Category Archive Mithali

Maana ya Mithali 19:15 ‘Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito;

Fahamu Maana ya Mithali 19:15 “Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa”.


Mara nyingi Sulemani kwa hekima ya Roho aliongozwa kuona uhusiano uliopo kati ya uvivu na umaskini. Kama tu kinyume chake, sehemu nyingine alivyoweka uhusiano kati ya bidii na utajiri(Mithali 10:4). Vivyo hivyo uvivu na umaskini havipishani.

Na kama anavyosema hapo, uvivu humpeleka mtu katika usingizi, lakini sio usingizi tu bali ule mzito, Kwasababu gani? Ni kwasababu mwili haupo katika hali ya kujishughulisha, na hivyo utalala tu, na Bado utaendelea kulala siku baada ya siku.. Na matokeo yake kutokuzalisha chochote kinachoonekana, hatimaye, umaskini unaingia.

Hivyo mstari huo unalenga Nyanja mbili. Ya kwanza ni ule uvivu wa mwilini, na ya pili ni ule uvivu wa rohoni.

Uvivu wa mwilini:

Mungu katuumbia kufanya kazi, watu wote (ikiwemo watakatifu). Maana yake ni kuwa ikiwa huna huduma yoyote ya madhabahuni Bwana amekuitia, ambayo inakufanya utumike muda wote hapo. Ni sharti ufanye kazi. Mtume Paulo alilionya kanisa juu ya watu ambao hawafanyi kazi kwamba ni sharti wajishughulishe ili wapate na kitu cha kuwagawia na wengine (2Wathesalonike 3:10)

Uvuvu wa rohoni:

Lakini pia Uvuvi wa rohoni. Mtakatifu anapokuwa mvivu, kusoma Neno, yaani muda wa Neno anakwenda kutazama filamu, anakwenda kijiweni kucheza drafti,.Anakuwa  mvivu kuomba, Unapofika huo muda tu anaona usingizi ni bora kuliko kuomba,.Au Mtakatifu hataki kushuhudia habari za Kristo kwa wengine, anasema jua kali. Sasa mtu huyo anajiandaa kuwa maskini kiroho. Yaani atakuwa katika wokovu usiokuwa na matunda, ukuaji wake wa kiroho utakuwa hafifu, Neema ya Mungu haitatenda kazi kwa wingi juu yake, na hivyo atakosa mema mengi ya Mungu katika safari yake wa wokovu hapa duniani.

Uvuvi wowote, una hasara, kwahiyo tuuweke katika orodha ya maadui zetu wa imani.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

Amwimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Mtu asiye na akili ni nani kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 19:11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake.

Fahamu Maana ya;

Mithali 19:11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake; Nayo ni fahari yake kusamehe makosa.


Mstari huo unatufundisha mtu aliyejaa  “Busara” moyoni ni mtu wa namna gani..

Anaeleza ni Yule ambaye anaouwezo wa kughahiri hasira yake, na pia kupenda kusemehe makosa. Ambayo ndio sifa ya Mungu, Aliyonayo, soma;

Kutoka 34:6 Bwana akapita mbele yake, akatangaza, Bwana, Bwana, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli;  7 mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne.

Hivyo na sisi hatuna budi kutokuwa watu wa kukasirika haraka, mpaka ikaleta athari nje, kwamfano umeumizwa na mke/mume wako, tunapaswa tujifunze kuachilia mara moja, lakini pia kusamehe, sio kuweka kinyongo, au uchungu moyoni. Au mtu amefanya kosa la kukuudhi ambalo anastahili adhabu, si vema kuwa wepesi wa kuadhibu bali kuahirisha hasira hizo kwasababu Mungu naye anatusamehe makosa yetu, hatuadhibu kila kosa.

Bwana alisema kusamehe kwetu hakupaswi kuwe na ukomo, alitumia lugha ya hata ‘saba mara sabini’ kwa siku(Mathayo 18:22). Kuonyesha kuwa kusamehe kwetu kunapaswa kuwe endelevu. Ili  tufikie hatua ya Kuona ‘fahari’ katika uwezo wa kusamehe, zaidi ya kuona fahari katika uwezo wa ‘kupata vitu’. Yaani tuhesabu ni watu wangapi tumewasamehe, hapo ndio iwe furaha yetu. Na kwamba tuipime busara yetu kwa kiwango cha kuiharisha hasira zaidi ya uwezo wa ‘kuwa na maneno mengi ya hekima’.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

NIFANYE NINI NIWEZE KUDHIBITI HASIRA?

Mungu anatufundisha kusamehe mara saba sabini, ila Kwanini yeye hakumsamehe Adamu alipoasi?

TAFUTA HEKIMA, MAARIFA, UFAHAMU NA BUSARA.

BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.

KWANINI TUWE WENYE BUSARA KAMA NYOKA?

SIKU YA HASIRA YA BWANA.

Wivu ni nini na kuna aina ngapi za Wivu?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 24:11 Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe?

SWALI: Nini maana ya Mithali 24:11 Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe; Nao walio tayari kuchinjwa uwaopoe.

JIBU:  Mstari huu una maana mbili,

Mana ya kwanza ni uhai kama ‘uhai’ alionao mwanadamu yoyote,

Maana yake ni kuwa uonapo, mtu asiyekuwa na hatia, amepangiwa njama za kuuliwa, au ndio anakaribia kufa, na wewe unaowezo wa kumsaidia huna budi kufanya hivyo wala usijifanye kama hiyo sio biashara yako.

Ni mfano wa Yule mtu aliyevamiwa na wanyang’anyi ambaye Bwana Yesu alimtolea mfano, akasema mlawi alimpomwona akapita kando, kuhani naye alipomwona akapita kando, lakini Yule msamaria akamuhurumia, akamtibu, akaokoa uhai wake. Na Yesu akasema huo ndio Upendo.(Luka 10:25-37)

Ni sawa na wakati ule Paulo amepangiwa njama na wayahudi wamvizie auawe, lakini mjomba wake alipogundua alikwenda kumjuza akida wa kikosi (Matendo 23:12-22). Huyo amemwopoa aliyekaribu na kuchinjwa.

Ni sawa na Mordekai alichofanya kwa Mfalme, Ahusuero, wale watu walipopanga njama ya kumuua akaenda kuwasemelea (Esta 6:1-12),. Ni sawa na Yonathani, alivyomtunza Daudi dhidi ya upanga wa baba yake Sauli ili asiuliwe. Hivyo hawa wote, walilitambua andiko hili, na wala hawakuogopa kutoa siri, za wale waliokusudia mabaya juu ya maisha ya wengine.

Hata leo, vifo vingi vya kikatili, vingeweza kuzuilika kwa sehemu kubwa, endapo baadhi ya wanaojua matukio hayo wangetoa taarifa mapema. Kwamfano utaona mtu anawekewa sumu kwenye chakula, wewe unayejua, ni wajibu wako kutoboa siri hiyo, ili uutunze uhai wa mtu. Utaona mwizi anapigwa, huna budi kuripoti polisi mapema maadamu jambo hilo lipo ndani ya uwezo wako, ili askari waje kumkamata wampe wao adhabu stahiki, lakini ukipita ukasema hainihusu, atachomwa moto. Lakini kumbuka uhai unathamani, hata wa mtu aliye mbaya, unathamani nyingi.

Lakini ukisema hainuhusu, Utakuwa unajipunguzia pia rehema nyingi kwa Mungu,  ndio maana mstari unaofuata unasema;

Mithali 24:11 “Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe; Nao walio tayari kuchinjwa uwaopoe.  12 Ukisema, Sisi hatukujua hayo; Je! Yeye aipimaye mioyo siye afahamuye? Naye ailindaye nafsi yako siye ajuaye? Je! Hatamlipa kila mtu sawasawa na kazi yake?”

Hivyo penda uhai, pia tunza uhai wa watu, popote pale uonapo unahatarishwa. Usiwe mzito kusaidia.

Lakini  maana ya pili ya mstari huu  ni ule Uhai wa rohoni.

Wapo watu ambao ibilisi, anakaribia kuwameza, na ukiwaacha ndani ya kipindi kifupi hakika wataangamia kabisa kiroho. Wengine wanakaribia kufa kwasababu ya huzuni mioyoni mwao, kukata tamaa, kwasababu ya dhiki na magonjwa, wengine wanakaribia kuzama katika ushirikina, wengine kwenye imani potofu ambazo zinakwenda kuwaua roho zao n.k. Hivyo makundi kama haya, unapoyaona, mwelekeo wao wewe kama mkristo uliyesimama huna budi kuwasaidia ili waokoke, wasipotelee katika mauti ya roho zao, na kwenye minaso ya adui mfano wa Yuda. Wala usisime hiyo sio shughuli yangu.

Yuda 1:22  “Wahurumieni wengine walio na shaka, 23  na wengine waokoeni kwa kuwanyakua katika moto; na wengine wahurumieni kwa hofu, mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili.

Hivyo tutunze Uhai, wa mwili na Roho za watu wa Mungu, naye Bwana atatunza na wetu.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

“Kinga kilichotolewa motoni “Kinafunua nini kibiblia?

Biblia inamaanisha nini inaposema “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake”?

Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE

Rudi nyumbani

Print this post

Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali 14:23 “Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu”


JIBU: Kitabu cha Mithali na Mhubiri ni vitabu vilivyobeba mafunzo mengi sio tu yale ya kiroho bali pia hata ya maisha ya kawaida. Mstari huo unaelezea uzito wa kitu kinachotendewa kazi zaidi ya kile kinachozungumzwa tu. Kwamfano hapo anaanza kwa kusema “katika KILA KAZI mna faida”.. Maana yake ni kuwa katika kazi yoyote (iliyonjema), inafaida nyuma yake,. Iwe ni ya kudharaulika au yenye heshima, iwe ni ngumu iwe ni rahisi, iwe ni ya kipato kikubwa au kidogo, maadamu kazi fulani inatendeka ni lazima faida tu itaonekana nyuma yake.

Lakini mtu akiwa ni wa mipango mikubwa, mikakati mingi, akili nyingi za kubuni namna ya kutenda kitu Fulani, vikao vingi,  halafu hakitendei kazi, Bwana anasema, badala ya faida kinyume chake ni hasara tu atapata..

Vivyo hivyo na katika roho. Bwana anataka tuwe watendaji wa Neno lake, Sio kusikia tu au kuomba tu peke yake. Unaweza ukaomba usiku kucha lakini kama sio mtendaji wa Neno lake uliombalo, ni unapoteza nguvu tu.

Kwamfano unaomba Bwana akusaidie uushinde uasherati, lakini bado unashikamana na vichocheo vyake vyote, una picha chafu kwenye simu yako, kinywa chako kinazungumza mambo ya kizinzi na vijana wenzako, unachati na watu wa jinsia tofauti muda wote, unatazama tamthilia zenye maudhui hayo, unasikiliza miziki ya kidunia, unaishi na boyfriend/girlfriend. Unategemea vipi tamaa zisikutawale? Utaomba usiku kucha na hutaona matokeo yoyote, kwasababu hukitendei kazi kile unachokiomba.

Bwana alisema kama vile mwili bila roho umekufa, vivyo hivyo imani bila matendo imekufa ndani yake.(Yakobo 2:17). Kukitendea kazi kile kimoja ukiombacho, kina nguvu sana kuliko maneno elfu unayoweza kumwomba Mungu mwaka mzima.

Yakobo 1:22  “Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu. 23  Kwa sababu mtu akiwa ni msikiaji wa neno tu, wala si mtendaji, mtu huyo ni kama mtu anayejiangalia uso wake katika kioo. 24  Maana hujiangalia, kisha huenda zake, mara akasahau jinsi alivyo”.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni”.

Nini maana ya huu mstari? “Yeye mwenyewe ataokolewa lakini ni kama kwa moto”

Mithali 14:4 ‘Zizi ni safi ambapo hapana ngombe;

Marijani ni nini katika biblia(Ayubu 28:18,Mithali 8:11)?

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

BWANA UNIJULISHE MWISHO WANGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Nyongeza ya majina ya watu katika biblia

Tunaona kuna baadhi ya watu ambao majina yao yameongezwa vionjo kwa mbele, kwa mfano Simoni Petro, Yuda Iskariote, Tomaso pacha, Simoni mkananayo, Yohana Mbatizaji n.k

Watu hawa ambao majina yao yanaonekana kuongezewa vionjo mbele yake ni kwa lengo la kuwatofautisha na watu wengine wenye majina kama ya kwao. Na vionjo hivyo vilivyokuwa vinawekwa ni aidha kulingana na mahali (miji) wanayotokea, au majina ya wazazi wao, au matendo/huduma  wanazozifanya.

Wafuatao ni baadhi ya majina ya watu yaliyoongezewa vionjo kulingana na Matendo waliyokuwa wanayafanya;

  1. Yohana Mbatizaji – Ili kumtofautisha na Yohana wengi ambao walikuwepo Israeli, aliitwa hivyo Yohana Mbatizaji kutokana na kazi yake ya kubatiza watu aliyokuwa anaifanya, Hivyo palipotajwa Yohana mbatizaji wote walijua analengwa nani.
  2. Simoni Petro- Maana ya Petro ni ‘Jiwe’ dogo la kurusha, na si “mwamba” kama inavyoaminika na wengi. Bwana Yesu alimpa Simoni jina Petro, kutokana na jinsi Bwana atakavyomtumia katika huduma yake, katika kuzipiga nguvu za shetani.
  3. Yohana na Yakobo (Boanerge)- Maana ya Boanerge ni ‘Wana wa Ngurumo’ Marko 3:17. Bwana aliwaita hivi kufuatia huduma zao, na ili pia kuwatofautisha na wengine wenye majina kama yao.

Kulingana na Mahali walipotokea;

  1. Yuda Iskariote- Iskaritote maana yake ni mtu wa Keriote/Keriothi.. Na Keriothi ni mji uliokuwepo katika Nchi ya Moabu.
  2. Simoni Mkirene- Kirene ni mji uliokuwepo Kaskazini-kusini mwa nchi ya Libya, Ili kumtofautisha Simoni huyu aliyeubeba msalaba wa Bwana na Simoni aliyekuwa mwanafunzi wa Bwana, ndipo akatajwa kulingana na mji aliotokea ambao ni Kirene.
  3. Simoni Mkananayo- Aliitwa hivi kufuatia mji aliotokea ulioitwa ‘’KANA’’ ndio kule Bwana alipogeuza maji kuwa Divai (Mathayo 15:22) na pia ulikuwepo pia mji mwingine katika nchi ya Tiro ulioitwa hivyo ‘Kana’, ambapo aliishi yule mwanamke aliyemlilia Bwana amponye binti yake aliyepagawa na pepo (Soma Mathayo 15:21-22).Mtu aliyetokea Kana, aliitwa Mkananayo.. Lakini pia Huyu Simoni Mkananayo sehemu nyingine pia alijulikana kama Simoni Zelote (Luka 6:15, Matendo 1:13), maana ya Zelote ni “Mpigania dini”, hivyo watu waliokuwa wanaishindania na kuipigania dini ya kiyahudi wakati huo waliitwa Wazelote, na huyu Simoni kabla hajaitwa na Bwana alikuwa anajulikana hivyo
  4. Mariamu Magdalene- Magdalene ni mji uliokuwepo huko Galilaya.. hivyo ili kumtofautisha Mariamu mamaye Yesu na yule aliyetokwa na pepo saba, ndipo huyu akaitwa Mariamu Magdalene.

Kwahiyo ili kumtofautisha na Simoni Petro au Simoni  mwingine yeyote, ndipo huyu akaitwa Simoni Mkananayo au Simoni Zelote.

    Kulingana na majina ya Wazazi/ Ndugu

1 .Yakobo wa Alfayo:  Yakobo alikuwa ni mtoto wa Mtu aliyeitwa Alfayo, Aliitwa hivyo ili kumtofautisha na akina Yakobo wana wa Zebdayo na wengine waliokuwepo kwa wakati huo.(Marko 3:18).

2. Yuda mwana wa Yakobo: Huyu alikuwa ni mwanafunzi wa Bwana Yesu ambaye pia aliitwa kwa jina lingine “Thadayo”(Marko 3:18). Ili kumtofautisha na Yuda aliyemsaliti Bwana Yesu, ndipo kwa jina lingine akajulikana hivyo kama Yuda wa Yakobo au Thadayo.

3. Tomaso aitwaye Pacha (Yohana 20:2)– Ni kuonyesha Tomaso kuwa alikuwa na Pacha lakini hakutajwa katika maandiko huyo pacha wake alikuwa ni nani, ila aliitwa hivyo ili kumtofautisha na wakina Tomaso wengine waliokuwepo pale.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Je jina lako ni nani? Na linabeba ujumbe gani?… >>JINA LAKO NI LA NANI?

Maran atha

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

MAANA YA MAJINA NA TAFSIRI ZAKE.

Kwanini mtu afanye miujiza na bado asiende mbinguni?

Yeremia alikuwa na umri gani alipoitwa?

NGUVU YA UPENDO WA KRISTO.

Rudi nyumbani

Print this post