Japo Wayahudi walikuwa wanamtazamia masihi wao kwa muda mrefu na kwa shauku nyingi, lakini tunasoma siku za kuzaliwa mwokozi duniani ni kikundi cha watu wachache sana ndicho kilichojua, tena kwa kufunuliwa. Wengine wote waliosalia hawakuelewa chochote, walizidi kuendelea katika mambo yao, hawakujua kuwa wakati mwingine umeshafunguliwa. Na pia ukichunguza wale waliofunuliwa kuzaliwa kwa Bwana duniani utagundua wote ni watu waliokuwa wanaenenda katika haki na kuzishika amri zote za Mungu bila lawama, mfano tunamwona Zekaria, pamoja na mke wake Elizabeti, Tunamwona Simeoni, Tunamwona Yusufu, tunamwona, Ana, wote hawa kama tukitazama habari zao ni watu waliokuwa wamemaanisha kweli kweli kuutafuta uso wa Mungu,ni watu ambao macho yao siku zote yalikuwa yanaelekea mbinguni wakiutazamia wokovu ambao Mungu aliokuwa amewaahidia kupitia Masiya wao, na ndio maaana mwisho wa siku walikuja kufunuliwa ule wakati ulipofika.
Lakini pia kama tunavyosoma yapo makundi mengine mawili, ambayo hayo yalifunuliwa lakini haikuwa kwa njia kama za hawa wa kwanza, kundi la kwanza ni wale mamajusi kutoka mashariki na kundi la pili lilikuwa ni wale wachungaji wa makondeni. Na kama ukichunguza hawa nao hawakufunuliwa wakiwa mmoja mmoja bali walifunuliwa kimakundi. Hawa hawakuwa wanaichunguza torati, wala kuijua sana dini, wengine walitoka mbali kabisa nje ya Israeli. lakini ni kwanini na wao pia Neema hii ya kipekee iliwafikia ?. Mungu alikuwa anayosababu kuwachagua na wale, Lakini Leo tutawaangalia wale wachungaji waliokuwa wakilinda makundi yao kule kondeni.
Kama tunavyosoma habari:
Luka 2:8 “Na katika nchi ile ile walikuwako wachungaji wakikaa makondeni na kulinda kundi lao kwa zamu usiku.
9 Malaika wa Bwana akawatokea ghafula, utukufu wa Bwana ukawang’aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu.
10 Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote;
11 maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.
12 Na hii ndiyo ishara kwenu; mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelala katika hori ya kulia ng’ombe.
13 Mara walikuwapo pamoja na huyo malaika, wingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu, na kusema,
14 Atukuzwe Mungu juu mbinguni, Na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.
15 Ikawa, malaika hao walipoondoka kwenda zao mbinguni, wale wachungaji waliambiana, Haya, na twendeni mpaka Bethlehemu, tukalione hilo lililofanyika, alilotujulisha Bwana.
16 Wakaenda kwa haraka wakamkuta Mariamu na Yusufu, na yule mtoto mchanga amelala horini.
17 Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto.
18 Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji.
19 Lakini Mariamu akayaweka maneno hayo yote, akiyafikiri moyoni mwake.
20 Wale wachungaji wakarudi, huku wanamtukuza Mungu na kumsifu kwa mambo yote waliyosikia na kuyaona, kama walivyoambiwa.”
Tukianzia juu kidogo tunafahamu baada ya Yesu kuzaliwa biblia inatuambia Mariamu na Yusufu walikosa sehemu ya kukaa kwani vyumba vya wageni vilikuwa vimejaa hivyo wakalazimika usiku ule ule kutafuta mahali pa kumlazia mtoto, wakaona kuliko kulala kando kando ya njia ni heri wajitulize chini ya zizi la kulizishia ng’ombe huko kwa muda. Mungu aliruhusu iwe hivyo kwa makusudi ili kutimiza kusudi Fulani. Kwani huyo mtoto atakuja kufananishwa na mwanakondoo, Hivyo mwanakondoo hawezi kuishi katikati ya majumba ya kifalme bali ni sharti katika mazizi ya mifugo.
Na ndio hapo tunakuja kuona muda huo huo wale malaika wakawaendea wale wachungaji waliokuwa wamekaa kule makondeni kuwapasha habari za kuzaliwa kwa mwokozi. Swali linakuja Ni kwanini basi wawe wale wachungaji na si watu wengine kama wakulima, au watoza ushuru, au wahasibu, au matabibu, au maaskari?. Embu jaribu kufikiria lingekuwa ni kundi la watoza ushuru ndio waliopelekewa taarifa zile, kwanza usiku ule wangekuwa wapo kitandani wamelala katika majumba yao ya kifahari, pili hawajui mambo ya zizini yalivyo, pengine wangefika tu pale wangetapika kwa harufu za vinyesi na mikojo ya ile mifugo, na pengine wangekutana na ile mbolea iliyoganda pale chini kwa vinyesi vya mifugo wasingeweza kukanyagisha miguu yao waingie ndani ya zizi lile, ule ungekuwa ni mtihani mkubwa sana.
Pia Jaribu kufikiria kama Herode angepelekewa yeye taarifa za kuzaliwa kwa mfalme, unadhani angeweza kuingia ndani ya zizi lile lililochakaa la kale?. Ni wazi kuwa asingeweza, utunzaji wa mifugo ni jambo ambalo linahitaji moyo wa kujitolea na wa kipekee sana na wa uvumilivu. Ukiwa mfugaji huna budi kuweka mbali kinyaa, na kukubali kuchafuliwa na mazingira ya mifugo yaliyopo.
Na ndio maana utaona hata wale wachungaji waliokuwa na mifugo, wakati mwingine walikuwa tayari hata kwenda kulala huko makondeni, kwenye hatari nyingi, wakikaa siku nyingi, usiku na mchana kulihudumia kundi, lisije likafa kwa kukosa malisho. Ni kazi ambayo inahitaji moyo sana.
Hivyo siku ile ya kuzaliwa jicho la Bwana lilipozunguza Israeli yote na kutazama ni watu gani watakaoweza kustahimili kukutana na mwokozi katika mazingira yale magumu ya zizini, ndipo walipoonekana wale wachungaji waliokuwa wamekaa makondeni.
Wakati ule Yusufu na Mariamu wakiwa katika hali ya upweke wakiwaza ni nani atakayekuja kuwatazama mahali hapa pachafu, ni nani atakayekuja kusaidia kuweka mazingira safi na kuwafariji mahali pale pasipostahili kukaa mtu. Ndipo ghafla wakaona kundi kubwa la wachungaji linaingia katika zizi lile kwa furaha na kwa shangwe. Haleluya! mahali pale paligeuka kuwa kama Ikulu. Pengine hata watu waliokuwa wanaishi kando kando ya zizi lile walishangaa umati huo wa wachungaji wametoka wapi usiku ule, wakishangilia kwa furaha kuu na vigelegele, Na kwa jinsi walivyokuja kulakiwa kwa shangwe hata Mariamu na Yusufu hawakujali tena kama wapo katika zizi la kulishia ng’ombe, mahali pale palichangamka ghafla, Kwasababu wenyeji wao wamewasili, haraka moja kwa moja wakaanza kuzoa mavi ya kondoo na ng’ombe yaliyokuwa yapo karibu na wao,kwani hilo ni jambo la kawaida kwao, mambo ambayo mhasibu yeyote asingeweza kufanya, mambo ambayo mtoza ushuru yeyote asingeweza kufanya, askari yeyote asingeweza kufanya.
Basi haraka haraka wakawaandalia wakawasaidia kufanya yale mambo ambayo hawakauweza kuyafanya peke yao, pengine uchafu ambao hawakuweza kuutoa,walisaidiwa na wale wachungaji na zizi lile likageuka kuwa mahali pa kukaa mtu. Na ndipo wakatoa habari zake, na kurudi makwao kwa furaha kuu na kwa shangwe. Ilikuwa ni furaha iliyokuja kwa kujua kuwa miongoni mwa wale wachache sana kati ya mamilioni ya waliokuwa Israeli, wao na walipata neema ile.
Lakini Mambo hayo kwa sasa yanafunua nini?, kama ilivyokuwa kuja kwa Bwana mara ya kwanza, ndivyo itakavyowa kuja kwa Bwana mara ya pili kulichukua kanisa lake. Kama kipindi kile Wayahudi wengi walikuwa wanamtazamia masihi wao siku moja aje kuwakomboa, ndivyo ilivyo kwa kanisa la sasa, Watu wote wanaojiita wakristo wanamtazamia Kristo kuja kulichukua kanisa lake.
Na kuja kwa sasa hivi sio kwa kuishi tena duniani kama alivyokuja mara ya kwanza, hapana bali ni kwa lengo la KUNYAKUA. Na yeye mwenyewe alituambia atakuja kwa siri kama mwivi ajavyo usiku, mfano tu wa jinsi alivyokuja kwa mara ya kwanza halikuwa ni jambo lililotangazwa mabarabarani kwa kila mtu aliyepita, bali walifunuliwa watu wachache sana, wale tu ambao muda wao wote walikuwa wanaenenda katika haki yote, na kuutazamiwa wokovu huo, mfano wa Ana na Simoni. Vivyo hivyo na leo hii watakaofunuliwa siku ile ni wale tu watu ambao macho yao na mawazo yao yote yanaelekea mbinguni, usiku na mchana wanatamani Bwana aje alichukue kanisa lake waende zao kwa Baba. Watu wa dizaini hiyo siku ile ikifika haitawajia kama mwivi bali watajua kwani ni Mungu mwenyewe atawafunulia.Watavuna walichokuwa wamekipanda kwa muda mrefu.
Lakini pia lipo kundi lingine, ambalo leo tutaliangalia, linalofananishwa na wale wachungaji waliokuwa kule makondeni. Kama tunavyofahamu Bwana akija hatakuja kwa ajili ya ulimwengu mzima, bali atakuja kwa ajili ya Kanisa lake. Hivyo siku ile atapita katika kanisa lake kwa siri kuwachukua walio wake na kuondoka. Na ndio maana tunaona hata Bwana kuja kwake kwa kwanza kulianzia katika HORI LA KULIA NG’OMBE, KATIKA ZIZI LA MIFUGO, mahali ambapo kondoo wapo, mahali ambapo kondoo wake wanalishiwa, wanapotengewa chakula ndipo alipokuja. Na kama tunavyojua kondoo wa Kristo wapo katika kanisa lake. Na ndiko huko huko Bwana atakapotulia. Hatakuja katikati ya taasisi Fulani ya serikali au chama Fulani cha kisiasa au jumuia Fulani ya kikabila, au katikati ya taifa fulani. Hapana bali katika kanisa lake teule,walipo kondoo wake.
Na hivyo kama vile UTUKUFU wa Bwana ulivyowaangazia kwanza wale wachungaji waliokuwa makondeni, vivyo hivyo Utukufu wa kurudi kwa pili kwa Bwana utawaangazia kwanza wachungaji wake wote waaminifu walio duniani wanaojitaabisha kwa ajili ya kulilisha kondoo, Usiku na mchana wanaokaa huko makondeni, wanaozunguka huku na kule, wanaotafuta hiki na kile kwa ajili ya kulilisha kundi lake, Na hivyo siku wasiyodhani utukufu wa Mungu utawaangazia wote kwa pamoja, wao ndio watakuwa wa kwanza kufahamu ujio wa Kristo, hata kama watakuwa hawana maarifa ya kutosha juu ya mafunuo ya Mungu, lakini siku hiyo ikifika fahamu tu ndio watakaokuwa wa kwanza kuuona utukufu wa Mungu. Hatabakia mchungaji yeyote aliye mwaminifu ambaye hata uona utukufu huo, hata awe mbali kiasi gani, atauona tu.
Wengi wanaona kulichunga kundi la Mungu, ni kazi ya kujichosha, isiyo na malipo kujitaabisha kwa ajili ya watoto wa Mungu, wanaona kama hakuna faida yoyote, wanaona ni kheri wakafanye shughuli zao nyingine, kuliko kuhangaika na vinyesi vya mifugo, ni kazi isiyopewa heshima yoyote. Lakini kumbuka kuwa Kristo hatakuja kwa waasibu, wala kwa wafanyabiashara, wala kwa wanasiasa, wala kwa madaktari, bali kwa kanisa lake, na hivyo ni sharti awaone kwanza wale walichungao kundi hilo kisha wafuate wengine. Atawatafuta kwanza wale watoa posho wake, aliowaweka katika kanisa lake, wawape watu wake posho kwa wakati.
Hivyo nataka kukutia moyo wewe ambaye utatoa muda wako kulitazaa kundi la Mungu, usikate tamaa, kwasababu ipo siku UTUKUFU MKUU wa Bwana utakuangazia na siku hizo si mbali. Zidi kulihurumia kundi la Bwana kwa jinsi Mungu anavyokupa neema, ikiwa ni usiku ikiwa ni mchana, endelea kuitenda kazi, fundisha, onya , karipia, Na wakati wa Bwana ukifika utakuwa wa kwanza kulipokea lile fungu la utukufu wake.
Ubarikiwe sana.
Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine, Na Bwana atakubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Zinazoendana:
KWANINI YESU ALIMUITA BABA YAKE “ABA”?
Mathayo 15.1 “Ndipo Mafarisayo na waandishi toka Yerusalemu walipomwendea Yesu wakisema,
2 Mbona wanafunzi wako huyahalifu MAPOKEO YA WAZEE, kwa maana hawanawi mikono walapo chakula.
3 Akajibu, akawaambia, Mbona ninyi nanyi huihalifu amri ya Mungu kwa ajili ya MAPOKEO YENU?
4 Kwa kuwa Mungu alisema, Mheshimu baba yako na mama yako, na Amtukanaye baba yake au mama yake kufa na afe.
5 Bali ninyi husema, Atakayemwambia babaye au mamaye, Cho chote kikupasacho kusaidiwa na mimi ni wakfu,
6 basi asimheshimu baba yake au mama yake. Mkalitangua neno la Mungu KWA AJILI YA MAPOKEO YENU.
7 Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema,
8 Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami.
9 Nao waniabudu bure, WAKIFUNDISHA MAFUNDISHO YALIYO MAAGIZOYA WANADAMU.
10 Akawaita makutano akawaambia
11 Sikilizeni, mfahamu; Sicho kiingiacho kinywani kimtiacho mtu unajisi; bali kitokacho kinywani ndicho kimtiacho mtu unajisi.
12 Ndipo wanafunzi wake walipomwendea, wakamwambia, Wajua ya kuwa Mafarisayo walipolisikia neno lile walichukizwa?
13 Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang’olewa.
14 Waacheni; hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili.
15 Basi Petro akajibu, akamwambia, Tueleze mfano huo.
16 Yesu akasema, Hata sasa ninyi nanyi mngali hamna akili?
17 Hamjafahamu bado ya kuwa kila kiingiacho kinywani hupita tumboni, kikatupwa chooni?
18 Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni;
navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.
19 Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa
uongo, na matukano.
20 HAYO NDIYO YAMTIAYO MTU UNAJISI; LAKINI KULA KABLA HAJANAWA MIKONO HAKUMTII MTU UNAJISI”
Habari hiyo ni baada ya Mafarisayo kuwashutumu wanafunzi wa Bwana Yesu, Ni kwanini hawanawi mikono kabla ya kula chakula.
Sasa katika Torati hakuna mahali popote Bwana Mungu aliwaagiza wana wa Israeli wanawe mikono kabla ya kula chakula, hakuna mahali popote kwenye biblia (katika Agano la Kale) Mungu alitoa maagizo ya namna hiyo..Yalikuwa ni mapokeo yalitengenezwa na wazee wa kiyahudi, kwamba ni lazima watu wanawe kabla ya kula,ni mambo waliyojitungia wao wenyewe tu!, na si kutoka kwa Mungu…Na ndio maana utaona hapo mafarisayo wanawalaumu wanafunzi wa Yesu “kwanini wanayahalifu wapokeo ya wazee”..na sio mapokeo ya Mungu.
Kwa ufupi utaratibu wa kunawa mikono kabla ya kula “yalikuwa ni mafundisho ya wanadamu” na si mafundisho ya Mungu. Sasa kwa kawaida tendo lolote au pokeo lolote la kimwili sio baya, lakini linapochukua nafasi ya mapokeo ya ki-Mungu ndipo linapokuwa ni Baya na lenye madhara makubwa sana.
Kwa mfano pokeo hilo la desturi ya kunawa mikono kabla ya kula chakula sio baya, ni lizuri na linafaa sana,hata kwetu tunalo, kwanza kwa ajili ya usafi na kwaajili ya ustaarabu. Lakini shida inakuja ni pale linapotumika kama ndio sababu ya Mungu kumbarikia mtu au kumlaani mtu. Na kutafsiriwa isivyopasa kwamba ndio kitu cha Muhimu sana Mungu anachokiangalia kwa mtu, na kwamba akikihalifu hicho basi ni dhambi kubwa sana kwa huyo mtu, Jambo ambalo Mungu hajaliagiza mahali popote pale kwa watu wake.Ndio maana Bwana Yesu alizidi kuwaambia maneno yale.
“8 Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami.
9 Nao waniabudu bure, WAKIFUNDISHA MAFUNDISHO YALIYO MAAGIZOYA WANADAMU”.
Sasa tukirudi kwenye kiini cha Somo a kinachosema ni kitu gani kimtiacho Mtu unajisi??
Sasa ni vizuri tukafahamu maana ya neno “unajisi” kama lilivyotumika hapa lina maana gani…Kumbuka unajisi uliotumika kwa wanyama “najisi” sio sawa na lilivyotumika hapa “kwamba vimtokavyo mtu moyoni ndivyo vimtiavyo mtu unajisi”…unajisi uliotumika kwa wanyama una maanisha “wanyama wasio safi” kwa kiingereza “unclean animals”..kwahiyo unajisi hapo kwa wanyama umetumika kama “kitu kisicho-kisafi”
Lakini katika mstari huu wa Mathayo 15:19 Bwana aliozungumzia kitu kimtiacho Mtu unajisi..hakumaanisha kuwa ni “kitu kimfanyacho mtu kutokuwa safi” hapana bali unajisi kama ulivyotumika pale ni “kitu kinacho mharibu mtu”..kwa lugha ya kiingereza ni “Thing that defiles a man”..Kwahiyo neno unajisi hapo limetumika kama “Uharibifu”…na sio “kitu kisichosafi”
Kwahiyo hiyo sentensi kwa ufasaha zaidi tunaweza kuutafsiri hivi..
“17 Hamjafahamu bado ya kuwa kila kiingiacho kinywani hupita tumboni, kikatupwa chooni?
18 Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni;navyo ndivyo VIMHARIBUVYO MTU.
19 Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano.
20 hayo ndiyo YANAYOMHARIBU MTU; lakini kula kabla hajanawa mikono Hakumharibu mtu”
Kwa sentensi hiyo basi tunaweza tukaona ni mambo gani yanayomuharibu Mtu…Ni mambo gani yanayoweza kuiharibu nafsi ya mtu, ni mambo gani yanayoweza kumletea mtu dhiki, na mateso, na mauti, wakati mwingine hata magonjwa…Hayo sio mengine zaidi ya matendo yote ya giza, kama uasherati, utukanaji, wizi, uuaji, mawazo mabaya n.k
Vyakula au kwa ufupi riziki za ulimwengu huu, haziwezi kutufanya tupatikane au tusipatikane na madhara, vyakula havina ulinzi wowote katika maisha yetu..Mali hazina ulinzi wowote katika maisha yetu, Bali vitokavyo mioyoni mwetu ndivyo vyenye ulinzi..Kadhalika vile vitokavyo mioyoni mwetu ndivyo vyenye kuleta kuharibu pia.
Tunajijenga kwa vile vyema vitokavyo mioyoni mwetu, na tunajiharibu kwa vile vibaya vitokavyo mioyoni mwetu… Huoni mawazo mabaya ndiyo yanayompeleka mtu kuua, kuiba, kuafanya uasherati, kutukana, kupandikiza chuki na masengenyo haya yote ndiyo yanayomletea mtu uharibifu wake mwenyewe..
Ndugu yangu ni vizuri kushika mapokeo tuliyopokea kwa waalimu wetu wa dini, au wazazi wetu kwamba tuzingatie mlo kamili, tujitunze kwa kila namna, tuchemshe maji ya kunywa, tufanye check-up kila mara ili tuepukane na magonjwa hatarishi, na tuwe watanashati..hayo ni mazuri sana na yanatufaa lakini pamoja na hayo ongezea kufahamu kitu hichi kimoja tena… “kikuingiacho mwilini mwako hakikuharibu wewe, bali kikutokacho moyoni mwako ndicho kikuharibucho”..Moyo wako msafi ndio utakaokupa afya mifupani mwako na maisha marefu ya kuishi sio aina ya vyakula unavyobadilisha, wala checkup unazozifanya kila wiki.
Mithali 4: 20 “Mwanangu, sikiliza maneno yangu; Tega sikio lako, uzisikie kauli zangu.
21 Zisiondoke machoni pako; UZIHIFADHI NDANI YA MOYO WAKO.
22 MAANA NI UHAI KWA WALE WAZIPATAO, NA AFYA YA MWILI WAO WOTE.
23 LINDA MOYO WAKO KULIKO YOTE UYALINDAYO; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
24 Kinywa cha ukaidi ukitenge nawe, Na midomo ya upotovu uiweke mbali nawe.
25 Macho yako yatazame mbele, Na kope zako zitazame mbele yako sawasawa.
26 Ulisawazishe pito la mguu wako, Na njia zako zote zithibitike;
27 Usigeuke kwa kuume wala kwa kushoto; Ondoa mguu wako maovuni”
Neno la Mungu linatuambia tulinde mioyo yetu kuliko vyote tuwezavyo kulinda maana ndiko zitokazo chemchemi za Uzima.
Ni matumaini yangu kuwa Bwana amekujalia kuona na kujua kile alichotaka ukione siku ya Leo. Na kutafuta Ulinzi wa Moyo wako.
Kama hujampa Bwana Yesu maisha yako, hujachelewa ni kheri ufanye hivyo sasa hivi, maana nyakati tunazoishi ni nyakati za hatari, miaka imesogea sana na Kristo yupo mlangoni kurudi..Anza mwaka huu kwa kuanza kuishi maisha mapya katika Kristo, tubu kwa kumaanisha kuziacha dhambi zako, na kisha katafute mahali wanapobatiza ubatizo sahihi wa maji tele na kwa Jina la Yesu Kristo, ukabatizwe kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako kulingana na Matendo 2:38, Na Bwana Yesu Mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu atakayeweza kukusaidia kushinda dhambi na kukuongoza katika kuijua kweli yote ya Biblia..Na kwa kufanya hivyo utakuwa umeokoka! Na kuwa na tumaini la Uzima wa Milele, na kwenda mbinguni na Bwana atakapokuja kulichukua kanisa lake.
Bwana akubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Zinazoendana:
MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.
DALILI ZIPI ZITAMTAMBULISHA MTU KUWA AMEFANYIKA KIUMBE KIPYA?
Kama ukichunguza watu wote walioathiriwa na ulevi wa kupindukia huwa wanaonyesha tabia zinazofanana, moja ya tabia hizo ni kutokujali jambo lolote linaloweza kuja mbele yake, mtu akishalewa hata hajali tena thamani ya utu wake, anaweza akavua nguo mbele za watu, utakuta kabla hajanywa alikuwa ni mtu mwenye heshima lakini akishalewa tu, matusi yaanza kumtiririka mdomoni mwake, anakuwa sio mtu wa kujali, sio mtu wa kujizuia, sio mtu wa kuchukua tahadhari kwa kitu chochote kile kitakachokuja mbele yake, anaweza akasimama katikati ya barabara kuu sehemu ambayo magari yanapita na kuanza kujiongelea mwenyewe bila kujali kuwa anaweza kugongwa na gari akafa. Na ndio maana hata ajali nyingi zitokeazo zinasababishwa na madereva kuwa walevi..Ni kwasababu gani? Ni kwasababu FAHAMU ZAO zinakuwa zimeshawatoka kwa wakati huo na kama ufahamu umeshawatoka basi hata ule uwezo wa kufikiri, wa kujitawala na wa kuchukua tahadhari unakuwa umeondoka ndani yao.
Lakini mtu huyo huyo uje umwangalie baadaye zile pombe zimeshaisha kichwani mwake, na hapo ufahamu wake umeshamrudia atajishangaa ni kwanini amelala mtaroni, ni kwanini alikuwa anawavunjia watu wengine heshima, na ni kwanini alikuwa hathamini uhai wake kusimama katikati ya barabara n.k..
Na ndio maana Biblia inasema Hosea 4: 11 “UZINZI NA DIVAI na divai mpya huondoa fahamu za wanadamu”.
Unaona? kwa namna hiyo hiyo pombe inavyoweza kuondoa ufahamu wa watu ndivyo hivyo hivyo hata UZINZI unavyoondoa FAHAMU za watu biblia inatuambia hivyo. Maneno hayo alithibitishiwa Nabii Hosea pale alipopewa maagizo na Mungu akaoe mke kahaba, na azae naye watoto, mwanzoni alidhani pengine atakuwa kahaba tu halafu basi wala hakutakuwa na madhara mengine yoyote ya ndani, lakini kwa jinsi alivyokuwa anakaa nae na kuona mwenendo wake jinsi ulivyokuwa wa hatari sana, jinsi huyo mwanamke asivyokuwa mtu wa kujali mambo ya Mungu, jinsi huyo mwanamke alivyokuwa anapoteza mapenzi na Mungu wake siku baada ya siku, jinsi huyo mwanamke anavyozidi kuwa mbali sana na wanawake wengine kwa kila kitu, jinsi roho yake ilivyozidi kupotea pasipo hata yeye mwenyewe kujitambua kutokana na ukahaba wake, ndipo alipopata ufahamu huo kutoka kwa Mungu na kusema maneno haya.
“Uzinzi na divai na divai mpya huondoa fahamu za wanadamu.”. Ni kwanini leo hii mtu hajali juu ya hatma ya maisha yake ya milele baada ya kufa hata kama aambiwe moto wa Jehanum ni mkali mara elfu ya huu, bado hajali, Sababu sio kwamba yeye ni sugu hasikii, hapana sababu ni roho iliyo ndani yake ya UZINZI imeshamwondolea ufahamu wa kujali maisha yake bila hata yeye mwenyewe kujijua, na ndio hapo hata akielezwe habari za hukumu inayokuja utaona anaanza kufanyia mzaha, au anapuuzia, au anakufuru Ni kwasababu ule UFAHAMU aliopewa na Mungu wa kupambanua na kufikiri, na kuchukua tahadhari ulishamtoka siku nyingi.
Utakuta mtu kuongea matusi ni kitu cha kawaida kwake hasikii hata kuhukumiwa ndani ya moyo wake, unadhani alianza hivyo? Hapana zamani alikuwa anaogopa kutukana lakini kwasababu muda wote amekuwa akiishibisha nafsi yake kwa uasherati, na uzinzi na zinaa, na maneno ya uchafu, na huku biblia ilishakataza hata uasherati usitamkwe vinywani mwetu, basi bila kujua yeye anaendelea kufanya hivyo hajui kuwa kidogo kidogo anaupoteza ufahamu wake, ndipo hapo anajikuta kutukana ni sehemu ya maisha yake.
Kwa nje! Anaweza akajiona ni mwenye akili na mjanja, anaonyesha kuwa yeye naye ni kijana, lakini nyuma ya pazia hajui kuwa FAHAMU zinamtoka kidogo kidogo, na roho ya kutokujali inamvaa mpaka inafikia wakati hata aelezejwe habari za Mungu hawezi tena kugeuka, ndio inakuwa basi tena, anaishia kupinga Neno la Mungu na kuutukana msalaba. Zinaa ni mbaya kama ulivyo ulevi. Tuikimbie zinaa ndugu!!
Na ndio maana sehemu nyingine biblia inasema
Mithali 6: 32 “Mtu aziniye na mwanamke HANA AKILI KABISA; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”.
Unaona, uasherati, uzinzi, ni mambo ambayo yanapoteza nafsi za watu kwa spidi kubwa kushinda hata mambo mengine yote. Na ndio maana shetani anapenda sana kuitumia hiyo kuwanasa watu, Anajua kabisa miili ya wanadamu ni mahekalu ya Roho Mtakatifu hivyo anafanya juu chini ayaharibu makao hayo ya Mungu ili Mungu akose mahali pa kutua, Na kama tunavyofahamu hata hii Dunia mfano kama Roho wa Mungu asingetua na kuanza kuipendezesha tena, basi ingeendelea kubakia katika hali ile ile ya utupu na ukiwa na giza milele, Sasa kama na sisi hatutaihifadhi miili yetu, na kumjengea Roho wa Mtakatifu mazingira ya kutua na kututengeneza unadhani tutapataje kupona au kuokoka?. Ni wazi kuwa tutaendelea kuwa katika giza mpaka siku ya hukumu na kuishia kutupwa katika ziwa la moto.
Ndugu/kaka kaa mbali na zinaa. Kaa mbali na vichochezi vyote vya zinaa, kaa mbali na mustarbation hivyo vyote vinaondoa ufahamu wako ndugu, unaweza ukajiona upo sawa lakini hujui ni jinsi gani nafsi yako inavyoharibika kwa spidi kubwa sana, kaa mbali na pornography na utazamaji wa picha za uchi mitandaoni, hivyo vinaondoa ufahamu wako kama vile pombe inavyoondoa ufahamu wa mtu. Weka mbali muvi na vitabu vinavyoonekana kuchochea zinaa ndani yako, hiyo ni kwa usalama wa roho yako ndugu kwa kizazi hichi Bwana anachokiona ni kizazi cha zinaa. Kaa mbali na watu au marafiki ambao muda wote mazungumzo yao ni habari za uasherati tu, disco na anasa..Hao watakupeleka kuzimu.
Usiruhusu roho ya kutokujali ikuingie, usikubali kupoteza ufahamu wako Mungu aliokupa, kwa Uzinzi. Mungu alikusudia wewe uwe mtakatifu kama yeye alivyo, hayo ndio mapenzi yake kwako
1Petro 1: 15 “bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;
16 kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu”.
Lakini ni kwanini ulikuwa ukisikia maneno hayo ya Mungu unapuuzia, na huku mwingine akiusikia anaogopa na kutetemeka, unadhani tatizo ni wewe? Hapana tatizo lipo kwenye ufahamu wako ambao umeshaliwa kwa roho za uasherati na uzinzi uliokuwa ndani yako. Lakini unayo sasa nafasi ya kugeuka, na kuacha mambo hayo ili Bwana ayatengeneze upya maisha yako. Embu tufuatilie pamoja maonyo haya mafupi Sulemani aliyotupa yahusianayo na mambo haya haya ya zinaa naamini yataongeza kitu katika mienendo yetu sote. Tusome:
MITHALI: MLANGO 7
1 Mwanangu, yashike maneno yangu, Na kuziweka amri zangu akiba kwako.
2 Uzishike amri zangu ukaishi, Na sheria yangu kama mboni ya jicho lako.
3 Zifunge katika vidole vyako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.
4 Mwambie hekima, Wewe ndiwe umbu langu; MWITE UFAHAMU JAMAA YAKO MWANAMKE.
5 WAPATE KUKULINDA NA MALAYA, Na mgeni akubembelezaye kwa maneno yake.
6 Maana katika dirisha la nyumba yangu Nalichungulia katika shubaka yake;
7 Nikaona katikati ya WAJINGA, Nikamtambua miongoni mwa vijana, Kijana mmoja asiyekuwa na akili,
8 Akipita njiani karibu na pembe yake, Akiishika njia iendayo nyumbani kwake,
9 Wakati wa magharibi, wakati wa jioni, Usiku wa manane, gizani.
10 Na tazama, mwanamke akamkuta, Ana mavazi ya kikahaba, mwerevu wa moyo;
11 Ana kelele, na ukaidi; Miguu yake haikai nyumbani mwake.
12 Mara yu katika njia kuu, mara viwanjani, Naye huotea kwenye pembe za kila njia.
13 Basi akamshika, akambusu, Akamwambia kwa uso usio na haya,
14 Kwangu ziko sadaka za amani; Leo hivi nimeziondoa nadhiri zangu;
15 Ndiyo maana nikatoka nikulaki, Nikutafute uso wako kwa bidii, nami nimekuona.
16 Nimetandika kitanda changu, magodoro mazuri, Kwa matandiko ya Kimisri yenye mistari.
17 Nimetia kitanda changu manukato, Manemane na udi na mdalasini.
18 Haya, na tushibe upendo hata asubuhi, Tujifurahishe nafsi zetu kwa mahaba.
19 Maana mume wangu hayumo nyumbani, Amekwenda safari ya mbali;
20 Amechukua mfuko wa fedha mkononi; Atarudi wakati wa mwezi mpevu.
21 Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi, Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda.
22 Huyo akafuatana naye mara hiyo, Kama vile ng’ombe aendavyo machinjoni; Au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu;
23 Hata mshale umchome maini; Kama ndege aendaye haraka mtegoni; Wala hajui ya kuwa ni hasara ya nafsi yake.
24 Basi, wanangu, nisikilizeni sasa, Mkayaangalie maneno ya kinywa changu.
25 MOYO WAKO USIZIELEKEE NJIA ZAKE, WALA USIPOTEE KATIKA MAPITO YAKE.
26 Maana amewaangusha wengi waliojeruhi, NAAM, JUMLA YA WALIOUAWA NAYE NI JESHI KUBWA.
27 Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu, Hushuka mpaka vyumba vya mauti”.
Unaona? Zinaa ni kama vile mtu apelekwaje machinjoni, wala hajui kuwa ni kwa hasara ya nafsi yake mwenyewe,Na biblia inatuambia walionaswa katika mtego huu si watu wawili au watatu, bali ni jeshi kubwa sana.. Hivyo mimi na wewe tusiwe miongoni mwa hilo jeshi kubwa, tuikimbie zinaa kama biblia inavyotuambia, tumpe Roho Mtakatifu nafasi ya kuyatengeneza upya maisha yetu. Ni dhambi mbaya ambayo mtume Paulo aliitaja inafanyika juu ya mwili wa mtu.
Ikiwa bado hujampa Bwana maisha yako bado hujachelewa muda ndio huu, unachopaswa kufanya ni kutubu mwenyewe kutoka ndani ya moyo wako, kukusudia kwa kumaanisha kabisa kuwa hutaki kurudia njia hizo mbovu za mauti, hutaki kuwa tena mlevi, hutaki kufanya zinaa tena, hutaki kufanya mustarbation(punyeto) tena, hutaki kutazama pornography tena, hutaki kuvaa “mavazi ya kikahaba” kama huyo mwanamke anayezungumziwa na Sulemani na mavazi ya kikahaba yanayozungumziwa kwa sasa ni vimini, suruali kwa wanawake, migongo wazi na vitop, na sketi zinazobana ambavyo ni vichocheo vikubwa vya uasherati n.k. hutaki tena kutazama picha za utupu na pornography na mengine yote. Ikiwa kweli umeonyesha nia hiyo mbele za Mungu ya kutaka kuacha basi Mungu naye kuanzia huo wakati atakupa NGUVU ya kuweza kuvishinda hivyo vyote.
Na mwisho wa siku utashangaa ni rahisi kuacha, hata mimi nilikuwa mzinzi, mlevi, mtazamaji wa pornography na kila kitu kiovu lakini siku ile Neema ya Bwana iliponifikia, nilipotubu kwa kumaanisha kuacha , Uwezo huo wa ajabu ulikuja ndani yangu, mpaka sasa dhambi ya zinaa si kitu kwangu. Na vivyo hivyo na wewe ukiamua kugeuka, Bwana atakupa Uwezo huo, Hivyo fanya maamuzi sasa angali nafasi unayo. Na mara baada ya kutubu kwako jambo linalofuata ni kubatizwa, kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako,hivyo tafuta mahali popote wanapobatiza ubatizo sahihi wa kimaandiko, nao ni ule wa kuzamwishwa katika maji mengi na uwe kwa Jina la YESU KRISTO. Kama hujafahamu bado mahali pa kubatiziwa na unahitaji msaada wa kwa jambo hilo,unaweza kuwasiliana nami nitakuelekeza mahali karibu na wewe unaweza kupata hudumu hiyo ya kiroho.
Mwisho kabisa nikutakie mwanzo mema wa Mwaka huu, uwe wa mafanikio kwako ya kiroho na ya kimwili, na ya kukaa mbali na zinaa kwa jina la Bwana wetu YESU KRISTO.
Amen.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine na Mungu atakubariki
Mada Zinazoendana:
MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.
‘’MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI’’..NA NDIVYO ILIVYO KWA UASHERATI
NINI TOFAUTI KATI YA UZINZI NA UASHERATI ?
Moja ya sikuku saba ambazo Mungu aliwaagiza Wana wa Israeli wazishike ni SIKUKUU YA VIBANDA..Nyingne sita ni 1) Sikuku ya Pasaka,
2) Sikukuu ya Mikate isiyotiwa chachu,
3) Sikukuu ya Malimbuko ya Mavuno,
4) Sikukuu ya Majuma au Pentekoste
5) Sikukuu za kupiga Baragumu
6) Sikukuu ya siku ya Upatanisho na
7) Sikukuu ya Vibanda ndiyo ya Mwisho na ya saba.
Kila sikukuu ilikuwa na umuhimu wake na maana yake kubwa kimaandiko, Kwahiyo wana wa Israeli waliambiwa wazishike sikukuu hizi kwa faida zao wenyewe.Kumbuka sikukuu hizi hazikuwa kwa ajili ya kunywa na kula kama zinavyofanyika leo..Sikukuu hizi zilikuwa ni kwaajili ya kufanya sala na ibada tu! Na kukumbuka Mambo makuu ambayo Mungu aliwatendea walipotoka Misri na walipokuwa jangwani..na Mungu alionya siku hizo zifanywe kuwa takatifu daima.
Leo tutaitazama hii sikukuu ya mwisho inayojulikana kama sikukuu ya Vibanda na umuhimu wake kwa Wana wa Israeli na umuhimu wake kwetu sisi watu wa agano jipya.
Zamani wakati Mungu anawatoa Wana wa Israeli katika nchi ya utumwa Misri, aliwapitisha njia ya JANGWA ndefu ili kuwafundisha huko, kumbuka sio kwamba hapakuwa na njia ya mkato wa kufika nchi ya Ahadi, hapana ilikuwepo tena nzuri tu lakini Bwana aliamua kuwapitisha njia ya jangwa, iliyo ngumu, ili kuwanyeyekeza mioyo yao na kuwafundisha wamtegemee yeye kwa kila kitu, wamfahamu yeye kuwa sio Mungu tu wa mahali penye kijani bali pia ni Mungu wa jangwani, na kwamba mtu hataishi tu kwa vilimo, na katika milima mizuri yenye chemchemi, au katika fukwe nzuri zenye maji baridi, au katika nchi laini yenye udongo mzuri bali anaweza akaishi pia katika jangwa lisilokuwa na chakula, wala msimu wa mvua, wala maji wala upepo mwanana na bado akawa na afya nzuri, akawa na raha, na asichakae, asiugue endapo tu atatembea na Mungu..hilo ndilo somo Bwana alilokuwa anataka watoto wake wafahamu wakiwa kule jangwani.
Kumbukumbu 8: 1 “Amri hii ninayokuamuru leo mtaishika kuitenda, mpate kuishi na kuongezeka, na kuingia katika nchi ile ambayo Bwana aliwaapia baba zenu; nanyi mtaimiliki.
2 Nawe utaikumbuka njia ile yote Bwana, Mungu wako aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili
akutweze, kukujaribu kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo.
3 Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua;
APATE KUKUJULISHA YA KUWA MWANADAMU HAISHI KWA MKATE TU, BALI HUISHI KWA KILA LITOKALO KATIKA KINYWA CHA BWANA.
