Category Archive Uncategorized @sw-tz

Baraka ni nini na kuna aina ngapi za baraka?.

Jibu: Baraka ni thawabu ya kipekee itokayo kwa Mungu na kumfikia mtu akiwa hapa duniani.


Baraka yaweza kutokana na matendo mtu aliyoyatenda au maombi aliyoyaomba.

Kwamfano utamwona mtu anayeitwa Yabesi alimwomba Mungu ambariki na Mungu akasikia na kumbariki.

1Nyakati 4:10 “Huyo Yabesi akamlingana Mungu wa Israeli, akisema, Lau kwamba ungenibarikia kweli kweli, na kunizidishia hozi yangu, na mkono wako ungekuwa pamoja nami, nawe ungenilinda na uovu, ili usiwe kwa huzuni yangu! Naye Mungu akamjalia hayo aliyoyaomba”

Baraka za MUNGU zimegawanyika katika makundi makuu mawili;

  1. BARAKA ZA ROHONI.

Hizi ni baraka zinazoinufaisha roho ya mtu na ndizo zenye umuhimu sana kuliko zile nyingine.

Baraka ya kwanza ya rohoni ni “WOKOVU”. Mtu aliyepata Neema ya kumwamini YESU na kuoshwa dhambi zake huyo amebarikiwa, kwasababu anao uzima wa milele.

Waefeso 1:3 “Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa BARAKA ZOTE ZA ROHONI, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo”.

Baraka ya rohoni inazaa Furaha, amani, utulivu na utakatifu kwa ujumla.

Watu waliobarikiwa rohoni hata wakose vyote vya mwilini bado wanaishi maisha ya raha, kwasababu roho zao zimebarikiwa kuwa ndani ya YESU ambaye ni kila kitu.

  2. BARAKA ZA MWILINI.

Baraka za mwilini ni vyote ambavyo mtu anavipokea kutoka kwa MUNGU vyenye manufaa ya mwili, ikiwemo afya, cheo, uzao au mali.

Mfano wa watu waliobarikiwa kwa baraka za mwilini ni Sulemani, alipewa utajiri mkubwa hata baada yake hakukuwa na mtu kama yeye,

Na wengine kwenye Biblia agano la kale ni Abramu na Ayubu hawa walibarikiwa vingi na MUNGU.

Lea naye alibarikiwa kuwa na watoto wengi, Samsoni alibarikiwa nguvu za mwilini n.k

Katika Agano jipya walikuwepo akina Yusufu wa Arimathaya, (Mathayo 27:57), na wanawake si haba, akina Yoana, Suzana na wengine wengi (Luka 8:3).

Na waliobarikiwa kwa vyeo, waliomwamini Bwana YESU walikuwa wengi sana wanaume na wanawake (soma Matendo 17:12-14).

Na kubarikiwa mwilini kunaweza kuwa ishara ya kubarikiwa pia rohoni, lakini sio ishara pekee kwasababu wapo matajiri wasiomwamini YESU na walikuwepo matajiri kabla ya Bwana YESU,

Na watakuwepo matajiri wengi katika ziwa la moto (Soma Luka 16:20-34).

Na tena Bwana Yesu alisema itamfaidia nini mtu apate kila kitu halafu apate hasara ya nafsi yake (Marko 8:34).

Na pia wapo maskini ambao hawajabarikiwa baraka za mwilini lakini wamebarikiwa mambo ya rohoni..

Yakobo 2:5 “Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao?”.

Kwahiyo tukiwa wote ndani ya Kristo, hatupaswi kudharauliana kwa hali zetu, bali tunapaswa tuhudumiane kwa viwango vya baraka tulivyobarikiwa..

kwasababu yule unayemwona ni maskini wa vya mwilini huenda ni tajiri wa vya rohoni sana, ndivyo Neno la Mungu linavyosema..

Ufunuo 2:9 “Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri)…”

Na yule unayemwona hana vya rohoni kama ulivyo navyo wewe basi amebarikiwa vya mwilini, ambavyo kupitia hivyo vinahitajika kwaajili ya injili, ili mambo yote yakae katika uwiano na wote tuheshimiane.

Na pia inawezekana mtu akabarikiwa kwa vyote vya rohoni na mwilini, kwa mapenzi ya MUNGU, lakini haiwezekani mtu aliyemwamini YESU akakosa vyote..

Ikitokea dalili ya kukosa vyote basi kuna kasoro katika imani, hivyo mtu huyo anapaswa aangalie jinsi alivyosikia na anavyoenenda.

Je umempokea YESU?..huo uchungu na hofu na wasiwasi ni ishara ya kupungukiwa baraka za rohoni.

Leo hii mpokee YESU ili uanze kula matunda ya baraka za rohoni.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAOMBI YA YABESI.

Fahamu maana ya Mithali 28:20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;

KILA MTU NA AMCHE BABA YAKE NA MAMA YAKE.

MUNGU HANA MBARAKA MMOJA TU!..MWAMINI.

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

Ipi tofauti ya Andiko na Neno.

Swali: Huwa tunasema.. “tusome maandiko” na wakati mwingine “tusome Neno”..ipi tofauti ya maneno haya mawili?.


Jibu: Tuanze na Neno au Neno la Mungu.

“Neno” ni sauti ya MUNGU yenye ujumbe inayokuja kwa mtu kwa  njia ya maono au ndoto au njozi..

Kwamfano katika biblia utaona lugha iliyotumika kwa manabii wote waliojiliwa na sauti ya Mungu iliyobeba ujumbe ni hiyo ya “Neno la Mungu”

Mwanzo 15:1 “Baada ya mambo hayo NENO LA BWANA likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.

Soma pia  1Wafalme 17:8, Isaya 38:4, Yeremia 1:11, Ezekieli 1:3, Ezekieli 12:21, Hosea 1:1, Yona 1:1, Mika 1:1, Sefania 1:1 n.k 

Hata sisi wakati mwingine tunapotaka kuzungumza na mtu, tunaweza kutumia lugha hiyo kwa kumwambia “nina neno nataka kusema nawe”… au kama kuna mtu amekuambia jambo unaweza kusema “mtu Fulani kaniambia neno”.. kwahiyo ni hivyo hivyo hata katika biblia, Neno la Mungu ni sauti ya MUNGU.

Sasa kama “Neno” tafsiri yake ndio hiyo, vipi kuhusu “Andiko”?

Andiko ni Neno la Mungu lililo katika maandishi… Kwamfano; hilo Neno lililomjia Abramu, kwake yeye ni Neno la Mungu lakini kwetu sisi ni andiko, ndio maana tunalisoma.. Na Nguvu ya andiko na Neno ni ile ile.

Hivyo maneno ya Mungu yote yaliyoandikwa katika Biblia ni “MAANDIKO”.. Hata wewe maneno yako unayoyasema unaweza kuyaandika katika kitabu, na yakawa ni maandiko kwasababu ni maneno yaliyoandikwa.. Hali kadhalika, kila Neno la Mungu kwenye Biblia ni andiko.

Hivyo mtu anayesema “tusome maandiko” na Yule anayesema “tusome Neno la Mungu” ni kitu kimoja.. na nguvu ni ile ile..

Na kila Andiko lenye pumzi ya Mungu linafaa kwa mafundisho, kuonya, kuongoza na kuadibisha..

2Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;

17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema”

Kwa urefu kuhusiana na kazi ya MAANDIKO inayofanya kwa mtu fungua hapa >>MAMBO MANNE(4) YAFANYAYO NENO LA MUNGU.

Je umempokea YESU?, Umebatizwa katika ubatizo sahihi?..una uhakika Bwana YESU akirudi unaenda naye?.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

EPUKA KUJIFANYA HUJUI.

MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?

TUUTAZAME PIA MWISHO WA UJENZI WETU.

ZIFAHAMU KARAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA UTENDAJI KAZI WAKE.

NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?

Simoni Mkirene aliubeba msalaba wa Bwana Yesu au la?

Swali: Katika  Mathayo 27:31-32 tunasoma kuwa Simoni Mkirene alimsaidia Bwana kuubeba msalaba wakati anaelekea mahali pa kusulibishwa, lakini tukirudi katika Yohana 19:17-18 tunasoma kuwa hakusaidiwa na mtu badala yake aliubeba mwenyewe mpaka Golgotha, je mwandishi yupi yupo sahihi?.

Jibu: Turejee mistari hiyo..

Mathayo 27:31 “Hata walipokuwa wakitoka, wakamwona mtu Mkirene, jina lake Simoni; huyu wakamshurutisha auchukue msalaba wake.

33 Na walipofika mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa”

Hapa ni kweli Simoni Mkirene alimsaidia Bwana kuubeba msalaba..

Lakini hebu tusome tena Yohana 19:17-18..

Yohana 19:16 “Basi ndipo alipomtia mikononi mwao ili asulibiwe; nao wakampokea Yesu.

17 Akatoka, hali akijichukulia msalaba wake, mpaka mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, au kwa Kiebrania, Golgotha.

18 Wakamsulibisha huko, na wengine wawili pamoja naye, mmoja huku na mmoja huku, na Yesu katikati”.

Hapa inaonyesha ni kama hakusaidiwa na mtu mpaka alipofika Golgotha..

Je kwa mantiki hiyo biblia inajichanganya?…

Jibu ni La! Biblia ni kitabu kisicho na makosa wala mkanganyiko mahali popote, isipokuwa fahamu zetu na pambanuzi zetu ndizo zinazojichanganya.

Sasa tukirejea katika habari hizo mbili, ni kwamba Mwandishi wa kitabu cha Yohana (ambaye ni Yohana mwenyewe) alijaribu kueleza safari ya Bwana kwenda Golgotha kwa ujumla, bila kuhusisha matukio madogo madogo yaliyokuwa yanatokea njiani.

Kwamfano utaona yeye kasema tu Bwana alijichukulia msalaba wake mpaka Golgotha, pasipo kutaja matukio kama ya kutemewa mate njiani, au wale wanawake kumlilia na Bwana kuwajibu kwamba wajililie nafsi zao na watoto wao (Luka 13:26-28).. Sasa matukio kama haya Yohana hajayataja lakini haimaanishi kuwa amesema hayapo, la! Bali ni kwamba kafupisha tu habari.. hata wewe/mimi tunaweza kuelezea jambo kwa urefu au ufupi kutegemea na mapenzi yetu.

Lakini sasa tukirudi kwa Mathayo yeye kataja safari ya Bwana kwa urefu kidogo, akihusisha matukio madogo madogo yaliyokuwa yanaendelea njiani katika safari yake..na mojawapo ya tukio ndio hilo la Simoni Mkirene aliyekuwa anatokea shamba na akashurutishwa kuubeba msalaba wa Bwana YESU.

Na utaona pia ijapokuwa Mathayo alirekodi tukio la Simoni Mkirene kumsaidia Bwana msalaba, lakini pia hakutaja tukio la wanawake waliomlilia Bwana njiani, ambapo tukio hilo linakuja kutajwa na mwandishi mwingine wa kitabu kingine ambaye ni Luka..

Luka 23:26 “Na walipokuwa wakimwondoa walimkamata mtu mmoja, Simoni Mkirene, aliyekuwa ametoka shamba, wakamtwika msalaba, auchukue nyuma yake Yesu.

27 Mkutano mkubwa wa watu wakamfuata, na wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea.

28 Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu.

29 Kwa maana tazama, siku zitakuja watakaposema, Heri walio tasa, na matumbo yasiyozaa, na maziwa yasiyonyonyesha”.

Umeona kwahiyo habari ya Bwana YESU kujichukulia msalaba mpaka Golgotha kama ilivyoandikwa na Yohana haipingani na ile iliyoandikwa na Luka, Mathayo au Marko.. kinachotofautisha habari hizo ni kwamba moja imeandikwa kwa urefu nyingine kwa ufupi.

Je umempokea YESU, je umeubeba msalaba wako na kumfuata?.. Je unajua ni kwanini Simoni Mkirene aliruhusiwa kubeba msalaba nyuma ya YESU?.. ni ufunuo kuwa tukitaka kumfuata YESU ni lazima tubebe msalaba tumfuate YESU nyuma.

Marko 8:34 “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.

35 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MANENO SABA YA YESU MSALABANI.

YESU MNAZARETI,  ANWANI YA MSALABA.

MSALABA NI ZANA YA UJENZI WA MAISHA YAKO.

Je! Bwana Yesu alisulubiwa juu ya msalaba au juu ya mti uliokuwa wima?

Kwanini Bwana Yesu alisema pale msalabani naona kiu?

Chakula kigumu mfano wake ni upi kama tunavyosoma katika Waebrania 5:12?

SWALI: Biblia inasema maziwa ni kwa watoto wachanga, lakini chakula kigumu ni cha watu wazima. Mfano wa chakula hichi kigumu ni kipi?

Waebrania 5:12 Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu. 13 Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga. 14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya

JIBU:

Kabla ya kufahamu hicho chakula kigumu, ni vema kujua kwanza maziwa ni yapi.

Hivyo ukiendelea kusoma  vifungu vinavyofuata anasema..

Waebrania 6:1 Kwa sababu hiyo, tukiacha kuyanena mafundisho ya kwanza ya Kristo, tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu; tusiweke msingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na uhai, na wa kuwa na imani kwa Mungu, 2 na wa mafundisho ya mabatizo, na kuwekea mikono, na kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele. 3 Na hayo tutafanya Mungu akitujalia.

Sasa hayo mafundisho ya kwanza ya Kristo ndio maziwa. Yaani Mafundisho ya toba, imani kwa Mungu, ubatizo, kuwekewa mikono, kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele ni mafundisho ya watoto wachanga..kiroho hujulikana kama maziwa..

Kimsingi mtoto akiendelea kunywa maziwa tu peke yake daima, kitakachotokea baadaye ni kudumaa kama sio kufa kabisa, hivyo itafika wakati tu atahitaji chakula kingine ili aendelee kuishi. Vivyo hivyo na sisi, vipo vyakula ambavyo tunapaswa tule, kwa jinsi tunavyoendelea kukua kiroho.

Vifuavyo ndio vyakula vigumu vya kiroho vya watu wazima:

1) Upendo kwa maadui

Mathayo 5:44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

Kwanini ni chakula kigumu?. Kwasababu jambo hilo linaenda kinyume na asili ya mwanadamu, linafunua asili ya ndani kabisa ya Kristo, ambayo si rahisi mtu aliyemchanga kiroho, kuielewa, au kulipokea nyakati za mwanzoni, yaani kumwombea  na kumpenda Yule ambaye anaiwinda roho yake au aliyemjeruhi, ..

2) Makusudi ya Mungu katika mateso

Wafilipi  1:29 Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;

Kwanini ni chakula kigumu?. Kwasababu mwamini mchanga, mara nyingi atapenda kuambiwa maneno ya faraja, baraka, na mafanikio, awapo kwa Kristo,  lakini mkristo aliyekomaa, anayaona mapenzi ya Mungu pia hata katika majaribu na kuyashangalia.

1Wathesalonike 3:3 mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo

Soma pia 1Petro 1:6-8, 4:13, Wakolosai 1:24, Luka 6:22-23

3) Upambanuzi wa kiroho

Waebrania 5:14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya

Mkristo aliyekomaa kiroho, anafundishwa na Mungu kutambua na kugawanya vema mambo yote, kujua vilivyo najisi na visivyo najisi, mafundisho ya kweli na yale ya uongo, anafundishwa, busara, ujuzi na hekima hata katika kuhubiri injili kwa makundi yote, bila kuanguka na kunajisika, kwasababu amepewa roho ya upambanuzi ambayo huja kwa kuzoeshwa na Mungu kwa kipindi Fulani cha muda kupitia  Neno lake.

