Isaya 35: 8 “Na hapo patakuwa na NJIA KUU, na njia, NAYO ITAITWA, NJIA YA UTAKATIFU; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; WASAFIRIO, WAJAPOKUWA WAJINGA, HAWATAPOTEA KATIKA NJIA HIYO”.
Mtu yeyote anayejiita ni mkristo ni wazi kuwa yupo safarini, Na kama yupo safarini ni lazima afahamu malengo yake ni nini, kwamba anatoka wapi, na anakwenda wapi? Na Sababu ya yeye kumfanya utoke pale alipo aende huko anendako ni ipi?, Kadhalika ni lazima ajue ni njia gani atakayoipita, na chombo kipi atakachokitumia kusafiria pamoja na gharama zake..! Lakini ukiwa ni msafiri halafu hujui hayo yote, ni dhahiri kuwa utaitwa MTORO, kama vile Kaini alivyoambiwa na Bwana Mungu kwamba atakuwa“mtoro na mtu asiye na kikao duniani (Mwanzo 4:12)”. Na huo uzao wa Kaini unatenda kazi miongoni mwa kundi kubwa linalojiita la wakristo, hawana vikao, hawajulikana ni watu wa ulimwengu huu, au ni wasafiri wa kwenda mbinguni, Kumbuka Kaini na Habili wote walikuwa ni ndugu, isipokuwa mmoja hakuonekana kuwa mkamilifu mbele za Mungu.
Mtu aliye makini katika safari yake, siku zote anaona mwisho wa safari yake utakuwa ni upi hata kabla hajaianza hiyo safari, na atatambua ya kuwa wakati akiwa njiani atakutana na mambo mengi tofuati tofauti, na majira mengi tofauti tofauti, hivyo atakuwa makini akijua kuwa yupo safarini kwahiyo hatayatilia maanani mambo yanayopita ya njiani, hata akifika kituoni labda kwa muda mchache tu atashuka kuchuka chakula na kurudi kwenye chombo chake cha usafiri na kuendelea na safari yake, hatashikamana au kuambatana na shughuli zinazoendelea katika hicho kituo alichofika kwa muda tu, huwezi kuona anakwenda kuzunguka tena mijini, labda kwenye viwanja vya michezo, na majukwaa ya sinema, na kutangatanga huku na huko ni kwasababu gani? Kwasababu anajua akifanya hivyo muda wake hautamtosha hivyo ataachwa na kile chombo alichokuwa anasafiria, na hapo pia si sehemu yake aliyotarajia kufika, Kwahiyo yeye mahali popote anapopita atatafahamu ni mpitaji tu,
kadhalika na katika ukristo wa kweli sisi ni wasifiriji tu, ulimwenguni sio kwetu,..Mkristo ni lazima afahamu yeye anatoka wapi, na anakwenda wapi, na kitu gani kinachompeleka huko aendako,,.Safari yetu sisi ni kutoka katika ulimwengu mmoja na kwenda katika ulimwengu mwingine, tunatoka katika ulimwengu huu uliopo sasa unaoharibika na kwenda katika ulimwengu mpya wa milele usioharibika, na ili kuufikia huo ulimwengu mpya ipo njia ya kuipitia, ndio hii Bwana anayoiita, “NJIA KUU”..Hii imeitwa Njia kuu kwasababu wanaopita juu yake ni wachache, na ni WATAKATIFU tu WALIOSAFARINI ndio watakaopita juu yake, Hakuna mtu mwingine yeyote atakayeweza kupita katika hiyo njia isipokuwa amekidhi hivyo vigezo.
Kumbuka katika huo ulimwengu ujao kutakuwa na MALANGO MAKUBWA ya kuuingilia, Na njia pekee itakayokuongoza kuuingia ni hiyo NJIA KUU inayojulikana kama Njia ya Utakatifu. Huko ndiko Yerusalemu mpya mji wa Mungu ulipo, (yaani bibi-arusi wa Kristo). Na ndio maana Bwana Yesu alisema,
Ufunuo 22: 14 “Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, NA KUINGIA MJINI KWA MILANGO YAKE.
15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya”.
Ndugu yangu, maneno ya Yesu Kristo ni kweli na uzima, hiyo njia ni NJIA KUU ni NJIA YA UTAKATIFU, haijasema ni njia ya dini, au ya dhehebu, au ya upako, au ya miujiza, au ya utajiri, au ya umaskini, hapana inasema ni NJIA YA UTAKATIFU, ikiwa na maana kuwa wale wasafiri ambao ni watakatifu ndio wanaoipita hiyo,na si mwingine yeyote unaweza ukadhani upo katika njia hiyo kwasababu tu wewe unayo dini, lakini ndugu kama huna UTAKATIFU haupo katika hiyo njia, hata kama utatoa zaka kiasi gani, kama wewe haujajiweka kama mtu anayesafiri, basi jua haupo katika njia hiyo. Biblia ipo wazi kabisa inasema.
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”;
Unaona hapo?, wewe unayesema ni mkristo na unasema upo safarini, umefika katikati ya safari yako umekutana na anasa na burudani za ulimwengu huu, unasahau kuwa wewe ni mkristo unayesafiri unaanza na wewe kushikamana na hivyo vitu vya ulimwengu huu vinavyopita, unaanza na wewe kuhudhuria karama za ulafi, unaanza kujishughulisha na rushwa, unaanza kujichanganya na watu waovu wa ulimwengu huu, ulikuwa ni mwombaji mzuri hapo mwanzo lakini sasa biashara na udanganyifu wa mali vinakusonga, wewe kila wakati ni mali tu, unasahau maisha yako ya rohoni, hujui kuwa muda unazidi kwenda na kile chombo ulichokuwa unasafiria (Neema) hakiwezi kikakusubiria muda wote huo,
Ulikuwa unavaa vizuri na kujisitiri hapo mwanzo, lakini ukafika kituo ukakutana na fashion za ulimwengu huu, ukasahau kuwa upo safarini ukauacha utakatifu uliokuwa nao hapo mwanzo na wewe ukaanza kuvaa suruali na kaptura, ukaanza kuvaa nguo fupi, ukaanza kuvaa nguo zinazochora maumbile yako, ukaanza kupaka ma-lipstick, na wanja, na hereni na ma-wigi kama wanawake wa ulimwengu huu, hujui kuwa muda unazidi kwenda na kile chombo ulichokuwa unasafiria kimeshaanza kukuacha.
Mwanzoni mwa safari yako mawazo yako yalikuwa yameelekea mbinguni tu, ulikuwa unatamani ufikie kilele cha safari yako mapema, ulikuwa unafikiria kila siku habari za mbingu mpya na nchi mpya lakini umefika mahali umegota safarini, umeiacha NJIA KUU YA UTAKATIFU, umeanza kutazama pornography, umeanza kusengenya, umeanza kutukana, umeacha upole wako na ukarimu wako, ndugu ukiendelea hivyo hivyo hautauingia ule mji Yerusalemu ya Bwana, usijidanganye na Dini yako ukadhani inatosha kukufikisha mbinguni, kwasababu biblia ilishasema..”
Mithali 14: 12 Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti”..Kumbuka kama ilivyosema..Pasipo huo utakatifu hakuna mtu atakayemwona Mungu…
Isaya 35: 8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, NJIA YA UTAKATIFU; WASIO SAFI HAWATAPITA JUU YAKE; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; WASAFIRIO, WAJAPOKUWA WAJINGA, HAWATAPOTEA KATIKA NJIA HIYO.
9 Hapo hapatakuwa na simba, wala mnyama mkali hatapanda juu yake; hawataonekana hapo; bali waliokombolewa watakwenda katika njia hiyo.
10 Na hao waliokombolewa na Bwana watarudi, watafika Sayuni wakiimba; na furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao; nao watapata kicheko na furaha, huzuni na kuugua zitakimbia”.
Umeona biblia inasema watakaopita katika njia hiyo, ulimwengu utawaona ni wajinga, wataonekana kama watu wasiostahili kuwa katikati yao, wanawake waliokataa mitindo ya ulimwengu huu wataonekana washamba na wajinga, wanaume wasiokuwa walevi, wala waasherati, watu wanaoishi maisha matakatifu watadharauliwa, lakini hao ndio Mungu aliowachagua wapite katika njia ile KUU, Biblia inasema wajapokuwa ni wajinga machoni pa ulimwengu lakini hawatapotea katika njia hiyo.
Kumbuka ndugu, biblia imetuonya tufanane na wasafiri wenzetu wa Imani waliotutangulia, ambao walijikana kweli kweli, watu ambao mawazo yao yote yalikuwa ni mbinguni tu, kama tunavyowasoma katika
Waebrania 11: 36 “wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani;
37 walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga; walizunguka-zunguka wakivaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi; walikuwa wahitaji, wakiteswa, wakitendwa mabaya;
38 (WATU AMBAO ULIMWENGU HAUKUSTAHILI KUWA NAO), walikuwa wakizunguka-zunguka katika nyika na katika milima na katika mapango na katika mashimo ya nchi.
39 Na watu hao wote wakiisha kushuhudiwa kwa sababu ya imani yao, hawakuipokea ahadi;
40 kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea sisi kitu kilicho bora, ili wao wasikamilishwe pasipo sisi…”
Waebrania 11: 13 Hawa wote wakafa katika imani, wasijazipokea zile ahadi, bali wakaziona tokea mbali na kuzishangilia, NA KUKIRI KWAMBA WALIKUWA WAGENI, NA WASAFIRI JUU YA NCHI.14 MAANA HAO WASEMAO MANENO KAMA HAYO WAONYESHA WAZI KWAMBA WANATAFUTA NCHI YAO WENYEWE.
15 Na kama wangaliikumbuka nchi ile waliyotoka, wangalipata nafasi ya kurejea.
16 Lakini sasa waitamani nchi iliyo bora, yaani, ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni haya kuitwa Mungu wao; maana amewatengenezea mji”.
Ndugu hawa watu walijikana nafsi zao kwasababu waliuona uzuri uliopo mbele yao, waliona furaha isiyokuwa na kifani kuingia katika ule mji, waliona ni heri maisha yao ya miaka 80 yasiwe ni kitu kulinganisha na miaka ya umilele inayokuja huko mbeleni. Ndugu kosa kila kitu lakini usikose mbingu, Biblia inasema wenye haki watang’aa kama jua, Mambo ambayo Mungu amewaandalia wampendao ni mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia, hakutakuwa na uchungu tena, wala kudharauliwa, watapewa miili ya utukufu wa ajabu, watatawala na Kristo Yesu kama wafalme na makuhani, milele na milele, tujitahidi tusikose huko.
Utajisikiaje unyakuo umepita na wewe umeachwa? Wenzako wamekwenda katika karamu ya mwanakondoo mbinguni na wewe umebaki?hapa duniani ukisubiria ziwa la moto?
Utajisikiaje??..Ifuate hiyo NJIA KUU LEO, kwa kumpa Yesu Kristo maisha yako kama hujafanya hivyo angali muda upo, ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa kwenye maji tele na kwa Jina la YESU KRISTO, upate ondoleo la dhambi zako (Matendo 2:38) na kisha utapokea kipawa cha Roho Mtakatifu kitakachokuwezesha kuwa mtakatifu ili uweze kuiendea hiyo NJIA KUU YA UTAKATIFU ili siku ile Uingie katika ile Yerusalemu mpya ya Bwana aliyowaandalia watakatifu wake
Ufunuo 21: 1 “Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.
2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.
3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.
4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.
5 Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.
6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.
7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
8 Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili..”
Ubarikiwe.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine ili nao wapone.
Mada Nyinginezo:
NJIA YA BWANA INATENGENEZWA WAPI?
UMEFUNGWA KATIKA GIZA NA UVULI WA MAUTI?
KATIKA 1YOHANA 5:6-9, (A) NI KWA NAMNA GANI YESU ALIKUJA KWA MAJI NA DAMU?
Kama unamchukulia mtu ni adui yako kwasababu amekusengenya, au amekudharau, au amekutukana, au amekuibia, au amekurusha, au amekuaibisha, au amekata mazungumzo na wewe ghafla, au amejisifia mbele zako na kukuona kama wewe si kitu kwasababu yeye pengine anaye mtoto na wewe huna. Hivyo umekuwa ukitamani Mungu amlipize kisasi, aanguke, au ashushwe au ikiwezekana afe kabisa, basi ni dhahiri kabisa dua hizo unazomtakia huyo adui yako kwa namna moja au nyingine zitakurudia wewe mwenyewe..
Kwasababu, kwa mambo kama hayo hayo yanakufanya na wewe kuwa adui kwa mtu mwingine(usiyemtarajia), inawezekana ulishawahi kumkwaza mtu pasipo wewe kujua, au kumuumiza hisia zake pasipo kukusudia kwa maneno yaliyowahi kutoka kinywani mwako, au uliacha kuzungumza naye pengine kwasababu za msingi kabisa pengine huna simu, hivyo yeye akalichukulia jambo lile kwa namna nyingine tofauti, pengine ulijifisia mtoto wako mbele zake kwa nia ya kutokujiinua, na yeye akaona kama vile umewadharau wa kwake, n.k..
Yeye pia atakuona wewe kama adui yake, na pengine yeye naye anaomba mbele za Mungu kama wewe ulivyokuwa unaomba, asambaratishwe, anamwomba Mungu amwinue ili uone mafanikio yake, anamwomba Mungu vikwazo vikukute, upate hasara, au udhaifu pengine hata ufe, anakutaja kila siku kwenye dua zake mbele za Mungu ushushwe chini..Lakini je! ni kweli wewe unastahili kufanyiwa hivyo vitu??. Na kama sio kwanini wewe unamfanyia mwingine? Biblia inasema “Msilaumu, msije mkalaumiwa,” Kwasababu kipimo tutakachopima ndicho hicho hicho tutakachopimiwa.(Luka 6:37)
Cha kuhuzunisha haya ndiyo yamekuwa maombi ya wakristo wengi katika siku hizi za mwisho. Kupelekea maombi mbele za Mungu, ..“Mungu mpige Adui yangu”…Kadhalika na mwenzako anakuombea na wewe upigwe!! Vile vile , hivyo yanakuwa ni maombi ya siri kila mmoja kwa mwenzake. Maombi ya namna hiyo mbele za Mungu huwa hayana matunda yoyote kinyume chake ni kumuhuzunisha Mungu.
Jambo mojawapo ambalo lilimfanya Ayubu aonekane ni MKAMILIFU na MWELEKEVU mbele za Mungu, ni kutokufurahia pale adui zake walipoanguka. Tukisoma katika Ayubu 31,
Ayubu 31: 29 “KAMA NILIFURAHI KWA KUANGAMIA KWAKE HUYO ALIYENICHUKIA, AU KUJIKUZA ALIPOPATIKANA NA MAOVU;
30 (NAAM, SIKUKIACHA KINYWA CHANGU KUFANYA DHAMBI KWA KUUTAKA UHAI WAKE KWA KUAPIZA);”
Unaona hapo?. Ayubu aliogopa hata kumwapiza adui yake mbele za Mungu, kwamba Mungu autoe uhai wake.Walikuwepo watu waliomdharau sana na kumchukia, waliomnenea vibaya, waliokuwa wanamtukana pengine kwa ajili ya haki yake, wapo waliokuwa wanamwonea wivu kwa kufanikiwa kwake, lakini hao hao Ayubu alipoona wameanguka, au wamepatikana na shida, au wamepata madhara au misiba. Ayubu hakusema sasa huu ni wakati wa kusheherekea, kwasababu Bwana amewalipiza kisasi wale waliokuwa wananichukia, maadui zangu wote,.kinyume chake yeye aliwahurumia, na kuwaombea, na kuwatakia heri siku zote, na ndio sababu iliyomfanya Ayubu alionekana kuwa mtu wa kipekee sana mbele za Mungu..mpaka Bwana akamwambia shetani “Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, MTU MKAMILIFU na MWELEKEVU, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu. (Ayubu 1:8)”.
Kadhalika pia tukimwangalia Bwana wetu YESU, hakuna mtu yoyote duniani aliyekuwa na maadui wengi kama yeye, Wewe unasema unao maadui, lakini hao maadui zako hawana hata mpango wowote wa kutoa maisha yako kwa gharama zozote, lakini Bwana wetu Yesu alikuwa na maadui ambao baadaye walifanikiwa kuja kumshika na kumtukana,kumdhihaki, kumtemea mate,kumvua nguo, kumpiga, kumwaibisha hadharani na hatimaye kumuuwa,,Lakini je! Aliwatakia laana mbele za Mungu?. Jibu ni Hapana kinyume chake tunaona aliwaombea, na kusema..”Ee Baba uwasamehe, kwa kuwa hawajui walitendalo”.Aliwaombea rehema badala ya Laana..Aliwaombea amani badala ya misiba.
Mahali pengine alifika maadui zake wakamkataa, na wanafunzi wake walipomshauri ashushe moto awaangamize kama Nabii Eliya alivyofanya lakini yeye aliwaambia,
Luka 9: 54 “Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?
55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]
56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine”.
Unaona hapo?. Swali ni lile lile na wewe leo ni roho gani ipo ndani yako?. Kuangamiza au kuokoa,? Biblia inatumbia “Upendo huvumilia yote”, Upendo HAUHESABU MABAYA,(1Wakorintho 13) , Unachopaswa kufanya ni kumwomba Mungu amwokoe na sio kumwangimiza kwa dua zako, Tunachopaswa kuomba, ni Mungu atuepushe na madhara yao, na sio Mungu awaangamize, na ndio maana Bwana Yesu alisema ili sisi tuwe WAKAMILIFU kama Ayubu, ili sisi tuwe WAKAMILIFU kama BABA yetu wa mbinguni tunapaswa tulizingatie Neno hilo…Alisema:
Mathayo 5: 43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?
48 Basi ninyi mtakuwa WAKAMILIFU, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo MKAMILIFU”.
Hivyo ndugu Mungu hapendezwi kila siku tunapompelekea mashtaka mabaya dhidi ya maadui zetu, hiyo inatufanya tunaonekana kuwa hatujakamilika mbele zake, sio kila mara tuzunguke huku na huku, tukisema ..Adui yangu apigwe!..Adui yangu afe!! Adui yangu ashushwe!!…Kwanini tusiseme Adui yangu Bwana ambadilishe!!..Kwanini tusiseme ..Mungu mpe rizki Adui yangu”…kwanini tusiseme Mungu mrehemu adui yangu, hajui alitendalo??… Badilika sasa, Acha kumgeuza mtu kuwa adui yako pale anapokusengenya, pale anapokutukana, pale anapokudharau, au anapojitukuza juu yako.. Kumbuka maisha yako ndiyo yatakayougeuza moyo wa huyo ndugu yako, Fuata ule ushauri wa Bwana, mwombee. Na ndivyo tutakavyoonekana kuwa WAKAMILIFU mbele za Mungu.
Ubarikiwe.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.
Mada Nyinginezo:
NoLuka 5: 1 “Ikawa makutano WALIPOMSONGA wakilisikiliza neno la Mungu, yeye alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti,
2 akaona vyombo viwili vimekaa kando ya ziwa, lakini wavuvi wametoka, wanaosha nyavu zao.
3 Akaingia katika chombo kimoja, ndicho chake Simoni, akamtaka akipeleke mbali kidogo na pwani. Akaketi, akawafundisha makutano ali chomboni.
4 Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki.
5 Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.
6 Basi, walipofanya hivyo walipata samaki wengi mno, nyavu zao zikaanza kukatika;
7 wakawapungia mikono washirika wao waliokuwa katika chombo cha pili, waje kuwasaidia; wakaja, wakavijaza vyombo vyote viwili, hata vikataka kuzama”.
Tukio hilo lililowapata wakina Petro linaweza likaonekana ni dogo lakini linabeba siri kubwa sana ya mafanikio hususani kwa wale watu ambao shughuli zao za kujipatia kipato haziendi sawa. Hivyo kama wewe ni mmoja wapo somo hili litakufaa sana. Soma hadi mwisho, lakini kama mambo yako yanaenda vizuri basi halitakuhusu sana., Zidi tu kuendelea kujifunza masomo mengine yahusuyo utakatifu na ufalme wa mbinguni.
Ukitafakari hiyo habari utaona Bwana Yesu, alikuwa akihangaika sana katika kuwafundisha makutano, yale mazingira yalikuwa ni magumu sana kutokana na kwamba watu wengi walimsonga na yeye alitaka kuwafundisha zaidi katika utulivu, hivyo hakuona kama akiendelea katika hali ile ile atatimiza kusudi lake, ndipo akaamua atafute madhabahu ya kuwakutanisha wale watu pamoja, mahali atakapotulia ili awafundishe wale watu katika ustaarabu na utaratibu ambao Mungu ameukusudia..
Na alipogeuka akaona vyombo viwili vimeegeshwa pwani na wenye navyo wametoka, ndipo akikichagua cha mmojawapo na kukigeuza kuwa madhabahu yake ya muda.
Sasa Chombo kinawakilisha nini katika mazingira tuliyopo leo?. Chombo kinawakilisha kitu chochote cha kujipatia kipato, kumbuka chombo hicho Bwana alichokitumia kilikuwa ni cha akina Petro cha kuvulia samaki, kwasasa hivi chombo kinaweza kikawa, elimu ya mtu, ujuzi wa mtu, biashara ya mtu, fremu ya mtu, shamba la mtu, kiwanja cha mtu,n.k.
Lakini tunasoma katika habari hiyo, tunaona Bwana alipotazama hakuchagua vyombo vilivyokuwa kando kando vyenye wavuvi au samaki, kumbuka vilikuwepo tu vingi vizuri zaidi ya hivyo vilivyokuwa vinazungukazunguka maeneo yale, lakini yeye hakuchagua chochote kati ya hivyo bali alivichagua vile visivyokuwa na kitu ndani yake…(Na ndio maana somo hili linawahusu sana wale ambao shughuli zao haziendi sawa),
Sasa kilichotokea ni kwamba wakina Petro walifanya kazi ya kuchosha usiku kucha wakihangaika kutafuta samaki ukanda mzima wa ziwa la Genesareti kwa shida, na kujitoa kweli kweli lakini wasipate kitu, mpaka kulipokucha wakakata tamaa ya kuendelea kuvua tena, wakaona kilichobakia tu ni kukipumzisha chombo na kuzitengeneza nyavu zao tena, kisha kuzihifadhi mpaka wakati mwingine,
Lakini baadaye kidogo ndio tunamwona Bwana Yesu akisumbuka na wale makutano, ndipo wao wakamruhusu Bwana kutumia vile vyombo ili kutimiza kusudi lake la kuhubiri,. Na baada ya Bwana kumaliza kuhubiri, sasa wakati makutano yote wameshaondoka ndipo akawageukia wale wamiliki wa vile vyombo, na kuwaambia NENDENI VILINDINI MKASHUSHE NYAVU ZENU, MVUE SAMAKI.
Lakini wao walimwambia, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha pasipo mafanikio, na walipokubali tu kwenda kuvua walipata matokeo makubwa ya kushangaza, mpaka nyavu zao kuanza kukatika, mpaka kufikia hatua ya kuomba msaada kwa wingi wa Baraka hizo, maana rizki imekuwa nyingi na kuwalemea mpaka hawawezi tena kuimaliza wao wenyewe ikawabidi wawaite na marafiki zao na maadui zao waokote na wao pia wapate kidogo..
Bwana Yesu hajabadilika, ni yeye Yule jana, na leo na hata milele, njia aliyotumia kumbarikia Petro ndiyo hiyo hiyo atakayoitumia sasahivi kukubariki na wewe uliyefanya kazi ya kuchosha miaka na miaka bila mafanikio yoyote. Umejaribu kufanya kwa bidii kazi lakini unachokipata hakijitoshelezi…
Leo hii hicho chombo chako kigeuze kuwa MADHABAHU YA KRISTO kwasababu anakitafuta hicho ili ilifanye kusudi lake, kumbuka pale Bwana hakutafuta sinagogi la kuwakusanya wale makutano waliokuwa wanamsonga, hakutafuta hekalu, wala hakutafuta mahali patakatifu bali alitafuta MAHALI PA KUJIPATIA KIPATO KWA MTU, mahali ambapo mtu anapopategemea kujipatia mkate wake wa kila siku, na pia fahamu tu, siku zote Bwana anapaangalia mahali ambapo palipo patupu kama kwako wewe, Mahali ambapo pamefanyika kazi ya kuchosha miaka mingi, miezi mingi pasipo mafanikio yoyote, hapo ndipo anapopataka kwa ajili ya kazi yake, na akishamalizana napo hapo, ndipo atakwambia nenda katupe nyavu zako kilindini uvue samaki, kwa wingi wa atakachokupa Bwana utaita mpaka na marafiki na zako na maadui zako waje nao kushiriki Baraka zako Mungu alizokuandalia.
Leo Kazi yako wewe ni ya ufundi, una ujuzi wa kutosha kuhusu masuala ya ujenzi, na unaona mahali unapokusanyikia pengine ni kanisani kuna kasoro Fulani ya ujenzi, na shughuli zako za kijenzi haziendi sawa, umekuwa ukipata mapato kidogo kupitia hiyo,wakati mwingine unakosa kabisa kazi, huo ndio wakati wa kwenda kumruhusu Bwana atumie hicho chombo chako (ujuzi),
nenda mahali unapokusanyika (kanisa), kazi ya Mungu inapofanywa, angalia kasoro zinazohusiana na taaluma yako, na utumie ujuzi wako kurekebisha tatizo hilo bila kutazamia malipo yoyote, pengine umeona ukuta wa kanisa umebomoka au una ufa, uzibe, umeona mfumo wa maji haujakaa sawa na una ujuzi wa kufanya hivyo, urekebishe hata kama hauna chochote, umeona kanisa halina choo kinachostahili, na wewe una ujuzi wa namna ya kutengeneza vizuri, nenda kafanye hivyo, kajenge kwa ustadi wote, na maarifa yako yote, umeona kuna kasoro ya umeme na mfumo wa nyaya, na una ujuzi huo nenda karekebishe usisubiri hata mtu akamwambie, mruhusu Bwana atumie hicho chombo, na mwisho wa siku utaona tofauti yako na mtu asiyefanya hivyo wakati Fulani ukifika.
Au wewe ni polisi au mlinzi, anza kutoa mchango katika sekta hiyo ndani ya kazi ya Mungu..Usiseme Mungu kweli ataweza kutumia taaluma hii/ujuzi huu kwenye kazi yake??..kumbuka Bwana Yesu alitumia mtumbwi wa wavuvi kuwapelekea maelfu ya watu katika ufalme wa mbinguni…Na wewe vivyo hivyo mpe Bwana chombo chako.
