Jibu: Turejee..
Kumbukumbu 28:13 “Bwana atakufanya kuwa KICHWA, WALA SI MKIA; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakapoyasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wako, nikuagizayo hivi leo, kuyaangalia na kufanya;
14 msipokengeuka katika maneno niwaamuruyo leo kwa lo lote, kwenda mkono wa kuume wala wa kushoto, kwa kuifuata miungu mingine na kuitumikia”.
Unaweza kutafakari kwanini hajasema Utakuwa KICHWA na wala si MGUU!.. kwasababu kichwa kipo juu na miguu ipo chini, na ndio sehemu ya mwisho ya mwili wa mtu… lakini badala yake anasema Utakuwa “kichwa”na si ”mkia”. Je kuna sifa gani mbaya katika mkia?
Sasa sote tunajua kuwa mwanadamu hajaumbwa na Mkia, bali kichwa tu peke yake, hivyo bila shaka hapo biblia imejaribu kutumia umbile la wanyama badala ya la mtu kufunua hali ya mtu atakayemcha MUNGU na yule ambaye hatataka kumcha MUNGU, kwasababu wanyama ndio wenye kichwa na mkia na si mwanadamu.
Sasa kichwa cha mnyama yoyote ndicho kinachoongoza mwili wote, na ndio sehemu ya kwanza ya mwili wa mnyama. Lakini Mkia ni sehemu ya mwisho kabisa ya mwili wa mnyama, na sehemu hii imeungana na sehemu ya haja kubwa ya mnyama. Kwahiyo wakati kichwa kinapokea chakula fresh, mkia unapokea uchafu (kinyesi).
Ikiwa na maana kuwa watu wanaomcha MUNGU, watapokea vilivyo visafi na vya kwanza na vizuri, na wasiomcha MUNGU ni kinyume chake, watapokea vile vya mwisho na visivyo na heshima vilivyo haribika.
Pia watu wanaomcha MUNGU watakuwa wa kwanza, kulingana na sifa ya kichwa, lakini wasiomcha MUNGU watakuwa wa mwisho kama ilivyo nafasi ya mkia katika mwili wa mnyama, sasa hebu tafakari unakuwa wa mwisho na bado unapokea vilivyo vichafu (mfano wa vinyesi)..ni jambo baya sana..
Ni tahadhari kwetu tunaoishi, kwamba tuwekeze nguvu kubwa katika kumtafuta MUNGU ikiwa tutataka tuwe vichwa, lakini tusipotaka kufanya hivyo, maandiko yanasema tutakuwa mkia na maadui zetu MUNGU atawaweka juu yetu na sisi tutakuwa wa mwisho.
Kumbukumbu 28:43 “Mgeni aliye kati yako atazidi kupaa juu yako; nawe utazidi kushuka chini.
44 Yeye atakukopesha, wala wewe usimkopeshe; YEYE ATAKUWA NI KICHWA, WEWE UTAKUWA MKIA.
45 Na laana hizi zote zitakujilia juu yako, zitakuandama na kukupata, hata uangamizwe, kwa kuwa hukuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, kushika maagizo yake na amri zake alizokuagiza”
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.
AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.
NI SAHIHI KABISA, HUU SI WAKATI WA TINI!
Maana ya Mafarisayo Hupanua HIRIZI zao, na kuongeza MATAMVUA yao
Ndio Maandiko yanatuonyesha kuwa tutatambuana tukifika mbinguni. Ifahamike kuwa fahamu zetu au kumbukumbu zetu za hapa ulimwenguni hazitaondolewa kabisa, tufikapo mbinguni, kila pito tulipitialo, na kila jambo lililowekwa na Mungu sasa hapa duniani, lina sehemu kubwa ya fundisho la maisha yajayo. Hivyo maisha ya duniani yana thamani kama yalivyo tu maisha yatakayokuja. Ndio maana kabla ya kuingia kule ilitupaswa kwanza tupitie hapa.
Zipo sehemu kadha wa kadha katika maandiko zinatuthibitishia kuwa tutatambuana kule mbinguni.
Tunaona Bwana wetu Yesu Kristo alipofufuka na mwili mpya wa utukufu, aliweza kutambuliwa . Kwamfano siku ile ya kwanza ya juma Mariamu Magdalena, akiwa pale kaburini alimtambua Bwana Yesu alipozungumza naye.
Yohana 20: 16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu).
Halikadhalika wakati ule Bwana Yesu anawachukua mitume wake watatu Petro, Yohana na Yakobo na kuwapeleka juu ya mlima ule mrefu, na kuwabadilikia sura, kama tunavyosoma watu wawili walitokea ambao ni Musa na Eliya.
Mitume waliweza kuwatambua ijapokuwa hawakuwahi kuwaona uso kwa uso hapo kabla.
Mathayo 17:3 Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye.
1Wakorintho 15:42 Kadhalika na kiyama ya watu. Hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutokuharibika; 43 hupandwa katika aibu; hufufuliwa katika fahari; hupandwa katika udhaifu; hufufuliwa katika nguvu; 44 hupandwa mwili wa asili; hufufuliwa mwili wa roho. Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko
Mstari huo unatuonyesha kuwa hatutaondolewa uhalisia wetu Tutabakia kuwa sisi sisi., isipokuwa tutavikwa utukufu wa juu zaidi. Maana yake ni kuwa tutatambuana.
1Wathesalonike 4:16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.
17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana
hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.
Tutarejeshwa, na kuonana. Hivyo kwa mujibu wa vifungu hivyo katika ulimwengu ujao sote tutajuana na kufahamiana.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Sheria ni agizo la shuruti linalotolewa na mamlaka kuu…, na KANUNI ni mwongozo au utaratibu maalumu unaotolewa kuhusiana na utekelezaji wa sheria iliyowekwa au agizo lililotolewa..
Kwamfano katika biblia kulikuwa na Sheria ya “kuishika Pasaka” lakini ilikuwepo pia kanuni (ambayo ni mwongozo wa namna ya kuiadhimisha hiyo siku), kwamba ni lazima kwanza iwe siku ya 14 ya mwezi wa kwanza wa kalenda ya kiyahudi, na pia siku hiyo ni lazima achinjwe mwana kondoo na kumwoka motoni na aliwe pamoja na mboga zenye uchungu n.k (Soma Kutoka 12:1-12).
Sasa huo mwongozo wote wa jinsi ya kuiadhimisha hiyo siku ndio unaoitwa Kanuni, lakini sheria ni hiyo moja tu kwamba Waishike Pasaka..
Hesabu 9:14 “Na kama mgeni akiketi kati yenu ugenini, naye ataka kuishika Pasaka kwa Bwana; kama HIYO SHERIA YA PASAKA ILIVYO, na kama amri yake ilivyo, ndivyo atakavyofanya; MTAKUWA NA SHERIA MOJA, kwa huyo aliye mgeni, na kwa huyo aliyezaliwa katika nchi”.
Katika biblia kila Amri au sheria ilikuwa na Kanuni zake na hukumu zake.
Tunayo sheria na amri ya Kristo pia ambayo ni UPENDO, lakini huu upendo unao kanunini…ni lazima tuzitafutae kanuni za upendo na tuzijue.
Isaya 28:13 “Kwa maana ni amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo”.
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini tarehe ya pasaka inabadilika kila mwaka?
PASAKA NI NINI? NA JE TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA?
Nini tofauti kati ya kileo na divai?
FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.
Je! kuna mwanamke mwingine aliyempaka Bwana marhamu (manukato) zaidi ya Mariamu ndugu yake Lazaro?
Jibu: Neno Utakatifu linatokana na Neno “utakaso”.. kitu lilichotakasika kinaitwa “kitakatifu”.. na kitu kilichotakasika/takata maana yake hakina uchafu.
Kwahiyo utakatifu kwa tafsiri rahisi maana yake ni “kuwa safi, (kutokuwa na uchafu)”.. Mtu anaweza kuwa msafi (mtakatifu) mwilini na rohoni.
Sasa kikawaida kitu chochote kinapokuwa safi, huwa kinatoa Mng’ao unaopendeza.. sasa ule mng’ao unaotafsiri usafi wa kitu kile ndio unaoitwa UTUKUFU, kwamfano dhahabu inaposafishwa na kuwa safi huwa inatoa mng’ao mzuri wa kipekee, sasa ule mng’ao ndio utukufu wa ile dhahabu au kito, na vitu vingine vyote ni hivyo hivyo.
Hali kadhalika mtu aliyetakaswa dhambi zake kwa damu ya YESU, na yeye mwenyewe kujilinda na kujitenga na uchafu wote wa rohoni na mwilini, basi mtu huyo ni mtakatifu na anao utukufu, ambao ni NURU inayong’aa, ambayo shetani na mapepo yake hayawezi kustahimili mwako wake.
Lakini zaidi sana MUNGU wetu aliyetuumba ndiye mwenye utukufu MKUU, ambao huo unatokana UTAKATIFU alionao, uzidio viumbe vyake vyote.. Mng’ao wa utukufu wake hata malaika wanainama mbele zake na kujifunika kwa mbawa zao, na utukufu wake unang’aa mpaka duniani.
Isaya 6:1 “Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu.
2 Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka.
3 WAKAITANA, KILA MMOJA NA MWENZAKE, WAKISEMA, MTAKATIFU, MTAKATIFU, MTAKATIFU, NI BWANA WA MAJESHI; DUNIA YOTE IMEJAA UTUKUFU WAKE”.
Naam nasi tuliompokea YESU ni lazima tufanane naye, na hatuwezi kuwa na utukufu bila kuwa watakatifu, na hatuwezi kukosa utukufu tukiwa watakatifu, na kuwa mtakatifu duniani inawezekana..
Zaburi 16:3 “Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JE UMEUFIKIA ULE UTUKUFU HALISI WA MANA?
NYUMBANI MWA BABA YANGU MNA MAKAO MENGI.
Swali: Kuna tofauti gani kati ya Ahadi na Nadhiri, kwa mujibu wa Biblia?
Jibu: Ahadi ni Neno/tamko la hiari mtu analolitoa kwa mtu mwenzake, kwamba atalitenda katika wakati mfupi au mrefu ujao.
Kwamfano mtu anaweza kuahidi kuwa kesho atawasili katika hafla, na hiyo kesho kweli akafika kama alivyoahidi, hapo anakuwa ameitimiza ahadi yake, lakini asipowasili kama alivyoahidia anakuwa hajaitimiza ahadi, na ni dhambi ikiwa hakuwa na sababu za msingi za kuivunja ahadi yake.
Lakini katika upande wa Nadhiri, hii ni ahadi (yaani tamko ya hiari) mtu analolitoa kwa MUNGU, na si kwa mtu.
Kwamfano mtu anaweza kuahidi kuwa endapo akipona ugonjwa unaomsumbua atamtolea MUNGU sadaka ya shukrani, au endapo Mungu akimtendea jambo Fulani basi atamtolea MUNGU sadaka Fulani, hiyo inakuwa ni nadhiri.
Na mtu asipotimiza Nadhiri aliyomwekea MUNGU inakuwa ni dhambi..
Mhubiri 5:4 “Wewe ukimwekea Mungu nadhiri, usikawie kuiondoa; KWA KUWA YEYE HAWI RADHI NA WAPUMBAVU; BASI, UIONDOE HIYO ULIYOIWEKA NADHIRI.
5 Ni afadhali usiweke nadhiri, Kuliko kuiweka usiiondoe.
6 Usikiache kinywa chako kuukosesha mwili wako; wala usiseme mbele ya huyo malaika ya kwamba umepitiliwa; kwani Mungu akukasirikie sauti yako, na kuiharibu kazi ya mikono yako?”
Kwahiyo ni muhimu kuitimiza ahadi tunazozitoa na pia Nadhiri uliomwekea MUNGU.
Ikiwa kuna sababu zozote za msingi zilizojitokeza za kutotimiza ahadi basi ni vizuri kufanya mapatano na uliyemhadi mapema ili isigeuke kuwa uongo.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JE! USIPOTIMIZA NADHIRI ZAKO ZOTE KWA BWANA. HAWEZI KUKUSAMEHE?
Swali: Kuna utofauti gani uliopo kati ya Hasira ya MUNGU na Ghadhabu ya MUNGU?
Jibu: Kujua tofauti yake turejee mistari michache katika biblia..
Zaburi 6:1 “Bwana, usinikemee kwa HASIRA YAKO, Wala usinirudi kwa GHADHABU YAKO”.
“Hasira” ni hisia ya “kuchukizwa” inayompata mtu kutokana na tendo Fulani baya alilofanyiwa, au lililomtokea kinyume na matakwa yake. Hii ni hisia ya ndani ambayo inaweza kumfanya mtu apoteze hamasa, au hamu au shauku ya jambo Fulani.
Lakini “Ghadhabu” yenyewe inaenda mbali zaidi haiishii kumfanya mtu ajisikie tu vibaya na kujitenga bali inampeleka kuadhibu, au kulipiza kisasi.
Kwamfano kuna mtu aliyepigwa na mwenzie, akaishia kukasirika na kujitenga na Yule mtu, (Huyu anahesabika kuwa anazo hasira, kakasirika).. Lakini kuna mwingine anaweza kupigwa na mwenzake asiishie tu kukasirika lakini akarudisha mapigo, sasa huyu maana yake kaghadhibika, hivyo hasira yake imerudisha majibu hasi kwa aliyemtendea.
Sisi wanadamu tuna hasira lakini pia tunazo ghadhabu.. Ila Biblia imetuonya tusiizalie matunda hasira hata kuwa ghadhabu.. kwasababu hasira iliyozidi hata kutenda dhambi ndio ghadhabu..
Waefeso 4:26 “Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka;
27 wala msimpe Ibilisi nafasi”.
Kwanini Biblia imezuia tusiwe watu wa kuwa na hasira ya kupitiliza?… Ni kwasababu hisia zetu zina mapungufu na hukumu zetu si kamili..
Lakini hukumu za MUNGU ni kamili kwani MUNGU anayo hasira na pia Ghadhabu.. Lakini mpaka ghadhabu ya MUNGU imemwaga basi ni hakika kuwa tumestahili, lakini sisi wanadamu hatujapewa ruhusa ya kuwa na ghadhabu, kwasababu hukumu utakayompimia mwenzako MUNGU akikuangalia nawe pia unastahili hiyo hiyo kwa makosa yako mengine (Mathayo 7:1), Lakini yeye MUNGU akihuhukumu hana wa kumhukumu kwakuwa ni mkamilifu, hivyo hukumu zake ni kamili!.
Na pia ni kwa maarifa ya ziada ya kujua ni hasira ya namna gani ambayo tumepewa ruhusa ya kuwa nayo, fungua hapa>>MWE NA HASIRA, ILA MSITENDE DHAMBI.
Sasa Maandiko yanasema MUNGU aliyetuumba si Mwepesi wa hasira (maana yake hakasiriki haraka) lakini ni Mwingi wa hasira (maana yake hasira yake inafikia kiwango cha ghadhabu), cha kuadhibiwa na kujilipiza kisasi,.
Nahumu 1:2 “Bwana ni Mungu mwenye wivu, naye hujilipiza kisasi; Bwana hujilipiza kisasi, naye ni mwingi wa hasira; BWANA HUJILIPIZA KISASI JUU YA ADUI ZAKE, huwawekea adui zake akiba ya hasira.
3 BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, ana uweza mwingi, wala hatamhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; Bwana ana njia yake katika kisulisuli na tufani, na mawingu ni mavumbi ya miguu yake”.
Kilichowapata watu wa nyakati za Nuhu ni Ghadhabu ya MUNGU, kilichowapata watu wa nyakati za Sodoma na Ghomora ni Ghadhabu ya MUNGU!, Ndio maana hawakupona, na kitakachotokea kwa dunia ya wakati wa Mwisho ni Gadhabu ya MUNGU, soma (2Petro 3:6-7 na Ufunuo 16:1).
Na MUNGU anaweza kuimimina Ghadhabu yake kwa Mtu mmoja, na kwa watu wengi kwa pamoja au kwa dunia nzima.. Mtu anayefanya dhambi kwa makusudi yupo katika hatari ya kukumbana na ghadhabu ya MUNGU yeye kama yeye…
Wakolosai 3:5 “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;
6 KWA AJILI YA MAMBO HAYO HUJA GHADHABU YA MUNGU”.
Hivyo Biblia (Neno la MUNGU) linatufundisha kuiogopa Ghadhabu ya MUNGU kwa kutembea katika mapenzi yake na pia kujizuia sisi na ghadhabu kwasababu hasira ya mwanadamu haiitendei haki ya MUNGU.
Yakobo 1:19 “Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; WALA KUKASIRIKA;
20 KWA MAANA HASIRA YA MWANADAMU HAIITENDI HAKI YA MUNGU.
21 Kwa hiyo wekeeni mbali uchafu wote na ubaya uzidio, na kupokea kwa upole neno lile lililopandwa ndani, liwezalo kuziokoa roho zenu”.
