Title March 2025

MUNGU AKETIYE MAHALI PA JUU PALIPOINUKA.

Isaya 6:1

[1]Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu.

Je unayajua makao hasaa ya Mungu?

Ni kweli tunafahamu Mungu anaketi katika kiti chake cha enzi, lakini ni kiti kilicho wapi hasaa?

Je! handakini? Mabondeni? Mapangoni? Kichakani? hasha!

Maandiko yanatueleza “Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana”

Kwahiyo na sisi lazima tuyajue makao hayo, ili tumfikie, vinginevyo tutajikuta tunaabudu Mungu mahali Ambapo kiti chake hakipo.

Katika biblia sehemu yoyote unapokutana na hili Neno “mahali pa juu”, Moja kwa moja utaona palihusishwa Na ibada..Yaani madhahabu zilijengwa pale ili kumtolea Mungu dhabihu. (1Samweli 9:12-13, 1Wafalme 3:2)

Yalikuwa ni maeneo yote yaliyoinuka mfano milimani. Kwasababu huko ndiko Mungu alikuchagua kujidhihirisha, na sio mabondeni, au mapangoni.

Ni kwanini?

Kwasababu Mungu anakaa sehemu Bora kuliko zote, sehemu iliyozidi vyote, sehemu ya juu ya juu kuliko zote. Hakai penginepo, Mungu hawekwi chini, haabudiwi mabondeni..kamwe hiyo sio sifa yake.

Hivyo ni vema ukafahamu sifa yake hii, ili tujue namna sahihi ya kumwendea.

Sasa sehemu zake za juu, kiroho tutaziona katika makundi matano(5), kisha tutaona namna anavyopaswa kufikiwa.

1). Makazi:

(Mbinguni)

Kimakazi Mungu anaketi mbinguni.. Kwasababu Mbingu ni bora kuliko dunia hii.

Isaya 66:1

[1]BWANA asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?

Ndio maana tuna ujasiri na Mungu, akatie sehemu Bora zaidi ya hii, ambayo alisema atatukaribisha katika makao hayo baadaye.

Bwana Yesu alituambia tukisali tuseme Baba yetu uliye mbinguni.. (Mathayo 6:9). Hata alipoomba aliinua macho yake juu(Yoh 17:1), na sisi tumtakaripo Mungu, tuiweke picha hiyo akilini mwetu. Kwamba Baba yetu yupo mbinguni.

Na kutoka huko ndio tunatarajia mema yetu yaje, Na wenyeji wetu kushuka.(Yerusalemu mpya).

2) Viumbe.

(Mwanadamu).

Mwanadamu ametukuka kuliko viumbe vyote, amemvika uwezo na mamlaka (Zab 8:4-6). ndio maana amechagua kuketi ndani ya moyo wa mwanadamu na sio kiumbe kingine chochote. Mungu hakai ndani ya swala, au sungura, au simba.. amechagua makao yake kuwa ndani ya mwanadamu tu.

Na aliyetufungulia lango hilo ni Yesu Kristo mwokozi wetu, kama mwanadamu wa kwanza ambaye Mungu alikaa ndani yake kikamilifu. Pasipo yeye kamwe Mungu asingekaa ndani ya moyo wa mwanadamu.

Ukimkosa Kristo umemkosa Mungu ndani yako.

Hivyo wewe uliyeokoka, fahamu kuwa Mungu anakaa ndani yako, hivyo wajibu wa kujichunga sana na kumpa Mungu ibada ya kweli( Warumi 12:1)

Ndio maana anapouheshimu mwili wako umemuheshimu Mungu. Kama mwanadamu ogopa sana kujiharibu kwasababu wewe ni mahali pa juu sana palipoinuka pa Mungu.

1 Wakorintho 3:16-17

[16]Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?

[17]Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi.

3) Tabia

(Utakatifu)

Mungu ni mtakatifu, hivyo amechagua usafi zaidi ya uchafu, yeye ni Nuru si giza, ni mkamilifu si mwenye kasoro.

Hivyo tufahamu kuwa, tukimwendea yeye? kwa kupenda usafi? Lazima tutamwona.Lakini tukisema tunamtafuta na huku ni wachafu, hapo bado hatujamfikia Mahali pake pa juu anapoketi.

Isaya 57:15

[15]Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.

Sehemu nyingine anasema..

Zaburi 24:3-4

[3]Ni nani atakayepanda katika mlima wa BWANA? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake?

[4]Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, Wala hakuapa kwa hila.

Soma pia, Zab 15

4) Uweza:

(Imani)

Mungu si dhaifu, hivyo jambo lolote linaloonekana lina Nguvu, lililotukuka, lipitalo uwezo au ufahamu wa kibinadamu ni lake.

Ndio maana mtu anayemwendea Mungu kuomba yasiyowezekana kibinadamu, amemfikia Mungu.

Anaitwa Mungu wa miungu, Ibrahimu alimwamini Mungu kwa yasiyowezekana akawa rafiki wa Mungu, watu wote walio wa Imani ndio wanaomwona Mungu, Akiwatendea miujiza. Fahamu kuwa Mungu anavutiwa zaidi na yale yasiyowezekana Kibinadamu kuliko yale yanayowezekana..Jifunze kuishi kwa Imani, maana hapo ni mahali pake pa juu.. ondoa mashaka Ndani yako. Utamfikia Bwana hakika.

5) Ibada:

(Heshima)

Katika eneo la ibada, Mungu hafanyiwi Ibada ilimradi ibada. akiabudiwa ni lazima iwe katika Roho na kweli. Tunamtolea ibada ya juu sana..ikiwa ni sadaka Hatumpelekei kilema, bali ile ya juu zaidi, ikiwa ni sifa tunamsifu kwa nguvu zetu zote, kama Daudi,bila kujali kitu, kama ni kumtukuza Basi tunamtukuza sana na kumwadhimisha kwa viwango vyote.

Kwasababu yeye ndiye Mungu wetu astahiliye sifa zote.

Hivyo yatupasa maeneo yote hayo, tuyatambue, kisha tumwabudu kiufasaha Mahali pake pa Juu palipoinuka.

Zaburi 113:5-6

[5]Ni nani aliye mfano wa BWANA,  Mungu wetu aketiye juu;  [6]Anyenyekeaye kutazama,  Mbinguni na duniani?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

SAA INAKUJA NA SASA IPO.

Jina la Mwokozi wa pekee YESU KRISTO libarikiwe.

Je unajua tupo katika kipindi cha UFUFUO?.. Utauliza ufufuo gani?.. Turejee maandiko yafuatayo..

Yohana 5:25 “Amin, amin, nawaambia, SAA INAKUJA, NA SASA IPO, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai.

