Category Archive maswali na majibu

Rahabu kwenye biblia.

Rahabu ni nani?

Jina “Rahabu” limeonekana mara kadhaa katika biblia likiwa na maana Zaidi ya moja. Maana ya kwanza ni linamwakilisha Mwanamke wa kikanaani aliyekuwa kahaba, aliyewahifadhi wapelelezi wa kiisraeli walioingia kuipeleleza Yeriko, na maana ya pili Taifa la Misri.

Kama tu vile neno “Mharabu” katika biblia linamaanisha Jamii ya watu wa Arabia, lakini pia linamaanisha “Mtu au Malaika anayeharibu Vivyo hivyo na jina Rahabu lina maana Zaidi ya moja.

     1.RAHABU (Kahaba).

Habari ya Rahabu aliywakuwa kahaba tunaipata katika kitabu cha Yoshua mlango wa 2 na wa 6. Mwanamke huyu aliwahifadhi wapelelezi wa kiisraeli walioingia Yeriko kuipeleleza nchi ile.

Yoshua 2:1 “Yoshua, mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kutoka Shitimu kwa siri, ili kupeleleza, akawaambia, Enendeni mkaitazame nchi hii, na Yeriko. Wakaenda wakafika nyumbani kwa kahaba mmoja jina lake aliitwa Rahabu, wakalala huko.

2 Mfalme wa Yeriko akaambiwa, kusema, Tazama, watu wawili wa wana wa Israeli wameingia humu leo usiku, ili kuipeleleza nchi.

3 Mfalme wa Yeriko akatuma watu kwa Rahabu, akasema, Watoe watu wale waliokuja kwako, walioingia ndani ya nyumba yako, maana wamekuja ili kuipeleleza nchi.

4 Yule mwanamke akawatwaa wale watu wawili, akawaficha, akasema, Naam, wale watu walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka”

       2.TAIFA LA MISRI.

Jina Rahabu pia katika biblia limetumika kuwakilisha Joka kubwa la baharini ambalo ufunuo wake ni Taifa la Misri.

Isaya 30:7 “Kwa maana Misri huwasaidia bure, bila faida; Kwa hiyo nimemwita, Rahabu aketiye kimya”

Isaya 51:10 “Si wewe uliyemkata-kata Rahabu? Uliyemchoma yule joka? Si wewe uliyeikausha bahari, Na maji ya vilindi vikuu; Uliyevifanya vilindi kuwa njia, Ili wapite watu waliokombolewa?”

Zaburi 87: 4 “Nitataja Rahabu na Babeli Miongoni mwao wanaonijua. Tazama Filisti, na Tiro, na Kushi; Huyu alizaliwa humo”

Soma pia Ayubu 26:12, na Zaburi 89:10..

Jambo kubwa na kuu tunaloweza kujifunza kwa RAHABU (Aliyekuwa Kahaba) ni IMANI.

Alikuwa na Imani juu ya mambo yatarajiwayo sawasawa na Waebrani 11:1. Aliziamini nguvu za MUNGU wa Israeli, hivyo akajua yatakayofuata baadaye kuwa ni anguko la Yeriko, hivyo akatafuta njia ya kujinusuru yeye na familia yake kwa kujiungamanisha na jamii ya Israeli.

Waebrania 11:31  “Kwa imani Rahabu, yule kahaba, hakuangamia pamoja na hao walioasi; kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa amani”.

Yakobo 2:25 “Vivyo hivyo na Rahabu, yule kahaba naye, je! Hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipowakaribisha wajumbe, akawatoa nje kwa njia nyingine?

26  Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa”.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

RAHABU.

LAANA YA YERIKO.

Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.

Je! Daudi hakuwa mtoto wa ndoa wa Yese? (Zab 51:5)

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Rudi nyumbani

Print this post

Machukizo ni nini?

Machukizo au Chukizo ni nini? kama tunavyosoma katika biblia?


Machukizo linatokana na neno “chukizo” na chukizo ni kitu kinachosababisha chuki/hasira. Kwa Mungu kitu chochote kinachoipandisha ghadhabu yake kinaitwa “chukizo”.

Na vitu vifuatavyo ndivyo vilivyokuwa machukizo kwa MUNGU.

   1. Ibada ya Sanamu.

Sanamu ya aina yoyote ile ilikuwa ni machukizo kwa Mungu na hicho ndicho kitu cha kwanza kilichokuwa kinaletea wivu kwa Mungu.

Kumbukumbu 27:15 “Na alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga, au ya kusubu, machukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi, akaisimamisha kwa siri. Na watu wote wajibu, waseme, Amina”.

Kumbukumbu 32:16 “Wakamtia wivu kwa miungu migeni, Wakamkasirisha kwa machukizo.

17 Walitoa sadaka kwa pepo, si Mungu, Kwa miungu wasiyoijua, Kwa miungu mipya iliyotokea siku zilizo karibu, Ambayo baba zenu hawakuiogopa”.

Soma pia Kumbukumbu 27:15, na 2Wafalme 23:24

   2. Uasherati na ulawiti.

Walawi 18: 22 “Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo”.

Soma tena Mambo ya Walawi 20:13

   3. Mavazi yasiyopasa.

Kumbukumbu 22:5 “Mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanamume, wala mwanamume asivae mavazi ya mwanamke; kwa maana kila afanyaye mambo hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako”

Mfano wa mavazi yasiyopasa, ni suruali kwa mwanamke, na nguo mfano wa magauni kwa wanaume.

   4. Sadaka yenye kasoro.

Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”.

Kumbukumbu 17:1 “Usimchinjie Bwana, Mungu wako, ng’ombe wala kondoo aliye na kilema, wala neno ovu lo lote; kwa kuwa hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako”.

Na yapo machukizo mengine mengi!.

Lakini pia lipo chukizo moja KUU na KUBWA ambalo litatokea kule YERUSALEMU, ambalo ni CHUKIZO LA UHARIBIFU, linalomhusu Mpinga-kristo.

Kwa upana juu ya CHUKIZO LA UHARIBIFU, basi fungua hapa >>CHUKIZO LA UHARIBIFU

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

VIPIMO MBALIMBALI VYA KIBIBLIA.

Kemoshi ni nani? (Yeremia 48:46)

Kwanini kuwe na kitabu Cha kumbukumbu la Torati na kwanini kiitwe vile?

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

Kemoshi ni nani? (Yeremia 48:46)

Swali: Huyu Kemoshi alikuwa nani, na nini tunajifunza kutoka kwake?


Jibu: Turejee,

Yeremia 48:46 “Ole wako! Ee Moabu, Watu wa Kemoshi wamepotea; Maana wana wako wamechukuliwa mateka, Na binti zako wamekwenda utumwani”.

“kemoshi” hakuwa mtu bali alikuwa ni “mungu” wa watu wa Moabu. Kumbuka kila taifa lilikuwa na mungu wake; Israeli walikuwa na MUNGU wao ambaye ni YEHOVA, Muumba wa mbingu na nchi, Tiro walikuwa na mungu wao anayeitwa “baali”, Sidoni walikuwa na mungu wao anayeitwa “ashtoreti”, wana wa Amoni walikuwa na mungu wao anayeitwa “milkomu”. N.k na hawa wana wa Moabu mungu wao ndio anayekuwa anaitwa “kemoshi” ambaye kiuhalisia ni “pepo”.

Sasa utaona Mungu aliwakataza wana wa Israeli wasiabudu miungu mingine tofauti na yeye…lakini wapo waliotii na wapo waliokaidi na kuamua kuifuata miungu hiyo ya mataifa mengine na kuiabudu na kuisujudia. Na Mfalme Sulemani alikuwa miongoni mwa waliokengeuka dakika za mwisho kwa kuifuata miungu hiyo ya mataifa, ingawa baadaye alikuja kutubu.

