Siku moja nilimsikia mtumishi mmoja redioni akifundisha na kusema asilimia 60 ya mafundisho ya YESU yaliegemea katika fedha, na hivyo YESU alikuja hapa duniani ili sisi tujue kanuni za kufanikiwa kiuchumi..na ndio maana mimi hapa ninahubiri pesa.. alizungumza maneno hayo huku watu waliokuwa naye katika meza ya mazungumzo wakimsapoti kwa furaha kabisa..
Ni kweli, mifano mingi Bwana Yesu aliyokuwa anawafundisha makutano na wanafunzi wake, ni mifano aliyoitoa katika Maisha yetu ya kawaida tunayoishi kila siku, na mingine alitumia mifano ya fedha na wafanyabiasha pia, kwa mfano utaona ule mfano wa mfanyabiashara aliyekuwa anatafuta Lulu nzuri, baadaye alipoipata akaenda kuuza vyote alivyo navyo ili ainunue, mfano wa wale watu waliopewa talanta 10 wakaambiwa wafanyie biashara wazalishe, wengine wakazalisha wengine hawakuzalisha n.k.. Lakini ukiangalia mifano hiyo ilikuwa haimuelekezi mtu akawe bilionea au milionea, bali Bwana YESU aliitumia ile mifano ili kuwafundisha watu juu ya ufalme wa mbinguni..Kwamba kila mtu anapaswa akakizalie matunda kile anachopewa katika roho n.k.
Lakini Bwana YESU hakuja kwa lengo la sisi kuzijua kanuni za kuwa utajiri hapa duniani, hilo halikuwa lengo lake la msingi tangu mwanzo, kinyume chake wakati fulani maelfu kwa maelfu ya watu walipokusanyika ili kumsikiliza mpaka wakawa wanakanyagana, ukisoma Luka 12 pale utaona katikati ya mahubiri alitokea mtu mmoja ili kumwomba amsaidie kumwambia ndugu yake ampe sehemu ya urithi aliochiwa na baba yake.. Lakini saa hiyo hiyo Bwana alimjibu maneno haya.. “ Mtu wewe, ni nani aliyeniweka mimi kuwa mwamuzi au mgawanyi juu yenu”?..
Unaona maneno hayo?, hakuishia hapo akaendelea na kusema..
“Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo”..
Kama wewe ni mtu wa kusoma maandiko kwa kuyatafakari vizuri, utaelewa hapo BWANA, alikuwa anamaanisha kuwa yeye amekuja ili kuwa mwamuzi wa uzima wa mtu, au mpatanishi wa dhambi za mtu, lakini yeye anataka kumfanya kuwa mwamuzi wa mali za ulimwengu huu..
Ndio sababu ya kuwambia maneno hayo “Mtu wewe, ni nani aliyeniweka mimi kuwa mwamuzi au mgawanyi juu yenu”..Yeye kawekwa kuwa mwamuzi wa dhambi, sio mwamuzi wa mali.
Sasa ukiendelea kusoma utaona anawapa mfano huu..
Luka 12:16 “Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana; 17 akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu. 18 Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu. 19 Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi. 20 Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani? 21 Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu”.
Luka 12:16 “Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana;
17 akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu.
18 Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu.
19 Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi.
20 Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?
21 Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu”.
Ndugu yangu, dunia ya sasa ya masumbufu imewafanya watu wengi wamkimbilie Mungu kwa lengo la kupata suluhisho la mali zao, na urithi wao, na biashara zao lakini hawataki kuambiwa habari za UZIMA wao, biblia inasema shina moja la mabaya ya kila namna ni kumpenda fedha (soma 1Timotheo 6:10), haimaanishi kuwa tusiwe na fedha au tusitafute fedha hapana, bali kuwa na tamaa ya fedha inatufanya tuangukie katika mambo mengi maovu, wengine wanawaua ndugu zao kikatili , kisa urithi tu, wengine wanakwenda kwa waganga, kisa urithi, wengine wanagombana mpaka kuwekeana visasi na vinyongo kisa mali tu, wengine wanatoa kafara za ndugu zao kisa mali, wengine wanawasaliti ndugu zao kisa mali na kuwatenga kisa fedha n.k..wengine wanaua watoto na watu wengine wasio na hatia kisa mali..
Hivyo kama wewe ni mkristo, pokea ushauri wa YESU anaotuambia jilindeni na choyo…usigombane na mtu kisa amekudhulumu, mtu akiichukua kanzu yako mwachie na joho pia, wala usimnyime mtu haki yake kwa tamaa ya mali..
Bwana akubariki sana.
Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba hizi
+225693036618/ + 225789001312
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
JE! UKRISTO UNAMPA MTU DHAMANA YA KUWA TAJIRI?
FIMBO YA HARUNI!
USIPIGE MATEKE MCHOKOO!
PEPETO LA MUNGU.
Rudi Nyumbani:
Print this post
Je unawajua Wasamaria walikuwa ni watu gani?…Wasamari ni watu wanaotokea mahali panapoitwa SAMARIA, ulikuwa ni mji uliokuwepo katikati ya Taifa la Israeli. Zamani za wafalme Israeli ilipogawanyika sehemu mbili, yaani kaskazini na kusini, Eneo la Samaria lilibaki sehemu ya Kaskazini mwa Israeli na Yerusalemu ilibaki sehemu ya Kusini… kukawa na mataifa mawili ndani ya Taifa moja, sehemu ya kaskazini ikabakia na jina lile lile Israeli, ambayo mji wake mkuu ulikuwa ndio huo Samaria na sehemu ya kusini ikaitwa Yuda ambayo mji wake mkuu ndio uliokuwa Yerusalemu…
Lakini Israeli ilipokuja kuchukuliwa tena utumwani, wale waliokuwa kaskazini walipelekwa Ashuru wakabaki watu wachache sana ambao waliwekwa ili kuyatunza mashamba, na wale waliokuwa upande wa kusini walipelekwa Babeli, lakini baada ya miaka 70 Mungu aliwarudisha tena baadhi yao katika nchi yao ya ahadi, lakini wale waliopelekwa Ashuru hawakurudi tena, walidumu huko huko kwenye mataifa mengine, lakini Yule mfalme wa Ashuru alitoa watu baadhi kutoka katika taifa lake, na kuwaleta Israeli ili wakae Samaria, Hivyo kwa jinsi siku zilivyokuwa zinazidi kwenda hawa Wasamaria wakawa ni watu waliochanganyika, nusu wapagani nusu wanaishika sheria ya MUSA.
