya ki-Mungu wakati mwingi kwasababu huko huko unabii unaweza kupita bila wewe kujijua… mwangalie kayafa
Yohana 11:49-52
[49]Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote;
[50]wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima.
[51]Na neno hilo yeye hakulisema kwa nafsi yake; bali kwa kuwa alikuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, alitabiri ya kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa hilo.
[52]Wala si kwa ajili ya taifa hilo tu; lakini pamoja na hayo awakusanye watoto wa Mungu waliotawanyika, ili wawe wamoja.
Hivyo kinywa cha ni kinywa cha Roho Mtakatifu usikifunge Bali kijaze Maneno ya Mungu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine: