Category Archive Mafundisho

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wathesalonike wa kwanza.

Kitabu hichi kama kinavyojitambulisha katika mwanzo wake  ‘Waraka wa kwanza wa Paulo mtume kwa Wathesalonike’.

Paulo ndiye mwandishi wa waraka huu. Aliuandika akiwa Korintho. Tumelijua hilo  kufuatana na ujio wa Timotheo kutoka Makedonia na kumpa ripoti nzuri ya maendeleo yao ya kiroho,  kuanzia eneo la imani, upendo na tumaini, ambazo tunazisoma katika kitabu cha Matendo ya mitume sura ya 18.

Kwasababu ya ugumu wa kuwafikia uliochangiwa na shetani,  Akasukumwa kuandika nyaraka hizi mbili kwa watakatifu hawa, kuwajenga katika maeneo kadha wa kadha,  ambazo zilipishana kwa miezi kadhaa tu.

Kitabu hichi kina sura tano (5)

Maudhui kuu ya waraka huu ni matatu(3)

  1. kwanza ni kuwahimiza watakatifu kudumu katika imani  husasani katika nyakati za dhiki.
  2. Pili kuwapa mwongozo wa mwenendo sahihi upasao ndani ya imani.
  3. Tatu, kuwapa majibu ya maswali yahusuyo ujio wa pili wa Yesu Kristo na kiyama ya wafu ambayo walikuwa nayo.

Tuyaangalie hayo maeneo matatu kwa ufupisho;

1) Kuhusu kudumu katika Imani.

Paulo anaanza kwa kuwashuhudia kwa maneno mengi dhiki alizozipata katika kuieneza injili kwao, na jinsi alivyoweza kustahimili, Na kwamba wao pia wanapopitia dhiki za namna mbalimbali kutoka kwa watu wa taifa lao, wasivunjike moyo na kuiacha imani. Wajue kuwa dhiki pia wamewekewa watakatifu.

1 Wathesalonike 2:14

[14]Maana ninyi, ndugu, mlikuwa wafuasi wa makanisa ya Mungu yaliyo katika Uyahudi, katika Kristo Yesu; kwa kuwa mlipata mateso yale yale kwa watu wa taifa lenu wenyewe, waliyoyapata na hao kwa Wayahudi;

[15]ambao walimwua Bwana Yesu, na hao manabii, na kutuudhi sisi; wala hawampendezi Mungu, wala hawapatani na watu wo wote;

1 Wathesalonike 3:3

[3]mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo.

2) Sehemu ya pili ambayo inahusu mwenendo upasayo wa imani.

Paulo anagusia maeneo mengi kuanzia upendo hadi utakatifu kwamba wana wajibu wa kuongezeka katika hivyo ili wasionekane katika lawama katika siku ile ya kuja Bwana wetu Yesu Kristo kutoka mbinguni.

1 Wathesalonike 3:12-13

[12]Bwana na awaongeze na kuwazidisha katika upendo, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu;

[13]apate kuifanya imara mioyo yenu iwe bila lawama katika utakatifu mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote.

> Anagusia pia katika eneo la kudhibiti miili yetu katika utakatifu na heshima na sio katika tamaa mbaya(4:1-5),

> Halikadhalika wakristo kuonyesha mwenendo wa adabu kwa walio nje, kwa kutenda shughuli zetu wenyewe ili tusiwe na uhitaji wa vitu vyao (4:11-12)

> Pia kama watakatifu ni mwiko kulipana baya kwa baya (5:15),

> Tunapaswa sikuzote tudumu katika kuomba, kufurahi, kushukuru kwa kila jambo, tusimzimishe Roho, tusipuuzie unabii, tujitenge na ubaya wa kila namna.(5:16-23)

> Lakini Paulo anahimiza mwenendo wetu unapaswa uende mpaka kwa wale wanaotusimamia na kutuchunga kwamba tuwastahi.

1 Wathesalonike 5:12-13

[12]Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni;

[13]mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi.

> Na katika yote ni wajibu wetu sote kufarijiana na kuonyana na kuvumiliana na kutiana nguvu(5:14-15)

3) Sehemu ya tatu ambayo anatoa majibu ya maswali yahusuyo ujio wa pili wa Kristo, na kiyama ya wafu

Paulo anawafiriji kwa kuwaambia wafu waliolala katika Kristo, siku ya mwisho wataamshwa wote..wasidhani kuwa hawatawaona wapendwa wao waliotangulia.

1 Wathesalonike 4:13-16

[13]Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.

[14]Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.

[15]Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.

[16]Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

Sambamba na hilo, anawafumbua macho juu ya nyakati na majira ya kurudi kwa Yesu kwamba hakutakuwa na taarifa zozote au viashiria vyovyote kwa watu wa dunia. Bali itawajilia kwa ghafla tena katika nyakati ambazo wanasema kuna amani na shwari.

Hivyo anawatahadharisha watakatifu nao kuwa macho wakati wote.

1 Wathesalonike 5:1-11

[1]Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

[2]Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

[3]Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.

[4]Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.

[5]Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.

[6]Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.

[7]Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku.

[8]Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.

[9]Kwa kuwa Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo;

[10]ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, kwamba twakesha au kwamba twalala.

[11]Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya.

Hivyo kwa ufupi ni kuwa waraka huu. Unawataka wakristo kuthibitika katika imani, haijalishi ni changamoto gani za kimaisha au ugumu gani watakutana nao kwa wapinga-kristo, Wanapaswa waendelee kusimama hivyo hivyo  mpaka mwisho katika Kristo Yesu.

Lakini pia wajue  Bwana anarudi, na atakuja ghafla, Hivyo yawapasa  wawe watu wa mchana sikuzote wasilale usingizi kwa kuhakikisha wanaishi maisha ya utakatifu, na adabu, ili atakaporudi Bwana wasiwe na lawama yoyote.

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Kama ni la, fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya wokovu. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha Wafilipi.

VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Yakobo.

Print this post

CHAGUA UTAKATIFU MWAKA HUU.

Zaburi 93:5 “Shuhuda zako ni amini sana; UTAKATIFU NDIO UFAAO NYUMBA YAKO, Ee BWANA, milele na milele”.

Ni kitu gani umekichagua kwenye nyumba ya MUNGU katika mwaka huu?..Je nafasi fulani, au cheo, au umaarufu, au nini?.

Kumbuka Nyumba ya MUNGU ni zaidi ya jengo la Ibada, bali pia Miili yetu ni nyumba ya MUNGU.

Yohana 2:20 “Basi Wayahudi wakasema, Hekalu hili lilijengwa katika muda wa miaka arobaini na sita, nawe utalisimamisha katika siku tatu?

21 Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake”.

1 Wakorintho 3:16 “Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?”

Soma pia 1Wakorintho 6:19, utazidi kuelewa vyema.

Sasa kama Miili yetu ni HEKALU LA MUNGU, yaani NYUMBA YA MUNGU ni kipi umekiamua juu ya Mwili wako katika mwaka huu mpya?, kwamaana Neno linasema Utakatifu ndio ufaao nyumba ya MUNGU, na tena haufai siku moja tu, bali milele…..

Zaburi 93:5 “Shuhuda zako ni amini sana; UTAKATIFU NDIO UFAAO NYUMBA YAKO, Ee BWANA, milele na milele”.

Chagua utakatifu wa mwilini na rohoni huu Mwaka, usiishi tena kwa kuuchafua mwili wako kama ilivyouchafua mwaka jana, au miaka iliyopita, anza mwaka na mambo mapya.

Anza kujenga ushuhuda mpya, badilika kimwonekano, watu watakapokutazama waone waseme hakika yule ni mkristo, na watakapokuuliza usema “UMECHAGUA UTAKATIFU KWA MAANA NDIO UFAAO NYUMBA YA MUNGU”.

Sema mwaka huu sio mwaka wa Kushindana na mtu kimavazi ndani ya nyumba ya MUNGU, sema mwaka huu ni wakati wa kuipamba nyumba ya MUNGU kwa utakatifu.

Sema mwaka huu ni mwaka wa kuhubiri UTAKATIFU kila mahali, kwamaana pasipo huo hakuna mtu atakayemwona Mungu (Waebrania 12:14).

2 Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”.

Hili ni neno fupi la mwaka kwako.

Bwana atusaidie sana..

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha Wafilipi.

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha wafilipi

Kama pale mwanzo kinavyojitambulisha “Waraka wa Paulo mtume kwa wafilipi”.

Paulo ndiye mwandishi wa kitabu hiki. Ni moja ya nyaraka ambazo Paulo aliziandika akiwa kama mfungwa, aidha kule Rumi.

Maudhui makuu ya waraka huu mfupi wenye sura nne(4) yalikuwa ni kuwatia moyo watakatifu na kuwahimiza waiendeleze furaha ya Mungu ndani yao,bila kukwamishwa na dhiki za aina yoyote, lakini pia sehemu ya pili ni kuwataka wapige hatua katika mwenendo wao ndani ya injili waliyoipokea.

Tukianza na hiyo sehemu ya kwanza:

1) Furaha ndani ya Kristo

Paulo anahimiza watakatifu kufurahi katika dhiki zote, ikizingatiwa kuwa Kanisa hili lilishuhudia vifungo na mapigo mengi ya Paulo. Kama tunavyosoma kwenye Matendo 16:16-40, Kule ambapo Paulo na Sila walipigwa sana na kutupwa gerezani, biblia inatuambia kulikuwa ni huku Filipi. Lakini hata katika waraka huu bado anashuhudia kuwa dhiki zake, zimekuwa wazi kwa maaskari, na watu wote wa huko (1:12-13).

Hivyo Paulo alijua watu wa Filipi huwenda wakawa na huzuni nyingi juu yake, au juu ya injili, kutokana na dhiki nyingi walizoziona kupitia yeye.

Lakini hapa anawaeleza kuwa yeye anafuraha sikuzote katika Kristo.

> Anaendelea kueleza furaha yake haiathiriwi na watu wanaomzushia fitna ili apitie mateso, maadamu anayeathirika ni yeye si Kristo. Basi bado anafurahi..(1:17-18)

> Anasema hata akihukumiwa kifo kwa ajili ya watakatifu, bado furaha yake itazidi zaidi wala haiwezi kuathiriwa..

Wafilipi 2:17-18

[17]Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote.

[18]Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami.

Hivyo anawahimiza pia na wafilipi wafurahi kama yeye, wala wasione huzuni kwasababu ya dhiki hizi, kwasababu tumewekewa kuwa sehemu yetu katika ushuhuda wa injili.

Wafilipi 1:29

[29]Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;

Hizi ni sehemu nyingine kadha wa kadha Paulo akihimiza jambo hilo hilo,

Wafilipi 3:1

[1]Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana.

Wafilipi 4:4

[4]Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.

Sehemu ya Pili:

2) Mwenendo upasao injili

Katika sehemu ya pili Paulo anahimiza watakatifu kuwa na mwenendo unaipasa injili waliyopokea. Na hiyo ni ili wasiwe na ila na lawama,na udanganyifu. Kuonyesha kuwa injili, inayo na taratibu zake..Sio kuamini tu na kusema nimeokoka…bali pia kutii agizo lake.

Wafilipi 1:27

[27]Lakini mwenendo wenu na uwe kama inavyoipasa Injili ya Kristo, ili, nikija na kuwaona ninyi, au nisipokuwapo, niyasikie mambo yenu, kama mnasimama imara katika roho moja, kwa moyo mmoja mkiishindania imani ya Injili;

Anaendelea kusema watakatifu wana wajibu wa kunia mamoja, kutenda mambo yote bila majivuno,wala manung’uniko, wala mashindano, wanapaswa kutenda yote bila ubinafsi bali na ya wengine..

