Maana ya 2Wakorintho 9:11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote

Maana ya 2Wakorintho 9:11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote

SWALI: Nini tafsiri  ya 2 Wakorintho 9:11-12

[11]mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu.


JIBU: Katika sura hii mtume Paulo analillsisitiza kanisa la Wakorintho, uthamani wa huduma ya utoaji kama njia mojawapo ya utiifu katika kuikiri wa injili (9:13).

Na hapa anaongezea kuwa Mungu hutoa utajiri katika vitu vyote (si tu vya rohoni tu, bali pia vya mwilini). Na kwamba yeye ndiye huwapa watu mbegu za kupanda na chakula.

Hivyo atutajirishapo lengo lake ni tutumie utajiri huo kwa kutenda mema (9:8), (yaani kuwapa maskini hususani watakatifu), kwasababu ndivyo ilivyokuwa kwa Kristo(9:9). Na si tutumie katika anasa na ufahari, na ubinafsi.

Ndio hapo anasema “mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote”. Na kama tukifanya hivyo, mitume wanasema shukrani zinamfikia Mungu kwa kutii kazi yao hiyo ya kutuhimiza sisi kutoa.

2 Wakorintho 9:11-12

[11]mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu. 

[12]Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani nyingi apewazo Mungu; 

Hivyo Bwana anatutaka kila atufanikishapo tujue amekusudia tuwasidie wengine walio maskini husasani watakatifu, kwasababu kwa njia hiyo shukrani nyingi humfikia Mungu.

Zaidi vifungu hivi vinasisitiza pia jinsi Mungu anavyoongeza baraka pale tunapotoa sana, akisema atoaye haba hatavuna haba,(9:6). kile tupandacho ndicho tutakachovuna kwake. 

Bwana atusaidie tuwe watoaji katika hali zote.

ubarikiwe.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> 

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

FAIDA NYINGINE MUHIMU YA KUMTOLEA MUNGU.

USITAFUTE FAIDA YAKO MWENYEWE BALI YA WENGINE.

Mistari ya biblia kuhusu shukrani.

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest

0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments