Title January 2025

Sosthene ni nani katika biblia? (Matendo 18:17)

Sosthene ni mmoja wa wahudumu wa injili Katika agano jipya. Mshirika mmojawapo wa mtume Paulo, katika kazi ya kuitetea injili.

Katika kitabu cha matendo anatajwa kama mkuu wa sinagogi, kule Korintho

Matendo ya Mitume 18:17

[17]Nao wote wakamshika Sosthene, mkuu wa sinagogi, wakampiga mbele ya

kiti cha hukumu. Wala Galio hakuyaona mambo hayo kuwa ni kitu. 

> Alikuwa ni mmoja wa wayahudi(washika-sheria), waliokutana na injili ya Paulo na kuamini. 

Paulo alipofika Korintho Mungu alimtokea katika maono na kumwambia asiogope aendelee kuhubiri kwasababu katika Mji huo anao “watu wake wengi”

Hivyo aliendelea kuhubiri kwa ujasiri mwingi kwa muda wa mwaka mmoja na nusu na watu wengi sana miongoni mwa wayahudi waliamini ikiwemo huyu Sosthene na Krispo.

Matendo 18:9-11

[9]Bwana akamwambia Paulo kwa maono usiku, Usiogope, bali nena, wala usinyamaze, 

[10]kwa kuwa mimi ni pamoja nawe, wala hapana mtu atakayekushambulia ili kukudhuru; kwa maana mimi nina watu wengi katika mji huu. 

[11]Akakaa huko muda wa mwaka mmoja na miezi sita akifundisha kati yao neno la Mungu

Baadaye wayahudi wenye wivu waliamka kinyume cha Paulo, na kumpeleka mbele ya Galio liwali ili ashitakiwe kwa kuleta machafuko ndani ya dini yao.

Lakini Galio akawatawanya kwasababu kesi yao haikuwa ya uhalifu au dhuluma bali ya mambo ya kiimani..Ambayo kwa mujibu wa sheria za kirumi hazisikilizwa kwenye mahakama zao.

Hivyo wayahudi kuona Paulo hajahukumiwa, wakamkata huyu Sosthene mkuu wa Sinagogi na kumpiga mbele ya kiti cha hukumu. Na hiyo yote ni kutokana na kwamba aliisapoti huduma ya Paulo, pengine aidha kwa kumruhusu ahubiri injili ndani ya masinagogi yao au kwa kutochukua hatua zozote stahiki dhiki ya injili ya mtume Paulo.

Lakini pia tunakuja kuona baadaye Paulo wakati anaandika waraka kwa Wakoritho anamtaja Sosthene kama mshirika mwenza wa utume wa Kristo.

1 Wakorintho 1:1

[1]Paulo, aliyeitwa kuwa mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu, 

Hiyo ni kuonyesha kuwa alikuja kuwa nguzo hasaa kwa watakatifu wa Korintho. Mpaka Paulo anamtaja kama mshirika mwenza.

Ni Nini cha kujifunza katika habari ya Sosthene?

Ni kuonyesha uweza wa Mungu wa kugeuza watu wa aina zote. Kikawaida kwa taratibu za kiyahudi mpaka mtu ameaminiwa kuwa mkuu wa sinagogi, maana yake ni kuwa mtu huyo amethibitishwa kuijua na kuishiya torati kwelikweli na nidhani zote za kiyahudi na taratibu zao.

Kwahiyo kwa mtu kama Sosthene kubadilika ghafla na kuwa mfuasi wa injili, haikuwa rahisi, ilihitaji neema ya Mungu kubwa, ndio maana kwa wayahudi alionekana kwa mwasi wakampiga sana.

Bwana anataka tusibague wa kuwahubiri injili, kwasababu injili ni uweza wa Mungu(Warumi 1:16), Umwonapo imamu mhubirie, Shehe mhubirie, Buddha mhubirie, baniani mhubirie, padri, askofu, mganga wa kienyeji..wahubirie kwasababu hapo ulipo kuna “watu wa Mungu wengi sana” hujua ni yupi Bwana aliyemkusudia kuwa chombo chake kama Sosthene.We hubiri tu.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MKUU WA GIZA.

Tikiko ni nani kwenye biblia?

Mhunzi ni nani? (Isaya 54:16)

 

 

Print this post

Tikiko ni nani kwenye biblia?

Tikiko ni mmoja wa washirika waliohudumu na mtume Paulo katika kazi injili. Ijapokuwa si mtu anayejulikana sana..lakini ametajwa sehemu kadha wa kadha katika vitabu vya agano jipya.

> Anatajwa kama mmoja wa watu waliomua kufuatana na Paulo katika ziara za injili maeneo mbalimbali (Makedonia na Asia).

Matendo ya Mitume 20:3-4

[3]Alipokwisha kukaa huko miezi mitatu, na Wayahudi kumfanyia vitimvi, alipotaka kwenda Shamu kwa njia ya bahari; basi akaazimu kurejea kwa njia ya Makedonia.

[4]Watu hawa wakafuatana naye, Sopatro Mberoya, mwana wa Piro, na Aristarko na Sekundo, watu wa Thesalonike; na Gayo mtu wa Derbe, na Timotheo; na Tikiko na Trofimo watu wa Asia.

> Paulo anamtaja pia kama Mhudumu mwaminifu katika Bwana. Maana yake aliupima uaminifu wake, akauthbitisha kuwa hauna unafiki, mpaka akamfanya kama mbeba taarifa zake za kihuduma kwa makanisa.

Waefeso 6:21

[21]

Basi ninyi nanyi mpate kuzijua habari zangu, ni hali gani, Tikiko, ndugu mpendwa, mhudumu mwaminifu katika Bwana, atawajulisheni mambo yote;

Wakolosai 4:7-8

[7]Tikiko, ndugu mpendwa, mtumishi mwaminifu, mjoli wangu katika Bwana, atawaarifu mambo yangu yote;

[8]ambaye nimemtuma kwenu kwa sababu iyo hiyo, ili mjue mambo yetu, naye akawafariji mioyo yenu;

> Lakini pia kwa jinsi Paulo alivyomtaja tunaweza kusema alisimama kama mwangalizi-mwenza wa viongozi wa makanisa.

2 Timotheo 4:12

[12]Lakini Tikiko nalimpeleka Efeso.

Tito 3:12

[12]Wakati nitakapomtuma Artema kwako au Tikiko, jitahidi kuja kwangu huku Nikopoli; kwa maana huku nimekusudia kukaa wakati wa baridi.

Hivyo ijapokuwa si mtu aliyemaarifu, lakini alifanyika nguzo si tu katika mafanikio ya huduma ya mtume Paulo lakini pia kwa makanisa ya Mungu.

Je! Makanisa yetu yaweza kuwa akina Tikiko, watu waaminifu kwa viongozi wao, na kwa kanisa la Kristo?

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je mwanamke Fibi, alikuwa ni askofu wa makanisa, kama mitume?

Silwano  ni nani,kama tunavyomsoma kwenye biblia?(1Petro 5:12)

Epafra ni nani katika biblia? (Wakolosai 1:7)


Rudi Nyumbani

Print this post

Bwana aliposema Maua hayasokoti alimaanisha nini? (Mathayo 6:28).

Jibu: Turejee…

Mathayo 6:28 “Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala HAYASOKOTI

29 nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo”

Maana ya kusokota kama inavyozungumziwa hapo ni “kitendo cha kusokota nyuzi na kuunda vazi”.

Zipo nguo/mavazi yaliyotengenezwa kwa kufuma na mengine kwa kusokota nyuzi aidha kwa mkono au mashine.

Kutoka 39:28 “na hicho kilemba cha nguo ya kitani nzuri, na zile kofia nzuri za kitani, na hizo suruali za nguo ya kitani nzuri iliyosokotwa”

Walawi 13:52 “Naye atalichoma moto vazi hilo, kwamba ni lililofumwa au kwamba ni lililosokotwa, kama ni la sufu, au la kitani, au kitu cho chote cha ngozi, ambacho kina hilo pigo ndani yake; kwa maana, ni ukoma unaokula; vazi hilo litachomwa moto”.

Soma pia Walawi 13:58..

