Title 2025

Je ni sahihi kutumia kumbi za kidunia kuendeshea ibada za kikanisa au semina?

Ni vema kufahamu Kanisa ni nini?

Kanisa sio jengo, au mahali, bali ni watu, walioitwa Na Mungu, waliookolewa wanakusanyika pamoja katika nia moja kumwabudu na kumtumikia yeye.

Hivyo watu hawa wanaweza kukusanyika maeneo yaliyo rasmi, lakini pia maeneo yasiyo rasmi kwa shughuli zao za kiibada..maadamu tu wamekidhi vigezo hivyo vya kiroho.

Kanisa la kwanza lilikusanyika Hekaluni (mahali rasmi kwa shughuli za kiibada tu). Lakini pia lilikusanyika majumbani…wakati mwingi pembezoni Mwa mito na kwenye madarasa..

Matendo ya Mitume 2:46

[46]Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,

Matendo ya Mitume 5:42

[42]Na kila siku, ndani ya hekalu na nyumbani mwao, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo.

Kama tunavyojua majumbani mahali ambapo, pana shughuli nyingi wakimaliza ibada huwenda sherehe zinafanyika hapo, au vikao vya kijamii, lakini hilo halikuwazuia kutimiza makusudi ya Mungu yaliyoyakusudia.

Hivyo yaweza kuwa ni sahihi endapo, hakuna mahali rasmi bado, ibada zinaweza kufanyika kwenye majengo ya shule, kwenye mabwalo, kwenye kumbi,.viwanjani, hata chini ya miti maadamu tu umoja huo upo na nia ni Kristo..hata hivyo yapo makanisa makubwa na yamefanikiwa lakini bado hayana maeneo yao rasmi ya kukutanikia…lakini kanisa Limesimama.

Mambo tu ya kuzingatia, ni nidhani yenu, adabu na utulivu wa mazingira ya kiroho kwa wakati huo,..ikiwa haya yapo hapo Mnapokusanyikia basi Mungu yupo nanyi..wala si dhambi.

Lakini ni busara na vema zaidi kanisa likatafuta eneo rasmi la kukusanyikia litakalokuwa ni kwa shughuli zao tu za kiibada.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?

MAISHA YA UVUGUVUGU, YANAMFANYA MUNGU AUMWE.

UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?

Print this post

Siku ya kujiliwa inayozungumziwa katika  1Petro 1:12, ni ipi?

1Petro 1:12 Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.

Siku ya kujiliwa ni wakati ambao, Mungu anashuka ulimwenguni, aidha kwa kuokoa au kuhukumu.

Zote mbili ni siku za kujiliwa.

Kwa mfano kwa lengo la kuokoa. Upo wakati ambao neema ya Mungu humjia mtu, au taifa, na hivyo wakati huo mara nyingi uamsho mkubwa huwa unapita, Kwamfano, kipindi cha Kristo, kilikuwa ni kipindi maalumu cha Israeli kujiliwa lakini hawakukubali ..isipokuwa wachache..(Luka 19:41-44)

Lakini kwa lengo la hukumu ni siku ambayo kila mmoja wetu atahukumiwa kulingana na matendo yake.

Hivyo tukirudi kwenye 1 Petro 1:12, inayosema ‘Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa’.

Maana yake, matendo mema ya mwamini, hupelekea watu kuupokea wokovu na kumtukuza Mungu,siku neema yao inapowafikia, kwamfano wapo watu ambapo kwa kukuangalia, kwa kipindi kirefu, siku ya kujiliwa inapowafikia inakuwa ni rahisi kuamini na kumtukuza Mungu, kwasababu walishawahi kuona watu waliokoka walivyo na sifa zao njema, mfano upendo, amani, uadilifu..Lakini ukiwa na mwenendo mbovu, siku yao ya kujiliwa inapowafikia, wakikumbuka mwenendo mbovu waliouna kwako , ni ngumu sana kumtukuza Mungu,

Ndicho ambacho mtume Petro alikuwa anakieleza hata mbeleni kidogo, kuhusiana na Wanandoa, kwa upande wa wanawake, akasema, ikiwa mtu ana mume asiyeamini, anao uwezo wa kumvuta ndani ya Kristo kwa mwenendo wake tu.. (1Petro 3:1).

