SWALI: Bwana Yesu alikuwa na maana gani kusema ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’.
Luka 13:33
[33]Pamoja na hayo imenipasa kushika njia yangu leo na kesho na kesho kutwa; kwa kuwa haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu.
JIBU: Bwana Yesu alikuwa anaeleza asili ya mji wa Yerusalemu nyakati zote ulivyokuwa wa mauaji, mji ambao ungepaswa uwe wa kupokea manabii wa Mungu, lakini kinyume chake uligeuka mji wa kuwaua Manabii…
Sasa kusema maneno yale ni kutokana na taarifa aliyoletewa na wale mafarisayo kuwa Herode anataka kumwangamiza, hivyo aondoke pale aende mji mwingine…ndipo Bwana Yesu akawaambia ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’ yaani haipaswi nabii afe nje ya Yerusalemu…
Manabii wengi wa Mungu, waliuliwa pale pale Yerusalemu hivyo hata na yeye kuangamia hapo si jambo geni, …
Na ndivyo ilivyokuwa
Mfano wa hao katika maandiko alikuwa;
Zekaria mwana wa Yehoyada (2Nyakati 24:20-21). Ambaye aliuliwa hekaluni
Mwingine ni Uria nabii (Yeremia 26:20 – 24)
Na manabii wengine wengi ambao hawajatajwa, moja kwa moja katika maandiko waliuawa Yerusalemu…ndio sababu ya Yesu kusema maneno Haya;
Mathayo 23:37-39
[37]Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!
[38]Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa.
[39]Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana.
Jambo hili hujirudi sasa rohoni..
Watu wote ambao wanaipinga injili mioyoni mwao leo, hata kama hawajashiriki moja kwa moja kuwarushia mawe watu wa Mungu, ni shirika moja tu na wale waliokuwa wanawaua manabii wa Bwana zamani.
Ndivyo walivyodhani mafarisayo kwamba wenyewe hawahusiki na mauaji ya manabii wa Bwana, angali wanampinga yeye waziwazi, kwa unafiki wao aliwaambia maneno haya..
Mathayo 23:29-36
[29]Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki,
[30]na kusema, Kama sisi tungalikuwako zamani za baba zetu, hatungalishirikiana nao katika damu ya manabii.
[31]Hivi mwajishuhudia wenyewe, ya kwamba ninyi ni wana wao waliowaua manabii.
[32]Kijazeni basi kipimo cha baba zenu.
[33]Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum?
[34]Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji;
[35]hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu.
[36]Amin, nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki.
Hii ni hatari kubwa sana kwa walio nje ya Kristo.
Mwamini Yesu leo uoshwe dhambi zako. Upokee uzima wa milele. Kwingineko si salama.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote (Yohana 16:23)
MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.
SWALI: Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote ’
Kwanini ajiangue kwa namna hiyo angali yeye ndiye mwokozi wa kutegemewa kila kitu?
Yohana 16:23
[23]Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.
JIBU:
Kama tunavyojua hakukuwahi kutokea kiongozi aliyekuwa na matokeo makubwa duniani kama Yesu Kristo.
Namna ya uongozi wake, Kwa jinsi ulivyokuwa thabiti na bora Matokeo yake ndio tunayoana mpaka sasa duniani kwenye imani.
Hivyo maisha yake na huduma yake sio tu vinatufundisha njia ya wokovu lakini pia vinatufundisha namna kiongozi bora anavyopaswa Awe.
Matokeo Ya mitume wake kuwa nguzo kwa makanisa ya vizazi vyote ni matokeo ya namna ambavyo alivyowakuza anawakuza.
Bwana Yesu hakutengeneza Wafuasi, bali alitengeneza watu kama Yeye…Na hivyo katika kuwafundisha wanafunzi wake aliwakuza Ki vitendo zaidi kuliko maneno ya vitabu vingi vya kidini na mapokeo.
Kwamfano utaona kuna mahali anawatuma wawili waenda kuhubiri injili mahali ambapo angepaswa kwenda yeye mwenyewe, lakini aliwaacha waende.
Luka 10:1
Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.
Mahali pengine aliwaacha watoe pepo na waliposhindwa hakusema ‘wanangu nyie ni wachanga, basi nitakuwa nawasaidia tu’…hapana Kinyume chake aliwakemea Kwa upungufu wa imani zao.
Vivyo hivyo katika tukio hili, wanafunzi wake walitarajia kila siku watakaa naye wamuulize maswali yeye, kisha awajibie kutoka kwa Baba.. Ni sawa na mtoto mchanga ambaye kila siku anasubiria atafuniwe tu chakula apewe…unadhani hilo litaendelea sana?
Vivyo hivyo hilo halikuwa lengo la Bwana Yesu, bali alitaka kuwafundisha kanuni za wao wenyewe kumuuliza Mungu na kujibiwa moja kwa moja kama yeye alivyokuwa anajibiwa…
Na njia moja wapo ilikuwa ni yeye kuondoka, kisha kwa kile kitendo cha wao kumkosa Bwana wa kumuuliza, wajifunze kuomba kisha Roho ajae ndani yao, ndipo waanze sasa kupokea mafunuo ya kweli na ujasiri kutoka kwa Mungu..
