Mambo ya Walawi 11:9-12
[9]Katika hao wote walio ndani ya maji mtakula hawa; kila aliye na mapezi na magamba, ndani ya hayo maji, na ndani ya bahari, na ndani ya mito, mtakula hao.
[10]Na hao wote wasio na mapezi na magamba, ndani ya bahari, na ndani ya mito, katika hao waendao majini, na katika wote wenye uhai, waliomo majini, hao ni machukizo kwenu,
[11]watakuwa machukizo kwenu; msiile nyama yao, na mizoga yao itakuwa machukizo kwenu.
[12]Kila asiye na mapezi wala magamba aliye ndani ya maji ni machukizo kwenu.
Mapezi ya samaki, ni vile vitu kama mbawa ngumu zenye mfano wa miiba zinazokaa Kwa juu, au pembeni au nyuma mwa mwili wa samaki.Ukitazama samaki kama perege, sato au sangara utaona mapezi Yao.Na faida za mapezi hayo ni kuwa yanasaidia kuogelea, kuelea vema kwenye maji, kukunja Kona, kuongeza kasi na kusimama au kugeuka Kwa haraka.
Halikadhalika samaki waliokuwa na magamba ndio tu walioruhusiwa kuliwa. Na magamba yaliwasaidia kujilinda na maadui au wadudu wavamiaji kwenye mwili. Kwani ngozi ya samaki ni laini hivyo isipofunikwa na magamba magumu kama yale, meno makali ya maadui yanapopita ni rahisi kujeruhiwa, Yanakaa kama dirii kifuani mwa askari.
Lakini si samaki wote walikuwa na haya mapezi na magamba, Bali wengine hawakuwa nayo mfano wa Hawa ni kama kambale, papa, pomboo, pwezi.
Kama tunavyofahamu agano la kale ni kivuli Cha agano jipya, sio kwamba viumbe hivyo vikiliwa vitamkosesha mtu mbingu, au vitamnajisi roho , hapana. Bali vilifanywa vile kwa makusudi ili kutupitishia sisi ujumbe wa Rohoni katika agano letu jipya. Kwamba na sisi kama tutafanana na mojawapo wa viumbe hivyo Rohoni basi tunakuwa najisi mbele za Mungu.
Samaki mwenye magamba ni mwenye ulinzi wa kutosha dhidi ya mashambulizi ya maadui. Na sisi tunapokosa ulinzi wa Rohoni mfano wa yule askari anayezungumziwa katika Waefeso 6, mwenye dirii ya haki kifuani, ngao ya Imani mkononi na chepeo ya wokovu kichwani. Tunakuwa ni wadhaifu, kiasi Cha kutoweza simama mbele ya adui yetu shetani. Hivyo ni kuhakikisha kuwa umesimama imara katika wokovu wako, lakini pia utambue haki uliyopewa katika msalaba wa Yesu Kristo na Imani Yako timilifu ndani ya wokovu wako. Hapo utakuwa umejidhatiti vya kutosha mfano wa samaki mwenye gamba gumu, au mamba aliyefunikiwa na ngozi yenye gamba.
Ayubu 41:13 “Ni nani awezaye kumbambua magamba yake? Ni nani atakayepenya dirii yake maradufu? 14 Ni nani awezaye kuifungua milango ya uso wake? Meno yake yatisha kandokando yake. 15 Magamba yake yenye nguvu ndiyo fahari yake, Yamefungamana pamoja kama kwa kufungwa kwa muhuri. 16 Jinsi yalivyoshikamana Hata upepo hauwezi kupita kati. 17 Yamefungamana pamoja; Yameshikamana, hata hayawezekani kutengwa”
Vilevile samaki aliyekuwa na mapezi alikuwa ni mwepesi kukatiza katika maji. Ni sawa na mabawa Kwa ndege, au miguu na kwa mtu. Hivyo na sisi katika ulimwengu huu wa dhambi ili tusionekane kuwa najisi tuvae mapezi yetu ambayo maandiko yanasema .Ndio ule utayari wa kuihubiri injili.
