Ulishawahi kuona mwanamke anajifungua mtoto bila kusikia utungu wowote? Hilo jambo bila shaka Litakuwa ni la ajabu… kwasababu haliendani kabisa na kanuni za asili …
hata maandiko yanasema hivyo..
Isaya 66:7-8
[7]Kabla hajaona utungu alizaa; Kabla maumivu yake hayajampata, Alizaa mtoto mwanamume. [8]Ni nani aliyesikia neno kama hili? Ni nani aliyeona mambo kama haya? Je! Nchi yaweza kuzaliwa siku moja? Taifa laweza kuzaliwa mara?..
[7]Kabla hajaona utungu alizaa; Kabla maumivu yake hayajampata, Alizaa mtoto mwanamume.
[8]Ni nani aliyesikia neno kama hili? Ni nani aliyeona mambo kama haya? Je! Nchi yaweza kuzaliwa siku moja? Taifa laweza kuzaliwa mara?..
Ni kanuni ya asili ili kiumbe kipya kizaliwe, mzaaji ni lazima apate utungu tu kama malipo ya kile akizaacho ..kila mwanadamu unayemwona chini ya jua, kuna mtu alipata maumivu kwa ajili yake..
Kanuni hii ipo rohoni pia…Kila mtakatifu unayemwona (aliyesimama), haikuwa bure bure…au kirahisi rahisi tu kama unavyodhani, kuna Waliopitia utungu juu yao…
Utauliza hili lipo wapi Kwenye maandiko?.
Paulo kwa Wagalatia,aliandika maneno haya;
Wagalatia 4:19
[19]Vitoto vyangu, ambao kwamba nawaonea utungu tena mpaka Kristo aumbike ndani yenu;
Paulo anawalilia wagalatia, kwa jinsi walivyoiacha neema ya Kristo, na kurudia mafundisho ya kiyahudi..anasema nawaonea utungu tena….tafsiri yake ni kuwa hapo nyuma alishawahi kuwaonea utungu…akawazaa…lakini sasa ni kama vile wanahitaji kuzaliwa tena….
Hivyo watu wote waliozaliwa mara ya pili wapo Waliowanea utungu.
1). Hulia na kuugua:
Maana yake hiki ni kipindi cha machozi na kuomba juu ya wale wote unaotamani wampokee Kristo..ndiyo tabia waliokuwa nayo mitume.
Matendo ya Mitume 20:31
[31]Kwa hiyo kesheni, mkikumbuka ya kwamba miaka mitatu, usiku na mchana, sikuacha kumwonya kila mtu kwa machozi.
Watu wengi wanatamani kuona geuko la dhati kwa jamii zao, rafiki zao, waume zao, watoto wao lakini hawana muda wa kuwaombea kwa kuzama sana kwa kipindi kirefu na wakati mwingine kufunga huku wakiwahubiria…wanaikwepa Kanuni hii ya kiumbe kipya kuzaliwa.
Hichi kipindi wanawake wengi huchungulia kifo, kwa sababu ya maumivu, au shinikizo au kutokwa na damu nyingi sana.
Ndivyo ilivyo pale unapojaribu, Kumvuta mwenye dhambi aifikie toba ya kweli, adui huanza kuinua vita, dhidi yako wewe na huyo unayemzaa.. lile joka litataka kufanya vita na wewe.
Ufunuo wa Yohana 12:1-4
[1]Na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili. [2]Naye alikuwa ana mimba, akilia, hali ana utungu na kuumwa katika kuzaa. [3]Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba. [4]Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake.
[1]Na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili.
[2]Naye alikuwa ana mimba, akilia, hali ana utungu na kuumwa katika kuzaa.
[3]Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba.
[4]Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake.
Ukijikuta katika wakati huu fahamu ni kung’ang’ana kumfuatilia kondoo huyo bila kujali hali au vipingamizi…unaweza kuona visababu sababu visivyoeleweka, mara hataki tena kukusikiliza, mara anaumwa, mara ndugu zake wanampinga, mara anakuwa mzito.hapa hupaswi kukata tamaa..endelea kumfuatilia kwasababu hizo ni hila za adui kumzuia asikate shauri kwa Bwana Yesu..
Fahamu tu kazi yako si bure upo wakati ataamini na kugeuka kabisa kabisa kwasababu Nguvu uliyonayo na kuu kuliko ya ibilisi..na furaha yako itakuwa ni pamoja na malaika mbinguni. (Luka 15:10).
Pia Biblia inasema…
Yohana 16:21
[21]Mwanamke azaapo, yuna huzuni kwa kuwa saa yake imefika; lakini akiisha kuzaa mwana, haikumbuki tena ile dhiki, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtu ulimwenguni.
Upo wakati utayafurahia matunda yako. Siku utakapoona kupitia hao makumi, mamia, maelfu ya watu wanaokoka..na siku ile Bwana anakupa thawabu kwa tunda hilo ulilomzalia.
Swali ni je utungu wako upo wapi?.. ni wapi unaweza kusema yule ni mwana wangu nimemzaa mimi katika Kristo?..
Kwenda tu kusema Yesu anakupenda okoka, halafu ukamwongoza Sala ya toba na kumwacha…hili halimaanishi huyo ni mtoto wako. Ndio maana wapo watu wengi wanaosema leo wamemkiri Yesu, lakini ukiwaangalia sio viumbe vipya..kwasababu hawakuzaliwa, bali waliaminishwa tu.
Tukubali kuzaa kwa kuwafundisha, kuwaombea sana, na kuwafuatilia mpaka watakapokata shauri la kweli kumpokea Yesu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
DALILI ZIPI ZITAMTAMBULISHA MTU KUWA AMEFANYIKA KIUMBE KIPYA?
MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.
MAUMIVU NYUMA-YA-HUDUMA.
Print this post
SWALI: Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote ’
Kwanini ajiangue kwa namna hiyo angali yeye ndiye mwokozi wa kutegemewa kila kitu?
Yohana 16:23
[23]Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.
JIBU:
Kama tunavyojua hakukuwahi kutokea kiongozi aliyekuwa na matokeo makubwa duniani kama Yesu Kristo.
Namna ya uongozi wake, Kwa jinsi ulivyokuwa thabiti na bora Matokeo yake ndio tunayoana mpaka sasa duniani kwenye imani.
Hivyo maisha yake na huduma yake sio tu vinatufundisha njia ya wokovu lakini pia vinatufundisha namna kiongozi bora anavyopaswa Awe.
Matokeo Ya mitume wake kuwa nguzo kwa makanisa ya vizazi vyote ni matokeo ya namna ambavyo alivyowakuza anawakuza.
Bwana Yesu hakutengeneza Wafuasi, bali alitengeneza watu kama Yeye…Na hivyo katika kuwafundisha wanafunzi wake aliwakuza Ki vitendo zaidi kuliko maneno ya vitabu vingi vya kidini na mapokeo.
Kwamfano utaona kuna mahali anawatuma wawili waenda kuhubiri injili mahali ambapo angepaswa kwenda yeye mwenyewe, lakini aliwaacha waende.
Luka 10:1
Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.
Mahali pengine aliwaacha watoe pepo na waliposhindwa hakusema ‘wanangu nyie ni wachanga, basi nitakuwa nawasaidia tu’…hapana Kinyume chake aliwakemea Kwa upungufu wa imani zao.
Vivyo hivyo katika tukio hili, wanafunzi wake walitarajia kila siku watakaa naye wamuulize maswali yeye, kisha awajibie kutoka kwa Baba.. Ni sawa na mtoto mchanga ambaye kila siku anasubiria atafuniwe tu chakula apewe…unadhani hilo litaendelea sana?
Vivyo hivyo hilo halikuwa lengo la Bwana Yesu, bali alitaka kuwafundisha kanuni za wao wenyewe kumuuliza Mungu na kujibiwa moja kwa moja kama yeye alivyokuwa anajibiwa…
Na njia moja wapo ilikuwa ni yeye kuondoka, kisha kwa kile kitendo cha wao kumkosa Bwana wa kumuuliza, wajifunze kuomba kisha Roho ajae ndani yao, ndipo waanze sasa kupokea mafunuo ya kweli na ujasiri kutoka kwa Mungu..
Lakini pia waombe jambo lolote kwa jina la Yesu, wapokee mahitaji yao. Na Kweli mambo hayo yalianza Kutokea baadaya ya Pentekoste.. wote walikuwa ni kama ‘Yesu-dunia’ hakuna hata mmoja alifikiri au kuwaza kwamba kuna umuhimu tena wa Yesu kutembea nao, kimwili bali waliweza kuyafanya yote.
Hiyo ni tabia ya kiongozi bora…huwafanya wanafunzi wake kuwa kama yeye, na wakati mwingine kutenda hata zaidi ya yeye…Yesu aliwainua zaidi kwa kusema.
Yohana 14:12
[12]Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.
Hiyo ndio sababu kwanini aliwaambia hayo maneno.
Yohana 16:23-24
Hata sasa Bwana anataka kuona ukomavu kama huu ndani ya maisha ya wakristo wengi.. Ikiwa kila siku utakuwa unategemea Mchungaji wako akuombee, ni lini utaweza wewe mwenyewe kuomba na kuwaombea wengine? Sababu ya watu wengi kutojibiwa maombi yao na Mungu ni hiyo.. Ameshakomaa kiroho, Mungu anaona anaouwezo wa kupambana na tatizo yeye mwenyewe, atataka kiongozi wake amsaidie..
Hicho kitendo kinapunguza utendaji Kazi wa nguvu za Mungu, kwasababu yeye hataki tumgeuze mwanadamu Mungu..Ukiokoka, fahamu kuwa Roho Mtakatifu yupo ndani yako, na kuanzia huo wakati na kuendelea unawajibu wa kuufanyia mazoezi wokovu wako, jifunze kuomba mwenyewe, jifunze kuombea watu, soma biblia mwenyewe Mungu akufundishe..
Hizo ndio hatua bora za ukuaji kiroho.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
KUNA WAKATI YESU ATAPITA NA WATU HAWATAJUA.
TOFAUTISHA KATI YA MAFUNDISHO YA YESU, NA YA WAANDISHI.
ALITOKA HUKO, AKAENDA MAHALI KARIBU NA JANGWA.
Kila mahali pana mamlaka yake, na mamlaka hizo huwa ni wajibu kwa walio chini yake kuzitii. Kwamfano katika familia Mungu ameweka mamlaka, Baba awe kichwa, na mama msaidizi wake, hivyo ni wajibu wa watoto kuwatii wazazi wao . Familia haiwezi kusimama,.kama mtoto atataka nafasi ya baba, kwamba yeye ndio atoe maamuzi ya mwisho, au ajiamulie la kufanya, awapangie wazazi wake majukumu ya ndani. hilo haliwezekani.
Vilevile katika ngazi ya utawala wa kidunia, Mungu kaziweka mamlaka na anataka watu wote wazitii, kwasababu hazijaamuriwa na mwanadamu bali yeye Mungu mwenyewe..
Warumi 13:1-2
[1]Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. [2]Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu.
[1]Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu.
[2]Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu.
Tito 3:1-2
[1]Uwakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema; [2]wasimtukane mtu ye yote, wasiwe wagomvi, wawe wema, wakionyesha upole wote kwa watu wote.
Sasa hizi ni mamlaka za kidunia. Zipi kuhusu Mungu, unadhani hana mamlaka?
Mungu pia ameweka mamlaka yake duniani, ambayo ni kuu kupita hizo zote, na kupitia hiyo huwahudumia watu wake. Na anataka tuitii na kuitetemekea kwasababu ni yeye mwenyewe atendaye kazi kupitia hiyo.
Je mamlaka hiyo kaiweka kupitia nani?
Bila shaka kupitia wachungaji wetu/waangalizi wetu, ndani ya kanisa
Ni vema kufahamu kuwa kiongozi yoyote wa kiroho (anayeisimamia kweli). Hakujiteua mwenyewe kwenye nafasi hiyo. Mitume wa Yesu hawakujichagua wao. Bali walichaguliwa na Mungu mwenyewe.
Mtu yeyote aliyepewa maono ya kuanza kanisa, na ukajikuta upo chini yake, au kateuliwa na Roho Mtakatifu mwenyewe ndani ya kanisa (Matendo 14:23), Huyo ni wa kumtii sana. Kama vile unavyowatii watawala au mazazi wako kwenye familia, haijalishi atakuwa na mapungufu kiasi gani, au umri wake ni mdogo au mkubwa kiasi gani, awe mwenye uwezo au asiye na uwezo kiasi gani.
Kwanini uwaheshimu.
Hivyo wajibu ni wako kurudisha moyo wa upendo, na kuwasikiliza.
1 Wathesalonike 5:12-13
[12]Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni; [13]mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi.
Hivyo ni wajibu kuonyesha moyo wa kunyenyekea kwao.
Waebrania 13:17
[17]Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.
Hapo kwenye Waebrania 13:17b anasema..
..ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi
Na matokeo yake utendaji kazi ndani ya kanisani utakuwa hafifu. Ukishaanza kuonyesha tabia ya kutosikiliza unachoelekezwa, unapewa jukumu hutekelezi, hurudishi mrejesho, unafanya tofauti na wengine, yeye anataka uende kulia wewe unaenda kushoto, , yeye anafundisha hiki wewe unafundisha kile. Fahamu kuwa jambo hilo litamhuzunisha kiongozi wako. Na hivyo kupelekea hamasa ya kuhudumu kupungua. Na madhara yake ni kuwa Mungu kukata utendaji kazi wake mahali hapo,
Wakati ule Haruni na Miriamu dada yake. walimnenea Musa maneno mabaya kwasababu na mke wake ambaye hakuwa myahudi. Mungu aliwaadhibu kwa kumpiga ukoma Miriamu kwasababu tu hiyo ya kutoonyesha adabu kwa mtumishi wake.
Hesabu 12:7-8
[7]Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote; [8]Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la BWANA yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?
[7]Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote;
[8]Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la BWANA yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?
Ni kosa kumnenea vibaya mchungaji wako. Epuka masengenyo na uasi na matabaka ndani ya kanisa. Uonapo kosa mwombee, au mfuate mweleze uwapo naye peke yake. Hilo litamjenga zaidi ya kutoa malaumu na manung’uniko. Adui hutumia sana njia hii kuleta mafarakano na magomvi, na mapigo kanisani.
Mheshimu mchungaji wako, zaidi ya raisi wa nchi kwasababu yeye ni balozi wa mbinguni na Mungu atakuinua (1Petro 5:1-6)
TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi
Ipi tofauti kati ya KUHANI na MCHUNGAJI.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1
Rudi Nyumbani
Matendo 11:25
Kisha akatoka akaenda Tarso kumtafuta Sauli;
Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, napenda leo tujifunza jambo moja ambalo huwenda linasahaulika miongoni mwetu kama watendakazi shambani mwa Bwana.
Hatuna budi kufahamu ,ufuatiliaji huenda sambamba na uinjilisti. Twaweza hubiria watu wakaokoka, wakamjua Kristo, wakati mwingine wakaweza hata kujisimamia wenyewe, lakini tusipojijengea tabia ya kuwafuatilia na kukaa nao, kuwaimarisha, basi kazi yetu yaweza kuwa bure, au isiwe na matunda mazuri kama ipasavyo.
tunajifunza kwa mtu mmoja aliyeitwa Barnaba, aliyejulikana pia kama mwana wa faraja. Huyu aliithamini huduma hii. Baada ya kusikia kuwa Paulo, amegeuka na kuwa mkristo, lakini akaenda mahali panaitwa Tarso, mbali kidogo na kanisa, Barnaba aliona si vema amwache huko. Ikabidi afunge safari yeye mwenyewe kutoka Antiokia aende kumtafuta.