Anasisitiza watakatifu wanapaswa wawe wanyenyekevu, wenye nia ya Kristo..ambaye yeye hapo mwanzo alikuwa kama Mungu lakini alijishusha kwa kukubali kuachia nafasi yake, akawa kama mtumwa, akajinyenyekeza mpaka mauti ya msalaba,lakini Mungu akamkweza zaidi ya vitu vyote..Na sisi tulioipokea injili tunapaswa tuwe na nia hiyo hiyo ya unyenyekevu.(2:1-16)

Anasisitiza zaidi Wakristo wanapaswa wawe wapole, pia wawe waombaji na wenye shukrani.(4:5)

Halikadhalika ni wajibu wetu sote kuutumiza wokovu tulioupokea kwa kuogopa na kutetemeka, kwasababu ndiye Mungu atendaye kazi ndani yetu.(2:12-13)

Pamoja na hayo Watakatifu wana wajibu pia wa kuyahakiki mambo yote yaliyo mazuri na kuyaiga, (2:1-2)

Wafilipi 4:8

[8]Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.

Lakini pia anawatahadharisha kujiepusha na wahubiri wa uongo akianzana na wayahudi (watu wa tohara), ambao wanahubiri wokovu kwa njia ya torati zaidi ya ile tuipatayo ndani ya Kristo Yesu kwa njia ya imani. (3:1–16,)

Pamoja watumishi ambao fundisho lao ni la mambo ya duniani tu, na sio yale ya kumwelekeza mtu mbinguni (3:17-21).

Mwisho, Paulo anatoa salamu zake, na shukrani kwa huduma ya utoaji kanisa hilo lililomfanyia, na linaloendelea kumfanyia.

Hivyo kwa hitimisho, waraka huu maudhui kuu ni kuwafariji watakatifu wafurahi katika mambo yote, tukizingatia tunda la Roho ni furaha. Yesu alisema tufurahi na kushangalia pale tunapoudhiwa, kwa ajili ya jina lake. Hivyo, hakuna eneo lolote furaha ya Mungu ndani yetu ,inastahili kukatishwa. Tupitiapo magonjwa kama Epafrodito(2:25-30), shida, njaa, tumefundishwa kuyaweza yote ndani ya Kristo(4:12-3). Hivyo furaha yetu haiwezi kuathiriwa..Ilinde furaha yako.

Lakini anahimiza mwenendo upasao injili. Kwamba huo utaweza kufanikiwa pale tunapokubali kuwa na nia kama ile ya Kristo, ya unyenyekevu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Watu wa nyumbani mwa Kaisari ni watu gani? (Wafilipi 4:22).

Epafrodito ni nani kwenye biblia?

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakolosai

Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.

Rudi Nyumbani

Print this post

Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.

Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.

Kama kitabu kinavyojitambulisha “Waraka wa Paulo Mtume kwa Waefeso”. Paulo ndiye aliyeuandika waraka huu.

Aliuandika akiwa kama mfungwa kule Rumi.

Waraka huu una sura sita(6), ambazo tunaweza kuzigawanya katika makundi mama mawili.

1) kundi la kwanza ni Sura ya 1-3,

Sura hizi zinaeleza asili ya Imani yetu iliyo katika Kristo Yesu jinsi ilivyo ya kipekee kwa nguvu na mamlaka, na ubora, na uweza na ukuu, na utajiri, na utukufu usiopimika, kwa akili za kibinadamu.(1:20-23).

2) Lakini kundi la pili ni Sura 4-6

Inaeleza juu ya mwenendo wetu, jinsi unavyopaswa uwe katika imani tuliyoipokea. Kwasababu ni vitu vinavyokwenda sambamba, haviwezi kutenganishwa, katika fundisho la ukristo.

Kwa ufupi; Katika Kundi la kwanza Yafuatayo ni mambo mama ambayo mwandishi ameyazungumzia juu ya mambo tunayoyapata ndani ya mwokozi wetu Yesu Kristo.

  1. Katika yeye tumebarikiwa katika baraka zote za rohoni (1:3). Akiwa na maana hakuna laana yoyote inayotukalia pindi tu tunapomwamini.
  2. Katika Kristo tunao ukombozi wetu ambao ni masamaha ya dhambi (1:7). Akiwa na maana dhambi zetu zote zimefutwa, wala kumbukumbu lake halipo.
  3. Katika yeye kwa njia ya masalaba wake kile kiambaza cha kati kimeondolewa, hivyo hakuna tofauti tena kati ya malaika walio mbinguni na sisi tuliopo duniani, mbele za Mungu (1:9-10), lakini si vya mbinguni na duniani tu, bali pia tofauti iliyokuwepo kati ya sisi na wayahudi imeondolewa kwa msalaba wake (3:5-11). Wote tunaitwa watoto wa Mungu (3:14)
  4. Katika Kristo tufahamu kuwa tulishachaguliwa kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, hivyo tutambue si suala lililojitokeza tu ghafla, au kwa bahati (1:4), bali Mungu alituona tangu zamani.
  5. Katika Kristo tumepewa hakikisho(Arabuni) la ukombozi, ndio Roho wake tuliopewa ndani yetu. Ndio muhuri wetu mpaka siku ya ukombozi( 4:30). Hivyo tuwe na hakika ya ukombozi.
  6. Katika Kristo tumeokolewa kwa neema na si kwa matendo yetu (2:8-9). Akiwa na maana ile mizigo ya sheria kama ndio tiketi ya kuokolewa imewekwa chini, Yesu tayari ameshafanyika sheria yetu, kwa kumwamini tu yeye tumeokolewa.

Haya ni mambo ya muhimu sana, ambayo tunapaswa tuyafahamu juu ya Kristo tuliyempokea ndani yetu. Kulingana na mwandishi tukiyajua hayo itatufanya tusiwe watoto wachanga, wa kuchukuliwa na kila upepo wa elimu ya uongo, kwa hila za watu, na ujanja, na njia za udanganyifu (4:14).

Lakini katika kundi la pili ambalo ni sura ya 4-6;

Tunaelezwa wajibu wetu kimwenendo, baada ya kumwamini Kristo, jinsi unavyopaswa uwe, kwamba hatupaswi kuenenda kama mataifa waenendavyo, bali kinyume chake tukue mpaka kuufikia utimilifu wake.

Ambayo hiyo huja Kwa njia ya kuhudumiana kwa karama mbalimbali sisi kwa sisi katika kifungo cha umoja, kama kanisa la Kristo. (4:16)

Anaeleza pia yampasa kila mmoja binafsi auvue ule utu wa kale wa dhambi, na kuuvaa mpya mpya wa utakatifu na haki (4:20-24),

kwa kuuvua uongo, pia tusiruhusu hasira zitutawale, tusiwe wezi, vinywa vyetu visitoe maneno mabaya na matusi, tuwe wafadhili sisi kwa sisi, tusimzimishe Roho, upendo wetu udumu, uasherati usitajwe, wala aibu, wala ubishi.

Kwasababu watendao kama haya kulingana na Mungu hawana urithi katika ufalme wa Mungu.

Waefeso 5:5

[5]Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu.

Halikadhalika Mwandishi anatoa pia agizo juu ya matendo ya giza kwamba tuyaonapo tuyakemee, vilevile tujiepushe walevi, bali tujazwe Roho wakati wote, kwa kumfanyia Mungu ibada.

Waefeso 5:18-20

[18]Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;

[19]mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;

[20]na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;

Mwandishi anazidi kugusia mienendo yetu mpaka katika ngazi za kifamilia na kikazi.

kwamba wake wanapaswa wawatii waume zao, vilevile waume wawapende wake zao. Watoto wawaheshimu wazazi wao, na wazazi wasiwachokoze watoto wao, Watumwa wawatii bwana zao, na mabwana wasiwatishe watumwa wao.(5:22-6:9)

Anagusia pia eneo la vita vyetu. Kwamba rohoni tupo vitani dhidi ya adui yetu shetani na mapepo yake, yenye kazi ya kuwapofusha watu macho, lakini pia kurusha mishale ya moto kutuangamiza. Hivyo tunapashwa tuvae silaha zote za Mungu, ili tuweze kusimama. (6:10-20). Anaorodhesha silaha hizo. ambazo zinakamilishwa kwa sala na maombi ya daima.

Na mwisho anatoa salamu zake kwa watakatifu, akiwaambia pia habari zake nyingine watakazisikia kwa Tikiko, aliyempeleka kwao.

Kwa ufupisho.

Kitabu hichi kinatupa ufahamu kuhusu ubora wa imani tuliyoipokea lakini pia wajibu wetu baada ya hapo, kwasababu tusipothamini na kulegea adui yetu shetani na majeshi yake yatashambulia imani yetu na hatimaye, tukayakosa tuliyohakikishiwa.

Ukishaamini tembea katika utakatifu. Ukiwa unapiga hatua kila siku kwenda mbali na dhambi, basi fahamu kuwa ukombozi wako ni hakika. Kwasababu msalaba una nguvu ya kukusaidia madhaifu yako.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Warumi.

Mwandishi wa kitabu cha Filemoni ni nani?

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.

Rudi Nyumbani

Print this post

ANZA MAPAMBANO MWANZO WA MWAKA MPYA.

Jina la Mwokozi Mkuu, YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze biblia.

Kosa moja maarufu Mfalme Daudi alilolifanya katika maisha yake, (ingawa baadaye alikuja kusamehewa na Bwana), lilikuwa ni kumuua Uria na kumchukua Mke wake aliyeitwa Bathsheba.

Lakini tukifuatilia chanzo cha kosa, tunaona lilianzia katika MWANZO WA MWAKA MPYA, wakati ambao Wafalme wanatoka kwenda vitani, ila yeye Daudi hakutoka kwenda vitani pamoja na wenzake badala yake akakaa nyumbani, na matokeo yake ni shetani kupata nafasi ya kumjaribu.

2Samweli 11:1 “Hata ikawa, MWANZO WA MWAKA MPYA, wakati watokapo wafalme kwenda vitani, Daudi akampeleka Yoabu, na watumishi wake pamoja naye, na Israeli wote; wakawaangamiza wana wa Amoni, wakauhusuru Raba. LAKINI DAUDI MWENYEWE AKAKAA YERUSALEMU.

2 Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho.

3 Naye Daudi akapeleka, akauliza habari za yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, Je! Huyu siye Bathsheba, binti Eliamu, mkewe Uria, Mhiti?

4 Basi Daudi akapeleka wajumbe, akamtwaa; naye akaingia kwake; naye akalala naye; (maana yule mwanamke amekwisha kutakasika unajisi wake); kisha akarudi nyumbani kwake.

5 Yule mwanamke akachukua mimba; basi akapeleka na kumwambia Daudi, akasema, Ni mja-mzito”.

Laiti Mfalme Daudi angalisimama na kwenda vitani pamoja na wenzake, asingeingia kwenye jaribu kubwa kama lile, ambalo liliuharibu mwaka wake wote na kumchafulia heshima yake kwa vizazi vyote.

Yote hayo ni makosa aliyoyafanya MWANZO WA MWAKA, kumbe kuna kitu katika Mwanzo wa Mwaka, vile vile na katika Mwisho wa Mwaka,..Mwanzo wa Mwaka ni wakati wa kuanza mapambano, si wakati wakulala tena, ni wakati wa kukusanya nguvu ya pamoja na kuingia katika mapambano, ni wakati wa kukusanyika katika nyumba ya MUNGU kupambana kiroho na kuangusha ngome, ni wakati wa kuomba sana.

Bwana atusaidie tuwe na mipango mema katika mwanzo wa Mwaka.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakolosai

Kama kinavyoanza kwa utambulisho wake, ‘Waraka wa Paulo mtume kwa Wakolosai’.