Lakini pia waombe jambo lolote kwa jina la Yesu, wapokee mahitaji yao. Na Kweli mambo hayo yalianza Kutokea baadaya ya Pentekoste.. wote walikuwa ni kama ‘Yesu-dunia’ hakuna hata mmoja alifikiri au kuwaza kwamba kuna umuhimu tena wa Yesu kutembea nao, kimwili bali waliweza kuyafanya yote.
Hiyo ni tabia ya kiongozi bora…huwafanya wanafunzi wake kuwa kama yeye, na wakati mwingine kutenda hata zaidi ya yeye…Yesu aliwainua zaidi kwa kusema.
Yohana 14:12
[12]Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.
Hiyo ndio sababu kwanini aliwaambia hayo maneno.
Yohana 16:23-24
[23]Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.
Hata sasa Bwana anataka kuona ukomavu kama huu ndani ya maisha ya wakristo wengi.. Ikiwa kila siku utakuwa unategemea Mchungaji wako akuombee, ni lini utaweza wewe mwenyewe kuomba na kuwaombea wengine? Sababu ya watu wengi kutojibiwa maombi yao na Mungu ni hiyo.. Ameshakomaa kiroho, Mungu anaona anaouwezo wa kupambana na tatizo yeye mwenyewe, atataka kiongozi wake amsaidie..
Hicho kitendo kinapunguza utendaji Kazi wa nguvu za Mungu, kwasababu yeye hataki tumgeuze mwanadamu Mungu..Ukiokoka, fahamu kuwa Roho Mtakatifu yupo ndani yako, na kuanzia huo wakati na kuendelea unawajibu wa kuufanyia mazoezi wokovu wako, jifunze kuomba mwenyewe, jifunze kuombea watu, soma biblia mwenyewe Mungu akufundishe..
Hizo ndio hatua bora za ukuaji kiroho.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Jambo jingine Kuu la kujifunza kama mkristo ni Kumshukuru Mungu kila wakati na kwa kila jambo, kwamaana maandiko ndivyo yanavyotufundisha..
1Wathesalonike 5:18 “shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu”.
Kuna mambo yanafunguka tu yenyewe baada ya kumshukuru Mungu!..haihitaji nguvu nyingi.. Maombi ya shukrani ni maombi yanayougusa moyo wa Mungu zaidi hata ya kupeleka mahitaji!, kwani ni yanauelezea uthamani wa Mungu katika maisha ya mtu, ni maombi ya kushuka sana na ya kuithaminisha kazi ya Mungu katika maisha yako au ya wengine, na hivyo ni maombi yenye nguvu sana na kuugusa moyo wa Mungu kuliko tunavyofikiri.
Na kiuhalisia maombi ya kushukuru ndiyo yanayopaswa kuwa maombi ya kwanza kabisa kabla haya yale ya toba na mahitaji..kwasababu, uzima tu ulionao ni sababu ya kwanza kumshukuru Mungu, kwasababu usingekuwa nao huo hata maombi mengine usingeweza kuomba..
Leo tuangalie faida moja ya kumshukuru Mungu, kwa kujifunza kupitia Bwana wetu YESU KRISTO.
Kama wewe ni msomaji wa Biblia utagundua kuwa kila wakati ambapo Bwana YESU alitaka kufanya MUUJIZA usio wa kawaida, alianza kwanza kwa kushukuru..
Kwamfano kipindi anaigawa ile mikate kwa watu elfu nne alianza kwanza kwa kushukuru..
Mathayo 15:33 “Wanafunzi wake wakamwambia, Tupate wapi mikate mingi hapa nyikani, hata kushibisha mkutano mkuu namna hii?
34 Yesu akawaambia, Mnayo mikate mingapi? Wakasema, Saba, na visamaki vichache.
35 Akawaagiza mkutano waketi chini;
36 akaitwaa ile mikate saba na vile visamaki, AKASHUKURU AKAVIMEGA, akawapa wanafunzi wake, nao wanafunzi wakawapa makutano.
37 Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate makanda saba, yamejaa”.
Pengine unaweza usione uzito wa shukrani katika huo muujiza wa mikate… hebu tusome mahali pengine palipoonesha kuwa ni SHUKRANI ya Bwana ndio iliyovuta ule muujiza mkuu wa mikate.
Yohana 6:23 “(Walakini zikaja mashua nyingine kutoka Tiberia mpaka karibu na mahali pale walipokula mikate, WAKATI BWANA ALIPOSHUKURU)”..
Hapo anasema.. “wakati Bwana aliposhukuru”… Kumbe! Ile shukrani ilikuwa na maana kwa sana kwa muujiza ule kutendeka.. Na wala pale hapaonyeshi kwamba Bwana YESU alimwomba Baba augawe ule mkate!.. la! Bali alishukuru tu kisha akaumega!, muujiza ukatendeka.
Kuna mambo mengine unahitaji kushukuru tu na kuendelea mbele!, na mambo yatajiweka sawa yenyewe, kuna nyakati hutahitaji kuomba sana.. bali kushukuru tu, na kumwachia Bwana..na maajabu yatatendeka..