Mithali 15:1 “Jawabu la upole hugeuza HASIRA; Bali neno liumizalo huchochea GHADHABU”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.
KIKOMBE CHA GHADHABU YA MUNGU KINAJAA.
NIMEAZIMIA KUWAKUSANYA MATAIFA. NIPATE KUWAMWAGIA GHADHABU YANGU
Biblia inamaana gani kusema ‘maana Mungu wetu ni moto ulao’ (Waebrania 12:29)
Katika agano la kale dhambi ilitokea na kuhesabiwa katika maeneo mbalimbali.
Kwamfano
> Kulikuwa na makosa ya jamii nzima. Yaani taifa zima kuasi. (Kutoka 32,)
> Makosa ya mtu binafsi. Mfano kutenda uzinzi, Wizi, uuaji n.k.
> Makosa ya kuwatendea vibaya wanyonge: Mfano maskini, wageni, mayatima na wajane (Amosi 5:11-12),
> Makosa ya kukaidi sherehe za kidini (Walawi 11-15),
> Makosa ya kuvunja maagano (Yeremia 17:21-23),
> Makosa ya kuabudu miungu mingine (sanamu).
Lakini pia kulikuwa na aina nyingine mbili za makosa..
> Aina ya kwanza ni makosa ya kukusudia
> Aina pili ni yale ya kutokusudia.
Ikiwa mtu alitenda dhambi kwa kutojua, alihesabika kuwa ni dhambi, hivyo alilazimika atoe sadaka ya dhambi. Lakini kama alitenda dhambi ya makusudi kinyume na mwenzake, ili kuondoa kosa Ilipasa atoe sadaka ya hatia.
Aina ya sadaka hizi zinaelezwa kwa urefu kwenye kitabu cha Walawi 4:1 – 5:13
Dhambi za kutokusudia Mfano wake ilikuwa ni kama kuvunja amri bila kujua au kutojua Sheria ya vitu safi au najisi ilivyo. Hivyo mtu alijikuta tu anatenda kwa kukosa ufahamu.
Walawi 4:1-3
[1]BWANA akanena na Musa, na kumwambia,
[2]Haya, nena na wana wa Israeli, uwaambie, Kama mtu ye yote akifanya dhambi pasipo kukusudia, katika neno lo lote ambalo BWANA amelizuilia lisifanywe, na kutenda neno lo lote la maneno hayo;
[3]kama kuhani aliyetiwa mafuta akifanya dhambi, hata analeta hatia juu ya watu; ndipo na atoe kwa ajili ya dhambi yake aliyoifanya, na kumsongeza kwa BWANA ng’ombe mume mchanga mkamilifu, kuwa ni sadaka ya dhambi.
Dhambi za kukusudia ni zote ambazo zilitendwa kinyume na mtu mwingine au mambo matukufu mfano wa hizi ni kama kuiba, kusema uongo, viapo Vya uongo, hivyo iliambatana pia na kutoa fidia ya vitu hivyo.
Sio tu kusamehewa bali pia kuweka mambo sawasawa kwa kulipia fidia.
Mfano wa tendo hili, tunaona kwa Zakayo, alipofikiwa na wokovu, alitubu kwa kurejesha mara nne ya vyote alivyodhulumu. (Luka 19:8) huo ni mfano wa sadaka ya hatia.
Katika agano jipya dhambi Zote Za kukusudia na kutokusudia na nyingine zote zinaondolewa na sadaka moja tu ya daima nayo ni DAMU YA YESU (Waebr 9:26, Isaya 53:10, 1Petro 2:24). Hiyo tu ndio inafuta hatia zote.
Lakini pamoja na hayo, sadaka hizi hutukumbusha pia kila tuombapo rehema, (kwa unajisi tunaojitia kila siku), hatuna budi kuomba sio tu kwa dhambi tuzijuazo bali pia kwa zile tusizozijua.
Kwasasa dhambi tusizokusudia ni kama vile kumkwaza mwenzako bila kufahamu, Kutowaombea wengine(2Samweli 12:23), kuwaza vibaya, kutotumiza nadhiri zetu, au wajibu wetu N.k.
Bwana akubariki.
Je umesamehewa na kuondolewa dhambi zako? Kama ni la! basi wakati ndio sasa, unapomgeukia Bwana Yesu, anakuondolea kumbukumbu lote la makosa. Hivyo fungua hapa kwa msaada huo wa kumpokea yeye >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ndio kipi? (Matendo 21:25).