Kwa ufupi ni kuwa mwenendo wako mwema hulainisha njia ya neema ya Kristo Kutenda kazi vema juu ya mtu.

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Biblia inamaana gani inaposema “Mungu wa neema yote” (1Petro 5:10)

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.

MILANGO YA KUZIMU.

Print this post

Pepo waliwaudhi vipi watu? (Matendo 5:16)

Jibu: Turejee..

Matendo 5:16 “Nayo makutano ya watu wa miji iliyoko kandokando ya Yerusalemu wakakutanika, wakileta wagonjwa, nao WALIOUDHIWA NA PEPO WACHAFU; nao wote wakaponywa”.

Katika Biblia, neno “Kuchukizwa” au “Kuchukiza” limekuwa na maana zaidi mbili, maana ya kwanza ya kuchukizwa ni ile hali/hisia ya “Kutopendezwa na jambo” inayozaa huzuri, au hasira mfano wa hiyo ni ile iliyompata Bwana Yesu alipokutana na Sauli alipokuwa anaenda Dameski kuwafunga wakristo..

Matendo 9:3 “Hata alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafula ikamwangaza kote kote nuru kutoka mbinguni.

4 Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, SAULI, SAULI, MBONA WANIUDHI?

5 Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, MIMI NDIMI YESU UNAYENIUDHI WEWE.

6 Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda”.

Hapa inaonyesha ni jinsi gani matendo ya Sauli ya kikatili yalivyokuwa yanamwudhi Bwana.. Lakini pia tunaona mahali pengine pakionyesha Wayahudi walikuwa wakimwudhi Bwana YESU kwasababu alikuwa anafanya miujiza siku ya sabato..

Yohana 5:14 “Baada ya hayo Yesu akamkuta ndani ya hekalu, akamwambia, Angalia, umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi.

15 Yule mtu akaenda zake, akawapasha habari Wayahudi ya kwamba ni Yesu aliyemfanya kuwa mzima.

16 Kwa sababu hiyo Wayahudi wakamwudhi Yesu, kwa kuwa alitenda hayo siku ya sabato.

17 Akawajibu, Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi”

Sasa si mahali pote katika Biblia neno hilo “kuudhi/kuudhiwa” limemaanisha “kukwazwa au kutopendezwa na jambo fulani” bali sehemu nyingine limemaanisha “KUTESWA”

Mfano wa sehemu hizo ni hapa katika kitabu cha Matendo ya Mitume..

Matendo 5:16 “Nayo makutano ya watu wa miji iliyoko kandokando ya Yerusalemu wakakutanika, wakileta wagonjwa, nao WALIOUDHIWA NA PEPO WACHAFU; nao wote wakaponywa”

Kuudhiwa kunakomaanishwa hapo ni ile hali ya “Kuteswa na Kuonewa” Hivyo hapo Biblia imemaanisha kuwa waliokuwa wanateswa na pepo wachafu walifunguliwa, hali kadhalika mahali pengine panapoonesha kuwa kuudhiwa kunakomaanisha kuteswa ni katika kitabu kile cha Ufunuo 12:13.

Ufunuo 12:13 “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume”.

Na katika Mathayo 5:10-12 ni Maudhi ya Mateso yanayozungumziwa hapo..

Mathayo 5:10 “Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

11 Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu.

12 Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu”

Je na wewe unaudhiwa kwaajili ya haki au kwaajili ya Mabaya?…Kama ni kwaajili ya Kristo basi fahamu kuwa thawabu yako ni kubwa mbinguni, lakini kama ni kwaajili ya mabaya, basi tubu leo na mpokee YESU akutoe katika hizo dhiki ambazo hazina faida yoyote bali mwisho wake ni hasara mara mbili katika siku ile ya mwisho.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

TENGENEZA NJIA YAKO.

Je unajua sababu nyingine ya MUNGU kuigharikisha dunia ya wakati wa Nuhu?

Mwanzo 6:12 “Mungu akaiona dunia, na tazama, imeharibika; MAANA KILA MWENYE MWILI AMEJIHARIBIA NJIA YAKE DUNIANI

13 Mungu akamwambia Nuhu, MWISHO WA KILA MWENYE MWILI UMEKUJA MBELE ZANGU; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia”.