2Wafalme 23:13 “Na mahali pa juu palipokuwapo mbele ya Yerusalemu, palipokuwa upande wa kuume wa mlima wa uharibifu, alipopajenga Sulemani, MFALME WA ISRAELI, KWA ASHTORETHI, CHUKIZO LA WASIDONI, NA KEMOSHI, CHUKIZO LA MOABU, NA MILKOMU, CHUKIZO LA WANA WA AMONI, mfalme akapanajisi”.

Hii miungu hata leo inaabudiwa katika sehemu mbalimbali ikiwemo Africa, isipokuwa katika majina mengine tofauti na hayo.

Mila nyingi za kiafrica asili yake ni miungu hii, kwamfano mungu wa wasidoni aliyeitwa Ashtorethi alikuwa ni mtu wenye kuchongwa maumbile ya mtu, na kusujudiwa, na kufanyiwa matambiko..na sasa jamii nyingi na makabila mengi (ikiwemo na wakristo) wanafanya hayo hayo wanapokutanika katika vijiji vyao, pasipo kujua kuwa ni ibada za sanamu kama zile zile tu ambazo mataifa wasiomjua Mungu walikuwa wanazifanya.

Bwana atusaidie tuepukane na ibada hizo za sanamu.

Mistari mingine inayomtaja huyo mungu “kemoshi” ni pamoja na Hesabu 21:9, Waamuzi 11:24, 1Wafalme 11:7, 1Wafalme 11:33, Yeremia 48:7, na Yeremia 48:13.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Moabu ni nchi gani kwasasa?

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UNAMFAHAMU MUNGU WA KWELI?

MNGOJEE BWANA

USIJITUMAINISHE JUU YA SIRA YAKO ANGALI UPO KATIKA DHAMBI.

Rudi nyumbani

Print this post

Antiokia ni wapi kwasasa?

Antiokia ipo nchi gani kwa sasa? Na nini tunaweza kujifunza kupitia mji huo?


Jibu: Antiokia ni mji uliopo kusini mwa Taifa la UTURUKI na Kaskazini mwa Taifa la SIRIA.

Mji huu una historia kubwa sana ya kanisa, kwani ndicho kitovu cha jina “Ukristo”. Maandiko yanasema Wanafunzi (yaani watu waliomwamini YESU na kumfuata) waliitwa “wakristo” kwanza hapo Antiokia na si Yerusalemu kanisa lilipoanzia.

Matendo 11:26  “hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. NA WANAFUNZI WALIITWA WAKRISTO KWANZA HAPO ANTIOKIA.

27  Siku zizo hizo manabii walitelemka kutoka Yerusalemu hata Antiokia”.

Antiokia ni mji uliomiminiwa uliokuwa na Neema ya Ukristo kuliko miji mingi, lililojaa Mitume, manabii na waalimu.. kwani hata Mtume Paulo safari yake ya kuanza kuhubiri injili ilianzia pale.

Matendo 13:1 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli.

2  Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.

3  Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.

4  Basi watu hao, wakiisha kupelekwa na Roho Mtakatifu wakatelemkia Seleukia, na kutoka huko wakasafiri baharini hata Kipro”.

Matendo 14:26 “Na kutoka huko wakaabiri kwenda Antiokia. Huko ndiko walikoombewa neema ya Mungu kwa ile kazi waliyokwisha kuitimiza”.

Mji wa Antiokia kwasasa umejaa wa Islamu kutokana na Taifa hilo la Uturuki kuwa la kiislamu, ingawa kuna asilimia ndogo ya wakristo wanaoishi humo. Mahali ambapo uamsho mkubwa wa injili ulianzia sasa adui kapateka na kupafanya kuwa mji wa kipagani… Na miji mingine imenyanyuka yenye uamsho kuliko huo, sawasawa na Neno lile..

Marko 10:31 “Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho; na wa mwisho watakuwa wa kwanza”

Hivyo hiyo ni tahadhari hata kwetu, “Tushike tulicho nacho, mpaka mwisho adui asije akatupokonya taji yetu”.

