Licha ya kulinda, jukumu lingine kuu mlinzi alilonayo ni kuhisi hatari kutoka mbali, Na ndio maana utaona mnyama ambaye Mungu alimuumba kutulinda sisi (Mbwa), licha tu ya kupewa ukali, lakini pia amepewa uwezo wa kunusa mbali, na kusikia, na ndio maana wakati wa usiku utaona mbwa wanabweka sana, hiyo ni kutokana na kuwasikia na kunusa vitu vilivyo mbali sana visivyo vya kawaida, ambavyo hata wewe huwezi kuvihisi au kuvisikia, ule wakati ambao unauona ni wa utulivu na salama lakini kwa Mbwa ni machafuko.
Vivyo hivyo na mlinzi yoyote, hana jukumu la kulinda tu pale adui anapokuja, bali pia anajukumu la kuhisi hatari, na hiyo inakuja kwa kupepeleza, kuchunguza, kutafiti na kutazama, na wakati mwingine kufanya doria, itakayomsaidia kuhisi tatizo kabla halijatokea.. na thamani ya mlinzi sikuzote ipo usiku n.k…
Isaya 21:11 “Ufunuo juu ya Duma. Mtu ananililia toka Seiri, Ee mlinzi, habari gani za usiku? Ee mlinzi, habari gani za usiku? 12 Mlinzi akasema, Mchana unakuja na usiku pia; mkitaka kuuliza, ulizeni; njoni tena.”
Isaya 21:11 “Ufunuo juu ya Duma. Mtu ananililia toka Seiri, Ee mlinzi, habari gani za usiku? Ee mlinzi, habari gani za usiku?
12 Mlinzi akasema, Mchana unakuja na usiku pia; mkitaka kuuliza, ulizeni; njoni tena.”
Ukisoma hata katika agano la kale utaona walinzi wa miji walikuwa wanakaa katika minara mirefu, ili kuwasaidia kuona kitu kinachokuja kutoka mbali, na wakiona hatari basi bila kuchelewa tarumbeta lilikuwa linapigwa na mji wote kujiweka tayari kwa vita.
Ezekieli 33:1 “Neno la Bwana likanijia, kusema, 2 Mwanadamu, sema na wana wa watu wako, uwaambie, Hapo nitakapoleta upanga juu ya nchi, watu wa nchi hiyo wakimtwaa mtu mmoja miongoni mwao, na kumweka AWE MLINZI WAO; 3 ikiwa, aonapo upanga unakuja juu ya nchi hiyo, apiga tarumbeta na kuwaonya watu; 4 basi mtu awaye yote aisikiaye sauti ya tarumbeta, wala haonywi, upanga ukija na kumwondoa, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe. 5 Aliisikia sauti ya tarumbeta, wala hakuonywa; damu yake itakuwa juu yake; lakini kama angalionywa, angalijiokoa roho yake.”
Ezekieli 33:1 “Neno la Bwana likanijia, kusema,
2 Mwanadamu, sema na wana wa watu wako, uwaambie, Hapo nitakapoleta upanga juu ya nchi, watu wa nchi hiyo wakimtwaa mtu mmoja miongoni mwao, na kumweka AWE MLINZI WAO;
3 ikiwa, aonapo upanga unakuja juu ya nchi hiyo, apiga tarumbeta na kuwaonya watu;
4 basi mtu awaye yote aisikiaye sauti ya tarumbeta, wala haonywi, upanga ukija na kumwondoa, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.
5 Aliisikia sauti ya tarumbeta, wala hakuonywa; damu yake itakuwa juu yake; lakini kama angalionywa, angalijiokoa roho yake.”
Lakini kama mji utakosa walinzi, au watazamaji, ni dhahiri kuwa utakuwa katika hatari ya kuvamiwa na maadui wakati wowote, na siku maadui watakapokuja watakuja ghafla wenyeji hawatajua chochote kwasababu hawakuwa na waonaji wanaoona mbele yao.
Ndivyo Bwana alivyotabiri jinsi itakavyokuwa katika hizi siku za mwisho, kuja kwake kutakuwa kwa ghafla, kama mwivi usiku wa manane.
(Ufunuo 16:15 “Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake”.)
vile vile mwisho wa dunia utawajia watu kwa ghafla,
(2Petro 3:10 “Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea”.)
na hiyo yote ni kwasababu wamekosa MLINZI katika mioyo yao.
Na ndio maana jambo kuu na la muhimu sana ambalo Bwana Yesu alituachia siku ile aliyokuwa anaondoka, alikuwa ni ROHO MTAKATIFU, akamwita ni msaidizi wetu, kwa namna nyingine ni mlinzi wetu, alijua kabisa, wakati wa giza utapita duniani, na sikuzote giza linaleta usingizi, hivyo kama hatakuwepo mtu wa kuwasaidia kukesha nao, watasinzia na uharibifu utawapata kwa ghafla…
Hivyo akatugawia Roho Mtakatifu, ambaye ndio tupo naye sasa, wote waliompokea kila siku anawashuhudia ndani ya mioyo yao hatari iliyopo duniani sasahivi na jinsi ya kuwa waangalifu. Anawataarifu kila iitwapo leo habari za mwisho wa dunia na kuja kwa Kristo. Na hawa ndio wale hata siku ile ya unyakuo itakapokaribia sana kufika wataifahamu, kwasababu mlinzi wa kuwapasha habari yupo mioyoni mwao.
1 Wathesalonike 5 :1 “Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie. 2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku. 3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa. 4 Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi”.
1 Wathesalonike 5 :1 “Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.
2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.
3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.
4 Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi”.
Unaona, wale waliojazwa Roho Mtakatifu ndio siku hiyo hatawapa kama mwivi kwasababu, atakuwepo kuwapasha habari juu ya mambo yote yanayokuja. Watajua kabisa wakati wa kuondoka umefika, kama wanavyoshuhudiwa hata sasa, itakapofika kipindi kifupi sana kabla ya unyakuo, mlio wa kengele utazidi kuongezeka ndani ya mioyo yao.
Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, NA MAMBO YAJAYO ATAWAPASHA HABARI YAKE”.
Lakini wale wengine, ambao hawana ROHO MTAKATIFU sasa, ndio wale hata wakisikia kuwa tunaishi siku za mwisho hawashtuki, mioyoni mwao hakuna mabadiliko yoyote, macho yao yamefumbwa, ukiwaambia Yesu Kristo yupo mlangoni kurudi, wanakudhihaki, Na wengine tayari walishampa Bwana maisha yao, zamani walikuwa wanaishi kama wana wa mbinguni lakini baada ya muda na wao wamegueka wakafanana na watu wengine wa kidunia, hao ndio wale ambao wamemzimisha ROHO MTAKATIFU ndani yao, Yule mlinzi anayewalinda amelala, na hivyo hawezi tena kuwapasha habari ya mambo yanayokuja na hatari iliyopo mbele yake.
Mtunzi wa Zaburi aliandika hivi, kwa wachao Mungu..
Zaburi 121:3 “Asiuache mguu wako usogezwe; ASISINZIE AKULINDAYE; 4 Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli. 5 BWANA NDIYE MLINZI WAKO; Bwana ni uvuli mkono wako wa kuume.”
Zaburi 121:3 “Asiuache mguu wako usogezwe; ASISINZIE AKULINDAYE;
4 Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.
5 BWANA NDIYE MLINZI WAKO; Bwana ni uvuli mkono wako wa kuume.”
Wapo ambao, awalindaye amesinzia, na hao ndio wale wanawali wapumbavu wanaozungumziwa katika Mathayo 25. Ambao kwa pamoja na wenzako (wale wanawali werevu) walikuwa wanamngoja Bwana wao, lakini kwasababu hawa hawakuwa na mafuta ya ziada katika chupa zao, wakarudi baadaye wakakuta mlango umeshafungwa, kule kuishiwa na mafuta ndio kumzimisha Roho..Kwasababu mwanzoni walikuwa nayo lakini baadaye yaliwaishia..Na mafuta siku zote katika biblia yanamwakilisha ROHO MTAKATIFU.
Ndugu yangu nataka nikuambue tunaishi katika siku za mwisho, hakuna mtu asiyejua kuwa Dalili zote zimeshatimia, Jiulize Kristo akirudi leo kulichukua kanisa lake, utaufichia wapi uso wako wewe ambaye bado unasuasua, kwa injili ulizokuwa unahubiriwa kila kukicha lakini bado hutaki kugeuka?. Roho Mtakatifu kila siku anagonga katika mlango wa moyo wako lakini hutaki kufungua. Biblia ipo wazi inasema na mtu yoyote asiyekuwa na Roho wa Kristo huyo sio wake (Warumi 8:9).
Ni maombi yangu utamruhusu huyu mlinzi ayaongoze maisha yako kuanzia sasa katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho kabla ya hii dunia kuisha..Kama ulikuwa umepoa, au umemzimisha Roho Mtakatifu ndani yako, ni wakati wa kutengeneza mambo yako upya sasa. Na kama hujamkabidhi Bwana maisha yako, unachopaswa kufanya ni kutubu kwa kudhamiria kabisa kuacha dhambi, kisha kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi, kwa jina la YESU KRISTO, kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako. Na ukishatii maagizo hayo mepesi Bwana mwenyewe atamshusha Roho wake Mtakatifu ndani yako, kuanzia huo wakati na kuendelea naye atakuongoza na kukupasha habari ya mambo yote yahusiyo saa tunayoishi na siku za mwisho, na hatimaye siku ile haijakujia kama mwivi.
Bwana akubariki sana.
Pia Kwa Maombezi/Ushauri/Ratiba za Ibada Wasiliana nasi Kwa namba
+225683036618/+225789001312
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Zinazoendana:
KAMA MWIZI USIKU WA MANANE:
JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?
HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA
JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.
Rudi Nyumbani
Print this post
Kitabu cha Jeografia, hawajaandikiwa watu ambao sio wanafunzi, kadhalika kitabu cha Fizikia na Baolojia…Vitabu vyote hivi wameandikiwa watu husika…yaani wanafunzi wa masomo hayo..Mtu mwingine yeyote akisoma hataelewa au hakitamsaidia sana…Na maudhui ya vitabu hivyo havijaandikwa kwa lengo la kusomwa tu, bali kujifunza…lengo la mwanafunzi kujifunza mambo yaliyoandikwa ndani ya kitabu kile ni ili kumpa maarifa ambayo yatamsaidia katika maisha yake na pia yatakayomsaidia kufaulu mitihani…asipokielewa kitabu hicho na kukisoma tu kama gazeti, anaweza kweli kukisoma chote ndani ya siku moja lakini utakapokuja mtihani atafeli…Kwasababu waandishi wa vitabu hivyo, lengo lao sio mwanafunzi asome ndani ya siku moja, bali ajifunze kidogo kidogo mambo yaliyopo kule na ayafanyie mazoezi na alinganishe mambo kutoka vitabu vingine, na ndio maana mpaka atakapohitimu inaweza kumchukua hata miaka 4 na zaidi.
Kadhalika na Biblia, NI KITABU CHA MAISHA. Kitabu hichi, hakimuhusu kila mtu, bali kinawahusu wanafunzi tu! Wengine watakisoma kama gazeti na hakitawasaidia chochote, lakini wanafunzi wanakisoma kama ni sehemu ya Maisha yao, future yao ipo hapo, Ndio ufunguo wa Maisha yao…Ndio maana biblia iliposema “Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; Mshike, maana yeye ni uzima wako.(Mithali 4:13)”…Mstari huo haukulenga Elimu ya darasani…hapana! Bali ulilenga Elimu ya Mungu (Elimu ya ufalme wa mbinguni) Mathayo 13:52..maana huo ndio uzima wetu…wengi wanaupeleka mstari huu moja kwa moja kwenye Elimu ya duniani, lakini hiyo si kweli.. “hiyo ni maana ya pili ya mstari huo lakini maana ya kwanza Kabisa Sulemani aliyomaanisha hapo ni ELIMU YA UFALME WA MBINGUNI”.
Na unapozungumzia Elimu huachi kuzungumzia, Shule, huwezi kuacha kuzungumzia,Waalimu, huwezi kuacha kuzungumzia wanafunzi, wala huwezi kuacha kuzungumzia Mtaala (ambao upo ndani ya vitabu husika).
Na kadhalika Maisha mapya katika Kristo yetu ndio shule yetu, Roho Mtakatifu ndio Mwalimu Mkuu wetu, Biblia ndio Mtaala wetu(Kitabu husika)..na wote waliomwamini Yesu Kristo kwa kuzaliwa mara ya pili, kwa kudhamiria kabisa kumfuata kwa kujikana nafsi zao ndio wanafunzi wake…Utasema hilo linapatikana wapi kwenye maandiko…soma
Luka 14:25 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia, 26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. 27 Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.
Luka 14:25 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,
26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
27 Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.
Sasa mwanafunzi kabla hajajiunga na shule yoyote ya kidunia, anakubali kuachana na wazazi wake, na ndugu zake, na hata marafiki zake, anakwenda kujiunga na shule ya Bweni…Huko shuleni hataishia tu kukaa mbali na wazazi wake kwa kipindi kirefu, bali atalazimika kuvikataa pia vile vitu vizuri alivyokuwa anavipenda akiwa nyumbani kama Tv, simu, uhuru, nk..anakwenda mahali ambapo hapana uhuru aliokuwa anautaka, mahali ambapo pengine atakutana na changamoto za chakula kibovu, na malazi mabaya.…Na katika Ukristo ndio hivyo hivyo unapoamua kumfuata Kristo ni sawa na umejiunga na shule mpya, Maisha yako ya kale unayakataa, pamoja na mapenzi ya wazazi wako…kwasababu unakwenda kutafuta Uzima wako wa baadaye (future). Na Ukristo sio mteremko kama wengi wanavyofikiri, ukiamua kumfuata Kristo kupungukiwa wakati mwingine kunakuwepo na pia kuna kupitia dhiki nyingi..tofauti na wale watu wanaowahidia watu uongo kuwa watakafanikiwa siku zote.
Vivyo hivyo unapoingia shuleni, unakutana na sheria za shule na moja ya sheria hizo ni mavazi, na mwiko kutoka nje ya uzio wa shule.…shuleni huwezi kujivalia utakavyo, kunakuwa na UNIFORM maalumu…na wote mnafanana…na huwezi kuingia na kujitokea kama unavyotaka, ukitoka bila sababu maalumu ndio umejifukuzisha hivyo…..kadhalika Unapozaliwa mara ya pili, mavazi yako na mwonekano wako ni lazima ubadilike, ulikuwa unavaa vimini ni sharti uache, ulikuwa unavaa suruali wewe mwanamke ni sharti uache, ulikuwa unanyoa kiduku na kuvaa nguzo zinazobana na milegezo wewe mwanamume sharti uache, ulikuwa unapenda kusikiliza miziki ya kidunia, na movie zisizo na maana na fashion za ulimwengu, na kuzurura huku na huko vyote hivyo unaacha!…Na pia Ukristo sio kuingia na kutoka…Ukiingia umeingia! Na ukitoka umetoka…Mwalimu Mkuu huwa hawi mkali kwa Watoto wa mitaani, huwa anakuwa mkali kwa Watoto walioko shuleni kwake, vivyo hivyo Roho Mtakatifu anavyowafundisha watu waliozaliwa mara ya pili ni tofauti na ambao wapo nje.
Baada ya kukubaliana navyo hivyo vigezo, ndipo unapewa MTAALA MAALUMU pamoja na Waalimu wa kukufundisha, na wewe mwenyewe unaongeza bidii zako binafsi kujisomea…Ukisubiri tu kila siku kufundishwa darasani na wewe mwenyewe hutaki kutafuta, utafeli mtihani wa Mwisho, na Katika Ukristo ni hivyo hivyo, umezaliwa mara ya pili, wewe kila siku unapenda tu kufundishwa Biblia, muda wa kujisomea mwenyewe huna, utafeli majaribu na hutaendelea mbele kila siku utakuwa unarudi darasa lile lile, miaka yote wakati wenzako wanaenda mbele..
