Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, Karibu katika kuyatafakari maneno ya uzima.
Sulemani, mtoto wa Daudi, katika kitabu chake cha mhubiri, kilichojawa na utafiti wa hali ya juu wa mambo mengi ya kimaisha yamuhusuyo mwanadamu, Tunaona mwishoni kabisa mwa utafiti wake alihitimisha kwa maneno haya;
Mhubiri 12:11 “Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; HAKUNA MWISHO WO WOTE WA KUTUNGA VITABU VINGI; NA KUSOMA SANA HUUCHOSHA MWILI. 13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu. 12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili. 13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu”.
Mhubiri 12:11 “Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; HAKUNA MWISHO WO WOTE WA KUTUNGA VITABU VINGI; NA KUSOMA SANA HUUCHOSHA MWILI.
13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.
12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili.
13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu”.
Sulemani alikuwa ni mtafiti sana, na kama kusoma na kutunga vitabu, basi alitunga vingi sana, na katika vyote (viwe Vya ki-Mungu na visivyo wa ki-Mungu ) alijaribu kutafuta siri, na mwongozo sahihi wa mwanadamu. Lakini tunaona akapata jawabu, ambalo ni rahisi sana kwa wote. Na jawabu lenyewe ni hili “kumcha Mungu na kuzishika amri zake”.
Akasema unaweza ukakesha kusoma vitabu vingi sana katika huu ulimwengu, na matokeo ya kusoma sana, ni kudhoofika, Na bado usipate ukweli mwingine zaidi ya ule ule “kumcha Mungu na kuzishika amri zake”. Ndio maana akahitimisha kwamba Mtu akizingatia sana hilo, laweza kuzidi usomaji mwingi tuuona hapa duniani.
Sasa kumcha Mungu na kuzishika amri zake maana yake ni nini?
Kumbuka biblia nzima inazungumzia habari za Yesu Kristo mwokozi wetu. Hivyo hapo ni sawa na kusema “Kumcha Yesu na kuzishika amri zake”. Hiyo Ni zaidi ya kuwa na maarifa ya vitabu milioni moja, au elimu za shahada elfu,. Ikiwa na maana yule mtu aliyemwamini Yesu, kisha akawa anaishi kwa kulifuata Neno lake, na kuitimiza amri yake kuu, ambayo alisema ni UPENDO. Huyo ni zaidi ya Msomi yoyote aliyewahi kutokea duniani. Au mtunzi yoyote mwenye hekima aliyewahi kuandika vitabu vingi. Ni mtu aliyemaliza kusoma vitabu vyote.
Yohana 13:34 Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. 35 Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.
Yohana 13:34 Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.
35 Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.
Hivyo, usisumbukie maarifa mengi, ukadhani kuwa ndio utamwelewa Mungu, sumbukia Kristo moyoni mwako, sumbukia upendo wa agape moyoni mwako. Kwasababu huko kote utakapokwenda kutakurudisha hapo hapo, ndicho alichokigundua sulemani katika usomaji wake mwingi, hakuna jipya ndani yake Ni kujisumbua tu, ndio maana biblia inasema, yapo mambo mengi aliyoyafanya Yesu na kama yangeandikwa basi vitabu vyote visingetosha duniani.
Yohana 21:25 Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa.
Umeona? Vitabu visingetosha kuandika mambo yote ya Yesu, kwasababu maudhui yake ndio yaleyale, tunayoyasoma katika maneno machache ya kwenye biblia. Ambayo ni wokovu na Upendo wa Mungu. Tukiyatimiza hayo ni sawa na kusoma vitabu vyote duniani.
Hivyo mimi na wewe tuanze kuweka juhudu, kimatendo, kutendea kazi Neno lake, zaidi ya kuhangaika kutafuta maarifa mengi. Kwasababu anasema mwenyewe chanzo cha maarifa ni kumcha yeye, na sio chanzo cha kumcha yeye ni maarifa.
Kumbuka pia asemapo kusoma kwingi huuchosha mwili, hamaanishi uwe mjinga usiwe msomaji kabisa hapana, Lakini anakupa shabaha ni wapi uweke juhudi zako nyingi ili ufanikiwe kuwa na Maarifa ya kweli ya kisomi, Usije ukawa unaufuata upepo.
Tumia nguvu nyingi kuyatendea kazi yale yaliyopo kwenye biblia tu, zaidi ya mihangaiko mingi huku na kule, na elimu nyingi za kidunia. Utaitwa Msomi na Mungu.
Bwana akubariki.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
JINSI YA KUSOMA BIBLIA.
Uchaji ni nini kama tunavyosoma katika 1Timotheo 2:10?
NI NANI ANAYEUFUNGA MLANGO WA MAARIFA?
Rudi Nyumbani
Print this post
Swali: Mathayo 21:19 inasema “mtini ulinyauka mara (maana yake muda ule ule uliolaaniwa)”.. lakini katika Marko 11:20 biblia inasema “mtini ulinyauka kesho yake, na sio siku ile ile ulipolaaniwa”.. Je mwandishi yupi yupo sahihi na yupi hayupo sahihi?.
Jibu: Awali ya yote ni muhimu kujua kuwa biblia haijichanganyi mahali popote na wala haijawahi kujichanganya mahali popote, isipokuwa pambanuzi zetu, fahamu zetu na tafakari zetu ndizo zinazojichanganya pale tunaposoma pasipo kutafakari kwa kina.
Sasa turejee habari hizo moja moja na kisha tuzitafakari tena..
Mathayo 21:18 “Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa. 19 Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; akauambia, Yasipatikane matunda kwako tangu leo hata milele. MTINI UKANYAUKA MARA. 20 WANAFUNZI WALIPOONA, WALISTAAJABU, WAKISEMA, JINSI GANI MTINI UMENYAUKA MARA? 21 Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng’oka, ukatupwe baharini, litatendeka”.
Mathayo 21:18 “Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa.
19 Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; akauambia, Yasipatikane matunda kwako tangu leo hata milele. MTINI UKANYAUKA MARA.
20 WANAFUNZI WALIPOONA, WALISTAAJABU, WAKISEMA, JINSI GANI MTINI UMENYAUKA MARA?
21 Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng’oka, ukatupwe baharini, litatendeka”.
Hapa tunaona mtini ulinyauka “Mara”.. Lakini turejea kitabu cha Marko ni kama tunasoma habari tofauti…
Marko 11:12 “Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa. 13 Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini. 14 Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia”
Marko 11:12 “Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa.
13 Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini.
14 Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia”
Turuke mpaka mstari wa 19-23..
“19 Na kulipokuwa jioni alitoka mjini. 20 NA ASUBUHI WALIPOKUWA WAKIPITA, WALIUONA ULE MTINI UMENYAUKA TOKA SHINANI. 21 PETRO AKAKUMBUKA HABARI YAKE, AKAMWAMBIA, RABI, TAZAMA, MTINI ULIOULAANI UMENYAUKA. 22 Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu. 23 Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng’oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake”
“19 Na kulipokuwa jioni alitoka mjini.
20 NA ASUBUHI WALIPOKUWA WAKIPITA, WALIUONA ULE MTINI UMENYAUKA TOKA SHINANI.
21 PETRO AKAKUMBUKA HABARI YAKE, AKAMWAMBIA, RABI, TAZAMA, MTINI ULIOULAANI UMENYAUKA.
22 Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu.
23 Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng’oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake”
Hapa tunasoma “MTINI ULINYAUKA SIKU INAYOFUATA na si muda ule ule”.. Sasa swali? habari ipi ni sahihi kati ya hizo mbili?
Jibu ni kwamba habari zote ni sahihi, waandishi wote wote wapo sahihi, hakuna hata mmoja aliye mwongo..…
Sasa kwa ufupi ni kwamba mtini haukunyauka muda ule ule Bwana alipoulaani, bali mpaka kufikia kesho yake ndio ulikuwa umekwisha nyauka kabisa..…Sasa swali, kama ni hivyo kwanini Mathayo aseme ulinyauka MARA?…
Jibu la swali hili ni kwamba…si kila mahali panapotumika neno “Mara” panamaanisha “dakika ile ile, au sekunde ile ile, au muda ule”… Hapana!.. Bali neno “Mara” linaweza kumaanisha kipindi fulani cha muda/wakati… ili tuelewe vizuri, tusome habari ifuatayo..
Marko 1:26 “Yule pepo mchafu akamtia kifafa, akalia kwa sauti kuu, akamtoka. 27 Wakashangaa wote, hata wakaulizana, wakisema, Nini hii? Ni elimu mpya! Maana kwa uweza awaamuru hata pepo wachafu, nao wamtii! 28 Habari zake ZIKAENEA MARA KOTEKOTE KATIKA NCHI ZOTE kandokando ya Galilaya”
Marko 1:26 “Yule pepo mchafu akamtia kifafa, akalia kwa sauti kuu, akamtoka.
27 Wakashangaa wote, hata wakaulizana, wakisema, Nini hii? Ni elimu mpya! Maana kwa uweza awaamuru hata pepo wachafu, nao wamtii!
28 Habari zake ZIKAENEA MARA KOTEKOTE KATIKA NCHI ZOTE kandokando ya Galilaya”
Hapo biblia inasema habari za Bwana YESU zikaenena “MARA KOTE KOTE KATIKA NCHI ZOTE”… Sasa swali??…Je zilienea sekunde ile ile, au muda ule ule, aliotoa Pepo?..Jibu ni la!...bali ni baada ya kipindi Fulani cha wakati labda masaa kadhaa mbele au siku moja mbele au siku kadhaa???… Kwani isingewezekana ndani ya sekunde ile ile muujiza ulipotokea, habari zifike Galilaya yote ambayo ilikuwa na vimiji vidogo vidogo Zaidi ya 400 kulingana na historia na miji hiyo ikiwemo Nazareti, Kapernaumu, korazini na Bethasaida, Na tena si Galilaya tu!, na hata nje ya Galilaya, maana hapo anasema taarifa zilifika miji yote ya kandokando ya Galilaya (maana yake nje ya Galilaya).
Kwa mantiki hiyo basi tutakuwa tumeelewa kuwa Mathayo alipotumia neno “kunyauka Mara” hakumaanisha sekunde ile ile, bali alimaanisha kuwa ni kwa kipindi Fulani cha masaa kadhaa, (haraka sana, ambako sio kwa kawaida kwa desturi ya miti kunyauka)… kwa maana kikawaida mpaka mti unyauke unachukua siku kadhaa, na huo ni kama umekatwa…sasa ule haukuonekana kama umekatwa, lakini ulinyauka kabisa (Hivyo ni muujiza).
Kwahiyo kwa hitimisho ni kuwa mtini mpaka kufikia asubuhi ndio ulionyesha kunyauka na wanafunzi walishagaa hiyo asuhubi hivyo biblia haijichanganyi mahali popote..
Je unaliamini Neno la Mungu?.. Na je umeokoka?…Kama bado ni nini kinachokusubirisha usimpokee Bwana YESU??.. Fahamu kuwa tunaishi katika siku za mwisho na YESU yu mlangoni.. hivyo usiyachezee maisha yako wala mtu mwingine yoyote asiyachezee..
MTINI, WENYE MAJANI.
KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?
MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.
ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.
BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA?
Swali: Je biblia takatifu inajichanganya katika habari ile ya binti wa Yairo?.. kwamaana katika Marko na Luka inaonyesha kuwa Binti alikuwa katika kufa! (Marko 5:23) Lakini katika Mathayo 9:18 inasema binti alikuwa amekwishakufa, sasa habari ipi ni sahihi kati ya hizo mbili?
Jibu: Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa biblia haijichanganyi mahali popote, isipokuwa pambanuzi zetu, na tafakari zetu ndizo zinazochanganyikiwa. Sasa ili tuelewe vizuri, turejee mistari hiyo..
Marko 5:21 “Hata Yesu alipokwisha kuvuka kurudia ng’ambo katika kile chombo, wakamkusanyikia mkutano mkuu; naye alikuwa kando ya bahari. 22 Akaja mtu mmoja katika wakuu wa sinagogi, jina lake Yairo; hata alipomwona, akaanguka miguuni pake, 23 akimsihi sana, akisema, BINTI YANGU MDOGO YU KATIKA KUFA; nakuomba uje, uweke mkono wako juu yake, apate kupona, na kuishi 24 Akaenda pamoja naye; mkutano mkuu wakamfuata, wakimsonga-songa.”…..
Marko 5:21 “Hata Yesu alipokwisha kuvuka kurudia ng’ambo katika kile chombo, wakamkusanyikia mkutano mkuu; naye alikuwa kando ya bahari.
22 Akaja mtu mmoja katika wakuu wa sinagogi, jina lake Yairo; hata alipomwona, akaanguka miguuni pake,
23 akimsihi sana, akisema, BINTI YANGU MDOGO YU KATIKA KUFA; nakuomba uje, uweke mkono wako juu yake, apate kupona, na kuishi
24 Akaenda pamoja naye; mkutano mkuu wakamfuata, wakimsonga-songa.”…..
Turuke mpaka mstari ule wa 35 na 36 ili tuimalizie habari hii kama ilivyoelezewa na Marko..
35 Hata alipokuwa katika kunena, WAKAJA WATU KUTOKA kwa yule mkuu wa sinagogi, WAKISEMA, BINTI YAKO AMEKWISHA KUFA; kwani kuzidi kumsumbua mwalimu? 36 Lakini Yesu, alipolisikia lile neno likinenwa, akamwambia mkuu wa sinagogi, Usiogope, amini tu”
35 Hata alipokuwa katika kunena, WAKAJA WATU KUTOKA kwa yule mkuu wa sinagogi, WAKISEMA, BINTI YAKO AMEKWISHA KUFA; kwani kuzidi kumsumbua mwalimu?
36 Lakini Yesu, alipolisikia lile neno likinenwa, akamwambia mkuu wa sinagogi, Usiogope, amini tu”
Katika kisa hiki ni kweli tunaona taarifa zinaanza na binti kuwa katika HALI YA KUFA, na zinaishia na BINTI KUFA.. Lakini tukirejea katika kitabu cha Mathayo tunaona habari nyingine ambayo inaonekana kama ni tofauti kidogo..
Turejee…
Mathayo 9:18 “Alipokuwa akiwaambia hayo, tazama, akaja jumbe mmoja, akamsujudia, akisema, BINTI YANGU SASA HIVI AMEKUFA; lakini njoo, uweke mkono wako juu yake, naye ataishi. 19 Akaondoka Yesu, akamfuata, pamoja na wanafunzi wake”……….
Mathayo 9:18 “Alipokuwa akiwaambia hayo, tazama, akaja jumbe mmoja, akamsujudia, akisema, BINTI YANGU SASA HIVI AMEKUFA; lakini njoo, uweke mkono wako juu yake, naye ataishi.
19 Akaondoka Yesu, akamfuata, pamoja na wanafunzi wake”……….
Hapa tunasoma kuwa Jumbe-Yairo anamwambia Bwana kuwa Binti yake amekwisha kufa, na si yu katika kufa!, hivyo aende kumwekea mikono afufuke.. sasa swali je! Biblia inajichanganya?
Jibu ni la!.. kama tulivyosema, biblia haijichanganyi, isipokuwa ni pambanuzi zetu.
Sasa ili tukiweke hiki kisa vizuri; ni kwamba Yairo alipotoka nyumbani mwake kumfuata Bwana YESU, binti yake alikuwa hajafa bado!, ila alikuwa katika hali ya kufa,..na alipokutana na Bwana akamwomba aende amwekee mikono ili apone, sawasawa na Marko alivyorekodi hapo katika Marko 5:23, tukio ambalo halijarekodiwa na Mathayo..
Lakini alipokuwa katika kumsihi Bwana kuna watu baadhi waliotokea nyumbani kwake na kumpa taarifa kuwa binti yake amekwisha kufa!…Sasa Yairo aliposikia kuwa mwanae kafariki hakukata tamaa, bali aliendelea kumsihi Bwana kuwa aende kumwekea mikono ili afufuke hata kama amekwisha kufa!, Na Bwana YESU aliposikia hayo akaahidi kwenda naye.
Lakini alipokuja mtu mwingine kutoka nyumbani mwake kumpa hizo hizo taarifa kuwa binti yake kashafariki hivyo asizidi kumsumbua mwalimu… (maana yake alikuwa anarudia rudia kumwambia, sasa hiyo kauli ya asizidi kumsumbua Marko 5:35) ndio iliyomfanya Bwana YESU amwambie ASIOGOPE!, kwani ndiyo inayokatisha tamaa, na yenye kuua Imani ya Jumbe (Marko 5:36).
Hivyo kwa hitimisho ni kuwa Mwandishi wa kitabu cha Marko alianzia kuelekezea tukio kuanzia mwanzo kabla ya binti kufa, na kutaja kuwa watu walikuwepo Zaidi ya mmoja waliokuja kumpa taarifa Yairo za kifo cha mwanae (Marko 5:35),
Lakini mwandishi wa kitabu cha Mathayo alianzia kuelezea tukio katikati wakati ambao tayari binti amekwishakufa na hakuelezea kabla ya kufa kwake…..Hivyo hakuna mkanganyiko wowote hapo, na wala mahali pengine popote katika biblia.
