Title October 2019

Bwana  alikuwa na maana gani aliposema. “leo na Kesho natoa pepo na kuponya siku ya tatu nakamilika?”

JIBU: Tusome:
Luka 13:32 “Akawaambia, Nendeni, mkamwambie yule mbweha, Tazama, leo na kesho natoa pepo na kuponya wagonjwa, siku ya tatu nakamilika.
33 Pamoja na hayo imenipasa kushika njia yangu leo na kesho na kesho kutwa; kwa kuwa haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu”.
Ili kuelewa vizuri sentensi hiyo vizuri, hebu tafakari mfano huu.. Mwalimu kawaambia wanafunzi wake “leo na Kesho tunazungumza lakini siku ya mtihani hamtaniona” Kwa sentensi hiyo, huwezi kusema kuwa baada ya siku ya Kesho kutwa basi siku inayofuata ndiyo siku ya Mtihani mwalimu anayoizungumzia! Bali utajua mwalimu anamaanisha kuwa siku hizi ambazo sio za mtihani ndio siku ambazo wapo huru kuzungumza na mwalimu wao, kazipa jina la ujumla Lakini itakuja siku moja maalumu huko mbeleni labda baada ya miezi kadhaa, au miaka ambayo wanafunzi hawatapata nafasi tena ya kuzungumza na mwalimu…na hiyo itakuwa siku ya mtihani..ambayo inaweza kuwa ni baada ya miezi kadhaa mbeleni au miaka kadhaa..Hivyo neno “leo na Kesho na Kesho kutwa” halimaanishi kipindi cha siku mbili au tatu, bali kipindi cha muda fulani mrefu kidogo.
Na hapo Kristo alimaanisha vivyo hivyo, kwamba leo na Kesho na Kesho kutwa (yaani kipindi chote ambacho yupo na wanafunzi wake) atakuwa anatoa pepo na kuponya lakini “siku ya tatu”, ambayo itakuja huko mbeleni kipindi atakapofufuka baada ya kusulubiwa na kukaa kaburini siku tatu..Hiyo ndiyo itakuwa siku yake ya kukamilka..
Kristo alipofufuka ndio ulikuwa Ukamilifu wa Huduma yake, asingefufuka basi ushuhuda wake ungekuwa wa Uongo, Lakini alifufuka kutuhakikishia sisi kuwa Yeye katumwa kutoka mbinguni, na kashinda mauti, hivyo anaweza kutuondolea nasi pia mauti ya rohoni, inayotokana na dhambi.
 
Bwana akubariki.
 

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 

Mada Nyinginezo:

ULE MSALABA UNAOWEKWA KWENYE KABURI, NA ILE IBADA INAYOFANYWA VINA UMUHIMU WOWOTE KWA MKRISTO?

KIFAA BORA CHA MATUMIZI.

JE! MBINGUNI KUNA MALAIKA WA KIKE?. NA JE! TUKIFIKA MBINGUNI TUTAFANANA WOTE?

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

NG’OMBE MWEKUNDU ALIYEZALIWA ISRAELI, ANAFUNUA NINI?

UNYAKUO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

NINI MAANA YA KULITAFAKARI NENO LA MUNGU?

Kuna tofauti kati ya kuwaza na kutafakari, kuwaza ni kitendo cha kurudia rudia kwenye akili yako ile kumbukumbu ambayo tayari unayo, kwa mfano labda mtu kutwa nzima alikuwa yupo sokoni anatafata mboga nzuri ya kununua….Sasa wakati yupo katika utulivu ametulia anajikuta akili yake inaanza kufikiria yale mambo ambayo alikuwa anayaona, aina za mboga, nafaka, matunda n.k…yaani mtu huyo akili yake inakuwa inazunguka kwenye kile tu alichokiona..

Lakini kutafakari ni tofauti na kuwaza, Kutafakari sio tu kurudia rudia kwenye akili kile ulichokiona au kukifanya, hapana bali kwenda mbali zaidi ni kitendo cha kutathimini kwa undani vile ulivyoviona..kwamfano tuchukue ule ule mfano  wa sokoni, mtu anayetafakari anajiuliza maswali mengine kichwani kwake, Je! Zile mbona zinatolewa wapi? Mbona sizioni zikilimwa mkoani kwetu, atajiuliza lile soko kwanini limewekwa pale, na kwanini aina ile ya nafaka inauzwa na watu wengi zaidi, je! Wanunuzi wa hapa ni watu wa aina gani, Je kazi wanaoifanya hapa inawalipa vizuri? n.k..,Sasa mtu anayewaza kwa namna hiyo, huyo ndiye anayetafakari , na utaona mtu wa namna hiyo  mwishowe huwa anakuja na suluhisho lilio bora zaidi, pengine na yeye utamwona siku moja pale sokoni amekuwa muuzaji.

Vivyo hivyo na katika biblia, tunapaswa tulitafakari Neno la Mungu, na sio kuliwaza tu, tunaposoma biblia tunapaswa tujiulize je! Hii hadithi inafunua nini rohoni?, Je! Tafsiri yake katika maisha yetu ni nini, Mungu hapa alikuwa na maana gani kusema hivi, ni kwanini afanye vile, na asifanya hivi,,Sasa mtu unapokuwa katika hali ya maswali na namna hiyo katika kusoma kwako biblia, mawazo yako yanapata kibali mbele za Mungu na ndipo Roho Mtakatifu anachuka nafasi ndani yake kukufundisha na kukumfunulia..

Zaburi 19: 14 “Maneno ya kinywa changu, NA MAWAZO YA MOYO WANGU, Yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu, na mwokozi wangu”.

Tofauti na Yule ambaye anasoma tu hadithi labda tuseme ile ya YONA jinsi alivyomezwa na samaki, anatoka pale anaifurahia ile hadithi anaiwaza tu juu juu jinsi alivyomezwa na samaki Yule na jinsi alivyotapikwa halafu basi ile hadithi inabakia tu kichwani kwake kama kumbukumbuku, hakuna kingine chochote za ziada anaweza kujiuliza juu ya hilo. Mtu kama huyo Neno la Mungu litabakiwa kuwa fumbo kubwa ndani yake, japo anaweza kujiona anaifahamu biblia nzima. .. Lakini kama mtu akiitafakari kwa undani ndipo hapo Roho Mtakatifu anampa ufunuo mkubwa kama ule wa YESU kukaa kaburini siku tatu kwa kupitia tu kuitafakari habari ya Yona.

Halikadhalika Bwana Yesu aliposema yatafakarini maua, watafakarini kunguru..(Luka 12:24) Ni zaidi ya kuwaangalia tu wanavyoruka, bali jinsi wanavyoishi, wanavyokula bila kupanda, bila kuvuna, wasivyojiwekea hazina ghalani, wasivyomeza vidonge n.k. Hivyo tukiweza kutafakari Neno la Mungu kwa namna hiyo  Roho Mtakatifu hatapata shida kutufunulia siri zake kiwepesi.

Ni wajibu wetu kulitafakari Neno lake kila siku.

Ubarikiwe sana.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.

JE! KUBET NI DHAMBI?

NYOTA ZIPOTEAZO.

HATARI YA KUTOKUITAFAKARI BIBLIA VIZURI?

TABIA ZA ROHONI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

MAMA WA MAKAHABA

Ufunuo 17:3 “Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi.

4 Na mwanamke yule alikuwa amevikwa nguo ya rangi ya zambarau, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake.

5 Na katika kipaji cha uso wake alikuwa na jina limeandikwa, la siri, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI.

6 Nikamwona yule mwanamke amelewa kwa damu ya watakatifu, na kwa damu ya mashahidi wa Yesu. Nami nilipomwona nikastaajabu ajabu kuu”

Kuna Maswali machache hapo ya kujiuliza;

1.Kwanini Yohana alichukuliwa katika Roho mpaka jangwani na si mpaka msituni…Ni wazi kuwa roho iliyopo jangwani si roho ya Mungu bali ya yule Adui..Kwasababu Bwana Yesu alisema katika Mathayo 12:43 “Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate”.  Mahali pasipo maji ni jangwani…Hivyo Yohana alichopelekwa kukiona jangwani ni roho ya yule Adui.

2. Swali la pili; Kwanini jambo la kwanza Yohana kuliona ni mwanamke?..Maana alimwona mwanamke na alipomtazama vizuri akamwona ameketi juu ya mnyama mwekundu…Hiyo ikifunua lengo kubwa la yeye kupelekwa huko ni kumwona huyo mwanamke. Na huyo Mwanamke ni nani? na anaonekana amelewa!..Huyo Si mwingine zaidi ya kanisa fulani ambalo tutakuja kuliona mbeleni kidogo. Kwasababu katika maandiko mwanamke anawakilisha kanisa (Waefeso 5:31-32, 2Wakoritho 11:2, Ufunuo 21:9,)

3. Jambo lingine ni kwanini Mnyama aliyempanda huyo mwanamke alikuwa mwekundu sana?..Rangi nyekundu siku zote inaashiria damu!..yaani umwagikaji wa damu! Maana yake huyo mnyama ni mwuuaji…Tengeneza picha Mtu aliyelewa amepanda simba na huku anachupa yake mkononi ya pombe, halafu anazunguka naye mtaani na huyo simba anaonekana ana ghadhabu nyingi, ana meno makali..Utapata picha gani? Ni wazi kuwa utaona huyo mtu kakusudia kudhuru watu kupitia huyo mnyama wake anayemwendesha. Ndivyo huyu mwanamke anavyoonekana hapa.

Hivyo kwa tafsiri yake ni kwamba kanisa hilo linatumia mfumo fulani kuua watu, lilitumia mfumo huo kuua watu katika enzi za zamani, na litatumia  huo mfumo kuua watu wakati wa dhiki kuu, huo mfumo ndio mnyama..

4. Jambo la Nne Mwanamke yule katika kipaji cha uso wake ana jina limendikwa kwa siri..kumbuka sio kwa wazi! kwa siri!  ikimaanisha hataki ajulikane yeye ni nani? na jina hilo linasomeka BABELI MKUU MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI.

Kwanini ni Babeli Mkuu?..Ikimaanisha kuwa kulikuwa na Babeli nyingine zilipita lakini sio KUU, Babeli ile iliyotengeneza mnara ilikuwa ni Babeli lakini sio kuu!..Babeli ya Nebkadneza ilikuwa ni Babeli lakini si kuu!…Hivyo hiyo Yohana aliooneshwa ndio kuu!!

Na kwanini tena ni MAMA WA MAKAHABA?, Ikimaanisha anao watoto ambao nao ni makahaba, na yeye mwenyewe anafanya ukahaba..Na kama yeye ni kanisa ni wazi kuwa waototo wake nao watakuwa ni makanisa na wote wanafanya ukahaba…..Kanisa linalofanya ukahaba kibiblia ni kanisa linaloabudu sanamu, na kuacha sheria za Mungu…Na mwisho inamalizia NA MACHUKIZO YA NCHI…Na sio machukizo ya Mbingu…maaana yake anafanya machukizo akiwa hapa hapa duniani! machukizo ni jambo lolote linalomchukiza Mungu.

Ndugu huyo mwanamke si mwingine zaidi ya KANISA KATOLIKI, Hilo ndio lililohusika kuua zaidi ya wakristo milioni 60 wakati wa kipindi cha giza. Ni kanisa la uongo, lenye kivuli cha ukweli..Na mpinga-Kristo atatokea katika kanisa hilo, na cheo chake kimeshafunuliwa, na hicho si kingine zaidi ya cheo cha PAPA!

Kwa kutumia mfumo wake huo  wa kikatili (yaani huyo mnyama) atawaua watu wengi sana katika kipindi cha dhiki kuu, wakati ambao unyakuo utakuwa umeshapita! Wale watakaoachwa watalazimishwa kupokea chapa ya huyo mnyama, na kupewa kila sababu ya kuingia katika lile ziwa la Moto.

Je! Una uhakika wa kwenda kwenye unyakuo ili uepukane na mambo hayo yote? Kuna mambo mengi sana yatatokea mpinga kristo atakayoyafanya katika siku hizi za mwisho tunazoishi, huu ni ufupisho tu.

Maran atha, Bwana wetu anakuja

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

CHAPA YA MNYAMA NI NINI?

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

MPINGA-KRISTO NI NANI?

NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

Uthibitisho wa kwanza wa mtu kuwa na Roho Mtakatifu ni Utakatifu atakaouonesha, na Utakatifu kwa ujumla ndio tunda la Roho. Na uthibitisho wa Pili ndio karama aliyo nayo…. Na Mtu Mtakatifu ni lazima aoneshe vitu 9 vifuatavyo..pamoja na vingine vingi, lakini hivi 9 ndio msingi wa UTAKATIFU WA MTU.

  1. UPENDO
  2. FURAHA
  3. AMANI
  4. UVUMILIVU
  5. UTU WEMA
  6. FADHILI
  7. UAMINIFU
  8. UPOLE
  9. KIASI

Tabia hizi 9 zinapatikana kutoka katika kitabu cha Wagalatia..

Wagalatia 5:22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. 

Mtu Mwenye Roho Mtakatifu lazima awe navyo hivi vyote kwa pamoja! hapaswi kukosa hata kimoja..kwasababu vyote kwa pamoja ndio vinaitwa TUNDA LA ROHO, na si MATUNDA YA ROHO…Ikiwa na Maana ni lazima viende kwa pamoja.

Ubarikiwe.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI.

HATARI YA KUTOKUITAFAKARI BIBLIA VIZURI?

EPUKA KUTOA UDHURU.

JE! NI SAHIHI KUJIPA CHEO MFANO MIGHTY PROPHET, CHIEF APOSTLE N.K?

BIBLIA INAKATAZA KUAPA KABISA, LAKINI KWANINI WATU WANAAPA MAHAKAMA?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Mpagani ni nani?

Mpagani ni mtu yeyote asiye Mkristo…Mtu yeyote anayeabudu miungu mingine tofauti na Mungu wa Israeli, ambaye anaabudiwa kwa kupitia mwanawe wa pekee Yesu Kristo, mtu huyo ni “Mpagani”…

Mchawi ni mpagani, watu wasio na dini ni wapagani, waabudu miti, mawe, sanamu wote ni wapagani, kadhalika na wakristo-jina wote ni wapagani, na waislamu ni wapagani. Upagani hauna tofauti sana na “ukafiri”

Mtu aliyemwamini Yesu Kristo, na kubatizwa katika ubatizo sahihi na kupokea Roho Mtakatifu, na kuuishia wokovu kulingana na Biblia, yaani kuishi maisha ya utakatifu na ya kumcha Mungu, mtu huyo pekee ndiye ambaye si MPAGANI.

Shalom.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KAFIRI NI NANI?

“HERI WALIO MASKINI WA ROHO MAANA UFALME WA MBINGUNI NI WAO” JE HATUNA RUHUSA YA KUWA MATAJIRI KATIKA ROHO?

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “WAACHE WAFU WAZIKE WAFU WAO

MATUMIZI YA DIVAI.

ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KAFIRI NI NANI KULINGANA NA BIBLIA?

KAFIRI NI NANI?

Kafiri ni Mtu yeyote asiyeamini IMANI fulani…kafiri Katika Biblia ni mtu yeyote asiyeuamini Ukristo, Ukafiri hauna tofauti sana na upagani, Mtu yeyote asiyemwamini Bwana Yesu Kristo kwamba alikuja, na kufa kwaajili ya dhambi za ulimwengu mtu huyo ni kafiri.

Mtu yeyote asiyeshika njia za Bwana Yesu Kristo na kumkana  mtu huyo  kafiri.

Yuda 1:14 “Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo”

Kwahiyo kafiri ni nani?…Jibu: Ni mtu yeyote asiyempenda Bwana YESU huyo ni kafiri, na tena Biblia inasema Amelaaniwa

2Wakorintho 16:22 “Mtu awaye yote asiyempenda Bwana, na awe amelaaniwa. Maran atha”.

Kwahiyo mtu yeyote akitaka asiwe kafiri, ni sharti amkiri Yesu Kristo, na kumwamini, na kumpa Maisha yake na kudhamiria kuacha dhambi.

Na makafiri wote hawataurithi uzima wa milele. kwasababu hawajamwamini Mwana pekee wa Mungu (Yesu Kristo)

Yohana 3:18 Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.

19 Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.

20 Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa.

Ubarikiwe sana.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MPAGANI NI NANI?

WAPUNGA PEPO NI WATU WA NAMNA GANI?

NINI MAANA YA KIPAIMARA?..NA JE! NI JAMBO LA KIMAANDIKO?

JE! MTU KUSIKIA SAUTI ZA WATU WALIO MBALI, KUNAWEZA TOKANA NA MUNGU?

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?


Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI MUNGU ALITUUMBA WANADAMU.

Tofauti na sisi wanadamu tulivyo, tukiunda kitu au tukiumba kitu Fulani ni kwa lengo moja tu ni ili kutusaidie sisi kufanya jambo fulani au kitunufaishe kwa namna moja au nyingine. Kwamfano mtu anaunda gari ni ili limsafirishe, anaunda meli ni ili imsaidie kutembea juu ya maji n.k. lakini kwa Mungu haiko hivyo yeye alituumba sisi kwa mapenzi yake/raha yake/furaha yake tu basi, (his pleasure).

Hakupungukiwa na kitu Fulani  na hivyo akatuumba sisi ili kwa kupitia sisi akipate hapana, wengine wanasema Mungu alituumba ili tumwabudu, kusema hivyo sio sahihi , ukweli ni kwamba tunamwabudu Mungu kwasababu alituumba, lakini sio alituumba ili tumwabudu, Mungu hajaishiwa sifa biblia inasema vyote vinatoka kwake..(Zaburi 139)

Wakolosai 1:16 “Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake”.

Hivyo fahamu tu kuwepo kwako wewe duniani ni furaha yake, anafurahi kukuona wewe upo kama ulivyo, anafurahia kukuona unafanya mambo mazuri kama yeye anayoyafanya, anafurahia kukuona wewe unayo amani kama yeye aliyonayo, unayo furaha, unao upendo kama yeye alionao, ..hakukuumba ili akutese, au akutumikishe hapana..Lakini ni kwasababu amekupenda tu na ametaka wewe uwepo…

Ni kwa vile tu tulizama katika dhambi, tukajiharibia maisha  wenyewe lakini mapenzi ya Mungu halisi yalikuwa ni milele tuishi ndani ya PENDO lake, lakini pamoja na hayo Pendo hilo limerejeshwa na YESU KRISTO, Kwa kupitia yeye huyo ndio tunaona ni jinsi gani alivyokuwa amtupenda tokea mwanzo….Jaribu kufikiria jinsi alivyomtuma mwanawe wa pekee, kutuokoa sisi tuliokuwa tumepotea, alichukua dhambi zetu, alichukua magonjwa yetu, alichukua masumbuko yetu…

Hata na wewe ukikaa ndani yake basi Pendo hilo nalo litakuja ndani yako..Nawe utamfarahia Mungu wako kama vile yeye anavyokufarahia, utampa sifa wa jinsi alivyokuumbwa kwa utashi wa hali ya juu namna hiyo, utamwabudu kwa uumbaji wake wote ulivyo mkuu, utamtukuza kwa jinsi anavyokulisha na kukupa riziki zako za kila siku..

Zaburi ZABURI 150

1 Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake.

2 Msifuni kwa matendo yake makuu; Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

3 Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;

4 Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;

5 Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6 Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana.

Haleluya.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

YESU NI NANI?

BASI MUNGU AKAMUADHIMISHA SANA.

JE! KUBET NI DHAMBI?

NI KWANINI MUNGU HAONEKANI?

UNYAKUO.

JINSI EDENI ILIVYOKUWA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

MAANA YA MAJINA NA TAFSIRI ZAKE.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Kuna Roho inayofuatana na Majina, katika Maandiko tunaona watu wengi sana walibadilishwa majina yao, wengine wakati wa kuanza huduma au kabla ya kuanza huduma. Ibrahimu hapo kwanza aliitwa Abramu (Mwanzo 17:5), Sarai jina lake lilibadilishwa na kuitwa Sara, Yakobo jina lake lilibadilishwa na kuitwa ISRAELI. nk Kwahiyo ni Muhimu kujua maana ya majina kabla ya kumpa mtoto jina au kabla hujajipa jina.

Angalizo: Ukimpa Mtoto jina hata kama liwe zuri au lina tafsiri nzuri kiasi gani, kama mtoto huyo hatakuzwa katika malezi ya kumcha Mungu bado atakuwa mbaya tu, na akifa ataenda Jehanamu ya moto..

Kadhalika, mtoto anaweza akawa na jina lenye tafsiri isiyo njema, lakini kama atakuzwa katika Njia sahihi, hiyo haimzuii Mungu kumtumia, na jina lake kuwepo katika kitabu cha Uzima

Kwasababu majina yaliyopo katika kile kitabu cha uzima hayajaandikwa kulingana na tafsiri, bali kulingana na matendo!! Watakuwepo wengi wenye majina mazuri katika ziwa la Moto, na watakuwepo pia wengi wasio na majina mazuri Mbinguni Kwahiyo Jina pekee halimfanyi mtu au mtoto kuwa mzuri bali malezi pia ya kumcha Mungu….Na malezi sio tu kumpeleka kanisani kila jumapili, bali pia na kumfundisha Njia za Bwana kila siku hata akiwa nyumbani! huku mzazi ukionesha kielelezo cha kumcha Mungu.

https://www.high-endrolex.com/17

Lakini yote katika yote ni vizuri kumpatia mtoto jina lililo zuri na lenye tafsiri bora!