Na jambo lingine baada ya kujiunga na shule za kidunia ni kwamba utakaa shuleni katika hayo mazingira ya kuteseka kwa muda mrefu kidogo inaweza kuchukua hata miaka kadhaa, lakini siku utakapokuja kufanya mtihani wa mwisho na kufaulu utapokea cheti, ambacho hicho kitaonyesha tofauti yako wewe uliyekwenda shule na yule ambaye hajakwenda…kulivumilia viboko vya shule na kula chakula kibovu na wakati mwingine kulala vitanda vyenye kunguni sio bure!…siku utakapohitimu na kupata cheti heshima yako ndio itakapoonekana kuwa hukuwa mjinga kujikana nafsi yako.
Kadhalika Roho Mtakatifu akishakupitisha katika madarasa yake na kuyahitimu vizuri faida zake utakuja kuziona hapa hapa duniani pamoja na katika ulimwengu ujao…lakini sana utakuja kuziona katika ulimwengu ujao kwasababu vitu vya hapa duniani havidumu, vinapita lakini vya huko mbinguni ni vya milele…Siku zile wateule walioshinda watang’aa kama jua mbele za malaika wa mbinguni…
Mathayo 19:27 “Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi?. 28 Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli. 29 Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele”.
Mathayo 19:27 “Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi?.
28 Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.
29 Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele”.
Umeona Umuhimu wa kuitafuta Elimu ya ufalme wa mbinguni sasa?..Elimu ya dunia hii inafunua elimu ya ufalme wa mbinguni, Kristo anapokuambia leo utubu na kuacha dhambi, na ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina lake na uache ulimwengu na mambo yake yote, na kisha umfuate sio kwamba anataka atutese, hapana ni kwasababu anataka atusajili kwenye shule yake ambayo baadaye itatupa cheti kilicho bora! Zaidi kuliko vyeti vyote.. Na heshima! Zaidi kuliko heshima zote….na kumbuka hakuna shule yoyote isiyokuwa na sheria ndio maana anakuambia ewe mwanamke jikane nafsi!! acha mavazi yako ya kikahaba, acha mawigi, acha kupaka wanja, acha mavipodozi baki katika hali yako ya asili…kama unapenda kujipamba subiri tukifika mbingu za mbingu utajipamba utakavyo kama kutakuwepo na kujipamba….lakini kwasasa upo shule!..fanya kile Mwalimu Mkuu anachokuagiza ukifanye kwa faida yako…
Ulipokuwa katika shule za kidunia ulipoambiwa uvae sketi za marinda ulitii na usisuke nywele ulitii bila shuruti lakini unapoitafuta elimu ya Roho Mtakatifu hutaki kutiii…nataka nikuambie ukweli bado hujaanza madarasa ya Roho Mtakatifu, bado upo nyumbani wala mtu asikudanganye kuwa upo sawa na Mungu bado haupo sawa, usidanganywe pia Mungu haangalii mavazi anaangalia Roho, ni kweli kabisa anaangalia roho lakini roho inamahusiano makubwa na mwili ndio maana ipo ndani ya mwili, kama vile elimu ya kidunia ilivyo na uvaaji wa wanafunzi wake..Elimu ni ufunguo wa Maisha, yaangalie Maisha yako ya baadaye yatakavyokuwa usijiangalie leo…dhambi za kitambo zisije kukuponza ukaja kujuta milele huko baadaye..Fanyika mwanafunzi wa Kristo leo.
Pia kwa Maombezi, Ushauri, au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba
+225693036618/+225789001312
NJIA YA MSALABA
BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA JIKANE MWENYEWE?
JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?
MJUE SANA YESU KRISTO.
1 Wakorintho 6: 19 “Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? WALA NINYI SI MALI YENU WENYEWE;”
Ukilijua Neno hili utauheshimu mwili wako, kuliko hapo kwanza. Kitu kikubwa kisichofahamika na wengi ni kuwa Miili hii tuliyonayo sio mali yetu..hatujapewa dhamana ya kuitawala asilimia 100. Kama ingekuwa ni mali yetu asilimia mia moja, tungekuwa na uwezo wa kuzisimamisha nywele zetu zisiote kwa amri zetu, tungekuwa tunaweza kuiambia mioyo yetu isimame kusukuma damu na ingetutii kama tu vile tunavyoamua kusimama au kukaa…
Kwahiyo unaweza kuona miili hii, tunamamlaka nayo sehemu ndogo sana, tena sana….huwezi kukiongoza chakula tumboni, kinajiongoza chenyewe, huwezi kuuongoza mwili wako utoe jasho unajitoa wenyewe, au kucha kukua…mwanamke hawezi kutengeneza kiumbe ndani ya tumbo lake, kiumbe kinajitengeneza chenyewe ndani kwa ndani, anajikuta tu, uchungu umemfikia na anajifungua mtoto… kadhalika hatuwezi kujifanya tukue..tangu tulipokuwa Watoto tunajikuta tu tunaongezeka kimo na ukubwa bila idhini yetu, vitu kama ini, figo, kongosho, seli zinafanya kazi pasipo hiyari zetu nk…chunguza utagundua kuwa hii miili yetu, tuna mamlaka nayo sehemu ndogo sana, karibia kila kitu kinaongozwa na nguvu nyingine..
Mamlaka tuliyopewa sisi ni uwezo wa kusogeza viungo vyetu vya nje kama miguu, mikono, macho, na uwezo wa kujisogeza kutoka sehemu moja hadi nyingine..basi hakuna kingine cha ziada…Hii yote ni kuonyesha kuwa HII MIILI SI MALI YETU NI MALI YA MWINGINE.
Ni kama tu mtu unapofungua account ya Facebook au ya Bank au anapoisajili laini ya simu…Unapofungua account ya facebook kwa mfano, account hiyo inakuwa ni ya kwako ina jina lako na password yako, kiasi kwamba hakuna mtu anayeweza kujua kinachoendelea ndani ya account hiyo, isipokuwa wewe umwonyeshe… kila kitu unaweza ukakifanya private mtu yeyote asijue unafanya nini, na unaweza kuitumia utakavyo…lakini pamoja na kwamba unao uwezo wa kuitumia utakavyo, bado kuna vitu utakuwa huwezi kufanya…kwamfano ukikiuka sheria za wamiliki wa facebook wanakunyanganya hiyo account, aidha wanakufuta kabisa au wanakublock kwa muda…na huwezi kuirudisha kwa namna yoyote ile,
Hiyo yote ni kuonyesha kwamba hiyo account si yako bali ni yao. Hata kama unauwezo wa kuweka password ngumu kiasi gani, lakini wenyewe wakitaka kujua kinachoendelea ndani ya account hiyo huwezi kuwazuia, wakitaka kukupokonya vile vile huwezi kuwazuia.
Na Zaidi ya yote, jinsi account za facebook na nyinginezo zinavyofanyiwa marekebisho, huwa mwenye account hahusiki, anajikuta tu kuna kitu Fulani kimeongezeka kipya, au kuna kitu Fulani kimeondolewa..Hiyo yote ni kuonyesha kuwa hiyo account ni ya kwako lakini bado sio ya kwako. Ni watu Fulani walikupa tu..
Na hii miili tuliyopewa ni hivyo hivyo, ni Mali ya Mungu…Si mali yetu kabisa, na ilivyowekwa hapa duniani na aliyeiweka (yaani Mungu) kaiwekea sheria na utaratibu wake, namna inavyopaswa iwe…Hakutupa kwa lengo la kuigeuza bango la matangazo, au chombo cha kuharibu wengine, au kituo cha roho nyingine chafu zinazoharibu kukaa…Mwili unaofanya hivyo utafungiwa haki ya kuishi (maana yake utakufa).
Ndio maana kuna umuhimu sana wa kuitunza hii miili tuliyopewa, na kuelewa kwa undani masomo kuhusu NAFSI, MWILI na ROHO.. kwasababu si MALI YETU WENYEWE…Ukiuchora mwili wako tattoo isingekuwa shida endapo ingekuwa ni mali yako…lakini kwasababu si mali yako ni ya mwingine usifanye hivyo, utajitafutia mabaya badala ya mazuri….Ni sawa sasahivi uanze kutumia hiyo account ya facebook vibaya, ukaanza kuitumia kuweka picha chafu na zisizofaa na kuharibu jamii, na kufanya uhalifu, wamiliki wakiligundua hilo unafungiwa mara moja na wala hutapata nafasi ya kuongea nao..kwasababu hata hawajawahi kuzungumza na wewe hapo kabla…password haimaanishi kuwa ndio umepata uhalali wa kuimiliki hiyo account asilimia 100. Kadhalika sio kwasababu unauwezo wa kusitiri siri ndani ya mwili wako kiasi kwamba hakuna mtu awezaye kujua kinachoendelea ndani mwako, na una uwezo wa kutembea kutoka sehemu moja hadi nyingine kama utakavyo, ndio iwe sababu ya kusema huo ni mwili wako…Huo sio wako ni mali ya Mungu, akiutaka anauchukua siku yoyote, na huwezi kumwuliza kwanini.
Hivyo ili tuweze kuishi ndani ya hii miili kwa muda mrefu na kwa kheri hatuna budi kuishi kwa kuzifuata sheria zake, Neno lake linasema…mwanamke avae mavazi ya kujisitiri (1 Timotheo 2:9) basi ni vizuri kutii…usiseme una uhuru juu ya mwili wako, na kuvaa utakavyo, kumbuka huo si wako…
Biblia inasema usichanje chale wala usichore alama (tattoo) katika mwili wako ni machukizo, basi usijifanye wewe ni mgunduzi wa huo mwili, yupo mwenye huo mwili ambaye akiutaka anao uwezo wa kuutahifisha muda wowote.
Walawi 19: 28 “Msichanje chale yo yote katika nyama ya miili yenu kwa ajili ya wafu, wala msiandike alama miilini mwenu; mimi ndimi Bwana”.
Biblia inasema uashareti hata usitamkwe kamwe kwenu (Waefeso 5:3)…Usiseme mwili wangu, nina uhuru wa kufanya nitakalo, Hivyo Mungu hawezi kunihukumu kwa kitu ambacho ni mali yangu…Ndugu huo sio mali yako, ingekuwa hii miili ni mali yetu katupa moja kwa moja, wala asingetusumbua kutuwekea sheria sheria,… tungekuwa na uhuru wa kila mtu kufanya atakalo…mtu angeamua kujirefusha kuwa kama mlingoti, ni sawa, mwingine angetaka kujifanya kuwa tembo pia ni sawa…lakini kwasababu ni mali yake, wote anatuweka kwenye kimo Fulani karibia kinachofanana na maumbile yanayofanana, kutimiza kusudi lake yeye na si la kwetu…Kwahiyo Uasherati ni moja ya dhambi mbaya sana ambayo inaweza kusababisha kifo cha ghafla kuliko dhambi nyingine zote..
1 Wakorintho 6: 18 “Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe”.
Na dhambi nyingine ambazo ni mbaya zinazopelekea kuharibu mwili ni Ulevi, uvutaji sigara, matumizi ya madawa ya kulevya na matumizi ya vipodozi na utoboaji mwili.
Kama uliyafanya hayo pasipo kujua, na ulikuwa hujui kuwa mwili huo ulionao sio mali yako, basi hii ndio nafasi yako ya kutubu, unatubu na kumwambia Bwana hutaki tena hayo mambo na hivyo unataka kutimiza kusudi lake alilolikusudia juu ya mwili wako, baada ya kutubu katafute ubatizo sahihi popote pale, kama hujafanya hivyo, ubatizo sahihi ni wa umuhimu kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako (Matendo 2:38) na ubatizo sahihi ni wa kuzama mwili wote katika maji na kwa jina la Yesu, na baada ya hapo Bwana mwenyewe atakupa Roho Mtakatifu atakayekusaidia kushinda dhambi na kukuongoza katika kuijua kweli yote ya Biblia. Hakuna mtu awezaye kushinda dhambi kwa nguvu zake mwenyewe, wote tunamtegemea Roho Mtakatifu kutuwezesha, hivyo Roho Mtakatifu ni wa muhimu sana baada tu ya kumwamini na kubatizwa, maana yeye ndio Muhuri wa Mungu (Waefeso 4:30)
Bwana akubariki.
WEWE NI HEKALU LA MUNGU.
MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.
JE! KUFANYA MASTURBATION (PUNYETO) NI DHAMBI?
‘’MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI’’..NA NDIVYO ILIVYO KWA UASHERATI
Rudi Nyumbani:
Moja ya Wafalme 19 waliopitia Yuda, na Wafalme 20 waliopita Israeli, enzi zile wafalme, tukiachilia wale wafalme watatu ambao waliitawala Israeli kabla ya kugawanyika yaani (Sauli, Daudi, na Sulemani)..Ni mfalme mmoja tu ambaye kuzaliwa kwakwe kulitabiriwa kwa namna ya ajabu sana, na mfalme huyu alijulikana kama mfalme Yosia,.
Mwanzoni kabisa wa ufalme kugawanyika, ambao tunajua ulisababishwa na kosa la Sulemani, la kuweka miungu migeni Israeli, Mungu alikasirishwa hadi kufikia hatua ya kutaka kumnyang’anya ufalme wote lakini kwasababu ya viapo ambavyo Mungu alimwahidia Daudi baba yake kuwa hatakosa mtu wa kuketi katika kiti cha enzi cha Israeli milele(2Nyakati 6:16),hivyo Mungu akambakishia Daudi kabila moja , yaani kabila la Yuda, na la Benyamini kama msindikizaji wake.
Lakini mengine yote kumi, alimgawia mtu mwingine ambaye alikuwa ni mtumwa wa Sulemani aliyeitwa Yeroboamu, ikiwa hujapata uchambizi wa vitabu vya wafalme, bofya hapa..⏩Vitabu vya biblia
Sasa siku ile Yeroboamu anaahidiwa ufalme huo Mungu alimwambia maneno haya:
1Wafalme 11:38 “Tena itakuwa, ukiyasikia yote nitakayokuamuru, na kuenda katika njia zangu, na kutenda yaliyo mema machoni pangu, ili kuzishika amri zangu na hukumu zangu kama Daudi mtumishi wangu alivyotenda, basi, nitakuwa pamoja nawe, nitakujengea nyumba iliyo imara, kama nilivyomjengea Daudi, nami nitakupa wewe Israeli. 39 Tena nitawatesa wazao wa Daudi kwa sababu hii, lakini si daima”.
1Wafalme 11:38 “Tena itakuwa, ukiyasikia yote nitakayokuamuru, na kuenda katika njia zangu, na kutenda yaliyo mema machoni pangu, ili kuzishika amri zangu na hukumu zangu kama Daudi mtumishi wangu alivyotenda, basi, nitakuwa pamoja nawe, nitakujengea nyumba iliyo imara, kama nilivyomjengea Daudi, nami nitakupa wewe Israeli.
