KUOTA UPO KANISANI.

KUOTA UPO KANISANI.

Kuota upo kanisani inamaanisha nini kimaandiko?


Hiyo ni ndoto njema itakayo kwa Mungu. Kamwe shetani hawezi kukuotesha ndoto ya namna hiyo..

Kama umeota ndoto hii kuna mawili. La kwanza ikiwa wewe ni mkristo uliyeokoka na umesimama imara, Hapo ni Mungu anakuonyesha kuwa upo katika njia sahihi, hivyo endelea kumtafuta Bwana kwa bidii Zaidi kwasababu Upo uweponi mwake..Daudi alisema..

Zaburi 122:1 “Nalifurahi waliponiambia, Na twende nyumbani kwa Bwana”.

Kwasababu huko ndipo Mungu alipo. Kanisani na nyumbani mwa Bwana, kwahiyo ukiota upo kanisani ni ishara kuwa inaishi kwa Mungu.

Lakini ikiwa umeiota ndoto hii upo kanisani, na huku nyuma unajijua kabisa hauna mahusiano yoyote na Mungu, au hata kanisani huendi, Maisha yako ni ya dhambi..

Basi ujue hiyo ni sauti ya Mungu, anayokuvuta kwake,..Anakuonyesha kuwa hapo ndipo unapopaswa uwepo, hapo ndipo nyumbani kwako.. Wewe sio wa ulimwengu huu.

Hivyo itii sauti ya Mungu, mgeukie yeye, kwasababu huwezi jua ni kwanini afanye hivyo kwako leo… Kumbuka duniani hapa sisi ni wapitaji pengine kesho inayodhani itakuwepo inaweza isiwe yako.

Hivyo fanya uamuzi haraka wa kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuucha ulimwengu moja kwa moja, na ukifanya hivyo YESU atakusamehe, Fahamu hiyo ndoto inatoka kwa kwa Mungu kabisa hivyo usiipuuzie. Mungu huwa anazungumza na watu wakati mwingine hata Zaidi ya mara moja.

Ayubu 33: 14 “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.

15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani”;

Pengine Mungu alishazungumza na wewe kwa njia mbalimbali utubu dhambi zako umgeukie. Leo hii usiifanye shingo yako kuwa ngumu.

Kama upo tayari kuokoka na kuanza Maisha mapya na Yesu Kristo basi huo utakuwa ni uamuzi wa busara sana kwako..Unaweza kusema mimi mboni ni muislamu, haijalishi wewe ni nani, Mungu anakuita, kwasababu amekuchagua wewe na anakupenda, na anataka kukuokoa upate uzima wa milele..Hivyo fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa  Sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Na hayo mengine yaliyosalia Bwana atakusaidia kuyashinda.

Group la whatsapp Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

KUOTA UPO UCHI.

Hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge.(Ufu 21:27)

FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.

Podo ni nini na umuhimu wake ni upi rohoni?

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Elizabeth
Elizabeth
10 months ago

Ameen