Jiunge >>> WHATSAPP <<< kwa mafundisho.
Biblia ni kitabu pekee chenye ukweli wote, umuhusuo Mungu, na mwanadamu, ni kitabu kinachoifunua njia ya uzima. Hivyo kuota unapewa biblia fahamu kuwa ndoto hiyo ni ya ki-Mungu, kwasababu kamwe shetani hawezi kukuongoza mahali ambapo utapata nuru ya maisha yako.
Zaburi 119:105 Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.
Hivyo ikiwa wewe bado hujamjua Kristo, basi fahamu Mungu anakupenda na hivyo anataka kukuongoza katika ukweli wote, Ndio maana umeota unapewa biblia haijalishi utakuwa mwislamu, mhindu, mpagani n.k Fahamu kuwa Yesu anakupenda, na anataka kukuokoa. Hivyo unachopaswa kufanya ni kumkubali tu maishani mwako, ili aweze kukufikisha katika ukweli wote, na majibu yote ya maisha yako.
Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu leo basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo ya imani >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Baada ya hapo, tafuta kitabu hichi (BIBLIA), Haraka iwezekanavyo uanze kusoma. Huku ukisaidiwa na waalimu sahihi wa Neno la Mungu. Kumbuka Wewe kufika hapa sio bahati mbaya, tovuti hii uliyopo sasa, Bwana ameiweka kwa ajili yako ina mafundisho mengi yatakayoweza kukusaidia kuielewa biblia vizuri. (www.wingulamashahidi.org). Itembelee mara kwa mara. Yapo mafundisho mengi sana, pamoja na majibu ya maswali mengi ya biblia. Lakini pia kama unatumia mtandao wa Whatsapp basi bofya hapa >>> WHATSAPP
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
SWALI: Biblia inamaana gani kusema jivikeni silaha ya nia ile ile? (1Petro 4:1)
1 Petro 4:1-3
[1]Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi.
[2]Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.
[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;
JIBU: Tukiangalia undani wa hilo neno hapo anaposema silaha ya nia. Ni kutuonyesha kuwa kumbe “Nia ”, inaweza kuwa silaha.
Mara nyingi tunapofikiria silaha kibiblia mawazo yetu moja kwa moja yanakimbilia zile za Waefeso 6:10-18, silaha za haki, kama vile upanga wa Roho ambalo ni Neno la Mungu, chapeo ya wokovu, ngao ya imani, dirii ya haki n.k.
Lakini hapa tunaonyeshwa kuwa ipo pia silaha ndani ya Nia, ambayo nayo tunashauriwa tuwe nayo, kwasababu ilikuwa kwanza ndani ya Kristo.
Na silaha yenyewe ilikuwa ni kukubali kuteswa katika mwili ili kuiua dhambi.
Bwana wetu Yesu Kristo alijua dhambi ina nguvu sana pale mwili unapopewa raha zake. Hivyo aliikubali Nia ya kuteswa, ili dhambi ife.
Kumbuka sababu ya yeye kuchukiwa na watu, kuudhiwa, kuwindwa auawe, kuteswa mpaka kusulubiwa ni kwasababu alitangaza uadui na dhambi, Vinginevyo asingepitia maudhi yale katika mwili. Na tunaona mwisho wake ulikuwa ni ushindi. Kwani kwa kifo chake dhambi ilihukumiwa kabisa kabisa.
Alisema..
Yohana 7:7
[7]Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi; bali hunichukia mimi, kwa sababu mimi naushuhudia ya kuwa kazi zake ni mbovu.
Hivyo maandiko yanatuambia na sisi pia, tujivike nia ile ile ya kukubali pia mateso kwa ajili ya Kristo. Kwasababu tukifanya hivyo tunaonyesha kuwa tumeachana na dhambi(tumeihukumu dhambi).
Kwa ufupi ni kuwa ukichukia maisha ya dhambi, tafsiri yake ni kukubali dhiki katika mwili kwa ajili ya Kristo. Hivyo zipende sasa dhiki hizo kama Kristo alivyozipenda, ili dhambi isikutawale. Hiyo ni Silaha kubwa sana.
2 Timotheo 3:12
[12]Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa.
kubali shida, kwasababu umeamua kuacha ile biashara haramu, furahia kutengwa na kuonekana mshamba, kwasababu umeamua kuacha mienendo ya marafiki wabaya, penda kupigwa na kufungwa kwasababu unahubiri kweli. Hiyo ndio SILAHA YA NIA. iwezayo kuishinda dhambi.
Ndio maana vifungu vinavyofuata anasema..
“Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.
[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;
Daima tujivike silaha hii, tukikumbuka kuwa vita vyetu si vikali tena kama vile alivyovipiga Kristo.
Waebrania 12:4
[4]Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi;
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?
NDUGU,TUOMBEENI.
DHABIHU ZA ROHO NI ZIPI? (1Petro 2:5)
KIKWAZO CHA EUODIA NA SINTIKE.
Rudi Nyumbani
Kitabu cha Wagalatia ni moja ya nyaraka ambazo mtume Paulo aliziandika kwa makanisa aliyoyapanda. Tunaona mwanzoni kabisa mwa waraka huu Paulo mwenyewe anajitambulisha akionyesha kuwa yeye ndiye mwandishi.
Waraka huu unamwonyesha Paulo akiwastaajabia watakatifu wa kanisa la Galatia kwa kuacha Imani ambayo aliwaachia hapo mwanzo, alipokuwa analisimamisha kanisa hilo, jambo ambalo lilimfanya mpaka imani yake impelekee kufikiri kuwa wamelogwa(Wagalatia 3:1), kwa jinsi tu walivyoiacha imani kwa haraka.
Kwa mujibu wa waraka huu, tunaona Paulo alilijenga kanisa hilo katika msingi wa imani katika neema ya Yesu Kristo.Na si katika msingi wa matendo ya sheria kama kigezo cha kukubaliwa na Mungu.
Kutokana na kuwa kanisa hili lilikuwa na mchanganyiko wa wayahudi pamoja na watu wa mataifa waliomwamini Kristo.Hapo ndipo tatizo lilipoanzia baada ya baadhi ya wakristo wa kiyahudi kuanza kuwashurutisha watu wa mataifa kwa kuwaambia kwamba hawawezi kuokolewa kama hawataishika torati ya Musa, kama hawatatimiza maagizo kama tohara, kushika siku, miezi, na miaka.(Wagalatia 4:8-10)
Hivyo hiyo ikawafanya watu kuacha kuishi tena kwa Imani iliyo katika neema ya Kristo Yesu, na kuangalia matendo ya sheria kama ndio kigezo cha kukubaliwa na Mungu?
Hivyo Paulo alipojua mageuzi hayo, ndio akawaandikia waraka huo kwa ukali, akiwaambia wokovu wetu huja kwa imani iliyo katika Yesu Kristo itendayo kazi katika upendo. Na si katika matendo ya sheria. Kwasababu kama ingekuwa hivyo Kristo alikufa bure. Torati ingeendelea tu kutawala.
Wagalatia 5:6
[6]Maana katika Kristo Yesu kutahiriwa hakufai neno, wala kutokutahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo.
Akasema torati, haikuwahi kumkamilisha mtu, na mtu anayeishi kwa hiyo ametengwa na Kristo, bado yupo chini ya laana.
kuishi kwa sheria ni kurudia mafundisho manyonge.
Lakini Swali ambalo alitarajia lingeulizwa na wagalatia, ni hili;
Je sasa hatuna haja ya kuyatazama matendo mema, tuishi tu, kama tunavyotaka kwasababu tunahesabiwa haki kwa neema ya Kristo tu?
Mbeleni kabisa katika sura ya tano, Mtume Paulo alitolea ufafanuzi, na kuwaambia tukishaokolewa, Maana yake ni kuwa tumeusulubisha mwili pamoja na tamaa zake mbaya..Hivyo hakuna nafasi ya dhambi kupata nguvu ndani yetu.
Wagalatia 5:24
[24]Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.
Je hilo inawezekanaje? kama hatuna sheria?