Sasa Wasamaria wao hawakuamini katika kuabudu katika lile Hekalu la Mfalme Sulemani kama wale wayahudi waliokuwepo Yerusalemu wakati huo….Hivyo ikasababisha kuwepo na matengano na kutokuelewana kwa muda mrefu…Waliokuwa wanaishi Yerusalemu yaani Yuda, waliwaona wasamari ni kama watu wa mataifa na hawajui sana dini. Na walikuwa hawachangamani, wakati mwingine hata kuzungumza walikuwa hawazungumzi. Waliendelea kuwa hivyo hadi wakati wa kutokea kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Bwana Yesu alikuwa yeye ni kutoka Uzao wa Daudi…Hivyo alikuwa ni myahudi ambaye ni wa upande wa Yerusalemu, yaani Yuda, na si msamaria. Siku moja alikuwa anapita kwenda Yerusalemu kutoka Galilaya na katika njia yake ilikuwa ni lazima akatize Samaria ili afike, kulikuwa hakuna njia nyingine, lakini alipofika Samaria wenyeji wakagundua kuwa anakwenda Yerusalemu kwa watu ambao hawaelewani kiimani..hivyo kwa jambo hilo tu, wakakataa asikae kwao wakamfukuza! Kwasababu walikuwa hawapatani.
Luka 9:52 “akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali. 53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu. 54 Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]? 55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.] 56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine”.
Luka 9:52 “akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.
53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu.
54 Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?
55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]
56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine”.
Je! Ingekuwa ni wewe ungejisikiaje labda unakwenda mahali fulani unazuiliwa kwasababu tu ya Imani yako?..labda unakwenda nchi fulani tuseme ya kiislamu, na kitendo cha kufika tu pale wenyeji wanagundua kuwa wewe ni mfuasi wa Imani ya kikristo, na wakakuzuilia hata kulala kwenye hoteli zao na kukwambia uondoke?..ungejisikiaje? bila shaka ungehuzunika sana, na kama si mkristo uliyesimama vizuri ungeweza hata kulaani..Ndicho kilichotokea kwa hawa wanafunzi waliwalaani Wasamaria, wakaona ni heri hata waangamizwe, hawana maana, wala roho nzuri…
Lakini Bwana Yesu alikuwa na moyo mwingine…akawaambia hamjui ni roho ya namna gani mliyonayo, Mwana wa Adamu hakuja kuangamiza roho bali kuokoa! Haleluya!..Tafsiri yake ni kwamba “yeye bado anawapenda hata kama wao wanamchukia”
Na kama ni msomaji wa Biblia ulishawahi kukutana na hili Neno..
“Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye (Mithali 16:7)”.
Sasa Bwana Yesu bila shaka njia zake zilimpendeza sana Mungu, na kama ni hivyo basi ni lazima maadui zake wangekuja kupatanishwa naye tu!..Na maadui wake wa kwanza ni hawa Wasamaria, hebu tuone ni wapi walikuja kupatanishwa naye…
Baada ya Wasamaria kumkataa Bwana hata kukataa alale nchini mwao, tunaona kipindi kifupi tu baadaye baada ya wao kumkataa labda miezi miachache tu mbeleni au wiki chache tu mbele, alikuwa anarudi tena Galilaya, na ikambidi apite tena pale pale Samaria walipomkataa kwanza…na kuna tukio la Ajabu sana liliotokea pale ambalo liliubadilisha mji wote wa Samaria kumpenda Bwana.
Tunasoma katika:
Yohana 4:3 “ aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya. 4 Naye alikuwa hana budi kupita katikati ya Samaria. 5 Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe. 6 Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita. 7 Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe. 8 Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula. 9 Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.) 10 Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai. 11 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo maji yaliyo hai? 12 Je! Wewe u mkubwa kuliko baba yetu, Yakobo, aliyetupa kisima hiki, naye mwenyewe akanywa maji yake, na wanawe pia, na wanyama wake? 13 Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena; 14 walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele. 15 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka. 16 Yesu akamwambia, Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa. 17 Yule mwanamke akajibu, akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume; 18 kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli. 19 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii! 20 Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia. 21 Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu. 22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi. 23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu. 24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli. 25 Yule mwanamke akamwambia, Najua ya kuwa yuaja Masihi, (aitwaye Kristo); naye atakapokuja, yeye atatufunulia mambo yote. 26 Yesu akamwambia, Mimi ninayesema nawe, ndiye…………….. 28 Basi yule mwanamke akauacha mtungi wake, akaenda zake mjini, akawaambia watu, 29 Njoni, mtazame mtu aliyeniambia mambo yote niliyoyatenda. Je! Haimkini huyu kuwa ndiye Kristo? 30 Basi wakatoka mjini, wakamwendea………………39 Na katika mji ule Wasamaria wengi walimwamini kwa sababu ya neno la yule mwanamke, aliyeshuhudia kwamba, Aliniambia mambo yote niliyoyatenda. 40 Basi wale Wasamaria walipomwendea, walimsihi akae kwao; naye akakaa huko siku mbili. 41 Watu wengi zaidi wakaamini kwa sababu ya neno lake. 42 Wakamwambia yule mwanamke, Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu; maana sisi tumesikia wenyewe, tena twajua ya kuwa hakika huyu ndiye Mwokozi wa ulimwengu”
Yohana 4:3 “ aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya.
4 Naye alikuwa hana budi kupita katikati ya Samaria.
5 Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe.
6 Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.
7 Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.
8 Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula.
9 Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.)
10 Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai.
11 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo maji yaliyo hai?
12 Je! Wewe u mkubwa kuliko baba yetu, Yakobo, aliyetupa kisima hiki, naye mwenyewe akanywa maji yake, na wanawe pia, na wanyama wake?
13 Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;
14 walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
15 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.
16 Yesu akamwambia, Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa.
17 Yule mwanamke akajibu, akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume; 18 kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli.
19 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!
20 Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.
21 Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.
23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.
24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.
25 Yule mwanamke akamwambia, Najua ya kuwa yuaja Masihi, (aitwaye Kristo); naye atakapokuja, yeye atatufunulia mambo yote.
26 Yesu akamwambia, Mimi ninayesema nawe, ndiye……………..
28 Basi yule mwanamke akauacha mtungi wake, akaenda zake mjini, akawaambia watu,
29 Njoni, mtazame mtu aliyeniambia mambo yote niliyoyatenda. Je! Haimkini huyu kuwa ndiye Kristo?
30 Basi wakatoka mjini, wakamwendea………………39 Na katika mji ule Wasamaria wengi walimwamini kwa sababu ya neno la yule mwanamke, aliyeshuhudia kwamba, Aliniambia mambo yote niliyoyatenda.
