Title January 2024

Kalafati ni nini? (Ezekieli 27:9)

Swali: Wenye kutia Kalafati ni watu gani?

Jibu: Neno “Kalafati” limeonekana mara mbili tu katika biblia, katika Ezekieli 27:9 na Ezekieli 27:27.

Na maana yake ni “Kamba nyembamba iliyotengenezwa kwa pamba” ambayo inawekwa katikati ya mianya ya mbao za merikebu, ili kuzuia maji yasipenye katika ile miunganiko. (Tazama picha juu)

Hivyo watu wanaofanya hiyo kazi ndio waliotajwa hapo katika Ezekieli 27:9,

Ezekieli 27:9 “Wazee wa Gebali na wenye akili wake walikuwa ndani yako, WENYE KUTIA KALAFATI; merikebu zote za bahari na mabaharia wao walikuwa ndani yako, ili kubadiliana biashara yako”.

Lakini habari hii inahusu nini?

Ukisoma kitabu hicho cha Ezekieli mlango wa 27 kuanzia mstari wa kwanza, utaona ni unabii unamhusu mfalme wa Tiro. (Kwa urefu kuhusu Taifa la Tiro fungua hapa >>>Miji ya Tiro na Sidoni ni miji gani kwasasa? 

Lakini hapa ni unabii wa Mfalme wa Tiro, Kwamba kwa kiburi chake na biashara zake nyingi alizozifanya juu ya nchi na katika bahari kupitia merikebu zake, siku inakuja ambapo ataanguka na kushuka chini kwasababu ya dhambi zake nyingi.

Na biashara za baharini alizokuwa anazifanya kupitia merikebu zake kubwa ambazo ndani yake kulikuwa na wana-maji, na “watiao Kalafati” na manahodha, zitaanguka na shughuli zao hizo zitaisha!

Ezekieli 27:27 “Mali zako, na bidhaa yako, na utajiri wako, wana-maji wako, na rubani zako, na WENYE KUTIA KALAFATI WAKO, na wafanya biashara wako, na watu wako wa vita wote, walio ndani yako, pamoja na jeshi lako lote lililo ndani yako, wataanguka katika moyo wa bahari katika siku ya kuangamia kwako”.

Ufunuo kamili pia kwa anguko la ulimwengu pamoja na dini zake za uongo katika siku za mwisho..

Ufunuo Ufunuo 18:2  “Akalia kwa sauti kuu, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli ule mkuu; umekuwa maskani ya mashetani, na ngome ya kila roho mchafu, na ngome ya kila ndege mchafu mwenye kuchukiza;

3  kwa kuwa mataifa yote wamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa nchi wamezini naye, na wafanya biashara wa nchi wamepata mali kwa nguvu za kiburi chake………………..

9  Na hao wafalme wa nchi, waliozini naye na kufanya anasa pamoja naye, watalia na kumwombolezea; wauonapo moshi wa kuungua kwake;

10  wakisimama mbali kwa hofu ya maumivu yake, wakisema, Ole, ole, mji ule ulio mkuu, Babeli, mji ule ulio na nguvu! Kwa kuwa katika saa moja hukumu yako imekuja.

11  Nao wafanya biashara wa nchi walia na kumwombolezea, kwa sababu hapana mtu anunuaye bidhaa yao tena;

12  bidhaa ya dhahabu, na fedha, na kito chenye thamani, na lulu, na kitani nzuri, na nguo ya rangi ya zambarau, na hariri, na nguo nyekundu; na kila mti wa uudi, na kila chombo cha pembe, na kila chombo cha mti wa thamani nyingi, na cha shaba, na cha chuma, na cha marimari;

13  na mdalasini, na iliki, na uvumba, na marhamu, na ubani, na mvinyo, na mafuta ya mzeituni, na unga mzuri, na ngano, na ng’ombe, na kondoo, na farasi, na magari, na miili na roho za wanadamu.

14  Na matunda yaliyotamaniwa na roho yako yamekuondokea; na vitu vyote vilivyo laini na vitu vya fahari vimekupotea; wala watu hawataviona tena kamwe.

15  Na wafanya biashara ya vitu hivyo, waliopata mali kwake, watasimama mbali, kwa hofu ya maumivu yake; wakilia na kuomboleza”

Je Umeokoka kwa kumwamini Bwana Yesu Kristo na kubatizwa, sawasawa na Marko 16:16?. Fahamu kuwa tunaishi katika siku za mwisho na Kristo amekaribia kurudi.

