Nakusalimu katika jina la Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tuzitafakari habari njema.
Tomaso alikuwa ni mtume wa Bwana. Lakini alikuwa na tabia ya kitofauti na wale mitume wengine 11. Yeye hakuwa msaliti kama Yuda, zaidi sana alikuwa hata radhi kufa na Bwana wake, kipindi Fulani aliposikia anatafutwa ili auawe (Yohana 11:16), hiyo ni ishara ya upendo wake kwa Yesu.
Lakini alikuwa na tabia nyingine ambayo ilimgharimu kwa sehemu Fulani, Na tabia yenyewe ni mashaka juu ya uweza wa Mungu, ni hiyo ikapelekea hata kuathiri mahudhurio yake, ya kiibada na kiutendaji kazi pale alipolazimika kuwepo na wenzake kama mtume.
Hakutaka kuamini kwamba Yesu anaweza kufufuka, hivyo wakati huo alipoitwa waombe pamoja, hakuwa tayari kukusanyika na wenzake, alipoitwa awafariji watu yeye kama mtume wa Bwana aliyepewa mamlaka hiyo, hakutaka kufanya hivyo kinyume chake akaenda kuendelea na shughuli zake. Walipokuwa wanatafakari maneno ya Yesu, yeye mawazo yake yalikuwa mbali kabisa na wenzake. Ni kama alikuwa amechoka.
Matokeo yake ikawa Yesu alipowatokea mitume wake, walipokuwa wamejifungia kuomba, yeye hakuwepo. Hata walipokuja kumuhadithia bado hakuamini, kwasababu moyo wake ulikuwa umeshahama kabisa.
Yohana 20:24 Walakini mmoja wa wale Thenashara, Tomaso, aitwaye Pacha, hakuwako pamoja nao alipokuja Yesu. 25 Basi wanafunzi wengine wakamwambia, Tumemwona Bwana. Akawaambia, Mimi nisipoziona mikononi mwake kovu za misumari, na kutia kidole changu katika mahali pa misumari, na kutia mkono wangu katika ubavu wake, mimi sisadiki hata kidogo. 26 Basi, baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwamo ndani tena, na Tomaso pamoja nao. Akaja Yesu, na milango imefungwa, akasimama katikati, akasema, Amani iwe kwenu 27 Kisha akamwambia Tomaso, Lete hapa kidole chako; uitazame mikono yangu; ulete na mkono wako uutie ubavuni mwangu, wala usiwe asiyeamini, bali aaminiye.
Wewe kama mtumwa wa Yesu usiwe tomaso, wakutanikapo wenzako kamwe kataa kujitenga, hata kama hakuna tumaini, dumu na wenzako, epuka utoro, epuka udhuru, dumu hapo. Zipo nyakati ambazo Bwana hamtokei mtu kivyake-vyake, bali wawapo wote. Zipo Baraka, ipo neema, katika umoja na wenzako, kupo kumwona Mungu unaposhikamana na wenzako kiuaminifu, katika kujengana na kutiana moyo.
Kamwe usifikiri kivyako, kataa hiyo hali, Bwana anasema ajitengaye na wenzake anatafuta matakwa yake mwenyewe, Tomaso alikuwa hivyo. Lakini fikra zake hazikuwa sahihi, aliligundua hilo baadaye aliporudi kujumuika na wenzake, ndipo akamwona Bwana, alidhani angemwonea kule alipokimbilia. Dumu na wenzako maadamu Bwana wenu ni mmoja, Roho wenu ni mmoja, Ubatizo wenu mmoja. Hiyo inatosha. Dumu hapo.
Bwana atusaidie.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Kwanini Tomaso atake kwenda kufa pamoja na Lazaro? (Yohana 11:14-16).
Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?
2 Petro 2:20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia MACHAFU YA DUNIA kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza”.
Mstari huo unatupa uelewa kwamba kumbe tukimjua mwokozi wetu Yesu Kristo, ni lazima kuambatane na kuyakimbia machafu ya dunia. Haiwezekani mtu akamjua Yesu Kristo halafu asiyakimbie Machafu ya dunia Kwa mujibu wa huo Mstari.
Machafu ya dunia ni Yale mambo maovu uliyokuwa unayafanya ulipokuwa mwenye dhambi, mfano ulevi, uzinzi, wizi, ushirikina, anasa, utoaji mimba, ulawiti, n.k.
Sasa ikiwa ukinaswa, na kushindwa kutoka huko, maandiko yanasema hali yako ya mwisho inakuwa mbaya kuliko Ile ya kwanza, maana yake kama ulikuwa ni mgonjwa kidogo, kutokana na madhara uliyoyapata katika Ile dhambi, basi ugonjwa unakuwa mara dufu zaidi, kama ulikuwa unaweza kujizuia usilewe mara Kwa mara, basi nguvu ya ulevi inakulemea mara mbili unakuwa mlevi yule wa kupindukia kabisa kabisa.. hiyo ni kutuonyesha ni jinsi gani tunapaswa tuwe makini kama vile maandiko yanavyosema pindi tuokokapo tuutimize wokovu wetu Kwa kuogopa na kutetemeka.
Wafilipi 2:12 “Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.
Bwana Yesu alitumia mfano wa Yule mtu ambaye alikuwa na pepo, lakini alipomtoka hakujiweka sawa, matokeo yake ikawa ni Yule pepo kuchukua pepo wengine saba waovu kuliko yeye, na hali yake ya mwisho ikawa mbaya kuliko ile ya kwanza. (Mathayo 12:43)
Ni kutubu haraka sana. Angali nafasi unayo. Kumbuka hapo anasema “akinaswa na kushindwa”
Maana yake ni kuwa kama umenaswa, ni kufanya hima ujinasue kabla mwindaji wako (ibilisi), hajakuweka mikononi mwako kabisa kabisa. Lakini ukishindwa.basi Ndio mwisho wako umefika.
Ikiwa ulirudia uzinzi, ulirudia ulevi, ulirudia anasa, ulirudia kujichua, kutazama picha chafu mitandaoni.. Acha haraka sana, toka huko kwa kasi zote, jitakase kwa Bwana, kisha maanisha kumfuata Yesu, huku ukiutimiza wokovu wako kwa kuogopa na kutetemeka, kwasababu huo tumekabidhiwa mara moja tu.
Na Bwana atakurehemu.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Ikiwa bado hujaokoka na utapenda leo kumpokea Kristo maishani mwako. Basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Shalom
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Wokovu wa milele/ Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)
SWALI: Warumi 14:7 Inamaana gani?
“Kwa sababu hakuna mtu miongoni mwetu aishiye kwa nafsi yake, wala hakuna afaye kwa nafsi yake”.
JIBU: Ni andiko linalotuonyesha uweza wa Mungu ulivyo wa kutawala/ kuendesha vitu vyote. Kwamba mwenye maamuzi yote yahusuyo maisha ya mwanadamu ni Mungu, Wala sio nafsi ya mtu kama atakavyo yeye mwenyewe.
ikiwa na maana kuishi kwako unalitimiza kusudi fulani la Mungu,(haijalishi wewe ni mwema au mtenda maovu) vilevile kufa kwako ni matokeo ya kusudi Fulani la Mungu.
Vifungu vinavyofuata vinazidi kuelezea vizuri zaidi…Anasema;
Warumi 14;8 Kwa maana kama tukiishi, twaishi kwa Bwana, au kama tukifa, twafa kwa Bwana. Basi kama tukiishi au kama tukifa, tu MALI YA BWANA.
Umeona? Wanadamu wote ni Mali ya Bwana, Hakuna mtu aliyejiumba mwenyewe..akawa na maamuzi yake yanayojitegemea yasiyopitishwa kwanza na Mungu.. mtu hawezi kusema kesho nitajitoa uhai wangu na kuurudisha, au kesho nitafanya hiki au kile, bila Mungu kulijua au kuliruhusu, au kulipanga ,. Au aseme baadaye nitaliamuru jua lisichomoze kwa matakwa yangu, Hilo jambo haliwezekani.
Sisi wote hatuishi Kwa nafsi zetu(mapenzi yetu ) wenyewe, Bali Kila jambo kama sio limeagizwa na Mungu, basi Mungu ameliruhusu.. Hata vifo vyetu vivyo hivyo. Na vitu vyote tuvifanyavyo. Kwasababu sote tunamilikiwa na Mungu.
Ndio maana ya hilo neno “hakuna mtu miongoni mwetu aishiye kwa nafsi yake, wala hakuna afaye kwa nafsi yake. ”
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Bwana Yesu alikuwa kabila gani?
Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?
Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)
Anaposema mwanamume mmoja katika elfu nimemwona anamaana gani?
SWALI: Nini maana ya Kumbukumbu 25:11
Kumbukumbu 25:11 “Washindanapo waume wao kwa wao, akakaribia mke wa mmojawapo, ili kumwokoa mumewe katika mkono wa ampigaye, yule mke akatoa mkono wake, na kumkamata tupu yake; 12 umkate ule mkono wake, lisiwe na huruma jicho lako”
JIBU: Bwana asifiwe, Haya ni mafundisho maalumu wayahusuyo wana-ndoa. Lakini pia kanisa la Kristo.
Kama ukiutafakari mstari huu, utaona picha ya mwanamke mwenye huruma, ambaye, ameona mume wake, anapigana na adui yake, na pengine alikuwa anakaribia kushindwa. Hivyo kwasababu ya upendo wake kwa mumewe, akaamua kwenda kumwokoa. Lakini tunaona njia aliyoitumia badala imletee alilolitarajia, ikamletea matatizo yeye mwenyewe.
Kwasababu gani? Kwasababu alikwenda kugusa sehemu zake za siri, Na hiyo ikawa kosa kwake, lililostahili adhabu ya kukatwa mkono. Laiti kama angemkamata mahali pengine labda tuseme mguuni, au penginepo, ni wazi kuwa kusingekuwa na adhabu yoyote au adhabu iliyo kali namna ile.
Ni mipaka ya mwanamke awapo ndani ya ndoa yake. Fikiria hata kwa adui ya mume wake huyu mwanamke, hukupaswa kuvuka mipaka ya kindoa, si zaidi kama angefanya hivyo kwa rafiki wa karibu wa mume wake ndio ingekuwa kosa kubwa kabisaa?. Leo hii kumekuwa na migogoro mingi ndani ya ndoa, na ukitazama utagundua tabia ya wanawake kutojiwekea mipaka yao, wakutanapo na wanaume wengine wa nje.
Kwamfano mwanamke yupo kazini. Halafu Boss wake/ mfanyakazi mwenzake anazungumza mazungumzo ya mizaha, ya kizinzi, utaona na yeye analiridhia hilo, au kulifurahia au anaona ni kawaida tu. Anashindwa kujiwekea mipaka, Anaipoteza nidhamu yake, anaruhusu mazoea yaliyopitiliza ambayo hayampasi mtu kama yeye kuwa nayo. Sasa hiyo ni hatari kubwa.
Wewe kama mwanamke unapaswa ujiwekee mipaka ya hali ya juu. Ukiona migororo inaendelea baina ya wanaume, jiwekee mipaka ya kitabia na kimwenendo. Uwe salama, ili mkono wako usifike kusikostahili. Uvaaji wako, usemi wako, uwe kama mtu aliye kwenye “KIFUNGO” cha ndoa. Watu wakuheshimu, wenye mizaha wakuonapo wakae kimya. Usiruhusu kabisa mazungumzo yako na mtu mwingine yafike kwenye maeneo ya sirini, iwe kwenye simu, ofisini, njiani, shuleni, mtaani, nyumbani, au popote pale. Weka MLANGO mkubwa wenye makomeo ya chuma . Mazungumzo hayo yawe na mume wako tu, na sio mwingine yoyote.
Halikadhalika inatupa na picha ya rohoni pia. Sisi kama kanisa ni lazima tufahamu kuwa wote ni “WAKE” wa Bwana wetu Yesu Kristo. Na hivyo anataka tuwe na tahadhari tuendapo kumuhubiri yeye kwa watu wa nje, tujichunge tusijaribiwe wenyewe, kwa vitendo vyao. Kwasababu itatugharimu kinyume chake.
Tukutanapo na wazinzi kuwahubiria, tusivutwe kwenye uzinzi wako, tukutanapo wa watukanaji, tusirudishe matusi, tukutanapo na wenye fedha, tusigeuzwe injili yetu. Bali tubaki kwenye mipaka yetu ile ile.
Wagalatia 6:1 Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;
Maana ya Mithali 29:21 “Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe”
Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.
USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.
Kwanini kuwe na kitabu Cha kumbukumbu la Torati na kwanini kiitwe vile?
Upo umuhimu mkubwa wa kuliita Jina la Bwana
Warumi 10:12 “Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao;
13 kwa kuwa, KILA ATAKAYELIITIA JINA LA BWANA ATAOKOKA”
Kuna umuhimu mkubwa wa kuliitia jina la Bwana kiusahihi, na kuna hatari kubwa ya kuliita au kulitaja jina la Mungu kimakosa.
Kutoka 20:7 “Usilitaje bure jina la Bwana, Mungu wako, maana Bwana hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure”.
Kwahiyo kama kwa kulitaja jina la Mungu bure ni dhambi, vile vile kinyume chake ni kweli kwamba tukilitaja inavyopaswa na kwasababu muhimu basi ni Faida kubwa kwetu.
Kwanini?, ni kwasababu jina la Mungu lina nguvu kuliko mwonekano wake…amelitukuza jina lake kuliko umbile lake, ndio maana amependa kutujulisha jina lake Zaidi ya sura yake.
Mithali 18:10 “Jina la Bwana ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama”
Leo kwa neema zake tutatazama njia sahihi ya kulitaja jina la Bwana Mungu kulingana na mazingira tunayopitia ili tupate wokovu, tumaini, faraja, ushindi, Amani na Nguvu!.
1.Katika kipindi cha mahitaji-Mwite YEHOVA-YIRE.
Yehova-Yire maana yake ni Mungu-Mpaji, (Mungu anayetoa kimiujiza)..Asili ya jina Yehova-Yire, ni kipindi Ibrahimu anakwenda kumtoa Isaka mwanae kama sadaka kwa Mungu, akiwa njiani mwanae Isaka alimwuliza Ibrahimu baba yake kuwa kuni zipo na moto pia upo lakini yupo wapi mwanakondoo?..Ndipo Ibrahimu kwa Imani alimjibu.. “Mungu atajipatia (Mwanzo 22:7-8)”.
Na walipofika katika mlima Moria ndipo wakamkuta kondoo ambaye tayari Bwana alikuwa amewaandalia. Ibrahimu akamwita Bwana YEHOVA-YIRE.
Vile vile na sisi tuwapo katika hali ya kuhitaji jambo Fulani (kama hitaji) tumwite Mungu kama YEHOVA-YIRE, itakuwa na mashiko Zaidi mbele zake kuliko kumwita au kumwomba tu kama MUNGU-MWENYEZI.
2. Katika nyakati za Magonjwa- Mwite YEHOVA-RAFA
Yehova-Rafa maana yake ni “Mungu-atuponyaye”. Wakati wana wa Israeli wanaelekea Kaanani, Bwana Mungu aliwaahidi “kutowaletea magonjwa yale aliyowapiga nayo wamisri” endapo wakidumu katika sheria zake na amri zake.. Hivyo wana wa Israeli baada ya kusikia hivyo wakawa wanamwita Mungu YEHOVA-RAFA, kipindi walipopitia magonjwa na maradhi, na Mungu alikumbuka ahadi yake hiyo na aliwaponya na magonjwa yao.
Kutoka 15:26 “akawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, mimi sitatia juu yako maradhi yo yote niliyowatia Wamisri; kwa kuwa Mimi ndimi Bwana nikuponyaye”.
Vile vile upitiapo magonjwa au maradhi, mwite Mungu kama YEHOVA-RAFA, na utauvuta uponyaji kirahisi Zaidi..ndivyo walivyofanya wana wa Israeli katika nyakati za magonjwa.
3. Katika Nyakati za vita- Mwite YEHOVA-NISI
Yehova-Nisi maana yake ni “Bwana ni Mungu wa vita”. Kipindi wana wa Israeli wanashambuliwa na Waamaleki, Mungu alimwambi Musa anyanyue mikono yake miwili juu, na aliponyanyua Israeli walishinda na aliposhusha waamaleki walishinda, na mwisho wa vita vile Israeli walishinda kwasababu Haruni aliitegemeza mikono ya Musa kuanzia asubuhi mpaka jioni (Kutoka 17:8-16).
Ndipo wana wa Israeli wakamwita Bwana YEHOVA –NISI, maana yake “Mungu wa Vita” (bendera yao).. Kwahiyo Nyakati za Vita walimwimbia Bwana, na kumsifu kama YEHOVA NISI na si Yehova Yire, na Bwana aliwaonekania.
Na sisi tukutanapo na vita mbele yetu viwe vya kiroho, kiimani au kiuchumi.. basi ni vizuri tukamwita Mungu wetu kama Yehova Nisi, tukamsifu na kumwimbia kwa jina hilo, na vita mbele yetu atavifanya maji!.. kwasababu yeye anaketi katika sifa.
4. Katika vipindi vya Hatari- Mwite YEHOVA–ROHI.
Yehova-Rohi maana yake ni “Bwana ndiye mchungaji wangu”. Daudi alipopita vipindi vya hatari, alimwita Bwana kama mchungaji wake, Yehova-Rohi na kumsifu kwa jina hilo (Zaburi 23). Na Bwana daima alionekana mbele yake alimwokoa na hatari za kifo na dhiki zilizopo mbele yake.
Vile vile na sisi tuonapo hatari, au tuhisipo hatari, jina jema la kumwita Bwana na kumtukuza nalo, na kumsifu nalo ni YEHOVA-ROHI.
5.Katika kipindi cha mambo yasiyowezekanika –Mwite YEHOVA-EL – SHADAI.
Yehova-Elshadai maana yake “Bwana ni Mungu-Mwenyezi” (anayeweza kufanya mambo yote).
Kipindi ambacho Ibrahimu anaona uwezekano wa kupata mtoto haupo kutokana na umri wa mke wake Sara, Bwana alijidhihirisha kwake kama Mungu mwenye uwezo wote (Mungu mwenyezi), na Sara akapata mimba, Hivyo Ibrahimu na Israeli wote wakaendelea kumwomba BWANA kama YEHOVA-ELSHADAI Katika vipindi vya mahitaji yaliyo magumu, kama utasa, ukame n.k
6. Katika nyakati za Upweke- Mwite YEHOVA-SHAMA.
Yehova-Shama maaana yake “Mungu yupo hapa” (Ezekieli 48:35). Nyakati ambazo unajiona upo peke yake, mwambie Bwana wewe upo hapa, YEHOVA-SHAMA, na uwepo wa kipekee utakufunika, ndivyo Israeli walivyomwita Bwana nyakati za upweke.
7. Nyakati za kukosa Amani- Mwite YEHOVA-SHALOM.
Yehova-Shalom, maana yake ni “Mungu Amani yangu”. Gideoni alipotokewa na yule malaika alihisi atakufa, lakini malaika yule alimwambia “hutakufa” na Gideoni akapata “amani”akamwita Mungu Yehova-Shalom.. Mungu ni Amani yangu.
Waamuzi 6:22 “Gideoni akaona ya kuwa ni malaika wa Bwana; Gideoni akasema, Ole wangu, Ee Bwana MUNGU! Kwa kuwa nimemwona Bwana uso kwa uso.
23 Bwana akamwambia Amani iwe pamoja nawe; usiogope; hutakufa.
24 Ndipo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu hapo, akaiita jina lake, Yehova-Shalomu; hata hivi leo iko huko katika Ofra ya Waabiezeri”.
Na sisi vitokeapo vipindi vya Amani ya moyo kupotea na hofu kutawala, hususani hofu ya kifo, basi tumwite Mungu kama Yehova-Shalom, na amani yake itatufunika.
8. Nyakati za kutamfakari Mungu kwa matendo yake- Mwite YEHOVA-ADONAI.
Yehova-Adonai maana yake ni “Mungu mwenye enzi yote(mfalme)” aliyeumba vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana. Sifa kwa ADONAI zina nguvu kama zikitajwa kwa maarifa hayo..
9.Katika vipindi vya Kupotea na kuhitaji wokovu- Mwite YEHOVA-MWOKOZI (YESU KRISTO)
Maana ya YEHOVA-MWOKOVU ni YESU,… Tafsiri ya jina YESU ni Yehova-Mwokozi. Hili ndilo jina lenye nguvu katika vipindi karibia vyote. Na ndilo jina la ukombozi, na hakuna jina lingine litupasalo sisi kuokolewa kwalo isipokuwa jina hili la YESU, (Matendo 4:12).
Ikiwa umepotea dhambini, liite jina la YESU naye atakusaidia, ikiwa hutajabatizwa ili ukamilishe wokovu sawasawa na andiko la Marko 16:16, na ukabatizwe kwa jina la YESU, (Matendo 2:38, Matendo 19:5 na Matendo 10:48).
Yapo na majina mengine mengi yafaayo kumwita Bwana wetu katika nyakati hizo, lakini hayo yatoshe kusema tu, kuwa Mungu wetu anatupenda na anataka tupate faida, na faida moja wapo ni hiyo ya kulitumia jina lake wakati wa mahitaji.
Lakini katika hayo yote fahamu jambo moja kuwa unapoamua kuanza kulitaja jina la Bwana ili uvute msaada kutoka kwake, hakikisha unaacha UOVU..
2Timotheo 2:19 “Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, KILA ALITAJAYE JINA LA BWANA NA AUACHE UOVU”
Je umempokea Yesu Kristo, na kusafishwa dhambi zako kwa damu yake?
Kumbuka tunaishi majira ya kurudi kwa YESU mara ya pili, na shetani anafanya bidii nyingi kuhakikisha watu wanaenda katika lile ziwa la moto pamoja naye.
Bwana atusaidie.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
ZIFAHAMU NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE SABA.
HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.
Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.
JE UMEJIANDAA KUTIMIZA UNABII UPI?
Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu Kristo, karibu tujifunze maneno ya uzima.
Kuna vitu ambavyo Mungu amepanga, vitokee kwa njia ya asili, na vingine amepanga vitokee ndani ya wakati wake alioukusudia. Kwamfano ikiwa amekusudia baada ya miaka kumi ndio uone majibu ya lile hitaji ulilomwomba, yeye mwenyewe ataanza kukuandalia njia sasa, na hatimaye ule wakati ukifika basi atafungua njia ya kukipata.
Lakini vipi kama utakihitaji kwa majira haya ya sasa. Na wakati huo huo iwe ni mapenzi ya Mungu na sio yako. Je hilo linawezekana? Maana yake ni kuwa uivuruge mipango yake ili afanye sasa hivi kile unachokihitaji. Je! Mungu anaruhusu tuwe watu wa namna hiyo?
Jibu ni ndio.
Na aliyetufundisha siri hiyo si mwingine zaidi ya Kiongozi wetu mkuu wa imani YESU KRISTO.
Embu tafakari haya maneno aliyoyasema.
Luka 18:1 Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa. 2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.
3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu. 4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,
5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima. 6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu. 7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?
8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?
Katika vifungu hivyo ni wazi kuwa Bwana anajifananisha na huyo kadhi, ambaye hakuwa tayari kumsaidia Yule mwanamke mjane haja yake kwa wakati ule. Lakini kutokana na hatua alizozichukua Yule mwanamke ilimbidi tu ampe kama alivyotaka.
Na ndivyo ilivyo kwa Mungu wako. Upo wakati unaweza kupata kile unachokitaka kwa wakati wako, na si kwa wakati wa Mungu? Zipo kanuni ambazo ukizitumia, zitakusaidia kuuvuta msaada wa Mungu kwa haraka zaidi.
Maombi ya kung’ang’ana yanaugusa sana moyo wa Mungu, zaidi ya sisi tunavyoweza kufikiri. Kwa bahati mbaya ni pale tunapoona Mungu amekaa kimya tunadhani, hasikii. Yeye mwenyewe anasema aliyeumba sikio utasemaje hasikii?? Tangu lini?. Mungu huwa anasikia, lakini anasubiri umakini wako wa kile unachokililia kwake, Kama alivyofanya huyo mwanamke. Kiwango chako cha kutokata tamaa, hupelekea majibu ya haraka ya maombi yako. Ukiomba leo hujaona kitu, unaendelea hivyo hivyo kesho, ikiwa kesho haipo, unaendelea kesho kutwa..hivyo hivyo hata kama ni kwa miaka 5, hakuna kusema, Mungu hatendi, au amenisusa. Omba bila ukomo, tena huku ukiamini asilimia mia kuwa Bwana analishughulikia ,Usibahatishe kuomba. Utapokea kinyume na wakati.
Vipingamizi vinaweza kutokea kwa wanadamu, na wakati mwingine hata katika Neno la Mungu. Kwa wanadamu ni kama vile kuvunjishwa tamaa. Na kuambiwa Mungu hayupo na wewe, au umemkosea Mungu. Hilo unaweza kukumbana nalo sana. Lakini vilevile, Mungu anaweza kukuuliza, unataka upokee hili kwa sifa ipi uliyonayo? Wewe utamjibuje? Hilo nalo utakumbana nalo moyoni mwako.
Embu fuatilia kisa hiki.
Mathayo 15:22 Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.
23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu. 24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie. 26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. 27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.
28 Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile.
Huyu mwanamke, alihitaji wokovu ambao wakati wake ulikuwa bado kwa watu wa mataifa, kwasababu Yesu alikuwa bado hajasulibiwa. Hivyo alipojaribu tendo ambalo lilikuwa ni gumu masikioni mwa watu. Moja kwa moja alikutana na vipingamizi. Cha kwanza ni kutoka kwa mitume walipoona Bwana hamjibu lolote, wakaanza kutaka afukuzwe, kwasababu anasumbua watu. Anapiga-piga kelele ovyo, anawavunjia wayahudi heshima, mpagani huyu. Lakini yeye hakujali yale maneno.
Baada ya hapo akakumbana na Bwana mwenyewe, ambaye hapo mwanzo alimtazama wala hakumjibu neno lolote. Kumbuka, tabia hiyo ya kutojibu watu hakuionyesha kwa huyu mwanamke tu, bali kwa watu wengine pia, lakini huyu tu habari yake ndio imerekodiwa kwasababu ya kitu alichokifanya. Na alipoambiwa habari za mbwa, hakusijikia vibaya, akawa na hoja hapo hapo za kutetea, kwamba hata mbwa wanapata yale masalio yaangukayo kutoka mezani mwa bwana zake. Na mwisho wa siku akapokea alichokihitaji kinyume na taratibu.
Vilevile na wewe unachomwomba Bwana, atakuuliza una vigezo gani vya kupokea hiki. Hezekia alikuwa na hoja za kumpa Bwana na hatimaye akaongezewa maisha kwa kuponywa ugonjwa wake. Na wewe pia jiandae kwa hoja nzito, na majibu yako kwa Bwana daima yawe ni haya “Bwana sistahili kupokea, lakini Kristo tayari alikufa kwa ajili yangu msalabani, kunistahilisha mbele zako ndilo linalonipa ujasiri huu wa kupokea chochote mbele zako kwa imani sawasawa (Waebrania 4:16)”. Ukifanya hivyo jiandae kupokea unachokihitaji.
Tendo la ziada, huvuruga mipango mingi ya Mungu. Kwamfano usipende kumwendea Mungu vilevile kwa desturi na mazoea ya sikuzote. Onyesha uhodari Fulani kwa Mungu, onyesha imani Fulani kubwa kwa Mungu. Mara nyingi Yesu alikuwa anafuatwa na Jeshi kubwa la makutano na kila mmoja alikuwa anahitaji ahudumiwe. Lakini utagundua wapo waliowahi kuhudumiwa kwasababu ya imani yao, na matendo yao ya kipekee kwake.
Zakayo hakufuata mkumbo, alibuni njia yake akapanda juu ya mkuyu Bwana akamwona. Yule mwanamke aliyetokwa na damu, hakufuata mkumbo, aliamini nikigusa tu pindo la vazi la Yesu nitapona. Yesu akaghahiri mwendo wake ili amtafute. Wale vipofu wawili Yeriko, waliposikia Yesu anapita, walipaza sauti zao kwa nguvu, wakisema Yesu turehemu. Yesu akawaponya
Vivyo hivyo na wewe, fanya jambo la ziada kwa Mungu wako. Kama ni kumsifu basi msifu zaidi ya kawaida ya sikuzote, uone kama hatafanya jambo kwako la ajabu. Kama ni kumtolea Mungu Mtolee zaidi ya kile kipimo cha kawaida. Fanya jambo kuu. Jimalize kwa ajili ya Bwana kwa kitu Fulani, Utaamsha moyo wa Mungu akuhudumie kwa haraka sana.
Esta, aliweza kuuvuruga utaratibu wa mfalme. Siku ambapo alipanga kumwendea bila kualikwa. Utaona kuwa alifuata kanuni ya kufunga pamoja na watu wake kwa siku tatu. Ndipo akamkabili mfalme. Na mfalme akatii jambo lile. Kwasababu ilikuwa ni kifo kumfuata mfalme kama hajakualika.
Vivyo hivyo na wewe umwombapo Mungu jambo fulani, hakikisha unaambatanisha mifungo. Kwasababu hiyo hukuongozea umakini wako mbele za Mungu.
Ikiwa utafuata utaratu huo, basi uwezekano wa kupokea mahitaji yako kinyume na njia za kawaida ni mkubwa sana. Uombapo katika eneo lolote liwe gumu au jepesi Bwana atakumulikia nuru zake.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.
KAZI ZA ROHO MTAKATIFU
KANUNI RAHISI YA KUPOKEA BARAKA MARA DUFU.
SWALI: Nini maana ya Mithali 16:30
Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka; Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya.
JIBU: Mstari huo haumaanishi mtu anayefumba macho yake, Huwa anaishia kuwaza mawazo mabaya, hapana kama ni hivyo basi, tungekuwa tunafanya makosa kufumba macho tunapoomba.
Zaidi sana mtu mwenye hekima huwa anapoona jambo la kutisha ovu, au lenye aibu Ndio anayekuwa wa kwanza kufumba macho yake asiruhusu kuona kinachoendelea.. kama vile walivyofanya watoto wa Nuhu.(Mwanzo 9:23)
Hali kadhalika anaposema mtu aikazaye (aifumbaye), midomo yake. Haimaanishi mtu asiyezungumza-zungumza, Huwa anaishia kuyazungumza maneno yasiyofaa. Kama ni hivyo biblia isingesema;
Mithali 21:23
[23]Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, Atajilinda nafsi yake na taabu.
Lakini je? Vifungu hivyo vilimaanisha Nini?
Hapo anaposema afumbaye macho yake ni kuwaza yaliyopotoka,..alimaanisha afumbaye macho asitazame kweli (ambayo ni Neno la Mungu), linapomfundisha au kumwonya. Mtu huyo lengo lake ni kuendelea katika mawazo yake mabaya ya dhambi. Mfano aambiwapo kuishi na mke ambaye si wako ni uzinzi, na wazinzi sehemu Yao ni Katika ziwa la moto, lakini hataki kuliona au kulisikia Hilo andiko, jibu lake ni kuwa anataka kuendelea katika matendo yake ya giza.
Ndicho kilichokuwa Kwa waliompinga Yesu., Ndio maana akasema maneno haya;
Mathayo 13:15 Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema,
Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya.
Vilevile anaposema “Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya”
Anamaanisha, aizuiaye midomo yake kusema maneno ya uzima, ya staha, ya kujenga, ya adabu, ya maarifa, ya busara n.k.. Mwisho wake utakuwa ni kunena maneno mabaya tu.
Bwana alisema..
Luka 6:45
[45]Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.
Vivyo na hivyo na sisi, hatuna budi tujipime na kujichunguza…macho yetu hutazama Nini, vinywa vyetu vimejawa na maneno gani.? Lakini fahamu kuwa huwezi kushinda jicho lako, au ulimi wako ikiwa Kristo hajaumbika ndani yako.
Je! Unataka msaada Kwa Yesu Kristo? Kama jibu ni Ndio, basi unachopaswa kufanya cha kwanza ni kuyaachilia maisha yako kwake. Ili akusamehe dhambi zako. Ndipo akupe nguvu ya kushinda dhambi.
Hivyo bofya hapa Kwa ajili ya Mwongozo wa Sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?
NI WAKATI UPI UTAUONA USO WA KRISTO?
Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?
Jina la Bwana na Mwokozi Mkuu YESU KRISTO lihimidiwe, karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu lililo hai, ambalo ndilo taa na mwanga wa njia yetu ya kwenda mbinguni (Zab.119:105).
Moja ya hubiri kubwa na kongwe la shetani, ni kuwahubiria watu kuwa “MUNGU HASAMEHI na ANACHUKIA WATU”.
Fundisho hili ni silaha kubwa sana ya kumfanya mtu asijaribu kumtafuta Mungu, au hata kama alikuwa ameshaanza hatua za kuutafuta uso wa Mungu, basi akate tamaa njiani. Anajua mtu akifahamu kuwa anaweza kusamehewa na Mungu basi hatampata tena, na yeye anataka watu waendelee kudumu katika dhambi ili hatimaye waukose uzima wa milele kama yeye alivyoukosa.
Sasa sifa moja kuu ya MUNGU aliyeumba mbingu na nchi, ni MSAMAHA. Maana yake “anatoa msamaha hata kwa mtu asiyestahili kusamehewa”.. Na hii ndio sifa ya kwanza inayomfanya yeye (MUNGU) kutisha!..na wala si tu yale matendo ya miujiza aliyoyafanya kule Misri, au anayoendelea kuifanya hata sasa, ambayo kimsingi tunadhani hayo ndiyo yanayomfanya Mungu atishe.
Muujiza Mkuu na wa kwanza unaomfanya Mungu kutisha, ni KUSAMEHE NDAMBI, na KUZIONDOA KABISA NDANI YA MTU.
Zaburi 130:3 “Bwana, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama?
4 Lakini kwako kuna msamaha, ILI WEWE UOGOPWE”.
Je! Unajihisi wewe ni mwenye dhambi, na unahisi dhambi yako haifutiki??…fahamu kuwa MUNGU kuna msamaha, na sio tu msamaha bali pia na ondoleo la dhambi, kiasi kwamba baada ya kusamehewa Mungu anaondoa mpaka msingi wa hiyo dhambi, kiasi kwamba wakati mwingine haitakuwa na nguvu juu yako.
Je unahisi mauaji uliyoyafanya hayawezi kusameheka?, je unahisi mawazo uliyowaza au unayowaza hayana msamaha?, je unahisi tendo ulilolifanya na tena umelirudia mara nyingi nyingi halina msamaha?..kama hayo mawazo yapo ndani yako basi fahamu kuwa ni adui ndiye anayekuambia hivyo.
Yote uliyoyafanya yanasameheka ikiwa utataka Bwana akusamehe!. Unachopaswa kufanya ni kutubu tu kwa kumaanisha kuacha hayo unayoyafanya, Ikiwa utatubu kweli kwa kumaanisha, basi kwa IMANI amini kuwa Mungu kashakusamehe, hauhitaji kutokewa na Malaika na akamwambie kwamba umesamehewa, wewe Amini tu, kwasababu ndivyo biblia inavyotufundisha kwamba “tuenende kwa Imani na si kwa kuona” (2Wakorintho 5:7).
Na ukishaamini namna hiyo, basi Mungu kashakusamehe lile kosa au yale makosa uliyoyafanya hata kama uliyafanya kwa kurudia rudia mara 100, tayari atakusamehe deni yako yote. Lakini kumbuka msamaha si ondoleo!.. Mtu anaweza kukusamehe tusi ulilomtukana, lakini kama ile roho ya kutukana haijaondoka ndani yako basi unaweza kurudia tena kesho na kesho kutwa kumtukana matusi yale yale.
Kwahiyo ili lile kosa lisijirudie rudie tena katika maisha yako, linahitaji kuondolewa kwa mizizi yake ndani yako. Sasa kanuni ya kuondoa mzizi wa dhambi ndio shetani amewafumba watu macho wasiione.
Lakini ashukuriwe Mungu kwasababu ipo wazi katika maandiko.
Tusome,
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.
Hapa Petro anawaonyesha hawa Makutano, kanuni ya KUONDOA MZIZI wa dhambi ndani yao, baada ya wao KUTUBU dhambi, kwamba WAKABATIZWE KWA JINA LAKE YESU KRISTO. Kama ishara ya kuuvua utu wa kale na kuuvaa utu upya, na kwa ishara hiyo ya maji basi ule mzizi wa dhambi utaondoka ndani yao, zile dhambi za kujirudia rudia zitakoma, kwahiyo mtu wa Mungu anabaki huru mbali na dhambi.
Na tena Mungu wetu kwa upendo wake anatuongezea na zawadi ya Roho Mtakatifu, ndani yetu kama Muhuri wa Mungu kwa kile tulichokitubia.
Je bado umezishikilia dhambi zako? Kwanini usiungame leo kwa kutubu na kubatizwa?. Na kumbuka ungamo sahihi ni lile la kutubu kwa kumaanisha, na ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi na kwa jina la BWANA YESU KRISTO, Kutubu kusikotoka moyoni, na ubatizo usio sahihi haviwezi kuleta matokeo yoyote kwa mtu.
Bwana akubariki.
Ikiwa utahitaji msaada katika kuongozwa sala ya Toba, au ubatizo basi waweza wasiliana nasi na tutakusaidia katika hilo.
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Je Imani yako imefifia?, je upendo wako umepoa?, je Amani yako imepungua?, na haki yako imepoa?.. Na hujui cha kufanya na ndani bado una haja sana ya kuwa na mambo hayo?.. Basi suluhisho lipo ndani ya biblia.
Ifuatayo ni kanuni moja nyepesi ya kurejesha joto la ROHO MTAKATIFU ndani yako. Kumbuka mtu aliyejaa Roho Mtakatifu ataonyesha matunda yafuatayo…
Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 23 upole, kiasi;…”.
Ikiwa mambo haya yalikuwa ndani yako lakini sasa huyaoni tena, au ikiwa hauna kabisa, basi tumia kanuni ifuatayo kuyarejesha/kuyajenga ndani yako.
KAA KARIBU NA WATU WATU WANAOMWITA BWANA.
Watu wanaomwita Bwana, kwa lugha nyingine ni watu waliookoka kikweli kweli,…Utauliza kwa namna gani?…Tusome maandiko yafuatayo..
2Timotheo 2:22 “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, PAMOJA NA WALE WAMWITAO BWANA KWA MOYO SAFI”.
Hapo mwisho anasema, ukatafute haki, Imani na upendo na amani “pamoja na wale wote wamwitao Bwana kwa moyo safi”.
Kumbe! Haki inapatikana kwa watu wanaomwita Bwana kwa dhamiri safi, kumbe tukikaa na watu waliomaanisha kumwita Bwana na kumtafuta basi Amani tutaipata, na upendo na Imani.
Kama maandiko yasemavyo kwamba “chuma hunoa chuma, Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake” (Mithali 27:17). Vivyo hivyo na sisi tunapokaa na watu wenye kumaanisha kumtafuta Mungu basi ule moto ulio ndani yao atahamia na kwetu pia.
Lakini tukijitenga na kubaki wenyewe, au tukijumuika na watu wengine wasio na nia ya dhati kumtafuta Bwana, ni ngumu kuuwasha ule moto wa Roho ndani yetu!, tutabaki kama tulivyo!.. Kanuni ni kukaa pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi!…Vile vile tunapojitenga na kuamua kukaa peke yetu kwa muda mrefu ni pia ni hatari!!.. Imani, amani, upendo na haki yako vinaweza kuathirika pakubwa.
Sasa tunawapatia wapi watu wamwitao Bwana kwa moyo safi?.
1.Katika kanisa lililo hai.
Hii ni sehemu pekee ambayo utawapata watu wamwitao Bwana kwa moyo safi, jiunge na kanisa la kiroho lililo karibu nawe, au hata lililo mbali ikiwa lililo karibu nawe halina utakatifu. Jumuika na watu hao, katika utii na unyenyekevu, na katika ibada zote, na hapo Roho Mtakatifu atakujenga ndani yako na kukujaza nguvu zake, utaona Imani yako inapata nguvu, upendo wako uliopoa unawaka tena, haki yako iliyopotea inarudi na Amani yako pia inahuika upya, na ifanye hiyo iwe desturi yako daima.
Waebrania 10:25 “wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine;..”.
Na utajuaje kanisa hilo, ni la kiroho?.
Kigezo cha kwanza ni mwonekano wa nje wa waabuduo wa mahali hapo!, ukiona mwonekano na mazungumzo ya waabuduo si ya kiMungu, kwamba wanazungumza kidunia na wanavaa kidunia, kiasi kwamba hauoni tofauti na mtu anayeenda disko na anayeshiriki mahali hapo, basi tuchukua tahadhari hapo si sehemu salama!.
Vile vile mafundisho yanayofundishwa mahali pale kama hayalengi TOBA, na UJIO wa PILI wa BWANA YESU, na UTAKATIFU wa MWILINI na ROHONI, pia hapo si sehemu salama, lakini kama kanisa lina vigezo hivyo vya Utakatifu wa kimafundisho na kimwonekano, basi ndani yake watakuwepo watu wamwitao Bwana kwa moyo safi, kaa hapo na utaona mabadiliko makubwa ya kiroho ndani yako.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Maran atha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?
Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.
Ikiwa wewe ni kijana basi fahamu basi fahamu mambo yafuatayo.
1.MAWAZO MABAYA YANAANZIA UJANANI.
Mwanzo 8:21 “Bwana akasikia harufu ya kumridhisha; Bwana akasema moyoni, Sitailaani nchi tena baada ya hayo kwa sababu ya wanadamu, MAANA MAWAZO YA MOYO WA MWANADAMU NI MABAYA TANGU UJANA WAKE; wala sitapiga tena baada ya hayo kila kilicho hai kama nilivyofanya”.
Mawazo ya kuidharau injili, mawazo ya ukaidi wa moyo na kiburi cha uzima yanaanzia ujanani.
Yeremia 22: 21 “Mimi nalisema nawe wakati wa kufanikiwa kwako; lakini ulisema, Sitaki kusikia. Hii ndiyo iliyokuwa desturi yako TANGU UJANA WAKO, KUTOKUITII SAUTI YANGU”.
2. MUNGU ANATAFUTWA UJANANI NA SI UZEENI!.
Mhubiri 12: 1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”.
Maana yake katika uzee “haitawezekana kabisa” kumtafuta Mungu kama utapuuzia wito wa Mungu katika ujana wako!!!. Wakati wa Ujana ndio wakati wa kujifunga NIRA YA MUNGU iliyotajwa na BWANA YESU katika Mathayo 11:29.
Maombolezo 3:27 “Ni vema mwanadamu aichukue NIRA WAKATI WA UJANA WAKE.
28 Na akae peke yake na kunyamaza kimya; Kwa sababu Bwana ameweka hayo juu yake”.
3. KAMA UTACHAGUA ANASA, BASI FAHAMU KUWA SIKU YA MWISHO UTASIMAMA HUKUMUNI.
Mhubiri 11:9 “Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya KWAMBA KWA AJILI YA HAYO YOTE MUNGU ATAKULETA HUKUMUNI”
Maana yake kama utachagua uzinzi katika ujana wako, au ulevi, au anasa nyingine yeyote basi pia jiweke tayari kusimama mbele ya kiti cha hukumu siku ile ya mwisho, ambapo maandiko yanasema kila mtu atatoa habari zake mwenyewe (Warumi 14:12), na tena kila neno la upuuzi litatolewa hesabu yake siku ile ya hukumu (Mathayo 12:36).
4. NEEMA YA WOKOVU HAIKUBEMBELEZI.
Ufunuo 22:10 “ Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.
11 MWENYE KUDHULUMU NA AZIDI KUDHULUMU; NA MWENYE UCHAFU NA AZIDI KUWA MCHAFU; NA MWENYE HAKI NA AZIDI KUFANYA HAKI; NA MTAKATIFU NA AZIDI KUTAKASWA”.
Ikiwa umechagua uchafu!, basi usiufanye kidogo!..ufanya sana, lakini kama umechagua USAFI, basi JITAKASE SANA, usiwe hapo katikati (vuguvugu!)..
5. UTAKAPOKUWA MZEE UTAPELEKWA USIKOTAKA.
Yohana 21:18 “Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na mwingine atakufunga na kukuchukua usikotaka”.
Uhuru ulionao si wa Daima, ipo siku utaisha, na wengine watakuwa na mamlaka juu yako…….
Je wewe kama kijana sasa umejipangaje?..je unawaza nini katika ujana wako huu? au unafikiri nini?…Kwanini usiamua kumgeukia Muumba wako leo!, na kuachana na udunia, na tamaa za ujanani, ambazo hazina faida yoyote Zaidi sana zina hasara nyingi?
2Timotheo 2:22 “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi”.
Bwana Yesu akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Ikiwa unahitaji msaada wa kuokoka na ubatizo basi wasiliana nasi kwa namba zetu tajwa hapo chini.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.
Je! Mke wa ujana wako ni yupi kibiblia?
ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.
Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?