26 Maana kama vile Baba alivyo na uzima nafsini mwake, vivyo hivyo alimpa na Mwana kuwa na uzima nafsini mwake”.

Hapo Bwana YESU (Mkuu wa uzima) anasema “SAA INAKUJA” na “SASA IPO”  Je unaielewa vizuri hii kauli?

Anaposema “Saa inakuja” maana yake kipindi Fulani cha mbeleni kinachokuja…. Na anaposema “sasa ipo” maana yake ni kipindi alichopo yeye.

Sasa swali alikuwa ana maana gani kusema vile?

SAA INAKUJA: Hiki ni kipindi cha mwisho wa dunia, (wakati wa unyakuo wa kanisa) ambapo wafu waliokufa katika Kristo watatoka makaburini na kuvikwa miili ya utukufu na kisha kumlaki Bwana mawinguni.

1Wathesalonike 4:13 “Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.

14 Maana, ikiwa twaamini ya kwamba YESU ALIKUFA AKAFUFUKA, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, MUNGU ATAWALETA PAMOJA NAYE.

15 Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.

16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; NAO WALIOKUFA KATIKA KRISTO WATAFUFULIWA KWANZA.

17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele”.

Hiko ni kipindi cha Ufufuo wa siku za mwisho ambacho yoyote aliyekufa hapaswi kukikosa..kwani si wote watakaofufuliwa na kwenda kwenye unyakuo.

NA SASA IPO: Hiki ni kipindi ambacho Bwana YESU alikuwepo duniani, ambapo watu walikuwa wanafufuliwa roho zao zilizokufa katika dhambi..

Kitendo cha kumwamini YESU na kutubu na kubatizwa ni sawa na kufufuka kutoka katika WAFU, utauliza kwa namna gani?..

Turejee kidogo ile habari ya mwana mpotevu ambaye alitapanya mali kwa maisha ya uasherati na alipozingatia kurudi kwa baba yake kutubu, baba yake alimtafsiri kama aliyekuwa amekufa na sasa amefufuka.

Luka 15:29 “Akamjibu baba yake, akasema, Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wo wote, lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu

30 lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona.

31 Akamwambia, Mwanangu, wewe u pamoja nami sikuzote, na vyote nilivyo navyo ni vyako.

32 Tena, kufanya furaha na shangwe ilipasa, kwa kuwa huyu ndugu yako ALIKUWA AMEKUFA, NAYE AMEFUFUKA; alikuwa amepotea, naye ameonekana”.

Umeona? Si kwamba huyu kijana alikuwa amekufa kimwili, La! Bali kiroho, na alipotubu na kugeuka akahesabika kama aliyefufuka..

Je bado na wewe ni MFU na ilihali tunaishi katika SAA YA UFUFUO?.. Kumbuka usipofufuliwa sasa utu wa ndani kama huyu kijana mpotevu, hutaweza kuupata ufufuo wa siku ile ya Mwisho Bwana YESU atakaporudi, na siku hiyo imekaribia sana..

Maisha unayoishi ya dhambi ni uthibitisho wa MAUTI iliyopo ndani yako, na hiyo itaathiri hata mambo yako mengine uyafanyayo.

Fufuka leo kwa kumwamini BWANA YESU KRISTO, ili akuoshe dhambi zako kama maandiko yasemavyo..

Waefeso 5:14 “Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza.

15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;

16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.

17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana”.

Saa ya UFUFUO Ni SASA… Saa ya Ufufuo ni Sasa, Saa ya UFUFUO NI SASA!

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

 

Nini maana ya “SAA INAKUJA” na “SASA IPO” (Yohana 4:23).

YEYE AJAYE ATAKUJA WALA HATAKAWIA.

TUNAYE MWOMBEZI.

MFALME ANAKUJA.

NINI MAANA YA KUISHI KWA KUUKOMBOA WAKATI?.

Print this post

EPUKA KUJIFANYA HUJUI.

Jina la Mwokozi YESU libarikiwe karibu tujifunze biblia.

Tabia ya kujifanya hujui na ilihali unajua ni mbaya na hatari, kwani ni sawa na kumjaribu  MUNGU.. Kipo kisa kimoja kwenye biblia cha watu waliojifanya hawajui mbele ya Bwana YESU na matokeo yake hayakuwa mazuri.

Marko 11:27 “Wakafika Yerusalemu tena; hata alipokuwa akitembea hekaluni, walimwendea wakuu wa MAKUHANI, NA WAANDISHI, NA WAZEE,

28 wakamwambia, Ni kwa mamlaka gani unatenda mambo haya? Naye ni nani aliyekupa mamlaka hii uyatende haya?

29 Yesu akawaambia, Nitawauliza neno moja, nanyi mnijibu, kisha nitawaambia ni kwa mamlaka gani nayatenda haya.

30 UBATIZO WA YOHANA ULITOKA MBINGUNI, AU KWA WANADAMU? NIJIBUNI.

31 Wakasemezana wao kwa wao, wakisema, Kama tukisema, Ulitoka mbinguni, atasema, Mbona, basi, hamkumwamini?

32 Ila tukisema, Ulitoka kwa wanadamu, waliogopa watu; maana watu wote walimwona Yohana kuwa nabii halisi.

33 WAKAMJIBU YESU, WAKASEMA, HATUJUI. YESU AKAWAAMBIA, WALA MIMI SIWAAMBII NINYI NI KWA MAMLAKA GANI NAYATENDA HAYA”.

Watu hawa walikuwa wanajua kabisa ubatizo wa Yohana ulikuwa umetoka kwa MUNGU, lakini wakawa wanajifanya hawajui, na walipomwuliza Bwana YESU wakitegemea kuwa atawapa jibu la moja kwa moja, kinyume chake Bwana aliwajibu “WALA MIMI SIWAAMBII NINYI NI KWA MAMLAKA GANI NAYATENDA HAYA”.

Kwahiyo kumbe kuna maombi, au haja au dua au maulizo ambayo tunaweza kumpelekea Bwana YESU na tusipewe majibu yake!.

Ndio! kama maandiko yamesema wazi kuwa wizi ni dhambi, na tunalijua hilo hatuwezi tena kwenda tena na kumwuliza MUNGU kama kuiba ni dhambi au la! Kwani tayari tumesoma na tunajua… ukienda kumwuliza ni kumjaribu na hakuna majibu yoyote yatakayotoka..

Kama maandiko yamesema wazi kuwa uzinzi na uasherati ni dhambi,  na tunajua hilo, hatuwezi tena kwenda kurudia kumuuliza MUNGU atufunulie kwenye ndoto au tuisikie sauti yake ikisema kuwa ni dhambi…hapo itakuwa ni kumjaribu.

