Category Archive Home

Wale Watakatifu waliofufuka na Bwana Yesu WALIKUWA WAPI KABLA YA KUFUFUKA kwao je! walikuwa Peponi au ni wapi?.

JIBU: Wafu wote waliokufa kabla ya Kristo kuja duniani walikuwa makaburini, au sehemu za wafu, mahali pengine katika biblia panapaita Kuzimu, Daudi aliomba katika roho akisema “Maana hutakuachia kuzimu nafsi yangu, Wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu.” (Zaburi 16:10) Aliomba asiende sehemu za wafu iliyo njia ya wote, lakini tunasoma alikufa na akakusanywa na baba zake huko, Lakini kumbe Unabii huo ulikuwa haumuhusu yeye bali Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni yeye pekee nafsi yake haikubaki huko. 

Hivyo biblia haielezi kwa mapana walikuwa wanaishije ishije huko..lakini ni mahali ambapo hatuwezi kusema palikuwa ni salama sana, kwa maana shetani naye kwa sehemu Fulani alikuwa anao uwezo wa kuwasiliana na hata watu wenye haki waliokuwa wamekufa zamani, tunalithibitisha jambo hilo kwa Samweli, (1 Samweli 28)…Na hiyo ni kwasababu ya kuasi kwetu ndipo kulipompa shetani baadhi ya funguo za kututawala sisi hata mpaka baada ya kufa kwetu..japo alikuwa hana uwezo wa kuwaondoa mahali walipokuwepo…Lakini Kristo alipokuja na kushinda vyote pale msalabani, ndipo akachukua funguo zote za kuzimu na mauti na sasa wafu wote anawamiliki yeye.

Ufunuo 1: 17 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

Hivyo leo hii hakuna mtu au pepo lolote, au shetani anayeweza kuwasiliana na mtu wa aina yoyote yule aliyekufa ile awe mwenye dhambi au asiye na dhambi isipokuwa YESU peke yake..Ukiona mtu anakuambia mzimu wa baba yangu, au bibi yangu umenijia basi ujue kuwa hilo ni PEPO lililojigueza na kuvaa sura ya yule mtu,na wala si yule mtu halisi..Sasa kukaa kwake Bwana kaburini zile siku tatu, kulikuwa ni kushuka kuzimu huko wafu wote walipo ili kuwatenga wale wafu waovu na wema kwa injili aliyokwenda kuwahubiria.

1Petro 3:18 “Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa,

19 AMBAYO KWA HIYO ALIWAENDEA ROHO WALIOKAA KIFUNGONI, AKAWAHUBIRI;

20 watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji”. 

Sasa wale wema ambao waliishi maisha ya haki duniani na ya kumcha Mungu walihamishwa na kupelekwa mahali pa raha zaidi, ambapo panajulikana kama PEPONI/PARADISO (Kule alipomwambia yule mwizi aliyesulibiwa kuwa atakuwepo naye siku hiyo hiyo peponi)…Lakini wale waovu waliosalia walisogezwa mahali pa shida zaidi huko huko kuzimu…. Na katikati yao kukawekwa SHIMO kubwa ili wa kule wasiweze kuja huku na wa huku kwenda kule katika Roho,..Wale wema walipandishwa juu, lakini waovu walizidi kukaa chini na ndio maana yule tajiri katika habari ya Lazaro utamwona akinyanyua macho yake na kumwona Lazaro upande wa pili kule kuzimu.

 Luka 16:19 “Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa.

20 Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi,

21 naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake.

22 Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.

23 Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.

24 Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.

25 Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.

26 Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.

27 Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu,

28 kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso.

29 Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.

30 Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu.

31 Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu”.

 Sasa tukirudi kwenye swali wale wafu walikuwa wapi, ndio hapo siku ile Bwana aliyofufuka utawaona wafu watakatifu wakitoka makaburini, na kuhamishiwa Peponi,..Hivyo mtu akifa leo katika haki moja kwa moja anapanda peponi/paradiso akisubiria UFUFUO wa Haki siku ile ya unyakuo..lakini atakayekufa katika dhambi, naye moja kwa moja atateremka Jehanum, kwenye mateso makali akingojea naye kufufuliwa siku ile ya hukumu mbele ya kiti kile cheupe cha Enzi cha Mwanakondoo ahukumiwe kisha atupwe kwenye lile ziwa la moto

 Hivyo huu ni wakati wa kuweka mambo yetu sawa, yasije yakatukuta kama yale ya yule tajiri, biblia inasema itatufaidia nini tuupate ulimwengu mzima na mwisho wa siku tupate hasara ya nafsi zetu.?. Kiburi cha mwanadamu ni maua leo kipo kesho kinanyauka, ikiwa leo utajikuta haupo tena duniani..Huko uendako utakuwa mgeni wa nani? Huko hakuna nafasi ya pili.

Wokovu unapatikana bure sasa, ukikupita leo kesho utautafuta kwa kilio na kusaga meno na hautauona.. Ni maombi ikiwa maisha yako yapo mbali na Kristo basi leo fanya uamuzi wa kumkabidhi yeye maisha yako na yeye ana upendo na ni mpole na ameahidi kukupokea, na kuwapokea wote wanaomkimbilia yeye.

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

DHAMBI ISIYO NA MSAMAHA.

UPONYAJI WA YESU.

HERI, WALE MUNGU ASIOWAHESABIA MAKOSA YAO.

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

MNGOJEE BWANA

VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA

TUSIPOUTHAMINI WOKOVU TUTAPATAJE KUPONA?


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wapunga Pepo wanaozungumziwa kwenye biblia ni watu wa namna gani?

SWALI: Tukisoma Matendo 19:13 Inasema pale “Baadhi ya Wayahudi wenye kutanga-tanga, NAO NI WAPUNGA PEPO….” swali,Naomba kufahamu hawa Wapunga Pepo ni watu wa aina gani ndugu zangu?

JIBU: Tafsiri ya Neno kupunga pepo ni kufukuza pepo…hiyo ni lugha iliyotumika katika tafsiri yetu ya Kiswahili inayosimama badala ya kufukuza pepo…Kwahiyo zamani na hata sasa zilikuwepo njia nyingi za kuondoa pepo ndani ya mtu…

Watu wa Mungu wanao uwezo wa kufukuza mapepo kwa kutumia jina la YESU, kadhalika na watu wa shetani wanauwezo wa kufukuza pepo.
Sasa njia wanayotumia watu wa Mungu kufukuza mapepo ni tofauti na njia wanazozitumia wachawi au waganga…

Wakristo wanafukuza pepo na kumfanya yule mtu kuwa huru kabisa kabisa, kwa kutumia jina la Yesu Kristo kwa Imani, mtu huyo anafunguka na kuwa huru..kama mtu alikuwa na pepo fulani lililomletea ugonjwa Fulani labda ugonjwa wa kuumwa tumbo, linapoondolewa kwa jina la Yesu linaondoka moja kwa moja pamoja na ule ugonjwa wake na madhara yake yote.