Pia utaona kipindi kile kabla ya Bwana kumfufua Lazaro alianza kwanza kwa KUMSHUKURU MUNGU..
Yohana 11:39 “Yesu akasema, Liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana, ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne.
40 Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?
41 Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, BABA, NAKUSHUKURU KWA KUWA UMENISIKIA.
42 Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia sikuzote; lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kwamba ndiwe uliyenituma.
43 Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje.
44 Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake”.
Umeona? Ni shukrani tu, ndio iliyomtoa Lazaro kaburini..
Je na wewe unayo desturi ya kumshukuru Mungu?.. Maombi ya shukrani yanapaswa yale maombi marefu sana, kwani tunazo sababu nyingi sana za kumshukuru Mungu, kama umeokoka, huo wokovu ulio nao ni sababu ya kumshukuru Mungu hata masaa sita mfululizo, kwasababu kama ungekufa kabla ya kuokoka leo ungekuwa wapi?.
Kama unapumua hiyo ni sababu ya kumshukuru Mungu, kwasababu wapo walioondoka na wengine ni wema kuliko hata mimi na wewe.
Na zaidi ya yote si tu kushukuru kwa mambo mema au mazuri Mungu anayokutendea, bali hata kwa yale ambayo yameenda kinyume na matarajio yako, ni lazima kushukuru, kwasababu hujui kwanini hiyo jambo limekuja kwa wakati huo, endapo Ayubu asingemshukuru Mungu kwa majaribu aliyokuwa anayapita zile Baraka zake mwishoni asingeziona.
Ni hivo hivyo mimi na wewe, hatuna budi kumshukuru Mungu kwa vyote, viwe vizuri au vibaya.. kwasababu tunajua mwisho wake utakuwa mzuri.
Yeremia 29:11 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho”.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
UNAZO KILA SABABU ZA KUMSHUKURU MUNGU
Kwanini BWANA awaagize wakoma wakajionyeshe kwa Makuhani?(Luka 17:14
KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU.
Maombi kama sehemu ya maisha ya mwamini mpya.
SWALI: Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, ni vita ya namna gani tunashindana nayo katika ulimwengu wa Roho?
JIBU: Katika biblia tunaposoma Neno “pepo”, ni vema tufahamu ufunuo wake upo katika namna mbili;
Yote mawili unapaswa kufahamu, Ili ujue ni nani unashughulika naye katika vita hivyo vya kiroho.
Kwamfano, ukisoma ile waefeso 6:12 inayosema kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama, bali juu ya falme na mamlaka na wakuu wa giza hili pamoja na majeshi ya mapepo wabaya.. Sasa hao wanaotajwa hasaa ni malaika waasi.
Lakini hawa malaika waasi, huwa na mapando yao, ambayo huyapanda ndani ya watu, mfano wa hayo ni magonjwa, ukichaa, ububu, udhaifu (Marko 9:25)uuaji, uchungu, majivuno, kiburi, masengenyo n.k.. na haya mapando wakati mwingine huitwa mapepo, kwasababu asili yao ni kutoka kwa hao malaika waasi.
Luka 13:11 Na tazama, palikuwa na mwanamke aliyekuwa na pepo wa udhaifu muda wa miaka kumi na minane, naye amepindana, hawezi kujinyosha kabisa.
Pepo linalozungumziwa hapo, hasaa sio yale mashetani, bali ni pando la udhaifu waliloliweka ndani ya huo mwanamke.
Hizi zote ni kazi za shetani na malaika zake duniani. Sasa mapando haya ndio tunaweza kuyaua (kwa kuyang’oa), lakini sio wale malaika waasi. Ndio maana Bwana Yesu alisema..
Mathayo 15:13 Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang’olewa
Wale malaika waasi (yaani wakuu wa giza, wafalme, majeshi ya mapepo yote)hatuwezi kuwaua, kwa maombi au kwa namna yoyote, isipokuwa tayari wameshawekewa hukumu yao, siku ile ya mwisho ambapo watatupwa wote kwenye lile ziwa la moto.
Na mapando haya, Bwana Yesu alitoa maelezo yake vema, wakati ambapo adui hupandwa ndani ya mtu..
alisema.
Mathayo 13:24 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.
27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?
28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?
29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.
30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.
Kumbe wakati ambapo watu wamelala, ndipo hupanda mbegu zake. Yaani wakati ambapo watu wamekuwa walegevu kiroho ndipo shetani hupata nguvu ya kuja kupachika, mbegu zake za uharibifu, zitakazokuja kusumbua baadaye. Ndio maana ni lazima ujue kanuni mbalimbali za kumpinga shetani.
Na haya mapando, yanaweza kuwekwa kwa mtu yeyote, hata mtu aliyeokoka, anaweza kuwa nayo. Ndio maana utaona wapo watu wengine wameokoka, lakini wanasumbuliwa na mapepo, kiuhalisia, hawana malaika wale waasi ndani yao, wanayo mapando yao.
