Title 2024

MAFUNZO YA BIBLIA KWA WATOTO

Darasa la Kwanza:

KUIFUNGUA BIBLIA.

Mwendelezo unakuja…..

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAOMBI YA KUOMBEA WATOTO.

NINYI AKINA BABA MSIWACHOKOZE WATOTO WENU

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! Utatu mtakatifu upo kibiblia?

Katika mapokeo ya kikristo, moja ya eneo ambalo limezuia mikanganyiko mingi, ni eneo hili linalohusiana na “Uungu wa Mungu” . Migawanyiko ya madhehebu mengi unayoyaona sasa chimbuko kubwa hasaa ni hapa.

Wapo wanaoamini Mungu ni mmoja amegawanyika katika nafsi tatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu), lakini wapo wanaoamini Mungu ni mmoja mwenye nafsi moja (Hajagawanyika), yaani Yesu ni Yule Yule Yehova aliyekuwa zamani zile, wengine hawaamini kabisa kama Yesu anastahili kuwekwa katika nafasi ya uungu, wengine hawaamini kuwa Roho Mtakatifu ni halisi, bali ni nguvu tu ya Mungu, ni Yesu na Mungu tu basi.  Je! Ukweli ni upi? Na Je tunapaswa tusimamie wapi?

Jambo la kwanza kufahamu, ni kuangalia kiini, cha kumjua Mungu? Kama kiini kimeharibika hapo ndipo penye shida kubwa. Tunaposema kiini, tunamaanisha idadi ya miungu. Cha ajabu ni kwamba makundi yote haya yanaamini “Mungu ni mmoja”, sawasawa na maandiko yanavyosema..

Marko 12:29  Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, BWANA MUNGU WETU NI BWANA MMOJA;

30  nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.

Tena kizuri zaidi ni kwamba wote wanaamini kazi ya Kristo ya ukombozi, wanaamini pia kazi za Roho Mtakatifu mioyoni mwetu.

Kinachotofautisha ni kutambua tu, nafasi zao za kiungu. Hilo tu, ambalo kimsingi halina nguvu sana, zaidi ya kuzitambua kazi zao mioyoni mwetu. Ni sawa na watu wawili wanaoshindania kama MUWA, ni jamii gani ya mmea, mmoja anasema ni tunda, mwingine anasema ni aina ya jani. Embu jiweke wewe katika hiyo nafasi, ukiulizwa swali hilo utasema ni nini?. Ni rahisi kusema “muwa” ni tunda, lakini kibaolojia muwa ni jamii ya “jani”, isipokuwa limerefu tu zaidi ya mengine na lina maji matamu, .

Sasa je! Kufahamu kama ni jani, au ni tunda? Maarifa hayo yanaweza kubadili asili yake? Kwamba ukifahamu sukari yake itaongezeka, au itawabadilikia maumbo. Wewe na yeye hamna tofauti, kiladha, isipokuwa kiufahamu tu.

Vivyo hivyo na kwenye uungu wa Mungu, Tunatafuta  “UJUZI”. Na ujuzi ni mzuri, lakini mara nyingi tunapoung’ang’ania sana haujengi, bali huleta matengano, Ni upendo tu  ndio unaojengwa.

1Wakorintho 8:1b…Twajua ya kuwa sisi sote tuna ujuzi. Ujuzi huleta majivuno, bali upendo hujenga

Ndio maana kwanini hatushangai kuona kanisa la kwanza, liliweza kutembea katika utimilifu wote wa ki-Mungu ijapokuwa hawakuwa na maarifa ya kutosha ya kutambua uungu wa Yesu, vema, isipokuwa baadaye sana katika nyaraka za mitume, ambayo hata hivyo waliita ‘Siri ya Mungu’. Lakini hao hao waliweza kumwabudu Kristo, lakini pia wakamwabudu Baba, bila shida yoyote, wapo waliotambua siri hii, lakini wapo ambao hawakutambua vema.

Kuonyesha kuwa hilo sio jambo la kung’ang’ania sana kana kwamba usipojua utakwenda kuzimu, kama inavyochukuliwa leo, mpaka kutupelekea matengano.

Ukweli ni kwamba Mungu wetu ni Yule Yule mmoja, isipokuwa ametenda kazi kwenye nafasi tatu tofauti kwa lengo la kumkamilisha mwanadamu, na sio yeye. Na sio kana kwamba ni watu watatu wamepatana katika jambo moja. Ni sawa na maji, mvuke na barafu. Vyote vitatu vikiwekwa pamoja vinaweza kuonekana na vitu tofauti tofauti kabisa, lakini ni kitu kile kile kimoja, ambacho ni maji. Ndivyo alivyo Mungu wetu.

Kutembea katika ofisi ya ubaba, na wakati huo huo mwana, na wakati huo huo Roho Mtakatifu, sio shida kwake, amefanya hivyo ili sisi tukamilishwe. Kama mwanadamu asingeanguka hakukuwa na haja ya Mungu kujifunua katika ofisi zote, angebakia katika ubaba wake ule ule mmoja,

Ni sawa na mtu aliyebuni simu, kama kusingekuwa na changamoto ya umbali ya nini mtu kuzungumza kupitia kifaa hicho?. Vivyo hivyo Mungu kuuvaa mwili, ni ili kutuunganisha sisi na yeye, katika mahusiano ambayo tuliyapoteza pale Edeni. Baadaye akaingia kabisa ndani yetu, kwa Roho wake Mtakatifu, kiasi kwamba sasa tunamwabudu Mungu wetu moja kwa moja ndani ya mioyo yetu.

Kwahiyo, Mungu wetu hajagawanyika. Ni Yule Yule mmoja, wala hana nafsi tatu, bali moja. Wala hakuna mahali kwenye maandiko yanathibitisha kuwa Mungu anazo nafsi tatu. Lakini hilo si jambo la kuzozana nalo, kwa wanaoamini Mungu anazo nafsi tatu, maadamu hawaamini miungu mingi. Akimwabudu Baba, ni Yule Yule, akimwambudu Yesu ni yuleyule Mungu, akimwabudu Roho bado haabudu Mungu mwingine zaidi yake yuleyule mmoja. Hilo ni suala tu la kiufahamu ambalo halimwondolei mtu wokovu.

Hivyo ikiwa wewe ni mkristo, umemwamini Kristo kama ni mwokozi wako, na mwenzako pia kampokea kama wewe tu ulivyopokea,  lakini haamini kama ni Mungu bali ni mwana wa Mungu. Lakutosha, usishindanie mambo ambayo ni ya ujuzi.  Mwombee tu, Mungu ampe ufahamu kamilifu, kwasababu kujua kama utatu mtakatifu ni sahihi au sio sahihi hilo haliwezi kumtenga na Mungu wake, maadamu haubudu nje ya hao.  Tukue kiufahamu, tusimpe adui nafasi ya kuleta mtengano yasiyo na maana.

Kwa maarifa ya ndani zaidi kuhusu, mafundisho ya uungu wa Mungu pitia haya masomo >>>

JE UNATAMANI KUMJUA MUNGU, NA HUJUI PA KUANZIA?

Je Yesu ni Mungu au Nabii?

MADHIHIRISHO MATATU YA MUNGU.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UUNGU NI NINI? (1Petro 1:3-4)

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.

Roho Mtakatifu ni nani?.

Rudi Nyumbani

Print this post

UKWELI KUHUSU UISLAMU Sehemu ya kwanza: (Msikiti wa AL-Aqsa).

Je msikiti wa Al-Aqsa ni nini, na unahusikaje katika unabii wa biblia?

Angalizo: Makala hii haina lengo la kushambulia Imani Fulani, wala kushabikia Imani Fulani, pia haina lengo la kumchafua mtu yoyote, wala kumdhalilisha, bali kutoa elimu sahihi kuhusiana na tunayoamini na yanayoaminiwa.

MSIKITI WA Al-Aqsa

Msikiti wa Al-Aqsa ni msikiti uliopo katika mji wa YERUSALEMU, ndani ya Nchi ya Israeli, Msikiti huu unaaminika kuwa ni sehemu ya tatu ya utakatifu kulingana na dini ya kiislamu, Sehemu ya kwanza ikiwa ni Makka (au Mecca), ya pili ni Al-masjid an Nabawi iliyopo Medina (nchini Saudi Arabia), na ya tatu ndio hii Al-Asqa.

Msikiti wa Al-Aqsa umejengwa pembezoni mwa jengo maarufu kama “Kuba ya Mwamba” (au Dome of Rock), tazama picha chini.

kuba ya mwamba

Msikiti huu wa Al-Aqsa unaaminika ulijengwa na mtu aliyeitwa Umayyad caliph Abd al-Malik kati ya Karne ya saba (7) na ya nane (8), baada ya KRISTO. Na kulingana na dini  ya kiislamu, inaaminika kuwa Muhamad ndipo alipopaa mbinguni na kwenda kupewa ufunuo wa kitabu cha Quran (Sasa kujua kama ni kweli au si kweli soma Makala hii mpaka mwisho)..

Mbali na kwamba katika msikiti huu ndio panaaminika kuwa mahali Muhamad alipopaa lakini pia zamani paliaminika na waislamu wa kwanza kuwa ndio maahali pa kutazama wakati wa sala, maarufu kama “kibla”. Hebu tuielezee hii Kibla kidogo..

Kibla ni neno la kiaramu lenye maana ya “Uelekeo”, Waislamu wanaposali kulingana na Imani yao, wanapaswa waelekee upande Fulani, sasa zamani Kibla ilikuwa ni katika huu msikiti wa Al-Aqsa uliopo Yerusalemu Israeli, lakini baadae walikuja kubadilisha kulingana na kuwa mahali pajulikanapo kama Makka (Mecca) huko Saudi Arabia, ambapo ndipo Muhamad alipozaliwa.

Hivyo sasa waslamu wote wanaposali wanaelekea kibla huko Makka Saudi Arabia na si tena Yerusalemu, na pia mtu anapozikwa anaelekezewa huko Makka, na vile vile mnyama anapochinjwa anaelekezewa huko huko Makka (kujua usahihi wa jambo hili na kama wakristo wanaruhusiwa kushiriki vyakula hivyo endelea kufuatilia Makala hizi)..

Sasa swali ni je! Huu msikiti ambao sasahivi upo pale Yerusalemu, unaoaminika na watu Zaidi ya Bilioni 1.9, kuwa ndio sehemu ya Tatu kwa utakatifu, je msikiti huu utaendelewa kuwepo pale milele au utakuja kuondolewa?.

Jibu: Kujua kama utaondolewa au la! Turejee Biblia..

Maandiko yanasema lile Hekalu la Kwanza lililojengwa na Sulemani, lilitengenezwa juu ya Mlima Moria, ambapo ni eneo lile lile Abrahamu alipotaka kwenda kumtoa mwanae Isaka kama sadaka ya kuteketezwa, na sasa ndio eneo hili hili ambalo msikiti wa Al-Aqsa umejengwa.

Na ilikuwaje Hekalu kuondolewa na msikiti kujengwa?..

Sababu iliyofanya Msikiti huo kujengwa mahali pale pale Hekalu lilipokuwepo… ni kuvunjwa kwa hekalu hilo mara ya kwanza na ya pili…na wayahudi (yaani waisraeli), kuondolewa katika nchi yao na kutapanywa katika mataifa yote mwaka ule wa 70 Baada ya Kristo.

Wayahudi walipoondolewa katika nchi yao kutokana na makosa yao kwa Mungu, ndipo Ngome ya kiarabu ikateka na kujenga msikiti huo.

Adhabu ya Mungu kwa Israeli, haikuwa ya milele, kwani aliahidi atawarudia tena, na kuwarudisha katika nchi yao, na tena watalijenga Hekalu. (soma Ezekieli 40-48), na kufikia mwaka 1948, Israeli walirejea nchini kwao na mpaka sasa wapo pale.

Na hatua ya kwanza ya matengenezo ni wao kuirudia torati waliyopewa na Musa, hivyo watalijenga Hekalu kama lile la kwanza na baadaye, watamwagiwa Neema na macho yao kufumbuliwa Zaidi kwa kumwamini Masihi YESU, aliye hekalu halisi, sawasawa na Warumi 11 (kwani kwasasa wengi wao hawaamini hivyo).

Warumi 11:1 “Basi, nauliza, Je! Mungu aliwasukumia mbali watu wake? Hasha! Kwa kuwa mimi nami ni Mwisraeli, mmoja wa wazao wa Ibrahimu, mtu wa kabila ya Benyamini.

2  Mungu hakuwasukumia mbali watu wake aliowajua tokea awali. Au hamjui yale yaliyonenwa na maandiko juu ya Eliya? Jinsi anavyowashitaki Waisraeli mbele za Mungu………………………

25  Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

26  Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake”.

Sasa kabla ya huo wakati wa Israeli kufumbuliwa macho,na kumjua Kristo kama Hekalu halisi, watasimamisha kwanza Hekalu la damu na nyama, na mahali litakapojengwa ni palepale lilipojengwa hekalu la kwanza. Na hapo si pengine bali ni eneo lile lile Msikiti wa Al-aqsa ulipo.

Maswali yafuatayo yananyanyuka:

Je! Ni ni kitatokea?..na je huo msikiti utaondolewa kupisha ujenzi wa Hekalu, na kama utaondolewa je utaondolewaje?..na ni lini?.

Jibu ni  kwamba Msikiti ule ni lazima utaondolewa pamoja na ile Kuba ya Mwamba (Dome of Rock)!!, kwasababu Neno la Mungu limeshasema hivyo kwamba Hekalu litajengwa…na Neno la Mungu halijawahi kupita (kilichotabiriwa katika Ezekieli 40-47  kitatimia kama kilivyo), hakuna shaka juu ya hilo, haijalishi ni muda gani utapita!!.. Wakati utakapofika wa unabii huo kutimia msikiti wa Al-Aqsa utaondoka.

Ni kwa njia gani utaondolewa?.. hakuna anayejua kama ni kwa njia ya Amani, au kwa njia nyingine, lakini dunia nzima itatii tu kwasababu ni Bwana ndiye aliyeyasema hayo, na kuyapanga si MTU, wala WATU wala Taifa la Israeli, bali ni MUNGU mwenyewe!!, hivyo hata wakati wa kuondolewa hakuna atakayejisifu kuwa ni nguvu zake, bali Mungu mwenyewe ndiye atakayehusika hapo.

Na dalili zote zinaonyesha kuwa tumekaribia sana hicho kipindi, kwani waisraeli wameshakusanya utajiri mkubwa na utaalamu mwingi, kiasi kwamba endapo ikitokea ukaanza leo, basi hakuna kizuizi chochote cha kifedha wala kiutalaamu.

Na ujenzi huo unauhusiano mkubwa sana na mpinga-Kristo ajaye, ambapo biblia inasema atatafuta kuingia katika hekalu hilo, ili atafute kuabudiwa yeye kama Mungu (2Wathesalonike 2:4), na maandalizi ya mpinga-kristo yapo ukingoni..nafasi yake ipo tayari, kinachongojewa ni parapanda.

HOJA NYINGINE ZISIZO SAHIHI.

  1. Je Muhamad alipaa??..

Je ni kweli Muhamad alipaa, na je ni kweli Qurani ni kitabu cha Mwenyezi Mungu?

Jibu ni la! Hakupaa!!..Kwasababu Biblia inatuambia manabii waliopaa ni wawili tu, Henoko na Eliya.. na BWANA YESU ambaye ndiye Mkuu wa Uzima. Hao ndio waliopaa, na wengine watakaopaa ni watu watakaofufuliwa na kwenda mbinguni siku ya unyakuo, na watakatifu watakaokuwa hai siku ya kurudi kwa Bwana, pamoja na wale manabii wawili waliotajwa katika Ufunuo 11, basi!

Na pia Quran sio kitabu cha mwenyezi Mungu chenye kumfikisha mtu mbinguni. Kinaweza kuwa kitabu chenye baadhi ya maonyo yaliyo sahihi ambayo mtu akiyafuata anaweza kuwa mzuri katika jamii, lakini si kuurithi uzima wa milele…Kwa ujumla kitabu hiko hakina mafundisho ya Uzima wa milele, kwasababu kinamkataa YESU kama NJIA PEKEE ya WOKOVU wa mwadamu.

Na kitabu chochote kisichoelekeza moja kwa moja Uzima wa milele uliopo ndani ya YESU, au  mtu yeyote yule asiyeamini kuwa YESU ndiye BWANA, na Mwokozi, na ndiye njia pekee ya UZIMA, huyo mtu hana uzima wa milele haijalishi atakuwa anafanya mambo mengine yanayoonekana mazuri machoni pa watu, lakini kama hatamwamini Bwana YESU baada ya kumsikia, matendo yake hayo hayatamsaidia chochote, kwasababu hakuna mwanadamu atakayeweza kusimama kwa matendo yake peke yake.

Yohana 3:18 “ Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu”.

Usikose mwendelezo kuhusiana na Kibla ya wanyama na “Kaaba”, na kama wakristo tunaruhusiwa kushiriki vyakula hivyo.. Pia usikose kufuatilia Makala hizi pamoja na nyingine nyingi, juu ya ukweli kuhusiana na Uislamu na Imani nyingine.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je!Sisi kama wakristo Tunaruhusiwa kuchangia ujenzi wa Imani nyingine?

WEWE NI HEKALU LA MUNGU.

JE! UNA MASIKIO YANAYOSIKIA?

UFUNUO: Mlango wa 11

Je! Wapalestina ni watu gani, na sehemu yao katika biblia ni ipi?

Rudi Nyumbani

Print this post

Ni dhiki ipi hiyo watu walio kwenye ndoa huipata sawasawa na 1Wakorintho 7:28?

1Wakorintho 7:28  Lakini, kama ukioa, huna hatia; wala mwanamwali akiolewa, hana hatia; lakini watu kama hao watakuwa na dhiki katika mwili nami nataka kuwazuilia hayo.

