Category Archive Home

Kwanini MUNGU alimzuia Daudi asimjengee HEKALU? (1Nyakati 17:12)

Jibu: Turejee…

1 Nyakati 17:11-12 “Hata itakuwa, siku zako zitakapotimia, uende na babazo, nitainua mzao wako nyuma yako, atakayekuwa wa wana wako; nami nitaufanya imara ufalme wake.

12 Yeye ndiye atakayenijengea nyumba, nami nitakifanya imara kiti cha enzi cha ufalme wake milele”.

Unabii huu unamuhusu BWANA YESU KRISTO, na si SULEMANI. yeye (YESU) ndiye atakayetokea na kuijenga nyumba ya MUNGU (Hekalu) lililo kamilifu na takatifu,  na nyumba hiyo ni MWILI wake (Yohana 2:19-22).

Lakini pamoja na hayo pia Hekalu la damu na Nyama, Mungu alimzuia Daudi asilijenge KWASABABU alimwaga damu nyingi za hatia na zisizo za hatia, na kwasababu hiyo Mungu hakumruhusu aijenge nyumba ile bali mwanae Sulemani.

1  Nyakati 28:3 “Lakini Mungu akaniambia, Wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu, kwa sababu umekuwa mtu wa vita, nawe umemwaga damu ………………

5 tena katika wana wangu wote (kwani BWANA amenipa wana wengi), amemchagua Sulemani mwanangu ili aketi juu ya kiti cha enzi cha ufalme wa BWANA, juu ya Israeli.

6 Akaniambia, Sulemani, mwanao, ndiye atakayeijenga nyumba yangu na nyua zangu; kwa kuwa nimemchagua awe mwanangu, nami nitakuwa babaye”

Na ni damu za akina na Daudi alizozimwaga?.

   1.DAMU ZA MAADUI.

Daudi alikuwa ni mtu wa vita tangu ujana wake, yeye pamoja na mashujaa wake walikuwa ni watu wa kuua maadui zao kwa upanga, hilo likawa kizuizi kwa Daudi kuijenga nyumba ya Bwana.

   2. DAMU YA URIA.

Damu ya Uria, jemedari aliyoimwaga Daudi, ilikuwa ni kikwazo kikubwa cha Daudi kupata ruhusu ya kuijenga nyumba takatifu ya Mungu atakayokaa..

Kwani laiti Daudi angeijenga nyumba ile pamoja na tendo lake hilo alilolitenda la kumuua Uria na kumchukua mke wake, basi maadui wa Bwana wangeiona hiyo nyumba aliyoijenga na kukumbuka Daudi aliyoyafanya, wangepata sababu ya kukufuru na kukashifu ile nyumba sawasawa na maneno ya Bwana.

2 Samweli 12:13 “Daudi akamwambia Nathani, Nimemfanyia BWANA dhambi. Nathani akamwambia Daudi, BWANA naye ameiondoa dhambi yako; hutakufa.

14 Lakini, kwa kuwa kwa tendo hili umewapa adui za BWANA nafasi kubwa ya kukufuru, mtoto atakayezaliwa kwako hakika yake atakufa”.

Ni lipi tunaloweza kujifunza hapo?

Bwana hakuwahi kupendezwa na mauaji tangu mwanzo, watu wa kale waliruhusiwa kuua kwasababu ya ugumu wa mioyo yao, lakini tangu mwanzo Bwana alikataza mauaji Soma Kutoka 20:13.

Hivyo hatuwezi kuishi sasa kwa kuyaangalia matendo ya Daudi, kama Daudi aliua basi na sisi ndio tuue, kama Daudi alioa wake wengi basi na sisi ndio tuoe wake wengi n.k.

Bali tunamtazama YESU KRISTO sasa aliye Ukamilifu na Utimilifu wa sheria, yeye anasema…

Mathayo 5:38 “Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino;

39 Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili.

40 Na mtu atakaye kukushitaki na kuitwaa kanzu yako, mwachie na joho pia.

41 Na mtu atakayekulazimisha mwendo wa maili moja, nenda naye mbili”.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Bwana alimaanisha nini kusema “Yeye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo”? (Mathayo 23:20)

Daudi alikuwa na wake wangapi, na je ni halali kuwa na wake wengi?

Je! Habari iliyo katika 1Nyakati 21:25, na 2Samweli 24:24, ya Daudi kununua kiwanja  inajichanganya?

MAANA ROHO HUCHUNGUZA YOTE, HATA MAFUMBO YA MUNGU.

Nini maana ya hekima ya maskini haisikilizwi? (Mhubiri 9:16)

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita;

SWALI: Biblia humaanisha nini kwenye vifungu hivi?

Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita; Lakini mkosaji mmoja huharibu mema mengi.


JIBU: Ni vema kwanza kufahamu kwanini watu wanapigana vita?

Zipo sababu nyingi,baadhi ya hizo ni hizi,

Kujilinda, kutoelewana, kulipiza visasi, kutofautiana kiitikadi, au kutanua ngome.

Hivyo ili watu kufikia malengo hayo, njia pekee waionayo ni kutumia silaha, kuuana. Lakini biblia inashauri njia iliyo bora zaidi ambayo inaweza kutumiwa na hatimaye yote hayo yakatatulika. Na njia hiyo ni hekima.

Hekima ni nini?

Hekima ni uwezo wa kipekee utokao kwa Mungu, unaomsaidia mtu kuweza kupambanua, au kutatua, au kuamua jambo Fulani vema. Hivyo kupitia hekima mtu anaweza kuponya vitu vingi pasipo uharibifu wowote, na kuunda mfumo bora.

Sulemani ambaye ndiye aliyeyaandika maneno hayo alijaliwa amani katika ufalme wake, sio kwamba hakuwa na maadui wanaomzunguka hapana, bali alipewa hekima ya kuishi nao, na kuzungumza nao, na kukubaliana nao, hivyo Israeli hakukuwa na kumwagika damu kama ilivyokuwa kwa baba yake Daudi, ambaye yeye kutwa kuchwa alikuwa vitani. Kilichoweza kumsaidia ni hekima ya Mungu ndani yake.

Lakini sehemu ya pili ya mstari huo anasema;

Lakini mkosaji mmoja huharibu mema mengi’.  Akiwa na maana mkosaji mmoja (wa hekima), jinsi anavyoweza kuharibu mipango mingi mizuri ambayo huwenda ilikuwa tayari imeshaleta matokeo mema. Na kweli hili angalia mahali penye viongozi wabovu, huathiri jamii nzima, hata Israeli, Wafalme wa kule ndio waliisababishia Israeli kunajisika kwa muda mrefu hadi kupelekea kwenda utumwani Babeli mfano wa hao walikuwa ni Yeroboamu na Ahabu.

Kwa ufupi vifungu hivi vinatueleza uzuri wa hekima, lakini pia madhara yasababishwayo pale hekima inapokosekana, hata kwa udogo tu.

Je! Mtu anawezaje kupata hekima?

Hekima chanzo chake ni kumcha Mungu. (Mithali 9:10). Ambapo panaanzia kwenye wokovu, kisha kuendelea kuishi maisha ya utii kwa Kristo baada ya hapo.

Mtu wa namna hii, huvikwa, ujuzi huo wa ki-Mungu, na hivyo anakuwa na uwezo wa  kuutibu ulimwengu kwa namna zote. Mioyo, Ndoa,kanisa, jamii, taifa, vyote huponywa kwa hekima msingi huu wa hekima ya ki-Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWA KUWA ROHO BORA ILIKUWA NDANI YAKE.

Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?

USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Matasa ni nini? (1Nyakati 28:17)

Jibu: Turejee..

1Nyakati 28:17 “na nyuma, na mabakuli, na vikombe vya dhahabu safi; na kwa MATASA ya dhahabu, kwa uzani kwa kila TASA; na kwa matasa ya fedha, kwa uzani kwa kila tasa”.

Ukisoma kuanzia juu utaona kuwa hivyo ni vyombo ambavyo vingepaswa viwepo ndani ya MUNGU aliyokusudia kuijenga Mfalme Daudi.

Lakini kwasababu haikuwa mapenzi ya MUNGU mfalme Daudi aijenge ile nyumba bali mwanae (Sulemani)…hivyo ilimbidi Mfalme Daudi ampe maelekezo ya namna ya kuijenga ile nyumba na viwango vyake.

Moja ya maagizo aliyompa kulingana na alivyooneshwa na Bwana ni uwepo wa MATASA ndani ya nyumba hiyo..(kwamba atakapoijenga basi aweke Matasa ya dhahahu ndani yake).

Sasa Matasa yalikuwa ni nini?

Matasa yalikuwa ni “Makarai/mabeseni” ya dhahabu yaliyowekwa ndani ya Hekalu kwa kusudi la kutawadha (kunawa).

Kwasababu ndani ya Hekalu kulikuwa na makuhani wengi waliokuwa wanafanya kazi mbalimbali na kwa zamu, na kulingana na desturi za wayahudi ilikuwa ni lazima kila Kuhani anawe

(atawadhe) kabla ya kuanza kazi ya kikuhani na hata baada ya kumaliza.

Hivyo vyombo hivyo (MATASA) vilitumika kuhifadhia maji kwaajili ya shughuli hiyo.

Na pia vilikuwepo VITASA hivi vilikuwa ni vibaluli vidogo vya kuweza kushikwa kwa mkono, tofauti na Matasa ambayo yalikuwa yanabeba ujazo mkubwa wa maji, na vitasa ndio vile vinavyotajwa katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana  mlango wa 15 na 16.

Ufunuo 15:5 “Na baada ya hayo nikaona, na hekalu la hema ya ushuhuda mbinguni lilifunguliwa;

6 na wale malaika saba, wenye mapigo saba, wakatoka katika hekalu, wamevikwa mavazi ya kitani safi, ya kung’aa, wamefungwa vifuani mwao mishipi ya dhahabu

7 Na mmoja wa wale wenye uhai wanne akawapa wale malaika saba VITASA SABA vya dhahabu, vimejaa ghadhabu ya Mungu, aliye hai hata milele na milele”.

Ni nini tunajifunza katika hayo?

Tunachoweza kujifunza ni kuwa matasa ya Hekalu la duniani yalijaa maji ya kuoshea makuhani lakini vile VITASA vya Hekalu la mbinguni vimejaa hasira na hukumu ya MUNGU kwa wanadamu wasiomcha yeye.

