Swali: Je sisi wakristo tunaruhusiwa kutumia emoji katika kufanya mawasiliano kwa njia ya kidigitali?.
Jibu: Biblia inasema…
Tito 1:15 “Vitu vyote ni safi kwa hao walio safi; lakini hakuna kilicho safi kwao walio wanajisi, wasioamini; bali akili zao zimekuwa najisi, na nia zao pia”.
Chochote kile (hata kiwe kizuri) endapo kikitumika vibaya kinaweza kuleta madhara au kikaingiza roho ya ibilisi ndani ya mtu, hata biblia ikitumika vibaya inaweza kumharibu mtu moja kwa moja, kuliko kumjenga, ingawa biblia si kitabu kibaya..
Sasa swali “Emoji” ni nini?…na je ni sahihi kutumiwa na mkristo?.
“Emoji” ni vijitaswira vidogo vidogo vyenye maumbile ya mfano wa mtu au vitu, ambavyo vinatumika kwenye simu za mikononi au komputa, vinavyosimama badala ya maneno au hisia.
Emoji hizi zinapotumika basi mtu anayevitazama anaweza kuelewa kirahisi ujumbe wa mwandishi au hisia za mwandishi.
Lakini pia ipo hoja kuwa emoji hizi zinapotumika basi nyuma yake zinakuwa na taswira nyingine au alama nyingine za ibilisi tofauti na zile zinazoonekana pale, hivyo mkristo au mtu yeyote anapozitumia anakuwa anapokea ile roho iliyopo nyuma ya vile viemoji, au anasambaza ile roho iliyopo nyuma ya emoji zile.
Je jambo hili lina ukweli?
Kabla ya kuona ukweli wa jambo hili, hebu tutafakari kwa pamoja jambo hili lingine.
Mtu anayetumia emoji fulani na kufikiri nyuma yake kuna alama/roho ya ibilisi je! anao uhakika gani kuwa ile herufu “A” au “B” au “C” anayoitumia kuandikia meseji kwenye simu/kompyuta nyuma yake hakuna roho ya ibilisi?.
Au ana uhakika gani kuwa herufi “Y” au “X” katika simu yake, nyuma yake haina alama ya ibilisi (freemason)?…na kwamba kila anapoandika ujumbe wenye herufi hizo anakuwa anasambaza roho ya ibilisi….je una uhakika gani kuwa haiko hivyo??…Kwa maana zote ni lugha za kompyuta.
Sasa kama mtu huyu ataona emoji zina shida na herufi anazozitumia (kama A,B,C ni salama (yaani hazina hatari yoyote)….basi bado hajatafakari vizuri.
Na kama ataona herufi pamoja na emoji zote za kwenye simu zimebeba roho nyuma yake basi matumizi yote ya simu si salama kwa mkristo, wala matumizi yote ya kompyuta, kwamaana yote yamejawa na hivyo vitu (viemoji na jamii ya hivyo)…kwamaana hata nembo ya whatsapp, au tweeter au application nyingine yoyote ya simu ni jamii ya hivyo vitu..
Sasa usalama upo wapi?… au tufanye nini? kama ile alama ya kibao cha barabarani nyuma yake ni alama ya freemason?..kama zile alama za msalani zinazoelekeza kuwa huku ni jinsia ya kiume na kule ya kike nyuma yake kuna roho ya ibilisi je tufanye nini?? (je tusitumie vyoo??)… tusitumie tena barabara?..tusinunue bidhaa zenye nembo hizo masokoni???..au tufanye nini?
Je tuondoke ulimwenguni???…maana kila mahali pana hatari (hakuna usalama)…
Yohana 17:15 “Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu”.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba matumizi ya herufi, au emoji katika simu au kompyuta si dhambi wala hazimwingizii mtu roho ya ibilisi, wala hazimsambazii mtu mwingine roho…ikiwa herufi hizo au emoji hazina maudhui ya machafu ya dunia.(kama zinaa, ushabiki, mizaha, magomvi, matusi n.k)
Lakini kama mtu atakuwa ni mchafu kwa utu wa ndani (maana yake hajatakasika)..hata pasipo matumizi ya hizo emoji kwake yeye yupo hatarini kupokea roho ya ibilisi na hata kusambaza kwa wengine, lakini kwa aliye mkamilifu hawezi kupokea roho kwa hizo wala kusambaza..
Lakini pamoja na hayo yote, si sharti kutumia hizo herufi wala emoji, wala si sharti wala amri kutumia simu wala kutumia kompyuta, wala chochote chenye alama hizo alama ikiwa mtu anapenda kujizuia na matumizi ya mambo hayo (kwa sababu zake binafsi) hafanyi dhambi.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
Print this post
Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”.
Je unaelewa maana ya kukaa ndani ya YESU (kuwepo ndani ya YESU) ??kwasababu ipo tofauti ya Bwana YESU kukaa ndani yako, na wewe kukaa ndani yake.
Kukaa ndani si Kumpa YESU maisha yako!!!…Ni zaidi ya hapo!.
Je ulishawahi kusikia mtu akisema “fulani nimemtoa ndani yangu kabisa au moyoni”..??
Utakuwa unaelewa maana ya hiyo kauli kwamba huenda katendewa kitendo kibaya sana, au cha kuumiza au kudhalilisha…ikasababisha kumtoa huyo mru moyoni kabisa.
Vile vile kuna mtu utamsikia akisema “mtu fulani yupo sana moyoni mwangu”…
Maana yake mpaka kusema hivyo huenda huyo mtu kamfanyia jambo jema sana au la kugusa moyo wake, au la kumvutia, mpaka kufanya aingie moyoni mwake.