Linawezekana kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Ambaye tumepewa na Mungu.
Wagalatia 4:6
[6]Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba.
Hivyo Paulo anaendelea kueleza ni wajibu wa kila mwamini kutembea katika Roho. Ili awasaidie Roho kuzishinda tamaa zote za mwili, na mambo maovu.
Wagalatia 5:16-21
[16]Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
[17]Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
[18]Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.
[19]Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
[20]ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
,[21]husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
Je waraka huu ulilenga hasa nini?
Kwamba kwa nguvu zetu, au dini zetu au torati kamwe hatuwezi kumpendeza Mungu bali tuitegemee neema ya Kristo ambayo kwa hiyo tumepokea Roho awezaye kutufanya wakamilifu.
Hivyo ni wajibu wako kama mkristo. Kila wakati wote kujawa Roho (Waefeso 5:18). Ambayo hiyo huja kwa kuwa waombaji, wasomaji Neno, na kufanya ibada mioyoni mwetu wakati wote..
Tukiwa watu wa namna hiyo sheria wala dhambi inakuwa haina nguvu ndani yetu. Kwasababu tunakuwa chini ya neema ya Yesu Kristo.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Wapelelezi wa uhuru wa wakristo ni watu gani (Wagalatia 2:4)?
Rudi Nyumbani
Msingi ni chimbuko, au mwanzo au kiini cha kitu fulani.
Ni wazi kuwa kila jambo lina msingi wake. taifa lina msingi wake, taasisi ina msingi wake, kabila lina msingi wake vilevile pia imani ina msingi wake.
Hivyo tukirudi katika ukristo. Msingi wa imani yake ni upi?
Msingi wa ukristo ni YESU KRISTO mwenyewe, na kazi yake aliyoikamilisha ya kufa na kufufuka kwake. Na sio kanisa, au dhehebu, au mapokeo fulani, au kikundi fulani cha wanaharakati.
Pasipo Yesu hakuna ukristo.
Yeye anafananishwa na lile jiwe kuu la pembeni, ambalo hakuna mjenzi aliyeweza kusimamisha jengo bila kuliweka hilo.
1 Petro 2:6
[6]Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, Na kila amwaminiye hatatahayarika.
Habari kamili za Yesu, na kazi yake aliyokuja kuifanya duniani unaipata katika kitabu kimoja tu kiitwacho BIBLIA. Hivyo huwezi kutenganisha biblia na Yesu Kristo.
Ili mtu ashawishwe kuipokea imani, ni sharti, aisikie kwanza injili yake ambayo hiyo utaipata katika Neno la Mungu yaani biblia..(Warumi 10:17)
Mpaka mtu aitwe mkristo ni lazima amtambue kwanza Kristo ni nani, na nini amekileta duniani, vinginevyo hawezi kuwa mkristo, hata kama atajiunga na kanisa, au dhehebu na kuyashika mapokeo yote aliyoyakuta huko, au kuisoma biblia yote, huyo bado hajawa mkristo.
Ni muhimu sana kumtambua Yesu ni nani kwetu. Kumtambua Yesu kama mwana wa Mungu bado inaweza isikupe wokovu, hata kumtambua Yesu kama Mungu bado inaweza isikupe wokovu (ijapokuwa vyote hivyo ni vyeo vyake). Lakini vyeo hivyo sio kiini cha ukristo.
Yesu ni nani na ni nini alikileta duniani?
Yesu ni MKOMBOZI, kama tafsiri ya jina lake linavyojieleza( Mathayo 1:21)
mkombozi wa nini?
Alikuja kutukomboa roho zetu, nafsi zetu na miili yetu, Na kama ilivyo kanuni ya kiroho ili jambo hilo liweze kukamilika ilipasa itolewe kafara isiyo na kasoro yoyote(yaani dhambi). Na aliyeweza kukidhi vigezo hivyo ni Yesu pekee.
Ndio maana ilimgharimu afe, kama fidia ili sisi tupokee ondoleo la dhambi na msamaha wa dhambi kwa kifo chake. Hivyo yoyote anayeamini(yaani anayeupokea wokovu huo aliouleta).
kwa toba ya kweli na ubatizo, Basi anakuwa ameokoka, hivyo ile ghadhabu ya Mungu kwa wenye dhambi wote haiwi tena juu yake, tangu huo wakati anaitwa mbarikiwa, au mkristo, kwasababu dhambi zake zinakuwa zimefutwa kabisa.
Na zaidi ya hayo mtu huyu moja kwa moja anapewa zawadi ya Roho Mtakatifu, ambaye tangu huo wakati na kuendelea anakuwa ndani yake kama msaidizi, kumsaidia madhaifu yake, katika kuomba, kuijua kweli, kumkumbusha aliyoyasema Yesu, kumpasha habari ya mambo yajayo, na kumtia nguvu ya kumtumikia Mungu, pamoja na kumpa nguvu ya kushinda dhambi.
Huyu ndiye mkristo.
Swali ni je! umemwamini ipasavyo? au umempokea kwa namna ile ya kidini?
Usifikiri kuhama dini, wewe ni Kristo, au kuzaliwa kwenye familia ya kikristo wewe ndio mkristo, au kusomea theolojia, hapana hizo ni kampeni tu, ukristo halisi huja kwa kumwelewa Kristo ni nani na ni nini amekifanya kwako.
Ikiwa bado hujaokoka na unataka kumpokea leo ili upate ondoleo la dhambi zako. Basi uamuzi huo ni bora sana kwako. Wasiliana nasi namba uzionazo chini kwa mwongozo wa sala ya toba.
Ubarikiwe.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
+255693036618/ +255789001312
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?
Rudi Nyumbani
Biblia kitabu kikamilifu, na kitakatifu kimeandikwa na waandishi Zaidi ya 40 kwa Uvuvio wa Roho Mtakatifu. Ndani ya biblia kuna taarifa zinazohusu maisha ya watu zilizobeba sauti ya Mungu nyuma yake, pia kuna taarifa za Mataifa mbalimbali pia zenye kubeba sauti ya Mungu nyuma yake, lakini Zaidi sana kuna Nabii za wakati ujao.
Ifuatayo ni orodha ya waandishi 40 wa Biblia kuanzia Agano la kale hadi Agano jipya.
Agano la kale.
Agano Jipya.
Kwanini waandishi wapo Zaidi ya 40 na si 40 kamili?.. Ni kwasababu biblia pia imewataja wana wa Kora, ambao hatujui walikuwa ni wangapi, zaidi sana yupo mwandishi wa kitabu cha Waebrania, ambaye hajatajwa ni nani, huenda akawa ni Mtume Paulo, lakini kama si yeye bali ni mwingine, basi ataongezeka katika idadi ya walioiandika biblia.
Kumbuka tena, biblia ni kitabu cha Mungu kilichoandikwa na WATU, kwa uvuvio wa ROHO MTAKATIFU, Hivyo maneno yaliyoandikwa ndani ya Biblia, yana uzima.
2Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;
17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema”.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.
Mwandishi wa kitabu cha Matendo ya mitume.
Mwandishi wa kitabu cha Mithali ni nani?
Swali: Je kipindi Ibrahimu anatoka Uru ya Ukaldayo, hakuwa anajua anakokwenda kwamba ni Kaanani? au alikuwa anaongozwa na Roho Mtakatifu mpaka pale alipofika, ndipo Bwana akamwambia hapo hapo atulie?…na mbona tukisoma Mwanzo 12:5 tunaona kama Abramu alikuwa anajua kabisa anakoelekea, au je biblia inajichanganya?
Jibu: Biblia, Neno la Mungu halijichanganyi kamwe..
Turejee …
Waebrania 11:8 “Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka ASIJUE AENDAKO”.
Hapa ni kweli panaonesha kuwa Ibrahimu alikuwa hajui aendako, lakini hebu tusome maandiko mengine ndipo tutapata kuelewa zaidi..
Mwanzo 12:1 “BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;
2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka………………
5 Abramu akamchukua Sarai mkewe, na Lutu mwana wa nduguye, na vitu vyao vyote walivyokuwa wamejipatia na hao watu waliowapata huko Harani, wakatoka ili kwenda nchi ya Kanaani; nao wakaingia katika nchi ya Kanaani”
Hapa panaonyesha kuwa Abramu alikuwa anajua anakokwenda, kuwa ni Kaanani, Je lipi ni sahihi?
Jibu ni kwamba Abrahamu alikuwa anajua anakokwenda isipokuwa alikuwa hajui kama nchi hiyo aiendeayo (yaani ya Kaanani) kama ndio itakuwa ya ahadi..
Hivyo alienda mpaka alipofika na alipofika ndipo Mungu akamtokea na kumwambia kuwa nchi hiyo aliyopo ndiyo itakuwa milki yake (ya ahadi).
Mwanzo 12:5 “Abramu akamchukua Sarai mkewe, na Lutu mwana wa nduguye, na vitu vyao vyote walivyokuwa wamejipatia na hao watu waliowapata huko Harani, wakatoka ili kwenda nchi ya Kanaani; nao wakaingia katika nchi ya Kanaani.
6 Abramu akapita katikati ya nchi mpaka mahali patakatifu pa Shekemu; mpaka mwaloni wa More. Na Wakanaani siku zile walikaa katika nchi hiyo.
7 BWANA akamtokea Abramu, akasema, Uzao wako nitawapa nchi hii. Naye huko akamjengea madhabahu BWANA aliyemtokea”
Sasa swali linakuja, je ni kitu gani kilichomwelekeza Abramu aende nchi ya Kanaani na si nchi nyingine?
Tulirejea ule mlango wa 11 wa kitabu cha Mwanzo, tunasoma kuwa wazo la kuhama Uru wa Wakaldayo na kuelekea Kanaani halikuanzia kwa Abramu, bali lilianzia kwa baba yake aliyeitwa Tera, huyo ndiye aliyefikiri kuhama Ukadayo na hata kuchukua hatua ya kuhama pamoja na watoto wake wote ikiwemo Abramu.
Mwanzo 11:31 “Tera akamtwaa Abramu mwanawe, na Lutu mwana wa Harani, mwana wa mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka wote katika Uru wa Wakaldayo, waende nchi ya Kanaani, wakafika mpaka Harani wakakaa huko”.
Umeona hapo?..sio Abramu aliyekuwa na wazo la kuondoka Ukaldayo bali ni Tera, na sababu za kuwaondoa kule hazijulikani, kwani biblia haijaweka wazi, labda huenda ni maasi ya nchi hiyo, au sababu nyingine za kijamii au kibiashara.
Lakini katika wazo hilo la kuhama, lilikuwepo pia kusudi la Mungu ndani yake, kwamba Abramu afike Kanaani.
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Abramu alijua anakoenda, lakini hakujua nchi atakayopewa mpaka alipofika.
Nini tunajifunza hapo?
Wakati mwingine Bwana anaweza kutumia wazo la mtu mwingine kukupeleka wewe mahali Mungu anapotaka uwe.
Hivyo wakati mwingine usinung’unike unapoona unahamishwa mahali ulipo, kwani pengine Mungu anakupeleka mahali anapotaka wewe uwe, na ukishafika ndipo atakuonyesha.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Je Mungu hapendezwi na dhabihu na matoleo, kulingana na mstari huo?
Jibu: Turejee..
Waebrania 10:5 “Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema,
Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari”.
Andiko hili limerejewa kutoka katika Zaburi 40:6, tusome ili tupate maana kamili.
Zaburi 40:6 “Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo,
Masikio yangu umeyazibua, Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka”.
Hapo imewekwa vizuri kuwa ni kafara na sadaka zinazotolewa kwaajili ya DHAMBI!! ndizo asizozitaka…
Sasa Dhabihu ni sadaka za kuteketezwa (ambazo ni kafara za wanyama) zilizokuwa zinatolewa kipindi cha agano la kale kwaajili ya kufunika dhambi..
Na kasoro ya dhabihu za wanyama ndio hiyo, ilikuwa haiondoi dhambi bali inafunika tu..
Kwahiyo hapo anaposema “Dhabihu na matoleo hukutaka”.. alimaanisha kuwa hizo dhabihu za wanyama hazifai katika kumwondolea mtu makosa yake na kumtakasa bali mwili wa Yesu na damu yake ndio iwezayo kumtakasa mtu na kumwondolea kabisa dhambi zake.
Ndivyo maandiko yasemavyo kuwa damu za mbuzi na mafahali haziwezi kuondoa dhambi na kumtakasa mtu bali zilikuwa zinafunika tu.
Waebrania 10:3 “Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka.
4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi”
Lakini dhabihu ya mwili wa YESU, kupitia kumwagika kwa damu yake, unaondoa kabisa dhambi… Na hiyo ndio sadaka Mungu aliyoihitaji na sio dhabihu za kondoo na mbuzi na mafahali.
Waebrania 10:10 “Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu”.
Lakini kuhusiana na utoaji wa sadaka ni kwaajili ya shukrani, au kwaajili ya kazi ya ufalme wa mbinguni ni jambo linalompendeza Mungu na lenye baraka.
Lakini kama ni kwaajili ya dhambi (hakuna sadaka inayoweza kuondoa dhambi)..isipokuwa damu ya YESU ambayo tayari tumeshalipiwa bureee… tunachopaswa kufanya ili sadaka hiyo ifanye kazi juu yetu ni KUTUBU TU kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi!.
Tukiweza kutubu kwa kumaanisha basi tunapata msamaha na ondoleo la dhambi bure.
Je unaye YESU maishani?.
Kumbuka daima kuwa mwisho wa dunia upo, kama tu vile mwisho wa maisha ulivyo, ikiwa leo hii damu ya YESU si kitu cha thamani kwako, utasimamaje siku ile ya mwisho mbele zake?..Tafakari mara mbili.
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
Swali: Je vitu kama giza, na maji viliumbwa siku ya ngapi, maana tunaona wakitajwa tu wanyama na mimea, je hivi vingine viliumbwa lini?
Jibu: Ni kweli katika kitabu cha Mwanzo tunaona uumbaji unaanza kwa kusema “giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji”, lakini haitaji ni lini giza liliumbwa wala ni lini maji yaliumbwa, badala yake tunaona uumbaji unaendelea na vitu vingine kama mimea pamoja na wanyama na wanadamu?..
Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.
2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji”.
Jibu la swali hili lipo katika mstari huo wa kwanza..
Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi”.
Neno “hapo mwanzo”… halimaanishi kile kipindi cha siku saba (7) bali linamaanisha mwanzo kabisa wa uumbaji kabla ya kitu kingine chochote, Mungu aliumba mbingu (hii yenye mawingu na sayari) pamoja na mbingu ile yenye Malaika watakatifu.
Na vile vile aliumba “NCHI” Au kwa lugha nyingine ARDHI/DUNIA. Na ili ardhi iweze kukamilika ni lazima iwe na malighafi zake zote kama udongo, mchanga, mawe, milima, mabonde, chuma, madini, moto na maji na mengineyo.
Vile vile ili mbingu ikamilike lazima iwe na nyota na mwanga uwepo na giza liwepo, kwahiyo vitu hivi vyote viliumbwa Hapo Mwanzo, kabla ya zile siku sita za uumbaji.
Na baada ya Mungu kuumba Mbingu na nchi, hatujui ni kitu gani kilitokea kikaifanya nchi/dunia yenye milima na mawe na madini na mabonde na maji kuwa UKIWA! Au kwamba Mungu ndio aliiumba ikae hivyo ukiwa kwa kipindi Fulani cha muda..hatujui!, labda tutakuja kujua tutakapomaliza maisha haya na kufika huko kwake, tutamwuliza, lakini tunajua kuwa alisema hakiumba ukiwa, bali ikaliwe na watu.
Isaya 45:18 “Maana Bwana, aliyeziumba mbingu, asema hivi; Yeye ni Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; ndiye aliyeifanya imara; hakuiumba ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu; Mimi ni Bwana, wala hapana mwingine”
Hivyo kama hakuiumba ikae ukiwa bali ili ikaliwe na watu, basi hana budi kuiikarabati na kumweka mwanadamu humo, na ndipo hapo siku sita za uumbaji wa wanyama na wanadamu na miti zilipoanza..
Lakini kiuhalisia tayari mbingu na nchi zilikuwa umeshaumbwa hapo kabla, na malighafi zake zote (kama maji, udongo, mawe, madini, giza, hewa n.k)..na ndio maana hatuoni vikitajwa katika uumbaji.
Lakini pamoja na hayo, upo unabii unaoonyesha kuwa dunia itakuja kuwa tena ukiwa siku za mwisho, kipindi ambacho ghadhabu ya Bwana MUNGU itakapokuja kumwagwa juu wa wanadamu wote wakosaji, ambayo hata mmoja wetu hapaswi kuwepo..
Isaya 13:9 “Tazama, siku ya Bwana inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ili iifanye nchi kuwa ukiwa, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.
10 Maana nyota za mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze”.
Isaya 24:1 “Tazama, Bwana ameifanya dunia kuwa tupu, aifanya ukiwa, aipindua, na kuwatawanya wakaao ndani yake”.
Jambo litakalotokea siku hiyo ni lile tunalolisoma katika kitabu cha 2Petro 3:10-12 na Isaya 34:4.
Lakini wateule, waliomwamini Bwana na kuoshwa kwa damu yake, hawatakuwepo katika siku hiyo ya ghadhabu yake, kwani watakuwa mbinguni pamoja na Bwana.
Bwana atubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
Swali: Biblia inasema kushindana kwetu ni dhidi wa pepo wachafu, je kulingana na mstari huo, wapo pepo wazuri?
Jibu: Turejee…
Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya MAJESHI YA PEPO WABAYA katika ulimwengu wa roho”
Biblia iliposema kuwa kushindana kwetu ni dhidi ya “pepo wabaya” haijamaanisha kuwa wapo pepo wazuri, bali inaelezea tu sifa ya hizo roho (mapepo) kwamba ni mbaya na chafu.
Ni sawa na biblia inapotaja Malaika watakatifu, (soma Mathayo 25:31, Marko 8:38 na Ufunuo 14:10) haimaanishi kuwa wapo Malaika wasio watakatifu, na kama wapo wasio watakatifu basi hawaitwi tena Malaika bali ni mapepo, vile vile hakuna mapepo wasafi na kama zipo hizo roho safi basi haziwezi kuitwa tena mapepo, bali zitaitwa Malaika.
Hivyo uzuri na usafi unaotajwa juu ya Malaika au Mapepo, ni kuelezea tu sifa zao na kazi zao, kwamba Malaika wote walioko mbinguni ni wasafi na watakatifu, na mapepo yote yaliyotupwa ulimwenguni ni machafu na mabaya.
Na kumbuka pia “Pepo na jini” ni kitu kimoja, isipokuwa ni lugha mbili tofuati tu!… Na hakuna jini wala pepo mzuri, wote ni wabaya na wachafu. Zipo dini zinazofundisha kuwa wapo majini (mapepo) wazuri, na kwamba watu wanaweza kuwa nao na wakawaletea mafanikio na hata kuwalinda.
Huo ni uongo wa shetani asilimia mia, kwani shetani ndiye baba wa uongo..
Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; KWA SABABU YEYE NI MWONGO, NA BABA WA HUO”.
Shetani hajawahi kuwa na urafiki wa kweli na mwanadamu, wala hajawahi kuwa na mapenzi na mwanadamu, kitu anachokipenda kutoka kwa mwanadamu ni utukufu tu!.. lakini hajawahi kumpenda mwanadamu, na hakuna unabii ya kwamba atakuja siku moja kumpenda mwanadamu, yeye ni adui wa mwanadamu wa milele.
Na Kama tu shetani asivyopendwa kuitwa shetani, bali anapendwa aitwe mungu, kadhalika hawezi kuruhusu mapepo yake yaitwe vibaya, kwa sifa mbaya?..atawakatakasa tu!.. na anawatakasaje?..si kwa njia nyingine bali kwa njia za dini za uongo, zinazohubiri na kufundisha kuwa wapo mapepo wazuri.
