Title October 2018

TUSIPOUTHAMINI WOKOVU TUTAPATAJE KUPONA?

Mathayo 5: 13 “NINYI NI CHUMVI YA DUNIA; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.

14 Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.

15 Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.

16 Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.”

Bwana Yesu aliwafananisha watakatifu waliopo duniani na CHUMVI,. Tunafahamu sifa ya chumvi, ni kiungo kisicholika chenyewe kama chenyewe, bali ni lazima kwanza kichanganywe na kitu kingine kama chakula ili kilete ladha, kadhalika chumvi huwa haitengenezwi na mchanganyiko mwingine wowote isipokuwa ni chumvi kama chumvi tu, ikichanganya na vingine inakuwa tena si chumvi bali ni kitu kingine.

Vivyo hivyo mkristo yeyote aliyekolewa, kwa kuzaliwa mara ya pili, mbele za Mungu ni kama chumvi katika ulimwengu. Anapoamua kuacha dhambi na maisha mabovu aliyokuwa anaishi huko nyuma, mbinguni yeye anaonekana kama chumvi safi katikati ya ulimwengu. Lakini chumvi tunafahamu inaharibika pale tu inapojichanganya na kitu kingine au inapomwagika. Kwa mfano chumvi ikiingia mchanga ni wazi kuwa hakuna mtu atakayeweza kutenganisha punje moja moja kutoka katika huo mchanga, badala yake itakuwa ni ya kutupwa tu, hata kama ilinunuliwa kwa thamani kubwa kiasi gani, haifai tena.

Na ndivyo ilivyo kwetu, tunapokuwa wakristo tunapaswa tuwe makini sana, tunapaswa tujilinde sana, tunapokaa katikati ya ulimwengu, kwasababu biblia inasema tunakuwa kama Nuru katikati yao, Kwa mienendo yetu na matendo yetu. Lakini sasa matendo yetu yakiwa mabovu ni sawasawa na chumvi iliyoharibika. Tunapotazamwa na dunia tuwe na mienendo inayostahili na bora kuliko yao halafu tunaonekana ni walevi, watukanaji, waasherati, wasengenyaji, watoaji wa maneno ya mizaha, wagomvi, fitna, wivu, na chuki, tunakosa nidhamu katika jamii, je! Tutatiwa nini hata tukolee?. Kilichobaki ni kutupwa tu nje! Na kukanyagwa na watu. Hatua hiyo ni sawa na ile hatua ya kutapikwa, kwasababu unakuwa vuguvugu na si baridi wala si moto,..Ni chumvi iliyoingia mchanga.

Biblia imesema katika 1Wakorintho 10: 12 “Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”. Unaona hapo? Ukristo ni wakutunzwa sana kuliko kitu kingine chochote, kwasababu ukristo wako ukishaharibika tu mara moja unakuwa haufai tena kwasababu maandiko ndivyo yanavyosema.

Wafilipi 2:11”… .UTIMIZENI WOKOVU WENU WENYEWE KWA KUOGOPA NA KUTETEMEKA

13 Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu,”

Tunapaswa tujilinde kila siku, kila mahali, kama tumekusudia kweli kwa kumaanisha kuacha mambo ya ulimwengu na kufanyika kuwa chumvi safi, tudumu katika hali hiyo hiyo, tusiitie chumvi uchafu, kwasababu chumvi si kama maharage ambayo yakianguka yanaweza yakaokoteka na kuosheka….Kwasababu biblia inasema sisi watakatifu IMANI tumekabidhiwa MARA MOJA TU (Yuda 1:3). Ikiwa na maana kuwa ukristo si wa kwenda na kurudi, kwenda na kurudi tu kama tunavyotaka..

2Petro 2: 20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, HALI YAO YA MWISHO IMEKUWA MBAYA KULIKO ILE YA KWANZA.

21 Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, KULIKO KUIJUA, KISHA KUIACHA ILE AMRI TAKATIFU WALIYOPEWA.

22 Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, MBWA AMEYARUDIA MATAPIKO YAKE MWENYEWE, NA NGURUWE ALIYEOSHWA AMERUDI KUGAA-GAA MATOPENI ”.

Hivyo kama wewe ni mkristo ambaye ulishaokolewa na hujasimama imara huu ni wakati wa kufanya hivyo maadamu mlango wa neema bado haujafungwa, unayo nafasi ya kuwa moto,unayo sasa nafasi ya kufanyika CHUMVI, Unachopaswa kufanya ni kuanza maisha yako ya ukristo upya na kuamua kujikana nafsi yako kila siku kwa Bwana, na kukaa mbali na vishawishi vyote vya dunia ambavyo vitakufanya ukristo wako uwe vuguvugu, marafiki, disco, anasa, uvaaji mbaya, fashion,ulevi, usengenyaji, pornography, kujihusisha na ku-chat na kupost vitu visivyofaa katika mitandao, n.k. vifanye kuwa ni adui yako, na Bwana mwenyewe atakuongezea nguvu ya kuvishinda.

Kama wewe hujazaliwa mara ya pili ni afadhali ukafanya hivyo sasa. Na kuzaliwa mara ya pili maana yake ni kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi zako, kisha kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi, katika JINA LA YESU KRISTO. Na Bwana atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu. Kumbuka Bwana Yesu alisema mtu asipozaliwa mara ya pili [yaani kwa maji na kwa Roho] hawezi kuuona ufalme wa mbinguni. Ni maombi yangu ufanye hivyo sasa.

Waebrania 2: 3 “SISI JE! TUTAPATAJE KUPONA, TUSIPOJALI WOKOVU MKUU NAMNA HII? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia;”

Bwana akubariki sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

Print this post

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

Wengi wetu tunafahamu kitu gani kilitokea kabla ya Edeni, kwamba ibilisi/ shetani, alimwasi Mungu na kuondolewa katika nafasi yake aliyokuwapo, biblia inasema alikuwa ni Kerubi aliyetiwa mafuta, na alinyanyuliwa juu ya Mlima wa Mungu, yaani juu ya malaika wengine wote, alikuwa ni mzuri na mkamilifu katika njia zake zote na alikuwa na hekima nyingi sana, mpaka siku ile uovu ulipoonekana ndani yake, Sasa kulingana na wingi wa sifa alizokuwa nazo, na wingi wa heshima uliomzunguka tunafahamu moyo wake ulinyanyuka akatamani kuwa kama Mungu.(ukisoma Ezekieli 28:11-18, Isaya 14:12 utaona jambo hilo.)

Sasa ni nani aliyemdanganya shetani?

Jibu ni kwamba hakuna aliyemdanganya shetani, bali alijidanganya yeye mwenyewe, pale alipoona amenyanyuliwa na Mungu, hivyo alitamani awe Zaidi ya pale alipo, HILO TU! alionywa lakini alikataa, mpaka alipotolewa katika ile nafasi na kufukuzwa katika yale makao ya nuru ya utukufu aliyokuwepo, na baada ya kufukuzwa Bwana Mungu hakumuua mpaka majira yatakapofika, wala hakumnyanganya HEKIMA, na UZURI aliokuwa nao, wala hakumnyanganya NGUVU alizokuwa nazo, alichomuondolea ni ile nafasi aliyokuwa nayo mbinguni ya utukufu wa Mungu, hivyo baada ya hapo kwa kujua muda wake ni mfupi akaanza kuujenga ufalme wake na wale malaika walioasi pamoja naye, kwa hekima aliyokuwa nayo na kwa nguvu alizokuwa nazo,

Ni sawa tu na mkuu wa majeshi aliyeasi na kuondolewa katika nafasi yake ya ukuu wa majeshi, na kuamua kuondoka na wafuasi wake wengi kwenda msituni, kuanzisha kikundi cha uasi, sasa huyo mwanajeshi aliyeasi atakua amepoteza nafasi yake katika nchi lakini sio uzoefu wake, au ujuzi wake, au akili zake, ndivyo ilivyo kwa shetani baada ya kuasi hakuondolewa ujuzi wake, wala uwezo wake wa kufanya mambo,wala akili yake. Wengi wanafikiri kuwa siku shetani alipolaaniwa alibadilika na kuwa kitu cha ajabu sana na cha kutisha chenye mapembe na sura mbaya kisichoweza kufikiri, hapana, bali aliondolewa utukufu ule wa Mungu ndani yake. Na tunafahamu kitu chochote kikiondolewa utukufu wa Mungu, basi kinakuwa ni kama mfu tu katika roho.

Sasa baada ya Bwana Mungu kuanza uumbaji wa mwanadamu wa kwanza (Adamu), tayari shetani alikuwa ameshatengeneza ufalme wake ulioasi, unaojulikana kama ufalme wa giza. Na huu Ufalme wake una kazi moja tu, “kuenda kinyume na kila kitu ufalme wa Mungu unachokifanya”. Ukiamini kuwa upo wakati utasimama wenyewe na kutawala kila kitu.

Kwahiyo baada ya Adamu kuumbwa, Shetani kwa hekima yake alijua Mungu kamweka mwanadamu katika nafasi ya juu sana, kama alivyokuwa yeye, hivyo njia pekee aliyojua anaweza kuuimarisha ufalme wake ni kumwangusha mwanadamu kwa kumletea mawazo kama aliyokuwa nayo yeye hapo kwanza, “mawazo ya kujiinua kutaka kuwa kama Mungu”. Alijua kabisa njia pekee Bwana Mungu anayochukizwa nayo kwake ni KUJIINUA, Hivyo akamletea sasa mawazo kama yale yale kupitia nyoka, Tunasoma.

Mwanzo 3: 1 “Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?

2 Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula;

3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa.

4 Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa,

5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, NANYI MTAKUWA KAMA MUNGU, mkijua mema na mabaya”.

Unaweza ukaona hapo, shetani kitu alichoona kinaweza kikawavutia sana ili waasi ni hili neno WATAKUWA KAMA MUNGU. Jambo ambalo hata yeye mwenyewe hakuweza kulifikia kuwa kama Mungu, badala yake lilimshusha chini kutoka katika nafasi yake ya ukuu mpaka kuwa pepo. Na tunaona Adamu na Hawa nao baada ya kula tunda, badala ya kuwa kama Mungu kama walivyoahidiwa na shetani, wakapoteza ile nafasi yao kama shetani alivyopoteza ya kwake, wakafukuzwa nao vile vile kutoka katika Edeni bustani ya Mungu aliyokuwa amewaumbia wao. Unaona? Shetani aliwafundisha wasiridhike na nafasi waliyokuwa nayo pale Edeni, aliwafundisha wanaweza kuwa Zaidi ya pale.

Sasa shetani na yeye hajabadilika; mbinu aliyoitumia kuwaangusha malaika wenzake walioasi naye, na aliyotumia kuwaangusha wanadamu wa kwanza Adamu na Hawa, anaitumia hata leo kuwaangusha wanadamu, kuhakikisha anawatoa katika nafasi zao, na hatumii njia nyingine Zaidi ya kuwaletea watu “roho ya kujiinua (KIBURI)” Anajua kiburi ndicho kilichomshusha yeye chini, na ndio hicho hicho anawapachikia watu ili washushwe chini kutoka katika nafasi zao. Na kama ilivyo kawaida yake, shetani analilenga kanisa kwanza Zaidi ya watu wa ulimwengu huu, hivyo anafanya juu chini kuipachika hii roho ndani ya kanisa,

Inatokea wananyanyuka watu wachache [ambao shetani anawatumia pasipo wao kujua ] ndani ya kanisa wanaoanza kumsifia labda mchungaji, au mwalimu, au askofu, utasikia wataanza kumwambia “unajua wewe askofu huwa ukizungumza tu, mimi huwa nakuona unakuwa kama malaika”..unajua wewe mchungaji ni wakipekee sana, yaani una karama zote, yaani tumezunguka kote hakuna mfano wako, yaani wewe ni shujaa na wakipekee sana, wewe ni kiboko yao,n.k. sasa kwa sifa zote hizo ni rahisi yule mtu wa Mungu kujiona yeye kweli ni bora kuliko wengine, pasipo kujua kuwa ni roho ya shetani inataka kumpeleka mahali fulani, ananyanyuka moyo na yeye kuanza kuamini kwamba ni bora kuliko wengine, na mwisho wa siku anajikuta ameshajiinua kupita kawaida.

Na mbinu nyingine shetani anayopenda kuitumia pasipo watu wengi kujua, ni mapepo, anapenda kutumia mapepo kuwapandikizia watu wengi kiburi, kwamfano inatokea mtu kaenda kumuombea mtu mwingine na yule mtu akalipuka mapepo, na yale mapepo, yakaanza kumsifia, “wewe ni mtu hatari sana, tunakuogopa, yaaani unatuunguza na unatutesa sana tangu siku nyingi, yataendelea kumwambia sisi tumetoka jupita tumewajaribu, wachungaji wengi tumewashinda ni wewe peke yako ndio unayetutesa”..na yataendelea kumwambia hadithi nyingi za uongo ambazo zote maudhui yake ni kumnyanyua yule mtumishi, na yule mtumishi pasipo kujua kwamba zile roho ni kongwe tangu Edeni na zinajua namna ya kumwangusha mwanadamu, atadhani kuwa zinamwambia ukweli, atadhani kuwa yeye kweli ndiye wa kipekee kuliko watu wote duniani, pasipo kujua kwamba “shetani ni mwongo tangu zamani na yeye ni baba wa uongo” maandiko yanasema hivyo. Sasa yule mtumishi atatoka pale na kuamini kuwa hakuna kama yeye na pasipo kujua kuwa amepandikiziwa roho ya kiburi tayari, atakwenda huku na huko kujisifu kuwa hakuna kama yeye.

Biblia inasema “inasema ajishushaye atakwezwa naye ajikwezaye atashushwa”

Ndugu/dada: mali, uzuri, cheo, ukubwa, umaarufu, utakatifu, utumishi,uchungaji, karama, kipaji, kipawa au chochote kile kisikupe kiburi, na kujiona kuwa unastahili heshima ya kipekee Zaidi kuliko wengine, visikufanye ujione kuwa baada ya Mungu mbinguni unafuata wewe. Hiyo ni roho halisi ya shetani kabisa aliyoiachia kuwaangusha watu. Ilimwangusha shetani na ndiyo hiyo hiyo anayotumia kuziangusha nyota nyingi za mbinguni leo (yaani watakatifu).

Biblia inasema katika 1Wakoritho 10: 12 “Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”. Unyenyekevu ndiyo silaha pekee ya kuishinda roho ya kiburi ya shetani. Kama biblia inavyosema katika..

1 Petro 5: 5“..Naam, ninyi nyote JIFUNGENI UNYENYEKEVU, mpate kuhudumiana; kwa sababu MUNGU HUWAPINGA WENYE KIBURI, lakini HUWAPA WANYENYEKEVU NEEMA.

6 Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;

7 huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.

8 Mwe na kiasi na kukesha; KWA KUWA MSHITAKI WENU IBILISI, KAMA SIMBA ANGURUMAYE, HUZUNGUKA-ZUNGUKA, AKITAFUTA MTU AMMEZE. ”

Je! Ni kiburi cha uzima kimekutawala mpaka unaona kuwa hata wokovu si kitu cha maana sana kwako?, Hebu tubu leo uoshwe dhambi zako, na kubatizwa katika ubatizo uliosahihi wa maji tele katika Jina la YESU, ili Bwana akupe ondoleo la dhambi zako. Ukae mbali na hila za ibilisi na mitego yake yote katika kizazi hichi.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Print this post

JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.

Ukiitafakari hii neema tuliyopewa sisi watu wa mataifa ambao hapo mwanzo tulikuwa ni watu wasio na Mungu duniani ni kubwa sana, kiasi kwamba Mungu tangu zamani aliwaficha watu wake wengi, hata manabii wake waliomcha yeye katika Israeli, hawakuweza kuielewa neema hiyo, Mungu aliiweka katika SIRI kubwa sana, ambayo aliitunza mpaka wakati ulipofika wa kufunuliwa kwake, na siri yenyewe Mtume Paulo aliisema katika

Waefeso 3:3 ikiwa mmesikia habari ya uwakili wa neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu;

3 ya kwamba KWA KUFUNULIWA NALIJULISHWA SIRI HIYO, kama nilivyotangulia kuandika kwa maneno machache.

4 Kwa hayo, myasomapo, mtaweza kuutambua ufahamu wangu KATIKA SIRI YAKE KRISTO.

5 SIRI HIYO HAWAKUJULISHWA WANADAMU KATIKA VIZAZI VINGINE; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho;

6 YA KWAMBA MATAIFA NI WARITHI PAMOJA NASI WA URITHI MMOJA, NA WA MWILI MMOJA, NA WASHIRIKI PAMOJA NASI WA AHADI YAKE ILIYO KATIKA KRISTO YESU KWA NJIA YA INJILI;.

Unaona hapo siri yenyewe ni kuwa kumbe hata sisi mataifa ni warithi wa ahadi za Ibrahimu kama wayahudi, katika Kristo. Watu ambao hapo mwanzo tulikuwa tunaonekana kama mbwa kwa wayahudi na ndivyo tulivyokuwa. Lakini Mungu alivyo wa upendo,alituingiza sisi kwa nguvu kupitia Yesu Kristo nasi tuwe warithi sawasawa na wao.

Hivyo ndugu kama wewe ni msomaji mzuri wa biblia utagundua kuwa tangu kipindi cha wana wa Israeli walipokuwa Babeli , Mungu alimfunulia mtumishi wake Danieli muda wa siku zilizobakia mpaka dunia kuisha, ukisoma Danieli 9 utaona kuwa Nabii Danieli aliambiwa muda wa MAJUMA 70 umewekwa kwa watu wake (yaani Waisraeli), mpaka kila kitu kitakapokamilika. Na kumbuka juma moja ni sawa na miaka 7 kibiblia, hivyo ukipiga hesabu utaona jumla yake ni miaka 490 [70×7=490] tu, tangu ule wakati walipotoka Babeli mpaka ulimwengu kuisha.

Lakini ukisoma pale utaona hayo majuma 70 yaligawanywa katika vipindi vitatu, yaani majuma 7 ya kwanza, halafu na majumba 62, kisha juma 1 la mwisho , kukamilisha majuma yote 70. Hatuna muda wa kueleza kwa urefu juu ya migawanyiko hiyo lakini biblia inasema lile juma la 69 litaishia na masihi (YESU KRISTO) kusulibiwa.

Danieli 9: 26 “Na baada ya yale majuma sitini na mawili, MASIHI ATAKATILIWA MBALI, naye atakuwa hana kitu; na watu wa mkuu atakayekuja watauangamiza mji, na patakatifu; na mwisho wake utakuwa pamoja na gharika, na hata mwisho ule vita vitakuwapo; ukiwa umekwisha kukusudiwa.”

Kisha linakuwa limebakia juma moja, ambalo ni sawa na miaka 7 tu ili kila kitu kiwe kimeisha.

Lakini juma hili la mwisho ukichunguza halikuendelea mara baada ya Kristo kusulibiwa, kwasababu kama lingeendelea basi mwisho ulipaswa uwe umeshafika miaka 7 tu mara baada ya kifo cha BWANA YESU, Lakini sasa tunaona imepitia takribani miaka 2000 na mwisho bado haujaja. Jambo ambalo halikuwahi kuonekana katika unabii wowote katika agano la kale. Jambo ambalo manabii wa Mungu hawakuliona wala kufunuliwa.

Na ndio maana hatupaswi kuacha kushukuru neema ya Kristo, kwasababu wokovu huu tunauona sasa ulipaswa uwe kwa WAYAHUDI tu peke yao watu wa Mungu. Jaribu kutengeneza picha kama mwisho ungefika ule wakati Kristo anaondoka duniani sisi wengine leo hii tungekuwa wapi?,Maana hata mitume wa Kristo walitazamia mwisho ungefika baada ya Bwana Yesu kufufuka..

Matendo 1:6 “ Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, JE! BWANA, WAKATI HUU NDIPO UNAPOWARUDISHIA ISRAELI UFALME?

7 Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.

8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.

9 Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, AKAINULIWA, WINGU LIKAMPOKEA KUTOKA MACHONI PAO.”

Kama Bwana asingesema hayo,sisi watu wa mataifa tungekuwa waabudu mizimu, na masanamu, tungekufa na baada ya kufa moja kwa moja ni kuzimu, lakini ashukuruwe Mungu neema ile haikutupita ambayo ililetwa na BWANA WETU YESU KRISTO, ambaye katika ule wakati wa kusulibiwa kwake aliusitisha muda wa WAISRAELI kwanza, usiishe ili atukomboe sisi watu wa mataifa, kwa neema yake, Alituhurumia sisi kwa kulitenga lile juma moja kwanza lililosalia mpaka dunia kuisha, ili hapo katikati atukomboe sisi watu wa mataifa. Na ndio hii miaka 2000 sasahivi tuliyopo ya hii neema. Kwamba kwa kipindi cha miaka takribani 2000 tuingie ndani ya safina sisi watu wa mataifa.

Lakini ndugu fahamu pia hii neema haitadumu milele, tupo ukingoni sana na leo hii tutaona ni jinsi gani ilivyokaribu kuondoka kushinda hata sisi tunavyofikiri, na ikiondoka Mungu anamalizia lile juma 1 moja la mwisho lililobakia (yaani miaka 7) kwa wayahudi WATEULE wake tu!! kisha mwisho wa dunia unawasili. Ndugu ukilijua hilo hutafanya mchezo na wokovu wako sasa.

Mungu aliwapiga upofu makusudi wayahudi(Waisraeli) wasiupokee wokovu tangu wakati ule Kristo kusulibiwa ili sisi tuupate, kwasababu kama wangeupokea wokovu wa KRISTO wakati ule basi dunia ingekuwa imeshakwisha. Mungu aliwajeruhi wayahudi kwa ajili yetu, na ndio maana unaona sasa hivi wengi wao hawamwamini Yesu kama ndiye yule masiya waliokuwa wanamtazamia.. Ni kwasababu gani?, ni kwasababu Mungu alipiga mwenyewe upofu ili tu sisi tuokoke, Mungu aliwatia mwenyewe jeraha sio kwasababu wao walikuwa na dhambi nyingi kushinda sisi hapana, kinyume chake sisi ndio tuliokuwa na dhambi nyingi kuliko wao, lakini Mungu alifanya vile kutuhurumia sisi (yaani mimi na wewe) tufikilie wokovu. Soma kitabu cha Warumi sura ya 11 yote utaona jambo hilo.

Lakini pamoja na hayo tunasoma miaka mingi iliyopita Mungu aliwaahidi kuwarudia watu wake wateule wayahudi, baada ya kipindi fulani mbele, na kuwaimarisha tena. Na Ndio sasa tunasoma katika kitabu cha Hosea, yeye anasema:

HOSEA 6:1 Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu.

2 BAADA YA SIKU MBILI ATATUFUFUA; SIKU YA TATU ATATUINUA, NASI TUTAISHI MBELE ZAKE.

3 Nasi na tujue, naam, tukaendelee kumjua Bwana; kutokea kwake ni yakini kama asubuhi; naye atatujilia kama mvua, kama mvua ya vuli iinyweshayo nchi.

Umeyaelewa maneno hayo?, Huo unabii unawahusu wayahudi tu! {yaani waisraeli}, Hosea anasema njoni tumrudie Bwana, akiwaambia wayahudi wenzake katika Roho, baada ya SIKU MBILI atatufufua na siku ya tatu atatuinua, nasi tutaishi mbele zake.

Kama ukisoma biblia katika kitabu cha 2Petro 3:8 utafahamu kuwa kwa Mungu SIKU MOJA NI SAWA NA MIAKA 1000, Hivyo hapo utaona kuwa unabii unaweza ukatafsiriwa hivi “Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu. baada ya miaka 2000 atatufua na mwaka wa 3000 atatuinua”.

Ndugu tangu Kristo kuondoka hadi sasa, miaka 2000 inakaribia kuisha, na miaka ya hivi karibuni tutaanza wa 3000, na huo mwaka wa 3000 utakuwa ni milenia ya ule utawala wa miaka 1000 wa Yesu Kristo duniani (Ufunuo 20:4). Sasa kama hapo anavyosema atatufufa, atafunga jeraha zetu na kutuponya, hiyo inamaanisha kuwa huo ndio utakuwa ule wakati wa wayahudi kurudiwa na Mungu wao, kumaliza lile juma moja la mwisho lililokuwa limesalia (yaani miaka 7) ili dunia kuisha. Utakuwa ni wakati wa Israeli kurudishiwa ufalme kama walivyomuuliza Bwana siku ile kabla ya kupaa kwake.

Ndugu neema ikishalirudia Taifa la Israeli, unyakuo wa kanisa utakuwa umeshapita, kitakachokuwa kimebakia katika mataifa yote ulimwenguni ni MAJUTO NA MAOMBOLEZO, fikiri Bwana ametuhurumia kwa kipindi kirefu hichi chote ili mtu tu yeyote asiangamie lakini bado unaichekezea hii neema iliyopo kwa kitambo tu. Bwana aliposema kutakuwa na kilio na kusaga meno, alimaanisha kweli wala hakutudanganya. Miaka 2000 hii inaisha, Taifa la Israeli linazidi kunyanyuka siku baada ya siku, ule mwisho unakaribia, je! Umejiwekaje tayari sasa?. Kwanini bado unaichezea hii neema ya msalaba ambayo sisi hatukistahili kuipata?. Utajibu nini siku ile?. Au utajitetea vipi?.

Waebrania 2: 3 “SISI JE! TUTAPATAJE KUPONA, TUSIPOJALI WOKOVU MKUU NAMNA HII? AMBAO KWANZA ULINENWA NA BWANA, KISHA UKATHIBITIKA KWETU NA WALE WALIOSIKIA;”

Hizi ni saa za majeruhi kama hujakamilishwa katika wokovu fanya bidi sana, utubu, ubatizwe katika ubatizo sahihi wa maji tele na katika Jina la Yesu Kristo, upate ondoleo la dhambi zako, kisha udumu katika ushirika wa Kristo na mafundisho ya biblia angali siku ile inakaribia.

Kwasababu moja ya hizi siku dunia itakuwa imekwisha kabisa.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu, na Mungu atakubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?

JE! DAMU INA UMUHIMU WOWOTE KATIKA MAISHA??

ZIFAHAMU NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE SABA.

JE! MTU ANAPOFUNGA KWA MUDA WA SAA 24,ANAPASWA KUNYWA MAJI AU KITU CHOCHOTE?

JE! NI SAHIHI KUMUITA MARIA MAMA WA MUNGU?


Rudi Nyumbani

Print this post

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

Imekuwa ni ngumu kwa watu wengi kuisikia sauti ya Mungu ikizungumza maishani mwao, hii ni kutokana na kwamba hawamjui wanayemwomba au, pengine jinsi walivyofundishwa na viongozi wao wa Imani, wakielezwa kuwa Mungu wakati wote akitasema na mtu huwa inasikika sauti kama ya mtu mwingine wa pili ndani yake akimpa maelekezo Fulani ya kufanya, na hali hiyo mtu haifikii mpaka atakapofikia kiwango Fulani cha kiroho…

Na ndio hapo utamwona mtu anapambana na kutumia nguvu nyingi kufikia hilo lengo la kusikia hiyo sauti ya Roho Mtakatifu ikizungumza naye ndani kama mtu Fulani, lakini kwa bahati mbaya anaishia kutokusikia chochote na mwisho wa siku kukata tamaa, akidhani kuwa Mungu hazungumzi naye na kumwona Mungu kama ni mgumu sana kufikika kirahisi… Lakini kumbuka Bwana anasema katika Neno lake.

Isaya 65: 12 “…….. NILIPOITA HAMKUITIKA; NILIPONENA, HAMKUSIKIA; bali mlitenda yaliyo mabaya machoni pangu, mlichagua mambo nisiyoyafurahia”.

Unaona hapo? Bwana anazungumza na kila mtu, ananena lakini hatusikii, anaita lakini sisi ndio hatuitiki, tatizo linakuja ni hatujui jinsi ya kuielewa sauti yake, tunataka Mungu azungumze kwa njia zetu sisi kama vile mtu anaongea na rafiki yake, lakini hatutaki yeye azungumze katika njia zake na hapo ndipo tunapomkosa. Njia pekee ambayo Mungu anatumia sikuzote kuzungumza na watu ni kwa kupitia Neno lake tu!, hivyo usipokuwa na Neno la Mungu ndani yako, ni ngumu kuielewa sauti ya Mungu,kwani ni kweli atazungumza na wewe lakini hautamwelewa hata kidogo..

Na ndio maana jambo la kwanza analolifanya Bwana kwa mtu, ni kulijaza Neno lake ndani yake ili atakapozungumza naye aweze kuisikia kiwepesi na kuielewa, tunaweza kuchukua mifano kadhaa ya maisha ya kawaida tu:

Inatokea mtu labda ni mwajiriwa, na amefanya kazi muda mrefu katika cheo cha kawaida tu,na amekuwa pengine akidharauliwa, au akichukiwa, au akinyanyaswa kazini hivyo akadhamiria kumwomba Mungu kwa machozi ampandishe cheo, amutoe mahali alipo na kumpandisha hatua moja zaidi, lakini mara tu alivyoomba hivyo, ndio kwanza mambo kazini yakazidi kubadilika na kuwa magumu zaidi, dharau zikaongezeka, manyanyaso yakazidi, chuki zikazidi kuongezeka na bado kazi zinazidi kuwa nyingi na akiangalia mshahara ni ule ule.

Sasa kwa namna ya kawaida huyu mtu,(Tumpe jina la Rachel) ni rahisi kusema moyoni mwake Mungu hasikii maombi yake, na Mungu hajajibu maombi, licha ya kufunga na kuomba kwa muda mrefu hakuna matokeo yoyote. Lakini kwasababu Neno la Mungu halijakaa ndani yake anaamua kughahiri na kusema Mungu hanisikii..

Lakini tujifunze wazo la Mungu juu ya Rachel lilikuwa ni lipi?

Tukirudi katika maisha ya Rachel ya nyumbani ya kawaida, ni mwanamke aliyeolewa na mume mmoja mkristo, anaishi na watoto wake wawili anaishi pia na kijakazi wake aliyemwajiri amsaidie kazi za nyumbani. Anawapenda na kuwajali sana watoto wake na mume wake lakini tatizo la Rachel lilikuwa ni moja, hakumjali sana mfanyakazi wake wa ndani, alikuwa akimwamsha asubuhi na mapema sana kabla yao kuamka, na kumpa majukumu ya kazi za nyumbani, na aliporudi nyumbani kutoka kazini akimkuta Yule kijakazi akiwa na baadhi ya shughuli hakumwacha apumzike hata kidogo, alimwongezea nyingine, na wakati Rachel na wanawe wanalala saa 3 usiku, Yule kijakazi wake aliendelea na kazi mpaka saa 5 usiku, licha ya kufanya kazi kwa muda mrefu hivyo Rachel hakulithamini hilo, wakati mwingine alikuwa akimkemea, na kumuudhi na zaidi ya yote hakutilia maanani suala la kumwongezea mshahara kwa wingi wa kazi alizompa. Lakini Yule kijakazi aliona ni haki yake kufanyiwa vile, wala hakuona vibaya wala kulalamika wala kuona kama anaonewa.

Sasa tukirudi katika maisha ya Rachel ya kazini kwake ndio tunamkuta anapitia hali kama ya Yule kijakazi wake nyumbani na hajui tatizo ni nini?. Boss wake hampendi, wakati mwingine anajitahidi kuonyesha bidii lakini hapandishwi mshahara..Lakini Kwasababu alifanya uamuzi wa busara kwenda kumwomba Bwana juu ya suala hilo, Bwana naye hakukawia kumjibu…Na majibu Bwana aliyompa ndio hayo; visa kazini kuwa vingi zaidi ya vile alivyokuwa navyo mwanzo, dharau kuongezeka, kuchukiwa na boss, wengine kupandishwa cheo na Rachel kubaki katika hali ile ile, n.k..

Lakini Rachel angetaka kujinyenyekeza zaidi na kutaka kulitafakari Neno la Mungu, angeelewa kuwa Mungu ameshamjibu, Alichopaswa kufanya ni kuchunguza matukio yaliyotokea baada ya yeye kuomba vile na kwa msaada wa Roho Mtakatifu angejua kuwa Mungu alimwambia maneno haya..

Mathayo 7:12 Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo;

Na pia…

Luka 6: 38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”.

Hiyo ilikuwa ni sauti ya Mungu kwa Rachel, Mungu kwa kuwa alimpenda, hivyo akamjibu kulingana na Neno lake, kwahiyo Rachel angeligundua lile haraka moja kwa moja angetubu, na kuacha kumwendesha na kamripia kijakazi wake vibaya, angeacha kumkemea pasipo sababu, angeacha kumdharau, angeacha kumshindilia kazi nyingi, mpaka saa za usiku wa manane, angempa muda mwingi wa kupumzika, angemwongeza mshahara kulingana na wingi wa kazi anazozifanya

Sasa bila kutumia nguvu nyingi angeanza kuona mabadiliko makubwa kazini ndani ya muda mfupi na yeye angeanza kufanyiwa kama anavyomfanyia kijakazi wake, Mungu atamfanyia fadhili ghafla anapandishwa cheo, kupendwa na watu waliokuwa wanamchukia, mara kaongezewa mshahara, mara anaanza kupendwa na mkubwa wake, anapata amani na watu wote,..kwasababu lile neno Bwana alilosema.

“. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”. Linatimia juu yake, Hivyo Mungu ni lazima ahakikishe Neno lake linatimia katika kazi yake. Na majibu ya maombi yake anayaona wazi.

Mfano mwingine utakuta Dada mwingine umri wake umeenda, kila mwanamume atakayemwona anamkimbia, anaona wengine wanaolewa hata walio wadogo kuliko yeye, lakini yeye anapitwa tu, kwahiyo anaamua kufanya uamuzi wa busara kumwomba Mungu ampe mume mzuri, ambaye atakuwa anajitambua, mcha Mungu, na anayejiheshimu na mwenye upendo na malengo.

Hivyo baada ya maombi hayo ya kina muda mfupi tu baadaye anakutana na mahubiri yanayolenga mwenendo wa mwanamke, na ndani ya mahubiri hayo anasikia mada ihusuyo uvaaji wa mwanamke umependezao Mungu, anasikia ndani yake ni machukizo kwa Mungu mwanamke kuvaa suruali na vimini na kaptura, haipendezi mbele za Mungu mwanamke wa kikristo kuweka mawigi, na lipstick,na wanja, anasikia Neno linalosema..

1 Timotheo 2: 9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa MAVAZI YA KUJISITIRI, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;

10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.”

Sasa kwasababu pengine mwanamke yule hajajifunza kusikia sauti ya Mungu jinsi inavyozungumza, moja kwa moja anapuuzia lile Neno na kuendelea na maisha yake ya uvaaji usiompendeza Mungu, wakati muda huo huo unakuta kuna mwanamume mahali Fulani Mungu kamweka mwenye vigezo vyote anavyovihitaji, lakini Yule mwanaume ni mkristo anasubiri Mungu amletee mwanamke mwenye vigezo vya usafi wa mwili na utakatifu, mwenye kujisitiri, asiyefanana na wanawake wa ulimwengu huu.

Sasa kwasababu Yule dada hana Neno la Mungu ndani yake kujua kwamba ile ni sauti ya Mungu, inayotaka kumtengeneza kumwandaa kumpata mume anayemuhitaji, anadharau anaona wanaohubiriwa yale ni wanawake waliokosa mwelekeo..Hivyo anajikuta anamkosa yule mwanamume na kuendelea katika hali hiyo hiyo ya kutokuolewa kwa muda mrefu na hata akiolewa ataoloewa na mtu ambaye hana vile vigezo anavyovitaka…Shida ni kwamba hajaielewa sauti ya Mungu ilipokuwa inasema naye.

Kadhalika unakuta mwingine ni mgonjwa pengine ana ugonjwa usiotibika labda HIV, Ikafikia wakati akahitaji Mungu amponye ugonjwa wake, aliomba kwa imani akijua kabisa Mungu kamsikia maombi yake, hivyo akaenda huku na kule kwa mtumishi huyu mpaka mtumishi Yule, kutoka taifa hili mpaka taifa lile, kutafuta uponyaji wake alifanya hivyo kwa muda mrefu lakini hakuona matokeo yoyote ya kupona ugonjwa wake. Mwisho wa siku akaamua kukata tamaa na kusema moyoni mwake Mungu hasikii wala hajibu maombi.

Lakini ukirudi nyuma ya maisha ya huyu mtu, siku ile ile alipoomba Mungu amponye, Mungu alimsikia, baada ya siku chache alifungua redio akasikia mahubiri yanayosema “chanzo cha mambo yote ni dhambi,” Chanzo cha magonjwa ni dhambi, chanzo cha kifo ni dhambi n.k… Hivyo akasikia mafundisho hayo na kweli yakamchoma moyo, na aliposikia kwamba atubu kwa kumaanisha kuacha dhambi kabisa, akabatizwe kwa jina lake Yesu Kristo apate ondoleo la dhambi zake, na kumwishia Mungu katika maisha ya utakatifu, hakutakuwa na jambo lolote au mlima wowote utakaosimama mbele yake, kwasababu waliomwamini yeye wamepewa amri zote za kukanyaga, nge, na nyoka na nguvu zote za Yule mwovu,..

Lakini yeye aliposikia habari za toba, za kuacha uasherati, kuacha rushwa, kuacha sigara, usengenyaji, n.k. akadhani kuwa yale ni mahubiri tu ya siku zote ya walokole pasipo kujua kuwa ile ni sauti ya Mungu inayotaka kumpeleka katika kupokea uponyaji wake.

Laiti angekuwa na Neno la Mungu ndani yake, angefahamu kuwa biblia inasema katika Mithali 3: 7 ”…..Mche Bwana, ukajiepushe na uovu. 8 Itakuwa afya mwilini pako, Na mafuta mifupani mwako”.

Yeremia 30: 17 “Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana,…”

Wakati mwingine magonjwa yanakuwa ya kimaagano na hayawezi kuondoka kama mtu hajaamua kwanza kuvunja maagano hayo na kuingia katika agano jipya la damu ya YESU. Watu wengi wanamkimbilia Mungu awaponye, awainue, awafundishe, lakini hawajui kanuni za Mungu za kuzungumza na wanadamu, wao wanataka wajibiwe tu kama wanavyotaka wao. Hapana Mungu haendi hivyo, siku zote Mungu yupo katika Neno lake. Na huko ndipo utakapoweza kuisikia sauti ya Mungu. Mahali pengine popote kwako itakuwa kama ngurumo tu. Kama wewe sio mkristo (nikimaanisha Mkristo wa kweli aliyesimama na Bwana na Neno la Mungu limejaa ndani yako ) kamwe hutaweza kuisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe, utaomba kila siku hutaona chochote, utafunga na kulia hutapata chochote, tatizo sio Mungu tatizo ni wewe..Sikiliza Mungu anavyosema..

Isaya 66: 4 “Mimi nami nitachagua mapigo yao, nitaleta hofu zao juu yao; kwa sababu nilipoita, hawakuitika; na niliponena, hawakusikia; bali walifanya yaliyo maovu machoni pangu, NA KUYACHAGUA NISIYOYAFURAHIA”.

Hivyo ndugu isikie sauti ya Mungu leo inayozungumza na wewe sasahivi, unataka kwenda katika unyakuo?? Tubu! dhambi zako ukaoshwe kwa damu ya Yesu, na kuishi maisha matakatifu. Unataka kuponywa?? Acha dhambi!.. unataka kufunguliwa?? Acha uasherati!!, acha kutazama Pornography, acha ulevi, acha sigara, acha usengenyaji, acha wizi, acha rushwa, acha uvaaji mbovu kama wanawake wa kidunia,..Acha kutazama vitu visivyokuwa na faida yoyote katika maisha yako ya kiroho badala yake anza sasa kujifunza Neno la Mungu ili atakapozungumza na wewe usikie, pale anapokujibu uelewe. Ndugu maombi hayajibiwi kwa mafuta ya upako, wala maji, wala chumvi, Mungu atakujibu na kukufungua  kwa NENO LAKE TU!!! Na si kingine.

Mungu akubariki.

Kwa mawasiliano/ Maombezi/Ushauri/ Piga:+255693036618/ +255789001312

Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

USIPOLITENDEA KAZI NENO LA MUNGU.

SAUTI AU NGURUMO?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

TOA HUDUMA ILIYO BORA.


Rudi Nyumbani

Print this post

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA TATU WA YOHANA.

Katika Kitabu hichi tunaona Mtume Yohana akiandika barua, kwa mtu, barua ya kumtakia mafanikio katika mambo yake yote, pamoja na afya njema, Hii ni barua ya kipekee sana mbali na barua nyingine zote tunazozijua za mtume Yohana ambazo aliziandika kwa makanisa, mfano ile ya ufunuo wa Yohana n.k.

Hii ilihusu kumtakia mtu mafanikio, katika Nyanja zote za maisha yake, ikiwemo kazi zake za mikono, biashara zake, miradi yake, elimu yake kama alikuwa nayo, mali zake, mipango yake, familia yake n.k…Na Zaidi ya yote katika upande wa afya, awe nayo tele..Ni wazi kabisa waraka huu ni wa faraja sana ambao hata sasa tunapenda kuutumia watu wengi, kumkumbusha Mungu kwamba alisema katika Neno lake “MPENZI NAOMBA UFANIKIWE KATIKA MAMBO YOTE NA KUWA NA AFYA YAKO, KAMA VILE ROHO YAKO IFANIKIWAVYO.”

Lakini ni muhimu tujifunze kitu, kabla Mtume Yohana hajazitoa hizo Baraka zote kwa uweza wa Roho wa Mungu je! ni kitu gani kilichomsukuma yeye kusema vile?.

Na ndio maana tunasoma mwanzoni tu wa nyaraka, kabla hajaeleza jambo lingine lolote alitoa kwanza mwongozo ule waraka unamuhusu nani, na ndio tunaona hapo anamtaja mtu mmoja anayeitwa GAYO. Kwamba waraka ule ulimuhusu yeye.

Tusome:

1Yohana 1“Mzee, KWA GAYO MPENZI, nimpendaye katika kweli.

2 Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”.

Kama tunavyosoma waraka huu hakuandikiwa kila mtu, kama nyaraka nyingine zilivyokuwa, haukuandikwa kwa kila mkristo, kama nyaraka nyingine zilivyokuwa, Kumbuka zipo nyaraka zilikuwa zimeandikwa kwa watu wote, kama vile waraka wa Yuda,na wa Petro, na Waraka wa kwanza wa Yohana, kadhalika zipo zilizokuwa zimeandikwa kwa wakristo tu kwamfano Wakorintho, wagalatia, wakolosai, warumi,ufunuo n.k. na zipo pia zilizokuwa zimeandikwa kwa watu maalumu {yaani mtu mmoja mmoja} mfano wa nyaraka hizo ni waraka wa Timotheo, Filemoni,Tito, 2Yohana, na waraka wa tatu wa Yohana ambao ndio huu sasa unaomuhusu mtu mmoja anayeitwa GAYO.

Wengi tunaupenda huu waraka lakini tunashindwa kufahamu uliandikwa kwa nani, kumbuka haukuandikwa kwa watu wote, bali kwa mtu mmoja anayeitwa Gayo. Hivyo ili kwamba Baraka zile zilizoandikwa katika waraka ule zitufikie na sisi tunapaswa tufanane na huyu mtu anayeitwa GAYO vinginevyo hata tukidai vipi kwamba ni za kwetu, lakini ukweli ni kwamba haziwezi kuwa za kwetu, hazitatuhusu kabisa.

Sasa Ni vizuri tukimsoma huyu GAYO alikuwa ni mtu mwenye TABIA GANI tusome.

3 Yohana 1“ Mzee, kwa Gayo mpenzi, nimpendaye katika kweli.

2 Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo.

3 Maana nalifurahi mno walipokuja ndugu na kuishuhudia kweli yako, kama uendavyo katika kweli.

4 Sina furaha iliyo kuu kuliko hii, kusikia ya kwamba watoto wangu wanakwenda katika kweli.

5 MPENZI, KAZI ILE NI YA UAMINIFU UWATENDEAYO HAO NDUGU NA HAO WAGENI NAO,

6 WALIOKUSHUHUDIA UPENDO WAKO MBELE YA KANISA; UTAFANYA VIZURI UKIWASAFIRISHA KAMA IPASAVYO KWA MUNGU.

7 KWA MAANA, KWA AJILI YA JINA HILO, WALITOKA, WASIPOKEE KITU KWA MATAIFA.

8 Basi imetupasa sisi kuwakaribisha watu kama hao, ili tuwe watenda kazi pamoja na kweli.

9 Naliliandikia kanisa neno, LAKINI DIOTREFE, APENDAYE KUWA WA KWANZA KATI YAO, HATUKUBALI.

10 Kwa hiyo, nikija, nitayakumbuka matendo yake atendayo, atoavyo upuzi juu yetu kwa maneno maovu; wala hatoshwi na hayo, ILA YEYE MWENYEWE HAWAKARIBISHI HAO NDUGU, NA WALE WATAKAO KUWAKARIBISHA, HUWAZUIA, NA KUWATOA KATIKA KANISA.

11 Mpenzi, usiuige ubaya, bali uige wema. Yeye atendaye mema ni wa Mungu, bali yeye atendaye mabaya hakumwona Mungu.

12 DEMETRIO ameshuhudiwa na watu wote, tena na ile kweli yenyewe. Nasi pia twashuhudia, nawe wajua ya kwamba ushuhuda wetu ni kweli.

13 Nalikuwa na mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kukuandikia kwa wino na kalamu.

14 Lakini nataraji kukuona karibu, nasi tutasema uso kwa uso. [15] Amani kwako. Rafiki zetu wakusalimu. Wasalimu hao rafiki zetu, kila mtu kwa jina lake”.

Ukisoma kwa makini utagundua kwanini GAYO alistahili kutamkiwa maneno ya Baraka kama yale, kwanza utagundua kuwa alikuwa ni mtu mwenye huruma juu ya kazi ya Mungu, pale alipoona kuna uhitaji wa injili kupelekwa mbele, alijitoa kikamilifu kuichangia kazi ya Mungu, kwa kuwasafirisha wale watumishi wa Mungu kuipeleka injili kila mahali palipohitajika pasipo kujali kupungukiwa kwa namna yoyote,tofauti na wakristo wengi waliokuwepo katika makanisa yale na zaidi ya yote alikuwa anawakaribisha pia wageni (wakristo) waliokuwa wanatoka mbali kwa ajili ya kwenda kuifanya kazi ya Mungu.

Ilifikia mpaka hatua wale wote waliokuwa wanaifanya kazi ya Mungu ambao walikuwa katika maeneo yale aliwasaidia kiasi kwamba wakawa hawana uhitaji wowote kutoka kwa watu wasioamini, yeye aliwahudumia kwa vyote, unaweza kutengeneza picha hakukuwa na kikwazo chochote cha kifedha na kimazingira kilichokwamisha kazi ya Mungu maeneo yale, alifanya hivyo kwa bidii mpaka sifa zake zikavuma katika makanisa yote ya Kristo, na habari kumfikia Mtume Yohana.

Lakini wakati huo huo pia alikuwepo mtu mwingine aliyeitwa DIOTREFE, yeye hakuwa kama Gayo, alimwona Gayo kama anapoteza mali nyingi, kwa kazi isiyokuwa na maana au faida, ya kuwachangia wengine katika kuipeleka Injili. Aliona kuwa ni jambo lisilokuwa na maana kuwakaribisha wageni watu wasiowajua katika makanisa yao, na Zaidi ya yote alikuwa anawafukuza wageni wa kikristo waliotoka mbali kuja kujumuika nao, aliona wote waliofanya hivyo hawana mipango rasmi ya maisha yao, aliwaona kama wana fedha za kuchezea, Ni wazi kuwa Diotrefe alikuwa ni kikwazo cha Injili ya Kristo kwenda mbele. Huku akijifanya kuwa ndiye kiongozi..Lakini ni kiongozi ambaye hakupenda kujitoa kwa Mungu, mfano wa viongozi wengi waliopo leo.

Na ndio hapo tunaona waraka huu mtume Yohana anamwandikia GAYO peke yake aliyekuwa mwaminifu kwa kujitoa na kuokujali nafsi yake peke yake kwa ajili ya injili.. Tunasoma alianza tu na kumwambia.. “ Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”. Maneno ya faraja kiasi gani!!

Unaona hapo baada ya wema wake kujulikana na taabu yake katika kujitoa katika kazi za Mungu, kudhihirika ndipo hapo Baraka nyingine zote zikafuata juu yake. Ni kwa vile biblia haiwezi kuandika kila kitu, lakini ni wazi kabisa Gayo kuanzia ule wakati alibarikiwa kwa namna isiyo ya kawaida, pengine alikuwa na shamba moja tu Mungu akampa 10, pengine alikuwa na nyumba 1 yenye vyumba vinne, alivyovifanya viwili vya kwake na vilivyosalia vya wageni, lakini Mungu alimwongezea nyumba nyingi nyingi, na mali na Zaidi ya yote, alipata afya njema na maisha marefu yenye heri yeye pamoja na familia yake yote. Alikuwa ni mfano wa Ayubu katikati ya jamii ya wakristo waliokuwepo wakati ule.

Lakini wengi wetu tunashindwa kufahamu kanuni za Mungu za kubarikiwa, Tunapenda kwenda kuombewa huku na kule, tunatoka kwa mtumishi huyu mpaka huyu, tunatamka haya maneno kila siku midomoni mwetu, Lakini bado tunaona hali ni ile ile, au matokeo ni machache.. Ni muhimu kujua kabla hatujamwomba Mungu atufanyie kitu Fulani tuangalia na vigezo vilivyowekwa nyuma yake ya kupata hicho kitu, vinginevyo tutaona kama Neno la Mungu ni uongo kwetu.

Leo hii unaona kazi ya Mungu katika kusanyiko lako inauhitaji Fulani, injili ya Kristo ili iende mbele kwa njia ya kupelekea wahubiri au vitabu, n.k. changia bila kujali itakugharimu kiasi gani,fadhili kwa chochote ulichonacho, wewe timiza tu wajibu wako kwasababu aliye juu anakuona. 

Unaona kazi ya Mungu mahali Fulani inakwama kwasababu imekosa ujuzi unaofanana na wa kwako ili iendelee, tumia huo ujuzi wako kurekebisha hilo eneo kwa bidii sana, na sifa zako zitavuma mbinguni..Siku moja hilo Neno “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote” litatamkwa juu yako pasipo hata wewe kujua, na ndipo Mungu atakapokufanikisha katika mambo yako yote na kukupa afya yako..FANYIKA GAYO KUANZIA LEO. Kumbuka Baraka zile zinamhusu GAYO peke yake.

Kuna kipindi wana wa Israeli waliacha kuijenga nyumba ya Mungu na kila mmoja akaenda shambani mwake kufanya mambo yake mwenyewe, pasipokujali nyumba ya Mungu imekaa katika hali gani, Jambo hilo lilimuhuzunisha sana Bwana mpaka akaamua kuwapiga kwa taabu na shida na uhaba wa vitu pasipo hata wenyewe kujua…Ndipo Bwana akawatumia Nabii Hagai na kuwaambia maneno haya.

Hagai 2: 2 “Bwana wa majeshi asema hivi, ya kwamba, Watu hawa husema, Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujenga nyumba ya Bwana.

3 Ndipo neno la Bwana lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema,

4 Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika?

5 Basi sasa, Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu.

6 Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo; mnakula lakini hamshibi; mnakunywa lakini hamkujazwa na vinywaji; mnajivika nguo lakini hapana aonaye moto; na yeye apataye mshahara apata mshahara ili kuutia katika mfuko uliotoboka-toboka.

7 Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu.

8 Pandeni milimani, mkalete miti, mkaijenge nyumba; nami nitaifurahia, nami nitatukuzwa, asema Bwana.

9 MLITAZAMIA VINGI, KUMBE VIKATOKEA VICHACHE; tena mlipovileta nyumbani nikavipeperusha. NI KWA SABABU GANI? Asema Bwana wa majeshi. NI KWA SABABU YA NYUMBA YANGU INAYOKAA HALI YA KUHARIBIKA, WAKATI AMBAPO NINYI MNAKIMBILIA KILA MTU NYUMBANI KWAKE.

10 Basi, kwa ajili yenu mbingu zimezuiliwa zisitoe umande, nayo nchi imezuiliwa isitoe matunda yake.

11 Nami nikaita wakati wa joto uje juu ya nchi, na juu ya milima, na juu ya nafaka, na juu ya divai mpya, na juu ya mafuta, na juu ya kila kitu itoacho nchi, na juu ya wanadamu, na juu ya wanyama, na juu ya kazi zote za mikono”.

Unaona hapo? Maombi yangu ni kwamba Bwana atufanye sote kuwa GAYO leo. Ili zile Baraka zote zilizoandikwa pale zisitupite.

Ubarikiwe.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 

Mada Nyinginezo:

KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.

YESU MPONYAJI.

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA

YONA: MLANGO 1

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

JIFANYIE RAFIKI KWA MALI YA UDHALIMU.


Rudi Nyumbani:

Print this post

MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI.

Katika agano la kale, wakati wana wa Israeli wakiwa safarini kuelekea nchi ya ahadi, walioahidiwa na Mungu mwenyezi, tunaona Bwana Mungu, alijua shida iliyokuwa mbele yao kwamba watapita katika nchi ya jangwa isiyokuwa na kitu, isiyokuwa na kupanda wala kuvuna, nchi kame, hivyo alikuwa ameshawaandalia namna ya kuwalisha kabla hata hawajatoa miguu yao Misri, na ndio tunaona, aliwashushia MANA itokayo juu mbinguni, lakini Bwana alikuwa na sababu kubwa sana ya kufanya vile, kutowapitisha njia yenye chakula tele, au yenye masoko ambayo wangeweza kununua chakula.

Sasa moja ya muujiza mkubwa wa ile mana, ni kwamba haikuwa mikate kama mikate, hapana bali zilikuwa ni chembe ndogo kama za mtama, ambazo walipoamka kila asubuhi walizikuta juu ya ardhi, na walipozikusanya walienda kuzisaga, na kuwa unga kisha kuzitengeneza kuwa mkate.

Wale waliokusanya mana nyingi, waliwapunguzia wale waliokusanya vichache hivyo hakuna aliyemzidi mwenzake…

Kutoka 16:14-18” Na ulipoinuka ule umande uliokuwa juu ya nchi, kumbe! Juu ya uso wa bara kitu kidogo kilichoviringana, kidogo kama sakitu juu ya nchi.

15 Wana wa Israeli walipokiona, wakaambiana, Nini hiki? Maana hawakujua ni kitu gani. Musa akawaambia, Ndio mkate ambao Bwana amewapa ninyi, mle.

16 Neno hili ndilo aliloagiza Bwana, Okoteni ninyi kitu hicho kila mtu kama ulaji wake ulivyo; kichwa pishi,kama hesabu ya watu wenu ilivyo ;ndivyo mtakavyotwaa,kila mtu kwa ajili ya hao walioko hemani mwake.

17 Wana wa Israeli wakafanya hivyo, wakaokota wengine zaidi, wengine kupungua.

18 Nao walipoipima kwa pishi, yeye aliyekuwa ameokota kingi hakubakiwa na kitu, na yeye aliyekuwa ameokota kichache hakupungukiwa; wakaokota kila mtu kama ulaji wake ulivyokuwa”

Sasa jambo tunaloweza kujifunza hapo, ni kwamba Bwana alitaka kuwafundisha watu wake kwamba waishi kama ndugu, wahudumiane kila mtu na nduguye, mmoja anapokusanya kingi na mwingine anapokusanya vichache, yule mwenye nyingi ampunguzie yule mwenye vichache, kwasababu wamepewa bure.

Jambo hilo hilo linaendelea sasa katika Roho, kama vile wana wa Israeli walipewa mana ya mwilini kuwafanya waishi kule nyikani, leo hii Bwana Mungu ametoa MANA YA ROHONI kutufanya sisi tuishi katika Jangwa hili la Roho, na kama vile mana ile ilishuka tu kwa wana wa Israeli na sio watu wote wa ulimwengu mzima, vivyo hivyo na mana hii ya sasa ya Rohoni, itawafaa wale tu, waliokuwa tayari kuchukua gharama za kutoka Misri(ya rohoni) na kuelekea kaanani.

SASA HII MANA NI IPI?

Hii mana mpya si mwingine Zaidi ya BWANA WA UTUKUFU, YESU KRISTO. Biblia inasema katika…

Yohana 6: 28 “Basi wakamwambia, Tufanyeje ili tupate kuzitenda kazi za Mungu?

29 Yesu akajibu, akawaambia, Hii ndiyo kazi ya Mungu, mmwamini yeye aliyetumwa na yeye.

30 Wakamwambia, Unafanya ishara gani basi, ili tuione tukakuamini? Unatenda kazi gani?

31 Baba zetu waliila mana jangwani kama vile ilivyoandikwa, Aliwapa chakula cha mbinguni ili wale.

32 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Siye Musa aliyewapa chakula kile cha mbinguni, bali Baba yangu anawapa ninyi chakula cha kweli kitokacho mbinguni.

33 Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.

34 Basi wakamwambia, Bwana, sikuzote utupe chakula hiki.

35 Yesu akawaambia, MIMI NDIMI CHAKULA CHA UZIMA; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe”.

Unaona hapo? Bwana Yesu ndio chakula cha uzima, mfano wa mana, sasa aliposema chakula hakumaanisha vyakula vya kupikwa na wanadamu, hapana! Ukisoma katika tafsiri nyingine za kiingereza tafsiri hapo ya chakula ni “bread” yaani “mkate”John 6: 35”Then Jesus declared, “I am the bread of life. Whoever comes to me will never go hungry”

Hivyo kama vile, MANA ilivyokuwa inaliwa na wana wa Israeli siku kwa siku, vivyo hivyo Mana hii mpya ya rohoni tuliyopewa na Baba, tunaila siku baada ya siku, ikiwa na maana kuwa, tunajifunza maneno ya YESU KRISTO siku kwa siku, hatuachi mpaka siku tutakayoingia kaanani yetu(mbingu mpya na nchi mpya).

Ndio maana tunashiriki meza ya Bwana,(divai na mkate) kipindi baada ya kipindi, kuashiria kuwa katika roho zetu tunakula maneno ya Yesu Kristo siku kwa siku.

Na kama vile ile mana si wote waliokota kwa kipimo kimoja, wengine waliokota kingi wengine pungufu, lakini aliyeokota vingi alimpunguzia yule aliyeokota vichache, vivyo hivyo na katika MANA hii ya rohoni, tumepewa agizo la kukusanyika pamoja ili Bwana atuhudumie Neno lake kila mtu kwa kipimo cha karama alichomkirimia, na ndio maana kuna umuhimu mkubwa sana wa kukusanyika pamoja.

Tunakuwa tunaula mwili wa Yesu kristo ambaye ndiye chakula kitokacho mbinguni siku baada ya siku. Na ndio maana Bwana aliendelea na kusema ..

Yohana 6: 48 “Mimi ndimi chakula cha uzima.

49 Baba zenu waliila mana jangwani; wakafa.

50 HIKI NI CHAKULA KISHUKACHO KUTOKA MBINGUNI, KWAMBA MTU AKILA WALA ASIFE.

51 Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.

52 Basi Wayahudi walishindana wao kwa wao wakisema, AWEZAJE MTU KUTUPA SISI MWILI WAKE ILI TUULE?

53 Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, MSIPOULA MWILI WAKE MWANA WA ADAMU NA KUINYWA DAMU YAKE, HANA UZIMA NDANI YENU. 

54 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.

55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.

56 AULAYE MWILI WANGU NA KUINYWA DAMU YANGU HUKAA NDANI YANGU”.

Umeona Umuhimu wa Yesu Kristo kwa wakati huu? Wana wa Israeli wasingeweza KUFIKA KAANANI pasipo kupitia njia ya jangwa Mungu aliyoikusudia wala pasipo kuila MANA chakula Mungu alichokichagua, Kadhalika na wakati huu wa sasa Hutuwezi kufika mbinguni pasipo kupitia njia ya jangwa wala pasipo kuila ile mana ya rohoni Mungu aliyoikusudia (yaani Yesu Kristo).

Njia zipo nyingi ndugu, lakini njia pekee ya kumfikia Mungu ni Yesu Kristo ndiye, na yeye alisema mwenyewe,..

Mathayo 16: 24 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.

25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona. 

26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake? “

Chukua gharama ya kutoka katika utumwa wa dhambi (Misri) na ingia gharama za kumfuata Bwana YESU katika njia ya jangwa kama unataka kufika mbinguni. Huko katika kaanani ya watakatifu, hawataingia waasherati, hawataingia walevi, hawataingia wasengenyaji, hawataingia wauaji, hawataingia wavaaji wa vimini wala wapakaji wanja wala watoaji mimba, hawataingia mashoga,wala watazamaji pornography, wala wasiosamehe, hawa wote sehemu yao itakuwa ni katika lile ziwa la moto biblia inasema hivyo. Wanaokuambia utaingia mbinguni kwa kufanya vitu hivyo wanakudanganya hawana haja na roho yako, wanataka vya kwako.

Hivyo geuka leo, ukatwae mkate wa uzima (Yesu Kristo). Mkate unaoshiriki kule kanisani, halafu bado ni muasherati, utapata hatia juu ya mwili wa Yesu Kristo na damu yake, kwasababu unashiriki isivyopasa.

1 Wakorintho 11: 23 “Kwa maana mimi nalipokea kwa Bwana niliyowapa nanyi, ya kuwa Bwana Yesu usiku ule aliotolewa alitwaa mkate,

24 naye akiisha kushukuru akaumega, akasema, Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.

25 Na vivi hivi baada ya kula akakitwaa kikombe, akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu; fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu.

26 Maana kila mwulapo mkate huu na kukinywea kikombe hiki, mwaitangaza mauti ya Bwana hata ajapo.

27 Basi kila aulaye mkate huo, au kukinywea kikombe hicho cha Bwana ISIVYOSTAHILI, ATAKUWA AMEJIPATIA HATI YA MWILI NA DAMU YA BWANA. 

28 Lakini mtu ajihoji mwenyewe, na hivyo aule mkate, na kukinywea kikombe.

29 Maana alaye na kunywa, hula na kunywa hukumu ya nafsi yake, kwa kutokuupambanua ule mwili.

30 Kwa sababu hiyo wako wengi kwenu walio hawawezi na dhaifu, na watu kadha wa kadha wamelala.

31 Lakini kama tungejipambanua nafsi zetu, tusingehukumiwa”.

Hivyo kula mana sasa, na hii hatuipati pengine mbali na pale wana wa Mungu wakusanyikapo.

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

CHAKULA CHA ROHONI.

TABIA ZA ROHONI.

NI HALALI KUBATIZA WATOTO WADOGO?

KUNA HUKUMU ZA AINA NGAPI?


Rudi Nyumbani

Print this post

VIGEZO VYA KUWA KARIBU NA YESU KRISTO KATIKA ULIMWENGU UJAO.

Wakati raisi wa Marekani Barack Obama alipokuja Tanzania mwaka 2013, japo wengi walifahamu kuwa ni ngumu kuketi meza moja naye au kumpa mkono lakini pamoja na hayo wengi waliona pia itakuwa ni bahati walau wakiuona msafara wake ukipita barabarani, Hilo tu lingewatosha watu kujiona kuwa ni wenye bahati sana kushuhudua tendo kama lile ambalo watu wachache sana wanaweza kuliona. Na mara nyingine unaweza ukafikiria wale watu wanaoongozana naye kila mahali ni watu ambao wamebahatika kuliko watu wote duniani. Kwasababu kiongozi ambaye ni mkubwa na anayeheshimika duniani kote mahali popote atakapokuwepo yupo nao. Kadhalika wewe nawe ungekuwa katika nafasi ile ungejiona kuwa ni mtu uliyebahatika sana (tunazungumza kwa namna ya kidunia).

Lakini biblia inatuambia YESU KRISTO, Ndiye Mfalme ambaye atakuja kuubatilisha ufalme wote wa hii dunia na kisha atauweka UFALME mpya wa milele usioasika, Biblia inasema yeye atakuwa ni MFALME WA WAFALME, na BWANA WA MABWANA. Ataitawala dunia yote kwa fimbo ya chuma, pale dunia wakati huo itakaporejeshwa katika hali yake ya mwanzo ya uzuri, basi chini yake kutakuwa na wafalme wengi na makuhani wengi, na mabwana wengi sana. Kumbuka wakati huo bahari haitakuwepo, kwani tunajua bahari imechukua asilimia 75% ya dunia, sasa bahari ikiondolewa unaweza ukaona kama ni mabara duniani yatakuwa mangapi?, kadhalika majangwa nayo hayatokuwepo, na wala hakutakuwa na sehemu yoyote ya dunia itakayokuwa ukiwa, sehemu zote zitakuwa zimejaa utukufu wa Mungu na wanadamu.

Kama biblia inavyosema Mfalme wetu YESU KRISTO atatawala na watakatifu wake kwa kipindi cha miaka 1000, kabla ya ule umilele kuanza. Unafahamu sasahivi Kristo ameketi katika kiti cha neema kama mkombozi lakini atakaporudi mara ya pili, sura yake itabadilika hatakuwa tena kama Yesu mwokozi bali YESU MFALME?. Na kama ni mfalme basi na tabia zile zote za kifalme ni lazima ziambatane naye. Na Ndio maana Mungu aliruhusu kwanza tupitie kuziona falme za ulimwengu huu, walau kwa sehemu tupate picha juu ya ule ufalme usiokuwa na mwisho utakavyokuja kuwa huko mbeleni.

Wengi wetu tunadhani, tukienda mbinguni basi watu wote watakuwa sawa kisha tutakuwa usiku na mchana tunamwimbia tu Mungu kama vile malaika. Lakini hiyo sio kweli, huko tunapokwenda biblia inatuambia kuna UFALME, na kuna MBINGU mpya na NCHI mpya. Ikiwa ni Ufalme basi kuna kutawala na kutawaliwa. Na kama vile watu wa ulimwengu huu wanavyoupigania ufalme mpaka waupate, kadhalika na ufalme wa mbinguni unapiganiwa, vinginevyo nguvu yako ikiwa ni ndogo kule hutatawala bali utatawaliwa (hapa tunawazungumzia waliookolewa, na sio watu wote, hao wenye dhambi wakati huo watakuwa katika ziwa la moto).. Na ndio maana Bwana YESU alisema.

Mathayo 11: 12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka”.

Unaona hapo?. Kuwa na uhakika wa kwenda mbinguni tu hautoshi, bali nafasi utakayokwenda kuwa nayo huko, na aina gani?

Na tena sasa baada ya wanafunzi wake kulisikia hilo, wakijua ya kuwa Kristo ndiye atakayekuwa mmilika wa ufalme wa Mungu, wawili kati ya wanafunzi wake walimwendea kwa siri na kumwomba wafanyiwe jambo kama tunavyosoma katika..

Marko 10: 35 “Na Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, wakamwendea, wakamwambia, Mwalimu, twataka utufanyie lo lote tutakalokuomba.

36 Akawaambia, Mwataka niwafanyie nini?

37 Wakamwambia, Utujalie sisi tuketi, mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika utukufu wako.

38 Yesu akawaambia, Hamjui mnaloliomba. Mwaweza kunywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi?

39 Wakamwambia, Twaweza. Yesu akawaambia, Kikombe ninyweacho mimi mtakinywea, na ubatizo nibatizwao mimi mtabatizwa;

40 lakini habari ya kuketi mkono wangu wa kuume au mkono wangu wa kushoto si langu kuwapa, ila wao watapewa waliowekewa tayari.

41 Hata wale kumi waliposikia wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana”.

Unaona hapo, mfano tu leo hii raisi wa hii nchi angekuwa na rafiki zake wawili ambao tangu zamani walijua kuwa atakuja kuwa raisi, ni wazi kuwa wangemwomba mmojawao awe makamu wake na mwingine waziri mkuu, lakini Raisi asingeweza kuwaambia neno “sawa” kirahisi rahisi tu, ni wazi kuwa yapo masharti yangepaswa wayafuate kutoka kwa raisi tangu kipindi kile kile ambacho kabla hajawa hata Raisi, pengine angewaambia, mkiwa na mimi katika kampeni zangu zote na kunipigia debe, ndipo nitawafanya wote kuwa hivyo, au wahakikishe siku zote wanamletea taarifa zote za maadui zake, kadhalika kwenye shida zote zitakazojitokeza wawe pamoja naye na zaidi ya yote wawe na angalau na ujuzi Fulani au maarifa Fulani kuhusiana na hayo mambo ya uongozi…Hivyo wakishinda hivyo vigezo, ule wakati ukifika basi atawafanya kuwa viongozi..

Kadhalika na kwa Bwana wetu Yesu Kristo, tunaona wanafunzi wake wawili walimfuata na kumwomba jambo gumu kama lile, kwamba katika ufalme wake awajalie mmoja aketi mkono wake wa kuume na mwingine wa kushoto, lakini yeye akawaambia je! KIKOMBE nikinyeacho mtakinywea?, kadhalika UBATIZO nibatizwao mtabatizwa??.

Hilo ni swali tunauliza hata sisi tunaotamani siku ile YESU KRISTO akiwa kama MFALME atatumbue kama watu wake wa karibu sana wenye heshima kubwa katikati ya wingi wa watakatifu na malaika watakaokuwepo siku zile atakapokuja kutawala dunia…JE! KIKOMBE nikinyeacho mtakinywea?, JE! UBATIZO nibatizwao mtabatizwa??.

Kwa maneno mepesi ni wazi kuwa kila mtu atatamka, Ndio nitaweza! Kama vile wale Yakobo na Yohana walivyotamka,,..Lakini Bwana kwa kuwa alikuwa anajua waliombalo akawaambia ni kweli mnaweza kufanya hivyo lakini yeye hawezi kutamka kuwa mtaketi naye isipokuwa wale Baba aliowaweka tayari..Kuna lugha nyepesi tunaweza kusema “wale ambao Mungu atawapa neema kunywea kukombe kama cha kwake, na kubatizwa ubatizo kama wa kwake hao ndio watakaoketi pamoja naye katika ufalme wake.”.

Swali Kikombe ni nini? Na Ubatizo ni upi?

Kikombe, kama wengi tunavyojua ni mateso kwa ajili ya ushuhuda ulionao, kama tunavyomwona Bwana wetu Yesu alivyopitia yale mateso Makali kama yale mpaka kufikia kufa, kwa kuliona lile kwa uchungu mwingi akatamani hata mateso yale yamwepuke, lakini Mungu alimpa nguvu ya kuyashinda…

Mathayo 26: 39 “Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe”.

Lakini UBATIZO ule unaozungumziwa pale haukuwa ubatizo wa maji tena hapana, kwani alikuwa ameshabatizwa wakati huo aliokuwa anazungumza hayo maneno.

Luka 12: 49 “Nimekuja kutupa moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi?

50 LAKINI NINA UBATIZO UNIPASAO KUBATIZIWA, nami nina dhiki kama nini hata utimizwe! “

Kama tunavyofahamu neno Kubatizwa ni kuzamwishwa/kuzikwa, tunapobatizwa ni ishara ya kuwa tunakufa na kufufuka na Kristo katika ubatizo wake. Na ndio maana tunasoma katika

Warumi 6: 3 “Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?

4 Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.”

Kwahiyo kama tunavyoona hapo ubatizo  Yesu Kristo aliokuwa anauzungumzia hapo ni kile kitendo cha KUFA, KUZIKWA, na KUFUFUKA. Huo ndio ubatizo aliokuwa anaungojea.

Lakini leo hii tunaona wengi tunapenda kumfuata Yesu lakini kuingia gharama hatutaki, Bwana Yesu alisema mtu hawezi kuwa mwanafunzi wangu kama asipoacha vitu vyote na kubeba msalaba wako na kunifuata, na pia kama yeye alivyoutoa uhai wake kwa ajili yetu, na sisi pia imetupasa kutoa uhai wetu kwa ajili ya Kristo , na pia maandiko yanasema hatujapewa kumwamini tu, bali hata kuteswa kwa ajili yake. Njia hiyo hiyo ya msalaba ya kudharauliwa ndiyo iliyowafanya Bwana wetu Yesu Kristo kuwa MFALME,

Waebrania 12: 2 “tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake ALIUSTAHIMILI MSALABA NA KUIDHARAU AIBU, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.

3 Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu”.

kadhalika pale itupasapo kupitia hayo, basi tujue kuwa Mungu ametuchagua kumkaribia yeye katika ufalme wake, ili siku ile na sisi tuwe na jina mbele zake. Kwanini mitume hawakuona ni kitu kuuliwa kwa ajili ya Kristo ni kwasababu walitamani kumkaribia Kristo katika ufalme wake.

Print this post

VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI

Yapo mengi ya muhimu mtu anapaswa kufahamu pindi tu anapozaliwa mara ya pili, vinginevyo shetani atatumia nafasi hiyo kumtesa na kumwangaisha mtu huyo kwa lengo tu la kumfanya auache wokovu mara: na moja ya mambo hayo, ni kumfanya mtu KULIHISI LILE DENI LA DHAMBI BADO LIPO NDANI YA MOYO WAKE.

Sasa mtu anapozaliwa mara ya pili [kumbuka, tunaposema kuzaliwa mara ya pili Neno linamaanisha mtu aliyekusudia kutubu kutoka moyoni mwake na kudhamiria kabisa kuacha dhambi zake, kisha akabatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa Jina la YESU KRISTO, kisha akapokea Roho Mtakatifu]. Mtu wa dizaini hiyo anakuwa kuanzia huo wakati amefanyika kiumbe kipya, na deni lote la dhambi liliokuwa juu yake, Mungu anakuwa ameshaliondoa, na anafanyika kuwa mtoto halali wa Mungu.

Lakini tatizo linakuja tu ni pale mara baada ya kuzaliwa mara ya pili vita vya kifikra vinaanza kuibuka ndani, shetani akishajua wewe umeshahesabiwa haki mbele za Mungu, na ile hatia ya dhambi zako haipo tena, kitu atakachofanya baada ya yeye kujua uchanga wako ataanza kuangalia sehemu zilizokuwa dhaifu katika maisha yako ulizokuwa unamwasia Mungu na kwa kupitia hizo atazigeuza kama mwiba wa kukushambulia wewe ujione kama haufai mbele za Mungu.

Jambo la muhimu la kufahamu kwa kila mtu, ni kwamba unapozaliwa mara ya pili hauwi kama robot, ambaye anaweza akaondolewa taarifa zake zote za kumbukumbuku na kuwekewa nyingine mpya (kuwa- formated), na kusahau vyote vya nyuma, pasipo kukumbuka hata kimoja. Hapana haiwi hivyo kwa mkristo pale anapozaliwa mara ya pili.

Mtu anapozaliwa mara ya pili kitu anachokifanya Roho Mtakatifu baada ya kumsamehe dhambi zake ni kuondoa ile kiu ya kutenda dhambi ndani ya mtu [anampa kila sababu ya kuona madhara ya dhambi], ndio hapo unakuta kama mtu alikuwa anakunywa pombe anaacha, alikuwa mvutaji sigara anaacha, alikuwa mwasherati hataki kufanya tena vile, alikuwa mwizi hofu ya Mungu inamwingia haibi tena, alikuwa mtukanaji ile kiu ya kutukana inakufa…

Lakini tatizo linalojitokeza ni pale anafanikiwa kweli kufanya hivyo lakini bado anaona kuna vitu havijaisha vizuri ndani yake..Kwamfano wapo watu wengi wanasema nimeacha uasherati lakini ndoto za uasherati zinanisumbua, mwingine anasema nimeacha uzinzi lakini na mawazo machafu yananisumbua, nashindwa kutawala mawazo yangu, kila ninapojaribu ninajikuta nimezama huko tena jambo ambalo linanikosesha raha, mwingine anasema nimeacha usengenyaji lakini kuna muda ninajikuta nimesengenya jambo ambalo baada ya hapo ninajisikia vibaya sana.

Mwingine anasema nimeacha kusikiliza miziki ya kidunia lakini zile nyimbo bado zinajirudia rudia kichwani mwangu, zinajiimba na sipendi zijirudie kwasababu nafahamu MUNGU hapendezwi nazo,,nifanyeje?. Mwingine atakwambia niliwahi kutoa mimba, nikatubu lakini ndani bado kuna kitu kinaniambia sijasamehewa jambo ambalo linanifanya nijihisi kama Mungu ananichukia,

mwingine anasikia wazo linamwambia amemkufuru Roho Mtakatifu hivyo dhambi yako hata atubuje hatasemehewa kwasababu alifanya dhambi Fulani zamani kwa makusudi.

Mwingine atakwambia baada ya kumpa Bwana maisha yangu na kuacha ushirikina, bado wachawi wananijia usiku, n.k. 

Kumbuka hawa wote ndani ya mioyo yao wanatumaini na wana dhamira safi ya kuwa wasafi na watakatifu lakini wanashindwa. Kwa Nje wanajitahidi kweli kuishinda dhambi lakini ndani ni vita vikali kweli vya kimawazo, n.k.

Sasa hawa wote kazi anayoifanya shetani ni kuzidi kuwakandamiza na kuwakandamiza kwasababu ya uchanga wao. Kwasababu hawajui kuwa tangu siku ile ya kwanza walipoamua kutubu na kufuata hatua zote za wokovu, Mungu alishawasamehe dhambi zao pasipo matendo yoyote. Mungu hakuangalia uelekevu wao, au utakatifu wao ndipo awasamehe, hapana aliwasamehe bure tu kwa neema yake. Hivyo walipofanyika kuwa wana wa Mungu tu, walihesabiwa kama watakatifu wa Mungu..

Lakini sasa jambo linaloendelea katikati yao ni kama vile gari lilokuwa katika mwendo kasi lililopigwa breki ghafla, haliwezi likasimama hapo hapo, hapana bali litaendelea na mwendo kidogo, japo kuwa matairi yatakuwa hayazunguki, vivyo hivyo hali yake mtu anayezaliwa mara ya pili,.Anakuwa ametoka kwenye dhambi fresh, ametoka kwenye dunia fresh, anatoka kwenye uasherati, anatoka kwenye matusi n.k.

Sasa Roho Mtakatifu anapopiga breki ghafla kwenye maisha yake ya dhambi, na kukata kiu yote ya dhambi ndani yake, kweli matairi yatasimama, ndio hapo yule mtu utakuta hataki kuendelea mbele na maisha ya dhambi tena, lakini kwasababu alikuwa kwenye mwendo kuna nguvu ya zamani iliyokuwa ndani yake iliyokuwa ikimsukuma kufanya zile dhambi haiwezi kusimama saa hiyo hiyo, itachukua muda kidogo ndio iondoke kabisa.. Na ndio maana Biblia inasema “kile apandacho mtu ndicho atakachovuna”, hapo ndipo utakapojua kuwa dhambi ina madhara makubwa, ina maumivu makali, inalipiza kisasi, na kuindoa itampasa mtu aingie gharama yake binafsi mbali na ile breki ya Roho Mtakatifu..

Ushahidi utakaokuonyesha kuwa wewe ni mtoto wa Mungu ni kwamba utaona unayachukia yale mambo ya kale lakini baadhi bado utayaona unayatenda pasipo wewe mwenyewe kupenda. Tofauti na hapo mwanzo ulipokuwa kwenye dunia, uliyatenda wala hakukuwa na kitu ndani kikikuhukumu, Na ndio maana Mtume Paulo aliandika..

Warumi 7: 14 “Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini, nimeuzwa chini ya dhambi.

15 MAANA SIJUI NIFANYALO, KWA SABABU LILE NILIPENDALO, SILITENDI, BALI LILE NILICHUKIALO NDILO NINALOLITENDA.

16 Lakini kama nikilitenda lile nisilolipenda, naikiri ile sheria ya kuwa ni njema.

17 Basi sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu

18 Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali kutenda lililo jema sipati.

19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo.

20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, SI MIMI NAFSI YANGU NILITENDAYE, BALI NI ILE DHAMBI IKAAYO NDANI YANGU.”

Unaona hapo? Ukiona hayo mambo yanakujia ujue kuna gharama ya kuziondoa hizo, hiyo ni kazi yako binafsi, na njia pekee ya kuviondoa ni kujitenga na kukaa mbali na vichocheo vya hizo dhambi, kwamfano, hapo mwanzo maisha yako yalikuwa ni ya uzinzi, ya kutazama pornography, na kufanya uasherati, na mustarbation zile picha na mawazo na kumbukumbu za yale matukio haziwezi kuisha mara, zitachukua muda kukutoka, unachotakiwa kufanya ni siku baada ya siku kuzidi kukaa mbali na mazingira yote yanayokupelekea wewe kuingia katika hayo mambo,

Kaa mbali na makundi yenye mazungumzo yasiyokuwa na maana muda wote yanazungumzia habari za uasherati, biblia inasema..

Waefeso 5: 3” Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu;

4 wala aibu wala maneno ya upuzi wala ubishi; hayo hayapendezi; bali afadhali kushukuru. ”

Kadhalika biblia inasema pia..1Wakorintho 15: 33”Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema”.

Sasa ukiendelea kudumu katika hali ya kuwa mbali navyo, kidogo kidogo vinaanza kuzikwa ndani yako na hatimaye kupotea kabisa, ile hali ya mawazo mabaya kukutumikisha inapotea, unakuwa na uwezo wa kutawala mawazo yako, zile ndoto ulizokuwa unaota kila siku unafanya uasherati hatimaye zinapotea kabisa.

Ulikuwa unasikiliza miziki ya kidunia, unachopaswa kufanya ili hayo mambo yazikwe kwenye akili yako, ni kufuta miziki yote kwenye simu yako au kompyuta yako, na wakati zile nyimbo zinapotaka kuanza kuja kichwani, weka nyimbo za injili za kumtukuza Mungu badala yake..jizoeshe kuzisikiliza hizo mpaka zenyewe zitakapochukua nafasi ya zile nyimbo za kidunia.

