Category Archive Home

NGUVU YA HEKIMA NA AKILI

Shalom Mtu wa Mungu, karibu tujifunze Maneno ya Mungu, Uzima wetu na Taa yetu ituongozayo katika njia sahihi ya kufika mbinguni…

Sulemani Mfalme wa Israeli mwana wa Daudi, Ni mtu aliyempendeza Mungu sana hata kufikia hatua ya kuambiwa aombe lolote naye atapewa…Tunaona Mfalme akachagua kuomba Hekima badala ya Mali, na Maarifa badala ya Ufahari na nguvu za kijeshi…sio kwamba alichagua hivyo kwasababu alikuwa hapendi utajiri au ufahari, hapana alikuwa anaupenda na kuutamani, lakini alipiga hesabu awe na utajiri na nguvu za kijeshi kuliko wafalme wote duniani, halafu akose akili ya namna ya kuwaongoza na kutatua matatizo ya watu wake itamfaidia nini?..Kwahiyo akaona jambo la kwanza la kuchagua ni akili na hekima kwanza , na hayo mengine yatafuata mbele ya safari kama yatakuwa na ulazima.

Hebu leo tupewe na sisi nafasi kama hiyo, Mungu atuambie tuombe lolote naye atatupa…Utaona wengi wetu mambo tutakayoyakimbilia kwanza, tupewe mali nyingi na utajiri ili tuishi kwa raha sisi na familia zetu, na ndugu zetu na ukoo mzima…Lakini ni wachache sana watachagua Mungu awape Hekima na akili za kuwapenda wenzi wao na ndugu zao, na akili na maarifa ya kuwalea watoto wao katika njia inayopasa kutokujali kiwango cha utajiri au umaskini walichonacho…Hilo ndio lingetakiwa liwe jambo la kwanza la kuomba kisha hayo mengine ndio yafuate..

Kwasababu itakufaidia nini, uwe na fedha nyingi na utajiri mwingi na kuwatimizia watoto wako mahitaji yote na Mwisho wa siku wanakuja kuwa mashoga au makahaba? Si ni afadhali wale chakula cha kawaida kila siku lakini ni matajiri wa akili na hekima, walizozipata kutoka kwako na mwisho wa siku watakapokuja kuwa wakubwa watakuwa msaada kwako na kwa wengine?..au itakufaidia nini uwe na mali nyingi na fedha nyingi lakini mke wako au mume wako haoni raha ya kuishi na wewe?..unapata mali lakini unakosa hekima ya jinsi ya kuishi na mume/mke. Hiyo ni hatari sana…

Ndio maana biblia inasema katika Mithali 16:16 “ SI AFADHALI KUPATA HEKIMA KULIKO DHAHABU? NAAM, YAFAA KUCHAGUA UFAHAMU KULIKO FEDHA.” ..Hayo ni maneno ya mtu aliyekuwa tajiri kuliko wote duniani anakushauri hivyo, kwasababu yeye ameyapitia mengi na kuyaona mengi…Ni afadhali na Njiwa wanakaa kwenye viota vilivyotengenezwa na nyasi lakini upendo wao ni wa milele, kuliko kuishi kwenye kasri ambalo ni malumbano kutwa kuchwa.

Mhubiri 4:6 Heri konzi moja pamoja na utulivu, Kuliko konzi mbili pamoja na taabu; na kujilisha upepo.

Sulemani aliliona hilo akachagua Kuwa na Hekima, ambayo hekima hiyo biblia inasema ilizidi ikapita mpaka wana wote wa Mashariki,

1 Wafalme 4: 29 ‘Mungu akampa Sulemani hekima, na akili nyingi sana, na moyo mkuu, kama mchanga ulioko pwani.

30 Hekima ya Sulemani ikapita hekima ya wana wote wa mashariki, na hekima zote za Misri.

31 Kwa kuwa alikuwa na hekima kuliko watu wote; kuliko Ethani Mwezrahi, na Hemani, na Kalkoli, na Darda, wana wa Maholi; zikaenea sifa zake kati ya mataifa yote yaliyozunguka.

32 Naye akanena mifano elfu tatu, na nyimbo zake zilikuwa elfu moja na tano.

33 Akanena habari za miti tangu mwerezi ulioko Lebanoni hata hisopo umeao ukutani; pia akanena habari za wanyama, na za ndege, na vitambaavyo, na samaki.

34 Wakaja wa mataifa yote ili waisikie hekima ya Sulemani, toka wafalme wote wa ulimwengu, waliokuwa wamepata habari za hekima yake”.

Aliona kuliko awe tajiri kama baba yake na kuwa na nguvu nyingi za kijeshi kama baba yake halafu kila kukicha ni kutokuwa na maelewano ndani ya nchi yake, kila kukicha kupambana vita na maadui zake, aliona huo ni udhaifu mkubwa sana…akamwomba Mungu ampe hekima na akili ya namna ya kutawala, na Mungu akampa…Ndio maana utaona Sulemani hakukumbana na vita yoyote kama baba yake, lakini utawala wake ulikuwa na nguvu kuliko wa Daudi baba yake..hakushika upanga kwenda vitani lakini Maadui zake walikuwa wanamwogopa. Hakumuua Goliathi kwa upanga wala kwa kombeo, lakini Wafilisti walimwogopa. Kwa ufupi hakuna mtu aliyekuwa anadhubutu kupanga vita juu ya Sulemani kwasababu walikuwa wanamwogopa na wanamheshimu. Kwa hekima yake ya kutatua mambo. Alikuwa anao uwezo wa kusulihisha mambo mengi ikiwemo vita kabla hata halijafikia katika vilele vyake, kwa hiyo hekima ambayo Mungu alimpa.

Hivyo ndivyo Sulemani alivyokuwa anatawala, na kwasababu alikuwa hapambani vita, hakutumia gharama zozote vitani, na hivyo uchumi wake ulikuwa unakuwa kwa kasi, tofauti na Baba yake Daudi au Sauli, wao kukitokea ugomvi ni rahisi kuingia kwenye mapambano pasipo mazungumzo, kwasababu walikuwa wanaamini Mungu kuwa amewapa vyote na maadui zao watakuwa chini yao siku zote, kila watakapokanyaga kama ni mapenzi ya Mungu, Mungu atawamilikisha na kweli ndivyo ilivyo, Mungu alikuwa na Daudi kila mahali alishinda vita nyingi..Lakini walitumia gharama nyingi zisizokuwa na maana na muda mwingi vitani jambo ambalo lingeweza kusulihishwa kwa njia ya hekima au akili, ndio maana unaona haikuwa hivyo kwa Sulemani, Mungu alimshindia vita Sulemani pasipo kupambana vita, alimpa Hekima kama Silaha yake badala ya mapanga na nguvu. Haleluya!!.

Ndugu Hekima ni silaha kubwa sana…Ndio maana utaona ni kwanini mtu mmoja anakaa na mke wake au mume wake mwenzi mmoja au mwaka mmoja wameachana, na mwingine hana fedha wala si tajiri lakini wameishi na mwenzi wake miaka zaidi hata ya 40 na bado wanapendana na kuvumiliana, ni kwasababu ya hekima iliyopo ndani ya hao wawili..Sio kwamba hawajawaji kukosana kabisa, wanakosana lakini kila kukitokea kutokuelewana kidogo tu! Mmoja wao anatumia hekima ya kiMungu kutatua hilo tatizo kabla hawajafika mbali kabla hawajakwenda kumwambia mama mkwe au babamkwe au marafiki, hekima iliyo ndani yao inawapeleka kwenye unyenyekevu, upendo, uvumilivu, ustaarabu, kusitiriana, kuchunguza jambo kabla ya kuchukua hatua, kujaliana, kusameheana nk.

Lakini hao wengine waliokosa hekima utaona kukitokea tatizo kidogo tu! Moja kwa moja mguu wa kwanza ni kwa marafiki na mashosti kuwaelezea kinachoendelea kati yao na wenzi wao..Na ndio huko huko shetani anapata nafasi wanapata ushauri wa kipepo wa kuachana na kuaibishana wakati mwingine, na mwisho wa siku ndoa inavunjika. Na sio tu katika Nyanja ya ndoa, bali katika Nyanja zote za maisha Hekima ni silaha kubwa.

Ndugu kama haya yanaendelea kwako, achana na hayo maombi unayoomba au unayoombewa kila siku ya mafanikio ya biashara yako na kazi yako, anza kuomba hekima..Biblia inasema..

Mithali 16:16 “ SI AFADHALI KUPATA HEKIMA KULIKO DHAHABU? NAAM, YAFAA KUCHAGUA UFAHAMU KULIKO FEDHA.”

Ukiona matatizo kama hayo yamekutokea na unashindwa namna ya kuyatatua ni dhahiri kuwa umepungukiwa hekima na sio kingine..Na kupungukiwa hekima sio dhambi, ni udhaifu tu ambao kila mtu anazaliwa nao, na hivyo unaweza ukaondoka endapo mtu akitaka uondoke!..Kwahiyo unachotakiwa kufanya ni KUOMBA HEKIMA KWA MUNGU!.

➽Yakobo 1: 15 ‘’LAKINI MTU WA KWENU AKIPUNGUKIWA NA HEKIMA, NA AOMBE DUA KWA MUNGU, AWAPAYE WOTE, KWA UKARIMU, WALA HAKEMEI; NAYE ATAPEWA.

6 Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.

7 Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.

8 Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote”.

Neno limetushauri kama tumepungukiwa na Hekima na tuombe, Sulemani aliomba hekima kwasababu aliona amepungukiwa..na sisi vivyo hivyo, tunapaswa tuombe! Kama tu nyimbo ya taifa letu TANZANIA, tunapoiimba tunamwambia Mungu aibariki nchi yetu, huku tukisema HEKIMA ni ngao yetu…yatupasaje sisi tunaoamini? Tunapaswa tuombe Ili tuongezewe hekima! Lakini tunapaswa tuombe kwa imani na pasipo kusitasita.

Sasa Maana ya kuomba kwa imani ni nini?.

Maana yake unapaswa uombe, ukiwa ndani ya IMANI ya YESU KRISTO, na ukiwa na uhakika kwamba Mungu unayemwomba anakusikia na anawapa thawabu watu wajinyenyekezao kwake!..ukiwa nje ya Imani ya Yesu Kristo ni ngumu kupokea hiyo hekima, kwasababu hiyo Hekima ndio Yesu Kristo mwenyewe. Na pia hutakiwi kusita sita..Maana ya kusitasita ni kuwa na mawazo mawili… “mawazo ya ..aa sijui itawezekana, sijui nimesikiwa?”..na mawazo ya kushika hili na lile kwa wakati mmoja!! Kwasasa lenga jambo moja tu! Kumwomba Mungu hekima, usianze kuomba; Bwana naomba hekima, unipe na utajiri nipate hela, unipe na magari matatu, nyumba, unipe maisha marefu, unipe na biashara kubwa ya kimataifa n.k

HUKO NI KUSITA-SITA KWENYE MAWAZO MAWILI na hakumpendezi Mungu, ni sawa na mwanajeshi anayekwenda vitani na kumwomba kamanda wake ampe bunduki tatu za kubeba, mabomu sita, ampe na ndege ya vita na kifaru cha kisasa, ampe na mboksi matatu ya risasi, visu ishirini, ampe na kombora moja la nyuklia..Ni wazi kuwa huyo mwanajeshi hajiamini na hafai kwenda vitani..Na sisi hatupaswi kuwa hivyo.Kusita sita kwa kushika mambo mawili kwa wakati mmoja, Tunatumia silaha MOJA YA HEKIMA KWANZA, hizo nyingine zitakuja baadaye. Kama Sulemani alivyofanya hakuanza kumwambia Mungu naomba hekima, unipe na watoto sita waje kuwa wafalme, unipe na maisha marefu, unipe na utajiri, unipe na umaarufu na ufahari dunia nzima wanijue…hapana hakufanya hivyo hakusitasita kwenye mawazo mawili aliomba jambo moja kuu kwanza HEKIMA, na hayo mengine Mungu atayafungua mbele ya safari.

Tunasoma..

1 Wafalme 3; 9 “Kwa hiyo nipe mimi mtumwa wako moyo wa adili niwahukumu watu wako, na kupambanua mema na mabaya; maana ni nani awezaye kuwahukumu hawa watu wako walio wengi?

10 Neno hili likawa jema machoni pa Bwana, ya kuwa Sulemani ameomba neno hili.

11 Mungu akamwambia, Kwa kuwa umeomba neno hili, wala hukujitakia maisha ya siku nyingi; wala hukutaka utajiri kwa nafsi yako; wala hukutaka roho za adui zako; bali umejitakia akili za kujua kuhukumu;

12 basi, tazama, nimefanya kama ulivyosema. Tazama, nimekupa moyo wa hekima na wa akili; hata kabla yako hapakuwa na mtu kama wewe, wala baada yako hatainuka mtu kama wewe.

13 NA MAMBO YALE USIYOYAOMBA NIMEKUPA, MALI NA FAHARI, HATA HAPATAKUWA NA MTU KATIKA WAFALME KAMA WEWE, SIKU ZAKO ZOTE”.

Unaona Mungu anamwambia Sulemani nimekupa HATA YALE MAMBO USIYOYAOMBA! Tatizo kubwa lililopo katika Ukristo leo hii, ni kushindwa kuelewa kuwa Mungu anajua mahitaji yetu kabla hata ya sisi kumwomba, hata pasipo kumwambia anaweza kukutimizia mahitaji yako endapo utakuwa UMESHIKA JAMBO MOJA KUU NA LA MUHIMU.

Mungu si mwanadamu, au hana udhaifu wa kibinadamu wa kusahau kuwa hitaji moja linategemea lingine, umemwomba kiatu anajua kabisa utahitaji na soksi, kwasababu huwezi kuvaa kiatu bila soksi, kwahiyo siku atakapokujibu ombi la kiatu atakupa na soksi hapo hapo..atakutengenezea na mazingira ya kupata fedha ya kwenda kukisafisha na kukipiga rangi pia… Lakini tanguliza kwanza ombi la msingi la kuomba kiatu, ili hayo mengine Bwana akuongezee.