Nini maana ya dhabihu na matoleo hukutaka? (Waebrania 10:5).
Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?
Luka 19:1 “Naye alipoingia Yeriko alipita katikati yake.
2 Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri.
3 Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo.
4 Akatangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu apate kumwona, kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile.
5 Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, SHUKA UPESI, KWA KUWA LEO IMENIPASA KUSHINDA NYUMBANI MWAKO.
6 Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha”.
YESU hawezi kuingia nyumbani kwako kama “hutashuka kwenye Mkuyu”..
Mkuyu ni kitu chochote kijiinuacho juu ya YESU,…. Kiburi cha mali ni mkuyu,… kiburi cha cheo ni mkuyu, kiburi cha uzuri ni Mkuyu n.k.. Mtu anavyovitumia hivi ili kumwona Bwana YESU au kumtumikia, Kristo yeye anaenda kinyume navyo..
Zakayo asingeweza kuzungumza na Bwana akiwa juu ya mkuyu..ilimpasa ashuke upesi… Sauti ile ilikuwa na mamlaka, ilipenya katika moyo wa Zakayo na kumfanya ashuke si tu chini ya Mkuyu, bali hata kiburi chake chote, kwani alikuwa ni mtu mkubwa kifedha…
Alipokubali tu kushuka na kiburi chake cha mali nacho kikashuka, kiburi chake cha cheo kikashuka akawa mtu mwingine, mnyenyekevu na YESU akaingia nyumbani mwake..
Nusu ya mali yake aliwapa maskini na wote aliowadhulumu aliwarudishia mara nne.
Luka 19:6 “Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha.
7 Hata watu walipoona, walinung’unika wote, wakisema, Ameingia kukaa kwa mtu mwenye dhambi.
8 Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang’anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.
9 Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu.
10 Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea”.
Na wewe leo, shuka chini ya Mkuyu.. kiburi cha Elimu kinaweza kuwa kizuizi cha Kristo kutembea na wewe, kiburi cha pesa kinaweza kuwa kikwazo cha YESU kuingia kwako, kiburi cha cheo na uzuri ni hivyo hivyo, lakini unyenyekevu unaleta Neema.
Yakobo 4:6 “Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
ALIYOKUTANA NAYO YESU, YERIKO.
LEO WOKOVU UMEFIKA NYUMBANI HUMU
Zekaria 10:1 “Mwombeni Bwana mvua wakati wa masika, naam, Bwana afanyaye umeme, naye atawapa manyunyu ya mvua, kila mtu atapewa nyasi kondeni”.
Umewahi kujiuliza kwanini hapo maandiko yanasema “Mwombeni Bwana mvua WAKATI WA MASIKA” na si wakati mwingine wowote kama kiangazi?..
Ni kwasababu msimu wa masika ni msimu wa mvua, hivyo inapotokea hakuna mvua si jambo la kawaida, kwahiyo tukiomba mvua msimu huo ni hoja yenye nguvu, lakini tunapoomba mvua msimu wa kiangazi zinakuwa si hoja zenye nguvu!.. Ndicho maandiko yanachokimaanisha hapo.
Maombi ya kuomba kwa wakati ni mazuri na yana majibu ya haraka kuliko yale ya kuomba nje ya msimu/majira.
Unaomba mume/mke na bado ni mwanafunzi, unaomba mali na bado unasoma, unaomba umtimikie MUNGU na bado hujaokoka!, maombi ya namna hiyo ni nadra sana kujibiwa!.. ni wachache sana wanaojibiwa hayo maombi!!.. sio kwamba ni maombi mabaya au vinavyoombwa ni vitu vibaya!. La! Ni vizuri lakini vinaombwa nje ya majira yake.
Hapo maandiko yanasema “Mwombeni Bwana Mvua wakati wa Masika”.. Maana yake ni lazima ujue uhusiano wa kile unachomwomba MUNGU na majira uliyopo. Kama kitu bado majira yake usitumie nguvu kubwa kuomba, shughulika na vile ambavyo sasa ndio majira yake.
Kama wewe ni mwanafunzi usiombe MUNGU akupe hela kwa sasa….badala yake mwombe akufanikishe katika masomo ufaulu, uwe kichwa, hayo mengine bado msimu wake!..
