Category Archive maswali na majibu

Je ni sahihi kwa kiongozi wa imani kujihusisha na siasa au kuwa mfanyabiashara?

SWALI: Je ni halali kiongozi wa imani (Wachungaji), kugombea nafasi za kiserikali kama vile udiwani au kuwa wanasiasa au wafanya-biashara?


JIBU: Kabla ya kuangalia kiongozi wa imani. Embu tuangalie kwanza kwa mtu aliyeamini.

Je mtu aliyeamini kugombea nafasi za kiutawala ni dhambi?

Kugombea nafasi ya kiutawala, biblia haijaeleza moja kwa moja  kuwa ni kosa au si kosa, Yategemea lengo/ nia ya huyo mtu, Ikiwa ataenda kule ili kutetea haki, huku akitembea katika misingi ya imani ni wazi kuwa hakuna kosa lolote yeye kufanya hivyo. Kwenye maandiko tunarekodi ya watu wa Mungu waliokuwa na vyeo katika nafasi ya kiserikali, lakini waliweza kuhifadhi misingi ya imani yao, mfano wa hao ni  Yusufu na Danieli, ijapokuwa walikuwa katika falme za kipagani lakini waliweza kutembea na Mungu hatimaye wakapendwa sana.

Mfano mwingine katika historia  kuna mkristo mmoja maarufu aliyeitwa William Wilberforce, yeye alizaliwa mwaka 1759, alipokuwa mtu mzima aligombea nafasi ya ubunge uko ulaya akaipata, lengo lake likuwa ni kuomba sheria ya biashara ya watumwa ifutwe ulaya, ijapokuwa shitaka lake lilipingwa na kupuuziwa kwa miaka mingi sana, lakini aliendelea kulipigania bila kuchoka mpaka mwisho wake lilikuja kupitishwa, hivyo kwa ajili yake yeye, biashara ya utumwa ilifutwa kule ulaya  karne ya 18. Hivyo ikiwa mkristo atajiunga kwa madhumuni kama haya, si dhambi.

Lakini tukirudi katika eneo la “kiongozi wa kiroho”. Mpaka aitwe kiongozi maana yake wapo watu chini anaowachunga, ambao Bwana amempa awaangalie, na siku ya mwisho atatolea hesabu kwa ajili yao.

Sasa ikiwa ni hivyo. Mtu kama huyu kujihusisha na nafasi ya serikalini, au siasa, au kuwa mfanya-biashara ni makosa.

Ikumbukwe kuwa Bwana Yesu alitoa mipaka juu ya utumishi wake. Akasema mtu hawezi tumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja. Aidha atampenda huyu na kumchukia huyo

Mathayo 6:24 Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpendahuyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.

Pengine utaliuza  vipi kuhusu Paulo? maana alikuwa fundi wa kushona mahema?.

Ndio kiongozi au mchungaji anaweza akawa na shughuli yake ndogo ya pembeni kumsaidia kupata kipato, ili tu aweze kujitimizia mahitaji yake ya msingi, (ikiwa ni lazima) mfano alivyofanya mtume Paulo, alipokwenda kushona mahema (Matendo 18:3). Lakini sio kwa lengo la kuwa mfanya-biashara na wakati huo huo askofu. Paulo alifanya vile ili kumudu tu mahitaji yake ya msingi. Tofauti na inavyochukuliwa na watu leo kuwa “Alishikilia mambo yote” maana kama ni hivyo Paulo asingemwambia Timotheo maneno haya;

Timotheo 2:4 Hakuna apigaye vita ajitiaye katika shughuli za dunia, ili ampendeze yeye aliyemwandika awe askari.

Umeona? Mlango wa kujihusisha na mambo mengine, haupo.

Ndio maana kipindi kile baada ya Bwana Yesu kufufuka Petro alijaribu kurudia kazi yake ya uvuvi, alipohangaika usiku kucha na kukosa, asubuhi yake alipokutana na Yesu, swali la kwanza aliloulizwa Je! Petro unanipenda?  Swali hilo aliulizwa mara tatu. Akajibu ndio…Yesu akamwambia basi lisha kondoo zangu.

Yaani toa akili zako huko kwenye uvuvi kafanye kazi ya utume uliyoitiwa. Baada ya hapo hatuoni mahali popote Petro, akivua huku anafanya utume. (Yohana 21). Na hata kama ilitokea basi haikuwa kwa lengo la kuwa mfanya-biashara, bali kupata riziki ya siku.

Ukishakuwa kiongozi wa kiroho, tambua wewe hujatengenezwa kwa utumishi wa mambo mengine, bali kumtumikia Mungu tu, kazi uliyonayo ni kubwa zaidi ya zote ulimwenguni, na bado inawatenda kazi wachache, Bwana Yesu alisema. Hivyo hii ni kazi inayoweza kukufanya uwe bize wakati wote. Hupaswi kuwa mkuu wa mkoa wakati huo huo, ni mchungaji, kuwa mbunge au waziri, wakati huo huo ni askofu, utakwama tu mahali pamoja.

Na  ni muhimu kufahamu kuwa huduma ya Kristo haipaswi kuhusishwa na utafutaji fedha ndani yake, bali ni kazi ya wito ambayo malipo yake hasa yapo mbinguni. Hivyo Bwana akikubariki, au asipokubariki, hilo halikufanyi uache huduma na kuwekeza akili yako kwingineko, lakini fahamu kuwa aliahidi hatakuacha wala kukupungukia kabisa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAMBO NANE (8), AMBAYO WEWE KAMA KIONGOZI UTAIGWA.

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Je! Kucheza Magemu ni sahihi kwa mkristo?

Wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini matajiri wanaambiwa walie na kupiga yowe (Yakobo 5:1-6)

Yakobo 5:1-6

Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia.

Biblia inatoa angalizo na tahadhari katika eneo la watu wanaoitwa matajiri. Kimsingi utajiri si dhambi, na ni mapenzi ya Mungu watu wake wafanikiwe, (lakini si katika hila).

Hivyo biblia inafunua siri za matajiri wengi wadhalimu, na kuwaonya mapema ili wajirekebishe kwasababu kuna adhabu kali wameandaliwa mbeleni kwa ajili yao.

Biblia inafunua vyanzo vikuu vya mafanikio yao, wala sio katika uchawi kama wengi wanavyodhani,.. bali vipo kwa “wale watu wawatumikiao”, walio chini yao, au wanaowatumia kufanya shughuli zao.

Matajiri wengi, huwatumia wao kama daraja la wao kufika juu, ndio hapo hutumia njia ya kuwatumikisha zaidi ya kawaida yao, na kuwalipa mishahara midogo, au hata wakati mwingine kuwadhulumu kabisa kutowapa kitu, na kuwanyanyasa, hawajali malalamiko yao, na changamoto zao na mahitaji yao. Wanachojali ni kiasi gani kimepatikana, au kazi ngapi zimekamilika. Ili wapate fedha wakazijaze hazina zao.

Lakini Hawajui kuwa Kilio chao kinamfikia Mungu mbinguni. Ijapokuwa wao wanaweza wasione chochote. Kumbe hawajui wanajikusanyia adhabu kali siku ile ya hukumu.

Biblia imetumia mfano wa “bwana na mkulima wake” aliyemwajiri kwenye shamba lake… akiwawakilisha watu wote wenye wafanya-kazi chini yao.

Anasema..

Yakobo 5:1-6

[1]Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia.

[2]Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo.

[3]Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho.

[4]Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi.

[5]Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo.

[6]Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.

Umeona? wamejilisha mioyo yao utajiri, wamejinenepesha tayari kwa machinjo yao wenyewe..

Hiyo ndio sababu pale mwanzo anatangulia kwa kusema “walie, na kupiga yowe”, kwa hiyo adhabu kali inayokuja juu yao…yaani akimaanisha watubu haraka sana, ili mabaya hayo yasiwakute.

Ujumbe huu ni hata sasa?

Yaweza kuwa bado hujafikia kiwango cha utajiri wowote lakini hata ukiwa na mtu/watu uliowaajiri chini yako, bado upo kwenye mkondo huo huo wa matajiri,

hivyo wajali sana watumwa wako wape maslahi yao,.sikiliza sana malalamiko yao, kuwa tajiri usiye na lawama, mfano wa Ayubu, ambaye aliwathamini sana watumishi wake mpaka akasema..

Ayubu 31:13-15

[13]Kama nimeidharau daawa(mashtaka) ya mtumishi wangu, au ya kijakazi changu, Waliposhindana nami;

[14]Basi Mungu atakapoinuka nitafanya nini? Naye atakapozuru, nitamjibuje?

[15]Je! Huyo aliyenifanya mimi ndani ya tumbo, siye aliyemfanya na yeye? Si yeye mmoja aliyetufinyanga tumboni?

Kuwa tajiri kwa kutenda mema, hapo ndipo baraka zitakapokuja.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.

Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

Elewa maana ya Mithali 18:23 Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali. 

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya jivikeni silaha ya nia ile ile? (1Petro 4:1)

SWALI: Biblia inamaana gani kusema jivikeni silaha ya nia ile ile? (1Petro 4:1)

1 Petro 4:1-3

[1]Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi. 

[2]Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani. 

[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;


JIBU: Tukiangalia undani wa hilo neno hapo anaposema silaha ya nia. Ni kutuonyesha kuwa kumbe  “Nia ”, inaweza kuwa silaha.

Mara nyingi tunapofikiria silaha kibiblia mawazo yetu moja kwa moja yanakimbilia zile za  Waefeso 6:10-18, silaha za haki, kama vile upanga wa Roho ambalo ni Neno la Mungu, chapeo ya wokovu, ngao ya imani, dirii ya haki n.k. 

Lakini hapa tunaonyeshwa kuwa ipo pia silaha ndani ya Nia, ambayo nayo tunashauriwa tuwe nayo, kwasababu ilikuwa kwanza ndani ya Kristo.

Na silaha  yenyewe ilikuwa ni kukubali kuteswa katika mwili ili kuiua dhambi. 

Bwana wetu Yesu Kristo alijua dhambi ina nguvu sana pale mwili unapopewa raha zake. Hivyo aliikubali Nia ya kuteswa, ili dhambi ife.

Kumbuka sababu ya yeye kuchukiwa na watu, kuudhiwa, kuwindwa auawe, kuteswa mpaka kusulubiwa ni kwasababu alitangaza uadui na dhambi, Vinginevyo asingepitia maudhi yale katika mwili. Na tunaona mwisho wake ulikuwa ni ushindi. Kwani kwa kifo chake dhambi ilihukumiwa kabisa kabisa.

Alisema..

Yohana 7:7

[7]Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi; bali hunichukia mimi, kwa sababu mimi naushuhudia ya kuwa kazi zake ni mbovu. 

Hivyo maandiko yanatuambia na sisi pia, tujivike nia ile ile ya kukubali pia mateso kwa ajili ya Kristo. Kwasababu tukifanya hivyo tunaonyesha kuwa tumeachana na dhambi(tumeihukumu dhambi).

Kwa ufupi ni kuwa ukichukia maisha ya dhambi, tafsiri yake ni kukubali dhiki katika mwili kwa ajili ya Kristo. Hivyo zipende sasa dhiki hizo kama Kristo alivyozipenda, ili dhambi isikutawale. Hiyo ni Silaha kubwa sana.

2 Timotheo 3:12

[12]Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa. 

kubali shida, kwasababu umeamua kuacha ile biashara haramu, furahia kutengwa na kuonekana mshamba, kwasababu umeamua kuacha mienendo ya marafiki wabaya, penda kupigwa na kufungwa kwasababu unahubiri kweli. Hiyo ndio SILAHA YA NIA. iwezayo kuishinda dhambi.

Ndio maana vifungu vinavyofuata anasema..

“Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani. 

[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali; 

Daima tujivike silaha hii, tukikumbuka kuwa vita vyetu si vikali tena kama vile alivyovipiga Kristo.

Waebrania 12:4

[4]Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi; 

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

NDUGU,TUOMBEENI.

DHABIHU ZA ROHO NI ZIPI? (1Petro 2:5)

KIKWAZO CHA EUODIA NA SINTIKE.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je kweli Abramu alikuwa hajui aendako kulingana na Waebrania 11:8?.

Swali: Je kipindi Ibrahimu anatoka Uru ya Ukaldayo, hakuwa anajua anakokwenda kwamba ni Kaanani? au alikuwa anaongozwa na Roho Mtakatifu mpaka pale alipofika, ndipo Bwana akamwambia hapo hapo atulie?…na mbona tukisoma Mwanzo 12:5 tunaona kama Abramu alikuwa anajua kabisa anakoelekea, au je biblia inajichanganya?


Jibu: Biblia, Neno la Mungu halijichanganyi kamwe..

Turejee …

Waebrania 11:8 “Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka ASIJUE AENDAKO”.

Hapa ni kweli panaonesha kuwa Ibrahimu alikuwa hajui aendako, lakini hebu tusome maandiko mengine ndipo tutapata kuelewa zaidi..

Mwanzo 12:1 “BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;

2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka………………

5 Abramu akamchukua Sarai mkewe, na Lutu mwana wa nduguye, na vitu vyao vyote walivyokuwa wamejipatia na hao watu waliowapata huko Harani, wakatoka ili kwenda nchi ya Kanaani; nao wakaingia katika nchi ya Kanaani”

Hapa panaonyesha kuwa Abramu alikuwa anajua anakokwenda, kuwa ni Kaanani, Je lipi ni sahihi?

Jibu ni kwamba Abrahamu alikuwa anajua anakokwenda isipokuwa alikuwa hajui kama nchi hiyo aiendeayo (yaani ya Kaanani) kama ndio itakuwa ya ahadi..

Hivyo alienda mpaka alipofika na alipofika ndipo Mungu akamtokea na kumwambia kuwa nchi hiyo aliyopo ndiyo itakuwa milki yake (ya ahadi).

Mwanzo 12:5 “Abramu akamchukua Sarai mkewe, na Lutu mwana wa nduguye, na vitu vyao vyote walivyokuwa wamejipatia na hao watu waliowapata huko Harani, wakatoka ili kwenda nchi ya Kanaani; nao wakaingia katika nchi ya Kanaani.

6 Abramu akapita katikati ya nchi mpaka mahali patakatifu pa Shekemu; mpaka mwaloni wa More. Na Wakanaani siku zile walikaa katika nchi hiyo.

7 BWANA akamtokea Abramu, akasema, Uzao wako nitawapa nchi hii. Naye huko akamjengea madhabahu BWANA aliyemtokea”

Sasa swali linakuja, je ni kitu gani kilichomwelekeza Abramu aende nchi ya Kanaani na si nchi nyingine?

Tulirejea ule mlango wa 11 wa kitabu cha Mwanzo, tunasoma kuwa wazo la kuhama Uru wa Wakaldayo na kuelekea Kanaani halikuanzia kwa Abramu, bali lilianzia kwa baba yake aliyeitwa Tera, huyo ndiye aliyefikiri kuhama Ukadayo na hata kuchukua hatua ya kuhama pamoja na watoto wake wote ikiwemo Abramu.

Mwanzo 11:31 “Tera akamtwaa Abramu mwanawe, na Lutu mwana wa Harani, mwana wa mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka wote katika Uru wa Wakaldayo, waende nchi ya Kanaani, wakafika mpaka Harani wakakaa huko”.

Umeona hapo?..sio Abramu aliyekuwa na wazo la kuondoka Ukaldayo bali ni Tera, na sababu za kuwaondoa kule hazijulikani, kwani biblia haijaweka wazi, labda huenda ni maasi ya nchi hiyo, au sababu nyingine za kijamii au kibiashara.

Lakini katika wazo hilo la kuhama, lilikuwepo pia kusudi la Mungu ndani yake, kwamba Abramu afike Kanaani.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Abramu alijua anakoenda, lakini hakujua nchi atakayopewa mpaka alipofika.

Nini tunajifunza hapo?

Wakati mwingine Bwana anaweza kutumia wazo la mtu mwingine kukupeleka wewe mahali Mungu anapotaka uwe.

Hivyo wakati mwingine usinung’unike unapoona unahamishwa mahali ulipo, kwani pengine Mungu anakupeleka mahali anapotaka wewe uwe, na ukishafika ndipo atakuonyesha.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya dhabihu na matoleo hukutaka? (Waebrania 10:5).

Swali: Je Mungu hapendezwi na dhabihu na matoleo, kulingana na mstari huo?


Jibu: Turejee..

Waebrania 10:5 “Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema,

Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari”.

Andiko hili limerejewa kutoka katika Zaburi 40:6, tusome ili tupate maana kamili.

Zaburi 40:6 “Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo,

Masikio yangu umeyazibua, Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka”.

Hapo imewekwa vizuri kuwa ni kafara na sadaka zinazotolewa kwaajili ya DHAMBI!! ndizo asizozitaka…

Sasa Dhabihu ni sadaka za kuteketezwa (ambazo ni kafara za wanyama) zilizokuwa zinatolewa kipindi cha agano la kale kwaajili ya kufunika dhambi..

Na kasoro ya dhabihu za wanyama ndio hiyo, ilikuwa haiondoi dhambi bali inafunika tu..

Kwahiyo hapo anaposema “Dhabihu na matoleo hukutaka”.. alimaanisha kuwa hizo dhabihu za wanyama hazifai katika kumwondolea mtu makosa yake na kumtakasa bali mwili wa Yesu na damu yake ndio iwezayo kumtakasa mtu na kumwondolea kabisa dhambi zake.