Na leo hii shika jambo hili moja kuu na la Muhimu “HEKIMA” Itafute hiyo na hayo mengine yote utazidishiwa, mali, maisha marefu, watoto, heshima,  n.k lakini la kwanza ni Hekima.

Mungu akubariki sana.Tafadhali “share” Ujumbe huu kwa wengine.

Kwa Maombezi, Ushauri, au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225789001312/ +225693036618

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

UMEFUNULIWA AKILI?

KUNA TOFAUTI GANI KATI YA SALA NA DUA?


Rudi Nyumbani

Print this post

MADHARA YA KUTAFUTA ISHARA.

Ni kweli kitendo cha Kufa na kufufuka kwa Bwana Yesu kilikuwa kimeshatabiriwa hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya dhambi za ulimwengu wote na kufufuka, Lakini pia tujiulize kwanini kufufuka kwake kulikawia kidogo, mpaka zikafika siku tatu, au kwanini zisiendelee na kuwa 10 au 20, kwanini ziwe ni zile tatu tu. Ndio tunaweza kusema hiyo ilikuwa ni kupisha muda wa kwenda kuzimu, lakini huko kuzimu kwanini kusingechukua siku moja au wiki, Ukweli ni kwamba siku ile ile aliyokufa, angepaswa afufuke siku hiyo hiyo, na angekuwa hajayatangua maandiko yoyote yale. Lakini kukaa kwake kaburini siku tatu, kulisababishwa na baadhi ya watu, ambao leo tutawaona, tunaweza kudhani kitendo kile ni kizuri sana kama watu wanavyodhani..Lakini nataka nikuambie ndugu tunapaswa tujitathimini sana.

Kumbuka wale watu Bwana aliokuwa nao (Wayahudi) sikuzote walikuwa ni watu wa kutokuamini, japo Mungu alijidhihirisha kwao kwa namna nyingi kwa kupitia manabii wake wengi huko nyuma lakini bado walikuwa hawataki kuamini mpaka waone ishara Fulani, sio kwamba Mungu alikuwa hawapi ishara alikuwa anawapa ishara nyingi njema lakini bado wakipewa walikuwa hawasadiki vile vile, mpaka ilipofikia wakati Mungu anakaribia kumleta Yesu duniani, Mungu aliwatangulizia Yohana mbatizaji kwanza kwa roho ya Eliya, lakini bado hawakutaka kuamini. Yaani kwa ufupi ni watu ambao walikuwa hawaeleweki wanataka kitu gani, au waone ishara ya aina gani ili waamini..Na ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 11:16 ‘Lakini nitakifananisha na nini kizazi hiki? Kimefanana na watoto wanaokaa sokoni, wanaowaita wenzao, wakisema,

17 Tuliwapigia filimbi, wala hamkucheza; tuliomboleza, wala hamkulia.18 Maana Yohanaalikuja, hali wala hanywi, wakasema, Yuna pepo.

19 Mwana wa Adamu alikuja, akila na kunywa, wakasema, Mlafi huyu, na mlevi, rafiki yao watoza ushuru na wenye dhambi! Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwakazi zake.

20 Ndipo akaanza kuikemea miji ile ambamo ndani yake ilifanyika miujiza yake iliyo mingi, kwa sababu haikutubu.

21 Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu zamani kwa kuvaa magunia na majivu.

22 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zao siku ya hukumu kuliko ninyi.

23 Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujizailiyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo.

24 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe”.

Pamoja na Kwamba Bwana Yesu alikuwa anawafanyia miujiza mikubwa kama ile, na ishara nyingi kiasi kile, lakini bado walikuwa wanataka waonyeshwe ISHARA nyingine zitakazowashawishi wamwamini

Hilo tunalithibitisha kwenye vifungu hivi vya maandiko:

Yohana 6:30 “Wakamwambia, Unafanya ishara gani basi, ili tuione tukakuamini? Unatenda kazi gani? 31 Baba zetu waliila mana jangwani kama vile ilivyoandikwa, Aliwapa chakula cha mbinguni ili wale.

32 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Siye Musa aliyewapa chakula kile cha mbinguni, bali Baba yangu anawapa ninyi chakula cha kweli kitokacho mbinguni.

33 Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima”.

Unaona? ni watu wa kupenda ishara tu, na hata walipopewa walikuwa bado hawaamini.Jiulize dakika chache tu nyuma Yesu aliwavunjia ile mikate 5 wakala maelfu ya watu, hilo hawakuliona kama ni ishara kwao inayofanana na ile ile ya Musa..hilo hawakuliona, Watu wa namna hiyo unadhani wataonyeshwa jambo gani waridhike?

Biblia imeweka wazi kabisa Wayahudi ni watu wa kupenda Ishara, soma (1Wakorintho 1.22) kwasababu Wayahudi wanataka ishara, na Wayunani wanatafuta hekima;

Sasa mambo hayo yalipozidi Bwana hakupendezwa nao kabisa, Na ndio akawaambia maneno haya.

Luka 11:29 “Na makutano walipokuwa wakimkusanyikia, alianza kusema, Kizazi hiki ni kizazi kibaya; kinatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ILA ISHARA YA YONA.

30 Maana, kama vile Yona alivyokuwa ishara kwa Waninawi, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu kwa kizazi hiki”.

Sasa wakati mwingine tunapaswa tujiulize ni kwanini Bwana hakuwachagulia ishara ya aina nyingine bali ile ya Yona?, kwanini asingewapa ishara kama ya Eliya kushusha moto, au ya Joshua kusimamisha jua, bali kawapa ile ya Yona?.

 

Embu turudi kumchunguza Yona kidogo, kumbuka Yona hakutumwa kwenda kuwaokoa wana wa Israeli, wala hakutumwa kwenda kutoa tu unabii na kuondoka kama alivyokuwa anafanya huko nyuma katika Taifa la Israeli, hapana bali alitumwa Ninawi kwenda kutangaza hukumu. Kwamba baada ya siku 40 Ninawi inaangamizwa kama wasipotubu..Sasa Hekima ya Mungu ilivyokuwa kubwa aliruhusu Yona akengeuke, ili amezwe na Yule samaki, ili akae siku tatu usiku na mchana kwenye tumbo lile. Na siku atakapotapikwa aende kuwahadithia watu wa Ninawi mambo yote yaliyomkuta…kwamba wale watu watathimini wenyewe kama yeye kwa kosa moja tu! La kutokuisikiliza sauti ya Mungu yamemkuta hayo, itakuwaje wao ambao maisha yao yote yapo kwenye dhambi watapataje kupona kama wasipotubu?.

Unaona Vivyo hivyo Mungu aruhusu Kristo amalize siku tatu kaburi, mfano wa Yona, ili somo lieleweke vizuri, kama ISHARA kwa WAYAHUDI. Lakini onyo haliendi kwao Bali linakuja kwetu sisi watu wa mataifa. Kama vile Yona hapo mwanzo alikuwa ni nabii wa Israeli tu, lakini ili afikie mataifa ilimpasa siku tatu zipotelee kwenye tumbo la samaki. Sasa leo hii tunafurahia Yona katapikwa na Yule samaki, lakini hatufahamu ujumbe Yona anaotuletea sisi, kuwa TUTUBU, kwani baada ya siku 40 mataifa yote yataangamizwa.

Upo usemi unaosema siku za mwizi ni 40, hiyo haimaanishi kuwa ni siku 40 kweli kweli hapana, bali ni lugha tu iliyopenda kutumia neno 40 kama kiashiria cha neema. Vivyo hivyo zile siku 40 za watu wa Ninawi walizopewa watubu ndio siku 40 zetu sisi katika roho watu wa mataifa..

Injili inahubiriwa miaka 2000 sasa, unaopoona kufa kwa Yesu na kukaa kwake kaburini siku tatu unaona ISHARA GANI NZURI HIYO?, Amefufuka na kutoka Kaburini ili kukuhubiria kuwa yapo mabaya mbeleni yanakuja kama hutatubu.

Ndugu hizi ni nyakati za mwisho, UNYAKUO upo karibu sana kutokea, vile vile na maangamizi ya dunia hii yapo karibu sana kutokea Biblia imesema hivyo. Tumepewa kipindi kirefu hichi cha kutubu, tusipofanya hivyo kama unyakuo hautatukuta basi kifo ni lazima, sasa tutawezaje kupona siku ile. Tutajitetea vipi mbele za Mungu kuwa hatukuwa na muda. Na ndio maana Bwana alimalizia na kuwaambia wale watu maneno haya.

“……32 WATU WA NINAWI WATASIMAMA SIKU YA HUKUMU PAMOJA NA KIZAZI HIKI, NAO WATAKIHUKUMU KUWA NA HATIA; KWA SABABU WAO WALITUBU KWA MAHUBIRI YA YONA, NA HAPA PANA MKUBWA KULIKO YONA”.

Yona alihubiri siku tatu akaenda kukaa kule mlimani akisubiria maangamizi, lakini Sisi tumekuwa tukiisikia injili ya Yesu Kristo kila siku na bado tunaendelea kusikia injili masikioni mwetu kwa njia mbalimbali kuonyesha ni jinsi gani Kristo anavyotuhurumia tusiangamie kwa hayo mambo mabaya yanayokuja huko mbele.

Ni maombi yangu, ikiwa bado upo katika dhambi utatubu leo, kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi zako, na hakika Bwana atakupokea na kukufanya kuwa kiumbe kipya..Na ikiwa pia wokovu wako ni wa kusua sua, mguu moja huku mwingine kule, ni vizuri leo ukafanya maamuzi ya kusimama imara, Hakikisha pia baada ya kutubu kwako, tafuta mahali ukabatizwe katika ubatizo ulio sahihi wa kimaandiko kukamilisha wokovu wako. Na ubatizo sahihi ni ule wa kuzamishwa katika maji tele na uwe katika Jina la YESU KRISTO.

Nakutakia kila la heri katika safari yako ya wokovu hapa duniani. Na Bwana akubariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri au Ratiba za Ibada basi Wasiliana nasi kwa namba

+225789001312/ +225693036618

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

SAUTI NYUMA YA ISHARA.

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA

MWEZI NI ISHARA GANI KWETU?

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.


Rudi Nyumbani

Print this post

TULICHUNGUZE UMBO LA YESU NA MWENENDO WAKE.

Kuna maswali mengi tunajiuliza juu ya mwonekano wa nje wa Bwana wetu Yesu Kristo ulikuwaje! Je alikuwa ni mweupe au mweusi, je alikuwa ni mrefu au mfupi, je alikuwa ni mnene au mwembamba?, je! Alikuwa mzuri au wa kawaida?..Biblia inasema nini juu ya jambo hilo?.

Sehemu pekee tunayoweza kuisoma kwenye maandiko na kutupa walau picha ndogo ya mwonekano wake ni Isaya 53:2 Inasema: “Maana alikua mbele zake kama mche mwororo, Na kama mzizi katika nchi kavu; YEYE HANA UMBO WALA UZURI; NA TUMWONAPO HANA UZURI HATA TUMTAMANI”.

Mstari huo unaonyesha kuwa Bwana wetu, alikuwa ni mtu mwenye mwonekano wa kawaida sana..mtu kusema hana umbo inamaanisha kuwa ukimweka katikati ya wanaume wanaovutia unaweza ukashangaa sana, kwenye uzuri tukisema tunamweka katikati ya wenye sura nzuri (ma-handsome) yeye anaweza akawa miongoni mwa wale wa mwisho mwisho pengine,..Ni mtu ambaye mtu akipishana naye barabarani hawezi kuyateka macho yako, kama mtu wa ajabu au ageuke nyuma amtazame, alikuwa ni wa kawaida sana kimwonekano, na ndicho kilichowakuta hata watu aliokuwa nao wakati ule, japo alijulikana sana, umaarufu wake ulienea duniani kote, lakini ilikuwa bado tu ni shida watu kumkariri sura yake, kwasababu si sura ambayo huwezi ukaitilia maanani ukimwona, alikuwa ni mtu wa kawaida. Bwana Yesu hakuwa kama hao watu wanaoonekana kwenye sinema, na kwenye picha wazuri, wanavutia. Sio kwamba alikuwa ni mtu mbaya kwa sura, kwasababu hakuna mtu mbaya duniani, watu wote ni wazuri, lakini tunaweza kusema alikuwa ni mtu wa kawaida.

Unajua kama ulishawahi kugundua jambo mfano umeenda mahali tuseme kwenye ofisi Fulani, ukakutana na wanafanyakazi wa pale, ukikaa tu dakika chake kuyasoma yale mazingira utaweza kumgundua boss wao ni nani, hata kabla ya kuambiwa chochote…utamgundua pengine kwa kiti chake anachokalia, utamgundua kwa wafanyakazi jinsi wanavyomnyenyekea, au anavyowaamrisha, utamgundua hata wakati mwingine kwa mavazi yake, na utembeaji wake…Lakini kwa Bwana YESU haikuwa hivyo, alipokaa na mitume wake kwa miaka zaidi ya mitatu na nusu bado makuhani, na watu wengi walishindwa kumtambua alipoketi katikati ya makutano au wanafunzi wake. mpaka walipotaka kumkamata iliwabidi wakaombe msaada kutoka kwa mmoja wa wanafunzi wake awasaidie.

Hilo tunalithibitisha siku ile Bwana aliyokuja kusalitiwa na Yuda..

Yohana 18:3 “Basi Yuda, akiisha kupokea kikosi cha askari na watumishi waliotoka kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo, akaenda huko na taa na mienge na silaha.

4 Basi Yesu, hali akijua yote yatakayompata, akatokea, akawaambia, NI NANI MNAYEMTAFUTA?

5 Wao wakamjibu, Ni Yesu Mnazareti. Yesu akawaambia, NI MIMI. Yuda naye aliyemsaliti alikuwa amesimama pamoja nao.

6 Basi alipowaambia, Ni mimi, walirudi nyuma, wakaanguka chini.

7 Basi akawauliza tena, Mnamtafuta nani? Wakasema, Yesu Mnazareti.

8 Yesu akajibu, Nimekwisha kuwaambieni ya kwamba ni mimi; basi ikiwa mnanitafuta mimi, waacheni hawa waende zao”.

Unaona?, Unaweza kudhani wale watu walikuwa wanajifanya kutokumjua, utauliza walishindwaje wakati kila siku walikuwa wanamwona Hekaluni akifundisha, lakini ni kweli ilikuwa ni ngumu kumtambua Bwana, hata wewe ungekuwepo bado ungehitaji msaada wa kusaidiwa kumtambua. Hiyo yote ni kwasababu ya mwenendo wake wa unyenyekevu, hakuwa na nguo za kipekee sana kumtofautisha na mitume wake, hakuwa mzuri wa uso zaidi ya mitume wake, hakujipiga scrabing kujionyesha kuwa yeye anatunzwa zaidi ya mitume wake, wala hakuwahi kujionyesha kuwa yeye ni mkuu zaidi ya wengine, kama ingekuwa ni hivyo wale watu wasingetumia nguvu kumtambua, lakini hawakuweza mpaka YESU alipowathibitishia mara mbili ya kuwa yeye ndiye.

Unyenyekevu wa Bwana wetu Yesu Kristo ulikuwa ni mkuu sana, na sisi tunapaswa tuuige mfano huo, unakumbuka pale alipokuwa anawatawadha wanafunzi wake miguu aliwaambia maneno haya: “Ninyi mwaniita, Mwalimu, na, Bwana; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo” (Yohana 13:13), lakini mimi mbele yenu ni kama atumikaye..nami nimewapa kielelezo kama mimi nilivyowatendea ninyi nanyi mkatende vivyo hivyo.” Akamalizia na kusema..

“MKIYAJUA HAYO HERI NINYI MKIYATENDA.”

Tusipende kuitwa wakuu, tusipende kujionyesha sisi ni tofauti na watu wengine hata kama Mungu katupa vipawa vikubwa kiasi gani, Heshima ya utumishi wako haipo katika uzuri wa sura yako ndugu mchungaji, ndugu nabii, ndugu mwalimu… heshima ya utumishi wako haipo katika mavazi unayoyabadilisha kila siku na magari na ma bodyguards, unaotembea nao na msafara au nyumba yake kama raisi. na kuwaonyesha ili watu wote wakuone..Usijidanganye ukidhani hapo ndipo umeupa heshima utumishi wako Mbele za Mungu, kama hutataka kujinyenyekeza kuna hatari mbele.

Imefikia hatua mpaka akionekana mtumishi yeyote wa Mungu anatembea kwa miguu au havai nguo zinazovutia kama watu wengine, anaonekana mlokole aliyekosa maarifa, hamjui Mungu, watu hawamsikilizi tena, Nataka nikuambie ungekuwa kipindi cha mwokozi wako wakati upo hapa duniani ungemfanyia hivyo hivyo tu. Sio kwamba na support uvaaji mbaya hapana, lakini vipo vipimo tofauti tofauti kulingana na mtu, huyu hivi Yule vile, usiutafute uzuri wa nje wa Bwana, hautaupata…kwasababu uso wake haukuwa wa umuhimu sana kwetu zaidi ya Maneno yake, ndio maana karuhusu maneno yake yahifadhiwe mpaka leo na hajaruhusu picha ya uso wake ihifadhiwe mpaka leo.

Kwahiyo ni vizuri kubadilika na kuwa kama YESU KRISTO, Tuipende kweli, tuuishi kweli na kuishika. Tukifahamu kuwa Uzima wa mtu haupo katika urembo alionao au wingi wa vitu alivyonavyo.

Na pia kama hujampa Bwana maisha yako, bado hujachelewa ni vyema ukafanya hivyo leo, saa ya wokovu ni sasa, maadamu mlango wa Neema bado haujafungwa, utafika wakati utafungwa na wengi watatamani kuingia wasiweze, hebu wewe usiwe mmoja wao, hivyo unachopaswa kufanya hapo ulipo ni kutubu kwa kudhamiria kuacha maisha yote ya nyuma ya dhambi ya uasherati, ya wizi, utukanaji, uzinzi, ulevi, uvaaji mbaya, nk na baada ya kutubu tafuta haraka sana kushiriki na wengine kanisani, ili upate kubatizwa kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako kama hujafanya hivyo..kumbuka ubatizo ni wa muhimu sana katika kukamilisha wokovu wako na ubatizo sahihi ni wa kuzamishwa mwili wote kwenye maji na kwa jina la Bwana Yesu Kristo (kulingana na Matendo 2:38) na Baada ya hapo Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu atakayekuongoza katika kuielewa biblia na kuijua kweli yote ya maandiko na atakayekusaidia kushinda dhambi, kwasababu kwa nguvu zako mwenyewe hutaweza kushinda dhambi hata kidogo.Kwahiyo Huu ndio wakati wa kukimbilia msalabani kwa Imanueli kusafishwa dhambi zako.

Ikiwa umebarikiwa na ujumbe huu.(naomba u – Share) kwa watumishi wengine na watu wengine nao wapone. Mungu akubariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba 

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Print this post

NOTI YA UFALME WA MBINGUNI

Shalom! Mtu wa Mungu karibu tujifunze Neno la Mungu, ambalo ndio Taa yetu ituongozayo uzimani.

Jinsi ufalme wa mbinguni unavyotenda kazi, kwa sehemu kubwa sana unafanana na namna ufalme wa duniani unavyotenda kazi, kwahiyo tukiulewa vizuri jinsi ufalme wa duniani unavyotenda kazi, tutauelewa pia vizuri jinsi ufalme wa mbinguni unavyofanya kazi.

Kwamfano katika ufalme wa duniani tunaona kunakuwa na wafalme, na mfalme mkuu, au kunakuwa na Raisi..Kadhalika na ufalme wa mbinguni ni hivyo hivyo, wapo wafalme na yupo mfalme wa wafalme (Yesu Kristo). Na kama vile hukumu za mwisho huwa zinapitishwa na Raisi wa hiyo nchi au Mfalme, na katika ufalme wa mbinguni ni hivyo hivyo hukumu ya Mwisho inapitishwa na Yesu Kristo aliye Mfalme wa wafalme.

Lakini pia tunaweza kujifunza katika jambo lingine linalofanyika katika ufalme wa ulimwengu huu, ambalo pia linafanyika katika ufalme wa mbinguni pasipo wengi wetu kulijua. Na jambo hilo si lingine zaidi ya UCHUMI, Yaani mzunguko wa fedha.

Kama wengi wetu tunavyojua, jamii kubwa karibia yote ya wananchi wa Taifa hili wanatafuta FEDHA, kama chombo cha kubadilishana, ili wayafikie mahitaji yao waliyotaka kwa wakati fulani, na kutimiza mipango yao, wengi wanautafuta utajiri kwa nguvu zote, ambao sio jambo baya ni jambo zuri. Na utajiri maana yake ni kuwa na fedha nyingi, kwahiyo tafsiri yake ni kwamba ni lazima mtu atafute fedha nyingi ndio awe tajiri.

Sasa FEDHA NI NINI?.. fedha ni kitu chochote ambacho kimekubaliwa na jamii husika kitumike kama chombo cha kubadilishana huduma au bidhaa,, kinaweza kuwa kuwa karatasi au safaru” na hicho kinakuwa kimepewa heshima ya kubeba THAMANI fulani, mahususi kwa ajili ya kununua kitu chenye thamani ya hiyo fedha…Hivyo Bila kuwa na fedha ni vigumu kupata huduma zile unazozihitaji.

Sasa ukichukua sarafu au NOTI labda tuseme ya shilingi elf 10 au elfu 5 , utagundua kuwa ina pande mbili, upande wa kwanza utaona ina alama fulani fulani hivi, pengine utaona picha zinazozungumzia utajiri wa nchi, au utaona kuna picha ya kiongozi wa nchi mkubwa aliyewahi kupita, au utamaduni wa nchi, na baadhi ya viishara ishara kama nembo ya taifa n.k..huo ni upande wa mbele na upande wa pili wa nyuma..utaona kuna picha za wanyama. Mambo hayo yote yanafunua kuwa fedha ina roho nyuma yake…Ukiipata katika njia sahihi itakuletea mafanikio makubwa kama inavyoonekana katika upande wa mbele, lakini pia usipoipata kwa njia halali, au ukiitumia kwa njia isiyopasa..ina roho ya unyama upande wa pili, itakuharibu badala ya kukujenga…Ndio maana unaona wengine fedha zinawashusha wengine fedha hizo hizo zinawapandisha n.k

VIvyo hivyo katika Ufalme wa mbinguni kuna UCHUMI, na pia kuna fedha..Na kila mtu ili aweze kudumu katika ufalme wa mbinguni ni lazima awe na fedha za kimbinguni, Na fedha hizo pia zipo katika mfumo wa makaratasi..NA HIZO SIO NYINGINE ZAIDI YA NENO LA MUNGU NDANI YA BIBLIA TAKATIFU. Biblia inasema Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu..(Wakolosai 3:16)..Ina maana kuwa Neno la Mungu ni kama fedha, tunapaswa tuwe nalo kwa wingi ili tuweze kujikimu na mahitaji yetu yote ya rohoni. Ukipungukiwa na Neno la Mungu basi utapungukiwa na  mahitaji yote ya kiroho, hutaweza kufanya chochote katika roho ni wazi kuwa  utashambuliwa na matatizo ya kila aina.

Biblia pia inasema katika Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.”..ikiwa na maana kuwa kama vile vile fedha inavyopatikana kwa nguvu na ufalme wa mbinguni ni hivyo hivyo..Wale wote wenye utajiri wa Neno la Mungu mioyoni mwao ndio wanaoteka baraka zote za rohoni, hawababaishwi na mapepo, wachawi, hofu, mashaka au chochote kile kwasababu wameupata utajiri mioyoni mwao.

Na kama vile tulivyojifunza kuwa fedha ina pande mbili, upande mmoja unaelezea utajiri wa nchi, nembo ya nchi, shughuli za kiuchumi za nchi, na nyuso za viongozi wakubwa waliotangulia, kadhalika pia katika NOTI za kimbinguni (yaani Neno lake)..Ina pande mbili…Upande mmoja unaelezea Uzuri wa Ufalme wa mbinguni, Mbingu mpya na nchi mpya ulivyo, na pia upande huo huo wa mbele unaonyesha nyuso za viongozi wakubwa waliotangulia..Ndio maana tukisoma Biblia tunaona maisha ya Mitume na Manabii, tunaona mashujaa wa Bwana kama wakina Paulo wakiishindania Imani waliokabidhiwa watakatifu mara moja tu! Hivyo Bwana akaruhusu maisha yao yawekwe kwenye alama ya fedha ya ufalme wa mbinguni Na utaona pia Bwana wetu YESU KRISTO KAMA MFALME WA WAFALME anatokea karibia katika kila Noti, (kila kitabu katika Biblia)..oo haleluya!! Lakini pia sehemu hiyo hiyo ya mbele utaona kunakuwa na Nembo ya nchi, inayoonyesha utamaduni na miiko ya nchi, na katika Biblia (ambayo ndio noti yetu ya kimbinguni) ndani yake tunasoma namna ya kuishi kulingana na utamaduni na utaratibu wa ufalme wa mbinguni.

Lakini pia haiishii hapo, Neno la Mungu (noti ya kimbinguni) inayo upande wa nyuma pia..Ambao huo una picha za wanyama..Kuonyesha kuwa Katika maandiko matakatifu wapo wanyama pia, na kama unavyojua tabia ya wanyama..ni kurarua na kuua, hawana akili..kadhalika katika maandiko matakatifu tunaonywa kuhusu MNYAMA ATAKAYEKUJA KUTOKA BAHARINI, kuwatia CHAPA WALE WOTE, WASIOKUWA NA MUHURI WA MUNGU (soma Ufunuo 13 & 17). Ikifunua kuwa yeyote Yule atakayeupokea ufalme wa mbinguni isivyopaswa ataangamizwa, na kuraruliwa na roho ya Yule mnyama anayetoka kuzimu..Kwahiyo ni kuwa makini sana na fedha hii ya kimbinguni. Ina UTAJIRI, na BADO INA HUKUMU.

Ufunuo 13: 1 “Kisha nikaona mnyama akitoka katika bahari, mwenye pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru.

2 Na yule mnyama niliyemwona alikuwa mfano wa chui, na miguu yake ilikuwa kama miguu ya dubu, na kinywa chake kama kinywa cha simba, yule joka akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi na uwezo mwingi.

3 Nikaona kimoja cha vichwa vyake kana kwamba kimetiwa jeraha la mauti, na pigo lake la mauti likapona. Dunia yote ikamstaajabia mnyama Yule”.

Ufunuo 17: 3 “Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi.

4 Na mwanamke yule alikuwa amevikwa nguo ya rangi ya zambarau, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake.

5 Na katika kipaji cha uso wake alikuwa na jina limeandikwa, la siri, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI.

6 Nikamwona yule mwanamke amelewa kwa damu ya watakatifu, na kwa damu ya mashahidi wa Yesu. Nami nilipomwona nikastaajabu ajabu kuu”.