Kama wewe ni binti/kijana na bado upo chini ya wazazi unawategemea, usiombe MUNGU akuonyeshe mume wako/mke wako, badala yake mwombe ulinzi juu ya tabia yako mpaka utakapofika wakati wa wewe kujitegemea na kufikiri kuingia katika ndoa.
Lakini kama umeshaingia katika msimu basi ni haki yako kumwomba BWANA!, Na unapomwomba Bwana jambo sahihi katika msimu sahihi, MUNGU ni mwenye huruma atakupa unachokihitaji haraka sana, na hata kikichelewa atakupa sababu kwanini kinachelewa, na sababu za BWANA zote ni Bora na wala si za kumwumiza Mtu, kwasababu yeye kamwe hawezi kuruhusu tujaribiwe kupita tuwezavyo.
Vumilia tu ukiona umeshaingia kwenye msimu na bado matokeo hujayaona!, yatakuja tu!..usikate tama a wala kuishiwa nguvu, mwamini MUNGU na mngojee, naye atakupa nguvu mpya kila siku.
Jambo la mwisho la kujua ni kwamba wokovu pia unao msimu wake, na msimu wa Wokovu ndio sasa..
Huu ndio wakati wa MUNGU kutupa wokovu na kutusikia maombi yetu, kwani utafika wakati ambapo hakutakuwa tena na wokovu wala maombi kusikiwa, ndivyo maandiko yanavyosema..
2Wakorintho 6:1 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.
2 (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia; tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)”
Sasa kama siku ya Wokovu ndio sasa, unasubiri nini usimpokee YESU?.. je unadhani itakuwa hivi siku zote?.. utafika wakati mlango wa Neema utafungwa, na hakutakuwa tena na msamaha wa dhambi wala ondoleo la dhambi, mti ulipoangukia huko huko utalala (Mhubiri 11:3).
Sasa unayadharau mahubiri na mafundisho ya uzima, unayoyapokea kila mahali yanayokuonya kuhusu dhambi, je unadhani hali itakuwa hivyo kila siku?…Majira yatabadilika ndugu, utafika wakati kutakuwa hakuna kuponywa tena mwili na roho!.
2Nyakati 36:15 “Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake;
16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, HATA ILIPOZIDI GHADHABU YA BWANA JUU YA WATU WAKE, HATA KUSIWE NA KUPONYA”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nzige, Parare, madumadu na tunutu ni wadudu gani? (Yoeli 2:25)?
MAASI KUONGEZEKA NI ISHARA YA NINI?.
JIFUNZE JAMBO KWENYE UKOO WA YESU, UWE NA AMANI
Kwanini madhabahu zilitengenezwa kwa mawe yasiyochongwa?
Kwanini Mungu auweke Mti wa Mema na Mabaya katikati ya bustani?
Swali: Kati ya Simoni Petro na Mariamu Magdalene ni yupi aliyekuwa wa kwanza kutokewa na Bwana YESU baada ya kufufuka kwake?, kwa maana katika Luka 24:34 tunasoma kuwa ni Simoni ndiye wa kwanza kutokewa na Bwana, lakini tukirudi katika Marko 16:9 tunaona ni Mariamu Magdalene je hii imekaaje?.
Jibu: Turee mistari hiyo..
Luka 24:33 “Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao,
34 wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, NAYE AMEMTOKEA SIMONI”.
Hapa tunaona anatajwa Simoni, lakini turejee Marko 16:9..
Marko 16:9 “Naye alipofufuka alfajiri siku ya kwanza ya juma, ALIMTOKEA KWANZA MARIAMU MAGDALENE, ambaye kwamba alimtoa pepo saba.
10 Huyo akashika njia akawapasha habari wale waliokuwa pamoja naye, nao wakali wanaomboleza na kulia”.
Hapa tunasoma ni Mariamu Magdalena ndiye aliyetokewa kwanza, sasa swali ni yupi aliye sahihi au biblia inajichanganya?..
Jibu ni La! Biblia haijichanganyi na wala haina kasoro yoyote… Sasa kama ni hivyo ni nani aliyetokewa wa kwanza?
