Title April 2025

Ipi tofauti ya utakatifu na utukufu?

Jibu: Neno Utakatifu linatokana na Neno “utakaso”.. kitu lilichotakasika kinaitwa “kitakatifu”.. na kitu kilichotakasika/takata maana yake hakina uchafu.

Kwahiyo utakatifu kwa tafsiri rahisi maana yake ni “kuwa safi, (kutokuwa na uchafu)”..  Mtu anaweza kuwa msafi (mtakatifu) mwilini na rohoni.

Sasa kikawaida kitu chochote kinapokuwa safi, huwa kinatoa Mng’ao unaopendeza.. sasa ule mng’ao unaotafsiri usafi wa kitu kile ndio unaoitwa UTUKUFU, kwamfano dhahabu inaposafishwa na kuwa safi huwa inatoa mng’ao mzuri wa kipekee, sasa ule mng’ao ndio utukufu wa ile dhahabu au kito, na vitu vingine vyote ni hivyo hivyo.

Hali kadhalika mtu aliyetakaswa dhambi zake kwa damu ya YESU, na yeye mwenyewe kujilinda  na kujitenga na uchafu wote wa rohoni na mwilini,  basi mtu huyo ni mtakatifu na anao utukufu, ambao  ni NURU inayong’aa,  ambayo shetani na mapepo yake hayawezi kustahimili mwako wake.

Lakini zaidi sana MUNGU wetu aliyetuumba ndiye mwenye utukufu MKUU,  ambao huo unatokana UTAKATIFU alionao, uzidio viumbe vyake vyote.. Mng’ao wa utukufu wake hata malaika wanainama mbele zake na kujifunika kwa mbawa zao, na utukufu wake unang’aa mpaka duniani.

Isaya 6:1 “Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu.

2 Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka.

3 WAKAITANA, KILA MMOJA NA MWENZAKE, WAKISEMA, MTAKATIFU, MTAKATIFU, MTAKATIFU, NI BWANA WA MAJESHI; DUNIA YOTE IMEJAA UTUKUFU WAKE”.

Naam nasi tuliompokea YESU ni lazima tufanane naye, na hatuwezi kuwa na utukufu bila kuwa watakatifu, na hatuwezi kukosa utukufu tukiwa watakatifu, na kuwa mtakatifu duniani inawezekana..

Zaburi 16:3 “Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE UMEUFIKIA ULE UTUKUFU HALISI WA MANA? 

NYUMBANI MWA BABA YANGU MNA MAKAO MENGI.

YESU NI ALFA NA OMEGA .

JINSI YA KUITUMIA VYEMA NEEMA YA MUNGU ILIYO JUU YANGU

Print this post

Ipi tofauti kati ya Ahadi na Nadhiri?

Swali: Kuna tofauti gani kati ya Ahadi na Nadhiri, kwa mujibu wa Biblia?


Jibu: Ahadi ni Neno/tamko la hiari mtu analolitoa kwa mtu mwenzake, kwamba atalitenda katika wakati mfupi au mrefu ujao.

Kwamfano mtu anaweza kuahidi kuwa kesho atawasili katika hafla, na hiyo kesho kweli akafika kama alivyoahidi, hapo anakuwa ameitimiza ahadi yake, lakini asipowasili kama alivyoahidia anakuwa hajaitimiza ahadi, na ni dhambi ikiwa hakuwa na sababu za msingi za kuivunja ahadi yake.

Lakini katika upande wa Nadhiri, hii ni ahadi (yaani tamko ya hiari) mtu analolitoa kwa MUNGU, na si kwa mtu.

Kwamfano mtu anaweza kuahidi kuwa endapo akipona ugonjwa unaomsumbua atamtolea MUNGU sadaka ya shukrani, au endapo Mungu akimtendea jambo Fulani basi atamtolea MUNGU sadaka Fulani, hiyo inakuwa ni nadhiri.

Na mtu asipotimiza Nadhiri aliyomwekea MUNGU inakuwa ni dhambi..

Mhubiri 5:4 “Wewe ukimwekea Mungu nadhiri, usikawie kuiondoa; KWA KUWA YEYE HAWI RADHI NA WAPUMBAVU; BASI, UIONDOE HIYO ULIYOIWEKA NADHIRI.

5 Ni afadhali usiweke nadhiri, Kuliko kuiweka usiiondoe.

6 Usikiache kinywa chako kuukosesha mwili wako; wala usiseme mbele ya huyo malaika ya kwamba umepitiliwa; kwani Mungu akukasirikie sauti yako, na kuiharibu kazi ya mikono yako?”

Kwahiyo ni muhimu kuitimiza ahadi tunazozitoa na pia Nadhiri uliomwekea MUNGU.

Ikiwa kuna sababu zozote za msingi zilizojitokeza za kutotimiza ahadi basi ni vizuri kufanya mapatano na uliyemhadi mapema ili isigeuke kuwa uongo.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! USIPOTIMIZA NADHIRI ZAKO ZOTE KWA BWANA. HAWEZI KUKUSAMEHE?

Ipi tofauti kati ya sadaka ya dhambi na sadaka za hatia?

LISIMAMISHE JIWE.

AINA TATU ZA UTAKATIFU

FUVU LA KICHWA.

Print this post

Ipi tofauti ya Hasira na Ghadhabu ya MUNGU?.

Swali: Kuna utofauti gani uliopo kati ya Hasira ya MUNGU na Ghadhabu ya MUNGU?

Jibu:  Kujua tofauti yake turejee mistari michache katika biblia..

Zaburi 6:1 “Bwana, usinikemee kwa HASIRA YAKO, Wala usinirudi kwa GHADHABU YAKO”.

 “Hasira” ni hisia ya “kuchukizwa” inayompata mtu kutokana na tendo Fulani baya alilofanyiwa, au lililomtokea kinyume na matakwa yake.  Hii ni hisia ya ndani ambayo inaweza kumfanya mtu apoteze hamasa, au hamu au shauku ya jambo Fulani.

Lakini “Ghadhabu” yenyewe inaenda mbali zaidi haiishii kumfanya mtu ajisikie tu vibaya na kujitenga bali inampeleka kuadhibu, au kulipiza kisasi.

Kwamfano kuna mtu aliyepigwa na mwenzie, akaishia kukasirika na kujitenga na Yule mtu, (Huyu anahesabika kuwa anazo hasira, kakasirika).. Lakini kuna mwingine anaweza kupigwa na mwenzake asiishie tu kukasirika lakini akarudisha mapigo, sasa huyu maana yake kaghadhibika, hivyo hasira yake imerudisha majibu hasi kwa aliyemtendea.

Sisi wanadamu tuna hasira lakini pia tunazo ghadhabu.. Ila Biblia imetuonya tusiizalie matunda hasira hata kuwa ghadhabu.. kwasababu hasira iliyozidi hata kutenda dhambi ndio ghadhabu..

Waefeso 4:26 “Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka;

27 wala msimpe Ibilisi nafasi”.

Kwanini Biblia imezuia tusiwe watu wa kuwa na hasira ya kupitiliza?… Ni kwasababu hisia zetu zina mapungufu na hukumu zetu si kamili..

Lakini hukumu za MUNGU ni kamili kwani MUNGU anayo hasira na pia Ghadhabu.. Lakini mpaka ghadhabu ya MUNGU imemwaga basi ni hakika kuwa tumestahili, lakini sisi wanadamu hatujapewa ruhusa ya kuwa na ghadhabu, kwasababu hukumu utakayompimia mwenzako MUNGU akikuangalia nawe pia unastahili hiyo hiyo kwa makosa yako mengine (Mathayo 7:1), Lakini yeye MUNGU akihuhukumu hana wa kumhukumu kwakuwa ni mkamilifu, hivyo hukumu zake ni kamili!.

Na pia ni kwa maarifa ya ziada ya kujua ni hasira ya namna gani ambayo tumepewa ruhusa ya kuwa nayo, fungua hapa>>MWE NA HASIRA, ILA MSITENDE DHAMBI.

Sasa Maandiko yanasema MUNGU aliyetuumba si Mwepesi wa hasira (maana yake hakasiriki haraka) lakini ni Mwingi wa hasira (maana yake hasira yake inafikia kiwango cha ghadhabu), cha kuadhibiwa na kujilipiza kisasi,.

Nahumu 1:2 “Bwana ni Mungu mwenye wivu, naye hujilipiza kisasi; Bwana hujilipiza kisasi, naye ni mwingi wa hasira; BWANA HUJILIPIZA KISASI JUU YA ADUI ZAKE, huwawekea adui zake akiba ya hasira.

3 BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, ana uweza mwingi, wala hatamhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; Bwana ana njia yake katika kisulisuli na tufani, na mawingu ni mavumbi ya miguu yake”.

Kilichowapata watu wa nyakati za Nuhu ni Ghadhabu ya MUNGU, kilichowapata watu wa nyakati za Sodoma na Ghomora  ni Ghadhabu ya MUNGU!, Ndio maana hawakupona, na kitakachotokea kwa dunia ya wakati wa Mwisho ni Gadhabu ya MUNGU, soma  (2Petro 3:6-7 na Ufunuo 16:1).

Na MUNGU anaweza kuimimina Ghadhabu yake kwa Mtu mmoja, na kwa watu wengi kwa pamoja au kwa dunia nzima.. Mtu anayefanya dhambi kwa makusudi yupo katika hatari ya kukumbana na ghadhabu ya MUNGU yeye kama yeye…

Wakolosai 3:5 “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;

6 KWA AJILI YA MAMBO HAYO HUJA GHADHABU YA MUNGU”.

Hivyo Biblia  (Neno la MUNGU) linatufundisha kuiogopa Ghadhabu ya MUNGU kwa kutembea katika mapenzi yake na pia kujizuia sisi na ghadhabu kwasababu hasira ya mwanadamu haiitendei haki ya MUNGU.

Yakobo 1:19 “Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; WALA KUKASIRIKA;

20 KWA MAANA HASIRA YA MWANADAMU HAIITENDI HAKI YA MUNGU.

21 Kwa hiyo wekeeni mbali uchafu wote na ubaya uzidio, na kupokea kwa upole neno lile lililopandwa ndani, liwezalo kuziokoa roho zenu”.

Mithali 15:1 “Jawabu la upole hugeuza HASIRA; Bali neno liumizalo huchochea GHADHABU”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.

IEPUKE GHADHABU YA MUNGU.

KIKOMBE CHA GHADHABU YA MUNGU KINAJAA.

NIMEAZIMIA KUWAKUSANYA MATAIFA. NIPATE KUWAMWAGIA GHADHABU YANGU

Biblia inamaana gani kusema ‘maana Mungu wetu ni moto ulao’ (Waebrania 12:29)

Print this post

Ipi tofauti kati ya sadaka ya dhambi na sadaka za hatia?

Katika agano la kale dhambi ilitokea na kuhesabiwa katika maeneo mbalimbali.

 Kwamfano 

> Kulikuwa na makosa ya jamii nzima. Yaani taifa zima kuasi. (Kutoka 32,)

> Makosa ya mtu binafsi. Mfano kutenda uzinzi, Wizi, uuaji n.k.

 > Makosa ya kuwatendea vibaya wanyonge: Mfano maskini, wageni, mayatima na wajane (Amosi 5:11-12),

>  Makosa ya kukaidi sherehe za kidini (Walawi 11-15), 

> Makosa ya kuvunja maagano (Yeremia 17:21-23), 

> Makosa ya kuabudu miungu mingine (sanamu). 

Lakini pia kulikuwa na aina nyingine mbili za makosa..

> Aina ya kwanza ni makosa ya kukusudia

> Aina pili ni yale ya kutokusudia.

 

Ikiwa mtu alitenda dhambi kwa kutojua, alihesabika kuwa ni dhambi, hivyo alilazimika atoe sadaka ya dhambi. Lakini kama alitenda dhambi ya makusudi kinyume na mwenzake, ili kuondoa kosa Ilipasa atoe sadaka ya hatia.

Aina ya sadaka hizi zinaelezwa kwa urefu kwenye kitabu cha Walawi 4:1 – 5:13

Dhambi za kutokusudia Mfano wake ilikuwa ni kama kuvunja amri bila kujua au kutojua Sheria ya vitu safi au najisi ilivyo. Hivyo mtu alijikuta tu anatenda kwa kukosa ufahamu.

Walawi 4:1-3

[1]BWANA akanena na Musa, na kumwambia, 

[2]Haya, nena na wana wa Israeli, uwaambie, Kama mtu ye yote akifanya dhambi pasipo kukusudia, katika neno lo lote ambalo BWANA amelizuilia lisifanywe, na kutenda neno lo lote la maneno hayo; 

[3]kama kuhani aliyetiwa mafuta akifanya dhambi, hata analeta hatia juu ya watu; ndipo na atoe kwa ajili ya dhambi yake aliyoifanya, na kumsongeza kwa BWANA ng’ombe mume mchanga mkamilifu, kuwa ni sadaka ya dhambi.

Dhambi za kukusudia ni zote ambazo zilitendwa kinyume na mtu mwingine au mambo matukufu mfano wa hizi ni kama kuiba, kusema uongo, viapo Vya uongo, hivyo iliambatana pia na kutoa fidia ya vitu hivyo.

Sio tu kusamehewa bali pia kuweka mambo sawasawa kwa kulipia fidia.

Mfano wa tendo hili, tunaona kwa Zakayo, alipofikiwa na wokovu, alitubu kwa kurejesha mara nne ya vyote alivyodhulumu. (Luka 19:8) huo ni mfano wa sadaka ya hatia.

Katika agano jipya dhambi Zote Za kukusudia na kutokusudia na nyingine zote zinaondolewa  na sadaka moja  tu ya daima nayo ni DAMU YA YESU (Waebr 9:26, Isaya 53:10, 1Petro 2:24). Hiyo tu ndio inafuta hatia zote.

Lakini pamoja na hayo, sadaka hizi hutukumbusha pia kila tuombapo rehema, (kwa unajisi tunaojitia kila siku), hatuna budi kuomba sio tu kwa dhambi tuzijuazo bali pia kwa zile tusizozijua.

Kwasasa dhambi tusizokusudia ni kama vile kumkwaza  mwenzako bila kufahamu, Kutowaombea wengine(2Samweli 12:23), kuwaza vibaya, kutotumiza nadhiri zetu, au wajibu wetu N.k.

 

Bwana akubariki.

 

Je umesamehewa na kuondolewa dhambi zako? Kama ni la! basi wakati ndio sasa, unapomgeukia Bwana Yesu, anakuondolea kumbukumbu lote la makosa. Hivyo fungua hapa kwa msaada huo wa kumpokea yeye >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ndio kipi? (Matendo 21:25).

Nini maana ya dhabihu na matoleo hukutaka? (Waebrania 10:5).

Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?

Print this post

SHUKA UPESI

Luka 19:1 “Naye alipoingia Yeriko alipita katikati yake.

2 Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri.

3 Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo.

4 Akatangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu apate kumwona, kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile.

5 Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, SHUKA UPESI, KWA KUWA LEO IMENIPASA KUSHINDA NYUMBANI MWAKO.

6 Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha”.

YESU hawezi kuingia nyumbani kwako kama “hutashuka kwenye Mkuyu”..

Mkuyu ni kitu chochote kijiinuacho juu ya  YESU,…. Kiburi cha mali ni mkuyu,… kiburi cha cheo ni mkuyu, kiburi cha uzuri ni Mkuyu n.k.. Mtu anavyovitumia hivi ili kumwona Bwana YESU au kumtumikia, Kristo yeye anaenda kinyume navyo..

Zakayo asingeweza kuzungumza na Bwana akiwa juu ya mkuyu..ilimpasa ashuke upesi… Sauti ile ilikuwa na mamlaka, ilipenya katika moyo wa Zakayo na kumfanya ashuke si tu chini ya Mkuyu, bali hata kiburi chake chote, kwani alikuwa ni mtu mkubwa kifedha…

Alipokubali  tu kushuka na kiburi chake cha mali nacho kikashuka, kiburi chake cha cheo kikashuka akawa mtu mwingine, mnyenyekevu na YESU akaingia nyumbani mwake..

Nusu ya mali yake aliwapa maskini na wote aliowadhulumu aliwarudishia mara nne.

Luka 19:6 “Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha.

7 Hata watu walipoona, walinung’unika wote, wakisema, Ameingia kukaa kwa mtu mwenye dhambi.

8 Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang’anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.

9 Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu.

10 Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea”.

Na wewe leo, shuka chini ya Mkuyu.. kiburi cha Elimu kinaweza kuwa kizuizi cha Kristo kutembea na wewe, kiburi cha pesa kinaweza kuwa kikwazo cha YESU kuingia kwako, kiburi cha cheo na uzuri ni hivyo hivyo, lakini unyenyekevu unaleta Neema.

Yakobo 4:6 “Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NINI MAANA YA KUTUBU

ALIYOKUTANA NAYO YESU, YERIKO.

JE YESU AMEJIAMINISHA KWAKO?

LEO WOKOVU UMEFIKA NYUMBANI HUMU

JE! WEWE NI MWANA WA IBRAHIMU?

Print this post

OMBA JAMBO KATIKA MAJIRA YAKE.

Zekaria 10:1 “Mwombeni Bwana mvua wakati wa masika, naam, Bwana afanyaye umeme, naye atawapa manyunyu ya mvua, kila mtu atapewa nyasi kondeni”.

Umewahi kujiuliza kwanini hapo maandiko yanasema “Mwombeni Bwana mvua WAKATI WA MASIKA” na si wakati mwingine wowote kama kiangazi?..

Ni kwasababu msimu wa masika ni msimu wa mvua, hivyo inapotokea hakuna mvua si jambo la kawaida, kwahiyo tukiomba mvua msimu huo ni hoja yenye nguvu, lakini tunapoomba mvua msimu wa kiangazi zinakuwa si hoja zenye nguvu!.. Ndicho maandiko yanachokimaanisha hapo.

Maombi ya kuomba kwa wakati ni mazuri na yana majibu ya haraka kuliko yale ya kuomba nje ya msimu/majira.

Unaomba mume/mke  na bado ni mwanafunzi, unaomba mali na bado unasoma, unaomba umtimikie MUNGU na bado hujaokoka!, maombi ya namna hiyo ni nadra sana kujibiwa!.. ni wachache sana wanaojibiwa hayo maombi!!.. sio kwamba ni maombi mabaya au vinavyoombwa ni vitu vibaya!. La! Ni vizuri lakini vinaombwa nje ya majira yake.

Hapo maandiko yanasema “Mwombeni Bwana Mvua wakati wa Masika”..  Maana yake ni lazima ujue uhusiano wa kile unachomwomba MUNGU na majira uliyopo. Kama kitu bado majira yake usitumie nguvu kubwa kuomba, shughulika na vile ambavyo sasa ndio majira yake.

Kama wewe ni mwanafunzi usiombe MUNGU akupe hela kwa sasa….badala yake mwombe akufanikishe katika masomo ufaulu, uwe kichwa, hayo mengine bado msimu wake!..

Kama wewe ni binti/kijana na bado upo chini ya wazazi unawategemea, usiombe MUNGU akuonyeshe mume wako/mke wako, badala yake mwombe ulinzi juu ya tabia yako mpaka utakapofika wakati wa wewe kujitegemea na kufikiri kuingia katika ndoa.

Lakini kama umeshaingia katika msimu basi ni haki yako kumwomba BWANA!, Na unapomwomba Bwana jambo sahihi katika msimu sahihi, MUNGU ni mwenye huruma atakupa unachokihitaji haraka sana, na hata kikichelewa atakupa sababu kwanini kinachelewa, na sababu za BWANA zote ni Bora na wala si za kumwumiza Mtu, kwasababu yeye kamwe hawezi kuruhusu tujaribiwe kupita tuwezavyo.

Vumilia tu ukiona umeshaingia kwenye msimu na bado matokeo hujayaona!, yatakuja tu!..usikate tama a wala kuishiwa nguvu, mwamini MUNGU na mngojee, naye atakupa nguvu mpya kila siku.

Jambo la mwisho la kujua ni kwamba wokovu pia unao msimu wake, na msimu wa Wokovu ndio sasa..

Huu ndio wakati wa MUNGU kutupa wokovu na kutusikia maombi yetu, kwani utafika wakati ambapo hakutakuwa tena na wokovu wala maombi kusikiwa, ndivyo maandiko yanavyosema..

2Wakorintho 6:1 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.

2 (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia; tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)

Sasa kama  siku ya Wokovu ndio sasa, unasubiri nini usimpokee YESU?.. je unadhani itakuwa hivi siku zote?.. utafika wakati mlango wa Neema utafungwa, na hakutakuwa tena na msamaha wa dhambi wala ondoleo la dhambi, mti ulipoangukia huko huko utalala (Mhubiri 11:3).

Sasa unayadharau mahubiri na mafundisho ya uzima, unayoyapokea kila mahali yanayokuonya kuhusu dhambi, je unadhani hali itakuwa hivyo kila siku?…Majira yatabadilika ndugu, utafika wakati kutakuwa hakuna kuponywa tena mwili na roho!.

2Nyakati 36:15 “Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake;

16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, HATA ILIPOZIDI GHADHABU YA BWANA JUU YA WATU WAKE, HATA KUSIWE NA KUPONYA”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nzige, Parare, madumadu na tunutu ni wadudu gani? (Yoeli 2:25)?

MAASI KUONGEZEKA NI ISHARA YA NINI?.

JIFUNZE JAMBO KWENYE UKOO WA YESU, UWE NA AMANI

Kwanini madhabahu zilitengenezwa kwa mawe yasiyochongwa?

Kwanini Mungu auweke Mti wa Mema na Mabaya katikati ya bustani?

Print this post

Je ni Petro au Mariamu Magdalene aliyekuwa wa kwanza kutokewa na Bwana YESU?

Swali: Kati ya Simoni Petro na Mariamu Magdalene ni yupi aliyekuwa wa kwanza kutokewa na Bwana YESU baada ya kufufuka kwake?, kwa maana katika Luka 24:34 tunasoma kuwa ni Simoni ndiye wa kwanza kutokewa na Bwana, lakini tukirudi katika Marko 16:9 tunaona ni Mariamu Magdalene je hii imekaaje?.


Jibu: Turee mistari hiyo..

Luka 24:33 “Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao,

34 wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, NAYE AMEMTOKEA SIMONI”.

Hapa tunaona anatajwa Simoni, lakini turejee Marko 16:9..

Marko 16:9 “Naye alipofufuka alfajiri siku ya kwanza ya juma, ALIMTOKEA KWANZA MARIAMU MAGDALENE, ambaye kwamba alimtoa pepo saba.

10 Huyo akashika njia akawapasha habari wale waliokuwa pamoja naye, nao wakali wanaomboleza na kulia”.

Hapa tunasoma ni Mariamu Magdalena ndiye aliyetokewa kwanza, sasa swali ni yupi aliye sahihi au biblia inajichanganya?..

Jibu ni La! Biblia haijichanganyi na wala haina kasoro yoyote… Sasa kama ni hivyo ni nani aliyetokewa wa kwanza?

Jibu, aliyetokewa wa kwanza na Bwana YESU alikuwa ni MARIAMU MAGDALENE, kama maandiko yanavyoonyesha hapo juu (Marko 16:9).. huyu ndiye aliyekuwa wa kwanza kumwona Bwana kwani baada tu ya kukuta jiwe limeviringishwa mbali na kaburi aliondoka na kwenda kuwafuata akina Petro kuwapasha yaliyojiri, na Petro pamoja na Yohana walipokwenda kaburini kuhakiki hizo taarifa za Magdalene,  walikuta tu vitambaa vya sanda, na walipoondoka ndipo Bwana YESU akamtokea Mariamu Magdalene kama mtu wa kwanza (na saa hiyo akina Petro wameshaondoka).

Yohana 20:1 “Hata siku ya kwanza ya juma Mariamu Magdalene alikwenda kaburini alfajiri, kungali giza bado; akaliona lile jiwe limeondolewa kaburini.

2 Basi akaenda mbio, akafika kwa Simoni Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, Wamemwondoa Bwana kaburini, wala hatujui walikomweka.

3 Basi Petro akatoka, na yule mwanafunzi mwingine, wakashika njia kwenda kaburini.

4 Wakaenda mbio wote wawili; na yule mwanafunzi mwingine akaenda mbio upesi kuliko Petro, akawa wa kwanza kufika kaburini.

5 Akainama na kuchungulia, akaona vitambaa vya sanda vimelala; lakini hakuingia.

6 Basi akaja na Simoni Petro, akaingia ndani ya kaburi; akavitazama vitambaa vilivyolala,

7 na ile leso iliyokuwako kichwani pake; haikulala pamoja na vitambaa, bali imezongwa-zongwa mbali mahali pa peke yake.

8 Basi ndipo alipoingia naye yule mwanafunzi mwingine aliyekuwa wa kwanza wa kufika kaburini, akaona na kuamini.

9 Kwa maana hawajalifahamu bado andiko, ya kwamba imempasa kufufuka.

10 Basi wale wanafunzi wakaenda zao tena nyumbani kwao.

11 Lakini Mariamu alikuwa akisimama karibu na kaburi, nje yake, analia. Basi akilia hivi, aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi.

12 Akaona malaika wawili, wenye mavazi meupe, wameketi, mmoja kichwani na mmoja miguuni, hapo ulipolazwa mwili wake Yesu.

13 Nao wakamwambia, Mama, unalilia nini? Akawaambia, Kwa sababu wamemwondoa Bwana wangu, wala mimi sijui walikomweka.

14 Naye akiisha kusema hayo, akageuka nyuma, akamwona Yesu amesimama, asijue ya kuwa ni Yesu.

15 Yesu akamwambia, Mama, unalilia nini? Unamtafuta nani? Naye, huku akidhania ya kuwa ni mtunza bustani, akamwambia, Bwana, ikiwa umemchukua wewe, uniambie ulipomweka, nami nitamwondoa.

16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu)”.

Hivyo baada ya kumtokea Mariamu Magdalena ndipo akamtokea Simoni Petro, katika tukio ambalo halijarekodiwa katika Biblia.

Kwahiyo Simoni Petro alikuwa ni Mtume wa kwanza kutokewa na Bwana YESU lakini si mtu wa kwanza, aliyekuwa wa kwanza ni Mariamu Magdalena na Simoni Petro anasimama kuwa wa kwanza kati ya Mitume wa Bwana.

Mtume Paulo analiweka hilo vizuri zaidi..

1Wakorintho 15:4 “na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko;

5 na ya kuwa ALIMTOKEA KEFA; tena na wale Thenashara;

6 baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano pamoja; katika hao wengi wanaishi hata sasa, ila baadhi yao wamelala;

7 baadaye akamtokea Yakobo; tena na mitume wote;

8 na mwisho wa watu wote, alinitokea mimi, kama ni mtu aliyezaliwa si kwa wakati wake”.

Je umempokea YESU?.. Unao uhakika wa kwenda naye mawinguni atakaporudi?… fahamu kuwa tunaishi majira ya siku za mwisho, siku yoyote parapanda ya mwisho inalia na wafu waliokufa katika Kristo watafufuliwa kuungana na walio hai katika Kristo na kunyakuliwa juu, je utakuwa wapi siku hiyo?, ikiwa leo habari ya msalaba kwako ni upuuzi mtupu!.

Neema ya Bwana YESU itusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mariamu Magdalene ni nani. Na hilo jina amelitolea wapi?

MAMBO YA KUJIFUNZA KWA KLOPA NA MKE WAKE!

Nyongeza ya majina ya watu katika biblia

MUONEKANO MPYA WA YESU BAADA YA KUFUFUKA.

UFUFUO WA UZIMA NA WA HUKUMU.

Print this post

ONDOA UDANGANYIFU KATIKA MAISHA YAKO.

Jina la Mwokozi YESU libarikiwe.

Wakati Fulani Bwana YESU aliuona “Mtini” (yaani mti unaozaa matuna aina ya Tini) usio na matunda na matokeo yake aliulaani.

Mathayo 21:18 “Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa.

19 Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; AKAUAMBIA, YASIPATIKANE MATUNDA KWAKO TANGU LEO HATA MILELE. MTINI UKANYAUKA MARA.

20 Wanafunzi walipoona, walistaajabu, wakisema, Jinsi gani mtini umenyauka mara?”

Sasa ukifuatilia vizuri hii habari utaweza kufikiri kwamba  Bwana YESU alikuwa anaweza kuwa amekosea kuulani.., kwani ule mtini haukuwa msimu wake wa kuzaa matunda…

Hata wewe ukienda kutafuta machungwa kwenye mchungwa nje na msimu wake ni wazi kuwa hutashangazwa pale utakapokuta ule mchungwa hauna tunda lolote.Zaidi sana utashangazwa kama endapo umefika msimu halafu hukukuta machungwa.. Lakini sasa tunasoma Bwana YESU ilikuwa kinyume chake alijua kabisa si msimu wake Mtini kuzaa lakini aliulaani hivyo hivyo.

Sasa kwanini aulaani??

Sababu zipo nyingi, lakini hii yaweza kuwa kuu kuliko zote… ULE MTINI ULIONYESHA SIFA ZOTE  ZA NJE  KUWA NA MATUNDA lakini haukuwa na matunda! (Maana yake ulikuwa unahubiri udanganyifu).

Unaonaje  umewekewa bahasha tatu mbele yako, halafu kati ya hizo bahasha tatu mbili zinaonekana kabisa kwa macho kuwa ndani hazina kitu, lakini moja inaonekana imetuna (kana kwamba ina fedha), halafu unaichagua hiyo iliyotuna kisha ndani unakuta hamna kitu, bila shaka utakwazika na unaweza ukaichana ile bahasha, ili isiendelee kudanganya wengine.

Vivyo hivyo Kristo alijua kabisa ule si wakati wa Tini kwani mitini mingine  yote ilikuwa na sifa zinazofanana kwa wakati huo, lakini ajabu ni kwamba huu Mtini mmoja ulikuwa na mwonekano wa tofauti kana kwamba unao matunda, pengine wakati mitini mingine ilikuwa imekauka inapukutisha huu ulikuwa na majani mabichi, ulikuwa unahubiri udanganyifu kwamba unao matunda na kumbe hauna, na ili kuondoa udanganyifu huo suluhisho ni kukatwa/kulaaniwa.

Naam na maisha ya wakristo wengi yamejaa UDANGANYIFU, ni kama wanasifa zote za kuitwa wakristo lakini ukichunguza kwa undani hawana matunda!. Kwa nje wana majina ya kikristo, ni wahubiri,  wana biblia nzuri na kubwa, wana nafasi katika kanisa, lakini ndani si wakristo, hawana matunda!, ni watu vuguvugu wale Bwana aliosema atawatapika katika Ufunuo..

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi”.

Toka katika uvuguvugu, ili kuepuka laana ya KRISTO, kama umekusudia kuwa Moto, kuwa Moto mpendwa, kama umeamua kuchagua baridi maandiko yanasema ni heri uwe baridi kabisa kuliko kuwa hapo katikati, vuguvugu..

Bwana YESU atusaidie sana.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Tafsiri ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;

Je Bwana YESU alipanda mlimani na wanafunzi wake baada ya siku sita au nane?

MWISHO WA MAVUNO, NI MWISHO WA DUNIA.

Biblia unapozungumzia kuhusu kupewa jina jipya inamaanisha nini?

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Print this post

Kuota unaongea na mchungaji maana yake ni nini?

Ili kuelewa maana ya ndoto yako, jambo la kwanza ni kujiuliza ni kwanini awe mchungaji, na si mwalimu wako, au boss wako, au rafiki yako, au ndugu yako au mtu mwingine yoyote?

Ukiwaza hivyo, tendo linalofuata ni kujua kazi ya mchungaji hasa ni nini?

Mshauri:

Mchungaji ni mwakilishi wa Mungu na hivyo anafanya kazi ya kutoa mashauri bora ya kiroho kwa mafundisho sahihi (Tito 1:7-9):  Kuonyesha kuwa maisha yako yanahitaji hekima ya ki-Mungu kukuongoza, zaidi ya hekima yako mwenyewe. Kila jambo au uamuzi unaojitokeza kwenye maisha yako, mshirikishe kwanza Mungu kimaombi, kisha angalia kwenye biblia jambo hilo Mungu analiagizaje, ikiwa si rahisi kutatulika, basi ni vema ukamshirikisha kiongozi wako wa kiroho kukusaidia.

Kutoa Maonyo:

Wachungaji pia wamepewa mamlaka ya kutoa maonyo kwa kondoo wao.

2Timotheo 4:2 lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho

Angalia pengine katika maisha yako Mungu anakuonya / anakutahadharisha katika jambo Fulani, ambalo sio sawa unalotaka kulifanya. Hivyo zingatia sana pia hilo.

Kufariji:

Kazi ya wachungaji ni kuwalinda, kuwafariji na kuwainua waliokata tamaa. Mfano wa Yesu kristo mwokozi wetu, na faraja yetu, aliyemchungaji mkuu (Mathayo 11:28, Zab 23). Hivyo Mungu anakuonyesha kuwa yupo na wewe katika safari yako, kukuchunga, usiogope.

Lakini sababu nyingine ya mwisho (ambayo si kubwa): Yaweza kuwa ni wazo la ki-akili. Kwasababu kumbuka si ndoto zote hutoka kwa Mungu au kwa shetani, nyingine ni wazo la bongo zetu, kufuatana na mazingira yanayotuzunguka (Mhubiri 5:3). Kwamfano ikiwa mara nyingi unakuwa karibu na mchungaji wako, kuota unaongea naye mara kwa mara, itakuwa ni jambo la kawaida. Au mtu ni mpishi, kujiona yupo jikoni mara kwa mara anapika litakuwa ni jambo kawaida kabisa kwake.

Hivyo kwa ufupi ni kuwa kuota unaongea na mchungaji wako, si ndoto mbaya, bali kwa asilimia kubwa ni ya ki-Mungu. Inategemea zaidi na maudhui yake. Hakikisha tu unapiga magoti na kuomba Bwana akufunulie ni eneo lipi hasaa, ndoto yako imeegemea ukilinganisha na maisha yako, na lile eneo ambalo unaona lina uzito zaidi basi ujue hapo ndipo Mungu anasema nawe hapo. Chukua hatua.

Je! Umeokoka?

Unafahamu kuwa hizi ni siku za mwisho na Yesu amekaribia sana kurudi? Ikiwa ni la! Basi muda ndio huu, mgeukie Kristo akuoshe dhambi zako, akupe uzima wa milele bure. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa, fungua hapa kwa msaada wa kuongozwa sala ya toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>  KUONGOZWA SALA YA TOBA

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kuota unavua samaki, kunamaanisha nini?

Kuota unakemea mapepo/ unashindana na nguvu za giza.

Kuota unapigana na mtu.

Print this post

YESU NI ALFA NA OMEGA .

Jina kuu la BWANA WETU YESU KRISTO Libarikiwe, karibu tuyatafakari maandiko.

Endapo akitokea mtu faulani mkuu sana  na kujigeuza na kujifanya mtumwa, na kuvaa nguo za chini ya hadhi yake, mtu huyo ni rahisi kupitia dharau kama watu wengine wa hadhi za chini, na kejeli, na hata kupitia mateso na kukataliwa….lakini laiti watu wanaomdharau wangemjua  kwa undani ni mtu wa namna gani, hakuna hata mmoja angeonyesha kejeli au dharau!.. wote wangemheshimu na kumwogopa!.

Ni hivyo hivyo kwa Bwana YESU, walimsulibisha lakini hawakujua yeye ni nani,  walidhani ni mwalifu tu, au mfano tu wa manabii wengine waliopita, kumbe! Hawakujua kuwa ni ALFA na OMEGA mwenyewe!. Naam hata mimi pengine ningekuwepo kipindi hiko, ningefanya hapo hayo! Kwasababu wanadamu sisi ni wale wale hatuna jipya!.

1Wakorintho 2:7 “bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu;

8 ambayo wenye kuitawala dunia hii hawaijui hata mmoja; maana kama wangaliijua, wasingalimsulibisha Bwana wa utukufu”.

Baada ya kuyatafakari hayo..hebu shika biblia yako ufuatilia maandiko yafuatayo maana leo utajua ya kwamba YESU KRISTO ni MUNGU mwenyewe katika MWILI wa kibinadamu!!?..na si mtu wa kawaida!.

Sasa si kwamba ukiishia kuamini tu ni Mwana wa MUNGU utakuwa umepotea!..la ni sahihi na ndio msingi!, lakini zaidi ya hapo, YESU ni zaidi ya tunavyomfikiria, ni jambo gumu kulielewa lakini unapolielewa linakuwa ni tamu na zuri..

Hebu tuyapeleleze maandiko kidogo kumhusu yeye katika kitabu cha Ufunuo..

Ufunuo 1:8 “Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi”.

Hapa MUNGU aliyeumba Mbingu na Nchi anajitambulisha kama Alfa na Omega!.. hapana shaka juu ya hilo, lakini hebu tuendelee mbele kidogo kumsoma huyu Alfa na Omega anaendelea kusemaje…

Ufunuo 21:5 “Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.

6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. MIMI NI ALFA NA OMEGA, MWANZO NA MWISHO. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.

7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu”.

Hapa tena huyu MUNGU wa mbingu na nchi ambaye ndiye ALFA na OMEGA, (yaani mwanzo na mwisho) anasema atayafanya yote kuwa mapya na atampa kila mwenye kiu ya maji ya uzima bure!.. Bila shaka hiyo ni karama ya MUNGU na njema sana… Lakini hebu tusogee tena mbele tumwone huyu ALFA na OMEGA anasema nini tena na anajizungumziaje..hapa ndipo tutashangaa!!.

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13 MIMI NI ALFA NA OMEGA, MWANZO NA MWISHO, WA KWANZA NA WA MWISHO.

14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.

15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.

16 MIMI YESU NIMEMTUMA MALAIKA WANGU kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi”.

Mstari wa 12 unaosema “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami,” na ule wa 16 unaosema “MIMI YESU NIMEMTUMA MALAIKA WANGU kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa.”… Mistari hii inatupa uzito kuendelea kumfikri YESU kama mtu wa kawaida, lakini inatulazimisha kumfikiri kama ALFA na OMEGA, kwamaana ndivyo alivyojitambulisha hapo.

Oo kumbe! YESU ni Alfa na Omega, na ndiye Mungu mwenyezi katika umbile la kibinadamu, sasa tunaelewa kwanini Mtume Paulo alisema siri ya UTAUWA (yaani Uungu) ni KUU, kwamba MUNGU alidhihirishwa katika mwili..

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.

Hayo maneno kwamba “Mungu alidhihirishwa katika mwili, na akachukuliwa juu katika utukufu” yanatufanya tufikiri mara mbili mbili kuwa YESU ni nani?.. Naam hata Bwana YESU mwenyewe kuna wakati aliwalazimisha watu kumfikiri yeye mara mbili mbili kuwa ni nani… Labda utauliza ni wapi hapo katika maandiko, twenda pamoja..

Mathayo 22:42 “Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi.

43 Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema,

44 Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako?

45 Basi, Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe?

46 Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu ye yote tangu siku ile kumwuliza neno tena”

Hawa walikuwa wanamjua Masihi (YESU) kama mwana wa Daudi, na ni kweli maandiko yamesema hivyo, lakini sasa inakuwaje Daudi amwite Masihi kama Bwana wake na wakati huo huo awe mtoto wake??.. hata mimi ningeulizwa hilo swali, ningekwama!..

Maana yake kuna siri nyingine katika YESU tusizozijua, ambazo ukisoma maandiko kwa makini na kwa msaada wa Roho Mtakatifu utaziona!..

Sasa si dhambi kujua kama YESU ni mwana wa Daudi peke yake, wala si kosa kutambua kuwa ni Mwana wa MUNGU peke yake, na hiyo haiwezi kumtolea mtu tiketi ya kuingia mbinguni, lakini maandiko yanathibitisha kuwa YESU KRISTO ni zaidi ya tunavyomjua au kumfikiri, kama YEYE ni MUNGU MWENYEWE KATIKA MWILI..NUKTA KUBWA!!!.

Huenda Lugha zetu za duniani na udhaifu wetu wa kufikiri unakuwa ni mgumu kupokea hilo!, lakini huo ndio ukweli na ni lazima tuupokee, kama tu ilivyo ngumu kufikiri na kupokea kwamba inakuwaje MUNGU hana mwanzo!.. hapo ukifikiri sana unakwama!, lakini unaamini hivyo hivyo kwasababu yeye ni MUNGU, vile vile kuhusu UUNGU wa YESU usiumize kichwa kutafuta kulifanya lieleweke kichwani mwako sasa, labda tutaelewa vizuri baada ya maisha haya, lakini hatuna budi kuamini hilo!.

Na kumwelewa YESU namna hii inatufanya tusiuchezee Wokovu wetu, maana hatujakombolewa na damu ya mtu, wala myahudi bali ya MUNGU mwenyewe!.

Kwa maarifa ya ziada Kuhusu Uungu wa YESU zaidi pitia Tito 2:13, na Isaya 9:6

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je Yesu ni Mungu au Nabii?

MJUE SANA YESU KRISTO.

Je Mariamu alikuwa na umri gani alipochukua mimba ya Bwana YESU?

MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.

KAMA SI YESU, HABARI YETU INGEKUWA IMEISHA ZAMANI SANA.

Print this post