Kwa urefu kuhusiana na pepo wachafu(majini) fungua hapa >>
Je umempokea YESU?.. kama bado ni nini kinakungojesha?
Bwana anarudi.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Jibu: Habari hii inamhusu Mtume Paulo, kipindi aliposhikwa na kufungwa akiwa Yerusalemu.. sasa ili tuelewe vizuri tuanze kusoma ule mstari wa 25
Matendo 22:25 “Hata walipokwisha kumfunga kwa kamba, Paulo akamwambia yule akida aliyesimama karibu, Je! Ni halali ninyi kumpiga mtu aliye Mrumi naye hajakuhumiwa bado?
26 Yule akida aliposikia, akaenda akamwarifu yule jemadari, akisema, Unataka kufanya nini? Kwa maana mtu huyu ni Mrumi
27 Jemadari akaja, akamwuliza, Niambie, u Mrumi? Akasema, Ndiyo.
28 Jemadari akajibu, MIMI NALIPATA WENYEJI HUU KWA MALI NYINGI. Paulo akasema, Na mimi ni Mrumi wa kuzaliwa”.
Wenyeji unaozungumziwa hapo ni “URAIA”.. Kwahiyo hapo kiswahili kingine cha andiko hili ni hiki .. “Jemadari akajibu, MIMI NALIPATA URAIA HUU KWA MALI NYINGI”.
Zamani za kanisa la karne ya kwanza, ufalme uliokuwa na nguvu duniani, ulikuwa ni ufalme wa Rumi, na ndio uliokuwa unatawala dunia chini ya Kaisari. Hivyo kutokana na nguvu ya ufalme huo, basi hata raia wake walikuwa na nguvu, na heshima.
Raia wa kirumi (yaani Mrumi) alikuwa hawezi kuadhibiwa bila kushitakiwa, na haki zake zilikuwa zinalindwa sana kuliko raia wa Taifa lingine lolote duniani,..ilikuwa ni kosa kubwa kumhukumu Mrumi kabla ya kumsikiliza.
Sasa hapa Paulo alikuwa ni Mrumi kwa kuzaliwa lakini kwaasili ni Mwebrania (yaani muisraeli), na hapa alikuwa amevunjiwa haki yake kama raia wa kirumi, na hivyo akida pamoja na jemedari wakaogopa, kwasababu ni kosa kumhukumu Mrumi kabla ya kumpandisha kizimbani na kumsikiliza.
Sasa swali la Msingi kwanini, Jemedari aseme Uraia wake kaupata kwa mali nyingi?
Zamani ili uwe Raia wa kirumi ni aidha uwe mzawa (yaani umezaliwa katika Taifa la Rumi) au Umeununua uraia.
Sasa kitendo cha kuununua Uraia hakikuwa rasmi, bali kilikuwa ni kwa njia ya rushwa, na waliopata uraia huo waliupata wakati wa sense, ambapo majina yako yaliongezwa katika orodha ya warumi kinyume cha sheria, baada ya kulipa pesa nyingi,
Na hapa huyu Jemedari aliyeitwa Klaudio Lisia (Matendo 23:26) anaonekana kumwambia Paulo kuwa Uraia wake “Aliununua” maana yake kwa asili hakuwa mrumi, bali alikuwa kuwa mtu wa Taifa lingine, huenda Ugiriki, kwasababu hilo jina la Pili la LISIA ni jina la kigiriki, lakini Paulo yeye alikuwa ni Mrumi kwa kuzaliwa na si kwa kununua uraia.
Upo uraia mwingine ambao ni wa Mbinguni…huo haupatikani kwa fedha, wala mtu haupati kwa rushwa bali bali kwa kuzaliwa mara ya pili.
Yohana 3:3 “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.
4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?
5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.”
Je umeupata uraia huu wa mbinguni kwa kuzaliwa mara ya pili?.. kama bado ni nini kinachokusubirisha??
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine: