Title 2019

NABII MUSA.

Musa alizaliwa huko Misri, miaka mingi kidogo baada ya Yusufu mwana wa Yakobo kufariki. Wakati wa kuzaliwa kwake, mama yake alimhifadhi mtoni kutokana na hofu ya amri ya Mfalme juu ya kuuawa kwa wazaliwa wote wa jinsia ya kiume.

Jina la Baba yake Musa ni Amramu na Mama yake ni Yokebedi. (Hesabu 26:59).

Musa alikuwa na Kaka yake wa damu aliyeitwa Haruni waliokuwa wamepishana miaka 3, Haruni alikuwa mkubwa kwa Musa, na ndiye yule aliyekuja kuwa Kuhani Mkuu, pia alikuwa na dada yake aliyeitwa Miriamu ambaye naye pia alikuwa ni Nabii wa Bwana.

Bithiani aliyekuwa Binti wa Farao alimwokota akiwa kwenye kijisafina kidogo, pembezoni mwa mto wakati akiwa anaoga. Musa aliishi katika Nyumba ya kifalme mpaka alipofikisha umri wa miaka 40, Baadaye aliasi nyumba ya Farao kutokana na kumsaidia mmoja wa ndugu zake wa Kiebrania, akakimbilia nchi ya Midiani. Huko alipata mke kutoka kwenye nyumba ya kuhani mmoja wa Midiani aliyeitwa Yethro.

Alikaa miaka 40 nyumbani kwa Yethro, akichunga mifugo yake, mpaka siku moja Bwana alipomtokea katika mwali wa moto, ndani ya kile kijiti, alipokuwa anachunga kundi la Yethro, Alipewa maagizo ya kuwaokoa Israeli waliokuwa wanateswa chini ya utawala mkali wa Farao.

Kwa Ishara nyingi na miujiza mingi Musa aliwaongoza wana wa Israeli miaka 40 mingine, na Alifariki akiwa na miaka 120, akiwa na nguvu zake zote. Macho yake hayakupofuka wala mwili haukupungua nguvu (Kumbukumbu 34:7)

Musa pekee ndiye Nabii aliyezungumza na Mungu uso kwa uso, wala baada yake hakuinuka nabii mfano wake yeye (Kumbukumbu 34:10-12)

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

1.Utaji uliokuwepo juu ya uso wa Musa ulikuwa unaashiria nini?

2.Haruni ni nani?

3. Miriamu ni nani?

HOME

Print this post

YEZEBELI ALIKUWA NANI

Yezebeli, alikuwa ni Binti wa Mfalme wa Wasidoni aliyeitwa Ethbaali (1 Wafalme 16:31). Sidoni ilikuwa ni nchi iliyokuwepo Kaskazini mwa Taifa la Israeli, kwasasa nchi hiyo ni nchi ya LEBANONI.

Desturi za Wasidoni zilikuwa ni kuabudu miungu, waliabudu mungu wao maarufu aliyeitwa BAALI.

Mfalme wa Israeli aliyeitwa Ahabu alimwoa Binti huyo wa kifalme na kumleta katika Taifa la Israeli na kuwa Malkia. Na hivyo kuingiza ibada za miungu migeni ndani ya Taifa la Mungu.

Yezebeli licha tu ya kulichafua Taifa la Israeli kwa kumshawishi sana Mumewe Ahabu, alikuwa pia ni mchawi (2 Wafalme 9:22). Aliwaua manabii wengi wa kweli wa Mungu, na aliikosesha Israeli kwa sehemu kubwa sana. Mahali pengine Inamtaja Yezebeli kuwa ni Nabii wa Uongo. (Ufunuo 2:20)

Yezebeli pia ndio mwanamke pekee kwenye Biblia nzima aliyekuwa anapaka WANJA usoni na kupamba uso. Desturi za wanawake makahaba.(2 Wafalme 9:30). Mwanamke huyu ndiye Mwanamke pekee aliyeshindana na maagizo ya Mungu kuliko wanawake wote kwenye Biblia, ndiye aliyemsumbua sana Eliya na hata kufikia hatua Nabii Eliya kumkimbia, kuogopa madhara atakayoyapata kutoka kwake.

Yezebeli alikuwa na mtoto wa kike, aliyeitwa ATHALIA ambaye naye alirithi tabia zote za mama yake ambaye naye pia alikuwa anaabudu Baali, Athalia alikuwa muuaji na aliutwaa umalkia kwa nguvu ndani ya kabila la YUDA.

Yezebeli hakudumu muda mrefu kwani alikufa sawasawa na unabii uliotolewa juu yake, kwamba atakufa na mbwa watalamba damu yake. Siku ya kufa Yezebeli aliangushwa kutoka juu ya ghorofa refu na kuchuruza damu ukutani mwote, na alipofika chini farasi alimkanyaga kanyaga..na Mbwa walikumla na kubakisha viganja tu vya mikono na kifuvu (2 Wafalme 9:35)

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

NABII ELIYA NI NANI?

Rudi Nyumbani

Print this post

Shetani ni nani?

Shetani ni nani?…Tafsiri ya Jina shetani ni ‘mshitaki’ au ‘mchongezi’.  Kazi yake ni kuwashitaki watakatifu mbele za Mungu.

Jina lingine la shetani ni “LUSIFA” Maana yake ‘NYOTA YA ALFAJIRI’. (Isaya 14:12) Jina  hili Lusifa aliitwa kabla hajaasi, baada ya kuasi ndio akawa shetani.

Alikuwa ni Malaika wa Sifa (Kerubi) huko mbinguni, alikuwa ni Mzuri kwa mwonekano na mkamilifu katika njia zake zote, aliishi katika taratibu za Mungu, na katika njia za Mungu,  na hivyo akapata heshima kubwa mbinguni zaidi ya Malaika wengi (Ezekieli 28:14).. Alikuwa mkamilifu mpaka siku uovu ulipoonekana ndani yake (Ezekieli 28:15).

Kwasababu ya uzuri wake Moyo wake ukainuka, akataka kujiinua awe kama Mungu, aabudiwe kama Mungu na kwa ujuzi wake mwingi akawashawishi theluthi ya Malaika mbinguni (1/3) waambatane naye.

Vita, vikali vikatokea Mbinguni kati ya Malaika waliokataa kuungana na Lusifa na malaika waliokubali kuungana naye. Biblia haisema vita hivyo vilipiganwa kwa muda gani, lakini inasema mwisho wa siku lusifa pamoja na malaika wake walishindwa vita vile, na kutupwa chini duniani (Ufunuo 12:7).

Na vita hivyo bado havijaisha, vita vya kwanza vilipiganwa mbunguni, kati ya Malaika walio upande wa shetani na wale walio upande wa Mungu na Malaika waliokuwepo Upande wa Mungu wakavishinda, lakini vita vya pili na vya mwisho vinapiganwa hapa duniani na hata sasa bado vinaendelea..Na vitaisha mwisho wa dunia. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

1. Je! Ni nani aliyemdanganya shetani?

2. Huduma 10 za shetani sasahivi duniani ni zipi?

3. Mpango wa shetani kwa watoto katika siku hizi za mwisho.

4. Agenda kubwa ya shetani kwa kanisa hili la siku za mwisho

5. Mafundisho ya Mashetani ni yapi katika siku hizi za mwisho?

6. Kazi ya Malaika watakatifu sasa ni nini?

HOME

Print this post

Yohana Mbatizaji anaigeuzaje mioyo ya mababa iwaelekee watoto?

Malaki 4:5 kama inasema  angalieni nitawapelekea Eliya Nabii, kabla haijaja siku ile ya BWANA, iliyo kuu na ya kuogfya. Naye ataigeuza mioyo ya Baba iwaelekee watoto wao na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana.”

Kama Mungu alivyoahidi angemtua Eliya nabii. ambaye kulingana na maandiko tunafahamu Yohana mbatizaji aliyatimiza hayo maandiko ( Yaani kuja kabla ya ile siku KUU YA BWANA) ambaye yeye alitangulia kuja kwake Kristo kwa mara ya kwanza kwa kusudi la kuigeuza Mioyo ya Baba iwaelekee Watoto.

Hii inamaanisha kwamba Yohana alihubiri injili ya kuwarejeza waalimu wa sheria na marabi wa torati pamoja na wote wanaoujia torati na kuifuatilia (ambao ndio mababa wa Torati) ili waiamini injili ya Kristo.

Na tonaona…Baadhi ya wanafunzi wake mwenyewe Yohana, waliiamini Injili yake na baadaye hao hao wakaja kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo, (mfano Andrea na Yohana) ambao walikuwa hapo kwanza wanafunzi wa Yohana Mbatizaji lakini wakaja kuwa wanafunzi wa Bwana Yesu..na ndio sasa mababa wetu wa Imani ya Kikristo leo.

Hivyo Yohana mbatizaji kazi aliyoifanya ni kuwageuza Mababa wa Torati kuwa Mababa wa Imani ya Kristo na mioyo ya watoto iwaelekee mababa.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

HOME

Print this post

YOHANA MBATIZAJI

Yohana Mbatizaji alizaliwa huko Uyahudi miezi michache kabla ya kuzaliwa Mwokozi wa Ulimwengu Yesu Kristo, Baba yake mzazi aliitwa Zekaria aliyekuwa Mlawi, ambaye alikuwa ni kuhani, akihudumu katika Nyumba ya Mungu illiyokuwepo huko Yerusalemu…Mama yake aliitwa Elizabeth ambaye alikuwa ana undugu wa karibu na Bikira Mariamu mama yake Yesu.

Habari za kuzaliwa kwake kimiujiza,  zinapatikana kwa urefu katika kitabu cha (Luka 1:1-60).

Maandiko yanasema Yohana Mbatizaji alijazwa Roho Mtakatifu tangu akiwa tumboni mwa mama yake (Luka 1:15). Na inasadikiwa kuwa miaka michache sana baada ya kuzaliwa kwake wazazi wake wote wawili walifariki. Na hivyo akaondoka na kwenda kukaa majangwani, mpaka siku alipotokea tena hadharani kuhubiri habari za msamaha na toba.

Aliitwa Yohana Mbatizaji kutokana na ufunuo alioupata wa ubatizo. Hapo kabla kulikuwa hakuna mwingine aliyekuwa anafanya ubatizo Zaidi yake, ndio maana alijulikana kama Yohana Mbatizaji, kumtofautisha na wakina Yohana wengine.

Yohana Mbatizaji sio Yohana yule aliyeandika kitabu cha Ufunuo, aliyeandika kitabu cha Ufunuo ni Yohana aliyekuwa mwanafunzi wake Yesu. Yohana Mbatizaji hakuandika kitabu chochote katika Biblia

Yohana Mbatizaji, maandiko yanasema alikuwa ndiye Eliya aliyetabiriwa atakayekuja kumtengenezea Bwana Njia (Luka 1:17). Atakayeigeuza mioyo ya baba iwaelekee Watoto.

1. Yohana Mbatizaji anaigeuzaje mioyo ya mababa iwaelekee watoto?

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

HOME

Print this post

Je! Ni Eliya mwenyewe atarudi au ni roho yake?

Tofauti na inavyodhaniwa na wengi kuwa Nabii Eliya mwenyewe ndiye atakayerudi.

Ili kuelewa vizuri juu ya jambo hilo hebu tafakari mfano ufuatao.

Ametokea kiongozi mmoja mashuhuri sana wa mambo ya kisiasa na akaleta mabadiliko makubwa sana katika taifa hilo, tuchukulie mfano Aliyekuwa Raisi wa Taifa la Tanzania, Hayati J. K. Nyerere baada ya kufa kwake, mwananchi mmoja akatabiri, Miaka ya huko mbeleni watazaliwa wakina Nyerere wengi ambao watafanya kama alivyofanya Baba wa Taifa.

Je! kwa sentensi hiyo ni sawa na kusema, Nyerere atazaliwa tena yule yule aliyefariki na kuishi na kuja kuwa Raisi tena?..Ni wazi kuwa hiyo siyo tafsiri yake, tafsiri yake ni kwamba atazaliwa au watazaliwa watu ambao watakuja kuwa mashujaa kama Nyerere

Na ndivyo ilivyo kwa unabii wa ujio wa Eliya, sio kwamba ni Eliya yule yule atazaliwa tena hapana bali atakuja mtu au watu watakaobeba huduma inayofanana na ya Eliya.

Na mtu wa Kwanza aliyeibeba huduma hiyo baada ya Eliya mwenyewe alikuwa ni Nabii Elisha na baada ya Elisha alifuata Yohana Mbatizaji..

1.Yohana Mbatizaji ni nani?

HOME

Print this post

NABII ELIYA

Historia inaonesha Nabii Eliya aliishi karne ya 9 kabla ya Kristo,  Ni Nabii aliyeshindana sana na Utawala wa kipagani wa Mfalme Ahabu wa Israeli na mkewe Yezebeli.

kadhalika Biblia hairekodi kama alikuwa na mke wala Watoto. Wala haielezi huduma yake aliifanya kwa miaka mingapi.

Miujiza mingi iliambatana na Nabii huyu, Miujiza maarufu iliyoambatana na Nabii huyu ni ule wa  KUSHUSHA MOTO na ule wa KUCHUKULIWA JUU NA MAJESHI YA FARASI.

Katika kitabu cha Malaki 4:5, biblia imeahidi kurudi tena kwa Nabii huyu.

1.Je! Ni Eliya mwenyewe atarudi au ni roho yake?

2.Je! Kazi ya Eliya atakaporudi itakuwa ni ipi?

3. Yezebeli ni nani?

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

HOME

Print this post

MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?


Siku moja nilikuwa ninamsikiliza Mh.Raisi akizungumza na wafanyabiashara Ikulu, nikapata kitu ambacho kiuhalisi ndio kinachoendelea katika Ukristo isipokuwa tu ni katika upande mwingine wa shilingi. Kwa kawaida mimi sio mfuatiliaji wa mambo ya siasa, lakini siku hiyo nilijikuta ninasikiliza mahojiano kati ya Raisi na wafanyabiashara ikulu ni hotuba wakipeleka changamoto zao na malalamiko yao wanayokumbana nayo katika taasisi cha kiserikali hususani TRA….Wengi wao walipewa nafasi ya kutoa kilicho moyoni mwao..Na baadaye Raisi akasema hawa watu wa taasisi za umma, wanatumia kauli mbiu yake ya kuchapa kazi, ili kuwakandamiza wafanyabiashara na wananchi kwa kuwapa makadirio makubwa kushinda uwezo wao wa kulipa..Na wakishamaliza kuwakandamiza wanatumia kauli ya HAPA KAZI TU!, yaani kwa lugha nyepesi tunaweza kusema wanaongezea makali kile Raisi anachokiamini kwa kutimiza matakwa yao binafsi, ambayo hayalengi kujenga bali kubomoa ..Hilo ni jambo ambalo lilimuhuzunisha sana Mh Raisi.

Sasa ukiangalia, ni kweli kauli mbiu ya Raisi ni kuwa kila mtu achape kazi, lakini hakuwa na lengo la kumaanisha kuzidi mipaka hadi kuwakandamiza watu wenye nia njema ya kulijenga Taifa..Bali kanuni hiyo ilikuwa inalengo la kuwahamasisha wananchi wafanya kazi kwa bidii..

Leo hii ukirudi katika ukristo utakutana pia na hili neno maarufu, “Hatuishi chini ya Sheria, bali tupo chini ya neema”(Warumi 6:14)..Na hivyo Mungu haangalii matendo yetu bali Roho zetu…Ukiangalia ni kweli kabisa biblia inatuambia hivyo, lakini tunashindwa kufahamu Neno hilo lilikuwa linawahusu watu wa namna gani..

Neno hilo lilikuwa linawahusu watu waliokuwa ndani ya Kristo na wala sio walio nje ya Kristo, ikiwa na maana kuwa katika bidii yako ya kuishi maisha ya kumpendeza Mungu ndani ya Kristo, Usihesabu kuwa hicho ndicho kinachokupa uhalali kwa kukubaliwa na Mungu au kwenda mbinguni..,Hapana, mbinguni ni mahali patakatifu sana, hakuna kinyonge kitakawezakuingia na kama hivyo hakuna mtakatifu yoyote ambaye angestahili kwenda mbinguni isipokuwa YESU KRISTO tu peke yake kwasababu yeye ndiye hakuwahi kutenda dhambi yoyote tangu kuzaliwa kwake hadi kufa kwake..

Hivyo ili na sisi tuhesabiwe kama watakatifu basi neema lazima ichukue nafasi yake, lakini huku tukiwa bado ndani ya Kristo, na tukijitahidi kuishi maisha makamilifu na matakatifu kwa kadiri tuwezavyo..Lakini leo hii utakuta, mtu anatembea uchi barabarani, anavaa vimini na suruali kama soksi, na bado anajiita mkristo, ukimuuliza kwanini unafanya hivi . Anakwambia Biblia inatuambia hatuishi chini ya sheria bali chini ya neema, Mungu haangalii vya nje bali vya ndani.

Hata mtu aliye nje ya wokovu utamsikia akizungumza maneno hayo hayo, hatupo chini ya sheria bali chini ya neema. Nataka nikuambie, biblia inasema katika siku za mwisho maneno haya ..“lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika. (2Timotheo 3:13)..

Usikubali kudanganyika, Maovu yanavyozidi kuongezeka shetani ndivyo anavyotumia silaha ile ile ya maandiko kudanganya watu wengi. Kama vile tu alivyojaribu kutumia silaha hiyo kumdanganya Bwana Yesu kule jangwani…Ukiendelea na mtazamo huo kuwa tunaokolewa kwa neema na sio kwa matendo na huku unafanya mambo maovu kwa makusudi, unawasababishia wengine watende dhambi ya kutamani kwa ajili yako, kuwa na uhakika tu siku ile utahukumiwa na Mungu kwa kushindwa kulipambanua Neno la Mungu ipasavyo.

Warumi 6:15 “Ni nini basi? Tufanye dhambi kwa sababu hatuwi chini ya sheria bali chini ya neema? Hasha!

16 Hamjui ya kuwa kwake yeye ambaye mnajitoa nafsi zenu kuwa watumwa wake katika kumtii, mmekuwa watumwa wake yule mnayemtii, kwamba ni utumishi wa dhambi uletao mauti, au kwamba ni utumishi wa utii uletao haki.”

Na Neno lingine lililo maarufu leo hii, utalisikia kila mahali ni hili ‘Usihukumu usije ukahukumiwa’..Na kwamba ikitokea mtu anahubiri kuwa walevi wote na waasherati wataenda motoni, kama biblia inavyosema anaambiwa kuwa anahukumu…Lakini mtu huyo huyo yupo tayari kumweleza kwa uwazi wote mtoto wake ikiwa anapotea mwisho wake utakavyokuwa, utasikia anamwambia usiposoma mwanangu, utaishia kuwa teja, au kuwa kibaka, au kuwa maskini…hilo kwake haoni kama ni hukumu, lakini yeye akihubiriwa kwamba endepo akiendelea kuwa mlevi ataishia jehanamu ya moto utasikia anakumbia unahukumu, mwenye uwezo wa kuhukumu ni Mungu tu!…Hiyo yote ni kutokana na kushindwa kulichambua vizuri neno la Mungu. Utakapokwenda mahali popote ukaanza kuwafundisha tu watu wadhara ya dhambi na mwisho wake ni upi, utasikia wakisema unawahukumu..

Na mambo mengine mengi tu, ya namna hiyo. Hivyo tunapaswa tukae mbali na misemo hiyo, ambayo inatumia kivuli cha maandiko kusitiri maovu na mabaya. Kwasababu siku ile Mungu hatakuwa radhi na sisi.

Kama bado haujafahamu thamani ya kuwa ndani ya Kristo, ni vema ufanya hivyo sasa kabla ya mlango wa neema haujafungwa..Unachopaswa kufanya ni kutubu kwa kumaanisha kabisa kuacha kufanya dhambi, kisha tafuta mahali wanapobatiza ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi, na kwa Jina la BWANA YESU KRISTO, upate ondoleo la dhambi zako kama bado hujafanya hivyo..kisha Uukulie wokovu mpaka siku ya kunyakuliwa..

Ubarikiwe sana. Tafadhali “Share” Ujumbe huu kwa wengine. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

1.Angalieni Jinsi Msikiavyo

2. Umesikia inavyopaswa?

3. Je! Una masikio yanayosikia?

.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Print this post

HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA.


Jina la Bwana Yesu Kristo, libarikiwe…

pamoja na kazi nyingine nyingi anazozifanya Roho Mtakatifu juu ya mtu aliyemwamini Yesu Kristo, nyingine ni kumwongoza katika kuijua kweli yote…Hilo tunalisoma katika..

Yohana 16:13“ Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake”

Neno kuongoza halina tofauti sana na kuelekeza, yaani mtu anayekuelekeza jambo Fulani hatua kwa hatua, mpaka kufikia hitimisho analotaka yeye ufikie, hana tofauti na mwongozaji…na kazi ya mwelekezaji au mwongozaji, sio tu kuonesha njia pekee bali hata kurekebisha baadhi ya makosa..Kwamfano mtu anapotaka kukuongoza kufika mahali Fulani, halafu wewe unampa mashauri yako ya njia ya kuipitia, ni wazi kuwa kama hayo mashauri yako sio sahihi basi atakurekebisha kwa nia ya kukuelekeza njia iliyo bora zaidi.

Na ndivyo ilivyo kwa Roho Mtakatifu, yeye ni mwongozaji wetu, na Roho Mtakatifu ndio jambo la kwanza kabisa mtu aliyemwamini Kristo anapaswa kuwa naye…Biblia inasema mtu asiye na Roho Mtakatifu huyo sio wake (Warumi 8:9) Ikiwa na maana kuwa mtu asiye na Roho Mtakatifu, hakuna uongozi wowote wa KiMungu unaoendelea juu ya Maisha yake..Ni kupotea tu!.

Hivyo mtu aliyeamini, katika hatua za awali kabisa, anakuwa hajui vitu vingi, hiyo ni kawaida kabisa, anakuwa kama mtoto mdogo aliyezaliwa, ambaye hajui chochote katika maisha haya, na vivyo hivyo mtu aliyezaliwa mara ya pili anakuwa ni mdhaifu katika roho. Lakini pamoja na udhaifu huo kunakuwa na kitu ndani yake kinachomfanya aelewe mambo mengi kwa muda mfupi kwasababu anakuwa na moyo wa unyenyekevu wa kutaka kujua au kufahamu Zaidi kuhusu Mungu, kama mtoto mchanga… hiyo Kiu ni ambayo Roho Mtakatifu kaiweka mwenyewe ndani ya mtu, ili itumike katika mstari wa kuwa chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu.

Roho Mtakatifu anaanza kumvuta, kidogo kidogo na kumtoa hatua moja hadi nyingine, aielekee njia ya utakatifu, ndio hapo mtu ataanza kutoka katika ulimwengu na kuona sababu ya kutafuta kanisa Fulani ambalo angalau ataweza kuipooza ile kiu iliyopo ndani yake ya kutaka kumjua Mungu…Atatoka kwenye dhambi na hatimaye kujiunga kanisa Fulani, atapata vitu ndani ya lile kanisa ambavyo vitamsisimua sana na kumfanya kukua kiroho kwa kiwango Fulani..na atakapofika mahali na kuona hali yake ya kiroho ipo pale pale, baada ya kukaa muda mrefu, kuna kitu kitamwambia hapo ulipo bado unahitaji kuwa na Mungu zaidi…..hiyo nguvu itamsukuma kutafuta hazina mpya ya chakula cha kiroho kwa hali na mali, utaona anazidi kutafuta mahali ambapo atapata chakula kilichobora zaidi…lengo lake sio kuhama kanisa au dhehebu hapana!.

Bali lengo lake ni kupata kuweka sawa hatima ya Maisha yake ya kiroho…Tofauti na wengi wanaohama makanisa sasahivi ni kwasababu tu wamesengenywa kidogo, au kwasababu wanahitilafiana na mchungaji wake kwa masuala ambayo hata sio ya kiimani, au kwasababu wanakemewa waache dhambi, au kwasababu wanataka kuolewa au kuoa, au kwasababu wamechoka tu kukaa pale na hivyo wanajaribu ladha mpya n.k…

Aliye na Roho Mtakatifu kweli haondoki mahali kwasababu kama hizo…Kinachomwondoa sehemu moja hadi nyingine ni ile kiu iliyopo ndani yake ya kutaka kumjua Mungu Zaidi, na anakuwa hana kiburi…Mahali alipokuwa anakaa hapo kwanza walikuwa hawana utaratibu wa maombi ya mfungo, hivyo anaona kuna kitu ndani ya roho yake kimepunguka anahitaji kuwa mwombaji zaidi na msomaji wa maandiko zaidi, kwahiyo anatafuta mahali ambapo atakuwa mwombaji Zaidi…Au mahali alipo kuna mchanganyiko wa Neno la Mungu na mambo ya ulimwengu huu hivyo anaondoka kwenda kutafuta mahali atakapoishibisha roho yake na Neno lisilochanganywa.

Au pengine mahali alipokuwa anakaa hakukuwa na desturi za kwenda kufanya uinjilishaji, na yeye anaona kuna kiu ndani yake ya kwenda kuwahubiria wengine habari njema popote pale, na hivyo mahali alipo haiwezekani kufanya hivyo, kwahiyo anaondoka kwenda mahali ambapo atatimiza agizo hilo la Bwana Yesu la kwenda kuhubiri injili kwa kila kiumbe..

Au pengine mahali alipokuwepo kunafanyika ibada za sanamu, na baada ya kuyachunguza maandiko vizuri anaona si sawa kufanya jambo hilo, na hivyo anaondoka kwenda kutafuta mahali ambapo hataabudu sanamu tena n.k.

Sasa katika hatua zote hizo utaona mtu huyu wa Mungu anaweza akawa ameshatembea sehemu nyingi zote akitafuta kukaa mahali salama….Na anavyozidi kusogea mbele ndivyo anavyozidi kuwa bora zaidi katika Imani. Na mtu anayekua kutoka sehemu moja hadi nyingine anakuwa hatamani tena kurudia yale ya nyuma…kwamfano mahali alipokuwepo ni mahali ambapo palikuwa hakuna utaratibu wa kusali au kuomba, wala palikuwa hakuna msisitizo wa kuishi maisha matakatifu akishatoka hapo hawezi tena kutamani kurudia hapo..

Sasa jambo hilo la kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa lengo la kutafuta Usalama wa maisha yako ya kiroho, na si sababu nyingine tofauti na hizo…sio dhambi! Bali ni kazi ya Roho Mtakatifu katika kukuongoza na kukuweka katika kweli yote…

Hiyo ndio kazi ya Roho Mtakatifu kutuhakikisha hatukwami sehemu moja kila siku bali tunakuwa kuufikia utimilifu,

Kosa moja linalofanyika na watu wengi, ni kujaribu kutafuta dhehebu Fulani la kuhamia na kutafuta lililobora zaidi ya lingine kwa kuangalia watu wengi wanakwenda wapi, au kwa kusikiliza ushauri wa watu, au kwa kuangalia uzuri wa kanisa….lakini hawasikilizi msukumo wa Roho Mtakatifu ndani yao, ambaye huyo ndiye angewaongoza katika kuwatia kwenye kweli yote…

Binafsi nimekutana na watu wengi, wakiniuliza nimeamini sasa nihame hapa niende kanisa gani?…Binafsi huwa nakosa jibu la hili swali..kwasababu Mungu hakuanzisha madhehebu, na Roho Mtakatifu hamwongozi mtu kwenda kwenye dhehebu lolote bali anamwongoza katika kuijua kweli…..Hiyo njaa na kiu ya Neno la Mungu ndio inayomsukuma mtu kutoka sehemu moja hadi nyingine kutafuta chakula, hivyo hata kama akikutana na chakula kilichochacha mbele yake atakula tu kwa huo muda ilimradi aweze kuishi..

Kanisa sio suluhisho la kuishi katika mapenzi ya Mungu, bali Roho Mtakatifu ndio suluhisho, unapokaa chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu kwa kuyasoma maandiko ndivyo unavyompa nafasi Roho Mtakatifu kukuonesha ni wapi ulikuwa unakosea, na ni wapi unapaswa urekebishe na ni wapi pa kukaa palipo salama…lakini sio kutafuta ushauri kutoka kwa watu, au kwa kuangalia ni wapi wengi wanakwenda. Wengi wanaofanya hivyo hakuna chochote katika maisha yao kitakachobadilika kwasababu ni sawa na wamehama dini moja na kujiunga na nyingine…huko wanakokwenda wanakwenda kuwa washirika wa dini tu na si wakristo halisi, na kuvamiwa na roho ya udhehebu ambayo ndiyo roho ya mpingakristo….roho ya kusema dini yangu inafundisha hivi, au dhehebu halisemi hivyo n.k Kumbuka madhehebu ya Mafarisayo na Masadukayo ndiyo yaliyoongoza kumpinga Bwana Yesu katika huduma yake…sasa roho hiyo hiyo ndiyo iliyopo katika madhehebu (yaani watu walioacha uongozi wa Roho Mtakatifu na kuwa washirika au washabiki wa dini)..Bwana alipokuwa anawaambia Mafarisayo hivi wenyewe wakawa wanasema Musa hakutufundisha hivyo, kwahiyo ikawafanya kuwa mbali na Mungu kuliko hata watu wa Ulimwengu wasio mjua Mungu, hiyo yote ni kutokana na Udhehebu na Udini uliokuwa ndani yao.

Ndio maana Biblia inatuambia tutoke huko (Ufu.18:4), Tunapomgeukia Roho Mtakatifu na kufuata uongozi wake ndio kutoka kwenyewe kunakozungumziwa hapo…yeye ndiye kiongozi wetu ambaye kila siku anarekebisha makosa yetu kulingana na Biblia na kutuweka katika mstari.

Usianze kutafuta kanisa la kwenda sasa, anza kutafuta maandiko yanasemaje kwanza…ndipo Roho atapokuongoza pa kwenda, Roho Mtakatifu anawaongoza watu wanaosoma maandiko sio wanaotafuta makanisa…

Bwana akubariki sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

MIISHO YA ZAMANI.

ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.

Shalom, mtu wa Mungu natumai u buheri wa afya kwa pumzi unayopewa na mwenyezi Mungu. Leo kwa furaha ya Bwana nakukaribisha tuutafakari ukuu wa Mungu na matendo yake jinsi yalivyo makuu.

Tabia mojawapo ya Mungu ni kuwa, huwa hajisifii au kujionyesha moja kwa moja mbele za watu kuwa yeye ni mkuu, badala yake huwa anawaacha wanadamu wavumbue wao wenyewe kazi zake, na pale wanapoona mambo ya kutisha na kusema he! Kumbe na hili kalifanya yeye, kumbe na lile kalifanya yeye!, na yule mtu kumpa Mungu utukufu Sasa hapo ndipo Mungu anapoipokea sifa yenyewe. Tofauti na sisi wanadamu, Kwanza tunataka tusifiwe kwa kitu ambacho si chetu, pili tunapenda kuwaonyesha watu kuwa sisi tunacho, kwa lengo la kujitafutia utukufu bandia..

Sasa yapo mambo ambayo, laiti watu wa vizazi vya Nuhu wangeona, leo hii wasingeangamizwa, vile vile yapo mambo ambayo laiti watu wa Sodoma wangeyaona leo hii wangemuheshimu Munguna kumwogopa sana, Halikadhalika yapo mambo ambayo mitume wangeyaona kama tunavyoyaona sisi , leo hii wangemtukuza Mungu kwa nguvu zao zote..Vile vile yapo mambo ambayo Mfalme Daudi angeyaona leo hii angemwabudu Mungu Zaidi hata ya pale alipomwabudu alipodondokewa na nguo.

Sisi watu wa leo hii Teknolojia imeturahisishia mambo sana, na hivyo kwa kutumia simu zetu tu au computa au television tunaweza kuona uweza mwingi wa Mungu duniani kote.

Mfano zamani, watu walikuwa wakitazama juu, walikuwa wanaona nyota na mwezi tu peke yake, napengine walidhani kuwa kuvifikia hivyo sio mwendo sana lakini sisi tunaoishi kizazi hiki ndio tunajua, kumbe baadhi ya zile nyota tunazoziona ni Ma-Jua mengine mengi, kama tu jua letu hili, na kila nyota inayo sayari zake nyingi kama Jua letu hili lilivyo na sayari 9, Dunia yetu ikiwa ni mojawapo ya sayari hizo.

Sasa karibu kila kitu unachokiona angani, vyote hivyo ni kama punje moja kati ya nyingi. Kama vile punje moja ya mahindi katikati ya gunia, sasa punje yetu tuliyopo sisi ndio inaitwa Milky way galaxy(Giligili), ambayo inatengenezwa na mamilioni ya mifumo ya jua..Hivyo ukiendelea juu zaidi unakutana na punje nyingine ambayo pia inayo ma-jua yake mengi, na sayari zake mabilioni kwa mabilioni, kama hii yetu ya Milk-way nayo inaitwa Andromeda Galaxy, sasa jumlisha punje zote hizi za Magalaxy, katengeneza Mungu mmoja, inasemekana yapo magunia mengine kama hayo mabilioni kwa mabilioni, hapo bado haijasisha ukiyajumlisha magunia hayo yote unatengeneza tena rumbesa moja lijulikanalo kama Clusters, sasa hayo marumbesa nayo yapo mabilioni kwa mabilioni, nayo ukiyajumlisha utapata kitu kimoja kinachoitwa Super clusters, Hizi nazo zipo mabilioni kwa mabilioni, ukijumlisha unapata kitu kinachotwa Universe,…Na hizi Universe nazo zinaonekana zipo mabilioni kwa mabilioni ambayo hayo upeo wa wanasayansi wa sasa hawajaweza kugundua chochote kinachoendelea juu Zaidi ya hapo.

Sasa tukizungumzia kutoka kwenye mfumo wetu tu wa Jua, kutoka sayari moja hadi nyingine, yaani sayari iliyo karibu na sisi ujulikanayo kama Mars inaweza kukuchuka Zaidi ya miaka 57.4 kufika kama ukisafiri kwa gari lenye spidi ya juu sana..sasa jiulize kukatisha kutoka galaxy moja hadi nyingine inaweza kukuchukua miaka mingapi?

Inasemekana zipo sayari zenye mfano wa dunia hii, na nyingine Zaidi hata ya dunia hiii nazo hizo zipo Zaidi ya BILIONI 40, Yaana kama kila mwanadamu apewe dunia yake, atepewa amiliki dunia 6.

Hapo bado hatujazungumza kwa viumbe vya ajabu vilivyogunduliwa hivi karibuni duniani, nabado vinaendelea kugunduliwa, laiti mfano watu wa zamani wangeweza kuyaona haya au kuyasikia wasingemchukulia Mungu katika taswira iliyo bora zaidi. Ukirudi baharini vipo viumbe vingi vya ajabu ambavyo kila siku vinazidi kugunduliwa…

Lakini sasa ni kwanini tunajikumbusha haya?

Hiyo yote ni kuonesha kuwa Mungu ni mkuu na mwenye uweza kushinda sisi tunavyoweza kufikiri, hata kama uliwahi kumwomba kitu na hujakipata, hilo lisikufanye kumuona kuwa Mungu hawezi kukupa chochote, kumbuka ikiwa anamiliki matrilioni ya Sayari angani, atashindwaje kukupa wewe kipande cha mita 20 za ardhi,? Jaribu kufikira tu hayo mambo.

Ikiwa anamlisha tembo kila siku kilo Zaidi ya 200 na maji Zaidi ya lita 100 atashindwaje kukupa wewe chakula kilo 2 tu kwa siku?, ikiwa umemwomba chakula na hujaona kimekuja kwa muda huo, basi usinung’unike ujue kuwa anakuandalia kilicho bora Zaidi..

Hali yoyote unayopitia leo, uwe ni shida, au magonjwa visikuvunje moyo ukadhani kuwa Mungu hakuoni, au hawezi kukutoa katika hali uliyopo..Anao uwezo huo, wewe endelea kuyatafakari tu matendo yake.Poteza muda mrefu, kuuchunguza ukuu,wake na kumsifu kwa kila unachokiona, Nakuambia wakati utafika utasema asante Mungu kwa kuwa umenipa au umenitendea katika wakati huu, ambao ndio bora ziadi kuliko kama ungenipa wakati ule.

Hivyo ikiwa wewe ni mkristo, usiache kuishindani Imani yako, uliyokabidhiwa mara moja tu… Pia kama bado upo nje ya Kristo, acha kuyahatarisha Maisha yako, mgeukie yeye sasa atakuponya Roho na Mwili wako.

Zaburi 46:8 “Njoni myatazame matendo ya Bwana, Jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.

9 Avikomesha vita hata mwisho wa dunia; Avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari.

10 Acheni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi.”

Bwana akulinde,Bwana akufunike, Bwana akubariki.

Shalom. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO.

MJUE SANA YESU KRISTO.

YESU MPONYAJI.

MUNGU WANGU,MBONA UMENIACHA?.

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

KIFAA BORA CHA MATUMIZI.


Rudi Nyumbani:

Print this post