  • MAANA YA JINA YESU.

Hili ndio jina lenye “nguvu” kuliko majina yote, hakuna lililo juu ya hili, kwa vizazi vyote mpaka mwisho wa dunia, halitakuwepo lililo kuu zaidi ya hili maana ya jina hilo ni YEHOVA MWOKOZI, Hivyo Yesu ndiye mwokozi wa Ulimwengu. (Tafadhali; Usimpe mwanao, wala usijipe mwenyewe hili jina, kwasababu ni jina tukufu la Mwana wa Mungu)

  • MAANA YA JINA YOHANA au JOHN

Maana yake ni “Yehova ni mwenye Neema”..Asili ya hili jina ni kiyahudi, Yohana Mbatizaji aliitwa hili jina pamoja na Yohana Mwanafunzi wa Yesu, ambaye ni ndugu yake Andrea.

  • MAANA YA JINA LUKA

Maana yake ni “Mlukania” Lukania ni mahali palipokuwa kusini mwa Italy..ambapo tafsiri yake haijajulikana mpaka leo.

  • MAANA YA JINA MATHAYO

Tafsiri yake ni “Zawadi ya YEHOVA” Asili yake ni lugha ya Kiebrania

  • MAANA YA YA JINA PAULO

Maana yake ni “Mnyenyekevu”

  • MAANA YA JINA YEREMIA

Maana yake ni “Yehova atapandisha au atanyanyua”..Asili ya jina hili ni lugha ya kiebrania.

  • MAANA YA JINA AYUBU au JOB

Maana yake. Ni “Anayechukizwa au anayeonewa” asili yake ni lugha ya kiebrania.

  • MAANA YA JINA SAMWELI

Maana yake “Mungu amesikia” asili yake ni lugha ya kiebrania.

  • MAANA YA JINA PETRO

Tafsiri yake ni jiwe dogo, kama la kurusha, asili ya jina hili ni lugha ya kigiriki.

  • MAANA YA JINA NEEMA au GRACE

Maana ya Neema, ni upendeleo wa kipekee ambao mtu au kitu kinaweza kupata, upendeleo huo hauna chanzo/sababu maalumu. Mungu pekee ndiye anayetoa Neema.

  • MAANA YA JINA ETHAN

Tafsiri yake ni “Aliye Imara, Thabiti” Asili ya jina hili ni lugha ya Kiebrania, katika Biblia alionekana Ethan mtu wa hekima katika Zaburi ya 89

  • MAANA YA JINA IVAN

Ivan na Yohana ni jina moja, isipokuwa kwa Ivan limewekwa kwa lugha ya kirusi ya sasa, lakini ni hilo hilo Yohana, ambalo tafsiri yake ni “Yehova ni mwenye Neema”

  • MAANA YA JINA CHARLES

Jina Charles limetokana na neno la kijerumani “karl” lenye tafsiri ya “mwanamume”.

  • MAANA YA IRENE

Jina Irene limetokana na neno la kigiriki “Eirene”…lenye maana ya “AMANI”

  • MAANA YA JINA CAROLINA

Jina Carolina au Caroline tafsiri yake ni “Mwanamke kwa kiingereza woman”. kwa jinsia ya kiume ni Carlos, au Charles

  • MAANA YA JINA CAREEN au CARREEN

Jina Careen ni mchanganyiko wa majina mawili (CAROLINA na IREEN). Maana ya Irene ni “Amani”, na Caroline ni “Mwanamke”. Kwahiyo tafsiri yake ni “Mwanamke wa Amani”

Group la whatsapp  Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JINA LAKO NI LA NANI?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

USILITAJE BURE JINA LA BWANA!


[embedyt] https://www.youtube.com/embed?listType=playlist&list=PLIIhnDzXkeEcXSNPlq09Q5yonU3MOLI0h&v=DWFSX1GfuC8&layout=gallery[/embedyt]

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUACHA KUVUTA SIGARA.

Unaweza ukawa umezunguka huku na huko, umejaribu hiki na kile kwa bidii zako ili kuacha kuvuta sigara lakini imeshindikana, ni uwazi usiopingika kwamba vitu vyote vyenye addiction (yaani ulevi ndani yake) ni ngumu sana kuviacha, sio pombe, sio ugoro, sio bangi, sio madawa ya kulevya sio sigara, sio mirungi vyote hivyo kwa bidii za mtu binafsi ni ngumu leo anaweza akaacha kwa muda tu lakini kikipita kipindi Fulani kifupi ile hamu ikimzidia anarudia tena , Ni utumwa mgumu sana ambao kwa bidii za kibinadamu ni kama haiwezekani, ..Lakini nataka leo nikupe habari njema nazo ni hizi:

Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.(Yohana 8:36).  

Mamia kwa mamia kama sio maelfu kwa maelfu ya watu duniani wanaacha kuvuta sigara, kwa kumruhusu tu YESU atende kazi maishani mwao. Sio tu kwa wavuta sigara bali pia hata na kwako wewe mnywaji pombe na mtumiaji wa ugoro na madawa ya kulevya, Kwasababu kwake yeye hakuna linaloshindikana, akikufungua habakishi hata chembe moja ndani yako, haijalishi wewe ni mtumwa wa hicho kitu kwa kiwango gani, hakuna utumwa ulio mkubwa zaidi ya utumwa wa DHAMBI lakini huo aliukomesha pale msalabani, si zaidi sigara ambayo ni kitawi kidogo sana cha dhambi yenyewe?.

Ikiwa umekusudia kweli na unataka kuacha leo basi, tiba ipo kwa YESU, Hatuhitaji kusema maneno mengi  Unachopaswa kufanya ni kuanzia sasa umgeukie tu yeye..Utubu dhambi zako kwanza kwa kumaanisha kuziacha, na kisha yeye mwenyewe atakuvika huo uwezo wa kuacha kuvuta sigara, ataiondoa hiyo kiu ya sigara ndani yako moja kwa moja..Lakini Ikiwa tu umemaanisha kuwa kiumbe kipya. Kama upo tayari basi nataka ufuatishe sala hii, lakini tafuta kwanza mahali pa utulivu kisha fuatisha sala hii kwa IMANI..Kwasababu yeye yupo hapo hapo ulipo kukuhudumia hauhitaji mchungaji, au mhubiri aje kukuombea, wewe mwenyewe hapo ulipo anakusikia, kwasababu sio mchungaji anayekuponya au mhubiri bali ni yeye huyo YESU MWOKOZI ndiye anayekwenda kushughulika na shida yako…

Sema maneno haya kwa sauti:

EE! BWANA YESU, NAJA MBELE ZAKO, NINAJIJUA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NIMEKUKOSEA KWA MAMBO MENGI, NA MOJAWAPO NDIO HILI LA KULIHARIBU HEKALU LAKO KWA KULIVUTISHA SIGARA, LEO HII NINAJUTA NA NINATUBU MBELE ZAKO KWA KUMAANISHA KABISA KUWA SITAKI KUVUTA SIGARA TENA, NA NIMEMAANISHA  KUACHANA NA MAISHA YA DHAMBI. NJOO NDANI YANGU BWANA YESU, UNIBADILISHE UNIFANYE KUWA UPYA NIFANANE NA WEWE, MIMI KWA NGUVU ZANGU NIMESHINDWA KUACHA SIGARA LAKINI WEWE ULISEMA KATIKA MATHAYO 11:28 KWAMBA TUJE KWAKO SISI WOTE TUNAOSUMBUKA NA KULEMEWA NA MIZIGO YA DHAMBI, NAWE UTATUPUMZISHA, NAWE UTATUPA RAHA NAFSINI MWETU NA LEO HII KWA UNYENYEKEVU WOTE NIMEKUJA KWAKO BWANA YESU ILI UNIFUNGUE  KATIKA VIFUNGO HIVI VYA DHAMBI NA MAUTI. NINAKIRI KUWA WEWE NDIO BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NA KWAMBA ULIKUFA NA UKAFUFUKA, NA SASA UPO HAI KUNISIKIA, HIVYO KUANZIA LEO NAAHIDI KUKUTUMIKIA NA KUKUISHIA WEWE DAIMA.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNISAMEHE NA KUNIPONYA NA SHIDA YANGU YOTE AMEN.

Ikiwa umesali sala hii kwa imani, basi fahamu kuwa Mungu amekusikia na kukusamehe dhambi zako zote sio hiyo ya sigara tu bali na nyingine zote, , hivyo unachopaswa kufanya ni kutupa sigara zote ziweke mbali nawe wakati Bwana YESU anaendelea kushughulika na hiyo kiu ya sigara ndani yako, Hivyo hakikisha, unatafuta  kanisa la kiroho, lililokaribu nawe  ili kukusaidia kukua kiroho, au wasiliana nasi kwa namba hizi 0789001312 ikiwa utahitaji msaada wetu.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 

Mada Nyinginezo:

WEWE NI HEKALU LA MUNGU.

YESU NI NANI?

FREEMASONS NI NINI? NA MTU ATATOKAJE HUKO?

JE! KUBET NI DHAMBI?

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU.

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUJIPAMBA NI DHAMBI?

Ni Muhimu kufahamu kama Je kujipamba ni dhambi? au  kujichubua ngozi ni dhambi? kama kuchonga nyusi ni dhambi, kupaka lipstick ni dhambi na kama kupaka wanja ni dhambi?

Kiuhalisia Kujipamba kunahusisha kupaka rangi uso, kujichubua ngozi, kuchonga nyusi, kupaka lipstick, kupaka wanja, kupaka hina,kusuka nywele, kuvaa hereni, bangili, na mikufu, kuweka kucha za bandia, kuweka nywele za bandia (wigi), kujipulizia  marashi makali.

Watu wengi hususani wanawake hawapendi kuambiwa ukweli, kutokana na kwamba wanahofia wataonekana wamepitwa na wakati. Lakini ukweli ni kwamba kujipamba ni DHAMBI, Tena ni dhambi ambayo inawapeleka wanawake wengi kuzimu, na wanaume baadhi wanaofanya hayo..

Katika Biblia kulikuwepo na mwanamke mmoja tu ambaye alikuwa anajipamba…Na huyo si mwingine zaidi ya mwanamke Yezebeli..

Ambaye tunamsoma katika kitabu cha Wafalme

2Wafalme 9:30 “Hata Yehu alipofika Yezreeli, Yezebeli akapata habari; akatia uwanja machoni mwake, akapamba kichwa chake, akachungulia dirishani”.

Mwanamke huyu biblia inasema alikuwa mchawi…na aliwakosesha sana wana wa Israeli na alimsumbua sana Nabii Eliya. Na alienda kuzimu! kwasababu anaonekana tena katika kitabu cha Ufunuo kutajwa kama Nabii wa Uongo, na Manaabii wa Uongo pamoja na wachawi, na waabudu sanamu wote biblia imesema sehemu yao ni katika lile ziwa la moto. Kasome (Ufunuo 2:20)

Na biblia inasema miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, hivyo hatuwezi kulifanya hekalu la Mungu kuwa nyumba inayofanana na nyumba za makahaba. Na Neno linasema mtu akiliharibu hekalu la Roho Mtakatifu, Mungu naye atamharibu mtu huyo.

Vivyo hivyo Biblia imezungumza katika Agano jipya.

1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;

10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu”. 

Hivyo kujipamba kwa aina yoyote ile ni dhambi..  kusuka nywele ni dhambi, kujichubua ngozi ni dhambi, kuchonga nyusi ni dhambi, kupaka lipstick ni dhambi, kupaka wanja ni dhambi nk Mwanamke anapaswa ajiweke katika hali yake ya asili, kadhalika na wanamume pia..Ni wajibu  wetu wote kujiweka safi na nadhifu, lakini si kuharibu uhalisia.

Mungu akubariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789 001312.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

WEWE NI HEKALU LA MUNGU.

NI KWA JINSI GANI MUNGU ANAPATILIZA MAOVU YA BABA ZETU SAWASAWA NA KUTOKA 20:5-6?

AMPOKEAYE NABII KWA KUWA NI NABII, ATAPATA THAWABU YA NABII; MSTARI HUU UNAMAANA GANI?.

SHETANI ANATOLEA WAPI FEDHA, ANGALI TUNAJUA FEDHA NA DHAHABU NI MALI YA BWANA?

ASKOFU MKUU NA MCHUNGAJI MKUU NI NANI?


Rudi Nyumbani:

Print this post