Mji wa Antiokia mwaka 2023, Februari 6 kulitokea tetemeko kubwa sana lililoua watu elfu 55, na kuharibu makazi mengi sana.

Bwana atusaidie tuwe na mwisho mwema.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Yerusalemu ni nini?

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

MJI WENYE MISINGI.

Babeli ni nchi gani kwasasa?

DANIELI: Mlango wa 8

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni Mungu au Malaika?

Swali: Je biblia inajichanganya katika Zaburi 8:4-5 na Waebrania 2:6-7. Maana sehemu moja inataja ‘Mungu’, na sehemu nyingine ‘Malaika’.


Jibu: Turejee.

Zaburi 8:4 “Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, Na binadamu hata umwangalie?

5 Umemfanya mdogo punde KULIKO MUNGU; Umemvika taji ya utukufu na heshima”.

Tusome tena Waebrania 2:6-7..

Waebrania 2:6 “Mwanadamu ni nini hata umkumbuke, Ama mwana wa binadamu, hata umwangalie?

7  Umemfanya mdogo punde kuliko MALAIKA, Umemvika taji ya utukufu na heshima, Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako”.

Katika Waebrania mwandishi ana nukuu maneno kutoka katika Zaburi, lakini ni kama ana nukuu kitu tofauti na kilichoandikwa kule, kwamaana yeye anataja Malaika na wakati mwandishi wa Zaburi alitaja Mungu.. Sasa swali biblia inajichanganya?.

Jibu ni La! Biblia haijichanganyi wala haijakosewa.. Isipokuwa fahamu zetu na pambanuzi zetu ndizo zinazojichanganya.

Sasa ili tuelewe ni vizuri kuzielewa kwanza lugha za kibiblia..

Si kila mahali panapotajwa Mungu, panamaanisha Mungu-muumba, La! Sehemu nyingine panamaanisha Ufalme wa Mungu (yaani jeshi la Mbinguni yaani Malaika na vyote vilivyopo kule)…Na sehemu mojawapo ambayo iliyotajwa Mungu ikimaanisha Jeshi la Mbinguni ni hii Zaburi 8:5 “…Umemfanya mdogo punde KULIKO MUNGU”.

Mungu inayotajwa hapo inamaanisha Ufalme wa Mungu (yaani jeshi la Malaika) na si MUNGU aliye Muumbaji, ambaye ni MMOJA.

Ni sawa na jina ISRAELI katika biblia,…kuna mahali linamaanisha mtu mmoja (ambaye ni Yakobo mwana wa Isaka, Mwanzo 35:10).. Lakini pia jina hili kuna mahali linamaanisha TAIFA (Ufalme, Kutoka 5:2).

Au “Yuda”, kuna mahali anatajwa kama Mtu (Mwana wa Yakobo), lakini pia kama Taifa.

Vivyo hivyo na Mungu, cheo hicho kinaweza kufunua “Ufalme” au nafasi ya MUNGU MWENYEWE kama Muumba.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba mwandishi wa kitabu cha Waebrania hajapishana na mwandishi wa Zaburi.

Kujua kwa mapana ni ufunuo uliopo nyuma ya andiko hili.. “Amefanyika bora kuliko Malaika” basi fungua hapa >>>AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Ielewe kwa kina Waebrania 13:5 maana yake.

MUNGU MWENYE HAKI.

UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.

JE! UNA MHESHIMU MUNGU?

Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani?

Rudi nyumbani

Print this post

Mbaruti ni mmea gani? (Mathayo 7:16)

Mbaruti ni nini?.(Mibaruti ni mimea ya aina gani) na umebeba ujumbe gani kiroho?.


Jibu: Turejee,

Mathayo 7:16 “Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?”

Soma pia 2Wafalme 14:9, 2Nyakati 25:18 na Hosea 10:4.

Mbaruti/Mibaruti ni jamii ya mimea yenye maua, ambayo mara nyingi inajiotea maporini. (Mimea hii inatoa matunda ambayo ina miiba inayoizunguka pande zote, kuifanya kutolika na wanyama walao nyasi). Tazama picha juu..

Katika biblia Bwana YESU alinukuu mimea huu wa mbaruti katika swali lililowahusu manabii wa uongo.. Aliuliza je watu huchuma tini katika mibaruti?,.. Maana yake ni jambo lisilowezekana kupata matunda ya “Tini“ kutoka katika jamii ya mimea hiyo ya maua ya mibaruti.

Vile vile akasema haiwezekani kuchuma zabibu kutoka kwenye miti ya miiba…

Kuonyesha kuwa Manabii wa uongo wanatoa matunda yenye MIIBA MIIBA!!.yasiyofaa kwa kuliwa bali yanaumiza na kuchoma!.

Moja ya matunda wanayotoa ni tamaa za fedha, (wakizitamani na kuwafundisha watu hizo)..ambazo biblia inasema wanaozama huko wanajichoma kwa maumivu mengi..

1Timotheo 6:10 “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi”.

Manabii wa uongo kamwe hawahubiri wala kufundisha Toba na Utakatifu, wala safari ya kwenda mbinguni hawaihubiri kwasababu huko hawaendi!.na wao si wasafiri wa kwenda huko, hivyo mioyo yao ipo hapa hapa duniani na wanahubiri vitu vya duniani, pasipo kuweka mambo katika uwiano.

Mathayo 7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.

16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?

17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.

18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.

19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni. 7.20 Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua”

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NI SAHIHI KABISA, HUU SI WAKATI WA TINI!

SHAMBA HUWA HALIMTAMBUI WALA KUMSUBIRIA MKULIMA.

UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?

Kwanini Bwana Yesu alivikwa taji ya miiba?

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kwa namna gani, haki yetu inapaswa izidi ya mafarisayo?

Bwana alimaanisha nini katika Mathayo 5:20 aliposema..

[20]Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni. 

Ni haki ipi hiyo.

JIBU: Katika andiko hilo tunaona Bwana akiainisha kigezo cha mtu kuingia kwenye ufalme wa Mungu..kwamba kigezo chenyewe ni “HAKI” …

Haki ni kitu kinachomstahilisha mtu kupokea kitu fulani. Kwamfano tunasema mtoto ana haki ya kulindwa…ikiwa na maana kilichomsababishia apate haki ya kulindwa ni ile hali ya utoto wake.

Mfano mwingine, tunasema ni mtu mzima ana haki ya kuoa au kuolewa na mtu amtakaye, katika wakati auchaguaye yeye. Tafsiri yake ni kwamba kinachompa haki ya kuwa hivyo ni kwasababu yeye ni “mtu-mzima”. Angekuwa mtoto asingekuwa na haki hiyo.

Sasa tukirudi katika habari hiyo tunaona kilichowafanya waandishi na mafarisayo wajihesabie haki kwamba wao ni warithi wa ufalme wa mbinguni. Ilikuwa ni kuitimiza sheria kwa matendo yao. Ambayo kimsingi wao wenyewe hawakuweza kuishika..kwa nje walionekana sawa lakini ndani walikuwa mbali na sheria yao. Kwasababu hakuwahi kutokea mtu hata mmoja aliyeweza kumpendeza Mungu kwa matendo yake, yeye mwenyewe.

Hivyo njia yao ya kupata haki, ambayo ni kwa matendo ya sheria haikuwa sawa. Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake na wale waliomsikia kwamba haki “ yao” isipozidi ya mafarisayo na waandishi kamwe hawataweza kuuingia ufalme wa mbinguni.

Swali je ya kwao inapaswa iweje. Je ya matendo ya sheria zaidi ya yale au vinginevyo?

Haki Yesu aliyoileta ambayo itampelekea mtu kurithi uzima wa milele ni kwa njia yake yeye mwenyewe .Ambayo sisi tunahesabiwa haki kwa kumwamini, kama mwokozi wa maisha yetu. Bila kutegemea matendo yetu ya haki. Yaani ni haki tuipatayo kwa neema.

Hivyo, wote wanaoipokea haki hiyo basi uzima wa milele ni wao. Na kwasababu ndio njia ambayo sisi tutamfikia Mungu. Basi neema yenyewe inatufundisha pia kuyazaa matunda ya Roho. Na hivyo tunaitimiza sheria ya Mungu mioyoni mwetu bila unafiki. Mbali na mafarisayo ambao walitegemea akili zako na nguvu zao.

Hata sasa ikiwa unategemea jitihada zako, zikupe haki mbele za Mungu, ndugu umepotea. Hutaweza Itegemee neema ya Mungu. Na hiyo itakusaidia kuyatimiza hayo mengine kwa Roho Mtakatifu.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

FUNDISHO KUU LA NEEMA YA MUNGU KWETU.

Nini maana ya kumsulibisha mwana wa Mungu mara ya pili?

Rudi nyumbani

Print this post

Mafuta mabichi ni mafuta ya aina gani? (Zaburi 92:10)

Swali: Mafuta Mabichi yapoje, na yanafunua nini kiroho?


Jibu: Tureje..

Zaburi 92:10 “Bali pembe yangu umeiinua kama pembe ya nyati, Nimepakwa MAFUTA MABICHI”.

Mafuta mabichi yanayozungumziwa hapo si mafuta ambayo hayajapitishwa kwenye moto yakaiva na kuchemka… La!.. bali ni mafuta yaliyo mapya (yaani freshi) ambayo yayajakaa muda mrefu.

Nyakati za biblia na hata sasa wayahudi wanatumia mafuta ya Mizeituni kwa matumizi ya chakula na ibada.

Asilimia kubwa ya vyakula vya wayahudi na baadhi ya jamii za mashariki ya kati wanatumia mafuta ya Mizeituni kama kiungo cha mboga, na wakati jamii nyingine mbali na hizo wanatumia mafuta ya Alizeti au mimea mingine katika mapishi.

Chakula kilichoandaliwa kwa mafuta mabichi (yaani mapya) ya Mizeituni kinakuwa ni kitamu na chenye ladha… utaona hata ile MANA jangwani, ladha yake ilifananishwa na ladha ya mafuta mapya. (soma Hesabu 8:11).

Vile vile katika shughuli za kiibada, pale ambapo mtu anatawazwa kuwa mfalme basi alipakwa Mafuta haya ya mizeituni kama ishara ya kuruhusiwa kuchukua madaraka hayo,

1Samweli 9:15 “Basi Bwana alikuwa amemfunulia Samweli, siku moja kabla Sauli hajamwendea, akisema,

16 Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mtu kutoka nchi ya Benyamini, NAWE MTIE MAFUTA ili awe mkuu juu ya watu wangu Israeli, naye atawaokoa watu wangu na mikono ya Wafilisti; maana nimewaangalia watu wangu, kwa sababu kilio chao kimenifikilia”

Soma pia1Wafalme 16:12, 1Wafalme 1:34, na 1Wafalme 19:15-16 utaona jambo hilo hilo..

Vile vile makuhani walitiwa mafuta kama ishara ya kuchaguliwa na Mungu kutumika katika nyumba yake.

Zaburi 133:2 “Ni kama mafuta mazuri kichwani, Yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni, Yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake”.

Sasa ilikuwa ni heshima na jambo jema kutiwa mafuta ambayo ni mapya.. Kwani Mafuta ya Mizetuni kama yamehifadhiwa vizuri yanadumu kwa miaka 2 tu, ukipita huo muda yanaharibika na kutoa harufu nyingine. Kwahiyo chakula kilichoandaliwa kwa mafuta yaliyokaa kinakuwa hakina ladha na pia kinatoa harufu mbaya…

Vile vile mtu aliyepakwa mafuta yaliyokaa sana au kuharibika si jambo la utukufu… lakini mafuta mabichi ilikuwa ni jambo la utukufu kwasababu ni freshi.

Sasa mafuta mabichi (yaani mapya) na yale yaliyokaa (yaani ya zamani) yanawakilisha nini sasa kiroho?..

Mafuta yanamwakilisha ROHO MTAKATIFU. Hivyo mafuta yaliyokaa (ya zamani) yanawakilisha utendaji kazi wa Roho Mtakatifu katika Agano la kale… na Mafuta mapya ni utendaji wa ROHO MTAKATIFU katika agano jipya.

Na sisi tunayahitaji mafuta mabichi katika UTUMISHI WETU,  na si yale yaliyokaa… kwasababu hayatatufaa sana..

Mafuta mapya yanatufundisha kuwa wakamilifu zaidi na katika kuyafanya mapenzi ya Mungu..kuliko yale ya zamani.

Mathayo 5:27  “Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini;

28  lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.

29  Jicho lako la kuume likikukosesha, ling’oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.

30  Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.

31  Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka;

32  lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.

33  Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako;

34  lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu”.

Je umempokea YESU KRISTO, aliye mjumbe wa Agano jipya?, kumbuka huwezi kuwa na ROHO MTAKATIFU, kama YESU KRISTO hayupo ndani ya maisha yako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza

Je tunaruhusiwa kujipaka mafuta au kujipulizia marashi?

MAANA YA KRISTO/ JINA KRISTO LINA MAANA GANI?

 Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako,katika kufanya maombezi?

Mfano wa wanawali kumi(Mathayo 25), unaelewekaje?

Rudi nyumbani

Print this post

Je kuwashwa mkono ni ishara ya kupata pesa?

Swali: Je ni kweli kwamba kiganja cha mkono wa kushoto au wa kulia kikiwasha basi ni ishara ya kupata pesa?


Jibu ni LA!.. hakuna uhusiano wowote  kiganja kuwasha na fedha kumjia mtu. Labda kama mtu huyo ana pepo la utambuzi ndani yake..

Kama mtu ana pepo la utambuzi basi anaweza kuhisi kitu Fulani kikimjia, ikiwemo pesa kutoka katika chanzo kisicho cha kiMungu, au akahisi hatari kutoka katika upande wa maadui zake (maana yake upande wa Mungu), na ishara hizo anaweza kuzihisi kwa njia kama hizo za kuwashwa mkono, au kuwashwa sehemu nyingine ya mwili.

Lakini mtu mwenye Roho wa Mungu hisia zake zipo katika Neno la Mungu..Anaposoma Neno la Mungu na kudumu katika uwepo huo basi anaweza kuhisi Baraka zijazo, au hatari ijayo.

Kwamfano Neno hili katika biblia linaweza kukupa hisia za Baraka zijazo…

Mithali 13:11 “Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa”.

Mtu akilisoma hili Neno la kulishika, tayari atakuwa anajua ni nini kitafuta katika shughuli anayoifanya.. lakini si kukisikilizia kiganja kinasema nini!.. Na maneno mengine yote ya Mungu ni hivyo hivyo..

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba,  Elimu ya kusoma viungo vya mwili na kutabiri mambo yajayo ni elimu ya adui na ya kupotosha..

Lakini pia kumbuka si kila anayewashwa mkono basi ana pepo la utambuzi!.. La!, mkono unaweza kuwasha kwa sababu nyingine yoyote ya kibaolojia, na mtu asiwe na pepo!.. (Hata hivyo asilimia kubwa ya wanaowashwa mikono hawana mapepo). Hivyo kilicho kikubwa na cha msingi ni kudumu katika Neno la Mungu.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KUOTA UNAPEWA PESA, KUNA MAANISHA NINI?

Pesa za bindoni ni nini?(Marko 6:8)

Je! fedha ni jawabu la mambo yote? (Mhubiri 10:19).

MADHARA YA KUTAFUTA ISHARA.

Biblia inaposema Yesu ameketi mkono wa kuume inamaana gani?

Rudi nyumbani

Print this post

Isaya 40:12 ‘maji kwa konzi ya mkono, na mbingu kwa shubiri’

SWALI: Naomba kufahamu nini maana ya Isaya 40:12 inaposema maji kwa konzi ya mkono, na mbingu kwa shubiri?

Isaya 40:12 “Ni nani aliyeyapima maji kwa konzi ya mkono wake, na kuzikadiri mbingu kwa shubiri, na kuyashika mavumbi ya dunia katika pishi, na kuipima milima kwa uzani, na vilima kama kwa mizani”?


 JIBU: Ukianzia kusoma vifungu vya juu na kuendelea vile vya chini, utaona Mungu anawaambia watu wake Israeli kuwa atawajilia kama mchungaji awachungaye kondoo wake , na kuwalisha, na kuwakuongoza, na kuwakusanya kifuani mwake, hata wale walio wachanga, ndivyo atakavyowatendea watu wake na hilo litawezekana.

Lakini Israeli waliona kama jambo hilo linaweza lisiwe rahisi, Ndio hapo akawaambia sasa katika vifungu vifuatavyo maneno hayo. Kwamba “Ni nani aliyeyapima maji kwa konzi ya mkono wake”? Maji anayoyazungumzia hapo ni maji mengi, mfano wa bahari, na maziwa Je! Kuna mtu yeyote anayeweza kuyakusanya maji mengi namna hiyo kwenye viganja vyake? Jibu ni hapana! Lakini kwa Mungu ni jambo dogo sana.

Vilevile anawauliza ni nani awezaye ‘kuzikadiri mbingu kwa shubiri’?. Shubiri ni kipimo cha urefu, wa kiganja, toka kidole gumba mpaka kile cha katikati vinaponyooshwa. Na ni wazi hakuna mtu anayeweza kupima ukubwa wa mbingu, toka sayari moja hadi sayari nyingine, kwa kipimo chochote kile cha kibinadamu. Lakini kwa Mungu hilo ni jambo dogo sana, ni kama kuzipima kwa shubiri.

Halikadhalika anauliza  ni nani awezaye kuyashika mavumbi ya dunia katika pishi?. Pishi ni kopo dogo, je kuna mwanadamu anaweza kuyakusanya mavumbi yote duniani, kama vile akusanyavyo yale machache kwenye kopo lake. Ni wazi hakuna awezaye kuwa na pipa la uwezo huo.

Vilevile anauliza ni nani anayeweza kuipima milima kwa uzani, na vilima kama kwa mizani?. Je! Kuna mizani yoyote ya kibinadamu inaweza kuiweka milima juu yake, na kutoa vipimo?. Jibu ni hakuna. Lakini kwa Mungu ni jambo dogo sana. Milima ni kama vipunje vidogo sana vya mchanga.

Ikiwa haya yanaonekana magumu kwa mwanadamu, lakini kwa Mungu ni mepesi. Vivyo hivyo jambo la kuwakusanya watu wake, au kuwasaidia, lisitizamwe kibinadamu, kwasababu uweza wa Mungu ni mkuu sana usioweza kufikirika kibinadamu. Maswali ya namna hii ndio kama yale Mungu aliyokuwa anamuuliza Ayubu, (Ayubu 38-41), na katika Mithali 30:4

Yesu kama mchungaji wetu mkuu, anauwezo wa kutukusanya kama kondoo wake. Haijalishi tutaonekana tumetawanyika mbali kiasi gani, lakini akisema jambo ni lazima liwe. Halikadhalika na katika mambo yetu yote ya kiroho na kimwili.

Hivyo kitabu cha Isaya sura ya 40 yote, kinaeleza uweza wa Mungu, usiopomika kibinadamu. Lakini Swali ni Je! Kristo amekusamehe dhambi zako? Kama ni la! Basi nafasi bado unayo leo. Mwamini yeye akuokoe. Na kukupa ondoleo la dhambi zako.

Kwa mwongozo wa namna ya kupokea wokovu basi fungua hapa>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)

Kuna Mbingu ngapi?

Mbinguni ni sehemu gani?

Rudi nyumbani

Print this post