Ndivyo maandiko yasemavyo kuwa damu za mbuzi na mafahali haziwezi kuondoa dhambi na kumtakasa mtu bali zilikuwa zinafunika tu.

Waebrania 10:3 “Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka.

4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi”

Lakini dhabihu ya mwili wa YESU, kupitia kumwagika kwa damu yake, unaondoa kabisa dhambi… Na hiyo ndio sadaka Mungu aliyoihitaji na sio dhabihu za kondoo na mbuzi na mafahali.

Waebrania 10:10 “Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu”.

Lakini kuhusiana na utoaji wa sadaka ni kwaajili ya shukrani, au kwaajili ya kazi ya ufalme wa mbinguni ni jambo linalompendeza Mungu na lenye baraka.

Lakini kama ni kwaajili ya dhambi (hakuna sadaka inayoweza kuondoa dhambi)..isipokuwa damu ya YESU ambayo tayari tumeshalipiwa bureee… tunachopaswa kufanya ili sadaka hiyo ifanye kazi juu yetu ni KUTUBU TU kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi!.

Tukiweza kutubu kwa kumaanisha basi tunapata msamaha na ondoleo la dhambi bure.

Je unaye YESU maishani?.

Kumbuka daima kuwa mwisho wa dunia upo, kama tu vile mwisho wa maisha ulivyo, ikiwa leo hii damu ya YESU si kitu cha thamani kwako, utasimamaje siku ile ya mwisho mbele zake?..Tafakari mara mbili.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Je maji na giza viliumbwa siku ya ngapi?

Swali: Je vitu kama giza, na maji viliumbwa siku ya ngapi, maana tunaona wakitajwa tu wanyama na mimea, je hivi vingine viliumbwa lini?


Jibu: Ni kweli katika kitabu cha Mwanzo tunaona uumbaji unaanza kwa kusema “giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji”, lakini haitaji ni lini giza liliumbwa wala ni lini maji yaliumbwa, badala yake tunaona uumbaji unaendelea na vitu vingine kama mimea pamoja na wanyama na wanadamu?..

Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.

2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji”.

Jibu la swali hili lipo katika mstari huo wa kwanza..

Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi”.

Neno “hapo mwanzo”… halimaanishi kile kipindi cha siku saba (7) bali linamaanisha mwanzo kabisa wa uumbaji kabla ya kitu kingine chochote, Mungu aliumba mbingu (hii yenye mawingu na sayari) pamoja na mbingu ile yenye Malaika watakatifu.

Na vile vile aliumba “NCHI” Au kwa lugha nyingine ARDHI/DUNIA. Na ili ardhi iweze kukamilika ni lazima iwe na malighafi zake zote kama udongo, mchanga, mawe, milima, mabonde, chuma, madini, moto na maji na mengineyo.

Vile vile ili mbingu ikamilike lazima iwe na nyota na mwanga uwepo na giza liwepo, kwahiyo vitu hivi vyote viliumbwa Hapo Mwanzo, kabla ya zile siku sita za uumbaji.

Na baada ya Mungu kuumba Mbingu na nchi, hatujui ni kitu gani kilitokea kikaifanya nchi/dunia yenye milima na mawe na madini na mabonde na maji kuwa UKIWA! Au kwamba Mungu ndio aliiumba ikae hivyo ukiwa kwa kipindi Fulani cha muda..hatujui!, labda tutakuja kujua tutakapomaliza maisha haya na kufika huko kwake, tutamwuliza, lakini tunajua kuwa alisema hakuiumba ukiwa, bali ikaliwe na watu.

Isaya 45:18 “Maana Bwana, aliyeziumba mbingu, asema hivi; Yeye ni Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; ndiye aliyeifanya imara; hakuiumba ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu; Mimi ni Bwana, wala hapana mwingine”

Hivyo kama hakuiumba ikae ukiwa bali ili ikaliwe na watu, basi hana budi kuiikarabati na kumweka mwanadamu humo, na ndipo hapo siku sita za uumbaji wa wanyama na wanadamu na miti zilipoanza..

Lakini kiuhalisia tayari mbingu na nchi zilikuwa zimeshaumbwa hapo kabla, na malighafi zake zote (kama maji, udongo, mawe, madini, giza, hewa n.k)..na ndio maana hatuoni vikitajwa katika uumbaji.

Lakini pamoja na hayo, upo unabii unaoonyesha kuwa dunia itakuja kuwa tena ukiwa siku za mwisho, kipindi ambacho ghadhabu ya Bwana MUNGU itakapokuja kumwagwa juu wa wanadamu wote wakosaji, ambayo hata mmoja wetu hapaswi kuwepo..

Isaya 13:9 “Tazama, siku ya Bwana inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ili iifanye nchi kuwa ukiwa, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.

10 Maana nyota za mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze”.

Isaya 24:1 “Tazama, Bwana ameifanya dunia kuwa tupu, aifanya ukiwa, aipindua, na kuwatawanya wakaao ndani yake”.

Jambo litakalotokea siku hiyo ni lile tunalolisoma katika kitabu cha 2Petro 3:10-12 na Isaya 34:4.

Lakini wateule, waliomwamini Bwana na kuoshwa kwa damu yake, hawatakuwepo katika siku hiyo ya ghadhabu yake, kwani watakuwa mbinguni pamoja na Bwana.

Bwana atubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Je kuna pepo wazuri kulingana na Waefeso 6:12?

Swali: Biblia inasema kushindana kwetu ni dhidi ya pepo wachafu, je kulingana na mstari huo, wapo pepo wazuri?


Jibu: Turejee…

Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya MAJESHI YA PEPO WABAYA katika ulimwengu wa roho”

Biblia iliposema kuwa kushindana kwetu ni dhidi ya “pepo wabaya” haijamaanisha kuwa wapo pepo wazuri, bali inaelezea tu sifa ya hizo roho (mapepo) kwamba ni mbaya na chafu.

Ni sawa na biblia inapotaja Malaika watakatifu, (soma Mathayo 25:31, Marko 8:38 na Ufunuo 14:10) haimaanishi kuwa wapo Malaika wasio watakatifu, na kama wapo wasio watakatifu basi hawaitwi tena Malaika bali ni mapepo, vile vile hakuna mapepo wasafi na kama zipo hizo roho safi basi haziwezi kuitwa tena mapepo, bali zitaitwa Malaika.

Hivyo uzuri na usafi unaotajwa juu ya Malaika au Mapepo, ni kuelezea tu sifa zao na kazi zao, kwamba Malaika wote walioko mbinguni ni wasafi na watakatifu, na mapepo yote yaliyotupwa ulimwenguni ni machafu na mabaya.

Na kumbuka pia “Pepo na jini” ni kitu kimoja, isipokuwa ni lugha mbili tofuati tu!… Na hakuna jini wala pepo mzuri, wote ni wabaya na wachafu. Zipo dini zinazofundisha kuwa wapo majini (mapepo) wazuri, na kwamba watu wanaweza kuwa nao na wakawaletea mafanikio na hata kuwalinda.

Huo ni uongo wa shetani asilimia mia, kwani shetani ndiye baba wa uongo..

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; KWA SABABU YEYE NI MWONGO, NA BABA WA HUO”.

Shetani hajawahi kuwa na urafiki wa kweli na mwanadamu, wala hajawahi kuwa na mapenzi na mwanadamu, kitu anachokipenda kutoka kwa mwanadamu ni utukufu tu!.. lakini hajawahi kumpenda mwanadamu, na hakuna unabii ya kwamba atakuja siku moja kumpenda mwanadamu, yeye ni adui wa mwanadamu wa milele.

Na Kama tu shetani asivyopendwa kuitwa shetani, bali anapendwa aitwe mungu, kadhalika hawezi kuruhusu mapepo yake yaitwe vibaya, kwa sifa mbaya?..atawatakasa tu!.. na anawatakasaje?..si kwa njia nyingine bali kwa njia za dini za uongo, zinazohubiri na kufundisha kuwa wapo mapepo wazuri.

Kwa urefu kuhusiana na pepo wachafu(majini) fungua hapa >>

MAJINI WAZURI WAPO?

Je umempokea YESU?.. kama bado ni nini kinakungojesha?

Bwana anarudi.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Naliupata wenyeji huu kwa mali nyingi, maana yake nini (Matendo 22:28)

Jibu: Habari hii inamhusu Mtume Paulo, kipindi aliposhikwa na kufungwa akiwa Yerusalemu.. sasa ili tuelewe vizuri tuanze kusoma ule mstari wa 25

Matendo 22:25 “Hata walipokwisha kumfunga kwa kamba, Paulo akamwambia yule akida aliyesimama karibu, Je! Ni halali ninyi kumpiga mtu aliye Mrumi naye hajakuhumiwa bado?

26 Yule akida aliposikia, akaenda akamwarifu yule jemadari, akisema, Unataka kufanya nini? Kwa maana mtu huyu ni Mrumi

27 Jemadari akaja, akamwuliza, Niambie, u Mrumi? Akasema, Ndiyo.

28 Jemadari akajibu, MIMI NALIPATA WENYEJI HUU KWA MALI NYINGI. Paulo akasema, Na mimi ni Mrumi wa kuzaliwa”.

Wenyeji unaozungumziwa hapo ni “URAIA”.. Kwahiyo hapo kiswahili kingine cha andiko hili ni hiki .. “Jemadari akajibu, MIMI NALIPATA URAIA HUU KWA MALI NYINGI”.

Zamani za kanisa la karne ya kwanza, ufalme uliokuwa na nguvu duniani, ulikuwa ni ufalme wa Rumi, na ndio uliokuwa unatawala dunia chini ya Kaisari. Hivyo kutokana na nguvu ya ufalme huo, basi hata raia wake walikuwa na nguvu, na heshima.

Raia wa kirumi (yaani Mrumi) alikuwa hawezi kuadhibiwa bila kushitakiwa, na haki zake zilikuwa zinalindwa sana kuliko raia wa Taifa lingine lolote duniani,..ilikuwa ni kosa kubwa kumhukumu Mrumi kabla ya kumsikiliza.

Sasa hapa Paulo alikuwa ni Mrumi kwa kuzaliwa lakini kwaasili ni Mwebrania (yaani muisraeli), na hapa alikuwa amevunjiwa haki yake kama raia wa kirumi, na hivyo akida pamoja na jemedari wakaogopa, kwasababu ni kosa kumhukumu Mrumi kabla ya kumpandisha kizimbani na kumsikiliza.

Sasa swali la Msingi kwanini, Jemedari aseme Uraia wake kaupata kwa mali nyingi?

Zamani ili uwe Raia wa kirumi ni aidha uwe mzawa (yaani umezaliwa katika Taifa la Rumi) au Umeununua uraia.

Sasa kitendo cha kuununua Uraia hakikuwa rasmi, bali kilikuwa ni kwa njia ya rushwa, na waliopata uraia huo waliupata wakati wa sense, ambapo majina yako yaliongezwa katika orodha ya warumi kinyume cha sheria, baada ya kulipa pesa nyingi,

Na hapa huyu Jemedari aliyeitwa Klaudio Lisia (Matendo 23:26) anaonekana kumwambia Paulo kuwa Uraia wake “Aliununua” maana yake kwa asili hakuwa mrumi, bali alikuwa kuwa mtu wa Taifa lingine, huenda Ugiriki, kwasababu hilo jina la Pili la LISIA ni jina la kigiriki, lakini Paulo yeye alikuwa ni Mrumi kwa kuzaliwa na si kwa kununua uraia.

Upo uraia mwingine ambao ni wa Mbinguni…huo haupatikani kwa fedha, wala mtu haupati kwa rushwa bali bali kwa kuzaliwa mara ya pili.

Yohana 3:3 “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.

4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?

5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.”

Je umeupata uraia huu wa mbinguni kwa kuzaliwa mara ya pili?.. kama bado ni nini kinachokusubirisha??

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Biblia inaposema ndugu wa kunyonya inamaanisha nini (Matendo 13:1)?

Swali: Katika kitabu cha Matendo 13:1, tunamsoma mtu mmoja akitajwa kama ndugu wa kunyonya wa Herode, je maana yake nini?.


Jibu: Maana ya “Ndugu wa kunyonya” ni “mtu aliyelelewa katika familia fulani, tangu utotoni, alipokuwa akinyonya” kwa lugha nyingine amekuwa “adopted” tangu utotoni, (katika umri wa kunyonya).

Hivyo mtu kama huyu anahesabika kuwa kama mwanafamilia, na watoto wa familia hiyo watamhesabu kama ndugu yao wa kunyonya, kwani amekulia katika familia yao.

Hivyo huyu Manaeni alilelewa pamoja na Mfalme Herode, katika familia moja, ingawa hawakuwa ndugu wa damu, lakini tangu utoto walikuwa pamoja.

Matendo 13:1 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na MANAENI ALIYEKUWA NDUGU WA KUNYONYA WA MFALME HERODE, na Sauli”.

Lakini kulikuwa na kusudi kwanini habari zake ziandikwe katika biblia, ukizingatia ya kuwa ndugu yake, ambaye alikuwa ni Herode pamoja na maherode wote walikuwa ni wakatili sana, waliwaua wakristo na kuwapiga vita vikali, lakini huyu Manaeni ambaye ni ndugu ya Herode, yeye alikuwa wa tofauti, kwani alikuwa ni miongoni mwa watu wa kwanza kabisa kugeuka na kuifuata Imani ya Kikristo, na kuwa miongoni mwa wasimamizi wa Imani katika kanisa la kwanza la watu wa mataifa, huko Antiokia.