Au wewe unafanya kazi ya upishi, na unaona kazi zako haziendi sawa, faida ndogo, na unaona kuna uhitaji mkubwa wa wapishi ndani ya nyumba ya Mungu, labda kwa ajili ya wazee wasiojiweza (wakristo), au wageni, au wenye mahitaji na mayatima (walio wakristo), ndani ya kanisa n.k usingoje uambiwe au uwe na kitu kwanza ndio ufanye, wewe mwenyewe anza kuchukua hatua ya kujitolea kwenda kuifanya, tena pasipo hata kuombwa.
Wewe ni mtengeneza bustani, na ndiyo kazi yako umekuwa ukifanya kwa ajili ya kujipatia kipato..Lakini mazingira ya kanisani ni machafu au hayavutii, panaonekana ni mahali pasipo tofauti na sehemu nyingine yoyote, Tumia chombo chako (ujuzi) kurekebisha mazingira ya Mungu, pakavutia kama vile unavyopendezesha bustani za watu wengine,..unaweza ukaona ni jambo dogo lakini linamaana kubwa na Bwana akisharidhika atakuambia shuka vilindini..utaona milango Mungu anayokufungulia katika hiyo hiyo kazi yako ilivyo ya ajabu.
Wewe ambaye ulikuwa unatafuta kazi,na bado hujapata, angali unao ujuzi Fulani, usiuache ulale utumie huo ujuzi katika kazi ya ufalme wa mbinguni, kwamfano labda wewe ni “ IT ” (mjuzi wa katika teknolijia ya Kompyuta), unaweza uka unda wavuti na tovuti kwaajili ya kutangaza ufalme wa mbinguni, unaweza ukabuni programu za kutangaza kazi ya Mungu kirahisi katika mitandao fanya kiuaminifu kabisa..Na Bwana akishamaliza kutenda kazi kwa kutumia chombo chako, atakuambia shuka vilindini…Utaona nafasi ambayo ulikuwa unaitafuta kwa kuhangaika kwa muda mrefu pasipo mafanikio kama wakina Petro walivyokuwa..unaipata ndani ya kipindi kifupi tena chenye faida mara 100 zaidi ya kile cha mwanzo ulichokuwa unakihangaikia..
Lakini hizo zote zinakuja kwanza kwa kumtolea Bwana chombo chako akitumie, kwa ajili ya kazi yake, lakini kuna wengine hawapendi kumpa Bwana nafasi lakini wanataka Baraka za Bwana, utakuta mtu analo eneo kubwa limekaa pasipo matumizi yoyote, hataki hata kukaribisha watu wafanyie kazi za mikutano ya injili hapo, na bado anataka Mungu ambariki, ndipo hapo zile roho za udanganyifu zilizoachiliwa katika siku za mwisho zinaanza kumdanganya na kumshawishi, akanunue mafuta ya upako, anunue chumvi na maji ya Baraka akanyunyuzie kwenye kiwanja chake na kwenye biashara yake, aanze kukemea roho za laana katika kiwanja chake, au biashara zake, ili mambo yake yaanze kwenda vizuri.
Utamkuta mwingine anazo fremu za vyumba na zimekosa mpangaji wa kufanyia biashara au tution,..na wakati huo huo kuna wakristo wenzake wamekuja kumwomba awape angalau fremu moja wawe wanafanyia bible study au maombi wakati wa jioni kwa muda huku wanatafuta eneo lingine..lakini kwasababu hajui uweza wa Mungu, anawazuilia na kuona bora tu ziendelee kuwa zimefungwa.na wakati huo huo anazunguka kutafuta kuombewa na kununua maji na mafuta ya upako huku na kule hata wakati mwingine nchi na nchi..Mtu wa namna hii hawezi kutazamia miujiza kama waliofanyiwa wakina Petro.
Bwana anasema nikaribieni, nami nitawakaribia… Wakati mwingine hilo pigo unalolipata la kuvuna haba, ni kwasababu kazi ya Mungu inakaa katika hali ya kusongwa songwa na wewe hutaki kulitazama hilo kwa kumzuilia Bwana chombo chako..(Soma Hagai 1:1-12). Anza leo kufanya kama akina Petro walivyofanya na Mungu atakubariki. Mtaijua kweli nayo kweli itawaweka huru.
Ubarikiwe.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu.
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Kwanza jambo la kufahamu ni kwamba kila mkristo anapaswa awe na Roho Mtakatifu, ambaye kwa huyo biblia inasema ATATUONGOZA NA KUTUTIA KATIKA KWELI YOTE.
Yohana 16: 13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake”.
Hivyo mtu yeyote asiyekuwa na Roho wa Mungu biblia inasema huyo si wake (Warumi 8:9), Haiwezekani kumjua Mungu kwa namna yoyote ile,. Sasa tatizo linatokea ni pale unakuta watu wengi walipokea kweli Roho Mtakatifu mwanzoni walipoamini, lakini ilifikia wakati Fulani wakamzimisha pasipo hata wao kujijua, Uthibitisho ni kwamba utasikia mtu anakwambia mwanzoni nilipompa Bwana maisha yangu nilikuwa ni moto sana, lakini siku hizi nimepoa, ile nguvu ya mwanzo sina..sasa hiyo ni dalili ya awali kabisa ya mtu aliyemzimisha Roho ndani yake, biblia inasema, katika (1Wathesalonike 5: 19 MSIMZIMISHE ROHO; )
Unaweza ukaona hapo, Roho wa Mungu anaweza kuzimishwa, na anazimishwa kwenye nini?, ,Jibu ni kwamba anazimishwa katika eneo la kuendelea kukuongoza katika kweli yote.. Na madhara ya kutofikia kile kiwango kinachohitajika na Mungu ni kukaa katika hali hiyo hiyo ya kutokuwa na ufahamu wa kutosha kumuhusu Mungu,hivyo ni rahisi kudanganywa na kuchukuliwa na mafundisho mengi ya uongo, unakuwa ni kama unyasi unaotikiswa na upepo.
Sasa njia pekee inayowasababisha wengi wamzimishe Roho ni UDINI na UDHEHEBU, Kwa mfano wakati Bwana Yesu alipokuwa duniani, aliwakuta watu wakiwa katika dini zao na madhehebu yao, nao si wengine zaidi ya mafarisayo na masadukayo, Hawa watu sio kwamba walikuwa ni wabaya sana, hapana, kwanza vitu vingi walivyokuwa wanashika yalikuwa ni maagizo ya Mungu, na walikuwa wanafanya bidii kweli katika kuvishika na kuvisimamia, lakini torati waliyokuwa wanaishika haikuwa imekamilika, na alipokuja Bwana kuwaeletea habari ya kuitimiliza torati, walimpinga na kumkataa, lakini ni kwasababu gani?, sababu ilikuwa si nyingine zaidi ya kujikinai katika Dini zao na udhehebu wao. Na kukataa kumruhusu Roho Mtakatifu awafundishe zaidi na kuwatia katika kweli yote…
Sasa matokeo yake wakaukosa uzima waliokuwa wanautazamia na kupelekea kugeuka kuwa wapinga-Kristo badala yake. Kwasababu walihama kabisa katika kuongozwa na Roho wakaenda katika kuongozwa na dini, na taratibu za madhehebu yao..Pengine walianza kusema dhehebu letu ndio la zamani na la kipekee, lina watu wengi, tuna masinagogi mengi duniani kote,..Tunaheshimika na mataifa yote, tuna wasomi wengi, tunafadhili miradi mingi ya kijamii, tunaongoza katika kusaidia maskini na yatima,..Sasa huyu mtu anayejiita YESU, na Yohana Mbatizaji wanatuletea habari za ubatizo wa maji, wanazitolea wapi? Mambo hayo hayapo kwenye torati, kwanza ni watu wa kawaida, wanatafuta wafuasi,..Lakini Bwana Yesu aliwaambia kwa ufunuo wa Roho Mtakatifu, Yohana 3:5 ”….Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.”
Sasa wao walibakia tu katika sheria za dini na madhehebu, kwamba usipotahiriwa huwezi kumwona Mungu,
Kadhalika na katika wakati huu wa sasa, hakuna mahali popote Mungu alianzisha dhehebu, sisi wote kwa pamoja ni wakristo, na mikusanyiko yote yanapaswa yawe na imani moja, ubatizo mmoja na Roho mmoja, Bwana mmoja, Mungu mmoja, (Waefeso 4:4-5), lakini hiyo imekuwa ni tofauti katika kanisa la leo, imani ni nyingi tofauti tofauti, batizo ni nyingi tofuati tofuati, na kibaya zaidi ni kwamba kila mmoja anaamini cha kwake ndio sahihi,..wengine wanasema sisi ni wa Luther, wengine wanasema sisi ni wa Branham, wengine wanasema sisi ni wa Hellen White, wengine wanasema sisi ni wa John Wesley, n.k… Lakini Mtume Paulo baada ya kuliona jambo kama hilo la kanisa kugawanyika vipande vipande katika madhehebu alisema hivi…
1Wakorintho 1: 12 Basi, maana yangu ni hii, ya kwamba kila mtu wa kwenu kusema, Mimi ni wa Paulo, na, Mimi ni wa Apolo, na, Mimi ni wa Kefa, na, Mimi ni wa Kristo.
13 Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulibiwa kwa ajili yenu? Au je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Unaona hapo? Kanisa la Kristo haligawanyiki kwasababu Kristo hajagawanyika, tungepaswa wote tunapokusanyika wote tunakuwa ni ndugu katika Imani moja. Sasa inapotokea Roho wa Mungu anapotaka kumwongoza mtu katika kuijua kweli zaidi, labda tuseme anamfundisha juu ya ubatizo sahihi ya kwamba anapaswa akazamishwe kwenye maji mengi, na kwa jina la YESU KRISTO,. Lakini mtu Yule mtu badala ya kuchunguza maandiko na kumwomba Roho Mtakatifu amsaidie, moja kwa moja atakwenda katika dhehebu lake, je! Wanaamini hivyo?, akikuta dhehebu lake hawaamini hivyo, basi na yeye analitupilia mbali. Hajui kwamba ameshamzimisha Roho pasipo hata yeye kujijua, na watu wa namna hiyo ukitazama maisha yao ya kiroho yanakuwa ni chini siku zote, na mwisho wa siku wanageuka kuwa wapinga-kristo kama walivyokuwa mafarisayo na masadukayo, kwa jambo dogo tu la udhehebu na udini. Wanaanza kuwapinga vikali wale wote wanaofundisha kinyume na mapokea yao.
Tukiyajua hayo sasa, biblia inaposema “TOKENI KWAKE ENYI WATU WANGU” (Ufunuo 18:4), haimaanishi kutoka kwa miguu, bali ni katika roho, na ufahamu, ni kutoka katika kamba za dini na madhehebu, kutoka katika makosa yaliyofanywa, kutokufungwa na mifumo ya dini na madhehebu inatakayokufanya usipige hatua moja ya kiroho (huko ndiko kumzimisha Roho).. Unapoona kweli sehemu Fulani inafundishwa, usikimbilie kulinganisha na dhehebu lako au dini yako inasemaje juu ya hilo..moja kwa moja kimbilia kulilinganisha na Neno la Mungu, hapo ndipo Roho Mtakatifu anaanza kupata nafasi ya kukufundisha na kukuongoza katika kweli yote…
Kwa mfano umesikia mahali unafundishwa ibada za sanamu ni machukizo mbele za Mungu, lakini katika dhehebu lako ni jambo ambalo mmekuwa mkilifanya siku zote. Sanamu imekuwa ni sehemu ya ibada zenu, sasa ili usimzimishe Roho, usikimbilie kwenda kuangalia dhehebu lako linasemaje, wewe kimbilia kuangalia Neno la Mungu linasemaje juu ya hilo, ndio Roho Mtakatifu unakuta anakuongoza katika huu mstari..
2Wakoritho 6: 15 “Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?
16 Tena pana mapatano gani kati ya HEKALU LA MUNGU, na SANAMU? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
17 KWA HIYO, TOKENI KATI YAO, MKATENGWE NAO, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.
18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,”
Sasa ukishalifahamu hilo kwa usalama wa Roho yako, unapaswa uondoke hapo, utafute sehemu nyingine ambayo sanamu haichanganywi na ibada tukufu ya Mungu…kadhalika na mambo mengine kama hayo, kwa jinsi utakavyompa Roho Mtakatifu nafasi atakuwa anakuongoza katika kweli yote mpaka unafikia kimo cha mtu mkamilifu mbele za Mungu.
Kwahiyo unapokaa katika mkusanyiko wowote unaojiita ni wa Kikristo, chunguza ni vipi vinavyoendana na Neno la Mungu, ndivyo ushirikiane navyo, na vile visivyotokana na Neno, jitenge navyo tena mbali sana. Uongozo wako uwe ni BIBLIA na hapo ndipo Roho Mtakatifu atakapotumia kukuongozea.
Pia ni muhimu kukumbuka madhehebu ndiyo yatakayokuja kuunda ile chapa ya mnyama huko mbeleni..kwahiyo ni kuwa makini sana. Kadhalika katika siku za mwisho Bwana Yesu alisema kutakuwa na makundi mawili ya wakristo,. Kundi la kwanza linajulikana kama wanawali wapumbavu na la pili kama wanawali werevu (Mathayo 25). Ukisoma pale utaona Wale werevu walibeba Taa pamoja na mafuta yao ya ziada wakati wa kwenda kumlaki Bwana wao, lakini wale wapumbavu hawakubeba mafuta ya ziada, na wakati Bwana wao alipokaribia kuja taa zao zikaanza kuzima, kwasababu hawakuwa na mafuta ya ziada, hivyo hawakufanikiwa kuingia katika karamu ya Bwana wao japo nao walikuwa wanamngojea Bwana wao..
Lakini wale wanawali werevu wanawawakilisha wakristo waliopokea Roho Mtakatifu na kwasababu ni werevu hawakuridhika na mafuta waliyonayo machache, walitembea na mafuta mengine ya ziada ambayo yanawakilisha ufunuo na mafundisho ya Roho Mtakatifu hivyo mpaka Bwana alipokuja wakakutwa taa zao bado zinawaka, na ndipo wakaenda naye karamuni (huko ndiko kutokumzimisha Roho). Lakini wale wapumbavu ni wakristo ambao baada ya kumpa Bwana maisha yao, wakaridhika tu katika mapokeo ya dini zao na madhehebu yao, na siku Bwana atakapokuja atawakuta katika hali hiyo ya uvuguvugu, kuzimika kwa taa zao (kwasababu walishamzimisha Roho Mtakatifu zamani)..Hivyo watatupwa katika lile giza la nje, ambalo hilo linawakilisha dhiki kuu na ziwa la moto.
Hivyo ndugu unaona madhara ya kutotembea na Roho Mtakatifu katika safari yako ya ukristo? anza sasa kumruhusu Roho atende kazi ndani yako, toka katika kamba za dini na madhehebu, dumu katika Neno ili Mungu akufikishe mahali alipokusudia ufike.
Ubarikiwe sana.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
MUUNGANO WA DINI NA MADHEHEBU YOTE, UMEKARIBIA.
UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA
HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA
JE! INAWEZEKANA MTU AKAWA ANAFANYA MIUJIZA NA BADO ASINYAKULIWE?
Shetani tangu zamani amekua akibuni njia mbali mbali za kumfanya mwanadamu aangumie kwa anguko litakalomfanya asiweze tena kurudi nyuma, Na amekua akifanya hivyo kwa kuchunguza ni njia ipi inayomchukiza Mungu zaidi kuliko nyingine, na akishaipata anakwenda kuwashawishi wanadamu waitende hiyo ili Mungu asiwe na huruma kwao, waangamizwe moja kwa moja.
Kwa mfano tukisoma katika agano la kale, Bwana aliwapa wana wa Israeli amri 10, na zile nne za kwanza, zilimuhusu Mungu mwenyewe, waliambiwa wasiwe na miungu mingine ila Mungu wa Israeli, waliambiwa pia wasijifanyie sanamu ya kuchonga, kwani yeye ni Mungu mwenye wivu, waliambiwa pia wasilitaje bure jina la Bwana Mungu wao,..Sasa ukichunguza utaona shetani alipoona kuwa hizi ndizo Mungu kazitilia msisitizo, na kaziwekwa za kwanza kabisa, tena alipogundua kuwa Mungu ni Mungu mwenye wivu, ndipo akaanza kuwekeza nguvu zake zote hapo, kuwashawishi watu waiendee miungu mingine, na kuabudu sanamu, ili tu, Mungu atiwe wivu, awateketeze watu wake kwa maangamizi yasiyoweza kuponyeka, Na ndio maana ukisoma agano la kale, makosa mengi yaliyokuwa yanawakosesha wana wa Israeli wakati wote mpaka kuwasababishia kupelekwa utumwani, ni IBADA ZA SANAMU.
Hiyo ndio imekuwa desturi ya shetani katika vizazi vyote, lakini pia katika kipindi hichi tunachoishi Mungu alitoa amri ya kile anachokichukia zaidi na ndipo hapo hapo shetani naye kaenda kuwekeza zaidi nguvu zake ili awaangamize watu wengi kirahisi.
Hivyo ni wajibu wa kila mmoja kufahamu kuwa tunaishi katika Kanisa la mwisho linaloitwa LAODIKIA, kulingana na unabii wa kibiblia, kumbuka yalikuwepo makanisa mengine sita, nayo yalishapita na jumbe zao, na sasa tupo katika kanisa la mwisho, na kanisa hili lilianza kuanzia mwaka 1906 na litaisha na unyakuo… Kwa urefu wa maelezo juu ya makanisa haya 7 unaweza ukasoma kwa kupitia link hii. >>>Nyakati saba za kanisa.
Sasa katika hili kanisa la 7 ambalo ndio tunaishi mimi na wewe, Mungu alizungumza na sisi na kutugawia amri ambayo inapaswa isivunjwe, kama tu ile amri ya kwanza ilivyokuwa katika agano la kale, kwamba mtu yeyote asiwe na miungu mingine ila yeye, kadhalika na katika kanisa hili la mwisho Bwana alitoa amri akasema “UWE MOTO!!”..akaongezea pia na kusema “KAMA HUWEZI KUWA MOTO, NI AFADHALI UWE BARIDI”..hakuishia hapo akaelezea jambo analolichukia kuliko yote, nalo ni “KUWA VUGUVUGU”..
Sasa shetani kwa kulijua hilo, ili amwangamize mwanadamu vizuri, na kumvunja vunja kabisa alikwenda kuwekeza nguvu zake zote mahali ambapo panamkasirisha Mungu zaidi, ili tu mwanadamu atakaponaswa hapo iwe ni ngumu kupona, aangamie milele..na sehemu hiyo sio nyingine zaidi ya kumfanya mtu awe vuguvugu.
Kumbuka shetani sasa hivi hatumii nguvu nyingi sana kuwafanya watu wawe BARIDI, yaani kuwafanya watu wasimjue Mungu kabisa, au kuwafanya wawe wa kidunia kabisa wasitake kujua Mungu au kanisa ni nini! Hapana, hatumii nguvu kubwa kuwafanya watu wasimsikie Yesu Kristo kabisa, yaani waendelee kuabudu miti, n.k. hapana hatumii nguvu kubwa huko kwasababu anajua hapo pana HERI pengine huko mbeleni neema ya Mungu ikipita juu ya huyo mtu kidogo tu anaweza kubadilika na kuwa MOTO..
Shetani anachofanya yeye sasa na majeshi yake, ni kuhakikisha kwa nguvu zote watu wanakuwa VUGUVUGU, yaani anahakikisha kuwa mtu anamfahamu Mungu, lakini amchanganye kidogo na mambo ya giza, anafanya juu chini mtu aende kanisani, baadaye akitoka aende disco, hataki awe ni mtu wa disco tu siku zote na asiende kanisani kabisa hata siku moja, hataki mtu awe ni wakidunia tu siku zote na hata siku moja hana habari na Mungu, anataka vyote vifanyike kwa pamoja kwasababu anajua Mungu kasema ni HERI mtu awe BARIDI kabisa kuliko VUGUVUGU. Kwasababu kama tulivyosema Shetani anajua mtu aliye baridi kabisa pengine huko mbeleni akisikia ukweli kidogo anaweza kubilika hivyo hawezi kuweka tegemeo lake kubwa kwa mtu wa namna hiyo kuliko Yule aliye vuguvugu.
Bwana Yesu alisema maneno haya kwa kanisa hili:
Ufunuo 3:14 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu.
15 Nayajua matendo yako, YA KUWA HU BARIDI, WALA HU MOTO; ingekuwa HERI kama ungekuwa baridi au moto16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, NITAKUTAPIKA UTOKE KATIKA KINYWA CHANGU ”.
Kama tunavyosoma, adhabu iliyonenwa hapo ya mtu atakayekuwa vuguvugu ni KUTAPIKWA,..Na mtu akishafikia hiyo hatua, basi hawezi kurudi nyuma kuokolewa tena, mtu huyo anakuwa tayari kashatengwa na uso wa Mungu milele, Ulishawahi kuona mtu yeyote akirudia kula matapishi yake tena?, Ni jambo lisilowezekana kabisa, yale matapishi sio chakula tena, ni sawa ni kinyesi tu, hata kuyatazama utaona kinyaa, na ndivyo ilivyo kwa mtu Yule aliye vuguvugu. Na ndio maana Bwana alisema ni heri uwe moto au baridi kuliko kuwa hapo katikati kwasababu mtu wa namna hiyo akishatapikwa kurudiwa tena ni ngumu.
Kumbuka kama tulivyoona shetani hapo ndipo anatilia mkazo, na kashafanikiwa kuwaweka watu wengi katika hali hiyo, mtu awe anajiita mkristo lakini bado ni mlevi, aende kanisani lakini bado anaenda kwa waganga wa kienyeji, kabatizwa katika ubatizo sahihi lakini bado anavuta sigara, anaimba kwaya lakini bado ni mwasherati, analipa zaka lakini bado anatoa hongo, anatabiri na kunena kwa lugha lakini bado anavaa mavazi ya kiasherati, anavaa vimini, suruali, kaptura, anapaka wanja, anahudhuria maombi lakini bado ni msengenyaji na bado anajiita mkristo, unafunga na kusali na babo unaishi na mwanamume au mwanamke ambaye hamjafunga ndoa, ni mshirika wa kwaya na bado umeachana na mke wako au mume wako..Hapo ndipo shetani anapotilia nguvu nyingi.
Sasa shetani ili kulifanikisha jambo hilo,aliwatia mafuta watumishi wake kuwafanya watu wawe BARIDI, pamoja na kuwa VUGUVUGU, wale wanaowafanya watu wawe baridi ndio hao waganga wa kienyeji, na vikundi vya kishetani, pamoja na watu waovu wa ulimwengu huu, lakini hao kama tulivyosema sio wabaya sana, Wapo watumishi wengine wa uongo waliochaguliwa na shetani mahususi kwa kuwafanya watu wawe vuguvugu…Hawa ndio wale mbwa mwitu Bwana aliowasemea katikakati ya kondoo,.
Mathayo 7: 15 “Jihadharini na MANABII WA UONGO, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.
16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? “
Unaona hapo? Hawa wanabeba biblia kama wewe, wanajiita watumishi wa Mungu, na njia pekee ya kuwagundua si kwa kuwatazama bali ni kwa matunda yao,..kwa kutazama jamii ya watu wanaowazalisha(ndio matunda yao), utaweza kufahamu hao watumishi ni wa aina gani…kama ni vuguvugu,moto, au baridi…
Ukiona umedumu kwa muda mrefu katika mafundisho yao, na hujaona mahali popote unagusiwa juu ya hatma ya maisha yako ya kiroho kuhusu mbinguni na kuzimu, ufahamu kuwa upo katika sehemu ya hatari zaidi kuliko ungeenda kujiunga na vikundi vya kichawi au vya waganga wa kienyeji,..ukiona haugusiwi habari za mbinguni kila siku ni biashara tu na mafanikio, upo katika eneo la hatari kuandaliwa kutapikwa na Bwana.,ukiona mahali hapo haugusiwi habari za kutubu dhambi na kuishi maisha matakatifu,badala yake unahubiriwa injili za faraja tu, huku maisha yako ya kiroho yanaporomoka kila siku fahamu kuwa upo mahali pa hatari sana, inusuru roho yako.
Ukiona mahali ambapo huubiriwi misingi ya imani ya kikristo, yaani ubatizo wa maji tele, na ubatizo wa Roho Mtakatifu badala yake ni kupewa tu maji, na chumvi, na sabuni, kama njia ya kufunguliwa, kwasababu biblia inasema mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho hawezi kuingia ufalme wa mbinguni (Yohana 3) jua tu upo katika eneo la hatari, ukiona mahali Neno la Kristo halipewi kipaumbele au muda mrefu kuhubiriwa fahamu kuwa unatengenezewa mazingira ya kuwa vuguvugu, ukiona upo mahali hauhubiriwi usafi wa mwili wako na roho yako, haufundishwi umuhimu wa kujisitiri kwa mwanamke,(1Timotheo 2:9) unakwenda kanisani na vimini, na hauambiwi chochote, ujue kuwa upo katika mikono ya watumishi wa shetani.. Dhumuni la shetani ni kukuweka chini ya mikono yao ili uendelee kuwa vuguvugu, ufikie kipindi Fulani utapikwe na Bwana.
Hata kama watafanya miujiza kiasi gani jiepushe nao Bwana Yesu alisema..
Mathayo 7: 22 “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.
Na ndio maana Bwana anasema ni HERI KUWA MOTO, AU BARIDI kuliko kuwa VUGUVUGU, kwa maana nyingine adhabu ya mtu atakayekuwa vuguvugu huko aendako itakuwa ni kubwa kuliko ya Yule aliye baridi kabisa.
Ndugu hii injili unayoisikia kila siku, na hutaki kubadilika, unasema wewe ni mkristo lakini ukiangalia maisha yako na maandiko ni mbalimbali, umejiweka katika eneo la hatari zaidi, shetani anakufurahia kukuona katika hali hiyo, akisubiria hiyo siku Bwana atakayosema basi yatosha! Ili utapikwe, shetani anataka awe na uhakika wewe unakuwa wake milele. Hataki kukupoteza kwa namna yoyote ile na ndio maana anataka uendelee katika hali yako ya UVUGUVUGU. Ujione upo sawa na Mungu kumbe haupo sawa, ujione unempendeza Mungu kumbe unamchukiza n.k, Ni mara ngapi umesikia sauti ya Mungu ikisema na wewe ndani ya moyo wako na hutaki kubadilika?.
Ndugu maneno ya Bwana YESU ni kweli na amina, hasemi UONGO wala HATANII akisema atakutapika ni kweli atakutapika, hivyo mgeukie leo Bwana kikamilifu kama hujafanya hivyo toka katika kamba za kidini na madhehebu zinazokulewesha kukufanya ujione ni mkristo kumbe sio, tafuta kweli ya Neno la Mungu kwa gharama zote. Hili ndilo SHAURI la BWANA YESU KWAKO NDUGU wa Kanisa hili la Laodikia..
Ufunuo 3: 16 “Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
18 NAKUPA SHAURI, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.
19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami”
Ubarikiwe!
Tafadhali “washirikishe na wengine ujumbe huu”
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
ZIFAHAMU NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE SABA.
MITUME WOTE WALIOPITA WALIKUWA NI WATU WEUPE, JE! NI KWELI NGOZI NYEUSI ILILAANIWA ?
SABATO HALISI NI LINI, JE! NI JUMAPILI AU JUMAMOSI?, NI SIKU GANI ITUPASAYO KUABUDU?
Je! Unafahamu yatakayotokea muda mfupi sana kabla ya kuondoka kwetu kwenda kumlaki Bwana mawinguni?..Ni kweli unyakuo utakuja tu ghafla kwa watakatifu wa Mungu?, Kama haufahamu Biblia ilishatupa mwangaza juu ya suala hilo tunasoma katika;
1Wathesalonike 5: 1 “Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.
2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.
3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.
4 BALI NINYI, NDUGU, HAMMO GIZANI, HATA SIKU ILE IWAPATE KAMA MWIVI.
5 Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.
6 Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.
7 Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku.
8 Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu”.
Unaona hapo maandiko yanaeleza wazi kabisa, siku ile itakuwa kama mwivi kwa wale mataifa(wasio watakatifu) wasiomjua Mungu, kwasababu wao wapo gizani siku zote na usingizi wa mambo ya ulimwengu huu umewalemea, lakini kwa watakatifu wa Mungu, muda mfupi kabla ya siku ya unyakuo kufika watafahamu, na hii ni kutokana na matukio ambayo yatakuwa yanaambatana nao katika siku ile.. Ni kweli biblia haijaeleza siku wala saa lakini imetoa majira(dalili) za kuja kwake, na hizi dalili zipo za ndani na za nje, Sasa za nje ndio kama hizi tunazozifahamu mfano, matetemeko, vita, manabii wa uongo, mji wa Israeli, chukizo la uharibifu n.k…Lakini za ndani zinahusu Ishara inayomuhusu Bibi-arusi wa Kristo peke yake, na hizo zipo tatu,
Leo tutazungumzia moja ya hatua (Ishara) ambayo ni ya mwisho kabisa, itakayowafanya watakatifu sasa wafahamu kuwa siku yao ya kuondoka imefika. Biblia imeeleza wazi unyakuo utaambatana na hatua tatu kuu. 1) MWALIKO WA BWANA, 2) ya pili ni SAUTI YA MALAIKA MKUU, 3) na ya tatu ni PARAPANDA YA MUNGU..
Hatua mbili kati ya hizo tulishazielezea kwa undani katika masomo yaliyotangulia, kama hujazijua unaweza ukazifuatilia kwenye somo linaloitwa UNYAKUO
Lakini leo tutamalizia na hatua ya mwisho ambayo ni PARAPANDA YA MUNGU, hii ni Ishara ya mwisho, kama tunavyoweza kuisoma katika…
1Wathesalonike 4: 13 “Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.
14 Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.
15 Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.
16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na MWALIKO, na SAUTI YA MALAIKA MKUU, na PARAPANDA YA MUNGU; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.
17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.
18 Basi, farijianeni kwa maneno hayo”.
Sasa wakwanza watakaoisikia sauti ya Bwana hawatakuwa watakatifu walio hai, bali ni wale watakatifu waliotangulia kulala mautini, wakati huo wakiwa huko PEPONI walipo wataisikia sauti ya Bwana ikiwaita kutoka makaburini ikiwaambia wakati umefika wa kutoka huko, kama kipindi kile Lazaro aliposikia sauti ya Bwana ikimwita kutoka makaburini ikimwambia,, “Lazaro njoo huku nje”(Yohana 11) Kadhalika sauti hii hii itasikika tena kwa wale watakatifu waliokuwa wamekufa katika Bwana, kama Bwana Yesu alivyosema katika Yohana 5: 25 “Amin, amin, nawaambia, Saa inakuja, na sasa ipo, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai.”..Hivyo hiyo itawafanya watoke makaburini na ile miili yao waliokuwa nayo zamani na kutembea duniani.
SASA SWALI KUU UNAPASWA UJIULIZE, BAADA YA HAO WATAKATIFU KUFUFUKA NI KITU GANI KITAFUATA?
Ili kuelewa vizuri mambo mafupi yatakayofuata hapo katikati, inatupasa tujifunze kwanza kwa yaliyotokea katika ufufuo wa kwanza, Kumbuka Bwana aliwafufua watakatifu wa kwanza, lakini hakuwapeleka mbinguni bali mahali panapoitwa (PEPONI/PARADISO). Lakini kabla ya kwenda huko kuna vitu vilionekana.
Tusome kwa ufupi ni vitu gani vilitokea baada ya wale watakatifu kufufuliwa katika ule ufufuo wa kwanza.
Mathayo 27: 50 “Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.
51 Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
52 MAKABURI YAKAFUNUKA; IKAINUKA MIILI MINGI YA WATAKATIFU WALIOLALA;
53 nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, WAKAUINGIA MJI MTAKATIFU, WAKAWATOKEA WENGI”.
Kumbuka huu ufufuo wa kwanza tunaouna hapo ni kivuli cha ufufuo wa pili, kama vile katika ufufuo wa kwanza kabla ya watakatifu kuingia Peponi waliingia mji mtakatifu na kuwatokea watakatifu wengine waliokuwa hai duniani kwa wakati ule, Vivyo hivyo na katika ule ufufuo wa mwisho wa watakatifu, kabla ya kutoweka duniani kwa watakatifu na kwenda mbinguni kutakuwa na kipindi Fulani kifupi sana ambacho wale watakatifu waliokufa katika Bwana kabla yao, watawatokea wale wanaoishi..
Kumbuka pia walikuwa hawawatokei tu ilimradi,labda kuwafurahisha hapana, bali walikuwa na huduma maalumu ya kuifanya kwa muda mfupi, na hii si nyingine zaidi ya kuwashuhudia wale watakatifu waliokuwa hai kwamba ni kweli wao waliisikia sauti ya waliyemsulibisha YESU KRISTO ikiwaita kutoka katika vifungo vya mauti, na kwamba yeye kweli ndiye MASIHI aliyetabiriwa kuwaokoa watu na uthibitisho ni wao,..
Embu jaribu kutengeneza picha wale wayahudi ghafla wanamwona Baba yao Ibrahimu, na Yakobo na Yusufu wamesimama mbele yao wakiwashuhudia habari za Yesu, unadhani wale watu kuanzia ule wakati walikuwa thabiti kiasi gani?, utawaeleza kitu chochote kuhusu Bwana Yesu?. Ni wazi kuwa yale matukio yaliwapa nguvu wale watakatifu ambao walikuwa wanamtumaini Bwana kama mwokozi wao.
Kadhalika pia na katika ufufuo wa mwisho wa wafu, biblia ilisema hatutawatangulia wale waliolala mautini, kwamba wao ndio watakaofufuliwa KWANZA, ikiwa na maana kuwa wao ndio watakaoisikia sauti ya Mungu kwanza,ikiwaita na kutoka makaburini,. Hivyo kuanzia huo wakati nao pia watawatokea watakatifu wengi watakaokuwa hai duniani. Na hawatawatokea ilimradi kuwafurahisha tu, hapana, bali nao pia watakuwa na hudumu ya muda mfupi sana, watawashuhudia kwamba, ni wameisikia sauti yake ikiwaita watoke makaburini, na ndio maana wapo pale, hivyo ule wakati kwa kwenda KUMLAKI BWANA MAWINGUNI UMEFIKA,
Jambo hilo litawapa nguvu wale watakaokuwa hai,na kwa matukio kama hayo itawaongezea imani kubwa sana ya kuondoka, hii kitakuwa ni kipindi kifupi sana, kumbuka pia watu wengine wasiokuwa watakatifu jambo hili litakuwa haliwahusu, hawatamwona mtu yeyote, hata wale watakatifu waliofufuka kwanza hawakumtokea tu kila mtu Israeli hapana bali watakatifu waliokuwa mji mtakatifu Yerusalemu…Na kwasasa hivi Mji Mtakatifu wa Mungu (Yerusalemu ya mbinguni) ni Kanisa lake takatifu, Hivyo watakao yaona hayo wafu wakipanda makaburini ni watakatifu tu, siku hiyo itakuwa ni furaha kubwa isiyokuwa ya kawaida, na ndio maana biblia inasema siku hiyo haitawajilia kama mwivi kwa kuwa hampo gizani,
Ndipo hapo utashangaa wakati huo, ndugu yako katika Bwana, aliyekufa pengine miaka 20 iliyopita anakutokea na kuzungumza na wewe na kukwambia ule wakati wa kwenda kwa Baba umewadia, wakati huo hata ukijaribu kuwashirikisha watu wengine wasiowatakatifu watakuona kama umerukwa na akili, au umeona mizimu, kwa kipindi hicho kifupi ufahamu wako utakuwa umebadilika na mawazo yako yatakuwa mbinguni,..Pengine utamwona dada aliyekuwa amelala muda mrefu nyuma ambaye alijisitiri kwa usafi wote wa roho na mwili mliokuwa mnafanya wote ushirika kanisani anakujia wakati upo katika shughuli zako za kujipatia rizki, akiwa pamoja na kundi la watakatifu wengine,
Sio hatu tu pia na watakatifu wengine wengi hata wa agano la kale watawatokea wengi…Na kwa muda mfupi sana kuanzia hapo, kufumba na kufumbua miili ya wote itageuka na kuwa ya utukufu, ataungana na wenzako kisha kwa pamoja mtaisikia Parapanda ya Mungu ikiwaita hapo juu, ..HALELUYA hapo tutamwona Bwana.…
Wakati huo dunia yote haitaelewa chochote mambo yanayoendelea, ndio ghafla wale watu ambao ulikuwa unaishi nao watakuona haupo, kumbuka watakaonyakuliwa watakuwa ni wachache sana duniani, hivyo halitakuwa ni jambo la kuishutusha sana dunia, wao wataendelea na shughuli zao kama kawaida wakingojea kufunuliwa kwa mpinga-kristo.
Lakini kama leo hii wewe ni mlevi, ni mwasherati, ni mzinzi, ni mtukanaji, mvaaji wa vimini, mtazamaji wa pornography na bado unajiita mkristo, unategemea mtakatifu gani akutokee siku ile?. Ni dhahiri kuwa haitakuhusu hivyo itakujia kama mwivi tu, kama leo hii tu unajitenga na watakatifu kutokana na uvaaji wako, na ulevi wako, na tabia zako,na anasa zako, kama umeshindwa kuungana nao hapa, utawezaje kuungana nao kule,?, utawezaje siku ile kutokewa na mtume Paulo, mtume Petro, Musa, Stephano, utawezaje siku ile kumwona mchungaji wako aliyekuwa akikufundisha na kukuonya uache dhambi na ukawa unakataa?. hatua ndogo tu kama hiyo ya kuwaona watakatifu ni shida, unategemea vipi kumwona BWANA mwenyewe MFALME WA WAFALME atakapokuja pale mawinguni..?.
Biblia inasema tusilale usingizini kama wengine walalavyo,bali sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu”(1Wathesalonike 5:7-8). Muda umeenda kuliko tunavyodhani Bwana yupo mlangoni kurudi je! Umempa Bwana maisha yako sasa, je! Umebatizwa katika ubatizo utakaokupelekea upate ondolea la dhambi zako na kupokea Roho Mtakatifu?, Kama hujafanya hivyo ni vema ufanye hivyo sasa kabla mlango wa neema haujafungwa, hatimaye siku ile nawe uwe mmojawapo wa watakaokwenda na watakatifu wa Mungu kumlaki Bwana mawinguni.
Biblia inasema Waebrania 12: 14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”;
Ubarikiwe sana.
Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!
Hekima ya dunia hii inasema “Samaki mkunje, angali mbichi”, Hii ikiwa na maana kuwa Samaki akisha kauka hawezi kukunjika tena, ukijaribu kufanya hivyo atavunjika, Na ndivyo ilivyo kwa watoto wetu, Hekima ya Neno la Mungu pia inatumbia, Mithali 22: 6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”.
Neno hili kinyume chake ni kweli mtoto asipolelewa katika njia impasayo, hataiacha hiyo njia mbovu hata atakapokuwa mzee. Hivyo Mungu yupo hapo sana katika kuhakikisha hatma yake inakuwa salama kadhalika na shetani naye yupo hapo kutaka kuharibu hatma ya maisha ya mtoto yule angali ni mchanga. Hivyo nguvu ya ziada inahitajika katika kutengeneza maisha ya mtu katika utoto wake kuliko katika utu uzima.