Waefeso 6:15
[15]na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;
Tusienende Kama watu wasio na kusudi maalumu la kufanya duniani, tuvae utayari, ndio mapezi yetu tutembee ulimwengu kote kiuhubiri/ kushuhudia habari njema.Kwasababu tukikosa haya, siku ile ya mwisho, tutatengwa samaki wema na waovu..Kisha wale waovu watatupwa nje.
Mathayo 13:47 ‘Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna;
48 hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa. 49 Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki’
Tusiwe samaki najisi.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Injili iliyopo kwa Samaki aina ya Eeli.
Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)
Mjombakaka ni nani kwenye maandiko? (Walawi 11:29)
Je! Ni kweli kuna samaki mtu (Nguva) Baharini.
Je! Ni dhambi kumpiga au kumuua mnyama bila sababu yoyote?
Nini tafsiri ya jina Adamu,
Adamu ni neno la kiebrania lenye maana ya “wa udongo” yaani aliyetokana na udongo/ardhi. Mtu wa kwanza kuumbwa alipewa jina hilo Adamu na Mungu mwenyewe kufuatia asili yake alipotolewa.
Mwanzo 2:7 “Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai”.
Na jina “Adamu” hakupewa mtu mmoja tu bali wote wawili (yaani mwanamume na mwanamke)
Mwanzo 5:1” Hiki ndicho kitabu cha vizazi vya Adamu. Siku ile Mungu alipoumba mtu, kwa sura ya Mungu alimfanya;
2 mwanamume na mwanamke aliwaumba, akawabariki AKAWAITA JINA LAO ADAMU, siku ile walipoumbwa”.
Kwa urefu na kina Zaidi, kwanini Mungu awape wote wawili jina moja fungua hapa >>> Kwanini Mungu aliwaita Adamu na Hawa jina moja?
Watoto wote waliozaliwa baada ya Adamu, wakaitwa Wana-damu. (wana wa aliyekuwa wa udongo). Hivyo na sisi wote asili ya miili yetu ni ardhini, ndio maana tunakufa na miili yetu inaoza ardhini.
Lakini baada ya maisha haya, kama tukishinda vita vya kiimani vya ulimwenguni, maandiko yanasema tutavikwa miili mipya ya kimbinguni, hivyo hatutaitwa tena wanadamu, wala hatutaishi kwa kula na kunywa kama wanyama, wala tamaa za mwili hazitakuwepo tena bali tutakuwa kama Malaika kwasababu tutapewa miili mingine isiyo ya udongo.
Marko 12:25 “Kwa maana watakapofufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika walioko mbinguni”.
Je una tumaini la kuvikwa mwili mpya wa kimbinguni?..
Kumbuka tumaini hilo na uhakika huo tunaupata tu endapo tupo ndani ya Kristo, na tunaishi maisha yanayompendeza yeye.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Mungu anatufundisha kusamehe mara saba sabini, ila Kwanini yeye hakumsamehe Adamu alipoasi?.
Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?
KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?
Kwanini Kristo aitwe Mwana-kondoo. (Yohana 1:29)
Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo Bwana Yesu. Karibu katika kujifunza maneno ya uzima ya mwokozi wetu.
Leo tutaona jinsi “moyo wa toba ya kweli” unavyopokelewa kitofauti sana na Mungu. Kama tunavyoifahamu ile habari ya mwana mpotevu, jinsi alivyoingiwa na tamaa, ya kwenda kuanzisha maisha yake ya anasa mbali na baba yake. Na siku zilipozidi kwenda, mali zilipoisha, njaa kali ikamkuta Akaanza kula vyakula vya majalalani ambavyo viliwastahili tu nguruwe. Lakini Biblia inasema, hakung’ang’ania tu kuendelea kutaabika katika hali ile ile milele mpaka kufa kwake. Bali alijinyenyekeza akazingatia kurudi kwa baba yake akiwa na moyo wa toba, ili baba yake amfanye tu mtumwa. Na alipofanya vile, akiwa njiani anarudi, biblia inatumbia kuna tukio lilitokea.
Na tukio lenyewe ni “kuonekana kwake tokea mbali” . Tusome;
Luka 15:17 “Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa. 18 Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; 19 sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako. 20 Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana. 21 Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena. 22 Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni; 23 mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi; 24 kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia”
Embu tafakari, iweje, Baba yake ndio awe wa kwanza kumwona tokea mbali na sio watumwa ambao sikuzote wao ndio wanaosimama mlangoni mwa nyumba au kuzunguka zunguka huku na huko, au kwanini isiwe hata ndugu zake wengine, badala yake baba yake ndio anayekuwa wa kwanza kumwona?
Sio kana kwamba hao wengine walikuwa hawali mboga za majani, hawaoni mbali mambo yao kuwa hafifu, hapana, bali Baba yake alikuwa na jicho lingine la rohoni kama DARUBINI. Hilo lilikuwa linaona mahangaiko, na manyanyaso ya mwanaye tokea mbali, kiasi kwamba alipofanya geuko moyoni mwake, tayari baba yake alishahisi, na akiwa njiani anakuja tayari baba yake alishajua kuwa mwanawe yupo njiani. Hivyo kabla hata mtoto hajamwona Baba, kabla hata hajaifikia nyumba yao akiwa kilomita kadhaa mbali, tayari baba alikwenda kukutana naye na kukumbatia na kumbusu sana.
Ndivyo ilivyo kwa Mungu wetu. Pale mtu anapokuwa na moyo wa toba ya kweli rohoni, haihitaji wewe kwenda kusema maneno mengi sana mbele za Mungu, kana kwamba ndio utasikiwa. Yeye anayo darubini yake, Lakini kule kuzingatia tu kurudi kwa Baba yako wa mbinguni, ukaanza kuchukua hatua. Hiyo ni toba kubwa sana ambayo itamfanya Mungu, kabla ya wewe kumfikia tayari ameshakufikia, haraka sana na kukupa tiba ya moyo wako, na raha nafsini mwako.
Hii ni kuonyesha kuwa toba ya kweli, ni ule moyo uliogeuka. Sio tu kuongozwa sala maalumu. Ndio tunajua sala ikiambatana na geuko ni vema sana, lakini ikiwa utasalishwa sala hizo elfu 10 halafu ndani yako, ni vilevile tu, hapo unapoteza muda wako ndugu.
Alikuwepo Yule mwanamke mwenye dhambi nyingi sana, alipokwenda kwa Bwana Yesu saa ile ile akaanza kulia akitubia dhambi zake, akidondosha machozi yake miguu pa Yesu, huku akiyapangusa kwa nywele zake. Lakini Yesu alipomwona akasema ‘Umesamehewa dhambi zako nyingi’, mwanamke Yule hakusalishwa sala yoyote.(Luka 7:36-50).
Ili Mungu afike kwako upesi, kuwa na toba ya kweli, ili upate kibali cha haraka kwa Mungu, sio wingi wa maombi yako, bali geuko la dhati. Na Bwana mwenyewe atakufikia kabla hujamfikia yeye.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
WALA HAKUACHA MTU ACHUKUE CHOMBO KATI YA HEKALU.
Kwanini Nuhu alimlaani Kaanani badala ya mtoto wake Hamu,
UMUHIMU WA KUISHI MAISHA YAMPENDEZAYO MUNGU SASA.
MUME / MKE BORA KUTOKA KWA BWANA UTAMWONA UKIWA KATIKA MAZINGIRA GANI?
Jina la Mwokozi Mkuu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia.
Mithali 2:10 “Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako;
11 Busara itakulinda; Ufahamu utakuhifadhi.
Haya ni mambo manne ambayo ni muhimu sana kuwa ndani yetu.
Mambo haya manne ni Bwana pekee anayeweza kuyatoa.. Mithali 2:6 “Kwa kuwa Bwana huwapa watu hekima; Kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu” .
Zifuatazo ni faida kuu tatu (3) za kupata Hekima, Maarifa, ufahamu na busara.