Na kumbuka Antiokia ndiko jina la Ukristo lilikozaliwa, kwani hapo kabla waliomfuata YESU walikuwa wanaitwa wanafunzi tu.

Matendo 11: 26 “hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi waliitwa Wakristo kwanza hapo Antiokia”

Sasa kufahamu kwa urefu ushuhuda alilolibeba Mtumishi huyu wa Mungu (Manaeni) na ujumbe tuupatao watu wa sasa katika Kanisa, fuatilia somo linalofuata…

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Neno “Msiche” maana yake nini? (Kumbukumbu 1:17)

Jibu: Msiche linatokana na Neno “kucha/kumcha”.. Na maana ya Neno “Kucha” ni “kuhofu”.

Hivyo mtu anapomwofu “mtu”, maana yake anamcha huyo mtu, na pia anapomhofu MUNGU maana yake anamcha Mungu, na matokeo ya kumcha MUNGU ni kumheshimu, kumtumikia, na kufanya mapenzi yake. Lakini mtu asiyemcha MUNGU basi hawezi kufanya hayo yote.

Vile vile mtu anayemcha mwanadamu mwenzake, tafsiri yake ni kwamba anamtumikia, anamheshimu, anamtii na kufanya yale yote mtu huyo anayomwagiza.

Vile vile mtu anayeicha miungu mingine tofauti na MUNGU wa mbingu na nchi, tafsiri yake ni kwamba anaitumikia ile miungu, na kuihofu na kuitii na kuiheshimu.

Hivyo Neno “msiche” ni kinyume cha “kucha/kumcha” na tafsiri yake ni “kutohofu”

1. Mfano wa mistari unayokataza uchaji wa mtu (kumcha mtu)

Kumbukumbu 1:17 “Msitazame nafsi za watu katika hukumu; mwasikize wadogo na wakubwa sawasawa; MSICHE USO WA MTU AWAYE YOTE; kwa kuwa hukumu ni ya Mungu; na lile neno liwashindalo mniletee mimi, nami nitalisikiza”.

Hapo Bwana MUNGU anakataza watu kuhofu wanadamu wenzao.. Na mistari mingine ni pamoja na Yoshua 10:25.

2. Mfano wa mistari inayotaja kuicha miungu mingine.

2Wafalme 17:35 “hao ambao Bwana alifanya agano nao, akawaamuru, akasema, MSICHE miungu mingine, wala kuisujudia, wala kuitumikia, wala kuitolea sadaka

37 na sheria, na hukumu, na torati, na amri, alizowaandikia, hizo ndizo mtakazozishika na kuzifanya hata milele; wala msiche miungu mingine.

38 Na hilo agano nililofanya nanyi, msilisahau; wala MSICHE miungu mingine”

3. Mistari inayotaja uchaji wa MUNGU wa mbingu na nchi. (yaani kumcha MUNGU wa mbingu na Nchi).

Yoshua 24:14 “Basi sasa MCHENI BWANA, mkamtumikie kwa unyofu wa moyo na kwa kweli; na kuiweka mbali miungu ambayo baba zenu waliitumikia ng’ambo ya Mto, na huko Misri; mkamtumikie yeye Bwana.”

Soma pia Kumbukumbu 13:4, 1Samweli 12:24, Zaburi 22:23, Zaburi 34:9, 1Petro 2:17, na Ufunuo 14:7.

Kwa hitimisho ni kwamba biblia imetukataza TUSICHE miungu yoyote wala mwanadamu yoyote, bali TUMCHE BWANA MUNGU MWETU, aliyetuumba.

Ufunuo 14:7 “akasema kwa sauti kuu, Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji”

Je umeokoka?, Je una uhakika BWANA akirudi leo unakwenda naye??… Je huna uhakika huo basi tayari huo ni uthibitisho kuwa akija hutakwenda naye, ni heri ukampokea BWANA YESU LEO, akutakase na kukupa uhakika wa uzima wa milele.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UNAMFAHAMU MUNGU WA KWELI?

Kuna Mbingu ngapi?

Mbinguni ni sehemu gani?

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

FAHAMU SEHEMU NNE (4)  APANDWAPO MWAMINI.

Rudi Nyumbani

Print this post