Umeona? Kumbe sababu nyingine ya Mungu kuigharikisha dunia ni “WATU KUHARIBU NJIA ZAO DUNIANI”.

Njia yako ina maana sana kwako na kwa MUNGU, ukiiharibu au mwingine akakuharibia basi na uwepo wako duniani utakuwa hauna maana..

Sasa Kila mtu anayo njia ya MAISHA YAKE duniani, na NJIA kila mmoja haifanani na ya Mwingine..lakini haijalishi njia ya mtu ipoje mwisho wake inapaswa imfikishe mtu katika Amani, Furaha, Utulivu, Ushindi, uchaji wa Mungu na mwisho Uzima wa Milele.

Lakini mtu aliyepoteza uelekeo wa njia yake, basi anakuwa anaishi katika tamaa za ulimwengu, dhambi, maasi na mwisho wake ni hukumu ya Mungu.

Lakini habari njema ni kwamba, haijalishi MTU kapoteza uelekeo  kiasi gani, au njia yake imeharibika kiasi gani, maadamu anaishi bado anao uwezo wa kuitengeneza na mapito yake yakawa yamenyooka kabla ya kifo, au hukumu ya Mungu kufika..

Mfano wa mtu katika Biblia aliyetengeneza njia zake kabla ya kufa kwake ni Mfalme Yothamu..

2Nyakati 27:6 “BASI YOTHAMU AKAWA NA NGUVU, KWA KUWA ALIZITENGENEZA NJIA ZAKE MBELE ZA BWANA, MUNGU WAKE.

7 Na mambo yote ya Yothamu yaliyosalia, na vita vyake vyote, na njia zake, tazama, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.

8 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka kumi na sita huko Yerusalemu.

9 Yothamu akalala na babaze, wakamzika katika mji wa Daudi; na Ahazi mwanawe akatawala mahali pake”.

SASA TUNATENGENEZAJE NJIA ZETU?

     1. Kwa kulitii Neno la Mungu

Zaburi 119:9 “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? KWA KUTII, akilifuata neno lako”.

Neno la Mungu (kwa ufupi Biblia) ndio taa na mwanga wa njia yetu (soma Zab. 119:105), maana yake tukitaka uelekeo wa maisha tunaupata ndani ya Biblia.

Biblia ni kitabu ambacho kimeelezea kwa ufasaha wote wa rohoni na mwilini namna ya kutembea Duniani, na mtu anayesoma Biblia kwa ufunuo kamwe hawezi kupoteza uelekeo wa Maisha, kwani ndani ya Biblia kuna kanuni za namna ya kupata amani, furaha, utulivu, uvumilivu, ushindi, mafanikio na zaidi sana UZIMA WA MILELE.

Mtu anayeikwepa Biblia na maonyo yake tayari kashajiweka katika hatari ya kuharibu njia yake Duniani, na mabaya yatamfikia tu kwasababu njia yake imeharibika..

Yeremia 26:13 “Basi sasa, tengenezeni njia zenu, na matendo yenu, mkaisikilize sauti ya Bwana, Mungu wenu; naye Bwana atayaghairi mabaya aliyoyanena juu yenu”.

Ukitaka kufikia Amani ya maisha yako, lisome na kulitii Neno la Mungu, Biblia inaposema usifanye jambo fulani basi usifanye, vile vile inaposema fanya jambo fulani basi tii na kufanya..njia yako ya Amani utakuwa umeinyoosha, vile vile njia yako ya furaha utakuwa umeinyoosha, vile vile njia yako ya mafanikio yako ya rohoni na pia UZIMA WA MILELE, zipo ndani ya Biblia.

Yeremia 7:3 “Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tengenezeni njia zenu, na matendo yenu, nami nitawakalisha ninyi mahali hapa”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Dhuluma/Kudhulumu ni nini kibiblia (Mathayo 6:11)?

Jibu: Turejee..

Mwanzo 6:11 “Dunia ikaharibika mbele za Mungu, dunia IKAJAA DHULUMA.

12 Mungu akaiona dunia, na tazama, imeharibika; maana kila mwenye mwili amejiharibia njia yake duniani.

13 Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia”.

Kwa tafsiri ya Kawaida Dhuluma/kudhulumu ni kitendo cha kumnyima au kumpokonya mtu haki yake kwamfano kwamfano umeazimwa pesa na haujairudisha na unao uwezo wa kufanya hivyo,  hiyo ni dhuluma.

Au mtu ana haki ya kupata huduma fulani kutoka kwako na humpatii kwasababu binafsi hapo unakuwa unamdhulumu haki yake.. Na dhuluma ya namna hii ni dhambi..

Lakini katika Biblia neno hili Dhulumu limeenda mbali zaidi likijumuisha mambo mengi zaidi ya “kumnyima tu mtu haki yake” bali limejumisha pia “vurugu, uonevu, ubaya na uasi”.

Hivyo Neno dhuluma linapotajwa kwenye Biblia linabeba maana pana zaidi ya tunayoifahamu na kuitumia sasa.. Kwamfano hapo katika Mwanzo 6:11-13 inapotajwa Dhuluma, imemaanisha vitendo vyote vya vurugu, uonevu, maasi, na kuwanyima watu haki zao, na hiyo ndio ikawa sababu ya Mungu kuigharikisha Dunia ya kwanza..

Mwanzo 6:11 “Dunia ikaharibika mbele za Mungu, dunia IKAJAA DHULUMA.

12 Mungu akaiona dunia, na tazama, imeharibika; maana kila mwenye mwili amejiharibia njia yake duniani.

13 Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia”.

Maandiko mengine yanayotaja dhuluma ni pamoja na Zaburi 55:9-11, Zaburi 82:2, Zaburi 119:78, Zaburi 119:134, Warumi 2:8 na Ufunuo 22:11.

Je umempokea YESU?.. au upo bado unatanga tanga na dhuluma za huu ulimwengu?.. Kumbuka maandiko yanasema Dunia ya kwanza iligharikishwa kwa maji lakini hii ya sasa imewekwa akiba kwa moto, kwasababu zile zile zilizoigharikisha Dunia ya kwanza (yaani ya kipindi cha Nuhu).

2Petro 3:6 “kwa hayo dunia ile ya wakati ule ILIGHARIKISHWA NA MAJI, ikaangamia.

7 Lakini mbingu za sasa na nchi ZIMEWEKWA AKIBA KWA MOTO, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu”.

Bwana YESU mkuu wa haki  (Zaburi 45:7) ANARUDI!

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

UZURI WA MAJIVU.

Isaya 61: 1-3

1 Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta …
kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, WAPEWE TAJI YA MAUA BADALA YA MAJIVU, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na Bwana, ili atukuzwe.

Kitu kikishachomwa na kuteketea kabisa, kinachosalia cha mwisho kabisa huwa ni majivu. Majivu hayana thamani yoyote, ni vumbi jembamba, ambalo likikanywagwa, hutoweka kabisa.

Hivyo zipo nyakati ambazo, watu wanakuwa kama majivu mbele ya macho yao wenyewe, au kwa wengine. Yaani Kila kitu kimekufa na kuteketea kabisa, yale maono aliyokuwa nayo yamefutika, wengine afya zao zimekuwa jivu,hawana matumaini ya kupona tena, wengine maisha yamevurugika, akiangalia muda aliochezea  moyo unapoa kabisa, wengine mahusiano yao yametafunwa, haoni kuendelea mbele.. Rohoni akijiangalia ni jivu tu, kila mahali ni jivu  hajasaliwa na chochote, isipokuwa kukata tamaa na kupotea kabisa..

Ndio maana katika enzi za biblia mtu aliyekuwa katika maombolezo Makali, alijimwagia majivu mwilini kama ishara kuwa umepukutika kabisa..Mfano wa hawa ni Ayubu na Mordekai (Ayubu 2:8, Esta 4:1 )

Lakini Mungu afufuaye matumaini, alitoa unabii huu juu ya mwanawe atakayekuja kuukomboa ulimwengu, akasema..

Amemtia mafuta, “ili awape watu wake taji ya maua badala ya majivu..”

Tafsiri yake, ni kuwa sio tu atamwondoa kwenye majivu  na kumwacha, Hapana, bali anambadilishia na kumpa taji la maua.

Maua huwakilisha heshima, cheo, hadhi, baraka, afya.

