Category Archive Wahubiri (Watumishi)

KWANINI TUNAPASWA KWENDA KUIHUBIRI INJILI KWA UJASIRI WOTE?

Karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu, lililo taa na mwanga wa njia zetu.

Je unajua ni kwanini tunapaswa kwenda kuihubiri injili kwa ujasiri wote, tena pasipo woga wowote?.. na tena sio kwa watu baadhi tu, bali kwa watu wote wa dunia yote na katika kila mtaa, na wilaya, na mkoa, na Taifa, na kila bara?.. Ni lazima tukijue kitu kinachotupa ujasiri wa sisi kufanya hivyo!, tusipokujua hicho tutakuwa waoga wa kuhubiri.

Sasa hebu tusome maandiko yafuatayo..

Mathayo 28:18  “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, NIMEPEWA MAMLAKA YOTE MBINGUNI NA DUNIANI.

19  Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

20  na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari”

Hicho ni kipindi ambacho Bwana Yesu aliwatokea wanafunzi wake baada ya kufufuka kwake.. Na siku hiyo alipowatokea alikuja na agizo maalumu kwao!.. Na agizo lenyewe ni hilo la “KWENDA KUHUBIRI INJILI DUNIANI KOTE”.

Lakini agizo hilo ni gumu na zito!.. Yaani kwenda ulimwenguni kote kusema habari za Masihi, kwenda katika jamii za watu wabaya, na wakatili na wauaji, kwenda katika jamii za wasomi na watawala, na tena ulimwenguni kote?, hilo jambo si jepesi hata kidogo!.

Sasa Bwana Yesu alijua hilo jambo sio dogo wala sio lepesi, hivyo akatanguliza kwanza SABABU za kwanini awaagize kwenda duniani kote, katika mitaa yote, na miji yote na vijiji vyote na kwa watu wote wakawahubirie watu..

Na sababu yenyewe ndio tunayoisoma katika mwanzoni mwa mistari hiyo.. hebu tusome tena mstari wa 18..

Mathayo 28:18  “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, NIMEPEWA MAMLAKA YOTE MBINGUNI NA DUNIANI.

19  Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu”

Hiyo sentensi ya kwanza kwamba “amekabidhiwa mamlaka yote mbinguni na duniani” ndio iliyowapa ujasiri Mitume wake kwenda kuhubiri injili kila mahali.

Hebu tafakari leo hii umetumwa kupeleka ujumbe kwa watu Fulani katika mkoa Fulani, halafu aliyekupa huo ujumbe ni mtu tu wakawaida..bila shaka itakuwa ni ngumu kwako kupeleka ujumbe kwa jamii ya hao watu kwasababu kwanza huenda wana nguvu kuliko wewe, hivyo ukiwapelekea vitu tofauti na itikadi zao au jamii zao ni rahisi kujitafutia madhara.. lakini hebu tengeneza picha ni Raisi ndio anakupa ujumbe uwapelekee watu Fulani, ni dhahiri kuwa mashaka yatapungua na ujasiri utaongezeka…kwanini?.. Kwasababu unajua kuwa Raisi amepewa mamlaka yote juu ya hii nchi!..

Vivyo hivyo na kwa mitume…waliposikia tu hayo maneno ya kwanza ya Bwana Yesu kwamba “amepewa mamlaka yote ya mbinguni na duniani” ikawa ni sababu tosha ya wao kuwa na ujasiri wa kwenda kila mahali, kwasababu wanajua kila mahali waendapo tayari ni milki ya Kristo, kwamba Kristo ana nguvu juu ya hilo eneo… na maana akawaambia waende kwasababu yeye atakuwa pamoja nao hata mwisho wa Dahari (yaani mwisho wa Nyakati). Na sasa tupo karibia na Mwisho wa Nyakati, Kwahiyo Kristo yupo na sisi pale tunapokwenda kuieneza injili.

Ndugu usisubiri Bwana Yesu akutokee na kukuambia nenda kahubiri!.. Tayari agizo lilishatoka miaka zaidi ya elfu 2 iliyopita… kwamba nenda kahubiri injili.

Wengi leo hii wanaogopa kwenda kuhubiri injili, kwasababu hawana vitu vya kuhubiri.. Bwana Yesu hakuwaambia wanafunzi wake wakanunue vyombo vya miziki kwanza, au spika au wapate nguo nzuri ndipo wakahubiri injili..hapana! kinyume chake aliwaambia wasibebe chochote kwasababu huko waendako watavipata vyote.

Na wewe unasubiri nini usiende kuhubiri injili? Ni wito gani unaoungoja?, ni sauti gani unayoingoja?.. na upako gani unaoungoja?…ni ujuzi gani unaousubiri?.. ukisubiri ufikie ujuzi Fulani au maarifa Fulani hutayafikia kwasababu kila siku tunakua kutoka utukufu hadi utukufu, hakuna siku tutasema tumeshajua!!.. kila siku tunajifunza..hivyo usiseme ngoja nifikia levo Fulani ndipo nikahubiri, hizo ni akili za kichanga!.. Nenda kahubiri injili..

Sasa unaanzia wapi kuhubiri injili?

Kabla ya kwenda mbali anza kuhubiri injili hapo hapo ulipo, kabla ya kufikiri kwenda nje ya mtaa anza katika mtaa wako, anza katika nyumba yako, anza katika ofisi yako, anza katika shule yako.. hakikisha hapo umemaliza kwanza na watu wameitii injili ndipo uende nje!.. na katika hatua hiyo ya awali kumbuka kuwa Kristo yupo na wewe, na kumbuka kuwa yeye amekabidhiwa mamlaka yote ya mbinguni na duniani, kwahiyo hakuna nguvu zozote wala mamlaka yoyote unayoweza kushindana na hilo agizo la Bwana Yesu.

Bwana Yesu akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

ENZI NA MAMLAKA AMEZIFANYA KUWA MKOGO

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

Ni sahihi kusema sikuitiwa kuhubiri ubatizo kama Paulo alivyosema (1Wakorintho 1:17)?.

TUNALINDWA NA NGUVU ZA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

Mtu yeyote aliyeokoka (Kwa kumaanisha kabisa), ni lazima Bwana ataweka huduma ndani yake, anaweza akawa mchungaji, au mwinjilisti, au mwalimu, au mwimbaji, shemasi, lakini pia anaweza akawa  mwandishi, mtunza bustani, mratibu wa vipindi, mwasibu wa kanisa,  n.k. maadamu tu zinafanya kazi ya kulihudumia kanisa  la Mungu, na si vinginevyo.

Licha ya kuwa utaifurahia kazi yako na kupata thawabu, lakini uhalisia wake ni kwamba, huduma yoyote Mungu anayokupa haitakuwa nyepesi kama wewe unavyoweza kudhani, yaliyowakuta mitume wakati fulani, yatakukuta na wewe, lakini yatamkuta hata na Yule ambaye atakuja kutumika baadaye.

Haya ni baadhi ya maumivu utakayokutana nayo;

KUACHWA:

2Timotheo 4:10  “Maana Dema aliniacha, akiupenda ulimwengu huu wa sasa, akasafiri kwenda Thesalonike; Kreske amekwenda Galatia; Tito amekwenda Dalmatia”

Tengeneza picha, Wakati ambapo mtume Paulo yupo katika kilele cha utumishi, halafu mtendakazi mwenzake mpendwa, anageuka ghafla, na kumwachwa alijisikiaje. Ni heri angemwacha na kwenda kutumika mahali pengine, lakini anamwacha na kuurudia ulimwengu. Ni maumivu makali  kiasi gani? Ni kuvunjwa moyo kiasi gani?

Mwaka 2016-2018, tulikuwa na rafiki yetu mmoja, hatukudhani kama siku moja tungekaa tutengane, kwasababu tulikuwa tumeshajiwekea malengo mengi makubwa ya kumtumikia Mungu, tuliishi kama Daudi na Yonathani, lakini tulipoanza kupiga hatua tu ya kutekeleza malengo yetu, ghafla alikatisha mawasiliano na sisi, akawa hapokei simu zetu, na baadaye kutu-block kabisa, akaurudia ulimwengu, hadi leo.

Tuyahifadhi haya ili yatakapotokea tusivunjike moyo tukaacha utumishi. Wakina Dema unaweza kupishana nao katika huduma Mungu aliyoweka ndani yako, ila usivunjike moyo.

UPWEKE:

Pale pale Mtume Paulo anamsihi Timotheo asikawie kumfuata, kwasababu Kreske, amekwenda Galatia, Tito, Dalmatia..

2Timotheo 4:9  “Jitahidi kuja kwangu upesi. 10  Maana Dema aliniacha, akiupenda ulimwengu huu wa sasa, akasafiri kwenda Thesalonike; Kreske amekwenda Galatia; Tito amekwenda Dalmatia. 11  Luka peke yake yupo hapa pamoja nami. Umtwae Marko, umlete pamoja nawe, maana anifaa kwa utumishi. 12  Lakini Tikiko nalimpeleka Efeso.

Kundi hili halikuondoka, kwasababu ya kuupenda ulimwengu kama Dema, hapana bali kwasababu ya huduma, hivyo mtume Paulo akabaki peke yake. Kuna wakati alikuwa na kundi kubwa la watenda kazi pamoja naye, lakini upo wakati alibaki peke na Luka tu.. Anamhizi Timotheo afike  pamoja na Marko, ili afarijike katika huduma, hali ya upweke imwache.

Kama mhudumu wa Kristo, zipo nyakati utakuwa peke yako, Hivyo usife moyo, ni vipindi tu vya Muda.

KUACHANA:

Moja ya ziara za mtume Paulo iliyokuwa na mafanikio makubwa sana, basi ni ile ziara ya kwanza. Ni kwasababu gani? Ni kwasababu alikuwa na Barnaba. Wote wawili walikuwa na nia ya Kristo, hawakuwa na fikra za kiulimwengu au kimaisha. Lakini cha kusikitisha hilo halikuendelea sana.. Walipishana kauli, kutokana na kwamba kila mmoja aliona uchaguzi wake ni bora kuliko wa mwingine.. Paulo alitaka kwenda Sila, lakini Barnaba kwenda na Marko. Lakini kama wangetoa tofauti zao, na kuwachukua wote, naamini huduma ingekuwa na mafanikio makubwa zaidi, lakini hilo lilikuwa halina budi kutokea.

Matendo 15:36 “ Baada ya siku kadha wa kadha Paulo akamwambia Barnaba, Haya! Mrejee sasa tukawaangalie hao ndugu katika kila mji tulipolihubiri neno la Bwana, wa hali gani.

37  Barnaba akaazimu kumchukua Yohana aliyeitwa Marko pamoja nao.

38  Bali Paulo hakuona vema kumchukua huyo aliyewaacha huko Pamfilia, asiende nao kazini.

39  Basi palitokea mashindano baina yao hata wakatengana. Barnaba akamchukua Marko akatweka kwenda Kipro”.

Nyakati za kupoteza kiungo chako muhimu katika huduma utapishana nacho.

KUFANYIWA UBAYA:

2Timotheo 4:13  “Lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa, ujapo ulilete, na vile vitabu, hasa vile vya ngozi. 14  Iskanda, mfua shaba, alionyesha ubaya mwingi kwangu; Bwana atamlipa sawasawa na matendo yake. 15  Nawe ujihadhari na huyo, kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu”.

Haijalishi, utampendeza mtu kiasi gani, utafanya wema mwingi namna gani, bado wapo watakaokupinga tu utumishi wako, na zaidi watakuwa ni kama maadui zako. Ni jambo ambalo mtume Paulo hakulitarajia lakini alikumbana nalo baadaye, kutoka kwa Iskanda.. Yaliyomkuta Kristo Bwana wetu kutoka kwa mafarisayo yakamakuta na yeye. Na huwenda yatakukuta na wewe wakati Fulani mbele. Usirudi nyuma.

KUDHANIWA VINGINE:

Watu wengi wanaweza kuchukizwa na wewe kwasababu matarajio yao kwako ni tofauti na walivyokutegemea, hili lilianza tangu wakati wa Bwana alipokuwa duniani. Watu wengi waliosikia habari zake, ikiwemo Yohana mbatizaji, walimtazamia Bwana angekuja kama mfalme Daudi, akipambana na utawala sugu wa kirumi, akivaa nguo za kifalme, akiogopwa na kila mtu. Lakini aliposikia analala kwenye milima ya mizeituni, anaongozana na wavuvi, anakaa na wenye dhambi..Imani ya Yohana ikatetereka kidogo na kutuma watu ili kuulizia kama yeye kweli ndiye, au wamtazamie mwingine..Lakini maneno ya Bwana Yesu yalikuwa ni haya;

“Naye heri awaye yote asiyechukizwa nami” (Mathayo 11:6).

Vivyo hivyo na mtume Paulo, alitarajiwa na wengi kuwa atakuwa ni mtu mkuu kimwonekano, mwenye mavazi ya kikuhani kama waandishi, kutoka na sifa zake, na nyaraka zake, kuvuma duniani kote..lakini walipokutana naye walimwona kama kituko Fulani hivi;

2Wakorintho 10:10  “Maana wasema, Nyaraka zake ni nzito, hodari; bali akiwapo mwenyewe mwilini ni dhaifu, na maneno yake si kitu.

11  Mtu kama huyo na afikiri hivi, ya kwamba jinsi tulivyo kwa maneno katika nyaraka tusipokuwapo, ndivyo tulivyo kwa matendo tukiwapo”

Hivyo si kila mtu atapendezwa na jinsi atakavyokukuta, wengine watakuacha au hawatakuamini kwasababu umekuja nje ya matarajio yao.

KUPUNGUKIWA:

Japokuwa vipo vipindi vyingi vya mafanikio, lakini pia vipo vipindi vya kupungukiwa kabisa. Paulo anamwagiza Timotheo pindi amfuatapo makedonia ambebe joho(Koti) lake, kwa ajili ya ule wakati wa baridi. Kama angekuwa na fedha ya kutosha wakati huo, kulikuwa hakuna haja ya kumwagiza, angenunua lingine tu alipokuwepo.

Mungu hawezi kukuacha, wala kukupungukia kabisa, atakupa, na kukufanikisha, lakini pia vipindi kama hivi utapishana navyo mara kwa mara na ni Mungu mwenyewe anaruhusu. Hivyo usitetereke.

Wafilipi 4:11  “Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hali yo yote niliyo nayo.

12  Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa. 13  Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”

KUUGUA:

Ukiwa mtumishi, haimaanishi wewe ni malaika, umejitenga na mateso ya hii dunia, Kazi hii itakufanya uumwe wakati mwingine, Timotheo alikuwa anaumwa mara kwa mara tumbo, kwasababu ya mifungo, kuhubiri sana, hivyo akashauriwa na Paulo atumie mvinyo kidogo kwa ajili ya kuweka tumbo lake sawa. Alikuwepo Epafrodito mtume, naye kwasababu ya injili, aliumwa sana, karibu na kufa lakini baadaye Bwana akamponya( Wafilipi 2:25). Elisha alikufa na ugonjwa wake.

Upitiapo vipindi vya magonjwa, usitetereke ukaacha utumishi bali jifariji kwa kupitia mashujaa hawa.

Hivyo, tukiyahifadhi haya moyoni, basi utumishi wetu hautakuwa wa manung’uniko au wa kuvunjika moyo, mara kwa mara. Kwasababu ndio njia ya wote. Hivyo tukaze mwendo katika kumtumikia Bwana, kwasababu malipo yake ni makubwa kuliko mateso tunayopishana nayo. Thawabu za utumishi ni nyingi sana,

Ufunuo 3:11  “Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako”.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

GHARAMA YA UFALME WA MBINGUNI.

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi kibiblia?

Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.

Je mbinguni itakuwa ni kuimba tu wakati wote?

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

KAMA MHUBIRI USIWE MFANO WA DIOTREFE.

Rudi nyumbani

Print this post

NAYAJUA MATENDO YAKO.

Mara kadhaa, Bwana Yesu kabla hajasema Neno lolote alianza kwanza na kauli hii “Nayajua matendo yako” Kwamfano Soma vifungu hivi uone alivyosema, (Ufunuo 2:2, 2:19, 3:1, 3:8).

Nikwanini aanze kwa kusema hivyo? Ni kwasababu anataka hilo tuliweke akilini, tufahamu kuwa yupo karibu sana na hatua zetu kuliko tunavyoweza kudhani, hususani zile ambazo tunafikiri kuwa yeye hazijui, au hazioni.  Tutawaficha wanadamu lakini yeye kamwe hatuwezi kumficha chochote.

Wewe ni mchungaji, unazini na washirika, unazungumza lugha za mizaha na wake za watu, unadhani Kristo hajui nia yako, halafu unasimama madhabahuni unahubiri habari za wokovu..Bwana anakupa onyo, tena kali sana, anayajua matendo yako, na hasira yake ipo juu yako.

Wewe ni mkristo, unasema umeokoka, umebatizwa, unashiriki meza ya Bwana, lakini kwa siri unatazama picha za ngono, unafanya uasherati..Ukija kanisani unasema Bwana Asifiwe! Tena bila aibu unasimama na madhabahuni kuimba..utamficha mchungaji, utawaficha washirika wote, utamficha hata na shetani..Lakini Yesu anayajua matendo yako nje-ndani..Anajua mnapokutania, mnapotekelezea mipango yenu miovu, anajua ni nini unachofanya unapokuwa chumbani mwenyewe.

Wewe ni mwanandoa, unaigiza kwamba unampenda mwenzi wako, muwapo pamoja, lakini akisafiri kidogo tu, mkiwa mbali, unachepuka, mke umetoa mimba nyingi, na huko nje wewe mume umezaa watoto, hata mkeo haujui, unadhani unamficha  nani rafiki? .

Leo hii lipo kundi kubwa la washirikina  miongoni mwa watakatifu, tukiachilia mbali wachawi, lakini cha ajabu hujawahi kumsikia hata mmoja akijivunia kazi yake hiyo au akijitangaza? Wameficha hirizi chini ya biashara zao, wana mazindiko kwenye nyumba zao, wanajifanya wana maadili na hodari wa kusema AMEEN!!..Lakini hawajui kuwa Bwana anayajua matendo yao.

Ufunuo 3:1  “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na hizo Roho saba za Mungu, na zile nyota saba. NAYAJUA MATENDO YAKO, ya kuwa una jina la kuwa hai, nawe umekufa.

2  Uwe mwenye kukesha, ukayaimarishe mambo yaliyosalia, yanayotaka kufa. Maana sikuona matendo yako kuwa yametimilika mbele za Mungu wangu.

3  Basi kumbuka jinsi ulivyopokea, na jinsi ulivyosikia; yashike hayo na kutubu. Walakini usipokesha, nitakuja kama mwivi, wala hutaijua saa nitakayokuja kwako”

Ndugu ni heri ukatubu, uwe na amani na Kristo katika nyakazi hizi za hatari, kwasababu ukiendelea na hali hiyo hiyo utakufa na kwenda kuzimu, na adhabu yako itakuwa ni kubwa sana.

Bwana anasema…

“Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema”. (Mithali 28:13)

Leo hii ziungame dhambi zako, usiyafiche moyoni hayo unayoyafanya, wala usione aibu, wakati ndio sasa, hata kama umeshindwa kuacha, au hujui cha kufanya kwa uliyoyatenda, embu mfuate kiongozi wako wa kiroho mshirikishe akupe ushauri,.aombe pamoja na wewe,  Ili Bwana akusamehe makosa hayo uliyoyofanya.

Unachopaswa kufanya ni kutubu tu kwa kumaanisha..Ukiwa na nia kweli ya kuacha, ili Bwana atakusamehe na kukusaidia kuyashinda, lakini ukiwa upo vuguvugu, hueleweki, bado unayo hatia ya dhambi..kwasababu anayajua matendo yako.

Ufunuo 3:15  “NAYAJUA MATENDO YAKO, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16  Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa change”.