Lakini waganga wa kienyeji au wachawi wanavyofukuza mapepo ni tofauti kabisa kwao haiwi hivyo..wao hawayafukuzi bali wanaleta mapepo mengine juu ya yule mtu yenye nguvu zaidi ya lile pepo lililopo ndani ya yule mtu, kwahiyo kinachotokea labda yule mtu alikuwa na pepo fulani lililomletea ugonjwa fulani labda wa kuumwa tumbo, Yule mtu anapokwenda kwa mganga (mpunga pepo)… yule mganga anamtumia pepo lingine lenye nguvu kuliko lile la ugonjwa wa tumbo linamwingia labda tuseme pepo la utasa na lile pepo la ugonjwa wa kuuma tumbo nguvu zake zinafunikwa na lile lingine la utasa lililomwingia.

Kwahiyo yule mtu baada ya kuaguliwa na yule mganga anaweza akajisikia unafuu wa kupona tumbo kwa muda…lakini baada ya kipindi fulani anakuja kujigundua tena kapata utasa au ugonjwa mwingine mkubwa zaidi…sasa hiyo hali ya kupunguza pepo hili nguvu kwa kulileta lingine lenye nguvu zaidi ya lile la kwanza ndiyo inayoitwa “kupunga pepo”.

Ni sawa kuleta nyoka ndani ili ale panya wanaokula mahindi yako ghalani, atawapunguza tu na kufurahi kwa muda lakini hawezi kuwamaliza wote, na zaidi ya yote huyo nyoka siku moja atakuletea madhara na wewe…

Kwahiyo waganga hawana uwezo wa kutoa mapepo, wanaongeza pepo juu ya pepo, kwasababu shetani hawezi kujifitini kwenye ufalme wake mwenyewe kama Bwana Yesu alivyosema…

Mathayo 12:26 “Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika juu ya nafsi yake; basi ufalme wake utasimamaje?”.

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

SEHEMU ISIYO NA MAJI.

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

JE! MBINGUNI KUNA MALAIKA WA KIKE?

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

NI UTHIBITISHO UPI UNAOONYESHA KUWA KUNA MBINGUNI NA KUZIMU?

UTEKA ULIOGEUZWA.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya Kipaimara?..Na je! Ni jambo la kimaandiko?

Nini maana ya Kipaimara?..je watu wanaweza kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono na kwa kupitia mafunzo fulani ya kipaimara?

JIBU: Kipaimara ni Neno lenye maana ya “uthibitisho”…Neno hili linatumika katika madhehebu baadhi kama vile Katoliki, Orthodoksi na Anglikana kama kanuni muhimu ya ukristo..Kwamfano Kanisa Katoliki lina kanuni saba za kufuata wanazoziita Sakramenti. Kwahiyo kipaimara Ni moja wapo ya hizo kanuni saba (sakramenti 7), ni kanuni ya Imani ambapo mtu anapaswa aipitie ili awe AMETHIBIKA MBELE ZA MUNGU. Na kanuni hiyo si nyingine zaidi ya KUWEKEWA MIKONO NA MAASKOFU WA KANISA… Madhehebu yanayotumia kanuni hii yanasimamia mistari kutoka katika kitabu cha.. 

Matendo 8: 14 “Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu, wakawapelekea Petro na Yohana;

15 ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu;

16 kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu.

17 NDIPO WAKAWEKA MIKONO YAO JUU YAO, NAO WAKAMPOKEA ROHO MTAKATIFU.”

Kwahiyo kinachotokea ni kwamba baada ya mtoto kubatizwa, atapaswa apitia mafunzo fulani yanayohusiana na kipaimara, na akishahitimu, ndipo atakusanyika kanisani na kuwekewa mikono na Askofu, na ndipo Roho Mtakatifu atashuka juu yake kama alivyoshuka juu ya hao wasamaria waliokuwa wamebatizwa tu lakini bado walikuwa hawajashukiwa na Roho Mtakatifu. Kwahiyo kwa lugha rahisi au nyepesi ni kwamba hao Wasamaria walipokea kipaimara kwanza kwa mikono ya akina Petro na Yohana, ndipo Roho Mtakatifu akashuka juu yao..ikiwa na maana kuwa kama wasingewekewa mikono na Mitume na Bwana Yesu Kristo kamwe wasingepokea kile kipawa cha Roho Mtakatifu. 

Kwahiyo Kanisa katoliki na mengine wakaichukulia hiyo kama ni kanuni ya MUHIMU SANA ya kufuata kwa kila mkristo, kwamba ili mtu athibitike kuwa mkristo kweli kweli na ili aweze kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu ni lazima abatizwe kwanza na kisha awekewe mikono na maaskofu wa kanisa, Na akishapitia hizo hatua kikamilifu ndipo anaweza kukubalika kama ni mshirika halali wa kanisa, na zaidi ya yote ni Mkristo..Kabla ya hapo anakuwa hajulikani kama ni mkristo.Sasa kwa namna ya kibinadamu, hiyo inaweza ikaonekana ni sawa, inaweza ikaonekana ni utaratibu mzuri, au ni kanuni ya kufuata siku zote,..Lakini je! Ni sahihi kulingana na maandiko?.

 Kwanza kabisa kabla ya kuelezea kipaimara, tuuzungumzie ubatizo kwa ufupi: ni muhimu kufahamu kuwa watoto wachanga hawabatizwi kulingana na Neno “Imani” lenyewe lilivyo, Ili iwe imani, ni lazima kwanza mtu aamini kitu fulani, sasa watoto wachanga hata kujielewa tu hawajajielewa, sasa wataaminije?..watamwamini vipi Yesu Kristo kuwa ni Bwana na mwokozi wa maisha yao, na kwamba amekufa kwa ajili yao, na kwamba wanapaswa watubu kwa ajili ya ondoleo la dhambi zao, wakati hata fahamu za kujitambua wao wenyewe hazipo ndani yao?Kwasababu biblia inasema..


Warumi 10: 13 “kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka.

14 Basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? TENA WAMWAMINIJE YEYE WASIYEMSIKIA? Tena wamsikieje PASIPO MHUBIRI?

15 Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema”

 Kwahiyo Ubatizo wa vichanga sio sahihi kulingana na uhalisia wa mambo yote, haihitaji ufahamu mwingi sana kuelewa jambo hilo. Kumbatiza mtoto mchanga ni sawa na kwenda mtaani na kumchukua mtu asiyemjua Mungu kabisa pasipo kumhubiria, wala kumfundisha chochote na kwenda kumzamisha kwenye maji na kumwambia tayari umebatizwa!…Hiyo ni kazi bure. Na pili, kuhusu kipaimara, Mitume hawakutoa kanuni Fulani kwamba mtu akitaka kupokea Kipawa cha Roho Mtakatifu ni lazima awekewe mikono na viongozi wao kwanza?..Hapana hawakutoa hiyo formula hata kidogo..Petro Na Yohana waliwawekea mikono wale wasamaria kwa wakati ule tu kwasababu ndio njia waliyoongozwa na Roho waitumie kwa wakati ule tu! Mahali pengine watu walishukiwa na Roho pasipo kuwekewa mikono na mtu yoyote.

Kama tu siku ya Pentekoste watu walishukiwa na Roho pasipo kuwekewa mikono na mtu yoyote. Na pia tunaona huyo huyo Petro alipokwenda nyumbani kwa Kornelio kumhubiria injili yeye na nyumba yake, Roho aliwashukia wale watu wote pasipo hata Mtume Petro kuwawekea mikono.. 

Matendo 10: 43 “Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.

44 Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno.

45 Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Unaona hapo? Wakati Petro akiwa anazungumza tu! Roho aliwashukia juu yao, Na sehemu nyingine Petro alipowahubiria watu zaidi ya elfu 3, na walipoamini..aliwaambia namna ya kupokea Roho Mtakatifu pasipo kuwekewa mikono akawaambia..”

Matendo 2:36 “Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.

37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”. 

Unaona na hapo? Petro Hakuwaambia watu tubuni mkabatizwe na kisha njooni tuwawekee mikono ndipo mpokee kipawa cha Roho Mtakatifu badala yake maneno hayo yanaonyesha kuwa mtu anaweza kupokea Roho Mtakatifu pasipo hata kuwekewa mikono na mitume. Kwahiyo kuwekewa mikono sio kanuni ya kupokea Roho Mtakatifu, kanuni ya kupokea Roho ni kutubu na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu.Mwingine anaweza akapokea Roho kwa kuwekewa mikono, mwingine anaweza apokee pasipo kuwekewa mikono…Na kwa jinsi Roho atakavyochagua njia ya kushuka juu ya huyo mtu, baada tu ya mtu kutubu na kubatizwa. 

Ni sawa na wakina Petro mahali pengine walikuwa wanatumia hata leso zao kuponya wagonjwa, na sehemu nyingine wanataja tu jina la Yesu pasipo kutumia chochote na watu wanafunguliwa..

kwahiyo ni njia tu ambayo Roho aliyokuwa anawaongoza kwa wakati husikia ndiyo waliyokuwa wanaitumia..lakini huwezi kuona Petro anatoa kanuni maalumu kuwa sehemu zote watu ili wafunguliwa lazima watumie leso, huwezi kuona jambo hilo.. Tofauti na ilivyo siku hizi za mwisho..Mafuta, chumvi, udongo ndio KANUNI ya kupokea uponyaji, kila tatizo linatatuliwa na maji ya maombezi, kila tatizo linatatuliwa na mafuta ya maombezi na chumvi…Inakuwa ni kanuni, jina la Yesu halitumiki tena…Ni roho hiyo hiyo iliyopo pia katika mifumo ya kipaimara na ubarikio. Kwahiyo kipaimara ni mfumo wa kimapokea ambao hausimami katika uhalisia wa kibiblia, ambao malengo yake ni kuwafanya watu waamini kuwa kuwekewa mikono na askofu, tayari wamekamilika na ndio tiketi ya kuthibitika mbele za Mungu..ni mfumo ambao unawafanya watu waridhike na kanuni za dini kuliko kanuni za biblia.

 Utamwuliza mtu unauhakika wa kwenda mbinguni, atakwambia ndio nimebatizwa na nimepokea kipaimara…lakini mwulize nini maana ya Roho Mtakatifu na matunda yake ni yapi?..atakwambia sijui?, muulize nini maana ya unyakuo atakuambia sijawahi kusikia hata hicho kitu, muulize umeokoka atakwambia dini yangu haifundishi hivyo, mwambie kuwa Tunaishi siku za mwisho atakuambia sijui?..lakini atajisifia kipaimara chake kwa sherehe kubwa aliyoifanya siku hiyo. Utakuta mtu analijua dhehebu lake kuliko anavyoijua biblia. Kwahiyo kanuni za kipaimara sio kanuni zilizokatibiwa na Mungu bali wanadamu, Mungu hajatoa kanuni maalumu kuwa mtu lazima apitie kipaimara au apakwe mafuta ya maombezi, au atumie chumvi ndipo afunguliwe au akubaliwe na yeye..yote hiyo ni mipango ya ibilisi kuwafanya watu wasitafakari maandiko kwa kina bali wapate njia za mkato za kutatua matatizo yao. Na kujiridhisha katika hizo kama ndio sababu ya kukubaliwa na Mungu, kumbe sio.

Ubarikiwe.

Mada Nyinginezo:

NI HALALI KUBATIZA WATOTO WADOGO?

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

SHETANI ANATOLEA WAPI FEDHA, ANGALI TUNAJUA FEDHA NA DHAHABU NI MALI YA BWANA?

UNAFANYA NINI HAPO?

MSTARI HUU UNA MAANA GANI? “YUKO MWENYE HAKI APOTEAYE KATIKA HAKI YAKE”?

WAPUNGA PEPO WANAOZUNGUMZIWA KWENYE BIBLIA NI WATU WA NAMNA GANI?

JE TATIZO LA KULA KUCHA NI ISHARA YA KUWA NA MAPEPO?


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! mtu kuhisi kitu fulani au kusikia sauti za watu wengine walio mbali, kunaweza tokana na Mungu?

Baba mmoja Ananisimulia akisema, “Mimi hapa huwa ninasikia watu wanaosema wanakuja kunikamata.akaniuliza je! Na wewe unawasikia? Nikamwambia hapana mimi siwaskii[saa hiyo ni yeye tu anawasikia]. Akanichukua akanishika mkono Akaniambia” Unasikia hiyo nyimbo yangu wanaimba? (Mimi siisikii yeye peke yake anasikia)” Nikamwambia hapana” ANAOGOPA SANA.

Sasa Juzi juzi Usiku nikamkuta amesimama hapa nje nyumbani kwetu Akiwa ameshika panga mkononi mwake akaniambia “Unamsikia bibi mmoja kule ng’ambo anasema nimebaka mjukuu wake[Kwa bibi huyo ni mbali na hapa kwetu]?” Nikamwambia hapana.Akarudi nyumbani na panga lake.[Wakati huo anaongea yuko siriazi kabisa].Wakati mwingine ananiambia aliowaona watu wamesimama mlangoni kwake. Sasa Swali:Ndugu kwa nyinyi Muonavyo Hicho ni kitu gani?? KARIBUNI [Nilijaribu kumueleza habari ya kumpa Bwana maisha akasema ATAPAMBANA KIJESHI[Nilijuwa anamaanisha kwa waganga],Lakini namuona sasa hawezi kupambana kijeshi alivyosema].Hali yake inazidi kuongezeka Ikifika mahali Si ajabu akawa kichaa kabisa.

JIBU: Shalom, Mambo yanayoendelea katika roho ni mengi, na shetani naye kila kukicha anaongeza mapana ya maarifa yake…mtu akizama katika maarifa ya shetani (mfano uchawi)..anakuwa anauwezo wa kufanya vitu ambavyo kwa namna ya kawaida haviwezekani kufanyika…sasa kwa mtu kama huyo aliyekuja kukusimulia kuwa anasikia sauti za nyimbo, na ana uwezo wa kusikia mtu akizungumza akiwa mbali, ni wazi kuwa kuna roho ipo ndani yake na hiyo ni roho ya yule adui. Kwanini ni roho ya adui, na si ya Mungu? kwasababu matunda ya hiyo roho ni ya yule adui, kumpeleka kwenye uovu na kumweka katika vifungo vya uoga,wasiwasi na mkandamizo… Kwasababu matunda ya Roho Mtakatifu sio hayo ingekuwa ni Roho Mtakatifu yupo ndani ya huyo mtu ungeona matunda ya Roho ndani yake kama yalivyoandikwa kwenye kitabu cha Wagalatia

Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.”

 Umeona hapo? Roho Mtakatifu akiwa ndani ya mtu hivyo vitu hapo juu lazima vionekane, amani, furaha,upendo n.k…Lakini roho iliyopo ndani ya huyo mtu haijamsukuma kwenye upole, wala haimpeleki kwenye furaha, wala uvumilivu, wala amani…zaidi ya yote umempeleka kwenye hofu, mashaka na ghadhabu…hivyo hiyo ni moja kwa moja roho ya yule mwovu ipo ndani yake. Sasa Roho Mtakatifu akiwa ndani ya mtu huwa ni lazima atoe na kipawa fulani juu ya huyo mtu, ndio hapo anawapa wengine vipawa vya unabii, wengine lugha, wengine miujiza,ishara,uchungaji, ualimu,uinjilisti n.k [kumbuka vipawa vya Roho ni tofauti na matunda ya Roho].

 kadhalika na roho za mashetani ni hivyo hivyo, mtu akiwa na pepo fulani la utambuzi, ni lazima litampa uwezo fulani,(ni kama karama yake fulani hivi) watu wengine shetani anawapa uwezo wa kufanya utambuzi, wanakuwa na uwezo wa kutambua siri za watu, au kuona vitu vinavyoendelea sehemu nyingine mbali na mahali walipo, hata wakati mwingine wanakuwa na uwezo wa kusikia sauti na mazungumzo ya watu waliopo mbali kama huyo mzee, wengine wanakuwa na uwezo wa kufanya viishara ishara fulani (mazingaumbe mazingambwe) wengine wanakuwa hawana huo uwezo lakini wanakuwa wanauwezo mwingine mkubwa wa ushawishi…wanaweza kumshawishi mtu au jamii na wakafanikiwa kuleta vitu vyenye madhara kwa kutumia hivyo vipawa walivyonavyo vya nguvu za giza.

 Kwahiyo kwa habari ya huyo mzee ni kwamba kafungwa na nguvu za giza, aidha kwa kujua au kwa kutokujua, na kwasababu hamjui Yesu Kristo, inawezekana yeye akajihisi anakipawa kutoka kwa Mungu cha uwezo wa kujua na kuwasikia maadui zake mahali walipo, lakini ni roho ya adui ipo ndani yake, pasipo yeye kujijua,hivyo nakushauri, tenga muda umhubirie injili, ili macho yake ya rohoni yafumbuke,umweleze uwezo uliopo katika Yesu Kristo, na tumaini lililopo ndani ya Yesu Kristo, na Bwana akimpa Neema ya kuamini injili na kuipokea, mwekee mikono na kumwombea kwa Jina la Yesu na hizo roho zitamwacha atakuwa huru kabisa.

Na akizingatia kutubu kwa kuacha dhambi zake kabisa na kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi, basi Bwana atampa kipawa cha Roho wake Mtakatifu kwasababu yeye mwenyewe alisema ahadi hiyo ni kwa watu wote waliompokea..Na akiisha pokea Roho Mtakatifu basi yale matunda ya Roho yataambata naye..atapata amani isiyokuwa ya kawaida, furaha ya ajabu, upendo wa ajabu, uvumilivu usioelezeka, upendo usiokuwa na mipaka na fadhili nyingi. 

Bwana akubariki.


Mada nyinginezo:

JE! UMECHAGULIWA KABLA YA KUWEKWA MISINGI YA ULIMWENGU?

NI JAMBO GANI LINALOMTAMANISHA SANA BWANA TUMWOMBE BILA KUKATA TAMAA?

VITA DHIDI YA MAADUI

“WOKOVU WETU U KARIBU NASI KULIKO TULIPOANZA KUAMINI”

NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?

NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA!


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ni kosa gani Daudi alilolifanya katika kuwahesabu watu, mpaka kupelekea vifo vya waisraeli wengi?

Mfalme Daudi aliwahesabu wana wa Yakobo apate kujua idadi yao kamili, 1Mambo ya nyakati 21:7, jambo lililoonekana chukizo kwa bwana, mpaka kusababisha watu elfu sabini waangamie kwa tauni. SWALI. ni uovu gani hapo Daudi aliufanya ulete madhara hayo yote? au torati ilisemaje kuhusu watu kuhesabiwa?


JIBU: Hakukuwa na uovu wowote mkubwa kivile katika kuhesabu watu, japo Daudi alifahamu hakupaswa kufanya vile kwa wakati ule lakini yeye aliendelea kufanya ndio maana baadaye alikuja kujutia makosa yake, na kumwomba Mungu msamaha!. Lakini sasa swali linabaki pale pale ni kwanini kwa kosa lake mwenyewe lisababishe zaidi ya watu ya elfu 70 kuangamia kwa tauni? Mpaka kufikia hatua Daudi mwenyewe kumlalamikia Mungu, na kumwambia kwanini unawaadhibu watu wengine wasio na hatia kwa kosa langu mwenywewe? Kwanini Mungu afanye vile? Kwanini awaadhibu na watu wasio na hatia kwa kosa la mwingine?… Daudi hakufahamu sababu ya Mungu kufanya vile. Sasa ukisoma vizuri biblia, hiyo habari katika kitabu cha Samweli utaona jambo fulani pale la kuzingatia …

2 Samweli 24: 1 “TENA HASIRA YA BWANA IKAWAKA JUU YA ISRAELI, AKAMTIA DAUDI NIA JUU YAO, akisema, Nenda, ukawahesabu Israeli na Yuda. 

2 Basi mfalme akamwambia Yoabu, jemadari wa jeshi la askari, waliokuwa pamoja naye, Zunguka sasa katikati ya kabila zote za Israeli, tangu Dani mpaka Beer-sheba, mkawahesabu watu, nipate kujua jumla ya hao watu”.

Unaona hapo ukisoma mstari wa kwanza utaona, kuna jambo wana wa Israeli walilifanya hapo kabla mpaka kupelekea hasira ya Mungu kuwaka juu yao..Kama ukisoma huko nyuma utagundua kuwa Mungu alikuwa hapendezwi na njia zao tangu siku nyingi, na ndio maana wakati mwingine alikuwa anawatia katika mikono ya wafilisti, na hapa pia vivyo hivyo, kuna mambo maovu walikuwa wanayafanya pengine kwa siri au hadharani (japo biblia haijaeleza hapo ni mambo gani) lakini ni dhahiri kuwa matendo yao yalimudhi Mungu sana, mambo kama kuabudu miungu migeni, rushwa, kudhulumu watu, mauaji yasioyo na hatia, kuhalifu sabato, kupitisha wana wao motoni, kuwaonea wajane na mayatima ni miongoni mwa vitu walivyokuwa wanavifanya wana wa Israeli kwa wakati ule..Hivyo Mungu akaamua kumtumia Daudi nia kama sababu ya kuwaadhibu makosa yao…

Na ndio hapo tunakuja kuona Daudi anaingiliwa na shetani kufanya vile, kama tu vile Mungu alivyotaka kumwangamiza mfalme Ahabu akaruhusu Pepo la uongo likawavae wale manabii wake 400, kadhalika na Daudi naye aliingiwa na shetani kufanya mambo ambayo Mungu hakumwagiza , na baadaye tunaona tauni inakuja kuachiliwa juu ya Israeli ili Mungu kujilipizia kisasi juu yao wote waliomuudhi.. Hivyo wakati mwingine hata sisi kama taifa au mtu binafsi, tunaweza kufanya makosa, na Mungu akakusudia kutuadhibu kwa kupitia viongozi wetu, na ndio hapo unaweza kushangaa viongozi wanaonyesha tabia za ajabu kwetu au kwako, anakuwa mkatili au dikteta,sisi tukidhani kuwa yule kiongozi ndio kakengeuka, lakini kumbe nyuma yake ni Mungu kasimama kumruhusu kwa makusudi kabisa mtu yule atumiwe na ibilisi ili au kutufundishwe sisi adabu.

Mfano unaweza kuona Mfalme Nebkadneza alikuwa ni diktekta, aliteka mataifa yote ulimwenguni kwa nguvu na akayatawala kwa mabavu..na hata Taifa la Mungu Israeli liliwekwa chini wa utawala wa Nebkadneza lakini ukiisoma biblia kwa makini utaona kuwa Mungu ndiye aliyemtia Nebkadneza nia ya kwenda kuteka mataifa yote ulimwenguni pasipo hata yeye Nebukadneza kufahamu chochote…Na Mungu alifanya vile ili kujilipizia kisasi kwa mataifa yote yaliyomwacha ikiwemo na Taifa la Israeli watu wake. Hivyo tunapaswa tuwe makini na njia zetu tumwombe Mungu kila siku..Ili wengine wasifanyike kuwa fimbo ya Mungu kutuadhibu sisi.

Ubarikiwe.


Mada nyinginezo:

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU:

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

KAMA MWIZI USIKU WA MANANE:

JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?

JE! NI HALALI KUTOA CHETI KWA WAKRISTO WANAOOA?

JE! MBINGUNI KUTAKUWA NA KULA NA KUNYWA?.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Biblia inakataza kuapa kabisa, lakini kwanini watu wanaapa mahakamani na katika vifungo vya ndoa?

JIBU: Ni vizuri kuelewa aina ya viapo mbalimbali vinavyozungumziwa katika biblia, ili usichanganyikiwe unapokutana na baadhi ya vifungu vinavyoonyesha wengine wakiapa lakini Biblia haiwahesabii kosa lolote kwa mfano pale mtume Paulo aliposema.

2Wakorintho 1: 23 “Lakini mimi NAMWITA MUNGU AWE SHAHIDI JUU YA ROHO YANGU, ya kwamba, kwa kuwahurumia sijafika Korintho”.

Warumi 1:9 “Kwa maana Mungu, nimwabuduye kwaroho yangu katika Injili ya Mwana wake, NI SHAHIDI wangu jinsi niwatajavyo pasipo kukoma”,

Hivyo kwa maelezo mafupi Vipo viapo vya aina mbili..aina ya kwanza ni viapo vya uaminifu, mfano wa hivi ni maagano au nadhiri.. Kwamfano Nadhiri ni kiapo, kinachomfunga mtu kwa Mungu wake kwamba unakuta mtu anamwambia Mungu ukinitendea hivi nitakutendea hivi, au sitafanya kitu fulani kwa wakati fulani mpaka nimalize kutimiza kusudi fulani..Hivi vyote mbele za Mungu ni viapo, na mtu anafungwa katika hivyo mpaka avitimize, asipovitoa kwake mtu huyo inakuwa ni dhambi.  

Hali kadhalika na pale wenzi wawili wanapofunga ndoa mbele za Mungu sawasawa na maagizo yake, moja kwa moja wanaingia katika viapo kwamba hakuna chochote kitakachowatenganisha mpaka kifo kitakapowakuta..Sasa iwe wamekiri hadharani au hawajakiri hadharani, wakishaingia kwenye ndoa tu, tayari maandiko yameshawafunga.   Hali kadhalika na mahakamani au katika mikataba ya kidunia: Ili mtu kujiridhisha na wewe uaminifu wako, huwa unaapishwa, kwamba unalolisema ni kweli, na kwamba utafanya sawasawa na mkataba au makubaliano mliyoingia..

Sasa viapo kama hivyo vyote haviji kwa lengo la kujihesabia haki, au kujiona wewe uko sawa mbele za mtu, au kujifanya wewe ni mkamilifu hapana bali ni vya kuthibitishwa tu.   Lakini sasa vipo viapo ambavyo vinakuja nje ya utaratibu wa Mungu, kwa mfano mtu pale anaposema HAKI YA MUNGU vile!!, au naapa juu ya kaburi la babu yangu, au naapa kwa kichwa changu, au naapa juu ya kiti cha enzi cha Mungu, n.k…

Unaona Vyote hivi ni viapo vinavyokuja kwa shinikizo fulani, au vinavyotokana na kiburi fulani, na mara nyingi viapo vya namna hii vinatoka katika kinywa cha mtu kwa makosa ya kushutumiwa, na si vinginevyo, hivyo watu wa namna hii mara nyingi hata bila kufikira anatoa maneno makuu kama hayo yaliyovuka mipaka, maneno ambayo hawezi hata kuyasimamia, kwamfano anaposema ninaapa kwa kichwa changu, utadhani kama yeye anajua hata hicho kichwa kiliundwaje undwaje, au mwingine anasema ninapa mbele ya kiti cha enzi cha Mungu utadhani yeye na Mungu ni mtu na mdogo wake, na hivyo ana uwezo sawa au unaokaribiana na Mungu n.k.  