Kama dhamiri yako inakushuhudia kabisa kuwa hilo unalolitenda, au hiko unakokivaa au unakokishikilia ni dhambi, na maandiko yamekudhihirishia wazi, huwezi tena kwenda kumwuliza MUNGU akuhakikishie, unaweza usipate majibu yoyote, na ukaishia kusema MUNGU hasikii maombi.

Sio kwamba MUNGU hasikii maombi, ni kwamba MUNGU anataka usikie kwanza Neno lake na kulitii, lililoadikwa katika kitabu chake kitakatifu BIBLIA.

Biblia ni sauti ya MUNGU isiyo na marekebisho, na iliyo ya wazi kabisa..  ukitaka kuisikia sauti ya MUNGU ya wazi kabisa, soma Biblia, wala usiende kwa mchungaji, wala askofu, wala usisubiri uote ndoto, wewe soma Biblia tu!, utapata utamsikia MUNGU.

Mwisho acha kujifanya hujui kama kuna Jehanamu, acha kujifanya hujui kuwa kuvaa kidunia ni makosa, acha kujifanya hujui kwamba ibada za sanamu ni makosa, acha kujifanya hujui kuwa matambiko na makosa, acha kujifanya hujui kuwa kuishi na mke/mume wa mtu ni dhambi!.

Usimwulize Bwana MUNGU kama pombe unazouza ni mapenzi yake au la!, na ili hali unajua kabisa pombe ni makosa, hutapata majibu yoyote, zaidi unaweza ukaisikia sauti ya shetani kinyume chake.

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kama Kristo alizichukua dhambi zetu na kutusamehe kwanini kila siku tunatubu?.

KILA SILAHA ITAKAYOFANYIKA JUU YAKO HAITAFANIKIWA.

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MFUNGO.

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wathesalonike wa kwanza.

IFUATE KANUNI SAHIHI YA MUNGU

Print this post

Je mtu anaweza kubatizwa mara mbili?

Jibu:  Kulingana na biblia UBATIZO unapaswa ufanyike mara moja tu katika kipindi chote cha maisha ya mtu, ikiwa mtu huyo atakuwa ametimiza vigezo hivi viwili.

  1. KABLA YA KUBATIZWA AWE AMEELEWA MAANA YA UBATIZO NA KUTUBU:

Maana ya Ubatizo ni kuzika utu wa kale na kufufuka katika utu upya, hivyo ikiwa mtu ameelewa kuwa lengo la ubatizo ni kuacha maisha ya kale na kuanza maisha mapya katika KRISTO, basi hiko ni kigezo cha kwanza cha Uthabiti wa Ubatizo wake,

Warumi 6:3 “Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu TULIBATIZWA KATIKA MAUTI YAKE?

4 Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.

5 Kwa maana kama mlivyounganika naye katika mfano wa mauti yake, kadhalika mtaunganika kwa mfano wa kufufuka kwake;

6 MKIJUA NENO HILI, YA KUWA UTU WETU WA KALE ULISULIBISHWA PAMOJA NAYE, ILI MWILI WA DHAMBI UBATILIKE, TUSITUMIKIE DHAMBI TENA”.

Na kwa kigezo hiki, watoto hawabatizwi kwani wanakuwa bado hawajatambua maana ya maisha mapya katika KRISTO ni nini?, watoto wanawekewa mikono tu na sio kubatizwa….Kwahiyo kama mtu alibatizwa utotoni hana budi kubatizwa tena upya.

  2. NI AINA GANI YA UBATIZO ALIOBATIZWA.

Hiki ni kigezo cha Pili, kama mtu alibatizwa sawasawa na maandiko kwa maji mengi na kwa jina la Mwokozi YESU sawasawa na Mathayo 28:19 na Matendo 2:38 na si kwa maji machache na kwa majina ya watu wengine, basi huyo mtu hahitaji kubatizwa tena.

Lakini kama alibatizwa kwa ubatizo wa maji machache hata kama alishatubu dhambi zake, ni lazima abatizwe upya mara nyingine, kwasababu katika biblia hakuna mahali popote panaonyesha mtu yeyote amebatizwa kwa kunyunyiziwa, kwasababu maana tu yenyewe ya ubatizo ni kuzamisha/kuzika

Vile vile kama mtu alibatizwa kwa ubatizo wa Yohana, au wa mtu Fulani tofauti na  YESU hana budi kubatizwa upya.. Biblia inatuonyesha watu waliobatizwa kwa ubatizo wa Yohana kurudia ubatizo wao baada ya kukutana na injili ya ubatizo wa jina la YESU.

Matendo 19:3 “Akawauliza, Basi mlibatizwa kwa ubatizo gani? Wakasema, Kwa ubatizo wa Yohana.

4 Paulo akasema, Yohana alibatiza kwa ubatizo wa toba, akiwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja nyuma yake, yaani, Yesu  

5 WALIPOSIKIA HAYA WAKABATIZWA KWA JINA LA BWANA YESU.

6 Na Paulo, alipokwisha kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza kunena kwa lugha, na kutabiri.

7 Na jumla yao walipata wanaume kumi na wawili.”

Hapa tunaona hawa watu walibatizwa upya baada ya kusikia kuwa ubatizo sahihi ni wa Bwana YESU sio tena wa Yohana..

Kwahiyo na sisi hatuna budi kujihakika kama kweli tumebatizwa ubatizo sahihi, kama tumebatizwa ubatizo sahihi kulingana na vigezo hivyo hapo juu basi hatuna haja ya kubatizwa upya, Huo ubatizo unatosha, kinachobakia ni kuendelea kuishindania Imani kwa kujinga na ulimwengu na kutimiza wito ulioitiwa..

Lakini kama ubatizo wetu haujakamilishwa na Neno la MUNGU, hatuna budi kurudia ubatizo kwani si dhambi.

Na kumbuka matokeo ya ubatizo sahihi ni kumfanya mtu asimame imara katika IMANI, wengi waliobatizwa ubatizo sahihi baada ya toba kamili na uelewa kamili juu ya ubatizo ni ngumu kuishi tena maisha ya dhambi baada ya hapo, bali wanakuwa wanasimama maisha yao yote, kwani ubatizo unawaongezea Neema ya ziada ya kuweza kuishi bila kurudi rudi nyuma.

Mtu aliyebatizwa kwa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU, halafu akarudi tena kwenye maisha ya dhambi kama mwanzo, basi kuna shida katika KUAMINI KWAKE tangu mwanzo, huenda hakuelewa maana ya ubatizo kabla ya kubatizwa, na hivyo hakutubu kisawasawa, lakini kama angetubu kisawasawa na akabatizwa asingeweza kurudi tena alikotoka, hiyo ndio nguvu ya ubatizo.