Na Bwana YESU ni hivyo hivyo, kuna watu wapo ndani yake (moyoni mwake)..na kuna watu hawapo kabisa moyoni mwake ijapokuwa wanaweza kukiri wanaye…
Kwanini?..
Jibu: Kwasababu hawajawahi kuugusa moyo wa Bwana hata kumfanya Bwana awaweke moyoni mwake..watu hawa kibiblia hawapo ndani ya YESU na Kristo ingawa wanaweza kukiri kwamba wanaye Kristo moyoni, na Bwana atawakana siku ile kwamba hawajui.
Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. 22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? 23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.
Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.
Yafuatayo ni mambo (Matendo) ambayo mtu anaweza kuyafanya yakaugusa moyo wa Bwana YESU , hata kumfanya mtu huyo awe ndani ya KRISTO (moyoni mwake).
Hili ni jambo la kwanza linalomzamisha mtu kwenye moyo wa KRISTO.
Yohana 6:56 “Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake. 57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi”.
Yohana 6:56 “Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake.
57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi”.
Kamwe usiidharau meza ya Bwana, lakini pia hakikisha unashiriki kulingana na Neno lake..Kwa kufanya hivyo utauteka moyo wa Bwana kwa kiwango kikubwa sana.
2.UMOJA.
Hili ni jambo la pili linalouteka moyo wa Bwana sana na kumzamisha mtu ndani ya moyo wake.
Yohana 17:21 “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. 22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja. 23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Yohana 17:21 “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.
23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Hivyo jenga sana desturi ya kutafuta Umoja wa Roho, usipende kukaa peke yako peke yako (huendi kanisani, hushirikiani na wengine..ni hatari kubwa sana).
3. MATOLEO.
Kumtolea Mungu kwa hiari pasipo kulazimishwa wala kushinikizwa, ni kitendo cha tatu kinachougusa sana Moyo wa Bwana (hauwezi kutoka moyoni mwake daima).
Mathayo 26:12 “Maana kwa kunimwagia mwili wangu marhamu hiyo, ametenda hivyo ili kuniweka tayari kwa maziko yangu. 13 Amin, nawaambieni, Kila patakapohubiriwa Injili hii katika ulimwengu wote, tendo hilo alilolitenda huyu litatajwa pia kwa kumbukumbu lake”.
Mathayo 26:12 “Maana kwa kunimwagia mwili wangu marhamu hiyo, ametenda hivyo ili kuniweka tayari kwa maziko yangu.
13 Amin, nawaambieni, Kila patakapohubiriwa Injili hii katika ulimwengu wote, tendo hilo alilolitenda huyu litatajwa pia kwa kumbukumbu lake”.
Huyu mwanamke amekuwa ndani ya moyp wa Kristo kwa vizazi vyote, mpaka sasa tunavyozungumza.
Usikwepe matoleo (sadaka) shetani amevuruga sana eneo hili la matoleo kwasababu anajua endapo mtu akipata ufunuo mkamilifu basi ataingia ndani ya Kristo moja kwa moja.
Unyenyekevu ni wa kukiri makosa, na kurudi kitubu na kuyokurudia rudia machafu, ni tendo kubwa sana linamwingiza mtu ndani ya YESU.
Luka 23:40 “Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo? 41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa. 42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako. 43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”
Luka 23:40 “Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?
41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.
42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.
43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”
Na yapo mambo mengine mengi katika maandiko yanayomwingiza mtu na kumdumisha ndani ya KRISTO.
Zifuatazo ni faida za kuwa ndani ya KRISTO.
Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”
2.Tunakuwa viumbe vipya.
2 Wakorintho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya”.
Hasara za kutokuwa ndani ya KRISTO ni kinyume cha faida hizo.
Bwana atusaidie tuingie na kudumu ndani yake.
Maran atha.
NITASHINDAJE HALI YA KUUMIZWA NA MANENO YA WATU!
USIWE MKRISTO WA KUKAA TU GHALANI,
JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.
JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.
JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.
Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu Kristo, Karibu tujifunze habari njema za uzima wa roho zetu.
Neno la Mungu linatuambia..
2 Wafalme 19:30
[30]Na mabaki yaliyookoka ya nyumba ya Yuda yatatia mizizi chini, na kuzaa matunda juu.
Unaelewa maana ya mstari huu? Anazungumzia kustawi kwa nyumba ya Yuda (ambao ndio sisi kanisa)..
Lakini kustawi kwake hakuji hivi hivi, matunda yake kutokea kule juu, anasema kanuni yake ni lazima pia mizizi yake ikite chini.
Haiwezekani mti ukazaa kama hauna mzizi, jiulize je wewe una mizizi imara ya rohoni, ya kukufanya uweze kuzaa matunda yampendezayo Bwana?
Kumbuka kuthamini kwako wokovu, ndivyo hueleza urefu wa mizizi yako yenye nguvu, itakayokuwezesha kustawisha matunda juu.
Jani haliihitaji mizizi yoyote ya maana, kwasababu halina matunda ya kutoa.
Ukiona huwezi kuzama ndani katika wokovu, hauwi siriazi na maisha yako ya rohoni ujue pia hautakuwa na matunda yoyote kwa Mungu wako.
Katika ule mfano wa mpanzi Bwana Yesu alieleza kitu kilichofanya ile mbegu ya nne kustawi mpaka kuzaa matunda..anasema ilizaa kwa kuvumilia.(Luka 8:15)
kuvumilia nini?
Kuvumilia hatua zote 3 za mwanzo. yaani alihakikisha adui haibi mbegu iliyopandwa ndani yake, ni mtu ambaye aliweza kuvumilia dhiki, na majaribu yaliyozuka kinyume na lile neno lililopandwa moyoni mwake, alijiepusha na anasa, na kutoruhusu masumbufu ya ulimwengu huu kumsonga akashindwa kuivisha chochote. Hayo ndio mambo aliyovumilia.
Huyu ni mtu ambaye yupo makini na wokovu alioupokea.
Swali la kujiuliza je tunayo matunda hayo? kumbuka Hayaji kwa kutamani au kusubiri yanakuja kwa urefu wa mizizi yetu yenye uwezo wa kufikia vyanzo vya chini kabisa vyenye virutubisho vyote vya kustawisha matunda.
Ndio maana biblia inasema
Zaburi 1:1-3
[1]Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha. [2]Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku. [3]Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.
[1]Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
[2]Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.
[3]Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.
Anza sasa kushughulika na mizizi yako, mpaka ifikie kwa hakika mito hiyo ya maji.
Usipoe kimaombi, kimifungo, kiibada, kiuinjilisti, na kiusomaji Neno.
KWA KUVUMILIA AKAIPATA ILE AHADI.
Unajua Kwanini Naamani atake kuingia tena katika nyumba ya Rimoni baada ya kuponywa? (2Wafalme 5:18)
Turejee..
2Wafalme 5:18 “Jambo hili Bwana amwachilie mtumwa wako; bwana wangu akiingia nyumbani mwa Rimoni ili aabudu humo, naye akitegemea mkononi mwangu, nami nikijiinama nyumbani mwa Rimoni, hapo ninapojiinama nyumbani mwa Rimoni, Bwana amwachilie mtumwa wako jambo hili”.
Katika kitabu hiki cha 2Wafalme 5, tunasoma uponyaji wa mtu mmoja aliyeitwa Naamani, aliyekuwa Jemedari wa jeshi la mfalme wa Shamu. Lakini huyu Naamani alikuwa ni mtu mwenye ukoma ingawa alikuwa shujaa wa vita.
Siku moja alienda kutafuta uponyaji kutoka kwa Mungu wa Israeli, kupitia taarifa alizozipitia kutoka kwa kijakazi wake aliyekuwa Mwishraeli kwa asili, na alipokutana na Nabii Elisha, kwa uongozo wa Roho wa Mungu aliagizwa akajichovye katika mto Yordani mara saba na ugonjwa wake (wa ukoma) utaondoka.
Mwanzo alikataa lakini baadaye alikubali na Bwana MUNGU akamponya ule ukoma, na ngozi yake ikarudi kama ya mtoto mchanga.
2Wafalme 5:14 “Ndipo akashuka, akajichovya mara saba katika Yordani, sawasawa na neno lake yule mtu wa Mungu; nayo nyama ya mwili wake ikarudi ikawa kama nyama ya mwili wa mtoto mchanga, akawa safi”.
Kwa uponyaji huo alioupata aliahidi kutotoa tena sadaka kwa miungu aliyokuwa anaitumikia hapo mwanzo ambayo haikumsaidia kitu. (na mungu aliyekuwa anamtumikia hapo mwanzo kabla ya kuponywa na Bwana alikuwa anaitwa rimoni) .
2Wafalme 5:17 “Naamani akasema; Kama sivyo, lakini mtumwa wako na apewe mzigo wa udongo wa baghala wawili; kwa maana mtumwa wako hatatoa tena sadaka ya kuteketezwa wala dhabihu kwa miungu mingine, ila kwa Bwana”.
Lakini pamoja na ahadi hiyo, aliona tatizo moja mbele yake..
Alijua atakaporudi kwa mfalme, bado atakuwa chini ya mfalme kama jemedari wake, na mara zote alikuwa anaongozana naye kuingia katika hekalu la mungu rimoni, naye pia alikuwa anasujudu.. Hivyo akajua atakaporudi hiyo desturi itaendelea.
Kwahiyo akatangulia kuomba radhi kwamba endapo jambo hilo likitokea basi Mungu amsamehe (yaani amwachilie), kwasababu hajadhamiria kufanya hivyo isipokuwa tu ni kwa kutimiza matakwa ya mfalme, lakini yeye ndani ya moyo wake au kwa hiari yake mwenyewe hajakusudia kumtolea mungu rimoni sadaka wala kumsujudia..
Hivyo Elisha akamruhusu aende na afanye kama anayoyaona moyoni mwake.
Ni jambo gani tunalojifunza?..
Ni kweli kwa Naamani tunajifunza Imani ya kupokea uponyaji baada ya kukubali mashauri, kwani kitendo cha kuamini tu taarifa kutoka kwa kijakazi, hiyo ni Imani kubwa, (kwamaana si wote wanaweza kuwasikiliza na kuwaamini watu walio chini yao kiuwezo, kielimu na hata kiufahamu), lakini Naamani aliweza hilo..Na hata sisi ili tuvute msaada wa Mungu na muujiza wake ni sharti tuwe watu wa Imani kama Naamani.
Na ndio Bwana YESU anakuja kurejea habari ya Imani yake katika kitabu cha Luka 4:27
Luka 4:27 “Tena, palikuwa na wenye ukoma wengi katika Israeli zamani za nabii Elisha, wala hapana aliyetakaswa ila Naamani, mtu wa Shamu.”
Lakini pamoja na hayo pia, lipo ambalo hatupaswi kujifunza kwa Naamani,..
NAAMANI MOYONI ALIMKIRI MUNGU WA ISRAELI kwa muujiza aliofanyiwa LAKINI KWA MATENDO ALIMTUMIKIA MUNGU RIMONI kwa heshima ya Mfalme.
Kwahiyo alikuwa ni VUGUVUGU..Moyo wake upo kwa Mungu wa Israeli,…lakini viungo vyake na utumishi wake upo kwa rimoni (mungu wa nchi yake).
Mfumo wa nchi yake ulimbana!, kazi aliyoifanya ilimfunga!..ijapokuwa alikuwa anatamani kweli kutotumika katika hekalu la mungu ambaye hakumsaidia, lakini tayari alikuwa ameshafungwa Nira, na hakuwa tayari kuikata hiyo nira.
Katika kitabu kile cha 2Wakorintho 6:15 Neno la Mungu linasema, tusifungwe Nira pamoja na wasioamini kwa jinsi isivyo sawasawa.
2Wakorintho 6:14 “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? 15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini? 16 Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha”
2Wakorintho 6:14 “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?
15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?
16 Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha”
Na sisi kama wakristo ni lazima tutoke katika mahekalu ya sanamu, ni lazima tutoke katika kazi zinazotulazimu kusujudia sanamu au kumwabudu shetani, ni lazima tuache makundi yanayoturudisha kumwabudu shetani.
Ni kweli inagharimu, lakini hiyo ndio maana ya “kuubeba msalaba na kujikana nafsi”, kama kazi inakuuzisha pombe, au mwili wako, au inakuabudisha sanamu…IACHEEE!!. Ili uondokane na uvuguvugu. Kwasababu Bwana YESU alisema atawatapika wale wote walio vuguvugu.
Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. 16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa change”.
Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.
16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa change”.
KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.
Agano ni nini? na kuna aina ngapi za maagano?
MADHIHIRISHO MATATU YA MUNGU.
Orodha ya Miji ilivyojulikana Agano Jipya na inavyojulikana sasa
JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?
Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, karibu tujifunze maneno ya uzima.
Katika nyakati hizi za hatari na udanganyifu mwingi, ni vizuri kujichunguza sana, ni Roho ipi umeipokea ndani yako. Kwasababu tabia unazozionyesha ni matokeo ya roho iliyopo nyuma yake, ikiwa wewe ni mpenda dunia basi roho ya dunia ipo ndani yako.
1Wakorintho 2:12 Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.
Vivyo hivyo ukijiona wewe ni mwizi, ujue roho ya wizi ipo nyuma yako.
Lakini maandiko yanasemaje kuhusu Danieli?
Yanasema ROHO BORA ilikuwa ndani yake.
Danieli 6:3 Basi Danieli huyo alipata sifa kuliko wakubwa na maliwali, kwa kuwa roho bora ilikuwa ndani yake; naye mfalme akaazimu kumweka juu ya ufalme wote
Maana yake ni kuwa Roho iliyozidi viwango, ndio iliyokuwa ndani yake.. Unajua mpaka inasema bora, maana yake zipo ambazo hazina ubora, kwa tafsiri nyingine “feki”, zenye mfano wa ile orijino. Ndicho shetani anachokibuni sana, ili awapoteze watu, wadhani wanaye Roho Mtakatifu, kumbe ni bandia.
Sehemu nyingine, inasema “Roho njema kupita kiasi”. Ilikuwa ndani yake..
Danieli 5:12 kwa kuwa roho njema kupita kiasi, na maarifa, na ufahamu, na uwezo wa kufasiri ndoto, na kufunua maneno ya fumbo, na kufungua mafundo, zilionekana katika Danieli huyo, ambaye mfalme alimwita Belteshaza. Basi na aitwe Danieli, naye ataionyesha tafsiri.
Umeona sifa ya roho hiyo ni lazima iwe ya ‘kupita kiasi’, sio ya kawaida, vinginevyo ni feki. Sifa za Roho wa Mungu, anapita kiasi. Katika ubora na wema.
Ndio iliyomfanya Danieli awe mkamilifu kama tunavyomsoma kwenye maandiko. Kiasi cha watu kutafuta kosa ndani yake, bila mafanikio.
Danieli 6:4 Basi mawaziri na maamiri wakatafuta sana kupata sababu za kumshitaki Danieli kwa habari za mambo ya ufalme; lakini hawakuweza kuona sababu wala kosa; kwa maana alikuwa mwaminifu, wala halikuonekana kosa wala hatia ndani yake.
Na mtu yeyote anayesema ameokoka, Roho hii naye ni lazima imkalie. Roho iliyo bora, na njema kupita kiasi. Uthibitisho wa kwanza wa Roho uliyempokea ni Roho Mtakatifu, atakusukuma, kuwa Mtakatifu kama jina lake lilivyo.
Lakini iweje tunasema, tumepokea Roho, tunanena kwa lugha usiku kucha, tunatabiri, lakini Ubora wa huyo Roho hauonekani ndani yetu? Cha kushangaza utaona huyo mtu anasema haiwezekani kuishi maisha matakatifu hapa duniani, ndio hapo tunamhubiri Kristo, wakati huo huo, tunaishi kidunia, tunafunga na kuomba wakati huo huo, tunavaa ovyo ovyo, tunaabudu pamoja lakini chini kwa chini tunavisasi na vinyongo. Tunatoa sadaka lakini nyuma kwenye biashara zetu ni za rushwa rushwa.
Je! Hiyo ni Roho bora? Au imechakachuliwa?. Tumepewa ruhusu ya kujipima (1Yohana 4:1). Jihakiki, tangu ulipookoka hadi leo je, kuna mabadiliko yoyote ndani yako? Kama huna ni aidha ulimzimisha alipokuwa anaugua ndani yako ugeuke, au huna kabisa Roho Mtakatifu.
Habari njema ni kuwa Roho bora, ukimwita, huja ndani yako, au huamka tena. Ni wewe kuamini, na kutii kwa moyo wako wote. Kuwa tayari kuacha vyote(vya kidunia), na kumgeukia yeye. Na hatimaye atakuongoza na kukuweka sawa. Lakini sharti kwanza uaminifu kuwa utakatifu unawezekana, lakini pia ulimwengu utaukana.
VIASHIRIA VINGINE VYA ROHO MTAKATIFU KUWEPO NDANI YAKO.
OMBA, TAFUTA NA BISHA.
JE UMEUPOKEA UWEZA WOTE WA UUNGU NDANI YAKO?
Swali: Sheshaki inayotajwa katika Yeremia 25:26 ilikuwa ni wapi?
Jibu: Turejee..
Yeremia 25:26 “na wafalme wote wa kaskazini, walio mbali na walio karibu, wote pamoja; na wafalme wote wa dunia, wakaao juu ya uso wa dunia; na MFALME WA SHESHAKI atakunywa baada yao. 27 Nawe utawaambia hivi, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nyweni, na kulewa, na kutapika, na kuanguka msiinuke tena, kwa sababu ya upanga nitakaoupeleka kati yenu”.
Yeremia 25:26 “na wafalme wote wa kaskazini, walio mbali na walio karibu, wote pamoja; na wafalme wote wa dunia, wakaao juu ya uso wa dunia; na MFALME WA SHESHAKI atakunywa baada yao.
27 Nawe utawaambia hivi, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nyweni, na kulewa, na kutapika, na kuanguka msiinuke tena, kwa sababu ya upanga nitakaoupeleka kati yenu”.
“SHESHAKI” ni jina lingine la Taifa la “Babeli”. Kama vile “YESHURUNI” ilivyo jina lingine la Taifa la Israeli.
Kumbukumbu 33:26 “Hapana aliyefanana na Mungu, Ee Yeshuruni, Ajaye amepanda juu ya mbingu ili akusaidie. Na juu ya mawingu katika utukufu wake”.
Soma pia Kumbukumbu 32:15 na Isaya 44:2, utaona Zaidi kuhusu Yeshuruni, na kwa urefu Zaidi fungua hapa >> Yeshuruni ni nani katika biblia?
Na vivyo hivyo na “Babeli”, jina lake lingine aliitwa “Sheshaki”… Majina haya yalitumika mara nyingi kwenye mashairi na methali za kiyahudi. Utalisoma jina hilo tena katika Yeremia 51:41, ambapo imetaja kwa uwazi kuwa ni Babeli.
Yeremia 51:41 “Jinsi Sheshaki alivyotwaliwa! Naye sifa ya dunia yote alivyoshambuliwa! Jinsi Babeli alivyokuwa ukiwa katikati ya mataifa. 42 Bahari imefika juu ya Babeli, Umefunikwa kwa wingi wa mawimbi yake. 43 Miji yake imekuwa maganjo; Nchi ya ukame, na jangwa; Nchi asimokaa mtu ye yote, Wala hapiti mwanadamu huko”.
Yeremia 51:41 “Jinsi Sheshaki alivyotwaliwa! Naye sifa ya dunia yote alivyoshambuliwa! Jinsi Babeli alivyokuwa ukiwa katikati ya mataifa.
42 Bahari imefika juu ya Babeli, Umefunikwa kwa wingi wa mawimbi yake.
43 Miji yake imekuwa maganjo; Nchi ya ukame, na jangwa; Nchi asimokaa mtu ye yote, Wala hapiti mwanadamu huko”.
Je Umeokoka?.. kama bado unasubiri nini?..
Maran atha!
NINAJUA MAWAZO NIKUWAZIAYO:
Babeli ni nchi gani kwasasa?
Mgawanyo wa Vitabu vya Biblia
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)
UFUNUO: Mlango wa 18
Bwana ametupa agizo na wajibu wa kwenda kuihubiri injili ulimwenguni kote, na kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi wake.(Mathayo 28:19)
Alisema pia mavuno ni mengi lakini watendakazi ni wachache. Ikiwa na maana lengo lake ni yeye apate mavuno mengi kutoka kwetu. Lakini huwenda tukaona sisi ni shida, kufanya hivyo.
Hata kama itakuwa kwetu ni shida kuvuta watu, bado Yesu anaona ni rahisi kwetu..Kwani mahali pengine alisema mashamba yameshakuwa meupe tayari kwa mavuno, wapo ambao tayari walishayataabikia, sisi ni kumalizia tu. Hivyo ni rahisi sana.
Lakini ili injili yetu itoe matokeo aliyoyakusudia, yatupaswa tujifunze kanuni zote za kiuinjilisti na kuzitumia, kisha miongoni mwa hizo Bwana azitumie kuleta matokeo yake. Kuliko kutegemea kanuni moja tu Fulani na kupuuzia nyingine.
Ni sawa na mvuvi ambaye anashikilia uvuvi wa ndoano tu, lakini hajui kuna wa nyavu, au wa mkuki au wa kutegea, lakini pia kuna wa majira mbalimbali ya kuvua, kuna ya usiku, au ya mchana.
Na sisi katika utumishi wetu wa kuwavuta watu kwa Yesu, tufahamu pia njia zote.
Sasa kibiblia zipo kanuni kuu (8), zinazovuta watu.
Hii ndio njia kuu na ya kwanza, ambayo ndio inasimama kama uti wa mgongo wa uinjilisti. Kwamba ni sharti kila mmoja wetu atumie kinywa chake, ujuzi wake, elimu yake, ufahamu wake, kumuhubiri Kristo kwa watu kwa namna yoyote. Utashuhudia shuleni, nyumba kwa nyumba, masokoni, barabarani, vijiweni, mitandaoni n.k. Ni agizo la Bwana na linapaswa lifanywe na wote.
Mathayo 5:16
[16]Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.
Wapo watu si rahisi kugeuka kwa kusikia unawaelezea habari za Yesu, ni rahisi kugeuka wanapomwona yule anayewahubiria mwenendo wake ni tofauti na wa kwao. Na hilo likamchoma moyo na kumfanya amgeukie Kristo moja kwa moja.
Hivyo angaza mwenendo wako, kwa watu, ikiwa hawataamini kwa lile Neno, basi waamini kwa mwenendo wako mzuri.
1Petro 3:1 Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; 2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu
Ni ile hali ya kujaribu kuchukuliana na mawazo ya wale watu, na wakati mwingine hali zao, kana kwamba ni mmojawao, kisha kutumia fursa hiyo kuwaeleza habari za Yesu. Wengine huvitiwa kwanza na jinsi unavyothamini hali zao, sio kwa jinsi unavyo eleza vema Neno au mwenendo wako. Ni njia ambayo aliitumia Paulo na ikamletea matokeo mengi sana ya waongofu.
1Wakorintho 9:19 Maana, ingawa nimekuwa huru kwa watu wote, nalijifanya mtumwa wa wote, ili nipate watu wengi zaidi. 20 Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria. 21 Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria. 22 Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu. 23 Nami nafanya mambo yote kwa ajili ya Injili ili kuishiriki pamoja na wengine.
1Wakorintho 9:19 Maana, ingawa nimekuwa huru kwa watu wote, nalijifanya mtumwa wa wote, ili nipate watu wengi zaidi.
20 Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria.
21 Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria.
22 Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.
23 Nami nafanya mambo yote kwa ajili ya Injili ili kuishiriki pamoja na wengine.
Zingatia kujichanganya sio kushirikana na dhambi zao, hapana, bali kuwepo katikati yao ili kuwaondoa huko, huku wewe mwenyewe ukijilinda nafsi yako usitekwe na dhambi zao.
Unaweza kudhani kila eneo unaweza kuhubiri na kuleta matokeo unayoyatazamia. sio kweli, Mitume walivua samaki usiku kucha lakini hawakupata kitu, baadaye Yesu akawaambia tupeni jarife upande wa kuume mtapata (Yohana 21), sehemu nyingine aliwaambia waende vilindini. Na walipofanya vile walipata samaki wengi. Paulo mwanzoni aliegemea injili yake kwa wayahudi sana, akapitia ukinzani, lakini kumbe Mungu alimkusudia aende kwa mataifa, na alivyotii agizo lile matokeo yakawa makubwa. (Matendo 22:21)
Hivyo ni muhimu kuomba Bwana akupe dira, lakini pia katika kuhubiri kwako utaona eneo Fulani lina matunda mengi, basi ujue hapo ni dira yako. Au njia Fulani ukiitumia wengi huvutiwa kwa Kristo, basi fanya hivyo. Lakini hili ni kuendelea kuomba na kuhubiri Mungu mwenyewe ataielekeza dira yako, kama ni hapo au kwingine, kama ni njia hiyo au njia nyingine, la kuzingatia ni kuwa mwepesi kutambua upepo wa Roho unakufanikisha wapi. Kisha ongeza nguvu nyingi sana hapo, kuliko kule kwingine.
Yapo makundi ambayo, Mungu anajua yakiona tu muujiza au ishara fulani huvutika kirahisi. Na hili pia ni eneo la kumwomba Bwana, ajalie kunyosha mkono wake kuponya maana lina mvuto mkubwa na wa haraka sana.
Kanisa la kwanza liliomba maombi ya namna hiyo.
Matendo 4:29 Basi sasa, Bwana, yaangalie matisho yao; ukawajalie watumwa wako kunena neno lako kwa ujasiri wote, 30 ukinyosha mkono wako kuponya; ishara na maajabu vifanyike kwa jina la Mtumishi wako mtakatifu Yesu
Hivyo popote uendapo pia hakikisha unawaombea na watu, shida zao. Kwasababu kwa njia hiyo Roho Mtakatifu hupata nafasi ya kupenyeza mvuto huo, kwao.
Busara ni namna nzuri kunena, hadi kuushawishi moyo wa mtu. Bwana Yesu anataka na sisi tujae busara ndani yetu aliyoifananisha na kama ile ya nyoka.
Mathayo 10:16 Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.
Nyoka alijua akimwendea Hawa kwa ukali, au kulazimisha isingewezekana, lakini alijishusha na kujifanya kama mtu wa mashauri, afichuaye siri, Jambo ambalo ni uongo. Na sisi hatuna budi kujua kunena kwa hekima, ili wale tuwahubirio tuishawishi mioyo yao, mpaka kumgeukia Kristo ambaye ndiye kweli. Tujifunze kueleza uzuri wa Yesu. Lakini pia tusiwe watu wa kauli mbaya kwa tunaowahubiria hata kama watatupinga.
Kuna la watu hatutaweza kulipata kama hatutaingia gharama kubwa kwa ajili yao. Wakati mwingine hata kuhatarisha maisha. Kwasababu mahali walipofungwa na adui, pana ngome nzito. Mfano wa hawa ni wale waliofungwa katika vifungo vikali sana vya kidini.
Kuwang’oa huko ni kujiandaa na dhiki. Cha kuomba hasaa hapa kwa Mungu ni ujasiri kwa kanisa la kwanza lilivyoomba.
Hichi ndio kilele cha juu kabisa cha kiuinjilisti. Ndio wito Yesu aliowaitia mitume wake utakaowafanya wafikie kona zote. Kuwa tayari kufa kwa ajili ya walio dhambini. Ndio maana si wote waliweza kuambatana nao, Bali walibakia tu kuwaadhimisha.
Matendo 5:12 Na kwa mikono ya mitume zikafanyika ishara na maajabu mengi katika watu; nao wote walikuwako kwa nia moja katika ukumbi wa Sulemani; 13 na katika wote wengine hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao; ila watu waliwaadhimisha;
Matendo 5:12 Na kwa mikono ya mitume zikafanyika ishara na maajabu mengi katika watu; nao wote walikuwako kwa nia moja katika ukumbi wa Sulemani;
13 na katika wote wengine hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao; ila watu waliwaadhimisha;
Kuna wengine si rahisi kuokoka ki-uinjilisti tu, bali pia kuwaombea. Hii ni njia inayolegeza nira za mwovu mioyoni mwa watu. Injili yako inaweza isiwe na shida lakini mioyo yao ya jiwe ikawa vile, hata uhubirije hawewezi kukuelewa.
Paulo alikuwa ni mtu wa kuwaombea sana watu wake wayahudi waokolewe. Maandiko yanasema ombeaneni ninyi kwa ninyi mpate kuponywa.
Warumi 10:1 Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe. 2 Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa.
Warumi 10:1 Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe.
2 Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa.
Usione shida kuwaombea ndugu zako ambao hawajaokoka, wafanyakazi wenzako, majirani zako, jamii yako n.k. Ni maombi yasiyo na ukomo fanya hivyo kila siku, maombi yako ni silaha kubwa sana ya kiuinjilisti. Lakini usiombe tu na kukaa ukasema namwachia Bwana. Hapana unawaombea na huku unawahubiria.
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba, tukijifunza njia zote hizi, na kuziachilia katika maisha yetu ya kiutumishi ni hakika kuwa lipo kundi litaokoka tu. Lakini kutegemea njia moja peke yake huubana utendaji kazi wa Roho Mtakatifu ndani yetu, . Ukihubiri changanya na hizo nyingine, kisha yeye aamue ni ipi itamvuta mtu kwa wakati huo.
KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI
UFUATILIAJI NI SEHEMU YA HUDUMA MUHIMU KWENYE UINJILISTI
TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO
NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?
2 Petro 1:3
[3]Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.
Kuna mambo makuu sana ya kujifunza ndani ya vifungu hivi;
Hapo tunaonyeshwa kuwa Mungu anao Uweza wake. Kama vile tu mwanadamu alivyo na uweza wake usiokuwa sawa na mbwa. Kwamfano mwanadamu anaweza kuunda silaha, ambayo inaweza teketeza mji mzima kwa maarifa yake. Anauwezo wa kuruka angani zaidi ya kiumbe chochote duniani kwa vyombo alivyovibuni, anaweza kuwasiliana na mtu aliye mbali sana hata na kuona uso wake kwa vyombo vya mawasiliana alivyojibunia.Mambo ambayo mnyama hawezi. Huo ni uweza wake wa kibinadamu.
Vivyo hivyo na Mungu wetu, anao uweza wake wa uungu, ambao ametukirimia sisi, Tunapoupokea huo tunakuwa na sifa kama zake.
Ndio hapo anasema…
“Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.
Lakini sasa nataka uone hapo uweza huo umeshushwa juu yetu, si katika kila kitu bali katika mambo mawili makuu.
1) La kwanza ni uzima.
2) la pili utauwa.
Yaani mambo yote yanayohusiana na uzima wetu, ametuwezesha yeye mwenyewe. Ndio maana kwa kumwamini Yesu tunapokea msamaha wa dhambi. Tunakuwa tumevuka kutoka mautini kuingia uzimani. Hatuangamii, tunakuwa na uzima wa milele ndani yetu.
Kwasababu Hatuna kifo ndani yetu, tunalala tu, kupumzishwa ili baadaye tuamshwe. Lakini Uzima huu hauwezi kuupokea kwa juhudi zako, au kwa elimu yako, au kwa matendo yako mema, au kwa dini yako nzuri, hapana..Ni zawadi ya Mungu kupitia Kristo Yesu. Pale unapomwamini tu, unapokea msamaha wa dhambi zako, kwa neema, huu ni uweza wake wa ajabu, ambao wanadamu wanausumbukia hawaupati, kwasababu mwanadamu hana matendo mema ya kutosha kuununua uzima. Isipokuwa Yesu tu peke yake alitununulia kwa damu yake.
Yohana 3:36
[36]Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia.
Lakini sio tu Uzima, uweza huo umetukirimia pia na katika Utauwa wote. Utauwa ni utakatifu.
Mtu ambaye hajaokoka hawezi yatoa maisha ya utakatifu ndani yake. Vinginevyo atajitahidi sana kwa kuutumikisha mwili kwa nguvu, na hatimaye atashindwa, au atafanya kinafki kama mafarisayo na waandishi, ambao walikuwa wananena mambo ambayo hawayatendi,.kwasababu uweza huu haukuwa ndani yao.
Utauwa haswaa ni kazi ya Mungu mwenyewe mioyoni mwetu kupitia Roho Mtakatifu. Ni pale mtu anapompokea Kristo kama mwokozi wake, kisha kukubali kumtii, kwa kujikana nafsi yake. Ndio hapo hapo yeye mwenyewe anakuongezea nguvu, ambayo inakufanya uyakimbie yale maisha ya kale ya dhambi. Lakini kumbuka hiyo inakuja kwa kukubali kumtii Yesu, kukubali kuwa kiumbe kipya. Wakristo wengi wanataka Bwana awasaidie lakini hawataki kujikana nafsi zao wasaidiwe na Bwana. Ukimpokea kwa mdomo tu uweza huu hautakuwa na matunda ndani yako. Lakini ukiwa ni wa geuko la kweli, uweza huo ni lazima utende kazi ndani yako.
Utaweza kushinda zile dhambi ambazo ulikuwa huwezi ziacha.
Yohana 1:12
[12]Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;
Unaposema Yesu ni BWANA wangu. Ni lazima, ujue unajifanya kuwa mtumwa wake.. sikuzote bwana yoyote humiliki mtumwa, chochote anachoagizwa.huwa ni amri kwake sio ombi. Kumbali kuongozwa na Yesu, acha kabisa wokovu wa mdomoni.
Kama mkristo, kuwa mtakatifu ni lazima sio chaguzi, ndio kitambulisho chako kuwa umepokea uzima wa milele. Kwasababu pasipo huo huwezi kumwona Mungu (Waebrania 12:14).
Hakikisha uweza wote huu umeupokea ndani yako. Usiseme hicho kingine cha utakatifu hakinihusu, vinginevyo utakuwa hujakamilika
Shalom.
Bwana akubariki
INJILI NI UWEZA WA MUNGU, UULETAO WOKOVU.
Je! Utatu mtakatifu upo kibiblia?
Hebu tengeneza picha umeajiriwa, halafu aliyekuajiri anakutumikisha kwa mateso makali na mwisho wa siku anakulipa mshahara wa kifo!, Je kabla ya kuanza hiyo kazi, utakubali kutia sahihi mkataba huo??
Bila shaka kwa mtu mwenye akili timamu, hawezi kukukubali.
Lakini ajabu ni kwamba Zaidi ya nusu ya wanadamu wa kizazi chetu, wametia sahihi na huyu boss, ambaye anawatumikisha halafu anawalipa mshahara wa kifo. Je unataka kumjua huyu boss mkatili, na tena mwenye mshahara mbaya wa kifo?.. Biblia imemtaja ni nani katika Yohana 8:34-35 na Mshahara wake ni upi katika Warumi 6:23.
Yohana 8:34 “Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambia, Kila atendaye dhambi ni MTUMWA WA DHAMBI”.
Mtu anayetenda dhambi, tajiri wake ni DHAMBI!.. Dhambi ni boss mbaya asiye na huruma…na huu ndio mshahara wake..
Warumi 6:23 “Kwa maana MSHAHARA WA DHAMBI NI MAUTI….”.
Huyu boss hamdhulumu mtu, bali “anamlipa mtu mshahara tena kwa wakati”… kwasababu kila anayefanya kazi anastahili malipo biblia inasema hivyo katika (Luka 10:7 na 1Timotheo 5:18).
Dhambi inaua.., dhambi inaua.., dhambi inaua…, dhambi inaua..! Dhambi inaua,..Dhambi inaua…
> Dhambi inaua ule Upendo mdogo uliopo ndani yako
> Yale mahusiano madogo uliyoyaanza na Mungu wako, dhambi inayaua, inakusababisha kabisa usioune uso wa Mungu,… Tena biblia inasema inasema “Inafarikisha”…kufarikisha sio “kufarakanisha”… Kufarikisha inatokana na neno “kufariki” yaani “kufa/kutengwa”
Isaya 59:2 “lakini maovu yenu YAMEWAFARIKISHA ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia”
> Dhambi inaua “furaha” ndogo na kubwa uliyonayo..
> Dhambi inaua “amani” na kuleta hofu.
> Dhambi inaua “wema” mtu alionao.
> Dhambi inaua “ndoa”
> Dhambi inaua huduma/karama/kipawa.
> Dhambi inaua “Heri” za mtu.
> Dhambi inaondoa “Baraka” za mtu
Mwisho dhambi inaua “Mwili”….. huyu ni boss asiyefaa, mwenye mkataba Mbovuuu!!!!…Tumkimbie! Na kumwendea Bwana YESU, ambaye yeye anasema Nira yake ni laini na mzigo wake ni mwepesi, nasi tutapata raha nafsini mwetu (Mathayo 11:28).
Tukimkimbilia Bwana YESU anatufungua kutoka kwa huyu mwajiri mbaya (dhambi) na kutuweka huru.
Yohana 8:35 “Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote. 36 Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”
Yohana 8:35 “Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote.
36 Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”
Bwana YESU anatulipa UZIMA badala ya KIFO…. na si Uzima tu, bali UZIMA WA MILELE.
Bwana anamlipa mtu uzima katika Nafsi yake.
Unaongeza uzima juu ya upendo wa mtu, lakini dhambi inaua!
Bwana YESU anaongeza Uzima juu ya Amani ya mtu, lakini dhambi inaua!
Bwana YESU anaongeza Uzima juu ndoa ya mtu na maisha kwa ujumla, lakini dhambi inaua!
Na Zaidi ya yote, Bwana YESU anamlipa Mtu UZIMA WA MILELE (Yaani maisha baada ya hapa)..Kwanini tusimchague huyu??.
Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.
Je unaye tayari?..kama bado unangoja nini?.. kwanini dhambi ikukaushie uzima wako wa hapa duniani na ule wa milele ujao??..na matunda ya dhambi ni yale yote yaliyotajwa katika Wagalatia 5:19-20.
Wakati uliokubalika ni sasa, mkaribishe YESU leo maishani mwako akuweke huru.
Ikiwa bado hujampokea Bwana YESU na unahitaji msaada huo basi wasiliana nasi, tutakusaidia buree.
TENDA JAMBO LA ZIADA.
ROHO MBAYA KUTOKA KWA BWANA.
Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.
Wote wanaokumbwa na mauti sasa ni kutokana na dhambi zao?
UFALME WAKO UJE.
bofya, juu, “download” ufungue makala yake usome..
KILINDI CHAPIGIA KELELE KILINDI.