Tunafahamu kabisa dunia ya sasa sio kama ile ya zamani, mambo maovu yaliyopo leo ni mengi kuliko yale ya zamani, ngoja nikupe kisa changu mwenyewe ambacho ni mfano hai kabisa ya mambo yanayoendelea katika ulimwengu wa watoto:
Nakumbuka tulipokuwa watoto (mimi na ndugu yangu), ilikuwa ni kati ya umri wa miaka 4-7 hivi, kuna vitu vilikuwa tunaviona vinaendelea katika mazingira yaliyokuwa yanatuzunguka, nyumbani kulikuwa na tv, na kwa kipindi hicho cha zamani kidogo, nyimbo za Michael Jackson, na nyimbo za kikongo ndizo zilikuwa zinavuma sana, hivyo ilikuwa ni ngumu kwenda katika nyumba yoyote yenye TV na kukosa mkanda wa (VHS) wa hizo nyimbo, Cha ajabu tulikuwa tunaona watu wazima wanaangalia na kufurahia lakini sisi tulikuwa tunaogopa kwamfano kama ulishawahi kutazama video za Michael Jackson nyingi zilikuwa na maudhui ya kutisha tisha tu, mara utaona anajigeuza kuwa mchanga, mara yupo makaburini,n.k. Sasa yale mambo watu wazima walikuwa wanaona ni kawaida tu, lakini sisi ilikuwa inatuathiri ndani kwa ndani na hauwezi ukasema kwasababu wewe ni mtoto na hujui maana ya hayo mambo, mpaka ilifikia kipindi vile vitu tulivyokuwa tunaviona kwenye TV vikaanza kujidhihirisha nje, tukaanza kuviona wazi wazi.
Tulikuwa tunaviona sana sana wakati wa usiku tunashutuka, na kuona vijiwatu vidogo vidogo vinafungua milango ya jiko, wanaingia na kuanza kucheza mbele yetu kama wale wale tuliokuwa tunawaona wanaocheza kwenye TV, ni wale wale tu isipokuwa hapa tunawaona dhahiri. Na mfano mtu mzima akijaribu kuingia ndani kwa ghafla vilikuwa vinakimbia na kujificha. Vilikuwa vinajidhihirisha kwetu tu, (kumbuka hizo sio ndoto au imagination, ni vitu dhahiri kabisa tulikuwa tunaviona, kwasababu wote wawili tulikuwa tunaviona, na mpaka sasahivi na utu uzima wetu tunavikumbuka) ..sasa ilifikia kipindi ilikuwa vikitokea tunaona kawaida tu, hatuoni tena ni ajabu, wala hatuviogopi, badala yake tunacheka, kumbuka wakati mambo haya yanaendelea hakuna mtu mwingine alikuwa anajua, kadhalika na vitu vingine vingi vya ajabu ajabu tulikuwa tunaviona ambavyo vilitokana na mambo tuliokuwa tunayatazama kwenye TV. Lakini mambo haya yalianza kupotea pale mzazi wetu mmoja alimpompa Bwana maisha yake.
Kadhalika mdogo wetu mmoja alituambia jambo kama hilo hilo liliwahi kumtokea alipokuwa mdogo, alikuwa anaona mtu anamtokea mwenye ngozi kama ya nyoka na kuzungumza naye usiku. Wakati huo wazazi hawaelewi chochote ni yeye tu na hilo pepo basi.
Sasa mambo hayo yalikuwa ni zamani wakati utandawazi haujawa mkubwa je! leo hii itakuwaje? Kwa watoto wa leo, siku hizi sio TV tu peke yake, kuna simu tena zenye internet, Kuna magemu, ya kila aina kwenye simu za wazazi, na kibaya zaidi magemu yenyewe ukiangalia karibu yote yanadhima za kipepo ndani yake, kwamfano, magemu kama , House of the dead, mortal combat, spiderman, Zuma, Diablo.Titan n.k.Pia Kuna magemu mengine yanakuwepo sana kwenye simu unakuta mtu analiendesha au anakimbizwa na limnyama fulani la ajabu kutoka pangoni , na yeye anajaribu kulikimbia,(Nadhani utakuwa unalifahamu) sasa vitu kama hivi watu waliovitengeneza hawajavibuni tu ilimradi hapana bali wamevitoa kama vilivyo katika ulimwengu wa roho wa kishetani (ni vikundi maalumu kabisa vya kishetani vinavyofanya hizi kazi), wanachofanya ni kuchukua taswira yenye uwezo wa kama hayo mapepo na kuyatengenezea magemu yanayofanana nao pamoja na kazi zao.
Kama vile tu wanavyotengeneza magemu ya mipira, utakuta aina ya mchezaji na uwezo wake ndani ya gemu ndio yuko hivyo hivyo katika ulimwengu wa kawaida duniani, kadhalika magemu yote yanayohusiana na viumbe na vitu vya ajabu ajabu vipo kweli katika ulimwengu wa roho,na kazi zao ndio hizo hizo, kukimbiza watu, kuua, kupaa, kutesa watu, kushusha watu kuzimu, kunywa damu za watu, n.k.
Sasa unakuta mtoto akitazama au akicheza magemu ya namna hiyo kidogo kidogo anaanza kuwa na ushirika na ile roho, mwisho wa siku kile kitu alichokuwa anakiona kwenye tv au gemu kinakuja kumtokea wazi, aidha kwa njia ya ndoto au dhahiri kabisa..Na kibaya zaidi mtoto hawezi kukwambia na wakati mwingine kinamwonya asikwambie, Kumbuka lile ni pepo kidogo kidogo linaanza kumpa maagizo, na uwezo wa kutenda kama lile pepo lilivyokuwa linafanya ndani ya gemu, ndio hapo unakuta mtoto anaanza kubadilika tabia anaanza kuwa mtundu, saa nyingine mtoto anafanya mambo yasiyoeleweka, anazungumza maneno yasiyoeleweka mara nyingine anakuwa na hisia ambazo unaona kabisa sio kawaida kwa mtoto kuwa nazo, unakutaa mtoto mdogo lakini anaonyesha tabia za kiutu uzima, tabia za kizinzi, mwingine anajithiri sehemu zake za siri,n.k. hii yote ni kutokana na hizo roho alizozipata kutoka katika ma- TV na Magemu,
Zipo shuhuda nyingi za namna hiyo, wazazi wanashuhudia baada ya watoto wao kwenda kufanyiwa mahojiano wanakiri kuwa vile vitu walivyokuwa wanaviona kwenye tv (cartoons,) na magemu vilikuwa vikiwatokea dhahiri, na kuwaendesha.
Hivyo wewe kama mzazi au dada, au kaka, una watoto wako au wadogo zako, unadhani unawapenda unapowawekea magemu kwenye simu, au unapowawekea programu za ajabu, unapowaruhusu watazame TV na miziki ya kidunia, unapowaruhusu watazame tamthilia na filamu zisizokuwa na misingi yoyote ya kikristo au kuelimisha, unadhani hapo umempenda mtoto? La! kinyume chake unamuharibu, biblia inasema mlee mtoto katika njia impasayo naye hataiacha hata atakapokuwa mtu mzima, mtoto anapolilia mambo hayo unatakiwa utumie nguvu pasipo hurumu tena akemewe kabisa aogope kuulizia vitu kama hivyo siku nyingine.
Kuna wazazi au walezi wengine wanaogopa na wengine hawataki kabisa kuwaadhibu watoto wao, kwa kisingizio eti tunaishi kazazi kipya kile ni cha zamani kimeshapita, watoto wa siku hizi hawapigwi wanaelekezwa tu…Huo ni uongo wa shetani, ndio inafikia hatua mpaka mtoto anamtukana mtu mzima na mzazi anamwangalia tu, anaiba na mzazi anamwangalia tu, akidhani kuwa akimwadhibu mwanaye atajisikia vibaya au atapata matatizo fulani ya kiafya,..Au ataona kama haonyeshi upendo kwa familia yake..Hivyo anaepuka kabisa kumudhi mwanae.. Lakini biblia inasema..
Mithali 22: 15 “Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali”.
Na pia inasema …
Mithali 23: 13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; MAANA UKIMPIGA KWA FIMBO HATAKUFA.
14 Utampiga kwa fimbo, NA KUMWOKOA NAFSI YAKE NA KUZIMU”. .
Unaona hapo siku ile wazazi wengi watawajibika kujibu ni kwanini watoto wao wapo kuzimu, angali wasingepaswa kuwepo huko. Tunasema watoto wa siku hizi wamebadilika, lakini ki-ukweli wazazi wa siku hizi ndio waliobadiliaka, watoto ni wale wale.
Unaweza ukadhani ukimwadhibu mwanao, atakuja kukuchukia baadaye, lakini akizoeshwa hivyo atakapokuja kuwa mtu mzima, na yeye kupata akili kama wewe atakushukuru sana kwa kumlea vizuri, kwasababu ndivyo hivyo Neno la Mungu linavyosema:
Waebrania 12: 11 “Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani”
Na matunda ya kumlea vizuri mwanao utakuja kuyaona mwishoni…Biblia inasema hivyo pia..Mithali 29: 17 “Mrudi mwanao naye atakustarehesha; Naam, atakufurahisha nafsi yako”
Wewe kama mzazi/mlezi anza kumjenga mwanao/mdogo wako leo katika misingi ya Kikristo, badala ya kumwacha asikilize miziki ya kidunia katika TV, anza kumfundisha kuimba tenzi za rohoni, mapambio na nyimbo za kumsifu Mungu, badala ya kumwacha aangalie Tamthilia zisizokuwa na maana anza kumfundisha hadithi za biblia (kama safari ya wana wa Israeli, hadithi za Eliya, wafalme, Yona, Danieli n.k.) kuliko kubaki kujazwa hadithi mbovu za watu wasioamini katika TV, Anza kumfundisha jinsi ya kutumia jina la YESU, mzoeshe kutumia jina la YESU kila mahali alipo, anza kumfundisha kusali, mfundishe umuhimu na madhara ya kuwa na tabia zisizofaa, mpeleke katika madarasa ya biblia ya watoto jumapili kanisani, kama watu wa dini nyingine wanafanya hivyo wewe kwanini usifanye.??..Kadhalika jenga desturi ya kuwaombea na kuwawekea mikono watoto wako mara kwa mara wewe mwenyewe na kuwatamkia maneno ya baraka.. Kwa kufanya hivyo utakuwa umeiokoa roho ya mwanao katika kizazi hiki kibaya kilichopotoka na dhidi ya roho chafu zinazozunguka kuwanasa watoto.
Ubarikiwe sana.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali “share” kwa wazazi wengine ujumbe huu ili na wanao pia wapone.
Mada Nyinginezo:
KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?
JE! WATAKAOENDA MBINGUNI NI WENGI?
JE! MKRISTO ANARUHUSIWA KULA NGURUWE, NA KUVUTA SIGARA NA KUNYWA POMBE?
Luka 4: 22 “Wakamshuhudia wote[YESU KRISTO], wakiyastaajabia maneno ya neema yaliyotoka kinywani mwake, wakasema, Huyu siye mwana wa Yusufu?
23 Akawaambia, Hapana shaka mtaniambia mithali hii, Tabibu, jiponye nafsi yako; mambo yote tuliyosikia kwamba yametendeka Kapernaumu, yatende na hapa pia katika nchi yako mwenyewe.
24 Akasema, Amin, nawaambia ya kwamba, Hakuna nabii mwenye kukubaliwa katika nchi yake mwenyewe.
25 Lakini, kwa hakika nawaambia, Palikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli zamani za Eliya, wakati mbingu zilipofungwa miaka mitatu na miezi sita, njaa kuu ikaingia nchi nzima;
26 wala Eliya hakutumwa kwa mmojawapo, ila kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.
27 Tena, palikuwa na wenye ukoma wengi katika Israeli zamani za nabii Elisha, wala hapana aliyetakaswa ila Naamani, mtu wa Shamu”.
Neno la Mungu ni mwongozo wa kutufundisha sisi kutokurudia makosa yaliyofanyika nyuma na waliotutangulia, Katika habari hii Bwana Yesu anatuonyesha madhara ya kulinganisha Neno la Mungu, na mazingira ya nyuma ya mtu, Kama tunavyosoma tunaona wale wayahudi baada ya kusikia na kuona maneno mazuri ya wokovu yaliyokuwa yanatoka kinywani mwa Bwana, badala ya kuyasadiki wao moja kwa moja wakaanza kutazama mambo mengine yasiyokuwa na msingi na kurejea kuchunguza ameitolea wapi neema hiyo kwa kuilinganisha na chimbuko lake..
Na ndio maana utaona wanasema..huyu sio yule seremala mwana wa Yusufu, dada zake na kaka zake sio hawa tunao hapa mjini kwetu?, na mama yake sio yule Mariam tunayemfahamu?, n.k. Sasa kama ndivyo katolea wapi ujuzi huu wote na maarifa haya yote,?. Wakahitimisha; hawezi akawa na jipya lolote la kutueleza sisi, tumeshamfahamu tangu zamani huyu ni wa hapa hapa…Kwahiyo kwa kufanya vile ikawapelekea ile neema iliyokusudiwa juu yao kuwapita. Na ule wokovu ambao wangepaswa wapate wao kwanza kutoka kwa Bwana kuupoteza.
Kadhalika na ndivyo ilivyokuwa kwa Nabii Eliya wayahudi hawakuupokea ujumbe aliokuwa anawapelekea siku zote, na badala yake wakayatazama maisha yake ya nyuma, pengine walisema huyu mzee kutoka Gileadi kwanza haijui vizuri Israeli, Ndugu zake si ndo hawa wakulima na wafugaji tunaowaona huku, hawana elimu,?..Hivyo wakahitimisha nao pia kuwa Eliya hawezi akawa na jambo la kuwaongezea kitu, kwasababu historia yake ipo wazi. Lakini wakati Bwana anakaribia kuleta njaa kuu juu ya nchi, Eliya hakutumwa kwa mojawapo ya wajane waliokuwepo Israeli kwa wakati ule badala yake alitumwa kwa mjane mmoja katika nchi ya mbali, asiyemjua hata vizuri Mungu wa Israeli lakini kwa kusikia tu kwamba mtu Yule katumwa na Mungu, alimuheshimu sana. Na kupelekea kupata neema ya chakula tele kipindi chote cha njaa.
Kadhalika hata katika kipindi cha Nabii Elisha jambo ni lile lile, walikuwepo wakoma wengi katika Israeli lakini wenyewe walimwona Elisha ni kama mtu wa kwao tu, hawezi kuwa mtumishi wa kulibeba Neno la Mungu, hawezi kuundoa ukoma wetu huu, tunamjua ni mfugaji, na baba yake na mama yake ndio wale wale wafugaji wasioijua sheria ya Mungu sana, kaka zake na dada zake kila siku tunawaona huku mtaani kwetu ni watu wa kawaida tu, hivyo tuende kufanya nini kwa mtu kama Yule?? Wakakwazika na maisha ya Elisha. Hivyo kwa dharau zao ziliwafanya wabakie na ukoma wao daima..Lakini mtu mmoja kutoka nchi ya mbali (Iitwayo Shamu) aliposikia habari za Elisha tu kutoka wa kijakazi wake, alimwamini na kuamua kufunga safari kwenda kuomba kuponywa, na ndivyo ilivyokuwa alipokea uponyaji wake wote, na wale wengine wenye kiburi walibakia na ukoma wao siku zote za maisha yao.Swali ni je! Kwanini hakukuwa na mkoma yoyote wa Israeli aliyeponywa?. Au mjane yoyote Israeli aliyepewa chakula na Eliya Na badala yake watu wasiomjua Mungu wa Israeli kutoka mbali kuja kuponywa na kupewa chakula?
Jambo hilo hilo linajirudia leo hii, kwanini wanaojiita wakristo wengi hawataenda mbinguni? Sababu ni ile ile, wanajua historia yote ya Bwana Yesu na biblia yote, wanajua mwanzo wote wa ukristo na utakavyokuwa mwisho wake, lakini bado ni wakoma wa rohoni, bado ni wajane wa rohoni, wasiotaka msaada,.. Wanapoletewa habari ya wokovu, na kuhubiriwa watubu dhambi, na waponywe nafsi zao, wanajiona hawawezi kuongezewa kitu kingine cha ziada, sababu tu wao wamezaliwa katika ukristo, na wamepitia mafundisho yote ya biblia na vyuo vyote vya biblia, lakini ndani yao wanapinga maneno ya neema ya Kristo yahusuyo wokovu, utakuta ni mkristo lakini ni mlevi, ni mkristo lakini ni mzinzi, ni mkristo lakini ni msengenyaji, ni mkristo lakini ni mtazamaji wa pornography na mfanyaji wa mustarbation, ni msagaji, ni mvaaji wa vimini, ni mtukanaji, mtu asiyesamehe n.k. Na akiambiwa habari za kutubu dhambi na kujazwa Roho atasema naifahamu biblia, nilishaenda katika mafundisho hayo zamani, huo ni ulokole tu, atakwambia hayo yote chimbuko lake ni hili au hili n.k. hivyo anakuona huna chochote cha kumwongezea yeye…
Biblia inasema siku zinakuja ambazo Bwana ataleta njaa juu ya nchi Soma
Amosi 8: 11” Angalia, siku zinakuja, asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Bwana.
12 Nao watatanga-tanga toka bahari hata bahari; na toka upande wa kaskazi hata upande wa mashariki; watapiga mbio, wakienda huko na huko, kulitafuta neno la Bwana, wasilione.
13 Siku hiyo wanawali wazuri na wavulana watazimia kwa kiu”.
Hizo siku ndio hizi ndugu, kama zilivyokuwa katika siku za Nabii Eliya..Leo hii duniani kote kuna njaa ya Neno la Mungu, ndani ya Ukristo na nje ya ukristo. Wajane na wakoma walikuwepo ndani ya Israeli na nje ya Israeli, Kadhalika na katika ukristo wenye njaa wapo ndani ya ukristo na nje…Lakini kama vile wale wa ndani waliipinga neema iliyoletwa kwao na Nabii Eliya na Nabii Elisha, na kupelekea watu wengine wa mbali kupewa neema, Vivyo hivyo na katika ukristo wanaoipinga neema hii sasa ihusuyo toba na ondoleo la dhambi, wakati utafika itaondolewa kwao na kuhamishiwa kwa watu wengine wasiomjua Mungu wa kweli na Bwana wetu Yesu Kristo na wao wataponywa roho zao, wakati wanaojiita wakristo watakuwa wanakufa kwa njaa.
Leo hii unajiita mkristo na bado ni mkoma wa rohoni, unajiita mkristo na bado ni mjane wa rohoni mwenye njaa, ni kwasababu gani? Ni kwasababu matendo yako hayaendani na ukristo halisi huku unadai unamfahamu Kristo?..Unakuwa huna tofauti na wale watu waliokuwa wanajua chimbuko la Bwana Yesu, mpaka kazi ya baba yake, na ndugu zake walivyo lakini wasione uzima uliokuwa ndani yake…ndivyo ilivyo kwa wewe unayejiita mkristo, unazini, unakunywa pombe, unatazama pornography, unasengenya, unaenda disco,n.k. Hujui kuwa chakula kile ambacho kingepaswa kije kwako kwanza kinapelekwa kwa mtu mwingine ambaye hata hajawahi kusikia habari za ukristo.
Kila siku unahubiriwa utubu dhambi ugeuke, unakataa, lakini wapo wasiomjua Mungu leo hii wanasikia tu mara moja na kugeuka wakati huo huo, waislamu, wahindu, wabudha, wasio na dini, ndio Bwana anaowaangalia kuwapa chakula chake huu wakati wa njaa..Wewe utaendelea kutangatanga huku na kule, hujui kama Mungu alishakuacha siku nyingi na mwisho wa siku utakufa kwa njaa na kuishia jehanum ya milele kwenye mateso yasiyoelezeka. ..
huu sio wakati wa kujisifia dini au kujisifia kuzaliwa katika ukristo, au ujuzi wa maandiko, au chuo cha biblia ulichopitia ,au vinginevyo, Huu ni wakati wa kunyenyekea na kutafuta wokovu na utakatifu kwa bidii kwasababu biblia inasema .
Waebrania 12: 14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;”
Ubarikiwe.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu na wao wapone.
Mada Nyinginezo:
HUDUMA YA (ELIFAZI, BILDADI, NA SOFARI).
BWANA ALIPOSEMA KUWA YEYE NI “MUNGU WA MIUNGU” ALIKUWA NA MAANA GANI?..JE! YEYE NI MUNGU WA SANAMU?
Mkumbuke Mke wa Lutu..
Luka 17:28 “Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga;
29 lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote.
30 Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu.
31 Katika siku ile, aliye juu ya dari, na vyombo vyake vimo ndani ya nyumba, asishuke ili kuvitwaa; na kadhalika, aliye shambani asirejee nyuma.
32 MKUMBUKENI MKEWE LUTU.
33 Mtu ye yote atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza; na ye yote atakayeiangamiza ataiponya”.
Ni wazi kuwa kizazi tunachoishi kinafananishwa na kile cha Sodoma na Gomora, kadhalika kinafananishwa pia na kizazi cha Nuhu, Na ni kwanini ni hichi na sio kizazi kingine?. Ni kwasababu yale mambo yaliyokuwa yanafanyika kule wakati ule ndio yanayofanyika sasa na zaidi hata ya pale, Kumbuka Jambo kuu lililopelekea Miji ya Sodoma na Ghomora kuteketezwa ni tabia ya ulawiti na ushoga, tafsiri ya neno lenyewe Sodoma ni Ulawiti, Hivyo wakati ule hiyo roho ya kuingiliana kwa watu kinyume na maumbile ilikuwa imekithiri jambo ambalo lilianza tena kuonekana likijirudia kwa kasi sana mwanzoni mwa karne ya 20 na kuendelea mpaka sasa.
Roho hii imekithiri katika karne hizi 2 kuliko vizazi vingine vyote vya nyuma vilivyotangulia. Mpaka sasa hivi vitendo hivyo vimehalalishwa kisheria, kwamba vimepewa haki ya kuitwa ndoa kama ndoa nyingine halali, Kama Bwana Yesu alivyotabiri siku hizo watu watakuwa wakioa na kuolewa. Sasa Kuoa na kuolewa kwenyewe kunakozungumziwa hapo sio ndoa za mke na mume hapana, bali ni ndoa za mume na mume, na mke na mke. Mambo ambayo tunayaona sasahivi yakihalalishwa hata katika nyumba zinazojiita ni za ibada.
Sasa madhara ya haya mambo ni nini?
Madhara yake ni kupelekea jamii nzima kuathiriwa na adhabu hata watu wanaoonekana kutokuwa na hatia wanashiriki adhabu yao. Kwamfano tukitazama katika kipindi cha Nuhu, makosa ya wanadamu yaliwasababisha hata wanyama wasiokuwa na hatia kuangamizwa, ilisabababisha nchi na mimea isiyokuwa na hatia kuharibiwa, ilisababisha watoto wachanga wasiotenda hayo makosa kuteketezwa pia. Kadhalika na katika kipindi cha Lutu vivyo hivyo Na ndivyo itakavyotokea hata katika kizazi hiki cha siku za mwisho, wataathirika hata na watu wengine na viumbe vingine visivyokuwa na makosa (visivyostahili hayo madhara).
Lakini kabla Bwana hajaleta maangamizi huwa anatuma kwanza wajumbe wa kuwaonya watu wajitenge na kizazi hicho, Na ndio tunakuja kuona katika wakati wa Nuhu waliotii sauti ya Mungu ni watu wachache (yaani watu 8 tu! kati ya mamilioni), Kadhalika katika wakati wa Lutu waliotii ni watu 4 tu lakini Yule wanne (ambaye leo tutajifunza habari zake) alilikuja kuangamia, na kupelekea watu 3 tu kupona kati ya maelfu na mamilioni waliokuwa mijini.
Siku zote tunajua ni jambo la kawaida kwa mwanadamu kufuata au kuamini kitu kinachopendwa na watu wengi, hata kama ni cha kipuuzi kiasi gani, kikiwa kimekubaliwa na wengi basi ni rahisi kupata wafuasi wengi pasipo hata kupata ukinzani.kwamfano jamii nyingi za zamani watu walikuwa na hofu ya kumiliki televisheni katika manyumba yao wakiogopa kuwa zinaweza kuharibu maadili ya familia au jamii zao, lakini kwa jinsi zinavyozidi kuongezeka na kuaminiwa na wengi, zinakuja kuwa ni kitu cha kawaida kadri muda ulivyozidi kuendelea hata wale wachache waliokuwa wanazitilia mashaka wanaanza kuona kama ulikuwa ni ushamba kuogopa kumiliki televisheni,
Kadhalika pia zamani mtoto mdogo kumiliki simu ya mkononi wengi iliwashangaza sana, kuona kama mtoto ataharibikiwa, lakini kutokana na simu kuwa nyingi na wazazi wanaowawaruhusu wanao kuzitumi kuongezeka, inapelekea hata wale wazazi waliokuwa wanazipinga zisimilikiwe na watoto wao, wajione kama walikuwa washamba na wanahofu ya bure tu!, hii inakuja kutokana na presha ya watu wengine, hivyo husababisha yale madhara yalikuwa yanadhaniwa mwanzo kumezwa na mabadiliko ya kijamii.
Mfano mwingine ni kuwasili kwa fasheni, zamani ilikuwa mwanamke akionekana amevaa suruali alijulikana kama ni kahaba Fulani hivi, lakini kwa siku zilivyozidi kwenda na wavaaji kuongezeka, suruali zikaanza kuonekana kuwa ni kitu cha kawada sana kwa wanawake, hata wale wachache waliokuwa wanazipiga vita wanaanza kujiona kuwa walikuwa ni washamba..Na ndivyo ilivyo hata kwa ushoga, zamani ilikuwa hata kutamkwa hilo neon tu, ilikuwa ni aibu lakini leo hi kutokana na kwamba mambo haya yanazidi kuongezeka hata Eneo linalojiita la Kanisa mada hizo zinazungumziwa na kupewa kipaumbele na kuhalalishwa, limekuwa ni jambo la kawaida hata wale waliokuwa wanapinga mwanzoni, wanaanza kujiona kama walikuwa watu wa itikadi kali…Kwahiyo roho hii ya kubadilika kutokana na mikumbo ya watu wengi imeendelea mpaka sasa katika kanisa la Mungu..
Sasa mambo haya ndivyo yalivyokuwa katika zama za Lutu, Na Mungu kwa kumuhurumia Lutu na familia yake akamwambia atoke, lakini kabla ya wao kutoka walipewa nafasi ya kwenda kuwahubiria ndugu zao pia , lakini biblia inasema walionekana kama wanacheza mbele zao (mwanzo 19:24), Hivyo ikawalazimu watoke wao tu.
Tukizidi kusoma habari ile tunaona, Mkewe Lutu alikuja kugeuka nyuma na kuwa nguzo ya chumvi.
Kwanini Mke wa Lutu ageuke nyuma na anamwakilisha nani Sasa?
Mke wa Lutu anamwakilisha MKRISTO ambaye alishaokolewa huko nyuma, kumbuku Mke wa Lutu mwanzoni aliitika kabisa wito wa kutoka Sodoma, kwa kuyatambua maovu yote yaliyokuwa yanatendeka kule, kwamba wale watu walikuwa wanastahili hukumu , kwa kujua hilo aliamua kabisa kuyaacha mambo ya Sodoma na kuondoka, Lakini baadaye katikati ya safari alianza kujiona anavutiwa na mambo ya nyuma kuliko ya mbele, akianglia mbele haoni majumba, mali, wala raha, akiangalia nyuma anaona fahari, mali, starehe, karamu, mashamba, n.k. Hivyo akaanza kushawishika kidogokidogo kuyafikiria na kuyatamani aliyoyoaacha nyuma Hivyo matokeo yake akageuka, akaangamia na kuwa jiwe la chumvi.
Mke wa Lutu alidanganyika kama vile kanisa linavyodanganyika leo, pengine aliambiwa maneno haya na wale watu aliowahubiria huko nyuma;…,
aah! Ni nyie tu wanne Mungu aliowaona ndio watakatifu kuliko watu wote hapa Sodoma!, Vipi kuhusu watoto,? Unataka kusema watoto wasio na hatia Mungu atawaangamiza pia?, Na vipi kuhusu viongozi wetu wa kidini tulio nao huku, wao nao wataangamizwa, nyie ni bora kuliko wao? Na majengo yetu, na masinagogi yetu Mungu ataanzia wapi kuyaangamiza?..
Kwa kosa gani kubwa hivyo mji wote uteketezwe?..Nyie ni lazima mtakuwa mmesikia roho zidanganyazo..ambazo haziwatakii mema, zinawataka muache mali zetu mkimbilie milimani na kufa huko!…Vipi kuhusu mifugo kwani nayo imemkosea nini Mungu, hata iangamizwe? Mungu ni wa haki bwana, hawezi kufanya hivyo vitu….wapo wengi waliojaribu kama nyie wakapotea, embu tulieni hapa, muwe kama sisi acheni hizo itikadi zenu kali rudini kwenu, msije mkawa vichaa.
Ndivyo mke wa Lutu alivyodanganyika wakati akiwa katikati ya safari yake kwa kuyatafakari hayo maneno, akagundua kweli inawezekana ni upuuzi anaoufanya, kwamba hakuna kitu kama hicho, Mungu hawezi kuleta madhara kama yale kwa idadi kubwa ya watu kama ile,ni kweli vipi kuhusu mali zetu, vipi kuhusu mifugo yetu, vipi kuhusu ndugu zetu na watoto, vipi kuhusu viongozi wa kidini n.k…Kwa ushawishi mwingi kama huo Mke wa Lutu akageuka nyuma moja kwa moja na kuangamia milele.Na ndio maana Bwana alisema “Mkumbukeni mkewe Lutu”
Ulikuwa mkristo mzuri zamani ulipoamini, macho yako yalikuwa yapo mbinguni, hukujali ulimwengu unakuchukuliaje, ulijua kabisa unaishi katika siku za mwisho na siku yoyote ghadhabu ya Mungu itamwagwa juu ya nchi, ulikuwa tayari kuacha sigara, pombe, uasherati, anasa, disco, ulawiti, usagaji, pornography, mustarbation, mizaha, matusi, vimini, suruali, mapambo yote ya kikahaba n.k. na zaidi ya yote ulikuwa umeshajumuika na wenzako katika safari ya kuukimbia ulimwengu.. Lakini ulifika wakati ukaanza kuona kama safari yako ni ngumu na ni wachache tu mpo, ukaanza kukumbuka mafundisho ya ya mashetani uliyohubiriwa huko nyuma..yaliyokuwa wanakuambia: Yesu haji leo wala kesho, ukakumbuka pia mtu mmoja alishawahi kukwambia dunia haiwezi kuangamizwa Mungu hawezi kuangamiza watu wasiokuwa na hatia, hawezi kuangamiza watoto wadogo, hawezi kuteketeza viongozi wetu wa kidini, kwani ni nyie tu kikundi kichache kinachojiona kitakatifu ndio mtakao okoka,? Mungu haoni wengine? Mungu ni Mungu wa upendo, Na zaidi ya yote unaacha uzuri wako, unaacha kujipa raha kama kijana unaenda kuwa mshamba,..utakumbuka kuna mwingine alikwambia kuna watu waliopita njia kama yako na mwisho wake ukawa ni matatizo, utakumbuka kuna kiongozi wa kidini alikuambia uzichunguze hizo roho…watakambia hizo ni roho za shetani zinazowafanya mtoke katika hali ya kawaida na kuwa katika hali ya kutazamia mambo yasiyokuwepo ya uongo n.k..
Sasa hapo na wewe unashawishika na kuyatazama mambo ya nyuma, ndugu/dada usigeuka nyuma maana kabla ya kurudi nyuma utakuwa umeshakuwa JIWE LA CHUMVI. Biblia inasema.
2Petro 2: 20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza.
21 Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa.
22 Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni”.
Ndugu yangu mkumbuke MKE WA LUTU. Kumbuka dunia ya leo hii imejaa maovu ya kila namna, hivyo usitazame wimbi la watu wengi wanafanya nini, usitazame kwasababu vijana wote wanafanya anasa na wewe ufanye, kwasababu wanawake wote wanavaa vimini na wewe uvae kwasababu watu wote wanazini na wewe uzini, Biblia ilishatabiri katika siku za mwisho watakatifu watakuwa wachache, na upendo wa wengi utapoa, kama zilivyokuwa katika siku za Nuhu na siku za Lutu, Hivyo ukiwa wewe ni mkristo na umeacha mambo ya ulimwengu huu, zidi kujitakasa, maana siku si nyingi Mungu atauteketeza huu ulimwengu kabisa na watakaopona ni watakatifu ambao watakuwa ni wachache sana, mimi na wewe tuwe miongoni mwao….
2Petro 3: 3 “Mkijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki, wafuatao tamaa zao wenyewe,
4 na kusema, Iko wapi ahadi ile ya kuja kwake? Kwa maana, tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa.
5 Maana hufumba macho yao wasione neno hili ya kuwa zilikuwako mbingu tangu zamani, na nchi pia, imefanyizwa kutoka katika maji, na ndani ya maji, kwa neno la Mungu;
6 kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia.
7 Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu.
8 Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.
9 Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.
10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.
11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,
12 mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka?”
Ubarikiwe.
Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine na Mungu atakubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.
TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.
ULE MSALABA UNAOWEKWA KWENYE KABURI, NA ILE IBADA INAYOFANYWA VINA UMUHIMU WOWOTE KWA MKRISTO?
Neno la Mungu limefananishwa na MBEGU (Luka 8:11), na siku zote mbegu ina uhai na inapopandwa ndani ya mtu, ule uhai wake unajidhihirisha ndani ya mtu huyo kulingana na umeaji wa mbegu hiyo. Hivyo kwa jinsi ile mbegu inavyoendelea kukua ndipo tabia ya Yule mtu inavyoendelea kubadilika kidogo kidogo. Kumbuka hapo sio mtu anajibadilisha kwa jitihada zake hapana bali ni ile mbegu iliyopandwa ndani yake ndiyo inayombadilisha kutoka hatua moja hadi nyingine kulingana na ukuaje wake.
Bwana Yesu alitoa mfano huu.
Marko 4: 26 “Akasema, Ufalme wa Mungu, mfano wake ni kama mtu aliyemwaga mbegu juu ya nchi;
27 akawa akilala na kuondoka, usiku na mchana, nayo mbegu ikamea na kukua, ASIVYOJUA YEYE.28 Maana nchi huzaa yenyewe; KWANZA JANI, tena SUKE, kisha NGANO PEVU, katika suke.
29 Hata MATUNDA yakiiva, mara atapeleka mundu, kwa kuwa mavuno yamefika”.
Huu mfano unalinganishwa na jinsi Neno la Mungu linavyomea ndani ya mtu, kwanza linaanza kama mbegu, pale mtu anapoliruhusu lile Neno liingie ndani yake, hii inakuja kwa kutamani kujifunza kila siku Neno lile,kwa kutamani kumjua Mungu, na kujifunza maandiko, sasa kidogo kidogo, kwasababu ile mbegu imetengenezewa mazingira yanayostahili kumea yenyewe inaanza kukua taratibu taratibu pasipo hata yeye mwenye kuipanda kujijua ndio hapo unakuta mtu Yule anaanza kubadilika tabia zake na mwenendo wake, anaanza kujikuta anachukia mambo ya kidunia ambapo hapo mwanzo alikuwa hawezi, na hii haiji kwa jitihada za mtu hapana yeye mwenyewe tu anajikuta anapoteza hamu ya kufanya hivyo vitu, hapa mtu anajikuta vitu kama kiu ya sigara, pombe, uasherati, mavazi yasiyo na heshima n.k. vinakata vyenyewe, ataona tu ni kama vile kwa akili zake ameacha hayo mambo lakini hajui kuwa ni ile mbegu ambayo amekuwa akiiruhusu imee ndani yake ndiyo iliyotenda kazi ndani yake
Na kwa jinsi atakavyoendelea kuiwekea mazingira mazuri zaidi ya kukua, kwa kujifunza na kutamani kudumu zaidi katika Neno la Mungu sasa ile mbegu inageuka na kuwa JANI, hapa ni pale mtu ufahamu wake wa kumjua Mungu unaongezeka na kuwa mpana pasipo hata yeye mwenyewe kujijua kumbuka hii mbegu inachohitaji ni kuwekewa mazingira tu ya kutuzwa, kuhusu ukuaji huwa inajikuza yenyewe. Hatua hii inamfanya mtu ufahamu wake wa rohoni kuongezeka, yale mambo ambayo alikuwa hayaelewi kuhusu maandiko anaanza kuyaelewa taratibu taratibu.
Hatua inayofuata ni SUKE. Hatua hii mtu anakuwa anatoka katika ile hali ya “unyasi unaotikiswa na upepo”.
Waefeso 4: 14 “ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu.
15 Lakini tuishike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, Kristo”.
Hapa unakuwa umekomaa kutoka katika jani na kuwa suke gumu, hatua hii shetani hawezi kukuchukua tena na kila wimbi la mafundisho ya uongo kwa sababu Neno la Mungu limeshaweka mizizi migumu ndani yako. Unafika hatua ya kuwa na ujuzi wa kuitofautisha Kweli ya Neno na Uongo, kwasababu yale mafuta ya Roho yanakaa ndani yako. Mpaka hapo mtu anakuwa tayari kwa hatua inayofuata ya kuzaa matunda.
NGANO PEVU: Hii ni hatua ya kudhihirisha matunda, Hapa inatokea lile Neno lilipandwa ndani yako lenyewe linakupa uwezo wa kwenda kulipanda kwa watu wengine..na kuzaa matunda, Hapa ndipo Mungu kwa maarifa aliyoyaweka ndani ya mtu, anampa neema na uwezo wa kwenda kuwafundisha na wengine, na hii nguvu ya kufanya hivyo haiji kwa jitihada za mtu binafsi au kujilazimisha hapana bali mtu anajikuta anatamani mwenyewe kufanya hivyo kutoka ndani kwasababu ile nguvu za kuzaa matunda imeshajitengeneza ndani yake..,Ni kama tu vile mwanamke anapofikia wakati wa kuzaa, ule uchungu unapokuja hawezi kujizuia, vivyo hivyo na mtu akishafikia hatua hii, anajikuta mwenyewe anaanza kumzalia Mungu matunda.
Na hatua ya mwisho ni Mavuno: Hapa ndipo kazi ya kila mtu itavunwa na Bwana mwenyewe, na hii itakuja katika mwisho wa dunia.
Hivyo ndugu je! Ni mbegu gani imepandwa ndani yako?, Ni ya Neno la Mungu au ni ya Yule mwovu.?..Na kama ni ya Neno la Mungu, je! Mbegu hiyo imekuwa kwako katika hatua gani, ni jani?, ni suke au ni ngano?. Kama huna uwezo wa kushinda ulevi, uasherati, sigara, uzinzi, usengenyaji basi ujue ile mbegu imekufa ndani yako.. Kwasababu uliposikia Neno la Mungu hukutaka kuliwekea mazingira mazuri ya kukua lenyewe. Kumbuka mkristo yoyote anayezingatia kulitunza na kujifunza Neno la Mungu kila siku katika maisha yake, hatapata shida kuishida dhambi. Kwasababu Biblia inasema..
1Yohana 3: 9 Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao [MBEGU]wake wakaa ndani yake ; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu.
Ni maombi yangu sisi sote tujue nguvu ya Neno la Mungu, tukijua kuwa tukilipinga Neno la Mungu ndani yetu ni kujitenga na uzima wetu wenyewe. Hivyo nakutia moyo ndugu usomaye haya usichoke kujifunza Neno la Mungu kila iitwapo leo, jifunze Biblia. Kwasababu hujui wewe lile Neno linatendaje kazi ndani yako. Wewe jifunze na kulitii tu, hata kama hutaona leo mabadiliko lakini fahamu tu, linakuwa kwa njia usioijua wewe, wakati Fulani ukipita ukiendelea hivyo utaona tofauti ya leo yako na jana yako ilivyokuwa.
Mungu akubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali share ujumbe huu kwa watu wengine na Mungu atakubariki.
Mada Nyinginezo:
NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.
ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.
NINI MAANA YA USIPUNGUZE WALA KUONGEZA NENO LA MUNGU?
JE! NI DHAMBI KUSHEREKEA SIKU YA KUZALIWA? BIRTHDAY!
JE! NI HALALI KWA MTU WA MUNGU KUTUMIA NJIA ZA UZAZI WA MPANGO?