Awali ya yote katika vifungu hivi, Mungu hashinikizi kwamba watu  wasioe au wasiolewe.  Ndoa ni jambo jema, na lina faida nyingi sana katika maisha na pia katika huduma, kwasababu humsaidia mtu akae mbali na uzinzi na tamaa mbaya, (1Wakorintho 7:2). Pia huondoa upweke (Mwanzo 2:18), wawili wawapo mwili mmoja, ni nguvu zaidi na faraja.

Lakini Mungu anatoa pia uchaguzi, kwa mtu ikiwa anao uwezo wa kujizuia yaani kutawala hisia zake (1Wakorintho 7:9), akaishi hivyo hivyo, bila shida yoyote, ni vema zaidi kihuduma. Kwasababu humfanya asisongwe na mambo mengi ya kindoa.

Kwasababu mtu aliye kwenye ndoa ni wazi kuwa upendo wake utagawanyika kwa sehemu, biblia inasema atatafuta ampendezeje mume/mke wake.

1Wakorintho 7:32  Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;

33  bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe.

Lakini pia atakutana na dhiki, zinazoambatana na ndoa. Kwamfano kutatua migogoro ya kifamilia,  malezi ya watoto, kuwagharamikia, kuwasomesha,matibabu, kuwafuatilia, kuivisha familia yako, na mambo kama hayo. Ni dhiki ambazo, zinaongezeka, na hivyo hutinga ufanisi wako kwenye utendaji kazi wa injili.  Paulo huiita “shida iliyo” sasa. Yaani Kusalitiana, upendo kupoa, kupishana,  ni vitu ambavyo mara kwa mara hujitokeza katika maisha ya ndoa.

1Wakorintho 7:26  Basi, naona hili kuwa jema, kwa ajili ya shida iliyopo, kwamba ni vema mtu akae kama alivyo.

27  Je! Umefungwa kwa mke? Usitake kufunguliwa. Umefunguliwa? Usitafute mke

Hivyo kihuduma mtu ambaye hajaoa/kuolewa, hujipunguzia dhiki, kuliko yule aliye kwenye ndoa. Hiyo haimaanishi kuwa aliye kwenye ndoa hawezi kutenda kazi vizuri, hapana kazi anaweza itenda hata zaidi ya Yule ambaye hajaoa, isipokuwa tu kwake dhiki na shida zitaongezeka.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA

NDOA TAKATIFU NI MKE MMOJA/MUME MMOJA.

NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA!

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

Rudi Nyumbani

Print this post

Je biblia inajichanganya kwa habari ya hukumu ya Mungu (Yohana 12:47 na Yohana 5:22, 27).

Swali: Katika Yohana 5:22 na 27 tunaona biblia inasema kuwa Mungu amempa Mwana (Yaani Bwana Yesu) hukumu yote…. lakini tukiruka mpaka ile sura ya 12:47 tunaona tena Bwana YESU anakanusha kuwa yeye hamhukumu mtu?.. Je biblia inajichanganya hapa?.


Jibu: Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa Biblia ni kitabu kilichovuviwa na Roho Mtakatifu, hivyo kamwe hakina makosa…kinachoonekana kinajichanganya si Biblia, iliyo Neno la Mungu, bali ni tafakari zetu na pambanuzi zetu.

Sasa turejee mistari hiyo..

Katika Yohana 5:22  “Tena Baba hamhukumu mtu ye yote, BALI AMEMPA MWANA HUKUMU YOTE………….

27  Naye AKAMPA AMRI YA KUFANYA HUKUMU kwa sababu ni Mwana wa Adamu”.

Hapa ni kweli Mwana kapewa mamlaka yote ya kufanya hukumu… Tusome tena ile Yohana 12:47..

Yohana 12:47 “Na mtu akiyasikia maneno yangu, asiyashike, MIMI SIMHUKUMU; MAANA SIKUJA ILI NIUHUKUMU ULIMWENGU, ila niuokoe ulimwengu”.

Tukisoma mistari hiyo kwa juu juu, ni rahisi kuona kuwa maneno hayo yanajichanganya… lakini kiuhalisia hayajichanganyi hata kidogo.. kwani ni suala la kuelewa lugha tu hapo!.

Katika Yohana 5:22, Baba amempa Mwana hukumu yote, maana yake Amri ya kuhukumu amempa yeye.. Maana yake mamlaka yote kapewa (Bwana YESU), kama vile Farao alivyompa Yusufu mamlaka yote ya Misri.

Sasa kama Bwana YESU kapewa mamlaka yote ya kufanya hukumu… ni chaguzi lake yeye ni nani amhukumu na nani asimhukumu, ni wakati gani afanye hukumu na ni wakati gani asihukumu…(kwasababu vyote vipo mikononi mwake).

Sasa kwasababu yote yamewekwa chini ya mapenzi yake, basi mapenzi yake ni “kumtomhukumu mtu yoyote duniani”…sawasawa na maandiko hayo ya Yohana 12:47.. ingawa anayo mamlaka  hayo ya kumhukumu mtu yoyote duniani kwasababu kashapewa na Baba.

Lakini hakutumia huo uwezo, wa kupitisha hukumu duniani kwa wote waliomkataa au wanaomkataa sasa, bali anawavumilia mpaka siku ya mwisho.. Mfano mzuri unaomwonyesha Bwana akiwa ameizuia hukumu yake ni ile habari tunayoisoma katika Luka 9:52-56.

Luka 9:52 “akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.

53  Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu. 54  Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?

55  Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]

56  Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine”.

Huo ni mfano wa hukumu ambayo Bwana angeweza kuito kwa Wasamaria hao, lakini alizuia… utasoma tena jambo kama hilo hilo katika Mathayo 26:51-53.

Mathayo 26:51 “Na tazama, mmoja wao waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono wake, akaufuta upanga wake, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.

52  Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga.

53  AMA WADHANI YA KUWA MIMI SIWEZI KUMSIHI BABA YANGU, NAYE ATANILETEA SASA HIVI ZAIDI YA MAJESHI KUMI NA MAWILI YA MALAIKA?”