39 Tena nitawatesa wazao wa Daudi kwa sababu hii, lakini si daima”.
Lakini kama tunavyosoma, huyu mfalme japo alijua kuwa ufalme umekuja kwake kwa kosa la Sanamu za Sulemani, yeye hakulitia hilo moyoni mwake badala yake, akawa mbaya kuliko hata Sulemani, na kiongozi yoyote ambaye alishawahi kutokea Israeli, alileta giza kubwa Israeli ambalo kuondoka kwake iligharimu miaka zaidi ya 400, ni huyu Yeroboamu…yeye alijenga madhabahu za ng’ombe kaskazini na kusini mwa ufalme wake, ili kuzuia watu wasiende kuabudu Yerusalemu kwenye Hekalu la Sulemani, mahali ambapo Mungu alipachagua mambo ya ibada yafanyike, hakuishia kuwazuia tu watu wasiende kuabudu bali akatunga mpaka na sikukuu zake mwenyewe za miezi yake mwenyewe ya kuabudu, hivyo kwasababu yeye ndiye aliyekuwa mfalme basi watu wote walimtii na kumfuata..
Sasa sikumoja wakati amekaa katika dhabihu ya jioni, anaifukuzia uvumba miungu yake, Nabii wa Mungu alitokea palepale kama tunavyosoma katika kitabu cha 1 Wafalme..
1 WAFALME: MLANGO 13
1 “Na tazama, akatoka mtu wa Mungu katika Yuda kwa neno la Bwana, akafika Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa akisimama penye madhabahu, afukize uvumba. 2 Basi mtu huyo akapiga kelele juu ya madhabahu, kwa neno la Bwana akasema, Ee madhabahu, madhabahu, Bwana asema hivi, Angalia, mtoto atazaliwa katika nyumba ya Daudi, JINA LAKE YOSIA; na juu yako atawachinja makuhani wa mahali pa juu, wanaofukiza uvumba juu yako, na mifupa ya watu itateketezwa juu yako. 3 Akatoa ishara siku ile ile, akasema, Hii ndiyo ishara aliyoinena Bwana, Tazama, madhabahu itapasuka, na majivu yaliyo juu yake yatamwagika. 4 Ikawa, mfalme Yeroboamu alipoyasikia maneno ya yule mtu wa Mungu, alipopiga kelele juu ya madhabahu huko Betheli, alinyosha mkono wake pale madhabahuni, akasema, Mkamateni. Basi ule mkono wake aliounyosha ukakatika, wala hakuweza kuurudisha kwake tena. 5 Madhabahu ikapasuka, majivu ya madhabahuni yakamwagika, sawasawa na ishara aliyoitoa mtu wa Mungu kwa neno la Bwana”.
1 “Na tazama, akatoka mtu wa Mungu katika Yuda kwa neno la Bwana, akafika Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa akisimama penye madhabahu, afukize uvumba.
2 Basi mtu huyo akapiga kelele juu ya madhabahu, kwa neno la Bwana akasema, Ee madhabahu, madhabahu, Bwana asema hivi, Angalia, mtoto atazaliwa katika nyumba ya Daudi, JINA LAKE YOSIA; na juu yako atawachinja makuhani wa mahali pa juu, wanaofukiza uvumba juu yako, na mifupa ya watu itateketezwa juu yako.
3 Akatoa ishara siku ile ile, akasema, Hii ndiyo ishara aliyoinena Bwana, Tazama, madhabahu itapasuka, na majivu yaliyo juu yake yatamwagika.
4 Ikawa, mfalme Yeroboamu alipoyasikia maneno ya yule mtu wa Mungu, alipopiga kelele juu ya madhabahu huko Betheli, alinyosha mkono wake pale madhabahuni, akasema, Mkamateni. Basi ule mkono wake aliounyosha ukakatika, wala hakuweza kuurudisha kwake tena.
5 Madhabahu ikapasuka, majivu ya madhabahuni yakamwagika, sawasawa na ishara aliyoitoa mtu wa Mungu kwa neno la Bwana”.
Huyu nabii alipomaliza kutoa Ishara ile akaondoka zake,..Lakini maneno yale yalisikiwa sio tu na wale waliokuwa pale, bali pia habari ile ilivuma Israeli yote, kwamba kuna mtoto atazaliwa naye ataitwa YOSIA ndiye atakayekuwa na ujasiri wa kuja kuibomoa madhabahu hiyo ya ndama iliyopo Betheli karibu na Yerusalemu, na nyingine zote, ziliyosimamishwa na Yeroboamu,..Na hatazaliwa katika Israeli ufalme wake, bali atazaliwa katika YUDA ufalme wa Daudi..
Basi pengine ilidhaniwa jambo hilo lingetokea kwa mzao aliyefuata wa mfalme wa Yuda aliyekuwa anatawala kipindi hicho, aliyeitwa Rehoboamu, lakini hakuwa huyo, wakatazamia pengine mjukuu wake, bado hakuwa huyo, wakatazamia pengine atakayefuata baada ya huyo bado haikuwa hivyo. Leo hii tukiona unabii wa Mungu unachelewa ni rahisi kusema mtu huyu si wa Mungu, hata kama Mungu alilithibitisha hilo kwa ishara kubwa kiasi gani, kitendo tu cha unabii kuchelewa basi tayari tunahitimisha kuwa yule ni nabii wa uongo….
Siku zikapita hivyo hivyo mpaka kikanyanyuka kizazi kingine kisichowajua manabii hao, Na siku zilivyokuwa zinazidi kwenda ndivyo uovu ulivyokuwa unashamiri katika Taifa ya Israeli na Yuda, mpaka enzi za mfalme Ahabu, lakini bado huyo Yosia hajulikani,..Watu wa kejeli walikuwepo, kama tu walivyo wengi sasa hivi, wanaosema huyo YESU aliyesema anarudi yupo wapi?. Wafalme 20 ishirini walipita juu ya Israeli, Yosia bado hajazaliwa…Mpaka taifa nzima linaondolewa na kuchukuliwa utumwani Ashuru, bado Yosia hajazaliwa, hapo ndipo unabii wa namna hiyo unathibitika kuwa ni batili, kwani mpaka taifa halipo tena hakuna chochote kinachoweza kutokea, hata akizaliwa leo atakuwa na faida gani…Lakini siku zilizidi kuendelea..
Miaka kama 300 baadaye tangu unabii ulipotolewa, wakati taifa la Yuda peke ndio liliobakia Israeli, mfalme mmoja aliyejulikana kama mfalme Amoni, akamzaa mtoto akamwita jina lake Yosia, mtoto huyu katika umri wa miaka 15 alianza kuutafuta uso wa Mungu kwa bidii sana, na alipofika umri wa miaka 19, alianza kusafisha, madhabahu zote za mabaali na maashera na mahali pa juu, ambazo baba zake walishindwa kufanya,.kwa muda miaka yote hiyo, alizifanya kuwa vumbi, yaani hakuacha sanamu yoyote katika Yuda, isitoshe hakuishia hapo alipanda mpaka kule Israeli ambapo sio hiyama yake, akasafisha kila madhabahu ya mabaali aliyokutana nayo njiani, aliipondoponda na kuiichoma, na alikuwa haondoki mpaka ahakikishe imekuwa jivu, akawaua wapunga pepo wote, na makuhani wao, vile vile akafukua makaburi ya makuhani wao waliokuwa wanaifukizia uvumba zamani, moja baada ya lingine, na kutoa mifupa yao, na kuisagasaga
Mpaka alipofikia kwenye kaburi moja lililokuwa kando-kando ya madhabahu zile, akaliona limekewa kumbukumbu juu yake, akaisoma, akasema hii ni kumbukumbu ya nani?..ndipo akaambiwa, hebu tusome ili tuelewe vizuri..
2 Wafalme 23:17 “Kisha akasema, Ni kumbukumbu la nani, hili ninaloliona? Na watu wa mji wakamwambia, Ni kaburi la yule mtu wa Mungu, aliyetoka Yuda, akayanena mambo hayo uliyoyatenda wewe juu ya madhabahu ya Betheli. 18 Akasema, Mwacheni; mtu awaye yote asiiondoe mifupa yake. Basi wakaiacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya yule nabii aliyetoka Samaria.”
2 Wafalme 23:17 “Kisha akasema, Ni kumbukumbu la nani, hili ninaloliona? Na watu wa mji wakamwambia, Ni kaburi la yule mtu wa Mungu, aliyetoka Yuda, akayanena mambo hayo uliyoyatenda wewe juu ya madhabahu ya Betheli.
18 Akasema, Mwacheni; mtu awaye yote asiiondoe mifupa yake. Basi wakaiacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya yule nabii aliyetoka Samaria.”
Ndipo hapo Israeli yote ikajua kumbe huyu ndiye aliyetabiriwa vile vile zamani, na Yosia akagundua kumbe Mungu alishauona wema wake tangu zamani, na kumwekea kumbukumbuku lake. Haleluya. Maandiko yanatuambia hakukuwa na mfalme aliyemwelekea Mungu kwa moyo wake wote kama ilivyokuwa kwa Yosia, Alimfanyia Mungu sherehe kubwa ambayo haikuwahi kufanywa Israeli tangu enzi za wafalme, isitoshe alikwenda kulikarabati hekalu la Mungu ambalo lilikuwa limechakazwa na wafalme waliotangulia.
2Wafalme 23:25 “Kabla ya huyo hapakuwa na mfalme mfano wake, aliyemwelekea Bwana kwa moyo wake wote, na kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na sheria zote za Musa; wala baada yake hakuinuka mmoja mfano wake yeye.”
Ndugu kanuni ya Mungu ni ile ile wala hana upendeleo biblia inasema, Mungu huwapa thawabu wale wote wamtafutao kwa bidii,(Waebrania 11:6), Na wewe pia unaweza ukawa YOSIA ya KRISTO leo, ikiwa tu utataka kumwelekea Mungu kwa moyo wako wote, kwa nguvu zako zote na kwa akili zako zote bila kujali dini yako inaamini hiki au uamini hiki, ndugu zako wanasema hivi au hawasemi hivi. Ukianza leo hakika kumbukumbu lako Bwana alishaliweka, kama hutalifahamu leo hii basi utafahamu siku ile unayomalizia mwendo kama vile YOSIA. Utakuja kugundua kuwa Mungu alishaziandika thawabu zako kabla hata hujazaliwa, kama ilivyo kwa Yosia, Hivyo habari ya Yosia ni habari ya kutupa moyo kukaza mwendo kwasababu Mungu anaijua hatima yetu na kazi zetu na bidi zetu kabla hata hatujazaliwa..
Na pia habari hii inatufundisha kuwa unabii wa Mungu alioutoa ni lazima uje kutimia haijalishi utachukua miaka mingapi, lakini ni lazima uje kutimia, hapa ulitolewa lakini ulikuja kutimia baada ya miaka 300, wakati ambao watu hawatazamii kama ungekuja kutimia, kadhalika Yesu alisema atarudi…hakika atarudi, na wala hadanganyi…Unabii huo upo karibuni sana kutimia, inaweza ikawa ni leo. Je! Umeokolewa? Wewe utakuwa ni miongoni mwa watakaoenda naye?
Kwa Maombezi, Ushauri, au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba
LAANA YA YERIKO.
MFALME ANAKUJA.
NEHUSHTANI (NYOKA WA SHABA).
NGUVU ZA ZAMANI ZIJAZO:
Tukisoma katika biblia mahali pengine Bwana alijitambulisha kama ALFA na OMEGA.
Ufunuo 22: 12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho”.
Hapo kuna vitu vitatu…1) Yeye ni Alfa na Omega…2) Yeye ni mwanzo na mwisho….3) Yeye ni wa kwanza na wa mwisho.
Hizo ni sentensi tatu zinazoelezea maumbile ya Mungu. Hebu tuzitame kwa ufupi moja baada ya nyingine.
ALFA NA OMEGA:
Tafsiri ya Alfa na Omega sio mwanzo na mwisho, kama inavyofahamika na wengi…ingekuwa ndiyo tafsiri yake hiyo, visingetenganishwa vitu vitatu hapo juu…Sasa Afla ni herufi ya kwanza kwenye alfabeti za Kingiriki..yenye alama hii (α) Na Omega ni herufi ya mwisho ya kwenye alfabeti za lugha ya kigiriki yenye alama hii (ω)…Kwenye alfabeti zetu sisi herufi ya kwanza ni (A) na ya mwisho ni (Z)….kwa kigiriki ya kwanza ndiyo hiyo alfa na ya mwisho ni omega.
Kwahiyo katika mstari huo aliposema yeye ni alfa na omega, alikuwa anajitambulisha uungu wake katika umbo la NENO. (Kumbuka hapo mwanzo kulikuwako Neno….naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa ni Mungu,…Vitu vyote vilifanyika kwa huyo wala pasipo yeye hakuna chochote kilichofanyika Yohana 1:1).
Kwahiyo akiwa katika Neno, yeye ndiye Neno la Kwanza na ndiye Neno la Mwisho, kwahiyo ili lijitambulishe lazima litumie Herufi kujitambulisha, (herufi ya kwanza na ya mwisho, alfa na Omega)… Kwanini hakutumia herufi ya A na Z?..ni kwasababu lugha zinazotumia alfabeti hizi kama vile kiingereza zilikuwa hazijazaliwa bado, na hata kama zingekuwa zimeshazaliwa bado zilikuwa ni lugha changa, kwani wakati Yohana anapewa haya maono lugha iliyokuwa kuu na uliyozungumzwa sehemu kubwa ya dunia ilikuwa ni kigiriki, hata lugha iliyotumika kuandika vitabu vingi vya agano jipya ni lugha hii, ndio maana yakatumika maneno ya kigiriki.
Yeye ni MWANZO NA MWISHO:
Sifa ya pili, Hapa Mungu anajitambulisha kwa umbo la MUDA….
Kama alivyosema mahali Fulani yeye ni UPENDO, na sio yeye ana upendo…kadhalika hapa, anajitambulisha kuwa yeye ni MWANZO na sio yeye ana mwanzo!..halikadhalika yeye ndiye MWISHO, na sio yeye mwenye mwisho…yeye hana mwanzo na wala hana mwisho, kwasababu yeye ndio mwanzo wenyewe na ndio mwisho wenyewe.
Ili uelewe vizuri hebu tafakari jambo hili: umewahi kuchunguza mwanzo wa magharibi ni upi? Au mwisho wa magharibi ni upi?…au mwanzo wa mashariki ni upi na mwisho wake ni upi?..utakuja kugundua kuwa mashariki haina mwanzo wake wala mwisho wake, vivyo hivyo na magharibi haina mwanzo wala haina mwisho, kwasababu mahali ulipo tayari panaweza kuwa ni mashariki ya mbali sana kwa sehemu nyingine halikadhalika panaweza kuwa ni magharibi ya mbali sana kutoka sehemu nyingine…kwahiyo hapo ulipo tayari ni mwanzo na mwisho wa magharibi na mashariki. Kuna mstari wanaouita kitaalamu IDL huo ndio wanasema umetenganisha mashariki na magharibi lakini kiuhalisia hakuna mstari pale…Wamebuni tu, ili kuwarahisishia kutimiza matakwa yao ya kijeografia, lakini hakuna mwanzo wa mashariki wala magharibi, ingawa kuna mashariki na magharibi..
Na ndio Mungu yupo hivyo hivyo, ingawa kuna kitu kinaitwa MWANZO na Mwisho, lakini yeye hana mwanzo, wala hana mwisho……kwasababu yeye pale alipo ndio mwanzo na ndio mwisho….Na kama vile tunavyozidi kuelekea sana mwisho wa mashariki ndivyo tunavyojikuta tunatokea mwanzo wa mashariki hiyo hiyo…kadhalika na Mungu…tunapodhani tunamjua sana na hivyo tumefika karibia na mwisho wa kumjua yeye…kumbe ndio tupo mwanzo wa kumjua yeye….Na pale tunapodhani yupo mbali sana na sisi kumbe ndio yupo karibu sana na sisi, na pale tudhaniapo kuwa tumemkaribia sana, kumbe bado sana tumfikie..Kwasababu yeye ndio mwanzo na ndio mwisho, akili zake hazichunguziki, wala hakuna mtu anayeweza kumwelezea asilimia mia na kusema sasa nimemjua Mungu.
Isaya 40:28 “Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.”
Yeye ni WA KWANZA NA WA MWISHO:
Sifa ya tatu na ya mwisho, Hapa Mungu anajifunua na kujitambulisha katika umbo la mtu…Lile Neno lililojitambulisha kwa herufi alfa na Omega, sasa linavaa mwili na kujitambulisha kama Mtu, na kusema Yeye ni wa Kwanza na wa Mwisho.
Hapa anaelezea Uungu wake kabla ya vitu vyote..Yeye alikuwepo kabla ya kiumbe chochote kile…kabla ya Malaika na kitu kingine chochote…ndiye wa Kwanza, akaitoa sehemu ya roho yake akatuumba sisi wanadamu na malaika…Na hivyo sisi wote tumetoka kwake…Na mwisho wa siku tutarudi kwake..kwasababu yote yametoka kwake..
Mungu wetu hakuna linalomshinda, wala hakuna asilolijua, utasemaje leo hakujui, wala hajui unayopitia?..huyu mwanzo na mwisho utasemaje kakusahau?..hajakusahau alisema “hata nywele za vichwa vyetu zimehesabiwa zote (Luka 12:7)”….kama anajishughulisha na mambo madogo sana ya nywele zetu atashindwaje kujishughulisha na mambo makubwa ya Maisha yetu, Hivyo kuna baraka nyingi sana katika kumwamini huyu Mungu.
Lakini pia huyu Mungu ni alfa na Omega, maneno yake ndio mwanzo na mwisho, akisema Neno lake ni lazima litimie, na halirekebishwi wala halina marekebisho…limehakikiwa na limejitosheleza, akisema roho itendayo dhambi itakufa…ni kweli itakufa, akisema mtu asipozaliwa mara ya pili hawezi kuurithi ufalme wa mbinguni…maneno yake hayo ni alfa na Omega..yatatimia kama yalivyo, akisema atakuja ni kweli atakuja..
Hivyo mpaka sasa bado anawaalika watu karamuni, je! Wewe ni mmoja wao wa walioalikwa?..kama bado unasubiri nini, usigeuke leo na kutubu? Siku ile utakuwa mgeni wa nani utakapojikuta upo kuzimu?..kumbuka hakuna nafasi ya pili kwa mtu yeyote atakayekufa katika dhambi leo,..wengi wanajifariji kuwa mbele ya kiti cha hukumu watakuwa na hoja za kujitetea, nataka nikuambie siku ile kutakuwa hakuna kujitetea…Kwasababu hakuna yeyote awezaye kumtega wala kumkamata Mungu kwa maneno.
Pia kwa Mawasiliano, Ushauri au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa +225693036618/ +225789001312
KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?
BADO KITAMBO KIDOGO HAMNIONI
UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?
Kutoka 34:29 “Hata ikawa, Musa aliposhuka katika mlima Sinai, na zile mbao mbili za ushuhuda zilikuwa mkononi mwa Musa, hapo aliposhuka katika mlima, Musa hakujua ya kuwa ngozi ya uso wake iling’aa kwa sababu amesema naye. 30 Basi Haruni na wana wote wa Israeli walipomwona Musa, tazama, ngozi ya uso wake iling’aa; nao wakaogopa kumkaribia. 31 Musa akawaita; Haruni na wakuu wote wa kusanyiko wakarudi kwake; Musa akasema nao. 32 Baadaye wana wa Israeli wote wakakaribia; akawausia maneno yote ambayo Bwana amemwambia katika mlima Sinai. 33 Na Musa alipokuwa amekwisha kusema nao, akatia utaji juu ya uso wake. 34 Lakini desturi ya Musa ilikuwa alipoingia mbele za Bwana kusema naye, kuuvua huo utaji mpaka atoke; akatoka akawaambia wana wa Israeli maneno yote aliyoambiwa. 35 Wana wa Israeli wakauona uso wa Musa ya kuwa ngozi ya uso wake Musa iling’aa; naye Musa akautia utaji juu ya uso wake tena, hata alipoingia kusema naye.”.
Kutoka 34:29 “Hata ikawa, Musa aliposhuka katika mlima Sinai, na zile mbao mbili za ushuhuda zilikuwa mkononi mwa Musa, hapo aliposhuka katika mlima, Musa hakujua ya kuwa ngozi ya uso wake iling’aa kwa sababu amesema naye.
30 Basi Haruni na wana wote wa Israeli walipomwona Musa, tazama, ngozi ya uso wake iling’aa; nao wakaogopa kumkaribia.
31 Musa akawaita; Haruni na wakuu wote wa kusanyiko wakarudi kwake; Musa akasema nao.
32 Baadaye wana wa Israeli wote wakakaribia; akawausia maneno yote ambayo Bwana amemwambia katika mlima Sinai.
33 Na Musa alipokuwa amekwisha kusema nao, akatia utaji juu ya uso wake.
34 Lakini desturi ya Musa ilikuwa alipoingia mbele za Bwana kusema naye, kuuvua huo utaji mpaka atoke; akatoka akawaambia wana wa Israeli maneno yote aliyoambiwa.
35 Wana wa Israeli wakauona uso wa Musa ya kuwa ngozi ya uso wake Musa iling’aa; naye Musa akautia utaji juu ya uso wake tena, hata alipoingia kusema naye.”.
Itakuwa hata wewe ulishawahi kugundua kitu hichi mfano ukikaa karibu na mtu ambaye amejipulizia marashi makali kwa muda mrefu, halafu ukaondoka utagundua kuwa vimelea vya yale marashi kwa sehemu Fulani vimebaki kwenye mwili wako,..Na ndivyo ilivyokuwa kuwa kwa Musa, baada ya kukaa uweponi mwa Mungu kwa muda wa siku nyingi, siku zaidi ya 80, ukijumlisha na zile 40 za Kwanza, alizokwenda kupewa amri na hukumu na zile mbao 2 za mawe, kwa wakati huo wote alipokuwa uweponi mwa Mungu kumbe kidogo kidogo utukufu wa Mungu ulikuwa unajiambukiza ndani yake pasipo yeye kujijua..Hadi siku aliposhuka chini na kuona watu wanamwogopa ndipo alipogundua kuwa Uso wake uling’aa sana kwa kule kumtazama Mungu.
Japo biblia haituambii ulikuwa unang’aa kwa namna gani hadi watu kumwogopa, lakini tunajua uling’aa kwa utukufu wa Mungu, pengine ulikuwa unameta meta kama almasi, mpaka watu wakaona huyu anaweza akawa asiwe mtu wa kawaida, pengine tukimgusa tunaweza tukafa..Ndipo Musa alipoona hivyo, akachukua utaji akaufunika uso wake, kupunguza makali ya utukufu ule, ili aweze kusimama mbele ya watu na kungumza nao.
Lakini japo uso wake uling’aa sana kwa namna ile, bado utukufu ule ulikuwa sio wa kudumu, kwasababu ulikuwa na wa kuhakisi tu, na sio kitu kilichotoka ndani yake, hivyo alipoondoka katika uwepo wa Mungu, kidogo kidogo ulikuwa unapungua hadi mwishowe ukatoweka kabisa…Japo biblia haituambii ni kwa kipindi gani utukufu huo ulidumu kwenye uso wake, pengine ulichukua siku, au wiki, au mwezi, au miezi, hatujui, lakini tunachojua ni kuwa ulikuwa ni utukufu usiodumu…Ulihitaji kuu-chaji, Na ndio maana ukisoma hapo juu utaona kila wakati Musa alipotoka kuzungumza na Mungu aliuvaa utaji ule, kwasababu utukufu wa Mungu ulijiakisi kwenye uso wake tena kwa wakati huo.
Hivyo ule utaji uliwazuia wana wa Israeli kuona hatma ya ule utukufu jinsi unavyokwisha, kwasababu Musa alikuwa anavaa utaji muda wote, Na ndio maana mtume Paulo, aliandika katika 2Wakorintho 3:13-16, kuwa hata leo hii wana wa Israeli utaji huo upo mbele yao, kwamba hawawezi kuona jinsi utukufu wake Torati ya Musa usivyokuwa wa kudumu..
“13 nasi si kama Musa alivyotia utaji juu ya uso wake, ili kwamba Waisraeli wasitazame sana mwisho wa ile iliyokuwa ikibatilika; 14 ila fikira zao zilitiwa uzito. Kwa maana hata leo hivi, wakati lisomwapo Agano la Kale, utaji uo huo wakaa; yaani, haikufunuliwa kwamba huondolewa katika Kristo; 15 ila hata leo, torati ya Musa isomwapo, utaji huikalia mioyo yao. 16 Lakini wakati wo wote watakapomgeukia Bwana, ule utaji huondolewa.”
“13 nasi si kama Musa alivyotia utaji juu ya uso wake, ili kwamba Waisraeli wasitazame sana mwisho wa ile iliyokuwa ikibatilika;
14 ila fikira zao zilitiwa uzito. Kwa maana hata leo hivi, wakati lisomwapo Agano la Kale, utaji uo huo wakaa; yaani, haikufunuliwa kwamba huondolewa katika Kristo;
15 ila hata leo, torati ya Musa isomwapo, utaji huikalia mioyo yao.
16 Lakini wakati wo wote watakapomgeukia Bwana, ule utaji huondolewa.”
Swali linakuja je! mwanadamu afanye nini ili awe na utukufu usio batilika kutoka kwa Mungu? Apate Utukufu unaodumu wakati wote?.
Jibu lipo pale pale juu, tunapaswa tusiuakisi utukufu wa Mungu, bali tugeuzwe tuwe kama yeye. Hiyo ndio dawa pekee. Kwa kuelewa zaidi angalia mfano wa mwezi na nyota, utagundua kuwa nyota siku zote zinaangaza tu, huwezi kuta zinaonekana nusu, lakini mwezi, leo utauona unaonekana wote, kesho nusu, kesho kutwa theluthi, ni kwasababu gani?, ni kwasababu wenyewe unategemea mwanga wa jua kuangaza, unalihakisi jua, lakini nyota hazihakishi chochote kutoka katika jua kwani watafiti wanasema Nyota ni ma-jua mengine, isipokuwa tu yapo mbali na dunia na ndio maana kuangaza kwa nyota hakubadiliki badiliki.
Vivyo hivyo, ili sisi tuangaze utukufu kamili wa Mungu, tunapaswa tuguezwe tuwe miungu duniani, na anayeweza kufanya hii kazi si mwingine zaidi ya YESU KRISTO mwenyewe.
Pale tunapoiamini injili kweli kweli kwa kudhamiria kumwishia Mungu, na kubatizwa katika ubatizo sahihi, tunapotubu dhambi zetu, kuanzia hapo Kristo anachofanya ni kutubadilisha asili zetu, na kuwa kama Mungu,..kuanzia huo wakati utukufu wa Mungu unakuwa unamulika ndani yetu milele NON-STOP..Kazi yako itakuwa ni kujiweka mbele zake katika hali ya utakatifu na usafi zaidi, na kulitii Neno lake, ili uzidi kuangaza kwa utukufu mwingi zaidi, hapo ndipo unapokuwa kutoka utukufu hadi utukufu, kwasababu kumbuka hata nyota zinatofautiana utukufu(1Wakorintho 15:41)..Isipokuwa tu utukufu wa zote hauwezi kuisha kabisa kama mwezi, kwasababu tayari ndani yao kuna Nuru ya jua, lakini ni wajibu wa kila mwaminio, atoke utukufu hadi utukufu.
2 Wakorintho 3:7 “Basi, ikiwa huduma ya mauti, iliyoandikwa na kuchorwa katika mawe, ilikuja katika utukufu, hata Waisraeli hawakuweza kuukazia macho uso wa Musa, kwa sababu ya utukufu wa uso wake; nao ni utukufu uliokuwa ukibatilika; 8 je! Huduma ya roho haitazidi kuwa katika utukufu? 9 Kwa maana ikiwa huduma ya adhabu ina utukufu, siuze huduma ya haki ina utukufu unaozidi. 10 Maana hata ile iliyotukuzwa haikuwa na utukufu hivi, kwa sababu ya utukufu uzidio sana. 11 Kwa maana, ikiwa ile inayobatilika ilikuwa na utukufu, zaidi sana ile ikaayo ina utukufu. 12 Basi, kwa kuwa mna taraja la namna hii, twatumia ujasiri mwingi; 13 nasi si kama Musa alivyotia utaji juu ya uso wake, ili kwamba Waisraeli wasitazame sana mwisho wa ile iliyokuwa ikibatilika; 14 ila fikira zao zilitiwa uzito. Kwa maana hata leo hivi, wakati lisomwapo Agano la Kale, utaji uo huo wakaa; yaani, haikufunuliwa kwamba huondolewa katika Kristo; 15 ila hata leo, torati ya Musa isomwapo, utaji huikalia mioyo yao. 16 Lakini wakati wo wote watakapomgeukia Bwana, ule utaji huondolewa. 17 Basi <Bwana> ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru. 18 Lakini sisi sote, kwa uso usiotiwa utaji, tukiurudisha utukufu wa Bwana, kama vile katika kioo, TUNABADILISHWA TUFANANE NA MFANO UO HUO, TOKA UTUKUFU HATA UTUKUFU, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho”.
2 Wakorintho 3:7 “Basi, ikiwa huduma ya mauti, iliyoandikwa na kuchorwa katika mawe, ilikuja katika utukufu, hata Waisraeli hawakuweza kuukazia macho uso wa Musa, kwa sababu ya utukufu wa uso wake; nao ni utukufu uliokuwa ukibatilika;
8 je! Huduma ya roho haitazidi kuwa katika utukufu?
9 Kwa maana ikiwa huduma ya adhabu ina utukufu, siuze huduma ya haki ina utukufu unaozidi.
10 Maana hata ile iliyotukuzwa haikuwa na utukufu hivi, kwa sababu ya utukufu uzidio sana.
11 Kwa maana, ikiwa ile inayobatilika ilikuwa na utukufu, zaidi sana ile ikaayo ina utukufu.
12 Basi, kwa kuwa mna taraja la namna hii, twatumia ujasiri mwingi;
13 nasi si kama Musa alivyotia utaji juu ya uso wake, ili kwamba Waisraeli wasitazame sana mwisho wa ile iliyokuwa ikibatilika;
16 Lakini wakati wo wote watakapomgeukia Bwana, ule utaji huondolewa.
17 Basi <Bwana> ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru.
18 Lakini sisi sote, kwa uso usiotiwa utaji, tukiurudisha utukufu wa Bwana, kama vile katika kioo, TUNABADILISHWA TUFANANE NA MFANO UO HUO, TOKA UTUKUFU HATA UTUKUFU, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho”.
Unaona ni faida gani, mtu aliyonayo aliyedhamiria kweli kumwamini Kristo, na sio kigeugeu,? Mtu wa namna hii hata katika ulimwengu wa roho mashetani na mapepo wanachokiona ni miale ya moto tu inapita, uchawi utampatae mtu kama huyo? Au LAANA?. Na ndio maana Shetani anachofanya sasa katika hichi kipindi cha mwisho ni kupofusha tu fikra za watu wapuuzie mambo haya ya msingi:
2Wakorintho 4:3 “Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea; 4 ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, ISIWAZUKIE NURU YA INJILI YA UTUKUFU WAKE KRISTO ALIYE SURA YAKE MUNGU.”
2Wakorintho 4:3 “Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea;
4 ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, ISIWAZUKIE NURU YA INJILI YA UTUKUFU WAKE KRISTO ALIYE SURA YAKE MUNGU.”