Ikiwa bado hujabatizwa na unahitaji kubatizwa basi wasiliana nasi kwa namba hizi, 0789001312, tutakupa mwongozo sahihi wa kujua maana ya ubatizo na hatimaye kukubatiza ikiwa utakuwa maeneo karibu na tulipo, na ubatizo ni bure.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

AGIZO LA TOBA LINAENDANA NA UBATIZO!.

Ni sahihi kusema sikuitiwa kuhubiri ubatizo kama Paulo alivyosema (1Wakorintho 1:17)?.

Ubatizo wa moto ni upi?

Je ni lazima kupitia mafundisho ya muda mrefu kabla ya kubatizwa?

Print this post

JE UTAKATIFU NI MATENDO YA SHERIA?

Ipo elimu kwamba kuishi maisha ya utakatifu ni kuishi kwa sheria, na biblia inafundisha kuwa “hatuishi chini ya sheria bali tunaishi chini ya Neema” na tunahesabiwa haki bure kwa imani si kwa matendo.

Dhana hii inazidi kwenda mbali  kwa kusisitiza kuwa maisha ya utakatifu ni ngumu kuishi, na ni vigumu kuishi maisha hayo kwasababu ni  sawa na kujifunga kwa sheria.

Ndugu kama na wewe ni mmoja ya watu wanaoamini hivi kwamba…“utakatifu ni kifungo kigumu cha sheria”…bali leo soma ujumbe huu mpaka mwisho, utapata kuelewa jambo.

Hebu tafakari mfano huu:

》 Upo jikoni unaandaa chakula kwa bahati mbaya ukagusa sufuria ya moto, bila shaka kitakachofuata baada ya hapo, ni wewe kutoa mkono wako sehemu hiyo ya moto kwa haraka sana..

》Au labda umeketi mahali na ghafla ukaona kuna kitu/uchafu unakaribia macho yako, ni wazi kuwa utafumba macho ghafla na kwa kasi.

》Au linapotokea jambo la kushtusha na mapigo ya moyo kuongezeka kasi na mwili kutetemeka

Sasa matendo hayo yote ya kuondoa mkono kwa kasi kutoka kwenye sufuria yenye moto na kufumba macho ghafla pale hatari inapoyakaribia macho yako, na mapigo ya moyo kuongezeka kasi, na mwili kutetemeka huwezi kusema ni matendo ya sheria uliyojiwekea wewe yanayokuongoza…

La! bali ni sheria mwili uliojiwekea isiyohusisha hiari yako wala maamuzi yako, unajikuta tu unafanya hayo matendo bila kupenda au kuamua au hata kutafakaro… yaani ni matendo yanayotokana na mwitikio wa mwili kutokana na mazingira ya nje yanayoendelea.

Na Lengo ni kuulinda mwili wako usidhurike au usiendelee kudhurika..

Hali kadhalika matendo ya utakatifu ni mwitikio wa nje wa imani iliyopo ndani ya mtu na si matendo ya sheria..

Mtu aliyeipokea imani kweli kweli na kubatizwa na Roho Mtakatifu, anajikuta tu kuna mambo anayafanya pasipo hiari yake.

Anapokaribia mazingira ya dhambi amani inatoweka yenyewe pasipo yeye kuamua na hivyo anayaepuka hayo mazingira haraka sana.

Akisikia masengenyo ni kama vile mtu aliyeketi kwenye mazingira ya takataka na akapata kichefuchefu katika mazingira yale, kile kichefuchefu hakupanga wala kuamia kije, bali kinakuja chenyewe tu, ili utoke katika yale mazingira, ni kwa namna hiyo hiyo mazingira ya usengenyaji, au mazungumzo mabaya ni kichefuchefu kwa mtu aliyezaliwa mara ya pili kweli kweli.

Na hilo sio jambo linalompa shida sana kulitekeleza, bali linatoka tu lenyewe ndani, dunia nzima inaweza kumwona kama hayupo sawa kiakili au yupo kwenye utumwa mzito wa sheria alizojiwekea, lakini kumbe ni kinyume chake, mambo anayoyafanya yanabubujika yenyewe ndani yake na si sheria alizojiwekea.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba. Matendo ya utakatifu si sheria bali ni matendo yanayotendeka ndani ya mtu pasipo sheria, hata kama yanaonekana kama yamekaa kisheria, na hayo ni mambo ya rohoni yanayotambulika na watu wa rohoni kama maandiko yanavyosema..

1 Wakorintho 2:14 “Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.

15 Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu”.

Mtu kamwe hawezi kuuishi utakatifu kama hatakuwa na ujazo wa Roho Mtakatifu..

Na hiyo inahitaji Maamuzi mazito, yaani kumwamini Bwana YESU, kutubu dhambi na kubatizwa kwa maji mengi na kwa Roho Mtakatifu.

Kwahiyo kama utaamua kufanya mageuzi ya kweli kweli ya kuamua kumfuata YESU kwa kutubu dhambi kabisa na kujikana nafsi na kujitwika msalaba wako na kumfuata na kujazwa Roho Mtakatifu, nakuhakikishia suala la kuutimiza utakatifu kwako halitakuwa sheria bali mwitikio wa hiari.

Hutakuwa unakunywa pombe kwasababu imeandikwa usilewe, bali utakuwa hunywi pombe kwasababu hiyo kiu wala shauku itakuwa haipo ndani yako.

Hutazini kwasababu maandiko yamesema usizini, bali hutazini kwasababu hiyo kiu au msukumo utakuwa haupo ndani yako

Hutasengenya kwasababu maandiko yanasema usisengenye bali hutasengenya kwasababu mazingira hayo kwako ni kichefuchefu.n.k

Sababu kubwa uminayomfanya mtu asipokee hii nguvu ya kuishi maisha masafi?..ni jinsi alivyopokea na alivyoamini.

Kama mtu ameamini au ameaminishwa kuwa hawezi kuishi maisha ya utakatifu duniani, na pia ukienda kwa YESU hakuna haja ya kujitoa wote (kujikana nafsi)..hapo ndipo tatizo linapoanzia..

Utatakaje matunda ya mtu na bado humtaki yule mtu,..utatakaje matunda ya Roho Mtakatifu na bado humtaki YESU??..Unampa asilimia moja ya maisha yako na asilimia nyingine 99 ipo kwa ibilisi na ulimwengu!…hapo kwanini matendo ya utakatifu yasiwe sheria ngumu kwako??.

Jikane nafsi, (hilo jambo usilikwepe)..Dhamiria kumfuata YESU kwa moyo wako wote…. Ingia gharama kubwa kuacha vingi katika maisha yako, jitoe wote halafu uone nguvu itakayoingia ndani yako.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

CHAGUA UTAKATIFU MWAKA HUU.

IFAHAMU NGUVU YA MAOMBI (Sehemu ya pili)

Wabadili fedha ni watu gani kwenye biblia? (Mathayo 21:21)

MGAWANYIKO WA ISHARA ZA UJIO WA BWANA YESU KRISTO.

Kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi, maana yake nini? (Zab.18:26)

Print this post

TOFAUTI KATI MAASKOFU, MASHEMASI, WAZEE WA KANISA NI IPI?

Katika kanisa, Mungu aliweka huduma mbalimbali, karama mbalimbali, na utendaji kazi tofauti tofauti, ili kulikamilisha kanisa lake na kuupanda ufalme wake duniani kama alivyokusudia.

Sasa katika upande wa huduma, Mungu aliziweka huduma kuu tano, ambazo zenyewe zinasimama kama kuliongoza kanisa, kulikuza, kulichunga, ni kama nguzo za kanisa ambazo husimama wakati wote, Nao ni;

Mitume, manabii, wainjilisti, wachungaji na waalimu. (Waefeso 4:10-12)

Kwa urefu wa maelezo ya huduma hizo jinsi zinavyotenda kazi basi bofya hapa upitie >>> TOFAUTI YA MITUME, MANABII, WAINJILISTI, WACHUNGAJI NA WAALIMU NI IPI?

Lakini sambamba na hizo aliweka wengine katika kanisa, wanaoshirikiana na hawa watano (5).

Ambao ni  WAZEE WA KANISA, MAASKOFU na MASHEMASI

Tuangalie kazi ya kila mmoja;

1) WAZEE:

Tamaduni za kiyahudi tangu zamani walikuwa na desturi ya kuteuwa wazee (watu waliokomaa kiumri), wenye hekima na busara na uzoefu wa Kidini  kufanya maamuzi na Kutoa hukumu mbalimbali katikati ya jamii ya wayahudi Soma (Kutoka 3:16, Kumbukumbu 1:9-18)

Hata baadaye kanisa lilipokuja kuanza, nyakati za mitume, tunaona bado walirithi utaratibu huo katika nafasi za kiuongozi ndani ya kanisa. Isipokuwa haikuhitaji awe ni lazima mzee Kiumri, lakini ni lazima Awe amekomaa Kiroho.

Nafasi hii hasaa iliwahusu wanaume, Kwasababu katika nyaraka za mitume hatuoni mahali popote kama kuna mfano wa mwanamke aliyeteuliwa kuwa  mzee wa kanisa.

Ukisoma Tito 1:6, inaeleza sifa zao, anasema wazee wawe waume wa mke mmoja..

Tito 1:5-6

[5]Kwa sababu hii nalikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji kama vile nilivyokuamuru;

[6]ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii.

(Matendo 14:23)

Zingatia: Hii haiwafanyi wanawake wasiwe na kazi yoyote katika kanisa hapana, wanaweza kusimama kama huduma-kivuli ambazo zaweza Kuonekana kama za wazee wa kanisa, waalimu, mashemasi, kama wasaidizi wenye huduma hizo, lakini sio rasmi kwao. Mfano wa hawa kwenye biblia walikuwa ni akina Fibi, prisila,

KAZI ZA WAZEE WA KANISA:

1). Kulichunga kundi,

Matendo 20:28

Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.

(Soma pia 1Petro 5:1-4)

ii) Kufundisha vema watu. 

1 Timotheo 5:17

[17]Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha.

Tito 1:9

[9]akilishika lile neno la imani vile vile kama alivyofundishwa, apate kuweza kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima, na kuwashinda wenye kupinga.

iii) Kutatua migogoro ya kiimani ndani ya kanisa.

Utakumbuka wakati ule makanisa ya mataifa yalikuwa yakitaabishwa, na wayahudi juu ya kushika torati, hivyo  kukatokea mkanganyiko mkubwa, na kuwalazimu wawafuate wazee kule Yerusalemu ili walitatue tatizo hilo, na kama tunavyosoma baada ya hoja nyingi, walifikia hitimisho sahihi la Roho Mtakatifu.

Matendo 15:6 Mitume na wazee wakakusanyika wapate kulifikiri neno hilo.

7 Na baada ya hoja nyingi Petro akasimama, akawaambia, Ndugu zangu, ninyi mnajua ya kuwa tangu siku za kwanza Mungu alichagua miongoni mwenu ya kwamba Mataifa walisikie neno la Injili kwa kinywa changu, na kuliamini

iv) Kuwaombea wagonjwa.

Yakobo 5:14-15

[14]Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.

[15]Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.

2) MAASKOFU.

Maana ya Askofu ni mwangalizi.

Kazi yake kubwa ni kuliangalia kanisa,/ kulisimamia, mfano kusimamia malengo ya kikanisa, kulinda fundisho, na kusimamia uchungaji ulio bora.

Japokuwa mahali pengine maaskofu wanatajwa kama wazee wa kanisa. (Tito 1:5-9).

Lakini tofauti yao hasaa ni kwamba wazee wanayasimamia makanisa madogo madogo, lakini maaskofu ni waangalizi wa makanisa (yote/baadhi), Wazee wanaweza kuwa wengi, lakini maaskofu ni cheo, cha uangalizi hivyo aweza kuwa mmoja au wachache, wazee wanaweza kuwa na wajibu wa kufundisha, na kuchunga, lakini maaskofu hasaa katika kuongoza. Vilevile kwenye maandiko hatuoni mahali popote nafasi hii ikihusisha wanawake.

Sifa za maaskofu na wazee, wa kanisa zinafanana.

Sifa za mtu kuwa mzee wa kanisa. (Tito 1:5-9, 1Timotheo 3:1-7)

  1. Awe mtu asiyelaumika
  2. Awe Mume wa mke mmoja,
  3. Mwenye kiasi
  4. Mwenye busara
  5. Mtu wa utaratibu
  6. Mkaribishaji
  7. Ajuaye kufundisha
  8. Si mtu wa kuzoelea ulevi
  9. Si mpiga watu
  10. Awe mpole
  11. Si mtu wa kujadiliana
  12. Asiwe mwenye kupenda fedha
  13. Awezaye kuisimamia nyumba yake vema
  14. Asiwe mwongofu mpya.

3) MASHEMASI.

Mashemasi ni mtumishi wa kanisa.  Huduma hii ilitokea katika kanisa kwa mara ya kwanza, mitume walipokuwa wanahudumu na kuona kuwa baadhi ya mapungufu kwamba wajane wanasahaulika katika huduma ya kila siku, ndipo ikalazimika wateue watu saba, ndani ya kanisa watakaoweza kusimamia mambo yote ya kimahitaji ya kundi.  (Matendo 6:1-7), mmojawapo alikuwa ni Stefano.