Jibu, aliyetokewa wa kwanza na Bwana YESU alikuwa ni MARIAMU MAGDALENE, kama maandiko yanavyoonyesha hapo juu (Marko 16:9).. huyu ndiye aliyekuwa wa kwanza kumwona Bwana kwani baada tu ya kukuta jiwe limeviringishwa mbali na kaburi aliondoka na kwenda kuwafuata akina Petro kuwapasha yaliyojiri, na Petro pamoja na Yohana walipokwenda kaburini kuhakiki hizo taarifa za Magdalene, walikuta tu vitambaa vya sanda, na walipoondoka ndipo Bwana YESU akamtokea Mariamu Magdalene kama mtu wa kwanza (na saa hiyo akina Petro wameshaondoka).
Yohana 20:1 “Hata siku ya kwanza ya juma Mariamu Magdalene alikwenda kaburini alfajiri, kungali giza bado; akaliona lile jiwe limeondolewa kaburini.
2 Basi akaenda mbio, akafika kwa Simoni Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, Wamemwondoa Bwana kaburini, wala hatujui walikomweka.
3 Basi Petro akatoka, na yule mwanafunzi mwingine, wakashika njia kwenda kaburini.
4 Wakaenda mbio wote wawili; na yule mwanafunzi mwingine akaenda mbio upesi kuliko Petro, akawa wa kwanza kufika kaburini.
5 Akainama na kuchungulia, akaona vitambaa vya sanda vimelala; lakini hakuingia.
6 Basi akaja na Simoni Petro, akaingia ndani ya kaburi; akavitazama vitambaa vilivyolala,
7 na ile leso iliyokuwako kichwani pake; haikulala pamoja na vitambaa, bali imezongwa-zongwa mbali mahali pa peke yake.
8 Basi ndipo alipoingia naye yule mwanafunzi mwingine aliyekuwa wa kwanza wa kufika kaburini, akaona na kuamini.
9 Kwa maana hawajalifahamu bado andiko, ya kwamba imempasa kufufuka.
10 Basi wale wanafunzi wakaenda zao tena nyumbani kwao.
11 Lakini Mariamu alikuwa akisimama karibu na kaburi, nje yake, analia. Basi akilia hivi, aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi.
12 Akaona malaika wawili, wenye mavazi meupe, wameketi, mmoja kichwani na mmoja miguuni, hapo ulipolazwa mwili wake Yesu.
13 Nao wakamwambia, Mama, unalilia nini? Akawaambia, Kwa sababu wamemwondoa Bwana wangu, wala mimi sijui walikomweka.
14 Naye akiisha kusema hayo, akageuka nyuma, akamwona Yesu amesimama, asijue ya kuwa ni Yesu.
15 Yesu akamwambia, Mama, unalilia nini? Unamtafuta nani? Naye, huku akidhania ya kuwa ni mtunza bustani, akamwambia, Bwana, ikiwa umemchukua wewe, uniambie ulipomweka, nami nitamwondoa.
16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu)”.
Hivyo baada ya kumtokea Mariamu Magdalena ndipo akamtokea Simoni Petro, katika tukio ambalo halijarekodiwa katika Biblia.
Kwahiyo Simoni Petro alikuwa ni Mtume wa kwanza kutokewa na Bwana YESU lakini si mtu wa kwanza, aliyekuwa wa kwanza ni Mariamu Magdalena na Simoni Petro anasimama kuwa wa kwanza kati ya Mitume wa Bwana.
Mtume Paulo analiweka hilo vizuri zaidi..
1Wakorintho 15:4 “na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko;
5 na ya kuwa ALIMTOKEA KEFA; tena na wale Thenashara;
6 baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano pamoja; katika hao wengi wanaishi hata sasa, ila baadhi yao wamelala;
7 baadaye akamtokea Yakobo; tena na mitume wote;
8 na mwisho wa watu wote, alinitokea mimi, kama ni mtu aliyezaliwa si kwa wakati wake”.
Je umempokea YESU?.. Unao uhakika wa kwenda naye mawinguni atakaporudi?… fahamu kuwa tunaishi majira ya siku za mwisho, siku yoyote parapanda ya mwisho inalia na wafu waliokufa katika Kristo watafufuliwa kuungana na walio hai katika Kristo na kunyakuliwa juu, je utakuwa wapi siku hiyo?, ikiwa leo habari ya msalaba kwako ni upuuzi mtupu!.
Neema ya Bwana YESU itusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mariamu Magdalene ni nani. Na hilo jina amelitolea wapi?
MAMBO YA KUJIFUNZA KWA KLOPA NA MKE WAKE!
Nyongeza ya majina ya watu katika biblia