Jimimine kwelikweli kwa YESU akusaidie..Wakati wa Yesu kuyahukumu mambo yote ya sirini, umekaribia sana, Hukumu ipo karibu. Jiepushe nayo. (Warumi 2:16, 1Wakor 4:5). Ni wakati wa lala-salama.

Ikiwa utapenda kupata msaada huo wa kumkaribisha tena Kristo upya maishani mwako. Basi waweza wasiliana nasi kwa namba hizi kwa ajili ya mwongozo huo bure. +255693036618 / +255789001312.

Bwana akubariki.

Shalom. (Bwana Yesu anarudi).

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KUONGOZWA SALA YA TOBA

NINI MAANA YA KUTUBU

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

SEMA KWA LUGHA NYINGINE.

Kupiga ramli ni nini katika biblia?

Kumwambia mtu mwenye dhambi kuwa atakwenda kuzimu asipotubu Je! ni kuhukumu?

Rudi nyumbani

Print this post

KAMA MHUBIRI USIWE MFANO WA DIOTREFE.

Je! Unamjua Diotrefe katika biblia?

Diotrefe alikuwa ni kiongozi katika kanisa moja ambalo mtu wa Mungu ,Gayo alikuwa akishiriki. Kiongozi huyu alianza vizuri na Bwana lakini mwisho wake ulikuwa mbaya.. mpaka Mtume Yohana anamwandikia Gayo waraka juu yake,  ili asiziige tabia zake..

Hebu tumsome huyu Diotrefe jinsi alivyokuwa na tabia zake..

3Yohana 1:8 “Basi imetupasa sisi kuwakaribisha watu kama hao, ili tuwe watenda kazi pamoja na kweli.

9  Naliliandikia kanisa neno, lakini Diotrefe, apendaye kuwa wa kwanza kati yao, hatukubali.

10  Kwa hiyo, nikija, nitayakumbuka matendo yake atendayo, atoavyo upuzi juu yetu kwa maneno maovu; wala hatoshwi na hayo, ila yeye mwenyewe hawakaribishi hao ndugu, na wale watakao kuwakaribisha, huwazuia, na kuwatoa katika kanisa”.

Sasa hebu tuzitazame hizi tabia 4 Diotrefe alizokuwa nazo.

1: ANAPENDA KUWA WA KWANZA:

 Hii ni tabia ya kwanza Diotrefe aliyokuwa nayo;  Sasa Kupenda kuwa wa kwanza si jambo baya, lakini mtu anapotaka kuwa wa kwanza kwa lengo la kutukuzwa na watu, au kwa lengo la kuwatawala wa wengine, au kwa lengo la kutumikiwa.. hususani ndani ya kanisa, basi hiyo ni mbaya sana na ni kinyume na Neno la Mungu..

Kwasababu Bwana Yesu alisema..

Mathayo 20:25  “Lakini Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.

26  LAKINI HAITAKUWA HIVYO KWENU; BALI MTU YE YOTE ANAYETAKA KUWA MKUBWA KWENU, NA AWE MTUMISHI WENU;

27  NA MTU YE YOTE ANAYETAKA KUWA WA KWANZA KWENU NA AWE MTUMWA WENU;

28  kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi”.

Kwahiyo kama Mhubiri wa Injili: Katika nafasi yoyote uliyopo aidha ni Mchungaji, au Mwalimu, au Nabii, au Mtume au Mwimbaji kumbuka kuwa unapaswa uwe Mtumwa wa wote!, kama unataka kuwa wa Kwanza, lakini kamwe usijiinue wala usitafute utukufu wa wanadamu kama huyu Diotrefe. Ni hatari kubwa!

2. ANANENA MANENO YA UPUUZI  JUU YA MITUME

Hii ni tabia ya pili Diotrefe aliyokuwa nayo.. Alikuwa anawachafua Mitume wa Bwana Yesu (Ikiwemo Yohana, Mtume wa Yesu ambaye alipendwa sana na Bwana Yesu). Ijapokuwa aliwajua kuwa wamechaguliwa na Bwana lakini yeye aliwachafua kwa maneno mabaya na kuwafanya waonekane si kitu mbele ya kanisa la Mungu…Na hiyo yote ni kutokana na wivu.

Roho hii pia ipo kwa baadhi ya watu, ambao kutokana na Wivu, basi wapo radhi hata kuwachafua watumishi wa kweli wa Mungu, na huku mioyoni wakishuhudiwa kuwa wanawachafua ni watumishi wa kweli wa Mungu, lakini kutokana na wivu wanaendelea tu kuwachafua!,.. Hili ni jambo la kuzingatia sana  wewe kama Mwimbaji, au Mchungaji, au Mtume au Nabii au Mwinjilisti.

3. HAWAKARIBISHI NDUGU

Hii ni tabia ya tatu ambayo Diotrefe alikuwa anaionyesha katika kanisa… Yeye alikuwa ni kiongozi lakini kamwe hakutaka kupokea Watumishi wengine waliokuja kuhubiri katika mitaa yake, au mji wake, au waliokuwa wakipita njia yake kuelekea sehemu nyingine kuhubiri. Na sababu ya kufanya hivyo ni ile ile ya wivu na kutaka kuwa wa kwanza..

 Aliona kama mtu mwingine akija kuhubiri katika mji wake basi yeye hadhi yake, au heshima yake itashuka, na Yule alitakayekuja atatukuzwa zaidi..Hivyo hiyo roho ikampelekea mpaka kukataa kupokea wahubiri walio wageni.

Vile vile na sisi hatuna budi kuikataa hiyo roho kwasababu ni roho kutoka kwa Yule adui, siku zote hatuna budi kuwakubali na kuwakaribisha Watumishi wengine wanaotaka kuja kuhubiri maeneo tuliyopo, maadamu tumewahakiki kuwa kweli ni watumishi wa Mungu kwa Neno la Mungu, na wamekuja kwa nia ya kuhubiri injili.

4. ALIWAZUIA WATU WENGINE WASIWAKARIBISHE NDUGU

Hii ni tabia ya mwisho aliyoionyesha huyu Diotrefe.. Hakuridhika tu kuwakataa Mitume waliokuja kuhubiri pande zake, bali pia aliwakataza washirika wa kanisa lile wasimpokee mtumishi mwingine yoyote atakayekuja kuomba hifadhi kwao, kwaajili ya kuhubiri injili.. Na hakuishia hapo, bali aliendelea na kuwafukuza katika kanisa wale wote waliodhubutu kuwakaribisha Mitume. (Uone jinsi hii roho ilivyoenda mbali).

Lakini huyu Diotrefe hakuanza hivi.. Alianza vizuri tu!, ndio maana hata akafikia hatua ya kuwa kiongozi wa Makanisa (Huenda alikuwa Askofu).  Lakini roho nyingine ya kujiinua ilimwingia na ya kupenda kutukuzwa na watu na kuinuliwa, na akaipalilia mwishowe ikawa ni roho ya uadui mbaya sana na iliyoiharibu kanisa.

Na sisi hatuna budi kujifunza katika haya, ili tusijikute tunaangukia katika makosa hayo hayo ya Diotrefe (Ndio maana Mungu karuhusu kisa cha Diotrefe kiwepo katika biblia hata kama kwa ufupi sana). Ili tujifunze na tujihadhari na roho ya kujiinua, na kupenda utukufu wa wanadamu zaidi ya utukufu wa Mungu, na tama nyingine zote za kiulimwengu.

Bwana atusaidie tuwe kama Mzee Gayo aliyekubali kupokea mashauri hayo.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Ni sahihi kusema sikuitiwa kuhubiri ubatizo kama Paulo alivyosema (1Wakorintho 1:17)?.

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

Rudi nyumbani

Print this post

Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?

SWALI: Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa? Kwani kunaendelea mabishano baina ya wakristo baadhi, wengine wanasema kwasasa huduma hizo hazitendi kazi tena kufuatana na andiko la Paulo katika

Waefeso 2:20 linalosema; 

[20]Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni.

…Lakini wengine wanasema huduma hizo hadi sasa zipo katika kanisa. Je ukweli ni upi?


JIBU: Kabla hatujafahamu kwanza kama huduma za mitume na manabii zinaendelea hadi sasa au la!…tutazame kwanza aina za manabii wa mwanzo, na mitume wa mwanzo walikuwaje..

Manabii wa zamani walikuwa wamegawanyika katika makundi mawili. 

1)Manabii wa kutia msingi wa wakati wote

2)Manabii wa kuthibitisha misingi.

1 ) Hawa manabii wa kutia misingi; Ndio wote waliotiwa mafuta na Mungu kaandika biblia takatifu…mfano wa hawa ndio kama  Yeremia, Isaya, Nahumu, Malaki, Yoeli, Yona, Habakuki..n.k. Kwamba nabii zao zisimame kama msingi na mwongozo wa daima wa kuliongoza kanisa la Mungu wakati wote.. 

2 ) Manabii wa kuthibitisha: Hawa Mungu aliwanyanyua kutoa mwongozo wa wakati fulani tu mahususi.. Walikuwa wanasema Neno la Mungu lakini la wakati fulani tu ambapo ukishapita basi, unabii huo hauna umuhimu tena kwa vizazi vijavyo.

Mfano wa hawa utawasoma wengi sana..wakina Mikaya, Aguri, Odedi, Azuri,  Ahiya, pia katika agano jipya walikuwepo wakina sila, agabo..n.k

Vivyo hivyo tukirudi na  katika Mitume wa Kristo.

Wapo ambao waliotiwa mafuta kwa lengo la kuweka misingi ya daima. Hawa ndio wote tunaosoma nyaraka zao katika maandiko..mfano Paulo, Petro, Yakobo, Yohana, Yuda,  Mathayo, Luka.

Na wapo waliowekwa kwa ajili ya kutihibitisha / kutia misingi midogo.midogo. Mfano wa hawa ni Epafrodito Wafilipi 2:25..

Sasa tukishafahamu…hilo…tunaporudi katika lile andiko linalosema..mmejengwa juu ya misingi ya mitume na manabii tunaweza kuelewa

Tusome; 

Waefeso 2:20

[20]Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni.

Maana yake ni kuwa sisi kama kanisa tumejengwa juu ya mafunuo ya manabii watangulizi na mitume watangulizi wale waliochaguliwa kuweka misingi ya daima..(Yaani kwa lugha rahisi tumejengwa juu ya  BIBLIA TAKATIFU)…

Hakuna namna tutajengwa juu ya misingi mingine mipya zaidi ya hiyo yao.. Hivyo kwasasa hatuna manabii na mitume kama wale watangulizi, ambao walipokea mafunuo ya moja kwa moja ya namna ya  kulijenga kanisa la Kristo..ni sawa na kusema hatuna mitume mfano wa Paulo au Petro au manabii mfano wa Yeremia au Isaya, kwasasa.

Lakini wapo mitume na manabii wa nyakati ndogo ndogo, ambao wanafanya kazi za kuthibitisha misingi ambayo tayari ipo lakini sio wa kuleta jambo jipya duniani..

Kwamfano kazi mojawapo ya mitume ilikuwa ni kwenda kupanda makanisani mapya maeneo mapya..hivyo, mtu yeyote mwenye huduma.hii ndani yake, ni mtume lakini kazi yake itakuwa ni kutembea katika mstari ule ule wa mitume wa kwanza..hapaswi kuja na jambo lake jipya..anapaswa ahubiri kilekile mitume walichokifundisha, hapo atakuwa amekidhi kuitwa mtume.

Ni sawa na mtu anayejenga nyumba ya gorofa..msingi mkuu ni mmoja..ule uliopo chini…lakini akitaka aweke nyumba juu yake ni sharti afuata ramani ya msingi wa chini….

Ndivyo ilivyo kwa huduma hizi za kitume na kinabii.. Ni lazima zirejee katika biblia takatifu chochote kitolewacho lazima kionekane katika biblia sio katika maono yao wenyewe wanayojitungia.

Paulo aliandika maneno haya; 

1 Wakorintho 3:10-15

[10]Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake.

[11]Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo.

[12]Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri.

[13]Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani.

[14]Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu.

[15]Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto.

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa tofauti ya wale na hawa ni kwamba wote kazi yao ni moja ya upandaji wa kanisa la Kristo,mahali na mahali, isipokuwa wasasa hawaleti fundisho jipya, au maono mapya isipokuwa yale ambayo tayari yameshaanzishwa na mitume.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nitamjuaje nabii wa Uongo?

JE! UMECHAGULIWA TANGU ASILI?

Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?

Hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.

JINSI MTUME PAULO ALIVYOUTHAMINI WITO WAKE, JUU YA WENYE VYEO.

VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni sahihi kusema sikuitiwa kuhubiri ubatizo kama Paulo alivyosema (1Wakorintho 1:17)?.

Katika 1Wakorintho 1:17, Paulo anasema hakuitiwa kubatiza, Je na mimi kama sijaitiwa kubatiza, bali nimeitiwa kuhubiri watu waokoke tu!, nitakuwa na hatia, nisipohubiri suala la ubatizo wala kuligusia kabisa?


Jibu: Ni muhimu kufahamu kuwa  kila mtumishi wa kweli wa Mungu, haijalishi awe nani, ameitiwa KULIHUBIRI NENO LA MUNGU KATIKA UKAMILIFU WOTE, pasipo kubagua kipengele chochote katika maandiko. Huo ndio wito tuliopewa..