Kwahiyo kwa kujifunza hayo tunaweza kuona ni jinsi gani, tunapaswa tuwe makini sana, tunapoutafuta ufalme wa mbinguni, kwamba tuutafuta kwa njia halali kama tunavyotafuta fedha, ili utupe utajiri wa rohoni, lakini tusipoutafuta kwa njia halali utatuangamiza na tutajikuta tumeangukia chini ya mikono ya Yule mnyama atokaye baharini, na huyo mnyama si mwingine zaidi ya Mpinga-Kristo, ambaye hivi karibuni atanyanyuka…naye atapewa kufanya kazi yake kuwaua wale wote watakaokataa kuipokea chapa ya mnyama. Na mnyama huyo sasa ameshaanza kufanya kazi, na anafanya kazi chini ya Kanisa la Kirumi (Kanisa Katoliki),  sasahivi yupo katika hatua za mwisho mwisho kukusanya madhebebu yote na dini zote ili kuunda Umoja wa dini zote na madhehebu yote, na itafikia wakati mtu yeyote au kanisa lolote likikataaa kuwa mshirika wa umoja huo, litafutiwa usajili, na mtu yeyote atakayekataa kuwa mshirika wa umoja huo hataweza kununua wala kuuza, na hataweza kufanya kazi maana ajira zote zitataka wahusika wawe katika ushirika huo, na yeyote atakayekubali kujiunga na ushirika huo (atakuwa tayari amepokea chapa ya mnyama)..katika usahili wa kuingizwa katika umoja huo vitatumika vitu mbali mbali, kama micro-chips kuingizwa katika mwili…mfumo wa chips utatumika sana sana kwa nchi zilizoendelea, na hizo chips sasahivi zipo tayari, zinasubiri wakati tu wa kuanza kutumika.

Kwa nchi zinazoendelea, sehemu baadhi zitatumika hizo chips lakini sehemu kubwa vitatumika vitambulisho vya kawaida tu, lakini vyenye taarifa zote za dini ya mtu husika, kila mtu atalazimishwa kwenda kuhakiki upya taarifa zake za msingi, na ndani ya kuhakiki huko watalazimishwa wataje ni madhehebu yao au dini zao ambazo zipo kwenye huo umoja..Na endapo mtu atakataa au atakuwa sio mshirika wa mojawapo wa muunganiko huo, ni wazi kuwa hatapata utambulisho huo, hivyo ataonekana ni muhalifu tu! Na hataweza kusafiri wala kwenda popote pale, kazini atafukuzwa, na kadi yake ya benki na ya simu itafungiwa kwasababu hajakamilisha usajili. Jambo hilo litakapoanza dunia yote, itafurahiwa itaonekana ni mfumo mzuri mpya, lakini wengi hawatajua kuwa ndio wanapokea chapa ya mnyama hivyo. Wakati huo unyakuo utakuwa umeshapita! Na kumbuka unyakuo utakuwa ni siri sana, sio wote watajua kuwa unyakuo umepita, hakutatokea ajali mabarabarani kama inavyosemekana, zitasikika habari chache tu za chini chini kwamba baadhi ya watu wametoweka (uvumi fulani tu)…wengi hawataamini kwasababu siku hizi yapo matukio mengi ya watu kutoweka, kwahiyo wengi watajua ni kutoweka kwa kawaida tu! Hivyo watapuuzia, na haitachukuliwa kwa uzito huo.

Baada ya huyo mnyama kumaliza kazi yake ya kuwatia chapa yake wale wote walioachwa kwenye unyakuo, ataanza kuwaua wale waliokataa kusajiliwa kwenye mfumo wake, atatumia nguvu ya serikali, atahimiza serikali zote ziwatoe hao waliokataa kupokea mfumo wao na watu wengi wataonyesha ushirikiano kumpa support huyo mnyama..ndugu atamsaliti ndugu yake ili auawe..kutakuwa hakuna kujificha siku hiyo, baba utaona anamkana wazi wazi mwanae, na kusema huyu mwanangu alikataa kwenda kuhakiki taarifa zake, ana kiburi mkamateni, watakamatwa watu wengi na kupelekwa magerezani na hatimaye kwenye kambi za mateso, sasa hao ndio watasingiziwa kuwa ndio chanzo cha matatizo yote yanayotokea kwenye jamii na duniani, hata kama kulikuwa na mtu ameiba mtaa wa pili, lawama zote watatupiwa hao, wataachwa huru wale wauaji na magaidi, watawageukiwa wao, kama vile tu Yesu, alivyofunguliwa Baraba muuaji akasulibiwa yeye. watateswa mateso yasiyokuwa ya kawaida kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu..Ni matezo ambayo hajawahi wala hayataka yatokee.

Ndugu yangu, sio kipindi kizuri hicho kikukute, mimi sitaki kinikute na wewe nakuambia sasa ili nawe kisikukute, kipo karibuni sana kutokea…leo hii itii injili ya Yesu Kristo, Utafute ufalme wa mbinguni kwa bidii zote kama unavyotafuta fedha, maana mwenye nguvu ndio wanaoupata..Anza kujikusanyia utajiri wa kimbinguni kwa kujifunza na kulitii neno lake ambalo ndio Noti yetu. Ndipo utakaposalimika katika dunia hii..

Mithali 2: 1 “Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu, Na kuyaweka akiba maagizo yangu;

2 Hata ukatega sikio lako kusikia hekima, Ukauelekeza moyo wako upate kufahamu;

3 Naam, ukiita busara, Na kupaza sauti yako upate ufahamu;

4 Ukiutafuta kama fedha, Na kuutafutia kama hazina iliyositirika;

5 Ndipo utakapofahamu kumcha Bwana, Na kupata kumjua Mungu.

6 Kwa kuwa Bwana huwapa watu hekima; Kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu;”

Usisahau, noti ina pande mbili, na biblia imetupa NJIA mbili za kuchagua kufuata..NJIA YA UZIMA na NJIA YA MAUTI. (Yeremia 21: 8 Nawe waambie watu hawa, Bwana asema hivi, Tazama naweka mbele yenu njia ya uzima, na njia ya mauti).

Ni maombi yangu kuwa utachagua njia ya uzima, kama hujampa Bwana Yesu Kristo maisha yako, ndio wakati wakufanya hivyo sasa, usisubiri leo ipite, kwasababu hujui lisaa limoja mbele nini kitatokea, hapo ulipo mwambie Bwana akusamehe makosa yako yote, na mwambie hutaki tena kuishi maisha ya dhambi, na baada ya kuomba sala hiyo, dhamiria ndani ya moyo wako kuacha dhambi kweli kweli, dhamiria kuacha pombe, sigara, rushwa, uasherati, uvaaji mbaya wa vimini na suruali na mapambo ya kidunia hii, dhamiria kuacha kampani mbovu, na mambo mengine yote yasiyofaa..Ukimaanisha kutoka moyoni mwako kuacha hayo mambo, nguvu ya ajabu itashuka juu yako kukusaidia kuyashinda hayo mambo yasikurudie tena…na ukishamaliza hiyo hatua nenda mahali popote wanapoamini ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, ubatizwe hapo, na Bwana mwenyewe atakusaidia kufanya yaliyosalia..

Bwana akubariki sana, tafadhali pia “share” kwa wengine nao waokoke.

Pia kwa Maombezi, Ushauri au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi  kwa namba hizi:
+225693036618/
+225789001312
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Zinazoendana:

EPUKA MUHURI WA SHETANI

ALAMA KATIKA VIPAJI VYA NYUSO.

CHAPA YA MNYAMA

TUNAPOSEMA TUISHI KWA NENO, INAMAANISHA TUISHI MAISHA YA NAMNA GANI?


Rudi Nyumbani

Print this post

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?

Shalom Mwana wa Mungu, karibu tuyatafakari maandiko na kujifunza.

Leo kwa Neema za Bwana tutajifunza, ni kwanini Mungu aruhusu katika agano la kale wana wa Israeli waoe mke zaidi ya mmoja. Huu umekuwa ni mjadala mkubwa sana, usio na mwisho miongoni mwa wakristo wengi wasio na ufunuo kamili wa Roho Mtakatifu kuhusu maandiko hayo.

Kwanza kabisa ni muhimu kufahamu kuwa Mungu hajawahi kumwagiza mtu yoyote mahali popote aoe mke zaidi ya mmoja. Hakuna mahali popote Mungu alishawahi kumpa Mwanadamu hayo maagizo…utaniuliza mbona kwenye kumbu 21:15 na kumbu 25:5  inazungumzia habari ya mtu kuwa na mke zaidi ya mmoja?. Ni kweli habari hizo zinazungumzia kuhusu kuwa na mke zaidi ya mmoja, lakini hiyo bado haimfanyi Mungu kuhalalisha mke zaidi ya mmoja..Nitakuthibitishia hilo leo kwa maandiko.

kulielewa vizuri hili suala, hebu tusome maandiko yafuatayo na kisha tuyatafakari..

Kumbukumbu 17: 14 “Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako ukaimiliki, na kukaa humo; nawe utakaposema, Nitaweka mfalme juu yangu mfano wa mataifa yote yaliyo kando-kando yangu;

15 usiache kumweka yule atakayechaguliwa na Bwana, Mungu wako, awe mfalme juu yako; umweke mmoja katika ndugu zako awe mfalme juu yako; usimtawaze mgeni juu yako, ambaye si ndugu yako.

16 Ila asifanye farasi wake kuwa wengi, wala asiwarudishe watu Misri, ili apate kufanya farasi kuwa wengi; kwa kuwa Bwana amewaambia, Tangu sasa msirudie tena njia ile.

17 Wala asijizidishie wake, ili moyo wake usikengeuke; wala asifanye fedha zake na dhahabu kuwa nyingi mno.

18 Tena na iwe, zamani aketipo juu ya kiti cha ufalme wake, ajiandikie nakala ya torati hii katika chuo, kufuata hicho kilicho mbele ya makuhani Walawi;

19 na awe nayo, asome humo siku zote atakazoishi; ili apate kujifunza kumcha Bwana, Mungu wake, ayashike maneno yote ya torati hii na amri hizi, kwa kuyafanya;

20 moyo wake usije ukainuliwa juu ya ndugu zake, wala asikengeuke katika maagizo, kwa mkono wa kuume wala wa kushoto; ili apate kuzifanya siku zake kuwa nyingi katika ufalme wake, yeye na wanawe, katikati ya Israeli”.

Sasa ukisoma mistari hiyo kwa makini, utaona kuwa Bwana anawapa maagizo wana wa Israeli jinsi mfalme wao anavyopaswa awe siku watakapokuja kumchagua…utaona Mungu anawaambia, mfalme huyo anapaswa asiwe mtu wa kujiongezea mali nyingi wala asiwe wa kujiongezea wake..

Sasa kwa maagizo hayo haimaanishi kuwa Mungu, tayari ndio kawapa amri ya wao kuja kuwa na Mfalme, haikuwa mpango wa Mungu kabisa wana wa Israeli waje kuwa na Mfalme, kwani mfalme wao ni mmoja tu yaani YEHOVA, lakini kwasababu Mungu aliona Mbele kwamba watakuja kukengeuka na kutaka kuwa na mfalme kama mataifa mengine walivyokuwa nao ndio hapo akamwambia Musa awape maagizo ya mfalme atakavyopaswa kuja kuwa..Kwahiyo kile kitendo chao cha kuwa na tamaa ya kutaka mfalme ilikuwa ni dhambi kubwa sana, na Mungu hakupendezwa nacho. Tunasoma hayo katika…

1 Samweli 8: 4 “Ndipo wazee wote wa Israeli wakakutana pamoja, wakamwendea Samweli huko Rama;

5 wakamwambia, Angalia, wewe umekuwa mzee, na wanao hawaendi katika njia zako; BASI, TUFANYIE MFALME ATUAMUE, MFANO WA MATAIFA YOTE.

6 Lakini neno hilo likawa baya machoni pa Samweli, waliposema, Tupe mfalme atuamue. Naye Samweli akamwomba Bwana.

7 Bwana akamwambia Samweli, Isikilize sauti ya watu hawa katika kila neno watakalokuambia; KWA MAANA HAWAKUKUKATAA WEWE, BALI WAMENIKATAA MIMI, ILI NISIWE MFALME JUU YAO.

8 Kwa kadiri ya matendo yote waliyonitenda tokea siku ile nilipowatoa katika Misri hata leo, kwa kuniacha mimi, na kwa kutumikia miungu mingine, ndivyo wanavyokutenda wewe”.

Umeona hapo kitu Mungu anachomwambia Nabii samweli?…

“hawakukukataa wewe bali wamenikataa mimi nisiwe mfalme juu yao”….Sasa ingekuwa Mungu amehalalisha wana wa Israeli kuwa na Mfalme kule  nyuma kwenye Kumbukumbu la Torati 17 …asingekasirika hapa kuona wana wa Israeli wanataka mfalme…asingelaumu, lakini badala yake unaona Mungu anachukizwa sana na kitendo hicho cha wana wa Israeli kutaka mfalme.

Umeona? Kwahiyo ni wazi kuwa kule kwenye kumbukumbu 17, Mungu alipotoa maagizo ya namna mfalme atakavyopaswa kuwa sio kwamba ndio alitoa ruhusa wana wa Israeli wawe na mfalme, badala yake ni maagizo yatakayotumika baada ya wao kukengeuka akili na kutaka mfalme..(Kwasababu ya mioyo yao kuwa migumu)

Kadhalika na katika suala la ndoa. Mungu alitoa maagizo katika agano la kale namna watakavyoishi endapo watajiongezea wake…lakini sio kwamba alitoa amri ya watu kuoa mke zaidi ya mmoja! Au kutoa talaka…Mungu hakuwahi kumwagiza mtu kufanya hivyo vitu, wala kumpa hayo maagizo…alizungumzia namna ya kuishi na mke zaidi ya mmoja ndio, na maagizo ya talaka kwasababu aliona tayari wana wa Israeli walishakengeuka na watazidi kuja kukengeuka na kuweka mioyo yao migumu na kuwa na shingo ngumu, kwa kutaka kila mtu kuwa na mke zaidi ya mmoja, na kila mtu kutaka kumwacha mkewe….na kwasababu walishamkataa Mungu katika fahamu Mungu naye akawaacha wafuate akili zao…Kama vile tu walivyomkataa Mungu asiwatawale na kujichagulia mfalme wao wenyewe, Mungu aliwaacha katika akili zao hizo. Lakini haukuwa mpango kamili wa Mungu tangu awali.

ndio maana Bwana Yesu alikuja kusema mambo hayo hayakuwa hivyo tangu mwanzo.…

Mathayo 19: 3 “Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa kila sababu?

4 Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,

5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?

6 Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.

7 Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?

8 Akawaambia, Musa, KWA SABABU YA UGUMU WA MIOYO YENU, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi”.

Kwahiyo kwa maandiko hayo yanatufundisha kuwa mke ni mmoja tu na mume ni mmoja tu! Na hairuhusiwi kumwacha mwanamke, kwasababu yoyote ile isipokuwa ya uasherati tu!..Mtu anayeoa wake wengi na bado anajiita ni mkristo, azini, asitumie kisingizio cha kuwa agano la kale liliruhusu, YESU ni mkuu kuliko nabii yoyote maandiko yanasema kuwa “katika yeye utimilifu wote wa Mungu unakaa kwa jinsi ya kimwili (Wakolosai 2:9)”.

2 Timotheo 2:15 “Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli.”

Bwana akubariki sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine..

Pia kwa Maombezi, Ushauri au Ratiba za Ibada Wasiliana  nasi kwa namba hizi…..

+225693036618

+225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana

UNALITUMIA KWA HALALI NENO LA KWELI?.

NDOA NA TALAKA

BIBLIA INASEMA ASKOFU ANAPASWA AWE MUME WA MKE MMOJA! JE! WALE WASIOOA KWA AJILI YA INJILI HAWAWEZI KUWA MAASKOFU?

NDOA NA HARUSI TAKATIFU.

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.


Rudi Nyumbani

Print this post

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

Isaya 55:1-2 “ Haya, kila aonaye kiu, njoni majini, Naye asiye na fedha; njoni, nunueni mle; Naam, njoni, nunueni divai na maziwa, Bila fedha na bila thamani.

2 Kwani kutoa fedha kwa ajili ya kitu ambacho si chakula? Na mapato yenu kwa kitu kisichoshibisha? Nisikilizeni kwa bidii, mle kilicho chema, Na kujifurahisha nafsi zenu kwa unono.”

Jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, Nakukaribisha katika kuyachunguze maandiko nilipokuwa ninautafakari huu mstari, picha iliyojitengeneza moja kwa moja katika kichwani kwangu ni sawa mtu mwenye Hoteli maarufu ya 5 STAR Dubai, ambayo kifungua kinywa chake tu asubuhi gharama zake ni sh laki 3, mbali na gharama za chakula cha mchana na jioni, na zile za kulala..halafu leo hii unamwona anajitokeza hadharani anawakaribisha watu wote waje kula na kunywa katika hoteli ile bure, pasipo gharama yoyote…

Na cha kushangaza zaidi anatoa kauli hii “njoo UNUNUE bure”, hakwambii njoo nikupe bure, hapana bali anasema njoo “UNUNUE” bure, hii ikiwa na maana,utakapofika pale utaandikiwa risiti ya ununuzi kama tu vile mtu aliyelipia gharama zote, na hiyo inakupa uhalali wa kuhudumiwa kwa viwango vile vile bila upendeleo sawa tu na mtu Yule ambaye ametoa pesa yote mfukoni.

Lakini utashangaa sana siku ile usipoona watu wengi katika hoteli hiyo maarufu, maswali mengi yanaweza yakaja kichwani mwako sindio?, pengine utasema hawa wameona kama wamedharauliwa au?, au wameshushwa hadhi?, au wanaogopa kwenda kutokana na hadhi ya hoteli ile au? Au wameona kama wanaingizwa mjini au ni nini?..Ni wazi kabisa utajiuliza kwa offer kubwa kama hiyo ni kwanini pakose watu?.

Isaya 55:1-2 “ Haya, kila aonaye kiu, njoni majini, Naye asiye na fedha; njoni, nunueni mle; Naam, njoni, nunueni divai na maziwa, Bila fedha na bila thamani.

Ndugu ndivyo Mungu anavyotufanyia sisi wanadamu, anatuita tuje tule, tunywe tujishibishe nafsi zetu kwa vinono kwake, bila gharama yoyote, lakini sisi tunapoona tunapewa vyote hivi kwa bei ya bure, tunaona kama havina thamani kubwa kwetu, na hiyo inatupelekea kuudharau wokovu na kwenda kutafuta vitu ambavyo vitatugharimu maisha yetu na mwisho wa siku visituletee faida yoyote katika roho zetu.

Nataka nikuambie, siku zote kitu kikiwa na thamani kubwa sana isiyoweza kufikiwa na wengi mara nyingi huwa kinageuka na kuwa bure, hiyo ni fact kwasababu kitakosa mnunuzi, hivyo thamani yake inarudi tena katika sifuri, na ndio maana ukitazama hata taifa linalodaiwa matrilioni ya pesa na mataifa tajiri, utaona mfano likishindwa kulipa, wale watu wanaandikiwa msamaha, sio kana kwamba hawaithamini au hawaihitaji ile pesa hapana, bali, wanaona huyu mtu hata atoe vitu vyake vyote hawezi kulipa deni hili hivyo ya nini kumdai!..Ni sawa na kupoteza muda tu! Lakini angalia wale wa madeni ya kati na madogo madogo, hao ndio wanaokuwa wa kwanza kusumbua, na usipowalipa kwa wakati watakupeleka mpaka kwenye mahakama za kimataifa, na utapigwa faini juu.

Na ndivyo ilivyo kwa Mungu wetu, siku zote vitu vyake vyote anavitoa bure kwasababu vina thamani kubwa sana, pumzi unayoivuta ingekuwa tunalipia tu hata kwa senti moja kila dakika ungekuwa unadaiwa sh. Ngapi mpaka sasa?,..babu wa babu yako angekurithisha madeni yake, maji ya mvua yanayolinyesha shamba lako pamoja na kuijaza na mito yote ya maji na chemchemi ungekuwa unalipia leo hii ungeotoa sh. Ngapi?,

Nishati inayotoka kwenye jua, ambayo kwa dakika 1 inayo uwezo wa kulihudumia taifa la Marekani tu kwa miaka milioni moja,uchunguzi unasema hivyo,sasa mfano tungekuwa tunapewa kwa gharama kama vile tunalipia luku tungelipa sh.ngapi?

Lakini hayo yote bado si kitu zaidi ya WOKOVU, ambao huo kama tukisema ni kuulipia basi tujue pesa zake ni sawa na hakuna mwisho…Mungu alimtuma mwanawe wa pekee ili kuuandaa wokovu huu na kuunda kwa muda wa miaka 33 na nusu, kila siku usiku na mchana alikuwa anauunda, katika vipindi vigumu na vya majaribu mazito tangu siku ya kwanza, alikuwa anatutengeneza sisi chakula hichi kizuri cha roho kwa kupitia mwanawe mpendwa YESU KRISTO, mpaka alipofikia karibu na kumaliza shughuli hii, Mungu mwenyewe akaingia gharama ya kumngongelea “hati ya dhambi zetu, pale msalabani”. Ili DENI lile kubwa sana lifutwe..ilichukua maisha ya mtu mtakatifu sana asiyetenda dhambi kulifuta Deni hili. Ili tu sasa kila mmoja awe na uwezo wa kuununua wokovu huo kwa bei ya bure.

Na ndio maana Bwana Yesu pale msalabani alimalizia na kauli hii..

IMEKWISHA!!.

Ile hati ya deni la dhambi imekwisha. Na leo anasema tena Haya,

“kila aonaye kiu, njoni majini, Naye asiye na fedha; njoni, nunueni mle; Naam, njoni, nunueni divai na maziwa, Bila fedha na bila thamani.

2 Kwani kutoa fedha kwa ajili ya kitu ambacho si chakula? Na mapato yenu kwa kitu kisichoshibisha? Nisikilizeni kwa bidii, MLE KILICHO CHEMA, NA KUJIFURAHISHA NAFSI ZENU KWA UNONO.”

Ununue wokovu huu kwa bei ya bure ndugu, wakati ndio huu, sauti inayokulilia kila siku utubu, haitadumu milele hiyo, mzigo wa dhambi ulionao, siku ile hutaweza kuulipia, unajua kabisa ukifa leo ni moja kwa moja jehanum kwa dhambi zako, siku hiyo utaulizwa kule ni nini shida? Hutakuwa na cha kujitetea, wote watakushangaa wokovu ulipatikana kwa bei ya bure, imekuwaje wewe haukuwa nao??. Isitoshe hizi ni siku za mwisho dalili zote zinaonyesha hatujui kama tunaweza kuwa na vizazi vingine mbele yetu,..Huu ni wakati wa kutafuta mambo ya wokovu wa roho yako sana kuliko mambo mengine yasiyotuahidia uzima wa milele.. Weka Msalaba mbele, dunia nyuma. Imani mbele mali nyuma, Itakufaidia nini upate fedha zote na nafsi yako iangamie?.

Ufunuo 22:17 “Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”.

Tafadhali “Share” Ujumbe huu kwa wengine. Na Bwana atakubariki.

Ikiwa utapenda kumpa Yesu Maisha yako, au kupata ubatizo sahihi, basi tupigie kwa namba zetu hizi +255789001312/ +255693036618. Na pia kama utapenda masomo haya yawe yanakufikia kila siku kwa njia ya Whatsapp. Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

NAYE ALIKUWA HANA BUDI KUPITA KATIKATI YA SAMARIA.

LAKINI SISI HATUKUIPOKEA ROHO YA DUNIA.

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

MAJI YA UZIMA.

“WOKOVU WETU U KARIBU NASI KULIKO TULIPOANZA KUAMINI”

TUSIPOUTHAMINI WOKOVU TUTAPATAJE KUPONA?


Rudi Nyumbani

Print this post

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Shalom!..Karibu tujifunze Maneno ya Mungu ya uzima, leo tunajifunza kwa uchache juu ya vitabu vya Biblia, jinsi vilivyoandikwa na maudhui yake, kwa neema za Mungu.

Zamani mwanzoni wakati nampa Bwana maisha yangu, nilikuwa siielewi biblia vizuri, vitabu nilivyokuwa navielewa vilikuwa ni vile vya injili tu! Yaani Mathayo,Marko, Luka na Yohana…na katika agano la kale kitabu cha Mwanzo kidogo na Kutoka ndio nilikuwa nikivisoma navielewa, na cha Esta pamoja na Ruthu…kwasababu mtiririko wa hadithi zake umejipangilia vizuri… Lakini vitabu vingine kama Zaburi, Mithali,Ezekieli, Yeremia, Isaya, Danieli, Habakuki, Malaki n.k nilikuwa sivielewi kabisa.. Kwasababu nilikuwa sijui viliandikwa kwa sababu gani..Na mwandishi alikuwa anaviandika katika mazingira gani na kwa malengo gani…kwaufupi vilikuwa vinanichanganya sana.

Kwahiyo niliishia kuhisi tu kuwa kitabu kama cha Isaya, kiliandikwa na Nabii Isaya pengine ndani ya siku moja au mbili, au ndani ya wiki moja, nilikuwa nadhani alikuwa anajifungia ndani na kisha maneno ya Mungu yanamshukia na anayaandika kwenye kitabu aya baada ya aya, hivyo pengine ilimchukua muda kama wa wiki moja hivi kumaliza kuandika sura zote 66…Na vitabu vingine nilijua ndio hivyo hivyo. Lakini kumbe ulikuwa ni uchanga tu wa kiroho.

Hakuna kitabu kizuri na kilichopangiliwa vizuri kama BibliaTakatifu, ni kitabu pekee kilichoandikwa kwa utaratibu mzuri na mpangilio endapo ukikielewa. Leo kwa ufupi tutaanza kujifunza mpangilio huu jinsi ulivyokaa na tutaanza na vitabu vichache..

1) Kitabu cha MWANZO:

Kitabu cha Mwanzo kiliandikwa na Nabii Musa, wakati akiwa jangwani baada ya kuwatoa tu wana wa Israeli Misri, Bwana alimpa ufunuo wa kilichotokea Edeni na hata kabla ya Edeni.

Alimpa ufunuo pia wa jinsi dunia ilivyoumbwa katika siku zile 6, na akaambiwa aandike vile ilivyoandikwa, kumbuka Musa ndiye Nabii pekee aliyekuwa anazungumza na Mungu uso kwa uso.

Lakini pia kitabu cha Mwanzo hakijabeba tu historia ya Adamu na Hawa, Bali pia kimebeba historia ya dunia kuangamizwa kwa gharika, habari za Nuhu na safina, habari hizo pia ziliandikwa na Nabii Musa, ingawa kabla ya Musa pia habari hizo zilikuwa zinafahamika na baadhi ya watu, pia historia ya Wana wa Israeli, kuanzia Ibrahimu mpaka Yusufu na mpaka walipoingia Misri wapo watu wachache walikuwa na rekodi ya chimbuko lako. Kwahiyo Musa wakati yupo jangwani na wana wa Israeli aliagizwa na Mungu aandike mambo hayo, na akayaandika kwenye kitabu na hicho kitabu ndio kinaitwa mwanzo.

 

2) Kitabu kinachofuata ni kitabu cha KUTOKA

Nacho kiliandikwa na huyo huyo Musa, akiwa jangwani pamoja na wana wa Israeli…Kilikuwa ni kitabu kirahisi kwasababu hakikuhitaji ufunuo wowote wa Roho kukiandika, ilikuwa ni kuandika tu mambo waliyokuwa wanayapitia siku baada ya siku,na waliyokuwa wanayaona..tangu Musa alipotumwa na Mungu kwenda kwa Farao, mpaka mapigo Farao aliyopigwa, mpaka kuvushwa bahari ya Shamu, mpaka walivyolishwa mana jangwani, mpaka wakati wa kukabidhiwa amri kumi na kupewa maagizo ya kutengeneza Maskani ya Bwana,…Kwahiyo hakikuwa kitabu kigumu kuandika kwasababu ni maisha waliyokuwa wanayaishi, na mambo waliyokuwa wanayaona..kulikuwa hakuna haja ya mtu kuwaadithia au kungojea ufunuo kutoka kwa Mungu ya jinsi ya maneno ya kuandika kama ilivyo kwenye kitabu cha UFUNUO.

3) Kitabu kinachofuata ni MAMBO YA WALAWI.

 Kitabu hichi kiliandikwa na huyo huyo Musa wakati wana wa Israeli bado wapo jangwani katika safari yao ya kuelekea Kaanani. Baada ya Mungu kuwapa sheria alimwagiza Musa awatenge wana wote wa Lawi, ambalo ndio kabila lake Musa, alifanye kuwa kabila la kikuhani..Na hivyo kama limeteuliwa kuwa kabila la ukuhani, hivyo ni lazima kutakuwepo na majukumu machache machache yanayowahusu hao makuhani walawi (yaani Kabila la Musa).

Kwahiyo Mungu akamwagiza Musa aandike kitabu kitakachowahusu hao walawi na majukumu yao katika utumishi wa kikuhani. Kama ukisoma kitabu cha mambo ya walawi utaona kulikuwa na majukumu mengi sana, ambayo yaliwahusu maana hao ndio waliochaguliwa na Mungu kuwa kama wawakilishi wake duniani, wajukumu yote ya namna ya kuwahudumia wana wa Israeli kuhusu masuala ya kiibada waliyabeba wao,

Kwahiyo ilipasa kiwepo kitabu pekee cha namna ya kuendesha ibada ndani ya hema ya kukutania, ndio maana utaona ndani ya kitabu hicho kimejaa maagizo kwa wana wa Lawi ya namna ya kumtolea Mungu sadaka, utaona wana wa HARUNI (Ambao ndio wana wa Lawi) wanaagizwa nini cha kuvaa wakati wakitumika kwenye hema, namna ya kuiandaa sadaka pindi inapoletwa na wahusika namna ya kuikata kata na kuiweka juu ya madhabahu, na wanafundishwa pia jinsi ya kutumika madhabahuni utaratibu na zamu,wanafundishwa namna ya kuvukiza uvumba, wanafundishwa jinsi ya kufanya upatanisho kwa dhambi za wana wa Israeli, wanafundishwa pia namna ya kumfanyia mtu utakaso pindi anapokuwa najisi, au anapotenda dhambi, wanafundishwa pia sheria za kuwafundisha watu na hukumu zake, ikiwa imetokea mtu amefanya kosa atendewe nini n.k

Kwahiyo kwa ufupi ni kitabu kinachohusu MAJUKUMU YA WANA WA LAWI ndio maana kinaitwa MAMBO YA WALAWI..Musa pamoja na Haruni ndugu yake walikuwa WALAWI. Kwahiyo kabila lao liliteuliwa na Mungu kuwa Kabila la KIKUHANI. Walikuwa hawana jukumu linguine zaidi ya hilo. Kitabu hichi pia kimeelezea maagizo na aina za sadaka wana wa Israeli wanazopaswa kumtolea Mungu..Na jinsi wanavyopaswa wazipeleke kwa makuhani WALAWI.

4) Kitabu  cha Nne ni kitabu cha HESABU:

Kitabu cha Hesabu kiliandikwa na Nabii Musa huyo huyo, wakati bado wakiwa katika safari yao jangwani. Kipindi wana wa Israeli wanatoka Misri walitoka kama jeshi la mtu mmoja..walikuwa ni wadhaifu kwa hiyo Mungu aliwapigania dhidi ya maadui zao kwa asilimia zote, hawakutumia hata upanga wao au visu vyao kushindania wokovu wao…

Ulikuwa ni mkono wa Mungu mwanzo mwisho, hawakunyanyua hata kisu kushindana na maadui zao, utaona Farao adhabu alizokuwa anapata ni Mungu mwenyewe ndio aliyekuwa anahusika mwanzo mwisho, hakuna hata jiwe la mwisraeli mmoja lililohusika, mpaka wanatoka Misri ndio ilikuwa hivyo..Lakini mbeleni utakuja kuona wana wa Israeli wanabadilika tabia, wanaanza kuukataa uongozi wa Mungu na kutaka kujiongoza wenyewe…Na ni kawaida Mungu anapowaonya watu na wanapokataa maonyo huwa anawaacha na kuwapa haja ya mioyo yao kama wanavyotaka..

Utaona walitaka kula nyama, wakati ambao haukuwa wakati wa kula nyama, lakini kwasababu walililia Mungu aliwapa nyama kama wanavyotaka, kadhalika utaona hata walipoingia nchi ya ahadi walijitakia Mfalme, jambo ambalo halikuwa mapenzi ya Mungu wao wawe na mfalme wa kibinadamu, lakini utaona Mungu aliwapa Mfalme kama walivyotaka.

Na kadhalika wakati wakiwa jangwani, baada ya kupewa zile amri 10 na Mungu..mioyoni mwao walikuwa tayari wameshaanza kuukataa uongozi na wokovu wa Mungu, wakaanza kutamani kupambana wao na maadui zao, jambo ambalo halikuwa ni mapenzi ya Mungu wana wa Israeli washike upanga kuuwa maadui zao, lakini kwasababu tayari mioyo yao ilishakuwa migumu, Bwana akawaacha watumie silaha zao kwa wokovu wao…

Lakini hakuwaacha kabisa, akaendelea kuwa nao hata kwa njia hiyo..lakini haikuwa mpango kamili wa Mungu, wokovu upatikane kwa njia ya upanga…Kusudi la Mungu ilikuwa ni kuwapa hiyo nchi ya Ahadi kwa mkono wake mkuu na matendo yake makuu kama alivyofanya kwa wa Misri, kusudi lake lilikuwa ni kuwatoa wakaanani kwa matendo ya kimiujiza pengine kama kwa mapigo yale ya Misri, pasipo hata wana wa Israeli kutumia upanga, Lakini wana wa Israeli waliuharibu mpango kutaka kujipigania..

Kwasababu hiyo basi, Mungu aliruhusu wana wa Israeli, wapange majeshi… WAHESABIWA KULINGANA NA IDADI YAO, wahesabiwe wanaume tu walio na miaka 20 na zaidi, WALIO NA UWEZO WA KWENDA VITANI, waandikwe majina yao na makabila yao, kwasababu ya vita wanavyokwenda kukutana navyo mbeleni. Ndio maana ukisoma pale mwanzo wa kitabu cha HESABU utaona:

Hesabu 1: 1 “Bwana akanena na Musa katika bara ya Sinai, hemani mwa kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya kutoka kwao nchi ya Misri, akamwambia,

2 Fanyeni HESABU ya mkutano wote wa wana wa Israeli, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina ilivyo, kila mtu mume kichwa kwa kichwa;

3 tangu mwenye miaka ishirini umri wake, na zaidi, WOTE WAWEZAO KUTOKA KWENENDA VITANI KATIKA ISRAELI; wewe na Haruni mtawahesabu kwa kuandama majeshi yao”.

Kwahiyo hiyo ndio sababu ya kuandikwa kitabu cha HESABU, Ni Kitabu cha orodha ya mashujaa watakaosimama vitani kulipigania Taifa la Israeli, na kuliingiza katika nchi ya Ahadi, kuanzia huo wakati Mungu akaanza kuwaokoa na kuwapigania wana wa Israeli kwa kutumia majeshi yao wenyewe, huo ndio ulikuwa mwanzo wa wana wa Israeli kupigana vita…wokovu ukawa unapatikana kwa upanga!..Ndio mashujaa kama wakina Yoshua wakatokea huko, kwa kutiwa nguvu za kiMungu ndani yao kama simba, waliyaangusha mataifa saba makubwa ya Kaanani kwa Upanga…

Kwahiyo kama ukikisoma kitabu hichi vizuri utaona mwanzo wa majeshi ya Israeli kwa Idadi yao na makabila yao, utaona jinsi yalivyojipanga kuizunguka hema, wakati wametulia na wakati wanasafiri..Na pamoja na hayo kitabu hichi pia ni ufupisho wa hatua moja moja waliyopitia wana wa Israeli tangu walipotoka Misri mpaka walipoikaribia Kaanani. Na pia Hesabu hiyo hiyo ya majeshi ya Israeli ndio iliyokuja kutumika katika kuigawa hiyo nchi ya Kaanani waliyokuwa wanaiendea, kwamba Kabila lenye watu wengi ndio waliopewa urithi mkubwa zaidi ya kabila lenye watu wachache.

Bwana akubariki sana…

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Kwa mwendelezo >>> VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

Na pia kama utapenda masomo haya yawe yanakufikia kila siku kwa njia ya Whatsapp basi bofya  link hii kujiunga moja kwa moja >>> JIUNGE- WHATSAPP Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.

SANDUKU LA AGANO LILIKUWA LINAWAKILISHA NINI KATIKA AGANO JIPYA?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

NUHU WA SASA.

MNARA WA BABELI

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “HERI WALIOTASA, NA MATUMBO YASIYOZAA, NA MAZIWA YASIYONYONYESHA”?


Rudi Nyumbani:

Print this post

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?

Kama umechunguza utagundua kuwa Wanajeshi vitani sikuzote huwa hawakimbii tu ovyo ovyo kila mahali na kuanza kurusha mabomu na silaha kwa maadui zao kama wanavyojisikia tu hapana, mambo hayawi hivyo vinginevyo wanaweza wakajikuta wao ndio wanakuwa shabaha ya maadui zao, bali huwa wanatulia kwanza na kutafuta mahali pazuri ambapo maadui zao hawatawaona na pia mahali ambapo patakuwa ni rahisi kwao, hapo watapiga maadui zao vizuri na kwa upesi, hata simba porini huwa halikimbilii tu bila malengo kundi la nyumbu analoliona mbele yake na kwenda kumrukia yoyote tu ampendaye hapana, vinginevyo hataambulia chochote lakini kinyume chake utamwona anatulia katika eneo zuri la utulivu na la maficho ambalo litamsaidia kuchora mpango wake kichwani na pia litakalompa wigo wa kuchomoka kwa kasi na haraka kumrukia mnyama kabla hata hajaanza kuongeza kasi ya kukimbia..

Na ndivyo ilivyo hata kwa shetani, si kila eneo atakujaribu tu mwaminio, Mtume Paulo aliwaandikia wakorintho maneno haya 2Wakorintho 2:11 ‘Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake…’

Hii ikiwa na maana kuwa kama tukikosa kuzifahamu fikira zake, basi itakuwa ni ngumu sana sisi kumshinda yeye. Hivyo leo tutazama baadhi ya vipengele vikuu muhimu ambavyo shetani anapenda sana kuvitumia kumshambulia mkristo. Kwa kuyatazama maisha ya Bwana wetu Yesu Kristo tunaweza kuvibainisha vipengele hivyo vikuu.

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?

1) Wakati unaingia katika maisha mapya ya rohoni:

Hii ipo wazi kabisa wakati tu Bwana Yesu anakuja duniani pale pale shetani alinyanyua vita vikubwa kutaka kumwangamiza mtoto Yesu kwasababu alijua akimwacha baadaye atakuja kuleta madhara makubwa sana katika ufalme wake, kwasababu aliiona nyota yake, na aliufahamu unabii wa kuja kwake, hivyo jambo analohakikisha ni kumwondoa Yule mtu tangu akiwa mchanga..Na mambo kama hayo hayo yatajirudia kwa mtu yeyote atayeingia katika wokovu leo. Hivyo usishtuke kuona mambo yanakubalikia, usishtuke kuona ndugu wanakugeuka au kukuchukia wakati mwingine, usishtuke kupitia majanga kwasababu ya imani yako.. hilo lisikusababishe kuwachukia ndugu zako au jamii, wala kuwalaani fahamu kuwa ni shetani ndiye anayeyasababisha hayo yote kutaka kukuzuia usiupende wokovu. Unachopaswa tu kufanya ni kudumu katika imani kwasababu Bwana atakuwa pamoja na wewe kukulinda na kila aina na madhara atakayojaribu kukuleta kama alivyomlinda mtoto YESU kipindi kile anazaliwa. Kadhalika pia tunaweza kujifunza katika Wanyama wawindao, Watoto wadogo wa Wanyama ndio wanaowindwa sana kuliko Wanyama waliokomaa…utaona mtoto wa tembo au mtoto wa twiga ni rahisi kuwa chaguo la Wanyama kama fisi au chui kuliko twiga mzima au tembo mzima…

2) Wakati ukiwa peke yako:

Sehemu nyingine unayopaswa uwe makini nayo sana ni pale unapokuwa peke yako. Mtu aliye peke yake siku zote nguvu yake inakuwa ni ndogo kuliko anapokuwa na wenzake, hiyo ipo wazi.Hivyo shetani akishagundua kuwa kuna wakati upo peke yako, hapo ndipo anaanza tena kuamsha majaribu yake. Bwana Yesu alipojitenga peka yake kule jangwani siku 40, tunaona shetani ndipo alipomtokea na kumjaribu. Tunaweza kumwona tena Daudi alipokuwa peke yake nyumbani ndipo shetani alipomjaribu na kufanikiwa kumdondosha katika dhambi ya uzinzi. Hivyo chukua tahadhari mara mbili, na ndio maana biblia inatuonya na kutushauri kila wakati katika Muhubiri..

Mhubiri 4: 9 ‘‘Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.

10 Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!

11 Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona moto?

12 Hata ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi

Hata Wanyama wanaowinda kama chui au fisi au simba, huwa wanapenda kumvizia yule mnyama aliye peke yake Zaidi ya kulivamia kundi zima…Na shetani naye ndio yupo hivyo hivyo.

3) Wakati upo katika hali ya udhaifu:

Fursa nyingine shetani anayopenda kuitumia ni pale mkristo anapokuwa katika hali ya udhaifu, shetani anapapenda sana hapo. Wakati Bwana alipofunga siku zile 40 hakumwona adui lakini alipoona tu njaa, ndipo hapo hapo adui akatokea na kuanza kumjaribu, shetani anapenda kutumia madhaifu, njaa, magonjwa, shida, tabu ili kukunaswa kwenye mitego yake.. Ayubu wakati wote hakuwahi kukutana na shetani akizunguza naye kumlaumu kuwa yeye kamkosea Mungu, siku zote hizo hakumwona shetani lakini alipoanza kupitia majanga yale ndipo shetani akamjia kwa vinywa vya wale marafiki zake watatu kumvunja moyo, na kumtaabisha wakimwambia kuwa yeye amemkufuru Mungu ndio maana yamemkuta yale yote..

Vivyo hivyo na wewe unayejijua ni mkristo, kumbuka shetani atakusubiria katika engo hiyo pia, wakati unapitia mazingira magumu, hatakuja wakati upo kwenye raha, au mafanikio, atakutafuta kwenye shida, na misiba, huko ndipo atakapokuletea hata vipengele vya maandiko kichwani mwako, ili tu kukutoa katika mstari wa imani, atakuleta vishawishi vingi, wa watu wengi wa ajabu, atakupa mpaka njia mbadala ya kufanya kama vile alivyomshauri Bwana Yesu ageuze jiwe liwe mkate.

Lakini nataka nikuambie kupitia shida, au udhaifu au taabu ya kitambo fahamu kuwa sio uthibitisho kuwa Mungu amekuacha maadamu unafahamu kuwa uhusiano wako na Mungu bado upo, usiikate imani ndugu..kuwa kama Daudi aliposema Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu nijapopita katika bonde la uvuli wa Mauti, sitaogopa kwa maana wewe upo pamoja nami, gongo lako na fimbo yako vyanifariji.(Zaburi 23).

Tukirudi pia katika mifano ile ile ya Wanyama wawindao kama simba au chui huwa wanapenda kumvamia yule aliye dhaifu, wakishakosa aliye peke yake katika kundi, au aliye mtoto katika kundi, huwa wanatafuta aliyedhaifu, au mgonjwa, kwasababu hawatasumbuka sana katika kumkamata..shetani naye ni kama simba angurumaye akitafuta mtu ammeze..maandiko yanasema hivyo… 1 Petro 5:8

4) Eneo lingine analolipenda kulitumia ni wakati unahama kutoka kiwango kimoja cha utukufu hadi kingine:

Kuna wakati Mungu atayaongeza mafuta yake kwako, kwa ajili ya utumishi wake, hapo napo shetani hatataka atulie kukuangalia tu unakwenda kufanikiwa kuutangaza ufalme wa Mungu, ni lazima alete mawimbi yake. Tunaona Bwana siku ile tu alipokwenda kubatizwa kule Yordani na Roho wa Mungu kushuka juu yake na kumtia mafuta yale ya utumishi mkuu kama ule, tunaona shetani akajidhihirisha kwake alipokwenda kule jangwani..Hii ni kawaida, kwa watumishi wa Mungu kukumbana na mkono wa shetani uso kwa uso safarini katika kuineza kazi ya Mungu. Lakini mwisho wa siku ataishia kushindwa tu, kwasababu vita ni vya Bwana.

Hivyo pia katika eneo hilo zingatia sana, tarajia kukutana naye na hakikisha umwachi atoke salama.

5) Eneo lingine ni Wakati upo katikati ya watu ambao unadhani wanaweza kuwa faraja au msaada mkubwa sana kwako katika imani:

Hii inatokea hususani kwa watu wa imani moja na wewe…Hichi ni chanzo ambacho Mtu hawezi kukitazamia kama shetani anaweza kupitia kukujaribu lakini biblia imekithibitisha chanzo hichi, na kinakuwa na matokeo makubwa sana kwa mtu kama asipokuwa makini. na hivyo tunapaswa tuwe makini katika eneo hilo pia. Hilo tunalithibitisha kwa Bwana wetu Yesu yeye ndiye aliyewachagua mitume wake 12, na yeye ndiye aliyewatenga kwenda kufanya kazi ya kutangaza ufalme wa mbinguni pamoja naye,.na wakati mwingine aliwasifia kwa utumishi wao kwa mfano Petro alipopokea ufunuo wa kuwa yeye ni nani (Mathayo 16) alimsifia lakini mbele kidogo shetani alimtumia kupitisha hila zake..Lakini Bwana alilitambua hilo haraka kwa mafuta yaliyopo ndani yake na kumwambia Nenda nyuma yangu, Shetani; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.(Marko 8:33).

Hali kadhalika tunaona baadaye kwa mwingine aliyeitwa Yuda,alikuja kumsaliti, yeye ndio aliyeifanikisha kazi ya shetani kwa ufasaha zaidi mambo ambayo mafarisayo pamoja na wingi wao na utajiri wao walishindwa kumwangamiza Yesu lakini Yuda mmoja tu alifanikiwa kumweka Bwana mikononi mwa maadui zake.

Hivyo ukiwa katika ukristo au katika utumishi hilo usilisahau akilini mwako, usiweke asilimia zako zote kwa mwanadamu mwenzako, kwasababu siku akikusaliti unaweza ukavunjika moyo kiasi cha kufa, jambo hilo lilishawahi kunikuta pia mimi, sipendi likukute na wewe, wewe kaa nao karibu, ombeaneni, pia aminianeni lakini usilitoe hili akilini kuwa inaweza kutokea nafasi shetani kumtumia kukushambulia wewe, Lakini kama ukiwa umelijua hilo mapema halitakusumbua na hivyo mishale hiyo ya shetani kwako ikija itakuwa si kitu. Bwana atakuwa upande wako.

Jambo la mwisho la kufahamu ni kuwa shetani akishaona umezijua njama zake hizi zote, na amezilita kwako na umezishinda, hatakuacha moja kwa moja, fahamu kuwa atatulia tu kwa muda fulani, halafu atarudi tena, Kama tunavyoona kwa Bwana wetu Yesu Kristo tukisoma katika

Luka 4.13 ‘Basi alipomaliza kila jaribu, Ibilisi akamwacha akaenda zake kwa muda’’.

Hivyo biblia inatuambia mambo hayo yaliandikwa ili kutuonya sisi…Na sehemu nyingine Bwana anasema “Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele”. (Mathayo 24.25).

Kwahiyo hatupaswi kulala, wala kusinzia, kwasababu adui yetu yeye hakati tamaa, na hiyo inatufundisha tuwe watu wa kukuesha katika roho kila wakati. Kumbuka shetani hawezi kutushinda, pindi tu tunapotaka kutulia katika Neno la Mungu, Hivyo usiogope ikiwa umeyakabidhi maisha yako kwa Bwana kweli kweli na umesimama basi fahamu USHINDI NI LAZIMA.

Bwana akubariki.

Tafadhali “share” ujumbe huu na wengine.

Na pia kama utapenda masomo haya yawe yanakufikia kila siku kwa njia ya Whatsapp  Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Print this post

JIWE LA KUKWAZA

Marko 6:1 ‘Akatoka huko, akafika mpaka nchi ya kwao; wanafunzi wake wakamfuata.

2 Na ilipokuwa sabato, alianza kufundisha katika sinagogi; wengi waliposikia wakashangaa, wakisema, Huyu ameyapata wapi haya? Na, Ni hekima gani hii aliyopewa huyu? Na, Ni nini miujiza hii mikubwa inayotendeka kwa mikono yake?

3 Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose, na Yuda, na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? WAKAJIKWAA KWAKE’’. 

Tunasoma pia…

1 Petro 2:6 ‘Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, Na kila amwaminiye hatatahayarika.

7 Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini, Jiwe walilolikataa waashi, Limekuwa jiwe kuu la pembeni.

8 Tena, JIWE LA KUJIKWAZA MGUU, na mwamba wa kuangusha, Kwa maana hujikwaza kwa neno lile,wasiliamini,nao waliwekwa kusudi wapate hayo’’.

Shalom! Mtu wa Mungu, karibu tujifunze Neno la Mungu…ambapo leo kwa neema zake tutajifunza juu ya jiwe la kukwaza..

Ulishawahi kutembea barabarani ghafla ukajikwaa, na ulipotazama chini ukagundua ni kipande kidogo cha jiwe ndicho kilichokukwamisha, ambacho hukutarajia kama kikengeweza kukuweka chini, na wakati mwingine unajikuta umepata jeraha Fulani, au kiatu chako kumeharibika, au kama ulikuwa umevaa sandals unakuta imekatika??..Basi kama tukio kama hilo lilishakutokea basi hiyo ni ajali inayoitwa KUJIKWAA.

8 Tena, JIWE LA KUJIKWAZA MGUU, na mwamba wa kuangusha, Kwa maana hujikwaza kwa neno lile,wasiliamini,nao waliwekwa kusudi wapate hayo

 Lakini pia kupo kujikwaa kwingine katika roho, ambapo na kwenyewe kuna hasara zake. Kama tunavyojua hakuna mtu yoyote anajikwaa akiwa amesimama, ni sharti awe katika mwendo Fulani…Na sisi wanadamu wote tupo katika mwendo, tupo safarini ndio maana tuna vipindi vya kuzaliwa, na vya kufa..hiyo ni kuonyesha kuwa duniani tunapita tu!.

Lakini Mungu amesema katika Neno lake, kuwa ameweka JIWE katika njia ya safari yetu. Ikiwa na maana kuwa tunaposafiri ni kama tunavyotembea tunapaswa tuwe makini sio tu kuangalia mbele bali pia kuangalia hatua zetu tunazozipiga, na kuangalia njia tunazozipita…Kwasababu wakati tunapita katika haya Maisha kila mtu lazima akutane na hilo JIWE, na sio kubwa kwa macho, linaonekana dogo na lakudharaulika lakini, linaweza kumweka mtu chini, Mtu akilipita pasipo kuliona atajikwaa na kuanguka, na kuumia lakini aliye makini ambaye anapita huku akitazama mbele na chini, atapunguza mwendo.. Maandiko yanasema..

‘Tazama, naweka katika Sayuni JIWE KUU LA PEMBENI, teule, lenye heshima, Na kila amwaminiye hatatahayarika….. Tena, JIWE LA KUJIKWAZA MGUU, na mwamba wa kuangusha’’

Ukisoma maandiko utajua kuwa hilo jiwe si linguine Zaidi ya YESU KRISTO.

Yeye ndio JIWE kuu na Teule..Tunasoma katika maandiko…wakati akiwa hapa duniani, watu hawakumjua kama ndiye Masihi aliyetabiriwa…hawakujua kuwe yeye ni chapa ya nafsi ya Mungu, waliona ni mtu wa kawaida tu! Kwasababu walikuwa wanamjua baba yake, mama yake, walikuwa wanamjua tangu utoto wake walikuwa wanamwona jinsi anavyokua, wanapajua kwao,wanawajua wadogo zake, dada zake, wanalikuwa wanajua mpaka kipato chake alichokuwa anakipata katika ajira yake.

Kwahiyo katika kumjua huko, wakamdharau, wakamwona huyu ni Bwana mdogo tu hawezi kufanya lolote,hawakujua kuwa jiwe dogo tu linaweza kumfanya mtu aanguke chini vibaya sana, dharau zile zikasababisha wasimjue kama Mwana pekee wa Mungu, wasimjue kama Mkombozi, wasimjue kama mpatanishi kati ya wanadamu na Mungu, wasimjue kama Bwana, na Masihi, wasimjue kama Adamu wa Pili, bali wamjue tu kama mwana Kijiji au kama mwananchi wa kawaida tu,Kwahiyo Wakajikwaa kwake..Ni kama mtu apite na ghafla akutane na jiwe na kujikwaa..ndicho kilichowatokea hawa watu.

Lakini sio kwamba hao wana bahati mbaya sana, kuliko watu wa kipindi hichi, hapana! hata Hata leo JIWE hilo lipo…Na kila mtu lazima akutane nalo.. Ni jiwe dogo sana mbele za macho ya watu! Lakini ni Teule mbele za Mungu, ni dogo kiasi kwamba barabarani unaweza usilione, lakini ukijikwaa kwa jiwe ni lazima uanguke..

Ndugu unayesoma ujumbe huu, kama hujampa Bwana maisha yako, ni vizuri ukajitathmini mara mbili mbili. Kwasababu katika safari yako ni lazima utasikia injili tu! Itakufikia popote pale..na Kama ukiikataa na kuidharau na kumdharau Yesu Kristo kwako atakuwa ni JIWE LA KUKWAZA. Utaanguka siku na saa usiyodhani, wakati unakazana mbele kukimbilia malengo yako, yatakatika ghafla utakapojikuta upo kaburini na hatimaye kwenye ziwa la moto.Hapa duniani usisafiri kwa kuangalia mbele tu, bali angalia pia njia unazopita…lipo JIWE limewekwa njiani..ni JIWE la KUKWAZA, kwa wale wasioliona. Hivyo usiwe mmoja wao KUKOSANA NA YESU KRISTO, BWANA WAKO aliyetoa uhai wako kwa ajili yako.

Isafishe njia yako kwa kulitii Neno lake leo, anapokwambia mwanangu NJOO!!! Isikie leo sauti yake ukatubu na kubatizwa kwa jina lake, ili upate msamaha wa dhambi zako na ondoleo la dhambi zako, haijalishi ulimkosea kiasi gani, watu wote tulimkosea lakini ametubadilisha, na wewe pia atakubadilisha, usipoteze muda mwingi kuangalia mambo ya ulimwengu huu, wakati hali yako ya kiroho inadorora kila siku, Isafishe njia yako leo.

Zaburi 119: 9 ‘’Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako’’. Bwana akubariki,

Tafadhali ‘share’ ujumbe hu una wengine.

Na pia kama utapenda masomo haya yawe yanakufikia kila siku kwa njia ya Whatsapp  Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

NITAFANYA YERUSALEMU KUWA JIWE LA KUWALEMEA .

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

UAMINIFU NI KIGEZO KIKUBWA CHA KUTUMIWA NA MUNGU.

UMEITIKIA WITO INAVYOPASWA?

JE! UMEFUNDISHWA?

KITABU CHA YASHARI NI KITABU GANI?

Kiyama ni nini?


Rudi Nyumbani

Print this post

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI.

Shalom! Mtu wa Mungu, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo litukuzwe daima, karibu tujifunze Neno la Mungu, na leo tutaenda kuona tabia za wanawake hawa wawili na naamini tutakwenda kujifunza kitu kikubwa hususani kwa upande wa wanawake wakristo. Watu hawa ambao tunakwenda kutazama tabia zao wa kwanza ni MKE WA HERODE, na wa pili ni Yule MKE WA PILATO.

Tunafahamu katika maandiko hawa wote walikuwa ni wake wa viongozi wakubwa waliokuwa wanaongoza Taifa la Israeli kipindi cha Bwana wetu Yesu Kristo, Herode alikuwa ni mtawala wa Galilaya upande wa kaskazini na Pilato alikuwa ni akida wa Yudea upande wa kusini wa taifa la Israeli, hawa wote hawakuwa wayahudi, walikuwa ni WARUMI.

Kumbuka wakati ule Dola ya kiRumi ndio iliyokuwa inatawala karibu dunia nzima, hivyo kama ngome yenye nguvu ilikuwa ni sharti iwe na majimbo mengi au makoloni mengi chini yake ya kuyaamrisha. Kama tu tunavyofahamu kipindi kile cha ukoloni katika nchi yetu hii ambayo mwanzo iliitwa Tanganyika lilikuwa ni koloni la wajerumani, na ndivyo ilikuwa katika kipindi kile cha Bwana Yesu nchi ya Palestina (yaani Israeli), ilikuwa ni moja ya koloni la Warumi, hivyo sheria zote, na maagizo yote yahusuyo utawala pamoja na kodi zote zilikuwa zikisanywa na kupelekwa Rumi makao makuu.

Sasa kipindi kifupi kabla ya kuzaliwa Bwana Yesu KAISARI AUGUSTO ambaye tunamsoma habari zake katika Luka 2:1, ndiye aliyekuwa mtawala mkuu wa Dola hii ya Kirumi huko RUMI. Hivyo yeye pamoja na baraza lake chini yake likamweka Herode kuwa kama mfalme wa taifa lote la Palestina na nchi zilizokuwa kando kando yake. Herode huyu mkuu ndiye anayesifika kwa kulikarabati lile Hekalu lililokuwa limebomoka, (Yohana 2:22) na huyu ndiye aliyetaka baadaye kuja kumwua Yesu pindi anazaliwa mpaka kupelekea Yusufu na familia yake kukimbilia uamishoni Misri.

Sasa baada ya kufa kwake, ilipasa awepo mtu wa kumrithi ufalme wake, hivyo aliacha waraka wa urithi na kusema nchi ile ya Palestina igawanywe kwa watoto wake wote, kwahiyo alipokufa waraka ule ulipelekwa Rumi makao makuu ili kuombwa uthbitishwe na Kaisari, hivyo kaisari akathibitisha migawanyo ile na Palestina ikagawanywa kwa watoto wa Herode mkuu, sasa sehemu zile unazoziona zinatajwa sana katika agano jipya (Ndani ya taifa la Israeli) walipewa watoto wake wawili, ambapo mmoja alipewa atawale Galilaya na mwingine akapewa atawale (Samaria, Yudea na Idumea) karibu nusu ya Taifa zima la Israeli, na watoto wake wengine wawili waliosalia walipewa nchi za kando- upande wa Yordani ng’ambo, Iturea na trakoniki na Dekapoli.(Luka 3:1).

Sasa huyu mtoto mmoja wa Herode ambaye alipewa Galiliya ndio Herode Yule tunayemsoma aliyekuja kumuua Yohana Mbatizaji, na ndio huyu huyu alikuwa anamwinda Bwana Yesu baadaye aje kumuua alipokuwa anahubiri lakini Bwana alimwita Mbweha..Na ndio Yule Yule siku ile ya kusulibiwa kwake Pilato alimpeleka kwake ili ahukumiwe,lakini yeye akamrudisha kwa Pilato tena.

Lakini tukirudi kwa Yule mtoto wa pili wa Herode mkuu, ambaye alipewa kutawala upande wa chini wa taifa la Israeli ambayo ni YUDEA NA SAMARIA yote sehemu kubwa ya Israeli historia inaonyesha naye alikuwa ni mkatili vile vile kama ndugu zake, awali ya yote yeye ndio alikuwa akimtafuta mtoto Yesu, ili amwangamize Yesu aliporudi kutoka Misri na wazazi wake hata baada ya baba yake kufa.

Mathayo 2:19 “Hata alipofariki Herode, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto huko Misri,

20 akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mamaye, ushike njia kwenda nchi ya Israeli; kwa maana wamekufa walioitafuta roho ya mtoto.

21 Akaondoka akamchukua mtoto na mamaye, akafika nchi ya Israeli.

22 Lakini aliposikia ya kwamba Arkelao anamiliki huko Uyahudi mahali pa Herode babaye, aliogopa kwenda huko; naye akiisha kuonywa katika ndoto, akasafiri pande za Galilaya,

23 akaenda, akakaa katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazorayo”.

Huyu alizidi kuwa mbaya sana, Historia inaonyesha alifikia hatua hata ya Kaisari kule Rumi kutopendezwa naye, na kumwondoa kwa nguvu madarakani na kumpeleka uamishoni huko ufarasa na kukaa huko mpaka kufa kwake. Ndipo sasa akahitajika mtu wa kuijaza nafasi yake na ndio tunakuja kuona nafasi yake ikachukuliwa na huyu liwali mpya aliyejulikana kama PONTIO PILATO…atawale miji yote ile ya upande wa kusini.

Sasa mpaka hapo natumai utakuwa umepata picha kidogo, jinsi utawala huo ulivyokuwa umejiganyika, hivyo kipindi kile cha Yohana mbatizaji, na Bwana Yesu, hawa viongozi wawili yaani Herode na Pontio Pilato ndio waliokuwa wanalishikilia taifa la Israeli.

Kwahiyo turudi katika kiini cha Somo letu, tunaona viongozi hawa ambao hata hofu ya Mungu haikuwa ndani yao, watu ambao walikuwa sio wayahudi bali wapagani walikuwa na wake zao kila mmoja na mahali pake. Lakini tunaona tabia za hawa wanawake zilitofautiana sana, hususani pale lilipotokea suala la kuwaangamiza watu wa Mungu.

Kama tunavyofahamu habari mke wa Herode japo alifahamu kabisa kuwa Yohana alikuwa ni nabii wa Mungu kweli, lakini yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kukitaka kichwa cha Yohana, zaidi hata ya wale mafarisayo ambao hao ndio wangestahili kukiomba kichwa cha Yohana lakini sio Yule mwanamke. Yeye alimshawishi mume wake amuue Yohana mbatizaji kwa faida zake mwenyewe..Na Herode naye kwa kutomwogopa Mungu akasikiliza viapo vya mke wake na kwenda kumwangamiza Yohana kule gerezani kwa kumkata kichwa.

Lakini tukirudi kwa mwanamke mwingine pili, ambaye naye pia alikuwa katika kiti cha kifalme, aliketi kama malkia, Tunaona Mume wake alipotaka kwenda kuwapa wayahudi amri ya kumuua Bwana Yesu, yeye alikuja na ushawishi mwingine tofauti na Yule wa kwanza, yeye alimwonya sana mume wake asidhubutu kufanya vile kwani ni mtumishi wa Mungu.

Anaeleza jinsi alivyoteswa sana katika ndoto usiku kabla ya Yesu kusulibiwa, embu jaribu kutengeneza picha analala mara ya kwanza, anaota kama yeye ndio anayemngongelea misumari mtu asiye na hatia, anashtuka anaona ni ndoto tu, halafu analala tena, anaota kitu kile kile, anaamka tena, analala jambo lile lile tena linajirudia, hata mara 10, halafu asubuhi anakutana na mtu Yule Yule aliyekuwa anamwona kwenye ndoto analetwa mbele yake…Sura ile ile ya upole inakuja mbele zake,..

Hakika huyu mwanamke Mungu alimwekea kitu kingine cha ziada ndani yake.

Unaweza ukajiulizwa kwanini mambo kama haya hayakumtokea na Yule mke wa Herode? Pengine Yohana angekuwa mzima mpaka wakati wa Kristo kufa kwake,. Kwasababu kumbuka huyu hana chochote cha kumshinda Yule, wala Yule hakuwa na cha ziada cha kumshinda huyu lakini kwanini haikutokea kwa Yule mwanamke mwingine?.

Kaka/dada Kuna wakati unajiuliza maswali mengi lakini unakosa majibu, kwamfano utakutana na dada mmoja mkristo atakwambia anajisikia aibu kuvaa nguo zinazobana, na zaidi atakwambia ninajisikia kuhukumiwa ndani yangu pale ninapojaribu kudhubutu kuvaa sketi fupi, atakwambia ninajiona kama ninajidhalilisha pale ninapovaa suruali na kutembea nayo barabarani mbele za watu na bado mpendwa huyo huyo atakwambia ninaona kama bado sijawa mkristo pale ninapovaa vimini na kuweka ma-make-up usoni na kwenda kanisani au kutembea mbele za watu…

Lakini wakati huo huo utakutana na dada mwingine naye anasema ameokoka atakwambia mbona mimi ninaona kawaida tu, Mungu haangalii mavazi anaangalia moyo..Utamkuta yupo confortable kutembea na vimini na suruali zinazobana barabarani, na wala hasikii chochote kinachomuhukumu ndani yake na bado anaona hakuna tatizo lolote ni sawa tu..

Embu jiulize ni roho ya aina gani ipo ndani yako?, Jichunguze ujiulize kama ni Roho wa Mungu mbona basi haiugui kwa namna moja na ya Yule mwenzako anayejisitiri?..Au unadhani ile ni roho ya shetani au ni mawazo yake tu yanampelekea kuwa vile? Na ya kwako ndio Roho ya Mungu?..Embu nenda kawaulize kabla ya kukutana na Kristo walikuwa wanavaaje watakueleza…watakuambia tofauti yao kabla ya kukutana na baada ya kukutana na Yesu.

Hujui kuwa unamsulibisha Kristo kwa matendo yako, tufauti yako na Yule mke wa Herode haipo, Roho ya Mungu imeshakufa ndani yako, HAIUGUI tena, unaona kila kitu ni okay!!. Utajitetea nipo katika mazingira magumu ya kuacha, lakini nataka nikuambie hawa wanawake wote wawili walikuwa katika mazingira ya level moja, walikuwa wake wa wakuu, tena wa kidunia, tena sio hata wayahudi, lakini mmoja alikuwa na hofu ya Mungu ndani yake na mwingine hakuwa nayo…Vivyo vivyo na wewe usidhani ni wewe peke yako upo katika mazingira magumu ya kuacha hivyo vitu..Wapo wengi tu, tena zaidi yako wewe lakini kwasababu wao wamekubali kuitii hiyo sauti inayougua ndani yao kila siku. Wamekuwa kama walivyokuwa leo hii..ambaye wewe unawaona washamba wamepitwa na wakati.

Ni maombi yangu utabadilisha mwenendo wako dada yangu, shetani anapenda kuwatumia wanawake, kuunyanyua ufalme wake, ni chombo chepesi cha shetani, alikitumia Edeni anakitumia na sasa..Hivyo wewe dada usifanyike kuwa chombo hicho chepesi chepesi tu cha shetani kukutumia anavyotaka. Sio kila mtindo wa dunia hii unaokuja mbele zako unakufaa.. mingi asili yake ni kuzimu,Biblia inasema unapaswa utufute mwenendo wa wanawake wacha Mungu mfano wa wakina Sara na Rebeka na Hana na sio wasanii wa nyimbo za kuzimu.

1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;

10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.

11 Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna”

Halikadhalika na kwa mwanaume unayeweka mlegezo, unanyoa kama jogoo, unachora mwili wako tattoo, na huku unajiita ni mkristo..Jiulize ni kwanini wewe unaonaekana tofauti na wacha Mungu wengine?. Au Roho iliyo ndani yako ni bora zaidi kuliko ya wale wengine..Jiulize ndugu, jitathmini…Tumeambiwa tuzijaribu hizi roho, tunapenda injili za “haijalishi”..Na huku nyuma roho zetu zinaangamiia.

Ni maombi yangu, na matumaini yangu injili itatubadilisha, na kuanza kuenenda katika njia kamilifu za Mungu huku tukitii ile sauti ya Roho Mtakatifu inayougua ndani yetu kila siku kutukumbusha namna kuenenda katika utakatifu wote, mpaka kufikia kuja kwa Kristo Bwana wetu na wote kwenda mbinguni bila hila wa mawaa.

Mungu akubariki sana.

+255693036618/ +255789001312

Na pia kama utapenda masomo haya yawe yanakufikia kila siku kwa njia ya Whatsapp. Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

Maherodi walikuwa ni akina nani, Na kazi yao ilikuwa ni ipi?

MWANAMKE YEZEBELI

TUZIJARIBU HIZI ROHO.

MAVAZI YAPASAYO.

MAANA YA RANGI KIBIBLIA.

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.


Rudi Nyumbani

Print this post