USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.

USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.

Usilale usingizi wakati wa kumngojea Bwana.


Luka 12: 35  “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka; 

36  nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara. 

37  Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia. 

38  Na akija zamu ya pili, au akija zamu ya tatu, na kuwakuta hivi, heri watumwa hao. 

39  Lakini fahamuni neno hili, Kwamba mwenye nyumba angalijua saa atakayokuja mwivi, angalikesha, wala asingaliacha nyumba yake kuvunjwa. 

40  Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu.”

Tusome mstari mwingine tena unaofanana na huo…

Marko 13:35 “Kesheni basi, kwa maana hamjui ajapo bwana wa nyumba, kwamba ni jioni, au kwamba ni usiku wa manane, au awikapo jimbi, au asubuhi; 

36  asije akawasili ghafula akawakuta mmelala. 

37  Na hilo niwaambialo ninyi, nawaambia wote, Kesheni”.

Hapa tunaona tukio la Mtu mmoja ambaye tajiri…ambaye ana nyumba yake yenye wafanyakazi wengi..na kila mfanyakazi ana majukumu yake kama tunavyojua…wapo wa wakutengeneza chakula, wakufanya usafi, wapo wa kulisha mifugo, wapo wakuhakikisha usalama, n.k Kila mmoja ana majukumu yake.

Lakini tunaona alitoka siku moja na kwenda arusini..akawaambia watumwa wake wakeshe!..hakuwaambia kwamba atarudi siku hiyo hiyo…lakini aliwaaambia tu atarudi siku yoyote…Hivyo akawaambia muda wowote wawe tayari..siku atakayokuja kama ni jioni, au asubuhi au usiku wa manane awakute wakiwa katika shughuli zao kama kawaida..waohusika na usalama basi wawe wa kwanza kumfungulia mlango atakapofika n.k

Akawasisitiza sana wawe macho muda wote kwasababu hawajui siku wala saa atakapokuja. Sasa endapo angekuja baada ya siku mbili mida ya saa 8 usiku akawakuta wamelala unadhani angejisikiaje?..Ni wazi kuwa angeudhika sana na kuwafukuza kazi wote..

Mfano huo huo unalinganishwa na kurudi kwake Bwana Yesu mara ya pili. Kumbuka mtu yoyote aliyeokoka kwa dhati ni mtumishi wa Yesu Kristo..Ni lazima kuna kitu Fulani ambacho amepewa na Kristo kwaajili ya kuundeleza ufalme…Na kitu hicho ni karama aliyopewa…Na karama hiyo Bwana Yesu anataka iendelee kufanya kazi muda wote mpaka siku atakayokuja.. Lakini akija na kukuta Karama aliyokupa imekufa haifanyi kazi…Na sio tu haifanyi kazi bali pia wewe mwenyewe umelala usingizi (yaani umechukuliwa na ulimwengu)..Basi kuna hatari ya kutupwa katika ziwa la moto.

Hivyo tukumbuke kila siku kwamba tupo kazini..na hivyo tuwe waaminifu na majukumu yetu tuliyokabidhiwa na Bwana.

usilale usingizi..Kwasababu Biblia inasema katika;

Waebrani 10:37  “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789 001 312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada nyinginezo;

BIRIKA LA SILOAMU.

TUUTAZAME PIA MWISHO WA UJENZI WETU.

VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA

MAUTI YA PILI NI NINI?

BONDE LA KUKATA MANENO.

LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?

USISIKILIZE DHIHAKA ZA SHETANI, ZITAKUKWAMISHA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments