NUHU ALIISHI MIAKA MINGAPI?

NUHU ALIISHI MIAKA MINGAPI?

Nuhu aliishi jumla ya miaka 950, hiyo ndio jumla ya miaka yake…Aliishi miaka 600 kabla ya Gharika, na aliishi miaka mingine 350 baada ya gharika.

Mwanzo 9:28 “Na Nuhu akaishi baada ya ile gharika miaka mia tatu na hamsini.

29 Siku zote za Nuhu zilikuwa miaka mia kenda na hamsini, akafa”.

Nuhu na wanawe ndio walikuwa watu wamwisho kuishi umri mrefu, kwani baada ya gharika Bwana Mungu alisema miaka ya Mwanadamu itakuwa 120 tu!

Tunajifunza kuwa si lishe bora ndiyo inayompa mtu maisha marefu, wala si kuzingatia mazoezi la hapana! Kinachompa mtu maisha marefu ni KUMCHA BWANA, Laiti kama wanadamu wa wakati ule wasingefanya maovu kiasi kile cha kuleta gharika juu ya nchi…mpaka leo wanadamu tungekuwa tunaishi mamia ya miaka, lakini kutokana na maovu yetu miaka yetu imeshusha namna hii.

Hivyo tukitaka tuishi maisha marefu katika haya maisha tuliyopewa hatuna budi kumcha Mungu, lakini tukivunja amri zake na kuishi maisha ya dhambi ndio tunakivuta kifo chetu karibu nasi.

Bwana atusaidie sana kwa hilo.


Mada Nyinginezo:

NUHU ALIKUWA NA WATOTO WANGAPI?

NUHU ALIJENGA SAFINA KWA MIAKA MINGAPI?

NUHU ALIWALETAJE LETAJE WANYAMA KWENYE SAFINA?

NUHU WA SASA NI YUPI?.


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments