Category Archive Uncategorized @sw-tz

Watu wa zamani walitumia nini kujua saa, dakika na sekunde?

Swali: Kwasasa tunatumia kifaa kinachoitwa saa (iwe na ukutani, mkononi au kwenye simu) kujua sekunde, dakika na saa.. Je watu wa zamani walijuaje sekunde, dakika na saa?


Jibu: Nyakati za Biblia siku iligawanywa katika masaa 12 ya mchana na masaa 12 ya usiku, tunalithibitisha hilo katika Yohana 11:19-20.

Yohana 11:9 “Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.

10 Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake”.

Hii ikimaanisha kuwa ni kweli enzi za Bwana YESU akiwa duniani, siku ilikuwa ikigawanywa katika mgawanyo wa masaa.. Lakini kuhusiana na mgawanyo wa sekunde Biblia haituonyeshi mahali popote kwamba watu wa kale waligawanya saa katika sekunde, hivyo hakukuwa na mgawanyo wa sekunde katika kila saa.

Sasa swali walijuaje kuwa lisaa limoja limekwisha na limeingia lingine, na hatimaye kumaliza yote 12 ya mchana na usiku? Na ilihali hawakuwa na saa kama za kwetu zinazohesabu masaa?

Watu wa kale hawakutumia saa za mkononi kama za kwetu, katika kuigawanya siku katika masaa, bali walitumia njia za asili kuigawanya siku katika masaa 12, na njia hizo ni kutazama Jua, kutumia kivuli cha jua, kipimo cha maji, na saa ya mchanga, kipimo cha nyota tutazamame kimoja baada ya kingine kwa ufupi.

  1. Kipimo cha kutazama jua.

Asuhuni kulipopambazuka walijua ni saa moja, na Jua lilipofika la utosini waliweza kujua ndio nusu ya siku, yaani saa sita mchana, na lilipozama waliweza kujua ni saa 12 jioni, hivyo wakati jua likiwa katikati ya moja na saa sita mchana waliweza kukadiria masaa hayo ya katikati, vivyo hivyo na jioni, na njia hii ndio iliyotumika sana na wayahudi katika kujua masaa.

   2. Saa ya kivuli cha Jua (Sundial).

Hii ni njia iliyotumika kwa kutazama mwelekeo wa kivuli cha jua, na ndio ile iliyotajwa katika Isaya 38:8, wakati wa mfalme Ahazi.

   3. Saa ya Maji.

Hii ilitumika zaidi wakati wa usiku, ambapo kiwango cha maji kilidondoka kidogo kidogo katika kifaa husika, na njia hii ilitumiwa sana na watu wa Babeli.

   4. Saa ya Mchanga.

Mchanga uliwekwa katika kifaa maalum, na baadaye kuachiwa kudondoka kidogo kidogo.

  5. Kipimo cha Nyota.

Kipimo hiki kilitumika nyakati za usiku ambapo waliangalia nafasi za makundi ya nyota kama vile Orioni, na Kilimia.

Kwahiyo kwa ufupi ni kwamba enzi za Biblia walitumia zaidi kipimo cha jua na kivuli cha jua kujua mgawanyo wa masaa.

Sasa kwa urefu kwanini Bwana YESU asema saa za mchana si 12, fungua hapa >>>NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.

FAIDA NYINGINE YA MAOMBI YA KUSHUKURU.

FUNGUA KINYWA CHA ROHO MTAKATIFU KIHUDUMU.

USIKAWIE- KAWIE KUUFUNGUA MOYO WAKO

JE! UMEFIKIA VIGEZO VYA KUWA BABA ROHONI?

Print this post

Je? ni sahihi kwa watu wa MUNGU kutumia majina ya wanyama kuwaita wengine.

SWALI:Je? ni sahihi kwa watu wa MUNGU kutumia majina ya wanyama kuwaita wengine.mfano “We kenge njoo hapa”, kama YESU alivyo tumia mbweha katika

luka 13:32.


JIBU: Katika biblia tunaona watu wakiitwa kwa majina mbalimbali ya wanyama mfano mbwa mwitu (Mathayo 7:15), kondoo(Yohana10:27), nyoka(Mathayo 13:34). Lakini pia mbweha, Njiwa, nguruwe, Simba, mbuzi.

Sasa ni vema kufahamu makusudio ya watu/jamii kuitwa hivyo yalikuwa ni nini, hayakuwa kwa lengo la kutukana, au kukejeli, au kudharau..

Hapana Bali kwa lengo la kuonyesha tabia ya mtu, jinsi ilivyo hilo tu.

Kwamfano Yesu alipomuitwa Herode Mbweha, hakuwa na kusudi la kumtukana, au kumdharau, bali alikuwa Anaeleza tabia zake zilizo mfano wa mbweha, ambaye anatabia ya kuvizia na kurarua wanyama wadogo na kuwaua. Maana hivyo ndivyo Herode alivyokuwa, jambo lililoonekana Hata kwa baba zake Kipindi Yesu anazaliwa walimwinda ili wamuue.

Sasa Ikiwa mtu atajulikana kwa namna kama hiyo, kibiblia sio tusi.

Lakini kinyume chake watu hutumia Majina ya wanyama kuwatukana Wengine, au kuwaabisha, au kuonyesha dharau kinyume chao, chuki au hasira, hayo biblia imekataza…na ni dhambi

Kusema “wewe kenge njoo hapa”..Moja kwa moja kauli hiyo inaonyesha chanzo chake ni hasira, dharau au chuki.

Waefeso 4:29

[29]Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia. 

Wakolosai 3:8

[8]Lakini sasa yawekeni mbali nanyi haya yote, hasira, na ghadhabu, na uovu, na matukano, na matusi vinywani mwenu. 

Mathayo 5:22

[22]Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto. 

Hivyo chunga kinywa chako. Kila Neno ulisemalo pima makusudi yaliyo nyuma yake.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VILIO VINAVYOUFIKIA MOYO WANGU.

 

JAWA SANA MOTO ULAO

USIWAOGOPE WAZAMZUMI

Print this post

VILIO VINAVYOUFIKIA MOYO WANGU.

Kilio kibiblia ni mafadhaiko, machozi, au maonezi yanayoendelea kwa muda mrefu, bila kuchukuliwa hatua, au kupatiwa utatuzi stahiki, Lakini sio tu machozi bali pia shangwe ovu..zinazoendelezwa kwa muda mrefu mbele za Mungu bila kuachwa nazo pia huitwa vilio.

Sasa Makosa kama haya, (ambayo huzaa vilio) ni tofauti na makosa mengine, kwasababu haya hujilimbikiza mpaka kuzama moyoni mwa Mungu, Na adhabu zake huwa ni nzito sana, kulingana na matukio kadha wa kadha tunayoyasoma katika maandiko.

Tutakwenda kuona aina tano (5)  vilio ambavyo vinatajwa katika biblia. Na yamkini pengine umekuwa mmojawapo uliyesababisha hivyo, Basi utubu mapema ili mabaya yasije kukukuta wakati wowote

1) Kilio cha wakulima.

Yakobo 5:1-6

[1]Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia.

[2]Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo.

[3]Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho.

[4]Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi.

[5]Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo.

[6]Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.

Mstari wa nne anasema. ‘Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna’

Hii ni aina ya kilio cha wafanyakazi Wote wa chini (humaanisha pia waajiriwa wote).

Ukweli Ni kwamba asilimia kubwa ya waajiri, huwadhulumu wafanyakazi wao mishahara au wanawatumikisha kupita kiasi na kuwapa mishahara midogo, Lengo ni ili wajilimbikizie mali, kwa manufaa yao wenyewe…

Sasa hilo ni jambo baya sana, kwasababu huku chini Mungu anasikia kilio chao hata kama hawasemi au hawaoni…mwisho wake utakuwa mbaya, hizo mali zitakutafuna kama yule tajiri wa Lazaro.

Hakikisha kuwa yule unayemwajiri, mpe stahiki zake, si tu kwenye ngazi za mashirika au makampuni lakini pia hata nyumbani kwako ikiwa umemwajiri msaidizi wa kazi, mpalilia bustani, msafisha choo, hakikisha iliyo haki yake unampa kwa wakati ili Bwana asiharibu ulivyo navyo. Vilio vyao vina nguvu sana mbele za Mungu.

2) Kilio cha Damu isiyo na hatia

Tunaona Kaini alipomuua ndugu yake, alidhani kila kitu kimekwisha…lakini Mungu akamweleza kinachoendelea katika ulimwengu Wa roho, kuwa damu yake inamlilia..Na adhabu yake ikawa ni mbaya sana…kulaaniwa na kukataliwa na nchi.

Mwanzo 4:10-13

[10]Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.

[11]Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;

[12]utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.

[13]Kaini akamwambia BWANA, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.

Kamwe usiue mtu. Au kuchochea mauaji Yasiyo na hatia

3) Kilio cha walioteswa.

Wana wa Israeli, walipokuwa Misri walitumikishwa na kuteswa na kunyanyaswa na Farao..wakamlilia Mungu, Bwana akasikia kilio chao

Kutoka 3:7-9

[7]BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;

[8]nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.

[9]Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.

Matokeo yakawa ni Misri kupoteza kila kitu, ambacho walikisumbukia kwa muda mrefu, pamoja na vifo vingi. Kamwe Usimtese mtu yeyote, awe mke wako, mtoto wa kambo, mkwe, kijakazi, yatima, mjane, fukara.

Hilo usiliruhusu kwasababu Vilio vyao vikimfikia Mungu, utakuwa mashakani.

4) Kilio cha mwenye Haki (Mtakatifu katika dhiki)

Ufunuo 6:9-10

[9]Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao.

[10]Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?

Watakatifu waliapo, ni mbaya zaidi, kuliko hata makundi mengine yote wamliliapo Mungu. Adhabu yake, Mungu huikusanya, ambayo sehemu ya hiyo inamwagwa hapa hapa duniani(Ufunuo 16:4-7), lakini pia sehemu kubwa zaidi inakuwa ni baada ya haya maisha.

Kamwe usimtese mtu wa Mungu, usimdhulumu, usimwaibishe, usiwe mwiba kwake..Kwasababu vilio vyao Mungu huvisikia kwa haraka sana.

5) Kilio (Shangwe) cha waovu.

Anasa, na matendo mabaya ambayo watu wanayafanya…wakidhani ndio maisha…kumbe hawajua ni kilio kikubwa kinachoufikia moyo wa Mungu kwa haraka, kikisema mbona huji kuteketeza? Ndivyo ilivyokuwa kwa Sodoma na Gomora.

Mwanzo 18:20-21

[20]BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,

[21]basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.

Hii ni hatari ambayo ndio inayoendelea sasa karibu dunia nzima. Matendo ya Sodoma na Gomora (ulawiti & ufiraji), anasa, ulevi, starehe, huvuta haraka sana, hukumu za Mungu. Na kama tunavyojua hizi ni nyakati za mwisho, moja ya hizi siku hukumu ya Mungu itamwagwa Duniani.

Je! Umemwamini Yesu?

Je una uhakika kuwa Kristo akirudi Leo utakwenda naye?

Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari kufanya hivyo sasa.. Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! Yohana alimtilia shaka Bwana YESU? (Mathayo 11:3)

ENDELEZA UPONDAJI.

USHUHUDA WA MATENDO NI MKUU KULIKO WA MANENO.

Print this post

Je kuna walioandikiwa mabaya  na wengine mema?

Swali: Unakuta mtu anapitia tatizo fulani, halafu anasema.. ndio nimeandikiwa hivyo! Na siwezi kubadilisha.. sasa je mtu anaweza kuwa ameandikiwa mabaya yampate na mwingine mema?


Jibu:  Kifungu cha Biblia kinachosapoti kuwa mtu anaweza kuwa ameandikiwa mabaya au mema ni kutoka katika kitabu cha Yeremia..

Yeremia 15:2 “Kisha itakuwa, hapo watakapokuambia, Tutoke, tuende wapi? Utawaambia, Bwana asema hivi, WALIOANDIKIWA KUFA, watakwenda kufa; au kufa kwa upanga, watakufa kwa upanga; AU KUFA KWA NJAA, WATAKUFA KWA NJAA, au kutekwa nyara, watakuwa mateka”.

Kwa haraka andiko hilo laweza kueleweka kwamba wapo watu walioandikwa na MUNGU matatizo tangu mwanzo, lakini kiuhalisia haiko hivo.. hakuna mtu aliyeandikiwa na MUNGU matatizo, au shida..

Sasa kama hivyo ndivyo, nini maana ya andiko hilo ya kwamba “waliondikiwa kufa watakufa? (Yeremia 15:2)”

Mantiki ya “kuandikiwa hapo” inarejea sheria za Mungu huko nyuma.. kwamba iliandikwa “Mtu asiyeishi kwa sheria za Mungu atadhibiwa kwa sheria”… Kwamfano iliandikwa hivi katika Kumbukumbu 28:15-18..