Kwahiyo ni kweli Bwana YESU amepewa hukumu yote, lakini hatumii uwezo wa hukumu yake yote, kwetu sisi tunaoishi sasa, laiti akifanya hivyo, hakuna mwenye mwili atakayepona.. Lakini anatuvumilia sana kwasababu hataki mtu yoyote apotee (2Petro 3:9).

Ila tukiudharau wingi wa huruma zake hizi, na kupuuzia Neema mpaka siku tunaondoka katika haya maisha au siku amerudi, basi tutahukumiwa na yeye pasipo huruma… Na atatuhukumu kupitia maneno yake hayo hayo.

Hivyo ndugu yangu, YESU sasa ni mwenye huruma na mvumilivu kwetu, lakini siku ile ya hukumu hatakuwa na huruma..kwahiyo si muda wa kudharau wema wake na uvumilivu wake kwetu, bali ni wakati wa kutengeneza maisha kabla ya ile siku ya hukumu..

Warumi 2:4 “Au waudharau wingi wa wema wake na ustahimili wake na uvumilivu wake, usijue ya kuwa wema wa Mungu wakuvuta upate kutubu?

5 Bali kwa kadiri ya ugumu wako, na kwa moyo wako usio na toba, wajiwekea akiba ya hasira kwa siku ile ya hasira na ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu,

6 atakayemlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake”

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

IKIWA MWENYE HAKI AKIOKOKA KWA SHIDA, MWENYE DHAMBI ATAONEKANA WAPI?

UFUNUO: Mlango wa 20

Kuna hukumu za aina ngapi?

Tirano alikuwa nani na darasa lake lilikuwaje? (Matendo 19:9)

Mithali 24:17 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?

Rudi Nyumbani

Print this post

Je wafu wanafufuliwa au hawafufuliwi kulingana na Ayubu 14:12 na 1Wakorintho 15:51?

Swali: Katika Ayubu 14:12 tunasoma kuwa wafu hawafufuliwi, lakini katika 1Wakorintho 15:51 tunaona tena biblia inasema wafu watafufuliwa, sasa tuchukue ipi tuache ipi?.. au je biblia inajichanganya yenyewe?


Jibu: Biblia kamwe haijichanganyi, wala haijawahi kujichanganya, isipokuwa tafakari zetu ndizo zinachojichanganya au kuchanganyikiwa.

Turejee mistari hiyo na kisha tuone majibu yake kupitia biblia hiyo hiyo..

Ayubu 14:10 “Lakini mwanadamu hufa, huifariki dunia; Naam, mwanadamu hutoa roho, naye yupo wapi?

11 Kama vile maji kupwa katika bahari, Na mto kupunguka na kukatika;

12 Ni vivyo MWANADAMU HULALA CHINI, ASIINUKE; Hata wakati wa mbingu kutokuwako tena, hawataamka, Wala kuamshwa usingizini.”

Ni kweli hapa maandiko yanasema kuwa MWANADAMU HULALA CHINI, ASIINUKE TENA… lakini hebu turejee agano jipya katika kitabu kile cha Wakorintho tuangalie biblia inatuambiaje..

1Wakoritho 15:51 “Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,

52  kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana PARAPANDA ITALIA, NA WAFU WATAFUFULIWA, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika”.

Na hapa maandiko yanatuambia, parapanda italia na wafu waliolala katika Kristo watafufuliwa. Sasa swali tuchukue lipi tuache lipi?, maneno kama hayo hayo yanarudiwa tena katika 1Wathesalonike 4:16.

Jibu ni Dhahiri kuwa “Wafu watafufuliwa siku ya mwisho”.. sawasawa na Yohana 5:25.

Kwanini maandiko hayo ya 1Wakoritho 15:51 yana nguvu kuliko yale ya Ayubu 14:12, yanayosema kuwa “wafu hawafufuliwi”?… Ni kwasababu Agano jipya ni ukamilifu wa agano la kale.

Manabii waliotangulia walifahamu mambo kwa sehemu, lakini Roho Mtakatifu katika agano jipya, amekamilisha yote na kufunua yote… Na kawaida ni kwamba unapokuja ule ufunuo mkamilifu, bali ule uliokuwa unajilikana kwa sehemu unabatilika ndivyo maandiko yasemavyo..

1Wakorintho 13:9 “Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;

10  lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika”.

Manabii wengi wa agano la kale hawakujua mengi kuhusiana na ufufuo, au mbingu mpya na nchi mpya, ingawa walikuwa wanafahamu siku moja watajua mambo yote..hivyo walitoa unabii kwa sehemu waliyopimiwa…lakini mwisho wa nyakati Roho Mtakatifu anakamilisha ufunuo wote sawasawa na hiyo 1Wakorintho 13:9-10.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Wafu watafufuliwa siku ya mwisho, na watahukumiwa.

Yohana 5:28  “Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.

29  NAO WATATOKA; WALE WALIOFANYA MEMA KWA UFUFUO WA UZIMA, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu”.

Na kumbuka hoja hii ya kufufuliwa kwa wafu ndiyo iliyoleta mgawanyiko mkubwa katikatika ya wayahudi hata kuzaliwa makundi (madhehebu) mawili ambayo ni MAFARISAYO NA MASADUKAYO, ambapo Mafarisayo waliamini ufufuo na masadukayo hawakuamini ufufuo kwa kutumia andiko hilo la Ayubu 14:12 pamoja na maandiko mengine machache..

Lakini Bwana YESU alikuja kuondoa huo utata kama tunavyosoma katika Mathayo 22:23-32..

Mathayo 22:23 “Siku ile Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza,

24  wakisema, Mwalimu, Musa alisema, Mtu akifa, akiwa hana watoto, ndugu yake na amwoe yule mkewe, ili ampatie nduguye mzao.

25  Basi, kwetu kulikuwa na ndugu saba; wa kwanza akaoa, akafariki, na kwa kuwa hana mzao, akamwachia nduguye mke wake.

26  Vivyo hivyo wa pili naye, na wa tatu, hata wote saba.

27  Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.

28  Basi, katika kiyama, atakuwa mke wa yupi katika wale saba? Maana wote walikuwa naye.

29  Yesu akajibu, akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu.

30  Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni.

31  Tena kwa habari ya kiyama ya watu, hamjalisoma neno lililonenwa na Mungu, akisema

32  Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu, bali wa walio hai”

Kwahiyo wafu watafufuliwa, lakini swala la msingi ni je!.. sisi tutakuwepo upande upi wakati huo wa ufufuo?.. Je tutafufuliwa ili tukavikwe taji na kuurithi uzima wa milele, au kwaajili ya hukumu ya ziwa la Moto?

Kumbuka wote walio nje ya Kristo, ambao hawajampokea Bwana YESU na kuoshwa dhambi zao kwa damu yake, wametabiriwa kuwa miongoni mwa watakaohukumiwa katika hukumu ya milele. Je umeokoka?..umebatizwa katika ubatizo sahihi?.. umejazwa Roho Mtakatifu?.

Kama bado unangoja nini?… Ni heri ukafanya maamuzi leo ya kubadili maisha yako.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUZIMU ni mahali pa namna gani, Je! huko wanaishi watu wakifa na kwenda kupata mateso au ni vinginevyo?

UFUFUO WA UZIMA NA WA HUKUMU.

UTALIPWA KATIKA UFUFUO WA WENYE HAKI.

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

Kuna ufufuo wa aina ngapi?

Rudi Nyumbani

Print this post

NIFANYE NINI NIMSHINDE SHETANI?

1) WOKOVU: 

Hilo ndio jambo la kwanza. Kamwe huwezi kumshinda shetani ikiwa upo nje ya Kristo, Ndicho kilichowakuta wale wana wa Skewa, walipotaka kutoa pepo kwa jina la Yesu. Lakini Yule pepo akawaambia Yesu namjua, na Paulo namfahamu, lakini je ninyi ni akina nani?

Matendo 19:13  Baadhi ya Wayahudi wenye kutanga-tanga, nao ni wapunga pepo, wakajaribu kutaja jina la Bwana Yesu juu yao waliopagawa na pepo wachafu, wakisema, Nawaapisha kwa Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo.

14  Walikuwako wana saba wa mtu mmoja Skewa, Myahudi, kuhani mkuu, waliofanya hivyo.

15  Yule pepo mchafu akawajibu, akawaambia, Yesu namjua na Paulo namfahamu, lakini ninyi ni nani? 16  Na yule mtu aliyepagawa na pepo mchafu akawarukia wawili, akawaweza, akawashinda, hata wakatoka mbio katika nyumba ile hali wa uchi na kujeruhiwa.

Wokovu, ni Kristo ndani yako, na kwa huo nguvu za adui zote huyeyuka mara moja. Mtu aliyempokea Yesu, shetani kamwe hamwezi, kwasababu anamwona Kristo ndani yake.

2) MAOMBI: huharibu mipango ya ibilisi.

Unaweza ukawa umeokoka, lakini shetani akapata nguvu za kukusumbua kwa majaribu, kwasababu unashindwa kutumiza baadhi ya wajibu wako kwa mwamini, Yesu alisema..

Mathayo 26:41  Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.

Yesu ijapokuwa alikuwa ni mkamilifu hana dhambi, alijaribiwa na adui, wewe ni nani usikutane na hayo? Usipokuwa mwombaji, uvivu ukakumeza, unaona shida kuomba kila siku, kuhudhuria mikesha ujue tayari upo majaribuni. Hata kama utajiona upo sawa, fahamu tu hapo ulipo kuna eneo Fulani adui anakusumbua, utakuja kugundua pindi utakapoanza kuwa mwombaji. Na ndio maana maisha ya wokovu hayatengwi na maombi. Shetani akimwangalia mwombaji anaona moto umemzunguka mkali, hawezi jiamulia tu kufanya analotaka kwake.

3) KUBALI KUWA MJINGA: Utamweka chini shetani.

Warumi 16:19  Maana utii wenu umewafikilia watu wote; basi nafurahi kwa ajili yenu, lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya. 20  Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. [Amina.]

Hapo anasema tuwe wajinga katika mambo mabaya. Ni nafasi kubwa kwa Mungu kumweka shetani chini ya miguu yetu. Kwamfano, unapokuwa hujui kuhusu mitindo mipya ya kidunia, sio mfuatiliaji wa miziki ya kidunia, muvi mpya mpya zilizotoka duniani, yaani kwa ufupi unapitwa na mambo ya kidunia yasiyokuwa na maana kwako, kinyume chake, unakuwa na ujuzi na hekima katika mambo ya rohoni jua hapo umemshinda shetani kwa sehemu kubwa. Hana kitu kwako, kwasababu bidhaa zake, huna mpango nazo, hununui chochote kwake.  Kuipenda dunia ni kuwa adui wa Mungu, na rafiki wa shetani.

4) WEKA NENO LA MUNGU NDANI: Utamfukuza shetani.

Kuweka Neno sio, kukariri vifungu vingi vya biblia, hapana, bali ni kufahamu “ukweli” (ufunuo)  wa kila Neno unaloliweka moyoni mwako. Pale jangwani, Yesu alipokutana na shetani, alimjaribu kwa Neno hilo hilo,lakini Yesu akamwambia kweli yote ipoje.

Mathayo 4:6  akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 7  Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.

Ni muhimu ukalifahamu Neno la Mungu katika kweli yake, na hiyo huchangiwa na kufundishwa kwa ufasaha Neno la Mungu na waalimu, kwasababu Roho Mtakatifu atasema na wewe kupitia wao. Lakini pia kumpa Roho Mtakatifu nafasi ya moja kwa moja kukufundisha. Vinginevyo adui atakudanganya sana, hususani kupitia manabii wa uongo, kwasababu hulijui Neno vema.

 5) LITII NENO: Utaweza yastamili majaribu yake yote.

Kulifahamu Neno, na kuijua kweli, ni jambo muhimu lakini bado shetani anaweza pata mianya ya kukunasa endapo hutaweza kulitii Neno. Penda utakatifu, penda kutendea kazi kile unachofundishwa. Yesu alisema, wapo watu wasikiao tu, lakini wapo wasikiao na kuyatendea kazi. Wote hujaribiwa kwa pepo, mafuriko na mvua za shetani. Sasa Yule aliyejijenga  juu ya fundisho tu, na sio kutendea kazi fundisho, ndio huyo anayechukuliwa na mafuriko.

Mathayo 7:26  Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;

27  mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.

Mateso mengine huwapata watu kwasababu ya dhambi. Kuishi maisha matakatifu, humnyima adui mlango wa kukushambulia kwa namna yoyote. Liishi Neno.

6) HUBIRI NENO: Utamwangusha adui kutoka juu.

Watu wengi hudharau ushuhudiaji. Tunapokuwa na moyo mmoja wa kuitenda kazi ya Mungu, adui hawezi kukaa juu ya anga hili, kutupinga. Tunalisoma wapi hilo? Utakumbuka wakati ule Bwana alipowatuma wanafunzi  wake wawili wawili kuhubiri, waliporudi kwa furaha, huku wakimwambia Bwana  hata mapepo yanawatii. Yesu akawaambia nalimwona shetani akianguka kutoka juu kama umeme. Kuonyesha kuwa kitendo cha wao kuhubiri adui alikuwa anaporomoka kwa kasi sana.

Mathayo 10:17  Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. 18  Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.

Hivyo ukizingatia mambo  hayo sita (6), Utakuwa sio tu umemdhibiti adui kila Nyanja, bali pia umemteka. Ni wajibu wako mimi na wewe kuboresha mahali ambapo hapako sawa, ili kwa pamoja tukaujenge ufalme wa Mungu na kuziangusha kazi za shetani.

Yakobo 4:7  Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ZIFAHAMU KAZI KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

USIWE ADUI WA BWANA

Rudi Nyumbani

Print this post

Mungu anaketi katikati ya sifa?

Swali: Kwa namna gani Mungu anaketi katikati ya sifa?


Jibu: Biblia haisemi “Bwana Mungu anaketi katikati ya sifa”…bali inasema “Mungu anaketi juu ya sifa za Israeli”.

Zaburi 22:3 “Na Wewe U Mtakatifu, Uketiye juu ya sifa za Israeli.

4 Baba zetu walikutumaini Wewe, Walitumaini, na Wewe ukawaokoa”

Ili tuelewe vizuri ni kwa namna gani Mungu anaketi juu ya sifa za watu wake, kwanza tusome andiko lifuatalo…

Mathayo 6:10 “Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni”.

Kwa mantiki ya andiko hilo, tunona kuwa kumbe mbinguni mapenzi ya Mungu yanaendelea kufanyika, na hivyo duniani pia yanapaswa yafanyike kama yanavyofanyika huko juu…

Sasa moja ya mapenzi ya Mungu yanayofanyika mbinguni ni SIFA, ambazo MALAIKA watakatifu WANAMPA MUNGU usiku na mchana.

Na ndio maana maandiko yanasema katika 1Samweli 4:4, 2Samweli 6:2, Zaburi 80:1, Zaburi 99:1, na Isaya 37:16 kuwa Mungu ANAKETI JUU YA MAKERUBI… Na kazi ya Makerubi si nyingine Zaidi ya KUMSIFU MUNGU, na KUMPA UTUKUFU usiku na mchana, soma Ezekieli 10:18 na Ezekieli 11:22.

Na ni wapi katika biblia panapoonyesha kuwa kiti cha Enzi cha Mungu kipo juu ya makerubi, na si chini??…soma Ezekieli 1:26 na Ezekieli 10:20.

Kwahiyo kama mbinguni wanavyompa Mungu utukufu, na kwamba Mungu anaketi juu ya yao wampao sifa, hali kadhalika na duniani, Mungu anaketi juu ya sifa za watu wake! Sawasawa na hilo andiko la Zaburi 22:3.

Zaburi 22:3 “Na Wewe U Mtakatifu, Uketiye juu ya sifa za Israeli”.

Hivyo tunapompa Mungu sifa, basi tunakamilisha Enzi yake katikati yetu, na hivyo Mungu anashuka. Na ibada ni lazima iwe na sifa,..Sifa ni kiungo cha muhimu sana katika kuuvuta uwepo wa Mungu, na hatumsifu tu Mungu kwasababu katuambia tumsifu….Lakini tunamsifu kwasababu AMESTAHILI!!.

Kitendo cha kumtoa mwanae kwaajili yetu sisi ambao tulikuwa hatustahili, ni Dhahiri kuwa ANASTAHILI SIFA ZETU, kitendo cha kuendelea kutupa uzima na ulinzi kila siku, hakika AMESTAHILI.

Bwana atusaidie kila siku tuone sababu za kumsifu yeye.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

ANGALIA USIJE UKANG’OA NGANO KATIKATI YA MAGUGU.

KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?

NAYE ALIKUWA HANA BUDI KUPITA KATIKATI YA SAMARIA.

Sifa ni nini?

Rudi Nyumbani

Print this post

Bwana YESU alibatizwa na umri gani?

Jibu: Umri kamili ambao Bwana YESU alikuwa nao wakati anabatizwa na Yohana katika mto Yordani, ni miaka thelathini (30).

Tunalithibitisha hilo katika Luka 3:21-23..

Luka 3:21 “Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka;

22  Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua; sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.

23  Na Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, ALIKUWA AMEPATA UMRI WAKE KAMA MIAKA THELATHINI”

Sasa kwanini Bwana Yesu abatizwe ukubwani na si utotoni?…Jibu rahisi ni kwamba alikuwa anatupa kielelezo, kwamba mwamini anapaswa abatizwe wakati ambao yeye mwenyewe kajitambua na kuona sababu zote za kubatizwa kwa hiari yake mwenyewe na si kwa kuamuliwa.

Kwa uthibitisho huo basi ni wazi kuwa “ubatizo wa utotoni” si sahihi.. Huenda waliosimamia ubatizo huo walikuwa na nia njema, lakini bado Neno la Mungu litabaki kuwa lile lile, kuwa ubatizo wa utotoni sio sahihi kimaandiko, hivyo hatuna budi kuweka mitazamo yetu pembeni, na mawazo yetu, na mapokeo yetu, na kulisimamisha Neno la Mungu.

