SWALI: Ayubu alimaanisha nini kusema..Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena huko uchi vilevile; Aliwezaje kurudi tena tumboni mwa mama yake tena uchi je hilo jambo linawezekana?
JIBU: Kauli hiyo aliisema Ayubu baada ya kupotelewa na familia yake na mali zake. Lakini Kwa ujasiri akamtukuza Mungu katika hali hiyo pia, kwa kusema maneno hayo;
Ayubu 1:21
[21]akasema, Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena huko uchi vilevile; BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe.
Lakini swali lipo hapo, katika kurudi tumboni mwa mama yake uchi. maana yake ni nini?
Ikumbukwe kuwa sisi hatukutoka tu katika tumbo la wanamke bali pia katika tumbo la ardhi, hiyo ndio mama wa ulimwengu. yaani mama wetu wa kwanza.
soma;
Zaburi 139:15
[15]Mifupa yangu haikusitirika kwako,
Nilipoumbwa kwa siri, Nilipoungwa kwa ustadi pande za chini za nchi;
Mhubiri 12:7
[7]Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa,
Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.
Hivyo Ayubu aliposema nami nitarudi tena huko huko hakumaanisha mama yake mzazi, bali mama wa ulimwengu wote yaani ardhi.
Na ndivyo ilivyo kwa kila mmoja wetu, hukuja na kitu, utaondoka bila kitu chochote. Ukiwa uchi vilevile.
lakini jambo lingine la kufahamu kuwa, wale walio ndani ya Kristo, wafikapo kule ng’ambo hawataonekana uchi, bali watapewa vazi jipya la rohoni la Kristo Yesu, ndio ile miili mipya ya utukufu isiyoona uharibifu idumuyo milele.
2 Wakorintho 5:1-3
[1]Kwa maana twajua ya kuwa nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii ikiharibiwa, tunalo jengo litokalo kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono, iliyo ya milele mbinguni.
[2]Maana katika nyumba hii twaugua, tukitamani sana kuvikwa kao letu litokalo mbinguni;
[3]ikiwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tu uchi.
Swali ni je! Umeandaliwa vazi lako baada ya kuondoka?
Kumbuka unalipokea kwa kumwamini Yesu Kristo leo, okoka tubu dhambi zako, ubatizwe, kisha upokee kipawa cha Roho Mtakatifu. vazi lako liwe limekamilika., ili siku ile usionekane uchi.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.
SIFA ZA MAMBA YULE MKUBWA WA AYUBU.
MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MFUNGO.
Rudi Nyumbani
SWALI: Je Daudi aliwachukia viwete na vipofu? Kama tunavyosoma katika 2Samweli 5:6-9. Je! habari hiyo tunaielewaje?
JIBU:
2 Samweli 5:6-9
[6]Kisha mfalme na watu wake wakaenda Yerusalemu ili kupigana na Wayebusi, wenyeji wa nchi ile; hao ndio waliomwambia Daudi, wakisema, Usipowaondoa vipofu, na viwete, hutaingia humu kamwe; huku wakidhania ya kuwa Daudi hawezi kuingia humo.
[7]Lakini Daudi aliipiga ngome ya Sayuni; huu ndio mji wa Daudi.
[8]Naye Daudi alisema siku hiyo, Yeye atakayewapiga Wayebusi, na apande kwenye mfereji wa maji, na kuwapiga viwete, na hao vipofu, ambao roho yake Daudi inawachukia. Kwa sababu hii watu husema, Wako vipofu na viwete hawawezi kuingia nyumbani.
[9]Basi Daudi akakaa ndani ya ngome hiyo, akaiita mji wa Daudi. Kisha Daudi akajenga toka Milo na pande za ndani.
Habari hii inazungumzia wakati ule ambao Daudi alikwenda kuiteka Yerusalemu na kuufanya kuwa mji wa Mungu.
Alipofika na kukutana na wenyeji wa mji huo, walimdharau na kumsema kimafumbo kwa kauli ya mzaha kumwambia “Usipowaondoa vipofu, na viwete, hutaingia humu kamwe;”
Wakiwa na maana vita yake ni ya kupambanishwa na watu dhaifu kabisa wa mji, mfano wa vipofu na viwete, hao ndio apambane nao, lakini sio majemedari wa nchi ile. Akiweza hao walau ndio aingie sasa kujaribu kuuteka, huku wakijua kuwa hata hilo Daudi hataweza kwasababu walimwona ni dhaifu.
Na ukweli wakati huo Daudi hakuwa na nguvu yoyote, kwasababu ndio kwanza ametoka kuupokea ufalme. Hawakujua kuwa nguvu zake tangu zamani zina Mungu, ndio zile zilizomwangusha Goliathi ni silaha zake kwa jiwe moja.