Mfikirie Kristo kwa jicho lingine, Yule huwa akimbadilisha mtu, anambadilisha kweli kweli, hasemi uongo kama sisi wanadamu tulivyo, Hakuja kufanya kazi ya kubahatisha duniani, kazi yake ni thabiti kabisa.
Kwa Maombezi, Ushauri au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba
+225693036618/ +255789001312
DHAMBI ZINAZOTANGULIA NA ZINAZOFUATA.
MADHAIFU
WATU WASIOJIZUIA.
UNAFANYA NINI HAPO?
Karibu katika mwendelezo wa vitabu vya Biblia, leo tutaendele na vitabu 4 vya mbele, yaani Wafalme wa kwanza (1Wafalme), na Wafalme wa Pili (2Wafalme), Mambo ya nyakati wa kwanza (1Nyakati) na Mambo ya nyakati wa pili(2 Nyakati).. Tumekwisha pitia vitabu 10 vya kwanza, hivyo ni vizuri kama hujapitia maelezo ya vitabu vilivyopita, ukavipitia kwanza ili tuende pamoja katika hivi vitabu vinavyofuata.
Kitabu cha Wafalme wa kwanza na Wafalme wa Pili, kilikuwa ni kitabu kimoja, isipokuwa kiligawanywa katika sehemu mbili…Na mwandishi wa kitabu hichi alikuwa ni Nabii Yeremia. Ingawa Nabii Yeremia alizaliwa mwishoni kabisa mwa enzi za Wafalme lakini aliweza kukusanya rekodi zote za habari za Wafalme, kwani habari za kila mfalme na matendo yake zilikuwa zinarekodiwa na kuhifadhiwa kwenye vitabu maalumu vinavyojulikana kama vitabu vya Tarehe.
Lakini kwa ufupi Kitabu hivi viwili vya wafalme kama jina lake lilivyo, vinazungumzia Utawala wa wafalme wa Israeli, Na vitabu viwili vinavyofuata vya (1 Nyakati na 2 Nyakati) Ni marudio ya habari hizo hizo za Wafalme isipokuwa yana habari chache chache sana ambazo hazikurekodiwa katika kitabu cha wafalme…Ni sawa na injili iliyoandikwa na Mathayo na Luka ni vitabu viwili vilivyoandikwa na waandishi wawili tofauti lakini vyote vinazungumzia habari moja..ndivyo ilivyo kitabu cha Wafalme na Mambo ya nyakati, vyote vinaelezea habari moja za Wafalme wa Israeli…isipokuwa hichi cha mambo ya nyakati kimeanzia nyuma kidogo, kwa mfalme Daudi. Na mwandishi wa kitabu cha Mambo ya Nyakati alikuwa ni EZRA..ambaye ndiye aliyekiandika kitabu cha Ezra pia..Huyu alikuwa ni mwandishi..ambaye habari zake tutakuja kuziona tutakapofika katika kitabu cha Ezra..
Sasa tukirudi katika habari za Wafalme..kumbuka haukuwa mpango wa Mungu, Israeli wawe na Mfalme juu yao tangu mwanzo, lakini kwasababu ndio ilikuwa nia yao kukataa uongozi wa Mungu, usiohusisha mwanadamu, Mungu akawapa haja ya mioyo yao, lakini pamoja na hayo hakuwaacha…tofauti na sisi wanadamu, mtu asipofanya tunavyotaka tunamtupa moja kwa moja, hatutaki hata kumsikia tena, lakini kwa Mungu haipo hivyo, hakuwatupa Israeli watu wake moja kwa moja ingawa walimuasi…Hivyo Mungu akatengeneza njia ya kuwaokoa kwa kupitia hao hao wafalme waliowataka…
Kwahiyo kitabu cha Wafalme wa Kwanza, kinaanza na Mfalme Sulemani, ambaye alikuwa ni mfalme wa tatu wa Israeli akitanguliwa na Sauli na Daudi ambao habari zao utazipata katika vitabu vya Samweli. Sulemani alikuwa ni mwana wa Daudi, na mama yake alikuwa ni yule mke wa Uria, ambaye Daudi aliyemtamani..Hivyo baadaye Mungu alikuja kumfanyia wema mwanamke yule na kumfanya mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli, Sulemani alitawala miaka 40 katika Israeli, alianza vizuri lakini hakumaliza vizuri, kwani pamoja na Hekima yote na ufahari wote aliopewa na Mungu alikuja kukengeuka dakika za mwisho, na kwenda kuoa wanawake wa kigeni, ambao Mungu alimkataza asioe, (Nehemia 13:25-26 )na hao wanawake wakamgeuza moyo akaenda kutengenezea maashera hiyo miungu migeni, ambayo ni machafuko makubwa sana mbele za Mungu, Ingawa alikuja kutubu dakika za mwisho, na Bwana alimsamehe lakini tayari alikuwa ameshaisababishia Israeli madhara makubwa sana..
Sasa kabla ya kwenda kwenye madhara aliyoisababishia Israeli, tutazame jambo moja jema na kuu alilolifanya.; Tunaona baada ya kufa baba yake, yeye ndiye aliyekuwa na dhamana ya kumtengenezea Mungu nyumba, biblia inasema Mungu hakai kwenye nyumba zilizotengenezwa na mikono, lakini pamoja na Daudi kulifahamu hilo bado alilazimisha kumjengea Mungu nyumba hivyo hivyo, na Mungu akaliona hilo akapendezwa naye na kumbariki, na kuuchagua mji wake na kabila lake kuwa makao makuu ya kuweka jina lake, japo Mungu alimzuia Daudi asimjengee kwasababu alimwaga damu nyingi, hivyo mwanawe ambaye ni Sulemani ndiye atakayejenga HEKALU kwa niaba yake. Na wakati ulipowadia Sulemani alimjengea Mungu hekalu, alitumia akili nyingi, na hekima nyingi kuijenga ile nyumba…
Alikwenda kutafuta miti maalum na ya thamani kutoka nchi za mbali, na vito maalumu kutoka kila kona ya dunia, na kuileta Israeli, Zaidi alikwenda kutafuta watu wenye akili nyingi, kutoka mataifa mengine kusaidia kuongeza ujuzi katika ujenzi, kwahiyo Hekalu lilijengwa kwa gharama kubwa na kwa ujuzi wa hali ya juu, kulikuwa hakuna mfano wake duniani kote. Na lilitengenezwa Yerusalemu, katika mji wa kabila la Yuda, hakukusikika kelele yoyote wakati wa ujenzi, hivyo ilipunguza hata kasi ya maadui, kuvamia kwasababu hakuna mtu aliyekuwa anaelewa kitu kinachoendelea ndani..wengi walidhani kazi imesimama tu!..lakini ilikuwa inaendelea ndani kwa ndani…ghafla wanakuja kushangaa nyumba hii hapa imekamilika!..Sasa inawekwa wakfu kwa Mungu.
Mungu akalibariki Taifa la Israeli na Mfalme, kwa jambo hilo, na kukawa na amani kwa Zaidi ya miaka 40, lakini Sulemani alipokuwa mzee akakengeuka, na hivyo Mungu hakupendezwa naye tena, hakumwua lakini alimnyang’anya sehemu ya Ufalme wake, kwani hapo kwanza alikuwa anatawala makabila yote 12, kama Sauli na Daudi walivyokuwa wanatawala, lakini matokeo yake akapokonywa 10 akabakiwa na mawili tu, yaani kabila la Benyamini pamoja na kabila lake mwenyewe Yuda…lakini hakunyakang’anywa kwenye utawala wake bali wa mwanae.
1 Wafalme 11:1 “Mfalme Sulemani akawapenda wanawake wengi wageni, pamoja na binti yake Farao, wanawake wa Wamoabi, na wa Waamoni, na wa Waedomi, na wa Wasidoni, na wa Wahiti, 2 na wa mataifa Bwana aliyowaambia wana wa Israeli, Msiingie kwao, wala wasiingie kwenu; kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu kuifuata miungu yao. Sulemani akaambatana nao kwa kuwapenda. 3 Akawa na wake mia saba binti za kifalme, na masuria mia tatu; nao wakeze wakamgeuza moyo. 4 Maana ikawa, Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine, wala moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake. 5 Kwa kuwa Sulemani akamfuata Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni na Milkomu, chukizo la Waamoni. 6 Sulemani akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wala hakumfuata Bwana kwa utimilifu, kama Daudi baba yake. 7 Sulemani akamjengea Kemoshi, chukizo la Wamoabi, mahali pa juu, katika mlima uliokabili Yerusalemu, na Moleki, chukizo la wana wa Amoni. 8 Na kadhalika ndivyo alivyowafanyia wake zake wa nchi za kigeni, waliofukiza uvumba, wakawatolea miungu yao dhabihu. 9 Basi Bwana akamghadhibikia Sulemani kwa sababu moyo wake umegeuka, naye amemwacha Bwana, Mungu wa Israeli, aliyemtokea mara mbili, 10 akamwamuru katika habari ya jambo lilo hilo asifuate miungu mingine; lakini yeye hakuyashika aliyoyaamuru Bwana. 11 Kwa hiyo Bwana akamwambia Sulemani, Kwa kuwa umefanya hayo, wala hukuyashika maagano yangu, na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme usiwe wako, nami nitampa mtumishi wako. 12 Walakini katika siku zako sitafanya haya, kwa ajili ya Daudi baba yako; nitaurarua utoke katika mkono wa mwana wako. 13 Lakini sitauondoa ufalme wote pia; nitampa mwana wako kabila moja, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, na kwa ajili ya Yerusalemu niliouchagua”
1 Wafalme 11:1 “Mfalme Sulemani akawapenda wanawake wengi wageni, pamoja na binti yake Farao, wanawake wa Wamoabi, na wa Waamoni, na wa Waedomi, na wa Wasidoni, na wa Wahiti,
2 na wa mataifa Bwana aliyowaambia wana wa Israeli, Msiingie kwao, wala wasiingie kwenu; kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu kuifuata miungu yao. Sulemani akaambatana nao kwa kuwapenda.
3 Akawa na wake mia saba binti za kifalme, na masuria mia tatu; nao wakeze wakamgeuza moyo.
4 Maana ikawa, Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine, wala moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake.
5 Kwa kuwa Sulemani akamfuata Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni na Milkomu, chukizo la Waamoni. 6 Sulemani akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wala hakumfuata Bwana kwa utimilifu, kama Daudi baba yake.
7 Sulemani akamjengea Kemoshi, chukizo la Wamoabi, mahali pa juu, katika mlima uliokabili Yerusalemu, na Moleki, chukizo la wana wa Amoni.
8 Na kadhalika ndivyo alivyowafanyia wake zake wa nchi za kigeni, waliofukiza uvumba, wakawatolea miungu yao dhabihu.
9 Basi Bwana akamghadhibikia Sulemani kwa sababu moyo wake umegeuka, naye amemwacha Bwana, Mungu wa Israeli, aliyemtokea mara mbili,
10 akamwamuru katika habari ya jambo lilo hilo asifuate miungu mingine; lakini yeye hakuyashika aliyoyaamuru Bwana.
11 Kwa hiyo Bwana akamwambia Sulemani, Kwa kuwa umefanya hayo, wala hukuyashika maagano yangu, na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme usiwe wako, nami nitampa mtumishi wako.
12 Walakini katika siku zako sitafanya haya, kwa ajili ya Daudi baba yako; nitaurarua utoke katika mkono wa mwana wako.
13 Lakini sitauondoa ufalme wote pia; nitampa mwana wako kabila moja, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, na kwa ajili ya Yerusalemu niliouchagua”
Hivyo hayo yote yalitokea wakati wa utawala wa mtoto wake Rehoboamu, na kuanzia huo wakati Israeli ikagawanyika sehemu mbili, kaskazini na kusini, upande wa kusini ndio huo uliokuwa na makabila mawaili (yaani Yuda na Benyamini) na upande wa kaskazini (makabila 10 yaliyosalia). Hivyo kaskazini wakawa na mfalme wao na Kusini wakawa na Mfalme wao…
Kaskazini PAKAITWA ISRAELI na kusini PAKAITWA YUDA. Hivyo Israeli ambayo hapo kwanza ilikuwa ni taifa moja ikagawanyika na kuwa mataifa mawili ndani ya Taifa moja…kutokana na dhambi ya Sulemani.
Hayo ndio madhara ya dhambi aliyoyaleta Sulemani, na ndio madhara ya dhambi, unaweza ukasema nikitenda dhambi fulani itaniathiri mimi peke yangu, haitawahusu wengine, nataka nikuambie ndugu, ukiwa mwamini ukifanya dhambi yoyote ya makusudi haitakuathiri wewe peke yako bali itaathiri na wengine na Zaidi ya yote itaathiri kazi ya Mungu, kwasababu jina la Mungu litatukanwa kwa ajili yako.
Baada tu ya Israeli kugawanyika katika sehemu hizo mbili, hapo ndio ikawa sehemu nyingine ya chanzo cha machafuko, watu waliokuwa wanakaa kaskazini (yaani yale makabila 10) yakaacha kabisa kumcha Mungu wa Israeli kama hapo kwanza kwasababu mfalme wao wa kwanza anayeitwa Yeroboamu aliwatengenezea sanamu ya ndama, waiabudu kama Mungu wao badala ya Mungu wa Israeli..hivyo ikawa ni machafuko makubwa zaidi, wakawa hawana tofauti na watu wa Mataifa.
Na yale makabila mawili yaliyosalia ambayo yalikuwa kusini angalau kidogo watu waliokuwa wanakaa kule walikuwa wanamwogopa Mungu ingawa si sana, na walikuwa wanamcha Mungu kwasababu tu Hekalu la Mungu lilikuwa huko nchini kwao Yuda, hiyo kidogo ikawafanya wawe na hofu ya Mungu. Lakini na wao pia wakaja kukengeuka baadaye…Hivyo mataifa haya mawili ndani Taifa moja yakawa na kila moja na mfalme wake, na itikadi zake, ingawa walikuwa wanatambuana kama ndugu, na hakukuwa na Mfalme mmoja kwa mataifa yote mawili, hapana kila moja lilikuwa na mfalme wake kuanzia huo wakati na kuendelea.
Walipita Wafalme karibia 20 katika Israeli ( yaani upande wa kaskazini)…lakini wote walifanya machukizo mbele za Mungu, kila aliyekuja alikuwa anafanya mabaya kuliko aliyemtangulia…Na miongoni mwa wafalme waliofanya mabaya sana ni Mfalme Ahabu ambaye alikuwa na mke wake aliyemtoa nchi za mataifa, ambaye alikuwa ni mchawi, aliyeitwa Yezebeli, hawa waliichafua Israelli kwa kiwango cha juu sana…Mpaka ikafika kipindi Bwana akaileta huduma ya Eliya duniani, na lengo la huduma ya Eliya ilikuwa ni KUWAREJESHA WANA WA ISRAELI WAMRUDIE MUNGU WAO. Mungu alitumia ishara nyingi katika huduma ya Eliya ili kuwarejesha wamgeukie yeye…(kwa maelezo marefu juu ya huduma hii ya Eliya tutumie ujumbe inbox tukutumie )…wachache wakawa wanatii na kugeuka lakini wengi wakawa hawatii..
Na katika Yuda pia walikuwa wanatumiwa manabii wengi, lakini angalau Yuda kidogo watu walikuwa si wagumu kama Israeli..Kwani kulikuwa kuna Wafalme katika Yuda ambao walikuwa wanamtii Mungu na kumheshimu kama alivyofanya Daudi, mfano wa wafalme hao alikuwepo mfalme Hezekia, na Mfalme Yosia hawa walikwenda katika njia za Mungu katika ukamilifu wote, hivyo katika vipindi vya utawala wao Mungu aliwabariki na kuwaepushia madhara,… Manabii wote tunaowasoma katika Biblia, kuanzia Eliya, Elisha, Habakuki, Isaya, Hosea, Nahumu, Yona, Amosi, Yeremia, Obadia, Habakuki, Mika n.k wote hawa walitokea kipindi hichi cha Wafalme kasoro nabii Danieli, Hegai, zekaria pamoja na Malaki hawa walitokea baada ya Isreali kutawanyishwa…
lakini hao wengine Walikuwa wanatumwa kuwaonya wana wa Israeli na wana wa Yuda pamoja na wafalme wao wamgeukie Mungu…Unapopitia kitabu hichi ili upate picha vizuri, ni vyema ukapitia pia vitabu vya manabii, uone Bwana alivyokuwa anawaonya Israeli kwa nguvu, na jinsi gani alivyokuwa anawatabiria kuwa watakwenda utumwani Babeli wasipotubu..Kwa muda wako soma kitabu cha Yeremia, Hosea, Nahumu, Isaya utayaona mambo hayo kwa urefu, …
Kwa miaka mingi Zaidi ya 400, walikuwa wanatumiwa manabii wa kuwarejesha lakini ni wachache tu ndio waliokuwa wanatii na kugeuka, hivyo uvumilivu wa Mungu ukafika kikomo, kukawa hakuna tena msamaha, Mungu akaamua kuwatoa Waisraeli wote kutoka katika nchi yao waliyopewa na Mungu, waliokuwa wanakaa upande wa kaskazini, yaani Israeli (yale makabila 10)..yalichukuliwa utumwani kwenda nchi inayoitwa ASHURU, na wale waliokuwa wanakaa kusini (yaani Yuda) baada ya miaka 125 mbeleni nao pia walichukuliwa na kupelekwa utumwani BABELI,..wao hawakuchukuliwa kipindi kimoja na Israeli kwasababu angalau kwao kulikuwa na hofu ya Mungu kuliko Israeli, lakini baadaye nao pia wakakengeuka kama Israeli na kuchukuliwa mpaka Babeli…Nchi ya Ahadi ikabaki nyeupe!! Wakaletwa makafiri wakaishi huko kwa niaba yao, nchi ya Israeli ikakaliwa na makafiri. Yuda Wakapelekwa utumwani miaka 70..
2 Nyakati 36:14 “Na zaidi ya hayo wakuu wote wa makuhani, na watu, wakakosa mno sawasawa na machukizo yote ya mataifa; wakainajisi nyumba ya Bwana aliyoitakasa katika Yerusalemu. 15 Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu ALIWAHURUMIA WATU WAKE, NA MAKAO YAKE; 16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, HATA ILIPOZIDI GHADHABU YA BWANA JUU YA WATU WAKE, HATA KUSIWE NA KUPONYA. 17 Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mkongwe; akawatia wote mkononi mwake. 18 Na vyombo vyote vya nyumba ya Mungu, vikubwa kwa vidogo, na hazina za nyumba ya Bwana, na hazina za mfalme, na za wakuu wake; vyote pia akavileta Babeli. 19 Wakaiteketeza nyumba ya Mungu, wakaubomoa ukuta wa Yerusalemu, wakayateketeza kwa moto majumba yake yote, wakaviharibu vyombo vyake vyote vya thamani. 20 Na wale waliookoka na upanga akawachukua mpaka Babeli; wakamtumikia yeye na wanawe hata kulipoingia milki ya Uajemi; 21 ili kulitimiza neno la Bwana kwa kinywa cha Yeremia, hata nchi itakapofurahia sabato zake; kwa maana siku zote ilipokaa ukiwa ilishika sabato, kutimiza miaka sabini.”
2 Nyakati 36:14 “Na zaidi ya hayo wakuu wote wa makuhani, na watu, wakakosa mno sawasawa na machukizo yote ya mataifa; wakainajisi nyumba ya Bwana aliyoitakasa katika Yerusalemu.
15 Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu ALIWAHURUMIA WATU WAKE, NA MAKAO YAKE;
16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, HATA ILIPOZIDI GHADHABU YA BWANA JUU YA WATU WAKE, HATA KUSIWE NA KUPONYA.
17 Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mkongwe; akawatia wote mkononi mwake.
18 Na vyombo vyote vya nyumba ya Mungu, vikubwa kwa vidogo, na hazina za nyumba ya Bwana, na hazina za mfalme, na za wakuu wake; vyote pia akavileta Babeli.
19 Wakaiteketeza nyumba ya Mungu, wakaubomoa ukuta wa Yerusalemu, wakayateketeza kwa moto majumba yake yote, wakaviharibu vyombo vyake vyote vya thamani.
20 Na wale waliookoka na upanga akawachukua mpaka Babeli; wakamtumikia yeye na wanawe hata kulipoingia milki ya Uajemi;
21 ili kulitimiza neno la Bwana kwa kinywa cha Yeremia, hata nchi itakapofurahia sabato zake; kwa maana siku zote ilipokaa ukiwa ilishika sabato, kutimiza miaka sabini.”
Mstari wa 16, unasema “lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, HATA ILIPOZIDI GHADHABU YA BWANA JUU YA WATU WAKE, HATA KUSIWE NA KUPONYA”.
Ndugu katika vitabu hivi tunajifunza kuwa..kuna wakati unafika ghadhabu ya Mungu, itajaa hata kusiwe na kuponya, wewe unayesema Mungu anakawia, wewe unayedharau na kuidhihaki na kuicheka injili leo, na kuwacheka na kuwafanyia mizaha watu wa Mungu, siku inakuja ambapo utalia na kutakuwa hakuna msaada, siku ya ghadhabu ya Mungu inakuja! Usidanganywe na watu wanaosema kuwa Mungu hawezi kuangamiza dunia, au hakuna mwisho wa dunia, ndugu watu wa kipindi cha Nuhu ndio walikuwa wanasema hivyo hivyo…lakini ghafla tu walishangaa siku moja mbingu zimefunga, zimekuwa nyuesi……Jiepushe na ghadhabu ya Mungu, Uvumilivu wa Mungu ni kukufanya wewe utubu, umgeukie Mungu, tubia uasherati wako, rushwa zako, utukanaji wako, usengenyaji wako, na kutokusamehe kwako…Wema wa Mungu unakuvuta leo kwasababu hataki upotee soma tena mstari wa 15 unasema…
“15 Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu ALIWAHURUMIA WATU WAKE, NA MAKAO YAKE; ”
Ni mara ngapi asubuhi na mapema umekutana na mahubiri, kwenye redio, kwenye Tv, mitandaoni, mitaani au hata sehemu zako za kazi?..Usipuuze unaposikia injili unayopewa bure pasipo hata kulipia hata sh. Moja..siku ile utakosa cha kujitetea..
Kuna wakati mlango wa rehema utafungwa, ambapo utatamani kutubu utashindwa: Wana wa Israeli walilia na kuomboleza, siku ile wanapochukuliwa mateka, lakini Mungu hakusikia chochote. Ndivyo itakavyokuwa kwa wale wanaochezea neema sasa.
Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze. 25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako; 26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu. 27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu. 28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje.”
Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.
25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;
26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.
27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.
28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno,
mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje.”
Hivyo unachopaswa kufanya ni kutubu hapo ulipo kwa kudhamiria kuacha dhambi zako, na kwenda kutafuta ubatizo sahihi kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako, ubatizo sahihi ni wa kuzamishwa mwili wote na kwa jina la Yesu Kristo kulingana na Matendo 2:38, na Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu.
Hakikisha unakisoma vitabu hivi mwenyewe, usiache kipengele hata kimoja, kwasababu ni habari zinazoeleweka na zimewekwa katika mfumo mrahisi wa kueleweka, haihitaji ufafanuzi sana kukielewa. Hapa tunajaribu kukupa picha tu, ili kukusaidia wewe mwenyewe kuvisoma vitabu hivyo kiurahisi, Hivyo tumia muda wako mwingi kuvisoma peke yako, Na Mungu atakufunulia mengi zaidi…
Usikose mwendelezo, na Pia washirikishe wengine habari njema..
Kwa mwendelezo >>> VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 6
Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312
Mada Nyinginezo:
BIDII YA MFALME YOSIA.
KITABU CHA YASHARI KINACHOZUNGUMZIWA KATIKA 2SAMWELI 1:17-18, NI KITABU GANI?
NABII ELISHA ALIKUWA ANA MAANA GANI KULIA NA KUSEMA”GARI LA ISRAELI NA WAPANDA FARASI WAKE”?
ROHO YA ELIYA KATIKA AGANO JIPYA INATENDAJE KAZI?
SAUTI NYUMA YA ISHARA.
KANUNI JUU YA KANUNI.
Mambo yote ambayo biblia imeyataja kama vile, kutazama bao(utambuzi), kubashiri, kuloga kwa kupiga mafundo. Kupandisha pepo/kupunga pepo, kuomba kwa wafu, kusihiri n.k. Yote haya kwa ufupi tunaweza kuyaweka katika kundi moja linalojulikana kama uchawi.
Na kazi hii imehasisiwa na shetani mwenyewe, baada ya kuona kuna upungufu wa taarifa Fulani za muhimu zimuhusuzo mwanadamu. na huku wanadamu wanao kiu ya kuzijua. ndipo hapo akabuni kitu kinachoitwa uchawi. Ni sawa na leo hii uone kisima kinachimbwa kijijini kwenu. Moja kwa moja utagundua kuwa ni kwasababu ya ukosefu au upungufu wa maji na ndio maana kisima kimekuja kuchimbwa.
Vivyo hivyo na Shetani naye, aliuleta uchawi baada ya kuona kuna taarifa Fulani zimuhusuzo mwanadamu zimekosekana au zimefichwa. Na aliyezificha ni Mungu mwenyewe kwa makusudi yake maalumu. ili wanadamu na viumbe vyake vyote viishi kwa kumtegemea yeye. Na si kwa kutegemea nguvu zao au akili zao.
Jambo hili lilimkasirisha shetani tangu mwanzo, na ndio maana aliasi ili ajitawale mwenyewe. Lakini alipoona ameshindwa kujua hata chanzo na mwisho wa maisha yake mwenyewe akaamua mawazo yake maovu ayalete kwa wanadamu kwa njia hiyo ya uchawi.
Hivyo uchawi wa kwanza aliouleta, ulianzia pale Edeni, Mungu alipomweka Adamu na Hawa. Akawaagiza na kuwaambia wale matunda ya kila mti lakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya wasile. kwasababu siku watakapokula, watakufa. Lakini tunamwona shetani akitokea ndani ya nyoka, Na kuanza kumwambia Hawa, Hakika hamtakufa…”Hilo Neno Hakika hamtakufa” Ndio Mwanzo wa siri za uongo, na vitu kama hivyo mwanadamu sikuzote anapenda kusikia,.akaendelea na kusema, kwasababu Mungu anajua siku mtakapokula mtafumbuliwa macho na kuwa kama Mungu: Mkijua mema na mabaya..
Unaona Yaani hapo shetani alikuwa anawafunulia siri kuu sana, kama tunavyojua mtu aliyefikia hatua ya kutambua mema na mabaya ni mtu aliyepevuka akili anaweza kujiongoza mwenyewe. na kujiamulia mambo yake mwenyewe,..Hivyo shetani hapo alikuwa anawaaminisha kuwa watakapoasi na kula tunda, basi watakuwa na uwezo wa kupanga na kuchagua juu ya maisha yao, bila msaada wowote wa Mungu. vile vile wanaweza kuamua lolote wajisikialo, huyu Mungu wa nini tena?..hawezi kuwaambia chochote kwani yeye ni nani?…Hivyo Hawa akavutiwa sana na taarifa hizo mpaka akadhubutu kufanya kile kitendo kiovu . Ambacho matokeo yake ndio tunayaona hadi sasa.
Na jambo hilo hilo shetani aliendelea kulileta ndani ya watu, kwa vizazi na vizazi watu wakiwa na tama ile ile kujua hatma za maisha yao zitakuwaje na huku hawataki kumwangalia Mungu. Shetani anapata nafasi ya kuwadanganya kwa elimu zake za uongo, za utazamaji nyota.
Anawadanganya kuwa kuwa alama za mikono zimebeba siri za maisha yao, anawadanganya miti Fulani au majani, ukiyapaka, au ukiyachanganya na vitu Fulani wataona mafanikio ya maisha yao. Na mambo chungu nzima,..huku anafahamu kabisa anayejua hatma ya maisha ya mwanadamu na mambo yake yote si mwingine zaidi ya Mungu lakini kwasababu watu hawamtaki Mungu. hivyo yeye anafanya hivyo kwa lengo moja tu, kuzidi kuwafanya watu wazidi kupoteza uelekeo wao kwa Mungu, ili awavute kwake, na wakishakita mizizi kwake, basi awaangamize waishie jehanum.
Sasa unaweza ukauliza lakini mbona kweli mganga Fulani, aliniambia kila ikifika mwezi wa 6 niwe ninavaa gauni jekundu. Kwasababu nyota yangu ya mafanikio ipo hapo, inaniagiza hivyo? na kweli nimekuwa nikivaa na kuona mafanikio makubwa katika huo mwezi.
sasa wewe unapokwenda pale kwa mara ya kwanza, au unapomsikiliza kwenye TV. Na kutii maagizo yake, kuvaa hilo gauni jekundu alilokuambia huo mwezi. Anachofanya ni anaagiza tu mapepo yake, kukufanyia wewe kazi unapofika huo mwezi wa 6. Na ndio hapo unaweza kuona kama ni wateja wako wanaongezeka, au kitu Fulani kinafanikiwa kirahisi katika huo mwezi..Lakini huo ni mtego wa awali anafanya hivyo kwako kwa mara ya kwanza ili umwamini yeye.
Na kwa namna ya kawaida mtu akishaona kafanikiwa atarudi tena kwa Yule mganga au msoma nyota aliyempa yale maagizo. Ashuhudie aombe msaada zaidi,.ndipo atapewa tena masharti mengi ya ziada. kwa kuahidiwa kuwa ili nyota yake ifanye kazi kiufasaha zaidi, anapaswa akapigiwe ramli nyumbani kwake, au alale chooni hicho kipindi. Na mambo ya ajabu ajabu mengi, na yeye atafanya. kwasababu alishaona mafanikio hapo mwanzo, baada ya muda tena aturudi kupewa maagizo mengine. Ataambiwa sasa atoe kafara ya mtoto wake ili kusafisha nyota, asipofanya hivyo wazee wa nyota yake watakasirika na hivyo atakufa, ataenda kufanya kwa woga.
Hivyo hivyo kesho kutwa tena ataambiwa tena, apae na ungo waende Jupita kuitembelea nyota yake, atapaa na ungo. siku moja atakasirishwa na jirani yake na ataenda kutafuta msaada na atapewa uwezo wa kumdhuru mtu (kuloga). mpaka mwisho wa siku anajikuta amekuwa mchawi mashuhuri. Na yeye anakuwa mganga wa kuwafundisha wengine mambo hayo. Na mtu huwa akishafikia hatua kama hizo kurudi tena ni Neema ya Kristo. Wengi wanafia huko, ninaweza kusema asilimia 99 wanafia kwenye uchawi… na kuishia motoni.
Leo hii utaona katika magazeti vipengele wanavyoviita NYOTA ZETU. kaa mbali na hayo mambo wala usisome, ni mtego wa ibilisi, anataka ukakijaribu kile kilichoandikwa pale, wala usidhubutu,kwasababu kweli anaweza kukuletea majibu chanya kutokana na kile ulichokisoma pale, lakini kumbe unaelekea shimoni.