4 Mavazi yako hayakuchakaa, wala mguu wako haukuvimba, miaka hiyo arobaini.
5 Nawe fikiri moyoni mwakoya kuwa kama vile baba amrudivyo mwanawe, ndivyo Bwana, Mungu wako akurudivyo.
6 Nawe uzishike amri za Bwana, Mungu wako, upate kwenda katika njia zake, na kumcha”.
Sasa kule jangwani kama tunavyojua Jangwani hakuna misitu, wala makazi wala wafanya biashara wala chochote kile..walikuwa ni wao kama wao tu! hakukuwa na nyumba za kukaa hivyo suluhisho pekee la kutatua changamoto hiyo ilikuwa ni kwenda kutengeneza vibanda vidogo vidogo vitakavyowahifadhi wakiwa kule jangwani..vibanda hivyo walivitengeneza kiasi cha kwamba havikuwa vya kudumu..bali vya muda mfupi tu, kwasababu wao walikuwa ni watu wa kusafiri, leo wapo hapa kesho wapo kule..kwahiyo waliishi ndani ya hivyo vibanda kwa miaka 40, Na walipofika nchi ya Ahadi Bwana aliwaahidia hawatakaa tena katika vibanda kama walivyokuwa jangwani, wala hawatakula tena chakula cha aina moja (mana)..bali watakula vyakula vingi vya aina nyingi tofauti tofauti kwasababu hiyo nchi itawazalia yenyewe pindi watakapofika na pia watakaa kwenye majumba makubwa ambayo hata hawajayajenga wao, kadhalika mataifa yote yatawaogopa nao watakuwa watu wakufanikiwa sana.
Lakini kwasababu Bwana anaijua mioyo yao mbeleni, alijua watakapokula na kushiba watamsahau yeye, wataacha kuyashika maagizo yake, na kumsahau Mungu ambaye aliwapigania katika hali ngumu za jangwani, na kumsahau Mungu wao kuwa ndiye Mungu pekee aliyewasaidia wakati wa matatizo..Hivyo Bwana Mungu kwa kulifahamu hilo, aliwaagiza watakapoingia hiyo nchi ya ahadi kila mwaka wafanye sikukuu ya siku saba kuadhimisha jinsi Mungu alivyotembea nao jangwani.
Aliwaagiza kila mwisho wa Mwaka wa saba wa kalenda ya kiyahudi, watu wote watoke katika nyumba zao za kifahari wanazokaa…waende milimani wakachukua fito na matawi ya miti kila mtu akajenge kibanda kidogo pembezoni mwa nyumba yake kama vile walivyotengeneza walipokuwa kule jangwani..kila mtu au familia akalale ndani ya hicho kibanda ndani ya siku saba..wakumbuke Uweza wa Mungu na matendo yake aliyowatendea jangwani miaka 40, kwamba walikaa ndani ya vibanda na walikuwa wanalishwa na kunyweshwa ndani ya lile jangwa nene kimiujiza, na wala walikuwa hawaugui wala mavazi yao kuchakaa.
Kwahiyo sheria hiyo Mungu aliiagiza ifanyike kwa vizazi vyote..Kwamba kila mwaka mwezi wa saba ni lazima ishikwe..kumbuka haikuwa sherehe ya kula na kunywa, wala watu walikuwa hawaendi kwenye kumbi za starehe kusheherekea..ilikuwa ni sherehe ya kumwimbia Mungu,kumsifu na kukaa katika vyumba vya ndani katika uwepo wake na kutafakari kwa muda mrefu matendo yake makuu. Ulikuwa ni wakati wa kuisoma torati yote upya na kujikumbusha mambo yaliyoandikwa kule, na pia ulikuwa ni wakati wa kuwafundisha watoto wale waliozaliwa hivi karibuni sheria za Bwana na torati. Hiyo ndiyo tafsiri ya sikukuu mbele za Mungu. Tunasoma:
Kumbukumbu 31: 10 “Musa, akawaamuru, akasema, Mwisho wa kila mwaka wa saba, wakati wa maachilio, WAKATI ULIOAMRIWA WA SIKUKUU YA VIBANDA,
11 Israeli wote wafikapo ili kuonekana mbele za Bwana, Mungu wako, mahali pale atakapopachagua, uisome torati hii mbele ya Israeli wote masikioni mwao.
12 Wakusanye watu, wanaume na wanawake na watoto, na mgeni wako aliyemo malangoni mwako wapate kusikia na kujifunza, na kumcha Bwana, Mungu wenu, na kuangalia kutenda maneno yote ya torati hii;
13 na watoto wao wasiojua, wapate kusikia na kujifunza kumcha Bwana, Mungu wenu, siku zote mtakazokaa katika nchi mnayoivukia Yordani ili kuimiliki”.
Nehemia 8: 14 “Wakaona ya kuwa imeandikwa katika torati, jinsi Bwana alivyoamuru kwa mkono wa Musa, ya kwamba wana wa Israeli WAKAE KATIKA VIBANDA, katika sikukuu ya mwezi wa saba;
15 na ya kwamba wahubiri na kutangaza katika miji yao yote, na katika Yerusalemu, kusema, Enendeni mlimani, mkalete matawi ya mzeituni, na matawi ya mzeituni-mwitu, na matawi ya mihadasi, na matawi ya mitende, na matawi ya miti minene, ili kufanya vibanda, kama ilivyoandikwa.
16 Basi watu wote wakatoka, wakayaleta, wakajifanyizia vibanda, kila mtu juu ya dari ya nyumba yake, na katika nyua zao, na katika nyua za nyumba ya Mungu, na katika uwanja wa lango la maji, na katika uwanja wa lango la Efraimu.
17 Na mkutano wote wa watu, waliorudi kutoka nchi ya uhamisho wao, wakafanyiza vibanda, wakakaa katika vibanda hivyo; maana tokea siku za Yoshua, mwana wa Nuni, hata siku ile, wana wa Israeli hawakufanya hivyo. Pakawa na furaha kubwa sana.
18 Tena siku baada ya siku, tangu siku ya kwanza hata siku ya mwisho, akasoma katika kitabu cha torati ya Mungu. Wakafanya sikukuu muda wa siku saba; na siku ya nane palikuwa na kusanyiko la makini, kama ilivyoagizwa”.
Sasa mambo haya ni kivuli cha mambo yaliyopo sasahivi, kwasababu agano la kale ni kivuli cha agano jipya, mambo yaliyokuwa yanafanyika agano la kale kwa namna ya mwilini yanafanyika leo katika agano jipya kwa namna ya roho. Kama Bwana alivyowatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya utumwa Misri, na sisi pia Bwana ametutoa katika nchi ya utumwa wa dhambi, na kama vile wana wa Israeli walivyobatizwa wote katika Bahari ya Shamu (1 Wakoritho 10:2) na kuwa huru na majeshi ya kimisri kikabisa kabisa na sisi pia kupitia ubatizo wa maji mengi kwa jina la Yesu tunawekwa huru mbali na dhambi kikabisa kabisa.
Na kama wana wa Israeli walivyofundishwa katika jangwa zito, na sisi pia Bwana ametupitisha katika majaribu mbali mbali kuijaribu imani yetu, na kama tutakuwa waaminifu Basi Bwana atatuingiza katika kaanani yake ya rohoni ambayo ni mbingu mpya na nchi mpya..Lakini kabla hajatuingiza katika hiyo Kaanani ya milele mahali pasipo kuwa na tabu wala shida..atatuingiza pia katika Kaanani ya miili yetu hii. Atatupa mara mia katika ulimwengu huu kama alivyoahidi katika Neno lake.
Na atakapokuingiza katika hiyo nchi, Ni wajibu wako kumfanyia Mungu sikukuu ndani ya moyo wako..Tenga siku, au wiki, au mwezi..funga yatafakari mambo yote makuu Mungu aliyokutendea wakati upo katika madarasa ya Mungu, Kipindi hauna chochote lakini Bwana anakupigania..kipindi unaumwa na huna msaada lakini Bwana anakuponya..kipindi ambacho ungestahili kufa kwenye lile jangwa la mateso lakini hukufa, kipindi ambacho ulipitia kila aina ya jaribu lakini Bwana hakukuacha..Zikumbuke hizo siku usizisahau, ibada ya kumbukumbu ya hizo siku ndiyo SIKUKUU INAYOMPENDEZA MUNGU.
Inayofananishwa na SIKU KUU YA VIBANDA, Unapozitafakari hizo siku, inakusaidia kutozisahau fadhili za Mungu alizokutendea nyuma, na hivyo siku zote unajikuta unaishi katika mstari wa Mungu…Kama wana wa Israeli ilikuwa ni amri kuishika sikukuu ya Bwana na sisi pia ni amri kukumbuka fadhili za Mungu na kuzitafakari siku zote za maisha yetu.
Kumbuka mema yote Mungu aliyokufanyia nyuma kwa kumfanyia ibada ya shukrani naye Mungu atakuangazia rehema zake daima.
Bwana akubariki sana, tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Zinazoendana:
SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?
Udhihirisho wa Bwana Yesu kabla ya kufufuka, ulikuwa ni tofauti na baada ya kufufuka..Kabla ya kusulibiwa Bwana Yesu alikuwa anaonekana kila mahali na sehemu nyingi, hata watu waliotaka kumwona na kumfahamu, walikuwa wakimtafuta kwa bidii wanampata mahali popote..Alifanya huduma yake kwa wazi sana..Lakini haikuwa hivyo tena baada ya kufufuka kwake. Baada ya kufufuka kutoka katika wafu, hakuwa anajidhihirisha kwa kila mtu, isipokuwa kwa watu wachache sana, tena,sana sana wale wanafunzi wake…Wengine wote waliosalia ambao walikuwa hawafuatani naye wala hawajishughulishi na mambo yake, walibakia kuamini uongo kwamba Bwana hajafufuka ameibiwa na wanafunzi wake usiku, na kuzusha kwamba amefufuka.
Kwahiyo waliokuwa wana uhakika kwamba Bwana Yesu kafufuka kweli kweli ni wale wanafunzi wake tu, na ndugu zake Bwana pamoja na kikundi cha watu wachache sana waliokuwa wanafuatana naye, mamilioni ya watu waliokuwa pale Yerusalemu hawakujua chochote..Na siku ya unyakuo itakuwa hivyo hivyo watakaomwona Kristo mawinguni watakuwa wachache sana kati ya mabilioni ya watu wanaoishi duniani.
Wakati hata ule mti ambao ulimsulibishia Bwana haujaoza, Tayari Bwana alikuwa anazungumza na wanafunzi wake katika vyumba vya ndani vya siri. Wakati ambao bado watu walikuwa wanamwombolezea tayari yeye ameshawatokea wengi na kuzungumza nao.
Wakati Pilato, Herode,mafarisayo, masadukayo pamoja na wayahudi wamestarehe wakisheherekea na kudhani Bwana sasa ni marehemu, kumbe maili kadhaa tu hapo,si mbali na wao Bwana anawaaga wanafunzi wake na kuchukuliwa juu mbinguni..
Matendo 1: 4 “Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu;
5 ya kwamba Yohana alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache.
6 Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme?
7 Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.
8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
9 Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao.
10 Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe,
11 wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.
12 Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato”.
Kwahiyo tunaweza tukaona kujidhihirisha kwa Bwana baada ya kufufuka kulikuwa ni kwa siri sana, sio wote waliokuwa wanajua kinachoendelea wakati ule.
Lakini jambo la kipekee tunaloweza kujifunza ni kwamba, Wakati Bwana anachukuliwa juu katika wingu..wale wanafunzi walikuwa wanamtazama kwa macho yao jinsi alivyokuwa anaondoka hatua kwa hatua..jinsi wingu lilivyomchukua mpaka kupotelea mawinguni…Lakini tunaona baada ya kudumu kwa muda mrefu wakiangalia mawinguni malaika wawili waliwatokea katikati yao na kuwahamisha akili zao wasibaki kuangalia mbinguni, kwa maana Kwa jinsi hiyo hiyo aliyoondokea ndio atakayorudia..hivyo waache kuangalia juu, wakaendelee na mambo mengine yanayohusiana na kuutangaza ufalme wa mbinguni..Mpaka wakati wa Bwana kurudi, wakawe mashahidi wa Yesu Kristo, wakiutangaza ufalme wa mbinguni kwa watu wengine.
Kwa wakati huo ulikuwa ndio ule wakati Bwana Yesu aliowaambia mafarisayo kwamba utafika wakati Bwana arusi ataondolewa na ndipo wanafunzi wake watafunga na kuomboleza.
Mathayo 9: 14 “Wakati ule wanafunzi wake Yohana wakamwendea, wakasema, Kwa nini sisi na Mafarisayo twafunga, bali wanafunzi wako hawafungi?
15 Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kuomboleza, muda bwana arusi akiwapo pamoja nao? Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana arusi; ndipo watakapofunga”.
Siku zote upo wakati ambao Bwana atatembea na Mtu, kama mtu na rafiki yake au mpenzi wake, na upo wakati ambao Bwana atatembea na mtu kama mtu na mtumwa wake..wakati huo Bwana ataondoka juu, na kukutuma kama mfanya kazi katika shamba lake.
Utakuwa ni wakati wa Bwana kugeuza hisia zako, na kukusukuma kwenda kuzaa matunda zaidi badala ya kukaa mwenyewe mwenyewe tu!..