Kazi za mashemasi:

i) Kulihudumia kundi katika masuala ya mahitaji ya mwilini ya kundi:

Hususani kwa maskini, wajane, wenye mahitaji,  mayatima.

ii) Kuongoza kwa mifano:

Lazima wawe kipaumbele kitabia, uaminifu, na nidhamu Na kuonyesha roho ya kiutumishi

iii) Kusimamia shughuli za kikanisa:

Ujenzi, taratibu za kiibada na mikutano, kusimamia hazina na mali za kanisa.

Sifa za mtu kuwa shemasi:

Zinatajwa kwenye 1Timotheo 3:8

1Timotheo 3:8 Vivyo hivyo mashemasi na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana,si watu wanaotamani fedha ya aibu.

9 wakiishika siri ya imani katika dhamiri safi. 10 Hawa pia na wajaribiwe kwanza; baadaye waitende kazi ya shemasi, wakiisha kuonekana kuwa hawana hatia.

11 Vivyo hivyo wake zao na wawe wastahivu; si wasingiziaji; watu wa kiasi, waaminifu katika mambo yote.

12 Mashemasi na wawe waume wa mke mmoja, wakiwasimamia watoto wao vizuri, na nyumba zao.

13 Kwa maana watendao vema kazi ya shemasi hujipatia daraja nzuri, na ujasiri mwingi katika imani iliyo katika Kristo Yesu

Hivyo wazee, maaskofu na mashemasi, ni nguzo muhimu za kulifanya kanisa kusimama, katika nidhamu ya kitabia na kimapokeo, pamoja na kihuduma.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ZIFAHAMU KARAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA UTENDAJI KAZI WAKE.

Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?

JINSI BWANA ALIVYOWACHAGUA MITUME WAKE.

Print this post

IFAHAMU NGUVU YA MAOMBI (Sehemu ya pili)

Maombi ya shabaha kwaajili ya Kazi/kibarua/shughuli/biashara/elimu.


UTANGULIZI: Ni muhimu kujua hili: lengo kuu au kiini cha Wokovu ulioletwa na BWANA YESU KRISTO sio sisi tuwe matajiri au tupate mafanikio ya huu ulimwengu!.

Mafanikio ya dunia hii ni moja ya faida za mwisho mwisho kabisa za kusudi la msalaba wa Bwana YESU kwasababuwalikuwepomatajiri kabla ya Bwana YESU kuja duniani, hivyo KRISTO asingeweza kuja kutegua mtego aukutatua tatizo ambalo lilishatatuliwa huko nyuma.

Ingekuwa lengo lake ni ili tufanikiwe tuwe matajiri, angetuambia tu tusikilize hekima za Sulemani na tungefanikiwa, hakukuwa na haja ya kuja kumwaga damu yake.

Lakini suala la ondoleo la dhambi hilo halikuwahi kufanyika huko nyuma, hakuna aliyewahi kuondolewa dhambi, kwani dhambi zilikuwa zinafunikwa tu! (Soma Waebrani 10:3-4)..

Sasa hiko ambacho kilishindikana kutendeka huko nyuma (katika Agano la kale) ndicho kilichokuwa cha kwanza na cha msingi kilichomleta BWANA YESU duniani, na kitu hiko si kingine zaidi ya ONDOLEO LA DHAMBI.…kiasi kwamba mtu akikosa ondoleo la dhambi hata awe na vitu vyote ulimwenguni bado anayo hasara kubwa soma (Mathayo 16:26).

Kwahiyo ni muhimu kujua msingi huu, ili tunapokwenda kujifunza juu ya MAOMBI JUU YA KAZI au BIASHARA, Usiweke moyo wako wote huko!.. Yatumie tu maarifa haya kama sehemu ya maisha, lakini jali zaidi hatima ya roho yako, kupitia damu ya YESU na UTAKATIFU.

Sasa tukirudi katika kiini cha somo!.. Ikiwa unafanya kazi za mikono, labda tuseme biashara, tumia kanuni hii ya Maombi kupata FAIDA YA KILE UNACHOKIFANYA!!.

Badala ya kuombea bidhaa zako, kama sabuni unazouza, au dawa unazouza, au kingine chochote kwamba kiwe na mvuto, kuanzia leo punguza kuomba maombi ya namna hiyo, badala yake omba maombi yafuatayo.

– Kila mteja anayekuja kwako mwombe neema ya Wokovu, ikiwa bado hajampokea YESU, maombi ya namna hiyo yanamtoa yule mtu kutoka katika vifungo vya ibilisi na hatimaye kumfungua kabisa, na anapofunguliwa aweza kuwa mteja wako wa ajabu sana, au akawaleta na wengine wengi mahali ulipo.

– Ikiwa tayari ameshampokea YESU mwombee azidi kusimama katika imani, na mwombee akawe Nuru kwa wengine wengi, ombea na familia yake kama unaijua, hiyo ndio njia bora ya kuombea kazi yako au biashara yako..

– Unafanya biashara ya chakula, na wateja wako ni watu wa kidunia, badala ya kuombea madishi na chakula unachokipika kwamba wakipende, hebu waombee wampende YESU, halafu uone kama hiko chakula chako hawatakipenda, zaidi ya vyakula vya wengine wote.

– Pale ofisini acha kuombea uso wako kwamba upate kibali, sawa waweza kuomba hivyo, lakini isizidi sana kiasi kwamba hujui kitu kingine cha kuomba zaidi ya hicho, badala yake anza kuomba watu wa ofisini kwako wamjue MUNGU, wakimjua MUNGU wewe utapata kibali tu!, wala hutatumia nguvu nyingi.

– Pale shuleni acha kuombea walimu wakupende, hebu waombee wamjue YESU na kumpenda, halafu uone kama hawatakupenda na wewe.

– Unauza bidhaa, waombee wateja wako wamjue YESU na kumpenda zaidi ya bidhaa zako, halafu uone matokeo.

Ukitaka kufunga kwaajili ya biashara yako!, Funga kwa maombi ya kuwaombea wateja wako wokovu na Neema zaidi, kama unayo list, anza mmoja baada ya mwingine, wapatanishe na KRISTO hivyo uone kama KRISTO pia hatakupatanisha nao, utaona kazi zako zinaenda, shule yako inaenda, biashara yako inaenda, kazi yako inaenda.

Lakini ukijikita tu kuziombea bidhaa kama vile waganga wanavyotoa dawa za kwaajili ya biashara, matokeo yake yatakuwa ni madogo sana.

Hivyo OMBA lakini omba kwa shabaha/target.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

IFAHAMU NGUVU YA MAOMBI:

MWONGOZO WA MAOMBI YA FAMILIA

KWANINI MUNGU HAJIBU MAOMBI?

Mistari ya biblia kuhusu maombi.

MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.

Print this post

Kwanini Mungu alimfunga tumbo Raheli, ilihali Yakobo alimtesekea miaka 14?

Jibu: Hakuna kosa lolote Raheli alilolifanya, lililomfanya afungwe tumbo asizae.. Lakini tukisoma maandiko twaweza kuona sababu kama mbili zilizopelekea yeye kufungwa tumbo na MUNGU mwenyewe.

 1. KUMNYENYEKEZA RAHELI na KUMTIA NGUVU LEA.

Tunasoma kuwa Lea ndiye aliyekuwa wa kwanza kuzaliwa, na Yakobo alimpenda zaidi Raheli kuliko Lea, (na jambo hilo lilikuwa wazi linaonekana) kwahiyo labda ingetokea Yakobo aliyebeba ahadi za MUNGU kumuoa Raheli, na tena akazaa naye mtoto wa ahadi, huenda jambo hilo lingemfanya Raheli kujivuna/kujigamba mbele ya Lea dada yake, na hivyo Lea angekuwa duni/mnyonge mbele ya mdogo wake, kwahiyo MUNGU akamfunga tumbo.

Mwanzo 29:28 “Yakobo akafanya hivi, akatimiza siku zake saba. Naye akampa Raheli binti yake kuwa mkewe.

29 Labani akampa binti yake Raheli mjakazi wake Bilha, awe mjakazi wake.

30 Akaingia kwa Raheli naye, AKAMPENDA RAHELI KULIKO LEA, akatumika kwa ajili yake miaka saba mingine

31 Bwana akaona ya kwamba Lea hakupendwa, naye akafungua tumbo lake; bali Raheli alikuwa hazai.

32 Lea akapata mimba akazaa mwana, akampa jina lake, Reubeni, maana alisema, Kwa kuwa Bwana ameona teso langu; sasa mume wangu atanipenda.

33 Akapata mimba tena akazaa mwana, akasema, Kwa kuwa Bwana amesikia ya kwamba mimi sikupendwa, amenipa na huyu; akamwita jina lake Simeoni.

34 Akapata mimba tena, akazaa mwana, akasema, Basi wakati huu mume wangu ataungana nami, kwa sababu nimemzalia wana watatu. Kwa hiyo akamwita jina lake Lawi.

35 Akapata mimba tena, akazaa mwana. Akasema, Mara hii nitamsifu Bwana; kwa hiyo akamwita jina lake Yuda; akaacha kuzaa”.

2. KUKITHAMINISHA KITAKACHOZALIWA BAADAYE.

Hii ni sababu ya pili ya Raheli kufungwa tumbo: Tunasoma ijapokuwa Raheli alifungwa tumbo muda mrefu, lakini ulifika wakati akazaa, na mwana aliyemzaa alikuwa wa tofauti na wale wengine 10 waliotangulia, kwani ndiye aliyekuwa YUSUFU, ambaye alikuja kuwa Mkuu zaidi ya ndugu zake wote, na tena Mkuu juu ya nchi yote ya Misri, baada ya Farao.

Ikifunua kuwa si kila kinachochelewa kina laana!.. Vingi vinavyochelewa ni kwasababu ya Utukufu wake, hivyo usimwone mtu kachelewa kupata mimba ukamdharau!.. Hujui atakayekuja kumzaa ni nani!..
Vile vile usihuzunike unapoona unachelewa kupata mtoto, kwani vizuri na vya thamani, vina gharama, na gharama yenyewe yaweza kuwa fedheha, matusi, kejeli na masimango.. Lakini vinavyokuja baada ya gharama hizo vinakuwa ni vizuri, endapo tu utazidi kusimama katika imani, haijalishi muda, vitatokea tu!.

Wagalatia 4:27 “Kwa maana imeandikwa, Furahi, wewe uliye tasa, usiyezaa; Paza sauti, ulie, wewe usiye na utungu; Maana watoto wake aliyeachwa pekee ni wengi Kuliko wa huyo aliye na mume”.
Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini Raheli aliiba miungu ya Baba yake, (Labani) Mwanzo 31:19.

Kwanini Labani aseme Yakobo ni Mfupa wake na nyama yake?(Mwanzo 29:14)

Raheli aliwalilia vipi watoto wake?

Zeri ya Gileadi ni nini?

Tunguja ni nini katika biblia? (Mwanzo 30:14).

Print this post

“Akaiona imefagiwa na kupambwa” Maana yake nini (Luka 11:26).

Swali: Bwana YESU alisema pepo anapomtoka mtu na baadaye akirudi na kukuta nyumba yake imefagiliwa na kupambwa huenda kuchukua pepo wengine saba,.. maaa yake nini kusafishwa na kupambwa?.. je mapepo wanapenda sehemu safi?


Jibu: Awali ya yote tuisome mistari hiyo.

Luka 11:24 “Pepo mchafu amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika; asipoona, husema,

25 Nitairudia nyumba yangu niliyotoka.

26 Hata afikapo, akaiona imefagiwa na kupambwa, ndipo huenda akachukua pepo wengine saba, walio waovu kuliko yeye mwenyewe, wakaingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza”.

Sasa kabla ya kujua nini maana ya “kufagia na kupambwa” hebu tuelewe kwanza maana ya nyumba kiroho..

Maandiko yanasema Miili yetu ni Hekalu la Roho Mtakatifu..

1 Wakorintho 6.19 “Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;

20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu”.

Soma pia 1Wakorintho 3:16 utaona jambo hilo hilo..

Sasa kama miili yetu imekusudiwa iwe Hekalu/nyumba ya Roho Mtakatifu, maana yake ni kwamba isipokaliwa na Roho Mtakatifu basi itakaliwa na roho chafu za mapepo, maana yake badala ya mwili kuwa Nyumba ya Roho Mtakatifu, sasa inakuwa ni nyumba ya mapepo.

Hivyo mpaka hapo tumeshaelewa kuwa Nyumba inayozungumziwa hapo katika Luka 11:25-26, si nyingine zaidi ya miili yetu.

Sasa swali la pili: Nini maana ya kupambwa na kufagiliwa.

Hebu tena tutumie maandiko tujue mapambo ya nyumba ya Mungu (yaani miili yetu) ni yapi, na mapambo ya mapepo ni yapi.

1Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, KUSIWE KUJIPAMBA KWA NJE, YAANI KUSUKA NYWELE; NA KUJITIA DHAHABU NA KUVALIA MAVAZI;

4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao”.

Angalia mstari wa tatu (3) anasema.. Kujipamba kwenu KUSIWE!, Zingatia hilo neno KUSIWE!!.. Maana yake ni kwamba mapambo yake ni kwamba mapambo yafuatayo si ya ki Mungu bali ni ya Ibilisi, ndio maana anasema hapo KUSIWE!.. Sasa hebu tuendelee tuangalie hayo mapambo..

…”Kujipamba kwenu, KUSIWE KUJIPAMBA KWA NJE, YAANI KUSUKA NYWELE; NA KUJITIA DHAHABU NA KUVALIA MAVAZI..”

Oo kumbe! kuweka wigi, kuvalia mavazi (ya kikahaba), na kuvaa dhahabu masikioni na shingoni na vikuku miguuni na mikononi ni mapambo ya mapepo, na tena tumeshaona kuwa “nyumba” tafsiri yake kiroho ni “miili yetu”, hivyo tunapoweka hereni masikioni, wigi kichwani, cheni shingoni na vikuku miguuni, tafsiri yake ni kwamba nyumba zetu (yaani miili yetu) tumeipambwa kwa mapambo ya kipepo, ambayo yale mapepo yakiona yanafurahi na kwenda kutafuta pepo wengine saba, na kurudi kumwingia mtu.. Hii ni ajabu sana!.

Na ndio maana wengi (wanaume na wanawake) wanaopamba miili yao na kuvaa kikahaba wanakuwa wanasumbuliwa na mapepo na ndoto mbaya!, kwanini?..kwasababu miili yao ni nyumba iliyofagiliwa na kupambwa..

Sasa utauliza kufagiliwa ni kufanya nini?…Kufagiliwa ni maandalizi ya mapambo!..Maandalizi yote ya kiroho na kimwili kabla ya mtu kujitia mapambo ya nje ni “kufagia”..

Lakini hebu tuangalie mapambo ya ki MUNGU ni yapi!.. Tuendelee na mistari ile..

“Kujipamba kwenu, KUSIWE KUJIPAMBA KWA NJE, YAANI KUSUKA NYWELE; NA KUJITIA DHAHABU NA KUVALIA MAVAZI;

4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu”.

Bali anasema mapambo yetu yawe Utu wa moyoni, yaani Roho ya Upole, na utulivu (kwa ufupi utakatifu).
Je! mama, dada, au kaka ni mapambo gani unayo?..ya nje au ya ndani??.. ni kweli utaonekana wa kisasa, unayekwenda na wakati, lakini fahamu kuwa mapambo hayo ndio mapepo wanayoyaangalia.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10 atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Print this post

VUNJA MADHABAHU, ANGUSHA NGUZO, KATA ASHERA NA CHOMA SANAMU.

Haya ni mambo manne yanayopalilia matatizo kuanzia ngazi ya kifamilia mpaka ya kitaifa!. (Madhabahu, Nguzo, Ashera na Sanamu).


Kumbukumbu 7:5-6 “Lakini watendeni hivi; zivunjeni madhabahu zao zibomosheni nguzo zao, yakateni maashera yao, ziteketezeni kwa moto sanamu zao za kuchonga.

6 Kwa maana wewe u taifa takatifu kwa BWANA, Mungu wako; BWANA Mungu wako, amekuchagua kuwa watu wake hasa, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa nchi”

Labda utauliza mambo haya ni mambo gani kwa undani wake na yanaathiri vipi maisha.

   1. Madhabahu:

Madhabahu ni mahali popote panapotolewa dhabihu (sadaka).

Sadaka ina nguvu, ndio maana hakuna mganga anayetoa huduma bila sadaka,

Sasa si kwamba sadaka anahitaji tu  kwaajili ya mahitaji yake..La! bali anajua uchawi wake hautafanya kazi ipasavyo pasipo sadaka, kwahiyo madhabahu ni mahali mahususi kwa sadaka..

Katika biblia BWANA MUNGU aliwaagiza wana wa Israeli wazivunje madhabahu za wakaanani..

Na zilikuwa ni nyingi na za aina tofauti tofauti…na pasipo kuchagua waliambiwa wazivunje zotewasibakishe hata moja, kwani zitakuwa ni chanzo cha matatizo..

Ikimaanisha kuwa madhabu za mashetani ni za kuvunja si za kuziacha, kwani zinapeleka harufu mbaya mbele za MUNGU, na hivyo kuleta matatizo mengi…

Ikiwa kuna mahali ipo madhabahu wanapotolea sadaka karibu nawe, na hiyo madhabahu inakuhusu kwa namna moja au nyingine (kimila), ivunje bila kuogopa!..kama alivyofanya Gideoni, usiiache kwani yaweza kukuletea matatizo.

     2. NGUZO

Nguzo ni miimo ya Mahekalu ya ibada, yaweza kuwa Hekalu la MUNGU (soma 1Wafalme 7:21 na Mwanzo 28:22),  au yaweza kuwa hekalu la mashetani (Soma 2Wafalme 10:26-27).

Maana yake mahali popote penye msingi wa hekalu la miungu ni lazima pabomoshwe.

   3. ASHERA.

Ashera ni miti na maua yaliyokuwa yanazunguka mahekalu ya miungu, ambapo mimea hiyo iliaminika na kuabudiwa kama sehemu ya miungu.

Bwana aliwaambia wana wa Israeli wakate-kate maashera yote lisibaki hata moja (Kutoka 32:12-14).

Hali kadhalika yapo maashera hata sasa, utakuta upo mti fulani unaaminika kama ni wa kiungu na watu wanaenda kufanya matambiko hapo (hiyo ni ashera), ni ya kukata, wengine si miti bali maua tu…

Ondoa maashera katika nyumba yako, ondoa katika nyua yako na uzio wako kwani yaweza kuwa chanzo cha matatizo mengi.

   4. SANAMU.

Sanamu ni kitu chenye umbile la mtu kinachowekwa katika mahekalu na kuabudiwa.

Hizi nazo Bwana aliagiza zichomwe moto,

Sasa swali linakuja, vipi kama Madhabahu hizi, na ashera, na nguzo na sanamu zipo mbali?.

Kama zipo mbali na upeo wa kuzifikia, tunazo silaha zinazosafiri masafa marefu zaidi ya silaha zote zilizowahi kutengenezwa na mwanadamu au zitakazokuja kutengenezwa.

Silaha hiyo ni Maombi.

Maana yake katika maombi Unazivunja madhabahu kwa Imani, unaangusha Nguzo kwa imani, unakata maashera kwa imani, na unazichoma moto hizo sanamu kwa imani kupitia jina la YESU.

Na kwa jinsi utakavyotamka, zitateketea kule zilipo kwa namna hiyo hiyo, lakini usiingie kwenye maombi ya vita kama wewe si askari mwenye silaha hizi za Waefeso 6:10-15.(utajitafutia matatizo zaidi).

Pia usiache kuzibomoa kwa mikono yako kama zipo mbele ya upeo wa macho yako. (Upo unaziona sio tu kuombea, bali kuzimoa kwa mikono kabisa).

Ukifanya hivyo utakuwa umeusafisha uwanda, hakuna laana juu ya mahali ulipo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post