Je umeokoka?.. Je unafahamu kuwa tunaishi katika majira ya siku za mwisho?, na Kristo yupo mlangoni?. Kama bado hujampokea unangoja nini?.. Mpokee leo na ubatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la BWANA YESU KRISTO, upate ondoleo la dhambi zako nawe utapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)
USIFE NA DHAMBI ZAKO!
ALIFANYIKA SADAKA KWA AJILI YETU!
MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 2)
Je biblia inajichanganya kwa habari za Yohana kuwa Eliya?
(Masomo maalumu kwa wanawake).
Kama wewe ni mwanamke na unatamani kupata kibali cha ndoa, au kupata mtu sahihi wa atakayekupenda, basi kuwa kama Esta, ambaye alikuwa na tabia ya kutokupenda-penda vitu!… Wengi wanadhani ubikira ndicho kigezo cha juu ya kupata kibali… Nataka nikuambie sivyo!.. walijitokeza mabikra wengi mbele ya Mfalme Ahasuero, lakini ni mmoja tu aliyechaguliwa..
Sasa ni kigezo gani cha juu kilichompa Esta umalkia??….Turejee maandiko tutapata majibu..
Esta 2:15 “Hata ilipowadia zamu yake Esta, binti Abihaili, mjomba wake Mordekai, ambaye alimtwaa kuwa binti yake, ili aingie kwa mfalme, YEYE HAKUTAKA KITU, ila vile vilivyoagizwa na Hegai, msimamizi wake mfalme, mwenye kuwalinda wanawake. Naye huyu Esta alikuwa amepata kibali machoni pa wote waliomwona. 16 Basi Esta alipelekwa kwa mfalme Ahasuero, katika nyumba ya kifalme, mwezi wa kumi, ndio mwezi wa Tebethi, mwaka wa saba wa kumiliki kwake. 17 MFALME AKAMPENDA ESTA KULIKO WANAWAKE WOTE, NAYE AKAPATA NEEMA NA KIBALI MACHONI PAKE KULIKO MABIKIRA WOTE; BASI AKAMTIA TAJI YA KIFALME KICHWANI PAKE, AKAMFANYA AWE MALKIA BADALA YA VASHTI”.
Esta 2:15 “Hata ilipowadia zamu yake Esta, binti Abihaili, mjomba wake Mordekai, ambaye alimtwaa kuwa binti yake, ili aingie kwa mfalme, YEYE HAKUTAKA KITU, ila vile vilivyoagizwa na Hegai, msimamizi wake mfalme, mwenye kuwalinda wanawake. Naye huyu Esta alikuwa amepata kibali machoni pa wote waliomwona.
16 Basi Esta alipelekwa kwa mfalme Ahasuero, katika nyumba ya kifalme, mwezi wa kumi, ndio mwezi wa Tebethi, mwaka wa saba wa kumiliki kwake.
17 MFALME AKAMPENDA ESTA KULIKO WANAWAKE WOTE, NAYE AKAPATA NEEMA NA KIBALI MACHONI PAKE KULIKO MABIKIRA WOTE; BASI AKAMTIA TAJI YA KIFALME KICHWANI PAKE, AKAMFANYA AWE MALKIA BADALA YA VASHTI”.
Esta hakuwa na tabia ya kupenda-penda vitu (kwa ufupi hakuwa na tamaa) na wala hakuwa na mambo mengi!!.. aliingia kwa mfalme yeye kama yeye, katika uhalisia wake!.. wakati wengine walitaka waingie kwa mfalme na marashi yao, na mitindo yao, na wapambe wao, ili wakubalike, Esta yeye hakutaka hayo yote, aliona ni ulimbukeni, aliingia yeye kama yeye, isipokuwa vitu vichache ambaye yule msimamizi aliyeitwa Hegai alimshauri.
Hata leo ni hivyo hivyo, Biblia bado ni Neno la Mungu lililo hai, kupitia hilo tunajifunza kanuni nyingi.. kama wewe ni binti!, au mwanamke!.. ukitaka kibali na Neema.. basi KUWA WEWE!!!... Usianze kujibadili maungo yako, au sauti, au chochote kile katika mwili wako ambacho umeumbwa katika ualisi wake, vile vile usiwe mtu wa tamaa ya vitu (kila unachokiona unakitamani)..
Ukiwa mtu wa namna hiyo ni rahisi sana kupata kibali.
Mistari ya biblia kuhusu kibali.
USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.
APENDAYE FEDHA HASHIBI FEDHA.
Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).
ESTA: Mlango wa 4
Ulawiti na Ufiraji vina tofauti gani, kulingana na 1Wakorintho 6:9?
Jibu: Turejee…
1Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, WALA WAFIRAJI, wala WALAWITI”
“Ulawiti” ni kitendo cha mwanaume kumwingilia mwanaume mwingine kinyume na maumbile… Na “Ufiraji” ni kitendo cha Mwanaume kumwingilia mwanamke kinyume na maumbile.
Mambo haya yote mawili ni machukizo makuu mbele za Mungu, na “wafiraji na walawiti” hawataurithi uzima wa milele sawasawa na maandiko hayo.
Kama wewe ni mwanaume na una mke jiepushe na Ufiraji!.. na kama wewe ni mwanamke na una mume kataa ufiraji, kama mwenzako anataka kukuacha kwasababu hiyo ya wewe kuukataa ufiraji, hapo yupo huru kuondoka!.. na wewe upo huru kuoa au kuolewa na mwingine mwenye kufanana na wewe, (asiyefanya mambo hayo na aliyeokoka)!
1Wakorintho 7:15 “Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika Amani”.
Neno “Ulawiti” limeonekana mara moja tu katika biblia na ni tendo baya kuliko ufiraji (Maana humu ndio wamo mashoga, jamii za wale watu wa Sodoma na Gomora).. Kwa ujumla Mkristo hapaswi kulawiti/kulawitiwa… kufira/kufirwa. Wote wafanyayo hayo, wana roho nyingine ndani yao, na sehemu yao itakuwa katika lile ziwa la moto.
Maran atha!
Mshahara wa Mbwa ni upi? Kama tunavyousoma katika Kumbukumbu 23:18
Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”
MSIWE NA UCHUNGU NAO!
Hapo ndipo, atakapompa Mungu Baba ufalme wake.
Fahamu maana 1Wakorintho 14:20 “Ndugu zangu msiwe watoto katika akili zenu;
Swali: Kwanini biblia ikataze kujiongezea hekima, kwani kuna ubaya gani katika kuongeza hekima?
Jibu: Turejee..
Mhubiri 7:16 “Usiwe na haki kupita kiasi; Wala usijiongezee hekima mno; Kwani kujiangamiza mwenyewe?”.
Hekima inayozungumziwa hapo si hekima ya KiMungu, ambayo hiyo tumeagizwa tuitafute sana..
Yakobo 1:5 “Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa”.
Tena maandiko yanasema mtu aonaye hekima (hiyo ya kiMungu), biashara yake ni Zaidi ya fedha..
Mithali 3:13 “Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu. 14 Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha, Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi. 15 Yeye ana thamani kuliko marijani, Wala vyote uvitamanivyo havilingani naye”.
Mithali 3:13 “Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu.
14 Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha, Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi.
15 Yeye ana thamani kuliko marijani, Wala vyote uvitamanivyo havilingani naye”.
Kwahiyo hekima iliyozungumziwa hapo katika Mhubiri 7:16b ambayo mtu akiwa nayo nyingi inamharibu si hekima ya kiMungu, bali ni HEKIMA YA KIDUNIA.. Ambayo hiyo kwa Mungu ni upuuzi sawasawa na 1Wakorintho 3:18
1Wakorintho 3:18 “Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima. 19 Maana HEKIMA YA DUNIA HII NI UPUZI MBELE ZA MUNGU. Kwa maana imeandikwa, Yeye ndiye awanasaye wenye hekima katika hila yao.”
1Wakorintho 3:18 “Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima.
19 Maana HEKIMA YA DUNIA HII NI UPUZI MBELE ZA MUNGU. Kwa maana imeandikwa, Yeye ndiye awanasaye wenye hekima katika hila yao.”
Umeona?.. kumbe hekima ya dunia ni upuuzi mbele za Mungu na hiyo mtu akijiongezea sana itamwangamiza!!!.
Sasa mfano wa hekima ya kidunia ni ile inayosema “mwanadamu asili yake ni nyani”.. sasa hii ni elimu/hekima ya kidunia..ambayo imetukuka miongoni mwa wasomi wengi wakubwa, kiasi kwamba mtu aliyezama sana katika hiyo hekima, anajiangamiza mwenyewe, kwani atafikia hatua ya kusema hakuna MUNGU.
Ndio maana hapo biblia inasema “usijiongezee mno”… Maana yake usizame sana katika kuzitafuta, kwani zimejaa upotofu mwingi na ukweli kidogo…
Bwana atusaidie.
Kwa maarifa Zaidi kwanini biblia iseme “usiwe na haki kupita kiasi” fungua hapa >>>>>USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.
Kwanini Mungu alimkataa Sauli? (1Samweli 15:23)
KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?
NINI MAANA YA KUISHI KWA KUUKOMBOA WAKATI?.
Mithali 24:17 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?
HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?
Wengi, tumeshasikia kuwa Yesu atarudi, lakini mpaka mtu anasema atarudi, maana yake ni kuwa alishawahi kuja hapo nyuma. Na kama tunavyojua Bwana wetu Yesu Kristo alikuja mara moja tu, miaka karibu elfu mbili iliyopita, akaishi, akafa,akazikwa, akafufuka, akapaa mbinguni. Lakini wakati wote alipokuwa hapa duniani aliwaahidi wanafunzi wake kuwa atarudi tena.
Hivyo somo hili, ni muhimu kufahamu, namna ambazo Yesu alisema atarudi, ili usikose maarifa, kwasababu wengi hapa wanakosa shabaha katika kutambua kauli za Yesu. Naomba Soma kwa utulivu somo hili mpaka mwisho.
Sasa kuhusu kurudi kwake duniani, alizungumza katika nyakati tofuati tofauti kurudi kwa namna mbili.
Tuangalie kwa undani, namna hizi mbili. Husasani tutailenga hiyo ya pili.
Je! ni kwa namna gani, alirudi kama Roho,Aliwaambia hivi mitume wake;
Yohana 14:18 “Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu. 19 Bado kitambo kidogo na ulimwengu haunioni tena; bali ninyi mnaniona. Na kwa sababu mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai. 20 Siku ile ninyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu”.
Yohana 14:18 “Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu. 19 Bado kitambo kidogo na ulimwengu haunioni tena; bali ninyi mnaniona. Na kwa sababu mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai.
20 Siku ile ninyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu”.
Soma pia, katika Yohana 16:16, amerudia maneno hayo hayo,
Unaona? Mitume walidhani hawatamwona tena, lakini siku ile aliyopaa mbinguni,siku kumi baadaye, biblia inasema walikuwa wamekusanyika wote mahali pamoja, akawajilia Roho Mtakatifu akawakalia wote, wakajazwa Roho Mtakatifu. Na kama tunavyojua tangu huo wakati na kuendelea, kila mmoja alijua anaye Yesu moyoni mwake, hakuna mtu aliyeuliza Yesu yupo wapi.
