Category Archive Home

UFUNUO: Mlango wa 17

Karibu tujifunze kitabu cha Ufunuo leo tukiwa katika mwendelezo wetu wa sura ya 17, Biblia inasema…

Ufunuo 17:1-6″
1 Akaja mmoja wa wale malaika saba, wenye vile vitasa saba, akanena nami, akisema, Njoo huku, nitakuonyesha hukumu ya yule kahaba mkuu aketiye juu ya maji mengi;

2 ambaye wafalme wa nchi wamezini naye, nao wakaao katika nchi wamelevywa kwa mvinyo ya uasherati wake.

3 Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi.

4 Na mwanamke yule alikuwa amevikwa nguo ya rangi ya zambarau, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake.

5 Na katika kipaji cha uso wake alikuwa na jina limeandikwa, la siri, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI.

6 Nikamwona yule mwanamke amelewa kwa damu ya watakatifu, na kwa damu ya mashahidi wa Yesu. Nami nilipomwona nikastaajabu ajabu kuu.

Tukirudi nyuma kidogo kwenye ile sura ya 13, tunamwona yule mnyama aliyetoka baharini mwenye vichwa saba na pembe 10, akielezewa, jambo hilo hilo tunaliona tena katika hii sura ya 17 mnyama yule yule mwenye vichwa 7 na pembe 10 na majina ya makufuru ametokea tena, isipokuwa hapa katika sura hii ya 17 tunaona kuna jambo lingine limeongezeka; anaonekana MWANAMKE  AKIWA AMEKETI JUU YAKE.

 Kwahiyo msisitizo mkubwa katika sura hii ni juu ya huyo mwanamke aliyepambwa kwa dhahabu, lulu na vito vya thamani aliyeketi juu ya huyo mnyama.

Sasa mwanamke huyu ni nani?

Mwanamke katika biblia anawakilisha KANISA, Sisi wakristo tunatambulika kama BIBI-ARUSI wa KRISTO,(2Wakoritho 11:2 Paulo anasema “..Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo BIKIRA SAFI. “) Na pia..

Ufunuo 19:7 inasema..” Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na MKEWE amejiweka tayari. Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu.  Pia Taifa la Israeli Bwana alilitambua kama MKE WAKE” [soma ezekieli16:1-63, ezekieli 23] utaona jambo hilo. Hivyo mahali popote Mungu anapozungumza juu ya kundi la watu wake huwa analifananisha na mwanamke.

Lakini hapa tunaona mwanamke mwingine ametokea ambaye anaonekana ni KAHABA,  amelewa kwa DAMU za watakatifu na za mashahidi wa YESU, na tena wafalme wa nchi wamezini naye, nao wakaao katika nchi wamelevywa kwa mvinyo ya uasherati wake.  Na katika kipaji cha uso wake ana jina limeandikwa, la SIRI, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI.

Hivyo tunaona tabia ya huyu mwanamke (ambaye anawakilisha KANISA fulani) kuwa ni KAHABA, Na kama tunavyofahamu kanisa la KRISTO haliwezi kuwa kahaba, kwasababu ni BIKIRA SAFI, na haliwezi kuua watakatifu wa Mungu, kwasababu lenyewe ni TAKATIFU, Hivyo hili Kanisa haliwezi kuwa lingine zaidi ya KANISA KATOLIKI chini ya uongozi wa PAPA.

Kwanini ni Kanisa  KATOLIKI na si kitu kingine?

Tunajua siku zote shetani anatabia ya kuunda “copy” inayofanana na ya Mungu ili aabudiwe kirahisi, au kudanganya watu kirahisi, vinginevyo asingeweza kupata wengi, ili noti feki iweze kufanya kazi ni lazima ifanane sana na orijino, shetani anataka kuabudiwa kama Mungu hivyo atatumia njia zote zinazofanana na za Mungu  ili apate wafuasi wengi. Na ndio maana Mungu alikataza Mtu kutengeneza mfano wa Kitu chochote kama Mungu ili kukiabudu kwasababu mtu anaweza akadhani anamwabudu Mungu kumbe anamwabudu shetani mwenyewe kwa kivuli cha ile sanamu pasipo kujua.ZIKIMBIE IBADA ZA SANAMU. Mimi sipo kinyume na wakatoliki, wala siwahukumu ndugu zangu wakatoliki, bali nipo kinyume na mifumo ya kanisa Katoliki kwasababu Mungu alishaihukumu, na kupiga mbiu watu wake watoke huko wasishiriki mapigo yake!.

Sasa mpango wa Mungu aliouunda tangu awali ni kumleta “MTU” atakayesimama kwa niaba yake ili kuwakomboa wanadamu (VICAR) katika dhambi zao hivyo akamleta mwanae anayeitwa YESU KRISTO, ambaye kwetu sisi ni Mungu mwenyewe katika mwili..shetani kuona hivyo akaanza kuiga kwa kumtengeneza mtu wake (VICAR), ambaye naye atasimama kwa niaba yake hapa duniani, na akampa jina lililo maarufu (VICARIUS FILII DEI) yaani tafsiri yake,  ni “Badala ya mwana wa Mungu duniani”, hivyo huyu mtu wake anasimama hapa duniani badala ya mwana wa Mungu (yaani YESU KRISTO), na  shetani akamvika uwezo wake bandia kwamba na yeye anaweza kusamehe dhambi duniani kama vile BWANA WETU YESU KRISTO alivyo na uwezo wa kusamehe dhambi.

Na kama vile Mungu alivyounda kanisa lake takatifu kwa kupitia BWANA YESU KRISTO, ambalo ndilo linaloitwa BIBI-ARUSI safi, vivyo hivyo shetani naye alilitengeneza Kanisa lake kwa kupitia huyu (VICARIUS FILII DEII) yaani PAPA, Kutimiza kusudi lake la kutaka kuabudiwa na kupeleka watu kuzimu na hilo KANISA  ndilo KAHABA, Na si lingine zaidi ya KANISA KATOLIKI. 

Na tunajua Kanisa la Kristo safi linaongozwa na ROHO MTAKATIFU kwa kupitia zile huduma na karama za roho, yaani mitume, manabii,wachungaji, wainjilisti na waalimu lakini hili kanisa kahaba na lenyewe limevuviwa vyeo vya uongozi  kama Upapa, Ukadinali, upadre, paroko, ukasisi n.k.

Kwahiyo unaweza ukaona ni jinsi gani cha uongo kinavyofanana na cha ukweli, na watu wengi wamepofushwa macho na shetani wakidhani kuwa wanamwabudu Mungu hapo kumbe ni shetani.

Na ni kwasababu gani ni kahaba?

Ni kahaba kwasababu biblia inasema wafalme wa nchi wamezini naye nao wakaao katika nchi wamelevywa kwa mvinyo wa usherati wake, si ajabu Kanisa hili lina nguvu nyingi katika mataifa mengi kwa utajiri wake kwa jinsi linavyotoa misaada na miradi mingi ya kimaendeleo na ya kijamii, linajenga mashule na mahospitali linatoa misaada ya majanga na kusapoti siasa za nchi, linafanya hivi kwa lengo moja tu! kupumbaza mataifa na wafalme wa nchi ili kuwalewesha kwa kupenyeza mafundisho na itikadi zake za uongo kwa watu ambazo zipo nje ya MANENO MATAKATIFU YA MUNGU.

Na ndio maana tunaona mwanamke huyu ana jina limeandikwa kwa SIRI katika kipaji cha uso wake “BABELI MKUU MAMA WA MAKAHABA, NA MACHUKIZO YA NCHI”..Umeona hapo, jina lake lipo katika SIRI, hivyo inahitaji HEKIMA kumtambua, kwasababu shetani huwa hafanyi vitu vyake kwa wazi wazi, anatumia kivuli cha “orijino” ili kuwadanganya watu.

Ni BABELI mkuu kwasababu tafsiri yenyewe ya neno BABELI ni “MACHAFUKO”, Hivyo Mji wa Babeli ndio ulikuwa chimbuko la machafuko yote, ibada za kipagani za kuabudu miungu mingi na uchawi ndipo zilipozaliwa, Nimrodi akiwa muasisi wa mji ule na mke wake Semiramis pamoja na mtoto wao Tamuzi, waliabudiwa kama miungu, ndipo baadaye Waroma wakaja kutohoa mfumo huo wa kuabudu miungi mingi, na sio ajabu tunaona baadaye wakaja kumweka Yosefu kama Nimrodi, Semiramis kama Mariam na Tamuz kama mtoto YESU ili kutimiza matakwa yao ya ibada zao za sanamu ambazo walikuwa nazo tangu zamani, kwakweli haya ni machafuko makubwa sana katika KANISA LA KRISTO.

Na mji huu huu wa Babeli baadaye ndio uliohusika kuutesa na kuuchukua uzao wa Mungu (ISRAELI) mateka, sasa hii ilikuwa ni Babeli ya mwilini iliyolichukuwa Taifa la Israeli mateka sasa hii iliyopo leo ni  BABELI YA ROHONI(ambayo ni kanisa Katoliki ) inawachukua wakristo wengi mateka kwa kuwafanya waabudu miungu mingine mbali na YAHWE  YESU KRISTO MUNGU WETU. 

Lakini Biblia inasema hakika BABELI HII ya sasa itaangushwa tu! kama ilivyoangushwa ile ya kwanza ya mwilini. Nadhani kuanzia hapo utakuwa umeanza kupata picha ni kwanini mwanamke yule anajulikana kama BABELI MKUU. Sasa tuone ni kwa nini anaitwa “MAMA WA MAKAHABA”.

Ni Mama wa makahaba kwasababu amezaa wabinti ambao nao pia ni makahaba kama yeye na si mengine zaidi ya madhehebu yote yanayoshirikiana naye, wale waliokuwa wanajiita ma-protestants mwanzo  sasa hivi hawapo hivyo tena, wanashirikiana naye kwa namna zote. Kanisa Katoliki limefanikiwa kuwalewesha na kuwavuta tena kwake, lutheran imeshaungana na katoliki rasmi, pamoja na madhehebu mengine mengi,na ndio maana linaitwa “KANISA MAMA”. Sasa ni rahisi kuelewa hapo kwanini ni “MAMA WA MAKAHABA”..Kwasababu yeye ameshakuwa kanisa mama, na mabinti wake wameshafuata mifumo yake ya ibada zisizotokana na NENO la Mungu.

Na ni kwanini ni “Mama wa Machukizo ya nchi”?.

Hili kanisa lenyewe ndio linalohusika na machukizo yote ya nchi yanayovuta ghadhabu yote ya Mungu juu ya nchi, kama ya kuwauwa watakatifu wa Mungu, kimwili na kiroho, kwa ibada zake za sanamu, kanisa hili limeua zaidi ya wakristo milioni 68 katika historia hiyo ni idadi kubwa sana, hata Bwana YESU  alishatabiri juu yao alisema..Yohana 16:1-3″Maneno hayo nimewaambia, msije mkachukizwa. Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania KILA MTU AWAUAYE YA KUWA ANAMTOLEA MUNGU IBADA. Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi. ” 

Hiyo ndio sababu ya yule mwanamke kuonekana amelewa kwa damu za watakatifu ..Haya yote ni machukizo makuu mbele za Mungu, na yule  mpinga-kristo atakayetokea huko ndiye atakayelisimamisha lile CHUKIZO LA UHARIBIFU lililotabiriwa na nabii Daneli na BWANA wetu YESU KRISTO, ndio  maana anajulikana kama “MAMA WA MACHUKIZO YA NCHI”.

SIRI YA YULE MNYAMA.

Tukiendelea Ufunuo 17:7-18 “7 Na yule malaika akaniambia, Kwani kustaajabu? Nitakuambia siri ya mwanamke huyu, na ya mnyama huyu amchukuaye, mwenye vile vichwa saba na zile pembe kumi.

8 Yule mnyama uliyemwona alikuwako, naye hayuko, naye yu tayari kupanda kutoka kuzimu na kwenda kwenye uharibifu. Na hao wakaao juu ya nchi, wasioandikwa majina yao katika kitabu cha uzima tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, watastaajabu wamwonapo yule mnyama, ya kwamba alikuwako, naye hayuko, naye atakuwako.

9 Hapo ndipo penye akili zenye hekima. Vile vichwa saba ni milima saba anayokalia mwanamke huyo.

10 Navyo ni wafalme saba. Watano wamekwisha kuanguka, na mmoja yupo, na mwingine hajaja bado. Naye atakapokuja imempasa kukaa muda mchache.

11 Na yule mnyama aliyekuwako naye hayuko, yeye ndiye wa nane, naye ni mmoja wa wale saba, naye aenenda kwenye uharibifu

12 Na zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme kumi, ambao hawajapokea ufalme bado, lakini wapokea mamlaka kama wafalme muda wa saa moja pamoja na yule mnyama.

13 Hawa wana shauri moja, nao wampa yule mnyama nguvu zao na mamlaka yao.

14 Hawa watafanya vita na Mwana-Kondoo, na Mwana Kondoo atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Mabwana, na Mfalme wa Wafalme, na hao walio pamoja naye ndio walioitwa, na wateule, na waaminifu.

15 Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha.

16 Na zile pembe kumi ulizoziona, na huyo mnyama, hao watamchukia yule kahaba, nao watamfanya kuwa mkiwa na uchi, watamla nyama yake, watamteketeza kabisa kwa moto.

17 Maana Mungu ametia mioyoni mwao kufanya shauri lake, na kufanya shauri moja, na kumpa yule mnyama ufalme wao hata maneno ya Mungu yatimizwe.

18 Na yule mwanamke uliyemwona, ni mji ule mkubwa, wenye ufalme juu ya wafalme wa nchi. “

Hapa pia tunaona Yohana anaonyeshwa siri ya yule mnyama ambaye ndio yule yule aliyeonyeshwa katika ile sura ya 13 ambaye ana vichwa 7 na pembe 10, isipokuwa hapa zile pembe 10 zinaonanekana hazina vilemba ikiwa na maana hazijapokea ufalme bado, na ndio maana tukisoma mstari wa 12 inasema watakuja kupokea ufalme(yaani kuvikwa vilemba) saa moja na yule mnyama.

Kumbuka vile vichwa saba vya mnyama, ni FALME 7, ambazo shetani alizikalia kuutesa au kutaka kuungamiza kabisa uzao wa Mungu, ambazo ni 1) MISRI   2)ASHURU  3)BABELI   4)UMEDI & UAJEMI  5) UYUNANI   6)  RUMI-ya-KIPAGANI   7) RUMI-ya KIPAPA…

kwa maelezo marefu juu ya huyu mnyama kama anavyoonekana kwenye sura 13 fungua hapa >> UFUNUO: Mlango wa 13

Lakini tunaona hapo wakati Yohana anaonyeshwa maono hayo aliona watano wameshakwisha anguka, na mmoja yupo na mwingine hajaja bado. Kumbuka wakati ule Yohana anapewa haya maono  AD 90 ,utawala uliokuwa unaitawala dunia wakati ule  ni RUMI ya kipagani, kwahiyo zile tawala tano za kwanza zilikuwa  zimeshapita yaani Misri, Ashuru, Babeli, Umedi&uajemi pamoja na Uyunani. Hivyo ule wa Urumi ndio uliokuwepo na ndio ule uliomsulibisha KRISTO.