Bwana atusaidie tumtafute, tusipotee wala kuangukia katika hukumu yake.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?

YAKINI NA BOAZI.

Je wakati Bwana YESU anazaliwa shetani alikuwa amefungwa?

Vihekalu vya fedha vya Artemi vilikuwaje? (Matendo 19:24).

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini Eliya afunge Mbingu miaka mitatu na nusu? (1Wafalme 17:1)

Swali: Ni ipi sababu ya Nabii Eliya kufunga mbingu, mvua isinyeshe kwa miaka mitatu na nusu?


Jibu: Turejee..

1Wafalme 17:1 “Basi Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu”.

Sababu kuu ya Mungu kufunga Mbingu kwa muda wa miaka mitatu na nusu kupitia kinywa cha Eliya nabii, ni MAOVU ya wana wa Israeli pamoja na mfalme wao aliyeitwa Ahabu.

kwani mfalme Ahabu wa Israeli alimwoa YEZEBELI, mwanamke wa nchi ya Lebanoni  aliyekuwa Mchawi na kahaba na mwenye kumwabudu mungu baali (2Wafalme 9:27), na hivyo akawakosesha Israeli wote, na kuwafanya wamwambudu mungu baali badala ya MUNGU WA MBINGU NA NCHI.

Sasa kitendo cha Taifa zima kumwacha Mungu wa Israeli na kwenda kuabudu miungu mingine, ni Kosa kubwa sana na lenye matokeo makubwa sana kwa Taifa..

Sasa kwa kosa hilo la Mfalme, na malkia wake na Watu karibia wote wa Israeli kumwabudu baali, ndio ikapelekea MUNGU kuadhibu nchi nzima kwa kufunga mbingu mpaka mioyo yao ilipofunguka na kumgeukia Bwana.

Na utaona MUNGU alishatangulia kuwatahadharisha wana wa Israeli kupitia kinywa cha Nabii Musa, kuhusiana na makosa ya kuabudu miungu mingine na matokeo yake, KUWA MBINGU ZITAFUNGWA..

Kumbukumbu 11:16 “Jitunzeni nafsi zenu, mioyo yenu isije ikadanganywa, mkageuka na kutumikia miungu mingine na kuiabudu;

17 hasira za Bwana zikawaka juu yenu, NAYE AKAFUNGA MBINGU KUSIWE NA MVUA, wala nchi isitoe matunda yake; mkaangamia kwa upesi mtoke katika nchi nzuri awapayo Bwana”.

Na utaona pia Maombi ya Mfalme Sulemani, wakati analiweka wakfu lile Hekalu yalilenga hayo hayo…

1Wafalme 8:35 “Ikiwa mbingu zimefungwa, hata hakuna mvua, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakiomba wakikabili mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kuiacha dhambi yao, wakati ule utakapowatesa;

36 basi, usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na ya watu wako Israeli; unapowafundisha njia iliyo njema, iwapasayo kuiendea; ukanyeshe mvua juu ya nchi yako, uliyowapa watu wako iwe urithi wao”.

Hivyo hiyo ndio sababu ya mbingu kufungwa wakati wa Eliya, (maovu ya kumwabudu baali), na ndio maana utaona pale walipojinyenyekeza tu na kutubia, basi Eliya aliomba na mbingu zikafunguka.

1Wafalme 18:38 “Ndipo moto wa Bwana ukashuka, ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa, na kuni, na mawe, na mavumbi, ukayaramba yale maji yaliyokuwamo katika mfereji.

39 Na watu wote walipoona, wakaanguka kifudifudi; wakasema, Bwana ndiye Mungu, Bwana ndiye Mungu.

40 Eliya akawaambia, Wakamateni hao manabii wa Baali, asiokoke hata mmoja. Wakawakamata; na Eliya akawachukua mpaka kijito cha Kishoni, akawaua huko.

41 Naye Eliya akamwambia Ahabu, Haya! Inuka, ule, unywe; kwani pana sauti ya mvua tele”.

Na jambo kama hili bado linaendelea kiroho na kimwili, kama tukimtumikia Bwana basi Bwana atatunyeshea mvua yake ya Baraka, lakini kama tutamwacha basi mbingu za Baraka zitafungwa, hivyo huu si wakati wa kusita sita katika mawazo mawili, bali ni wakati wa kufanya maamuzi thabiti ya kusimama na Bwana.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Baali alikuwa nani?

YEZEBELI ALIKUWA NANI

RUHUSU TOHARA IPITE JUU YA KARAMA YAKO.

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

Rahabu kwenye biblia.

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Yohana 20:22 Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa;

SWALI: Biblia inaposema ‘Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa’. Je tuna mamlaka ya kufanya hivyo wakati wote?

Yohana 20:22 Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu. 23 Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa.


JIBU: Mstari huu ukitafsirika vibaya unaweza kuleta maana isiyosahihi ikidhaniwa kuwa kwa uweza wetu, tunaweza kuwaondolea watu dhambi, na kuwafungia pale tutakapo. Hapana.

Biblia inatuambia mwenye uweza wa kusamehe dhambi kwa namna hiyo ni Bwana Yesu tu.

Luka 5:21 Basi, wale waandishi na Mafarisayo wakaanza kuhojiana wakisema, Ni nani huyu asemaye maneno ya kukufuru? N’nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?

22 Na Yesu alijua hoja zao, akajibu akawaambia, Mnahojiana nini mioyoni mwenu? 23 Lililo jepesi ni lipi? Kusema, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, uende? 24 Lakini, mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (alimwambia yule mwenye kupooza). Nakuambia, Ondoka, ujitwike kitanda chako, ukaende zako nyumbani kwako.

Lakini kwanini Bwana Yesu atoe mamlaka yake Kwa mitume wake?

Ni kufuatana na ahadi aliyowaahidia ndani yao, ambayo ni Roho Mtakatifu tunayoisoma katika huo mstari wa 22. “Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu”.

Kazi ya Roho Mtakatifu ni kumshuhudia Kristo. Hivyo mitume walipewa ushuhuda wa Kristo ndani yao (ndio Injili). Na kwa kupitia hiyo, mamlaka ya kufunga na kufungua wanakuwa nayo, ndani ya hiyo hiyo injili.

Hivyo walipokwenda kuhubiri, na watu wakaamini. Walipotamka kusamehewa dhambi zao, basi wale watu walisamehewa. Vilevile walipokwenda kuhubiri, kisha injili yao ikapingwa, wakakatishwa tamaa na kuacha kuhubiri hapo, mpaka wakafikia hatua ya kuwakung’utia mavumbi yao, Basi hiyo nyumba au huo mji rohoni umefungiwa dhambi. Hauwezi kuokoka kwa namna nyingine yoyote, mpaka watakapokuwa tayari kugeukia injili ya wale waliopelekwa.

Mathayo 10:13 Na nyumba ile ikistahili, amani yenu na iifikilie; la, kwamba haistahili, amani yenu na iwarudie ninyi.

14 Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, kung’uteni mavumbi ya miguuni mwenu.

15 Amin, nawaambia, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule.

Hiyo ndio namna ambayo watu wa Mungu, huondoa dhambi na kufungia dhambi wanadamu.

Mamlaka hii pia Yesu ameiweka katika kanisa.

Kwasababu kanisa pia ni mwili wake, Hivyo ikiwa yupo mwamini mmoja ambaye alitenda dhambi, akakutwa na mabaya, basi kanisa linaweza kumwombea, akasamehewa dhambi (Yakobo 5:14).

Lakini pia ikiwa yupo ambaye ni mwasi, ameiacha njia, anapoonywa mara kadhaa kisha harejei kwenye mstari, ndugu anapomwacha au kanisa linapomtenga moja kwa moja, basi Mungu naye anamhesabu kama mtu wa mataifa asiyeamini.(Mathayo 18: 15-18,)

Hivyo ni vema kufahamu, mamlaka hii ipo, kwenye injili ya Kristo, lakini pia ipo ndani ya kanisa. Kila mmoja anapaswa amtii Kristo kupitia watumishi wake. Kwasababu lolote walitendalo si wao bali ni Roho Mtakatifu ndani yao, aliyewavuvia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya andiko hili  “Sauti yake hamkuisikia wakati wo wote, wala sura yake hamkuiona.(Yohana 5:37)”

MAOMBI KWA WENYE MAMLAKA.

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Warumi.

Kitabu hichi kama kinavyojitambulisha, “Waraka wa Paulo kwa Warumi” mwandishi wake ni Mtume Paulo.

Kitabu hiki alikiandika akiwa Korintho mahali palipoitwa Kenkrea (Warumi 16:1)

Tofauti na nyaraka nyingine ambazo Paulo aliziandika kwa makanisa ambayo alikuwa tayari ameshayatembelea/ameyapanda hapo nyuma. Waraka huu tunaonyeshwa Paulo hakuwahi kufika Rumi. Lakini alisikia mwitikio wao wa injili, hivyo likawa ni tamanio lake pia awafikie na wao, lengo likiwa sio kupanda juu ya msingi wa watu wengine bali wajengane kiimani.(1-18),

Na kweli tamanio lake tunaona lilikuja kutimia baadaye, kama tunavyosoma kwenye kitabu cha matendo ya mitume, katika ile ziara yake ya mwisho kama mfungwa, alifika Rumi, na huko akafanikiwa kuhubiri injili sawasawa na tamanio lake (Matendo 27-28).

Hichi ni kitabu kinachoeleza misingi ya imani  ki-mpangilio . Kuanzia asili ya wokovu wetu, haki ya Mungu, na mwenendo wa kikristo. Hivyo kuna umuhimu mkubwa sana kwa mkristo yoyote kukielewa vema kitabu hichi.

Migawanya mikuu ya kitabu hichi.

     1) Nguvu ya injili? (1: 1-17)

Baada ya Paulo, kueleza tamanio lake la kuwafikia katika utangulizi wake, tunaona katika mistari hiyo anasisitiza kwanini afanye hivyo? Ni kwasababu ya ‘Nguvu ya Injili yenyewe’, Akisema Injili ni uweza wa Mungu uuletao wokovu. Na hivyo haionei haya kuihubiri kwa watu wote..kwa wayahudi na watu wa mataifa pia.

