SWALI: Neno ‘huisingizia sheria na kuihukumu sheria’ maana yake nini? (Yokobo 4:11)
Yakobo 4:11 Ndugu, msisingiziane; amsingiziaye ndugu yake, au kumhukumu ndugu yake, huisingizia sheria na kuihukumu sheria. Lakini ukiihukumu sheria, huwi mtenda sheria, bali umekuwa hakimu.
JIBU: Ili kuelewa vifungu hivyo Mtume Yakobo kwa uongozo wa Roho alikuwa na maana gani aliposema Mtu amsingiziaye ndugu yake au amuhukumuye ndugu yake huisingizia sheria na kuihukumu sheria, Tafakari mfano huu.
Raisi ya nchi amendea mahali Fulani kwa ajili ya shughuli zake za kimaendeleo, lakini katika kupita pita kwake akaona familia moja iliyo fukara sana, na alipotathimini tatizo nini akaona walikuwa wote ni walemavu hawawezi kufanya kazi kabisa, hivyo kwa huruma zake akaagiza wajengewe nyumba, wapewe na msaada wa chakula kutoka serikali kila mwezi, walipiwe na pia bili za maji na chakula kwa kipindi chote wawapo hai.
Lakini Yule raisi alipoondoka, mkuu wa mkoa wa eneo lile, akaenda kuitazama ile familia ikoje, badala ya kutekeleza agizo la mkuu wake, akaanza kuwashitaki na kusema hawa hawana ulemavu wa kuwafanya wasifanye kazi, wanajifanya tu wadhaifu, ni wavivu, wanaweza kuendesha maisha yao, hakuna haja ya kuwapa chochote, hivyo akaanza kuwaonea na kuwashutumu, na kuwanyima mahitaji yao kwa wakati, na kuwashurutisha wajitume.
Sasa Kimsingi mtu kama huyu, ni rahisi kudhani, anawaudhi na kuwashutumu tu wale maskini, Lakini kiuhalisia anamudhi na kumshitaki raisi aliyetoa amri ile kwamba walishwe. Kwa tabia hiyo ni kwamba anamshtaki raisi hafikirii vizuri, anatumia fedha za uma vibaya, anatafuta sifa kwa watu, ana maamuzi yasiyokuwa na maana, hata kama huyo mkuu wa mkoa hawazi hivyo, anampenda raisi wake, na anathamini mali zake, lakini kitendo tu cha kuwashutumu wale, ni sawa na anamshutumu aliyewafadhili.
Ndivyo ilivyo na katika kifungu hicho, Wewe kama mwamini, unapomsingizia ndugu yako, Maana yake unakwenda kinyume na sheria ya Kristo tuliyopewa ya kupendana, unapomhukumu ndugu yako unakwenda kinyume na sheria ya Kristo inayosema Usikuhukumu (Mathayo 7:1).
Hivyo unaihukumu hiyo sheria kwamba ina makosa, wakati Bwana aliiona ni bora, lakini wewe unakwenda kinyume na hiyo.
Hivyo sisi kama wana wa Mungu hatujaitwa tuwashutumu watu, tutafute kasoro ndani ya ndugu zetu, kana kwamba sisi, hatuna maboriti kwenye macho yetu, ila tumeitwa tuitende sheria, na kuonyana, na kuelekezana, na kujengana, katika upendo, lakini sio kutoa hukumu kwa wengine, kana kwamba sisi ni mahakimu.
Tumeagizwa tunapomwona ndugu yetu ameghafilika tumrejeshe kwa upendo, sio kwa mashutumu, hiyo ndio sheria ya Kristo.
Wagalatia 6:1 Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.
2 Mchukuliane mizigo na KUITIMIZA HIVYO SHERIA YA KRISTO. 3 Maana mtu akijiona kuwa ni kitu, naye si kitu, ajidanganya nafsi yake.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Je Yesu ni Mungu au Nabii?
MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?
JE! UMEYABATILISHA MAMBO YA KITOTO?
Print this post
Jibu: Turejee..
Wakolosai 4:6 “Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea MUNYU, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu”.
“Munyu” ni kiswahili kingine cha “chumvi”. Neno hili limeonekana mara moja tu katika biblia..
Hivyo hapo maandiko hayo yanaweza kusomeka hivi…
“Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea CHUMVI, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu”.
Sasa swali; Maneno yaliyokolea Munyu/chumvi ndio maneno gani?.
Kabla ya kuyaangalia haya maneno hebu tujifunze matumizi ya chumvi.
Mbali na kwamba chumvi ni kiungo cha kuongeza ladha ya chakula, lakini pia ilitumika kwaajili ya kuhifadhia vitu ili visiharibike.
Enzi za zamani hakukuwa na friji kama tulizo nazo sasa, hivyo kitu pekee kilichotumika kuhifadhia chakula ambacho hakijapikwa ilikuwa ni chumvi?.
Kwahiyo chakula kilichotiwa chumvi kilidumu muda mrefu, na kitu kingine chochote..
Soma zaidi kuhusu Agano la chumvi hapa》》Agano la Chumvi ni nini? (2Nyakati 13:5)
Sasa tukirudi katika “maneno” ni hivyo hivyo… “maneno yaliyokolea chumvi/munyu” mbali na kwamba ni maneno yaliyokolea ladha za kiroho..Lakini pia ni “maneno yenye kidumu muda mrefu”…yasiyopita!
Ni maneno yenye kidumu si mengine zaidi ya yale yenye kutangaza habari za uzima wa milele.
Ni maneno yenye kutangaza tumaini lililopo ndani ya YESU..maneno yenye kumpa mtu hamasa ya kumtumikia Mungu ili awe na nafasi katika ule mji mtakatifu..
Ni maneno yote yaliyonenwa na YESU mwenyewe…
Mathayo 24:35 “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”.
Lakini maneno yasiyo na munyu ni yale yote yenye kunia na kutukuza mambo ya duniani ambayo yapo leo na kesho hayapo..
Yakobo 4:13 “Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida; 14 walakini hamjui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka”.
Yakobo 4:13 “Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida;
14 walakini hamjui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka”.
Bwana atusaidie maneno yetu yakolee munyu daima.
IMANI YENYE MATENDO
Agano la Chumvi ni nini? (2Nyakati 13:5)
Ninyi ni chumvi ya dunia, Andiko hilo lina maana gani?
HAMJAFAHAMU BADO?
JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.
Rudi Nyumbani
Ipo hali ambayo tunapaswa tukutwe nayo wakati wa kuja kwake Bwana YESU…na endapo akitukuta tupo nje na hiyo hali basi hatutaenda naye, badala yake tutabaki na kukumbana na hukumu ya MUNGU.
Sasa “hali” hiyo ni ipi?..
Hebu tusome maandiko yafuatayo.
1 Wathesalonike 5:23 “Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, WAKATI WA KUJA KWAKE BWANA WETU YESU KRISTO”.
Kumbe Bwana YESU atarudi tena!!!!….. na wakati atakaporudi anatazamia tuwe tumetakasika katika maeneo hayo matatu 1) NAFSI 2) ROHO na 3)MWILI.
Vinginevyo mambo hayo matatu yasipokuwa masafi wakati wa kuja kwake Bwana YESU basi kuna hatari kubwa sana.
1.NAFSI.
Ndani ya nafsi kuna maamuzi, hisia na mawazo.. Hivi vinapaswa viwe visafi daima.
Na vinakuwaje visafi?… Kwa kumpokea YESU, kusoma Neno na kuomba.
Usipokuwa mwombaji nafsi yako haiwezi kuwa safi utakuwa mtu wa hasira tu, mtu wa uchungu tu..usipokuwa msomaji wa Neno la Mungu kamwe nafsi yako haiwezi kustahimili majaribu na pia utakuwa mtu usiye na mwongozo n.k.
2.ROHO.
Ndani ya roho ya mtu kuna uzima, na ndio chumba pekee cha ibada ambacho kinaongozwa na Imani.
Roho ya mtu isipokuwa safi, mtu huyo hawezi kwenda na Bwana siku ya unyakuo…na hata maisha yake ya duniani hawezi kumwona Mungu.
3. MWILI.
Mwili ni vazi la roho ya mtu, na ndilo limejumuisha viungo vyote vya ndani na nje.
Na mwili unapaswa uwe safi (usafi wa kimatendo)..Mwili mchafu kibiblia sio ule wenye jasho au vumbi…mwili mchafu ni ule unaofanya uasherati na zinaa, ni ule unaojichua, ni ule unaotembezwa uchi barabarani, ni ule unaoshika fedha za wizi na utapeli.
Huo ndio mwili mchafu, ambao kama hautatakaswa wakati wa kuja kwake Bwana utampoteza mtu huyo.
Na mtu hautakasi mwili wake kwa kuoga na maji moto, au kwa kumeza vidonge vya matibabu au mitishamba…bali kwa kuacha matendo yote ya mwili yanayotajwa katika Wagalatia 5:19-20.
Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, 20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.
Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.
Kwa hitimisho ni kwamba kila mtu lazima ajitakase na kuhifadhi utakaso wake ambao ndio tiketi ya kumwona Bwana siku atakaporudi.
Je umempokea Bwana YESU?…Kama bado unasubiri nini??… Na kama tayari umeshampokea je! umetakaswa nafso yako, roho yako na mwili wako?..
Kwa mwongozo wa maombi ya kujijenga kiroho juu ya mambo hayo matatu (nafsi, mwili na roho) basi wasiliana nasi inbox.
Maran atha!.
MCHE MWORORO.
KWANINI TUNAPASWA KWENDA KUIHUBIRI INJILI KWA UJASIRI WOTE?
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
JITAHIDI KUJA KABLA YA WAKATI WA BARIDI.
Biblia inamaanisha nini kusema Yeye aliye na sikio, na asikie?
(Masomo ya kanuni za kuomba).
Mathayo 9:38 “Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake”.
Maombi ni jambo kuu na la msingi sana.
Hapa biblia inasema TUOMBE (Bwana apeleke watenda kazi).
Kumbe Maombi ya kuomba uamsho wa watenda kazi ni muhumu!. Kwasababu hiyo basi ni lazima tujiwekee utaratibu wa mara kwa mara kuomba Bwana aongezee watenda kazi.
Na yafuatayo ni baadhi ya maeneno yanayohitaji watenda kazi zaidi.
1.KANISANI.
Hii ni sehemu ya kwanza inayohitaji watenda kazi. Waalimu wa madarasa ya jumapili wanahitajika zaidi ndani ya kanisa, halikadhalika waalimu wa watoto, pia watendakazi katika kuongoza sifa na maombi na wengine wengi.
Hivyo ni muhimu kutenga muda wa kutosha kumwomba BWANA anyanyue watenda kazi yeye anajua yupi anatafaa mahali fulani sisi kazi yetu ni kuzidi kumsihi Bwana awanyanyue wengi.
2. MASHULENI.
Shule kuanzia zile za awali (chekechea) mpaka zile za juu (vyuoni) panahitajika sana watenda kazi, watakaofanya kazi ya mavuno..
Hivyo ni muhimu watu wa Mungu kuomba ili Bwana anyanyue jeshi la watenda kazi (wahubiri) kwenye mashule.
Kwani mbali na mambo mazuri yanayopatikana mashuleni lakini.huko huko pia ndio kitovu cha watoto kujifunza tabia chafu na kupokea maroho ya mapepo.
Na wakati mwingine ni ngumu mtu wa nje kuwafikia na kuwahubiria, hivyo mimi na wewe tukisimama kumwomba Bwana anyanyue watenda kazi katikati yao, basi Bwana atatusikia na kunyanyua vijana miongoni mwao huko huko waliko ambao watawatengeneza wenzao au atawanyanyulia walimu miongoni mwa walimu wanaowafundisha na watawafundisha na kuwakuza kiroho.
3. MAHOSPITALINI.
Hii ni sehemu ya tatu inayohitaji watenda kazi. Vituo vingi vya afya vinategemea kupokea watumishi kutoka nje kwaajili ya maombi kwa wagonjwa…
Wakati mwingine jambo hili linakuwa ni gumu sana, kutokana ni vizuizi vya kiserikali na uchache wa watenda kazi…na hivyo wagonjwa wengi wanakufa katika dhambi na wengine kuonewa vikali na ibilisi na mapepo yake yachocheayo magonjwa.
Lakini tukisimama kuomba kwamba Bwana anyanyue watenda kazi basi, Bwana atasikia kwasababu ndiye aloyetuambia tuombe.
Na matokeo ya kuomba ni madaktari wengi kuokoka na manesi na wahudumu wa vituo hivyo vya afya na hivyo wagonjwa wengi wataombewa na kufunguliwa na kumpokea BWANA YESU, pasipo kusubiri watumishi kutoka nje.
4. SERIKALINI.
Hii ni sehemu ya nne inayohitaji watenda kazi wengi…kwani huko serikalini ikiwemo katika mabunge, wizara na mahakama, adui anadhulumu wengi na kuwapoteza wengi, na hiyo ni kutokana na upungufu wa watenda kazi.
Lakini tukisimama kuomba, Bwana YESU atasikia na kunyanyua watenda kazi ndani ya serikali..Watanyanyuka watu mfano wa akina Danieli na Yusufu ambao watahubiri na kufundisha na kukemea kazi za ibilisi katika mahakama, bunge na katika asasi zote za serikali.
5. MITAANI.
Hili ni eneo la tano linalohitaji watenda kazi wengi…Kwani katika mitaa ndiko watu wanakofanyia kazi, wanakokusanyika katika vigenge vya mizaha, au wanakofanyia mabaya.
Hivyo kunahitajika injili sana, ili watu waokolewe… na wakati mwingine inakuwa ni ngumu kufika kila mtaa kuhibiri, au watumishi wa Mungu kuzunguka kila mahali kuhubiri na kuombea watu.
Lakini kama tukisimama kumwomba BWANA anyanyue watenda huko basi kazi (katikati ya hao hao wahuni, au hao hao wanaofanya kazi haramu, au wanaoketi katika vijiwe vya mizaha) basi kazi ya injil itakuwa nyepesi sana na yenye matunda mengi.
Tutashangaa kuona wale waliokuwa walevi namba moja ndio wahubiri namba moja, wale waliokuwa makahaba namba moja ndio wainjilisti namba moja n.k
6. MITANDAONI
Hii ni sehemu ya sita na muhimu sana inayohitaji watenda kazi.
Kwani katika mitandao ndiko watu wanakojifunzia mambo yote maovu, ndani ya mitandao watu wanajifunza mauaji, kiburi, uasherati, uchawi, utapeli, wizi na mambo yote mabaya ambayo biblia inayataja kama malango ya kuzimu.
Na wanaotumia mitandao hiyo kuhubiri habari njema ni wachache ukikinganisha na wale wanaoitumia kusambaza maovu.
Lakini tukisimama na kumwomba Bwana awageuze watu na kuwafanya watenda kazi shambani mwake, tutaona mageuzi makubwa.
Kwani wale waliokuwa wanahamasisha wizi, uasherati, utapeli na uhuni ndio watakaokuwa vipaumbele kuitumia mitandao hiyo hiyo kumhubiri YESU na kusaidia wengi,..
Wale waliokuwa watangazaji watageuzwa na kutangaza habari njema, wale waliokuwa waigizaji wa tamthilia za mapenzi ya kishetani sasa wanatengeneza mafundisha ya kuwajenga watu kiroho n.k
Lakini ikiwa tutaomba kwa bidii sana.
Hayo ni meneo sita yanayohitaji watenda kazi, yapo na maeneo mengine mengi lakini haya sita ndio yenye vipaumbele zaidi.
Hivyo kama mtu uliyeokoka usiishie tu kuombea familia yako, au kazi zako au ndugu zako au kanisa lako..
Piga hatua zaidi kuombea ongezeko la watenda kazi katika shamba la Mungu, kwani maombi hayo ni ya muhimu na yenye thawabu nyingi.
Maran atha.
MAVUNO NI MENGI
MWISHO WA MAVUNO, NI MWISHO WA DUNIA.
Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?
Fahamu Namna ya Kuomba.
VIACHENI VYOTE VIKUE HATA WAKATI WA MAVUNO.
Je ni malaika wawili au mmoja
Swali: Katika Luka 24:4-6, biblia inasema ni malaika wawili..lakini tukirudi katika Marko 16:5-6 tunasoma ni malaika mmoja. Je biblia inajichanganya, au mwandishi yupi yupo sahihi?.
Marko 16:5 “Wakaingia kaburini wakaona kijana ameketi upande wa kuume, amevaa vazi jeupe; wakastaajabu”.
Ni kweli hapa biblia inasema ni malaika mmoja, tena ni kijana.
Lakini hebu twende kwenye Luka, tuanzie ule mstari wa 4 hadi wa 6.
Luka 24:4“Ikawa walipokuwa wakifadhaika kwa ajili ya neno hilo, tazama, watu wawili walisimama karibu nao, wamevaa nguo za kumeta-meta; 5 nao walipoingiwa na hofu na kuinama kifudifudi hata nchi, HAO WALIWAAMBIA, Kwa nini mnamtafuta aliye hai katika wafu? 6 Hayupo hapa, amefufuka. Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa akaliko Galilaya”
Luka 24:4“Ikawa walipokuwa wakifadhaika kwa ajili ya neno hilo, tazama, watu wawili walisimama karibu nao, wamevaa nguo za kumeta-meta;
5 nao walipoingiwa na hofu na kuinama kifudifudi hata nchi, HAO WALIWAAMBIA, Kwa nini mnamtafuta aliye hai katika wafu?
6 Hayupo hapa, amefufuka. Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa akaliko Galilaya”
Je ni kwamba biblia inajichanganya? Au kuna mwandishi ambaye hayupo sahihi?.
Jibu ni la! Biblia haijichanganyi na wala haijawahi kujichanganya kabisa isipokuwa tafakari zetu ndio zinajichanganya.
Sasa katika maandiko hayo hakuna mwandishi aliyekosea wala anayempiga mwenzake.
Waandishi wote wapo sahihi na malaika waliowatokea ni wanawake wale walikuwa ni wawili na si mmoja.
Isipokuwa malaika aliyesema na wanawake wale ni mmoja kati ya wale wawili na ndiye huyo aliyetajwa na Marko.
Tunajuaje kuwa ni malaika mmoja ndiye aliyekuwa anazungumza na mwingine amenyamaza?.
Tunafahamu kupitia mwandishi wa kitabu cha Luka ule mstari wa 5 unaosema…. “nao walipoingiwa na hofu na kuinama kifudifudi hata nchi, HAO WALIWAAMBIA, Kwa nini mnamtafuta aliye hai katika wafu?….
Hapo anasema “Hao waliwaambia”…sasa kwa kauli hiyo isingewezekana wote waseme kwa pamoja maneno hayo kama maroboti…Ni wazi kuwa ni malaika mmoja ndiye aliyetoa hiyo kauli na hivyo ikawa ni sawa wote wamesema.
Na huyo mmoja aliyetoa hiyo kauli ndiye anayetajwa na Marko…lakini Luka anataja uwepo wa wote wawili.
Ili tuelewe vizuri tutafakari mfano huu… wanahabari wawili wanaripoti hotuba ya Raisi na wa kwanza akasema hivi…. “Raisi wa nchi ya Tanzania amezuia matumizi ya vifungashio vya plastiki”…
Na mwandishi mwingine wa nje aripoti hivi..”Watanzania wazuia matumizi ya vifungashio vya plastiki”.
Je waandishi hawa watakuwa waongo?…au je kuna mmoja atakuwa anampinga mwenzake?..
Jibu ni la! Wote watakuwa sahihi kwani kauli na Raisi ni kauli ya watazania wote…atakalosema Raisi ni sawa na watanzania wote wamesema.
Sawa sawa kabisa na hiyo mwandishi wa Luka…alitaja kauli ya ujumla ya malaika wote wawili na Marko akataja ya mmoja tu (yule aliyetoa kauli).
Je umempokea Bwana YESU KRISTO?.
Kama bado unasubiri nini?..ule mwisho umekaribia sana na Bwana YESU amekaribia kurudi sana.
Ikiwa utahitaji msaada wa kumpokea Bwana YESU basi waweza wasiliana nasi na tutakuongoza sala ya kumkiri Bwana YESU baada ya wewe kumwamini.
Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?
WAZAZI WA YOHANA NA YAKOBO
Forodhani ni mahali gani?
Biblia inaposema Yesu ameketi mkono wa kuume inamaana gani?
DANIELI: Mlango wa 11
SWALI: Naomba kufahamu maana ya unabii unaozungumzia taifa la Tiro (Isaya 23). Kwamba litafanya ukahaba na falme zote ulimwenguni kisha utajiri wake utakuwa wakfu kwa Bwana. Tafsiri yake ni nini?
Isaya 23:17-18 inasema..
[17]Hata itakuwa mwisho wa miaka sabini, BWANA ataizuru nchi ya Tiro, naye atarudi apate ujira wake, atafanya ukahaba pamoja na falme zote za ulimwengu juu ya uso wa dunia. 18 Na biashara yake na ujira wake utakuwa wakfu kwa BWANA, hautawekwa hazinani wala hautawekwa akiba; bali mapato ya biashara yake yatakuwa mali zao wakaao mbele za BWANA, wapate kula na kushiba, na kuvaa mavazi ya fahari.
[17]Hata itakuwa mwisho wa miaka sabini, BWANA ataizuru nchi ya Tiro, naye atarudi apate ujira wake, atafanya ukahaba pamoja na falme zote za ulimwengu juu ya uso wa dunia.
18 Na biashara yake na ujira wake utakuwa wakfu kwa BWANA, hautawekwa hazinani wala hautawekwa akiba; bali mapato ya biashara yake yatakuwa mali zao wakaao mbele za BWANA, wapate kula na kushiba, na kuvaa mavazi ya fahari.
JIBU: Ukianza kusoma toka mstari wa kwanza wa hiyo sura ya ishirini na tatu (23), utaona Mungu anazungumzia adhabu, aliyoitoa kwa hilo taifa la Tiro lililokuwa na utajiri na mali nyingi kutokana na biashara zake lilizofanya na dunia nzima. Hata kuyakosesha na mataifa mengine, kwa bidhaa zake. Na jambo hilo Mungu akalihesabu kama ni ukahaba, hivyo akalipiga na kuliangusha kabisa likawa si kitu tena kwa muda wa miaka sabini(70).
Ni mfano tu, mataifa yanayokosesha ulimwengu sasa, kwa kuuza bidhaa ambazo ni machukizo kwa Mungu, utakuta taifa linazalisha nguo za mitindo ya nusu uchi, na kuyauzia mataifa mengine, au linatengeneza sinema zenye maudhui za kizinzi na kuyasambazia mataifa mengine yaliyokuwa na maadili.. Huo ndio mfano wa ukahaba ambao taifa la Tiro lilikuwa linafanya.
Isaya 23:15
[15]Basi, itakuwa katika siku ile, Tiro utasahauliwa miaka sabini, kadiri ya siku za mfalme mmoja; hata mwisho wa miaka sabini, Tiro utakuwa kama vile ulivyo wimbo wa kahaba.
Lakini baadaye Mungu alilirudia tena, na kuruhusu lifanikiwe, kama pale mwanzo. Likajikusanyia tena utajiri mwingi sana kwa biashara zake.. Lakini Kwasababu halikutubu, kitabia Mungu akalipiga kwa namna nyingine kwa kuzuia utajiri wao wasiule au kwa lugha nyingine hazina zao zisitunzwe kwa maendeleo yao, Bali Bwana atazizuia zije kutumika kwa kazi yake yeye mwenyewe na watu wake.
Na unabii huo ulikuja kutimia..
ndio maana ya huo mstari wa 18, unaosema..
[18]Na biashara yake na ujira wake utakuwa wakfu kwa BWANA, hautawekwa hazinani wala hautawekwa akiba; bali mapato ya biashara yake yatakuwa mali zao wakaao mbele za BWANA, wapate kula na kushiba, na kuvaa mavazi ya fahari.
Hii ni kufunua nini?
Kufanikiwa kwake mwovu, kunatimiza makusudi mawili la kwanza ni aidha kwenda kujiangamiza mwenyewe (Mithali 1:32, Zab 92:7), au kumkusanyia mtu mwingine mwenye haki.
biblia inasema..
Mithali 28:8
[8]Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.
Watu wengi wanaofanikiwa isivyo halali,mara nyingi mali zao, hula wengine..Ndicho alichokifanya Mungu kwa taifa la Tiro.
Ni kutufundisha pia fedha na dhahabu ni mali ya Bwana. Yeye ana uwezo wa kuzuia na kuachilia, anauwezo wa kuwapa watu wake hazina za gizani ambazo hawajazisumbukia, kwa ajili ya kazi yake.
Hivyo kumbuka Bwana akufanikishapo, tembea na Kristo, kinyume na hapo, mambo hayo mawili yanaweza kukukuta, aidha mafanikio hayo yazidi kukuangamiza ufe uende kuzimu, au yaliwe na watu wengine kabisa wema usiowajua na kazi yako ikawa bure.
Shalom.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Masomo mengine:
Miji ya Tiro na Sidoni ni miji gani kwasasa?
Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)
Je ni halali kwa mkristo kufanya biashara ya Forex?
(Masomo maalumu kwa wahubiri).
Kama Mhubiri basi fahamu mambo haya manne..
2 Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki”.
Nataka tuone mambo haya manne (4), ambayo Neno la Mungu linafanya, ili tusikose shabaha katika utumishi wetu.
Hapo anasema “kila andiko lenye pumzi ya Mungu lafaa kwa MAFUNDISHO, na KUONYA na KUONGOZA na KUADIBISHA”
Na hakusema kila andiko lenye pumzi ya Mungu lafaa kwa “kuchekesha na kuburudisha na kuchangamsha na kusisimua”
Hebu tuangalie jambo moja baada ya lingine ambalo Neno la Mungu linafanya.
1. KUFUNDISHA.
Hapo Neno linasema “..lafaa kwa mafundisho”.. sasa mafundisho yanayozungumziwa hapa si yale ya jeografia au sayansi bali yale ya Uzima (yampayo mtu uzima wa roho yake).
Tito 2:1 “Lakini wewe nena mambo yapasayo mafundisho yenye uzima”.
Mafundisho yenye uzima ni yale yote yamtoayo mtu katika mkondo wa dhambi, kwani dhambi ndio adui wa kwanza wa mtu aletaye mauti (Warumi 6:23).
Hivyo msingi wa mafundisho ya kila mhubiri ni lazima yategemee Neno la Mungu (yaani biblia).
2. KUWAONYA WATU MAKOSA YAO.
Kuna tofauti ya kuonya na kuhukumu.
Kuhukumu ni kutoa tamko la mwisho la mwenendo wa mtu, jambo ambalo ni Mungu pekee ndiye awezaye kufanya..
Lakini “Kuonya” ni kumtahadharisha mtu kuhusiana na hatari iliyopo mbele yake kulingana na mwenendo anaoenda nao, ikiwa hatabadilika.
Kwamfano mtu anayeiba, ukimwambia aache wizi na ukamtahadharisha madhara yake kuwa yanaweza kumpelekea hata kifo (kuchomwa moto na watu)....hapo hujamhukumu bali umemwonya.
Na vivyo hivyo unapomtahadharisha mtu kuhusiana na madhara ya kuiba au dhambi/mwenendo mwingine wowote ulio mbaya kwamba ataenda kuchomwa kwenye moto wa milele kama asipobadilika hapo hujamhukumu bali umemwonya, na ndio kazi ya Neno la Mungu lenye pumzi ya uhai, ni kuwaonya watu makosa yao.
2 Timotheo 4:2 “lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho”.
Na kuonya inapaswa iwe sehemu ya mahubiri kwa kila mhubiri ya kila siku..
Waebrania 3:13 “Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa udanganyifu wa dhambi”.
Wapo watu wasemao kuwa zisihubiriwe sana habari za hukumu ijayo kwani kwa kufanya hivyo ni kuhukumu na kuwatisha watu.
Ni kweli mambo yajayo yanatisha, lakini sasa yamewekwa wazi katika biblia pasipo vificho, sasa kama kwenye biblia imeyaweka wazi pasipo maficho kuna haja gani ya mhubiri kuyaficha??.
Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.
Soma tena Wagalatia 5:19-20 na 1Wakorintho 6:9 utaona mambo hayohayo.
Kwahiyo kama mhubiri Onya, karipia na kemea.
3. KUONGOZA.
Biblia inasema Neno la Mungu ni mwanga na taa ya njia yetu (Zaburi 119:105).
Kama vile taa inavyoweza kumwongoza mtu katika giza nene vivyo hivyo na Neno la Mungu.
Mtu anaposikia Neno la Mungu na kulitii basi lile Neno linakuwa ni dira ya maisha yako, na mwongozo sahihi wa namna ya kuishi.
Kwasababu ndani ya biblia kuna mwongozo sahihi wa namna ya kuishi duniani, ( kiroho na kimwili)..
Zaburi 119:9 “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake?
Kwa kutii, akilifuata neno lako”
4. KUADIBISHA.
Kuadibisha maana yake ni kumfanyaa mtu awe na adabu.
Ili mtu awe na adabu katika mwenendo ni sharti apokee Neno la Mungu lenye uzima, na ni lazima kila mtu aliyempokea Bwana YESU awe na adabu.
Warumi 13:12 “Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru. 13 Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu”.
Warumi 13:12 “Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru.
13 Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu”.
1 Wathesalonike 4:12 “…mwenende kwa adabu mbele yao walio nje, wala msiwe na haja ya kitu cho chote”.
Bwana atusaidie tuyafanye hayo na zaidi ya hayo, tuwapo katika kufundisha au kuhubiri, vile vile tuadibike, na kuonyeka, na kufundishika na kuongozeka tusikiapo Neno la MUNGU.
Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; (Mithali 11:16)
Adabu ni nini biblia?
HERI, WALE MUNGU ASIOWAHESABIA MAKOSA YAO.
MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.
MAFUNDISHO YA NDOA.
Swali: Je sisi wakristo tunaruhusiwa kutumia emoji katika kufanya mawasiliano kwa njia ya kidigitali?.
Jibu: Biblia inasema…
Tito 1:15 “Vitu vyote ni safi kwa hao walio safi; lakini hakuna kilicho safi kwao walio wanajisi, wasioamini; bali akili zao zimekuwa najisi, na nia zao pia”.
Chochote kile (hata kiwe kizuri) endapo kikitumika vibaya kinaweza kuleta madhara au kikaingiza roho ya ibilisi ndani ya mtu, hata biblia ikitumika vibaya inaweza kumharibu mtu moja kwa moja, kuliko kumjenga, ingawa biblia si kitabu kibaya..
Sasa swali “Emoji” ni nini?…na je ni sahihi kutumiwa na mkristo?.
“Emoji” ni vijitaswira vidogo vidogo vyenye maumbile ya mfano wa mtu au vitu, ambavyo vinatumika kwenye simu za mikononi au komputa, vinavyosimama badala ya maneno au hisia.
Emoji hizi zinapotumika basi mtu anayevitazama anaweza kuelewa kirahisi ujumbe wa mwandishi au hisia za mwandishi.
Lakini pia ipo hoja kuwa emoji hizi zinapotumika basi nyuma yake zinakuwa na taswira nyingine au alama nyingine za ibilisi tofauti na zile zinazoonekana pale, hivyo mkristo au mtu yeyote anapozitumia anakuwa anapokea ile roho iliyopo nyuma ya vile viemoji, au anasambaza ile roho iliyopo nyuma ya emoji zile.
Je jambo hili lina ukweli?
Kabla ya kuona ukweli wa jambo hili, hebu tutafakari kwa pamoja jambo hili lingine.
Mtu anayetumia emoji fulani na kufikiri nyuma yake kuna alama/roho ya ibilisi je! anao uhakika gani kuwa ile herufu “A” au “B” au “C” anayoitumia kuandikia meseji kwenye simu/kompyuta nyuma yake hakuna roho ya ibilisi?.
Au ana uhakika gani kuwa herufi “Y” au “X” katika simu yake, nyuma yake haina alama ya ibilisi (freemason)?…na kwamba kila anapoandika ujumbe wenye herufi hizo anakuwa anasambaza roho ya ibilisi….je una uhakika gani kuwa haiko hivyo??…Kwa maana zote ni lugha za kompyuta.
Sasa kama mtu huyu ataona emoji zina shida na herufi anazozitumia (kama A,B,C ni salama (yaani hazina hatari yoyote)….basi bado hajatafakari vizuri.
Na kama ataona herufi pamoja na emoji zote za kwenye simu zimebeba roho nyuma yake basi matumizi yote ya simu si salama kwa mkristo, wala matumizi yote ya kompyuta, kwamaana yote yamejawa na hivyo vitu (viemoji na jamii ya hivyo)…kwamaana hata nembo ya whatsapp, au tweeter au application nyingine yoyote ya simu ni jamii ya hivyo vitu..
Sasa usalama upo wapi?… au tufanye nini? kama ile alama ya kibao cha barabarani nyuma yake ni alama ya freemason?..kama zile alama za msalani zinazoelekeza kuwa huku ni jinsia ya kiume na kule ya kike, nyuma yake kuna roho ya ibilisi je tufanye nini? (je tusitumie vyoo??)… tusitumie tena barabara?..tusinunue bidhaa zenye nembo hizo masokoni? ..au tufanye nini?
Je tuondoke ulimwenguni???…maana kila mahali pana hatari (hakuna usalama)…
Yohana 17:15 “Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu”.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba matumizi ya herufi, au emoji katika simu au kompyuta si dhambi wala hazimwingizii mtu roho ya ibilisi, wala hazimsambazii mtu mwingine roho…ikiwa herufi hizo au emoji hazina maudhui ya machafu ya dunia.(kama zinaa, ushabiki, mizaha, magomvi, matusi n.k)
Lakini kama mtu atakuwa ni mchafu kwa utu wa ndani (maana yake hajatakasika)..hata pasipo matumizi ya hizo emoji kwake yeye yupo hatarini kupokea roho ya ibilisi na hata kusambaza kwa wengine, lakini kwa aliye mkamilifu hawezi kupokea roho kwa hizo wala kusambaza..
Lakini pamoja na hayo yote, si sharti kutumia hizo herufi wala emoji, wala si sharti wala amri kutumia simu wala kutumia kompyuta, wala chochote chenye alama hizo alama ikiwa mtu anapenda kujizuia na matumizi ya mambo hayo (kwa sababu zake binafsi) hafanyi dhambi.
Bwana atusaidie.
Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”.
Je unaelewa maana ya kukaa ndani ya YESU (kuwepo ndani ya YESU) ??kwasababu ipo tofauti ya Bwana YESU kukaa ndani yako, na wewe kukaa ndani yake.
Kukaa ndani si Kumpa YESU maisha yako!!!…Ni zaidi ya hapo!.
Je ulishawahi kusikia mtu akisema “fulani nimemtoa ndani yangu kabisa au moyoni”..??
Utakuwa unaelewa maana ya hiyo kauli kwamba huenda katendewa kitendo kibaya sana, au cha kuumiza au kudhalilisha…ikasababisha kumtoa huyo mru moyoni kabisa.
Vile vile kuna mtu utamsikia akisema “mtu fulani yupo sana moyoni mwangu”…
Maana yake mpaka kusema hivyo huenda huyo mtu kamfanyia jambo jema sana au la kugusa moyo wake, au la kumvutia, mpaka kufanya aingie moyoni mwake.
Na Bwana YESU ni hivyo hivyo, kuna watu wapo ndani yake (moyoni mwake)..na kuna watu hawapo kabisa moyoni mwake ijapokuwa wanaweza kukiri wanaye…
Kwanini?..
Jibu: Kwasababu hawajawahi kuugusa moyo wa Bwana hata kumfanya Bwana awaweke moyoni mwake..watu hawa kibiblia hawapo ndani ya YESU na Kristo ingawa wanaweza kukiri kwamba wanaye Kristo moyoni, na Bwana atawakana siku ile kwamba hawajui.
Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. 22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? 23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.
Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.
Yafuatayo ni mambo (Matendo) ambayo mtu anaweza kuyafanya yakaugusa moyo wa Bwana YESU , hata kumfanya mtu huyo awe ndani ya KRISTO (moyoni mwake).
Hili ni jambo la kwanza linalomzamisha mtu kwenye moyo wa KRISTO.
Yohana 6:56 “Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake. 57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi”.
Yohana 6:56 “Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake.
57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi”.
Kamwe usiidharau meza ya Bwana, lakini pia hakikisha unashiriki kulingana na Neno lake..Kwa kufanya hivyo utauteka moyo wa Bwana kwa kiwango kikubwa sana.
2.UMOJA.
Hili ni jambo la pili linalouteka moyo wa Bwana sana na kumzamisha mtu ndani ya moyo wake.
Yohana 17:21 “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. 22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja. 23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Yohana 17:21 “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.
23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Hivyo jenga sana desturi ya kutafuta Umoja wa Roho, usipende kukaa peke yako peke yako (huendi kanisani, hushirikiani na wengine..ni hatari kubwa sana).
3. MATOLEO.
Kumtolea Mungu kwa hiari pasipo kulazimishwa wala kushinikizwa, ni kitendo cha tatu kinachougusa sana Moyo wa Bwana (hauwezi kutoka moyoni mwake daima).
Mathayo 26:12 “Maana kwa kunimwagia mwili wangu marhamu hiyo, ametenda hivyo ili kuniweka tayari kwa maziko yangu. 13 Amin, nawaambieni, Kila patakapohubiriwa Injili hii katika ulimwengu wote, tendo hilo alilolitenda huyu litatajwa pia kwa kumbukumbu lake”.
Mathayo 26:12 “Maana kwa kunimwagia mwili wangu marhamu hiyo, ametenda hivyo ili kuniweka tayari kwa maziko yangu.
13 Amin, nawaambieni, Kila patakapohubiriwa Injili hii katika ulimwengu wote, tendo hilo alilolitenda huyu litatajwa pia kwa kumbukumbu lake”.
Huyu mwanamke amekuwa ndani ya moyp wa Kristo kwa vizazi vyote, mpaka sasa tunavyozungumza.
Usikwepe matoleo (sadaka) shetani amevuruga sana eneo hili la matoleo kwasababu anajua endapo mtu akipata ufunuo mkamilifu basi ataingia ndani ya Kristo moja kwa moja.
Unyenyekevu ni wa kukiri makosa, na kurudi kitubu na kuyokurudia rudia machafu, ni tendo kubwa sana linamwingiza mtu ndani ya YESU.
Luka 23:40 “Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo? 41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa. 42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako. 43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”
Luka 23:40 “Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?
41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.
42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.
43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”
Na yapo mambo mengine mengi katika maandiko yanayomwingiza mtu na kumdumisha ndani ya KRISTO.
Zifuatazo ni faida za kuwa ndani ya KRISTO.
Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”
2.Tunakuwa viumbe vipya.
2 Wakorintho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya”.
Hasara za kutokuwa ndani ya KRISTO ni kinyume cha faida hizo.
Bwana atusaidie tuingie na kudumu ndani yake.
NITASHINDAJE HALI YA KUUMIZWA NA MANENO YA WATU!
USIWE MKRISTO WA KUKAA TU GHALANI,
JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.
JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.
JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.
Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu Kristo, Karibu tujifunze habari njema za uzima wa roho zetu.
Neno la Mungu linatuambia..
2 Wafalme 19:30
[30]Na mabaki yaliyookoka ya nyumba ya Yuda yatatia mizizi chini, na kuzaa matunda juu.
Unaelewa maana ya mstari huu? Anazungumzia kustawi kwa nyumba ya Yuda (ambao ndio sisi kanisa)..
Lakini kustawi kwake hakuji hivi hivi, matunda yake kutokea kule juu, anasema kanuni yake ni lazima pia mizizi yake ikite chini.
Haiwezekani mti ukazaa kama hauna mzizi, jiulize je wewe una mizizi imara ya rohoni, ya kukufanya uweze kuzaa matunda yampendezayo Bwana?
Kumbuka kuthamini kwako wokovu, ndivyo hueleza urefu wa mizizi yako yenye nguvu, itakayokuwezesha kustawisha matunda juu.
Jani haliihitaji mizizi yoyote ya maana, kwasababu halina matunda ya kutoa.
Ukiona huwezi kuzama ndani katika wokovu, hauwi siriazi na maisha yako ya rohoni ujue pia hautakuwa na matunda yoyote kwa Mungu wako.
Katika ule mfano wa mpanzi Bwana Yesu alieleza kitu kilichofanya ile mbegu ya nne kustawi mpaka kuzaa matunda..anasema ilizaa kwa kuvumilia.(Luka 8:15)
kuvumilia nini?
Kuvumilia hatua zote 3 za mwanzo. yaani alihakikisha adui haibi mbegu iliyopandwa ndani yake, ni mtu ambaye aliweza kuvumilia dhiki, na majaribu yaliyozuka kinyume na lile neno lililopandwa moyoni mwake, alijiepusha na anasa, na kutoruhusu masumbufu ya ulimwengu huu kumsonga akashindwa kuivisha chochote. Hayo ndio mambo aliyovumilia.
Huyu ni mtu ambaye yupo makini na wokovu alioupokea.
Swali la kujiuliza je tunayo matunda hayo? kumbuka Hayaji kwa kutamani au kusubiri yanakuja kwa urefu wa mizizi yetu yenye uwezo wa kufikia vyanzo vya chini kabisa vyenye virutubisho vyote vya kustawisha matunda.
Ndio maana biblia inasema
Zaburi 1:1-3
[1]Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha. [2]Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku. [3]Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.
[1]Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
[2]Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.
[3]Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.
Anza sasa kushughulika na mizizi yako, mpaka ifikie kwa hakika mito hiyo ya maji.
Usipoe kimaombi, kimifungo, kiibada, kiuinjilisti, na kiusomaji Neno.
KWA KUVUMILIA AKAIPATA ILE AHADI.