Title July 2024

Nyota ya bahati yangu ni ipi?

Je ni kweli kuna watu wenye nyota ya bahati? Na je nitaipate nyota hiyo maishani mwangu?


JIBU: Nyota ya bahati inasadikika ni pale mtu anapobahatika kupata kitu kwa haraka au kwa wepesi, au bila matarajio yake,au nguvu zake nyingi katika kukipata tofauti na wengine. Kwamfano labda mtu ni mchimba madini, mara ghafla anatapa dhahabu nyingi tofauti na wachimbaji wengine. Au mwingine amehitimu chuo, mara anapata kazi nzuri, yenye cheo, zaidi hata ya wengine wengi waliomtangulia. Au ni mfanya-biashara mara anapata tenda kubwa ambayo inainua biashara yake kwa kasi zaidi ya wengine. N.k.

Sasa mtu kama huyu wengi husema ana nyota ya bahati. Lakini je ni kweli?

Ukweli ni kwamba twaweza kusema ana-bahati –tu, lakini hana nyota-ya-bahati. Kwavipi.

Kwasababu mafanikio hayo, yanaweza kuondoka tena kwake, na kama yakibaki, bado bahati hiyo hainunui tunu za rohoni. Mfano amani, upendo, utu wema,  imani, adili, unyenyekevu, na uzima baada ya kifo. N.k., Ni mafanikio ambayo hata mashetani huyatoa.

Lakini ni lazima ujue nyota halisi ya bahati ni ipi? Ambayo katika hiyo unaweza kupata vyote, Kisha uifuate.

Hiyo si nyingine zaidi ya YESU KRISTO. Vitabu vitakatifu vinasema hivyo, Vilevile Watu wote wanalijua hilo, ikiwemo wachawi wote, wanajimu wote, malaika wote, na mashetani yote.

Soma hapa;

Mathayo 2:1  Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, MAMAJUSI WA MASHARIKI walifika Yerusalemu, wakisema,

2  Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana TULIIONA NYOTA YAKE MASHARIKI, nasi tumekuja kumsujudia.

3  Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye. 4  Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi?

5  Nao wakamwambia, Katika Bethlehemu ya Uyahudi; kwa maana ndivyo ilivyoandikwa na nabii,

6  Nawe Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, Hu mdogo kamwe katika majumbe wa Yuda; Kwa kuwa kwako atatoka mtawala Atakayewachunga watu wangu Israeli.

7  Kisha Herode akawaita wale mamajusi faraghani, akapata kwao hakika ya muda tangu ilipoonekana ile nyota.

8  Akawapeleka Bethlehemu, akasema, Shikeni njia, mkaulize sana mambo ya mtoto; na mkiisha kumwona, nileteeni habari, ili mimi nami niende nimsujudie.

9  Nao waliposikia maneno ya mfalme, walishika njia; na tazama, ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, hata ikaenda ikasimama juu ya mahali alipokuwapo mtoto.

10  NAO WALIPOIONA ILE NYOTA, WALIFURAHI FURAHA KUBWA MNO.

11  Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane.

Ikiwa Yesu yupo moyoni mwako. Ikiwa umemwamini, kisha ukamfanya Bwana na kiongozi wa maisha yako. Jambo la kwanza analolifanya ndani yako ni kuondoa laana yote ya dhambi, ambayo humfanya mwanadamu aende kuzimu, ambayo kila mwanadamu anayo. Na wakati huo huo huyo mtu anaitwa mbarikiwa, anaitwa mtakatifu, makosa yake yote yanakuwa yamefutwa, hahesabiwi dhambi tena.

Na moja kwa moja anapewa, Roho Mtakatifu. Sasa Kazi ya huyu Roho Mtakatifu, ni kumtengeneza roho yake,kumsafisha kutoka katika ubaya kumweka katika wema, na kumfanya aweze kushinda dhambi na maovu yote.

Ndio hapo kama alikuwa mlevi, kiu hiyo inaondolewa, alikuwa mzinzi, hamu ya mambo hayo yanakufa ndani yake, alikuwa ana uchungu, furaha inaanza kujengeka, alikuwa ni mwenye hasira, upendo wa ki-Mungu unaumbika sana moyoni mwake, anaanza kupenda watu wote.

Na zaidi sana, anapokea uzima wa milele, hata akifa ghafla, haendi kuzimu, hapotei, bali anakuwa amelala tu, anasubiri siku ya ufufuo, aamshwe aende mbinguni.

Pamoja na hilo, hata yale mengine ambayo alikuwa anayatafuta au anayapata kwa shida, Yesu anampa mafanikio pia  kiwepesi kwasababu aliahidi hivyo. Zile bahati ambazo anatamani azipate, Yesu anamletea mara mia (100), katika maisha yake.

Mathayo 19:28  Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.

29  NA KILA MTU ALIYEACHA NYUMBA, AU NDUGU WA KIUME AU WA KIKE, AU BABA, AU MAMA, AU WATOTO, AU MASHAMBA, KWA AJILI YA JINA LANGU, ATAPOKEA MARA MIA, NA KUURITHI UZIMA WA MILELE.

Umeona, mwisho wa siku unakuwa umepata vyote, kwasababu kwa Yesu vipo vyote.

Huoni kuwa hiyo ni NYOTA nzuri sana ya bahati? Kwanini uende wa waganga wa kienyeji, kutafuta laana, huko? Kwasababu wale wanakurushia mapepo, ambayo mafanikio yao ni batili, ni kitanzi, mwisho wa siku ni kukuangamiza, sasa unakuwa umepata faida gani? Wakati mafanikio ya Yesu Kristo, hutajirisha wala hayana huzuni ndani yake, biblia inasema hivyo;

Mithali 10:22 Baraka ya Bwana hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo

Ungoja nini usimpokee Yesu leo? Ikiwa umedhamiria kwa dhati kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa namna ya kuokoka leo >>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Falaki ni elimu gani? (Isaya 47:13).