Hii ni faida ya kwanza ya kupata Hekima, Ufahamu, busara na Maarifa; “Kumwokoa mtu na njia ya uovu”
Mithali 2:10 “Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako;
11 Busara itakulinda; Ufahamu utakuhifadhi.
12 ILI KUKUOKOA NA NJIA YA UOVU, Na watu wanenao yaliyopotoka;
13 Watu waziachao njia za unyofu, Ili kuziendea njia za giza;
14 Wafurahio kutenda mabaya; Wapendezwao na upotoe wa waovu;
15 Waliopotoka katika njia zao; Walio wakaidi katika mapito yao”
Njia ya Uovu ni njia yoyote ile ambayo itampelekea mtu kufanya maovu, mfano wa hayo ni yale yanayotajwa katika Wagalatia 5:19-21 “uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo”.
2. KUKUOKOA NA MALAYA:
Mithali 2:16 “…Ili kuokoka na malaya, Naam, malaya mwenye kubembeleza kwa maneno yake..”
Mtu aliye Malaya ni yule anayefanya uasherati aidha kwa lengo la kutafuta pesa au kujifurahisha, na hili ni neno linalotumika kuwakilisha jinsia zote mbili za watu wenye tabia hizo. Na Malaya anaweza kuwa ni mtu aliye ndani ya ndoa au nje ya ndoa.
Mtu mwenye busara (Maana yake anayeona mbele), hawezi kunaswa na mtego wa Malaya.. Mfano wa mtu aliyekuwa na busara katika biblia ambaye aliokoka na mtego wa Malaya ni Yusufu, ambaye alitegewa mtego na mke wa Potifa, lakini aliushinda mtego ule wa ibilisi.
Lakini kama Yusufu hangekuwa na Busara akilini mwake, basi angenaswa katika mtego ule wa uasherati alipobembelezwa na mke wa Potifa, na hivyo angekuwa amejiingiza katika matatizo makubwa sana, ambayo yangehatarisha hata maisha yake ya kimwili na kiroho.. kama biblia inavyosema hapa..
Mithali 2:16 “Ili kuokoka na malaya, Naam, malaya mwenye kubembeleza kwa maneno yake;
17 Amwachaye rafiki wa ujana wake, Na kulisahau agano la Mungu wake.
18 Maana nyumba yake inaelekea mauti, Na mapito yake yanakwenda kwenye wafu.
19 Katika hao wamwendeao harudi hata mmoja, Wala hawazifikilii njia za uzima”
Soma tena maandiko mengine yanayohusu tabia za Malaya, jinsi anavyobembeleza katika Mithali 7:7-23, Mithali 22:14 na Mithali 23:27.
Ukiona mtu kanaswa na mtego basi ni matokeo ya kupungukiwa Hekima, busara, maarifa na ufahamu.. kama biblia inavyosema katika Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake” .Kwasababu mtu aliyejaa mambo hayo hawezi kunaswa na mitego hiyo.
3. KUKUPELEKA KATIKA NJIA YA WATU WEMA
Faida ya kwanza tuliona ni “kumwokoa mtu katika njia ya uovu” lakini Hii ya tatu na ya mwisho, ambayo ni “Kukupeleka mtu katika njia ya watu wema”.. Hekima, busara, Maarifa na ufahamu haviishii tu kumwokoa mtu na njia mbaya na kumwacha hapo katikati bali pia kumpeleka/kumwongoza katika njia nzuri.
Mithali 2:20 “Ili upate kwenda katika njia ya watu wema, Na kuyashika mapito ya wenye haki.
21 Maana wanyofu watakaa katika nchi, Na wakamilifu watadumu ndani yake.
22 Bali waovu watatengwa na nchi, Nao wafanyao hila watang’olewa”.
Watu wema wana Njia yao, wapo katika mkondo wao, si kila mahali wanapita, na hao ndio wanaodumu katika nchi, … Sasa ili kuiona hiyo njia waliyopo basi Hekima, Busara, Maarifa na ufahamu vinahitajika. Na vyote hivyo vinatoka kwa Mungu.
Sasa swali? Mtu anapataje Hekima, Ufahamu, Busara na Maarifa ili kuepukana na hayo yote, na kupata faida hizo.
Tukitaka Hekima, Maarifa, Ufahamu na Busara biblia imetupa kanuni rahisi katika kitabu cha Ayubu.
Ayubu 28:20 “Basi hekima yatoka wapi? Na mahali pa ufahamu ni wapi?
21 Kwa kuwa imefichwa mbali na macho ya wote walio hai, Na kusitirika na ndege wa angani.
22 Uharibifu na Mauti husema, Tumesikia habari zake kwa masikio yetu.
23 Mungu ndiye aijuaye njia yake, Naye anajua mahali pake.
24 Maana anatazama hata miisho ya nchi, Na kuona chini ya mbingu nzima.
25 Apate kuufanyia upepo uzito wake; Naam, anayapima maji kwa kipimo.
26 Hapo alipoiwekea mvua amri, Na njia kwa umeme wa radi.
27 Ndipo alipoiona na kuitangaza; Aliithibitisha, naam, na kuichunguza.
28 Kisha akamwambia mwanadamu, Tazama, KUMCHA BWANA NDIYO HEKIMA, NA KUJITENGA NA UOVU NDIO UFAHAMU”.
Kumcha Bwana na kuepukana na Uovu ndio chanzo cha Hekima, maarifa, busara na ufahamu.
Maana yake Jishughulishe sana na masuala ya kiMungu sana, Jifunze Neno la Mungu, kusanyika na wengine katika maombi, ibada na kufanya uinjilisti na mambo mengine yote yanayofanana na hayo, kwa kufanya hivyo ndivyo Hekima, na hayo mambo mengine yatakayoingia ndani yako na kujaa.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?
Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.
Mjombakaka ni nani kwenye maandiko? (Walawi 11:29)
Nini maana ya “Mwenye hekima huvuta roho za watu”
JIBU: Kibiblia ni neno linalomaanisha “mvurugano” au “mvurugiko”
Neno hilo utalisoma katika kifungu hiki;
Isaya 17:13 “Mataifa wananguruma kama ngurumo ya maji mengi; Lakini atawakemea, nao watakimbia mbali sana, Watafukuzwa kama makapi milimani mbele ya upepo, Na kama mavumbi vuruvuru mbele ya tufani. 14 Wakati wa jioni, tazama, kuna hofu; Na kabla ya mapambazuko hawako; Hilo ndilo fungu lao watutekao, Na ajali yao wanaotunyang’anya mali zetu”.
Hapo ni Bwana anawahakikishia watu wake ulinzi madhubuti dhidi ya adui zao. Anasema mambo matatu yatawakumba hao wanaojaribu kuwaangamiza watu wa Mungu.
La kwanza,watakemewa na kukimbia mbali sana: Ni kama wakati wa washami kipindi cha nabii Elisha, Bwana alipowasikilizisha kelele za majeshi wakakimbia wakashindwa hata kuchukua na nyara zao nyuma(2Wafalme 7).
La pili ni “ watafanana na makapi mbele ya upepo: Kwa kawaida ngano inapopepetwa yale makapi huwa yanarushwa na upepo mbali sana, ndivyo watakavyofanywa waadui wa watoto wa Mungu wanapokaribiwa, watatoweka ghafla.
Na la tatu anasema watakuwa kama mavumbi ‘vuruvuru’ mbele ya tufani: Kwa kawaida upepo mkali wa kisulisuli au tufani inapopita juu ya ardhi iliyokuwa kavu, ule upepo wake mkali unatabia ya kuvuruga mavumbi, na kuyafanya yaruke hewani yasambae tu ovyo vyo, na hiyo husababishia hali ya hewa kuchafuka sana. Hivyo, Bwana anasema, ndivyo itakavyokuwa kwa watu hao, watavurugwa, kiasi cha kutokuelewana, kila mmoja atakuwa na lake, ni kuchanganyikiwa tu, Ndio maana ya hilo andiko.
Lakini ni nini Bwana anataka tujifunze?