  1. Hatia kwa wanadamu wote (1:18- 3:20)

Sehemu ya pili Paulo anaeleza jinsi wanadamu wote walivyopungikiwa na utukufu wa Mungu kuanzia watu wa mataifa ambao wameshindwa kuitii kweli ya Mungu iliyofunuliwa kwao kwa mambo yake yaliyo dhahiri kabisa yanayotambulika hata pasipo sheria, kwamba mambo ya asili yanafundisha haki ya Mungu, lakini walikataa kutii. Vilevile na wayahudi  pia ambao walikuwa na sheria lakini walishindwa kuyatenda yote kulingana na yaliyoandikwa. Hivyo hakuna hata mmoja mwenye haki,  wote wamewekwa chini ya hukumu ya ghadhabu ya Mungu, kwa kushindwa kutenda haki yote.

  1. Haki kwa Imani (3:21-5:21)

Kwa kuwa wanadamu wameshindwa kuwa wakamilifu, Paulo anaeleza njia ambayo Mungu ameitoa kwa  mwanadamu kuweza  kuhesabiwa haki. Ni njia ambayo inadhihirishwa bila matendo ya sheria, tunayoipata kwa kumwamini tu Yesu Kristo. Yaani pale mtu anapomwamini Bwana Yesu kwamba kifo chake kimeleta ukombozi wa roho yake, basi mtu huyo anakuwa amehesabiwa haki kuwa ni Mtakatifu mbele za Mungu.

Kulithibitisha hilo Paulo akaendelea kueleza  kwa mfano wa Ibrahimu jinsi Mungu alivyomhesabia haki bila sheria yoyote, na kwamba sisi pia tutahesabiwa kwa njia hiyo hiyo.

  1. Maisha mapya ndani ya Kristo (6:1-8:39)

Katika sehemu hii Paulo anaeleza maisha baada ya kuhesabiwa haki, kwamba mkristo anapaswa aendelee kutakaswa na kuwa kama Kristo. Lakini kutokana na mashindano kati ya mwili na roho. Ili aweze kuushinda mwili anapaswa ajifunze kuishi kwa Roho, kwa kuruhusu utendaji kazi wake ndani yake. Maneno hayo ameyarudia pia katika waraka wake kwa Wagalatia (Wagatia 5:16). Kwamba mtu anayeenenda kwa Roho kamwe hawezi kuzitimiza tamaa za mwili.

Lakini mbele kidogo anaendelea kuhimiza upendo wa milele wa Mungu, uliodhihirishwa kwetu kupitia Yesu Kristo, ambao hauwezi kutenganishwa na kitu chochote tukijuacho duniani au mbinguni.

  1. Uhuru wa Mungu wa kuchagua, na kusudi lake kwa Waisraeli (9:1- 11:36)

Kwenye sura hizi, Paulo anaeleza uhuru wa Mungu wa kuchagua, na siri iliyokuwa nyuma ya Israeli kukataa injili. Anaeleza mpango wake wa wokovu kwa mataifa na waisraeli, kwamba iliwapasa wao wakatae injili ili sisi watu wa mataifa tuipokee injili. Na hivyo anaeleza sisi pia tunapaswa tuupokee wokovu kwa unyenyekevu wote kwasababu tusipokaa katika kuamini tutakatwa, kama wao walivyokatwa.

  1. Tabia ya maisha mapya katika Kristo (Warumi 12:1- 15:3 )

Paulo anaeleza jinsi tunavyopaswa kuitoa miili yetu kama dhabihu iliyo hai takatifu yenye kumpendeza Mungu, tunawajibu wa kupendana sisi kwa sisi, tusiwe watu wa kulipa kisasi, tuishi kwa heshima, tuhudumiane katika karama mbalimbali tulizokirimiwa na Mungu, tutii mamlaka zilizowekwa, vinywa vyetu vitoe baraka, tumtumikie Mungu kwa bidii, tudumu katika sala, tuishi kwa amani sisi kwa sisi, pia tuweze kuchukiliana katika viwango mbalimbali vya imani bila kuhukumiana.

Kwa ufupi sura hizi zinaeleza tabia zetu zinapaswa ziweje baada ya wokovu.

  1. Hitimisho  (15:14- 19:27)

Paulo anaeleza mpango wake wa kuwafikia Warumi pindi atakapokuwa anasafiri kwenda Spania kuhubiri injili. Akiomba akumbukwe katika maombi dhidi ya watu wabaya, na mwisho anatoa salamu kwa watakatifu wote walio Rumi, pamoja na angalizo kwa watu waletao fitna katika injili waliyoipokea wajiepushe nao

KWA UFUPI.

Kitabu hichi kinaeleza

Haki ya Mungu ikoje, ambapo hapo mwanzo ilidhaniwa inapatikana kwa sheria au matendo ya mwanadamu, kumbe sio, hayo yalishindwa bali kwa njia ya Yesu Kristo, lakini pia kinaeleza namna ambavyo tunaupokea wokovu huo kwa neema kwa njia ya Imani, na pia jinsi Mkristo anavyopaswa aishi kulingana na wokovu alioupokea. Kwamba sio kwasababu amehesabiwa haki bure bila matendo, basi aishi maisha kama atakayo, hapana vinginevyo atakufa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NJIA/BARABARA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.