Ni sawa, na mtu ambaye anamilika chombo kama komputa, akiwa anaitumia kwa matumizi yake tu ya sikuzote, tu ambayo ni lazima, si rahisi computa hiyo kuvamiwa na virusi, lakini akianza kutembea mitandaoni, kisha kubofya, au kupakua kila kitu anachokiona ni wazi kuwa chombo hicho kipo hatarini kuvamiwa na virusi, na matokeo yake ni kuwa mfumo wote wa kumpyuta unaliwa, au kuharibifu chombo kabisa, ndio maana wanaweka ulinzi (anti-virus) sikuzote,
Vivyo hivyo na maisha ya mwanadamu yakiwa ovyo ovyo, hawezi kukwepa mapando ya mashetani ambayo yamezaa kila mahali. Mtu yeyote ambaye hajaokoka tayari kuna pepo fulani ndani yake.
Kwamfano, mwingine, labda mkristo ameokoka, halafu akiwa kanisani, anaanza kuruhusu masengenyo kinyume na mchungaji wake, au mama-mchungaji, sasa mtu kama huyo akiwa anaendelea na tabia hiyo..matokeo yake ni kwamba pepo la uchungu litamvaa, ataanza kuwachukia viongozi wake hata bila sababu, na kuzusha vita, na uharibifu hata wengine. Yeye atadhani ni tabia yake kumbe sio, bali pepo limeshamvaa la uchungu.
Nikupe huu ushuhuda, Kulikuwa na mama mmoja kanisa, kipindi chote ulikuwa ukikutana naye, anamzungumzia vibaya mama mchungaji wa kanisa alilokuwa mwanzo, hapo mwanzo alikuwa vizuri tu kiroho, lakini kwa jinsi siku zilivyozidi kwenda, akiendeleza chuki zake, , hali yake ilikuja kubadilika ghafla, akaomba tumwombee, tulipomwombea alilipuka mapepo, lile pepo likawa linasema “mama mchungaji” yaani asili yangu ni chuki kwa mama mchungaji, tulipolikemea likamwacha akarudia hali yake ya kawaida, akawa mtu mzuri tu.
Samsoni, alipokwenda kuwashindana na wafilisti, hakushughulika kwanza na wafilisti, bali mashamba yao ya ngano. (mapando yao). Kwa kuyachoma moto. Vivyo hivyo na sisi ili tuyamalize nguvu haya mashetani, tuangushe ngome zao. Ni lazima fikra zetu hasaa zielekee mapando yao.
Injili:
Kwamfano kuwaangusha wakuu wa giza sio kuwatumia makombora ya moto hapo angani. Hapana, bali ni kwenda kuhubiri injili ili watu wamsikie Kristo waokoke,
Ndio maana Yesu alipowatuma wanafunzi wake wawili wawili kuhubiri waliporudi Yesu aliwaambia ‘nalimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme’.
Kumbe anguko lake lilikuwa katika kuhubiri na si kumtumia makombora.
Maombi:
Hii ni silaha kubwa, ya kumpinga shetani. Maombi huruhusu, utendaji kazi wa Mungu ndani ya maisha ya mwamini, usipokuwa mwombaji tarajia shetani kuyapangalia maisha yao. Yesu alituagiza tukeshe kuomba tusije ingia majaribuni.
Upendo:
Upendo hupinga, wivu, chuki, uchungu, mashindano, uzinzi, n.k. ambayo haya yote huzaliwa mahali ambapo hapana upendo. Ni lazima kila siku wewe kama mwamini kila siku ujifunze kutendea kazi upendo….ili uondoe mazingira ya mashetani kuangua mayao yao hapo.
Neno:
Ukiwa na Neno la Mungu la kutosha ndani yako, adui hawezi kukushinda. Utakumbuka kule jangwani, shetani alipojaribu kumpandia Kristo maneno ya uongo kwa kupitia biblia, yeye mwenyewe alilitumia Neno la Kweli, kumpinga. Watu wengi wanavamiwa na maroho ya upotevu, kwasababu hawana Neno la Mungu mioyoni mwao. Jifunze kusoma biblia. Ni silaha inayoitwa Upanga.
Imani:
Imani huzaa ujasiri, na ujasiri hutoa mamlaka ndani yako. Biblia huiita imani “Ngao” Shetani anapenda kutumia silaha ya woga, ili kuzimisha utendaji kazi wa Mungu mioyoni mwetu. Hatuna budi kusimama kwa utimilifu wa imani kumtumikia Mungu.
Kukemea:
Fahamu adui ni mpingamizi sikuzote, hapembelezwi, bali analazimishwa kutoka, Yesu alimkemea shetani alipotaka kumjaribu kwa kinywa cha Petro, aliyakemewa mapepo yote sugu, yaliyokuwa ndani ya watu yawatoke. Hivyo na wewe pia ukutanapo na kazi hizi za mwovu, jifunze kutumia kinywa chako, kwa mamlaka uliyopewa na Kristo kukemea haraka sana, kila pepo, au kimelea chochote cha uovu kinachozaliwa na adui.
Hivyo kwa hitimisho ni kuwa, mashetani hawafi, lakini kazi zao zinakufa.. Hatuwaui hao, bali tunaziua kazi zao. Usipoteze muda mwingi kumrushia shetani mabovu hawezi kufa, bali tuma nguvu zako nyingi kurushia mabovu mapanda yake, kwa kanuni hizo tulizojifunza. Utawashinda kabisa kabisa.
Bwana akubariki
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?
MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.
SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.
Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?
Ili tuelewe vizuri utofauti uliopo kati ya Agano jipya na la kale, tutafakari mifano ya kawaida ya maisha;
Hebu tafakari juu ya Elimu ya Awali (msingi) na Elimu ya Sekondari.. Utaona ulipokuwa shule ya msingi ulijifunza mahesabu ya kujumlisha na kuzidisha kwa kutumia vitu vya asili kama vijiti au mawe.. Lakini ulipofika sekondari ulitumia kikokotoo (yaani calculator).
Sasa mabadiliko hayo hayaifanyi elimu ya msingi kuwa batili, kwasababu tu vipo vikokotoo..La bali zinaithibitisha zaidi ile elimu ya msingi.. kwasababu kikokotoo (calculator) kinapiga mahesabu yale yale ya kujumlisha na kuzidisha kwa kasi na ufasaha zaidi.
Ni hivyo hivyo kwa Agano la kale na Agano jipya..
Mambo yaliyopo ndani ya Agano jipya ni mambo yale yale yaliyopo ndani ya agano la kale isipokuwa katika ufunuo bora zaidi na ufasaha mkubwa zaidi..
Tafakari tena mfano huu…
Toleo la kwanza la simu yako miaka 15 iliyopita..bila shaka lilikuwa ni mfano wa “tochi”, lenye mipaka mingi ya matumizi lakini toleo la pili la sasahivi ni “smart” ambalo unaweza kuingia internet, kupakua applications, kutazama video na hata kusikiliza nyimbo.
Kwahiyo Toleo jipya halijaja kuondoa chochote kilichopokuwepo kwenye toleo la kale, isipokuwa limeboresha zaidi vile vilivyopo na kuongeza vingine vya ziada.. maana yake Kama mtu alikuwa anasikiliza tu sauti pekee, sasa katika toleo jipya atasikika sauti pamoja na picha ya anayeongea..
Hali kadhalika kama toleo la kwanza la simu lilikuwa linachukua muda kuwaka na linahifadhi nambari za simu za watu 100 tu, basi toleo jipya litakuwa linawahi kuwaka na pia kuhifadhi namba za watu hadi 1,000.
Ni hivyo hivyo katika habari ya Agano la kale na Agano Jipya..
Agano jipya ni toleo bora zaidi la agano la kale, ni kitu kile kile isipokuwa kimeandikwa na kutendeka katika ubora mkubwa zaidi, na ufunuo mkubwa zaidi..
Kwamfano katika agano la kale, kafara na dhabihu zilikuwa ni za wanyama lakini tunapokuja katika Agano jipya dhabihu zimeboreshwa zaidi, badala ya kutumika damu za wanyama, inatumika damu ya MTU, YESU KRISTO (Ambayo ni bora zaidi).
Vile vile katika Agano la kale, amri ziliandikwa kwenye mbao za mawe kule mlima Sinai, lakini katika agano jipya amri na sheria za Mungu zinaandikwa katika mioyo yetu kiufunuo zaidi.
Yeremia 31:31 “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.
32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.
33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu”.
Katika Agano la kale Uzinzi ulijulikana katika mwili tu (Kutoka 20:14) lakini katika Agano jipya uzinzi unajulikana katika mwili na roho kwa ufunuo bora zaidi (Soma Mathayo 5:28)
Katika Agano la kale uuaji ulijulikana katika mwili tu (Kutoka 20:13), lakini katika Agano jipya uuaji unajulikana katika mwili na roho kwa ufunuo bora zaidi (Soma Mathayo 5:21-22).
Katika Agano la Kale ni watu wachache tu ndio walishukiwa na Roho wa Mungu, (ambao walikuwa ni Manabii na Waamuzi) lakini katika Agano jipya watu wote wanayo fursa la kushukiwa na Roho Mtakatifu (Matendo 2:17-18).
Kwahiyo Agano jipya ni mwendelezo wa Agano la kale katika ubora zaidi na utimilifu na ufunuo mkamilifu, ndio maana Bwana YESU alisema hakuja kuitangua torati bali kuitimiliza.
Mathayo 5:17 “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza”.
Na Roho Mtakatifu ndiye Msaidizi wetu tuliyepewa ambaye atatusaidia kulielewa Agano la Kale na Agano jipya, hivyo hatuna budi kumtafuta huyo kwa bidii zote.
Na Roho Mtakatifu ni ahadi ya Bure kwetu kwa watu wote pasipo kujali umri (Matendo 2:37-38), tukimpata Roho Mtakatifu basi tutazidi kuielewa Biblia.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Orodha ya majina ya Miji ya Biblia (Agano la kale) na Sasa
Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?
Neno “Mashehe” tunaliona likitajwa katika biblia(Agano la kale); Hawa mashehe ni wakina nani?
Mithali 4:23 “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako CHEMCHEMI ZA UZIMA”.
Chemchemi kazi yake ni kutoa “maji ya kunywa” lakini pia ya maji ya “kustawisha mimea”.
Kama chemchemi ikitoa maji ya chumvi au ya magadi, ni wazi kuwa maji yake hayatafaa kwa matumizi yoyote yale, hivyo mahali hapo hapana uhai, watu hawawezi kuishi wala wanyama wala mimea..
Lakini kama chemchemi ikitoa maji safi yasiyo na magadi wala chumvi, na tena masafi, basi mahali pale kila kitu kitasitawi ikiwemo watu, wanyama na mimea, na hata shughuli zote nyingine za kiuchumi.
Mfano wa maji machungu na yasiyofaa ni yale wana wa Israeli waliyokutana nayo kule ‘Mara’
Kutoka 15:22 “Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji.
23 Walipofika mahali palipoitwa Mara hawakupata kuyanywa yale maji ya Mara, kwa kuwa yalikuwa machungu; kwa ajili ya hayo jina lake likaitwa Mara.
24 Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema, Tunywe nini?
25 Naye akamlilia Bwana; Bwana akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na hukumu huko, akawaonja huko”.
Sasa Biblia inafananisha “Mioyo yetu na chemchemi zinazotoa maji”… Maana yake yanayotoka mioyoni mwetu yanaweza kukuza, kustawisha au kudhoofisha afya zetu, wanyama wetu, mimea yetu…kwaufupi kila kitu kinachotuzunguka ikiwemo kazi zetu, elimu zetu, nafasi zetu, kibali chetu na mambo mengine yote yanategemea sana yanayotoka mioyoni mwetu.
Sasa najua utauliza haya maji machungu au matamu ni nini?.. Turejee maneno ya Bwana Yesu.
Mathayo 12:34 “Enyi wazao wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake.
35 Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya”.
Tusome tena Mathayo 15:18-20…
Mathayo 15:18 “Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.
19 kwa maana MOYONI hutoka MAWAZO MABAYA, UUAJI, UZINZI, UASHERATI; WIVI, USHUHUDA WA UONGO, NA MATUKANO
20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi…….”.
Umeona hapo?.. kumbe moyoni ndiko kunakotoka matukano, uzinzi, wizi, uongo n.k mambo ambayo ndiyo yanayomtia mtu unajisi, na bila shaka hayo ndiyo Maji machungu yatokayo moyoni kupita kinywani, ambayo hayafai kwa kustawisha chochote…
Wengi wamepoteza na kuharibu maisha yao kwasababu ya uzinzi, na wengine kwasababu ya wizi, na wengine kwasababu ya mauaji, wapo waliopoteza kibali kwa Mungu na kwa watu kwasababu ya wizi, au uzinzi, au mauaji..wapo walipoteza kazi zao za mikono na huduma zao zilizokuwa zenye utukufu kwasababu ya uzinzi, au wizi au matukano..
Wapo walioharibu ndoa zao zilizokuwa za heshima na mfano kwasababu ya uzinzi, uongo, na mauaji (utoaji mimba) Kwanini?.. kwasababu chemchemi zao zinatoa maji machungu yanayoua ndoa, kazi, huduma, kibali, heshima na nguvu.
Yakobo 3:8 “Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.
9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu.
10 Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo.
11 Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu?
12 Ndugu zangu, Je! Mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Kadhalika chemchemi haiwezi kutoa maji ya chumvi na maji matamu”.
Lakini kama moyoni kukutoka mambo masafi, ambayo ni upendo, ukweli, utu wema, uvumilivu (kwa ujumla utakatifu)… hakika hiyo ni chemchemi bora inayostawisha kila kitu, maji yake yatastawisha wokovu, kazi ya Mungu, kazi ya mikono, elimu, heshima, ndoa, nafasi na mambo mengine yote mazuri.
Je wewe chemchemi ya moyo wako inatoa maji ya aina gani?.. machungu au matamu?.. Kama inatoa machungu ipo dawa leo?.. dawa hiyo ni Roho Mtakatifu… Mwamini YESU leo kisha ukabatizwe na Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukutakasa moyo wako Bureeeee kabisa!
Baada ya hapo ndoa yako iliyokufa itafufua upya, huduma yako, kazi yako, elimu yako au kitu kingine cha thamani ulichopewa na Bwana, kitafufuka kwani tayari maji yatokayo ndani yako ni masafi..
Lakini labda tayari chemchemi yako ni safi, nayo inatoa maji masafi.. bado kuna jambo lingine la ziada la kufanya nalo ni KUILINDA chemchemi yako..
Mithali 4:23 “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako CHEMCHEMI ZA UZIMA”.
Utaulinda moyo wako kwa MAOMBI, kusoma NENO, kujihadhari na ulimwengu na kushiriki ibada pamoja na watu wenye imani moja na wewe kila mara.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nini maana ya Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu?
Fahamu Maana ya Mithali 15:24 Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;
JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.
SWALI: Nini maana ya Yeremia 31:30 “Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi”.
JIBU: Zamani za agano la kale katika taifa la Israeli, kulikuwa na usemi maarufu, unaosema “Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi”.