Kwa msaada Zaidi katika kumpokea Kristo fuatiliza sala hii ya Toba >>KUONGOZWA SALA YA TOBA  au wasiliana nasi kwa namba zetu zilizoanishwa mwisho wa somo hili.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.

Tarshishi ni mji gani kwasasa?

Mashonde ni nini? (Ezekieli 4:15).

Kuna tofauti gani kati ya  “Edeni” na “Adeni”?

Rudi nyumbani

Print this post

ONA FAHARI JUU YA BWANA.

Je! Unaona Fahari juu ya nini? Ni kitu gani unachokionea Fahari?.. Je ni mali?, ni vyeo?, au uwezo ulio nao?..


Kama Bwana amekujali kukupa hivyo vyote, basi mshukuru lakini usijionee fahari juu ya hivyo, kwasababu vyote hivyo ni “UBATILI”….bali ona FAHARI juu ya BWANA YESU kama umeshamjua!.

Kwasababu kumjua YESU ni UTAJIRI mkubwa, na CHEO kikubwa na UWEZO mkubwa.. kuliko utajiri wowote wa kiduni, wala cheo chochote cha kidunia wala uwezo wowote wa kidunia.

Maana yake Kama ni kuringa, au kutamba…basi tamba kwa kuwa UMEMJUA YESU!. (Furahia kwa kuwa umekipata kitu kikubwa na cha thamani, furahi kwa kuwa umelenga shabaha)..ndivyo maandiko yanavyotufundisha..

1Wakorintho 1:30  “Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu HEKIMA itokayo kwa Mungu, na HAKI, na UTAKATIFU, na UKOMBOZI;

31  kusudi, kama ilivyoandikwa, YEYE AONAYE FAHARI NA AONE FAHARI JUU YA BWANA”.

Hapo anasema YESU KRISTO amefanyika kuwa HEKIMA itokayo kwa Mungu, maana yake kama yeye  yupo ndani yetu, basi ni hekima ya Mungu imeingia ndani yetu. (sasa kwanini usione fahari juu yake kama yupo ndani yako)

Na tena amefanyika kuwa “HAKI”, Maana yake ni kwamba kama yeye yupo ndani yetu, basi tumepata haki ya kuishi milele, na kupata yote tunayoyahitaji ambayo ni mapenzi ya Mungu, (sasa kwanini usione fahari juu yake huyo kama yupo ndani yako?).

Na tena amefanyika “UTAKATIFU”.. Maana yake akiingia ndani yetu, tunahesabika na kuitwa watakatifu, (Kwanini usione fahari juu ya huyo).

Zaidi sana amefanyika “UKOMBOZI”. Maana yake anapoingia  ndani yetu, tunapata ukombozi wa Laana, na zaidi sana tunapata Kuokoka na hukumu ya milele ijayo, ya ziwa la moto aliloandaliwa shetani na malaika zake (Ufunuo 12:9)Kwanini usione fahari juu ya huyo aliyekupa ukombozi..

Aibu inatoka wapi!!!, ikiwa YESU KRISTO, aliye hekima ya Mungu yupo ndani yako?… Aibu ya kubeba kitabu chake (biblia) na kutembea nacho kikiwa wazi inatoka wapi? Ikiwa yeye ni mwokozi wako?

Aibu ya kuzungumza habari zake mbele za watu inatoka wapi? Ikiwa yeye ni Haki yako?… Aibu ya kushika amri zake inatoka wapi ikiwa yeye amekupa wokovu kutoka katika hukumu ya milele?.

ONA FAHARI JUU YAKE!.. wala usimwonee haya (aibu), maana alisema mtu akimwonea haya katika kizazi hiki yeye naye atamwonea haya mbele za malaika zake wa mbinguni.. Maana yake ni kwamba kama tukimwonea fahari, naye pia atatuonea fahari mbinguni (Marko 8:38)

ONA FAHARI JUU YAKE,…MTANGAZE KWA KUJITAMBA KABISA!.. MDHIHIRISHE KWA WATU, WAONE KUWA ULIYE NAYE NI KILA KITU KATIKA MAISHA YAKO!… Na itakuwa baraka kubwa kwako.

Wagalatia 6:14 “Lakini mimi, hasha, nisione fahari juu ya kitu cho chote ila msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo ulimwengu umesulibishwa kwangu, na mimi kwa ulimwengu”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Maana ya Mithali 19:11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake.

Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.

KWANINI NABII ISAYA ALIAGIZWA KUHUBIRI UCHI?

VAZI KUU AMBALO MUNGU AMETUANDALIA KILA MMOJA WETU.

Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 6:30 Watu hawamdharau mwivi, Akiiba ili kujishibisha

SWALI: Je!  Mithali 6:30 inamaana gani?

Watu hawamdharau mwivi, Akiiba ili kujishibisha, iwapo aona njaa;  31 Lakini akipatikana, atalipa mara saba; Atatoa mali yote ya nyumba yake.

JIBU: Chukulia mfano mtu hajala siku tatu, halafu akaona kuna duka lipo wazi pale jirani, na mwenyewe ametoka, akashawishika kuingia haraka  na kubeba mkate, ili akale. Lakini mwenye duka aliporudi na kuona mkate umeibiwa, alianza kumfuatilia, mwishowe akamkuta amejificha mahali Fulani anakula akiwa katika hali mbaya.

Kibinadamu, atakapoona hali halisi ya mwizi, huwenda ataishia kukasirika tu, au kumgombeza, au kwenda kumwajibisha, kwa mambo madogo madogo. Kwasababu anaona alichokifanya ni kwa ajili ya kusalimu maisha yake tu, ale asife, lakini sio kwa lengo la kuchukua vya watu, akauze, au kuleta hasara kwa wengine.

Lakini sehemu ya pili ya mstari huo anaendelea kusema kama “akipatikana atalipa mara saba; Atatoa mali yote ya nyumba yake”.

Maana yake ni kuwa kama “atapatikana na kosa”, basi atalipa mara saba. Atagharimikia vyote alivyoviiba mara saba. Sasa kauli hiyo haimaanishi kwamba mwizi huyo huyo aliyeiba kwa ajili ya kujishibisha tumbo lake ndio atalipa mara saba, hapana, vinginevyo mstari huo ungekuwa unajipinga unaposema “watu hawamdharau mwizi akiiba kwa kujishibisha”, bali  anamaanisha kama akipatikana na hatia tofauti na hiyo..mfano aliiba vitu ili akauze, aliiba fedha ili akajiendeleze kwenye mambo yake, alete hasara kwa wengine. Huyo atalipa gharama zote mara saba.

Ndio maana utaona adhabu nyingi za wezi huwa ni kubwa sana zaidi ya vile walivyoviiba, wanapigwa faini kubwa, wengine mpaka wanauliwa, kwa wizi tu mdogo. Hapo ni sawa na wamelipa mara saba.

Je! Hili linafunua nini rohoni?

Kama njaa ya mwilini, inaweza kumfanya mwizi asihesabiwe kosa. Kwasababu watu wanaelewa umuhimu wa kunusuru uhai kwa chakula, vipi kuhusu rohoni. Hata kuna wakati Daudi alikula mikate ya makuhani ambayo  hawakupaswa watu wengine kula, lakini kwasababu alikuwa na njaa yeye na wenzake haikuhesabiwa kwake kuwa ni kosa (1Samweli 21).

Vivyo hivyo rohoni, Mungu anatufundisha sio kwamba tuwe wezi, hapana, lakini anataka tuthamini sana roho zetu, pale zinapokuwa hazina kitu, zina njaa. Iweje mtu unakaa hadi unakufa kiroho halafu unaona ni sawa kuwa hivyo hivyo kila siku. Hufanyi jambo Fulani la kujinasua katika hiyo hali yako mbaya rohoni, unaendelea tu hivyo hivyo. Tafuta kwa bidii chakula cha kiroho usife ndugu. Jibidiishe.

Iba muda wako wa kufanya mambo mengine ili ukipate chakula cha kiroho. Ni kweli ulipaswa kuwepo mahali Fulani pa muhimu, embu ghahiri muda huo, nenda kasome biblia, nenda kaombe, nenda kasikilize mahubiri yatakayokujenga. Ulipaswa uwepo kazini, lakini kwasababu ibada ile ni muhimu embu usione shida kughahiri.

Huna biblia Iba hata pesa yako ya matumizi ya muhimu kanunue, acha uonekane mjinga nenda kanunue biblia au vitabu vya rohoni vikujenge. Tafuta ile MANA iliyofichwa.

Siku hizi ni za mwisho. Na Bwana alishatabiri duniani kutakuwa na njaa, sio ya kukosa chakula au maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Mungu ya kweli. Usipojiongeza katika eneo la ukuaji wako kiroho.  Ni ngumu kuvuka hizi nyakati mbaya  za manabii wengi wa uongo, na mafundisho ya mashetani. Usipoyajenga maisha yako ya kiroho, shetani akusaidie kuyajenga kwake.

Amosi 8:11 “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Bwana”

Penda biblia, penda kujifunza, penda maombi zaidi ya vingine.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

YEYE ALIYEUWASHA HUO MOTO LAZIMA ATALIPA.

NJAA ILIYOPO SASA.

(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

(Opens in a new browser tab)KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.(Opens in a new browser tab)

Rudi nyumbani

Print this post

MKUMBUKE TOMASO.

Nakusalimu katika jina la Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tuzitafakari habari njema.

Tomaso alikuwa ni mtume  wa Bwana. Lakini alikuwa na tabia ya kitofauti na wale mitume wengine 11. Yeye hakuwa msaliti kama Yuda, zaidi sana alikuwa hata radhi kufa na Bwana wake, kipindi Fulani aliposikia anatafutwa ili  auawe (Yohana 11:16), hiyo ni ishara ya upendo wake kwa Yesu.

Lakini alikuwa na tabia nyingine ambayo ilimgharimu kwa sehemu Fulani, Na tabia yenyewe ni mashaka juu ya uweza wa Mungu, ni hiyo ikapelekea hata kuathiri mahudhurio yake, ya kiibada na kiutendaji kazi pale alipolazimika kuwepo na wenzake kama mtume.

Hakutaka kuamini kwamba Yesu anaweza kufufuka, hivyo wakati huo alipoitwa waombe pamoja, hakuwa tayari kukusanyika na wenzake, alipoitwa awafariji watu yeye kama mtume wa Bwana aliyepewa mamlaka hiyo, hakutaka kufanya hivyo kinyume chake akaenda kuendelea na shughuli zake. Walipokuwa wanatafakari maneno ya Yesu, yeye mawazo yake yalikuwa mbali kabisa na wenzake. Ni kama alikuwa amechoka.

Matokeo yake ikawa Yesu alipowatokea mitume wake, walipokuwa wamejifungia kuomba, yeye hakuwepo. Hata walipokuja kumuhadithia bado hakuamini, kwasababu moyo wake ulikuwa umeshahama kabisa.

Yohana 20:24  Walakini mmoja wa wale Thenashara, Tomaso, aitwaye Pacha, hakuwako pamoja nao alipokuja Yesu. 25  Basi wanafunzi wengine wakamwambia, Tumemwona Bwana. Akawaambia, Mimi nisipoziona mikononi mwake kovu za misumari, na kutia kidole changu katika mahali pa misumari, na kutia mkono wangu katika ubavu wake, mimi sisadiki hata kidogo. 26  Basi, baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwamo ndani tena, na Tomaso pamoja nao. Akaja Yesu, na milango imefungwa, akasimama katikati, akasema, Amani iwe kwenu 27  Kisha akamwambia Tomaso, Lete hapa kidole chako; uitazame mikono yangu; ulete na mkono wako uutie ubavuni mwangu, wala usiwe asiyeamini, bali aaminiye.

Wewe kama mtumwa wa Yesu usiwe tomaso, wakutanikapo wenzako kamwe kataa kujitenga, hata kama hakuna tumaini, dumu na wenzako, epuka utoro, epuka udhuru, dumu hapo. Zipo nyakati ambazo Bwana hamtokei mtu kivyake-vyake, bali wawapo wote. Zipo Baraka, ipo neema, katika umoja na wenzako, kupo kumwona Mungu unaposhikamana na wenzako kiuaminifu, katika kujengana na kutiana moyo.

Kamwe usifikiri kivyako, kataa hiyo hali, Bwana anasema ajitengaye na wenzake anatafuta matakwa yake mwenyewe, Tomaso alikuwa hivyo. Lakini fikra zake hazikuwa sahihi, aliligundua hilo baadaye aliporudi kujumuika na wenzake, ndipo akamwona Bwana, alidhani angemwonea kule alipokimbilia. Dumu na wenzako maadamu Bwana wenu ni mmoja, Roho wenu ni mmoja, Ubatizo wenu mmoja. Hiyo inatosha. Dumu hapo.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Kwanini Tomaso atake kwenda kufa pamoja na Lazaro? (Yohana 11:14-16).

Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

KWANINI MITUME WAMUULIZE BWANA FARAGHANI?