Na kama alivyoambiwa mmoja bado hajaja(ambaye ni wa 7), Na kwamba atakapokuja itampasa akae muda mchache, sasa  huo  si mwingine bali ni ule utawala wa RUMI ya kidini chini ya upapa ulioongoza dunia nzima kuanzia kile kipindi cha karne ya 4, ni ule ule tu wa RUMI sema hapa umegeuka ukawa wa kidini chini ya upapa.

Tukiendelea kusoma mstari wa 11 inasema..” Na yule mnyama aliyekuwako naye hayuko, yeye ndiye wa nane, naye ni mmoja wa wale saba, naye aenenda kwenye uharibifu.”.Hivyo tunaona mnyama mwingine wa 8 anajitokeza hapo, lakini biblia inasema huyu wa 8 ndio yule yule wa 7, hii ikiwa na maana kuwa ni kile kile kichwa cha saba isipokuwa kimebadilisha taswira, kwasababu yule mnyama tayari anavyo vichwa saba hawezi akawa tena na vichwa nane,

Na huyu mnyama wa 8 biblia inasema ambaye alikuwako naye hayupo naye anaenda kwenye uharibifu, tukirudi kwenye historia tunamwona  huyu mnyama (ambaye ndio kile kichwa cha 7 -Rumi ya kidini chini ya Upapa wa Kanisa Katoliki) ulikuwa na nguvu kipindi kile cha utawala wake, lakini baadaye ulikuja kutiwa jeraha la mauti na wale wanamatengezo, hivyo nguvu zake za kutawala dunia nzima zilikufa, lakini tunaona lile jeraha lilianza kupona tena, kuanzia kile kipindi cha vita vya pili vya dunia mpaka leo linaendelea kupona, utakapofika wakati atakaporejeshewa nguvu zake tena alizopoteza ndipo atakapoingia katika UHARIBIFU, naye ataitawala dunia kwa kipindi kifupi cha miaka mitatu na nusu ndio kile kipindi cha dhiki kuu, ndio maana biblia inasema alikuwepo naye hayupo, naye anajiandaa kwenda kwenye uharibifu. Kwasababu hapo mwanzo alishawahi kutawala na atakuja kutawala tena.

Sasa Zile pembe 10 za yule mnyama ambayo ni yale mataifa 10 ya ULAYA(EU), Biblia inasema  yatakuja kupata nguvu wakati mmoja na yule mnyama. Na haya ndiyo mpinga-kristo PAPA atakayoyatumia kuwatesa wale ambao hawataipokea chapa ya mnyama katika kile kipindi cha dhiki kuu.

Lakini mstari 16 tunaona jambo lingine..” Na zile pembe kumi ulizoziona, na huyo mnyama, hao watamchukia yule kahaba, nao watamfanya kuwa mkiwa na uchi, watamla nyama yake, watamteketeza kabisa kwa moto.” 

Mwisho wa yote baada ya dhiki kuu kukaribia kuisha yale mataifa 10 ya Ulaya yatagundua kuwa utawala wa mpinga-kristo(PAPA) Chini ya kanisa katoliki hauna manufaa yoyote wala haujasaidia chochote kutimiza matakwa yao, na suluhu zao za AMANI, sasa kwa pamoja yatamchukia yule mwanamke(yaani PAPA) na Makao yake VATICAN  na kumwangamiza kabisa, hiyo ndio HUKUMU ya YULE KAHABA MKUU kama mstari wa kwanza unavyosema.

” Akaja mmoja wa wale malaika saba, wenye vile vitasa saba, akanena nami, akisema, Njoo huku, nitakuonyesha hukumu ya yule kahaba mkuu aketiye juu ya maji mengi;”

Huo utakuwa ndio mwisho wa Utawala wa Upapa na Kanisa Katoliki, kwasababu makao makuu yake VATICAN yatakuwa yameshateketezwa, hukumu hii imeelezewa kwa urefu kwenye SURA YA 18, jinsi Babeli ulivyoanguka na kuwa ukiwa mfano wa ile Babeli ya kwanza ilivyokuwa.

Baada ya huyu mwanamke Babeli mkuu kuhukumiwa, sasa mstari wa 14 unasema. zile pembe 10 (yaani yale mataifa ya ulaya)” ndio yatafanya vita na Mwana-Kondoo, na Mwana Kondoo atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Mabwana, na Mfalme wa Wafalme, na hao walio pamoja naye ndio walioitwa, na wateule, na waaminifu.” Kumbuka hii itakuwa ndio ile vita ya MUNGU MWENYEZI yaani “HARMAGEDONI”  inayozungumziwa kwenye ufunuo 16:16.

Ufunuo 18:1-5″

1 Baada ya hayo naliona malaika mwingine, akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka kuu; na nchi ikaangazwa kwa utukufu wake.

2 Akalia kwa sauti kuu, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli ule mkuu; umekuwa maskani ya mashetani, na ngome ya kila roho mchafu, na ngome ya kila ndege mchafu mwenye kuchukiza;

3 kwa kuwa mataifa yote wamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa nchi wamezini naye, na wafanya biashara wa nchi wamepata mali kwa nguvu za kiburi chake.

4 Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni, ikisema, TOKENI KWAKE, ENYI WATU WANGU, MSISHIRIKI DHAMBI ZAKE, WALA MSIPOKEE MAPIGO YAKE.

5 Kwa maana dhambi zake zimefika hata mbinguni, na Mungu amekumbuka maovu yake.”

Hivyo ndugu unaona ni HATARI! gani  iliyo mbele yetu?, ni wazi kabisa muda umeshaisha Yule mnyama siku yoyote anaingia katika uharibifu, kumbuka wakati huo kanisa ambaye ni BIBI-ARUSI safi atakuwa ameshanyakuliwa, bibi-arusi asiyeabudu sanamu, bibi-arusi aliyebikira kwa NENO tu na sio pamoja na mapokeo mengine yaliyo nje na NENO LA MUNGU Kama kusali Rosari na ibada za wafu. Bibi-arusi Anayemwabudu Mungu katika Roho na kweli  sio katika mifumo ya ki-DINI  na ya-kimadhehebu, Bibi-arusi aliyepokea kweli ubatizo wa Roho Mtakatifu, na kama tunavyofahamu asili ya bibi-arusi ni kuvaa vazi refu la kujisitiri, je! na wewe mwanamke mavazi yako ni ya kujisitiri?, Utakuwa mkristo na bado uwe  kahaba kwa mavazi unayovaa? kumbuka fashion zote ni dhambi! lipstic,vimini, wigy,suruali, wanja nk. vitakupeleka kuzimu mwanamke.

BWANA YESU ANASEMA…

12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.

14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.

15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, NA HAO WAABUDUO SANAMU, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.

16 Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi.

17 NA ROHO NA BIBI-ARUSI WASEMA, NJOO!  Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure.

TUBU ANGALI MUDA UPO.

Mungu akubariki. Kwa mwendelezo >>UFUNUO: Mlango wa 18

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara,  kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.


Mada zinazoendana…


MNARA WA BABELI

CHAPA YA MNYAMA

SIRI YA KUASI KATIKA KANISA LA MUNGU.

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

NILIMWONA SHETANI, AKIANGUKA KUTOKA MBINGUNI.

UFUNUO: Mlango wa 18


Rudi Nyumbani

Print this post

UFUNUO: Mlango wa 15

Karibu tujifunze mwendelezo wa kitabu cha ufunuo, leo tukiendelea na sura ya 15;

Ufunuo 15:1-4 

1 Kisha nikaona ishara nyingine katika mbingu, iliyo kubwa, na ya ajabu; malaika saba wenye mapigo saba ya mwisho; maana Katika hayo ghadhabu ya Mungu imetimia.

2 Tena nikaona kitu kama mfano wa bahari ya kioo iliyochangamana na moto, na wale wenye kushinda, watokao kwa yule mnyama, na sanamu yake, na kwa hesabu ya jina lake, walikuwa wamesimama kando-kando ya hiyo bahari ya kioo, wenye vinubi vya Mungu.

3 Nao wauimba wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa.

4 Ni nani asiyekucha, Ee Bwana, na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako u Mtakatifu; kwa maana mataifa yote watakuja na kusujudu mbele zako; kwa kuwa matendo yako ya haki yamekwisha kufunuliwa.

Katika sura hii ya 15 tunaona Yohana akionyeshwa ishara nyingine kuu mbinguni kama vile alivyoonyeshwa kwenye ile sura ya 12 juu ya yule mwanamke aliyekuwa na utungu wa kuzaa ambaye tuliona anawakilisha taifa la Israeli, na ishara nyingine kuu aliyoonyeshwa mbinguni ni juu ya lile joka kubwa jekundu lililokuwa limejiandaa kummeza yule mtoto pindi atakapozaliwa, na huyu si mwingine zaidi ya shetani akipingana na YESU KRISTO na uzao wa Mungu.

Lakini katika sura hii ya 15 tunaona Yohana akionyeshwa ishara nyingine tena mbinguni iliyo kubwa na ya ajabu “malaika saba wenye mapigo saba ya mwisho; maana katika hayo ghadhabu ya Mungu imetimia.”

Hawa Malaika 7 wanaoonyeshwa hapa ndio wale watakaohusika katika kumimina vile vitasa 7 vya ghadhabu ya Mungu, kumbuka katika kipindi cha ile miaka mitatu na nusu ya mwisho kati ya ile saba, Mungu atamuhukumu yule KAHABA MKUU, (utawala wa mpinga-kristo chini ya Kanisa Katoliki ) kwa kupitia zile pembe 10 ambazo zitakuja kumchukia yule mwanamke na kumtowesha kabisa kama inavyoelezewa katika (ufunuo 16:10, pamoja na Ufunuo 17 & 18),

Sasa itakayofuata ni HUKUMU YA MATAIFA yote yaliyozini na huyu mwanamke kahaba Babeli mkuu, biblia inasema…

Ufunuo 14:9-11″ Na mwingine, malaika wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kuu, Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake,

10 yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo.

11 Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku, hao wamsujuduo huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina lake.

Hivyo hii HUKUMU YA MATAIFA itatekelezwa na Hawa malaika saba wenye mapigo saba ya mwisho ambayo katika hayo ghadhabu ya Mungu itatimia, na mapigo haya tunayaona yakitekelezwa katika sura inayofuata ya 16.

Tukiendelea mstari wa 2-4 tunaona Yohana akiona kitu kama mfano wa bahari ya kioo iliyochangamana na moto, na wale wenye kushinda, watokao kwa yule mnyama, na sanamu yake, na kwa hesabu ya jina lake, walikuwa wamesimama kando-kando ya hiyo bahari ya kioo, wenye vinubi vya Mungu.

Hii bahari ya kioo iliyochanganyikana na moto inaonyesha watakatifu waliosafishwa kwa moto (yaani waliopitia dhiki kuu), ndio maana ile bahari imeonekana kama imechanganyikana na moto, kama vile tunavyoona kwenye ufunuo 4:6 bahari nyingine ya kioo mfano wa bilauri na sio ya moto. Kwahiyo hawa ni watakatifu waliotoka kwa yule mpinga-kristo.

Na pia ukiendelea kusoma utaona wameshinda kutoka kwa yule mnyama na sanamu yake na hesabu ya jina lake, hawa ndio waliokataa kushirikiana na yule mnyama hivyo iliwapasa kutoa maisha yao, kwa ushuhuda wa Yesu Kristo. Kumbuka wakati huo unyakuo utakuwa umeshapita yule mwanamwali mwerevu atakuwa ameshaondoka(kwenye unyakuo), amebaki yule mpumbavu (ukisoma Mathayo 25 utaona jambo hilo), hivyo kwasababu ya upumbavu wake wa kutokuwa na mafuta ya ziada kwa kujiweka tayari kumlaki Bwana wake wakati ajapo, aliachwa!, kumbuka tayari alikuwa ni mwanamwali wa Bwana isipokuwa alikuwa ni mpumbavu, hivyo itambidi akumbane na ghadhabu ya mpinga-kristo ambayo asingepaswa apitie.

Wakati unyakuo unapita sio watu wote watafahamu, utakuwa ni wa siri, na ni wachache tu watakaonyakuliwa wala hakutakuwa na ajali, wala mshtuko wowote duniani maana watakuwa ni wachache sana, Bwana Yesu alisema kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu na kama ilivyokuwa katika siku za luthu, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake mwana wa Adamu, sasa jiulize? katika siku za Nuhu walipona watu wangapi? ni watu 8 kati ya mamilioni, siku za Luthu walipona wangapi? ni 3 kati ya mamilioni na Bwana Yesu anasema ndivyo itakavyokuwa katika siku za kuja kwake. Je! na wewe utakuwa miongoni mwa hao wachache watakaokwenda na Bwana katika Karamu yake?..

Mstari unaofuata unasema ..”3 Nao wauimba wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa.”

Hapo tunaona kuna aina mbili za nyimbo zikiimbwa 1) wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu ikiashiria watu wam Israeli watakaouawa kipindi hicho na mpinga-kristo kwa kukataa kumsujudia, 2) Wimbo wa mwana-kondoo ikifunua wakristo watakaouawa wakati wa dhiki kuu watakaokataa kuipokea ile chapa na kumsujudia. Kwahiyo hayo ni makundi mawili yatakayopitia dhiki kuu.

Tukiendelea mlango wa 15 kuanzia ule mstari wa 5 hadi wa 8 ambao ndio wa mwisho tunasoma habari ifuatayo.

Ufunuo 15:5-8

5 Na baada ya hayo nikaona, na hekalu la hema ya ushuhuda mbinguni lilifunguliwa;

6 na wale malaika saba, wenye mapigo saba, wakatoka katika hekalu, wamevikwa mavazi ya kitani safi, ya kung’aa, wamefungwa vifuani mwao mishipi ya dhahabu.

7 Na mmoja wa wale wenye uhai wanne akawapa wale malaika saba vitasa saba vya dhahabu, vimejaa ghadhabu ya Mungu, aliye hai hata milele na milele.

8 Hekalu likajazwa moshi uliotoka kwenye utukufu wa Mungu na uweza wake. Wala hapakuwa na mtu aliyeweza kuingia ndani ya hekalu, hata yatimizwe mapigo saba ya wale a malaika saba.