Ndugu Ukweli wa maisha yetu upo mikononi mwa Mungu peke yake. Ikiwa utapenda kufahamu chochote kuhusu maisha yako ni heri ukapiga magoti na kumwomba akufunulie. Akikufunulia ni sawa asipokufunulia ni sawa vile vile ishi maisha ya amani ukijua kabisa wote waliomtumaini yeye watakuwa salama mikononi mwake…Pia hatima yetu imeandikwa kwenye Neno lake. Ukilisoma vizuri na kulielewa basi utakuwa umejua hatima ya Maisha yako. Njia za haraka haraka na za mkato kujua kesho yako itakuwaje, au za kutaka kujua ni nini kinaendelea kukuzunguka. Au za kutafuta mali za ghafla ziogope! Shetani kaweka mitego kila mahali.
Mungu aliwaonya sana wana wa Israeli juu ya jambo hili watakapofika nchi ya Kaanani.
Wasidhubutu mambo hayo, kwasababu hayo ndiyo yaliyomkasirisha Mungu mpaka wakaondolewa wale wenyeji wa Kaanani..
Kumbukumbu 18:10 “Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri. 11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu. 12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako. 13 Uwe mkamilifu kwa Bwana, Mungu wako. 14 Maana mataifa haya utakaowamiliki huwasikiliza wanaoshika nyakati mbaya na kutazama bao; bali wewe, Bwana, Mungu wako, hakukupa ruhusa kutenda hayo.’’
Kumbukumbu 18:10 “Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri.
11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.
12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.
13 Uwe mkamilifu kwa Bwana, Mungu wako.
14 Maana mataifa haya utakaowamiliki huwasikiliza wanaoshika nyakati mbaya na kutazama bao; bali wewe, Bwana, Mungu wako, hakukupa ruhusa kutenda hayo.’’
Ndugu kama ulishawahi kujaribu mambo yoyote katika hayo. Tubu sasa, uombe rehema Mungu atakusamehe na uanze sasa kumfanya Mungu kuwa tumaini lako. Na yeye mwenyewe ndiye atakayekuongoza katika njia salama. Kwasababu hukumu ya Mungu ipo juu ya watu wote wanaojaribu kusikiliza mafundisho ya mashetani.
Malaki 3:5 “Nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami nitakuwa shahidi mwepesi juu ya wachawi,”
Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi. na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.”
Ubarikiwe sana.
Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba
+225693036618/ +225789001312
HADITHI ZA KIZEE.
MAFUNDISHO YA MASHETANI
JE!MUNGU ANAWEZA KULETA MAJIBU KUPITIA NGUVU ZA GIZA KAMA TUNAVYOSOMA NABII SAMWELI KUPATA MAJIBU KWA MWANAMKE MCHAWI?
Shalom! Karibu tujifunze Biblia..
Haruni alikuwa ni kaka yake Musa, waliozaliwa tumbo moja…isipokuwa Haruni alikuwa ni Mkubwa kwa Musa kwa miaka 3, Lakini Bwana alimchagua Musa kubeba kusudi lake la kuwatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya Misri kuelekea Kaanani…Na biblia inasema Mungu alimchagua Haruni kaka yake Musa kuwa kama Nabii wa Musa…Na pia walikuwa na dada yao aliyeitwa Miriamu ambaye naye pia alikuwa ni Nabii (Kutoka 7:1).
Lakini haikuishia hapo, Mungu alilifanya kabila la Musa kuwa kabila la kikuhani,(Kabila la LAWI) na alimchagua Haruni kaka yake Musa, baadaye kama Kuhani Mkuu wa kwanza katika Israeli’’.
Na wote wawili hawa, Musa na Haruni Mungu alikuwa anatembea nao kwa namna ya kipekee sana, na wote walipewa mamlaka Fulani na Mungu. Lakini kama ukijifunza Biblia kwa makini utaona, Mungu alitembea na Musa sana kwa kutumia ile fimbo aliyokuwa nayo kule nyikani aliyokuwa anaitumia kuchungia kondoo za Mkwe wake (aliyeitwa Yethro) baada ya kumkimbia Farao zamani..Fimbo ambayo alikuwa anatumia kuchungia mifugo ilikugeuka baadaye kuwa fimbo ya kuwachunga wana wa Israeli, na fimbo ya adhabu kwa Farao.
Sasa hii fimbo mara ya kwanza ilikuwa ni ya Musa, na ilikuwa ni ya kwake tangu akiwa kwa Yethro, lakini baada ya Musa, kutomwamini Mungu na kuanza kujitetea kwamba yeye si msemaji, ndipo Mungu akamfanya Haruni awe anazungumzaji kwa niaba yake, …na ile fimbo akapewa Haruni kwasababu yeye ndiye atakayekwenda kufanya zile ishara zote mbele ya Farao kwa niaba ya Musa, kwahiyo ile fimbo ikaitwa FIMBO YA HARUNI. Ndio ile ile fimbo iliyogeuka nyoka mbele ya Farao, na kuwameza wale nyoka wa Farao, na ndio ile ile fimbo iliyogeuza maji yote ya Misri kuwa Damu.(Kutoka 7:19),na ndiyo ile ile iliyogeuza mavumbi kuwa chawa, na ndio iliyoigawanya bahari ya Shamu ili wana wa Israeli wapite na ndiyo iliyoifunga bahari ya Shamu ili Jeshi la Farao liangamie n.k
Sasa ilikuwa ni fimbo ya hukumu na mamlaka…Kama mchungaji, kazi ya fimbo ya mchungaji ni kuwaweka kondoo kwenye mstari na pia kuwapiga maadui wanaotaka kuwadhuru kondoo.
Sasa wakiwa jangwani katika safari ya kwenda Kaanani kuna baadhi ya watu walinyanyuka kinyume cha Musa na Haruni, na kusema inatosha sasa nyie kujifanya wakubwa juu yetu…Hivyo wakataka wao ndio wawe viongozi wa lile kundi lote…Mungu hakupendezwa na kile kitendo hivyo akawaua wote walijaribu kutekeleza hilo zoezi..Unaweza kusoma hayo katika kitabu cha Hesabu mlango wa 16.
Watu hao pamoja na kuona miujiza yote bado walikuwa wanadhani ni Musa na Haruni kwa akili zao ndio walioamua kuwatoa Misri, hawakujua kuwa ni Mkono wa Mungu, kwa ile fimbo ya kichungaji ndiyo iliyowatoa Misri…hivyo badala ya kumwangalia Mungu na uweza wake wakaanza kuwashambulia Musa na Haruni kana kwamba wao ndio waliowatoa Misri, waliwachoka hivyo wakataka kujichagulia watu wengine wa kuongoza.
Lakini Mungu kuthibitisha kuwa si mwanadamu anayeokoa bali ni Mungu, na kuwathibitishia kuwa hapangiwi mtu wa kulibeba kusudi lake..aliwaambia wakuu wote wa makabila kila mmoja alete fimbo yake mbele ya agano la ushuhuda, kwahiyo zikaletwa fimbo 12, Na hizi fimbo hazikutwaliwa tu kutoka kwa watu wa kawaida, hapana bali zilitwaliwa kutoka kwa Wakuu wa kila kabila la Israeli..Wakuu wa makabila walikuwa ni watu wa Mungu, na walioheshimika na kila kabila lilikuwa na mkuu mmoja, na kila mkuu alikuwa na fimbo yake kama vile Musa alivyokuwa na fimbo…Na hao Mungu aliwajalia hekima katika kuongoza, na pia fimbo zao zilikuwa na miujiza Fulani, hazikuwa fimbo za kawaida..
Kwahiyo fimbo zao zikakusanywa zote, na kila fimbo ikaandikwa jina la mhusika…. na katika kabila la Lawi wakaichagua ile fimbo ya Haruni, kwahiyo zikapelekwa mbele ya hema ya kukutania.
Hesabu 17:1 “Kisha Bwana akanena na Musa, akamwambia, 2 Nena na wana wa Israeli, kisha upokee kwao fimbo, fimbo moja kwa ajili ya nyumba ya kila baba, katika wakuu wao wote, kama nyumba za baba zao zilivyo, fimbo kumi na mbili; kisha andika jina la kila mtu katika fimbo yake. 3 Na katika fimbo ya Lawi utaliandika jina la Haruni; maana, itakuwa fimbo moja kwa kila kichwa cha nyumba za baba zao. 4 Nawe utaziweka katika hema ya kukutania mbele ya huo ushahidi, hapo nikutanapo pamoja nanyi. 5 Kisha itakuwa, mtu huyo nitakayemchagua, fimbo yake itachipuka; nami nitayakomesha kwangu manung’uniko ya wana wa Israeli, wanung’unikiayo juu yenu. 6 Basi Musa akawaambia wana wa Israeli, ndipo wakuu wao wote wakampa fimbo, fimbo moja kwa kila mkuu, kama nyumba za baba zao zilivyokuwa, fimbo kumi na mbili; na fimbo ya Haruni ilikuwa kati ya fimbo zao. 7 Kisha Musa akaziweka hizo fimbo mbele za Bwana katika hema ya kukutania”.
Hesabu 17:1 “Kisha Bwana akanena na Musa, akamwambia,
2 Nena na wana wa Israeli, kisha upokee kwao fimbo, fimbo moja kwa ajili ya nyumba ya kila baba, katika wakuu wao wote, kama nyumba za baba zao zilivyo, fimbo kumi na mbili; kisha andika jina la kila mtu katika fimbo yake.
3 Na katika fimbo ya Lawi utaliandika jina la Haruni; maana, itakuwa fimbo moja kwa kila kichwa cha nyumba za baba zao.
4 Nawe utaziweka katika hema ya kukutania mbele ya huo ushahidi, hapo nikutanapo pamoja nanyi.
5 Kisha itakuwa, mtu huyo nitakayemchagua, fimbo yake itachipuka; nami nitayakomesha kwangu manung’uniko ya wana wa Israeli, wanung’unikiayo juu yenu.
6 Basi Musa akawaambia wana wa Israeli, ndipo wakuu wao wote wakampa fimbo, fimbo moja kwa kila mkuu, kama nyumba za baba zao zilivyokuwa, fimbo kumi na mbili; na fimbo ya Haruni ilikuwa kati ya fimbo zao.
7 Kisha Musa akaziweka hizo fimbo mbele za Bwana katika hema ya kukutania”.
Kesho yake walipoingia ndani ya Hema… wakaikuta ile fimbo ya Haruni imechipuka na kuzaa matunda, na zile nyingine hazijachipuka…Ndipo wana wa Israeli wakajua kuwa ni Mungu ndiye aliyekuwa pamoja na Musa na Haruni, Na Mungu amewachagua hao kubeba kusudi lake.
“8 Ilikuwa siku ya pili yake, Musa akaingia ndani ya hema ya ushahidi; na tazama, ile fimbo ya Haruni iliyokuwa kwa nyumba ya Lawi ilikuwa imechipuka, imetoa michipukizi, na kuchanua maua; na kuzaa malozi mabivu. 9 Kisha Musa akazileta nje hizo fimbo zote kutoka hapo mbele za Bwana na kuziweka mbele ya wana wa Israeli wote; nao wakaangalia, na kila mtu akaitwaa fimbo yake. 10 Kisha Bwana akamwambia Musa, Irudishe fimbo ya Haruni mbele ya ushahidi, ili itunzwe iwe ishara juu ya hawa wana wa maasi; ili uyakomeshe manung’uniko yao waliyoninung’unikia, ili wasife. 11 Basi Musa akafanya vivyo; kama Bwana alivyomwagiza, ndivyo alivyofanya ”.
“8 Ilikuwa siku ya pili yake, Musa akaingia ndani ya hema ya ushahidi; na tazama, ile fimbo ya Haruni iliyokuwa kwa nyumba ya Lawi ilikuwa imechipuka, imetoa michipukizi, na kuchanua maua; na kuzaa malozi mabivu.
9 Kisha Musa akazileta nje hizo fimbo zote kutoka hapo mbele za Bwana na kuziweka mbele ya wana wa Israeli wote; nao wakaangalia, na kila mtu akaitwaa fimbo yake.
10 Kisha Bwana akamwambia Musa, Irudishe fimbo ya Haruni mbele ya ushahidi, ili itunzwe iwe ishara juu ya hawa wana wa maasi; ili uyakomeshe manung’uniko yao waliyoninung’unikia, ili wasife.
11 Basi Musa akafanya vivyo; kama Bwana alivyomwagiza, ndivyo alivyofanya ”.
Malozi ni matunda Fulani yanayojulikana kama matipisi, au sehemu nyingine yanajulikana kama mapindigesi au mapichi. Ni matunda ambayo yakiiva yanakuwa matamu sana na yana mbegu ngumu sana ndani, na pia maua yake ni mazuri sana kupita kiasi..Sasa tabia ya mti wa Mlozi au mtipisi ni kwamba hautoi matunda msimu mmoja na maua, msimu wa maua huwezi kukuta tunda hata moja unakuta mti wote ni maua tu, na maua yake ni mazuri sana, ni mchanganyiko wa rangi ya pink na nyeupe..kadhalika msimu wa matunda huwezi ukakuta ua hata moja, mti wote unakuwa ni kijani tu, na umejaa matunda..lakini hapa kwenye hii fimbo ya Haruni unaona mwujiza matunda na maua yamechipuka kwa wakati mmoja…
Tabia yake nyingine ya kipekee ya mti wa Mlozi (mtipisi)..ni kwamba unachukua muda mrefu sana mpaka ukomae na kufikia kiwango cha kuzaa matunda, sio mti mkubwa sana ni kama mchungwa tu! Lakini unaweza kuchukua hata miaka 12 mpaka ufikie hatua ya kuzaa matunda…Lakini hapa katika hii fimbo ya haruni unaona imechukua usiku mmoja tu kuzaa, ina maana kubwa sana ambayo tutakuja kuona hapo mbeleni.
Na mti wa Mtipisi, ni mti ambao unahitaji mizizi mirefu ili iweze kukua, mizizi ya mti huu inakadiriwa kuwa na urefu mara mbili ya mti wenyewe…kwahiyo unaweza kuona ni mti unaohitaji sana mizizi ili ukue..lakini hapa kwenye fimbo ya Haruni kulikuwa hakuna mizizi.
Kwahiyo ile fimbo ya Haruni ilikuwa inawakilisha Mkono wa Mungu juu ya wana wa Israeli, kwamba anawachunga wana wa Israeli kwa miujiza, kwa fimbo ya kimiujiza, kwamba Bwana anatoa chakula mahali ambapo hakuna chanzo cha chakula, ndio maana umeona ile fimbo imechipua na haina mizizi, Wana wa Israeli walikula mana na nyama jangwani mahali ambapo hakuna mashamba wala mvua… pia Bwana anaweza kuumba jambo leo leo kwa jambo ambalo lingeweza kuchukua miaka mingi kufanyika ndio maana unaona ile fimbo imechipuka kwa usiku mmoja tu na kuzaa matunda mengi.
Pia Bwana ana uwezo wa kuikusanya misimu miwili au zaidi na kuileta pamoja, kwa Bwana inawezekana kuzaa na kuchanua kwa wakati mmoja ndio maana unaona ile fimbo ilizaa matunda na kuzaa maua kwa wakati mmoja.
Kadhalika Kristo ndiye Kiongozi wetu sasa, yeye ndiye aliyepokea mamlaka yote ya Mbinguni na Duniani kutoka kwa Baba kama vile Haruni alivyopokea uongozi kutoka kwa Musa na fimbo ya kichungaji, na sisi leo tukimpokea Kristo na kumwamini, basi tutakuwa chini ya FIMBO YA KICHUNGAJI YA BWANA YESU KRISTO, ambayo hiyo haina msimu maalumu wa kutupa mema, hiyo tukiumwa haihitaji mamia ya miaka ndipo tupone, ni papo kwa hapo…hiyo haihitaji kuhofia tutakula nini wala tutakunywa nini?…inatoa chakula mahali pasipo na chakula na kutoa maji mahali pasipo na maji, kama fimbo ya Haruni ilivyotoa maji mwambani kule jangwani… na inatengeneza njia mahali pasipokuwa na njia..