Tutatofautiana tu namna ya kuhubiri, kwasababu tunazo karama mbali mbali lakini INJILI NI MOJA KWETU WOTE!, Na wote tutahubiri kitu kimoja.. Hakuna mahali tumepewa maagizo ya kuhubiri tofauti tofauti au kulipunguza Neno la Mungu.

Sasa tukirudi kwenye swali, ni kwanini Paulo aseme sikuitiwa kubatiza?

Hebu tusome, mstari huo kwa utarati kisha tuendelee..

1Wakorintho 1:17 “Maana Kristo HAKUNITUMA ILI NIBATIZE, bali niihubiri Habari Njema; wala si kwa hekima ya maneno, msalaba wa Kristo usije ukabatilika”.

Hapa hakusema “MAANA KRISTO, HAKUNITUMA NIHUBIRI UBATIZO,” lakini badala yake anasema “KRISTO HAKUNITUMA NIBATIZE”. Maana yake kuhubiri Ubatizo Paulo alikuwa anauhubiri kama kawaida,(Soma Matendo 19:1-5 utalithibitisha hilo), lakini kitendo cha kufanya Ubatizo hakuwa anakifanya sana, bali mara moja moja sana… Ndio maana tukirudi juu kidogo katika mistari hiyo tunaona yeye mwenyewe anajishuhudia kubatiza watu baadhi..

1Wakorintho 1:14 “Nashukuru, kwa sababu sikumbatiza mtu kwenu, ILA KRISPO NA GAYO;

15 mtu asije akasema kwamba mlibatizwa kwa jina langu.

16 TENA NALIWABATIZA WATU WA NYUMBANI MWA STEFANA; zaidi ya hao, sijui kama nalimbatiza mtu ye yote mwingine”.

Umeona hapo anasema aliwabatiza Krispo, na Gayo Pamoja na watu wa nyumbani mwa Stefana.. Kuashiria kuwa alikuwa anabatiza, lakini hakuwa anaifanya hiyo huduma mara kwa mara, kulinganisha na huduma ya kwenda kuzunguka huku na huko kuhubiri Neno kwa watu aliyokuwa anaifanya.. Na wote walioamini injili yake aliwaongoza katika makanisa wabatizwe au watu maalumu wakabatizwe!..ili yeye apate nafasi ya kuendelea kuhubiri injili sehemu nyingine…Na ilipotokea hakuna mtu wa kuwabatiza kwa mahali hapo, basi alichukua yeye hilo jukumu la kuwabatiza!. kama hapo kwenye Matendo 19:2-6.

Ni sawa na jinsi Mitume walivyogawanya jukumu la kuwahudumia wajane, kwa wale Mashemasi 7 ili wao wadumu katika kulihubiri Neno.

Matendo 6:2 “Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, HAIPENDEZI SISI KULIACHA NENO LA MUNGU NA KUHUDUMU MEZANI.

3 Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili;

4 na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno.

5 Neno hili likapendeza machoni pa mkutano wote; wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, na Prokoro, na Nikanori, na Timoni, na Parmena, na Nikolao mwongofu wa Antiokia;

6 ambao wakawaweka mbele ya mitume, na walipokwisha kuomba wakaweka mikono yao juu yao”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba, Hakuna mtu yeyote ambaye ameitiwa kufundisha Neno moja la kwenye biblia na kuliacha lingine…Wote tunapaswa tuhubiri injili yote, iliyo kamili, yaani injili ya toba, ubatizo, Imani, Roho Mtakatifu, na mambo mengine yote ya kiimani, pasipo kupunguza chochote wala kuongeza. sawasawa na (Ufunuo 22:18-19).

Sababu kuu inayowafanya asilimia kubwa ya wahubiri wabague baadhi ya maneno kwenye biblia na kufundisha baadhi tu, ni kwasababu wanaogopa kuumiza hisia za watu au kupoteza waumini!, na wala si kitu kingine!!.. Jambo ambalo ni la hatari sana!.. kuacha kuhubiri Neno la Mungu kwasababu ya kohofia hisia za mtu, atajisikiaje, au atakuonaje.

Ni heri kuonekana hufai, lakini umelizungumza Neno la Mungu katika ukamilifu wote, Ni heri mtu ahuzunike moyoni kwasababu ya kweli ya Neno uliyomweleza, kwasababu itamuumiza moyo sasa, lakini baadaye itakuwa ni tiba kwake na atakuja kumshukuru Mungu sana kwaajili yako..

2Wakorintho 7:10 “Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti”.

Lakini unajua kabisa ubatizo aliobatizwa sio sahihi, mavazi anayovaa sio ya kiimani, kazi anayoifanya sio halali, na kwasababu unaogopa usiumie utakapomwambia ukweli, unaishia kumfariji kuwa wewe hujaitiwa kuhubiri ubatizo au Mavazi au kazi mtu anayoifanya, wewe umeitiwa kumhubiria amwamini Yesu tu!.. Fahamu kuwa ndio unazidi kumpoteza huyo mtu!.

Maran atha!

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Je! Ni kanisa lipi sahihi kumuabudia Mungu?

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

Rudi nyumbani

Print this post

Maana vitu vyote ni watumishi wako(Zaburi 119:91)

SWALI: Biblia inamaana gani kusema “ maana vitu vyote ni watumishi wako”?. Je wanaotumia vifaa vya upako kama vile chumvi, maji, udongo, kuombea watu, wanatimiza kusudi lile lile la Mungu kwasababu na vyenyewe vinafanya kazi ya Mungu kwa nafasi hiyo? Je kwa mujibu wa andiko hilo ni sawa?

Zaburi 119:90 “Uaminifu wako upo kizazi baada ya kizazi, Umeiweka nchi, nayo inakaa.

91 Kwa hukumu zako vimesimama imara hata leo, MAANA VITU VYOTE NI WATUMISHI WAKO”.


JIBU: Ni kweli kama andiko hilo linavyosema, vitu vyote tunavyoviona katika mbingu na  katika nchi ni watumishi wa Mungu, yaani, jua, mwezi, nyota, mawingu, milima, moto, maji, upepo, mafuta, udongo, mende, mbu, nzi, konokono, kipepeo vyote vinamtumikia Mungu.

Lakini swali ambalo tunapaswa tujiulize je vinamtumkia Mungu katika utumishi gani?

Ulishawahi kwenda kumuomba mjusi akusaidie kuomba rehema mbele za Mungu? Ulishawahi kuliomba jua likupe ridhki, ulishawahi kuamka asubuhi na kuuambia mwezi ukuponye magonjwa yako, na ukuepushe na ajali?

Kwanini usifanye hivyo, ilihali vyote vinamtumikia Mungu?.. Lazima ufahamu utumishi wao ni upi mbele za Mungu, kwa mfano, biblia inasema..

Zaburi 19:1 “Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, Na anga laitangaza kazi ya mikono yake”.

Ikiwa na maana kuwa tutazamapo mbingu na anga, basi tunahubiriwa utukufu wa Mungu kwa kupitia hivyo,  hapo tayari vimeshamtumikia Mungu, lakini hatuwezi kwenda kutumia mawingu ili Bwana atujibu maombi yetu.

Mungu kaweka njia kwa kila jambo, Na njia pekee ambayo alituchagulia sisi ili tumfikie Mungu, na kupokea wokovu wetu, na baraka zetu ni kwa kupitia YESU KRISTO tu na JINA LAKE Hapo ndipo tunapoweza kusaidiwa  mahitaji yetu, na dua zetu. Kwasababu hatuna jina lingine au kitu kingine chochote kiwezacho kutuokoa sisi isipokuwa Jina lake tu. . (Matendo 4:12)

Sasa wapo watu wanasema, mbona, Yesu alitumia udongo, mbona manabii walitumia chumvi,..Wanashindwa kuelewa yapo MAINGILIO YA MUNGU. Ambapo  Mungu mwenyewe upo wakati anashuka mahali Fulani kwa muda , kulitimiza kusudi lake Fulani, ndipo anapotumia chochote apendacho, kisha baada ya hapo hakuna kitu kingine cha ziada katika hicho kitu.

Ndio maana utaona wakati  ule alipomtumia punda kuzungumza na Balaamu, hatuona tena, punda wakitumika kuzungumza na watu, kana kwamba ndio kanuni, hali kadhalika, Elisha alipoambiwa alale juu ya yule kijana kisha atakuwa mzima, hatuona tena, tendo hilo likifanyika hadi leo hii, tukilala juu ya wagonjwa ili  wapate afya.

Ipo hatari kubwa sana ya kutumia vitu vya Mungu na kuvigeuza kuwa  ndio kanuni za uponyaji, kosa mojawapo lililowafanya wana wa Israeli Mungu achukizwe nao, hadi kupelekwa tena utumwani Babeli, lilikuwa ni kuitumia ile sanamu ya shaba, Musa aliyoagizwa na Mungu aitengeneze kule nyikani, watu waiangaliapo wapone.

Hivyo watu wasiomjua Mungu, na MAINGILIO YAKE YA MUDA, wakaigeuza kuwa ndio sehemu ya ibada, walipofika nchi ya ahadi wakaiundia madhabahu kisha wakaanza kumwomba Mungu kupitia ile, mwisho wa siku wakawa wanaabudu mapepo pasipo wao kujijua na matokeo yake wakapelekwa Babeli utumwani.

Hivyo nawe pia ukiona mahali popote uendapo, vitu kama hivyo vimefanywa kama kanuni, kila wiki ni maji ya upako, mafuta, chumvi, au kingine chochote, ujue kuwa huna tofauti na wale waabudu sanamu, na jua na mwezi, na unayemwabudu hapo sio Mungu bali ni shetani mwenyewe. Na Unamkasirisha Bwana sana.

Jina ambalo tumepewa sisi, tulitegemee kwa kila kitu, na kila saa ni jina la YESU KRISTO TU.. Hilo ndio uligeuze kuwa sanamu yako, na si kitu kingine chochote. Kama ulikuwa unafanya hivyo basi acha mara moja.

Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.

Hivyo, kwa hitimisho ni kuwa, mstari huo  haumaanishi  maji, au chumvi, au udongo, au kitu kingine chochote kinaweza kufanya shughuli ya upatanisho wa mwanadamu. Hapana ni uongo.  Vinamtumikia Mungu, lakini sio katika mambo ya wokovu wetu.

Bwana atuepushe na sanamu.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

NEHUSHTANI (NYOKA WA SHABA).

USIJARIBU KUMGEUZA MUNGU MGANGA WA KIENYEJI,UTAKUFA.

KWA KUWA WASEMA MIMI NI TAJIRI.

Bwana alimaanisha nini kusema“maana mtenda kazi astahili posho lake”

Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani,

Nini maana ya “chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu”?

Unyenyekevu ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Bwana alimaanisha nini kusema“maana mtenda kazi astahili posho lake”

Moja ya maagizo ambayo Bwana Yesu aliwapa wanafunzi wake alipowatuma kwenda kuhubiri injili mbali, lilikuwa ni kutokulipisha fedha katika huduma yoyote watakayoitoa, hali kadhalika   kutokubeba chochote katika safari yao. Yaani wasiwe na maandalizi yoyote ya njiani, Lakini mwishoni kabisa mwa maagizo yake aliyasema maneno haya “maana mtenda kazi astahili posho lake”.. Sasa swali linakuja Je hili posho ni lipi alilostahili huyu mtandakazi ili hali ameitwa atoe bure?

Mathayo 10:8 “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.

9 Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu;

10 wala mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, wala fimbo; maana mtenda kazi astahili posho lake”.

JIBU: Posho aliyostahili ni ile ambayo Bwana Yesu mwenyewe atampa katika kazi ya injili anayoipeleka, kwa kupitia watu wakarimu ambao Bwana Yesu mwenyewe atawagusa moyo huko waendako aidha kwa kuwapa maji, au chakula, au nguo, na wakati mwingine hata fedha.

Hiyo yote ni kuonyesha kuwa Bwana Yesu anaweza kumtunza mtumwa wake, katika mazingira yoyote atakayomtuma. Na ndiyo maana mwishoni kabisa akawaambia maneno haya;

Luka 22:35 “Akawauliza, Je! Hapo nilipowatuma hamna mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu? Wakasema, La!

Ni kufunua kuwa hatupaswi kuwa na wasiwasi wa maandilizi yoyote ya huduma ya Kristo, pale ambapo hatuna chochote,  Bwana anataka tuwe wepesi (SIMPLE), tusijali sana tutakula nini, tutavaa nini huko tuendako, kesho tutatolea wapi nauli ya kurudi, hilo jambo Bwana hataki sisi kama watumwa wake tulifikirie, kwasababu ameahidi kabisa ikiwa tunatenda kazi yake kiuaminifu, basi tumestahili posho yake, hivyo anza kutumika.

Lakini haimaanishi kuwa, wakati wote, hata kama unacho, ndio ujifanye hauna, hapana, bali, upo wakati wewe kama mtumishi wa Mungu utabarikiwa na utakuwa navyo vya kuendea huko katika ziara, hivyo vitumie hivyo, Na ndio maana wakati mwingine Bwana aliwaambia wajibebe fimbo ya njiani, na kujifungia viatu, wakati sehemu nyingine kama tuliyosoma hapo juu aliwakataza.(Marko 6:8-9)

Kwahiyo, kwa vyovyote vile, Bwana atatutunza, ilimradi tunamtumkia yeye kwa uaminifu. Tusiwe na wasiwasi na huduma yake, Haleluya..

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

ANGALIENI MWITO WENU.

WITO WA MUNGU HAUVUKI NENO LAKE.

MAAGIZO AMBAYO HAYAJAAGIZWA!

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA TITO.

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Mtu ambaye hajaoa anaruhusiwa kulichunga kundi?

SWALI: Shalom… Pastor naomba kuuliza je ni sahihi mtumishi kuongoza kanisa hajafunga ndoa? na anaweza kubatiza washirika? Amina.


JIBU: Kigezo cha mtu kuwa Kiongozi wa kanisa, na kufanya kazi zote za madhabahuni, ikiwemo kubatiza, kuwawekea watu mikono ya utumishi, n.k. vimetolewa katika kitabu cha 1Timotheo 3:1-7

1 Timotheo 3 : 1-16

1 Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema.

2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;

3 si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha;

4 mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu;

5 (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)

6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.

7 Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.

Askofu maana yake ni mwangalizi wa kanisa, Hivyo yeyote anayelichunga kanisa, awe ni mchungaji, mwalimu, Mtume, maana yeye ndio mwangalizi basi vigezo hivyo vinamuhusu.

Lakini katika vigezo hivyo vyote, hakuna hata kimoja, kinachosema, ni lazima aoe.. Isipokuwa anasema Askofu ni lazima awe ni mume wa mke mmoja..Akiwa na maana kwamba ikiwa ni mwana-ndoa basi, anapaswa awe ni mume wa mke mmoja, na si Zaidi, kama anao wake wawili au watatu, tayari ameshakidhi vigezo vya kutostahili kuitwa mchungaji.

Lakini ikiwa ni mtu ambaye, hajaoa lakini ameshika vigezo vyote, hivyo, yaani, ni mtu asiyelaumika, si mlevi, mpole, si mpenda fedha, aliyeshuhudiwa na watu ni mwema, amekomaa kiroho. Basi huyo anavigezo vyote vya kuwa mchungaji, au kiongozi yoyote wa kanisa.

Mtume Paulo hakuwa ameoa, lakini alikuwa ni mwangalizi wa makanisa yote yaliyokuwa Asia, na mataifa mengine, Na Zaidi sana yeye ndiye aliyetoa mwongozi wa mafundisho ya ndoa.

Hivyo kuoa/ kutokuoa, si takwa, la kuwa askofu.

Kinyume chake mtume Paulo,alishauri  watu wote wawe kama yeye (yaani wasioe), kwasababu watu wasiooa inawapa wigo mpana wa kumtumikia Mungu bila kuvutwa na mambo mengine, ikiwa wamemaanisha kweli kujikita kwa Bwana.

1Wakorintho 7:32 “Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;

33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe”.

Lakini ikiwa huwezi kuishi Maisha hivyo, kwa jinsi ulivyoitwa, basi hakikisha unatumika kiuaminifu, hapo utakuwa umekidhi vigezo vya kulichunga kundi , kubatiza, n.k.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Ndoa na Talaka

Ndoa ya serikali ni halali?

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

Uvuvi bora hauchagui wa kuvua.

Askofu na mchungaji mkuu ni nani?

WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.

Rudi nyumbani

Print this post

NJIA RAHISI YA KUMUHUBIRI KRISTO KWA MATAIFA.

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo. Ni siku nyingine tena Bwana ametupa neema ya kuiona, hivyo nakukaribisha sasa tuzidi kuyatafakari maneno matukufu ya Mungu wetu, Maadamu katujalia kuiona leo.

Kwanini leo hii imekuwa ngumu sana kuipeleka injili kwa watu walio nje, ili wamwamini Yesu Kristo (Tukisema walio nje, tunamaanisha watu wa kidunia, au watu walio katika dini nyingine), Tunaweza kusema Mungu anawajua walio wake, ni kweli, lakini hicho sio kisingizio, ipo sababu nyingine ambayo tumeikosa sisi kama kanisa na sababu yenyewe ni kukosa UMOJA.

Tukiupata huo kama kanisa basi hatutamia nguvu nyingi sana kuulezea ulimwengu uzuri wa Yesu, bali huo  umoja wenyewe tu utauaminisha ulimwengu yeye ni nani.

Bwana Yesu alilizungumza hilo katika..

Yohana 17:21 “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ILI ULIMWENGU UPATE KUSADIKI YA KWAMBA WEWE NDIWE ULIYENITUMA.

22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.

23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ILI ULIMWENGU UJUE YA KUWA NDIWE ULIYENITUMA, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.

Umeona, kumbe ulimwengu unaweza kumwamini Yesu, kuwa ndiye mwokozi wa ulimwengu, ikiwa tu tutajitengeneza sisi kwanza katika umoja. Lakini tunapaswa tujue si kila umoja, ni umoja sahihi unaotokana na Mungu..Hapo Bwana hazungumzii  umoja wa kichama au umoja wa kidini, au umoja wa kimadhehebu, kama unaoendelea sasa hivi ulimwenguni.. bali umoja anaouzungumzia hapo ni umoja wa Roho,. Kwasababu haiwezekani watu wawili wanaamini vitu viwili tofauti, halafu wawe na umoja, huo sio umoja utakuwa ni umoja wa kimaslahi tu, lakini sio wa Roho.

Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.

4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.

5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.

6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”.

Umeona vifungu hivyo? Agizo mojawapo ni kwamba tuutambue ubatizo mmoja na sahihi ni upi, kisha wote tuwe nao, ambao ni ule wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo sawasawa na Matendo 2:38, 8:16, 10:48, 19:5, kisha wote tumpokee Roho mmoja, ambaye ndiye Roho Mtakatifu, tuwe na Bwana mmoja ambaye ni YESU KRISTO jiwe kuu la pembeni, na sio mtume mwingine, au mtakatifu mwingine pembeni yake hapana,.. Na vilevile tuwe na Imani moja, ambayo mzizi wake na shina lake ni BIBLIA TAKATIFU na sio dini au dhehebu.

Tukizingatia hayo, kisha tukashirikiana na ulimwengu ukatuona, basi hatutatumia nguvu kubwa kuwaamishi Kristo kwao, kwani huo umoja wenyewe tu utawahubiria watu uzuri wa Kristo. Lakini tukizidi kuupoteza umoja huo, kila mtu na imani yake, dhehebu lake,. Ni ngumu sana kuugeuza ulimwengu. Hivyo ni wajibu wetu sisi, kama kanisa la Kristo tujipime, je! Umoja huu uliosahihi upo ndani yetu? Kama haupo, basi ipo kasoro. Tujitahidi sana tuunde kwa bidii zote, ili Bwana aaminiwe katikati ya mataifa, matunda mengi yaje kwake..

Hilo ni agizo la Bwana, na sio la mwanadamu.

“Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ILI ULIMWENGU UJUE YA KUWA NDIWE ULIYENITUMA, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.

Shalom.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post