Title March 2023

Pande zote twadhikika, bali hatusongwi;(2Wakorintho 4:8)

Unaweza kushushwa chini, lakini simama usivunjike moyo.

2Wakorintho 4:8  “Pande zote twadhikika, bali hatusongwi; twaona shaka, bali hatukati tamaa; 9  twaudhiwa, bali hatuachwi; twatupwa chini, bali hatuangamizwi”

Kwa kuwa bado tupo duniani, dhiki, mateso, manyanyaso hayaepukiki katika baadhi ya vipindi, Kiongozi wetu Yesu alituweka wazi, kwamba “duniani mnayo dhiki, lakini jipeni moyo mimi nimeushinda ulimwengu”(Yohana 16:33)

Utaudhiwa na mume/mke/baba/mtoto, kwasababu ya imani, utapigwa bila sababu, utatishiwa kufukuzwa kazi, utakuwa na mashaka pande zote, mwingine hujui kesho utaamkaje, ule nini, magonjwa hayana mwisho..Lakini katika yote, bado neema ya Mungu itatushika na kutusaidia, hatutasongwa kiasi hicho mpaka kuicha imani, hatutakata tamaa, hata turudi nyuma, Bwana atakuwa upande wetu.

Mambo hayo ni ya kitambo tu, hata kama tutauawa, bado tunao uzima wa milele, hata kama tutapoteza kila kitu bado mwenye vitu vyote yupo ndani yetu. Tutadhikika pande zote, tutasongwa kila mahali lakini hatutakata tamaa. Tukumbuke tu,  Kila pito linasababu yake, lakini katika yote, tujue Bwana anatuwazia mawazo mema, tukishakwisha kukamilishwa tutatoka kama dhahabu.

Yakobo 1:2  “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; 3  mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi. 4  Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno”.

Bado maandiko yanasema..

1Petro 1:6  “Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;

7  ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo”.

Bwana awe nawe.

Maombi yangu:

“Baba mwema, nakushukuru kwa neema ya wokovu uliyonipa, Najua kama sio wewe nisingefika hata hapa nilipo, nakuomba Mungu wangu unione katika dhiki zangu, uyaone machozi yangu, uniondoe katika mateso yangu. Lakini zaidi unipe nguvu ya kuweza kukabiliana na dhiki zote za ulimwenguni, nisirudi nyuma wala kukata tamaa. Nikutumikie wewe katika mazingira yote. Upendo wako usipunguke ndani yangu. Ninaomba nikiamini katika jina la Yesu Kristo. Amen”.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

UYATIE MACHOZI YANGU KATIKA CHUPA YAKO EE! BWANA.

Furaha ni nini?

Unyenyekevu ni nini?

JE! UTATOA HESABU YA NINI KATIKA SIKU ILE?

Nini maana ya kumpenda Bwana kwa moyo,roho, akili na nguvu zetu zote?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.

Swali: Kwanini Mungu aliwapeleka wana wa Israeli Misri kwa miaka 400, Ni kosa gani kubwa walilolifanya mpaka Mungu kuwauza kwa Farao miaka yote hiyo?

Jibu: Hakuna kosa lolote walilolifanya mpaka kufikia hatua hiyo ya kupelekwa Misri katika nyumba ya utumwa. Bali Mungu aliruhusu iwe hivyo, kwa makusudi maalumu. Ni kama tu Yusufu alivyoenda kuuzwa kwa Misri kwa Potifa, maandiko hayaonyeshi kuwa Yusufu alifanya kosa lolote lililompelekea kwenda kuuzwa kama mtumwa kwa Potifa, lakini maandiko yanaonyesha kuwa Mungu alimpeleka Misri kwa lengo la kuwaokoa watu wengi siku za mbeleni, tunalisoma hilo katika Mwanzo 45:4-8

Mwanzo 45:4 “Yusufu akawaambia ndugu zake, Karibuni kwangu; basi, wakakaribia. Akasema, Mimi ni Yusufu, ndugu yenu, ambaye mliniuza kwenda Misri. 

5 Basi sasa, msihuzunike, wala msiudhike nafsi zenu, kwa kuniuza huku; MAANA MUNGU ALINIPELEKA MBELE YENU KUHIFADHI MAISHA YA WATU.

 6 MAANA MIAKA HII MIWILI NJAA IMEKUWA KATIKA NCHI, NA IKO TENA MIAKA MITANO ISIYO NA KULIMA WALA KUVUNA. 

7 MUNGU ALINIPELEKA MBELE YENU KUWAHIFADHIA MASAZO KATIKA NCHI, NA KUWAOKOA NINYI KWA WOKOVU MKUU

8 Basi si ninyi mlionipeleka huku, ila Mungu; naye ameniweka kama baba kwa Farao, na bwana katika nyumba yake yote, na mtawala katika nchi yote ya Misri”.

Hali kadhalika Mungu aliwapeleka wana wa Israeli Misri na kuwafanya kuwa watumwa, kwa malengo makuu mawili.. ambayo yanafanana na yale ya Yusufu.

1.MUNGU KUTANGAZA UKUU WAKE.

Kupitia wokovu wa Israeli kutoka Misri kwa mapigo yale 10 aliyompiga nayo Farao, na kwa kupitia ishara za ajabu alizozofanya jangwani kama kushusha Mana, kuleta Kware, kudhihirisha Nguzo ya Wingu na Moto n.k, ulimwengu umeweza kumjua Mungu wa Ibrahimu kuwa ni Mungu mkuu na wa haki na mwenye nguvu nyingi na maajabu mengi.

Kwahiyo ijapokuwa Israeli waliteswa Misri lakini maisha yao baadaye yalikuja kuwa mahubiri makubwa sana kwa ulimwengu kumjua Mungu wa kweli, pengine wasingepitia hiyo njia ya mateso tusingemjua Mungu kwa kiwango hicho.

2. KUTANGAZA NJIA YA WOKOVU

Lengo la pili la wana wa Israeli kupitia yale maisha ni kutangaza njia ya Wokovu. Maisha yao kuanzia Misri mpaka Kaanani, ni ufunuo kamili wa maisha ya Wokovu kutoka Dhambini(Misri), kueleka mbinguni (Kaanani) mji wa raha.

Tunapomwamini Bwana Yesu na kutubu dhambi zetu, katika roho ni kama tumetoka Misri..na hivyo Kristo anatuweka huru mbali na vifungo vyote vya dhambi, kwasababu maandiko yanasema “atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi (Yohana 8:34)”.

Hii inatufundisha nini?.. Si kila mateso tunayoyapitia yanatokana na makosa tuliyoyafanya?.. Yusufu hakuna kosa alilolifanya mpaka kufikia kuuzwa Misri kwa Potifa na hata kufungwa gerezani, vile vile wana wa Israeli hakuna kosa walilolifanya mpaka kufikia kuwa watumwa kwa muda ule, bali Mungu aliruhusu hayo yatokee ili mwisho wake aonyeshe utukufu wake!..

Kwahiyo hatutakiwi kukata tamaa tunapopitia shida, maadamu tuna uhakika tupo sawa na Mungu (yaani tunaishi maisha yanayompendeza yeye), vile vile tunapopitia magonjwa ya muda mrefu hatupaswi kukata tamaa wala kulaumu, bali tunapaswa kushukuru na kuendelea kuomba na kuishi maisha yanayompendeza, kwasababu Mungu anataka kufanya maisha yetu kuwa ushuhuda..

Hata Kristo maisha yake yalikuwa ni ya ushuhuda, alikuwa kama namna ya mtumwa (Wafilipi 2:7-8), lakini alijua mwisho wake utakavyokuja kuwa, na sisi hatuna budi kuwa watu wa namna hiyo hiyo, kwasababu mwisho wetu utakuwa mzuri hata kama mwanzo wetu umekuwa mbaya na wa kukatisha tamaa, maadamu tupo katika Neno lake na amri zake, basi hatuna haja ya kuwa na hofu, ni suala la muda tu.

Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWA MIOYO YAO WAKAREJEA MISRI.

MAJARIBU 10 WANA WA ISRAELI WALIYOMJARIBU MUNGU.

JIHADHARI NA MKUTANO WA WATU WALIOCHANGANYIKANA.

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Nini tofauti ya Mtumwa, Mjakazi na kijakazi?

Rudi nyumbani

Print this post

UNAFAHAMU KUWA YESU HUWA ANAJITENGA NA BAADHI YA WATU?

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, utukufu na heshima vina yeye milele na milele amina.

Zipo tabia kadhaa za Yesu ambazo watu wengi huwa hatuzitambui. Kwamfano utakumbuka wakati ule, anakwenda Yerusalemu kwenye sikukuu, biblia inasema alipita mahali penye birika Fulani iliyojulikana kama Bethzatha, Birika hii kuna kipindi ilitoa uponyaji, hivyo, watu wengi maelfu kwa maelfu walikuwa wakikusanyika, kungojea bahati zao, ambayo ilitokea kwa nadra sana pengine mara moja kwa mwaka.