40 Basi wale Wasamaria walipomwendea, walimsihi akae kwao; naye akakaa huko siku mbili.
41 Watu wengi zaidi wakaamini kwa sababu ya neno lake.
42 Wakamwambia yule mwanamke, Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu; maana sisi tumesikia wenyewe, tena twajua ya kuwa hakika huyu ndiye Mwokozi wa ulimwengu”
Watu waliomkataa akae kwao sasa wanamwomba kwa kumsihi sana akae kwao angalau siku mbili…Hili Neno likatimia: Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye (Mithali 16: 7)” Mji mzima Samaria ulimgeukia Bwana…Na utaona hata baadaye walitaka kuja kumfanya kuwa mfalme wao, lakini Bwana akakataa.
Hakuna mahali ambapo Bwana Yesu alipokelewa vizuri kama kwa wasamaria ambao hapo kabla walimkataa.
Bwana wetu Yesu Kristo ni mfano kamili wa sisi kujifunza?..Alikuwa na maadui lakini waligeuzwa wote kuwa Rafiki zake, Hata wale waliomsulubisha msalabani aliwaombea msamaha na kwa kupitia damu yake kwa yeye ulimwengu umepatanishwa na yeye…Ndio maana mpaka leo Rafiki wa kweli amebakia kuwa Yesu tu!
Lakini maandiko yanatuambia katika:
Wafilipi 2:5 “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu”
Je! Waislamu ni maadui zako?”
Jifunze kwa Bwana Yesu hapo juu, je! Majirani zako ni maadui zako kiasi cha kutaka hata moto ushuke uwateketeze? Kama ndivyo basi Bwana Yesu anakuambia “hamjui ni roho ya namna gani mliyonayo!..Jifunze kwa Bwana Yesu hapo juu Paulo anasema Iweni na nia iyo hiyo …Je! Wafanyakazi wenzako ni maadui zako kiasi kwamba hawataki hata kukuona upo karibu nao?..Jifunze kwa Bwana Yesu hapo juu…Na likumbuke hili neno : Njia za mtu zikimpendeza Bwana hata adui zake hupatanishwa naye!…Tafuta kupatanishwa na maadui zako na si kugombanishwa nao. Kwasababu hiyo ndio Nia ya Kristo kwetu.
Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu
Kwa Maombezi/Ushauri/Maswali/Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba hizi
+225693036618/+225789001312
JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..
UCHUNGU WA KUIBIWA.
ROHO MBAYA KUTOKA KWA BWANA.
Baragumu ni nini/ Nini maana ya Baragumu.
Baragumu kwa lugha rahisi tunaweza kusema ni “Tarumbeta” au “Parapanda” au Mbiu!..Matarumbeta au Mabaragumu yalikuwepo ya aina nyingi kulingana na Nyakati.
Nyakati za zamani mabaragumu yalikuwa yanatengenezwa kwa pembe za wanyama, Tofauti na nyakati zetu hizi Mabaragumu yanatengenezwa kwa shaba na wakati mwingine chuma.
Katika nyakati za zamani Mabaragumu yalitumika katika nyimbo, hata sasa yanatumika katika Nyimbo, Katika maandiko tunasoma Daudi alisema kwa uweza wa Roho..
Zaburi 150:3 “Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;”
Na Baragumu lilitumika pia kuashiria Mwanzo wa Jambo fulani au mwisho wa Jambo fulani..Kwamfano katika biblia Wana wa Israeli wana wa Israeli walipokwenda vitani, Baragumu ndio iliyokuwa inatambulisha mwanzo wa vita au mwisho wa vita.
Na katika kitabu cha Ufunuo pia Mlango wa 8, Tunaona malaika wakiwa na Baragumu saba, kutangaza mambo yatakayokwenda kutokea kipindi kifupi kijacho
Ufunuo 8:1 “Hata alipoifungua muhuri ya saba, kukawa kimya mbinguni kama muda wa nusu saa. 2 Nami nikawaona wale malaika saba wasimamao mbele za Mungu, nao wakapewa baragumu saba”.
Ufunuo 8:1 “Hata alipoifungua muhuri ya saba, kukawa kimya mbinguni kama muda wa nusu saa.
2 Nami nikawaona wale malaika saba wasimamao mbele za Mungu, nao wakapewa baragumu saba”.
Je! na kwetu sisi wakristo Baragumu ni nini?.
Kadhalika Pia sisi wakristo hivi karibuni Baragumu moja la Mwisho litapigwa kwetu, baragumu(tarumbeta) hilo ni parapanda ya mwisho ambayo watakatifu wote waliooshwa kwa damu ya Mwana kondoo watanyakuliwa juu na kwenda kuonana na Bwana juu mbinguni. Baragumu hilo halijatengenezwa kwa pembe za wanyama wala shaba! bali kwa malighafi ya kimbinguni. Sauti ya Baragumu hilo itapenya mpaka kwa wafu na wataisikia sauti yake na kutoka makaburini.
Siku hiyo itakuwa ni siku ya shangwe na furaha isiyo na kifani, lakini pia itakuwa ni huzuni kwa walioachwa. Ni wajibu wetu kujitahidi kuingia kwa kupitia mlango mwembamba..
Bwana akubariki.
Kwa Maombezi/Ushauri/Maswali/ Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba
+225693036618/ +225789001312
JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?
NI KWANINI MUNGU HAONEKANI?
KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?
BWANA ALIPOSEMA “SIKUJA KUTANGUA TORATI BALI KUITIMILIZA” ALIKUWA ANAMAANISHA NINI?
KATIKA 1YOHANA 5:6-9, (A) NI KWA NAMNA GANI YESU ALIKUJA KWA MAJI NA DAMU?
KATIKA MARKO 2:2-12, KWANINI BWANA YESU ALICHUKUA HATUA YA KUSAMEHE DHAMBI KWANZA KABLA YA KUMPONYA YULE KIWETE?
WhatsApp
JIBU: Katika ukristo kitendo chochote cha kutafuta msaada wa rohoni au mwilini kwa kupitia nguvu nyingine mbali na nguvu za Mungu, biblia inakiita Uchawi,…Na ni wazi kuwa hakuna nguvu nyingine iliyo kinyume na Mungu zaidi ya nguvu za shetani, Na uchawi kwa ujumla umebeba mambo mengi, kuloga, kuagua, kutazama utabiri wa nyota, kubashiri, kusihiri, kuabudu sanamu, hata kuamini baadhi ya movie au magemu ambayo yanatoa maagizo fulani kukuaminisha kuwa unaweza kupata maelekezo ya maisha yako mbali na nguvu za Mungu ni uchawi n.k. vipo vingi, kwa ujumla vyote hivyo vinaitwa uchawi.
Kumbukumbu 18:10 “Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri, 11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.’’
Kumbukumbu 18:10 “Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,
11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.’’
Hivyo katika biblia uchawi umekemewa sana, tangu kipindi cha wana wa Israeli kuingia nchi ya Kaanani Mungu aliwaonya sana, mtu yeyote miongoni mwao asionekane anafanya mojawapo ya mambo hayo, Ni jambo ambalo lilikuwa linamuudhi Mungu kiasi kwamba adhabu yake ilikuwa ni kifo tu (Walawi 20:27, Kutoka 22:18)
Vile vile Biblia katika agano jipya inatuaeleza pia mtu yeyote anayejihusisha na uchawi hawezi kuurithi ufalme wa mbinguni..
Ufunuo 22:14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake. 15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.
Ufunuo 22:14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.
15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.
Kama tulivyoona hapo juu kujihusisha na uchawi sio tu kupaa na ungo, lakini pia hata kwenda tu kwa mganga tayari wewe ni mchawi, hata tu kuamini kuwa ipo nguvu nyingine mbali na nguvu ya Mungu inayoweza kukuongoza, au kukutabiria mambo yako, au kukusaidia kuamua mambo fulani tayari ni uchawi, kuamini kama mti Fulani au ua Fulani au nguo Fulani au tarehe Fulani, au mwezi au jua vinaweza kukuletea bahati nzuri au mbaya, huo tayari ni uchawi ambao unaangukia katika lile kundi la kutazama nyakati mbaya (Kumb 18:10) sehemu yako siku ile itakuwa ni katika lile ziwa la moto. Wewe na Yule mchawi anayewanga usiku hamna tofauti.
Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.”
Hivyo kama wewe upo huko, au ulishawahi kujihusisha na mojawapo ya mambo kama hayo, unachopaswa kufanya ni kuamua kuacha kufanya hivyo tena, na kisha unatubu kwa kudhamiria kuacha kabisa hayo mambo kisha nenda kachome vitu hivyo, au katupe, halafu mfuate mchungaji wako au mtumishi yeyote mwaminifu wa Mungu akuombee, ili Roho wa Mungu aje juu yako, Kisha nawe utakuwa mmojawapo wa wana wa NURU. Lakini ukiendelea na mambo hayo, fahamu kuwa ukifa leo ni moja kwa moja kuzimu. Kwasababu ufalme wa giza ni kinyume na ufalme wa Nuru.
Ubarikiwe.
+25683036618/ +225789001312
JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.
FREEMASONS NI NINI? NA MTU ATATOKAJE HUKO?
JE NI KWELI MTU ANAWEZA KUCHUKULIWA MSUKULE?
VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.
NYOTA ZIPOTEAZO.
JINSI ITAKAVYOKUWA KATIKA SIKU ILE.
SWALI: Tukisoma Ufunuo 2:17 inasema “Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”..Ningependa kufahamu Sentensi hiyo ina maana gani? kwanini liwe sikio?.
JIBU: Kwasababu kuna uwezekano kabisa mtu akawa na masikio lakini asisikie!
Bwana Yesu alisema…katika Marko 8: 18
“Mna macho, hamwoni; mna masikio, hamsikii? Wala hamkumbuki?”..
Hao si viziwi Bwana aliokuwa anazungumza nao, wala sio vipofu! Bali ni mitume wake ndio aliokuwa anawaambia maneno hayo.
Kwahiyo kusikia kunakozungumziwa hapo ni kusikia kwa masikio ya ndani na si ya nje! (Yaani kuwa na uwezo wa kukichambua na kukielewa kile kitu kwa undani wake kama kinavyotakiwa kieleweke).
Hivyo na sisi tunaposoma Biblia tunapaswa tuisikie sauti nyuma ya kile tunachokisoma sio tusome tu kama habari..hapana bali kwa ufunuo…
Tunapaswa tuisikie SAUTI ya NENO lake, na sio Neno lake tu peke yake, wengi tunaisoma biblia lakini hatuisikii sauti nyuma ya kile tunachokisoma..Angalia hapa..
Zaburi 103:20 Mhimidini Bwana, enyi malaika zake, Ninyi mlio hodari, mtendao neno lake, Mkiisikiliza sauti ya neno lake.
Na ndio maana tunabakia kuona kama ni hadithi fulani tu Zilezile zinazojirudia kila siku.
Kwamfano Bwana aliposema kimwingiacho mtu hakimtii unajisi bali kimtokacho, hatupaswi tuanze kutafakari juu ya vyakula fulani tunavyokula kama nguruwe, kambale na nyama nyingine, au kuanza kutafakari juu ya vitu vitutokavyo mwilini kama vile majasho na mikojo n.k..badala yake tunapaswa tuelewe kwa sikio la ndani kuwa vitu vitutokavyo ndani kama vile, tamaa, matusi wivu, uasherati n.k ndio vitutiavyo unajisi, kwa maana vinatoka moyoni…Na mambo mengine yote tunapaswa tuyasikie hivyo hivyo kwa masikio la ndani.
Ndio maana sehemu nyingi utamwona Bwana akisisitiza neno hili mwenye masikio na asikie.
Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba
HATARI YA KUHUBIRI INJILI TOFAUTI NA ILIYOANDIKWA KWENYE BIBLIA.
ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!
UFUNUO: Mlango wa 18
MTU ANAPOKUFA ANAENDA WAPI?
Ikiwa imetokea umekufa ghafla, muda huo huo utawaona malaika wa Mungu wamesimama pembezoni mwako, ili kukuchukua na kukupeleka mahali panapokustahili, Sasa ikiwa wewe ni mtakatifu (Yaani ulipokuwa hapa duniani uliishi kwa KRISTO, na kujitenga na uovu) basi malaika hao wanakuchukua kwa furaha na kwa shangwe na kwa nyimbo na kukupeleka moja kwa moja sehemu inayotwa Peponi wengine wanaiita Paradiso (Luka 23:43)..
Bwana Yesu alitumia ule mfano wa Lazaro kueleza picha halisi ya kinachomtokea mtakatifu mara baada ya kufa..
Luka 16:22 “Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa”.
Kifuani mwa Ibrahimu ndio peponi kwenyewe kwa lugha nyingine, ni mahali pazuri sana, ni sehemu ya mbingu japo sio kule mbinguni kabisa Mungu alipo, ni sehemu ya kitambo tu ambapo watakatifu wanahifadhiwa wakisubiria siku ile ya Unyakuo ifike warudi makaburini kuichukua miili yao, na kwa pamoja sasa waungane na wale watatakatifu ambao watakuwa hai wakati huo, kisha wote kwa pamoja wapewe miili ya utukufu waende kumlaki Bwana Yesu mawinguni, baada ya hapo safari ya mbinguni moja kwa moja inaanza, kwenda kula karamu ya mwana-kondoo kwa Baba mahali ambapo hakuna hata mmoja wetu amefika kwasasa, huko ndipo tutakapomwona Mungu wetu uso kwa uso..tutaona vitu ambavyo hatujawahi kuona, wala kusikia.
Lakini kinyume chake ni nini kinatokea baada ya kifo kwa mwenye dhambi? ikiwa amekufa akiwa mlevi, mzinzi, muuaji, mtukanaji, yaani kwa ufupi yupo nje ya Kristo, basi wale malaika ambao Mungu aliwaandaa kwa kazi ya kuyatenga magugu na ngano (waovu na wema) wanafanya kazi yao hapo,..
Mathayo 13:49 Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki, 50 na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Mathayo 13:49 Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki,
50 na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Kumbuka biblia inaposema Mwisho wa dunia inamaanisha mwisho wa aina mbili, aina ya kwanza ni ule mtu anapokufa ndio unakuwa mwisho wake wa dunia, vilevile siku ile ya kiama ambapo dunia yote itahukumiwa nayo pia inaitwa mwisho wa dunia, vyote viwili malaika watafanya kazi hiyo..
Hivyo basi mtu kama ni mwovu, akifa bila kupoteza muda atachukuliwa na malaika hawa na kwenda kutupwa mahali panapoitwa JEHANAMU, huku Jehanamu ni mahali tofauti kabisa na ZIWA LA MOTO, Jehanamu ni kama mahabusu, watu waovu wanahifadhiwa kwa muda tu, wakisubiria hukumu ya mwisho, kisha ndio wakatupwe kwenye lile ziwa la moto siku ile ya mwisho, kama hujafahamu bado Jehanum ni mahali pa namna gani utanitumia ujumbe inbox nikutumie maelezo yake..
Sasa huko ni mahali pa mateso sana, sehemu mbaya, ndio kule Yule tajiri wa Lazaro alipopelekwa
Luka 16.22 “Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa. 23 Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake. 24 Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu. 25 Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa. 26 Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu. 27 Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu, 28 kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso. 29 Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao. 30 Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu 31 Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu”.
Luka 16.22 “Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.
23 Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.
24 Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.
25 Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.
26 Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.
27 Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu,
28 kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso.
29 Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.
30 Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu
31 Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu”.
Mtu huyu atakaa huko huko katika mateso hayo muda wote huo akisubiria ufufuo ambao utakuja mara baada ya ule utawala wa miaka 1000 kuisha, ndipo atakaposimama sasa mbele ya kiti cha hukumu cha mwana-kondoo kisha atahukumiwa kutokana na maovu yake yote, na kisha kutupwa katika lile ziwa la moto mahali ambapo pana mateso makali sana ya moto usiozimika…Na Baada ya hapo habari yake itakuwa imeisha.(Ufunuo 20:11-15)
Hivyo usidanganyike kuwa baada ya kifo kutakuwa na nafasi ya pili, hapana biblia imeweka wazi kabisa katika..Waebrania 9:27 “Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu”;
Ukishakufa leo, shughuli zote za hukumu zinaendelea juu yako, hakuna maisha tena hapo..
Swali linakuja je! Na wewe umejiwekaje tayari ikiwa siku hiyo imekukuta kwa ghafla?, Je! Unao uhakika wa kusikia sauti nzuri za malaika wakikuimbia nyimbo za ushindi wakikunyanyua na kukupeleka kule peponi walipo watakatifu wengine au kuwaona wakija katika hasira kali kukukokota ili kwenda kukutupa Jehanum?. Jibu lipo moyoni mwako,
Na mara nyingine malaika hawa huwa wanawatokea watu hata kabla hawajakata roho vizuri, japo si mara zote, Na ndio maana utaona muda mfupi kabla hawajafa, wengine wakiwa na amani sana, wengine wakitabasamu, wengine wakisema wanaona malaika karibu yao wakizungumza nao, n.k. ukiona hivyo ujue hawa hatma yao ni njema, lakini wapo wengine pia utaona kabla hawajafa muda mchache wanahangaika sana, au wanateseka, wengine wanakufa wakiwa na mwonekano kama vile wamenyongwa, au wameuawa n.k. Ujue kuwa malaika hao wanawachukua kwa hasira na kuwapeleka kule Jehanamu.
Je! Wewe utakuwa upande gani,?Jibu unalo badilika, tengeneza maisha yako kwa Bwana YESU sasa, ikiwa bado unasua sua, kwasababu hiyo kesho unayoisumbukia pengine inaweza isiwe yako. Na baada ya kufa ni hukumu
KARAMU YA MWANA-KONDOO.
KUNA UFUFUO WA AINA NGAPI?
KUNA HUKUMU ZA AINA NGAPI?
SIKU YA HUKUMU ITAKUWAJE?
UNYAKUO.
AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.
Shalom! Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima!
Karibu tujifunze Biblia, kwa Neema Bwana aliyotupa.
Biblia inasema katika Wagalatia 1:7b
“…. lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo. 8 Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe. 9 Kama tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo mliyoipokea, na alaaniwe”.
“…. lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo.
8 Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe.
9 Kama tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo mliyoipokea, na alaaniwe”.
Maneno hayo aliyazungumza Mtume Paulo kwa Uweza wa Roho, na Roho Mtakatifu mwenyewe akayatia Muhuri yafae kwaajili ya kutuonya na kututahadharisha sisi watu wa vizazi vyote. Ni maneno ambayo huwezi kuamini kama yapo kwenye Biblia Takatifu hususani katika agano jipya, lakini yapo!
Kuna hatari kubwa sana ya kuigeuza Injili ya Yesu Kristo kwa makusudi..ili tu mtu upendwe, au upate wafuasi wengi, au ujulikane…Kufundisha Injili nyingine tofauti na hiyo iliyohubiriwa na Mitume ndio “kuongeza Neno la Mungu” kunakozungumziwa katika biblia….ambapo Biblia imesema mtu wa namna hiyo ataongezewa mapigo katika siku ile.
Ufunuo 22: 18 “Namshuhudia kila mtu ayasikiaye maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mtu ye yote akiyaongeza, Mungu atamwongezea hayo mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki”.