Hivyo haijalishi utakuwa katika hali isiyoeleweka kiasi gani, Yupo Yesu wa kukuondoa majivuni na kukuvika maua, ‘Majivu yako leo ndio maua yako baadaye, lakini ikiwa tu utakuwa ndani ya Kristo’.

Usihofu wala usiogope, wala usikate tamaa..Magonjwa hugeuzwa afya.

Yusufu alikuwa majivu gerezani, lakini Mungu alimfanya maua katika kiti cha Farao. Petro alikuwa jivu kwa kumkana Bwana wake, lakini ndiye alikuwa mjenzi wa  kanisa la Kristo. Ruthu alikuwa mjane kwa kufiwa na mumewe, lakini Bwana alimwekwa kama mama wa uzao wa kifalme, Haijalishi hutafaa kwa jinsi gani leo, Kristo yupo kukugeuza, na kukuondoa majivuni.

Lakini hii inahitaji kumpokea na kuendelea kuishi ndani yake. Je upo tayari kuyakabidhi leo maisha yako kwake?

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAISHA YA UVUGUVUGU, YANAMFANYA MUNGU AUMWE.

Kwanini mkono wa Musa uingie ukoma?

UMESAMEHEWA DHAMBI ZAKO.

Print this post

UFIKIE UWEPO WA MPONYAJI.

Watu wengi wanatamani kuona Kristo, akiwatendea miujiza, akiwaponya, akiwabariki, lakini hawataki kufikia kiwango cha uwepo wake ambacho, anaweza kuachilia nguvu zake kukuhudumia kiharaka.

Katika biblia tunaona kuna nyakati Yesu, alikuwa anatembea kufanya huduma, na umati mkubwa ulikuwa unamfuata, lakini walioponywa haukuwa umati wote, bali watu baadhi, ambao walifanya kitu cha ziada.

Yule mwanamke aliyetokwa na damu kwa miaka 12, ambaye alihangaika kwa waganga wa kila namna, asipate, uponyaji, alipomwona Yesu, na kutazama umati mkubwa wa watu, haku “assume” (dhani), kwamba kwa kumwona tu Yesu inatosha, kwa kusikia tu sauti yake inatosha, mimi kufunguliwa na yeye..

Bali alijua ni lazima nimfikie alipo, nifanye chochote, kwa namna yoyote ikiwa nitashindwa kumkumbatia, basi nitalishika tu pindo la vazi lake Inatosha..maadamu tu, kuna mahali nimeji “connect” na yeye, Nimekaribia vya kutosha.

Ndipo akaonyesha jitihada nyingi kulivuka lile Kundi, na wale walinzi (mitume wake), waliokuwa wakimlinda Yesu. Hatimaye akafanikiwa.

Luka 8:43 Na mwanamke mmoja, ambaye ametokwa na damu muda wa miaka kumi na miwili, [aliyekuwa amegharimiwa mali zake zote kwa kuwapa waganga] asipate kuponywa na mtu ye yote,
44 alikwenda nyuma yake, akaugusa upindo wa vazi lake; na mara hiyo kutoka damu kwake kulikoma.

Wakristo wengi leo, wanaona uvivu kumkaribia sana Kristo, wanataka waponywe wakiwa mbali, wakiwa maofisini mwao, wamekaa kwenye viyoyozi,  wanatazama mahubiri youtube, lakini muda wa Kwenda ibadani hawana,  wanataka wafunguliwe kwa kuletewa mafuta ya upako yaliyoombewa makanisani, lakini wao wenyewe kukaa chini kuomba hawataki, wanataka, waponywe kwa kuombewa na watumishi, lakini wao wenyewe kuutafuta uso wa Mungu hawataki..

Ndugu, lazima uutafute uwepo wa Kristo kwa nguvu.. Mambo mengine hayatoki, hivi hivi, onyesha bidii kufikia walau pindo la vazi la Yesu, umguse.

Kumgusa Yesu, ni kuhudhuria maombi ya masafa marefu, mfano mikesha..Kumgusa Yesu, ni kuwepo kwenye ibada, mahali ambapo mwili wa Kristo umeungana wote kwa uwepo wa watakatifu wengi,  kumgusa Yesu ni kumsifu na kumwabudu Mungu kwa muda  wa kutosha, kufunga na kuifanya kazi yake..

Lakini tuwapo walaini laini, tunangojea Yesu aletwe na watu kama barua za posta, wakati wewe mwenyewe unaouwezo wa kumfikia, utakawia sana ndugu, kama wale makutano, utafuata sana, mpaka utachoka, ni wasaa wa kuamka na kujiunganisha na Yesu wako.. Mguse, Mguse, utapokea hitaji lako kwa haraka zaidi, kuliko kuwa mbali

Ondoa uvivu wa kiroho, anza sasa kujishughulisha kwake, na yeye atakuhudumia kwa neema zake.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

YESU MPONYAJI.

MISTARI YA BIBLIA YA UPONYAJI.

NA JINA LAKE AITWA, NENO LA MUNGU.

Print this post

UMESAMEHEWA DHAMBI ZAKO.

Siku moja Yesu alipokuwa anahubiri katika nyumba fulani, watu wengi walikusanyika mahali pale, na ghafla wakamletea mtu aliyepooza mwili mzima hawezi kufanya lolote, wakamweka Mbele yake ili amponye. Lakini tunaona mwitikio wa Yesu ulikuwa ni tofauti na matarajio yao. Bwana Yesu hakumwekea mikono na kumwambia simama uende, bali alimwambia..

Rafiki, umesamehewa dhambi zako.

Luka 5:17-20

[17]Ikawa siku zile mojawapo alikuwa akifundisha, na Mafarisayo na waalimu wa torati walikuwa wameketi hapo, waliotoka katika kila kijiji cha Galilaya, na Uyahudi, na Yerusalemu; na uweza wa Bwana ulikuwapo apate kuponya.

[18]Na tazama, wakaja watu wanamchukua kitandani mtu mwenye kupooza; wakataka kumpeleka ndani na kumweka mbele yake.

[19]Hata walipokosa nafasi ya kumpeleka ndani kwa ajili ya lile kundi la watu, walipanda juu ya dari wakampisha katika matofali ya juu, wakamshusha yeye na kitanda chake katikati mbele ya Yesu.

[20]Naye alipoiona imani yao, alimwambia, Ee rafiki, umesamehewa dhambi zako.

Jicho la mwanadamu linaona uponyaji ni kutendewa muujiza wa nje, lakini kwa Mungu Uponyaji hasaa ni kusamehewa dhambi. Mtu akishasamehewa dhambi, mengine yote hufuata..

Tunasamehewaje dhambi?

Kwa kumwamini Bwana Yesu na kumaanisha kumfuata kwa toba ya kweli. Hapo ndipo tunapopokea Msamaha Wa dhambi zetu, na hatimaye uponyaji Wa mambo yetu mengine yote.

Wakolosai 1:13-14

[13]Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;

[14]ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;

Matendo ya Mitume 26:18

[18]uwafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na kuielekea nuru, waziache na nguvu za Shetani na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi.

Ni ajabu Kuona, watu wanakwenda kwa Yesu na mapooza Yao, wengine katika afya zao kama huyu, wengine mapooza ya shughuli zao, wengine katika familia Zao n.k. wakitarajia Yesu awaponye kwa njia zao.

Lakini wanapokutana Na injili za wokovu na kuacha dhambi.. wanazikwepa wanakimbilia kwenye maombezi na mafuta Ya upako.

Ndugu fahamu kuwa asili ya kila tatizo ni dhambi..Mahali ambapo maisha yako yanawekwa wazi, yanamulikwa hapo ndipo uponyaji wako halisi upo. Usikimbie, usitange-tange.

Pokea kwanza msamaha wa dhambi mengine yafuate…kubali wokovu, kubali uzima, uponywe. Itakufaidia nini upate ulimwengu wote, afya yote, amani yote kisha ukateketee tena jehanamu milele baadaye?

Ikiwa bado hujaokolewa (yaani hujapata msamaha wa dhambi zako) basi wakati ndio huu.. wasiliana nasi kwa namba hizi kwa mwongozo wa kumpokea Yesu.

Bwana akubariki.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NITAACHAJE DHAMBI?

MAFUNZO YA BIBLIA KWA WATOTO

UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?