Hatujui safari yake ilichukua siku ngapi, wiki ngapi, miezi mingapi. Lakini hatimaye akampata ..Alipomwona huwenda hakuridhishwa na mazingira ya kihuduma aliyokuwa nayo, hakuridhishwa na hali ya kiroho aliyokuwa nayo. Kwasababu hata mtume Paulo kuondoka Yerusalemu ilikuwa si kupenda kwake ni kutokana pia na kukataliwa na kanisa, na hatari ya kuuliwa na wayahudi.
Lakini Barnaba alipomuona. Akamchukua amlete mahali bora zaidi, ambapo kanisa lipo hai. Akafika akaendelea na huduma, akaanza kuwa moto tena na kutokea hapo ndipo Mungu alipomfanya mhubiri wa kimataifa.
Leo hii tunasoma ushujaa wa Paulo, lakini kusimama kwake kulichangiwa na nguvu ya kufuatiliwa kwa waliomtangulia kiroho.
Je na sisi tumejiwekea desturi hii? kuwafuatilia mara kwa mara tunaowashuhudia injili?
Kamwe usimdharau mwongofu mpya, hata kama atakuwa anasua-sua, au mdhaifu sasa. Fahamu kuwa huyo ndio Paulo wa baadaye. Usihubiri tu ukaacha, ukadhani atajikuza mwenyewe. Shughulika naye, omba naye, mfuate alipo, mfundishe, ikiwezekana mwamishe eneo alilopo ikiwa linamfanya asisimame kiroho. Na kazi yako itazaa matunda, usichoke.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.
MAMBO NANE (8), AMBAYO WEWE KAMA KIONGOZI UTAIGWA.
WhatsApp
Uwapo katika nafasi yoyote ya uongozi, katika kanisa au kwenye huduma, labda mchungaji, mwalimu, mtume, nabii, shemasi, askofu, mzee wa kanisa. Na una watu walio chini yako, fahamu mambo ambayo utaigwa, Na hivyo kuwa makini sana katika maeneo hayo uyajenge.
Mtume Paulo aliyaona kwa mwanawe Timotheo, akayaandika;
2 Timotheo 3:10-11
[10]BALI WEWE UMEYAFUATA mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu, [11]na upendo, na saburi; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili, naye Bwana aliniokoa katika hayo yote.
[10]BALI WEWE UMEYAFUATA mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu,
[11]na upendo, na saburi; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili, naye Bwana aliniokoa katika hayo yote.
Paulo ametaja mambo saba ambayo Timotheo aliyaona kwake akayaiga, ni kama yafuatayo;.
la kwanza ni
Wewe kama kiongozi kumbuka unachofundisha ndicho watakachofundisha wafuasi wako, ikiwa injili yako ni ya mafanikio, hicho hicho watakifuata na kukifundisha, ikiwa ni mafundisho ya wokovu watakifundisha hicho hicho, ikiwa ni shuhuda za wachawi nao pia watakuwa nazo hizo hizo kama kiini cha injili yao. Hivyo kuwa makini na fundisho lako vinginevyo utajikuta unapotosha jamii yako ya waaminio, na utatoa hesabu juu ya hilo, mbele za Bwana siku ile.
Ukiwa ni mtu wa kidunia, usitazamie utazaa watu wa rohoni, uvaaji wako, unawafundisha wafuasi wako, kauli zako zitazungumzwa hizo hizo na washirika wako, ukiwa na tabia ya maombi, wanaokufuata nao pia wataiga mwenendo huo wa maombi, ukiwa ni mtakatifu nao pia watakuwa hivyo hivyo. Jichunge mwenendo wako, wewe ni kioo unaigwa mpaka hatua zako. Hivyo usifanye mambo kiwepesi wepesi, ukidhani wote wamekomaa wanaweza kujiamulia tu mienendo bila kukuangalia wewe. Liondoe hilo kichwani.
Makusudi ya mtume Paulo, yalikuwa ni kuhubiri injili kwa mataifa kotekote wamjue Mungu (2Wakorintho 1:15-20). Hakuwa na kusudio la umaarufu, fedha, kuheshimiwa na wanadamu, hapana, bali kuhubiri injili tu peke yake, bila kujali dhiki, au kupungukiwa, ilimradi watu waokoke. Hivyo Timotheo naye alipoliona kusudi hilo akaiga, naye pia akawa mhubiri tu wa injili, asiyetafuta vya kwake ndani ya kazi ya Mungu. Halidhalika na wewe pia, nia yako hutakumbulikana mahali ulipo, Je! Unachokifanya ni injili ya Mungu kweli au una lengo lingine. Ikiwa ni Yesu wa mikate, basi ujue watu wako pia watakuwa hapo kumtafuta Mungu huyo huyo wa kwako. Kuwa na kusudi la Kristo ambalo aliliweka pia ndani ya mitume wake, yaani kulitumikia na kulichunga kundi, kama mtendakazi asiyekuwa na faida. Ukijua kuwa thawabu yako ipo mbinguni, usiwe na makusudio mengine, kwasababu wewe ni kioo.
Imani, katika mambo yote, wewe kama kiongozi ukiwa ni mtu wa mashaka juu ya mambo ya rohoni. Ikiwa huamini uponyaji wa ki-ungu, na wale pia watakuwa hivyo hivyo, huamini miujiza, na karama za Roho, vivyo hivyo na washirika wako watakuiga, ikiwa huamini katika mifungo, ikiwa huamini kuwa duniani kuna watakatifu, au mtu hawezi kuwa mtakatifu, vivyo hivyo watu wako nao watakuwa hivyo, Ikiwa unaamini katika ibada za sanamu, watakuwa kama wewe. Jenga imani yako kwenye neno la Mungu tu, kuwa mtu wa imani usiwe Sadukayo. Fahamu kuwa mtumishi wa Mungu tafsiri yake ni kuwa mtu wa Imani.
Kama kiongozi ni ukweli usiopingika utapitia vipindi mbalimbali vya kushinda na kushindwa, vipindi vya kukatishwa tamaa, kusemwa vibaya, vipindi vya kuachwa peke yako n.k. Mtume Paulo alipitia vipindi vyote, na wanafunzi wake wakawa wanamwangalia, wakaiga mwenendo ule walipoona mafanikio yake yalipotanguliwa na vipindi vingi vya kuvunjwa moyo lakini akastahimili. Hivyo na wewe pia kama kiongozi wa wengine, simama imara, uvumilivu wako ni funzo kubwa kwa wengine. Wakati mwingine Mungu anaruhusu uyapitie hayo ili kuwaimarisha wengine katika dhiki zao, wakuonapo wewe unasimama katika changamoto, na wao pia hupokea nguvu ya kushindana na changamoto zao.
Kama kiongozi, upendo ni sehemu, kubwa sana, ambalo mtume Paulo alifanya bidii kulionyesha kwa wanafunzi wake na kanisa. Unapolipenda kundi lako, vivyo hivyo na wale wataiga tabia hiyo na kuidhihirisha kwa wengine. Unapoonyesha chuki, nao pia watakuwa watu wa chuki, unapowajali nao pia watawajali wengine. Unapowasikiliza, tafsiri yake ni kuwa unawafundisha kuwasikiliza na wengine. Hivyo ni kuangalia sana na kuongeza bidii katika eneo hilo, uwe kielelezo.
Saburi ni kitendo cha kungojea ahadi za Mungu hata katika mambo magumu yanayokinzana na wewe, bado unasubiria tu. Kama kiongozi watu watatazamia jinsi unavyoyashikilia maono yako, bila kuyumbishwa, waige, na wenyewe kushikilia ya kwao. Kamwe usiwe mtu wa kusita-sita, utawavunja moyo wengi, na hatimaye watashindwa kusimama aidha pamoja na wewe, au wao wenyewe. Ijenge saburi yako, wala usiidharau, ni nguvu kwa mwingine aliye chini yako. Leo unaona jinsi gani saburi ya Ayubu ilivyo na fundisho kubwa kwetu. Vivyo hivyo na yako ujue ni darasa kwa wengine.
Ukweli ni kwamba watu watatamani kusikia ushuhuda wa mapito yako au kuyaona mapito yako hususani yale magumu sana. Lakini waweza kudhani, haliwafahi sana kiroho, lakini wengine pia wakaiiga njia hiyo ya mateso kama yako, kwasababu wameona mwisho wake ulivyo mzuri. Hivyo usiogope kupitia mateso kwa ajili ya Bwana wala usione haya wakati mwingine kueleza shida ulizopitia kwa wengine, hilo nalo huigwa, Leo hii tunaposoma mapito ya mtume Paulo ni wazi kuwa yanatutia nguvu na sisi, kuwa tusonge mbele.
Hivyo, zingatia mambo hayo saba, kwa faida yako na wale walio chini yako. Kwasababu ndicho Paulo alichokiona kwa watoto wake.
Shalom.
ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO
Fahamu maana ya Mithali 29:4 “Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.
IMANI “MAMA” NI IPI?
Bwana alimaanisha nini kusema “Mwanafunzi hawi mkuu kuliko mwalimu wake”?
Mafundisho maalumu kwa watumishi wa Mungu na Watenda kazi wote katika shamba la Bwana.
Maombolezo 2:19
[19]Inuka, ulalamike usiku, Mwanzo wa makesha yake; Mimina moyo wako kama maji usoni pa Bwana; Umwinulie mikono yako; KWA UHAI WA WATOTO WAKO WACHANGA WAZIMIAO KWA NJAA, Mwanzo wa kila njia kuu.
Ikiwa wewe ni mzazi au mlezi unaelewa ni uchungu mwingi kiasi gani unakupata pale unapoona mtoto wako anaangamia kwa kukosa mahitaji yake muhimu, mfano wa chakula. Ndicho kilichotokea kwa mama Hajiri siku alipofukuzwa kwa Ibrahimu, akiwa kule jangwani amepotea hali ilikuwa mbaya sana, kwani chakula na maji viliwaishia kabisa, huwenda zilipita siku kadhaa hawakuona dalili yoyote ya kupata msaada. Hivyo alichokifanya Hajiri, ni kwenda mbali kidogo na kumlilia sana Mungu wake, na Mungu akasikia, akaonyeshwa palipo na maji, akaenda kumpa mwanae, kuonyesha ni jinsi gani alivyouthamini uhai wa Ishmaeli.
Mwanzo 21:14 Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba. 15 Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja. 16 Akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, AKAPAZA SAUTI YAKE, AKALIA. 17 Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko. 18 Ondoka, ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa. 19 Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana.
Mwanzo 21:14 Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba.
15 Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja.
16 Akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, AKAPAZA SAUTI YAKE, AKALIA.
17 Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko.
18 Ondoka, ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa.
19 Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana.
Umeona kama Hajiri asingemtafuta Mungu katika hali ile, ni wazi kuwa Yule kijana ambaye alikuwa amekusudiwa awe taifa kubwa angefia jangwani na yale maono yasingetokea.
Ndicho tunachojifunza katika vifungu hivyo, kwenye kitabu cha Maombolezo, anasema kesha, ulie, kwa ajili ya watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa. Leo hii tuna watu wengi ambao wameokoka kwa kuisikia injili yetu. Lakini je, watu hao wanasimama au wanakufa?, Unapomhubiria mtu, hatutakiwi kusema yaliyobaki namwachia Mungu, bali ni kuhakikisha hafi kiroho kwa kukosa chakula cha uzima. Na hiyo inakuja kwa kuendelea kumfuatilia kumfundisha, Lakini zaidi sana KUMWOMBEA kwa Mungu usiku na mchana akue kiroho.
Tukiiga mfano wa Epafra jinsi alivyokuwa akiwaombea sana watu wa kolosai walioamini kwa injili yao.
Wakolosai 4:12 Epafra, aliye mtu wa kwenu, mtumwa wa Yesu Kristo, awasalimu, akifanya bidii siku zote kwa ajili yenu katika maombi yake, ili kwamba msimame wakamilifu na kuthibitika sana katika mapenzi yote ya Mungu.
Umeona? Ukomavu wa watu walio wachanga wa kiroho hutegemea sana maombi ya kina kwa waliowazaa. Hivyo wewe kama mtenda kazi hakikisha unakuwa na maombi mengi kwa ajili ya wale uliowahubiria injili wakaokoka vinginevyo watakufa kiroho, katika ulimwengu huu wa njaa na kiu ya Neno la Mungu, tenga masaa kuwaombea. Na maombi hayo yawe ya rohoni kabisa, sio ya juu juu, bali ya kuzama, ili Mungu awakuze, na matokeo ya kazi yako utayaona tu baada ya kipindi fulani, jinsi watakavyozidi kubadilika na kukomaa kidogo kidogo, hatimaye kuwa watumishi imara katika shamba la Mungu.
NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.
NJAA ILIYOPO SASA.
LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.
SWALI: Nini maana ya
Mithali 25:25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu, Ndivyo ilivyo habari njema itokayo katika nchi ya mbali.
JIBU: Biblia inalinganisha burudiko kubwa mtu analolipata pale anaposikia habari fulani njema na mfano wa mtu mwenye kiu halafu ghafla akaletewa kikombe cha maji ya baridi, sasa katika mazingira kama hayo ni wazi kuwa maji yale atayafurahia sana kwasababu yupo katika kiu.
lakini kiini cha mstari huo ni hapo anaposema ni habari njema ITOKAYO KATIKA NCHI YA MBALI.
Tukumbuke kuwa zipo habari njema nyingi..kwamfano habari za kupewa tenda fulani ya kibiashara ni habari njema, habari za kufaulu darasani ni habari njema, habari za kuzaliwa mtoto duniani ni habari njema, habari za kupandishwa cheo ni habari njema n.k…lakini zote hizi hazina jipya kwasababu ni za hapa hapa tu duniani.
Bali zipo habari njema zinazotoka katika nchi ya mbali na huko si kwingine zaidi ya MBINGUNI, hizo ndizo watu wana kiu nazo, wakizisikia tu ni lazima mioyo yao ni lazima iburudike sana.
Na habari zenyewe ni zile zinazomuhusu Yesu Kristo.
Alisema.
Yohana 6:33-35
[33]Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima. [34]Basi wakamwambia, Bwana, sikuzote utupe chakula hiki. [35]Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.
[33]Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.
[34]Basi wakamwambia, Bwana, sikuzote utupe chakula hiki.
[35]Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.
Yesu ndio maji yakatao kiu, alileta habari njema iliyotoka mbinguni, alikuja kutuletea ukombozi na msamaha wa dhambi, alikuja kutufungua katika vifungo vyetu, na shida zetu mbalimbali, na kutumwagia karama za rohoni, mambo ambayo mwingine yoyote hawezi kutoa. Lakini zaidi sana alikuja kutuambia habari za ufalme wake, kwa habari ya mambo yanayokuja, kuhusu mbingu mpya na nchi mpya, na Yerusalemu mpya, na umilele, na uzuri na thawabu alizotuandalia sisi tuliomwamini. Mambo ambayo ukisikia kama wewe unapenda kweli maisha…utayafurahia sana.
hivyo yatupasa mimi na wewe tuwe na mwitikio huu, wa habari hizi njema kwa kuwashuhudia pia na wengine maji haya, kwasababu ni wazi kuwa wengi wana kiu, na hivyo wanahaja ya kuzisikia hizi habari njema zimuhusuyo Yesu Kristo.
Sote kwa pamoja tuamke tukahubiri injili. Tukijua kuwa inahitajiwa sana.
shalom
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
INJILI NI NINI?
Maana ya Mithali 17:22 Moyo uliochangamka ni dawa nzuri;
KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.
(Masomo maamulu kwa watumishi wa Mungu).
Je wewe ni mtumishi wa MUNGU?..Basi fuatilia mfululizo wa masomo haya katika tovuti yetu hii (www.wingulamashahidi.org).
Kama mtumishi wa Mungu kuna Anwani au nembo au Lebo ambayo inapaswa iambatane na kila fundisho unalolitoa kwa wahusika. Na Anwani/lebo hiyo/nembo hiyo si nyingine Zaidi ya “TOBA”. Hakikisha mahubiri yako yanalenga Toba, au kuwakumbusha watu umuhimu wa kujitakasa.
Kwanini iko hivyo?
Hebu tujifunze kwa mmoja ambaye ni mjumbe wa Agano, tena ndiye Mwalimu wetu MKUU na Mwinjilisti MKUU YESU KRISTO.
Yeye katika mahubiri yake yote alihubiri “Toba”.. Huenda unaweza kusoma mahali akiwa anafundisha na usione likitajwa neno Toba, lakini fahamu kuwa alikuwa anahubiri Toba kila siku katika mafundisho yake yote… Kwani biblia inasema kama yote aliyoyafanya BWANA YESU kama yangeandikwa basi dunia isingetosha kwa wingi wa vitabu.
Yohana 21:25 “Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa”
Kwahiyo Mahubiri ya BWANA WETU YESU yote Yalikuwa yamejaa toba.. sasa tunazidi kulithibitishaje hilo?.. hebu tusome maandiko yafuatayo..
Mathayo 4:17 “Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia”
Nataka tuutafakari kwa undani huu mstari… anasema “Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia”…. Zingatia hilo neno “TOKEA WAKATI HUO….TOKEA WAKATI HUO…TOKEA WAKATI HUO”.. Maana yake “kilikuwa ni kitu endelevu”, sio kitu cha kusema mara moja na kuacha, (hiyo ndiyo ilikuwa lebo ya mafundisho yake daima).. Kila alipohubiri lazima aliwahubiria pia watu watubu.
Umeona?. Je na wewe Mchungaji, na wewe Mwalimu wa injili, na Wewe nabii, na wewe Mtume, na wewe Mwimbaji wa injili.. LEBO YA MAHUBIRI YAKO NI IPI????.
Je! injili yako unayohubiri ni ya TOBA, au ya kuwafariji watu katika dhambi zao??.. Je unazunguka huku na kule kuhubiri injili ya namna gani?..Je ni injili ya Toba au ya Mali tu!.
Luka 24:45 “Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko. 46 Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; 47 na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu. 48 Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya”
Luka 24:45 “Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.
46 Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;
47 na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu.
48 Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya”
Hakuna furaha, hakuna mafanikio, hakuna Amani ikiwa mtu yupo katika maisha ya dhambi.. utamhubiria afanikiwe lakini hata akiyapata hayo mafanikio basi dhambi itamuua tu na kumkosesha raha.. Raha pekee na Amani mtu ataipata baada ya kutubu, ndivyo maandiko yasemavyo..
Matendo 3:19 “Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana”
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Toba ni nini?
VYA MUNGU MPENI MUNGU.
NAYAJUA MATENDO YAKO.
Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?
WEKA KUMBUKUMBU YA MAMBO BWANA ANAYOKUFANYIA KWASABABU YATAKUFAA MBELENI.
Rudi nyumbani
SWALI: Na je! Walawi na makuhani katika kanisa la sasa ni watu wa namna gani?
JIBU: Mungu alilichagua kabila moja kati ya kumi na mbili liwe kabila lake takatifu litakalosimama katika kazi na shughuli zote za kidini na ibada Israeli.
Sasa katikati ya hawa walawi ndipo walipotolewa makuhani ndani yake. Hivyo makuhani wote walikuwa ni walawi lakini walawi wote si makuhani.
Kwasasa, kila mkristo, ni Mlawi. Kwasababu tayari ameshapewa uwezo ndani yake na karama, ya kuifanya kazi ya Mungu pale tu anapookoka. Kila mmoja ni kiungo kwa mwenzake ndani ya kanisa. Lakini mkristo anabadilika kutoka kuwa mlawi mpaka kuwa kuhani pale anaposimama hasaa kwa ajili ya huduma/kazi ya Mungu kwa watu wake.
Anapobeba maono Fulani, labda tuseme kulichunga kanisa, huyo ni kuhani wa Mungu, na hivyo anaposimama na kuwabariki watu basi Baraka hizo huwafikia watu moja kwa moja kutoka kwa Mungu, mfano tu wa makuhani wa agano la kale. Au anapotumika katika kuwafundisha, kuwaombea wengine, kuwasimamia wengine, haijalishi ngazi aliyopo, au mahali au jinsia, huyo rohoni ni kuhani wa Mungu.
Hivyo kila mkristo anaouwezo wa kuwa kuhani wa Mungu, kwasababu lengo la Mungu ni sote tuwe makuhani wake, sio tu walawi, Na Yesu Kristo Bwana wetu akiwa ni kuhani Mkuu.
1Petro 2:9 Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;
Je! Kristo yupo moyoni mwako?
Kama ni hapana, basi wakati ndio huu, mgeukie, akusamehe dhambi zako, kwa kutubu na kumaanisha kabisa kuziacha, naye atakukomboa. Ikiwa upo tayari kwa ajili ya mwongozo huo, basi waweza fungua hapa kwa mwongozo >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini auPiga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Kwa namna gani tumefanyika Makuhani na Ufalme?.(Ufunuo 1:6)
WALAWI WALIKUWA WENYE MIOYO YA ADILI KWA KUJITAKASA KULIKO MAKUHANI.
Kwanini Yesu aliwaambia wale wakoma wakajionyeshe kwa makuhani?
Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).
2Nyakati 29:34 Lakini makuhani walikuwa wachache, wasiweze kuchuna sadaka zote za kuteketezwa; basi ndugu zao Walawi wakawasaidia, hata ilipokwisha kazi, na hata makuhani walipojitakasa; kwa kuwa Walawi walikuwa wenye mioyo ya adili kwa kujitakasa kuliko makuhani.
Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu.
Fundisho hili linawahusu sana sana viongozi wa kiroho / Watumishi wa Mungu wanaohudumia kundi la Mungu. Mfano wachungaji au maaskofu.
Kuna wakati wale walioteuliwa kuwa viongozi wa juu kabisa wanaweza wasiwajibike ipasavyo katika nafasi zao, je! Wewe kama mwangalizi wao ufanye nini?
Mfano tukirejea habari hiyo tunaona Mfalme Hezekia alipokusudia kulitakasa hekalu la Mungu, ambalo lilikuwa limefungwa na kusahauliwa, na baba yake.
Alitafuta makuhani wa kuhudumu upya katika nyumba ya Mungu. Ikumbukwe kuwa makuhani tu ndio walioruhusiwa kufanya shughuli zote za madhahabuni, ikiwemo kuvukiza uvumba na kuandaa zile sadaka zilizoletwa mbele ya nyumba ya Bwana.
Lakini hapo biblia inatuambia, Makuhani walikuwa wachache!. Utajiuliza ni kwanini? Sio kwamba hawakuwepo kabisa, walikuwepo, lakini biblia inatuambia waliokuwa na mioyo ya adili ya kuipenda kazi ya Mungu ndio walikuwa wachache.
Pengine, wengine walikuwa na udhuru zao, wakiona kuahirisha shughuli zao, na kwenda kuhudumu madhabahuni ni kuvurugiwa ratiba ni kazi ya kuchosha, haina faida, wengine hawakuwa tayari kujitakasa, kwa kuacha mambo mabovu yasiyowapasa makuhani, wengine wakawa wazito, wanavutwa vutwa sana, kazi ambayo inapaswa ifanyike haraka n.k..
Hivyo hiyo ikapelekea kundi la viongozi wa juu kabisa likawa chache sana. Na kimsingi ni lazima wawepo wahudumu wa kutosha katika kazi hiyo ya madhabahuni. Sasa wafanyaje. Ndipo hapo utaona Walawi ambao kazi zao ni za nje, ya hema kama vile usimamizi wa malango, kulinda hekalu, na kuimba. Ikabidi sasa waingizwe ndani kwa ajili ya kusaidia kazi za kikuhani.
Na sababu ya kufanya hivyo biblia inasema, wenyewe walikuwa ni “wenye mioyo ya adili kwa kujitakasa kuliko makuhani”.
Walikuwa na moyo wa kumtumikia Mungu zaidi hata ya wale wanaostahili. Hivyo wakapewa kazi za juu zisizowastahili na wakafanya vizuri na Mungu akawabariki, ijapokuwa ilikuwa ni kinyume na taratibu.
Hata sasa katika kanisa, ni rahisi kuona wenye ngazi za chini, ni wepesi na wenye mioyo ya uaminifu katika nyumba ya Bwana kuliko wale viongozi wa juu. Utaona ni kiongozi wa wakina mama, lakini kwenye maombi haudhurii, kuwafuatilia wanawake wenzake haangahiki. Lakini hapo hapo utaona kabinti kadogo, kanajibidiisha, haachi maombi yapite, anawapigia simu yeye kuwakumbusha kana kwamba ndio kiongozi mkuu, anatoa taarifa za maboresho na changamoto kwa kiongozi wake, mambo ambayo hata huyo kiongozi hajui.
Sasa katika mazingira kama haya? Unadhani kiongozi ni nani? …Uongozi sio cheo, uongozi ni MOYO, uaminifu na kujitoa. Ikiwa wewe ni mwangalizi, hakikisha huyu aliye na MOYO ndio unampa wajibu na majukumu yote ya uongozi katika nafasi hiyo. Hata kama hajawekewa mikono, au hana uzoefu wowote, au hajatambulika rasmi.
Huyo huyo ndiye Mungu aliyemchagua, hao wengine ni makapi.
Kwani Bwana Yesu alishatangulia kusema maneno haya.
Mathayo 19:30 “Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza”.
Sio kwamba Mungu anao upendeleo.. Lakini alisema.. “ walioalikwa hawakustahili”(Mathayo 22:8).
Halidhalika hata katika ngazi nyingine zote, ikiwa mchungaji msaidizi haipendi kazi yake, usione vibaya, kumpa kazi hiyo shemasi mwenye MOYO wa kuwahudumia watu. Mungu atamtengeneza mwenyewe. Lakini ikiwa wewe ni kiongozi-mlegevu, tubu geuka, ipende nafasi yako, hudumu hapo kwa uaminifu kwasababu umepewa dhamana ambayo utakuja kuitolea hesabu yake siku ile ya hukumu.
Bwana awe nawe.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Uadilifu ni nini kibiblia?
Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji zilikuwaje?