Rudi nyumbani

Print this post

KIMBIA MACHAFU YA DUNIA. (2Petro 2:20)

2 Petro 2:20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia MACHAFU YA DUNIA kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza”. 

Mstari huo unatupa uelewa kwamba kumbe tukimjua mwokozi wetu Yesu Kristo, ni lazima kuambatane na kuyakimbia machafu ya dunia. Haiwezekani mtu akamjua Yesu Kristo halafu asiyakimbie Machafu ya dunia Kwa mujibu wa huo Mstari.

Machafu ya dunia ni yapi?

Machafu ya dunia ni Yale mambo maovu uliyokuwa unayafanya ulipokuwa mwenye dhambi, mfano ulevi, uzinzi, wizi, ushirikina, anasa, utoaji mimba, ulawiti,  n.k.

Sasa ikiwa ukinaswa, na kushindwa kutoka huko, maandiko yanasema hali yako ya mwisho inakuwa mbaya kuliko Ile ya kwanza, maana yake kama ulikuwa ni mgonjwa kidogo, kutokana na madhara uliyoyapata katika Ile dhambi, basi ugonjwa unakuwa mara dufu zaidi, kama ulikuwa unaweza kujizuia usilewe mara Kwa mara, basi nguvu ya ulevi inakulemea mara mbili unakuwa mlevi yule wa kupindukia kabisa kabisa.. hiyo ni kutuonyesha ni jinsi gani tunapaswa tuwe makini kama vile maandiko yanavyosema  pindi tuokokapo tuutimize wokovu wetu Kwa kuogopa na kutetemeka.

Wafilipi 2:12  “Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Bwana Yesu alitumia mfano wa Yule mtu ambaye alikuwa na pepo, lakini alipomtoka hakujiweka sawa, matokeo yake ikawa ni Yule pepo kuchukua pepo wengine saba waovu kuliko yeye, na hali yake ya mwisho ikawa mbaya kuliko ile ya kwanza. (Mathayo 12:43)

Lakini ikitokea tayari umeshaanguka kwenye machafu ya dunia, ambayo uliyaacha huko nyuma. Je ufanyaje?

Ni kutubu haraka sana. Angali nafasi unayo. Kumbuka hapo anasema “akinaswa na kushindwa”

Maana yake ni kuwa kama umenaswa, ni kufanya hima ujinasue kabla mwindaji wako (ibilisi), hajakuweka mikononi mwako kabisa kabisa. Lakini ukishindwa.basi Ndio mwisho wako umefika.

Ikiwa ulirudia uzinzi, ulirudia ulevi, ulirudia anasa, ulirudia kujichua, kutazama picha chafu mitandaoni.. Acha haraka sana, toka huko kwa kasi zote, jitakase kwa Bwana, kisha maanisha kumfuata Yesu, huku ukiutimiza wokovu wako kwa kuogopa na kutetemeka, kwasababu huo tumekabidhiwa mara moja tu.

Na Bwana atakurehemu.

Bwana akubariki.

Ikiwa bado hujaokoka na utapenda leo kumpokea Kristo maishani mwako. Basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Wokovu wa milele/ Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?

MFALME ANAKUJA.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.

TABIA ZITAKAZOMTAMBULISHA MPINGA-KRISTO AJAYE.

Rudi nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Warumi 14:7 hakuna mtu miongoni mwetu aishiye kwa nafsi yake.

SWALI: Warumi 14:7 Inamaana gani?

“Kwa sababu hakuna mtu miongoni mwetu aishiye kwa nafsi yake, wala hakuna afaye kwa nafsi yake”. 

JIBU: Ni andiko linalotuonyesha uweza wa Mungu ulivyo wa kutawala/ kuendesha vitu vyote. Kwamba mwenye maamuzi yote yahusuyo maisha ya mwanadamu ni Mungu, Wala sio nafsi ya mtu kama atakavyo yeye mwenyewe.

ikiwa na maana kuishi kwako unalitimiza kusudi fulani la Mungu,(haijalishi wewe ni mwema au mtenda maovu) vilevile kufa kwako ni matokeo ya kusudi Fulani la Mungu.

Vifungu vinavyofuata vinazidi kuelezea vizuri zaidi…Anasema;

Warumi 14;8 Kwa maana kama tukiishi, twaishi kwa Bwana, au kama tukifa, twafa kwa Bwana. Basi kama tukiishi au kama tukifa, tu MALI YA BWANA. 

Umeona?  Wanadamu wote ni Mali ya Bwana, Hakuna mtu aliyejiumba mwenyewe..akawa na maamuzi yake yanayojitegemea yasiyopitishwa kwanza na Mungu.. mtu hawezi kusema kesho nitajitoa uhai wangu na kuurudisha, au kesho nitafanya hiki au kile, bila Mungu kulijua au kuliruhusu, au kulipanga ,. Au aseme baadaye nitaliamuru jua lisichomoze kwa matakwa yangu, Hilo jambo haliwezekani.

Sisi wote hatuishi Kwa nafsi zetu(mapenzi yetu ) wenyewe, Bali Kila jambo kama sio limeagizwa na Mungu, basi Mungu ameliruhusu.. Hata vifo vyetu vivyo hivyo. Na vitu vyote tuvifanyavyo. Kwasababu sote tunamilikiwa na Mungu.

Ndio maana ya hilo neno “hakuna mtu miongoni mwetu aishiye kwa nafsi yake, wala hakuna afaye kwa nafsi yake. ”

Bwana akubariki

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Bwana Yesu alikuwa kabila gani?

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)

Anaposema mwanamume mmoja katika elfu nimemwona anamaana gani?

NJIA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

Rudi nyumbani

Print this post

Makasia ni nini? (Yona 1:13).

Swali: Kuvuta Makasia maana yake nini?


Likiwa moja linatiwa ”Kasia”, yakiwa mengi ni “Makasia” … Hizi ni  “Zana” ya kukisaidia chombo kutembea juu ya maji. Zana hii kwa mwonekano ni kama “Mwiko mkubwa”, (tazama picha juu), ambapo mabaharia walipoyavuta basi chombo kilisogea mbele..

Yona 1:13 “Lakini wale watu WAKAVUTA MAKASIA kwa nguvu, ili wapate kurudi pwani, wasiweze; kwa maana bahari ilizidi kuwachafukia sana”.

Unaweza kusoma Zaidi kuhusu makasia katika mistari ifuatayo; Marko 6:48, Yohana 6:19,  Isaya 33:21, na Ezekieli 27:6.

Je ni nini tunajifunza katika habari ya Yona na mabaharia hawa kuvuta makasia kurudi pwani?.. Fungua hapa >>>YONA: Mlango 1

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

YONA: Mlango wa 2

HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI.

MADHARA YA KUTAFUTA ISHARA.

YONA: Mlango wa 3

YONA: Mlango wa 4

Rudi nyumbani

Print this post

Upepo wa Mbisho maana yake nini? (Mathayo 14:24)

Swali: Pepo za Mbisho ni nini?


Jibu: Turejee kuanzia mstari wa 23.

Mathayo 14:23 “Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake.

24  Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; MAANA UPEPO ULIKUWA WA MBISHO.

25  Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.

26  Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu”.

Maana ya neno “Mbisho” ni “Ukinzani”. Hivyo hapo aliposema “Upepo ulikuwa wa Mbisho”, maana yake upepo ulikuwa ni wa ukinzani, (yaani ulikuwa unavuma kinyume na uelekeo waliokuwa wanauendea).

Utasoma tena aina ya upepo huu ikitajwa katika Matendo 27:4,

Matendo 27:4 ”Kutoka huko tukatweka, tukasafiri chini ya Kipro ili kuukinga upepo, kwa maana PEPO ZILIKUWA ZA MBISHO”.

Safari yoyote ya majini, ikikutana na pepo za mbisho, safari hiyo inakuwa ni ngumu sana.. Kwasababu upepo utakuwa unavuma kinyume na ile merikebu na hivyo kuchelewesha safari au hata kuirudisha nyuma.

Lakini pepo za Mbisho zinafunua nini kiroho?

Pepo za mbisho kiroho ni kila aina ya matatizo, na shida na dhiki na vikwazo kutoka kwa yule adui vinavyokawisha au kurudisha nyuma safari yetu ya Imani hapa duniani.

Ndio maana utaona katika habari hiyo ya Mathayo 14:23-36, kabla wanafunzi wa Bwana YESU kufika nchi ya Wagerasi kwaaijli ya huduma ya kufundisha na kuponya wagonjwa na kuwafungua walioteswa na shetani, adui aliwatumia “Upepo huu wa mbisho”, lengo ni ili wasifanikiwe safari yao hiyo.

Lakini BWANA YESU alipoingia ndani ya chombo kile ule upepo ukakoma na misuko suko yake, kufunua kuwa zile zilikuwa ni hila za ibilisi.

Hivyo hata sisi tunapokutana na pepo za namna hii katika Imani, suluhisho ni kuzikemea kwa Imani na kwa jina la YESU, na zitatii.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

UPEPO WA KUSI HULETA MVUA;

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

Rudi nyumbani

Print this post

Kufufuka kwa Bwana kulitabiriwa wapi katika agano la kale?

Swali: Bwana Yesu alitabiriwa wapi katika agano la kale kwamba atafufuka?


Jibu: Kabla ya kuona ni wapi alitabiriwa kufufuka, tutazame kwanza ni wapi alipotabiriwa kuteswa, na kuzikwa, na kukaa kaburini siku tatu.

  1.KUTESWA

Unabii wa mateso ya Bwana Yesu kwaajili ya dhambi zetu upo wazi katika unabii wa Isaya.

Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.

5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.

   2. KUZIWA NA KUKAA KABURINI SIKU TATU (3)

Unabii wa Bwana Yesu kukaa kaburini siku tatu, umejificha nyuma ya maisha ya nabii YONA,..Bwana YESU mwenyewe alisema kama vile Yona alivyokaa tumboni mwa samaki siku tatu mchana na usiku ndivyo na yeye atakavyokaa katika moyo wa nchi siku tatu.

Mathayo 12:39 “Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.

40  Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi”.

Kwahiyo maisha ya Yona yalibeba unabii wa Bwana YESU wa kukaa kaburini siku tatu. Na ndiyo ishara pekee iliyofanikiwa kuwafanya watu wa Ninawi waokoke na adhabu kutoka kwa Mungu. Vivyo hivyo kwa kuamini ishara ya Bwana Yesu ya kufa na kufufuka tunapata kuokoka na ziwa la moto, aliloandaliwa shetani na malaika zake.

     3. KUFUFUKA

Unabii wa kufufuka kwa Bwana Yesu kwa sehemu tunaupata katika habari hiyo hiyo ya Yona, kwani Yona baada ya kukaa katika tumbo la samaki mwishowe alitapikwa na yule samaki, vile vile kwa KRISTO, baada ya siku tatu alifufuka kutoka kaburini.

Lakini Zaidi sana pia Daudi, kwa kuwa ni nabii aliona ufufuo wa YESU (Masihi)..na kutabiri kuwa “hataona uharibifu wala roho yake haitasalia kuzimu” (Soma Zaburi 16:10). Lakini Mtume Petro anakuja kuuweka vizuri unabii huo wa Daudi katika kitabu cha Matendo ya Mitume mlango wa pili.

Matendo 2:29 “Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo.

30  BASI KWA KUWA NI NABII, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi;

31  yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, ALITAJA HABARI ZA KUFUFUKA KWAKE KRISTO, YA KWAMBA ROHO YAKE HAIKUACHWA KUZIMU, WALA MWILI WAKE HAUKUONA UHARIBIFU.

32  Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake”.

Na ndivyo ilivyotokea kama Daudi alivyotabiri “mwili wa Bwana haukuona uharibifu (yaani haukuoza)” na vile vile “roho yake haikubaki kuzimu” ndio maana alifufuka baada ya siku tatu.

Kwahiyo biblia ilishatabiri yote kuhusiana na maisha ya Bwana Yesu kuanzia kuzaliwa kwake mpaka kufa kwake na mpaka kupaa na kurudi kwake mara ya pili, na utawala wake wa miaka elfu hapa duniani, na nafasi yake katika umilele ujao.

Unabii wa Bwana Yesu kuzaliwa Bethlehemu kasome Mika 5:2, unabii wa Bwana Yesu kuingia Yerusalemu kwa shangwe akiwa juu ya mwana-punda huku akiimbiwa Hosana Hosana kasome Zekaria 9:9, unabii wa Bwana Yesu kusalitiwa na Yuda kasome Zaburi 41:9, unabii wa mavazi ya Bwana Yesu kugawanywa kwa kura kasome Zaburi 22:18.

Unabii wa Bwana Yesu kupewa kuzungumza maneno yale “Mungu wangu mbona umeniacha” kasome Zaburi 22:1,  Unabii wa Bwana Yesu kupewa Siki badala ya maji kasome Zaburi 69:21, unabii wa Bwana Yesu kusulibiwa pamoja na wahalifu upo katika Isaya 53:12 n.k N.K

Je umempokea huyu YESU?..kama bado basi fahamu kuwa nafasi yako ni leo na si kesho. Kwasababu upo unabii wa kurudi kwake ambao tupo mbioni kuushuhudia, saa yoyote KRISTO anatokea mawinguni na kuwanyakua walio wake, je wewe ambaye hujaokoka utakuwa wapi?

Mpokee Bwana Yesu leo na kubatizwa na kujazwa Roho Mtakatifu.

Ikiwa utahitaji msaada leo katika kuokoka basi wasaliana nasi kwa namba zetu zilizoanishwa mwisho wa somo hili au fungua hapa >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

TUNAMHITAJI SANA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUYAELEWA MAANDIKO.

MADHARA YA KUTAFUTA ISHARA.

Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?

YONA: Mlango 1

YONA: Mlango wa 2

Rudi nyumbani

Print this post

Edomu ni nchi gani kwasasa?

Swali: Edomu ni wapi kwa sasa?


Maana ya “Edomu” ni “mwekundu”.. Asili ya jina hili kabla halijawa jina la Taifa, ni mwana wa kwanza wa aliyeitwa “Esau”. Biblia inasema Esau alipozaliwa alikuwa mwekundu mwili mzima kama vazi la nywele, tofauti na ndugu yake Yakobo!.

Mwanzo 25:21 “Isaka akamwomba Bwana kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye Bwana akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba.

22 Watoto wakashindana tumboni mwake. Naye akasema, Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini? Akaenda kumwuliza Bwana.

23 Bwana akamwambia, Mataifa mawili yamo tumboni mwako,Na kabila mbili za watu watafarakana tangu tumboni mwako.Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili,Na mkubwa atamtumikia mdogo.

24 Siku zake za kuzaa zilipotimia, tazama! Mapacha walikuwamo tumboni mwake.

25 Wa kwanza akatoka, NAYE ALIKUWA MWEKUNDU MWILI WOTE kama vazi la nywele. Wakamwita jina lake Esau”.

Baadaye Esau ambaye aliitwa jina lingine “Edomu”(Soma Mwanzo 36:8 na 25:30 na 36:19) alisafiri pande za kusini pamoja na familia yake na Bwana akawabariki na kuzaliana na kuwa Taifa kubwa, na ndipo Taifa hilo likaitwa Edomu, kufuatia jina la baba yao Esau, kama tu vile Taifa la Israeli linavyoitwa leo, kufuatia jina la baba yao Yakobo, aliyeitwa Israeli.

Mwanzo 36: 1 “Hivi ndivyo vizazi vya Esau, ndiye Edomu.

2 Esau alitwaa binti za Kanaani, kuwa wakeze; Ada, binti Eloni, Mhiti, na Oholibama, binti Ana, binti Sibeoni, Mhivi;………………………………

6 Esau akawatwaa wakeze, na wanawe, na binti zake, na watu wote wa nyumbani mwake, na ng’ombe zake, na wanyama wake wote, na mali yake yote, aliyoyapata katika nchi ya Kanaani; AKAENDA MPAKA NCHI ILIYO MBALI NA YAKOBO NDUGUYE.

7 Maana mali yao yalikuwa mengi wasiweze kukaa pamoja, wala haikuweza nchi ya kusafiri kwao kuwachukua, kwa sababu ya wanyama wao.

8 Esau AKAKAA KATIKA MLIMA SEIRI, ESAU NDIYE EDOMU.

9 Hivi ni vizazi vya Esau, baba ya Edomu katika mlima Seiri”

Eneo la Edomu kwa sasa ni sehemu katika nchi ya Yordani upande wa kusini magharibi na  katika nchi ya Israeli upande wa kusini, Taifa hili kwasasa halipo tena!!, lilishapotea… isipokuwa eneo Taifa hilo lilipokuwepo ndio sasa linamilikiwa na Israeli pamoja na Yordani katika upande wa kusini wa nchi hizo mbili.

Kufahamu unabii na ujumbe tunaoweza kuupata kupitia Taifa hili la Edomu soma kitabu cha Obadia, au fungua hapa >>>VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 14 (Yoeli, na Obadia).

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MWINUE YESU KRISTO KATIKA MAISHA YAKO.

NG’OMBE MWEKUNDU ALIYEZALIWA ISRAELI, ANAFUNUA NINI?

MWINUE YESU KRISTO KATIKA MAISHA YAKO.

SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

Rudi nyumbani

Print this post