Uchambuzi na Mwandishi wa kitabu cha Wagalatia

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Rudi Nyumbani

Print this post

USIOGOPE.. USIOGOPE…

Danieli 10:19 “Akasema, Ee mtu upendwaye sana, usiogope; amani na iwe kwako, uwe na nguvu, naam, uwe na nguvu. Aliposema nami nikapata nguvu, nikasema, Ee Bwana wangu, na aseme Bwana wangu; kwa maana umenitia nguvu”.

HOFU ni mlango wa Adui, lakini UJASIRI katika Neno la MUNGU ni UFUNGUO wa mafanikio.

Ifuatayo ni mistari michache ya kusimamia wakati wa tufani, na mashaka, na vitisho vya adui na majaribu yake yotw yajapo.. Simama nayo, na utauona Wokovu wa Bwana.

  1. USIOGOPESHWE NA SAUTI YA KIFO.

Waamuzi 6:23 “BWANA akamwambia Amani iwe pamoja nawe; usiogope; hutakufa”.

2 Samweli 12:13 “Daudi akamwambia Nathani, Nimemfanyia BWANA dhambi. Nathani akamwambia Daudi, BWANA naye ameiondoa dhambi yako; hutakufa”.

  1. USIOGOPSHWE MAJARIBU MAZITO.

Isaya 41:10 “usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu”.

  1. USIOGOPE KUMTUMIKIA MUNGU.

1 Nyakati 28:20 “Kisha Daudi akamwambia Sulemani mwanawe, Uwe hodari, mwenye moyo mkuu, ukatende hivyo; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa BWANA, Mungu, Mungu wangu, yu pamoja nawe; yeye hatakupungukia wala kukuacha, hata itakapomalizika kazi yote ya huo utumishi wa nyumba ya BWANA”.

Matendo 18:9 “Bwana akamwambia Paulo kwa maono usiku, Usiogope, bali nena, wala usinyamaze”.

  1. USIOGOPE UNAPOBAKI PEKE YAKO.

Isaya 41:13 “Kwa maana mimi, BWANA, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia”.

  1. USIOGOPE JUU YA UZAO WA TUMBO LAKO.

Isaya 43:5 “Usiogope; maana mimi ni pamoja nawe; nitaleta wazao wako toka mashariki, nitakukusanya toka magharibi”.

Mwanzo 35:17 “Ikawa alipokuwa anashikwa sana na utungu, mzalisha akamwambia, Usiogope, maana sasa utamzaa mwanamume mwingine”.

Mwanzo 21:17 “Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko”.

  1. USIOGOPE KUINGIA MJI MWINGINE.

Yoshua 1:9 “Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.

Kumbukumbu 1:21 “Tazama, BWANA, Mungu wako, ameiweka nchi mbele yako; haya panda, itamalaki, kama BWANA, Mungu wa baba zako, alivyokuambia; usiogope wala usifadhaike”.

Mwanzo 46:3 “Akasema, Mimi ni Mungu, Mungu wa baba yako, usiogope kushuka mpaka Misri; maana nitakufanya uwe taifa kubwa huko.

4 Mimi nitashuka pamoja nawe mpaka Misri; nami nitakupandisha tena bila shaka; na Yusufu ataweka mkono wake juu ya macho yako”.

  1. USIOGOPE MAJESHI YA ADUI YANAPOJIPANGA.

2 Wafalme 6:16 “Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao”.

Zaburi 27:3 “Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea”.

  1. USIOGOPESHWE NA TAARIFA ZA GHAFLA ZENYE KUHUZUNISHA.

Mithali 3:25 “Usiogope hofu ya ghafula, Wala uharibifu wa waovu utakapofika.

26 Kwa kuwa BWANA atakuwa tumaini lako, Naye atakulinda mguu wako usinaswe”.

BWANA AKUBARIKI.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

UWE KIKOMBE SAFI 

UTAJUAJE KAMA WEWE NI MTUMISHI WA MUNGU NA KRISTO YU PAMOJA NAWE?.

Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 10:1 Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;

SWALI: Naomba kuelewa tafsiri halisi ya maneno tuyasomayo kwenye Mithali 10:1.

Mithali 10:1

[1]Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye.


JIBU: Mpumbavu kibiblia ni mtu yeyote aliyemkosa Mungu ndani yake, ambaye kwa njia hiyo anaweza kuonyesha tabia yoyote mbaya, aidha wizi, au kiburi, au umalaya, au uchawi, au hasira, mwingine atakuwa mlevi, mtukanaji, mwongo, jambazi, mchoyo, mbinafsi, mkorofi n.k.

Chimbuko ni kumkosa Mungu ndani yako.

Sasa mwana wa namna hii kibiblia sio tu anaiathiri roho yake lakini pia hata waliomzaa.

Mithali 10:1

[1]Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye.

Lakini kauli hiyo inapaswa eleweke vizuri, sio kwamba mwana akiwa na hekima ni furaha ‘tu’ kwa baba, mama hausiki, au akiwa mpumbavu ni mzigo tu kwa mama baba hausiki.

Hapana, mambo hayo yanawapata wote.. akiwa na hekima wote hufurahi, vilevile akiwa mpumbavu wote huhuzunika.. Ndio maana sehemu nyingine anasema..

Mithali 17:25

[25]Mwana mpumbavu ni huzuni kwa babaye, Na uchungu kwa mamaye aliyemzaa.

Wazazi wote hufurahishwa au huhuzunishwa kwa tabia husika za watoto wao.

Lakini alipoonyesha kama kuwatenganisha, ni kuelezea ‘hisia za juu zaidi’ zitokeazo kulingana na mzazi na mzazi.

Kimsingi mtoto akiwa na hekima, baba huwa anajivunia sana mtoto huyo, utaona baba anajigamba kwa ajili ya mwanae..Mfano tu wa Sulemani kwa Daudi, hekima yake ilikuwa ni fahari ya babaye Daudi.

Lakini akiwa ni mpumbavu, tengeneza picha mtoto ni teja, na kibaka, na mlevi, kiuhalisia utaona akina mama ndio wanateseka zaidi na kuumia juu ya watoto wao. Wanapatwa na mzigo mzito sana moyoni. Na hiyo huwa inawasukuma kuzunguka huku na huko kutafuta msaada. Tofauti na wababa, watamwonya, mara ya kwanza, mara ya pili, mara ya tatu wakiona haonyeshi geuko lolote, ni rahisi kuachana nao.

Ni nini tunaonyeshwa rohoni?

Si mwilini tu. Rohoni Kristo anafananishwa na Baba, na Kanisa lake ni Mama.

Wote sisi ni watoto ambao Kristo ametuzaa ndani ya kanisa lake, tuwapo na hekima (tunamcha), tunatembea katika misingi ya Neno lake, kwa kuzingatia viwango vya upendo na utakatifu, tujue kuwa Kristo hutukuzwa na hujivunia sana sisi. Lakini tuwapo wapumbavu, tunajiumiza zaidi sisi wenyewe. Kwamfano sababu mojawapo ipelekeayo makanisa kupoteza furaha na amani,  ni kukosekana umoja na upendo.

Bwana atusaidie.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.

MJUE SANA YESU KRISTO.

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

Rudi Nyumbani

Print this post

USIKOSE MAZIKO (Mhubiri 6:3)

SWALI: Naomba kufahamu nini maaana ya mhubiri 6:3?

Mhubiri 6:3

[3]Mtu akizaa watoto mia, akaishi miaka mingi, nazo siku za maisha yake ni nyingi, lakini nafsi yake haikushiba mema; tena ikiwa, zaidi ya hayo, amekosa maziko; mimi nasema, Heri mimba iliyoharibika kuliko huyo;


JIBU: Mhubiri katika jicho la kibinadamu anaelezea jinsi inavyoonekana kama ni hasara kubwa sana, kwa mtu ambaye amejitaabisha maisha yake yote, kutengeneza heshima, kwanza kwa kuwa na watoto wengi, lakini pia kwa kujinyima raha, kuwekeza vema vitu vyake ili siku za kufa iwe heshima kubwa kwake, hata baada ya hapo aache jina kwa uzao wake wote.

Lakini mambo yanatokea kinyume chake, anakufa kama mtu asiye na kitu, au kwa aibu,  hata baada ya hapo anasahaulika kabisa ijapokuwa aliwekeza muda wake mwingi kujijengea jina.. Sasa mhubiri anasema ni heri mimba iliyoharibika kuliko huyu kwasababu kimsingi mimba huwa inasahaulika kweli muda mfupi,na haiwi na maziko ya watu, lakini haijatabika kwa lolote, kuliko huyu ambaye ametabika sana maisha yake yote, kuacha kumbukumbuku , halafu amesahaulika mfano ule ule wa kama mimba iliyoharibika.

Mfano wa watu kama hawa alikuwa ni Ahabu, ambaye alikuwa na watoto sabini, na ufalme mkubwa lakini alikufa kwa aibu, damu yake ililambwa na mbwa. Pamoja na mkewe Yezebeli ambaye mzoga wake uliliwa kabisa na mbwa, hakuwa na maziko. Ikawa ni fedheha kubwa sana kwao (1Wafalme 22),

Lakini maana hasaa ya huo mstari rohoni ni ipi?

Maziko halisi ni yale ya Mungu. Kukosa maziko ya kibinadamu, hakuwezi kukufanya udharauliwe milele. Lakini ukikosa maziko ya Mungu ni aibu na kudharaliwa milele.

Ukipata fedha zote duniani, ukazaa watoto wengi ambao watalirithi jina lako, ukawa mtu maarufu, mpaka ukawa mfalme wa nchi, jina lako likakumbukwa hata vizazi elfu baadaye, kama hujafa ndani ya Kristo. Ni heri mimba iliyoharibika kuliko wewe. Huna kumbukumbu lolote mbinguni

Mwamini Kristo leo, akuoshe dhambi zako. Jiulize ukifa leo katika dhambi, huko uendako utakuwa mgeni wa nani? Wokovu ni sasa, saa iliyokubaliwa ni leo. Fungua moyo wako mpokee Yesu, hata kufa kwako kuwe kuna thamani.

Zaburi 116:15

[15]Ina thamani machoni pa BWANA Mauti ya wacha Mungu wake.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Maana ya Mhubiri 1:9 “wala jambo jipya hakuna chini ya jua”. 

Nini maana ya hekima ya maskini haisikilizwi? (Mhubiri 9:16)

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Rudi Nyumbani

Print this post

MHESHIMU MCHUNGAJI WAKO.

Kila mahali pana mamlaka yake, na mamlaka hizo huwa ni  wajibu kwa walio chini yake kuzitii. Kwamfano katika familia Mungu ameweka mamlaka, Baba awe kichwa, na mama msaidizi wake, hivyo ni wajibu wa watoto kuwatii wazazi wao . Familia haiwezi kusimama,.kama mtoto atataka nafasi ya baba, kwamba yeye ndio atoe maamuzi ya mwisho, au ajiamulie la kufanya, awapangie wazazi wake majukumu ya ndani. hilo haliwezekani.

Vilevile katika ngazi ya utawala wa kidunia, Mungu kaziweka mamlaka na anataka watu wote wazitii, kwasababu hazijaamuriwa na mwanadamu bali yeye Mungu mwenyewe..

Warumi 13:1-2

[1]Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu.

[2]Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu.

Tito 3:1-2

[1]Uwakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema; [2]wasimtukane mtu ye yote, wasiwe wagomvi, wawe wema, wakionyesha upole wote kwa watu wote.

Sasa hizi ni mamlaka za kidunia. Zipi kuhusu Mungu, unadhani hana mamlaka?

Mungu pia ameweka mamlaka yake duniani, ambayo ni kuu kupita hizo zote, na kupitia hiyo huwahudumia watu wake. Na anataka tuitii na kuitetemekea kwasababu ni yeye mwenyewe atendaye kazi kupitia hiyo.

Je mamlaka hiyo kaiweka kupitia nani?

Bila shaka kupitia wachungaji wetu/waangalizi wetu, ndani ya kanisa

Ni vema kufahamu kuwa kiongozi yoyote wa kiroho (anayeisimamia kweli). Hakujiteua mwenyewe kwenye nafasi hiyo.  Mitume wa Yesu hawakujichagua wao. Bali walichaguliwa na Mungu mwenyewe.

Mtu yeyote aliyepewa maono ya kuanza kanisa, na ukajikuta upo chini yake, au kateuliwa na Roho Mtakatifu mwenyewe ndani ya kanisa (Matendo 14:23), Huyo ni wa kumtii sana. Kama vile unavyowatii watawala au mazazi wako kwenye familia, haijalishi atakuwa na mapungufu kiasi gani, au umri wake ni mdogo au mkubwa kiasi gani, awe mwenye uwezo au asiye na uwezo kiasi gani.

Kwanini uwaheshimu.

1) Wanajitaabisha kwa ajili yako kukuchunga, kukuonya na kukuombea.

Hivyo wajibu ni wako kurudisha moyo wa upendo, na kuwasikiliza.

1 Wathesalonike 5:12-13

[12]Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni; [13]mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi.

2) Watasimama mbele ya kiti cha hukumu siku ya mwisho kutoa hesabu juu yako.

Hivyo ni wajibu kuonyesha moyo wa kunyenyekea kwao.

Waebrania 13:17

[17]Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.

Madhara ya kutowasikiliza/ kutowatii.

i) Watafanya kazi ya Mungu kwa kuugua.

Hapo kwenye Waebrania 13:17b anasema..

..ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi

Na matokeo yake utendaji kazi ndani ya kanisani utakuwa hafifu. Ukishaanza kuonyesha tabia ya kutosikiliza unachoelekezwa, unapewa jukumu hutekelezi, hurudishi mrejesho, unafanya tofauti na wengine, yeye anataka uende kulia wewe unaenda kushoto, , yeye anafundisha hiki wewe unafundisha kile. Fahamu kuwa jambo hilo litamhuzunisha kiongozi wako. Na hivyo kupelekea hamasa ya kuhudumu kupungua. Na madhara yake ni kuwa Mungu kukata utendaji kazi wake mahali hapo,

ii) Dhara lingine ni kuwa utajisababishia adhabu kwa Mungu.

Wakati ule Haruni na Miriamu dada yake. walimnenea Musa maneno mabaya kwasababu na mke wake ambaye hakuwa myahudi. Mungu aliwaadhibu kwa kumpiga ukoma Miriamu kwasababu tu hiyo ya kutoonyesha adabu kwa mtumishi wake.

Hesabu 12:7-8

[7]Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote;

[8]Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la BWANA yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?

Ni kosa kumnenea vibaya mchungaji wako. Epuka masengenyo na uasi na matabaka ndani ya kanisa. Uonapo kosa mwombee, au mfuate mweleze  uwapo naye peke yake. Hilo litamjenga zaidi ya kutoa malaumu na manung’uniko. Adui hutumia sana njia hii kuleta mafarakano na magomvi, na mapigo kanisani.

Mheshimu mchungaji wako, zaidi ya raisi wa nchi kwasababu yeye ni balozi wa mbinguni na Mungu atakuinua (1Petro 5:1-6)

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi

Ipi tofauti kati ya KUHANI na MCHUNGAJI.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Rudi Nyumbani

Print this post