Lakini sharti kwanza lazima ukubali kuwa kondoo wake, ndipo uchungwe na unakuwa kondoo wake kwa kumwamini na kwa kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha na kisha kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu, na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, hapo utakuwa kondoo wake, na utashiriki Baraka zote za uchungaji wake..
Fimbo za wengine hazina nguvu ya kiungu, haziwezi kufanya lolote haziwezi kuchipuka zinahitaji mizizi, zinahitaji muda mrefu kukupatia msaada, vile vile haziwezi kukutetea, wakati wa maadui, fimbo ya Haruni iligeuka pia kuwa nyoka kwa Farao pale ilipopasa…Si zaidi fimbo ya BWANA wetu YESU KRISTO?.
Zaburi 23:1 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu. 2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza. 3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. 4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, GONGO LAKO NA FIMBO YAKO VYANIFARIJI”.
Zaburi 23:1 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.
2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, GONGO LAKO NA FIMBO YAKO VYANIFARIJI”.
Ubarikiwe.
NABII MUSA NI NANI?
HARUNI ALIKUWA NI NANI?
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1
NI KWASABABU YA YESU KRISTO.
Bwana wetu Yesu Kristo japo alikuwa ni Mungu mwenyewe katika mwili lakini hakuwa mnafiki kutokuonyesha hisia zote wanadamu wanazopitia wakiwa hapa duniani, Kama wengine walivyotazamia kuwa Mungu akiuvaa mwili, basi yeye atakuwa ni kama malaika duniani, Na ndio maana Waebrania 2:16-18 inasema:
16 Maana ni hakika, hatwai asili ya malaika, ila atwaa asili ya mzao wa Ibrahimu. 17 Hivyo ilimpasa kufananishwa na ndugu zake katika mambo yote, apate kuwa kuhani mkuu mwenye rehema, mwaminifu katika mambo ya Mungu, ili afanye suluhu kwa dhambi za watu wake. 18 Na kwa kuwa mwenyewe aliteswa alipojaribiwa, aweza kuwasaidia wao wanaojaribiwa.
16 Maana ni hakika, hatwai asili ya malaika, ila atwaa asili ya mzao wa Ibrahimu.
17 Hivyo ilimpasa kufananishwa na ndugu zake katika mambo yote, apate kuwa kuhani mkuu mwenye rehema, mwaminifu katika mambo ya Mungu, ili afanye suluhu kwa dhambi za watu wake.
18 Na kwa kuwa mwenyewe aliteswa alipojaribiwa, aweza kuwasaidia wao wanaojaribiwa.
Unaona? Bwana alilia palipopaswa kulia, sehemu nyingine aliomba Mungu amwepushe, na kikombe cha mateso ikiwa ni sawa sawa na mapenzi ya Baba yake, kwa namna ya kawaida tunaweza kusema hofu ya kibinadamu ya kuuawa ilimwingia.
Vile vile Japo siku zote alifahamu Baba yake yupo pamoja naye, hawezi kumwacha, na alishamweleza kitu kuhusu maisha yake, na mwisho wake utakavyokuwa, na yatakayotokea baada ya hapo, lakini kuna saa huzuni ilikuwa inamwingia….Halikadhalika Bwana akiwa pale msalabani alijua kabisa siku zisizodi tatu atakuwa utukufuni, akijua kabisa safari yake imeshakwisha kikamilifu, amebakisha dakika chache tu aondoke duniani lakini katika hatua ile ile ya mwisho, tunaona anamwambia baba yake maneno haya:
Mathayo 27:46 “Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
Fahamu kuwa alikuwa hazungumzi maneno haya ili kujifanya, ni kweli kabisa ndani ya moyo wake, hakuwa anaona uwepo wowote wa ki-Mungu, ndani yake hakukuwa na chochote, alikuwa hana tofauti na wale wezi aliosulibiwa nao, ni kama vile kaachwa Solemba, alikuwa kama mtu ambaye Mungu hajawahi kuzungumza naye kabisa, ndivyo alivyojiona ndani yake..
Tukitafsiri kwa lugha ya leo tunaweza kusema, Ee! Mungu mbona katika siku za raha ulikuwa pamoja nami, ulikuwa unatembea nami, wala hakukuwa na shida yoyote, iweje leo katika shida zangu, umejitenga mbali nami?. Mungu wangu, Mungu wangu, upo wapi mbona umeniacha?.
Hali kama hii hii ilimkuta Daudi wakati anakimbizwa na Sauli, wakati anapitia shida nyingi mapangoni, wakati yupo katika kukataliwa, na dhiki, akaona kama vile Mungu hajihusishi tena, kamwacha peke yake, tunasoma:
Zaburi 10:1 “Ee Bwana, kwa nini wasimama mbali? Kwani kujificha nyakati za shida?”. Zaburi 13: 1 Ee Bwana, hata lini utanisahau, hata milele? Hata lini utanificha uso wako? 2 Hata lini nifanye mashauri nafsini mwangu, Nikihuzunika moyoni mchana kutwa? Hata lini adui yangu atukuke juu yangu? 3 Ee Bwana, Mungu wangu, uangalie, uniitikie; Uyatie nuru macho yangu, Nisije nikalala usingizi wa mauti.
Zaburi 10:1 “Ee Bwana, kwa nini wasimama mbali? Kwani kujificha nyakati za shida?”.
Zaburi 13: 1 Ee Bwana, hata lini utanisahau, hata milele? Hata lini utanificha uso wako?
2 Hata lini nifanye mashauri nafsini mwangu, Nikihuzunika moyoni mchana kutwa? Hata lini adui yangu atukuke juu yangu?
3 Ee Bwana, Mungu wangu, uangalie, uniitikie; Uyatie nuru macho yangu, Nisije nikalala usingizi wa mauti.
Nawe pia Wakati mwingine unaweza ukawa unapitia hali ngumu, magonjwa ya kutisha ambayo madaktari wamekuambia hakuna matumaini hapa, watu wanakutisha na kukupa shuhuda za waliokufa kwa magonjwa ya namna hiyo, unaumwa Kansa, unaumwa Ukimwi, Presha, Kisukari na magonjwa yote ya ajabu yaliyo duniani siku hizi. Umeombewa sana, ila hali bado ipo vilevile.
Na kweli ndani ya moyo wako unajua kabisa Mungu wako hawezi kukuacha, lakini bado unahisi kama vile hakuoni katika hali unayopitia sasa, unahisi kama vile, amekaa kimya, hachukui hatua yoyote kwa hilo tatizo ulilonalo kwa muda mrefu..
Nataka nikutie moyo, Biblia inasema Mungu hakuwahi kulidharau teso la mteswa. Na maneno hayo yafaraja tunayapata katika Kitabu cha Zaburi, kitabu kile kile ambacho Bwana YESU alikinukuu akiwa pale msalabani, ndicho hicho hicho Mungu alimpa majibu ya maneno yake…
Tusome:
ZABURI 22 1 Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha? Mbona U mbali na wokovu wangu, Na maneno ya kuugua kwangu? 2 Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu Na wakati wa usiku lakini sipati raha. 3 Na Wewe U Mtakatifu, Uketiye juu ya sifa za Israeli. 4 Baba zetu walikutumaini Wewe, Walitumaini, na Wewe ukawaokoa. 5 Walikulilia Wewe wakaokoka, Walikutumaini wasiaibike. 6 Lakini mimi ni mdudu wala si mtu, Laumu ya wanadamu na mzaha wa watu. 7 Wote wanionao hunicheka sana, Hunifyonya, wakitikisa vichwa vyao; 8 Husema, Umtegemee Bwana; na amponye; Na amwokoe sasa, maana apendezwa naye. 9 Naam, Wewe ndiwe uliyenitoa tumboni, Ulinitumainisha matitini mwa mama yangu. 10 Kwako nalitupwa tangu tumboni, Toka tumboni mwa mamangu ndiwe Mungu wangu. 11 Usiwe mbali nami maana taabu i karibu, Kwa maana hakuna msaidizi. 12 Mafahali wengi wamenizunguka, Walio hodari wa Bashani wamenisonga; 13 Wananifumbulia vinywa vyao, Kama simba apapuraye na kunguruma. 14 Nimemwagika kama maji, Mifupa yangu yote imeteguka, Moyo wangu umekuwa kama nta, Na kuyeyuka ndani ya mtima wangu. 15 Nguvu zangu zimekauka kama gae, Ulimi wangu waambatana na taya zangu; Unaniweka katika mavumbi ya mauti 16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; Kusanyiko la waovu wamenisonga; Wamenizua mikono na miguu. 17 Naweza kuihesabu mifupa yangu yote; Wao wananitazama na kunikodolea macho. 18 Wanagawanya nguo zangu, Na vazi langu wanalipigia kura. 19 Nawe, Bwana, usiwe mbali, Ee Nguvu zangu, fanya haraka kunisaidia. 20 Uniponye nafsi yangu na upanga, Mpenzi wangu na nguvu za mbwa. 21 Kinywani mwa simba uniokoe; Naam, toka pembe za nyati umenijibu. 22 Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu, Katikati ya kusanyiko nitakusifu. 23 Ninyi mnaomcha Bwana, msifuni, Enyi nyote mlio wazao wa Yakobo, mtukuzeni, Mcheni, enyi nyote mlio wazao wa Israeli. 24 MAANA HAKULIDHARAU TESO LA MTESWA, WALA HAKUCHUKIZWA NALO; WALA HAKUMFICHA USO WAKE, BALI ALIPOMLILIA AKAMSIKIA. 25 Kwako zinatoka sifa zangu Katika kusanyiko kubwa. Nitaziondoa nadhiri zangu Mbele yao wamchao. 26 Wapole watakula na kushiba, Wamtafutao Bwana watamsifu; Mioyo yenu na iishi milele. 27 Miisho yote ya dunia itakumbuka, Na watu watamrejea Bwana; Jamaa zote za mataifa watamsujudia. 28 Maana ufalme una Bwana, Naye ndiye awatawalaye mataifa. 29 Wakwasi wote wa dunia watakula na kusujudu, Humwinamia wote washukao mavumbini; Naam, yeye asiyeweza kujihuisha nafsi yake, 30 Wazao wake watamtumikia. Zitasimuliwa habari za Bwana, Kwa kizazi kitakachokuja, 31 Nao watawahubiri watakaozaliwa haki yake, Ya kwamba ndiye aliyeyafanya.
ZABURI 22
1 Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha? Mbona U mbali na wokovu wangu, Na maneno ya kuugua kwangu?
2 Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu Na wakati wa usiku lakini sipati raha.
3 Na Wewe U Mtakatifu, Uketiye juu ya sifa za Israeli.
4 Baba zetu walikutumaini Wewe, Walitumaini, na Wewe ukawaokoa.
5 Walikulilia Wewe wakaokoka, Walikutumaini wasiaibike.
6 Lakini mimi ni mdudu wala si mtu, Laumu ya wanadamu na mzaha wa watu.
7 Wote wanionao hunicheka sana, Hunifyonya, wakitikisa vichwa vyao;
8 Husema, Umtegemee Bwana; na amponye; Na amwokoe sasa, maana apendezwa naye.
9 Naam, Wewe ndiwe uliyenitoa tumboni, Ulinitumainisha matitini mwa mama yangu.
10 Kwako nalitupwa tangu tumboni, Toka tumboni mwa mamangu ndiwe Mungu wangu.
11 Usiwe mbali nami maana taabu i karibu, Kwa maana hakuna msaidizi.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, Walio hodari wa Bashani wamenisonga;
13 Wananifumbulia vinywa vyao, Kama simba apapuraye na kunguruma.
14 Nimemwagika kama maji, Mifupa yangu yote imeteguka, Moyo wangu umekuwa kama nta, Na kuyeyuka ndani ya mtima wangu.
15 Nguvu zangu zimekauka kama gae, Ulimi wangu waambatana na taya zangu; Unaniweka katika mavumbi ya mauti
16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; Kusanyiko la waovu wamenisonga; Wamenizua mikono na miguu.
17 Naweza kuihesabu mifupa yangu yote; Wao wananitazama na kunikodolea macho.
18 Wanagawanya nguo zangu, Na vazi langu wanalipigia kura.
19 Nawe, Bwana, usiwe mbali, Ee Nguvu zangu, fanya haraka kunisaidia.
20 Uniponye nafsi yangu na upanga, Mpenzi wangu na nguvu za mbwa.
21 Kinywani mwa simba uniokoe; Naam, toka pembe za nyati umenijibu.
22 Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu, Katikati ya kusanyiko nitakusifu.
23 Ninyi mnaomcha Bwana, msifuni, Enyi nyote mlio wazao wa Yakobo, mtukuzeni, Mcheni, enyi nyote mlio wazao wa Israeli.
24 MAANA HAKULIDHARAU TESO LA MTESWA, WALA HAKUCHUKIZWA NALO; WALA HAKUMFICHA USO WAKE, BALI ALIPOMLILIA AKAMSIKIA.
25 Kwako zinatoka sifa zangu Katika kusanyiko kubwa. Nitaziondoa nadhiri zangu Mbele yao wamchao.
26 Wapole watakula na kushiba, Wamtafutao Bwana watamsifu; Mioyo yenu na iishi milele.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka, Na watu watamrejea Bwana; Jamaa zote za mataifa watamsujudia.
28 Maana ufalme una Bwana, Naye ndiye awatawalaye mataifa.
29 Wakwasi wote wa dunia watakula na kusujudu, Humwinamia wote washukao mavumbini; Naam, yeye asiyeweza kujihuisha nafsi yake,
30 Wazao wake watamtumikia. Zitasimuliwa habari za Bwana, Kwa kizazi kitakachokuja,
31 Nao watawahubiri watakaozaliwa haki yake, Ya kwamba ndiye aliyeyafanya.
Ukisoma ule mstari wa 24, anasema: 24 MAANA HAKULIDHARAU TESO LA MTESWA, WALA HAKUCHUKIZWA NALO; WALA HAKUMFICHA USO WAKE, BALI ALIPOMLILIA AKAMSIKIA.
Na wewe vile vile ambaye umeokoka, umepitia hali ya shida kwa muda mrefu, bila kuona dalili yoyote ya kuponywa au kutoka katika mahali ulipo, fahamu kuwa Mungu hajalidharau teso lako, wala hachukizwi nawe, wala hajauficha uso wake kwako, bali siku ile ya kwanza ulipomlilia alishakusikia, hivyo hutakufa. Kwahiyo kaa katika matumaini ya kuipokea muujiza wako, wakati aliokuandalia utaufurahia wema wake, ulio mwingi. Ilikuwa ni lazima Mungu aruhusu Bwana Yesu ayapitie yale ili alete faida kubwa zaidi katika ufalme wa mbinguni ndio maana Mungu alikaa kimya kwa wakati ule, lakini alipomaliza kazi yake, mateso yale yamekuwa sababu ya mimi na wewe kuupata wokovu. Vivyo hivyo na wewe usitishwe na kitu chochote, maadamu yupo pamoja na wewe sikuzote. Atakupigania.
Songa mbele na Bwana Yesu Kristo atakuonekania.
Ubarikiwe sana. Tafadhali “Share” Ujumbe huu na kwa wengine. Na Mungu atakubariki.
BASI MUNGU AKAMUADHIMISHA SANA..
MNGOJEE BWANA
MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU:
USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.