Uyatima uliondoka kabisa, kabisa, ndipo wakatambua maana ya yale maneno. Hivyo tumeshaona kurudi kwake kwa kwanza duniani, kulikuja kwa namna hiyo ya Roho Mtakatifu, na mpaka sasa Kristo yupo ndani ya mioyo ya waliomwamini, na kupokea Roho Mtakatifu.
Lakini pia katika maneno yake mengine, alisema atarudi kama mwizi.
Soma,
Mathayo 24:43 Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa. 44 Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.
Mathayo 24:43 Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
44 Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.
Unaona tena?, Hajasema, atarudi kama askari, au mfanya biashara, bali kama mwizi. Sasa ni vema tujue sifa za mwizi, ni zipi kibiblia, ndipo tuelewe jinsi kurudi kwake kwa namna hiyo kutakavyokuwa.
Ukisoma Yohana 10:10 Yesu anasema hivi; “Mwivi haji ila AIBE na KUCHINJA na KUHARIBU; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele”.
Kumbe mwizi hasaa, anayezungumziwa ni mfano wa jambazi, na sio wale wadokozi, ni wale wanaobeba silaha, ili kuharibu na kuua wanaowaona, wachukue mali yao waondoke.
Na Yesu ndivyo atakavyokuja katika siku za mwisho hizi, atatimiza sifa hizo zote tatu.
1.) Jambo la kwanza Atakuja saa tusiyodhani, Kisha ATAIBA kitu chake cha thamani duniani. Ni hicho si kingine zaidi ya watakatifu wake. Hapo ndio suala la unyakuo linapoibukia.
Mathayo 24:40 Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa; 41 wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.
2) Lakini pamoja na hilo, kuja kwake kutaambatana na KUCHINJA.
Maana yake ni kwamba, kama unyakuo utakupita, dunia itakuwa inajiandaa kuingia katika siku ile ya mapigo ya ghadhabu ya Mungu, ambayo mwisho wake utaishia na Kristo kuonekana katika umbile la kibinadamu kabisa, kuwaua mataifa yote ambayo yatakusanyika kupigana naye katika ile vita kuu ya Harmagedoni.
Ufunuo 19:11 Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita. 12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe. 13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu. 14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi. 15 NA UPANGA MKALI hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi. 16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANAWA MABWANA.
Ufunuo 19:11 Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.
12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.
13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.
14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.
15 NA UPANGA MKALI hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.
16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANAWA MABWANA.
Huu ni wakati ambao Yesu, atauangamiza ulimwengu, mfano wa mwizi, asiyekuwa na huruma. Usitamani uwepo wakati huo ndugu, ni majuto vilio na kusaga meno.
3) Lakini mwisho kabisa, ATAHARIBU.
Tunafahamu kuwa mwizi, huvunja, mahali ili aingie, huvuruga kila kitu anachokiona, vivyo hivyo na hii dunia itafumuliwa yote, mifumo yote itaangushwa, itafinyangwa upya, yote hayo yatatokea katika siku hiyo hiyo ya Bwana, ambayo itaharibu kila kitu.
2Petro 3:10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. 11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa, 12 mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka?
Soma pia,(Ufunuo 16:17-21), kuongeza maarifa..
Hivyo ndugu, wakati huu wa Yesu kurudi kama mwizi umekaribia sana, ambao utaanza Kwanza kwa tukio la unyakuo. Bwana anatutaka sisi tukeshe(rohoni), asitukute tumelala. Ili Siku hiyo isitujilie ghafla, tukabaki hapa duniani.
1Wathesalonike 5:1 Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie. 2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku. 3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa. 4 Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi. 5 Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza. 6 Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi. 7 Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku. 8 Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.
1Wathesalonike 5:1 Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.
2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.
3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.
4 Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.
5 Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.
6 Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.
7 Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku. 8 Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.
Bwana atupe macho ya kuona haya.
Je! Umempokea Yesu maishani mwako, Je! Ameziondoa dhambi zako? Kama jibu ni la, unasubiri nini? Hujui kesho kama utakuwepo, hujui kama leo atarudi. Hivyo tubu sasa, mwamini Yeye upate ondoleo la dhambi zako, kisha utapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Ikiwa utapenda kupokea wokovu basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii bure. Bwana akubariki.
USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.
KAMA MWIZI USIKU WA MANANE.
Kuna tofauti gani kati ya “Mwivi” na “Mwizi”?
Fahamu Namna ya Kuomba.
SWALI: Naomba kuelewa tafsiri ya mithali 30:32-33, isemayo;
Mithali 30:32 Ikiwa umefanya kipumbavu kwa kujikuza; Au ikiwa umewaza mabaya; Basi weka mkono wako juu ya kinywa chako. 33 Kwa maana kupiga maziwa huleta siagi; Na kupiga pua hutokeza damu; kadhalika kuchochea hasira hutokeza ugomvi.
Mithali 30:32 Ikiwa umefanya kipumbavu kwa kujikuza; Au ikiwa umewaza mabaya; Basi weka mkono wako juu ya kinywa chako.
33 Kwa maana kupiga maziwa huleta siagi; Na kupiga pua hutokeza damu; kadhalika kuchochea hasira hutokeza ugomvi.
JIBU: Hekima inatueleza matokeo ya kila tendo linapofanyiwa kazi liwe ni zuri au baya litaleta majibu fulani tu. Hapa anatumia mfano wa siagi ambayo inatolewa katika maziwa. Kwa kawaida siagi huwa imejificha ndani ya maziwa, hivyo ili kuipata tu ile siagi, ni kitendo cha kuipiga basi hutokea kwa juu yote,
Sasa kupiga hapo sio kuyachapa maziwa hapana, bali kuyakoroga, ndani chombo Fulani maalumu kwa muda mrefu, baadaye maziwa na siagi hujitenga vyenyewe.
Halikadhalika, pia damu huwa ipo ndani ya pua, lakini haiwezi kutoka yenyewe tu bila kuisumbua pua kwa kuipiga. Kwamfano mtu akikupiga ngumi ya pua ni wazi kuwa damu itatoka tu.
Ndivyo anavyofananisha na ugomvi, kwamba ni jambo ambalo lipo tu, wakati wowote katikati yetu. Mfano tu wa siagi ndani ya maziwa na damu ndani ya pua. Lakini mpaka ugomvi huo ujitokeze, unahitaji kuchochewa, kukorogwa, korogwa, kupigwa pigwa.
Anasema hasira inapoanza, aidha kwa kuzungumza maneno mabaya, mwenzako akakereka, haraka sana, weka mkono wako kinywani, usiendelee kuzungumza, kwasababu kitakachofuata ukiendelea sana ni ugomvi, yaani mapigano, na kudhuriana.
Mauaji, visasi, chuki, asilimia kubwa vimetokana na hasira zilizochochewa.
Lakini, uwezo huu wa kujizuia, una nguvu endapo mtu yupo ndani ya Kristo. Je! Umemwamini? Kama bado na upo tayari kumpokea leo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu chini.
Bwana akubariki
UPEPO WA KUSI HULETA MVUA;
Kwanini iwe ni nchi ibubujikayo maziwa na asali?
Maziwa yasiyoghoshiwa ni nini? Kwanini biblia inatumia mfano huo?
SIKU YA HASIRA YA BWANA.
Waamuzi 16:28 “Samsoni akamwita Bwana, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili”.
Samsoni haombi kujilipiza kisasi kwaajili ya Nywele zake zilizokatwa, bali kwajili ya “MACHO YAKE MAWILI”.. Maana yake macho yake yalikuwa ni bora kuliko nguvu zake… Laiti angeambiwa achague nguvu ziondolewe na macho yabaki, ni Dhahiri kuwa angechagua macho yabaki.. Na huo ungeweza kuwa uchaguzi wa kila mtu.
Macho ni Zaidi ya mikono, ni Zaidi ya miguu, ni Zaidi ya nguvu za mwili.. Na ndicho shetani alikitafuta kwa SAMSONI.. Macho yake!!!!… lakini ni jinsi gani angeyatoa?? Inahitajika kuziondoa kwanza nguvu zake za mwili.. Shetani alikuwa haziogopi nguvu za Samsoni, alichokuwa anakiogopa ni macho yake…
Kwani baada ya kumtoa macho alizitumia nguvu zake kusaga ngano za wafilisti…
Na leo hii adui anatafuta macho ya watu kama shabaha yake ya kwanza.. na macho anayoyatafuta si ya kimwili, bali yale ya kiroho..na anaanza kwanza kwa kudhoofisha nguvu za kiroho za mtu na kisha anamaliza kwa kumpofusha Macho ya kiroho … (hapo anakuwa amemaliza kazi!).. na hapo anaanza kumtumikisha kama alivyomtumikisha Samsoni.
2Wakorintho 4:4 “ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.
Lakini habari njema ni kwamba ipo NEEMA kuu juu yetu Zaidi ya ile iliyokuwa juu ya Samsoni. Kwani Samsoni alipomwomba Mungu amrejezee Nguvu zake alirejeshewa kweli na kuwaaharibu maadui zake lakini bado aliendelea kuwa kipofu..
Lakini katika wakati huu wa agano jipya tunaponyenyekea kwa Baba na kuomba msaada, kwa kumaanisha kabisa mbele zake, basi zile nguvu zetu adui alizoziteka zinarejea tena upya na pia macho yetu yanatiwa nuru.. Hiyo ndio faida ya kuwa ndani ya KRISTO.
Je nguvu zako za Kuomba zimeisha???, nguvu zako za kufunga zimeisha??..Nguvu za kumtumikia Mungu zimeisha??…. Kama ndio jua hiyo pia ni dalili ya kupofushwa macho na Ibilisi… Hivyo huwezi kuona mbele wala kutafakari yaliyopita… unahitaji msaada wa Mungu, kwa nguvu zako huwezi!!!
Huu ni wakati wa wewe kunyenyekea kwa Mungu kama Samsoni ili Bwana azirejeshe nguvu zako upya na macho yako yatiwe nuru.
Omba kwa kumaanisha, na ikiwezekana funga! Ili Toba yako iwe na nguvu.. Na matokeo utayaona!
Waefeso 1:18 “macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo”
JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?
KITENDAWILI CHA SAMSONI
UMEFUNULIWA AKILI?
BUSTANI YA NEEMA.
Nini maana ya kumpenda Bwana kwa moyo,roho, akili na nguvu zetu zote?
Kiburi ni hali ya moyo wa mtu kuinuka kutokana na kitu fulani alichonacho, au alichokipata au atakachokipata ambacho kinamtofautisha au kitamtofautisha yeye na mwingine.
Hali hii inamfanya mtu anakuwa na majivuno, dharau na jeuri na asiyetii na hata kukosa staha.
Mtu huyu anakuwa ni mgumu kushaurika, na wakati wote yeye ndio anajiona yupo sahihi na wengine wote wana kasoro.
Vifuatavyo ni vitu vichache ambavyo vinatengeneza kiburi ndani ya mtu.
1.MALI
Hiki ni kitu cha kwanza ambacho kinatengeneza kiburi ndani ya mtu, na kiburi chenyewe ni “kiburi cha uzima” tunachokisoma katika 1Yohana 2:16.