Sasa sisi wanadamu ili tuweze kuvaa vazi zuri lililofumwa au kusokotwa ni lazima tufanye kazi za  kujiingizia kipato ili tukanunue mavazi hayo ya kusokota au sisi wenye tusokote kwa mikono yetu au mashine na kujivika…lakini kwa kawaida haiwezekani tule chakula halafu mavazi mazuri ya kusokotwa yatokee mwilini kama vile kucha inavyotokea mwilini…hilo jambo haliwezekani.

Lakini kwa upande wa MAUA ya kondeni hilo linawezekana.. yenyewe hayafanyi kazi yoyote ya kusokota lakini yanavikwa kwa rangi nzuri na za kupendeza ambazo hata Sulemani hakuwahi kuvikwa kama mojawapo ya hayo.

Kadhalika na hali yake mtu amwaminiye Bwana YESU, atakuwa hana haja ya kuhangaika sana kupata mavazi au chakula, kwasababu Bwana anajua anahitaji hayo yote.

Hata ikotokea anapitia vipindi vya kupungukiwa basi huenda ni darasa tu la muda anapitishwa lakini haitaliwa hivyo siku zote.

Mathayo 6:30 “Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?

31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa”

Kwa urefu kuhusiana na kuvikwa kwa maua ya kondeni na mfalme Sulemani fungua hapa》》》》Hii ni maana ya Mathayo 6:29 hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini pawekwe MITI pale bustanini na si kitu kingine?.

Kwanini MUNGU alimzuia Daudi asimjengee HEKALU? (1Nyakati 17:12)

Silwano  ni nani,kama tunavyomsoma kwenye biblia?(1Petro 5:12)

Mwerezi ni nini?

 UNAUELEWA, HISOPO UMEAO UKUTANI?

Rudi Nyumbani

Print this post

Tatizo la kula udongo linasababishwa na nini?

Si jambo la kawaida mwanadamu kula Udongo!.. Hivyo inapotokea mtu anakula udongo kupitiliza, basi hilo laweza kuwa tatizo la kiroho zaidi ya kuwa tatizo la kisayansi..

Ndio zipo tafiti chache zinazoonesha kuwa mwanamke anapokuwa mja mzito anaweza kuwa na hamu ya kula udongo, na pia mtu aliyepungukiwa na madini Fulani mwilini anaweza kula udongo..

Tafiti hizi zaweza kuwa kweli kwa sehemu, lakini inapotokea Mtu chakula chake kinageuka kuwa udongo, na wengine hata baada ya kumaliza kubeba ujauzito bado wanaendelea kula udongo, na hata kwenda kununua basi hilo ni tatizo la kiroho Zaidi.

Kwasababu maandiko yanasema anayekula mavumbi/udongo ni nyoka tu peke yake.

Mwanzo 3:14 “Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, NA MAVUMBI UTAKULA SIKU ZOTE ZA MAISHA YAKO”

Hivyo kama unaona unalo tatizo la kula udongo kwa kiwango cha kushindwa kujizuia, basi ipo roho inayokutumikisha katika hilo, kama tu vile roho ya kujichua, hivyo suluhisho kwanza ni kumkaribisha BWANA YESU katika maisha yako, kwa kutubu na kumaanisha kuacha dhambi, kisha kutafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la BWANA YESU, na baada ya hapo hiyo roho itaondoka yenyewe na utarudi kuwa mtu wa kawaida.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TATIZO LA VISIGINO KUUMA KIBIBLIA

JE TATIZO LA KULA KUCHA NI ISHARA YA KUWA NA MAPEPO?

TATIZO LA NDANI LINALOWASUMBUA VIJANA, WALIOOKOKA.

Kunyoa denge ni kufanyaje na je ni dhambi? (Walawi 19:27).

Rudi Nyumbani

Print this post

Makumbi ni nini? (Isaya 1:31)

Jibu: Turejee.

Isaya 1:31 “Na mtu hodari atakuwa kama MAKUMBI, na kazi yake kama cheche ya moto; nao watawaka pamoja, wala hapana atakayewazima”.

“Makumbi” ni malighafi yoyote inayotumika katika kuanza au kuchochea moto, mfano; mbao, vijiti au nyasi kavu.

Katika kitabu hiko cha Isaya, biblia imemtaja mtu hodari kwamba siku hizo atakuwa si kitu bali kama tu vijiti vishikavyo moto na kuteketea.