Paulo ndiye mwandishi wa waraka huu.

Madhumuni makuu ya waraka huu ulikuwa ni kuwasisitiza Wakolosai  jinsi Yesu alivyo UTOSHELEVU WOTE, ambaye kwa kupitia yeye Uumbaji wote umekamilishwa ndani yake, lakini si hilo tu bali na  utimilifu  wote wa ki-Mungu unapatikana ndani yake, pamoja na hazina zote za hekima na maarifa.

Akiwa na maana kuwa mtu akimpata Kristo, hahitaji kitu kingine cha pembeni kumkamilisha yeye, Utoshelevu wote upo kwake.

Hivi ni vifungu mama,

1:15-17

“15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. 16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. 17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye”.

2:3

ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.

 

2:9

 “Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili”.

Lakini Sababu ya kusisitiza jambo ni ipi?

Anaeleza kwa undani katika sura ile ya pili, kwamba ni kutokana na uwepo wa watu waliolivamia kanisa na kuwadanganya kwa maneno ya ushawishi, nia zao ni kuwafanya mateka kwa elimu isiyo na matunda, ya mapokeo ya kibinadamu, yasiyo ya Kristo (2:8). Kwamba mtu akishika hayo, ndio utimilifu wote unapatikana.

Vilevile kuonekana kwa baadhi ya desturi za kiyahudi ndani ya kanisa, kama vile kushika sikukuu, tohara,  sabato, na mwandamo wa mwezi. Vikidhaniwa kuwa vitu hivyo vinaweza kuleta ukamilifu wote pamoja na Kristo (2:11-23)

Na pia kuzuka kwa ibada bandia za kuabudu viumbe vya rohoni (malaika), kwa mawazo kuwa mtu ataupokea ukamilifu.(2:18)

Paulo anaeleza yote hayo hayana wokovu, isipokuwa kwa njia ya haki tuliyoipokea kwa msalaba wake uliofuta hati ya mashtaka yetu, kwa mateso yake pale msalabani ambayo kwa kupitia njia hiyo tumepokea msamaha wa dhambi, pale tu tunapoamini na kubatizwa (2:12-17)

Maisha mapya ndani ya Kristo.

Sehemu ya tatu Paulo anaeleza kwamba kuamini ni pamoja na kuuvaa utu upya wa Kristo. Hivyo huyu mtu hatarajiwi kuendelea kuishi hivi hivi tu, kisa Kristo amemkamilisha kwa kila kitu, bali anapaswa aenende kwa Kristo mwenyewe, ayafikiri yaliyo juu, (3:1-17),

Kwa namna gani?

Kwa kuzifisha tabia za mwilini, kama uasherati, uchafu, kutamani, mawazo mabaya, ghadhabu, matusi. Lakini pia kujivika utu wema, moyo wa rehema, unyenyekevu, upole, uvumilivu, kusameheana, upendo, ibada. Vilevile si tu katika mambo ya rohoni , bali mpaka kwenye ngazi za kifamilia, kwamba wake kuwatii waume zao, na waume kuwapenda wake zao, na watoto kuwatii wazazi. Hizo ndio tabia za utu mpya.

Katika sura ya 4.

Bado Paulo aendelea kueleza huo mwenendo ndani ya Kristo, unapaswa uonekane mpaka kwa mabwana, kwa watumwa wao. Kwamba mabwana wawape watumwa haki zao, Lakini pia watakatifu wote, wanapaswa kudumu katika maombi, na kuenenda kwa hekima kwa watu wasioamini, katika usemi bora, na kujifunza kuukomboa wakati.

Na mwisho.

Paulo anawasilisha salamu za washirika wenzake wa injili, kwa Wakolosai ikiwemo, Epafra, Luka, Dema, marko, Aristarko, Yusto.

Hitimisho.

Kwa ufupi waraka huu, hueleza kwamba utoshelevu wote upo ndani ya Kristo tu na sio zaidi ya hapo, hatuhitaji kitu kingine cha pembeni kutukamilisha sisi, Lakini ni wajibu wa huyu mkristo kutembea katika maisha mapya ndani yake. Kwasababu mambo yote mawili yanakwenda sambamba hayatengani. Kristo huokoa na kutakasa wakati huo huo. Unapookolewa, saa hiyo hiyo umevikwa utu upya. Huwezi kuendelea katika dhambi.

Ni kipi cha ziada tunachoweza kujifunza katika waraka huu?.

Maombi ya Paulo na Eprafa yasiyokoma kwa kanisa hili(1:3, 9, 4:12):

Hatuna budi kujijengea desturi ya sikuzote kuliombea kanisa la Bwana, hususani mahali tulipo, pamoja na watakatifu wengine tuwajuao. Kwasababu kusimama kwa kanisa hutegemea sana maombi yasiyokoma.

                                        Bwana akubariki.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                     ||kiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii. Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya kuabudu malaika? (Wakolosai 2:18)

Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,

Tafsiri ya Wakolosai 2:18 Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu,

Epafra ni nani katika biblia? (Wakolosai 1:7)

Uchambuzi na Mwandishi wa kitabu cha Wagalatia

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita;

SWALI: Biblia humaanisha nini kwenye vifungu hivi?

Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita; Lakini mkosaji mmoja huharibu mema mengi.


JIBU: Ni vema kwanza kufahamu kwanini watu wanapigana vita?

Zipo sababu nyingi,baadhi ya hizo ni hizi,

Kujilinda, kutoelewana, kulipiza visasi, kutofautiana kiitikadi, au kutanua ngome.

Hivyo ili watu kufikia malengo hayo, njia pekee waionayo ni kutumia silaha, kuuana. Lakini biblia inashauri njia iliyo bora zaidi ambayo inaweza kutumiwa na hatimaye yote hayo yakatatulika. Na njia hiyo ni hekima.

Hekima ni nini?

Hekima ni uwezo wa kipekee utokao kwa Mungu, unaomsaidia mtu kuweza kupambanua, au kutatua, au kuamua jambo Fulani vema. Hivyo kupitia hekima mtu anaweza kuponya vitu vingi pasipo uharibifu wowote, na kuunda mfumo bora.

Sulemani ambaye ndiye aliyeyaandika maneno hayo alijaliwa amani katika ufalme wake, sio kwamba hakuwa na maadui wanaomzunguka hapana, bali alipewa hekima ya kuishi nao, na kuzungumza nao, na kukubaliana nao, hivyo Israeli hakukuwa na kumwagika damu kama ilivyokuwa kwa baba yake Daudi, ambaye yeye kutwa kuchwa alikuwa vitani. Kilichoweza kumsaidia ni hekima ya Mungu ndani yake.

Lakini sehemu ya pili ya mstari huo anasema;

Lakini mkosaji mmoja huharibu mema mengi’.  Akiwa na maana mkosaji mmoja (wa hekima), jinsi anavyoweza kuharibu mipango mingi mizuri ambayo huwenda ilikuwa tayari imeshaleta matokeo mema. Na kweli hili angalia mahali penye viongozi wabovu, huathiri jamii nzima, hata Israeli, Wafalme wa kule ndio waliisababishia Israeli kunajisika kwa muda mrefu hadi kupelekea kwenda utumwani Babeli mfano wa hao walikuwa ni Yeroboamu na Ahabu.

Kwa ufupi vifungu hivi vinatueleza uzuri wa hekima, lakini pia madhara yasababishwayo pale hekima inapokosekana, hata kwa udogo tu.

Je! Mtu anawezaje kupata hekima?

Hekima chanzo chake ni kumcha Mungu. (Mithali 9:10). Ambapo panaanzia kwenye wokovu, kisha kuendelea kuishi maisha ya utii kwa Kristo baada ya hapo.

Mtu wa namna hii, huvikwa, ujuzi huo wa ki-Mungu, na hivyo anakuwa na uwezo wa  kuutibu ulimwengu kwa namna zote. Mioyo, Ndoa,kanisa, jamii, taifa, vyote huponywa kwa hekima msingi huu wa hekima ya ki-Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWA KUWA ROHO BORA ILIKUWA NDANI YAKE.

Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?

USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini Eliya afunge Mbingu miaka mitatu na nusu? (1Wafalme 17:1)

Swali: Ni ipi sababu ya Nabii Eliya kufunga mbingu, mvua isinyeshe kwa miaka mitatu na nusu?


Jibu: Turejee..

1Wafalme 17:1 “Basi Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu”.

Sababu kuu ya Mungu kufunga Mbingu kwa muda wa miaka mitatu na nusu kupitia kinywa cha Eliya nabii, ni MAOVU ya wana wa Israeli pamoja na mfalme wao aliyeitwa Ahabu.

kwani mfalme Ahabu wa Israeli alimwoa YEZEBELI, mwanamke wa nchi ya Lebanoni  aliyekuwa Mchawi na kahaba na mwenye kumwabudu mungu baali (2Wafalme 9:27), na hivyo akawakosesha Israeli wote, na kuwafanya wamwambudu mungu baali badala ya MUNGU WA MBINGU NA NCHI.

Sasa kitendo cha Taifa zima kumwacha Mungu wa Israeli na kwenda kuabudu miungu mingine, ni Kosa kubwa sana na lenye matokeo makubwa sana kwa Taifa..

Sasa kwa kosa hilo la Mfalme, na malkia wake na Watu karibia wote wa Israeli kumwabudu baali, ndio ikapelekea MUNGU kuadhibu nchi nzima kwa kufunga mbingu mpaka mioyo yao ilipofunguka na kumgeukia Bwana.

Na utaona MUNGU alishatangulia kuwatahadharisha wana wa Israeli kupitia kinywa cha Nabii Musa, kuhusiana na makosa ya kuabudu miungu mingine na matokeo yake, KUWA MBINGU ZITAFUNGWA..

Kumbukumbu 11:16 “Jitunzeni nafsi zenu, mioyo yenu isije ikadanganywa, mkageuka na kutumikia miungu mingine na kuiabudu;

17 hasira za Bwana zikawaka juu yenu, NAYE AKAFUNGA MBINGU KUSIWE NA MVUA, wala nchi isitoe matunda yake; mkaangamia kwa upesi mtoke katika nchi nzuri awapayo Bwana”.

Na utaona pia Maombi ya Mfalme Sulemani, wakati analiweka wakfu lile Hekalu yalilenga hayo hayo…

1Wafalme 8:35 “Ikiwa mbingu zimefungwa, hata hakuna mvua, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakiomba wakikabili mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kuiacha dhambi yao, wakati ule utakapowatesa;

36 basi, usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na ya watu wako Israeli; unapowafundisha njia iliyo njema, iwapasayo kuiendea; ukanyeshe mvua juu ya nchi yako, uliyowapa watu wako iwe urithi wao”.

Hivyo hiyo ndio sababu ya mbingu kufungwa wakati wa Eliya, (maovu ya kumwabudu baali), na ndio maana utaona pale walipojinyenyekeza tu na kutubia, basi Eliya aliomba na mbingu zikafunguka.

1Wafalme 18:38 “Ndipo moto wa Bwana ukashuka, ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa, na kuni, na mawe, na mavumbi, ukayaramba yale maji yaliyokuwamo katika mfereji.

39 Na watu wote walipoona, wakaanguka kifudifudi; wakasema, Bwana ndiye Mungu, Bwana ndiye Mungu.

40 Eliya akawaambia, Wakamateni hao manabii wa Baali, asiokoke hata mmoja. Wakawakamata; na Eliya akawachukua mpaka kijito cha Kishoni, akawaua huko.