Print this post

Kwanini mkono wa Musa uingie ukoma?

Swali: Kwanini MUNGU aliufanya mkono wa Musa kuwa na ukoma kama ishara kwa wana wa Israeli? (Kutoka 4:6).

Jibu: Turejee..

Kutoka 4:6 “Bwana akamwambia tena, Sasa tia mkono wako kifuani mwako. Akautia mkono wake kifuani mwake; naye alipoutoa, kumbe! Mkono wake ulikuwa una ukoma, umekuwa mweupe kama theluji.

7 Akasema, Tia mkono wako kifuani mwako tena. Akautia mkono wake kifuani mwake tena, na alipoutoa kifuani mwake, kumbe! Umerudia hali ya mwili wake.

8 Basi itakuwa, wasipokusadiki, wala kuisikiliza sauti ya ishara ya kwanza, wataisikiliza sauti ya ishara ya pili”.

Sababu kuu ya BWANA MUNGU, kuutia mkono wa Musa ukoma na kisha kuuponya ni kutoa ujumbe kwa wana wa Israeli kuwa yeye ni Mungu awaponyaye.. Kwa hivyo wana wa Israeli walipoiona ile ishara walitambua kuwa Mungu wao ni Mungu anayeponya na kuondoa maradhi, misiba, mateso na hata utumwa..

Jambo hilo tunalithibitisha mbele kidogo katika ile sura ya 15 alipowaambia jambo hilo pale alipoyaponya maji yaliyokuwa machungu..

Kutoka 15:22 “Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji.

23 Walipofika mahali palipoitwa Mara hawakupata kuyanywa yale maji ya Mara, kwa kuwa yalikuwa machungu; kwa ajili ya hayo jina lake likaitwa Mara.

24 Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema, Tunywe nini?

25 Naye akamlilia Bwana; Bwana akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na hukumu huko, akawaonja huko;

26 akawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, mimi sitatia juu yako maradhi yo yote niliyowatia Wamisri; KWA KUWA MIMI NDIMI BWANA NIKUPONYAYE.

26 kawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, MIMI SITATIA JUU YAKO MARADHI YO YOTE NILIYOWATIA WAMISRI; KWA KUWA MIMI NDIMI BWANA NIKUPONYAYE”.

Na hata sasa bado MUNGU wetu ana sifa hiyo hiyo, “YEYE NI MUNGU ATUPONYAYE”… Ikiwa tutasikiliza kwa bidii sauti yake na kufanya yale anayotuelekeza.. Magonjwa yote hayatakuwa sehemu yetu, mateso yote hayatakuwa sehemu yetu na kila aina ya mabaya ya ibilisi hayatatutawala.

Je umempokea YESU KRISTO kama Bwana na Mwokozi pekee wa maisha yako?

Kama bado unasubiri nini?.. mwamini leo uokolewe na kuponywa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

FIMBO YA HARUNI!

MAMBO SITA, AMBAYO MUNGU HUTUMIA KUONDOA UOVU NDANI YA MTU.

Kwanini Mungu alimchagua Musa, na si mtu mwingine?

NABII MUSA.

Print this post

MBONA MMESIMAMA HAPA MCHANA KUTWA BILA KAZI?

Mathayo 20:6

[6]Hata kama saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?

Bwana Yesu alizungumza mfano ambao unagusia kabisa uhalisia wa kiroho uliopo sasa katika kazi ya Mungu (Ushuhudiaji).

Mfano huo unahusu mtu mmoja aliyetoka asubuhi sana kuajiri wafanyakazi ili kwenda kulilima shamba lake ambalo lilihitaji watu wengi kulihudumia.

Hivyo akatoka alfajiri sana, kuwatafuta na kwa bahati nzuri akawakuta, akawapeleka shambani mwake, akatoka tena saa tatu, akawakuta wengine wamekaa bila kazi, akawatuma shambani, akaenda tena saa sita na saa tisa vivyo hivyo akafanya…Mpaka ilipofika saa kumi na moja akatoka na kuwakuta watu wengine wamesimama tu toka asubuhi mpaka jioni…hawafanyi chochote wapo “Idle”

akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi? 

Mathayo 20:1-7

[1]Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu.

[2]Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu.

[3]Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi;

[4]na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda.

[5]Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile.

[6]Hata kama saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?

[7]Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, enendeni nanyi katika shamba la mizabibu.

Embu jiulize swali moja.. Je! Unadhani watu hawa wa saa kumi na moja hawapo leo?

Kukaa bila kufanya kazi ya Mungu, wakati Kazi ipo kubwa kwa kisingizio kuwa hakuna wa kukuajiri ni ulegevu kiroho… yule Bwana hakuwa na muda wa kusikiliza sababu zao, kwamba waendelee kukaa na kumalizia tu siku kwasababu muda umeenda, bali aliwatuma haraka sana shambani.

Yafuatayo ni mambo yanayowafanya watu kukaa muda mrefu bila kuitenda kazi ya Mungu.

1) Hofu ya kutumika

Kusema mimi siwezi, Mimi bado mchanga kiroho, sijui biblia vizuri, Mimi bado mdogo kiumri, mimi siwezi Kuongea nina aibu, nina kigugumizi..sina fedha, sina elimu n.k…haya ndio mambo yanayowakawiisha watu wengi wasimtumikie Mungu..

Ndugu fahamu kuwa Mungu hategemei ukamilifu wetu, kutimiza kusudi lake kamilifu, bali hututumia katika hali zetu hizi hizi, hivyo usingojee siku fulani utakuwa mzoefu ndio umtumikie Mungu..haitafika, anzia na hali yako hiyo hiyo.(1Wakoritho1:26-29)

2) Kungojea muda fulani sahihi.

Kudhani Kuwa upo muda fulani maalumu utaitwa na Bwana rasmi umtumikie, hilo pia limewafanya wengi, kungoja muda mrefu na hatimaye kutoona mafanikio.. saa ya kutumika ni sasa..tayari Wote tulishaitwa tumtumikie yeye tangu siku tulipookoka..ukishaokoka umepewa na vibali vyote na mamlaka ya kumtumikia Bwana..usingoje utokewe na Yesu kama Paulo Dameski, Usingoje usikie sauti fulani ikikwambia nenda kawafundishe watu. Anza sasa na Bwana ataungana na wewe mbele ya safari.

3) Masumbufu ya maisha

Mizigo mingi ya kimaisha, utakula nini, utavaa nini, utaishije, linawapunguza watu kasi ya kufikiria kwamba wanahitaji kwanza kuyaandaa maisha yao yawe safi ndipo waamke kwenda kumuhubiri Kristo.

Ndicho walichokifanya wayahudi walipokuwa wanajenga hekalu la pili, ilifika wakati wakaacha ujenzi kila mmoja akaenda kwenye mambo yake, Kwasababu tu, ya kujiangalia hali zao.

Hagai 1:2-4

[2]BWANA wa majeshi asema hivi, ya kwamba, Watu hawa husema, Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujenga nyumba ya BWANA.

[3]Ndipo neno la BWANA lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema,

[4]Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika?

Usingoje ufanikiwe, uoe, uwe na maisha ndio sasa uanze kuifanya kazi ya Mungu, ukijitazama Sana, hutamtumikia Mungu ndugu.. fahamu kuwa wengi wanaokuletea wewe habari njema sio wenye mafanikio, lakini Bwana hawaachi.

4) Ulegevu.

Kupendelea mambo ya kirahisi rahisi, zaidi ya kujitoa..wakati mwingine kukataa kutaabika kwa ajili ya injili..kutaka ijiendeshe Yenyewe, bila kuwa mfuatiliaji na mwombaji, pia hukawiisha utendaji kazi wa injili.

Hivyo, ndugu muda ni mfupi sana, tupo katika saa la kumi na moja yetu, usihudhurie tu kanisani, kuwa sehemu ya utumishi kanisani, usisikilize / kusoma tu mahubiri, hubiri na kwa wengine unachojifunza, Shamba la Bwana linatuhitaji wote.

Ni wakati wa kuamka usingizini, bado hatujachelewa, ikiwa tutatimiza kusudi la Mungu vema, basi tutalipwa sawasawa tu na wale waliowahi..Hivyo amka sasa.. anza kushuhudia.

Shiriki injili kwa kushea na wengine habari hizi

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post