Hakuna mahali popote katika maandiko, watoto walibatizwa, au watu walibatizwa kwa maji machache… Zaidi sana maandiko yanatuonyesha watu walisafiri kwenda mpaka Ainoni alipokuwa akibatiza Yohana, kwasababu kule kulikuwa na MAJI TELE.

Yohana 3:23 “Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni, karibu na Salimu, kwa sababu huko kulikuwa na MAJI TELE; na watu wakamwendea, wakabatizwa”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yohana mbatizaji alibatizwa na nani?

Yeremia alikuwa na umri gani alipoitwa?

Je! Ni sahihi kuoa/kuolewa na mtu uliyemzidi umri?

Je ni kweli miaka yetu ya kuishi ni 80 tu (kulingana na Zaburi 90:10).

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Ndugu Yule anayezungumziwa kwenye 2Wakorintho 8:18 ni nani?

SWALI: Kwenye 2Wakorintho 8:18, Mtume Paulo anamtaja ndugu ambaye jina lake hajaliweka wazi. Ni kwanini afanye hivi tofauti na alivyozoea kufanya katika nyaraka zake nyingine, kuwataja aliowatuma?

 2Wakorintho 8:18 Na pamoja naye tukamtuma ndugu yule ambaye sifa zake katika Injili zimeenea makanisani mwote.19  Wala si hivyo tu, bali alichaguliwa na makanisa asafiri pamoja nasi katika jambo la neema hii, tunayoitumikia, ili Bwana atukuzwe, ukadhihirike utayari wetu.


JIBU: Katika waraka huu, tunaona Paulo akiwaandikia kanisa la Korintho, suala la changizo kwa ajili ya watakatifu maskini waliokuwa Yerusalemu. Hivyo akawatuma pia na watatu ili kulifanikisha jambo hilo. Wa kwanza ni Tito, Ukisoma mstari wa 16-17, katika sura hiyo hiyo ya 8, anatajwa, wa pili ndio huyu ambaye sifa zake za injili zilivuma kwenye makanisa, na watatu ni ndugu mwingine ambaye pia hajatajwa jina, isipokuwa Paulo alimwita kama ‘ndugu yetu’ ambaye tunamsoma kwenye mstari wa 22

2Wakorintho 8:22  Nasi pamoja nao tumemtuma ndugu yetu tuliyemwona mara nyingi katika mambo mengi kuwa ana bidii, na sasa ana bidii zaidi sana kwa sababu ya tumaini kuu alilo nalo kwenu.

Watu hawa watatu ndio waliotumwa kwa ajili ya huduma hiyo ya changizo kwa wakorintho. Lakini swali huulizwa huyu ndugu wa pili ni nani hasaa?

Wengine husema ni Luka, wengine Barnaba, wengine Apolo, wengine Marko, Aristako. Kutokana na kwamba wengi wa hawa walisifika kwa usambazi injili, lakini pia walikuwa na Paulo mara nyingi kwenye huduma.

Lakini Hayo ni makisio tu, anaweza akawa miongoni mwa hawa, lakini pia asilimia kubwa anaonekana sio kabisa miongoni mwao, waliowahi kutajwa na Paulo.

Jambo la muhimu  ambalo, linalengwa hapo, kufichwa kwa jina lake. Sio kwamba Mungu anataka tumchunguze ni nani? Hapana Lakini alipenda kutuonyesha kwamba SIFA, hujitambulisha zaidi kuliko jina.

Ukichunguza hapo, utaona Paulo anasema sifa zake zimeenea kwenye “makanisa yote”. Ikiwa na maana kuanzia huko Akaya mpaka Makedonia. Alijulikana kuwa mhubiri mwenye juhudi na mwenye kuthamini injili. Na si hivyo tu, walimchagua mwenyewe kusafiri pamoja na Paulo. Hivyo Paulo kuandika waraka huo, kwa kueleza sifa zake, aliona hilo latosha tu, kumtambulisha bila hata ya jina. Kwasababu hakuna mwingine zaidi yake. Yaani kwa namna nyingine Paulo anasema, “Mpaka hapo mmeshamtambua ni nani”.

Sikuzote wanaotambulishwa kwa majina huwa ni watu wasiojulikana, au wasio na sifa za kutosha kwenye jamii husika.

Ndivyo ilivyokuwa pia kwa Yule mtu wa tatu ambaye Paulo alimwita kama “NDUGU YETU”. Kulikuwa hakuna haja ya kumtambulisha kwa jina kwasababu walikuwa wanamwona wakati wote akiwa na akina Paulo katika ziara zake na huduma. Hivyo kumtafaja tu ndugu yetu ilitosha, alijua kila mmoja alielewa ni nani aliyekuwa anazungumziwa, kwasababu mitume hawakuwa na ndugu mwingine zaidi ya huyo, aliyekuwa karibu nao.

Hata leo, Bwana anapenda sisi tutambuliwe kwa SIFA zetu, zaidi ya MAJINA yetu. Kiasi kwamba kazi itakayoonekana kwa ajili ya Kristo, itutambulishe sisi, sio sisi tuyatambulishe majina yetu katikati ya watu.

Utaona baadhi ya wahubiri wanachokifanya, ni kutumia nguvu kubwa kutangaza majina yao, na sura zao, ili wajulikane, lakini kazi zao hazitambuliki. Hilo sio lengo la mhubiri, au Mtumishi wa Mungu. Bwana wetu Yesu Kristo alipokuwa duniani, haikuwa na muda wa kujitangaza, wakati mwingine hakutaka mambo yake yadhihirishwe kiwepesi, mpaka atakapomaliza kazi yake, Na sisi pia tupende aina hii ya utumishi.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Epafrodito ni nani kwenye biblia?

Epafra ni nani katika biblia? (Wakolosai 1:7)

Je ni sawa kuukubali udhaifu kama mtume Paulo alivyojisifia kwa huo? (2Wakorintho 12:9-10)

Rudi Nyumbani

Print this post