Viapo vya namna hii ndivyo Mungu kavikataa kwasababu vinatoka moja kwa moja kwa yule mwovu, Mungu hapendi watu wanaojikweza na wenye viburi..Hivyo mtu akijikuta katika hali kama hiyo ya kushutumiwa hapo maneno yake ndio yanapaswa yawe Ndio ndio, au Siyo siyo.. Basi,   Lakini ikiwa ni kama vitu kama nadhiri, au maagano,au mapatano ya ndoa, au mikataba, au mahakamani..Hayo hayaji kutokana na kushutumiwa au kiburi bali yanakuja kwa lengo la kujiridhisha, kukiri uaminifu wako tu, na si zaidi ya hapo, na hiyo huwa mtu hafikii hatua ya kujikweza au kujihesabia haki, au kujihalalishia mamlaka ya kutendewa alichosema kama imethibitika kuwa hajasimamia alichosema.

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

NADHIRI.

KWANINI AWE NI PUNDA NA MWANA-PUNDA?

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA JIKANE MWENYEWE?

KUNA HUKUMU ZA AINA NGAPI?

JE! ADAMU ALIWASALIANA NA MUNGU KWA LUGHA IPI PALE BUSTANINI?

LULU YA THAMANI.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Tamaa yako itakuwa kwa mumeo.Ni tamaa ipi ya Hawa?

SWALI: Ndugu zangu baada ya yule mwanamke Hawa kuvuka mpaka wa maagazo ya Bwana na kula lile tunda alilokatazwa asile:Baada ya Pale tunaona Bwana akimuadhibu kwa adhabu tofauti-tofauti mojawapo ni kuzidishiwa uchungu wa kuzaa. Nataka kufahamu hii adhabu nyingine hapa anaambiwa [TAMAA YAKO ITAKUWA KWA MUMEO.Mwanzo3:16]-Ni tamaa Ipi hiyo Bwana Mungu aliyozungumzia hapo ndugu zangu?


JIBU: Kumbuka jambo la kwanza shetani alilolidadisi kwa mwanamke kwa muda mrefu na kuliona ndani yake ni TAMAA. Tamaa ya kuwa fulani, tamaa ya kuwa juu, tamaa ya kuwa juu ya vitu vyote, tamaa ya kutawala, tamaa ya kudiriki hata kutaka kuwa kama Mungu mwenyewe aliyemuumba..Na ndio maana nyoka alipokuja kumdanganya mwanamke hakumwambia maneno mengine yeyote labda utakuwa mzuri, au utapendwa zaidi au vinginevyo lakini badala yake alimwambia pindi utakapokula tunda utafumbuliwa macho na KUWA KAMA MUNGU!..

 Unaona? “Kuwa kama Mungu”.

Jambo hilo lilimfurahisha sana, pengine labda kwa kujiona yeye aliumbwa wa mwisho zaidi ya viumbe vingine vyote, halafu leo hii anasikia habari za kuwa kama Mungu lilimpa faraja sana..Lakini jambo hilo halikuwa ndani ya Adamu wakati wowote, japo yeye ndiye aliyeumbwa wa kwanza hakuwahi kutamani kuwa kitu fulani zaidi ya pale alipo, hakuwahi kuwa na tamaa ya kuwa juu ya kila kitu japo Mungu alimtawaza juu ya vyote, wala hakuwahi kumtawala mwanamke japo alitoka katika ubavu wake,. Sasa mwanamke alipoasi tu, mambo yakageuka, Ndipo Mungu akamlaani na kumwambia “tamaa yako itakuwa kwa mumeo”..

Hiyo tamaa ya kutaka kuwa juu, hiyo tamaa ya kutaka kuwa kichwa, ya kutaka kutawala sasa imehamishwa na kupelekwa kwa mumeo na matokeo yake, yeye ndiye atakayekutawala. Na ndio maana hayo mambo tunayaona sasa..wanaume wanatawala nyumba zao kwa nguvu, wanataka kujionyesha kuwa wao ni vichwa kati ya wake zao,wanawatiisha wanawake chini, wanataka waonekane kuwa wao ni watawala tu, wao wapo juu tu na wanawake wapo chini. jambo ambalo kiuhalisia halikupaswa kuonyeshwa kwa mwanaume yeyote yule, japo yeye ndiye aliyeumbwa wa kwanza. Umeona hiyo ndiyo laana iliyomkumba mwanamke.. na ndio maana mpaka leo jambo hilo ni Mwiba kwao, hususani kwa wanaume ambao hawajampa Bwana maisha yao, Lakini pia kumbuka Laana sio maagizo..Hatujaagizwa kuwatawala wanawake kwa mabavu katika maandiko.

 Tunanapokuwa wakristo na kumpa Bwana maisha yetu, tunabadilika kutoka katika laana hiyo, na badala yake tunakuwa sio wa kuwaonyesha mabavu yetu kwa wanawake badala yake tunatumia mamlaka yetu KUWAPENDA na kuwajali na kuwatunza kama vile Kristo alivyoonyesha kielelezo kwa kanisa.. mwanaume anapaswa ampende mke wake, kwa Upendo wote…Lakini hilo haliwapi wanaume mamlaka ya kuwatawala wanawake kwa namna isiyopasa bali tuwapende na tusionyeshe tabia kama hizo katika ndoa zetu. 

Waefeso 5:25 “Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;

26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;

27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.

28 Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.

29 Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa.

30 Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake”. 

Unaona?. Kristo hatupigi sisi, Kristo hatutesi sisi, Kristo haonyeshi tabia ya kutokutujali sisi, au kutokutupenda sisi..Vivyo hivyo na wanaume wanaomcha Mungu wanapaswa waonyeshe tabia hizo hizo kwa wake zao.. Na wanawake pia wafahamu wasipojinyenyekeza na kujishusha na badala yake kutaka wao wawe vichwa katika nyumba, hawatawaki kuwatii waume zao, wafahamu kuwa laana hiyo haikwepeki juu yao..Watatawaliwa tu kwa mabavu, wapende au wasipende!!.

Ndio maana ya hilo neno Tamaa yako itakuwa kwa mumeo

Ubarikiwe.


Mada nyinginezo:

UZAO WA NYOKA.

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.

MUNGU WANGU,MBONA UMENIACHA?.

SI SHETANI BALI NI WEWE. (CHAGUA MEMA)

DHAMBI ZINAZOTANGULIA NA ZINAZOFUATA.

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

UKWELI UNAOPOTOSHA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! mtu anaweza kutamka Neno zuri au baya kwa akili zake na likaja kutokea ikiwa si Mungu?

SWALI: Bibi yangu amenihadithia kuna Kaka yake mmoja alimuoa mke na akawa anamtesa na baadaye huyo kaka akaja kumkataa huyo mke baada ya kuzaa naye,Yule mke alipokuwa anarudi kwao Arusha alisema huyo Mume wake ataoa wake 1-12,kisha huyo wa 12 atakuwa kama fisi ammalize.Sasa baba huyo anaendelea kuoa leo mke huyu kesho yule kwasasa wameshafika takribani wake 6..Anaendelea..Swali je! Maneno yale ya yule mwanamke yanasimamiwa na Mungu au na Shetani?.


JIBU: Mtu yoyote akizungumza Neno kwa imani ni lazima litokee, uwezo huo Mungu amemuumbia mwanadamu ndani yake..Mwanadamu anaweza akaumba jambo lolote katika kinywa chake na likaenda kutokea kama lilivyo ikiwa atalifanya kwa imani.   Lakini Imani imegawanyika katika sehemu kuu tatu,..  

1.Imani inayotokana na Mungu, hii inakuja kwa kumwamini Mungu, na Neno lake, kwa mfano mtu anaweza kuamrisha ugonjwa utoke kwa Jina la Yesu, na ugonjwa huo ukatii, anaweza akatamka uzima kwa maiti na maiti ile ikarudia uhai,.Sasa imani ya namna hii ni ile imani ya Ki-Mungu na hii haina mipaka.  

2.Pili kuna imani inayotokana na shetani. Hii ni imani ile ambayo mtu anaweza akawa ni mchawi, au mshirikina au ana pepo fulani, kwa hiyo akizungumza Neno kwa imani, zile nguvu zilizopo ndani yake zinachanganyika na nguvu za giza kuhakikisha kuwa lile jambo linakwenda kutimia..kwa lugha ya sasa ndio unaweza ukasema mtu kalogwa au kafanyiwa jambo fulani la kichawi.  

3.Na tatu kuna imani ya mtu binafsi..hiyo haitokani na shetani wala Mungu..bali inatokana na nia ya mtu mwenyewe..kwamfano unapounyanyua mkono wako juu, hiyo ni roho yako unaunyanyua huo mkono kwa Imani, mkono wako lazima utii na kunyanyuka juu, vinginevyo usingenyanyuka kama maagizo yasingetoka rohoni, unapotaka kupaa mpaka mawingu, mpaka mwezini, ni jambo ambalo haliwezekani kwa namna ya kawaida, japo sasa mwanadamu hana mabawa lakini aliposema ninataka kufika kule juu, alifika kwa imani yake..sio Mungu wala shetani anayefanya hivyo ni wewe(roho yako)..Sasa kwa namna hiyo hiyo pia roho ya mtu inaweza ikazungumza jambo na likatimia vilevile, kama Mungu hataingilia kati..(Mathayo 17:20)   Mara nyingi Baraka za wazazi au laana za wazazi, huwa zinatokana na aina hii ya tatu ya imani, utakuta mzazi hamjui Mungu kabisa, wana hana habari yoyote na Mungu, lakini anaweza akambariki mtoto na mtoto anapata zile Baraka, au akamlaani na laana ile ikamfikia.

Kwahiyo kwa suala kama la huyo mwanamke kama sio Mkristo au kama hatumii nguvu za giza, basi inawezekana kaumizwa na tukio hilo sana na akaamua kuzungumza Neno lile la laana kwa Imani, na kama ni kama Mungu hatoliingilia kati basi ni lazima litimie.   Hivyo tuwe makini na sisi katika vinywa vyote, na ndio maana biblia inatushauri wakai wote tubariki wala tusilaani, maana hatujui maneno yetu tunayotoa yatakwenda kumuathiri yule kwa kiwango gani.(Warumi 12:14)

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

WATU WASIOJIZUIA.

KISASI NI JUU YA BWANA.

CHACHU YA MAFARISAYO NA CHACHU YA HERODE.

MAVAZI YAPASAYO.

DAMU YA ZAKARI BIN BARAKIA.

KWA MUNGU ASIYEJULIKANA.



Rudi Nyumbani:

Print this post

Je, kama hauna ubatizo sahihi hauwezi kuwa na Roho Mtakatifu?

JIBU: Utendaji kazi wa Roho Mtakatifu ni kama ufuatavyo, Mungu anapomchagua mtu aliye dhambini, huwa anamtumia Roho wake mtakatifu kumvuta mtu yule ndio hapo mtu huyo anaanza kusikia kuhukumiwa dhambi zake moyoni, na hatimaye anafikia toba, sasa huyo ni Roho Mtakatifu siku hizo zote anakuwa anamvuta mtu yule, anakuwa anatembea na yule mtu kama rafiki yake wa pembeni, lakini bado hajaingia ndani yake, ni kama mwanamume anapokuwa katika hatua za awali za kumchumbia mwanamke, anakuwa anaweza kuwa karibu naye, kumpa zawadi chache chache, kuzungumza naye maneno mazuri, kumwonyesha vitu vyake n.k, hayo yote mwanamume anayafanya ili tu kumvuta yule mwanamke, lakini bado yule mwanamke sio mali yake mpaka siku atakayoamua kumkubalia na kufunga naye ndoa, ndipo siku hiyo atakuwa milki halali ya yule mwanamume.

 Na Roho Mtakatifu ndio hivyo hivyo, katika hatua za awali, Roho Mtakatifu anaweza akazungumza na mtu, wakati mwingine akampa hata maono,kumfanikisha katika mambo yake n,k lakini akawa bado hajaingia ndani yake, yote hayo Roho Mtakatifu anayafanya ili kuzidi kumshawishi kuielekea njia sahihi ya wokovu……Na kama mtu yule bado atakuwa hajachukua hatua ya kumkaribisha ndani ya moyo wake kwa kutubu kabisa kwa kumaanisha kuacha dhambi zake na kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi, ataendelea kumshiwishi ndani yake mpaka siku atakapokubali.. 

Sasa siku yule mtu yule atakapoamua kubatizwa katika ubatizo sahihi, siku ile ile yule Roho Mtakatifu ambaye alikuwa anatembea naye anaingia ndani yake na kuwa milki halali ya Roho Mtakatifu mwenyewe, wanakuwa ni kama wamefunga ndoa na Roho Mtakatifu, kwasababu ubatizo ndio kibali cha Roho Mtakatifu kuingia ndani ya mtu, ni ishara ya dhambi za mtu kuondolewa kwa damu ya Yesu, na ni muhimu sana na ndio maana Bwana aliyaagiza, sasa baada ya hapo ndipo Roho Mtakatifu anakuja kufanya makao ndani ya yule mtu. Biblia inasema Roho Mtakatifu ndio Muhuri wa Mungu, kama unavyojua barua yoyote isiyokuwa na muhuri halisi hiyo ni batili. Roho Mtakatifu ni kama Pete ya ndoa kwa wanandoa. 

Waefeso 4: 30 “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi”.

2Wakorintho 1: 22 “..naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu”. 

Na akishaingia ndani ya yule mtu anaanza kupitishwa madarasa mengine ya kiroho zaidi, na huyo mtu shetani hawezi kumpata tena kwasababu ni kama kashakatiwa leseni mbinguni kuwa milki halali ya Roho mtakatifu, Na pia maandiko yanasema katika ….Warumi 8:9 “……Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.”…kwa lugha nyepesi mtu yoyote ambaye hajafunga ndoa na Roho Mtakatifu kwa njia ya UBATIZO SAHIHI huyo sio wake, haijalishi Roho Mtakatifu anamwonyesha maono, anazungumza naye n.k bado huyo sio wake. 

Mwingine atasema mbona wapo ambao wamebatizwa huo ubatizo sahihi lakini bado ni waovu? je! wewe unamkosoa Bwana wako aliyekupa hayo maagizo kwamba alichokisema hakina umuhimu sana katika kazi ya ukombozi?..Mbona husemi hivyo kwa mitume waliobatizwa kwa njia hiyo?.. Nakushauri usiwaangalie wanadamu kama ni kipimo cha wokovu wako, hujui mtu huyo aliuendea ubatizo kwa kidini tu, au kuwaridhisha wanadamu, au kwa faida zake mwenyewe..Lakini fahamu kuwa Ubatizo sahihi wafaa sana kwa wokovu wako mwenyewe. 

Ubarikiwe.


Mada nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA.

NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?

NINI MAANA YA KUTOKA KATIKA MADHEHEBU?

ROHO ZILIZO CHINI YA MADHABAHU:

MKATAE SHETANI NA MAWAZO YAKE YA KIBINADAMU.

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Mungu anaupendeleo kwa wanaume zaidi ya wanawake?

JIBU: Ndivyo inavyodhaniwa na wengi, hususani linaposomwa lile andiko lisemalo

1Timotheo 2:13 “Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye.”

Maneno hayo yanathibitisha kuwa Adamu ndiye aliyepewa kipaumbele cha kwanza kuliko mwanamke..   Lakini ifahamike kuwa Mungu ni Mungu wa utaratibu. Tunapotaka wote tufanane, wote tuje kwa wakati mmoja, na wote tuwe na mamlaka yanayofanana, basi maisha yangekuwa hayana maana. Hivyo Ili Mungu kutimiza kusudi lake, na kuweka mambo yote katika utaratibu ilimpasa aweke ngazi lakini hilo halimaanishi kuwa mmoja ni bora zaidi ya mwingine..Kwasababu kama tukichukulia kigezo cha kuumbwa kwa mwanaume kwanza zaidi ya mwanamke ndio tiketi..

Kumbuka pia wanyama na mimea yote iliumbwa kwanza kabla hata ya Adamu kuumbwa..Sasa hapo tuseme wanyama wamepewa upendeleo mkubwa zaidi ya sisi?.   Jibu ni hapana, lakini tatizo kubwa linakuja pale wanaume wanapotaka kuwa kama wanawake na wanawake wanapotaka kuwa kama wanaume, katika utendaji kazi wao Mungu aliowawekea, hususani pale katika suala la UONGOZI katika kanisa, na nyumbani. Biblia inasema je! MAUMBILE NAYO HAYATUFUNDISHI?(1Wakorintho 11:14).

Tujifunze katika maumbile ya kila mmoja, jinsi alivyoumbwa, ili tupate kulijua kusudi la Mungu katikati yetu, jaribu kufikiria suala la uleleaji wa mtoto, baba hata aweze kufanya shughuli zote za ndani namna gani, hata aonyeshe upendo kwa mtoto mkuu dizaini gani bado hataweza kumtolea mtoto chakula mwilini mwake.   Hiyo shughuli nzito na jukumu la kipekee namna hiyo ameumbiwa mwanamke tu (mama). Shughuli nzito ya kumlea akiwa kijusi tumboni, mpaka kiumbe kipya duniani na changamoto zake zote, wakati mwingine hata wengine kupoteza maisha yao kwa changamoto hizo, ni mama peke yake ndiyo aliyeumbiwa, mwanaume hata awe shujaa kiasi gani,..akijaribu kufanya hivyo atakuwa anapoteza muda wake…..hawezi kufanya hivyo hata atamanije!!….Kadhalika kazi ya ulinzi, uangalizi wa nyumba, kazi za kutumia nguvu nyingi, mwanamke hata akijitahidi vipi kwenda kubeba viroba vya michanga atakuwa anajiumiza tu mwenyewe.

Shughuli hizo na taabu hizo Mungu kamuumbia mwanaume. Japo zipo zinazofanywa na wote hilo lipo wazi, lakini tatizo linakuja ni pale kila jambo, ambalo mwanaume ametawazwa na Mungu kulifanya mwanamke naye anataka kulifanya..asilimia 50 kwa 50..Na hilo ndio limekuwa tatizo kubwa.Ambao ni mpango mkamilifu wa shetani, mwanaume anavaa suruali mwanamke naye anataka kuvaa suruali, mwanaume anavaa kaptura mwanamke naye anataka kuvaa kaptura, mwanaume ananyoa nyewe zake, mwanamke naye ananyoa kipara afanane na mwanaume.   Kwa mfano tukirudi kwenye kanisa:

Biblia inasema

1Wakorintho 14.34 “Wanawake na wanyamaze katika kanisa, maana hawana ruhusa kunena bali watii, kama vile inenavyo torati nayo..”Na pia inasema 1Timetheo 2: 12 “Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu”.  

Utakuta Baadhi yao wanaona kama Mungu kawaweka nyuma katika kazi yake, na hivyo wanaamua kuyahalifu kwa makusudi maagizo ya Mungu na kwenda kufundisha makanisani, na kuwatawala waume zao. Wakidhani kuwa ndio wanajenga, kumbe hawajui kuwa wanabomoa. Hekima ya Mungu ni kubwa zaidi ya mwanadamu, akisema hivi anamaanisha hivyo, yeye anajua ni jinsi gani mwanaume atatenda vizuri katika eneo hilo zaidi ya mwanamke na ndio maana akasema hivyo..  

Lakini kwa anayemwona Mungu hapo kakosea kuweka ngazi, na mamlaka katika kazi yake mwenyewe aliyoibuni duniani biblia ipo wazi yanasema hivi:

1Wakorintho 14: 37 “Mtu akijiona kuwa ni nabii au mtu wa rohoni, na ayatambue hayo ninayowaandikia, ya kwamba ni maagizo ya Bwana. 38 LAKINI MTU AKIWA MJINGA, NA AWE MJINGA”.  

Baki katika nafasi uliyoitiwa, Biblia haina mfumo dume hapana bali ina utaratifu. Na utaratibu huo ni Mungu mwenyewe ndio kauweka kulingana na jinsia.  

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

RABONI!

MARIAMU

UZAO WAKO UTAMILIKI MALANGO YA KUZIMU;

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

UTAWALA WA MIAKA 1000.

UNYAKUO.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post