1Wakorintho 9:20 Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria.

21 Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria. 22 Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.

Soma pia, 1Wakorintho 8:6-13, Yohana 2:1-12, Mathayo 11:19.

Kwanini ni chakula kigumu? Kwasababu mtu ambaye ni mchanga kiroho, akijihusisha katika viwango hivyo, hupotea na kunajisika kama sio kupotea kabisa. Ndicho kilichowatokea Adamu na Hawa kuuvamia mtu wa ujuzi wa mema na mabaya nje ya ratiba ya Mungu, matokeo yake wakayavuna mabaya, wala sio mema.

4) Kuikubali Fimbo ya Mungu.

Katika wokovu ipo fimbo ya Mungu; Mzazi yoyote huwa hatoi zawadi tu, sikuzote, hacheki na mwanawe siku zote, lakini pia kuna wakati fimbo hutumika, Vivyo hivyo Mungu ni Baba yetu, huadhibu, pale tunapokosea..

Waebrania 12:11 Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.

Kwanini ni kigumu? Kukubali marekebisho kwa kuadhibiwa kama sehemu ya kutengenezwa na Mungu, si jambo rahisi mtu kulikubali mkristo ambaye hajakomaa. Yeye atakachojua tu, kuwa Mungu ni upendo.

5) Kujikana na kuubeba msalaba.

Luka 9:23 Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.

Kwanini ni chakula kigumu? Aliye mchanga kiroho kukubali kukataa mapenzi , kuingia gharama kuacha vyote na kuyakubali ya Mungu tu, si jambo rahisi kwa mwanafunzi wa ngazi ya chini.

6) Unyenyekevu na kujitoa kwa wengine.

Wafilipi 2:3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.

4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.

5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;

6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba

Kwanini ni chakula kigumu?.

Mkristo mchanga kiroho, si rahisi kuangalia mambo ya wengine, mfano wa Kristo, si rahisi kujinyenyekeza na kukubali kutembea kama mtumwa ili kuwatumikia wengine.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Kanisa kama sehemu ya maisha ya mwamini mpya.

Kama mwamini mpya ni lazima ufahamu kuwa kanisa sio jengo, bali kanisa ni watu wa Mungu waliookolewa na kuwekwa pamoja ili kumwabudu Mungu, na kuhudumiana.

Zifuatazo ni namna mbalimbali ambazo kanisa hutambulika kimaandiko.

i) Kanisa,  hujulikana kama mwili wa Kristo.

1 Wakorintho 12:27

[27]Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.

Kama vile viungo vinavyoshirikiana, vivyo hivyo na wewe huna budi kuwa na ushirika wote wa kanisa, sio kuwa mtembeleaji. Kila mwamini ni kiungo Katika mwili huo.

ii) Hujulikana pia Kama Bibi-arusi wa Kristo.

Waefeso 5:25-27

25 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; 26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;

Kristo anataka ujue kuwa unapookoka, unakuwa katika kifungo chake, mfano tu wa mwanamke aliye katika ndoa. Bwana mmoja, mwili mmoja, huku akimtii yeye katika yote. Vivyo hivyo na wewe, tangu huu wakati uliokoka ni wajibu wako, kumtumikia Kristo tu, na kumtii katika yote atakayokuagiza ndani ya kanisa.

iii) Kanisa hujulikana pia kama familia ya Mungu. (Waefeso 2:19)

 Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu”.

Kama mwanafamilia unakuwa na haki ya kupokea na kurithi ahadi zote ambazo Mungu alizoahidi kwa watu wake, kwasababu wewe  tayari umeshafanywa kuwa mwana wake.

iv) Lakini pia linajulikana  kama hekalu la Mungu

1Wakorintho 3:16 -17

16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? 17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi.

Kwamba ukishaokoka, wewe na waamini wenzako mnaitwa nyumba ya Mungu, hivyo ni wajibu wako kuifanya nyumba hiyo safi sikuzote kwa  kuishi maisha ya utakatifu, kwasababu Mungu haishi mahali pachafu, bali pasafi. Wewe ni nyumba ya Mungu, iheshimu nyumba yake.

Kwanini kanisa ni muhimu.

  1. Ukuaji Wa kiroho.

Kwa kupitia mafundisho, mahubiri, madarasa ya uanafunzi, uyapatayo ndani ya kanisa, pamoja na madhihirisho mbalimbali ya  karama za Mungu, utajikuta unajengeka kwa haraka sana na Matokeo yake utajengwa na kukua kiroho, tofauti Na kama ungekuwa peke yako. (Waefeso 4: 11-13)

  1. Kuabudu

Mahali Bora pa kumwabudu, na kumsifu Mungu kwa uhuru na nguvu, ni Pale uwapo katika mkusanyiko. Daudi alisema;

Zaburi 95:6

[6]Njoni, tuabudu, tusujudu, Tupige magoti mbele za BWANA aliyetuumba.

  1. Maombi na kusaidiana.

Kanisa lina misingi ya maombi na Maombezi. Bwana Yesu alisema;

Yakobo 5:16

[16]Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.

Huwezi kusaidika pale unapoishiwa na nguvu, kama huna jamii ya watu nyuma yako kukushika mkono  kimaombi au kihali usimame. Kanisa la kwanza, lilipokusanyika, lilisaidiana katika mahitaji, lakini pia lilitatua migogoro, mbalimbali iliyozuka katikati yao. Hivyo mtu anayekosa kanisa, ukweli ni kwamba anaishi kama yatima wa kiroho.

  1. Kuandaliwa Kwa huduma.

Kanisa Ni kama karakana ya Mungu inayowaandaa watu, kuwa watendakazi. Ni mahali ambapo utatambua Karama yako. Kisha kuitumia hiyo kuwahudumia wengine na kuipeleka mbele kazi ya Mungu.

Matendo 2:41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali

Je mahudhurio  ya kikanisa yanapaswa yawe mara ngapi?

Mengi kwa jinsi uwezavyo..

Biblia inatuambia tuonyana kila inapoitwa leo (yaani kila siku).

Waebrania 3:13 Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa udanganyifu wa dhambi. 14 Kwa maana tumekuwa washirika wa Kristo, kama tukishikamana na mwanzo wa uthabiti wetu kwa nguvu mpaka mwisho;

Pamoja na hilo, watakatifu wa zamani, ukiachilia mbali makusanyiko ya katikati ya wiki, ilikuwa ni lazima siku ya kwanza ya juma wote wakusanyike. (1Wakorintho 16:2). Yaani kila jumapili ilikuwa ni siku ya Bwana.

Ni nini kinatokea pale unapojitenga na kanisa?

  1. Unakuwa dhaifu kiroho, Na mwepesi wa kushindwa na majaribu.
  2. Unakosa Washauri na maongozo ya kiroho.
  3. Karama yako haiwezi kukua na kudhihirika, kwasababu karama hasaa ziliandaliwa kwa ajili ya kanisa.

Kanisa ni kama Shule kwa mwanafunzi. Tunajua Shule kama Shule sio elimu. Bali shule hutoa elimu. Kwasababu ndani yake wapo waalimu, zipo nidhamu, wapo wanafunzi wenzako , yapo majaribio, Vipo vitabu n.k. ambavyo vinakusaidia Kufaulu vizuri katika masomo yako.

Halikadhalika wewe kama mwamini mpya, ni lazima uwe na kanisa. Mwamvuli wako, ujengwe ukue, uandaliwe. Kanisa ni chombo maalumu alichokiunda Mungu, siku ile ya pentekoste ili watu wake wamwone yeye.

Zingatia sio kila mkusanyiko unaosema ni wa-kikisto ni kweli ni kanisa la Mungu. Kwasababu manabii, na wapinga-Kristo wapo sasa duniani.

Hii ni aina ya mikusanyiko ambayo unapaswa ujiepushe nayo;

> Epuka mikusanyiko isiyo mfanya YESU KRISTO kama ndio msingi, na wokovu wa mahali hapo.

> Epuka mikusanyiko isiyokurejeza katika maisha haki na utakatifu.

> Epuka mikusanyiko isiyokukumbusha juu ya hatma ya maisha yajayo, yaani kuzimu na mbinguni

> Epuka mikusanyiko isiyoamini katika utendaji kazi wa karama za Roho Mtakatifu.

Omba, kwanza, kisha fanya maamuzi.

Ikiwa bado hujawa na uhakika wa pa kukusanyika. Basi wasiliana na sisi tukusaidie mahali sahihi pa kukusanyika..

Vifungu hivi visitoke akilini mwako:

Waebrania 10:25

[25]wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.

Mhubiri 4:9-10

[9]Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja;  Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.

[10]Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!

Zaburi 122:1

[1]Nalifurahi waliponiambia,  Na twende nyumbani kwa BWANA.

Haya ni mafundisho ya ziada yatakayokupa mwangaza  juu ya kanisa na taratibu zake.

Kwanini tunakwenda kanisani?

WALA TUSIACHE KUKUSANYIKA PAMOJA

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU

EPUKA KUCHELEWA IBADA.

KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.

KAMA MKRISTO NI LAZIMA UWE NA DESTURI HII.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Maombi kama sehemu ya maisha ya mwamini mpya.

Maisha Mapya ya wokovu yanasukumwa na maombi. Kama Neno ni chakula, basi maombi ni maji. Vilevile huwezi tenganisha maisha ya wokovu na uombaji.

Maombi ni nini?

Ni tendo la kuongea na Mungu, lakini pia kumsikia. Maombi sio maneno matupu tu, au utaratibu wa kidini, bali ni mahusiano halisi kati ya sisi na Mungu.

Yeremia 33:3

[3]Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.

Je! tunapaswa tuombe wakati gani?

Maandiko hayatoi ukomo wa maombi. Zaidi sana yanasisitiza tuombe kila wakati na bila kukoma.

1Wathesalonike 5:17 ombeni bila kukoma;

Waefeso 6:18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;

Hivyo Maombi ni tendo endelevu la wakati wote.

Faida za kuomba kwa mwamini.

i) Tunashinda  majaribu:

Mathayo 26:41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.

ii) Tunajazwa Roho

Luka 3:21 Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka.

iii) Tunatatua Matatizo yote:

Mathayo 17:20 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.

21 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]

iv) Tunapewa haja zetu:

Wafilipi 4:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.

Aina za maombi.

Zipo aina mbalimbali za maombi, ili kufahamu kwa kina bofya hapa >>   KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Je! tunapaswa tuombaje?

Ramani kuu ya maombi tulishafundishwa na Bwana Yesu Kristo. Ambayo ndio ile Sala, ijulikanayo kama “Sala ya Bwana”. Hivyo kufahamu namna ya kuiomba fungua hapa >>>>  Namna bora ya kuiomba sala ya Bwana

Miongozo mingine itakayokusaidia kutanua upeo wako wa uombaji kwa lengo la ukuaji wa kiroho  Bofya hapa >>> MWONGOZO WA MAOMBI YA KUJIKUZA KIROHO.

Haya ni mafundisho, mengine yatakayokusaidia kujua kwa undani kuhusu maombi;

IFAHAMU NGUVU YA MAOMBI.

Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?

MWONGOZO WA MAOMBI YA ASUBUHI.

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

JINSI YA KUVURUGA MIPANGO YA MUNGU.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Namna sahihi ya kusoma Neno (biblia).

Kama tulivyotangulia kuona kuwa kusoma Neno kunazidisha Ujazo wa Roho Mtakatifu Ndani Yetu..lakini pia ndio Chakula kikuu cha Roho zetu. Bila NENO ni sawa na mwili bila chakula, hauwezi kuishi.

Mathayo 4:4

[4]Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.

> Kusoma biblia ndiko kunakoweza kukukuza kiroho, (1Petro 2:2,),

> Pia ndipo unapoweza kufanywa upya ufahamu wako (Warumi 12:12).

> Lakini pia Ndani ya biblia kuna unabii wa maisha yako, kuna faraja, Kuna maonyo, kuna mashauri na miongozo (Zaburi 119:105).

Hivyo hakuna Namna mtu atayatenganisha maisha ya wokovu na usomaji Neno.

Sasa unapotaka kuanza kusoma unapaswa ufahamu Kuna usomaji wa aina mbili kuu.

  1. Kusoma kwa lengo la kuijua biblia nzima.
  2. Kusoma kwa muktadha.

Aina hizi mbili Ni muhimu kuendana nazo. Kuijua biblia yote ni jambo la msingi, kwasababu ili Kuelewa muktadha wa biblia ni lazima kwanza kuzielewa  habari mbalimbali zilizo katika biblia.

Hivyo ni lazima Uwe na nidhamu ya kusoma kila siku. Na kama ukifanya Hivyo kwa kusoma sura 6-7 kwa siku, basi ndani ya miezi sita (6), utakuwa umeimaliza biblia yote. Ukimaliza kuisoma rudia tena na tena.

Lakini kusoma kwa muktadha ni kusoma kwa mnyumbuliko, kunahitaji pia mkufunzi Wa kukusaidia kuelewa. Pamoja na utafakariji sana wa Neno, na kwenda taratibu taratibu ili Roho Mtakatifu Akusaidie kuelewa.

Mambo Ya kufanya uanzapo kusoma biblia yako.

1) Hakikisha unakuwa na biblia yako, wewe kama mwanafunzi mpya wa Kristo, yenye agano la kale na lile jipya. Biblia yenye vitabu 66

2) Tenga Muda wa utulivu wa kujisomea kila siku. Ni vema ukawa na mahali pako pa utulivu, ili kuweza kusoma kwa umakini zaidi.

3) Kuwa na daftari Na kalamu, ili Kuandika kila unachojifunza, kwa kumbukumbu zako za baadaye.

4) Omba kwanza kila unapoanza kujisomea biblia ili Mungu Akupe uelewa.

5) Mwisho Hakikisha unakitendea kazi kila unachokisoma.

Kujisomea na wengine pia ni jambo jema la ziada. Uwezavyo kupata rafiki ambaye anapenda biblia, basi kutana naye mara kwa mara, utafakari Naye maandiko. Epuka kampani za watu wasio- na kiu ya Mungu  wakati wako huu, tumia muda wako mwingi katika kumtafakari Mungu, ili ukue kiroho kwa haraka, mtoto mchanga huwa ananyonya hata mara saba kwa siku. Kwasababu mwili wake upo katika kukua unahitaji maziwa wakati wote. Vivyo hivyo na wewe hakikisha una muda wa kutosha wa kusoma biblia kila siku.

Vifungu hivi unaweza ukavikariri viwe Kama nanga ya maisha yako ya usomaji Neno.

Zaburi 119:11

[11]Moyoni mwangu nimeliweka neno lako,  Nisije nikakutenda dhambi.

Waebrania 4:12

[12]Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.

Yoshua 1:8

[8]Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.

Bwana akubariki.

Haya ni mafundisho yanayoweza kukusaidia kupata mwongozo wa usomaji biblia mzuri.

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

BIBLIA TAKATIFU.

Mtiririko wa vitabu vya biblia kwanini upo vile?

CHAMBUZI ZA VITABU VYA AGANO JIPYA.

NIFANYE NINI ILI NISILALE NINAPOSOMA BIBLIA.

Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Ahadi Ya Roho Mtakatifu.


Ahadi ya Roho Mtakatifu ni ya kila mwamini. (Matendo 2:39). Ni msaidizi ambaye Mungu alitupa ili kutuwezesha kuishi maisha ya wokovu  kwa viwango vya ki-Mungu hapa duniani.

Hivyo siku ile ulipomkubali Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yako. Tayari ulipokea Roho Mtakatifu siku hiyo hiyo.

Isipokuwa Huwezi ukahisi chochote ndani, bali kwa jinsi unavyoendelea kutii kwa kumfuata Bwana utaziona tu kazi zake ndani yako.

Na hizi ndio kazi zake kuu azifanyazo  Roho Mtakatifu anapokaa ndani ya mtu;

1)  Humwongoza mtu katika njia sahihi, kuyaelewa maandiko. (Yohana 16:13)

Yohana 16:13

[13]Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

2) Humpasha habari juu ya mambo yaliyopita na yajayo..(Yohana 16:13b)

Yohana 14:26

[26]Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.

3) Humsaidia kuomba.

Warumi 8:26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.

4) Kumsaidia kuyashinda mambo ya mwilini

Wagalatia 5:16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana
hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.

5) Humshuhudia  mwamini  kwa habari Ya dhambi.

Hivyo humfanya aendelee kuishi maisha ya utakatifu (Yohana 16:8)

Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu

6) Humwekea vipawa vyake ndani yake, ili aweze kulihudumia kanisa. (1Wakorintho 12:7)

1Wakorintho 12:7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.
8 Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo
Roho yeye yule;
9 mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule
mmoja;
10 na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho;
mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha;
11 lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake
kama apendavyo yeye

7) Humpa Nguvu ya kumshuhudia Kristo kwa ujasiri wote katika ulimwengu.

Matendo 1:8

 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi
wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.

Hivyo faida zote hizi hudhihirika ndani ya mtu kwa wingi , hutegemea jinsi mtu huyo anavyompa Roho Mtakatifu nafasi ndani yake. Ndio maana ni vema wewe kama mwamini mpya ujue mambo haya ili usije ukajikuta unamzimisha Roho Mtakatifu ndani yako. Ukawa unaisha maisha ya kama mtu ambaye hajaokoka.

Hizi ndio njia ambazo Unapaswa uzifanye  ili ujawe Roho, yaani utendaji Kazi wa Roho Mtakatifu uwe dhahiri ndani yako.

1) Jitenge na dhambi.

Moja ya agizo la Bwana Yesu kwetu sisi, ni kwamba “tujikane nafsi”. Kujikana maana yake ni kuyakataa matakwa yetu wenyewe ya mwilini na kukubali yale ya Mungu tu. Ulikuwa mlevi unakuwa tayari kukaa mbali na ulevi, ulikuwa ni kahaba unauaga ukahaba wako. n.k.

2) Wekewa mikono na viongozi wako wa imani:

Kuwekewa mikono kunanyanyua mafuta Ya Roho Mtakatifu ndani ya mtu kwa namna nyingine. Na matokeo yake ni kuwa unaambukizwa pia neema.. Katika maandiko tunaona wapo watu kadha wa kadha waliojazwa Roho kwa namna hii. (Matendo 8:17, Matendo 19:6 , 2 Timotheo 1:6 )

3) Kuwa mwombaji wa Kila siku. 

Kiwango cha chini ambacho Bwana alituagiza ni SAA moja. Zaidi Pia katika maombi yako mwambie Bwana nijalie kuomba kwa Roho ( kwa  kunena kwa lugha)  ikiwa bado kipawa hichi hakijakushukia, Ni muhimu pia.

Zingatia: Katika uombaji wako, jifunze kutoa sauti, pia jiachie mbele zake. Huwezi kunena kwa lugha moyoni.. ni lazima kinywa kihusike hivyo Jifunze kuomba huku kinywa chako kikitoa maneno kabisa. Hiyo ni nidhamu nzuri katika hatua za ujazwaji Roho.

4) Soma Neno la Mungu kila siku. 

Tunajazwa Roho Kwa kuitambua sauti yake inatuagiza nini. Na sauti yake ni biblia. mahali Pekee penye uwepo wote wa Mungu ni kwenye Neno lake.

Hivyo zingatia sana hilo. Mkristo ambaye hasomi NENO, kamwe hatakaa aweze kumsikia wala kumwelewa Roho Mtakatifu.

Ukizingatia hayo basi, utaona uzuri wa Roho Mtakatifu ndani yako.

Mafundisho ya ziada kuhusu Roho Mtakatifu

YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO.

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi?

NAMNA YA KUNENA KWA LUGHA MPYA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Nipo Tayari Kubatizwa.

Ubatizo ni agizo la Bwana katika hatua za awali za wokovu. Wapo watu wanaosema Ubatizo hauna maana, ndugu usijaribu kufanya hivyo, unaweza usiwe na maana kwako, lakini unaomaana kwa yule aliyekupa hayo maagizo.

Kwanini tunabatizwa?

  • Ni agizo la Bwana.

Mathayo 28:19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

  • Tunafuata kielelezo chake yeye mwenyewe:

Ikiwa yeye hakuwa na dhambi wala kasoro yoyote alibatizwa, kwanini sisi tusibatizwe?

Mathayo 3:13 Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe.

  • Ni ishara ya nje ya kazi iliyotendeka ndani

Ubatizo ni ishara ya nje ya kile ulichokiamini, kuwa umekufa kwa habari ya dhambi, kisha ukafufuka katika upya na  Kristo.

Warumi 6:3-4

[3]Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?

[4]Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.

Ni nani anayepaswa kubatizwa.

Ni yule aliyeamini, yaani kuupokea ujumbe wa injili kwa geuko(toba).

Matendo 2:41

Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa;…

Ni wakati gani anapaswa abatizwe?

Haraka sana, tangu siku ile alipoamini. Ubatizo sio mpaka  umekomaa kiroho au kimafundisho, hapana, bali ulipopokea tu wokovu, wakati huo huo unastahili ubatizo.

Matendo ya Mitume 2:38

[38]Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Ubatizo sahihi ni upi?

Ni ule wa kuzamishwa katika maji tele (Yohana 3:23, Matendo 8:36-38 ),

Na kwa jina la Yesu Kristo.(Ambalo ndio Jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu) [Mathayo 28:19, matendo 8:16, 10:48, 19:5]

Ikiwa Sikubatizwa kwa kuzamishwa katika maji mengi, au nilibatizwa nikiwa mtoto mchanga yanipasa nibatizwe tena?

Ndio, ili kufuata mkondo sahihi wa kimaandiko, huna budi kubatizwa tena.

Msaada wa ubatizo:

Kwakuwa umeokoka, na bado hujapata huduma hiyo basi waweza tafuta Kanisa la kiroho, ambalo linaamini katika ubatizo wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo ili utimize agizo hilo.

Lakini ikiwa utapenda kusaidiwa na sisi. Basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi kwa msaada huo:

+255693036618 / +255789001312

Bwana akubariki.

Mistari ya kusimamia kila ukumbukapo tendo la ubatizo.

Wakolosai 2:12 Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu.

Wagalatia 3:27 Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo.

Bwana akubariki.

Kwa mafundisho zaidi kuhusu ubatizo

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Tofauti kati ya dhehebu na dini ni ipi?

Dini ni mfumo au utaratibu wa kumwabudu Mungu. Kwamfano ukienda mahali ukaona watu wamekusanyika na kukubaliana kuabudu kitu Fulani, ni lazima utaona tu utaratibu, au mwongozo au miiko wamejiwekea ya kuifuata na kuishika, ili ibada yao iwe na matokeo. Sasa huo utaratibu ndio unaitwa dini.

Hata imani yetu ndani ya Kristo, inasukumwa na dini. Hatumwabudu tu Mungu kama tunavyotaka bali Mungu aliweka utaratibu na njia ya kuifuata.

Lakini Dhehebu, ni “aina ya dini”. Ambayo huzalika ndani ya imani ile ile moja. Kwamfano utaona wakristo imani yao ni moja kwa Kristo Yesu, na msingi wa kuegemea ni biblia ile ile moja takatifu. Lakini ndani yao kuna michipuko mingi tofauti tofauti ya kitaratibu na ufanyaji ibada, kulingana na walivyoielewa biblia. Ndio hapo utaona wengine wanajiita wapentekesto, wengine wakatoliki, wengine wasabato, n.k. Sasa hii yote ni michupuko, ambayo mengine inakaribiana sana na uhalisia, na mengine inakwenda mbali na kweli ya Mungu.

Lakini cha kumshukuru Mungu ni kuwa biblia imeshaeleza asili ya dini ya kweli inapaswa iweje….

Yakobo 1:26 Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai. 27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.

Kwamba ni lazima itakuwa ya kimatendo zaidi. Yaani utafunzwa utakatifu, na kujitoa.

Swali lingine je! Dhehebu linampeleka mtu mbinguni?

Hapana, kwasababu Yesu hakuja kuleta dhehebu jipya duniani. Kwani alipokuja alikuta tayari yapo madhehebu mengi yamesha-zaliwa kama tu ilivyo sasa, mfano Mafarisayo, na masadukayo. Lakini hakuwahi kutetea lolote kati yao. Bali alisisitiza watu kumwamini yeye, kama ndio njia ya kweli na uzima mtu asipofanya hivyo hawezi  kumwona Baba (Yohana 14:6).

Ikiwa na maana haijalishi una dhehebu zuri kiasi gani. Ukikosa shabaha ya Ukristo, bado mbinguni huendi. Waamini wengi wanashikilia zaidi dini, jambo ambalo ni jema, lakini dini ni kisaidizi cha imani. Sio imani yenyewe, ni sawa na shule na elimu, tunaweza kusema shule ni kisaidizi cha elimu, lakini sio elimu yenyewe.

Hivyo ni busara kuchukua tahadhari ya dhehebu unalotaka kumwabudia Mungu, kwasababu ukweli ni kwamba madhehebu mengine hayana ubora wa kumfanya mtu awe mkristo kamili.

Kwamfano dhehebu lisilo, patana na imani katika Kristo Yesu tu, au lisilofundisha utakatifu, au lisilo amini juu ya vipawa vya Roho Mtakatifu, au linalochanganya ibada ya Mungu na sanamu, bali linasisitiza mambo ya mwilini tu, hilo halikujengi, bali linakupoteza.

Lifananishe  kwanza na biblia yako, huku ukimwomba Roho Mtakatifu akusaidie, kisha ndio ufanye maamuzi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE NI YESU YUPI UNAYE? WA KIDINI AU WA UFUNUO!

Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?