NYOTA YA ASUBUHI.(Opens in a new browser tab)

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu.

Ni nini tunajifunza katika maisha ya Nuhu, ambaye Mungu alimshuhudia kuwa mwenye haki katika kizazi chake? Lakini baadaye akaja kunaswa katika ulevi uliomletea aibu kubwa nyumbani mwake?

Mwanzo 9:20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;  21 akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.

Ulishawahi kujiuliza kama Nuhu asingekuwa mkulima wa mizabibu, angekuwa na wazo la kutengeneza divai? Na hatimaye kuanguka kwenye makosa?

Jibu ni la! Kwasababu bila shaka Nuhu alikuwa mkulima, ili ajipatie rizki, na sio ili atengeneze divai. Lakini hakujua kuwa nyuma ya kazi yake ya halali upo mtego wa dhambi. Na hivyo akauridhia na ndio ikamshawishi mpaka kutoa bidhaa isiyopasa katika maisha yake kwa kazi hiyo.

Hata sasa watoto wengi wa Mungu wanashindwa kujua kuwa “shughuli za ulimwenguni zilizo za halali kabisa” zina udanganyifu Fulani nyuma yake, unaolewesha ambao unaweza mpelekea mtu anguko kubwa sana, kama asipokuwa makini.

Bwana Yesu alisema..

Marko 4:18  Na hawa ndio wale wapandwao penye miiba; ni watu walisikiao lile neno, 19  na SHUGHULI ZA DUNIA, NA UDANGANYIFU WA MALI, na tamaa za mambo mengine zikiingia, hulisonga lile neno, likawa halizai.

Kwamfano labda ni kijana, ameokoka, hapo mwanzo alikuwa amesimama vizuri tu, katika Bwana, anapata muda wa kuomba, kushuhudia, kujisomea Neno n.k. lakini akapata kazi nzuri, na ile kazi ikawa inamlazimu, awe bize wiki nzima, isipokuwa jumamosi na jumapili. Sasa katika miezi ya mwanzo, alikuwa anatimiza majukumu yake ya ushuhudiaji/ kuhudhuria mikusanyiko ya nyumbani na maombi, bila shida siku ya jumamosi, na jumapili anahudhuria ibadani , kama kawaida. Lakini baada ya miezi kadhaa, alivyozidi kufanikiwa, uvivu na udanganyifu wa mali ukaanza kumuingia, akasema, huu muda wangu wa jumamosi, nifanye kitu kingine cha kuniingizia kipato, (jambo  ambalo si baya), lakini hajui kuwa analisogeza mahali ambapo sio sahihi. Na kweli akajiongezea kitu cha kufanya, matokeo yake jumamosi yake yote ikawa ni kazi zake za miradi. Hakuna ushuhudiaji tena, hakuna ibada za jumuiya tena, hakuna maombi.

Na inapofika jumapili, anaamka amechoka, anasema, aa wiki hii napumzika, wiki ijayo nitaenda..anaanza kuwa mdokoaji-dokoaji wa ibada,  hivyo baada ya miezi miwili, anapokea mialiko ya marafiki zake, kwenda kwenye party, picnic, vikao vya kirafiki, sinema, n.k. vyote hivyo vinapaswa vifanyike siku ya jumapili ambayo yupo free. Matokeo yake anahudhuria kanisani mara moja kwa mwezi au miezi miwili. Hilo linaendelea mwaka mzima. Hajui kuwa mwili unafurahia kweli, lakini roho yake inadhoofika siku baada ya siku. Sasa baada ya kipindi kirefu hapo ndipo anashangaa haoni tofauti yake ni watu wa kidunia, kila jambo la ki-Mungu anaona ni mzigo kulifanya, yeye ambaye alikuwa anawaombea wengine anakuwa wa kuombewa, yeye ambaye alikuwa anawaokoa wengine, anafikiwa kuokolewa tena.Hana nguvu tena, ameshaleweshwa, shetani kamweka chini.

Sasa huyu ndio mfano wa Nuhu, Amelewesha na kazi yake. Na utumishi wake. Kwasababu hakujiwekea mipaka,.

Ndio maana maandiko yanatutaka tuwe na kiasi, katika huu ulimwengu.

1Wakorintho 7:31  Na wale wautumiao ulimwengu huu, kama hawautumii sana; kwa maana mambo ya ulimwengu huu yanapita.

Kuwa buzy kupita kiasi, si afya ya kiroho au kimaisha. Ni lazima upate nafasi ya kutosha kujijenga nafsi yako kwa Mungu. Ni vema utumie siku za tano, usiku na mchana kama ni hivyo kuwekeza na kupangilia ratiba yako, lakini upate pia nafasi nyingi ya kumwabudu na kumkaribia Mungu bila masumbufu. Umeajiriwa katika kazi ambayo siku zote saba za wiki, upo kazini, hupewi muda wa kupata ibada yako na Mungu, fahamu hiyo si kazi itokayo kwa Mungu. Fikiria kutafuta kazi nyingine.

Kama ubize, basi Mungu angekuwa buzy zaidi yetu sisi, kwasababu yeye ndio aliyeumba ulimwengu mzima, lakini alijipa pumziko Siku ya saba, akaiweka wakfu, akatuambia na sisi. Tufanye hivyo. Kumbuka hizi ni siku za mwisho, na wengi wataikosa mbingu kwa ubize usiokuwa na tija wa mambo ya ulimwengu huu, yanayopita.

Ni heri ukose vya dunia, lakini nafsi yako itajirike, kuliko kutajirika duniani na huku nafsi yako unaangamia. Uzima wako upo katika mambo ya rohoni, Jinsi unavyojitenga na Mungu ndivyo unavyojiua mwenyewe.

Kamwe usiyaige ya Nuhu mabaya ya ajira yake, bali yale mema aliyoyafanya kabla ya Gharika.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?

UMUHIMU WA KUBATIZWA.(Opens in a new browser tab)

NUHU WA SASA.(Opens in a new browser tab)

(Opens in a new browser tab)KWANINI NI NUHU, AYUBU NA DANIELI?(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Mlango la kondoo ulikuwaje?(Yohana 5:2)

Swali: Ule mlango wa kondoo unaotajwa katika Yohana 5:2, ulikuwa ni mlango wa namna gani?, na umebeba ujumbe au ufunuo gani sasa?


Jibu: Turejee.

Yohana 5:2 “Na huko Yerusalemu penye mlango wa kondoo pana birika, iitwayo kwa Kiebrania Bethzatha, nayo ina matao matano”.

Mlango wa kondoo unaozungumziwa hapo ulikuwa ni mlango mdogo katika hekalu la Mungu, uliokuwa unatumika kupitishia kondoo kwaajili ya sadaka ya kuteketezwa (dhabihu).  Ulikuwepo mlango wa kuingilia watu na wa kuingizia wanyama ndani ya hekalu (katika Ua wa ndani).

Utaona lango hili linatajwa pia katika Nehemia 3:1, Nehemia 3:32 na Nehemia 12:39.

Nehemia 3:1 “Ndipo akaondoka Eliashibu, kuhani mkuu, pamoja na nduguze makuhani, wakalijenga LANGO LA KONDOO; wakazitia boriti zake, wakaisimamisha milango yake; mpaka mnara wa Hamea wakalitakasa, mpaka mnara wa Hananeli”

Lango hili la kondoo lilikuwa linamfunua BWANA YESU, kwani yeye mwenyewe katika Yohana 10:7 ametajwa kama LANGO LA KONDOO..

Yohana 10:7 “Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, MIMI NDIMI MLANGO WA KONDOO.

8  Wote walionitangulia ni wevi na wanyang’anyi; lakini kondoo hawakuwasikia.

9  Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.

10  Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele”

Kama vile ule mlango wa kwanza wa kondoo ulivyokuwa lango la yule aliyekuwa hawezi kwa miaka 38 kuponywa na Bwana YESU katika birika lile la Bethzatha vile vile  BWANA YESU ambaye ndiye LANGO halisi amebeba uponyaji wote wa roho zetu na miili yetu.

Je umempokea?

Kama bado fahamu kuwa upo katika hatari kubwa sana ya kuharibiwa na adui, kwani unakuwa upo nje ya zizi, ambapo yupo adui ambaye kazi yake ni kuchinja, kuharibu na kuua.

Yohana10:9 “Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.

10  Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USIMZIMISHE ROHO.

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

JE! UNAMPENDA BWANA?

WALIKUWA WAMECHOKA NA KUTAWANYIKA KAMA KONDOO WASIO NA MCHUNGAJI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kuota unakemea mapepo/ unashindana na nguvu za giza.

Kunaweza maanisha namna tatu, ya kwanza, ni kwamba unapitia kweli vita vya kiroho, lakini ya pili ni unaonyeshwa na Mungu uhalisia wa vita vya kiroho, na tatu unaonyeshwa uwezo wa hali yako ya  kiroho.

Maandiko yanasema

Waefeso 6:12  Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

13  Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama

Tukianza na maana ya kwanza,

Mara nyingine adui huanzisha mashambulizi kuanzia ndotoni, wakati mwingine utakuta mtu anaota ameumwa labda na nyoka kidoleni halafu  anapoamka, anashangaa kinauma kweli, na kama haiishii hapo, anaanza kuona kidole kinazidi kutengeneza kidonda, mpaka kuleta madhara mwili mzima, sasa hayo ni mashambulizi ya kipepo. Na hivyo ikiwa ndoto yoyote umeiota ambayo unaona uhalisia wake mpaka nje, unashindana na mapepo halafu linakukaba, unahangaika kitandani. Ujue ni mashambulizi ya adui, hapo unayo mamlaka ya kubatilisha, kwa jina la Yesu.

Lakini mara nyingine, utajikuta unaota tu unakemea mapepo, unashindana nayo. Si kwamba utakuwa unamashambulizi ya adui, lakini unaonyeshwa tu uhalisia wa vita vya kiroho, na hivyo vipo halisi, au vitakuja mbeleni katika safari yako ya maisha, na unapaswa uvishinde, kwa jina la YESU, kwa simama imara ndani yake..

Na mwisho ni Mungu anakuonyesha kiwango cha kiroho, ulichopo au unachopaswa uwe nacho. Mwingine atakuwa ameokoka, lakini anahofu ya kutoa pepo au kuombea watu, Mungu anakuonyesha uwezo wa kushindana na nguvu za giza unao, au unapaswa uanze kazi ya kuwaombea wengine wanaosumbuliwa na nguvu za giza. Lakini pia pale unapojiona umezidiwa nguvu zao, ni kuonyesha uongeze kiwango chako cha kiroho, kwa maombi, utakatifu, na Neno, ili uwe thabiti rohoni kuzipinga hila za adui.

Kwahiyo kwa vyoyote vile kuona unakemea mapepo, au unashindana na wachawi kwa jina la Yesu. Ni kuonyesha kuwa ni wakati wa kusimama  imara na Bwana. Kwasababu shetani ni adui wako, na adui za ndugu zako, na hivyo unapaswa umpinge sikuzote kwa kuwa thabiti rohoni kwa wewe ambaye umeokoka.