Lakini hapa tunamwona Bwana Yesu, akiingia katikati ya mkusanyiko huo, na kumponya Yule mtu aliyekuwa amepooza, Cha kushangaza ni kwamba Yesu hakuendelea kubaki mule mule kuwaponya watu wengine kama ilivyo desturi yake, bali aliondoka mara moja, kwa haraka ambayo hata aliyeponywa hakuweza kumkariri.

Hata baadaye makuhani walipomuuliza, ni nani kakupa amri hiyo ya kujitwika godoro lako uende, Yule aliyepooza hakuweza kumtambua,.

Lakini ni nini kilichompelekea Yesu aondoke pale?

Tusome kidogo;

Yohana 5:12  “Basi wakamwuliza, Yule aliyekuambia, Jitwike, uende, ni nani?

13  Lakini yule mtu aliyeponywa hakumjua ni nani; MAANA YESU ALIKUWA AMEJITENGA, KWA SABABU PALIKUWA NA WATU WENGI MAHALI PALE.

14  Baada ya hayo Yesu akamkuta ndani ya HEKALU, akamwambia, Angalia, umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi.

15  Yule mtu akaenda zake, akawapasha habari Wayahudi ya kwamba ni Yesu aliyemfanya kuwa mzima.

Sababu ya kujitenga maandiko yanasema ni kwamba palikuwa na watu wengi.. Watu wengi ambao wanatafuta miujiza na uponyaji wa miili yao, na sio roho zao. Na ndio maana Yesu hakuweza kustahimili kuendelea kuwepo pale muda mrefu, akaondoa mara..

Mpaka Yule mtu alipopata akili, akaona pale sio sehemu yake, akaenda zake HEKALUNI kutulia uweponi mwa Bwana, kukaa kusali na kujifunza sheria za Mungu, Ndipo Yesu akajidhihirisha kwake alipokuwa kule hekaluni,..akamwambia “usitende dhambi tena!”, “usitende dhambi tena!”, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi”. Akampa siri ya matatizo yake, na suluhisho la kudumu.

Lakini kama mtu Yule asingekwenda hekaluni, badala yake akaendelea kumtafuta  Yesu kila siku pale birikani, kamwe asingekaa amwone, na ugonjwa wake ungemrudia muda si mrefu, kwasababu, angeenda kurudia dhambi yake ile ile aliyoitenda.

Ni nini Bwana anataka tufahamu.

Hii ni picha kamili ya kinachoendelea sasa katika ulimwengu wa wakristo. Kinachowakimbiza kwa Mungu ni ishara na miujiza, na uponyaji, Hivyo wanayaacha makanisa yanayowafundisha Njia za wokovu, na kujitenga na dhambi, wanakimbilia kwenye vituo vya maombi na maombezi, huko ndipo walipojazana, wakisikia kuna mafuta ya upako, wanamiminika mpaka wanakanyagana, Lakini ukweli ni kwamba sio wote wanaopokea uponyaji, bali ni wachache sana..na tena hao wachache ni Yesu ndiye anayewafuata huko kwa huruma zake, na kuwadhihirishia uponyaji wake.. Lakini huko hayupo..Utasubiri sana, na kulia sana, na kungoja sana.

Huwezi kuliacha Hekalu lake, ukakimbilia mikusanyiko ya miujiza na uponyaji, ambayo hukemewi dhambi, hufundishwi kusali, hufundishwi habari za kwenda mbinguni, hufundishwi utakatifu, ukadhani utamwona Yesu..Ataendelea tu kujitenga nawe kwasababu yeye hakai katika mikusanyiko ya watu wa namna hiyo.

Wanaoponywa wanakuwa wanarudiwa matatizo yaleyale, baada ya muda, kwasababu hawafundishwi chanzo cha matatizo yao, kwamba ni dhambi, Bali wanamgeuza Mungu mganga wa kienyeji, anayetoa tu dawa, hajali kujua machafu yako.

Embu leo tubu na ugeuke, ondoka huko, Usikae mahali ambapo Yesu hayupo, hata kama kuna utiriri wa watu, Yesu hapokei umati wa watu,kama tulivyoona hapo anapokea watu waliotayari kumwabudu katika roho na kweli haijalishi watakuwa wawili au watatu.

Epuka upepo wa watu, asilimia kubwa Yesu hayupo huko.

Tubu dhambi zako, maanisha kwa moyo wako wote, kumfuata Yesu. Kumbuka hizi ni siku za mwisho,  majira yale ya  makristo na manabii wa uongo ndio haya Yesu aliyoyatabiri, Kaa katika Kristo Yesu, hakikisha umejitwika msalaba wako na kumfuata Yeye. Parapanda inakaribia kulia, Hukumu ipo karibu, umejiwekaje na Kristo wako?.

Bwana akubariki

Amen.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

KUNA WAKATI YESU ATAPITA NA WATU HAWATAJUA.

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.

USIJARIBU KUMGEUZA MUNGU MGANGA WA KIENYEJI,UTAKUFA.

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)

Usimwache mwanamke mchawi kuishi! Biblia ilimaanisha nini?

Afadhali mtu akutwe na dubu aliyenyang’anywa watoto wake.

Rudi nyumbani

Print this post

WANNE WALIO WAONGO.

Biblia imetuonya imetutahadharisha vitu vitatu vilivyo na udanganyifu kuliko vitu vyote.

1.MOYO

Moyo wa mtu ndio kitu kilicho kidanganyifu kuliko vyote..

Yeremia 17:9 “Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?”

Hakukuwa na shetani mwingine mbinguni aliyemdanganya shetani, bali kilichomdanganya shetani ni moyo wake mwenyewe… Moyo wake ulimtuma kuamini kuwa anaweza kuwa kama Mungu. Na hivyo akaufuata moyo wake na mwisho akaangukia upotevuni.

Na mioyo yetu sisi wanadamu ni midanganyifu sana, na mara nyingi inatuongoza pabaya…Mithali 16:2 “Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe…” Na maandiko yanatufundisha kulinda mioyo yetu kuliko vyote tulindavyo, kwasababu huko ndiko zinakotoka chemchemi za uzima (Mithali 4:23).

Na tunailinda kwa kuangalia yale tunayoyasikia au tunayojifunza, na biblia ndio kitabu pekee cha kutusaidia kupima mambo yote.

2. DHAMBI.

Dhambi ni adui wa pili wa kumwongopa kuliko “shetani”. Na dhambi siku zote inadanganya, (inavutia kwa nje lakini mwisho wake ni Mauti, Warumi 6:23). Ulevi unaonekana kama unavutia lakini mwisho wake ni Mauti, Anasa zinaonekana kama zinavutia, lakini mwisho wake ni Mauti, Vivyo hivyo na Zinaa, na usengenyaji, na wizi, na rushwa n.k Vyote hivyo vinavutia kwa nje lakini ndani yake ni Mauti.

Waebrania 3:13 “Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa UDANGANYIFU WA DHAMBI”.

3. SHETANI.

Maandiko yanasema wazi kuwa shetani ni baba wa Uongo.

Shetani atakuambia kuabudu sanamu si dhambi, kunywa pombe si dhambi, kuupenda ulimwengu si dhambi, kujiburudisha kwa anasa si dhambi n.k  Na kumbe anasema Uongo, kwasababu yeye ni baba wa huo, ndivyo alivyomdanganya Hawa na ndivyo anavyoendelea kudanganya watu mpaka leo.

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo”

4. MALI

Maandiko pia yanasema kuwa Mali zinadanganya!.. Mali zinasema ukizipata utaheshimika, ukizipata utapendwa, ukizipata utaishi vizuri.. jambo ambalo si kweli, Kristo pekee ndiye ukimpata mambo yote, yatakuwa sawa hata pasipo hizo mali… Kama alisema “mtu hataishi kwa mkate tu, bali Neno la Mungu”…si zaidi Mali???.

Lakini Mali zenyewe zinatuhubiria kinyume chake kuwa pasipo hizo, maisha yetu hayawezi kwenda au yatakuwa ya shida, maisha yetu yatakuwa ya tabu na mateso…

kwahiyo kama hatutaongeza umakini katika kumjua Mungu na uweza wake tutadanganyika na udanganyifu huo ambao Mali zinauhubiri.. tutajikuta tunatumia muda mwingi kuzisaka na kutumia muda mchache kumtafuta Mungu.. na hivyo kupotea..

Mathayo 13:22  “Naye aliyepandwa penye miiba, huyo ndiye alisikiaye lile neno; na shughuli za dunia, na UDANGANYIFU WA MALI hulisonga lile neno; likawa halizai”.

Mali zisikudanganye na kukupotezea muda wako mwingi, Mali zisikuambie kuwa usipoenda kuzisaka siku ya jumapili utakufa njaa!!, mali zisikudanganye kuwa usipotumia usipotumia muda mwingi kuzisaka basi zitakukimbia!!..  Jihadhari na udanganyifu huo.

Bwana atubariki na kutusaidia.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

Kwanini Paulo aungane na wale watu wanne wenye nadhiri?

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

KWA WALE WALIO NJE “YOTE” HUFANYWA KWA MIFANO.

Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).

Rudi nyumbani

Print this post