Ni kwamba tuwapo ndani Kristo, hatuna haja ya kuwa na hofu, kwasababu shetani na majeshi yake, yatakutana kwanza na jeshi la Bwana kabla ya kutufikia sisi. Ndicho Elisha alichomwambia Gehazi, kwamba jeshi letu ni kubwa kuliko la kwao.
Hivyo mtakatifu yoyote unayedumu katika wokovu (usio wa mdomo bali wa roho), ulinzi huu unao. Lakini kinyume chake ni kweli ikiwa upo nje ya Kristo, huna ulinzi wowote kwa Bwana, na matokeo yake shetani anaweza kufanya lolote atakalo juu yako, hata kukuua.
Swali ni Je! Umeokoka?
Kama bado na upo tayari kufanya hivyo sasa basi fungua hapa kwa ajili ya mwongozo was ala hiyo. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je! Sulemani alienda mbinguni?
Uga ni nini? Na kazi yake ni ipi kibiblia?
Ila atapewa mara mia sasa,Ndugu wake(Marko 10:30)
SWALI: Kwanini Nuhu alimlaani Kanaani badala ya mtoto wake Hamu, ambaye ndiye aliyekuwa na makosa?
JIBU: Ni kweli kama tunavyosoma katika maandiko, pindi ambapo Nuhu amelima shamba lake la mizazibu akaaanda divai nyingi akanywa akalewa mpaka akalala uchi hadharani, tunaona mtoto wake mmoja aliyeitwa Hamu alipomuona hakuchukua hatua stahiki kumsitiri Baba yake
Lakini wale watoto wake wawili (yaani Yafethi na Shemu) walipomwona baada ya kuambiwa na Hamu, hawakutaka kutazama bali walichukua mavazi yao mabegani Kisha wakaenda kinyume nyume wakamfunika Baba Yao.
Nuhu alipopata taaarifa, aliyoyafanya mwanawe wa mwisho alimlaani, lakini laana yake haikuwa Kwa Hamu Moja Kwa Moja Bali Kwa mtoto wake aliyeitwa Kaanani..Sasa swali ni je Kwanini afanye hivyo Kwa Kaanani mjukuu wake, angali kitendo kimetendwa na Hamu.
Mwanzo 9:20-25
[20]Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu; [21]akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake. [22]Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje. [23]Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao. [24]Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea. [25]Akasema, Na alaaniwe Kanaani; Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.
Ipo mitazamo mingi katika jambo hilo, wapo wengine wanaomini kuwa Shemu alikuwepo na mwanaye huyo mkubwa Kaanani, na huwenda yeye naye alipuuzia kumsitiri Babu yake, au alifanya jambo baya kwake, wengine wanasema Hamu tayari alikuwa amebarikiwa na Mungu hivyo Baba yake asingeweza Tena kumlaani mtu ambaye amebarikiwa (Mwanzo 9:1),ndio maana laana akaisogeza kwa mjukuu wake.
Wengine wanaaanimi aliposema alaaniwe Kaanani, ni lugha tu iliyomaanisha pia “Baba wa kaanani”
Lakini ni vema tukaona muktadha wa uandishi wote, ikumbukwe kuwa aliyekiandika kitabu hicho ni Musa, na tunafahamu hatma ya taifa la Israeli, ilikuwa si katika mataifa yote duniani, bali pale Kaanani. Hivyo, ulikuwa ni unabii, wa Nuhu, kuonyesha moja wa uzao Shemu uitwao kaanani utalaaniwa. Hivyo tunapokuja kusoma juu ya anguko la wenyewe wa taifa lile, walivyoangamizwa na kuteketezwa na taifa la Israeli, ni kutukumbusha kuwa tayari Kaanani ilikuwa imeshalaaniwa tangu zamani, kuangamizwa kwao na maovu yao ni matokeo ya laana iliyotajwa zamani.
Shalom
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Nchi ya Nodi ambayo Kaini alikimbilia ndio nchi gani kwasasa?(Mwanzo 4:16).
Wakaanani walikuwa ni watu gani?
saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada
KWANINI NABII ISAYA ALIAGIZWA KUHUBIRI UCHI?