Hapa mtu anakuwa anaamini anao uzima au maisha kupitia vile alivyonavyo.. Hivyo hahitaji kuambiwa kingine chochote ambacho kitampa yeye uzima, tayari yeye anakuwa anaamini mali alizonazo ndizo jawabu la mambo yote..hivyo hata ukimpelekea Neno la Mungu ambalo ndilo uzima hawezi kukusikiliza…
Na kiburi hiki pia kwa sehemu kipo kwa watu wasio na mali, wanaozisaka wakiamini kuwa watakapozipata zintawapa majibu yote…na hawa ndio wale ukiwapelekea Neno la Mungu wanadharau na kukejeli na kuulizia pesa.
Lakini Bwana YESU alisema kuwa uzima wa mtu haupo katika wingi wa vitu mtu alivyonavyo..(Luka 12:15).
2. ELIMU
Maarifa hususani ya kidunia ni mlango wa pili wa kuzalisha kiburi ndani ya mtu.
Hapa ni pale mtu kapata elimu ambayo ni ya juu kuliko wengi..moyo wake unanyanyuka na kuona wengine wote hawawezi kumzidi akili au uwezo wa kutafakari..
Hivyo anapoletewa Neno la Mungu basi anaanza kumpima yule aliyemletea na anapogundua kuwa ana elimu ndogo ya kidunia kuliko yake, basi hamsikilizi akiamini kuwa atakuwa na upambanuzi hafifu…pasipo kujua kuwa elimu ya mbinguni haipatikani katika shule za wanadamu..kwani hata Mitume wa Bwana Yesu hawakusoma isipokuwa Mathayo tu..lakini leo mafunuo yao tunayasoma na kutusaidia.
3. KIPAWA/KARAMA
Kipawa/kipaji/Karama mtu alichonacho ni mlango wa tatu wa kuzalisha kiburi ndani ya mtu.
Hapa ni pale mtu anapotambua kuwa anao uwezo pengine wa kuimba kuliko wengine, anauwezo wa kufundisha kuliko wengine, ana uwezo wa kutenda jambo fulani kuliko wengine, na badala atumie uwezo huo kujaza pale palipopunguka, kinyume chake anautumia uwezo huo kujisifia au kujionyesha yeye ni bora na hivyo hata kusikiliza wengine au kushawishwa na wengine inakuwa ni ngumu.
4. CHEO/NAFASI.
Cheo au nafasi ni mlango wa nne wa kiburi kuzalika ndani ya mtu..
Hapa ni pale mtu anapopata nafasi fulani katika kanisa, au jamii au kazi…na kuona wote walio chini yake hawawezi kumwongezea chochote.
5. MWONEKANO
Huu ni mlango wa tano ambao unatengeneza kiburi ndani ya mtu..
Hapa ni pale mtu inatokea kujiona anavutia kimwonekano kuliko wengine, na kuamini kuwa yeye ni mzuri/mrembo zaidi ya wote na hakuna wa kumzidi..
Na kiburi hiki kinazalika pale anapopokea maoni ya kusifiwa na mtu mmoja au wawili.. Mtu kama huyu anapotokea mtu mwingine na kutaka kuzungumza naye inakuwa ni ngumu kumsikiliza kwasababu alijiona kama atachafuliwa mwonekano wake.
Sasa yafuatayo ni madhara ya kiburi juu ya mtu kibiblia.
1.Kiburi kinaondoa Neema ya Mungu.
Petro 5:5 “Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema”.
Neema ya Mungu inapokuwa juu ya mtu inamwongezea kibali kwake Mungu na kwa wanadamu…
Mtu mwenye neema ya Mungu tele juu yake, inakuwa ni vyepesi kwake kushinda dhambi tofauti na yule ambaye amepungukiwa neema, vike vile inakuwa vyepesi kwake kufanya jambo likafanikiwa.
2. Kiburi kinamletea mtu Aibu.
Mithali 11:2 “Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu…”
Watu wengi wenye kiburi wanaishia kuabika, kutokana na majivuno yao na dharau zao hivyo mwisho wake huwa hawapati vile wanavyovitafuta na hivyo wanakuja kuaibika baadaye.
3. Kiburi kinaharibu Nyumba
Mzazi mmoja au wote wanapokuwa na kiburi wanaiharibu familia yao wenyewe…
Mithali 15:25 “BWANA ataing’oa nyumba ya mwenye kiburi..”
4. Kiburi kinamshusha mtu chini (kimaisha).
Wote wenye kiburi Mungu anawashusha chini..
Mithali 29:23 “Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa”.
5. Kiburi kitamshusha mtu kuzimu.
Wote wenye kiburi hawataurithi uzima wa milele.
Isaya 2:12 “Kwa maana kutakuwa siku ya BWANA wa majeshi juu ya watu wote wenye kiburi na majivuno, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini…….. 17 Na majivuno ya mwanadamu yatainamishwa, na kiburi cha watu kitashushwa; naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo”
Isaya 2:12 “Kwa maana kutakuwa siku ya BWANA wa majeshi juu ya watu wote wenye kiburi na majivuno, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini……..
17 Na majivuno ya mwanadamu yatainamishwa, na kiburi cha watu kitashushwa; naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo”
Tabia nyingine ya mtu wenye kiburi pia ni mashindano na ubishi
Mithali 21:24 “Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi; Hutenda mambo majivuno ya kiburi chake”.
Mithali 13:10 “Kiburi huleta mashindano tu…”
Jihadhari na kiburi..Na tunajihadhari nacho kwanza kwa kuokoka kisha kujazwa Roho Mtakatifu katika maisha yetu na kujitahidi kwa bidii kukaa mbali na mazingira yote yanayochochea kiburi.
Kiburi cha Uzima ni nini? (1Yohana 2:16)
MUNGU HUWAPINGA WENYE KIBURI.
Unyenyekevu ni nini?
Babeli ni nchi gani kwasasa?
DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI: