Je madhabahu ni sehemu ya kufanyia mizaha, utani, vichekesho au vituko?..
Zaburi Sura ya kwanza kabisa na mstari wa kwanza unasema…
” Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha”.
Mtu anayefanya mizaha madhababuni au utani ni wazi kuwa hamheshimu Mungu..na hofu ya Mungu imeshaondoka ndani yake..hamwogopi tena Mungu…Yeye pale madhabahuni haoni tofauti na kumbi za kidunia. Na mtu akishafikia hali kama hiyo ni ngumu kutubu. Kama ilivyokuwa kwa wana wa Eli, ofni na Fineasi…waliidharau Nyumba ya Mungu na kuigeuza kituo cha kufanyia ukahaba..kwani walikuwa wanalala na wanawake waliokuwa wanahudumu katika hema ya Mungu(1Samweli 2:22)…Na walipoonywa hata hawakutaka kusikia.
Mithali 15:12 “Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa; Wala yeye hawaendei wenye hekima”.
Madhabahuni sio sehemu ya kufanyiana mizaha, sio sehemu ya kujipigia piga picha (selfie), sio sehemu ya kupigia stori, sio sehemu ya kulia chakula, sio sehemu ya kuchumbiana, wala si sehemu ya kusimama huku unatafuna vitu mdomoni…wala si sehemu ya kupanda pale na huku umevaa kihuni au kikahaba…
Kadhalika madhabahuni si sehemu ya kuchezea DANSI, Kwamba unapanda na kucheza kidunia…wala si sehemu ya kwenda kufanya vituko kama vile jukwaa la vichekesho…Ni sehemu ya Ibada kwa Mungu wetu..
Mungu wetu hashuki pale kuja kukutana na vichekesho vyetu au mizaha yetu, au utani wetu…. anashuka pale kuja kukutana na haja zetu na dua zetu na mahitaji yetu…Hivyo kuigeuza kuwa sehemu ya vichekesho na mizaha ni kumkufuru Mungu na hivyo kujitafutia laana badala ya baraka.
Hata madhabahu za mashetani huwa hazifanyiwi mizaha si zaidi madhabahu ya Mungu aliye hai?
Kumbuka pale ni sehemu iliyorasimishwa kwa Mungu muumba wa mbingu na nchi, aliye msafi na mtakatifu na wala asiyekuwa na mizaha..Hivyo kama yeye mwenyewe anapaheshimu na kushuka hapo inatupasaje sisi?..Ukisoma katika kitabu cha Ufunuo 4 utaona Mungu anaonekana ameketi katika kiti chake cha enzi huku akiwa amezungukwa na wazee 24..Wale ni wazee na sio vijana, ikimaanisha kuwa wamekomaa kiakili na wenye busara na si mizaha…Hao ndio wanaomsogelea Mungu mbinguni..
Na sisi tunapomsogelea Mungu katika nyumba yake hatuna budi kuivaa hekima kama ya wazee ili tuweze kumkaribia Mungu kwa baraka na si laana..kwasababu yeye hapendi mizaha na wanaofanya utani.. kwasababu anatuheshimu sana hivyo na sisi tunapaswa tumheshimu zaidi sana.
Kama ni mchungaji, mwalimu au Askofu…
>ACHA! kufanya mizaha madhabahuni mwa Mungu aliye hai.
>ACHA KUTUMIA MASAA KUCHEKESHA WATU BADALA YA KUTIMIZA WAJIBU WAKO WA KUHUBIRI INJILI KAMILI YA YESU KRISTO
>ACHA Kutaniana na watu madhabahuni..Siku ile utatoa hesabu kila Neno lisilo na maana linalotoka katika kinywa chako.
> Kama wewe ni muumini, Madhabahuni na hata kanisani kwa ujumla sio mahali pa kukatiza katiza bila kuwa na shughuli yoyote ya maana, wala si mahali pa kupiga piga makelele…Ufikapo nyumbani mwa Mungu paheshimu, zima simu yako.. Na ukae utulie..Hata kama ni mtoto wa mchungaji au mke wa Mchungaji…Huna Ruhusa ya kupageuza pale Nyumbani..Hiyo ni kwa faida yako binafsi.
BWANA WETU ANAKUJA.
Mada Nyinginezo:
Ni kwasababu ile ile kwanini Henoko alitwaliwa, na wengine wakabaki, Na Eliya alinyakuliwa na wengine wakabaki. Mungu aliruhusu kwa makusudi kabisa watu hawa wawe mfano wa mambo hayo ili kutupa sisi picha halisi kitakachotokea siku ile ya Unyakuo…Tukianzana na Henoko biblia imeshatupa majibu kabisa ni kwanini alinyakuliwa ..Inasema Ni kwasababu alitembea na Mungu (alimpendeza Mungu) kwa miaka mia tatu (Mwanzo 5:22).
Mwanzo 5:24 “Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa”.
Waebrania 11:5 “Kwa imani Henoko alihamishwa, asije akaona mauti, wala hakuonekana, kwa sababu Mungu alimhamisha; maana kabla ya kuhamishwa alikuwa ameshuhudiwa kwamba amempendeza Mungu”
Unaona Hawa ni watu ambao walivuka viwango vya kawaida vya kuishi Maisha ya kumpendeza Mungu tofauti na watu wengine..Na hivyo Mungu akaona si vema waendelee kuwepo mpaka siku ya mwisho ya uhai wao, akawatwaa. Ndivyo itakavyokuwa siku ile ya Unyakuo. Wengi tunavyodhani watakaonyakuliwa watakuwa ni wengi sana, kwamba hata kama mtu anaishi Maisha ya kutouthamini wokovu wake hapa duniani, naye pia atakwenda..Jibu ni hapana, watakuwa ni wachache sana nao ni wale watu ambao watakidhi hivyo vigezo vya kumpendeza Mungu kama Henoko…Soma Mathayo 7:14,na Luka 13:23.
Na ndio maana siku ile muda mfupi kabla ya kuja kwa Bwana biblia inatuonyesha kuwa kutakuwa na makundi mawili wa wakristo. Kundi la kwanza litajulikana kama wanawali wapumbavu, na kundi la pili litakuwa la wanawali werevu (Mathayo 25). Hawa werevu ndio wale ambao watatambua majira ya kujiliwa kwao, kutokana na dalili za mwisho wa dunia zinavyojionyesha, hivyo wataanza kutengeneza mambo yao sawa mapema kabisa kabla ya wakati ule kufika kama Henoko alivyojuwa kuwa dunia inakaribia kuangamizwa akatengeneza mambo yake sawa …
Hivyo ule wakati utakapokaribia na Mungu kuiona Imani yao , na utayari wao kuwa macho yao siku zote yapo mbinguni..Hao ndio watakaonyakuliwa na kutoweka ghafla..hawataonekana…Mungu atawaepusha na ile hukumu inayokuja pamoja na dhiki kuu.
Lakini wengine ambao ndio wale wanawali wapumbavu, wanasema wanamngojea Bwana lakini Maisha yao sio kama watu wanaomngojea Bwana kama biblia inavyotuasa katika Luka 12:35-36..Nusu dunia, nusu Mungu, hawajibidiishi kwa Mungu, wao wakishaokoka na kubatizwa hiyo tu inatosha,hakuna haja ya kujua Zaidi chochote kinachohusiana na Maisha baada ya hapa, kusikia habari za kwenda mbinguni kwao ni kama habari za kale,..Sasa hawa ndio siku ile watajikuta wameachwa…
Sasa Tukirudi kwa Eliya naye Kama vile Elisha alivyomshuhudia akiondoka mbele zake, na akalia kilio kikubwa sana..Ndivyo itakavyokuwa kwa kundi hili la wakristo hawa
vuguvugu,watakavyolia siku ile.. kwasababu siku hiyo watakuwa karibu sana na wale watakaonyakuliwa au watawashuhudia wakitoweka ..
Mathayo 24:40 “Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa;
41 wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa”.
Unaona, unabii huu utatimia siku hiyo kwao, kwasababu watakuwa karibu sana na wale watakaonyakuliwa kwasababu wote ni watu wa kanisani?. Je! Utajisikiaje siku ile yule jirani yako anayejulikana kama mlokole ambaye unajua alikuwa amejikana nafsi hayupo?..Huyo rafiki yako ambaye unaenda naye ibadani kila siku ghafla tu anatoweka mbele ya macho yako? Utajisikiaje..Kuona huyo mke wako/mume wako ambaye hakuruhusu Maisha ya dhambi yamkaribie usiku ule ukiwa naye nyumbani ghafla anatoweka..Utajisikiaje, tafakari ndugu kuona mchungaji wako aliyekuwa anakukemea kila siku habari za kuvaa vimini, na suruali, na uzinzi hayupo tena.. Itakuwa ni kilio na kusaga meno kwako wewe unayejiita mkristo lakini ni vuguvugu..Na cha kusikitisha ni kuwa kundi hili litakaloachwa litakuwa ni kubwa sana.
Wakati huo wenye dhambi hawataelewa chochote, watasikia tu uvumi, lakini kwao haitakuwa habari ya kushutua kama kwako..Wenyewe watasikia tu kwenye vyombo vya habari kuwa watu fulani wachache sana wamepotea lakini watapatikana,..kwasababu hawatakuwa wengi, kama tunavyodhani leo hii… kumbuka alinyakuliwa Henoko tu peke yake kati ya mamilioni ya watu waliokuwa duniani wakati ule, alinyakuliwa Eliya tu kati ya mamilioni ya watu waliokuwa duniani wakati ule..Vivyo hivyo watanyakuliwa wachache sana katika ya mabilioni ya watu waliopo duniani leo hii..