Kumbukumbu 28:15 “Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata.

16 Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani.

17 Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia.

18 Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako”.

Sasa kulingana na andiko hilo, mtu Yule ambaye ataacha kusikiliza sauti ya Bwana na atafanya mabaya… basi maandiko hayo ya laana yatampata, na hapo ni sawa na kusema kwamba “ameandikiwa laana”

Lakini si kwamba Mungu anamchagua mtu na kumwandikia laana na mwingine anamchagua na kumwandikia Baraka!… La!..Bali laana zake na Baraka zake zinakuja juu ya mtu kwasababu ya matendo ya mtu.

Kwahiyo mtu aliyekufa kwa upanga huwenda ni kwasababu aliua kwa upanga, na hivyo andiko hili ndio aliloandikiwa na limetimia kwake..

Ufunuo 13:10 “Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga….”

Na makosa mengine yote ni hivyo hivyo, yameshaandikiwa adhabu yake.. kwahiyo mtu akiyatenda atakuwa anapokea malipo ya yaliyoandikwa na kuichukua hiyo nafasi.

Bwana atusaidie, tusitimize maandiko ya Laana, bali tutimize maandiko ya Baraka ili tuwe miongoni mwa waliondikiwa Baraka.

Je umempokea YESU, Umebatizwa kwa Roho Mtakatifu?.. kama bado unasubiri nini?…fahamu ya kuwa unyakuo wa kanisa umekaribia sana na siku yoyote parapanda ya mwisho inalia na wafu wanafufuliwa.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UVUKISHE MIPAKA UPENDO WAKO.

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

FAIDA NYINGINE YA MAOMBI YA KUSHUKURU.

ILI TUONEKANE SAFI MBELE ZA MUNGU TUFANYE NINI?

LINDA CHEMCHEMI YA MOYO WAKO.

Print this post

USHUHUDA WA MATENDO NI MKUU KULIKO WA MANENO.

Jina la Bwana YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze Biblia Neno la MUNGU wetu lililo Taa na Mwanga wa njia  yetu (Zab. 119:105).


“Maneno” yanafaa kuthibitisha jambo, lakini “matendo” ni bora zaidi.. Hebu tujifunze kwa Bwana YESU ambaye alitumia matendo zaidi kuliko maneno.

Kipindi ambacho  Yohana Mbatizaji anawatuma wanafunzi wake kwa YESU kumwuliza kama yeye ndiye au wamtazamie mwingine, jibu la YESU halikuwa “Ndio mimi ndiye”.. bali aliwaambia wale watu wamrudie Yohana wamwambie wanayoyaona, viwete wanatembea, vipofu wanaona..

Mathayo 11:2 “Naye Yohana aliposikia huko gerezani matendo yake Kristo, alituma wanafunzi wake, kumwuliza,

3 Wewe ndiwe yule ajaye, au tumtazamie mwingine?

4 Yesu akajibu akawaambia, Nendeni mkamweleze Yohana mnayoyasikia na kuyaona;

5 vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema”.

Umeona hapo KRISTO hakutumia maneno kujieleza yeye ni nani bali matendo.. Kwa ufupi kazi zake zilimshuhudia yeye ni nani, na sio hapo tu bali kila mahali ilikuwa ni hivyo hivyo..

Yohana 10:24 “Basi Wayahudi walimzunguka, wakamwambia, Hata lini utatuhangaisha nafsi zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi.

25 Yesu akawajibu, Naliwaambia, lakini ninyi hamsadiki. Kazi hizi ninazozifanya kwa jina la Baba yangu ndizo zinazonishuhudia”.

Umeona, kumbe kazi (yaani matendo) ya YESU ndio yaliyomshuhudia??…  Je na sisi tutumie kipi kutangaza ushuhuda wetu?.. maneno yetu au kazi zetu?..Bila shaka Matendo yetu yanafaa zaidi kuliko maneno.

Tutatambulika kuwa sisi ni wakristo kwa matendo na si maneno tu.. tutatambulika sisi ni watumishi kwa matendo na si maneno matupu tu!, tutatambulika sisi ni wakweli kwa matendo na si kwa maneno tu.

Ukisema umepata badiliko moyoni, uthibitisho wa badiliko hilo ni matendo ya mwilini, kwamba kama umebadilishwa tabia basi huwezi kuendelea kuiba, au kutukana au kuvaa vibaya au kufanya uzinzi, uthibitisho wa badiliko la ndani ni matendo ya nje, na si maneno tu..

Mathayo 5:16 “Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni”.

Hivyo tutie bidii kutengeneza matendo yetu zaidi ya maneno yetu.

Bwana YESU atusaidie..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU

ENDELEZA UPONDAJI.

USHUHUDA WA RICKY:

MBONA MMESIMAMA HAPA MCHANA KUTWA BILA KAZI?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Print this post

BABA AKIMBIAYE

Luka 15:20

[20]Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana. 

Habari ya mwanampotevu hufunua picha halisi ya rehema na huruma nyingi za Mungu kwetu. Baada ya yule mwana mdogo, kupoteza kila kitu, kwa maisha ya anasa..mwishowe alizingatia kurudi kwa baba yake, Akiwa na fikra za aidha kulaumiwa, Kutengwa, au pengine kuadhibiwa na kufanywa mtumwa…lakini mambo yalikuwa mbali sana na mategemeo yake..tena sanaa..

Kabla hata hajamwona Baba yake, Baba yake alishamwona kwanza yeye kwa mbali… lakini si hilo tu, mzee yule hakungoja kijana wake amfikie, bali alitoka saa ile ile akaanza kukimbia kumwelekea mwana wake..

Hilo jambo La ajabu sana, kwani kwa tamaduni za zamani, hata sasa…mtu mzima kukimbia, Ni aidha kuna jambo la taharuki sana…au la hisia kubwa kupita kiasi…kwasababu watu wazima hawakimbii ovyo..

Lakini kwa huyu mzee, ilibidi akaidi kanuni hiyo..akimbie kama mtoto mdogo kumwelekea mwanawe na alipomfikia akamkumbatia na kumbusu sana…unaweza tengeneza picha ni hisia gani kali yule baba alikuwa nazo kwa mwanawe..

Mambo kama hayo ni rahisi kuyaona kwa mzazi ambaye pengine mtoto wake ampendaye alikuwa amesafiri kwa wakati mrefu na sasa amekuja kumsalimia Nyumbani…lakini si rahisi kuona mzazi anaonyesha hivyo kwa mtoto mtukutu, mwenye kiburi, aliyeshindikana…pengine angemkaribisha tu, na kumsamehe, na kuongea naye kawaida…lakini huyu alichinjiwa mpaka mnyama na karamu juu..

Hii ni habari inayofunua hisia za Mungu kwa mwenye dhambi atubupo kwa dhati…

Kabla Hata hujamaliza ombi la toba tayari Mungu ameshakukimbilia na kukukumbatia, neema yake ya kusamehe inazidi wingi wa dhambi tulizomtenda…

Yawezekana wewe umekuwa mwana mpotevu kwa kurejea kwenye Dhambi ambazo ulishaziacha zamani…vipi kama ukitubu leo kwa kumaanisha.?

Ulitoka nje ya ndoa Yako…tubu sasa…ulirudia tabia ya uzinzi na kujichua..tubu sasa, Umerudia ulevi na anasa..embu tubu..Mungu yupo tayari kukukimbilia…Na kukusamehe zaidi ya matarajio yako.

Na kukusaidia…yule mwana mpotevu “alizingatia” embu na wewe zingatia pia leo.. kuacha hayo maisha ya kale…haijalishi umefanya makosa Mengi ya aibu namna gani..Tubu tu leo na kutupa hivyo vikoba vya kiganga, na ufiraji, na wizi na rushwa uzifanyazo. na Bwana atakuponya.

Kumbuka ukifa katika dhambi zako ni moja kwa moja kuzimu..kwanini iwe hivyo wakati akusameheaye anakukimbilia?

Usimzuie, achilia akili zako mrudie muumba wako.

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

BWANA NISAIDIE, KUTOKUAMINI KWANGU

JAWA SANA MOTO ULAO.

TENGENEZA NJIA YAKO.

Print this post

JAWA SANA MOTO ULAO.

Waebrania 12:29

[29]maana Mungu wetu ni moto ulao.

Mungu huitwa moto, lakini si moto tu bali moto ulao, maana yake si ule wa kuunguza tu, bali Ule wa kulamba kila kitu, kutafuna Na kutowesha kabisa

Mfano wake ni kama ule ulioshuka juu ya madhabahu Aliyoijenga Eliya, uliposhuka, juu yake haukuchagua maji, wala kuni, wala sadaka..mahali pale palimezwa kila kitu…(1Wafalme 18:38)

Tofauti na mioto Mingine ambayo itaivisha tu kitu, au kugeuza umbile n.k. moto huu haubadilishi umbile Kama hii mioto mingine tuliyonayo…ambayo ikipita Juu ya chuma Haiwezi kuila yote, bali huiyeyusha Tu na kuibadili umbile, huo wa Mungu hulamba Vyote bila kubagua…

Huu ni moto wa rohoni sio mwilini.. ukijazwa huu, basi fahamu hakuna chochote ambacho hakifai kisichoungua….ugusapo popote..huharibu kabisa Kabisa kazi za shetani, ukaapo ndani yako huchoma kabisa kabisa mambo maovu.

Hivyo Bwana ametutaka kama watoto wake aliotuzaa tujawe na moto huu ndani yetu.. na namna ya kuupokea..ameeleza katika vifungu vifuatavyo;

Isaya 33:14

[14]…. Ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto ulao; ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto uteketezao milele?

[15]Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung’utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.

Umeona ni nani Awezaye kukaa na moto ulao? Kumbe si wote…bali ni wenye sifa hizo zilizotajwa..

Maana yake, kwa kauli ya ujumla ni yule yeye atafutaye kuishi maisha matakatifu na ya haki.

Hii ndio mbio yetu wote…

Nguvu ya ukristo baada ya kuokoka ni utakatifu. Ndio moto wetu ulao.

Bwana akubariki.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kutawa ni nini? Sawasa na Luka 1:24

Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.

Yohana aliwatiaje waasi akili za wenye haki? (Luka 1:17)

Print this post

Kutawa ni nini? Sawasa na Luka 1:24

Swali: Kutawa kwa Elisabeti miezi mitano maana yake nini?


Jibu: Turejee..

Luka 1:24 “Hata baada ya siku zile mkewe Elisabeti alichukua mimba AKATAWA miezi mitano, akisema,

25 Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana katika siku zile alizoniangalia ili kuniondolea aibu yangu mbele ya watu”.

Tafsiri ya “Kutawa” ni “kujitenga”.. hivyo Kiswahili kingine cha mstari huo ni hiki… “Hata baada ya siku zile mkewe Elisabeti alichukua mimba AKAJITENGA miezi mitano”

Hivyo Elisabeti alijitenga na jamii ya watu pengine kwasababu za kumshukuru MUNGU kwa muujiza aliomtendea wa kubeba mimba uzeeni, au kwa nia ya kuepusha uadui kutoka kwa watu ambao ungetokana na wivu, au pengine kwasababu nyingine za kupumzika na kumtafakari MUNGU kwa faragha!. Mojawapo ya hizo au zote zaweza kuwa sababu za kujitenga kwake.

Na tunaona lilikuwa ni jambo jema kwa Elisabeti kwani baadaye alipokutana na Mariamu ndugu yangu, alijazwa Roho Mtakatifu na kuzungumza  kiusahihi habari za Mariamu na Bwana Yesu aliye tumboni mwa Mariamu.

Hiyo inatufundisha nini?

Si kila Baraka kutoka kwa MUNGU inapokuja ni wakati wa kutangaza na kushuhudia wakati huo huo, wakati mwingine ni vizuri kujitenga/kutawa kwa muda ili kutumia kumshukuru MUNGU, na kuomba ulinzi wa Baraka ile,..kuwahi kutangaza Baraka za MUNGU au mlango MUNGU aliokufungulia kabla ya kupata utulivu ni hatari kwako na kwa utakaoenda kuwaambia.

Hivyo ni vizuri kutokuwa mwepesi wa kuzungumza bali ni vizuri kuwa mwepesi wa kupata faragha na MUNGU na kutafakari fadhili zake kabla ya kuzungumza au kushuhudia.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MARIAMU AKUTANA NA ELISABETI.

Yohana aliwatiaje waasi akili za wenye haki? (Luka 1:17)

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

JE BIKIRA MARIAMU ALIZAA WATOTO WENGINE?

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

Print this post

Yohana aliwatiaje waasi akili za wenye haki? (Luka 1:17)

Jibu: Turejee kuanzia ule mstari wa 11..

Luka 1:11 “Akatokewa na malaika wa Bwana, amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia.