Isaya 1:28 “Lakini kuharibika kwao wakosao nao wenye dhambi kutatokea wakati mmoja, nao wamwachao Bwana watateketezwa.

29 Kwa maana watatahayarika kwa sababu ya mialoni mliyoitamani, nanyi mtaaibishwa kwa sababu ya bustani mlizozichagua.

30 Maana mtakuwa kama mwaloni ambao majani yake yakauka, na kama bustani isiyo na maji.

31 Na mtu hodari ATAKUWA KAMA MAKUMBI, na kazi yake kama cheche ya moto; nao watawaka pamoja, wala hapana atakayewazima”.

Bwana hata sasa atusaidie tusimwache, bali tuzishike amri zake na maagizo yake ili tusiteketee kwa moto wake.

Yeremia 5:11 “Maana nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda wamenitenda kwa hiana sana, asema Bwana.

12 Wamemkataa Bwana, na kusema, Si yeye; wala hayatatupata mabaya; wala hatutaona upanga wala njaa;

13 na manabii watakuwa upepo, wala neno lake halimo ndani yao; basi ndivyo watakavyotendwa.

14 Kwa sababu hiyo Bwana, Mungu wa majeshi, asema hivi, Kwa sababu mnasema neno hili, tazama, nitafanya maneno yangu katika KINYWA CHAKO KUWA MOTO, NA WATU HAWA KUWA KUNI, NAO MOTO UTAWALA”

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TUZIDI KUWA HODARI KATIKA BWANA.

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

Nimrodi ni nani?

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Rudi Nyumbani

Print this post

Amali ni nini?(Mhubiri 4:4).

Amali ni nini (Mhubiri 4:4)

Jibu: Turejee…

Mhubiri 4:4 “Tena nikafikiri amali zote, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.

Amali ni “kazi ya tabu/kuchosha”.. Mtu anayefanya kazi yenye kuchosha mwili na akili, kazi yake hiyo inaitwa “Amali”.

Hivyo mstari huo wa Mhubiri 4:4 unaweza kueleka hivi….

Mhubiri 4:4 “Tena nikafikiri KAZI ZOTE ZA TABU, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.

Maana yake kazi nyingi za kuchosha zinatokana zinahusisha mambo maovu ikiwemo Tamaa, Uchungu, Wivu, uchoyo, hasira na visasi.

(Ingawa pia si zote, yaani si wote wenye kufanya kazi za taabu/kuchosha wapo juu ya misingi hiyo, wapo wengine nia zao ni njema kabisa wana amani na Bwana anawatunza na kuwaonekania.. lakini wengi wao msingi wao ni uovu).

Mhubiri 4:8 “Kuna mtu aliye peke yake, wala hana wa pili wake; naam, hana mwana wala ndugu; hata hivyo amali yake haina mwisho, wala macho yake hayashibi utajiri. Basi asema, Ni kwa ajili ya nani nafanya kazi, na kujinyima nafsi yangu mema? Hayo nayo ni ubatili, naam, ni taabu kubwa”.

Lakini kama mtu atakuwa na Amali na akamcha Bwana ana heri, kwani tabu yake si bure kama maandiko yasemavyo, ila kwa mwenye kumweka Bwana pembeni, amali yake itakuwa bure.

Mistari mingine yenye kutaja Amali ni pamoja na Mhubiri 5:19, na Mhubiri 8:15.

Ikiwa kazi yako ya mikono, inakulemea akili na nguvu na huoni faida yake basi kimbilia kwa Bwana YESU naye atakutia mizigo sawasawa na ile Mathayo 11:28.

Zaburi 127:2 “Kazi yenu ni bure, mnaoamka mapema, Na kukawia kwenda kulala, Na kula chakula cha taabu; Yeye humpa mpenzi wake usingizi”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Paulo aliwapaje watu karama ya rohoni?

Swali: Hii karama ya rohoni Mtume Paulo aliyowaahidi Warumi kuwa atawapa ni ipi?..na aliwapaje?.


Jibu: Turejee.