Lakini Ikiwa hujaokoka, basi ni vema ukafanya hivyo leo kwa kumkaribisha Yesu moyoni mwako, ukifahamu kuwa kamwe huwezi kumshinda adui kwa nguvu zako unamwita Kristo.

Ikiwa upo tayari  waweza kufungua hapa kwa mwongozo wa sala ya kuupokea wokovu. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UMEFUNGWA KATIKA GIZA NA UVULI WA MAUTI?(Opens in a new browser tab)

Je Mungu anaketi katika giza? (1Wafalme 8:12)

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini Mungu aliupenda ulimwengu?

Mungu aliupenda ulimwengu kwasababu asili yake upendo, Maandiko yanasema yeye ni UPENDO.

1Yohana 4:16  Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.

Lakini ifahamike kuwa aliposema ameupenda ulimwengu haimaanishi kuwa amependa kila kitu ulimwenguni, ikiwemo mifumo ya ulimwengu huu, hapana, kazi nyingi za ulimwengu ni mbovu, na hivyo hawezi kuzipenda, tena alizikemea (Yohana 7:7), bali aliwapenda walio-ulimwenguni (yaani sisi wanadamu). Bila kujali jinsia zetu, rangi zetu, jamii zetu, mataifa yetu, waovu, na wema, wote alitupenda sawa.

Ni upendo uliodhihirika katika hali yetu ya kupotea. Mahali ambapo tulikuwa hatuna tumaini lolote, hatuna uzima wowote wa milele ndani yetu, tumeteswa na ibilisi, yeye mwenyewe kwa mapenzi yake akatuhurumia, ndipo akatujia tena ili kutuokoa katika hali ya kifo na mauti tuliyokuwa nayo bure.

Na hivyo hakutupenda kwa mdogo tu, bali aliingia gharama. Na gharama yenyewe ni kumtoa mwanawe wa pekee Yesu Kristo, kuja katika mwili wa kibinadamu ili afe kama fidia ya dhambi zetu, ili sisi tupone kwa kifo chake yeye. Tupokee uzima wa milele.

Maana yake mtu yeyote ambaye ataukubali wokovu huo, ulioletwa kwa kufa na kufufuka kwake, basi uzima wa milele unaingia ndani yake. Ndio maana ya hilo andiko;

Yohana 3:16  Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

Lakini ijapokuwa uzima umeletwa kwetu bure kwa gharama kubwa, wapo wengine hawaukubali, wakidhani kuwa wataweza kuushinda huu ulimwengu kwa nguvu zao, au kwa dini zao, au kwa matendo yao wenyewe.

Yohana 3:19  Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.

Je! Umeupokea uzima huu wa milele?. Ikiwa bado basi fungua moyo wako sasa, mwamini Yesu, mpokee kama ‘Bwana’ kwako, umfuate kwa moyo wako wote, uokoke, dunia hii ni ya kitambo tu, vilevile kesho yako huijui kama utakuwa hai au maiti. Ikiwa upo tayari kuokoka leo, basi fungua hapa kwa msaada wa mwongozo wa sala ya wokovu >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ulimwengu wa Roho ni nini? Na mtu anawezaje kuwa wa rohoni?

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini tunakwenda kanisani?

Maisha ya wokovu, hayatoshi tu kusema nimeokoka, halafu basi, nitamwabudu Mungu kivyangu. Hapana, Mungu hajaagiza hivyo, na kuna hatari kubwa ya kuenenda kwa namna hiyo, tutaona ni kwanini?

Ni sawa na mwanafunzi anayesema mimi sihitaji shule, nitajisomea tu nyumbani peke yangu, nitapata elimu yote, na maarifa yote kupitia vitabu na tafiti zangu. Ukweli ni kwamba si rahisi akipate anachokitafuta, kwasababu shuleni wapo waalimu atawahitaji wamfundishe vitu asivyovijua, atauliza maswali pale ambapo hajaelewa, wapo wanafunzi wenzake atajadiliana nao, zipo nidhamu atajifunza, ipo hamasa ataipata, tofauti na akiwa peke yake, na mambo mengine kadha wa kadha, .

Vivyo hivyo na maisha ya rohoni. Wokovu ni mtu binafsi, lakini kusimama katika wokovu na kuendelea mbele na kukua kunahitaji kanisa. Mungu aliagiza hivyo akasema, tusiache kukusanyika pamoja.

Waebrania 10:25  wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia

Akasema pia, heri walio wawili kuliko mmoja, kwasababu katika wingi, kuna kutiana nguvu ya kuendelea mbele.

Mhubiri 4:9 Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.

10 Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!

11 Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona moto?

12 Hata ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi.

Mkusanyikapo pamoja mtatiana moyo, mtaomba pamoja n.k.

Vilevile Kanisa la kwanza lilikuwa na desturi ya kukusanyika pamoja, kusikiliza fundisho la mitume, kumsifu Mungu na kumega mkate,  nyumba-nyumba kwa nyuma pamoja na Kutambuana.

Matendo 2:46  Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,

Lakini pia kusaidiana kimahitaji, Kutiana moyo  (Warumi 1:12), Kuonyana  (Wagalatia 5:13)

Lakini pia kufaidiana kwa karama za Roho Mtakatifu. Yaana kuruhusu uweza wa Mungu kutenda kazi katikati ya waamini.(Waefeso 4:11, 1Wakorintho 12) Mambo ambayo huwezi kuyapata ukiwa peke yako.

Hivyo huwezi kutenganisha maisha ya wokovu na kanisa. Kila mwamini ni lazima awe na mkusanyiko, kwa uthabiti wa maisha yake ya rohoni. Usiabudu kivyako vyako.

Amen.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WALA TUSIACHE KUKUSANYIKA PAMOJA

FUNDISHA NENO KANISANI NA NYUMBANI.

(Opens in a new browser tab)WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA; NAO WATAMWOMBOLEZE

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?(Opens in a new browser tab(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Huyu Mkeni shemeji yake Musa alikuwa ni mtu wa namna gani? (Waamuzi 1:16)

Jibu: Turejee…

Waamuzi 1:16 “Hao wana wa Mkeni, HUYO SHEMEJI YAKE MUSA, wakakwea juu kutoka katika huo mji wa mitende, pamoja na wana wa Yuda, na kuingia hiyo nyika ya Yuda, iliyo upande wa kusini wa Aradi; nao wakaenda na kukaa pamoja na watu hao”.

Wakeni walikuwa ni jamii ya watu waliokuwa wanaishi katika nchi ya “Midiani” (karibu na jangwa la Sinai).. Kwa urefu kuhusiana na waMidiani fungua hapa >>Midiani ni nchi gani kwasasa?.

Miongoni mwa hawa waMidiani ndiko alikotokea Babamkwe wake Musa aliyeitwa Yethro au jina lingine Rueli.. Huyu Yethro/Reueli ndiye aliyemzaa  Sipora aliyekuwa mkewe Musa.

Na huyu Yethro alikuwa na watoto wengine wa kiume mbali na wale mabinti wake saba tunaowasoma katika Kutoka 2:16, na mmoja wa mtoto wake wa kiume aliitwa “Hobabu” ambaye sasa “ndiye shemeji yake Musa (maana yake kaka yake Sipora, mke wa Musa)”.

Huyu Hobabu shemeji yake Musa alikataa kusafiri na wana wa Israeli, kwani wana wa Israeli walimtumaini yeye awatangulie njia kwani aliifahamu Zaidi, lakini alikataa kama maandiko yanavyosema..

Lakini maandiko mbeleni yanaonyesha alikubali, kwani uzao wake ulionekana ndani ya nchi ya Ahadi

Hesabu 10: 28 “Ndivyo zilivyokuwa safari zao wana wa Israeli kwa majeshi: yao; nao wakasafiri kwenda mbele.

29 Kisha Musa akamwambia Hobabu, mwana wa Reueli Mmidiani, mkwewe Musa, Sisi twasafiri kwenenda mahali ambapo Bwana amenena habari zake hivi, Nitawapa ninyi mahali hapo; uje pamoja nasi, nasi tutakufanyia mema; kwa kuwa Bwana ametamka mema juu ya Israeli.

30 Naye akamwambia, Siendi mimi; ila nitairudia nchi yangu mwenyewe, na kwa jamaa zangu mwenyewe.

31 Naye akamwambia, Usituache, tafadhali; kwa kuwa wewe wajua jinsi tutakavyopanga nyikani, nawe utakuwa kwetu badala ya macho.

32 Itakuwa, ukienda pamoja nasi, naam, itakuwa mema yo yote Bwana atakayotutendea sisi, tutakutendea wewe vivyo

34 Na wingu la Bwana lilikuwa juu yao mchana hapo waliposafiri kwenda mbele kutoka kambini.

35 Ilikuwa, hapo sanduku liliposafiri kwenda mbele, ndipo Musa akasema, Inuka, Ee Bwana, adui zako na watawanyike; na wakimbie mbele zako hao wakuchukiao”.

Kwa funzo refu kuhusiana na habari hii ya Hobabu na Musa fungua hapa >>>>Kwanini Musa amtake Hobabu na tayari kulikuwa na Wingu linalowaongoza?

Kwahiyo huyu Hobabu ndiye aliyekuwa shemeji yake Musa na wanawe (yaani watoto wake) ndio hao wanaotajwa hapo katika Waamuzi 1:6 na Waamuzi 4:11 na pia wanatajwa katika sehemu mbali mbali za biblia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kuiaua Nchi ni kufanya nini? (Waamuzi 18:2).

BWANA NITIE NGUVU TENA. (Waamuzi 16:28)

MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

Dina akatoka kuwaona binti za nchi. (Mwanzo 34:1)

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini Musa amtake Hobabu na tayari kulikuwa na Wingu linalowaongoza?

Swali: Kwanini Nabii Musa amtake Hobabu (shemeji yake) kama dira yake ya kuelekea Kaanani na tayari Mungu alishawafunulia juu yao nguzo ya wingu wakati wa mchana na Nguzo ya moto wakati wa usiku kama dira yao na kama kitu cha kuwaongozea?


Jibu: Lipo jambo kubwa sana hapa la kujifunza..

Awali ya yote kama bado hujamfahamu Hobabu ni nani na inakuwaje awe shemeji yake Musa fungua hapa >>>Huyu Mkeni shemeji yake Musa alikuwa ni mtu wa namna gani? (Waamuzi 1:16)

Sasa kwa muhtasari ni kwamba kipindi wana wana wa Israeli wanatoka Misri kuelekea Kaanani, ni kweli Bwana aliwapa wingu na nguzo ya moto iwaongoze mchana na usiku.

Lakini Zaidi ya hayo Musa alitafuta tena mtu ambaye atamwongoza njia yao kuelekea nchi ya ahadi.. sasa swali ni alifanya makosa?… na tena akataka kumfanya kama “Macho” katika safari hiyo..

Waamuzi 10:28 “Ndivyo zilivyokuwa safari zao wana wa Israeli kwa majeshi: yao; nao wakasafiri kwenda mbele.

29 Kisha Musa akamwambia Hobabu, mwana wa Reueli Mmidiani, mkwewe Musa, Sisi twasafiri kwenenda mahali ambapo Bwana amenena habari zake hivi, Nitawapa ninyi mahali hapo; uje pamoja nasi, nasi tutakufanyia mema; kwa kuwa Bwana ametamka mema juu ya Israeli.

30 Naye akamwambia, Siendi mimi; ila nitairudia nchi yangu mwenyewe, na kwa jamaa zangu mwenyewe.

31 NAYE AKAMWAMBIA, USITUACHE, TAFADHALI; KWA KUWA WEWE WAJUA JINSI TUTAKAVYOPANGA NYIKANI, NAWE UTAKUWA KWETU BADALA YA MACHO.

32 Itakuwa, ukienda pamoja nasi, naam, itakuwa mema yo yote Bwana atakayotutendea sisi, tutakutendea wewe vivyo

34 NA WINGU LA BWANA LILIKUWA JUU YAO MCHANA HAPO WALIPOSAFIRI KWENDA MBELE KUTOKA KAMBINI.

35 Ilikuwa, hapo sanduku liliposafiri kwenda mbele, ndipo Musa akasema, Inuka, Ee Bwana, adui zako na watawanyike; na wakimbie mbele zako hao wakuchukiao”.

Jibu ni La!.. Musa hakuwa Mjinga, wala hakuwa mtu wa kumtegemea Mwanadamu.. Daima alijua Mungu ndiye Ngao yake na watu wake, na wala hakuna mtu yeyote awezaye kumsaidia kazi.  Lakini Nabii Musa alifikiri Zaidi, Alijua watu aliona ni  watu wenye mioyo migumu, na shingo ngumu.

Alijua Imani yao kwa Mungu ilikuwa ni ndogo, na wengi wao ni watu wa mwilini, na alijua wasipopata mtu wa kuwapanga vyema kule nyikani, aliyemzoefu wa jangwa na njia, zitanyanyuka shida nyingi na hatimaye watamkufuru Mungu na kuadhibiwa wote.

Hivyo kwa faida ya watu wasiangamia aliwatafutia mwalimu wa mwilini ili awaongoze, na kuwafundisha jinsi ya kukaa jangwani, na hiyo ikawa dawa kwa sehemu kubwa sana.

Na utaona hii familia ya Yethro (babamkwe wake Musa na mashemeji zake), ilikuwa msaada mkubwa sana kiushauri katika safari ya wana wa Israeli jangwani na kwa Musa kwa ujumla. Kwani kipindi ambacho Musa alikuwa anawaamua watu wote peke yake kuanzia asubuhi mpaka jioni, alipokuja huyu babamkwe wake alimpa ushauri bora sana wa kuweka wakuu wa maelfu, wakuu wa mahamsini na wakuu wa mamia na wakuu wa makumi (Soma Kutoka 18:12-27).

NINI TUNAJIFUNZA KWA MUSA:

Musa alikuwa na “Macho juu” ambaye ni Roho Mtakatifu juu (kama wingu likimwongoza na watu wake) lakini pia alikuwa na “macho chini” (Hobabu, shemeji yake) kwaajili ya watu wake. Mambo haya yanaenda pamoja..

Wewe kwama Mzazi, unaye Roho Mtakatifu anayekuongoza wewe na familia yako kama Macho ya Juu, lakini hayo hayatoshi pekee, ni lazima watoto wako uwapatie waalimu watakaowafundisha njia za Roho Mtakatifu katika mashule yao waliopo, katika makanisa yao, katika shughuli zao n.k

Ukisema utawaacha na kuongozwa na Roho Mtakatifu kama wewe uongozwavyo, utawapoteza…wawekee waalimu.

Vilevile Mtumishi wa Mungu weka waalimu kwa watoto wako wa kiroho, weka wachungaji watakaowaangalia, itakuwa afya na heri kwao.

Bwana atusaidie

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

KAZI ZA ROHO MTAKATIFU

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

Je Musa kumwoa Sipora, Mkushi alifanya dhambi?

Kiti cha Musa ni kipi? (Mathayo 23:2)

Rudi Nyumbani

Print this post

Bafe ni nini (Mwanzo 49:17)

Neno hilo utalisoma katika ule utabiri wa Yakobo kwa watoto wake, alipokuwa anawabariki, na alipofikia kwa Dani, yeye alimfananisha na Bafe. Swali ni je Huyu bafe ni nani?

Tusome

Mwanzo 49:17 Dani atakuwa nyoka barabarani, Bafe katika njia, Aumaye visigino vya farasi, Hata apandaye ataanguka chali. 18 Wokovu wako nimeungoja, Ee Bwana.

Bafe ni nyoka aina ya kifutu. Hivyo Yakobo alimwona Dani kama nyoka, ambaye ijapokuwa maisha yake ni ya mavumbi, lakini ameng’ata farasi kisigo hatimaye farasi Yule akashindwa kuendelea na hapo hapo mpanda farasi naye akashindwa kuvifikia vita vyake.

Akimaanisha kuwa Dani anaweza dharaulika, lakini ana wokovu mkuu kwa watu wake, pale ambapo wangetarajia mpanda farasi arushiwe mikuki na majeshi ya watu, au avamiwe kijeshi, yeye anauma tu kisigo cha farasi wao, sumu inaingia na nguvu yao inaisha.

Ni kufunua kuwa kila mmoja wetu amepewa karama yake tofauti na mwingine, na kama ikitumika kifasaha huweza kumweka adui chini, sawa tu na zile karama ambazo huonekana zina heshima mbele ya macho ya watu kama vile, utume, uchungaji, uinjilisti n.k.

Kamwe usidharau karama yako, kumbuka sikuzote vile visivyoonekana  kwa urahisi ndio huwa vina umuhimu mkubwa. Unaweza usiwe mguu au mkono, lakini ukawa moyo, au figo, vilivyojificha ndani, ambavyo tunajua uthamani wake ulivyo.

Halikadhalika, katika Baraka zile, Yuda aliitwa simba, Isakari aliitwa punda, Dani aliitwa Bafe, Lakini wote waliitwa Israeli. Taifa la Mungu.

Je ! unaitumia vema karama yako, au umeidharau? Na kutamani za wengine?

Kwa msaada wa jinsi ya kuitambua karama yako fungua hapa >>> NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

UFUNUO: Mlango wa 6(Opens in a new browser tab)

Maana ya Mithali 11:17 Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake(Opens in a new browser tab)

(Opens in a new browser tab)MIHURI SABA(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

AINA SABA (7), ZA SIFA KIBIBLIA.

Katika biblia zipo aina mbalimbali za kumsifu Bwana, lakini kuna kuu saba ambazo zilitambuliwa na wayahudi kwa wakati wote. Hivyo ni vema kuzifahamu ili wigo wako uwe mpana zaidi katika eneo hili la sifa. Kwasababu ndio huduma kuu tuliyonayo duniani kwa Mungu wetu. Kumbuka chakula chetu ni Neno, lakini chakula cha Mungu wetu ni Sifa zetu. Hivyo ni lazima tujue tunamsifuje yeye kiufasaha kwa jinsi apendavyo.

Hizi ni aina saba za sifa.

1.) Kucheza: Kwa kiyahudi huitwa ‘Hallal’

Hii ni aina ya kumsifu Mungu ambayo, mwimbaji hujidai, hujigamba mbele za Mungu wake kwa kuuhusisha mwili wake, yaweza kuwa kuruka kuruka, au kucheza.

Agizo hilo lipo katika Zaburi 149:3 Na walisifu jina lake kwa kucheza, Kwa matari na kinubi wamwimbie.

Ndio lile Daudi na Israeli wote walilolifanya walipokuwa wanalileta sanduku la Bwana Yerusalemu,

 2Samweli 6:14 Daudi akacheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote; na Daudi alikuwa amevaa naivera ya kitani.

15 Basi Daudi na nyumba yote ya Israeli wakalileta sanduku la Bwana kwa shangwe, na kwa sauti ya tarumbeta.

16 Ikawa, sanduku la Bwana lilipoingia mji wa Daudi Mikali, binti Sauli, akachungulia dirishani, akamwona mfalme Daudi akiruka-ruka na kucheza mbele za Bwana; akamdharau moyoni mwake.

Hivyo na wewe kama mtu uliyeokolewa na Kristo, kujidai kwa ujasiri wote mbele ya Mungu wako usijizuie, angalizo tu ni kwamba usifanye kidunia, kana kwamba unacheza dansi, huku moyoni mwako hakuna ibada. Hiyo sio sawa, lakini kumwimbia Mungu kwa kucheza hakuna kosa lolote ikiwa ni jambo la kububujika  moja kwa moja kutoka moyoni mwako.

2) Kuinua mikono: Kwa kiyahudi huitwa ‘Yadah’.

Hii ni aina ya kumsifu Mungu kwa kuinua mikono juu, Kama ishara ya kutambua tegemeo lako kwake, kama mtoto mdogo kwa mzazi wako anapomlilia. Na kuonyesha upendo wako wa dhati kwa Mungu wako.

Zaburi 63: 3 Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai; Midomo yangu itakusifu.  4 Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai; Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.

Kama mtakatifu jizoeze mara nyingi, kunyanyua mikono yako juu wakati unamwabudu Mungu, au wakati mwingine unapoomba. Binafsi, nimeona tofauti kubwa sana, niinuapo mikono yangu, pindi niombapo au nisifupo, najikuta nazama rohoni kwa haraka sana, zaidi ya napoweka mikono yangu chini. Kumbuka ile habari ya Musa, alipoinua mikono juu, Israeli ilishinda, lakini alipoweka mikono chini, Waamaleki walishinda. (Kutoka 17:11) Hivyo jifunze sana, kuiinua mikono yako juu, katika ibada zako.

3) Kuinama, kujusudu, kupiga magoti: Kwa kiyahudi huitwa ‘Barak’.

Hii ni aina ya kumsifu Mungu kwa kumbariki Mungu, lakini kwa kuonyesha heshima kubwa kama mfalme, kujishusha chini, kusujudu au kupiga magoti, kuonyesha yeye ni mkuu sana wa kuogofya zaidi ya wafalme wote na wakuu wote ulimwenguni.

Zaburi 5:7 Bali mimi, kwa wingi wa fadhili zako, Nitaingia nyumbani mwako; Na kusujudu kwa kicho, Nikilielekea hekalu lako takatifu.

Kama mwamini, sifa zako zisiwe za mdomo tu wakati wote, jifunze kupiga magoti, au kusujudu ni ishara ya unyenyekevu  wa hali ya juu. Fanya hivyo nyakati za sifa, nyakati za maombi.

4) Kusifu kusiko na maandalizi: Kwa kiyahudi huitwa Tehillah:

Aina ya kusifu moyoni mwako, kwa namna isiyo na maandalizi Fulani maalumu, mfano wa kwaya, ni nyimbo ambazo zitainuka  katikati ya mapito yako fulani, wakati mwingine unapopitia kutendewa mema mengi na Mungu, na hapo ghafla tu moyoni mwako unasikia kumsifu Mungu, kumpa utukufu.

Kwamfano Daudi alipokuwa anapitia magumu,au anashindaniwa na Mungu, akimtafakari Mungu, mara anaachilia kinywa chake, Mungu anaanza kububujisha nyimbo mpya ulimini mwake.

Mfano mwingine wa sifa kama hizi, ni pale Mungu alipowavusha wana wa Israeli, bahari ya Shamu, na kuona maadui zao wamefunikwa na habari, ndipo Israeli wote, pamoja na Miriamu na wanawake wakasimama kumwimbia Mungu nyimbo za Furaha (Kutoka 15).

Mfano mwingine ni pale Mariamu alipomtembelea Elizabeti, na kutolewa unabii kuwa atamzaa Masihi, alishangalia na ghafla  akafungua  kinywa chake kwa wimbo, kumsifu Mungu kwa namna hii,  (Luka 1:46-56)

Hivyo kila mkristo, katika majira yote, vipindi vyote, viwe vyepesi, viwe vingine, hana budi kutafakari na kufungua kinywa chake kumsifu Mungu kwa aina hii ya sifa ya Tehillah. Ni muhimu sana, na inampendeza, Mungu, hii haina maandalizi, haina mpangilio maalumu, hutoka moyoni mwako, kwasababu Fulani Mungu alizokuonekania.

5) Kusifu kwa vyombo vya muziki: Kwa kiyahudi huitwa “Zamar”.

Mungu aliwaagiza pia watu wake, wamwimbie si kwa vinywa vyao tu na makofi, lakini pia pamoja na kuchanganya zana mbalimbali za muziki.

Zaburi 150:3 Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;

4 Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;  5 Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6 Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya.

Ni wazi kuwa kuchanganya ala mbalimbali,kama vile gitaa, vinanda, filipi, tarumbeta, ngoma, zeze, marumba, n.k. Katika kumwimbia Mungu, huongeza ladha na hisia njema katika kumsifu, na hivyo hupendeza sana machoni pake. Wapo watu hawaamini katika matumizi ya vyombo. Lakini maandiko yanatuagiza tumsifu Mungu kwa hivyo.

6) Kusifu kwa kupaza sauti kuu: Kwa kiyahudi huitwa “Shabach”.

Aina hii ya sifa, ni kwa kupaza sauti yako juu sana kwa Mungu. Hii Huonyesha ujasiri wa Mungu unayemwabudu, na kuutangazia umati na ulimwengu kuwa yupo Mungu mahali hapo anayeabudiwa.

Zaburi 47:1 Enyi watu wote, pigeni makofi, Mpigieni Mungu kelele kwa Sauti ya shangwe.

Sifa hizi zina nguvu sana, ndio zile ambazo ziliangusha kuta za Yeriko. Wana wa Israeli walipoambiwa wapaze sauti zao kwa Mungu. Zile sauti hayakuwa makelele tu, bali zilikuwa ni sauti za kumtukuza Mungu.(Yoshua 6:20).

Tumwimbiapo Mungu, hatupaswi tuwe kama mabubu, au tuimbe kinyonge, au kwa kutegea-tegea. Mungu anajivunia sana watu wale wanaomwabudu kwa ujasiri, kwa kufumbua vinywa vyao na kupaza sauti zao kwa nguvu  kumwadhimisha yeye.

7) Kusifu kwa ukiri, shukrani, kutoa: Kwa kiyahudi huitwa “Todah”.

Ni aina ya sifa inayofanana na ile ‘Yadah’,ya  kumwinulia Mungu mikono kumwimbia. Isipokuwa hii, ni kumwadhimisha Mungu, kwa matendo ambayo bado hujayaona kwa macho. Kutambua uweza wa Mungu, hata kama huoni matokeo yoyote, na kumshukuru katika hayo. Hata pale ambapo hujisikii.  .

Mfano ya sifa hizi, ni labda wewe ni mgonjwa, daktari amekuambia una siku chache za kuishi, ukiangalia umeombewa mara nyingi hakuna matokeo yoyote, lakini unakumbuka Neno la Bwana linalosema ‘kwa kupigwa kwake sisi tumepona’. Unaanza kufurahi, ukimwinulia mikono Mungu na kumshukuru ukisema asante, Bwana kwa kuniponya, huku ukimsifu katika hali yako hiyo hiyo ya udhaifu.

Sifa hizo ni muhimu sana kwetu, na zinaugusa moyo wa Mungu kwa namna ya kipekee, Kwasababu kamwe haziwezi kuwa na unafiki ndani yake.

Hizi zinapaswa ziwepo ndani yetu wakati wote. Unakumbuka ahadi za Mungu ambazo bado huoni zimetimia, unamsifu Mungu sana kwa furaha kana kwamba umekwisha vipata vyote sasa, umetafuta kazi umekosa, unamsifu Mungu kana kwamba umepokea ripoti ya kuajiriwa.

Hizi ndio aina saba za sifa, ambazo ukiziachilia katika maeneo yako yote ya kiibada. Utampendeza Mungu sana. Lakini pia zinapaswa ziwe katika Roho na Kweli, tafsiri yake, ni sharti mtu umsifuye Mungu uwe umeokoka, umeshatambua kazi ya Kristo ya ukombozi kwenye maisha yako ipoje. Tayari wewe ni  mfuasi wa Kristo. Ndipo sifa hizo zitakubalika. Vinginevyo haziwezi kumpendeza Mungu hata kama utazifanya zote kwa ufasaha.

Ikiwa bado hujaokoka, na upo tayari kufanya hivyo leo. Basi kwa msaada unaweza fungua hapa kwa msaada wa mwongozo huo wa kumkaribisha Yesu maishani mwako.>>>>  KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

SAFINA NI NINI?

Je kumwimbia Mungu kwa kucheza ni sahihi kibiblia?

(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post