12 Zakaria alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.

13 Lakini yule malaika akamwambia, Usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yohana.

14 Nawe utakuwa na furaha na shangwe, na watu wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.

15 Kwa sababu atakuwa mkuu mbele za Bwana; hatakunywa divai wala kileo; naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mamaye.

16 Na wengi katika Waisraeli atawarejeza kwa Bwana Mungu wao.

17 Naye atatangulia mbele zake katika roho ya Eliya, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, NA KUWATILIA WAASI AKILI ZA WENYE HAKI, NA KUMWEKEA BWANA TAYARI WATU WALIOTENGENEZWA”.

Haya ni maneno ya Malaikaa aliyokuwa anamwambia mzee Zakaria kuhusu mtoto atakayezaliwa (ambaye ni Yohana Mbatizaji), kwamba mtoto huyo atajazwa Roho Mtakatifu tangu akiwa tumboni, na atatembea na roho (yaani huduma) ya Eliya, lakini pia atawatejeza wengi wa Mungu, na kumwekea Bwana tayari watu waliotengenezwa, na zaidi sana KUWATILIA WAASI AKILI ZA WENYE HAKI!

Sasa kabla ya kutazama ni kwa namna gani Yohana Mbatizaji “aliwatilia waasi akili za wenye haki” hebu kwanza tutazame alimwekeaje Bwana tayari watu waliotengenezwa..

Ikumbukwe kuwa baadhi ya wanafunzi wa Bwana YESU kabla ya kuwa wanafunzi wa Bwana Yesu walikuwa kwanza wanafunzi wa Yohana mbatizaji.. baadhi ya hao walikuwa ni Andrea na nduguye Petro (Soma Yohana 1:35-41).

Kwahiyo akina Andrea na wengine ni watu waliotengenezwa kiroho kabla ya kuanza kutembea na Bwana, hivyo kwao haikuwa ngumu kumwamini Bwana au kumwelewa.. (hiyo ndio maana ya kumwekea tayari Bwana watu waliotengenezwa)

Sasa terejee sehemu ya Pili ambayo ni “Kuwatilia waasi akili za wenye Haki

Hapa kuna mambo mawili, 1. Waasi, 2.Akili za wenye haki.

Waasi wanaozungumziwa hapo ni Wana wa Israeli ambao wameiasi sheria ya MUNGU na kumwacha Mungu (Soma 2Nyakati 29:6), Na anaposema “akili za wenye haki”.. maana yake zipo “akili za wasio haki” maana yake akili za watu wasiomjua MUNGU, Lakini akili za watu wanaomjua MUNGU/wenye haki ni zile zinazomfanya Mtu amwangalie Muumba wake katika jicho la usafi na utakatifu, ndio zile alizowaambia katika Luka 3:8-14..

Luka 3:7 “Basi, aliwaambia makutano ya wale waliomwendea ili awabatize, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?

8 Basi, toeni matunda yapatanayo na toba; wala msianze kusema mioyoni mwenu, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba katika mawe haya Mungu aweza kumwinulia Ibrahimu watoto.

9 Na sasa hivi shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.

10 Makutano wakamwuliza, Tufanye nini basi?

11 Akawajibu akiwaambia, Mwenye kanzu mbili na ampe asiye na kanzu; na mwenye vyakula na afanye vivyo hivyo.

12 Watoza ushuru nao wakaja kubatizwa, wakamwuliza, Mwalimu, tufanye nini sisi?

13 Akawaambia, Msitoze kitu zaidi kuliko mlivyoamriwa.

14 Askari nao wakamwuliza, wakisema, Sisi nasi tufanye nini? Akawaambia, Msidhulumu mtu, wala msishitaki kwa uongo; tena mtoshewe na mshahara wenu”.

Akili za wasio haki, zinafundisha DINI tu, kwamba wao ni wayahudi wanaye Baba ambaye ni Ibrahimu, kwahiyo ni uzao mteule, lakini akili za wenye haki zinafundisha kwamba pamoja na kwamba wanaye Baba ambaye ni Ibrahimu bado wanapaswa kujitakasa maisha yao ili wakubaliwe na MUNGU, kuwa tu mwana wa Ibrahimu haitoshi, inahitaji matendo yanayoendana na hiyo Imani.

Hivyo wengi walipojua hilo walitubu na kumrudia Mungu kwa matendo yao.

Hali kadhalika hata leo tunahitaji hizi akili za wenye haki.. hatuwezi kusema sisi ni wakristo wenye madhehebu makubwa, na majina mazuri ya kibiblia halafu matendo yetu hayaendani na asili ya imani yetu, ni lazima tupate akili za wenye haki.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je kuna Yohana wangapi katika biblia?

Je biblia inajichanganya kwa habari za Yohana kuwa Eliya?

YOHANA MBATIZAJI

Nini maana ya “SAA INAKUJA” na “SASA IPO” (Yohana 4:23).

MGAWANYIKO WA ISHARA ZA UJIO WA BWANA YESU KRISTO.

Print this post

ENDELEZA UPONDAJI.

Mwanzo 3:15

[15]nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa..

Kitu pekee Ambacho kilitabiriwa kuweza kuvunja vichwa vya majoka(shetani), ni uzao wa mwanamke tu. Aliyetabiriwa kwenye (Mwanzo 3:15)

Uzao huu wa mwanamke ni Yesu Kristo.. kwasababu ni yeye tu pekee ndiye aliyezaliwa Bila mwanamume, sisi wote ni uzao wa mwanamume…kwasababu mbegu yetu imetoka kwa Baba zetu, lakini Kristo ni mbegu iliyoshuka Kutoka mbinguni, ndio maana hapo anatajwa Kama uzao wa mwanamke.

Yeye kwa ushindi alioupata dhidi ya nguvu za giza kwa kufufuka kwake kutoka kwa wafu na kupaa mbinguni..ni pigo Kubwa sana kwa shetani, ambalo lilimlenga moja kwa moja katika kichwa chake.

Kwasababu kwa njia hiyo wanadamu tumevuka kutoka mautini kwenda uzimani…

Lakini habari njema ni kuwa yeyote amwaminiye, anakuwa sehemu ya uzao huo kwa imani. Na hivyo anapokea mamlaka ile ile ya kuvunja mafuvu ya majoka…mpaka ufalme wa giza kutokomea kabisa katika uso wa ulimwengu..

Wagalatia 3:29

[29]Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.

Luka 10:19

[19]Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Kumbuka uwezo huu, hakuna uzao mwingine wowote unaoweza kumuharibu shetani, waafrika hawawezi, wazungu hawawezi, wachina hawawezi, waarabu hawawezi, ukoo wa kiyahudi hauwezi, familia za kichifu, haiwezi, wanadamu wote hawawezi kuponda majoka, hata waungane kwa vifaru vyao na makombora ya nyuklia, bado hawawezi kinyume chake wao ndio watafanyika chakula cha hao majoka.Ni uzao mmoja tu wa Yesu Kristo ndio wenye nguvu hizo..

Swali ni je! Tunapondaje vichwa vya majoka.

Ni kwa kuendelea kuhubiri. Ukikaa tu bila kushuhudia habari za Kristo kwa wenye dhambi, kukaa bila kujishughulisha na shamba la Bwana..Fahamu kuwa ‘mabuti’ yako uliyopewa huko miguuni huyatendei Haki..yapo tu!

Unamridhia shetani, unafurahishwa na uwepo wake shambani mwa Bwana, ndugu njia pekee inayomdosha shetani kwa wepesi ni wewe kukutana na mwenye dhambi mmoja na kumshuhudia habari za wokovu.

Mitume walipoenda kuhubiri baada ya kutumwa na Yesu, waliporudi na ushindi, Yesu aliwaambia nalimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme..

Luka 10:18

[18]Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.

Simama tumia mabuti yako vizuri, endeleza kuponda, ponda kweli kweli, haribu kisawasawa, kwa njia ya injili.

Sio kwa kuimba “nakuponda shetani” au

Kusema “toka shetani” bali kwa injili

Kuponda kwingine ni maombi na kuishi maisha ya utakatifu, huku nako kunahubiri injili ya Kristo na hivyo shetani anaumizwa vibaya sana.

Amka tumia buti zako, kila kichaka katika shamba la Bwana ambacho majoka yamejificha Ni kwenda kuponda tu, mpaka habari njema za ufalme zifike ulimwenguni kote.

Bwana awe nawe.

Amen.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

IHUBIRI INJILI, KILA MAHALI KWASABABU AKUZAYE NI MUNGU.

INJILI NI UWEZA WA MUNGU, UULETAO WOKOVU.

MBONA MMESIMAMA HAPA MCHANA KUTWA BILA KAZI?

Print this post