Kikawaida zabibu au matunda mengine yenye asidi nyingi mtu alapo , huwa meno yanatia ganzi, lakini kamwe haiwezekani mtu mwingine akatiwa ganzi kwa ulaji wa mwingine.
Hapa Waisraeli wakiwa wanamaanisha kuwa adhabu za Mungu huwa zinatembea hata kwa kizazi cha watu, Lakini Mungu kwa kinywa cha Yeremia anawasahihisha kuwa hilo si jambo lake..Anawaambia kila mtu ataadhibiwa sawasawa na uovu wake, wala watoto hawatauchukua uovu wa wazazi wao..Jambo ambalo alilirudia pia kwa kinywa cha Nabii Ezekieli (Ezekieli 18:20).
Lakini pia ukisoma muktadha wa vifungu hivyo, utaona anatoa unabii wa agano jipya ambalo atalifanya na watu wake kupitia Yesu Kristo, akimaanisha kuwa wokovu wake pia , utakuwa ni wa mtu binafsi, mmoja mmoja. Tusome habari yote tokea juu.
Yeremia 31: 27 Tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapoipanda nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda, mbegu ya mwanadamu na mbegu ya mnyama.
28 Tena itakuwa, kwa kadiri nilivyowaangalia, ili kung’oa, na kubomoa, na kuangusha, na kuangamiza, na kutesa; kwa kadiri iyo hiyo nitawaangalia, ili kujenga, na kupanda, asema Bwana.
29 Siku zile, hawatasema tena, Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi.
30 Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi.
31 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.
32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.
33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
Hivyo vifungu hivi, vinatupa kutambua kuwa wajibu wa kulitunza agano la Mungu ni la mtu binafsi, sawasawa na alivyokuja kulifunua katika agano jipya kupitia Yesu Kristo, kwamba ijapokuwa wokovu umeachiliwa kwa wote, lakini haupokelewi kijumuiya, kifamilia, au kikabila, bali kibinafsi.
Kila mtu atalibeba furushi lake mwenyewe. (Wagalatia 6:5)
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Tafsiri ya Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.
Yeremia alikuwa na umri gani alipoitwa?
Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?
SWALI: Je! Ni sahihi kwa mkristo kujifunza, au kufundishwa na AI (Artificial Inteligence), mfano wa Chatgpt, deepseek n.k.
JIBU: Ili kujibu swali hili ni vema, kutambua mashine hizi za akili bandia (AI), zinafanya kazi gani.
Kwa ufupi ni kuwa AI, inafanya kazi ya kuchakata taarifa nyingi, kutoka katika vyanzo vingi vilivyopo mitandaoni, mfano vitabu, makala, sauti, machapisho n.k, na hivyo inazichanganya taarifa hizo zote kwa kuangalia muktadha unaofanana na kuzifupisha, na kukujibu.
Hivyo kimsingi, ni chombo ambacho kinatoa msaada mkubwa katika ulimwengu wa sasa, na ndio ukweli usiopingika..Kwasababu kinarahisisha utafutaji wa taarifa. Lakini pamoja na hayo haimaanishi kuwa kinatoa kwa ufasaha wote.
Sasa tukija kwenye eneo la kiroho. Je ni vema mkristo kwenda kuuliza AI, au kuandaa maombi au masomo kupitia hiyo, n.k.
Ukweli ni kwamba Imani, sio taarifa, ni zaidi ya taarifa.. Hizi AI, zinatoa tu taarifa lakini hazitoi mafunuo. Hazina pumzi ya Roho Mtakatifu ndani yake.
Ikiwa unataka kuongeza maarifa kwa sehemu fulani zinaweza kukusaidia, lakini sio kukujenga nafsi, kwani inahitaji pumzi ya Mungu na miongozo ya Mungu wewe kujengwa nafsi, na sio taarifa.
Kwamfano ikiwa wewe ni mchungaji halafu, kila inapokaribia jumapili unachowaza ni kwenda chatgpt, kuiambia ikuandalie somo la kufundisha jumapili, ndugu hapo hesabu kuwa umepotea kama sio kukengeuka… Tumia hiyo kwenye biashara zako, masomo yako, projekti zao lakini sio kwenye mambo ya kiroho. Hilo liepuke kabisa.
Kufundisha Neno inahitaji ‘Neno’ mwenyewe (Yesu) akae ndani yako, kwasababu ni UHAI sio taarifa (Waebrania 4:12) ndio hapo itakupasa kupiga magoti kwanza uombe, kwa muda mrefu, utafakari moyoni mwako, ukae kwenye utulivu wa kutosha, ndipo Mungu alipande somo lake moyoni mwako. Ambalo yeye mwenyewe anajua litakuwenda kuwagusa vipi watu wake, wenye changamoto mbalimbali, kwamfano, pengine mtu mmoja alikuwa anakaribia kwenda kujinyonga kwasababu ya ugumu wa maisha na mateso fulani, na Mungu kamwona anataka amsaidie, kwa kuliweka somo linalohusiana na mapito ya Ayubu ili ainuliwe imani. Kinyume chake kwasababu ya uvivu wako wewe unakwenda kuiambia chatgpt (akili bandia), ikuandalie somo. Halafu jumapili utakwenda na taarifa zao sio mafunuo. Badala uokoe roho inayokwenda kujinyonga, unaiambia, “leo tunajifunza kanuni kumi za kudumisha ndoa na mahusiano kibiblia”. Hapo unafanya nini sasa?
Au Neno fulani Bwana anataka kukupa la wakati wako, sasa ikiwa unakimbilia AI ikusaidie, hutaki kuchukua muda wako binafsi kutafakari na kuomba ‘jiandae kukutana na ukame wa kiroho.
Visaidizi hivi, hatupaswi kuvifanya ndio sehemu ya imani yetu, kwamba kila kitu tutegemee kule, hivi ni tone dogo sana kati ya bahari kubwa. Roho Mtakatifu alishatuandalia njia zake, kuu za kujengwa na yeye.
Wekeza zaidi, kuomba msaada kwa wakufunzi wako, viongozi wako, ndugu zako katika Kristo, wekeza katika maombi, mifungo, tafakari, na kujisomea mwenyewe Neno. kwa njia hizi hakika Bwana atasema nawe na kujengwa zaidi kuliko visaidizi. Lakini pia ikiwa pana umuhimu wa kujiongezea taarifa kwa vile unavyovijua, visaidizi hivi vitakufaa (Katika uangalizi maalumu), vinginevyo utajidumaza kiroho.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Uinjilisti kama agizo kuu la Bwana.
Mathayo 12:36 “Basi, nawaambia, KILA NENO LISILO MAANA, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu.
37 Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa”.
Mfano wa maneno yasiyo na maana ni maneno yote ya kukufuru, kulaani, kutukana, mizaha, mashindano, mazungumzo machafu, nyimbo za kidunia na mengine yanayofanana na hayo.
1. Mizaha
Unapotumia baadhi ya mistari ya kwenye Biblia au matukio kwaajili ya kufanya utani, au mzaha au vichekesho…maneno hayo utayatolea hesabu siku ile. Biblia sio kitabu cha comedy.
Zaburi 1:1 “Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha”.
2. Dhihaka.
Unapotoa dhihaka juu ya Neno la Mungu, au Watumishi wa Mungu ambao unajua kabisa ni wa kweli, siku ya mwisho utatoa hesabu..
3. Mabishano na Mashindano.
Unapobishana na ukweli, kwasababu tu unataka uonekane unajua au unatafuta ushindi wa maneno.. basi fahamu kuwa siku ya mwisho utatoa hesabu ya maneno yako yote… Biblia inasema mashindano ya dini yote ni maneno yasiyo na maana..
1Timotheo 6:20 “Ee Timotheo, ilinde hiyo amana; ujiepushe na maneno yasiyo ya dini, yasiyo na maana, na mashindano ya elimu iitwayo elimu kwa uongo”
4. Kufuru
Unapotoa kufuru na kashfa juu ya kazi ya Mungu, na moyoni unajua kabisa ni kazi kamili ya Mungu, mbeleni kuna kutoa hesabu ya maneno yaliyotoka kinywani.
Mafarisayo walinena maneno ya kumkufuru Roho Mtakatifu katika kitabu hiko cha Mathayo 12, na ndio sababu ya Bwana YESU kusema maneno hayo kuwa “kila neno lisilo maana watu watatoa hesabu yake siku ya mwisho”.
5. Nyimbo za kidunia.
Maneno yaliyopo kwenye nyimbo za kidunia hayana maana na yanamtukuza shetani, na hivyo hata maneno ya nyimbo hizo yatatolewa hesabu.
Amosi 6:5 “ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda, na kujifanyizia vinanda vya namna nyingi, kama vile Daudi”.
6. Mazungumzo machafu.
Mazungumzo machafu ni yale yote ya kijiweni au ya mtu na mtu, ambayo ni mazungumzo ya uasherati, ushabiki, uhuni, na mipango mibaya, matusi na mambo mengine yote mabaya.. yote hayo mtu atayatolea hesabu siku ya mwisho.
Sasa nini maana ya kutoa hesabu?
Kutoa hesabu maana yake ni kutoa “maana au tafsiri ya kina ya kile kilichotoka kinywani”. Kwamfano kama mtu umemtukana mtu na kumwita yeye ni Mbwa, basi siku ile utaeleza sababu za kumwita vile, na kama kweli yeye ni mbwa kama ulivyosema… kwaufupi maneno ambayo sisi tuliyatamka kwa utani tu na ufupi, kule yatarefushwa na kuwa mada ndefu mno.
Hivyo hatuna budi kuwa makini na yanayotoka kinywani mwetu.. kwamaana yanarekodiwa yote, na pia ni vizuri kama tumekosea kwa vinywa vyetu kuwahi kurudi kutubu kwa tuliyemtolea maneno mabaya, au tuwahi kurudi kwa Mungu kutubu ili tusiangukie hukumu.
Hukumu inakuja, hukumu inakuja, tumwamini YESU na kutubu na tuyashike sana maungamo yetu.
Ubarikiwe.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
KILA MTU ATATOA HABARI ZAKE MWENYEWE.