Huu sio wakati wa kumwangalia mjomba, au shangazi, au ndugu, ili kumfuata YESU, Huu ni wakati wa kujitwika msalaba wako wewe kama wewe. Sio wakati wa kusema mbona fulani yupo hivi, mbona mchungaji wangu anaishi vile.. kumbuka wewe sio yeye, na yeye sio Mungu kwamba unaouhakika siku ile atanyakuliwa..Fanya bidii wewe kama wewe kuutafuta uhusiano wako binafsi na Kristo ili siku ile isikupite. Vivyo hivyo na mimi ninafanya hivyo..Na mtu mwingine yeyote anayejiita mkristo anapaswa afanye hivyo. Kwasababu kwenda katika unyakuo sio lelemama..
Tusipumbazwe na kundi hili kubwa la wanawali wapumbavu tulionao katika ukristo. Sisi tusonge mbele na Bwana atakuwa pamoja na sisi hadi siku ile ya uyakuo itakapofika.
Ubarikiwe sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?
MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?
Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?
WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.
NDUGU,TUOMBEENI.
Ufunuo 16:15 “(Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.)”
Vazi ni kitu kinachositiri mwili…Mwili ukikosa mavazi unakuwa tupu/uchi. Na ni aibu kuwa uchi…Lakini pia upo utu wa ndani ambao nao pia unahitaji mavazi..ukikosa mavazi nao pia ni sawa na upo uchi na aibu yake huo ndio kubwa zaidi.
Katika hichi kipindi cha kumgoja Bwana..Biblia inatuasa tuhakikishe nafsi zetu zina mavazi yapasayo…na Mavazi yenyewe si mengine zaidi ya matendo mazuri ya utakatifu. Tunasoma hilo katika
Ufunuo 19:7 “Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.
8 Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu”.
Kitani inayozungumziwa hapo ni “vazi zuri refu la thamani na leupe”…Hivyo hilo ndio vazi la utu wetu wa ndani..Na ndio Vazi la harusi Bwana Yesu alilolizungumzia katika..
Mathayo 22:11 “Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa VAZI LA ARUSI.
12 Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? Naye akatekewa.
13 Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
14 Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache”.
Maana yake hakuna mtu atakayeingia katika karamu ya Mwana-kondoo mbinguni kama hana hilo vazi la harusi ambalo ni UTAKATIFU
Biblia inazidi kulisisitiza hilo katika kitabu cha Waebrania..
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;”
Unaona? Anasema “huo utakatifu”..maana yake “Hilo vazi”..pasipo kuwa nalo hakuna mtu atakayemwona Mungu.
Tunaishi kizazi ambacho watu wanasema hakuna watakatifu duniani…Na hiyo ni kutokana na watu kutoelewa nini maana ya utakatifu…utakatifu maana yake sio kujizuia kukanyaga sisimizi barabarani, au kujizuia kutokuchinja kuku…Hiyo sio maana ya utakatifu…Maana kwa viwango hivyo basi kusingekuwa na mtakatifu duniani….(Ukipenda kufahamu kwa urefu maana ya utakatifu fuatilia somo tuliloliandika kipindi cha nyuma kidogo lenye kichwa kinachosema ‘mtakatifu ni nani’ au kama itakuwa ngumu kulifikia unaweza kututumia ujumbe inbox tutakutumia).
Hivyo Nyakati hizi za mwisho wako wasiojua maana ya utakatifu na kadhalika wapo shetani aliowafumba macho wakidhani wao ni watakatifu na kumbe sio…wakidhani kuwa wana VAZI HILO LA HARUSI…kumbe hawana…wapo uchi..kama Bwana Yesu alivyosema katika ufunuo 3.
Ufunuo 3:16 “Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, NA UCHI.
18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, NA MAVAZI MEUPE UPATE KUVAA, AIBU YA UCHI WAKO ISIONEKANE, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona”.
Je unataka unayataka mavazi hayo uyavae na uchi wako usionekane?…Hatua za awali za kufanya ni kutubu na kumkaribisha Bwana Yesu moyoni mwako…Unatubu kwa kudhamiria kabisa kuacha ulimwengu na mambo yake yote…Unakusudia kuacha ulevi, uasherati, wizi, rushwa, anasa, utoaji mimba, usagaji, ufiraji, ulawiti, utoaji mimba, utazamaji picha na video za ngono, na mambo mengine yote ya kidunia..Na kisha ndio unamwambia Bwana akusamehe kabisa na Bwana Yesu atakusamehe kwasababu anatamani wewe utubu kuliko wewe unavyotamani…Na kama leo hii umeamua kufanya hivyo kwa kumaanisha kabisa…
Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, .
NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani … Hatua inayofuata ni Ubatizo, na kudumu katika Kujifunza Neno la Mungu..… VAZI HILO UTAKUWA UMEVIKWA katika roho yako…..Hivyo unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu Hiyo itakusaidia kuliweka safi vazi lako kila siku…. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Kumbuka haya maneno ya Bwana Yesu kila siku.. “Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.)”
Huu ni wakati wa kumalizia, hatuna muda mwingi..
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
Kwanini yule mtu hakukutwa na vazi la arusi wakati alialikwa?
WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.
USIMPE NGUVU SHETANI.
Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?
NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!
HAKIKISHA UNALIELEWA NENO.
Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?