Warumi 1:11 “Kwa maana ninatamani sana kuwaona, nipate kuwapa KARAMA YA ROHONI, ili mfanywe imara”

Awali ya yote ni vizuri kuzingatia kuwa hasemi “karama za rohoni” kana kwamba ni nyingi…bali anasema “karama ya rohoni”  ikiwa na maana ni “moja tu”.

Na hiyo si nyingine zaidi ya ile iliyokuwa ndani ya Paulo (Karama aliyokuwa nayo Paulo).

Sasa anaposema “apate kuwapa karama ya rohoni”…hamaanishi kumpa tu mwingine karama kama aliyokuwa nayo yeye, au awawekee mikono wapokee karama za rohoni kama unabii, au lugha, au imani La! Hakumaanisha hivyo, kwasababu vipawa na karama ni Mungu pekee ndiye atoaye na si mwanadamu.

Lakini maana ya “kuwapa karama ya rohoni”…ni kuwanufaisha wale watu kwa karama iliyokuwemo ndani yake Paulo.

Mtu mwenye karama ya unabii na anapompa mwingine unabii kwa uongozo wa Roho Mtakatifu maana yake “amempa mtu huyo karama ya rohoni”..mtu mwenye karama ya uponyaji anaombea wengine na wakapokea uponyaji, maana yake amewapa wale watu karama ya rohoni na ndicho Mtume Paulo alichokimaanisha pale.

Ili tuelewe vizuri tusome tena maandiko yafuatayo..

Warumi 12:6 “Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, TUTOE unabii kwa kadiri ya imani;

7 ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake”.

Umeona hapo?…anasema ikiwa unabii, ualimu, au karama nyingine yoyote basi TUTOE kwa wengine?.

Kwahiyo Mtume Paulo alikuwa amelenga kuwanufaisha watu kwa ile karama Mungu aliyoiweka ndani yake, na si kuwagawia karama za roho mtakatifu zile zinazotajwa katika 1Wakorintho 12.

Na zaidi sana Paulo alikuwa anashauku sana kufanya hivyo kwa makundi yote ya watu (Wayunani na Wayahudi).

Warumi 1:13 “Lakini, ndugu zangu, sipendi msiwe na habari, ya kuwa mara nyingi nalikusudia kuja kwenu, nikazuiliwa hata sasa, ili nipate kuwa na matunda kwenu ninyi pia kama nilivyo nayo katika Mataifa wengine.

14 Nawiwa na Wayunani na wasio Wayunani, nawiwa na wenye hekima na wasio na hekima”.

Je na wewe unaitoa karama yako kwa wengine??..fahamu kuwa kila mtu aliyempokea KRISTO anayo karama ya rohoni, na ni lazima utumike kuwajenga wengine na kuwavuta kwa KRISTO zaidi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Je yule mkoma aliyeponywa alifika kwanza kwa makuhani kisha ndio akarudi kumpa Yesu shukrani au alirudi kabla hajafika kwa makuhani?

JIBU: Baada ya Yesu kukutana na wale wenye ukoma kumi, na kuwaagiza waende kujionyesha kwa makuhani

biblia inatuonyesha walipokea uponyaji wote wakiwa bado wapo njiani, lakini tunaona yule mkoma mmoja hakuendelea na safari yake. Palepale ilimbidi ahairishe kwanza safari yake Na kuja kumshukuru Yesu, na ndipo pengine aendelee na safari yake ya kuelekea kwa makuhani.

Luka 17:14-19

[14]Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.

[15]Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;

[16]akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.

[17]Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?

[18]Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?

[19]Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa.

Kwanini afanye vile ni kwasababu aliona umuhimu wa kumshukuru Yesu Kristo kwanza zaidi ya wahudumu wake.

Jambo lolote Mungu analotaka kututendea kupitia wahudumu wake..Tujue kuwa Shukrani zetu za kwanza zinapaswa zimrudie yeye.

Amina.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini BWANA awaagize wakoma wakajionyeshe kwa Makuhani?(Luka 17:14

Kwa namna gani tumefanyika Makuhani na Ufalme?.(Ufunuo 1:6)

UKOMA NA UJANE ULIO NDANI YAKO, UMEUPATIA TIBA?

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza 

Kitabu hichi ni moja ya nyaraka   zilizondikwa na  mtume Paulo katika agano jipya, 

Waraka huu amegusia mambo mengi, hasahasa katika eneo la marekebisho na maonyo. Unagusia nidhani na taratibu za kikristo zinazopaswa zifuatwe ndani ya  kanisa, unazungumzia pia eneo la uhalisia wa ufufuo wa wafu katika siku ya mwisho pamoja eneo la upendo.

Na huu ndio uchambuzi wake katika maeneo mama; 

1) Matabaka ndani ya kanisa. (1:10-17, 3:1-4:21)

Paulo anatoa onyo juu ya migawanyo ambayo ilianza kutokea ndani ya kanisa iliyozaa  wivu na fitina, ambayo ilisababishwa kwa baadhi ya watu kujiwekea matabaka kwa kujivunia viongozi kwa kusema mimi ni wa Paulo, mimi ni wa Apolo, mimi ni wa Kefa. Akiwatahadharisha na kuwasihi  kwa kuwaeleza kwamba wao ni wahudumu tu katika nafasi mbalimbali, bali mkuzaji ni Kristo. Na hivyo hawapaswi kujivunia wao, bali Kristo

2) Usahihi juu ya hekima ya Mungu

Kristo ni hekima ya Mungu na nguvu ya Mungu.(1:18- 2:16)

Eneo la pili Paulo anatoa ufahamu hasaa juu ya hekima anayoitambua Mungu, akionyesha kuwa hekima ya ulimwengu huu, kwa Mungu ni upuzi, bali hekima ya Mungu ameificha ndani ya Kristo Yesu, na hivyo amewachagua watu wadhaifu na wanyonge kuwadhihirishia hiyo. Akionyesha kuwa mtu asitegemee sana kumwona Mungu katika mambo yanayodhaniwa kuwa ni makuu, bali katika Kristo Yesu.

1 Wakorintho 1:24

[24]bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu. 

3) Nidhamu ya kimwili ndani ya kanisa la Kristo, (1Wakorintho 5-6)

 Katika eneo hili Paulo anastaajabishwa kwa kuzuka kwa zinaa mbaya ambayo haionekani hata  kwa mataifa yaani mtu na mzazi wake kuzini,. Akiwaagiza kutoa hukumu juu ya watu kama hao, hata kwa kuwakabidhi shetani (lengo ni waponyeke)

Kwasababu wakiachwa mwisho wao huwa ni kulichafua kanisa, (kulitia unajisi), 

Vilevile tunaona Paulo akitoa agizo kuwa kanisa halipaswi kuchangamana na wazinzi.

Akisisitiza kuwa mtakatifu sio tu awe amehesabiwa haki bali pia awe ameoshwa  na kutakaswa na udhalimu wote.

Anawaagiza pia watakatifu hawapaswi kupeleka mashtaka yao kwa watu wa kimataifa, bali kanisa ni zaidi ya mahakama ambayo watakatifu wanapaswa watatulie migogoro yao hapo. 

4) Ndoa na useja. (1Wakorintho 7)

Paulo anaeleza kwa upana, taratibu ya kindoa, katika eneo la haki zao za ndani na kuachana, na wito wa utowashi(useja). Katika eneo la haki, anasisitiza kuwa kila mwanandoa anapaswa atambue kuwa hana haki juu ya mwili wake mwenyewe, bali mwenzake, lakini pia katika kuachana, anaeleza ikiwa mwanandoa mmoja haamini, Yule aliyeamini hapaswi kumwachwa mwenzake, ikiwa bado anataka  kuendelea kuishi naye. Lakini pia anatoa pendekezo lake Mtu akitaka kumtumikia Mungu kwa wepesi zaidi bila kuvutwa na mambo ya mwilini na dhiki za kiulimwengu. Basi akikaa bila kuoa/kuolewa afanya vema zaidi.

5) Uhuru wa mkristo.(1Wakorintho 8-10)

Anaeleza jinsi gani mkristo anapaswa kukabiliana na dhamiri yake na ile ya wengine,katika maamuzi ayafanyayo kwa ujuzi wake,  akigusia eneo la vyakula (hususani vile vilivyotolewa sadaka kwa sanamu), kwamba hivyo havituhudhurishi mbele za Mungu, lakini tukila pia tuangalie wengine wanaathirikaje. Tusije tukawakwaza kwa ujuzi wetu. Paulo anaeleza ili tuweze kufikia hapo yatupaswa kuyafanya yote katika upendo.

1 Wakorintho 8:11-13

[11]Na yule aliye dhaifu aangamizwa kwa ujuzi wako, naye ni ndugu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake. 

[12]Hivyo, mkiwatenda dhambi ndugu zenu na kuitia jeraha dhamiri iliyo dhaifu, mnamtenda dhambi Kristo. 

[13]Kwa hiyo, chakula kikimkwaza ndugu yangu, hakika sitakula nyama hata milele, nisije nikamkwaza ndugu yangu. 

Lakini pia anaeleza haki waliyonayo mitume, kwamba wanaouwezo wa kula katika fungu la kanisa, lakini hawakutumia ujuzi wao wote, ili waweze kuifikisha injili kiwepesi kwa watu bila kuwazuilia na wengine.

6) Adabu na nidhani katika kukusanyika ndani ya  kanisa la Mungu( 1Wakorintho 11)

Paulo anatoa utaratibu wa ki-Mungu wa namna ya kuhudumu, kufuatana na hali ya kijinsia. Kwamba kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha mwanamume ni Kristo na kichwa cha Kristo ni Mungu. Hivyo mwanawake anapaswa wafunikwe vichwa awapo ibadani, ili kuonyesha kichwa chake(mumewe) kinamilikiwa na Kristo. Na kwamba wanawake wanapaswa watii uongozi (1Wakorintho 14:34-40)

Paulo anaeleza pia nidhani katika kushiriki meza ya Bwana, kwamba inapaswa ifanywe katika ufahamu na utaratibu sahihi wa rohoni, vinginevyo itapelekea hukumu badala ya baraka

7) Karama za Roho (1Wakorintho 12-14)

Paulo anazungumzia kwa undani karama mbalimbali ambazo Mungu ameziweka katika kanisa na kwamba zinapaswa ziwe kwa lengo la kufaidiana na kujengana. Lakini anaeleza kipawa kilicho bora zaidi ya karama zote, nacho ni upendo, ambacho anakieleza kwa urefu katika sura inayofuata ya 13, kwamba hichi kimezidi vyote.

1 Wakorintho 13:1-8

[1]Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. 

[2]Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. 

[3]Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu. 

[4]Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 

[5]haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; 

[6]haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; 

[7]huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. 

[8]Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika. 

8) Kufufuliwa kwa wafu. (1Wakorintho 15)

Katika eneo hili Paulo anahimiza  fundisho la kufufuliwa kwa wafu, akionyesha jinsi lilivyo umuhimu katika imani ya kikristo, na hiyo ni kutokana na baadhi ya watu waliozuka ndani ya kanisa kufundisha fundisho la kisadukayo kwamba hakuna ufufuo wa wafu. 

Akieleza jinsi Bwana atakavyokuja kwamba siku ya kurudi kwake parapanda italia na wote kwa pamoja (tulio hai na waliokufa) tutaipokea miili mipya ya utukufu itokayo mbinguni.

9) Michango kwa watakatifu. (1Wakorintho 16)

Katika sehemu hii ya mwisho Paulo anawaagiza juu ya utaratibu wa changizo kwa ajili ya watakatifu, kwamba vifanyike kila siku ya kwanza ya juma wakutanikapo, anawaagiza pia wakeshe, wawe hodari, na mambo yao yote yatendeke katika upendo.

Kwa hitimisho ni kuwa waraka huu unalenga hasa marekebisho, juu ya mambo mengi yaliyokuwa yanatendeka kwasababu ya ujinga, upumbavu, na dhambi ndani ya kanisa la Kristo. Na Ukweli ni kwamba mambo kama haya haya ni rahisi kuonekana hata katika kanisa la leo. Waraka huu tuusomapo yatupasa tuutazame kwa jicho la kikakanisa je! makosa kama ya wakorintho yapo katikati yetu, kama ni ndio basi tujirekebishe haraka sana.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Warumi.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini BWANA awaagize wakoma wakajionyeshe kwa Makuhani?(Luka 17:14

Jibu: Turejee kuanzia ule mstari wa 12..

Luka 17:12 “Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,

13 wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!

14 Alipowaona aliwaambia, Enendeni, MKAJIONYESHE KWA MAKUHANI. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika”.

Sababu kuu ya Bwana YESU kuwaagiza hawa wakome wakajinyeshe kwa Makuhani ni kwasababu Makuhani ndio watu wa mwisho kutangaza kama mtu ni Mkoma au si Mkoma, baada ya uchunguzi.

Kwani zamani mtu akihisiwa au akijihisi mwenyewe kama ni mkoma basi sheria ilikuwa ni kwamba anaenda kwa Kuhani, na kisha kuhani anauchunguza mwili wake na baada ya uchunguzi akibainika kwamba anao Ukoma, basi huyo mtu anakuwa najisi na anatengwa,

Sheria hiyo tunaisoma katika kitabu cha Mambo ya Walawi Mlango wa 13.

Walawi 13:9 “Pigo la ukoma litakapokuwa katika mtu, ndipo ataletwa kwa kuhani;

10 na kuhani ataangalia, na tazama, ikiwa pana kivimbe cheupe katika ngozi yake, na malaika yamegeuzwa kuwa meupe, tena ikiwa pana nyama mbichi iliyomea katika kile kivimbe,

11 ni ukoma wa zamani ulio katika ngozi ya mwili wake, na kuhani atasema kuwa yu najisi; hatamweka mahali, kwa kuwa yeye yuna unajisi”

Kwahiyo endapo wale watu kumi wenye ukoma wangefika kwa Kuhani na baada ya kukaguliwa wakakutwa na madhaifu hayo yaliyotajwa hapo juu, basi wangekuwa NAJISI..maana yake ni wenye ukoma ambao haujatakasika/kupona.

Na kama tayari walishachunguzwa zamani na kubainika wanao ukoma, na sasa wanarudia tena vipimo kwa kuhani ili kubaini kama ukoma wao umepona basi endapo wangekutwa. bado wanao basi wangeendelea kuwa najisi na kutengwa….

Lakini tunaona watu hao kumi (10) wakiwa njiani kuwafuata Makuhani ili waangaliwe, wakiwa njiani walijikuta wametakasika ule ukoma, walijikuta ngozi zao zimerudia hali zao za zamani, kama Naamani alivyoponywa ukoma wake. (2Wafalme 5:14).

Luka 17:14 “Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.

15 Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;

16 akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.

17 Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?

18 Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu”

Mambo makuu mawili ya kujifunza kufuatia habari hiyo

   1.Uponyaji wa YESU unahitaji imani yenye Matendo.

Laiti kama  hawa wenye ukoma wangeyadharau maneno ya Bwana YESU  aliyowaambia kuwa wakajionyeshe kwa Makuhani, na wangeenda njia nyingine, hakika wasingepona, wangebaki vile vile.

Lakini walipochukua hatua ya kwenda kwa Makuhani, kumbe maili kadhaa mbele muujiza wao ulikuwa unawangoja, kama tu ilivyokuwa kwa Naamani alipoambiwa akajichovye mara saba Yordani.

Hali kadhalika na wewe, shida au ugonjwa wowote ulio nao, kazi uliyobakiwanayo ni moja tu, kuyaamini maneno ya Bwana YESU na kuendelea mbele katika Neno lake, Muujiza wako utakutana nao mbele, usianze kuutafuta dakika hiyo hiyo.

  2. Kurudi kumpa MUNGU utukufu na kushuhudia.

Hili ni jambo la pili la kujifunza. MUNGU wetu anapendezwa na watu wa Shukrani.

Angalia mtu huyu alirudi kumshukuru MUNGU na kutoa ushuhuda na Bwana YESU akatafsiri tukio hilo ni kama kumpa MUNGU utukufu..

Huwenda MUNGU alishakutendea jambo fulani kubwa je uliwahi kurudi na kumtukuza mbele ya wengi?..Au je una mpango wowote wa kumtukuza katika hilo unalomwomba sasa akutendee?..Jibu unalo wewe.

Je tayari umempokea YESU?..Unao uhakika Bwana akirudi leo unaenda naye?.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post