Kadhalika ulikuwa na tabia za kwenda kwa waganga wa kienyeji, na baada ya kumpa Kristo maisha yako bado zile nguvu za giza zinakujia jia, endelea kudumu katika maombi, na kujifunza Neno la Mungu, visikuogopeshe wewe tayari ni mwana wa Mungu haviwezi kukudhuru, ni vitisho tu vya shetani, kwa jinsi unavyoendelea kukaa katika kujifunza Neno la Mungu na kukusanyika na watakatifu wengine vile vitu vinaondoka vyenyewe kidogo kidogo mpaka kufikia kutoweka kabisa, hutakaa uone mambo hayo yote tena..

Unajikuta umeingia katika usengenyaji, na hali hupendi kufanya hivyo, unachopaswa kufanya ni kukaa mbali na mazingira yote yatakayokupelekea kumzungumzia mtu mwingine vibaya, vikao vya kwenye masaluni, marafiki wasio kujenga, vijiwe n.k. unakata, sasa ukiendelea kujizoesha hivyo ile hali ya kusengenya inaondoka yenyewe ndani yako, baada ya kipindi fulani hata ukija kukaa katikati ya hao watu, utajikuta huwezi kusengenya kwasababu hiyo tabia imeshakufa tayari ndani yako..

Na mambo mengi yote, unayoshindwa kufanya kwa nguvu zako, usianze kuwaza kushindana nayo, hutaweza kwa siku moja ,huo ni ukumbi wa shetani,utajikuta unatazama matendo kuhesabiwa haki mbele za Mungu, badala ya kusonga mbele katika Imani. wewe kimbilia chanzo cha hayo mambo kisha kaa nayo mbali, kwa muda Fulani utaona matokeo mazuri, hutajisikia kuhukumiwa, wala kujilaumu, mawazo yako yatakuwa safi, ndoto zako zitakuwa sio za uchafu kila wakati, n.k..

Kadhalika shetani anapokuletea mawazo ya kukuhukumu kwa madhaifu yako, unayakataa. Ukijua kuwa Mungu ndiye aliyekuchagua wewe, na sio wewe uliyemchagua Mungu. Na hatuhesabiwi haki kwa matendo bali kwa neema yake.

Pia ni jukumu la kila mtakatifu kujitakasa kila siku kama maandiko yanavyosema. (Ufunuo 22:10 )Na tutajitakasa tu pale tutakapozidi kukaa mbali na mambo yote yanayochochea uovu ndani yetu.

Lakini kumbuka mambo haya yote mtu hawezi kuyashinda kama hajazaliwa mara ya pili. Na kuzaliwa mara ya pili ni kwa njia ya kutubu, na kubatizwa katika ubatizo sahihi, na kupokea Roho mtakatifu. Hivyo kama haujafanya hivyo ni vema uchukue uamuzi sasa kwasababu majira haya sio ya kukawia tena..Bwana yu karibu kurudi.

Tafadhali “share/print” ujumbe huu na kwa wengine. Mungu atakubariki.

Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Print this post

MAWE YALIYOKWISHA KUCHONGWA MACHIMBONI.

Hekalu la kwanza kama tunavyofahamu lilitengenezwa na Mfalme Sulemani, Ni hekalu lililochukua kipindi cha miaka 7 mpaka kukamilika, na kitu cha kipekee tunachoweza kujifunza katika ujenzi wa lile hekalu ni jinsi uundwaji wake ulivyokuwa. Maandiko yanatuambia katika kipindi chote cha ujenzi, hakukusikika mlio wa nyundo, wala shoka au mlio wa nyenzo yoyote ya ujenzi. Tunasoma;

1Wafalme 6: 7 “Na nyumba ilipokuwa ikijengwa, IKAJENGWA KWA MAWE YALIOKWISHA KUCHONGWA CHIMBONI; WALA NYUNDO, WALA SHOKA, WALA CHOMBO CHA CHUMA CHOCHOTE, SAUTI YAKE HAIKUSIKIWA ILIPOKUWA IKIJENGWA NYUMBA”.

Unaweza ukajenga picha ni JENGO la aina gani hilo linajengwa pasipo kusikika kelele ya aina yoyote ile?, ni wazi kuwa litakuwa limejengwa kwa utashi wa hali ya juu sana ambao kwa namna ya kawaida haujazoleka katika ujenzi tulionao..

Ghafla tu wananchi waliokuwa wanakaa Yerusalemu wakati ule walishangaa JENGO hili hapa limeshakamilika, wakati wanadhani kwamba jengo ndio linaanza kujengwa, kumbe hawajui kuwa ndio linakaribia kumalizika..kwasababu wakati wa ujenzi wake wenyewe walitegemea wasikie milio ya nyundo, na mashine, na mashoka, na misumeno, na sauti za kelele nyingi za wafanyakazi, ili wajue kuwa ujenzi ndio unaanza lakini mambo hayakuwa hivyo. Kwa nje! Ilionekana kama ni kazi iliyolala tu, 

Lakini biblia imetupa siri ni kwanini haikusikika kelele wakati wa ujenzi wake, tunasoma hapo juu ni kwasababu “mawe ya ujenzi yalikuwa yanachongewa mbali sana huko machimboni na kukamilika huko huko kisha kuletwa eneo la ujenzi, tayari kwa kuchomekwa tu! kimya kimya.”..Muda wa mamiezi mengi ulipotea huko machimboni kuchonga miamba, lakini baada ya kukamilika kipindi cha ujenzi kilichukua muda mfupi sana.

JAMBO HILO LINAFUNUA NINI KWA WAKATI WA SASA?.

Kama biblia inavyosema Kanisa la Kristo ni Hekalu la Mungu,(1Wakorintho 3:16). Na kama vile Sulemani alivyokuwa analijenga Hekalu lile, vivyo vivyo YESU KRISTO naye analijenga HEKALU lake, ambalo ndilo kanisa takatifu (bibi-arusi safi).

Na kama vile lile la Sulemani lilikamilika ndani ya miaka 7, kadhalika na hili la Kristo nalo linakamilika katika nyakati 7 za kanisa (Ufunuo 2&3). Na kama vile watumishi wa Sulemani walivyokuwa machimboni duniani kote kutafuta na kushughulika na uchongaji wa yale mawe vivyo hivyo na Bwana Yesu Kristo leo amewatuma watumishi wake waaminifu duniani kote kuwatengeneza watu wake wateule kwa ujenzi wa mwisho kanisa lake tukufu litakalokwenda kukamilika hivi kwaribuni kwa tukio la unyakuo…[hao ndio yale mawe yachongwayo machimboni]

Na kama vile mwishoni mwa mwaka wa 7 jengo la Sulemani lilikamilika na utukufu wa Mungu kushuka mwingi juu yake siku ile. kadhalika na hili kanisa la mwisho la 7 la Laodikia tunaloishi mimi na wewe, ndio tutakalolikamilisha HEKALU la Mungu kisha kumalizia na unyakuo siku ile, jiwe la mwisho litakapoletwa eneo la ujenzi (yaani kondoo wa mwisho atakapoingia katika neema ya msalaba).

Hii inatuonyesha wazi kuwa hatua za UNYAKUO hazitajulikana na watu wengi [yatakuwa ni mambo ya siri]…Wakati watu wanadhani kwamba kanisa la Mungu bado sana linyakuliwe, hawajui kuwa ndio lipo katika hatua za mwisho mwisho, wakati wanasubiri waone na wasikie milio ya matarumbeta na maonyesho, na kushuka moto, hawahafamu kuwa mawe yalishakamilika kuchongwa tangu mwambani.

Ndugu Leo hii Mungu anawaanda watu wake Ki-binafsi, (yaani mmoja mmoja)..na sio kimkusanyiko au kidhehebu, Mungu hawaandai watu kama shirika au jumuiya au kusanyiko hapana, Mungu anamwandaa mtu wake ki-binafsi.

Unaweza ukadhani sasa hakuna watu wa Mungu duniani, kwasababu haulioni kanisa lililosimama lenyewe kikamilifu mbele za Mungu, lakini jua tu kanisa halisi la rohoni la Kristo linazidi kuimarika siku baada ya siku. Na moja ya hizi siku litakamilika, hapo ndipo watapokusanywa wote kwa pamoja kama mtu mmoja na kukutanika mawinguni kwenda mbinguni kwenye karamu ya mwana-kondoo.

Mambo ya ulimwengu huu yanatufundisha, kwenye dunia tunayoishi sasahivi ya teknolojia na utandawazi, watu mfano wakitaka kukutanika kufanya vikao, wengi wao hawatumii zile njia za kale tena. Yaani zile njia za kuitana kwa matangazo na kutangaza kila mahali, na kwenda kukodi makumbi ya mikutano, na vipaza sauti n.k. kiasi kwamba hata wale ambao kikao hicho hakiwahusu wanapata taarifa, siku hizi sio hivyo tena majira yamebadilika, watu wanatumia mitandao kufanya vikao vyao.

Mtu mmoja anaweza akawa yupo nyumbani kwake, mwengine yupo nchi nyingine, mwingine yupo ofisini, mwingine yupo chuoni n.k. lakini wote wakitaka kukutanika kufanya kikao wanakutanika mitandaoni na kumaliza mambo yote, na kutimiza malengo yale yale kama tu vile wangekutanika kimwili. Cha msingi tu kila mmoja awe na kifaa husika kitakachoweza kuwakutanisha wote pamoja, na kifaa hicho kinaweza kikawa ni simu, au kompyuta. N.k.

Vivyo hivyo na katika ukristo sasahivi, Ufalme wa mbinguni unayo hekima kuliko ufalme wa duniani. Kristo naye anakusanya wateule wake duniani kote, kwa njia ya utulivu na hekima nyingi, isiyojulikana na wengi..Ni wale tu watakaokuwa na chombo maalumu kitakachoweza kuwaunganisha wote pamoja na Mungu wao kama vile simu ndio watakaoelewa kinachoendelea katika ratiba ya ukombozi ya Mungu.

Na chombo hicho si kingine Zaidi ya BIBLIA (NENO LA MUNGU), na kama vile simu isiyokuwa na network au chaji inakuwa ni sawa na kazi bure, kadhalika Neno la Mungu lisilovuviwa na ROHO MTAKATIFU ndani ya mtu linakuwa ni kazi bure. Ndivyo maandiko yanavyosema.

2Wakoritho 3:6 “….. kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha.”

Na ndio maana ni muhimu kuwa na ROHO MTAKATIFU katika kizazi hichi tunachoishi, hiyo ndiyo tiketi pekee ya kuunganishwa katika mtandao wa watakatifu..Hata siku ile watakapoitwa juu mbinguni uwe pia ni mmojawapo wa watakaoisikia sauti ya Mwana wa Adamu. Vinginevyo, unyakuo utakuwa kwako kama ni kitu cha kushtukiza tu.

1Wathesalonike 5: 1 “Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.

4 Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.

5 Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.

6 Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.

7 Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku.

8 Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.

9 Kwa kuwa Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo; 

Na JE! NA WEWE NI JIWE LINALOCHONGWA CHIMBONI SASA??…Au unasubiria wakati Fulani ufike ukagongelewe kwenye jengo?…Jenga maisha yako kwa Kristo sasa, utubu dhambi zako, ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji tele na uwe ni kwa jina la YESU KRISTO ndipo upokee kipawa cha ROHO MTAKATIFU. Ambaye yeye atakuwa kama network na chaji ya simu zetu..

MAANA SIKU ILE KANISA LITAKAPONYANYULIWA JUU, HAKUTASIKIKA KELELE WALA TAHARUKI YOYOTE DUNIANI..ITAKUWA NI TENDO LA GHAFLA TU!..ee!! fulani hayupo!!, mbona sikuwahi kumwona kama alikuwa ni mtu wa dini sana? Ee!! Mbona tulitazamia tuone kwanza jambo fulani likitokea duniani? Hawajui kuwa mawe yalikuwa yanachongewa machimboni.

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Print this post