Lakini Daudi aliipowafuatia na kuwapiga, na kuwaangamiza, naye alitumia pia jina hilo hilo la vipofu na viwete kimizaha akiwaita wayebusi waliomwonyeshea dharau..pamoja na hilo Daudi alionyesha kuwachia sana.
Lakini mistari hiyo hakumaanisha kuwa anawachukia viwete na vipofu. Hapana Kama ingekuwa hivyo asingemkaribisha Mefiboshethi mtoto wa Yonathani katika nyumba yake ya kifalme kuketi mezani pake daima..(2Samweli 9). Na ikumbukwe kuwa Daudi alikuwa anamcha Mungu na kuwakumbuka sana wanyonge.
Lakini pale inaposema….
“Kwa sababu hii watu husema, Wako vipofu na viwete hawawezi kuingia nyumbani”.
Ni kwamba kufuatana na Daudi kuwasema viwete na vipofu akiwarejea wayebusi, ukazuka msemo huo, ‘vipofu na viwete hawana ruhusu kuingia nyumbani mwa Mungu;. Lakini haikuwa hivyo’..
Misemo na namna hii ilikuwepo tangu zamani hata kuhusu ile habari ya mfalme Sauli, ya kutabiri (1Samweli 19:24), na kuhusu ike habari za mtume Yohana, pale wale mitume wengine waliposikia Kauli ya Bwana Yesu inayosema ikiwa nataka huyu awepo mpaka nijapo, wakadhani kuwa Yohana hata onja mauti kamwe, mpaka Yesu atakaporudi kumbe hawakumuelewa Bwana Yesu, hakumaanisha vile.(Yohana 21:22-23)
Na ndivyo ilivyodhaniwa kwa Daudi kwamba anawachukia vipofu na viwete, kumbe aliwamaanisha wayebusi.
Lakini ni nini hasaa tunaweza jifunza..katika tukio hilo?
Ni kawaida ya adui yetu anapokaribia kushindwa hunyanyua ujasiri wake kwa kiwango cha juu sana. Mji ambao uligeuzwa kuwa wa Bwana, na mwema kuliko yote, ulitanguliwa na dhihaka nyingi za kukatisha tamaa. Hata ukuta aliokuwa anaujenga Nehemia, ambao sehemu yake iliendelea kudumu kwa mamia ya miaka mbeleni ulitanguliwa na dhihaka nyingi za kuvunjishwa moyo. wakisema hata mbweha akipita juu yake utaanguka.
Silaha hiyo hiyo anaitumia adui leo, unapoona maono makubwa ya kuitenda kazi ya Bwana ndani yetu, vitisho vya adui huanzia hapo, aah wewe huna upako, wewe huwezi kuhubiri, huna pesa, huna elimu ya kukutosha, huna uzoefu, utafungwa..hizo zote ni dhihaka, Daudi alishazitambua toka kwa Goliathi, ndio maana akawashinda wayebusi.
Hivyo ni kusimama imara kuitetea injili, kwa imani tukijua hakuna linaloshindikana kwake yeye aaminiye. Na palipo na dhihaka nyingi ndipo palipo na mafanikio makubwa.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
Katika agano la kale, Israeli walikuwa na makusanyiko mengi, ambapo walikutanika kumfanyia Mungu ibada, na kuzishika sikukuu. Lakini pia yalichaguliwa makusanyiko mengine yaliyoitwa mikutano/makusanyiko ya makini. Makusanyiko haya yalifanyika katika siku ya saba ya sikukuu ya Pasaka, na siku ya nane, baada ya sikukuu ya vibanda. Katika siku hiyo hawakuruhusiwa kufanya kazi yoyote. Bali ilitengwa kwa ajili ya kujitakasa, au kujisogeza karibu na Mungu,
Hivi ni vifungu baadhi vinavyoielezea siku hiyo;
Hesabu 29:35 Tena siku ya nane mtakuwa na kusanyiko la makini sana; hamtafanya kazi yo yote ya utumishi;
36 lakini mtasongeza sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kusongezwa kwa moto, harufu ya kupendeza kwa Bwana; ng’ombe mume mmoja, na kondoo mume mmoja, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza wakamilifu saba.
Walawi 23:34 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Siku ya kumi na tano ya mwezi huo wa saba ni sikukuu ya vibanda muda wa siku saba kwa Bwana.
35 Siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu; msifanye kazi yo yote ya utumishi.
36 Mtamsongezea Bwana sadaka kwa moto siku saba; siku ya nane kutakuwa na kusanyiko takatifu kwenu; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka kwa moto; ni mkutano wa makini huu; msifanye kazi yo yote ya utumishi
Kumbukumbu 16:8 Siku sita utakula mikate isiyotiwa chachu; na siku ya saba na uwe mkutano mtukufu kwa Bwana, Mungu wako, usifanye kazi yo yote.
Huo mkutano mtukufu ndio kusanyiko la makini.
Hekalu la kwanza pia lilipomalizika liliwekwa wakfu katika siku hii ya kusanyiko la makini
2Nyakati 7:9 Hata siku ya nane wakaita kusanyiko la makini; kwa maana walishika kuitakasa madhabahu siku saba, na sikukuu siku saba.
Sehemu nyingine mikusanyiko hii iliitishwa rasmi, kwa lengo la kujimimina kwa Mungu kuomba, kwa ajili ya maovu na majanga ambayo yanaipata nchi. (Yoeli 1:14 – 2:15). Kusanyiko hili liliitwa pia kama kusanyiko kuu.
Je! Ufunuo wake ni upi leo?
Kama vile tulivyo na mikusanyiko ya aina mbalimbali leo, mfano ya shule ya jumapili, ya semina, ya injili n.k. Vivyo hivyo hatuna budi kuwa na makusanyiko ya makini. Ambayo ni mikusanyiko ya mifungo na maombi. Ambapo tunapata muda wa kujimimina kwa undani kabisa uweponi mwa Mungu, kumtaka aingilie kati mambo yetu.
Je! unaithamini? Mungu aliyesema tusiache kukusanyika pamoja (Waebrania 10:25). Hakumaanisha tu mikusanyiko ya jumapili, lakini pia ya mifungo na maombi.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
SWALI: 2Timotheo 3:7, ina maana gani inaposema;
wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.
JIBU: Katika kitabu cha 2Timotheo sura ya tatu(3), kuanzia mstari 1-9. Kinaeleza sifa za watu watakaozuka katika siku za mwisho. Tabia ambazo hapo mwanzo hazikuwepo. Sasa ukisoma pale utaona zimeorodheshwa baadhi ikiwemo kutokea watu wenye kupenda fedha, watu wakali, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu,..na nyinginezo
Lakini ipo sifa nyingine inatajwa pale, kuwa litazuka kundi la watu wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake..ndio hao ambao anaeleza sasa mbeleni, wanajifunza sikuzote ila wasiweze kuufikia ujuzi wa kweli.
Tusome;
2 Timotheo 3:5-9
[5]wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.
[6]Kwa maana katika hao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu, na kuchukua mateka wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi, waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi;
[7]wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.
[8]Na kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo na hawa wanapingana na ile kweli; ni watu walioharibika akili zao, wamekataliwa kwa mambo ya imani.
[9]Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa dhahiri.
Maana ya ujuzi;
Ujuzi maana yake ni ufanisi au kukifanya kitu kwa utashi wote. Mtu anaweza akafanya jambo lakini akiwa hana ujuzi nalo litakuwa ni kituko kama sio hasara kabisa. Kwamfano mtu atasema, mimi naweza kujenga (na hajasomea ujenzi). Hivyo akaenda kununua tofali na kuanza kupandisha, unajua ni nini kitamkuta? kwasababu hajui kanuni za ujenzi anaenda kufanana na yule mtu aliyejenga nyumba yake juu ya machanga.
Ndivyo ilivyokuwa kwa hawa watu, hawakuufikia huo ujuzi wa kweli, kwasababu walikuwa na nia zao wenyewe za tofauti na sio ya Kristo, walilenga kuwakusanya wanawake waliokuwa na mizigo ya dhambi, kama daraja lao, na hifadhi yao ya kihuduma, ili watumize malengo yao. Sasa Kwa urefu wa tabia za wanawake hao bofya link hii uwasome >>> Wanaowachukua wanawake wajinga mateka ni akina nani?
Lakini huo ujuzi wa kweli ni upi?
ujuzi wa kweli ni UTAUWA/ UTAKATIFU. Mtu anayefikia kilele cha kuifahamu kweli ya Kristo huishia katika utakatifu wa kweli. Tunalisoma hilo katika;
Tito 1:1
[1]Paulo, mtumwa wa Mungu, na mtume wa Yesu Kristo; kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu, na ‘ujuzi wa kweli’ ile iletayo utauwa;
Umeona ujuzi wa kweli, lazima ulete utauwa.
Lakini watu hawa walikuwa na mfano wa utauwa lakini walizikana nguvu zake kimatendo, ndio maana hawakufikia..waliitwa wakristo lakini wakristo jina, waliitwa mitume, wainjilisti, manabii, waalimu, watakatifu, lakini nia zao zipo penginepo. Walikuwa na elimu za vyuoni, wanajua kuyachambua maandiko, na vifungu vyote, lakini maisha ya utakatifu yapo mbali na wao.
Ndilo linalotendeka leo hii, maarifa tuliyonayo kuhusu Mungu ni mengi, zaidi hata watu wa kale, tuna wingi wa vyuo vya theolojia, na makanisa, na mafudisho mengi. Lakini maisha ya wengi hayamwakisi Kristo katika utakatifu wa kweli.
ndio hili neno linatimia,
wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli
Ni swali la kujiuliza na sisi, je! wokovu wetu umefikia ujuzi wa kweli? Kumbuka hizi ni siku za mwisho, mafundisho uliyonayo yanakusukuma kwenye nini? FUATA UTAKATIFU.
Bwana akubariki
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?
Rudi Nyumbani
SWALI: Bwana Yesu alikuwa anamaanisha nini kusema.. “Yatosha kwa siku maovu yake”.
Mathayo 6:34
[34]Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.
JIBU: Bwana, hataki tuwe na hofu ya vitu vya huko mbeleni (ambavyo bado havijafikiwa), si mpango wa Mungu tubebe mizigo mingi kwa wakati mmoja, kwasababu hatujaumbiwa asili hiyo, ndio maana hata katika ile sala ya Bwana tunasema; utupe “siku kwa siku” rikizi yetu.
Hasemi utupe riziki ya “mwaka mzima” kana kwamba tukikosa vyote leo hatutaishi.. bali siku kwa siku..
Kwanini iwe hivyo?
Sasa katika hali yetu ya kibinadamu tunajua kabisa mihangaiko yetu, taabu zetu, shughuli zetu za kila siku, mara nyingi huwa haziwi safi kama tunavyotarajia, wakati mwingine kama sio kujikwaa, basi tunakutana na mambo mengi pia ya kukosesha yasiyompendeza Mungu. Hayo ndio maovu yake.
Tunakutana na watukanaji, na wazinzi, na waharibifu, wenye mizaha, wasumbufu, n.k. hivyo kiuhalisia katika mambo yetu mema, maovu pia hutokea. Hivyo kitendo cha kuyataabikia sana ya mbeleni, tafsiri yake ni kuwa tunayaleta na maovu yake pia leo. Na matokeo yake tutalemewa na maovu kichwani Na kujikuta tunamkosea Mungu.
Bwana anataka tupambane kwanza na yale ya leo, ya kesho tutapewa nguvu ya kushindana nayo. Kwa tafsiri nyingine ikiwa wewe ni wa kubeba mambo mengi ya mbeleni, dhambi itakulemea na kukushinda.
Yatosha kwa siku maovu yake.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Ni kwa jinsi gani Mungu anapatiliza maovu ya baba zetu sawasawa na Kutoka 20:5-6?
Nilikuwa naomba kujua utofauti kati ya DHAMBI, UOVU na KOSA kibiblia.asante!!
Rudi Nyumbani
Kama unao uhakika huo basi ni jambo jema lakini swali, ni kitu gani kinachokupa uhakika huo?.
Je! Ni imani uliyonayo?..au Ni dhehebu ulilonalo?, Au ni matendo unayoyafanya?…au ni nini?.
Kama ni Imani (kwamba unamwamini na akija ni lazima uende naye) basi fahamu kuwa anaweza akaja na usiende naye ijapokuwa unayo imani.
Kama ni dhehebu ndilo linalokupa uhakika wa kwenda na Bwana pindi atakaporudi, basi fahamu kuwa hio pekee haitoshi..
Pamoja na dhehebu lako bora, na jina lako bora bado unaweza usimwone siku atakaporudi..
Je ni Matendo yako mema ndiyo yanayokupa uhakika? (Kwamba hudhulumu mtu, hutukani,huibi, unasaidia wengine n.k)
Kama ni matendo tu, ndio yanayokupa uhakika wa kwenda na Bwana, basi fahamu kuwa atakaporudi unaweza pia usimwone.
Sasa ni kitakachopaswa kumpa mtu uhakika ya kwamba atakapokuja BWANA basi ataenda naye??.
Hebu tuangalie jibu lake katika biblia, kupitia maneno ya Bwana YESU (Atakayerudi).
Yohana 3:1 “Basi palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi.