Hapa tunaona hekalu la hema la ushuhuda mbinguni likifunguliwa na kujazwa moshi uliotoka kwenye utukufu wa Mungu ikiwa na maana kuwa ni hukumu ya Mungu, kumbuka popote palipo na hekalu la Mungu au hema ya ushuhuda utukufu wa Mungu huwa unashuka kama “wingu” kuashiria neema na rehema za Mungu mahali hapo aliposhukia lakini hapa tunaona hekalu limejaa “moshi” ikiashiria ghadhabu na hukumu ya Mungu, na kama vile inavyosema wala hakuna mtu aliyeweza kuingia ndani ya hekalu mpaka yatimizwe yale mapigo ikionyesha kuwa mlango wa rehoema na neema mbaada ya haupo utakuwa umeshafungwa,

Na tunaona wale malaika saba walipewa vile vitasa 7 ili kumimina ghadhabu ya Mungu juu ya nchi ili kuleta mapigo yale yote Mungu aliyoyakusudia kwa wale wote waliomsujudia yule mnyama na kupokea chapa yake au hesabu ya jina lake. Katika kipindi hicho huruma Mungu haitakuwepo na watu wengi sana wataangamia. Kwa mwendelezo wa sura inayofuata ya 16 inayohusu juu ya ghadhabu ya Bwana ambayo ndio vile vitasa saba tutajifunza katika sura inayofuata…

Ndugu tunaishi katika muda wa nyongeza, na KARAMU YA MWANAKONDOO imekaribia, na watakaoshiriki ni wale watakaokwenda katika UNYAKUO TU!. Wakati wateule wa Mungu wanapokea thawabu zao na kuwa wafalme na makuhani wa Mungu milele, wewe nafasi yako saa hiyo itakuwa wapi?,

wakati watakatifu wanafutwa machozi yao na Bwana YESU wewe utakuwepo wapi?. Huu ni wakati wa kutengeza taa zetu na kujiweka tayari kwenda kumlaki Bwana, huu sio wakati wa kuambiwa uumpe Bwana maisha yako bali ni wakati wa KUFANYA IMARA UTEULE WAKO NA WITO WAKO(2petro 1:10), vinginevyo utakuwa mwanamwali mpumbavu ambaye alibeba TAA pasipo mafuta ya ziada,

Kumbuka chapa ya mnyama imeshaanza kufanya kazi, na inaanzia ndani kisha ije nje Kumalizia! na hii inatenda kazi katika madhehebu yote yaliyofanya uzinzi na kanisa kahaba KATOLIKI, ni mara ngapi unaambiwa biblia inasema hivi, wewe unasema dhehebu letu haliamini hivyo?, ni mara ngapi unaulizwa wewe ni mkristo unajibu mimi ni wa-dhehebu fulani? Je unadhani ni ROHO MTAKATIFU ndiye aliyeleta hiyo migawanyiko? jibu ni hapana shetani ndiye aliyeleta hiyo migawanyiko, na bila kujua hilo dhehebu lako lina ushirika kamili na lile kanisa mama kahaba na ndio tunaona lile jina MAMA WA MAKAHABA limezaliwa huko. Sasa kwa dizaini hii utaachaje kushawishika kuipokea ile chapa?..umeshaipokea tayari moyoni mwako kilichobaki ni udhihirisho wa nje tu! ambao hauna tofauti na ule wa ndani. Biblia inasema tokeni kwake enyi watu wangu wala msishiriki dhambi zake, kutoka sio kwa miguu tu, bali kutoka moyoni kwanza kwa kubadilisha namna ya kumwabudu Mungu, Mungu ni ROHO nao wamwabuduo imewapasa kumwabudu katika roho na kweli, na sio kwa kupitia sanamu, wala dhehebu wala papa wala bikira Mariamu, wala kwa mapokeo wala kwa mtu mwingine yoyote, bali katika roho na kweli (ndani ya YESU KRISTO).

Na pia Kumbuka kanisa tunaloishi sasa ni kanisa la mwisho linaloitwa LAODIKIA, na mjumbe wake ameshapita na ujumbe wetu tuliopewa na BWANA YESU KRISTO ni huu..

Ufunuo 3:15 Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.

19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.

20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. “

Umeona hapo?, hili ni kanisa vuguvugu, anasema ni heri uwe moto au baridi kuliko kuwa vuguvugu, hivyo chagua moja,

Ufunuo 22:10″ Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.

11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.

12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.

14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.

15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.

16 Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi.

17 Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure. “

Amen!

Kwa Mwendelezo >>> UFUNUO: Mlango wa 16

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara,  kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.


Mada zinazoendana..


KARAMU YA MWANA-KONDOO.

UNYAKUO.

WALIOITWA NI WENGI, ILA WATEULE NI WACHACHE.

UMEITIKIA WITO INAVYOPASWA?

KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.


Rudi Nyumbani.

Print this post

UFUNUO: Mlango wa 14

Kama tunavyofahamu baada ya wakati wa mataifa kuisha yaani unyakuo kupita itakuwa imebaki miaka 7 tu mpaka dunia kuisha, ndani ya hicho kipindi kifupi Mungu atakuwa anashughulika na Taifa la Israeli, na kuwatia muhuri wale wayahudi 144,000 kama tunavyosoma katika sura ya 7 ya kitabu cha Ufunuo, kwahiyo ile miaka mitatu na nusu ya kwanza itakuwa ni injili kwa wayahudi na ile miaka mitatu na nusu ya mwisho itakuwa ni wakati wa ile DHIKI KUU.

Tukiendelea na ufunuo sura ya 14 ambayo ni mwendelezo wa habari ya wale wayahudi 144000 waliotiwa muhuri na Mungu, kama haujapitia sura ya 7, unaweza ukaanzana nayo kwa kufuata link hii kisha ndio tuendelee na sura hii ya 14 >>> Ufunuo: Mlango wa 7

Ufunuo 14:1-5″ Kisha nikaona, na tazama, huyo Mwana-Kondoo amesimama juu ya mlima Sayuni, na watu mia na arobaini na nne elfu pamoja naye, wenye jina lake na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao.

2 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni, kama sauti ya maji mengi, na kama sauti ya radi kuu. Na hiyo sauti niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi, wakivipiga vinubi vyao;

3 na kuimba wimbo mpya mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele ya wale wenye uhai wanne, na wale wazee; wala hapana mtu aliyeweza kujifunza wimbo ule, ila wale mia na arobaini na nne elfu, walionunuliwa katika nchi.

4 Hawa ndio wasiotiwa unajisi pamoja na wanawake, kwa maana ni bikira. Hawa ndio wamfuatao Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamenunuliwa katika wanadamu, malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.

5 Na katika vinywa vyao haukuonekana uongo. Maana hawana mawaa.

Hapa tunaona wale wayahudi 144000 wakionekana wakiwa na mwanakondoo juu ya mlima Sayuni ikifunua nafasi za hawa wateule wa Mungu mbele za YESU KRISTO,katika utawala unaokuja wa miaka 1000, watakapomiliki na kutawala na YESU katika mlima Sayuni (yaani Yerusalemu), pia hawa wanaonekana ni bikira ikiwa na maana kwamba hawajajitia unajisi wowote na mafundisho ya dini za uongo,

Na pia kama tunavyoona walijifunza wimbo mpya ambao ni wao tu waliouweza kuuimba, sasa huu wimbo unamaana kuwa ni “furaha ya Roho Mtakatifu”, kama vile sisi wakristo tunapompokea Kristo na Bwana anapotuokoa na kutupa pumziko pale tunapomfurahia na kumshukuru wimbo mpya wa Mungu unazalika ndani ya mioyo yetu ambao hakuna mwingine anayeweza kuuimba isipokuwa mwenye Roho wa Mungu kama sisi

..Daudi alisema katika Zaburi 40:1 “Nalimngoja Bwana kwa saburi, Akaniinamia akakisikia kilio changu.

2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.

3 AKATIA WIMBO MPYA KINYWANI MWANGU, Ndio sifa zake Mungu wetu. Wengi wataona na kuogopa, Nao watamtumaini Bwana “.

Kwahiyo hawa 144000 baada ya kutiwa muhuri wa Mungu kwa kupokea Roho Mtakatifu na kupata ufunuo kwamba mwokozi wao anaishi na ndiye atakayekuja kuwapigania wimbo mpya utazaliwa ndani ya mioyo yao ambao hakuna mwingine yoyote atakayeweza kujifunza isipokuwa wao,

Na pia kumbuka watu hawa hawakuwa mbinguni, bali ni hapa hapa duniani, ukisoma kwa makini utaona sio wale 144000 ndio waliokuwa mbinguni mbele ya kiti cha enzi wakiimba hapana bali ni sauti ilisikiwa mbinguni wakiimba na hawa si wengine zaidi ya malaika, na ndio wale 144000 walionekena wakijifunza wimbo ule. Hivyo hawa 144000 hawakunyakuliwa mbinguni, bali watakuwa hapa hapa duniani.

INJILI YA MILELE:

Tukiendelea..

Ufunuo 14:6-13″ 6 Kisha nikaona malaika mwingine, akiruka katikati ya mbingu, mwenye Injili ya milele, awahubiri hao wakaao juu ya nchi, na kila taifa na kabila na lugha na jamaa,

7 akasema kwa sauti kuu, Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji.

8 Kisha mwingine, malaika wa pili, akafuata, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli, mji ule ulio mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake.

9 Na mwingine, malaika wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kuu, Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake,

10 yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo.

11 Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku, hao wamsujuduo huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina lake.

12 Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao amri za Mungu, na imani ya Yesu.

Katika mistari hii tunaona baada ya wale 144,000 kutiwa muhuri, na Bwana akiwaweka mbali na yule mnyama watafunguliwa pia na mlango wa kuhubiri INJILI YA MILELE. Na ndio wale malaika watatu tunaona wakiruka katikati ya mbingu wakihubiri injili ya milele juu yao wakaao juu ya nchi, kumbuka Mungu hajawahi kutumia malaika kuhubiri injili duniani, siku zote huwa anawatumia wanadamu, biblia inasema malaika ni roho zitumikazo kuwahudumia watakatifu(waebrania 1:14). Hivyo watakaozihubiri hizi jumbe za wa hawa malaika warukao ni wale wayahudi 144000.

Kumbuka Injili tuliyonayo sasa ni Matendo 2:38 “…Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu “. Injili hii ni ya kuwafanya watu kuwa wakristo lakini INJILI YA MILELE ni kwa watu wote na inayojulikana na watu wote, kwamfano inajulikana kuwa ushoga ni kosa,usagaji, kuua ni kosa, kuzini, kutukana,ufiraji, kuzini na wanyama,kufanya maasi ni kosa, dhamiri ya mtu ikimshuhudia kabisa kuwa anachokifanya sio sahihi bila hata kuhubiriwa n.k. ni injili ambayo kwa ufupi hahiitaji biblia kuijua, inajulikana na watu wote wenye dini na wasio na dini. Hiyo ni hofu ya Mungu ambayo ipo kwa kila mwanadamu.

Kwahiyo INJILI hii ya MILELE itahubiriwa tena kwa mara ya mwisho kwa wanadamu wote waliopo ulimwenguni wanaotenda maasi ili mtu asiwe na udhuru wa kusema sijasikia, kwa maana kwa wakati huo maasi yatakuwa ni mengi sana duniani kama tunavyoyaona leo…

Warumi 1:18 “Kwa maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu.

19 Kwa kuwa mambo ya Mungu yanayojulikana YAMEKUWA DHAHIRI NDANI YAO , kwa maana Mungu aliwadhihirishia.

20 Kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; yaani, UWEZA WAKE WA MILELE NA UUNGU WAKE; hata wasiwe na udhuru; ……..

32 ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao. “

Hivyo injili hii ya MILELE itagusa makundi yote hata wasiokuwa na dini, kwasababu ni mambo yaliyodhahiri ambayo yanajulikana na kila mtu.

Malaika wa pili akafuAata akisema “8 Kisha mwingine, malaika wa pili, akafuata, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli, mji ule ulio mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake.”

Hawa watu 144000 baada ya kupokea ufunuo wa Mungu kuwa anayetawala dunia nzima na dini zote ni mpinga-kristo (PAPA) na jinsi kanisa Katoliki lilivyohusika kuwaua watakatifu wengi na litakapokwenda kuishia, kwamba Mungu ameshalihukumu hivyo watahubiri ujumbe wao katika dunia nzima, hukumu ya Babeli mkuu.

Tukiendelea mstari wa 9-11 tunasoma..

“9 Na mwingine, malaika wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kuu, Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake,

10 yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo.”

Sasa hili ni onyo la mwisho litakalohubiriwa kwa watu wote, kwamba mtu yoyote atakayemsujudia yule mnyama na sanamu yake (yaani Kushirikiana na Kanisa Katoliki na mafundisho yake au kuwa mshirika wa umoja wa madhehebu) au kuipokea chapa katika mkono wake au katika kipaji cha uso wake, atashiriki mapigo yote ya Mungu yanatakayofuata huko mbeleni.

Kumbuka hapo kanisa litakuwa limeshaondoka, watanyakuliwa watu wachache sana wakati huo ulimwengu hautajua chochote, dhiki zote zitawakuta wale waliobaki duniani, je umeokolewa?. kama biblia inavyoendelea kusema.. “13 Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao. “

SHINIKIZO LA GHADHABU YA MUNGU:

14 Kisha nikaona, na tazama, wingu jeupe, na juu ya wingu hilo ameketi mmoja, mfano wa Mwanadamu, mwenye taji ya dhahabu juu ya kichwa chake, na katika mkono wake mundu mkali.

15 Na malaika mwingine akatoka katika hekalu, akimlilia kwa sauti kuu yeye aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu, Tia mundu wako, ukavune; kwa kuwa saa ya kuvuna imekuja; kwa kuwa mavuno ya nchi yamekomaa.

16 Na yeye aliyeketi juu ya wingu akautupa mundu wake juu ya nchi, nchi ikavunwa.

17 Kisha malaika mwingine akatoka katika lile hekalu lililoko mbinguni, yeye naye ana mundu mkali.

18 Na malaika mwingine akatoka katika ile madhabahu, yule mwenye mamlaka juu ya moto; naye akamlilia kwa sauti kuu yule mwenye mundu ule mkali, akisema, Tia mundu wako mkali, ukachume vichala vya mzabibu wa nchi, maana zabibu zake zimeiva sana.

19 Malaika yule akautupa mundu wake hata nchi, akauchuma mzabibu wa nchi, akazitupa zabibu katika shinikizo hilo kubwa la ghadhabu ya Mungu.

20 Shinikizo lile likakanyagwa nje ya mji, damu ikatoka katika shinikizo mpaka kwenye hatamu za farasi, kama mwendo wa maili mia mbili. “

Mistari wa 14-20 unaelezea maandalizi juu ya ile vita ya Harmagedoni, vitakavyopigwa Israeli, Hapa tunaona malaika akiwa ameshika mundu mkali na kuvuna mzabibu wa nchi kuashiria maovu ya wanadamu yamefikia kilele, kikombe cha ghadhabu ya Mungu kimejaa wakati wa rehema hakuna tena, kinachofuata ni hasira ya Mungu kumwagwa juu ya nchi, na ndio maana unaona zile zabibu zikatupwa katika lile shinikizo kubwa la ghadhabu ya Mungu na damu ikatoka pale mpaka kwenye hatamu za farasi kwa mwendo wa maili 200, kumbuka farasi anawakilisha vifaa vya kijeshi, hii ni picha halisi inayoonyesha jinsi hiyo vita itakavyokuwa ya kumwagika damu nyingi hayo yatatimia katika kumiminwa kile kitasa cha sita kati ya vile saba vya ghadhabu ya Mungu..

Ufunuo 16:12-16″

12 Na huyo wa sita akakimimina kitasa chake juu ya mto ule mkubwa Frati; maji yake yakakauka, ili njia itengenezwe kwa wafalme watokao katika maawio ya jua.

13 Nikaona roho tatu za uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo.

14 Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.

15 (Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.)

16 Wakawakusanya hata mahali paitwapo kwa Kiebrania, Har-Magedoni.

Pia Ufunuo 19:11-16 Inasema…”11 Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, NAYE ANAKANYAGA SHINIKIZO LA MVINYO LA GHADHABU YA HASIRA YA MUNGU MWENYEZI .

16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA.”

Hii itakuwa ni vita ya mwisho mabilioni ya watu watakufa, na baada ya kumiminwa kile kitasa cha mwisho cha saba mwisho wa dunia utakuwa umefika. 

Hivyo ndugu kumbuka shetani hapendi ukifahamu kitabu cha UFUNUO kwasababu anajua siku ukiyajua mambo ya kutisha yanayokuja huko mbeleni utatubu na kuishi maisha ya uangalifu hapa duniani, yeye anachotaka ujue ni kuwa dunia itadumu milele na ni raha tu siku zote lakini biblia usisahau inasema 1wathesalonike 5:3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.”

Huu ni wakati wa jioni sana BWANA YESU yupo mlangoni kurudi kulinyakua kanisa lake je! na wewe utakuwa miongoni mwa wale watakaokwenda naye? Ni mara ngapi umesikia injili ubadilike lakini bado unaabudu sanamu, unapenda mambo ya ulimwengu huu zaidi ya Mungu , unavaa vimini, unapaka lipstick, unazini, mlevi, msengenyaji, mtukanaji,? Injili hiyo halitadumu milele, upo wakati mlango wa neema utafungwa hapo ndipo Bwana Yesu anasema kutakuwa na kilio na kusaga meno.

Mpe Bwana maisha yako leo uokolewe.

Mungu akubariki.

Kwa Mwendelezo >> UFUNUO: Mlango wa 15

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara,  kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.


Mada zinazoendana..


INJILI YA MILELE.

ALAMA KATIKA VIPAJI VYA NYUSO.

JE! KUBET NI DHAMBI?


Rudi Nyumbani

Print this post

UFUNUO: Mlango wa 13

Tukisoma kitabu cha Ufunuo mlango wa 13 tunaona kuna wanyama wawili wanaozungumziwa pale; wa kwanza akiwa ni yule mwenye vichwa saba na pembe 10 aliyetoka baharini na wa pili ni yule aliyekuwa mfano wa mwanakondoo mwenye pembe 2 akitoka katika nchi.

Kwa ufupi tuwatazame hawa wanyama wanawakilisha nini na wanachukua nafasi gani katika siku hizi za mwisho:

MNYAMA WA KWANZA:

Ufunuo 13:1-5″ Kisha nikaona mnyama akitoka katika bahari, mwenye pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru.

2 Na yule mnyama niliyemwona alikuwa mfano wa chui, na miguu yake ilikuwa kama miguu ya dubu, na kinywa chake kama kinywa cha simba, yule joka akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi na uwezo mwingi.

3 Nikaona kimoja cha vichwa vyake kana kwamba kimetiwa jeraha la mauti, na pigo lake la mauti likapona. Dunia yote ikamstaajabia mnyama yule.

4 Wakamsujudu yule joka kwa sababu alimpa huyo mnyama uwezo wake; nao wakamsujudu yule mnyama, wakisema, Ni nani afananaye na mnyama huyu? Tena ni nani awezaye kufanya vita naye?

5 Naye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya makufuru. Akapewa uwezo wa kufanya kazi yake miezi arobaini na miwili.

6 Akafunua kinywa chake amtukane Mungu, na kulitukana jina lake, na maskani yake, nao wakaao mbinguni.

7 Tena akapewa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda, akapewa uwezo juu ya kila kabila na jamaa na lugha na taifa.

8 Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia.

9 Mtu akiwa na sikio na asikie.

10 Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye subira na imani ya watakatifu. “

Hapa tunamwona huyu mnyama akiwa na vichwa saba na pembe 10, na juu ya zile pembe zake ana vilemba 10, sasa hivi vichwa 7 inafahamika vinawakilisha ngome/mamlaka ambazo shetani alizikalia na kuzitumia kupambana na kuuharibu uzao wa Mungu hapa duniani tangu taifa la Israeli lilipoundwa. Na tawala hizi tunaweza tukaziona katika biblia nazo ni 1) MISRI   2) ASHURU, 3) BABELI 4) UMEDI & UAJEMI   5) UYUNANI   6) RUMI   7) RUMI -KIDINI.

Lakini Yohana alimwona yule mnyama akiwa na PEMBE 10 katika kichwa chake, kumbuka zile pembe 10 hazikuwa zimesambaa juu ya vichwa vyote saba kama inavyofikiriwa na watu wengi, bali zote 10 Yohana alizoziona zilikuwa juu ya kichwa KIMOJA TU! na sio kingine zaidi ya kile kichwa cha saba. Kwahiyo kile kichwa cha saba ndicho Yohana alichokikazia macho kwasababu kilikuwa ni tofauti na vingine vyote.

Hivyo zile pembe 10 kulingana na maono aliofunuliwa Danieli juu ya ile sanamu ya Nebukadneza alioiona yenye miguu ya chuma na nyayo zenye vidole 10 zilizochanganyikana nusu chuma, nusu udongo, kama inavyojulikana ile miguu ya chuma ni utawala wa RUMI na vile vidole ni utawala wa RUMI uliokuja kugawanyika na kuwa yale mataifa kumi ya ULAYA wakati ule ambayo yalikuwa bado hayana nguvu kwasababu yalikuwa bado hayajavikwa vilemba(CROWNS). Hivyo vile vidole 10 ndio zile pembe 10 zinazoonekana juu ya yule mnyama na ni mataifa 10 yaliyopo katika umoja wa ULAYA (EU), na kama tunavyoona sasa kwa huyu mnyama zile pembe 10 zimetiwa VILEMBA inaashiria kuwa utakuja wakati haya mataifa yanayounda umoja wa ulaya yatapewa nguvu ya utawala na yule mnyama kutenda kusudi la kuwaua watakatifu katika kipindi cha ile miaka mitatu na nusu ya mwisho ya dhiki kuu.

Leo hii tunaona umoja wa ulaya unaundwa na mataifa zaidi ya 10, lakini yatakuja kuishia kuwa 10 tu ili kutimiza unabii wa kwenye biblia na yapo mbioni kuvikwa vilemba( yaani kupewa utawala wa dunia) yakiwa chini ya yule mnyama ( RUMI) chini ya utawala wa PAPA ambaye ndiye mpinga-kristo biblia inayomwitwa “mtu wa kuasi”, mwana wa uharibifu ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa.(2Thesalonike 2). Leo hii bado hayana nguvu kwasababu Danieli alionyeshwa kuwa vile vidole kumi nusu yake vitakuwa na nguvu na nusu yake vitakuwa vimevunjika ndivyo ilivyo sasa hivi Umoja wa ulaya hauna nguvu sana, lakini utakuja kupata nguvu duniani kote ili kutimiza kusudi la yule mnyama(mpinga-kristo)

Tukiendelea kusoma mstari wa tatu tunaona moja ya kichwa chake (ambacho ndio kile kichwa cha saba) kimetiwa jeraha la mauti nalo likapona. Kumbuka Rumi-ya kidini(UKATOLIKI) iliyokuwa chini ya UPAPA katika historia ilikuwa inatawala dunia nzima, na ilifanikiwa kupata nguvu dunani kote kiasi cha kwamba mtu yeyote aliyeonekana anakwenda kinyume na hiyo dini adhabu ilikuwa ni kifo tu, mamilioni ya wakristo waliouwa wote waliokataa kuisujudia miungu yao ya kipagani, jambo hili liliendelea na hii dini ilizidi kupata nguvu hadi kufikia karne ya 16 wakati wa matengenezo ya kanisa ambapo Mungu alianza kuwanyanyua watu wake kama Martin Luther ambaye alianza kufundisha watu “kuhesabiwa haki kwa imani” na kukosoa mafundisho potofu ya kanisa Katoliki lakini PAPA alipotaka kumuua mfalme wa Ujerumani alisimama kumuhifadhi Luther, ndipo watu wengi wakaanza kuacha hii dini ya uongo na kuligeukia NENO la Mungu hivyo Ukatoliki ukaanza kupungua nguvu, na wakati huo huo Mungu aliwanyanyua wengine kama Calvin, Zwingli, Knox n.k. ili kulitengeneza tena kanisa lililokuwa limeharibiwa na mafundisho ya uongo ya Kanisa katoliki.

Hapo ndipo ulipokuwa mwanzo wa lile jeraha la yule mnyama lakini pigo hasa lilikuja karne ya 18 mwaka 1798 katika mapinduzi huko Ufaransa Jenerali Berthier alipeleka vikosi vyake Roma na kumng’oa PAPA katika utawala wake, akamchukua mateka pamoja na mali zake zote za dini yake, Hivyo ikapelekea dini ya kikatoliki iliyokuwa inatiisha dunia kuwa karibuni na kutoweka kabisa, hilo lilikuwa pigo kubwa sana lilofananishwa na jeraha la mauti lakini tunaona Biblia inasema lile JERAHA LA MAUTI lilipona,

 Je! Jeraha hili liliponaje na lilipona lini?.

Wakati wa vita vya kwanza na vya pili vya dunia, matatizo yalikuwa mengi duniani, uchumi ulishuka sana, mataifa ya ulaya yaliaanza kuanguka na kupoteza nguvu zao kutokana na athari ya vita, Hivyo kiu ya kutafuta amani duniani ikaongezeka kumbuka wakati huo huo Marekani ilianza kupata nguvu, na likiwa kama taifa la kikristo (protestant) lenye nguvu kubwa ya kiuchumi na kijeshi hivyo kwa kushirikiana na mataifa ya ulaya kwenye harakati za kutafuta amani, (isiyokuwa ya kivita) walianza kuutambua umuhimu wa PAPA Kwasababu alionekana kuwa ni mtu mwenye mvuto na anayekubalika na watu wengi duniani, hivyo mataifa mengi yakaanza kutuma mabalozi wake kwa papa ajihusishe na masuala ya AMANI YA DUNIA. Sasa kuanzia hapo jeraha lake la mauti likaanza kupona, wale ambao walikuwa wanafanya mageuzi kinyume chake(protestants) wakaanza kushirikiana nae tena, uprotestant ukabakia kuwa jina tu na ndio huko inapoundiwa ile sanamu ya mnyama nitakayoielezea zaidi mbeleni…

Tukiendelea mstari 4 & 5, Tunaona lile joka ambaye ni Shetani mwenyewe alimpa nguvu yule mnyama naye akaanza kunena maneno makuu ya makufuru. Tukisoma pia kitabu cha Danieli alizungumziwa kama ile PEMBE ndogo iliyozuka na kungo’a wale wafalme watatu na kunena maneno ya makufuru Danieli 7:25 “Naye atanena maneno kinyume chake Aliye juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye juu; naye ataazimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake kwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati. “ Na huyu si mwingine zaidi ya mpinga-kristo ambaye ni PAPA,..Si ajabu PAPA leo anasimama “badala ya mwana wa Mungu duniani”..Vicarivs filii Dei, ..Papa leo amejivika uwezo wa kusaheme dhambi jambo ambalo BWANA YESU KRISTO mwenyewe ndiye anayeweza kulifanya ..haya yote ni maneno ya makufuru, na yapo mambo mengi zaidi ya hayo ambayo ni makufuru. Kumbuka ninaposema PAPA namaanisha kile “CHEO”..kwahiyo yeyote anayekikalia hicho cheo amejitwika cheo cha mpinga-kristo mwenyewe.

Na tunaona wakati wa mwisho atapewa uwezo wa kutenda kazi miezi 42, hii ni miaka mitatu na nusu, kati ya ile miaka saba ya mwisho ya lile juma la 70 la Danieli. Hichi kitakuwa kipindi cha DHIKI KUU, sasa hivi PAPA anaonekana kama mtu asiyekuwa na madhara yoyote, anakuja kwa njia ya kujipendekeza ili apate nguvu kiurahisi, kama kitabu cha Danieli kinavyomtabiri, leo hii duniani kote anajulikana kama “MTU WA AMANI”, Ni mtu mwenye wafuasi wengi duniani, na aneyekubalika kuliko mwanasiasi yoyote duniani, dini nyingi zimeanza kuvutiwa naye, hata waislamu sasa wanamwona kama ni mtetezo wao mtu anayejali watu wote, PAPA anasema wote tunamwabudu Mungu mmoja ila kwa njia tofauti tofauti (yaani wakristo, waislamu wahindu, wabudha tunamwabudu Mungu mmoja), angali biblia inasema YESU ndiye njia pekee ya kumfikia Mungu, na cha ajabu umaarufu wake unaongozeka na watu wanamfurahia ili kutimiza ule unabii kwamba “watu wote ambao majina yao hayajaandikwa katika kitabu cha uzima cha mwanakondoo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu ndio watakaomsujudia.” Na kumsujudia sio kumpigia magoti bali ni kukubaliana na mifumo yake na imani yake.

Ndugu yangu mpinga-kristo hatakuja na mapembe kichwani, akilazimisha watu wamwabudu, kumbuka biblia inasema shetani ana HEKIMA kuliko Danieli, na sehemu nyingine biblia inasema ile roho itataka kuwadanganya yamkini hata wateule. Siku zote anakuja kama malaika wa nuru, usitazamie kuwa mpinga-kristo atakuwa muislamu au muhindi au freemason, hapana ndugu yupo kanisani amebeba biblia na anafanya kampeni za amani duniani na watu wanamshangilia na kumbusu, biblia inasema hapo ndipo “PENYE HEKIMA ” .

Kwahiyo inahitajika Hekima kumjua vinginevyo utachukuliwa na mafuriko yake kama wengi walivyochukuliwa huu ni wakati wa kuwa macho sana, jali maisha yako ya umilele yanayokuja. Chunguza maandiko kama watu wa Beroya, sio kila roho inayoshabikiwa na wengi unaipokea moyoni mwako kwasababu biblia inasema IPO NJIA IONEKANAYO KUWA NJEMA MACHONI PA WATU..LAKINI MWISHO WAKE NI UPOTEVU, na BWANA YESU alisema njia iendayo upotevuni ni PANA na wengi wanaiendea hiyo.

MNYAMA WA PILI:

Ufunuo 13:11-18″

11 Kisha nikaona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka katika nchi; naye alikuwa na pembe mbili mfano wa Mwana-Kondoo, akanena kama joka.

12 Naye atumia uwezo wote wa mnyama yule wa kwanza mbele yake. Naye aifanya dunia na wote wakaao ndani yake wamsujudie mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.

13 Naye afanya ishara kubwa, hata kufanya moto kushuka kutoka mbinguni uje juu ya nchi mbele ya wanadamu.

14 Naye awakosesha wale wakaao juu ya nchi, kwa ishara zile alizopewa kuzifanya mbele ya huyo mnyama, akiwaambia wakaao juu ya nchi kumfanyia sanamu yule mnyama, aliyekuwa na jeraha la upanga naye akaishi.

15 Akapewa kutia pumzi katika ile sanamu ya mnyama, hata ile sanamu ya mnyama inene, na kuwafanya hao wote wasioisujudu sanamu ya mnyama wauawe.

16 Naye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, au katika vipaji vya nyuso zao;

17 tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake.

18 Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita. “

Tunaona huyu mnyama wa pili ana pembe kama mwanakondoo, lakini sio mwanakondoo, na huyu anaonakana ametoka katika nchi na sio katika bahari na yeye hana vichwa saba Kama yule mnyama wa kwanza, ikiwa na maana kuwa utawala wake haukuanzia mbali kama yule mnyama wa kwanza bali ulizuka mwishoni. Hivyo huyu mnyama si mwingine zaidi ya MAREKANI. Ukiangalia katika ile nembo ya Marekani katika ile dola yao utaona yule tai akiwa ameshika mishale 13, ile piramidi kuna ngazi 13, kuna nyota 13 juu ya yule tai, matawi 13 ya ule mzeituni ulioshikwa ..nk. kila mahali 13..13… na taifa la Marekani linaonekana katika UFUNUO 13.

Pia huyu mnyama alipewa uwezo wa kufanya watu wote wakaao duniani wamsujudie yule mnyama wa kwanza na kuunda ile SANAMU YA YULE MNYAMA.

Sasa Sanamu ya mnyama ni ipi?

Marekani kama taifa lilokuwa la kiprotestant ambalo hapo kwanza lilikuwa halishakamani wala halishirikiani na kanisa Katoliki kwa namna yoyote, lakini katika karne ya 20 baada ya vita ya pili Vya dunia liliacha njia ya kweli ya NENO LA MUNGU, na kurudi kuiga tabia za yule mnyama,kazi nzuri na juhudu zote zilizofanywa na wale wana-matengenezo zikawa ni bure, ni sawa na mbwa aliyerudia matapishi yake.

Baada ya kuibuka jopo kubwa la madhehebu ya kiprotestant duniani, viongozi wa madhehebu ya kimarekani walikutanika kwa agenda ya kutaka kuondoa tofauti katikati ya wakristo ili kufikia muafaka mmoja wa IMANI, ndipo walipounda BARAZA LA MAKANISA ULIMWENGUNI (World Council Of Churches), na NATIONAL COUNCIL OF CHURCHES , na ndio chimbuko la EKUMENE. (Ecumenical council)

Na Kanisa Katoliki likiwa kama washirika wao wa karibu wakiwasaadia.

Baraza hili la UMOJA WA MAKANISA liliazimu kuyarudia mambo yale yale ya ukahaba yaliyofanywa na kanisa Katoliki, Iimekuwa ni SHIRIKA LA KI-DINI, na Linasheria zake na itakadi zake ambazo zinaenda kinyume na mpango na NENO LA MUNGU. Kwahiyo UMOJA HUU ndio unaoitwa SANAMU YA MNYAMA..Kwasababu tabia zote zilizokuwa katika kanisa kahaba katoliki zipo nazo kule na hivi karibuni yule mnyama (America) ataenda kuipa PUMZI ILE SANAMU INENE, ili watu wote waiabudu, hii ikiwa na maana siku sio nyingi watu wote duniani watenda kulazimishwa kuwa washirika wa muunganiko wa hayo makanisa mtu yeyote atakayeonekana kwenda kinyume atauawa.

Na kama tunavyoona huyu mnyama wa pili (MAREKANI) anaweza kufanya ishara kubwa hata kufanya moto kushuka kutoka mbinguni, jambo hili linatupa picha nguvu za kijeshi walizonazo Marekani kama uwezo wa kushusha makombora makubwa ya vita kutoka angani mabomu ya atomic n.k.

Hili baraza la makanisa duniani sasa linafanikiwa kuzivuta dini zote ulimwenguni pamoja, ikiasisiwa na PAPA kiongozi wa kanisa katoliki duniani, itafika wakati kama hautakuwa mshirika wa dini au kanisa ambalo halijaunganishwa katika huu UMOJA WA MAKANISA NA DINI hutaweza kuuza wala kununua wala kuabudu, wala kuishi katika jamii,

Leo hii tunaona vitendo vya kigaidi na vya mauaji vikiongezeka, wanasiasa wameshindwa kuirejesha amani ya dunia, na matatizo yote yahusuyo amani yanatokana na mizozo ya kidini tunaweza kuona mambo yanayoendelea mashariki ya kati mfano Israeli, syria-kuna ISIS,Iraq, Lebanoni-kuna hezbolah, myanmar huko Asia kuna warohighya, sehemu za Afrika nchi kama Nigeria kuna Boko kuna haramu, Somalia-alshabaab, central Africa- antibalaka ..na makundi mengine mengi sana,. tunaona mizizi yote ya migogoro inaanzia katika DINI. Hivyo atahitajika mtu wa KIDINI mashuhuri kutatua migogoro ya kidini na sio wanasiasa au watu wa kijamii – Na huyu atakuwa si mwingine zaidi ya PAPA kwasababu yeye ndiye anayekubaliwa na dini zote pamoja na wafalme wote wa dunia.

Hivyo atapokwisha kupata nguvu, ataibua mfumo mmoja wa kutambua watu wote duniani kwa imani zao, kwa kivuli cha kuleta amani na kukomesha vitendo vya uvunjifu amani duniani kumbe nia yake itakuwa ni kuwateka watu wote duniani na kuwatia ile CHAPA YA MNYAMA. Wakati huo watu wengi duniani wataufurahia huo mfumo pasipo kujua ndio wanaipokea chapa hivyo. Wengi watasajiliwa katika madhehebu na dini zao zilizokuwa na ushirika huo wa UMOJA WA MAKANISA ULIMWENGU , Vitatumika vitu kama CHIPS, IDS, na utambulisho mwingine utakotengenezwa ili kuyafikia makundi yote, sasa wale watakaokaidi ndio watakaopitia dhiki kuu, hao ndio watakaoonekana magaidi na wavunjifu amani, kama sivyo kwanini wasikubali utambulisho huo mpya? na kumbuka watakuwa ni wachache sana watakaogundua kuwa ndio CHAPA YENYEWE ,

Hivyo ndugu injili tuliyonayo sasa hivi inasema ..UFUNUO 18:4-5″ Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni, ikisema, TOKENI KWAKE, ENYI WATU WANGU,MSISHIRIKI DHAMBI ZAKE, wala msipokee mapigo yake.Kwa maana dhambi zake zimefika hata mbinguni, na Mungu amekumbuka maovu yake. “

Ndugu toka katika mifumo ya madhehebu kwasababu yameshirikiana na yule mnyama(kanisa katoliki) kufanya ukahaba, na kuua watakatifu wa Mungu wengi, yeye anaitwa BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA ikiwa na maana kama yeye ni mama wa makahaba ni dhahiri kuwa anao mabinti na wao pia ni makahaba kama mama yao alivyo na hao mabinti sio wengine zaidi ya madhehebu yote yaliacha uongozo wa Roho mtakatifu na kuandamana na desturi za kanisa kahaba Katoliki, hivi karibuni tumesikia WALETHERANI wameungana rasmi wakatoliki.!! Biblia inasema TOKENI KWAKE ENYI WATU WANGU, kama ukishirikiana naye inamaanisha kwamba na wewe pia utashiriki mapigo yake ndivyo Mungu anavyokuchukulia.

Ufunuo 14:9 ” Na mwingine, malaika wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kuu, Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake, yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo. “

Bwana ametuita kuwa BIKIRA SAFI, na bikira tu ndiye atakayeingia katika karamu ya mwanakondoo, toka kwenye mifumo ya madhehebu umwabudu Mungu katika ROHO NA KWELI.

Mungu akubariki, na Mungu atusaidie katika safari yetu tuumalize mwendo salama

Amen.

Kwa Mwendelezo >> UFUNUO: Mlango wa 14

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara,  kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.


Mada zinazoendana…


CHAPA YA MNYAMA

DANIELI: Mlango wa 2

MUUNGANO WA DINI NA MADHEHEBU YOTE, UMEKARIBIA.

UFUNUO: Mlango wa 21


Rudi Nyumbani

Print this post

UFUNUO: Mlango wa 12

MAELEZO JUU YA “UFUNUO 12”

Ufunuo 12

1 Na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili.

2 Naye alikuwa ana mimba, akilia, hali ana utungu na kuumwa katika kuzaa.

3 Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba.

4 Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake.

5 Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi.

6 Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali palipotengenezwa na Mungu, ili wamlishe huko muda wa siku elfu na mia mbili na sitini.

7 Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;

8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.

9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.

10 Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.

11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.

12 Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.

13 Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.

14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.

15 Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule.

16 Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.

17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.

Ukisoma Ufunuo mlango wa 11, utaona habari ya wale MASHAHIDI WAWILI wakifanya kazi ya kuwahubiria injili wale Wayahudi 144,000 na kutiwa muhuri (Ufunuo 7). Na tunaona walifanya kazi yao miezi 42, (yaani miaka mitatu na nusu) na baada ya kumaliza ushuhuda wao yule mnyama atokaye kuzimu atawaua lakini baada ya siku tatu na nusu tunaona Mungu atawafufua.

Kumbuka baada ya kanisa kunyakuliwa, injili itahamia Israeli na itakuwa imebakia miaka 7 tu mpaka mwisho wa dunia utakapofika kulingana na unabii wa Danieli 9:27, kwenye lile juma moja la mwisho kati ya yale majuma 70 aliyoonyeshwa.

Hivyo ndani ya hii miaka 7, nusu yake yaani miaka mitatu na nusu ya kwanza, hawa manabii wawili watafanya kazi ya kuwahubiria wayahudi, na nusu ya pili iliyobaki itakuwa ni kipindi cha ile DHIKI KUU (yaani miaka 3.5 ya mwisho).

Sasa tukiendelea kusoma kitabu cha Ufunuo 12 tunaona Yohana akiona ishara kuu mbinguni, yule mwanamke aliyevikwa jua na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake na juu ya kichwa chake taji ya nyota 12.

Ukiangalia huyu mwanamke anawakilisha taifa la Israeli, ukisoma mwanzo 37:9 utaona ile ndoto aliyoota Yusufu aliona jua na mwezi na zile nyota 11 zikimwinamia ambayo tafsiri yake tunafahamu ilikuwa ni Yakobo kama jua, mwezi kama mama zake, na wale wana 11 wa Israeli kama zile nyota. Hivyo yule mwanamke ni taifa la Israeli.

Ukiendelea kusoma mstari wa pili utaona yule mwanamke alikuwa na mimba, na katika hali utungu wa kutaka kuzaa, na akamzaa mtoto mwanamume ambaye atawachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Maana ya ule utungu ni unabii au matarajio ya kuzaliwa masiya katika Israeli ambaye alikuwa akisubiwa kwa muda mrefu, Na huyu mtoto mwanamume si mwingine zaidi ya BWANA YESU KRISTO yeye ndiye atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma katika ule utawala wa miaka 1000 (Ufunuo 2:27).

Ukizidi kusoma utaona pia katika mstari wa 3-6, utaona ishara nyingine ilionekana lile joka kubwa jekundu (ambalo ni shetani) likiwa limejiandaa pale atakapozaliwa yule mtoto limmeze, lakini halikufanikiwa, jambo hili tunaliona lilitimia wakati Bwana YESU anazaliwa Mfalme Herode, alipopata habari kuwa mfalme aliyetabiriwa kazaliwa katika Israeli alifadhaika na kutaka kumwangamiza mtoto YESU, Lakini hakufanikiwa mpaka Mungu alipomchukua juu mbinguni katika kiti chake cha enzi.

Tukiendelea kusoma kuanzia ule mstari wa 7-12, Tunaona habari nyingine inayohusu vita vinavyoendelea mbinguni, kati ya Malaika watakatifu na shetani pamoja na malaika zake, kwa maelezo marefu juu ya vita hivyo unaweza kufungua hapa >> Vita vinavyoendelea mbinguni

Lakini tukiendelea mstari wa 13 tunaona baada ya yule mtoto kunyakuliwa juu (yaani Yesu kupaa AD 30) yule joka aliendelea kumuudhi yule mwanamke,tunaona katika historia alizidi kumuudhi kwa takribani muda wa miaka 2000 mpaka sasa, aliwatesa na kuwaua wayahudi katika nyakati tofauti tofauti, mfano wakati wa utawala wa Adolf Hitler aliwaua wayahudi zaidi ya milioni 6, katika historia tunaona wayahudi ni watu wamekuwa wakichukiwa na mataifa mengi n.k.

Mstari wa 14, tunasoma mwanamke yule baada ya kuudhiwa muda mrefu akapewa MABAWA MAWILI YA TAI yule mkubwa ili aruke aende mbali na yule Joka aliyetupwa chini ili kufanya vita na watakatifu kwa muda wa miaka mitatu na nusu. Yale mabawa ya Tai ni injili ya wale manabii wawili wa ufunuo 11, watakaowahubiria wayahudi ili kuwafanya wamjue yule joka kubwa jekundu ni nani (MPINGA-KRISTO), na utendaji kazi wake na namna ya kumuepuka, na ndiye anayetaka kukaa katika Hekalu la Mungu kuabudiwa kama Mungu.

Kumbuka wale manabii wawili katika injili yao ndio watakaomfunua yule mpinga-kristo kwa wayahudi kuwa si mwingine zaidi ya kiongozi maarufu anayetoka katika utawala wa RUMI, mwenye kivuli cha Amani kumbe ndani yake ni joka linalotaka kuabudiwa, Kama tu vile lile joka lilivyokuwa ndani ya HERODE-Mrumi kutaka kumwangamiza YESU vivyo hivyo hilo joka litakuwa ndani ya mpinga-kristo atakayetoka katika utawala ule ule wa Rumi kutaka kuwaangamiza wayahudi.

Hivyo wale wayahudi 144,000 (ufunuo 7), watakapoamini ile injili ya wale manabii wawili watakayoihubiri ile miaka mitatu na nusu ya kwanza, pamoja na zile ishara na yale mapigo yatakayofuatana nao, Hawa wayahudi wachache 144,000 watafahamu kuwa yule joka anawawinda, na kwamba DHIKI KUU itaanza hivi karibuni, hivyo Mungu atawafungulia mlango wa kuwaficha mbali na yule JOKA pale dhiki itakapoanza,

Kwahiyo hili kundi dogo litaondoka ISRAELI, Mungu atawapeleka mahali alipowaandalia mahali ambapo yule mpinga-kristo hataweza kuwafikia (hii ndio maana ya kupewa mabawa ya Tai), lakini kumbuka sio wayahudi wote wataikubali ile injili ya wale manabii wawili bali ni wale tu 144,000 tu.

Watakaosalia ile miaka mitatu na nusu ya mwisho itakapoanza (ambacho ndio kipindi cha dhiki kuu), watapata mateso mengi yasiyokuwa na mfano tangu ulimwengu kuumbwa na hayatakuwepo hata baada ya hapo, kumbuka dhiki hii itajumuisha pia watu wote wa mataifa watakaokataa kuipokea ile chapa ya mnyama wakati huo unyakuo utakuwa umeshapita.

Kama tu vile kipindi cha kuzaliwa kwa YESU wale mamajusi walipomletea Herode habari ya kuzaliwa mfalme Israeli, malaika walimwonya Mariamu na mwanawe waondoke Israeli kwasababu mpinga-kristo(Herode) anakwenda kuleta dhiki, walikimbilia Misri kabla ya ile dhiki kuanza, lakini yule Herode alipoona kuwa wale mamajusi wamemlaghai, alikasirika akaenda kufanya vita na uzao wote uliobakia wa watoto wa Israeli,

Tunaona kulikuwa na maombolezo makuu Yerusalemu watoto wote walichinjwa. Vivyo wale manabii wawili (Ufunuo 11) wanafananishwa na wale MAMAJUSI ambao walimtangazia Herode habari mbaya za kuzaliwa mfalme, na wakati wa mwisho wale MANABII WAWILI pia watamtangazia mpinga-kristo kwamba mfalme kazaliwa tena mioyoni mwa WAISRAELI na kwamba anayepaswa kuabudiwa ni yule mtoto na sio yeye, na kama vile Herode alivyowakasirika mamajusi pamoja na Mariamu na mtoto vivyo hivyo mpinga-kristo wakati wa mwisho atawakasirikia wale MASHAHIDI WAWILI na kuwaua, lakini baadaye hakufanikiwa kuwaangamiza kabisa kwani walifufuka kama vile wale mamajusi walivyopewa njia ya kumtoroka Herode,

Na kama vile ni mwanamke mmoja tu (Mariamu) kati ya wanawake wote wa Israeli ndiye aliyekuwa na mimba ya mwokozi ndani, vivyo hivyo ni lile kundi dogo tu (144000) ndio litakalokuwa na ufunuo wa YESU mioyoni mwao utakaoletwa na wale manabii wawili wanaofananishwa na mamajusi.

Na pia kama tunavyoona Mariamu alipelekwa peke yake Misri mbali na Herode vivyo hivyo na wale 144,000 ndio tu watakaopelekwa mbali na mpinga-kristo wakati wa dhiki itakapoanza walioabakia wote yaani mamilioni ya waisraeli itawapasa wapitie DHIKI KUU kama tu wale wanawake wengine wa Israeli walivyouliwa wana wao.

Kwahiyo hawa 144,000 hawataguswa na yule joka kubwa jekundu na ndio maana tunawaona katika Ufunuo 14 wakiwa wamesimama na mwanakondoo juu ya mlima Sayuni, bikira safi wa Mungu, hawa wataingia katika ule utawala wa miaka 1000, pasipo kupitia madhara yoyote.

Kwa ujumla Ufunuo sura ya 12, inaelezea ISRAELI na jinsi yule mwanamke alivyofananishwa na taifa la Israeli.

Kwahiyo ndugu tazama ni wakati gani tunaishi, je! umepokea kweli Roho Mtakatifu? umebatizwa katika ubatizo sahihi? Maisha yako yanastahili unyakuo?. Kumbuka sasa Taifa la Israeli linanyanyuka, dalili zote zinaonyesha kuwa unyakuo upo mlangoni na injili inakaribia kurudi Israeli, Maombi yangu utubu,

Fahamu tu yule JOKA kubwa jekundu alishatupwa chini akiwa na ghadhabu nyingi akijua muda wake umebaki mchache, Hivyo utendaji wake wa kazi wa sasa sio kama ule wa zamani anatafuta kukupeleka kuzimu kwa gharama zozote, hivyo ni wakati wako wewe kusimama imara na kuuthibitisha wokovu wako.

Mungu akubariki.

Kwa mwendelezo >> UFUNUO: Mlango wa 13

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara,  kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.


Mada zinazoendana..


MARIAMU

UZAO WA NYOKA.

MPINGA-KRISTO

HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.


Rudi Nyumbani

Print this post

BWANA YESU ALIKUWA ANAONYESHA KUWA MUNGU NI MUNGU MWENYE AKILI TIMAMU.

Bwana Yesu mara nyingi alikuwa akiwaaminisha watu kwa mifano, yaani ni jinsi gani Mungu alivyo na akili timamu na alivyo na kumbukumbu nzuri sana katika mambo yake yote, alijaribu kila namna kuwatolea watu ile dhana ya kuwa Mungu ni kiumbe cha ajabu kilicho mbinguni kinahitaji kuabudiwa tu wakati wote, na hakina muda wa kutazama mambo mengine manyonge yawahusuyo wanadamu, nikisema mambo manyonge ninamaanisha mambo yanayozunguka maisha ya mwanadamu ya kila siku, kama vile majukumu, afya, chakula, malazi, matamanio ya maisha bora, raha, sherehe n.k..

Yesu alituhakikishia kuwa Mungu anatuzingatia sana, kwa kutumia mifano mirahisi kabisa iliyo hai ili kutuonyesha sisi ni jinsi gani Mungu alivyo na kumbukumbu ya haraka sana juu ya watu wake na viumbe vyake vyote..Embu chukua muda tafakari huu mfano kama ulivyo, najua unaweza kuwa na tafsiri nyingi unazozifahamu lakini naomba kwa sasa usiongeze chochote utafakari tu kama ulivyo, naamini utajifunza kitu kikubwa sana ndani yake…

Mathayo 6:26 “Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. NINYI JE! SI BORA KUPITA HAO?”.

Nataka nikuambie Mungu hategemei msaada wako wewe ili akutimize mahitaji yako ya riziki, yeye anaweza kufanya hayo yote bila msaada wako na ukaishi vizuri tu,,..Huoni kama hilo linaweza kuwa ni faraja kwako katika kile UNACHOKIFANYA sasahivi, kiwe ni kinakidhi au hakikidhi?, pengine umekata tamaa ya maisha kwa namna moja au nyingine na kuona kama vile Mungu haoni unayopitia, lakini nataka nikumbie kama ndege hawamwongezei chochote na analo jukumu la kuwalisha, wewe hupaswi kuwa na hofu hata kidogo..Kwasababu wewe ni mara nyingi sana zaidi ya wao.

Mfano mwingine ni huu..

Mathayo 6:30 “Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?”.

Nilipokuwa ninautafakari sana huu mstari na kujiuliza ni wapi maua yanamzidi Sulemani kwa kuvikwa vizuri, nikagundua japo kuwa hayajisumbukii kwa chochote yapo pale pale, lakini kumbe rangi za maua huwa hazifubai, lakini mavazi ya Sulemani yalikuwa yanachakaa na kila siku anahitaji yabadilishwe apewe mapya.

Japo Sulemani alikuwa anaoga kila siku lakini aliishia kutoa jasho lakini maua hayana historia ya kuoga lakini yanatoa harufu nzuri miilini mwao, ambazo ndio hizo wanadamu hutumia kujinakshi miili yao na majumba yao na kutengenezea marhamu mbali mbali…Kwa Hapo Sulemani ameachwa mbali sana na maua ya kondeni.

Lakini nataka nikuambie, hata wewe utajiri wako, au mali zako, au UMASKINI wako hauwezi kumsaidia Mungu, kukupendezesha au kukufanya mpya zaidi na kuvutia.. Fahamu tu ukipenda kudumu katika kuutafuta ufalme wake basi, lile Neno “Je! hatazidi sana kuwavika ninyi enyi wa imani haba” litakuwa ni la kwako, iwe ni katika uchache au katika wingi..

Mfano mwingine tena ni huu…

Mathayo 7:11 “Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamwombao?”.

Watoto wetu wakituomba, tuchukulie mfano baiskeli tutafanya juu chini kwenda kuwanunulia…hata kama hakitakuja kwa wakati husika lakini kwa jinsi wanavyoendelea kusumbua tutafanya juu chini tuwanunulie tu hata kwa kukopa au kujichanga…

Sasa kama wewe unaelewa hali ya mwanao, kwanini yeye Mungu wetu wa mbinguni asielewe yako?, mpaka unapaniki na kuogopa na kukosa raha ya maisha kama vile yeye sikio lake ni zito, yupo mbali hakuoni wala hakusikii.. Nataka nikuambie huna haja ya kufunga na kuomba juu ya hilo, Mungu yupo “very sensitive, more than any living creature on Earth or Heaven”..Anao upeo mpana wa kufikiri na kuhisi mambo kuliko wewe unavyodhani, anaweza kuhisi tatizo lako ni lipi kabla hata halijaingia akilini mwako. Biblia inalithibitisha hilo.

Mathayo 6: 7 “Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi.

8 Basi msifanane na hao; MAANA BABA YENU ANAJUA MNAYOHITAJI KABLA NINYI HAMJAMWOMBA”.

Unaona?, Anajua hata unalokwenda kumwomba wiki ijayo,,, ashindweje kujua taabu au shida unayopitia sasa hivi, anajua unaumwa na unateseka katika magonjwa na unahitaji kupona, analijua hilo, anafahamu una haja na kuwa na maisha mazuri anajua, anajua unahitaji kuolewa na umri umeshakwenda, anajua unahitaji pesa uvae nguo nzuri upendeze, anajua unahitaji uishi katika nyumba yako mwenyewe uwe na uhuru wako binafsi, anajua kwasasa ungependa uwe na usafiri wako,,..anafahamu hayo yote…Lakini unajiuliza inakuwaje sasa?

Sasa sikiliza hekima zake zinavyomalizia na kusema..

Mathayo 6:31 “Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33 BALI UTAFUTENI KWANZA UFALME WAKE, NA HAKI YAKE; NA HAYO YOTE MTAZIDISHIWA.

34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”.

Anasema Utafute kwanza ufalme wake…rafiki, tamani kumjua kwanza Mungu maishani mwako, tamani kufahamu hukumu zake na mapenzi yake kwako,..Weka mambo yako ya wokovu wako sawa sasa, uwe unahukika kwamba hata leo ukifa Mbingu ni yako, uwe na uhakika kwanza hata unyakuo ukipita leo usiku wewe utakuwa wa kwanza kuisikia sauti ya Bwana Yesu ikikuita mawinguni…Na kisha hayo mengine mwachie yeye atamalizana nayo.. NA HAYO YOTE MTAZIDISHIWA.

Fahamu kuwa Mungu anazo akili timamu zaidi ya unavyofikiri.

Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

JE! UMEFUNDISHWA?

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

KWA KUVUMILIA AKAIPATA ILE AHADI.

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

WALIO NA HEKIMA NDIO WATAKAOELEWA


Rudi Nyumbani

Print this post

NEHUSHTANI (NYOKA WA SHABA).

Musa alipewa maagizo na Mungu atengeneze nyoka wa shaba, amning’inize ili wale wote waliomuasi Bwana watakapomtazama nyoka Yule wapone saa ile ile.

Hesabu 21: 8 ‘’Bwana akamwambia Musa, Jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti, na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo ataishi.

9 Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti, hata ikiwa nyoka amemwuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya shaba, akaishi’’.

Lakini Mungu hakuwahi kuwaagiza Wana wa Israeli kuwa wakati wowote watakapokutana na madhara au matatizo basi wamsimamishe nyoka wa shaba wamtazame ili wapone, hakuwahi kufanya hivyo, lakini wana wa Israeli walitazama wakagandua SIRI ndani yake, wakasema ni lazima kutakuwa na uponyaji Fulani kwenye nyoka wa shaba kama sivyo Mungu asingemwagiza Musa kuiunda, hivyo ngoja tujijengee utaratibu wetu, wa kuifanyia ibada, na kumwomba Mungu kupitia ile naye Mungu atatusikia dua zetu..

Hivyo hilo jambo lilikuja kuendelea hivyo kwa mamia ya miaka mbeleni, mpaka likajengewa madhabahu kubwa na kuwa jambo maarufu sana Israeli, watu wakawa wanakwenda kuiinamia ile sanamu ya nyoka na kumwomba Mungu wa Israeli kupitia ile awaponye matatizo yao, wakaifukizia uvumba..

Hawakujua hilo lilikuwa ni chukizo kubwa sana kwa Mungu ndilo lililowapelekea hata kukumbana na matatizo yote yale ikiwemo kuchukuliwa utumwani tena.. Ndipo sasa baada ya miaka mingi sana kupita akatokea mfalme mmoja anayeitwa Hezekia yeye ndiye aliyefanikiwa kuliona hilo chukizo mara moja, Tusome:

2 WAFALME: 18:1 ‘’Ikawa katika mwaka wa tatu wa Hoshea, mwana wa Ela, mfalme wa Israeli, Hezekia, mwana wa Ahazi, mfalme wa Yuda, alianza kutawala.

2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na kenda katika Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Abiya, binti Zekaria.

3 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, mfano wa yote aliyoyafanya Daudi, baba yake.

4 Alipaondoa mahali pa juu, akazibomoa nguzo, akaikata hiyo Ashera; akaivunja vipande vipande ILE NYOKA YA SHABA ALIYOIFANYA MUSA; maana hata siku zile wana wa Israeli walikuwa wakiifukizia uvumba; naye akaiita jina lake NEHUSHTANI

5 Alimtumaini Bwana, Mungu wa Israeli; hata baada yake hapakuwa na mfano wake katika wafalme wote wa Yuda, wala katika hao waliomtangulia’’.

Embu jaribu kutafakari kwa utulivu uone kitu hapo! AGIZO lilikuwa ni la Mungu mwenyewe lakini sasa linageuka kuwa kitanzi na kikwazo kikubwa sana kwa watu…Tunaweza kuwalaumu wale tukasema walipungukiwa na akili lakini nataka nikuambie sisi wa kizazi hiki ndio tuliopungukiwa akili zaidi ya wale..Tutaona ni kwa namna gani tunafanya makubwa zaidi ya wao.

Mungu alimwagiza Musa achonge nyoka wa shaba kama ISHARA tu! ya kitu Fulani tu rohoni, nacho ndicho tunakuja kukiona sisi watu wa agano jipya, kuwa tendo lile Mungu aliliruhusu lifanyike vile kumfunua Bwana wetu Yesu Kristo atakapotundikwa msalabani kwamba kila mtu atakayemwamini aokolewe, hilo tunalithibitisha kwa maneno yake mwenyewe..

Yohana 3:14 ‘’Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyohivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa;

15 ili kila mtu aaminiye awe na uzima wa milele katika yeye’’.

… lakini hakukuwa na kitu chochote cha maana ndani ya ile SHABA, uponyaji halisi haukuwa ndani ya shaba ile bali ulitoka kwa Mungu mwenyewe..matokeo yake watu wakaacha kumtazama Mungu ambaye ni mponyaji wao wakaigeukia shaba isiyoweza kusema, wala kunena, wala kuzungumza..

Leo hii tunajua ni kweli Mungu alimwagiza Elisha achukue CHUMVI na kuitia katika chemchemi ya maji iliyokuwa inazaa mapooza..Na baadaye maji yale yakawa matamu,.Lakini kumbuka sio chumvi iliyotibu maji bali ni Mungu ndiye aliyefanya vile, lakini ni kwanini leo hii tunaihusisha chumvi na mambo ya ibada ikiwa hatujaongozwa kuitumia?.Nasi tunasema vile vile kama wana wa Israeli, Mungu kaweka uponyaji wa kiungu ndani ya chumvi,..tunasema kuna nguvu fulani ndani ya chumvi kama sivyo kwanini Mungu alimwagiza Elisha aiweke katika maji?…Tunamtia Mungu wivu pasipo sisi kujijua..

Halikadhalika tunayapa MAJI heshima, na kusema maji yana nguvu ya kusafisha mtu ndani yake, na kumtakasa, Tunamweka nyuma Mungu tunayapa maji heshima, ndugu Huko ni sawa kuiabudu sanamu ya Shaba.

Vivyo hivyo na vitu vingine vyote, tunasema UDONGO unabeba uhai, kwahiyo tukiumwaga kwenye biashara zetu, utazifufua, huku tukishikilia kile Bwana Yesu alichokifanya alipotengeneza TOPE ardhini na kumpaka Yule kipofu machoni, na macho yake kufumbuka, tunasema kama udongo usingekuwa na uponyaji Fulani Yesu asingeagizwa kutengeneza tope na kumpa kipofu..na kibaya zaidi mpaka tumeshavipa majina kama VITENDEA KAZI VYA KIROHO.

Tunahusisha MISALABA katika Ibada zetu. Kama unapenda msalaba wako kwanini usiunig’inize nyumbani kwako kama kumbukumbu lako la Bwana kukufia msalabani, lakini ni kwanini unakwenda kuuinamia, kuomba kupitia huo, unadhani unampa Mungu heshima hujui kuwa ni ASHERA hilo umeiweka moyoni mwako.

Na mambo mengine mengi, tunayafanya hatujui kuwa ndivyo tunavyomtia Mungu wivu. Fumbua macho yako, utoke kwenye uchanga wa kiroho, ikiwa Mungu amekuongoza kutumia mojawapo ya vitu hivyo kama ishara ya kitu Mungu anachokifanya rohoni ni sawa, kama amekuongoza kutumia maji tumia, amekuongoza kutumia mafuta tumia, na uthibitisho wa kuwa umeongozwa na Mungu kufanya hivyo, ni kwamba hakitakuwa unakirudia rudia,….Elisha halikuwa hatumii chumvi kila tatizo linalokuja mbele yake…Wala sio kila mgonjwa aliyekuja mbele yake alikuwa anamwambia akaoge mto Yordani mara saba. Alikuwa anafanya vile pale alipokuwa anaongozwa tu! Na sisi tunapaswa tuwe hivyo hivyo.

lakini kama tunageuza Imani yetu kutoka katika nguvu ya uweza wa DAMU YA YESU inayoweza kufuta na kuondoa kila kitu na kuvipa vitu hivyo visivyo na uhai heshima Fulani ya kiroho kwamba vina nguvu Fulani au uwezo Fulani wa wa kusababisha mambo, basi tujue moja kwa moja tunamfanyia ibada shetani. Na Mungu anachukizwa nazo kupindukia kwa namna ile ile anavyochukizwa na waabudu baali na Jua.

Na madhara yake ni kwamba, Mungu atatupiga kwa kukosa kwetu maarifa, wakati mwingine badala ya tatizo kuisha ndivyo litakavyoongezeka, kwasababu biblia inasema ni heri ungekutana na ghadhabu ya Mungu kuliko WIVU wake, na ibada zote za sanamu zinaleta wivu mbele za Mungu.

Mithali 27:4 ‘Ghadhabu ni kali, na hasira ni gharika; Lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya WIVU’.

Wimbo uliobora 8: 6“………….wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu.”

Huu ni wakati wa kutubu (yaani kugeuka), na kumwabudu yeye katika Roho na Kweli.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo lihimidiwe milele na milele. Amin.

 Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa  Maombezi, Ushauri au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312



Mada Zinazoendana:

FIMBO YA HARUNI!

HISIA YA MUNGU ILIYO MBAYA KULIKO ZOTE.

MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.

FAHAMU ZA WATU HUWA ZINAONDOLEWA NA NINI?


Rudi Nyumbani

Print this post

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.

 Shalom. Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Neno la Kristo linasema:

1 Petro 3:7 “Kadhalika ninyi waume, KAENI NA WAKE ZENU KWA AKILI; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.”

Agizo hilo biblia iliyotoa linawahusu wanaume waliooa , na si kila mwanamume tu!..kwasababu utasikia mtu ambaye anaishi na mwanamke ambaye hawajaoana, au anaishi na mwanamke ambaye si mke wake, bali ni mke wa mtu mwingine…. anakwambia… “Biblia imetuambia tuishi na wake zetu kwa akili”… nataka nikuambia ndugu hapo utakuwa huishi kwa akili, bali kwa kukosa akili…kwasababu mtakuwa mnafanya uzinzi na uasherati! Utasema hilo lipo wapi katika maandiko

Mithali 6: 32 “Mtu aziniye na MWANAMKE HANA AKILI KABISA; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake. 33 Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima; Wala fedheha yake haitafutika”.

Umeona? Akili inayozungumziwa hapo?..sio akili ya kuwa beberu ndani ya nyumba, au kuchepuka.. Ikiwa na maana kuwa moja wapo ya akili anazotakiwa mwanamume awe nazo anapoishi na mke wake ndio hiyo… “ KUWA MWAMINIFU KATIKA NDOA YAKE KWA KUJIEPUSHA NA ZINAA NJE YA NDOA YAKE”.

Kwasababu biblia inasema mtu aziniye na mwanamke atapata jeraha na kujivunjiwa heshima yake..itakufaidia nini unafanya zinaa nje ya ndoa yako halafu siku moja unafumaniwa na watu wanaanza kukunyooshea kidole?..hapo utakuwa umefanya jambo la kipumbavu, na biblia inasema fedheha yako haitafutika..Ni doa la daima.

Na hiyo AKILI ya kushinda, uasherati inakuja kwa kumwamini Yesu Kristo tu!, na kuoshwa dhambi zako kwa damu yake na kufanyika kiumbe kipya…haiji kwa kuongeza mke wa pili au watatu…Yesu pekee ndiye atakayeweza kukuondolea kiu ya mambo yote machafu ya ulimwengu huu.

⏩Maana nyingine ya kuishi na mke kwa akili, ni kumpenda na kumjali, upendo husitiri mambo mengi sana..Na hakuna mtu anayechukia kupendwa, kwahiyo upendo wa kweli na wa dhati ukiwepo hakuna matatizo yoyote yatakayojitokeza katika maisha ya ndoa..kutakuwa siku zote ni furaha, hiyo nayo ni akili.

⏩Maana nyingine ya kuishi na mke kwa akili, ni kugundua kasoro zake, na mapungufu yake, na kujua namna ya kuyatatua hayo ki BIBLIA!..Zingatia hilo neno KI BIBLIA! Sio kwa kutumia hekima za waswahili, au wasanii, au mila, au marafiki hapana! Bali biblia…epuka sana kutafuta suluhisho la “wahenga walisema”..au “wazee wazamani walisema” au “watu wanasemaga”…badala yake ni lazima UJIFUNZE kutafuta suluhisho kutoka kwenye Biblia(Maandiko matakatifu). Hekima za watu wa ulimwengu huu, zinafaa kwa baadhi ya mambo lakini si yote! Asilimia kubwa ya hekima za dunia hii zinazoshauri kuhusu masuala ya ndoa zinapotosha nyingi ni za Yule adui.

Kwahiyo hapo, ni lazima MWANAMUME ulijue NENO LA MUNGU kwa wingi ndani yako, hiyo ndio AKILI ya kuishi na mke wako?.

⏩Na maana ya mwisho ya kuishi kwa akili ni kuishi kwa Malengo Fulani ya kimaisha, ambayo hayakinzani na Neno la Mungu, hapa ndio linakuja suala la kupanga maisha na namna ya kujiongezea kipato kwa kazi zinazompa Mungu utukufu na mambo yote yanayofanana na hayo kwa ajili ya maisha mazuri ya familia.

⏩Lakini pia kumbuka Neno la Mungu halijamzuia pia mwanamke kuishi na mwanamume kwa akili, kwasababu na yeye kapewa akili vile vile, nanapaswa na yeye pia aishi na mume wake kwa akili, Kwa kujiepusha na zinaa na mambo yote tuliyojifunza hapo juu.

Pia wewe kama mwanamke soma vifungu hivi vitakusaidi kujua mwanamke mwenye akili kibiblia ni yupi..si yule wa kukaa vibarazani na kuwasema watu.

Mithali 31: 10 “Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani.

11 Moyo wa mumewe humwamini, Wala hatakosa kupata mapato.

12 Humtendea mema wala si mabaya, Siku zote za maisha yake.

13 Hutafuta sufu na kitani; Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo.

14 Afanana na merikebu za biashara; Huleta chakula chake kutoka mbali.

15 Tena huamka, kabla haujaisha usiku; Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula; Na wajakazi wake sehemu zao.

16 Huangalia shamba, akalinunua; Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.

17 Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi; Hutia mikono yake nguvu.

18 Huona kama bidhaa yake ina faida; Taa yake haizimiki usiku.

19 Hutia mikono yake katika kusokota; Na mikono yake huishika pia.

20 Huwakunjulia maskini mikono yake; Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake.

21 Hawahofii theluji watu wa nyumbani mwake; Maana wote wa nyumbani mwake huvikwa nguo nyekundu.

22 Hujifanyia mazulia ya urembo; Mavazi yake ni kitani safi na urujuani.

23 Mume wake hujulikana malangoni; Aketipo pamoja na wazee wa nchi.

24 Hufanya nguo za kitani na kuziuza; Huwapa wafanya biashara mishipi.

25 Nguvu na hadhi ndiyo mavazi yake; Anaucheka wakati ujao.

26 Hufumbua kinywa chake kwa hekima, Na sheria ya wema i katika ulimi wake.

27 Huangalia sana njia za watu wa nyumbani mwake; Wala hali chakula cha uvivu.

28 Wanawe huondoka na kumwita heri; Mumewe naye humsifu, na kusema,

29 Binti za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe umewapita wote.

30 Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa. 31 Mpe mapato ya mikono yake, Na matendo yake yamsifu malangoni.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa Maombezi, Ushauri au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225683036618/ +225789001312



Mada Zinazoendana:

FAHAMU ZA WATU HUWA ZINAONDOLEWA NA NINI?

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

‘’MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI’’..NA NDIVYO ILIVYO KWA UASHERATI

NINI TOFAUTI KATI YA UZINZI NA UASHERATI ?


Rudi Nyumbani

Print this post

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

Ukisoma vitabu vya Injili utaona mfano wa kwanza kabisa BWANA YESU alioutoa ni ule mfano wa Mpanzi, utaona jinsi mpanzi alivyotoka na kwenda kupanda mbegu zake, ukiendelea kusoma pale utagundua kuwa ule mfano haukueleweka kwa wengi, sio tu kwa makutano bali pia kwa wanafunzi wake..Lakini walipomfuata na kumwomba awafafanulie kuna kauli Bwana Yesu aliitoa pale nataka tuione; nayo ni hii:

Marko 4.13 ‘Akawaambia, Hamjui mfano huu? BASI MIFANO YOTE MTAITAMBUAJE?’.

Tafakari hilo Neno, BASI MIFANO YOTE MTAITAMBUAJE?..Kumbe Mfano huo ni msingi wa kuielewa na mifano mingine yote iliyobakia, kwa watu wanaofahamu somo la Hisabati vizuri wanaelewa kuwa kanuni ya PAI π..Ni kiungo kikuu cha Hisabati, ukitaka kutafuata Eneo la kitu chochote kile iwe ni duara au tufe, pipa, n.k. basi PAI ni lazima itumike.

Vivyo hivyo tukirudi kwenye maandiko ili kuielewa mifano yote Yesu aliyokuwa anaifundisha kuhusiana na ufalme wa mbinguni basi tafsiri ya mfano ule wa Mpanzi ni lazima kuulewa vinginevyo hutaambulia chochote.

Sasa tukirudi katika huo mfano kwa kuwa unajulikana hatutaweza kuuleza wote hapa, lakini mpanzi Yule alipotoka kwenda shambani malengo yake yalikuwa ni mbegu zake zote zimee vizuri na kuzaa nyingine 30, nyingine 60, nyingine 100. Lakini tunasoma zilikumbana na changamoto kadhaa kabla ya kufikia hatua ya kuzaa matunda.

Sasa kabla hatujafika mbali nataka tuone mifano miwili iliyofuata mbele yake baada ya huo..Ili itusaidie kuunga kiini cha somo letu la leo vizuri ..

Tusome..

Marko 4:26 ‘Akasema, Ufalme wa Mungu, mfano wake ni kama mtu aliyemwaga mbegu juu ya nchi;

27 akawa akilala na kuondoka, usiku na mchana, nayo mbegu ikamea na kukua, asivyojua yeye.

28 Maana nchi huzaa yenyewe; kwanza jani, tena suke, kisha ngano pevu katika suke.

29 Hata matunda yakiiva, mara atapeleka mundu, kwa kuwa mavuno yamefika.

30 Akasema, Tuulinganishe na nini ufalme wa Mungu? Au tuutie katika mfano gani?

31 Ni kama punje ya haradali, ambayo ipandwapo katika nchi, ingawa ni ndogo kuliko mbegu zote zilizo katika nchi,

32 lakini ikiisha kupandwa hukua, ikawa kubwa kuliko miti yote ya mboga, ikafanya matawi makubwa; hata ndege wa angani waweza kukaa chini ya uvuli wake.

33 Kwa mifano mingi ya namna hii alikuwa akisema nao neno lake, kwa kadiri walivyoweza kulisikia’.

AMEN.

Sasa Nataka tuichukue kwa pamoja mifano hii mitatu, tuunde kitu ambacho kitatusaidia wote,..Mifano hii, yote inaonyesha historia ya mbegu, jinsi zilipotoka na jinsi zilivyoishia isipokuwa katika TABIA tofauti tofauti na mapito tofauti tofauti.

Kumbuka kule nyumba kabisa kwenye mfano wa mpanzi Bwana Yesu alitoa tafsiri ya Ile mbegu kuwa lile ni NENO LA Mungu (Luka 8:11) lililopandwa ndani ya moyo wa mtu. Hivyo Neno la Mungu linapopandwa katika moyo wa mtu katika hatua za awali penda lisipende litapita katika nyakati TATU kulingana na mifano hiyo mitatu.

1) ⏩Kwanza ni lazima lipitie changamoto: Mtu aliyepandwa atakumbana na udhia, na misongo ya hapa na pale, kulingana na ule mfano wa mpanzi, Hili ni jukumu la mhusika mwenyewe kuhakikisha kuwa haling’olewi na Yule adui, wala halisongwi.

2)⏩ Pili Litakuwa linamea lenyewe: Hili sio jukumu tena la mtu, bali ni jukumu la Mungu mwenyewe, wakati linavumilia vipindi vigumu vya hatihati ya kung’olewa au kusongwa, huku kwa nyuma siku baada ya siku linakuwa lenyewe taratibu.

3) ⏩Na Tatu japo litaanzia katika udogo sana, likishafikia ukomavu litakuwa kubwa kuliko miti mingine yote. Hivyo mwisho wa safari ya utunzaji wa mbegu ile. Basi litakuwa baraka kubwa sana kuliko chochote kile duniani.

Hivyo ndugu, ndio maana sasa baada ya mifano ya namna hiyo kuisha YESU akaanza kuwafundisha watu mifano inayoelezea thamani ya mbegu hiyo akiifananisha na Hazina kubwa sana na lulu za thamani ..utaona anasema, ufalme wa mbinguni umefanana na mfanyabiashara aliyekuwa anatafuta Lulu ya thamani kubwa, na alipoina akaenda kuuza vyote alivyonavyo na kwenda kuinunua lulu ile, anasema tena ni sawa na mtu aliyeona hazina iliyositirika katika shamba, alipoiona akaificha na kwa furaha akaenda kuuza vyote alivyonavyo na kwenda kulinunua shamba lile.

Hiyo yote ni kuonyesha kuwa ana AKILI sana mtu yule anayelisikia Neno la Mungu na kuzingatia kuliweka moyoni mwake, na kwenda kufanyia kazi kile anachofundishwa, anafanya bidii kulifakari Neno la Mungu, analiona kama almasi, anatafuta huku na kule huku akilinganisha na maandiko, akivulimilia dhiki zote zinazokuja kutokana na ukristo wake na itikadi zake kali za kuliishi Neno, na shutuma na kuchekwa, na kudharauliwa, na kutengwa, na kuchukiwa, akivumilia yote bila kuliacha hilo Neno lililopandwa moyoni mwake kudondoka, akihakikisha shughuli za ulimwengu huu hazimsongi mpaka anakosa muda wa kuwa karibu na Mungu wake, akihakikisha anapata muda mrefu wa kulitafakari Neno la Mungu kuliko kuchati..

Sasa Biblia inaeleza mtu huyo kuna faida kubwa inamngoja mbeleni yake.. Yeye kwa wakati huo hatajua chochote, wala hatafahamu kama kuna kitu kinakuwa ndani yake, anaweza kuona kama anafanya kitu ambacho hakimletei faida yoyote katika mwili, hakimwingizii pesa, hakimpi umaarufu, lakini kumbe kidogo kidogo, ile mbegu inamea, kutoka KUWA MBEGU MPAKA JANI MPAKA SUKE.. Na japo ilianza ndogo sana kama chembe ya haradali itakuwa yenyewe, kumbuka haihitaji msaada wowote kukuzwa na mtu, itakuwa na kuwa kubwa kuliko miti yote, na ndipo hapo watu watakuja kushangaa, kumetokea nini kwa mtu huyu tusiyemtazamia amekuwa hivi ghafla…Ndipo kama mfano unavyosema ndege watakuja kukaa chini ya huo mti, ndivyo itakavyokuwa kwa mtu huyo, atakuja kuwa msaada mkubwa kwa watu wengi kwa kila kitu. Kwa vitu vya rohoni na mwilini.

Hiyo ilimtokea kiongozi wetu mkuu YESU KRISTO, Biblia inasema alikuwa ni mtu wa kudharauliwa, wa kutokuaminiwa siku zote, lakini yeye alilitunza Neno la Mungu tangu utoto wake, mpaka utu uzima, mpaka alipofikia kilele sasa cha Neno lenyewe kutaka kuanza kuzaa matunda, ndipo walipomtambua kuwa Yule hakuwa mwanadamu wa kawaida..Utasoma pale walianza kujiuliza huyu sio Yule seremala, na ndugu zake tunao wote hapa? Sasa katolea wapi hekima yote hii ambayo hajasoma, na miujiza yote hii, ulimwengu mzima ulimfuata kumsikiliza, yeye ni nani hasa? Ukisoma biblia utaona kuna watu walitoka mpaka Uyunani huko kuja kutaka kumwona Bwana Yesu…Hayo ndio maajabu ya Neno la Mungu likitunzwa vizuri ndani ya mtu…Linafanya mambo makubwa, na ndio maana shetani katika hatua za kwanza atahakikisha kwa bidii zote analiondoa ndani yako.

Hizi ni siri kutoka kwa MKUU wetu YESU KRISTO, Kwamba kama na sisi tukizitumia, tutafika pale alipo yeye. Leo hii, mbegu nyingi zinatupwa ndani yako, unazidharau, kwasababu labda mtu huyo anayekuhubiria hajulikani, ni mtu tu wa mtaani unayemfahamu, lakini kumbuka ufalme wa Mungu ndani ya mtu unaanza kama chembe ya haradali, ndogo sana, maneno ambayo mtumishi yoyote yule wa kawaida anaweza akayabeba ndani yake, inaanza kwa maneno machache sana ya wokovu, ambayo baadaye yakiisha kukua ndani ya mtu yanaweza kuupindia ulimwengu mzima.. Usipuuzie Neno la Mungu leo unapolisikia, embu chukua hatua ya kuanza kulitunza, anza kulifanyia kazi, hakikisha shetani hakichukui hichi ulichokisia moyoni mwako, na dalili zitakazoonyesha hiyo mbegu inakuwa ni maadui kutokea, shetani atafanya juu chini kuing’oa lakini wewe zingatia kanuni hizo, UVUMILIE yote, iwe ni dhiki, iwe ni misongo ya mambo ya ulimwengu huu..Fanya bidii kulitunza Neno la Mungu, faida yake utaiona baada ya muda Fulani.

Ni matumaini yangu, utatubu leo na kumkabidhi Bwana maisha yako. Huo ndio mwanzo wa kuitunza mbegu yao.

Ubarikiwe sana.

Amen.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa Maombezi, Ushauri, au Ratiba za Ibada wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312


Mada Zinazoendana:

JE! WEWE NI MBEGU HALISI?

USIACHE KUJIFUNZA NENO LA MUNGU

NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.

TUNAPOSEMA TUISHI KWA NENO, INAMAANISHA TUISHI MAISHA YA NAMNA GANI?


Rudi Nyumbani

Print this post

OKOA BADALA YA KUANGAMIZA!

Shalom, Mwana wa Mungu karibu tujifunze maandiko…Leo tutajifunza kwa Neema za Bwana namna ya kuokoa roho.

Bwana Yesu alisema “sikuja kuziangamiza roho bali kuziokoa (Luka 9:56)” sentensi hiyo aliisema baada ya wanafunzi wake kumwomba ashushe moto uwaangamiza wale watu wa Samaria waliokataa kumpokea…Lakini kwanini alisema vile kuwa hakuja kuziangamiza bali kuziokoa?…ni kwasababu alikuwa na uwezo wa kuziangamiza lakini hakutaka kufanya vile..kinyume chake alitafuta namna ya kuwafikishia wokovu na sio kuwaua.

Wakati mwingine tunaweza tukawa na silaha mikononi mwetu au midomoni mwetu tulizopewa na Mungu kihalali kabisa za kujeruhi na kuangusha watu wote wanaokwenda kinyume na sisi..lakini tukikosa hekima kama aliyokuwa nayo Bwana tutajikuta tunaangamiza roho badala ya kuokoa.

Hebu mtafakari Musa, wakati wana wa Israeli wanamkosea Mungu kule jangwani…Mungu alimwambia Musa ajitenge na wale watu ili apate kuwaangamiza…na atamfanya Musa kuwa Taifa kubwa, atampa uzao utakaoirithi nchi….ingekuwa ni mmojawapo wa sisi tungesema asante Mungu, kwa kuwa umeteta nao wanaoteta nami, lakini tunaona Musa, alilipindua wazo la Mungu na kuanza kuwaombea msamaha ndugu zake na kuwatafutia upatanisho na Mungu, na Mungu akalisikiliza ushauri wa Musa na kughairi mawazo yake…

Sasa tuchukulie mfano Musa, angekubali kujitenga nao, unadhani, kulikuwa kuna kosa lolote pale? hapana Mungu kweli angewaangamiza wale watu na angeenda kumfanya Musa kuwa Taifa kubwa kama alivyomwahidia..Lakini Musa angekuwa hajatenda kwa busara mashauri yale yalitoka kweli kwa Mungu, angekuwa hajastahili kuwa kiongozi bora kwasababu hakuizuia ghadhabu ya Mungu juu ya watu wake. Kwahiyo pengine hata Mungu asingemtukuza Musa kwa kiwango hichi alichomtukuza sasa.

Kutoka 32:9 “Tena Bwana akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu

10 basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.

11 Musa akamsihi sana Bwana, Mungu wake, na kusema, Bwana, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu?

12 Kwa nini Wamisri kunena, wakisema, Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi? Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako.

13 Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele.

14 Na Bwana akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake”.

Kwahiyo hiyo inatufundisha kuwa siyo kila fursa au mamlaka tunayopewa na Mungu, tuyatumie tu bila kutafakari vizuri..Mungu wetu hajatuumba kama maroboti kwamba yeye ni wa kusema na sisi ni wakufuata tu pasipo kutafakari..hapana! huo ni utumwa na sisi sio watumwa sisi ni wana, tunazungumza na Baba yetu na kushauriana naye…ametuumba tuzungumze naye, tusemezane naye, tupeane naye mashauri.

Isaya 1: 18 “Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu”.

Ndio maana Musa alisemezana na Bwana na akasafisha dhambi za wana wa Israeli zilizokuwa nyekundu kama bendera, na akazifanya kuwa nyeupe kama sufu. Haleluya!

Mungu anaweza kumweka mtu anayekuchukia, au anayekupiga vita mikononi mwako, au mtu ambaye alikufanyia visa Fulani, ukapata madhara fulani…Mungu anaweza kumweka mikononi mwako kiasi kwamba ukisema tu neno moja umemmaliza, au ukifanya jambo Fulani tu, habari yake imekwisha ikawa ni kweli Mungu kamtia mikononi mwako ili kumlipizia kisasi, kwa ubaya aliokufanyia….kama vile Mungu alivyomtia Sauli mikononi mwa Daudi..akajua kabisa hii ni fursa ya kummaliza lakini hakufanya hivyo…nasi pia huo usiwe wakati wa kummaliza, badala yake uitumie fursa hiyo kumgeuza kwa Kristo, huo ndio wakati wa kusemezana na Bwana juu ya dhambi zake zote, na kumwombea Msamaha…hakika ukifanya hivyo na kuigeuza hasira ya Bwana, Bwana atakupenda zaidi ya anavyokupenda sasa…atakutukuza zaidi ya anavyokutukuza sasa…

Utasema hiyo habari ya Musa na Daudi ilikuwa ni ya agano la kale, vipi kuhusu agano jipya, je! Kuna mtu yeyote alishawahi kufanya hivyo..Jibu ni ndio! Hata katika agano jipya tunayo hiyo mifano.

Tunasoma habari za Paulo na wenzake, wakati mmoja walipokwenda Makedonia kuhubiri, walikutana na mtu mwenye pepo na walipomtoa Yule pepo, ndipo wakuu wa mji wakawakamata na kuwachapa bakora na kisha kuwatupa gerezani.

Sasa lile jambo halikumpendeza sana Mungu, na hivyo Bwana akawatengenezea njia ya kutoka mule gerezani, akamtuma malaika wake usiku ule wakati Paulo na Sila walipokuwa wanamsifu Mungu, ghafla vifungo vikalegea na milango ya gereza ikafunguka…sasa Lengo la Yule malaika kufungua milango ya gereza haikuwa tu kuwafurahisha wale watu , hapana ilikuwa ni ili Paulo na Sila watoke!!, waondoke mule gerezani,..Kama vile Yule malaika alivyomtoa Petro gerezani wakati Fulani alipokuwa amefungwa.

Lakini tunasoma Paulo na Sila walilitengua agizo la Bwana, badala ya kutoka na kwenda zao, waliendelea kukaa mule gerezani japokuwa Mungu aliwafungulia mlango wa kutoka…lakini walitafakari mara mbili mbili, endapo tukitoka na kwenda zetu tutakuwa kweli hatujatenda dhambi lakini tutaacha madhara makubwa huku nyuma, tutasababisha kifo badala ya kuokoa roho, na zamani zile utawala wa Rumi, mfungwa yoyote akitoroka kinachobakia kwake ni kifo tu, na ndio maana Yule askari ilikuwa nusu ajiue, lakini Paulo na Sila wakamzuia.

kwahiyo wakaitumia ile nafasi sio kwa faida yao bali kwa faida ya wengine, ndio tunaona wakaenda kumwuhubiria Yule askari injili pamoja na familia yake wote wakaokoka, na mwisho wa siku kesho yake asubuhi wakatolewa gerezani, kwahiyo ikawa faida kwao mara mbili.

Matendo 16: 22 “Makutano wote wakaondoka wakawaendea, makadhi wakawavua nguo zao kwa nguvu, wakatoa amri wapigwe kwa bakora.

23 Na walipokwisha kuwapiga mapigo mengi, wakawatupa gerezani, wakamwamuru mlinzi wa gereza awalinde sana.

24 Naye akiisha kupata amri hii akawatupa katika chumba cha ndani, akawafunga miguu kwa mkatale.

25 Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.

26 GHAFULA PAKAWA TETEMEKO KUU LA NCHI, HATA MISINGI YA GEREZA IKATIKISIKA, NA MARA HIYO MILANGO IKAFUNGUKA, VIFUNGO VYA WOTE VIKALEGEZWA.

27 Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia

28 Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa.

29 Akataka taa ziletwe, akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila;

30 kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka?

31 Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.

32 Wakamwambia neno la Bwana, yeye na watu wote waliomo nyumbani mwake.

33 Akawakaribisha saa ile ile ya usiku, akawaosha mapigo yao, kisha akabatizwa, yeye na watu wake wote wakati uo huo.

34 Akawaleta juu nyumbani kwake, akawaandalia chakula, akafurahi sana, yeye na nyumba yake yote, maana amekwisha kumwamini Mungu.

35 Kulipopambauka makadhi wakawatuma wakubwa wa askari wakisema, Waacheni watu wale waende zao.

36 Yule mlinzi wa gereza akamwarifu Paulo maneno haya akisema, Makadhi wametuma watu ili mfunguliwe; basi, sasa tokeni nje, enendeni zenu kwa amani”.

Sasa hebu fikiri endapo Paulo na Sila wangeondoka usiku ule mule gerezani, na kusema safi sana! Mungu katupigania! Kawaaibisha maadui zetu!…. ni wazi kuwa wangeshampoteza Askari na kusudi la wao kwenda makedonia lingekuwa ni sifuri kwa maana wenyewe walikwenda kwa nia ya kuhubiri injili, na sasa hapa ni sawa na wamemsababishia wengine mauti.

Kwahiyo ndugu tunajifunza, sio kila fursa ya kumpiga adui yako ni mapenzi kamili ya Mungu, sio kila mlango Mungu anaokufungulia ni wa kuutumia pasipo kutafakari, aliyekutukana, aliyekuaibisha, aliyekupiga, aliyekunyima kazi wakati Fulani tena akakufanyia na visa juu, aliyekurusha, aliyekuharibia mipango yako na maisha yako, sasa Mungu kamleta mikononi mwako..huo sio wakati wa kuitumia hiyo fursa Mungu aliyokuwekea mbele yako pasipo hekima!! Itumie hiyo KUOKOA ROHO, BADALA YA KUANGAMIZA. Hicho ndio kitu Mungu anachotaka kuona kwetu!.

Kuna muhubiri mmoja, ambaye alikuwa ni Nabii, siku moja wakati anahubiri kanisani kwake malaika wa Bwana alimwambia atazame mwisho kabisa wa kanisa, na alipotazama akaona watu wawili kwa mbali mwanamume na mwanamke wanafanya kitendo kichafu cha kunyonyana ndimi na hiyo ilikuwa ni katikati ya ibada…Yule muhubiri akakasirika sana, akawa anawaendea…wakati yupo njiani anawaendea Yule malaika aliyemwambia atazame nyuma ya kanisa, huyo huyo akamwambia sema Neno lolote na mimi nitalitimiza hilo neno saa hivi hivi kama ulivyosema…yaani maana yake angesema “Bwana naomba waanguke sasa hivi wafe, wangekufa saa ile ile”..na alipofika pale Yule muhubiri..kitu fulani kikamwingia ndani yake, kama huruma Fulani hivi… akasema “nimewasamehe”…Baadaye alivyomaliza ibada, sauti ikazungumza ndani ya moyo wake na kumwambia..”hicho ndio nilichokuwa nataka kusikia kutoka kwako”…msamaha…

Ni wazi kuwa hao watu kwa msamaha huo, baadaye walitubu na kumgeukia Mungu kwa kumaanisha.

Umeona? Epuka injili unazohubiriwa kila wakati piga adui yako, usiposamehe kuna wakati nawe utafika utamkosea Mungu, naye Mungu hatakusamehe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa Maombezi, Ushauri, au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Print this post