Nakumbuka kipindi cha kwanza kwanza nampa Bwana maisha yangu, nilikuwa sitamani kitu kingine chochote zaidi ya kuondoka kwenye hii dunia na kwenda kwa Baba..Nilikuwa natamani leo Kristo arudi niondoke..(sio kwamba hata sasa bado sikitamani,nakitamani hicho kitu sana) na nilikuwa namwona Bwana akinifariji kwa namna ya kipekee kwa njia hiyo, nilikuwa naona maono, na ishara baadhi kuthibitisha njia hiyo..Lakini ilifika wakati mambo yalibadilika ndani…
Nilianza kuhisi kuna majukumu Fulani nayakwepa, Nilianza kusikia msukumo mwingine tofauti na ule wa kwanza, badala ya kukaa peke yangu na kujifunza tu Neno, na kusikiliza tu mahubiri na kusoma vitabu..huku nikitamani siku yoyote parapanda ilie niondoke…Nilianza kuhisi kuna umuhimu wa kwenda kusambaza habari za Yesu Kristo kwa watu wengine..Jambo hilo lilikuja ndani kwa nguvu sana kwa muda mrefu kidogo..mpaka ikafika wakati siku ikipita pasipo kufanya chochote katika kuisambaza kazi ya Mungu, nakosa amani, hata nguvu za mwili naona zinapungua kabisa..Kwahiyo nikahama kutoka kutazama tu mbinguni na kuanza kazi nyingine ya kuhubiri, ndio angalau unafuu ndani ya nafsi ukarudi.
Kwahiyo ikawa nikiona tu ndani amani imetoweka najua sehemu ya kwenda kuirudisha.. “ni kwenda kuwahubiria wengine habari njema”..amani inarudi kama kawaida na siku yangu inaenda vizuri, tofauti na hapo kwanza ambapo hata nisipofanya hivyo..nikisoma tu Neno na kusikiliza mahubiri na kusali basi Napata amani.
Nimetoa ushuhuda huu mfupi tu wa mimi binafsi kuonyesha kwamba kuna nyakati na majira, kuna wakati wa kukaa na Bwana arusi (Yesu Kristo) na kuna wakati wa Bwana arusi kuondolewa.. Waliooa au walioolewa wanafahamu kuwa kuna wakati wa mume na mke kukaa pamoja kwa raha na furaha, wakiwa wawili tu..na kuna wakati wa majukumu, wakati ambao watoto wamezaliwa wanahitajika kutunzwa, wakati huo upendo lazima ugawanyike kidogo, sehemu Fulani lazima uelekee katika kuwatunza watoto. Upendo unahamia kwa watoto.
Na katika Ukristo nako ni hivyo hivyo, upo wakati wa kufurahi na Bwana, kipindi cha mwanzo cha wokovu lakini pia upo wakati wa kwenda kuzaa matunda, kipindi ambacho Bwana arusi ataondolewa..wakati ambao unalazimika kujihusisha na watoto wa kiroho zaidi, kuliko kitu kingine zaidi…Kama ilivyokuwa kwa wanafunzi, walikaa na Bwana miaka mitatu na nusu kwa raha…na siku Bwana anaondoka walidhani wataendelea kutembea naye na kula naye kama hapo kwanza..walimwuliza Bwana huu ndio wakati wa kurejeshewa ufalme (Yaani wakati wa kutawala na Bwana wao kwa raha na furaha pasipo usumbufu)..Lakini Bwana aliwaambia huo ni wakati wa kupokea nguvu kuwa mashuhuda wake, na kupeleka injili duniani kote na kuleta mazao mengi katika ufalme wa mbinguni…huo sio wakati wa kustarehe tena, ni wakati wa kufunga,na kuombeleza, ni wakati wa kupambana vita.
Kwa kupitia ujumbe huu mfupi, naamini utakuwa umeongeza kitu katika vile Bwana alivyokujalia kuvijua, ni maombi yangu kuwa Bwana atakusaidia Katika hilo, utapofikia katika hiyo hatua au kama upo katika hiyo hatua Bwana akufanikishe sana na azidi kukutia nguvu katika kuifanya kazi yake.
Kama hujampa Bwana maisha yako, nakushauri ufanye hivyo leo, kabla mlango wa Neema haujafungwa, kwa Kristo atakuja na wala hatudanganyi..Yeye anatupenda ndio maana amejitoa maisha yake kwa ajili yako na yangu.Hivyo mgeukie leo ukatubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, na yeye atakupokea kama alivyoahidi, na pia haraka tafuta mahali ukabatizwe ikiwa haukubatizwa ipasavyo, ili upate ondoleo la dhambi zako, na utakuwa na uhakika wa Uzima wa milele na kuiona Mbingu.
Bwana akubariki, Tafadhali “share” Ujumbe huu kwa wengine,
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Zinazoendana:
MUNGU KUSEMA NA WEWE PEKEE, HAITOSHI KUKUPA USHINDI.
NINI MAANA YA KUHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE?
Siku hiyo itakuwa ni siku ya namna gani?, Siku hiyo ya watakatifu wote kunyakuliwa, siku hiyo ambayo itakuwa ni mwisho wa taabu zote kwa wana wa Mungu..Siku ambayo tutakutana na YESU uso kwa uso, siku ambayo Bwana atakapokwenda kuweka wazi mambo yake yote aliyokuwa ametuandalia tangu zamani , makao yetu ya milele, Biblia inasema ni mambo ambayo hata malaika watakatifu wanatamani kuyachulingulia wayaone yakoje..
Ni kama tu vile na sisi tulivyo na shauku ya kuona walau kwa uchache jinsi mbingu ilivyo, kwani tumekuwa tukiisikia uzuri wake usio wa kawaida tangu zamani jinsi ulivyo lakini tusiuone, Na kwa namna hiyo hiyo malaika nao sasa huko juu mbinguni, wanatamani kwa shauku kubwa walau waonjeshwe mambo walioandaliwa wateule wa Mungu na YESU KRISTO mwenyewe siku ile itakavyokuwa. Huko walipo Malaika watakatifu wanasikia tu! kuwa kuna utukufu mkubwa Bwana amewaandalia watakatifu wake, wanafahamu kuwa ni utukufu ulio mkuu sana usioneneka. lakini bado hawajauona ni wa namna gani, wanajua kuwa siku ya ukombozi wa watoto wa Mungu ni siku KUU sana, mambo yasiyoneneka wala kutamkika yatafunuliwa katika siku hizo, hivyo hiyo inawafanya wao nao waitamani siku hiyo ije kwa haraka wao nao wayashuhudie mambo hayo ya ajabu.
1Wakorintho 2:9 “Lakini, kama ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao”.
Na Sio malaika tu peke yao, hata viumbe vingine vyote vinaitamani hiyo siku ifike, Mtume Paulo anasema ..
Warumi 8:18 “Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu kama UTUKUFU ULE UTAKAOFUNULIWA KWETU.
19 Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia KWA SHAUKU NYINGI kufunuliwa kwa wana wa Mungu.
20 Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili; si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye atiyevitiisha katika tumaini;
21 kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu”.
Kwasasa hatuwezi kusema mengi kwasababu bado hatujafunuliwa mambo yenyewe lakini tunafahamu sifa moja ya Mungu KUWA YEYE HUWA HASEMI UONGO, na kama alivyosema “ kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu”..Alimaanisha kuwa tunaweza kuchukulia hivyo vitu kwa upeo wetu wa kibinadamu kiwepesi wepesi lakini siku tutakapokuja kuyaona hayo mambo ndipo tutakapojua kweli mawazo yake yalikuwa mbali sana na sisi tulivyokuwa kufikiri.
Siku hiyo sisi tutakapoondoka hapa duniani, haitakuwa heri kwetu tu sisi na viumbe vyote, bali itakuwa heri pia kwa Malaika wote walioko mbinguni. Kutakuwa na shangwe na furaha isiyoneneka.
Hivyo ndugu tukikaa na kuyatafakari hayo kwa utulivu, basi hatutajali ni mambo mangapi yatapita mbele yetu mabaya, sisi siku zote tutaelekeza macho yetu mbinguni, hatutajali ulimwengu unasemaje, sisi tutamtazama mwokozi wetu YESU KRISTO daima, huku tukingojea kwa saburi yale Mungu aliyoutandalia, tutaishi kama wapitaji na wasafiri tu hapa duniani.
1Petro 1:9-16
“9 KATIKA KUUPOKEA MWISHO WA IMANI YENU, YAANI, WOKOVU WA ROHO ZENU.
10 Katika habari ya wokovu huo manabii walitafuta-tafuta na kuchunguza-chunguza, ambao walitabiri habari za neema itakayowafikia ninyi.
11 Wakatafuta ni wakati upi, na wakati wa namna gani ulioonywa na Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, ambaye alitangulia kuyashuhudia mateso yatakayompata Kristo, NA UTUKUFU UTAKAOKUWAKO BAADA YA HAYO.
12 Wakafunuliwa ya kuwa si kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yenu walihudumu katika mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiri ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. MAMBO HAYO MALAIKA WANATAMANI KUYACHUNGULIA.
13 Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo.
14 Kama watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu;
15 bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;
16 kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
Tukaze mwendo, ikiwa maisha yako sasa yapo mbali na Kristo, huu ni wakati wa kumrudia yeye maadamu mlango wa neema bado upo wazi, kumbuka siku ile ukijikuta umeachwa majuto hayatakuwa kwasababu unakwenda Jehanum, hapana majuto makubwa yatakujia kwasababu umekosa mambo mazuri ya umilele Mungu aliokuwa amewaandalia watoto wake tangu zamani.
Hivyo tubu kabisa kwa kudhamiria kuanza maisha mapya katika Bwana, na haraka bila kukawia nenda ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa kwenye maji tele, na kwa Jina la YESU KRISTO..Ili upate ondoleo la dhambi zao kulingana na Matendo 2:38., kisha Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu kama alivyoahidi, na kuanzia hapo nawe utakuwa umeingizwa na kuwa mmojawapo wa waliostahili kuuona huo utukufu ambao utakuja kufunuliwa siku za hivi karibuni. Tunaishi katika siku za mwisho Zidi kudumu katika utakatifu, na ushirika na kusali daima.
Bwana akubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali “share” Ujumbe huu kwa wengine.
Mada Zinazoendana:
VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA
Ufunuo 16:15 “ (Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.)”
Umewahi kujiuliza kwanini Bwana Yesu sehemu nyingi ujio wake anaufananisha na mwizi. Kwanini Bwana anajifananisha na wezi na sio watu watakatifu.. Tunafahamu wizi sio kitu kizuri, na moja ya Amri za Mungu ni “USIIBE”. Lakini hapa tunaona Bwana anajifananisha na mwizi. Kwanini anafanya hivyo?.
Ni wazi kuwa kuna hekima tunaweza kuiona hata katika waovu..Ndio maana Bwana alisema mahali pengine tuwe na “Busara kama nyoka”..Nyoka sio kiumbe chenye ishara nzuri, kuanzia Edeni mpaka sasa, shetani alikitumia kupenyeza dhambi ulimwenguni.. Lakini Bwana alituambia tuwe na Busara kama nyoka…Na zaidi ya yote yeye mwenyewe Bwana anajifananisha na Yule nyoka wa shaba Musa aliomnyanyua kule jangwani.
Yohana 3: 14 “Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa;
15 ili kila mtu aaminiye awe na uzima wa milele katika yeye”.
Na sehemu nyingine tena Bwana anajifananisha na yule Kadhi dhalimu:
Luka 18: 1 “Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.
2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.
3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.
4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,
5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.
6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.
7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?
8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?”
Tena Sehemu nyingine Bwana anatufundisha kupitia mfano wa WAKILI DHALIMU aliyekuwa mwizi wa mali za Bwana wake na mwisho akatenda kwa Busara, Bwana akasema nasi pia tujifanyie rafiki kwa mali ya udhalimu ili itakapokosekana watukaribishe kwenye makao ya milele.
Luka 16: 1 “Tena, aliwaambia wanafunzi wake, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyekuwa na wakili wake; huyu alishitakiwa kwake kuwa anatapanya mali zake.
2 Akamwita, akamwambia, Ni habari gani hii ninayosikia juu yako? Toa hesabu ya uwakili wako, kwa kuwa huwezi kuwa wakili tena.
3 Yule wakili akasema moyoni mwake, Nifanyeje? Maana, bwana wangu ananiondolea uwakili. Kulima, siwezi; kuomba, naona haya.
4 Najua nitakalotenda, ili nitakapotolewa katika uwakili, wanikaribishe nyumbani mwao.
5 Akawaita wadeni wa bwana wake, kila mmoja; akamwambia wa kwanza, Wawiwani na bwana wangu?
6 Akasema, Vipimo mia vya mafuta. Akamwambia, Twaa hati yako, keti upesi, andika hamsini.
7 Kisha akamwambia mwingine, Na wewe wawiwani? Akasema, Makanda mia ya ngano. Akamwambia, Twaa hati yako, andika themanini.
8 Yule bwana akamsifu wakili dhalimu kwa vile alivyotenda kwa busara; kwa kuwa wana wa ulimwengu huu katika kizazi chao wenyewe huwa na busara kuliko wana wa nuru.
9 Nami nawaambia, Jifanyieni rafiki kwa mali ya udhalimu, ili itakapokosekana wawakaribishe katika makao ya milele”.
Sehemu zote hizo Bwana hatumii watu wazuri au watakatifu kutufundisha Bali anatumia watu waovu, sio kwamba anataka tujifunze uovu wao, au tuige tabia zao hapana bali anataka tujifunze hekima yao. Kwasababu wana wa ulimwengu huu (wasiomjua Mungu biblia inasema wana hekima katika mambo yao).
Sasa tukirudi kwenye ule mfano wa Mwivi Bwana alioutuoa na kusema “Tazama naja kama mwivi”…Tunajua mwivi sio mtu mzuri, anakuja kwa lengo la kuiba…Lakini busara ya mwivi siku zote hapendi kusumbuliwa wala hapendi kumsumbua Yule anayemwibia..atafanya mambo yake kimya na taratibu na akishaiba anakwenda zake..Kwasababu hiyo basi anasubiria watu wakati wamelala na wamechoka usiku wa manane ndio anakuja na kuingia ndani na kuiba kisha kuondoka…Anakuja wakati ambao mali anayoitafuta na mwenye mali wamejitenga vizuri kabisa, anakuja wakati ambao nafasi ya matengano ni kati ya mali na mwenye mali ni kubwa sana..Hiyo ni hekima ya hali ya juu.
Na ndio Bwana Yesu naye ataitumia hekima hiyo hiyo wakati wa kuja kulichukua kanisa lake..atakachofanya kwanza ni kuja wakati ambao magugu na ngano vimeshajitenga..wakati ambao ulimwengu umelala usingizi na kumsahau Mungu, wakati ambao watakatifu wametengwa na ulimwengu wote, wakati ambao watakatifu wanaonekana ni watu wasiokuwa na maana, ulimwengu umewachoka, ulimwengu umeacha kuthamini mambo ya muhimu yahusuyo roho zao, Huo ndio wakati Bwana Yesu anakuja kuwaiba watu wake kutoka ulimwenguni.
Kama vile mwizi anapokuja, huwa anakuja wakati ambao watu hawaangalii tena tv zao ndani wamezichoka, wakati ambao watu hawatumii tena magari yao ya thamani wameyaacha yapumzike..wakati ambao simu zao za mikononi wamechoka kuzitumia n.k Huo ndio wakati mwizi anakuja kuzichukua.
Mteule wa Mungu hizi nyakati ni za hatari, nyakati ambazo ulimwengu haumtaki tena Kristo..Wakati ambao Watakatifu wanaonekana hawana thamani tena ulimwenguni, wakati ambao watakatifu wamechokwa na watu wa ulimwengu huu, ujue ni wakati wa matenganisho..vitu vya thamani vimechokwa kutumiwa, huo ndio wakati mwivi anakuja..wakati ambao usingizi wa anasa, na uasherati na ulevi umewavaa wengi huo ndio wakati Kristo anapoivamia nyumba.
Na siku ya kuwanyakuwa watu wake hakuna mtu atakayejua siku hiyo..baada ya kipindi Fulani kupita ndipo hapo watakapojua kuwa kuna baadhi ya watu hawapo? Watu wetu wa muhimu na wa thamani waliokuwa wanatuhubiria habari njema za maisha ya umilele na utakatifu wametoweka.
Na kama vile mtu anavyopata uchungu wa kuibiwa mali yake ya thamani..ndivyo watu wengi siku hiyo watakavyopata uchungu wa kuachwa ulimwenguni na wapendwa wao wa thamani..watazidi kupata uchungu mwingi watakapoanza kupitia dhiki ya mpinga kristo na siku ya BWANA inayotisha. Watalia na kujuta na kuomboleza.. Kumbuka kitakachowaumiza sana sio mapigo yale bali ni “kwanini hawakukesha”..hicho ndicho kitakachowaumiza sana.. Ni kwanini wenzao wameondoka na wao wamebaki?? Na kwamba wenzao wapo utukufuni mbinguni milele na wao wataenda kwenye lile ziwa la moto, watasikia wivu uliochanganyikana na hasira mbaya sana.. Uchungu huo unafananishwa na uchungu wa mtu KUIBIWA MALI YAKE USIKU, na siku hiyo watu wote walioachwa watamchukia Bwana Yesu kuliko hapo kwanza. Watamchukia kwa ukomo wa chuki, Kama vile watu wanavyowachukia wezi baada ya kuibiwa. Watamkufuru na kumtukana, na dhiki watakazopitia zitaongeza hasira yao.
Ufunuo 16: 8 “Na huyo wa nne akakimimina kitasa chake juu ya jua, nalo likapewa kuwaunguza wanadamu kwa moto.
9 Wanadamu wakaunguzwa maunguzo makubwa, NAO WAKALITUKANA JINA LA MUNGU ALIYE NA MAMLAKA JUU YA MAPIGO HAYO; WALA HAWAKUTUBU WALA KUMPA UTUKUFU.
10 Na huyo wa tano akakimimina kitasa chake juu ya kiti cha enzi cha yule mnyama; ufalme wake ukatiwa giza; wakatafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu,
11 WAKAMTUKANA MUNGU WA MBINGU KWA SABABU YA MAUMIVU YAO, NA KWA SABABU YA MAJIPU YAO; WALA HAWAKUYATUBIA MATENDO YAO”.
Watu wengi wanasema kutakuwa na nafasi ya kutubu wakati huo?? Ndugu yangu, ndugu yangu nataka nikuambie huo ni uongo wa shetani, siku hiyo hakutakuwa na nafasi ya kutubu. Utakuwa ni wakati wa maombolezo na vilio na hasira na uchungu..Wanadamu wote walioachwa watataka kufanya vita na mwanakondoo, watamchukia Yesu Kristo..
Kama ulishawahi kuibiwa unaweza ukaulewa uchungu wa kuibiwa..ni mbaya sana, wengi wasiomjua Mungu wanaishia kuwachukia wezi maisha yao yote… Ndio maana Bwana naye anatuonya kwasababu anauona UCHUNGU utakaokuja huko mbeleni kwa wanadamu wote watakaoachwa..anatuonya na kutuambia “KESHENI” naja upesi.
Luka 21:34 “ Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo;
35 kwa kuwa ndivyo ITAKAVYOWAJILIA WATU WOTE WAKAAO JUU YA USO WA DUNIA NZIMA.
36 BASI, KESHENI NINYI KILA WAKATI, mkiomba, ili mpate kuokoka katika haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
Mathayo 24: 42 “Kesheni basi; kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu.
43 Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
44 Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja”.
Kukesha hapo sio kukesha kwa mwili kutojizuia kulala, hapana bali ni kukesha katika roho,kwa kuishi maisha ya uangalifu, na utakatifu, kuishi kwa kuzisoma nyakati na kuyaelewa majira tunayoishi, kuishi kwa kuweka kando uasherati, ulevi, anasa, mavazi yasiyompendeza Mungu, matusi, rushwa, na mambo yote mabaya na kudumu katika kujifunza Neno la Mungu kila wakati. Hiyo ndio maana ya kukesha. Siku zinakuja hizi ni za hatari sana, tuwe macho wapendwa.
Maneno ya Mungu yaliyofunga kitabu cha biblia ni maneno ya Bwana Yesu na maneno hayo aliyoyasema ni haya..
Ufunuo 22:20 “Yeye mwenye kuyashuhudia haya asema, Naam; naja upesi. Amina; na uje, Bwana Yesu.
21 Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi nyote. Amina.”
Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine, BWANA akubariki sana.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Zinazoendana:
LUKA 12:20 INASEMA “USIKU HUU WA LEO WANATAKA ROHO YAKO!” NI WAKINA NANI HAWA WANAOITAKA ROHO YAKE?
NINI MAANA YA KUISHI KWA KUUKOMBOA WAKATI?.
Tukisoma kitabu cha Mwanzo biblia inatuambia “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi”, pia tukirudi kusoma tena maandiko biblia inatuambie vile vile “Mungu ni Roho” (Yohana 4:24), Hivyo katika mstari huo ni sawa na kusema hapo mwanzo “Roho wa Mungu aliziumba mbingu na nchi, 2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.”..
Kwahiyo hapo tunaona Roho wa Mungu alifanya kazi mara mbili, katika utengenezaji wa ulimwengu. ya kwanza ni kuumba mbingu na nchi, na ya pili ni kuja kuitengeneza tena nchi ili kutimiza lengo Fulani ambalo amelikusudia, na lengo hilo si lingine zaidi ya kuifanya nchi IZAE, isibaki tena katika hali ya ukiwa. Ipo sababu kwa nini Mungu aliacha nafasi kati ya kuumbwa kwa dunia baada ya kukaa katika ukiwa wa muda mrefu na kuja kutengenezwa tena Ipo sababu.
Lakini Mungu kutujuza hayo kwa ufupi ni kutufundisha kanuni zake utendaji kazi. Na kanuni hiyo hiyo Mungu anaitumia kwa mtu yeyote anayempa Kristo maisha yake leo.
Jambo la kwanza pale mtu anadhamiria kwa dhati kabisa kutoka moyoni mwake kumpa Kristo maisha yake, kwa kutubu na kuacha dhambi zake zote, na kwenda kubatizwa katika ubatizo ulio sahihi wa kimaandiko, basi mtu huyo anakuwa ni sawa kaumbwa kwa mara ya kwanza, Roho wa Mungu anakuwa amefanya kazi yake ya kumuumba na kuwa kitu halisi kinachoonekana,. Mtu kama huyo anakuwa ameshatiwa muhuri na Roho Mtakatifu kuwa ni milki halali ya Mungu. Ni kazi ya Mungu iliyo tayari kwa matumizi yake. Lakini hawi kitu kilichokamilika mbele zake, anakuwa anafananishwa na nchi iliyokuwa imeumbwa na Roho Mtakatifu ambayo ipo katika hali ya ukiwa.
Sasa ile hatua ya pili ambayo Roho wa Mungu anatua mwenyewe juu ya nchi ya kuifanya kuwa nchi izaayo, ni jambo lingine ambalo hilo lilichukua muda kidogo tofauti na lile la kwanza la uumbaji. Hali hiyo hiyo inakuwa pia na kwa mtu aliyezaliwa mara ya pili leo.Kumbuka kama biblia inavyosema Roho Mtakatifu ni ahadi kwa wale wote watakaomjia na kumpokea:
Matendo 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 KWA KUWA AHADI HII NI KWA AJILI YENU, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.
Hii ikiwa na maana kuwa mtu yeyote yule pindi tu anapompokea Yesu Kristo kwa kudhamiria kabisa kuacha maisha yake ya dhambi na kutaka kumwishia yeye basi siku hiyo hiyo Roho wa Mungu anaingia ndani yake kuyageuza maisha yake na kumfanya kuwa kiumbe kipya, hii haichukui nguvu, wala muda, ni jambo la kudhamiria na kuzingatia maagizo yote yanayoambatana na kuamini kwako. lakini hiyo haimaanishi kuwa Roho wa Mungu atatua juu ya mtu kama huyo siku hiyo hiyo aliyoamini.. Hilo ni jambo lingine.
Ukisoma biblia utaona Bwana wetu Yesu Kristo yeye alijazwa Roho Mtakatifu tangu alipokuwa tumboni mwa mama yake, lakini Roho Mtakatifu hakuwa juu yake tangu akiwa tumboni mwa mama yake, isipokuwa alipofikisha umri wa miaka 30, na ndivyo ilivyokuwa kwa Yohana Mbatizaji, yeye pia alijazwa Roho tangu akiwa tumboni mwa mama yake lakini Roho Alimfuata nyikani miaka mingi baadaye.. Vivyo hivyo na mitume wote wa Yesu Kristo, pale Bwana alipowachagua, siku ile wote walipochukua uamuzi wa kumfuata Bwana na kuacha mambo yao yote maovu na njia zao, na kazi zao, na familia zao kwa ajili ya Bwana, na kubatizwa walipokea Roho Mtakatifu ndani yao, ndiye aliyewapa uwezo wa kustahimili mambo yote kwa kipindi chote walichokuwa wanakipitia na Bwana. Lakini Roho Mtakatifu kuja juu yao haikuwa siku ile ile ni kitendo kilichowachukua muda wa miaka mitatu na nusu baadaye..
Kwasababu Kitendo cha Roho wa Mungu kutua juu ya mtu, ni lazima kwanza mtu ajue ni kwasababu gani Roho huyo aje juu yake, kwahiyo hakiji kiuwepesi kama kile cha kwanza cha kufanywa kuwa kiumbe kipya, bali hichi kinakuja kwa makusudi maalumu, hivyo yule atakaye kipokea ni sharti kwanza ayatambue makusudi hayo ni yapi na ndio hapo itamgharimu mtu apitie huyo hata madarasa Fulani fulani, ya kutosha pamoja na kuomba sana bila kukata tamaa kwa ajili ya Roho.
Na makusudi hayo tunayaona ndio kama yale Roho Mtakatifu alivyotua tena juu ya nchi tena, nayo si mengine zaidi ya kuifanya nchi IZAE na iwe mahali pa KUISHI wanadamu.
Na ndivyo itakavyokuwa pale Roho wa Mungu atakapotua juu ya mwamini baada ya kukamilishwa, atamfanya mtu huyo kuwa ni chombo cha kuzaa zaidi na cha kuhudumia kundi lake ziadi ya matakwa ya mtu binafsi. Tunaona mara baada ya Bwana kushukiwa na Roho juu yake ndio tunaona tangu huo wakati na kuendelea akaanza kuleta uamsho Israeli yote na dunia nzima, kadhalika ndivyo ilivyokuwa kwa Yohana mbatizaji na mitume wa Yesu Kristo siku ile ya Pentekoste. Kwasababu Roho ameshawatia mafuta na kuwafanya kuwa nchi izaayo kwa ajili ya kusudi lake.
Vivyo hivyo na sisi hatupaswi kuridhika na mahali tulipo, ni kweli tulipompa Bwana maisha yetu na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kimaandiko tulitiwa muhuri kwa Roho wake, tulizaliwa kwa Roho mtakatifu, tulifananishwa na nchi iliyoumbwa hapo mwanzo na Roho wa Mungu,lakini hiyo haitoshi kwasababu tukiendelea kubakia hivyo hivyo tutazidi kuwa katika hali ya UTUPU na UKIWA. Yatupasa sisi sasa tuongeze bidii katika kumwomba Mungu na kumtafuta Roho Mtakatifu kwa nguvu zetu zote, ili alete uhai katika kanisa lake kupitia sisi, alete uamsho tena katika kanisa lake kupitia sisi, auondoe ukiwa uliopo sasa duniani, inatupasa kila siku usiku na mchana tumwombe Mungu amlete Roho Mtakatifu aipindue tena dunia.
Kumbuka hatuzungumzii kumwomba atende miujiza na ishara hapana bali alete mageuzi katika kizazi chetu kama aliyoyaleta pale alipoitia mafuta nchi tena..kumbuka mitume walikuwa wanatenda miujiza hata kabla ya siku ya Pentekoste lakini biblia haitupi rekodi ya tunda lolote walilofanikiwa kulileta siku zote walizokuwa wanazunguka kufanya miujiza isipokuwa walipofikia kipindi cha Pentekoste, Roho wa Mungu aliposhuka juu ya kanisa na kuanza kuchoma mioyo ya watu,hapo ndipo badiliko kubwa lilionekana (yaani ndani ya siku moja waliokoka watu zaidi ya elfu 3), Nguvu hizo za uamsho ndizo tunazozihitaji siku za leo.
Embu fuatilia ushuhuda huu naamini na sisi utatupa jambo la kujifunza kwa kupitia hili.
EVAN ROBERTS.
Ni kijana aliyezaliwa katika nchi ya Wales huko bara la Ulaya mwaka 1878, Ni muhubiri mashuhuri sana anayejulikana katika vitabu vya historia za kidini, aliyesifika kwa kuletea uamsho mkubwa sana huko nchini Wales mwaka 1904-1905.
Inarekodiwa kuwa Evan tangu enzi za utoto wake alikuwa ni kijana aliyependa sana kuhudhuria kanisani , na aliyekuwa anakariri mistari mingi ya biblia. Ni kijana mdogo aliyejulikana kwa kutumia masaa yake mengi katika maombi binafsi hususani wakati wa usiku akimwomba Roho Mtakatifu ampe moyo usiogawanyika, na pia alijumuika katika vikundi vya maombi na watu wengine, Evan anasema alikuwa anamwomba Roho Mtakatifu kwa zaidi ya miaka 11 aitembelee tena Wales kwa nguvu ya uamsho wa kipekee watu wengi wamgeukie Mungu. Anasema tangu huo wakati alikuwa anaweza kukaa usiku kucha akitumia muda wake mwingi kusoma, na kuzungumzia tu habari za uamsho . Evans alikuwa akiungana na vijana wenzake wengine wakiomba juu ya uamsho wa Roho uje katika kijiji chao.
Mpaka ilipofikia wakati Mungu kusikia sauti yao, Mungu alileta Roho ya Mageuzi makubwa katika nchi ile ndogo ya Wales, watu ghafla wakawa wanachomwa na mafundisho ya Evan katika kanisa dogo alilokuwa anasali, watu wakaanza kumgeukia Mungu, hata wale ambao waliokuwa vuguvugu, kwa kuhudhuria tu mikutano ile katika kanisa lile dogo watu wote walikata shauri kwa moyo mmoja na kumgeukia Mungu kwa dhati kabisa, watu waliomtafuta Mungu waliongeza kwa haraka sana mikutano mingi ikaanza kupangwa katika miji mingine,na vijiji vingine na wote waliokuwa wanasikia walichomwa mioyo na kujihisi kumrudia Mungu wao kwa mioyo yao yote.
Magazeti na vyombo ya habari vikaanza kurekodi, badiliko kubwa la watu kumgeukia Mungu katika mji ule, watu walikuwa wanawahi kufunga maduka yao kabla hata ya wakati wao wa kawaida wa kufunga ili tu wawahi ibadani za kila siku jioni, makanisa yalijawa na watu mpaka yakawa hayana nafasi tena ya kuwahifadhi watu wanaofika makanisani, watu wanasimama nje, watu ambao walikuwa watukanaji, barabarani walikuwa wakitembea na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, Uhalifu ulishuka kwa asilimia kubwa sana katika mji wa Wales, hata mabaa mengi yaliyokuwa mashuhuri ya kuuza pombe yalifungwa kwa kukosa wateja, kwasababu mji mzima ni kama ulipigwa butwaa hata wakuu wa nchi walishangaa nchi ile imekumbwa na nini kwa uamsho mkubwa namna ile ulioletwa kijana mdogo tu Evan Roberts pamoja na vijana wenzake.
Kwa kipindi kisichozidi miezi 9, zaidi ya watu 150,000 katika nchi ile ndogo walitubu na kugeuka Mungu kabisa na kuwa wakristo waliosimama mbele za Mungu, uamsho ule ulizidi kuendelea mpaka nchi jirani za Wale.Jambo hilo lilimfanya Evan kuwa mtu maarufu sana duniani kwa wakati ule, Lakini Uamsho ule ulidumu kwa muda wa miezi 9 tu.(Mwaka 1904-1905).
Sasa hiyo yote ilikuja kutokana na maombi yasiyokoma ya Evans Roberts kwa ajili ya nchi yake. Vivyo hivyo na sisi, tunapokuwa wakristo haitoshi tu kusema Roho Mtakatifu ni wa kwangu tu peke yangu, yatupasa tuingie katika kuliombea kanisa , na kuwaombea wengine Mungu mwenyewe alete Roho ya mageuzi alete UAMSHO mpya katika jamii zetu ili watu waokolewe. Mungu aachilie Roho ya kuwavuta wengi kwake..Na tukiwa watu wa tabia hiyo basi hata siku hiyo ikifika, Mungu atakapoleta UAMSHO huo atatupa sisi kipaumbele cha kwanza kuwa vyombo vyake vya kuokoa watu, kuliko tukikaa tu hivi hivi..
Na ndio maana Bwana Yesu alisema:
Na ndio maana Bwana YESU alitoa mfano huu na kusema:
Luka 11.5 “Akawaambia, Ni nani kwenu aliye na rafiki, akamwendea usiku wa manane, na kumwambia, Rafiki yangu, nikopeshe mikate mitatu,
6 kwa sababu rafiki yangu amefika kwangu, atoka safarini, nami sina kitu cha kuweka mbele yake;
7 na yule wa ndani amjibu akisema, Usinitaabishe; mlango umekwisha fungwa, nasi tumelala kitandani mimi na watoto wangu; siwezi kuondoka nikupe?
8 Nawaambia ya kwamba, ijapokuwa haondoki ampe kwa kuwa ni rafiki yake, lakini kwa vile asivyoacha kumwomba, ataondoka na kumpa kadiri ya haja yake.
9 Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa.
10 Kwa kuwa kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.
11 Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe au samaki, badala ya samaki atampa nyoka?
12 Au akimwomba yai, atampa nge?
13 Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa ROHO MTAKATIFU HAO WAMWOMBAO?”.
Unaona hapo?. Mistari hiyo inatupa picha kuwa kumbe Roho mtakatifu sio ahadi tu kwa yeyote aaminiye bali pia anapaswa kuombwa, tena kwa kurudia rudia, bila kukata tamaa, Kama Bwana Yesu alivyokuwa, mtu wa dua sana na maombi kama biblia inavyosema katika Waebrania 5:7 Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;
Unaona hapo? Aliendelea hivyo hivyo Mpaka siku ile Roho wa Mungu aliposhuka juu yake na kumtia mafuta zaidi ya watu wote duniani, siku hiyo ndiyo alipoachwa kuitwa YESU, na kuitwa YESU KRISTO. Nasi tunaona UAMSHO wake jinsi ulivyoleta madhara makubwa mpaka sasa katika vizazi vyetu.
Hivyo ni wajibu kwa kila mkristo anayeihurumia jamii yake na anayetaka jamii yake iokolewe, anayelipenda taifa lake liokolewe anayependa watu wengi waokolewe kuomba bila kukata tamaa Bwana ampe Roho Mtakatifu kwa lengo la kuzaa. Kwa lengo la kuleta Mageuzi, kwa Lengo la Uamsho,. Na kwakuwa yeye mwenyewe kashasema ikiwa sisi waovu tunaweza kuwapa watoto wetu vipawa vyema pale wanapotuomba je! si zaidi sana Baba yetu aliyembinguni?
Luka 18:7 “Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?8 Nawaambia, atawapatia haki upesi;” Hivyo sisi sote tuanze sasa, kuomba juu watu kuokolewa kwa bidii zote. Na Bwana atatusikia na kutujibu kwa wakati wake.
Bwana akubariki sana.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali “Share” ujumbe huu kwa wengine. Na Mungu atakubariki.
Mada Zinazoendana:
WAISRAELI WENGI SANA WANARUDI KWAO SASA.
KWANINI SAMWELI ALIRUHUSUIWA KUHUDUMU HEKALUNI KAMA VILE WALAWI WAKATI YEYE NI MU-EFRAIMU?
Luka 19: 37 “Hata alipokuwa amekaribia matelemko ya mlima wa Mizeituni, kundi zima la wanafunzi wake walianza kufurahi na kumsifu Mungu kwa sauti kuu, kwa ajili ya matendo yote ya uwezo waliyoyaona,
38 wakasema, Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana; amani mbinguni, na utukufu huko juu.
39 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, uwakanye wanafunzi wako. 40 Akajibu, akasema, Nawaambia ninyi, wakinyamaza hawa, MAWE YATAPIGA KELELE”.
Zamani nilijua kuwa Mimi nisipofanya kazi ya Mungu, basi kazi ya Mungu itasimama katika eneo nililopo..Ndivyo nilivyokuwa nafikiri hivyo kwa muda mrefu sana..Nilijua tunapoihubiri Injili ni kama tunamsaidia Mungu, kwamba pasipo sisi kujitoa basi watu wengi hawataokolewa..Na ndivyo nilivyofundishwa hata mimi.
Lakini namshukuru Mungu, nilikuja kuelewa zaidi ya hapo…kwamba Mungu hasaidiwi kazi, wala hajalemewa na kazi, wala haitaji msaada wowote kutoka kwa Mwanadamu…Mungu alipoiumba dunia na watu ndani yake, hakuiweka pasipo mipango kama sisi wanadamu tunavyofanya kwamba tunafikia mahali tunabanwa na majukumu yanayotuumiza kichwa mpaka wakati mwingine tunakata tama ya kuendelea..
Mungu hayupo hivyo, alipoumba kila kiumbe chini ya jua alikwisha kiwekea sehemu yake katika dunia kwamba kitazaliwa wapi, kitahitaji kiasi gani cha chakula mpaka kife, kitahitaji hewa ya ujazo kiasi gani n.k …Hayo yote Mungu alishayaweka kabla hata ya hicho kiumbe kuzaliwa au kuwepo..
Kadhalilka na kila mwanadamu anayezaliwa chini ya Mbingu, Bwana alishampangia azaliwe wapi, aishi miaka mingapi, ale chakula kiasi gani, aokolewe wakati gani, afe wakati gani n.k Kwahiyo mwanadamu anapozaliwa ni kama anakuja tu kutimiza maandiko kwa yale aliyoandikiwa.
Kwahivyo basi hakuna mwanadamau yoyote anayeweza kumsaidia Mungu majukumu yake…Yeye mwenyewe anatenda kazi zake kama alivyopanga…Kama alipanga nchi ya Tanzania ifikie idadi ya watu milioni 60 mpaka mwishoni mwa mwaka 2019..penda tusipende hiyo idadi itafika tu!!..Hata kama mtu fulani akatae kuzaa watoto…hiyo haizuii idadi ile kufika..Bwana atatumia wengine kufidia nafasi yake.
Kadhalika tunapokuja katika suala la watu kuokolewa..Bwana Yesu alisema “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu asipovutwa na Baba aliyenipeleka”..Sentensi hii inaonyesha kwanza wokovu ni wa kuchaguliwa..Sio kila mtu tu anaweza kuupokea..Ni lazima uchaguliwe na kisha uitwe/uvutwe kwa Bwana ndipo umfuate..ikiwa na maana kuwa kama mtu hajasikia mvuto wowote au msukumo wowote ndani yake wa kwenda kumfuata au kumpokea Bwana Yesu huyo hawezi kamwe kumwamini ni sawa na kumlazimisha mtoto mdogo aliyezaliwa leo azungumze haitawezekana.
Kwahiyo kama Bwana amekusudia idadi fulani ya watu wamfuate yeye mwaka huu katika mji fulani labda wa Dar es salaam, hakuna yoyote atakayeweza kupunguza au kuongeza idadi hiyo..wala hakuna mtu yoyote atakayeweza kuisimamisha kazi yake.
Atanyanyua watu wake (watumishi wake) wanawake kwa wanaume, vijana kwa wazee labda tuchukue mfano watumishi 5,000 kwa mji wa Dar es salaam..atawatuma wakaihubiri injili katika huo mji na endapo hao aliowatuma walipaswa wavune idadi ya wale watu milioni 20 wale waliokusudiwa uzima wa milele, na ile idadi ikatimia basi kazi yao itakuwa imeisha watapelekwa mji mwingine..Lakini mfano endapo kati ya wale 5,000 waliotumwa 2,000 wakawa wavivu wasilete mazao..basi Bwana atawanyang’anya ile kazi na kuwapa watu wengine lakini mwisho wa siku ile idadi ya watu milioni 20 waliokusudiwa kuokolewa itatimia tu!..kwa vyovyote vile itatimia tu! Wataondolewa wale wavivu watapewa wale wachapa kazi.
Kwahiyo ndugu huu sio wakati wa kufikiri kazi ya Mungu itasimama endapo sisi (mimi na wewe) leo hii tukikataa kuitenda kazi..Hiyo haitakuwa hasara kwa Mungu bali itakuwa ni hasara kwetu.. kwasababu Nafasi zetu watapewa wengine walio na bidii kuliko sisi endapo tukizembea..Na sisi tutakosa thawabu mbele za Mungu siku ile.
Ukikataa leo kuwashuhudia wengine habari njema za wokovu usidhani umeathiri kazi ya Mungu kwa vyovyote vile..Kazi ya Mungu itafanyika tu na watu wale waliokusudiwa kuokolewa wataokolewa..Bwana alipotuambia tuenende ulimwenguni kote tukahubiri injili kwa kila kiumbe sio kwa faida yake yeye..Ni kwa faida yetu sisi, Hatutumi ili tukamsaidie kazi yake hapana! Yeye hasaidiwi..katutuma ili tukapate faida sisi sio yeye..
Wewe usipoihubiri injili mtaani kwako, mjini kwako au nchini kwako. Kazi ya Bwana haitasimama, Mungu atanyanyua mwingine na kumleta hapo mjini kwako, au nchini kwako kuitangaza habari yake na wale waliokusudiwa kuokolewa wataokolewa tu!..lakini utakuwa umejizuiliwa thawabu yako mwenyewe..
Wewe ukikataa kuichangia kazi ya Mungu mahali ulipo, usifikiri itasimama kwa vyovyote vile.. Hapana Mungu hasaidiwi kazi wala hategemei mfuko wa mtu hata kidogo..atanyanyua wengine kutoka mahali pengine watakaoipalilia ile kazi…Anapotushauri tumtolee yeye sio kwa faida yake yeye bali ni kwa faida yetu sisi..Yeye tayari ana kila kitu..sasa ana haja na nini tena? Dunia yote ni yake sasa ni nini tutamwongezea yeye??
Anapokuambia umtafute yeye, au umtegemee yeye..sio kwamba yeye ana uhaba wa watu au wa sifa, au anahitaji sana utukufu..hapana ndugu anao mabilioni ya malaika watakatifu huko mbinguni wanaomsifu usiku na mchana…anakuambia umsifu wewe kwa faida yako?? Sio kwa faida yake..
Ni sawa na mtu mwenye kampuni kubwa tajiri lililoendelea sana na lenye wafanyakazi wengi wanaojitosheleza, na akamwona mtu maskini na kwa huruma zake akaona ampatie nafasi ya kazi kwenye lile kampuni, sasa sio kwamba kampa ajira kwa sababu anaupungufu wa faida kwenye kampuni lake hapana bali kampa ajira kwasababu amemuhurumia yule maskini na anataka na yeye apate kitu..lakini endapo yule maskini akikataa ile nafasi basi hasara haitakuwa kwa yule mwajiri bali kwake yeye kwasababu yeye tayari anao wafanyakazi wengi wanaojitosheleza….Na kwetu sisi katika kumtumikia Baba yetu wa mbinguni ndio ivyo hivyo.
Ndio maana mahali fulani Bwana Yesu alipokuwa anaingia Yerusalemu aliwaambia mafarisayo maneno yale..
“ 39 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, uwakanye wanafunzi wako. Akajibu, akasema, Nawaambia ninyi, wakinyamaza hawa, MAWE YATAPIGA KELELE”.
Umeona! Hapo…Bwana alikuwa anataka kuwaonyesha kuwa sio kwamba Mungu ni maskini wa sifa..kwamba pasipo wao kumsifu yeye basi ndio hana sifa mahali pengine..hapana hata mawe yatapiga kelele endapo wao wakinyamaza.
Kama Mtume Paulo alivyosema pia kwa uwezo wa Roho…2 Timotheo 2: 13 “Kama sisi hatuamini, yeye hudumu wa kuaminiwa. Kwa maana hawezi kujikana mwenyewe”.
Kwahiyo tukiyafahamu hayo ni wakati wa kumtumikia Mungu kwa Nguvu zote..kwa talanta tulizopewa..tukijua kuwa ni kwa faida yetu, kwasababu siku ile inakuja katika Mbingu mpya na nchi mpya..ambapo Bwana hatakuwa na upendeleo kule..Kila mtu atakuwa na nafasi yake kule, kulingana na talanta alizozifanyia kazi hapa duniani.. Katika mbingu mpya na nchi mpya watakuwepo wafalme, na watu wakawaida, nafasi mtu atakayokuwa nayo kule ndio itakuwa yake hiyo milele..Kwahiyo tujitahidi tupige mbio tukiyatazamia mambo yale yanayokuja kama vile Mtume Paulo alivyokuwa anayatazamia..
Ufunuo 22: 10 “Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.
11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.
12 TAZAMA, NAJA UPESI, NA UJIRA WANGU U PAMOJA NAMI, KUMLIPA KILA MTU KAMA KAZI YAKE ILIVYO.
13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho. 14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”.
Tukaze mwendo, tumtumikie Bwana katika nafasi alizotuweka, naye atatuhifadhi kwa reema zake.
Bwana akubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.
Mada Nyinginezo:
WALIO NA HEKIMA NDIO WATAKAOELEWA.
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo lihimidiwe!
Karibu tujifunze pamoja Neno la Mungu ambapo leo tutajifunza juu ya KARAMA ILIYO KUU. Kama maandiko yanavyosema katika kitabu cha wakorintho..
1 Wakorintho 12: 28 “Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha.
29 Je! Wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza?
30 Wote wana karama za kuponya wagonjwa? Wote wanena kwa lugha? Wote wafasiri?
31 TAKENI SANA KARAMA ZILIZO KUU. Hata hivyo nawaonyesha njia iliyo bora”.
Tukisoma hapo juu tunaona maandiko yanasema kuna karama zilizo kuu, na kama kuna karama zilizo kuu ina maana kuwa kuna karama moja iliyo kuu zaidi ya nyingine zote. Na hiyo endapo mtu akiipata atakuwa mwenye huduma kubwa kuliko ya wote.
Tukirudi kwenye huo mstari hapo juu tunaona Mtume Paulo akitaja karama kadha wa kadha hapo, mfano Mitume, waalimu, miujiza, karama za uponyaji,karama za lugha, karama za kufasiri lugha,karama za masaidiano, karama za maongozi, karama za kinabii, karama za masaidiano n.k…Ametaja nyingi sana lakini tunaona hajataja karama iliyo kuu zaidi ya yote.
Sasa kwa akili zetu za kibinadamu tunaweza kufikiri kati ya hizo karama Mtume Paulo alizozitaja hapo juu kuna moja au mbili zilizo bora zaidi ya nyingine..au kuna moja kati ya hizo iliyo kuu kuliko zote..mwingine anaweza akafikiri karama ya uponyaji hapo ndio karama kuu Paulo aliyokuwa anaizungumzia…mwingine anaweza akafikiri karama ya kitume hapo ndio karama kuu Paulo aliyokuwa anaizungumzia kwamba tuitake.. Mwingine anaweza akasema karama ya kinabii ndio kuu kati ya hizo zote, mwingine karama ya lugha n.k Kila mtu anaweza kusema ya kwake kati ya hizo hapo juu.
Lakini je! Paulo aliposema takeni sana karama zilizo kuu alikuwa analenga moja wapo ya hizo alizozitaja hapo juu?.. Ili kuelewa ni karama ipi iliyo kuu kuliko zote ambayo Mtume Paulo alikuwa anailenga katika kifungu hicho cha mistari hebu tusome tena ule mstari wa 31..
“31 TAKENI SANA KARAMA ZILIZO KUU. Hata hivyo nawaonyesha njia iliyo bora”.
Umeona hapo? Anasema “hata hivyo nawaonyesha njia iliyo bora”…au kwa lugha rahisi na nyepesi Mtume Paulo alichokuwa anamaanisha ni kwamba “ hata hivyo nawaonyesha karama iliyo bora”
Sasa hiyo njia iliyo bora au karama hiyo iliyo bora ni ipi Mtume Paulo aliyokuwa anaizungumzia?
Tukiendelea kusoma mstari unaofuata baada ya huo wa 31,tunaona Mtume Paulo ameizungumzia hiyo njia iliyo bora au karama iliyo kuu, ambayo tunapaswa tuitafute sana..
1 Wakorintho 13:1 “ Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.
3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.
4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;
7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.
8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika”.
Umeona! Biblia inasema nijaposema kwa lugha za wanadamu na malaika; hii ikiwa na maana kuwa nijapokuwa na karama ya kuweza kunena lugha za malaika na za wanadamu wote kama sina karama hiyo kuu ya UPENDO mimi sio kitu. Anaendelea kusema nijapokuwa na karama ya KINABII kama sina UPENDO ni bure!..kwahiyo karama ya kinabii si kitu mbele ya karama ya upendo..Mtume Paulo anazidi kueleza nijapokuwa na karama ya Imani timilifu hata kuweza kuhamisha milima kama sijaipata hii karama iliyo kuu ya UPENDO mimi si kitu kabisa. Na karama nyingine zote nijapokuwa nazo lakini nikikosa karama moja iliyo kuu yaani ya UPENDO basi mimi sio kitu kabisa.
Kwahiyo karama iliyo kuu Mtume Paulo aliyokuwa anaizungumzia hapo ni UPENDO. Unaweza ukauliza kwanini UPENDO na si karama nyingine kama unabii, utume, lugha, imani, ualimu n.k kwanini upendo?
Karama ya UPENDO imekuwa ni karama KUU kuliko zote kwasababu NI KARAMA YA MUNGU MWENYEWE. Biblia inasema MUNGU NI UPENDO…(1 Yohana 4:8 “Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo”.)..Mungu sio MTUME, wala MWINJILISTI, wala MUHUBIRI, wala MNENAJI WA LUGHA wala kitu kingine chochote Mungu ni UPENDO..Hiyo ndio sababu UPENDO umekuwa ni karama kuu kuliko zote.
Mungu hakutuumba sisi kwasababu yeye ni nabii, hakutupatia pumzi kwa sababu yeye ni mponyaji, hatusamehi makosa yetu kwasababu yeye ni mwinjilisti, wala hatutimizii mahitaji yetu kwasababu yeye ni mtenda miujiza..Hapana Mungu ametuumba na kutupa pumzi na kutuokoa na kututimizia mahitaji yetu kwasababu yeye ni UPENDO wenyewe ni kama ni hivyo basi ni mwingi wa UPENDO.
Kwahiyo ndugu katika huu mwaka unaoanza pamoja na kwamba tumemwomba Mungu mambo mengi atutimizie, tumwombe pia tuwe kama yeye mwenye UPENDO alivyo, Ambao upendo huu unakuja kwa kujifunza Neno la Mungu, na pia kuchukua hatua ya kujifunza kupenda, kujifunza kusamehe kama yeye alivyotusamehe sisi, mwaka huu usianze na kinyongo na mtu, au na kisasi na mtu, mwaka huu uwe mwaka wako wa kupenda na kufadhili, wasamehe wote waliokuudhi huko nyuma, ili Mungu naye apate nafasi ya kukusamehe mambo yote maovu uliyomtendea mwaka wote wa jana ulioisha, bariki wengine kutoka moyoni kabisa ili na wewe uende kubarikiwa mwaka huu, Kwasababu biblia inasema kipimo kile kile upimacho ndicho na wewe utakachopimiwa..
Umefungua ukurasa mpya, basi uwe mpya kweli kweli katika roho yako pia,hapo utakuwa umemjua Mungu, naye Mungu mwenyewe atakupenda na kukutunza na kukuhifadhi kwasababu yeye mwenyewe ni UPENDO..
Ni maombi yangu kuwa Bwana atatujalia mambo hayo yote na zaidi ya hayo katika mwaka huu, Nakutakia Kheri ya Mwaka mpya 2019, Bwana akakutunze na kukuhifadhi dhidi ya yule mwovu wewe na watu wako na nyumba yako,na familia yako, akakulinde na kukupa afya njema, tangu mwanzo wa mwaka huu hadi mwisho wa mwaka, Bwana akakufanikishe katika mambo yote unayoyafanya yanayompendeza yeye katika JINA LA YESU KRISTO.
Amen!.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
MUNGU NDIYE ANAYEISHAWISHI MIOYO.
NI RAHISI KWA NGAMIA KUPENYA KATIKA TUNDU LA SINDANO, JE! NI SINDANO IPI HIYO INAYOZUNGUMZIWA?
SHETANI ANATOLEA WAPI FEDHA, ANGALI TUNAJUA FEDHA NA DHAHABU NI MALI YA BWANA?