2 Huyo alimjia usiku, akamwambia, Rabi, twajua ya kuwa u mwalimu, umetoka kwa Mungu; kwa maana hakuna mtu awezaye kuzifanya ishara hizi uzifanyazo wewe, isipokuwa Mungu yu pamoja naye.
3 Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu”
Umeona sifa ya mtu atakayemwona Bwana siku ile?.
Si dhehebu kwasababu Nikodemo alikuwa ni wa dhehebu la Farisayo lililo bora (Matendo 26:5), wala si Imani kwa Mungu, kwasababu Nikodemo alikuwa tayari anamwamini Mungu na pia amemwamini YESU.
Lakini Bwana YESU anaonyesha kuwa hayo yote hayawezi kumsaidia mtu, isipokuwa kuzaliwa mara ya pili (kuwa kiumbe kipya katika roho).
Ni nini maana ya kuzaliwa mara ya pili???..Bwana YESU amefafanua katika mistari inayofuata kwamba ni kuzaliwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu (yaani ubatizo wa maji kama ishara ya utangulizi wa utakaso, na ubatizo wa Roho Mtakatifu).
Ubatizo wa Roho Mtakatifu ndio ukamilifu wa utakaso wa Mtu, na mtu anapoupokea huo pamoja na ubatizo wa Maji, anafanyika kuwa kiumbe kipya kupitia kazi za Roho Mtakatifu ndani yake.
Jambo hili limewekwa vizuri zaidi na Mtume Paulo kupitia waraka wake kwa Tito.
Tito 3:4 “Lakini wema wake Mwokozi wetu Mungu, na upendo wake kwa wanadamu, ulipofunuliwa, alituokoa;
5 si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu”.
Je swali umejazwa Roho Mtakatifu kama tiketi ya kumwona Bwana na kwenda naye siku ile?.
Waliojazwa Roho Mtakatifu, wanaongozwa na Roho Mtakatifu, na mtu aliyejaa Roho Mtakatifu, hawezi kuwa mtu wa kidunia, wala kuupenda ulimwengu..kwasababu roho iliyopo ndani yake inamsukuma kufikiri yaliyo ya juu.
Mtu alijaa Roho mtakatifu kama muhuri wa kumwona Bwana, hawezi kufanana kimwonekano na watu wa ulimwengu, badala yake anakuwa nuru kwao, na hawezi kushirikiana na matendo ya giza.
Na kama hauna uhakika Bwana akirudi hautaenda naye, ni vizuri ukapata huo uhakika…
Pengine unaweza kuhitimisha kwa kusema siku atakapokuja, kama nitaenda naye au sitaenda naye…“Mungu anajua”…lakini hebu fikiri hili…
“Mwalifu anatangaza kuwa atakuja kukudhuru”
Halafu wewe unasema siku atakapokuja, “yeye anajua kama atanidhuru au hatanidhuru”.
Umeona?..kama hautachukua tahadhari ni wazi kuwa atatimiza lengo lake..lakini kama utajidhatiti basi utapata uhakika kama atatimiza lengo lake au la!.. wala huwezi kamwe kumwachia maamuzi afanye yeye!!.
Vivyo hivyo na sisi ni lazima tuwe na uhakika kwamba atakapokuja tutakwenda naye au hatutakwenda naye, na si kumwachia yeye atufanyie maamuzi..
Tukimwachia yeye tutakuwa tumemfanya yeye kuwa mwenye upendeleo, na yeye hana upendeleo.
1Petro 1:17 “Na ikiwa mnamwita Baba, yeye ahukumuye kila mtu pasipo upendeleo, kwa kadiri ya kazi yake, enendeni kwa hofu katika wakati wenu wa kukaa hapa kama wageni”
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.
Waoga ambao hawataurithi uzima wa milele ni watu wa namna gani?(Ufunuo 21:8).
BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?
Shetani huwa ana kauli zake, za uongo ambazo hupenda kuwaaminisha watu, kuwa kuna mambo mwanadamu hawezi kuyafanya akiwa hapa duniani hata iweje.
Tukisoma habari ya Ayubu wakati ule shetani alipokwenda kumshitaka kwa Mungu.
Mungu alipomuuliza kuhusu mwenendo wake, majibu ya shetani yalikuwa ni kwamba Mungu amemzungushia wigo, kutunza alivyonavyo, Na kama atapotezewa alivyonavyo, basi atamkufuru Mungu waziwazi. Hivyo Mungu akaruhusu shetani amjaribu Ayubu, amchukulie alivyo navyo vyote, lakini uongo wa kwanza, ukashindwa, alipoona Ayubu anamtukuza Bwana katika misiba yake. Hiyo ni kuonyesha kuwa mwanadamu yoyote anaweza kuishi bila msukumo wa mali,wala mtu wala kitu chochote katika hii dunia.