Biblia inaposema wazi kuwa waasherati na waabudu sanamu pamoja na walevi watakwenda kwenye ziwa la moto, na wewe unasema “si kweli acha kuhukumu”..unaposema biblia imeruhusu pombe!! hapo ni sawa na unahubiri Injili nyingine tofauti na ile Iliyohubiriwa na hivyo “Umelaaniwa”
1Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, 10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”
1Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,
10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”
Biblia inaposema wazi katika Agano jipya kwamba Wanawake wavae mavazi ya kujisitiri, si kwa kusuka nywele!..
1Timotheo 2: 9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani; 10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu”.
1Timotheo 2: 9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu”.
Wewe unasema “Mungu haangalii mavazi anaangalia roho” sentensi ambayo haipo kwenye Biblia nzima…uliisikia kutoka kwa mtu fulani asiyefahamu maandiko nawe ukai-copy bila kuchunguza imetoka wapi!…..fahamu kuwa unahubiri Injili nyingine ambayo haipo kwenye Biblia…Na hakuna mtu yoyote anakuhukumu hapo..bali biblia yenyewe ndio inayokuhukumu kwamba UMELAANIWA!
Biblia inaposema katika Marko 16:16 “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”. Wewe unasema kuwa ubatizo haujalishi sana! Si lazima ubatizwe, Hapo unahubiri Injili ya Laana!
Pengine ulikuwa hujui kwamba hizo injili ni za laana! Na ulikuwa unazihubiri, Lakini leo umejua..Tubu mlipize shetani kwa uongo aliokudanganya kwa muda mrefu! Tubu nenda kachome vimini vyote ulivyokuwa unavaa,(na nguo zote zinazochora maungo yako) na kamwe usihubiri Injili hiyo uliyokuwa unaihubiri ya Laana kwamba Mungu haangalii mavazi…Ulikuwa unasuka nywele!, kafumue ziweke katika hali yake ya asilia Mungu alizokuumbia, ulikuwa unavaa mawigi, na kupaka lipstick pamoja na mapambopambo ya kidunia..jirudishe katika hali yako ya asili..Umesoma haya kwa macho yako! Hutasema siku ile hujaambiwa, wala hukusikia, au haujafafanuliwa vizuri!..
Ukikubali maonyo na kugeuka ni vizuri! Utakuwa umeisalimisha roho yako, lakini ukikataa pia ni vizuri, kwasababu Injili sio kitu cha kulazimishwa……isipokuwa hakikisha kama unajipamba jipambe kikweli kweli, Kama unavaa vimini tafuta vile vikali kabisa, kama unasuka, suka mitindo yote na ya kila namna…unapaka poda, uwanja, weka mwingi wa kutosha unavaa wigi tafuta za kila mtindo….usiwe nusu nusu, ili siku ile katika ziwa la moto usije ukajuta kwanini hukujipamba sana, utakapoona ulijipamba kidogo tu na bado umetupwa katika ziwa la moto!…usije ukajuta kwanini ulikuwa una nguo moja tu! Kimini ambacho ulikuwa unakivaa mara moja tu kwa mwezi katika tukio maalumu…na nguo nyingine ndefu za kujisitiri ulikuwa unazivaa kila siku na bado umetupwa kwenye ziwa la Moto!
Kama umechagua kwenda kuzimu usikubali kinguo kimoja tu kikupeleke kule! Tafuta madebe ya vimini na suruali zile zinazobana kabisa, pamoja na maboksi ya lipstick yatumie… kwasababu Bwana Yesu alisema mwenyewe katika Ufunuo.
Ufunuo 22:10 “ Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia. 11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa. 12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo. 13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho”.
Ufunuo 22:10 “ Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.
11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.
12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.
13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho”.
Maran atha.
Maran atha!
NGUVU YA UPOTEVU.
CHUKIZO LA UHARIBIFU.
LAANA YA YERIKO.
INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA.
INJILI YA MILELE.
JE! KUBET NI DHAMBI?
Kerubi au Makerubi ni Malaika wa Mungu,..Moja ya makundi ya malaika walioko mbinguni ambao kazi yao hasaa ni kuilinda enzi ya Mungu, na kumtukuza..Shetani naye alikuwa ni kerubi kabla hajaasi, lakini sasa sio kerubi tena,..
Ezekieli 28:14 “Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto. 15 Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako. 16 Kwa wingi wa uchuuzi wako watu walikujaza udhalimu ndani yako, nawe umetenda dhambi; kwa sababu hiyo nimekutoa kwa nguvu katika mlima wa Mungu, kama kitu kilicho najisi; nami nimekuangamiza, Ewe kerubi ufunikaye, utoke katika mawe hayo ya moto”.
Ezekieli 28:14 “Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto.
15 Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako.
16 Kwa wingi wa uchuuzi wako watu walikujaza udhalimu ndani yako, nawe umetenda dhambi; kwa sababu hiyo nimekutoa kwa nguvu katika mlima wa Mungu, kama kitu kilicho najisi; nami nimekuangamiza, Ewe kerubi ufunikaye, utoke katika mawe hayo ya moto”.
Makerubi utaona wakitajwa katika kitabu cha Mwanzo mara baada ya Adamu na Hawa kufukuzwa katika bustani ya Edeni wakawekwa ili kuilinda njia ya mti wa Uzima wasiifikie (Mwanzo 3:24), Utaona pia Musa alipoagizwa atengeneze sanduku la Agano ndani ya Hema ya kukutania alipewa masharti afanye makerubi wawili juu ya sanduku lile ili kukifunika kiti cha rehema..(Kutoka 25:17-22), vile vile hata katika hekalu maagizo hayo yalitolewa.
2Nyakati 3:10 “Na ndani ya nyumba ya patakatifu pa patakatifu akafanyiza makerubi mawili ya kuchonga; wakayafunikiza kwa dhahabu. 11 Na mabawa ya makerubi hayo urefu wake ulikuwa mikono ishirini; bawa moja mikono mitano, likiufikilia ukuta wa nyumba; na bawa la pili mikono mitano, likishikana na bawa la kerubi la pili. 12 Na bawa la kerubi la pili lilikuwa mikono mitano, likiufikilia ukuta wa nyumba; na bawa la pili mikono mitano, likishikana na bawa la kerubi la kwanza. 13 Yakaenea mabawa ya makerubi hayo mikono ishirini; yakasimama juu ya miguu yao, na nyuso zao ziliielekea nyumba”.
2Nyakati 3:10 “Na ndani ya nyumba ya patakatifu pa patakatifu akafanyiza makerubi mawili ya kuchonga; wakayafunikiza kwa dhahabu.
11 Na mabawa ya makerubi hayo urefu wake ulikuwa mikono ishirini; bawa moja mikono mitano, likiufikilia ukuta wa nyumba; na bawa la pili mikono mitano, likishikana na bawa la kerubi la pili.
12 Na bawa la kerubi la pili lilikuwa mikono mitano, likiufikilia ukuta wa nyumba; na bawa la pili mikono mitano, likishikana na bawa la kerubi la kwanza.
13 Yakaenea mabawa ya makerubi hayo mikono ishirini; yakasimama juu ya miguu yao, na nyuso zao ziliielekea nyumba”.
Tunawasoma pia katika kitabu cha Ezekieli makerubi ni malaika wenye sifa ya kuwa na mabawa manne, mawili walitumia kupaa, na mawili walitumia kufunika miili yao, na kila mmoja mwenye nyuso nne, (Ezekieli 10)..wanafananishwa na wale wenye uhai wanne tunaowasoma katika kitabu cha Ufunuo 4
Hivyo kwa ufupi makerubi na malaika wanaoonekana kuwa karibu sana na kiti cha enzi cha Mungu kuliko malaika wengine wote, wakimsifu na kuuhubiri ukuu wake usiku na mchana (Soma Ufunuo 4:6-9).
Nasi tunapokuwa katika hali ya kumsifu Mungu na kumwimbia kwa nguvu zetu zote, basi kundi hili la malaika linakuwa karibu sana na sisi, tufauti na tunaposali au kuhubiri.
HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.
KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.
MALAIKA WA MAJI NI YUPI? NA JE KUNA MALAIKA WA AINA NGAPI?
JE! MBINGUNI KUNA MALAIKA WA KIKE?. NA JE! TUKIFIKA MBINGUNI TUTAFANANA WOTE?
ANGUKO LA UFALME WA SHETANI:
KAZI YA UZURURAJI WA SHETANI.
Amani ya Bwana Ni nguzo ya Muhimu sana katika kumwongoza Mkristo.
Moja ya njia Mungu anazotumia kuzungumza na Mtu ni kwa kupitia amani…
Vivyo hivyo na Mungu wetu anazungumza na sisi mara nyingi kwa kupitia AMANI.
Akitaka kukuzuilia jambo fulani lililo nje ya mapenzi yake, utaona umekosa amani ghafla ya kufanya jambo hilo.
Hata katika maombi..moja ya uthibitisho kama maombi yako yamejibiwa ni AMANI UTAKAYOIPATA; Kama moyo wako umekuwa mzito, pengine una majonzi, huzuni, umekosa furaha na unatamani Mungu azungumze na wewe, ingia kwenye magoti omba mpaka uone amani fulani imeingia ndani yako..Ukiona kuna amani imekuja ndani yako ya kipeee Hapo jua Roho Mtakatifu katenda jambo.
Na amani hii inapokuja juu yako utaona inakufanya unazidi kumpenda Mungu zaidi, na utaona inakusukuma kutenda wema zaidi kuliko ubaya…utajikuta kama kuna mtu au kitu kilikuwa kimekuudhi ghafla unaona unahaja ya kusamehe, ghafla unasikia kama vifungo fulani vimeachia…ulikuwa unampango wa kulipiza unajikuta unasamehe, ulikuwa na hasira ghafla unajikuta furaha fulani imekuvaa..kadhalika uchangamfu fulani unakuingia..n.k hiyo ndiyo amani ya Kristo..Amani ya ulimwengu huu, matunda yake ni kutenda dhambi…ulikuwa na hasira na ulipofikiria kwenda kulipiza kisasi amani fulani ikakuingia kwenda kufanya hicho kitendo hiyo ni amani ya ulimwengu huu..
Bwana Yesu alisema katika kitabu cha Yohana..
Yohana 14:27 “Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga”.
Ni muhimu kuitafuta sana Amani ya Kristo.
Wafilipi 4:6 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. 7 Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.”
Wakolosai 3:14 “Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu. 15 Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani”.
Hii Amani ya Mungu chanzo chake ni KUOKOKA! na mtu unaokoka kwa kutubu kwanza na kudhamiria kuacha dhambi zako na kisha kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu.
Itafute Amani ya Mungu, ambayo ndio amani ya moyo inayolenga mapenzi ya Mungu. kwasababu inapatikana…kumbuka alisema mwenyewe kuwa “Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo.”
KUONGEZEKA KWA MAARIFA.
UMUHIMU WA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUZAA MATUNDA.
MAFUMBO YA MUNGU.
TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!
KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA
Waefeso 5.12 “kwa kuwa yanayotendeka kwao kwa siri, ni aibu hata kuyanena”.
Zamani ilikuwa ni rahisi kumtambua mtu mwenye dhambi kwa kumtazama tu au kumwangalia mienendo yake kwasababu karibu kila ouvu uliokuwa unafanyika chanzo chake kilikuwa ni cha nje kabisa kinachoonekana, kwa mfano zamani ilikuwa ili kuwapata watu wanaotembea tupu au makahaba ilikuwa ni lazima uende mahali kama kasino, au disco za usiku, au kwenye madanguro lakini sasa hivi mambo hayo yote unayapata mitandaoni na kwenye simu za mikononi bure, maovu yanayotendeka sasa hivi kwa siri ni mabaya zaidi kuliko hata yale ya kipindi kile,..mtu anaweza akatembelea madanguro hata 30 katika simu yake katika siku moja.
Unaweza ukajifanya mwema kwa nje, haunywi pombe, hauendi disco, hauzini na wanawake, au wanaume, tena umebatizwa, na unasema wewe ni mkristo, lakini ndani ya simu yako kwa siri ume download video za pornography unatazama na hakuna mtu anayejua, nataka nikuambie biblia inasema hilo nalo litafika hukumuni siku ile..
Mhubiri 12:14 “Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja NA KILA NENO LA SIRI, likiwa jema au likiwa baya
Wala usijidanganye, kusema mengine yote nimeyashinda ni hili tu ndio linalonisumbua siku ile Mungu atanihurumia, ndugu kuzimu utakwenda, biblia inasema
Yakobo 2:10 “Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote”.
Kila unapoingia mtandaoni kazi yako ni kutafuta picha na video za watu wa kidunia wanaozini, kila update ya video za ngono wewe unayo, Kumbuka Moja ya vitu sita ambavyo Mungu anavichukia ni pamoja na mtu aliye na miguu miyepesi kukimbilia maovu..(Mithali 6:18)
Wewe hujui ni kwa namna gani unamkasirisha Mungu, Badala uwe mwepesi kutafuta maneno yake mitandaoni wewe unatumia wepesi huo kwenda kutafuta miziki ya kidunia ambayo maudhui yake ni uasherati tu, na matusi, ni kibaya zaidi unajiita mkristo.
Hujui kuwa unatimiza maandiko ya wale wakristo baridi wanaozungumziwa kuwepo katika siku za mwisho, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu.(2Timotheo 3:4 )
Ni heri ukatupilia mbali hiyo simu kama inakukosesha kuliko kuwa mtumwa wa ibilisi na ukaenda kuzimu, biblia inasema kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate….wapo watu wengi kuzimu leo hii, wanatamani wakuhubirie wewe injili, uache kutazama hayo mambo machafu unayoyatazama huko mitandaoni, lakini hawawezi kutoka huko, laiti ungewaona, wanavyohangaika na ule moto kwa kosa moja kama unalolifanya wewe leo hii, usingetamani hata kutazama pornography, fahamu kuwa asilimia 99 kama sio 100, ya watu wote wanaoigiza mikanda hiyo ni mawakala wa kuzimu, tena wale wa hali ya juu sana, wanapokea maagizo hayo kutoka kwa ibilisi baba yao, na wanaelekezwa namna ya kufanya mambo hayo, sasa wewe usiyejua unavutiwa kwenda kutazama, hujui kuwa kuna roho mbaya zenye nguvu mara 7 zaidi ya zile zilizokuwepo Sodoma na Gomora, zimetegeshwa pale, unapotazama kidogo tu, moja kwa moja, zinakuvaa na ndio hapo tamaa zisizo za kawaida zinakuvaa, zinakufanya uwe kama mnyama aliyerukwa na akili asiyeona aibu kufanya jambo lolote lile, na hizo hazitoki leo wala kesho, ndio hao wengine wanaishia kuwa mashoga na wasagaji, wengine wanazini na wanyama, wengine na wazazi wao, wengine na watoto wao, wengine ndugu zao, wengine na majirani zao, wengine wanafanya mustarbation… sasa hizo zote ni roho za mauti, ambazo mwisho wake ni kuzimu na hizo roho huwezi kuzishinda kama utaendelea kuwa mbali na Kristo..
Lakini ukidhamiria kuacha Kabisa na kutubu dhambi zako, Kristo atakuvika uwezo wa kushinda hivyo vyote, Wengi hawawezi na wamekuwa watumwa wa hayo mambo ni kwasababu hawajadhamiria kwa miguu yao yote kumfuata Kristo, moyoni mwao anasema nikimfuata YESU inamaanisha sitakunywa pombe tena, sitatukana tena, sitakwenda disco tena, sasa watu wa namna hiyo hata kama leo hii wakitubu na kusema wamemkabidhi YESU maisha yao, na huku wanavitamani bado vitu hivyo, hawawezi kuvikwa huo uwezo utokao juu wa kuyashinda hayo yote, hata wafanye nini lakini ukidhamiria kwa dhati na kusema, kuanzia leo dunia bye! Bye!
Mimi kwa miguu yote naenda kwa Kristo bila kugeuka nyuma, kwasababu nataka niende mbinguni, nakuambia wewe mwenyewe utaona jinsi itakavyokuwa rahisi kuishinda dhambi, hata sisi tulikuwa huko, tukatolewa ile kiu ya pombe Yesu ataimaliza yote, ile kiu ya sigara itamalizwa yote, ile tamaa ya uzinzi Mungu ataiua, ile tamaa ya kufanya punyeto, itakufa yote, ile tamaa ya ushoga na usagaji itakufa yenyewe..Lakini sharti kwanza useme nimeamua kwa moyo wangu wote, na akili zangu zote, na nguvu zangu zote kuanzia leo kumfuata Kristo. Ukafuta video zote ulizozidownload, ukaacha kutembelea website zote ngono unazotembelea, ukafuta miziki yote ya kidunia, na ukakaa mbali na wazinzi wote, basi Mungu atakubadilisha haraka sana.
Kitu ambacho watu wengi hawajui ni kwamba.. “Mungu hawezi kutupa maagizo ambayo anajua sisi hatuwezi kuyafanya”…
Hawezi kutuambia tusizini na huku anajua hatuwezi kuishi bila kufanya uzinzi, kwahiyo anajua kabisa kuna namna mwanadamu anaweza kuishi bila kuzini kabisa! Ipo namna! Na ni rahisi sana…anajua hilo, hivyo ni jukumu letu kuivumbua hiyo, na Hiyo namna ipo kwa Yesu tu mwanawe mpendwa basi!! Ukivifuta hivyo vitu na kuviacha yeye si mwongo kutupa mzigo tusioweza kuubeba…utashangaa tu! Uwezo wa ajabu umekuja juu yako unaokufanya usitamani tena huo uchafu milele!
Kama ni hivyo, na unataka kumkabidhi Bwana YESU maisha yako tena, basi sali sala hii ya toba : hapo ulipo Piga magoti, kisha chukua muda mchache mweleze Mungu kuwa ulimkosea, kwa kuwa vuguvugu, na kutenda dhambi nyingi kwa siri, mwelezo bila kumficha chochote kwasababu mambo yote uliyokuwa unayafanya kwa siri yote anayajua, hivyo mweleze kuwa hutaki kufanya hivyo tena, na kwamba umedhamiria kuacha maisha ya kidunia na sasa unamfuata Kristo..
Ukishasema hivyo kwa kumaanisha kabisa..Ujue kuwa Bwana YESU amekusikia,..baada ya sala hiyo, ni kufuta sasa hivi bila kuangalia kushoto wala kulia kila picha, mziki, video chafu yoyote uliyonayo kwenye simu, flash, laptop au popote pale na Hatua inayofuata ni kutafuta kanisa la kiroho wanalobatiza ubatizo sahihi wa maji mengi kwa jina la YESU KRISTO nenda ukabatizwe kwa ajili ya kukamilisha wokovu wako, kulingana na Matendo 2:38, Kisha Mungu atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu bure atakayekuwa msaidizi wako, kukufundisha na kukuongoza kulielewa Neno na kuishi Maisha ya utakatifu…Vile vile usiache kwenda kanisani kuanzia leo ili Mungu ayakamilishe maisha yako mpaka siku ile ya wokovu.
Bwana akubariki sana. Ikiwa utapenda kuendelea kujifunza Neno la Mungu pamoja na sisi jinsi ya kukua kiroho, basi usiache kutembelea website yetu hii (www wingulamashahidi org).
Maran Atha!
KWANINI MAHUSIANO YA JINSIA MOJA NI DHAMBI?
DALILI NYINGINE INAYOUTAMBULISHA UZAO WA NYOKA.
EPUKA MUHURI WA SHETANI.
KUZIMU NI WAPI.
MLIMA WA BWANA.