41 Naye Eliya akamwambia Ahabu, Haya! Inuka, ule, unywe; kwani pana sauti ya mvua tele”.

Na jambo kama hili bado linaendelea kiroho na kimwili, kama tukimtumikia Bwana basi Bwana atatunyeshea mvua yake ya Baraka, lakini kama tutamwacha basi mbingu za Baraka zitafungwa, hivyo huu si wakati wa kusita sita katika mawazo mawili, bali ni wakati wa kufanya maamuzi thabiti ya kusimama na Bwana.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Baali alikuwa nani?

YEZEBELI ALIKUWA NANI

RUHUSU TOHARA IPITE JUU YA KARAMA YAKO.

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

Rahabu kwenye biblia.

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Warumi.

Kitabu hichi kama kinavyojitambulisha, “Waraka wa Paulo kwa Warumi” mwandishi wake ni Mtume Paulo.

Kitabu hiki alikiandika akiwa Korintho mahali palipoitwa Kenkrea (Warumi 16:1)

Tofauti na nyaraka nyingine ambazo Paulo aliziandika kwa makanisa ambayo alikuwa tayari ameshayatembelea/ameyapanda hapo nyuma. Waraka huu tunaonyeshwa Paulo hakuwahi kufika Rumi. Lakini alisikia mwitikio wao wa injili, hivyo likawa ni tamanio lake pia awafikie na wao, lengo likiwa sio kupanda juu ya msingi wa watu wengine bali wajengane kiimani.(1-18),

Na kweli tamanio lake tunaona lilikuja kutimia baadaye, kama tunavyosoma kwenye kitabu cha matendo ya mitume, katika ile ziara yake ya mwisho kama mfungwa, alifika Rumi, na huko akafanikiwa kuhubiri injili sawasawa na tamanio lake (Matendo 27-28).

Hichi ni kitabu kinachoeleza misingi ya imani  ki-mpangilio . Kuanzia asili ya wokovu wetu, haki ya Mungu, na mwenendo wa kikristo. Hivyo kuna umuhimu mkubwa sana kwa mkristo yoyote kukielewa vema kitabu hichi.

Migawanya mikuu ya kitabu hichi.

     1) Nguvu ya injili? (1: 1-17)

Baada ya Paulo, kueleza tamanio lake la kuwafikia katika utangulizi wake, tunaona katika mistari hiyo anasisitiza kwanini afanye hivyo? Ni kwasababu ya ‘Nguvu ya Injili yenyewe’, Akisema Injili ni uweza wa Mungu uuletao wokovu. Na hivyo haionei haya kuihubiri kwa watu wote..kwa wayahudi na watu wa mataifa pia.

  1. Hatia kwa wanadamu wote (1:18- 3:20)

Sehemu ya pili Paulo anaeleza jinsi wanadamu wote walivyopungikiwa na utukufu wa Mungu kuanzia watu wa mataifa ambao wameshindwa kuitii kweli ya Mungu iliyofunuliwa kwao kwa mambo yake yaliyo dhahiri kabisa yanayotambulika hata pasipo sheria, kwamba mambo ya asili yanafundisha haki ya Mungu, lakini walikataa kutii. Vilevile na wayahudi  pia ambao walikuwa na sheria lakini walishindwa kuyatenda yote kulingana na yaliyoandikwa. Hivyo hakuna hata mmoja mwenye haki,  wote wamewekwa chini ya hukumu ya ghadhabu ya Mungu, kwa kushindwa kutenda haki yote.

  1. Haki kwa Imani (3:21-5:21)

Kwa kuwa wanadamu wameshindwa kuwa wakamilifu, Paulo anaeleza njia ambayo Mungu ameitoa kwa  mwanadamu kuweza  kuhesabiwa haki. Ni njia ambayo inadhihirishwa bila matendo ya sheria, tunayoipata kwa kumwamini tu Yesu Kristo. Yaani pale mtu anapomwamini Bwana Yesu kwamba kifo chake kimeleta ukombozi wa roho yake, basi mtu huyo anakuwa amehesabiwa haki kuwa ni Mtakatifu mbele za Mungu.

Kulithibitisha hilo Paulo akaendelea kueleza  kwa mfano wa Ibrahimu jinsi Mungu alivyomhesabia haki bila sheria yoyote, na kwamba sisi pia tutahesabiwa kwa njia hiyo hiyo.

  1. Maisha mapya ndani ya Kristo (6:1-8:39)

Katika sehemu hii Paulo anaeleza maisha baada ya kuhesabiwa haki, kwamba mkristo anapaswa aendelee kutakaswa na kuwa kama Kristo. Lakini kutokana na mashindano kati ya mwili na roho. Ili aweze kuushinda mwili anapaswa ajifunze kuishi kwa Roho, kwa kuruhusu utendaji kazi wake ndani yake. Maneno hayo ameyarudia pia katika waraka wake kwa Wagalatia (Wagatia 5:16). Kwamba mtu anayeenenda kwa Roho kamwe hawezi kuzitimiza tamaa za mwili.

Lakini mbele kidogo anaendelea kuhimiza upendo wa milele wa Mungu, uliodhihirishwa kwetu kupitia Yesu Kristo, ambao hauwezi kutenganishwa na kitu chochote tukijuacho duniani au mbinguni.

  1. Uhuru wa Mungu wa kuchagua, na kusudi lake kwa Waisraeli (9:1- 11:36)

Kwenye sura hizi, Paulo anaeleza uhuru wa Mungu wa kuchagua, na siri iliyokuwa nyuma ya Israeli kukataa injili. Anaeleza mpango wake wa wokovu kwa mataifa na waisraeli, kwamba iliwapasa wao wakatae injili ili sisi watu wa mataifa tuipokee injili. Na hivyo anaeleza sisi pia tunapaswa tuupokee wokovu kwa unyenyekevu wote kwasababu tusipokaa katika kuamini tutakatwa, kama wao walivyokatwa.

  1. Tabia ya maisha mapya katika Kristo (Warumi 12:1- 15:3 )

Paulo anaeleza jinsi tunavyopaswa kuitoa miili yetu kama dhabihu iliyo hai takatifu yenye kumpendeza Mungu, tunawajibu wa kupendana sisi kwa sisi, tusiwe watu wa kulipa kisasi, tuishi kwa heshima, tuhudumiane katika karama mbalimbali tulizokirimiwa na Mungu, tutii mamlaka zilizowekwa, vinywa vyetu vitoe baraka, tumtumikie Mungu kwa bidii, tudumu katika sala, tuishi kwa amani sisi kwa sisi, pia tuweze kuchukiliana katika viwango mbalimbali vya imani bila kuhukumiana.

Kwa ufupi sura hizi zinaeleza tabia zetu zinapaswa ziweje baada ya wokovu.

  1. Hitimisho  (15:14- 19:27)

Paulo anaeleza mpango wake wa kuwafikia Warumi pindi atakapokuwa anasafiri kwenda Spania kuhubiri injili. Akiomba akumbukwe katika maombi dhidi ya watu wabaya, na mwisho anatoa salamu kwa watakatifu wote walio Rumi, pamoja na angalizo kwa watu waletao fitna katika injili waliyoipokea wajiepushe nao

KWA UFUPI.

Kitabu hichi kinaeleza

Haki ya Mungu ikoje, ambapo hapo mwanzo ilidhaniwa inapatikana kwa sheria au matendo ya mwanadamu, kumbe sio, hayo yalishindwa bali kwa njia ya Yesu Kristo, lakini pia kinaeleza namna ambavyo tunaupokea wokovu huo kwa neema kwa njia ya Imani, na pia jinsi Mkristo anavyopaswa aishi kulingana na wokovu alioupokea. Kwamba sio kwasababu amehesabiwa haki bure bila matendo, basi aishi maisha kama atakayo, hapana vinginevyo atakufa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NJIA/BARABARA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.

Uchambuzi na Mwandishi wa kitabu cha Wagalatia

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Rudi Nyumbani

Print this post

USIOGOPE.. USIOGOPE…

Danieli 10:19 “Akasema, Ee mtu upendwaye sana, usiogope; amani na iwe kwako, uwe na nguvu, naam, uwe na nguvu. Aliposema nami nikapata nguvu, nikasema, Ee Bwana wangu, na aseme Bwana wangu; kwa maana umenitia nguvu”.

HOFU ni mlango wa Adui, lakini UJASIRI katika Neno la MUNGU ni UFUNGUO wa mafanikio.

Ifuatayo ni mistari michache ya kusimamia wakati wa tufani, na mashaka, na vitisho vya adui na majaribu yake yotw yajapo.. Simama nayo, na utauona Wokovu wa Bwana.

  1. USIOGOPESHWE NA SAUTI YA KIFO.

Waamuzi 6:23 “BWANA akamwambia Amani iwe pamoja nawe; usiogope; hutakufa”.

2 Samweli 12:13 “Daudi akamwambia Nathani, Nimemfanyia BWANA dhambi. Nathani akamwambia Daudi, BWANA naye ameiondoa dhambi yako; hutakufa”.

  1. USIOGOPSHWE MAJARIBU MAZITO.

Isaya 41:10 “usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu”.

  1. USIOGOPE KUMTUMIKIA MUNGU.

1 Nyakati 28:20 “Kisha Daudi akamwambia Sulemani mwanawe, Uwe hodari, mwenye moyo mkuu, ukatende hivyo; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa BWANA, Mungu, Mungu wangu, yu pamoja nawe; yeye hatakupungukia wala kukuacha, hata itakapomalizika kazi yote ya huo utumishi wa nyumba ya BWANA”.

Matendo 18:9 “Bwana akamwambia Paulo kwa maono usiku, Usiogope, bali nena, wala usinyamaze”.

  1. USIOGOPE UNAPOBAKI PEKE YAKO.

Isaya 41:13 “Kwa maana mimi, BWANA, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia”.

  1. USIOGOPE JUU YA UZAO WA TUMBO LAKO.

Isaya 43:5 “Usiogope; maana mimi ni pamoja nawe; nitaleta wazao wako toka mashariki, nitakukusanya toka magharibi”.

Mwanzo 35:17 “Ikawa alipokuwa anashikwa sana na utungu, mzalisha akamwambia, Usiogope, maana sasa utamzaa mwanamume mwingine”.

Mwanzo 21:17 “Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko”.

  1. USIOGOPE KUINGIA MJI MWINGINE.

Yoshua 1:9 “Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.

Kumbukumbu 1:21 “Tazama, BWANA, Mungu wako, ameiweka nchi mbele yako; haya panda, itamalaki, kama BWANA, Mungu wa baba zako, alivyokuambia; usiogope wala usifadhaike”.

Mwanzo 46:3 “Akasema, Mimi ni Mungu, Mungu wa baba yako, usiogope kushuka mpaka Misri; maana nitakufanya uwe taifa kubwa huko.

4 Mimi nitashuka pamoja nawe mpaka Misri; nami nitakupandisha tena bila shaka; na Yusufu ataweka mkono wake juu ya macho yako”.

  1. USIOGOPE MAJESHI YA ADUI YANAPOJIPANGA.

2 Wafalme 6:16 “Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao”.

Zaburi 27:3 “Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea”.

  1. USIOGOPESHWE NA TAARIFA ZA GHAFLA ZENYE KUHUZUNISHA.

Mithali 3:25 “Usiogope hofu ya ghafula, Wala uharibifu wa waovu utakapofika.

26 Kwa kuwa BWANA atakuwa tumaini lako, Naye atakulinda mguu wako usinaswe”.

BWANA AKUBARIKI.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

UWE KIKOMBE SAFI 

UTAJUAJE KAMA WEWE NI MTUMISHI WA MUNGU NA KRISTO YU PAMOJA NAWE?.

Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)

Rudi Nyumbani

Print this post