Lakini baadaye tena, akaendelea mbele kuzungumza uongo mwingine, alipoona Ayubu bado yupo na Mungu, akamwambia Mungu, yote yanawezekana kwa mwanadamu kuvumilia, lakini hili la kuugusa mfupa wake,kumtesa, kamwe hawezi kuvumilia atakukufuru tu. Mimi ninawajua wanadamu uwezo huo hawana, nilishawafundisha pia huko duniani.
Ayubu 2:4 Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Ngozi kwa ngozi, naam, yote aliyo nayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake.
5 Lakini sasa nyosha mkono wako, uuguse mfupa wake na nyama yake, naye atakukufuru mbele za uso wako.
6 Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yeye yumo mkononi mwako; lakini tunza tu uhai wake. 7 Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana, akampiga Ayubu na majipu mabaya tangu wayo wa mguu hata utosi wa kichwa.
8 Naye akashika kigae cha kujikunia; akaketi majivuni. 9 Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe.
10 Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.
Hilo nalo likashindikana. Kumbe mtu, hata kuupoteza uhai wake kwa ajili ya Kristo, linawezekana.
Ni nini Bwana anatufundisha kwa mawazo ya adui kwetu sisi ?
Leo hii ni rahisi sana kusikia, kauli kama, hakuna mtakatifu duniani! Ni rahisi kuona mtu anaanguka ovyo katika dhambi, na kutumia kisingizio kuwa yeye sio malaika. Utasikia kauli kama haiwezekani mtu kuacha vyote alivyonacho kwa ajili ya Kristo. Ndugu tambua kuwa hizo ni kauli za ibilisi ndani ya moyo wako. Adui anapenda kumshusha thamani mtu, kumweka kama kiumbe ambaye hawezi kujisimamia, hafundishiki, haaminiki.
Ni kweli mwanadamu kuwa na ukamilifu wa Mungu haiwezekani (Ndio sababu Yesu akaja kutukomboa), lakini kuna viwango Fulani Mungu anajua tunaweza kuvifikia, akalithibitisha hilo kwa Ayubu. Kama Ayubu ameweza kwanini wewe ushindwe, usijishushe thamani.
Neema haijaja kutuambia kuwa sisi hatuwezi, bali imekuja kutuwezesha zaidi kuwa wakamilifu mbele za Mungu, yaani pale Ayubu aliposhindwa sisi tunasaidiwa kwa hiyo, na kutufanya tupokelewe kikamilifu mbele za Mungu, hiyo ndio kazi ya Neema (Soma Tito 2:11-12).
Kamwe usiruhusu hayo maneno ya kushushwa thamani na ibilisi, kwamba wewe huwezi mpendeza Mungu, huwezi kuacha vyote kwa ajili yake. Yesu alisema tutakuwa wakamilifu kama Baba yetu alivyomkamilifu. Tunachopaswa kufanya ni kuamini kuwa hilo linawezekana na kuonyesha bidii katika hilo kumpendeza yeye. Na neema ya Mungu itatusaidia kufikia kilele Hicho cha juu kabisa.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini Labani aseme Yakobo ni Mfupa wake na nyama yake?(Mwanzo 29:14)
Rudi Nyumbani
Warumi 7:18 “Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa KUTAKA NATAKA, bali KUTENDA LILILO JEMA SIPATI.
19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo”.
Je na wewe ni miongoni mwa watu wanaosumbuliwa na utumwa wa namna hiyo?.. UNATAKA na kutamani lakini unajikuta HUPATI au HUWEZI au HUFANYI au HUPOKEI?.
> Unataka kumtumikia Mungu lakini unajikuta huwezi..
> Unataka kuwa msomaji wa Neno lakini unajikuta hufanikiwi.
> Unataka na kutamani kufanya mema na mazuri kwaajili ya Mungu wako lakini hufanikiwi n.k
Kama UMETAKA mambo mengi na huoni uelekeo wa kulipata, basi huwenda NJIA unayoitumia kutaka na kutafuta hayo mambo ina kasoro..
Hebu jaribu njia hii, ya kutaka mambo halafu uone kama hutapata uyatakayo,
Na njia hii si nyingine Zaidi ya ile aliyoitumia Danieli.
Danieli 9:3 “Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ILI KUTAKA kwa MAOMBI, NA DUA, PAMOJA NA KUFUNGA, NA KUVAA NGUO ZA MAGUNIA NA MAJIVU.
4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake”
Umeona kanuni Danieli aliyoitumia??… HAKUTAKA mambo kwa kupiga ramli, au kwenda kwa waganga wa kienyeji, wala kwa kwenda Kuwadhulumu watu au kukorofishana na watu au kula rushwa, au kujipendekeza kwa watu bali KWA MAOMBI, NA DUA NA KUFUNGA NA KUVAA NGUO ZA MAGUNIA NA MAJIVU, na matokeo yake alipata alichokuwa anakitafuta..
Na sisi tunajifunza mambo hayo hayo…
> Tukitaka Amani nyumbani.. kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.
> Tukitaka Amani katika ndoa.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.
> Tukitaka Amani kazini.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.
> Tukitaka Akili darasani.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.
> Tukitaka Ulinzi na afya.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.
> Tukitaka Ujazo wa Roho Mtakatifu.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.
Luka 11:13 “Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”
Kama Bwana YESU alivyosema kuwa “kuna mambo hayawezekaniki, isipokuwa kwa kufunga na kuomba”
Wafilipi 2:13 “Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, KUTAKA KWENU na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.
14 Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano”
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.
Nini maana ya “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi”?
Yafuatayo ni mambo saba (7) ya kuzingatia wakati wa Mfungo.
1.MAOMBI
Mfungo wowote ili uwe ni mfungo ni lazima uambatane na Maombi.. Mfungo usiokuwa na maombi ni sawasawa na bunduki isiyo na risasi.
Marko 9:28 “Hata alipoingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kwa faragha, Mbona sisi hatukuweza kumtoa?
29 Akawaambia, Namna hii haiwezi kutoka kwa neno lo lote, isipokuwa kwa kuomba”.
Mathayo 17:21 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]
Kila siku utakayofunga hakikisha unaomba, (tena maombi ya masafa marefu, tofauti na siku nyingine).
2. KUWA MTULIVU.
Unapofunga usiwe mtu wa kuhangaika na kuzurura huku na kule, bali kuwa mtu wa faragha muda mwingi, wakati wa mfungo si wakati wa kuzurura kwenye makao ya watu, au vijiwe..kuwa mtulivu, tafuta maeno tulivu na omba.
3. ZUIA KINYWA.
Mfungo sio tu kujizuia kula na kunywa, bali pia kujizuia kuzungumza kupita kiasi…. Unapofunga si wakati wa kusema na kila mtu, si wakati wa kujiachia (hususani kwa watu wasio wa kiroho) bali ni wakati wa faragha wewe na Mungu wako (kwa kutafuta sauti ya Mungu kupitia maneno yake)
4. EPUKA MATENDO YA MWILI.
Kama ni mwanandoa jizuie kwa kiwango kikubwa au chote kukutana kimwili na mwenzi wako..Vile vile Kama unafanya shughuli fulani inayohusisha mwili wako, ipunguze kwa kiwango kikubwa..
5. PUNGUZA KIWANGO CHA KULA.
Mfungo sio kuhamisha mlo wa asubuhi na mchana na kuupeleka jioni..La! bali ni kuunyima mwili ili roho yako ije juu (inufaike).. Maana yake wakati wa kufungua (kufuturu) usile kiwango kikubwa cha chakula, kwa kufidia mlo wa asubuhi na mchana.. Ukifanya hivyo utakuwa hutendi dhambi, lakini mfungo wako unaweza usiwe na matokeo makubwa kama wa yule ajizuiaye kweli kweli.
6.USILE VYAKULA VITAMU-TAMU.
Wakati wa kufungua epuka kula vyakula vitamu tamu, hususani vile unavyovipenda sana, ambavyo vinakuburudisha sana.. “Kumbuka tena mfungo ni kuunyima mwili na si kuupendeza mwili”… Sasa unapoupa vile vitu ambavyo unavipenda sana, hapo bado kuna kaukasoro katika mfungo wako..
Danieli alikuwa ni mtu aliyejinyima vitu vitamu wakati wa mfungo… na hatimaye mfungo wake ukawa na matokeo makubwa.
Danieli 10:2 “Katika siku zile mimi, Danielii, nalikuwa nikiomboleza muda wa majuma matatu kamili.
3 Sikula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwangu, wala sikujipaka mafuta kabisa, hata majuma matatu kamili yalipotimia”.
7. USIWE MTU WA KUJITANGAZA.
Mathayo 6:16 “Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana; maana hujiumbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao.
17 Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso;
18 ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.
Mfungo unapaswa uwe siri hususani kwa watu walio wa nje (yaani wasiohusiana na wewe).. Kwa ndugu yako wa karibu sana, au mke au mume au watoto, mfungo wako ni ngumu kuwa siri kwao, kwasababu unaishi nao katika maisha ya kila siku (hata usipowaambia watafahamu tu)..Hivyo unaweza kuwashirikisha ikiwa lengo lako si upokee utukufu kutoka kwao.
Vile vile kiongozi wako wa kiroho, au mpendwa mwenzako (wa Imani moja na wewe) unaweza kumshirikisha mfungo wako (ikiwa lengo lako si kupata utukufu kutoka kwake) bali kupokea hamasa au kumhamasisha (Hilo ni jambo jema).
Lakini kama lengo lako ni wewe uonekane kwao ili utukuzwe, basi mfungo huo unaweza usizae matunda yale mtu anayoyategemea..
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?
JUMATANO YA MAJIVU NI TENDO LA KIMAANDIKO?
SWALI: Neno ‘huisingizia sheria na kuihukumu sheria’ maana yake nini? (Yokobo 4:11)
Yakobo 4:11 Ndugu, msisingiziane; amsingiziaye ndugu yake, au kumhukumu ndugu yake, huisingizia sheria na kuihukumu sheria. Lakini ukiihukumu sheria, huwi mtenda sheria, bali umekuwa hakimu.
JIBU: Ili kuelewa vifungu hivyo Mtume Yakobo kwa uongozo wa Roho alikuwa na maana gani aliposema Mtu amsingiziaye ndugu yake au amuhukumuye ndugu yake huisingizia sheria na kuihukumu sheria, Tafakari mfano huu.
Raisi ya nchi amendea mahali Fulani kwa ajili ya shughuli zake za kimaendeleo, lakini katika kupita pita kwake akaona familia moja iliyo fukara sana, na alipotathimini tatizo nini akaona walikuwa wote ni walemavu hawawezi kufanya kazi kabisa, hivyo kwa huruma zake akaagiza wajengewe nyumba, wapewe na msaada wa chakula kutoka serikali kila mwezi, walipiwe na pia bili za maji na chakula kwa kipindi chote wawapo hai.
Lakini Yule raisi alipoondoka, mkuu wa mkoa wa eneo lile, akaenda kuitazama ile familia ikoje, badala ya kutekeleza agizo la mkuu wake, akaanza kuwashitaki na kusema hawa hawana ulemavu wa kuwafanya wasifanye kazi, wanajifanya tu wadhaifu, ni wavivu, wanaweza kuendesha maisha yao, hakuna haja ya kuwapa chochote, hivyo akaanza kuwaonea na kuwashutumu, na kuwanyima mahitaji yao kwa wakati, na kuwashurutisha wajitume.
Sasa Kimsingi mtu kama huyu, ni rahisi kudhani, anawaudhi na kuwashutumu tu wale maskini, Lakini kiuhalisia anamudhi na kumshitaki raisi aliyetoa amri ile kwamba walishwe. Kwa tabia hiyo ni kwamba anamshtaki raisi hafikirii vizuri, anatumia fedha za uma vibaya, anatafuta sifa kwa watu, ana maamuzi yasiyokuwa na maana, hata kama huyo mkuu wa mkoa hawazi hivyo, anampenda raisi wake, na anathamini mali zake, lakini kitendo tu cha kuwashutumu wale, ni sawa na anamshutumu aliyewafadhili.
Ndivyo ilivyo na katika kifungu hicho, Wewe kama mwamini, unapomsingizia ndugu yako, Maana yake unakwenda kinyume na sheria ya Kristo tuliyopewa ya kupendana, unapomhukumu ndugu yako unakwenda kinyume na sheria ya Kristo inayosema Usikuhukumu (Mathayo 7:1).
Hivyo unaihukumu hiyo sheria kwamba ina makosa, wakati Bwana aliiona ni bora, lakini wewe unakwenda kinyume na hiyo.
Hivyo sisi kama wana wa Mungu hatujaitwa tuwashutumu watu, tutafute kasoro ndani ya ndugu zetu, kana kwamba sisi, hatuna maboriti kwenye macho yetu, ila tumeitwa tuitende sheria, na kuonyana, na kuelekezana, na kujengana, katika upendo, lakini sio kutoa hukumu kwa wengine, kana kwamba sisi ni mahakimu.
Tumeagizwa tunapomwona ndugu yetu ameghafilika tumrejeshe kwa upendo, sio kwa mashutumu, hiyo ndio sheria ya Kristo.
Wagalatia 6:1 Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.
2 Mchukuliane mizigo na KUITIMIZA HIVYO SHERIA YA KRISTO. 3 Maana mtu akijiona kuwa ni kitu, naye si kitu, ajidanganya nafsi yake.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine: