Category Archive Home

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

Shalom, Mtu wa Mungu, karibu tujifunze biblia, Jukumu kubwa tulilopewa miongoni mwa mengi ni jukumu la kumfahamu sana YESU KRISTO, Na lengo kuu la kumfahamu sio kwasababu yeye anauhitaji sana wa Utukufu, au uhitaji sana wa kutafuta ajulikane, hapana! Hilo sio lengo…kwasababu pale tu alipo tayari anajulikana…Lakini bado anatuasa tunapaswa tumfahamu sana yeye…Hivyo hiyo ikimaanisha kuwa kwa jinsi tunavyomfahamu yeye ni tofauti na yeye anavyotaka sisi tumfahamu…

Kwasasa Mtu maarufu kuliko wote duniani kwa wakati wote ni YESU KRISTO, hakuna mwanadamu yeyote aliyewahi kufikia kiwango cha umaarufu alionao Bwana Yesu Kristo, ukienda kwa wachina, wahindu, wabudha wote wanamjua Yesu Kristo…Hata watu ambao sio wakristo kwa namna moja au nyingine walishawahi kumsikia Yesu Kristo katika Maisha yao..kwahiyo yeye ni maarufu tayari.

Biblia inasema katika…Waefeso 4: 13 “ …hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;

14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu”

Na kwanini anataka sisi tumfahamu sana yeye? Mstari wa 14, hapo juu umetupa majibu… Ni ili tusiendelee kuwa Watoto wachanga, tukitupwa huku na huko, tukidanganywa na kila upepo wa elimu, na kuishia kuzifuata njia za udanganyifu.

Kwahiyo hakuna Elimu nyingine itakayoweza kutufanya tusiweze kudanganyika na elimu ya mashetani, isipokuwa Elimu ya kumfahamu Yesu Kristo, hakuna namna yoyote utakayoweza kuifahamu na kuidhibiti noti bandia pasipo kwanza kuijua noti halali ilivyo, ukishaifahamu noti halali ilivyo na tabia zake ndivyo utakavyoweza kuijua noti bandia..Kadhalika tunajukumu kubwa sana la kumfahamu Yesu Kristo kwa undani ili tuweze kuyadhibiti mafundisho ya mashetani na wapinga Kristo.

Leo tutajifunza kwanini Yesu Kristo, anajulikana kama Mwana wa Daudi na kwanini ni MFALME.

Sasa ni Dhahiri kabisa tunajua kuwa Yesu hakuwa na Baba wa kimwili, lakini kuna mahali kwenye maandiko kajitambulisha kuwa Mwana wa Daudi.. Sasa kwanini alijiita hivyo?

Sababu pekee ya Bwana Yesu kujulikana kama mwana wa Daudi, ni kutokana na Baraka Daudi alizozibeba, lakini si kutokana na undugu wa kidamu..Wewe unaitwa mwana wa Baba yako kutokana na uhusiano wa kidamu..lakini unaweza ukaitwa mwana wa Raisi wako, ila si kwa uhusiano wa kidamu bali wa pengine wa kiitikadi fulani….

Kwamfano pia sisi wakristo tunaitwa Wana wa Mungu, si kwasababu tumezaliwa familia moja na Muumba wetu, hapana au kwamba tuna damu moja na Mungu, hapana ni kutokana na Baraka za kimbinguni zinavyohusiana na sisi ndio maana tunaitwa wana wa Mungu.

Vivyo hivyo tunajulikana kwamba ni wana wa Ibrahimu , sio kwasababu sisi tuna damu moja na Ibrahimu, hapana bali ni kwasababu ni warithi wa Ahadi zile zile alizopewa Ibrahimu na Mungu, ndio maana na sisi tunajulikana kama wana wa Ibrahimu, Na Bwana Yesu ndio hivyo hivyo, Baraka alizopewa Daudi na mnyororo wa ukoo wake wote zilimhusu pia Bwana wetu Yesu Kristo…Daudi alikusudia kumjengea Mungu, Nyumba na hivyo Mungu akambarikia yeye na uzao wake kuwa uzao wa kifalme milele.(soma 2 Samweli 7:1-12)

kwasababu alizaliwa katika nyumba ya Yusufu ambaye alikuwa ni wa ukoo wa Daudi uliobarikiwa (ukoo wa kifalme),..Moja ya Baraka za ukoo wa Daudi ni kwamba utakuwa ni ukoo wa kifalme, kwamba wazao wote wa Kwanza wa Daudi walipakwa Mafuta na Mungu wawe wafalme soma (2 Wafalme 8:19,). Na ndio maana Bwana Yesu alipozaliwa katika nyumba ya Yusufu kama mzaliwa wa kwanza, roho ya kifalme ilikuwa juu yake. Kwahiyo kwa namna yoyote ile ni lazima angekuja tu kuwa Mfalme..

Je! Unajua kuwa Yusufu baba yake Yesu angepaswa awe mfalme wa Israeli kwa kipindi kile, kulingana na ahadi Mungu aliyomuahidia Daudi?…Lakini kutokana na dhambi zao, Taifa la Israeli lilikatwa na uzao wa Daudi wa kifalme ukasimamishwa katika kutawala na ulisimamishwa kipindi gani?..

Kama ukisoma kitabu cha Wafalme, baada ya Daudi kufa, akafuata mwanawe Sulemani akawa mfalme kweli kulingana na ile Ahadi lakini naye pia akafa, na ikaendelea hivyo hivyo, kwa wajukuu na vitukuu vya Daudi, mpaka mfalme wa mwisho aliyetawala Yuda aliyeitwa Sedekia, ambaye alikuwa ni kitukuu cha 20 cha Daudi, huyu ndiye mfalme wa Mwisho kutawala Yuda, baada yake yeye, ndio Watu wakapelekwa Utumwani Babeli, hiyo ndiyo siku waliokatwa na waliporudi kukawa hakuna mfalme tena katika Israeli…vitukuu vya Daudi vilivyozaliwa baada ya Sedekia Mfalme wa Mwisho kufa, wakawa ni watu tu wa kawaida, kama watu wengine…

Ndio maana Yusufu baba yake Yesu alikuwa ni mtu wa kawaida tu maskini, ingawa alikuwa ni mwana wa kifalme…(Kwa urefu fuatilia ukoo huu wa Yesu kwenye kitabu cha Mathayo 1:1-17), laiti Israeli asingeasi na kupelekwa utumwani, Yusufu baba yake Yesu angekuwa mfalme wa Yuda, na Kristo angezaliwa huko…

Hivyo Israeli iliendelea kuwa kama mti uliokatwa baada ya kutoka Babeli…Wayahudi wakakaa mamia ya miaka bila mfalme….kukawa hakuna dalili yoyote ya Mfalme kunyanyuka katika uzao wa Daudi,..kwani Utawala wa Rumi ulikuwa umekamata dunia nzima, na Warumi waliwaweka watu wao kwenye makoloni yao yote, mpaka Israeli ilikuwa ni koloni la Warumi..Hivyo mtawala aliyetawala koloni la Israeli alikuwa ni Mrumi…jambo hilo liliendelea kwa miaka mingi…lakini Biblia ilitabiri katika Isaya Mlango wa 11 kuwa litatoka chipukizi katika shina la Yese….Kumbuka Yese alikuwa ni Baba yake Daudi, kwahiyo ni sawa na kusema litatoka chipukizi katika shina la Daudi au katika uzao wa Daudi. Tunasoma hayo katika…

Isaya11:1 “ Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda.

2 Na roho ya Bwana atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana”.

Kama ni msomaji mzuri wa maandiko utagundua kuwa…hilo shina linalozungumziwa hapo si lingine Zaidi ya BWANA YESU KRISTO mwenyewe…Biblia inasema litatoka shina, ikiwa na maana kuwa ni kutoka katika mti uliokatwa, nalo litazaa sana matunda… Kama ulishawahi kuona mti mkubwa uliokatiwa chini kabisa..linakuwa linabaki tu kama gogo…halafu baada ya kipindi fulani unaona kitawi kidogo cha kijani kinajitokeza ubavuni mwa lile gogo, na kama hakitakatwa na chenyewe, baada ya kipindi fulani kitakuwa kikubwa na hatimaye kuwa tena mti mkubwa kama ulivyokuwa mwanzo…

Ndicho kilichotokea baada ya uzao wa Daudi kukatwa na kupelekwa Babeli…ni sawa na mti uliokatwa…lakini chipukizi likatoka, katika uzao huo huo wa Daudi..

Bwana Yesu, Mwana wa Daudi, mzao wa kifalme, mwenye ahadi ya kifalme juu yake, alizaliwa huko Bethlehemu, alikuwa ni mfalme aliyetoka katika shina lililokatwa ndio maana utaona alizaliwa katika zizi la ng’ombe, familia ya kimaskini, laiti Yusufu baba yake angekuwa mfalme basi naye pia angezaliwa katika familia ya kifalme..Lakini kinyume chake alizaliwa katika ufalme uliokatwa…

Lakini maandiko yanatabiri, huyo atakuja kuwa mti mkubwa na utazaa sana matunda, na ufalme wake utaenea duniani kote…kipindi alichokuja miaka 2000 iliyopita, roho ya Bwana ilikuwa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana” Kwa hekima, na maarifa aliyoyabeba alituletea sisi Wokovu…ambao mpaka sasa tunanufaika nao…., Lakini katika utawala wa miaka 1000 ijayo, ndio tutamwona vizuri kama Mfalme, aliyeketi katika kiti cha Kifalme…katika wakati huo, yeye pamoja na sisi ambao sasa tumemwamini, tutatawala naye, sisi tutakuwa wafalme na yeye atakuwa kama Mfalme wa wafalme.

Wakati huo Mamlaka yote ya kifalme atakuwa nayo yeye, utakuwa sio wakati wa wokovu tena bali wakati wa utawala, sasa hivi ndio tupo wakati wa wokovu, nyakati hizo zitakuwa ni nyakati za utawala mkuu wa Yesu Kristo. Dunia yote itajawa na kumcha Bwana, kutakuwa hakuna vurugu, kutakuwa na Amani isiyo ya kawaida..simba na kondoo watakaa pamoja na hawatadhuriana, mtoto atacheza na nyoka, na hakutakuwa na madhara yoyote.

Tusome tena Isaya hii 11 Mpaka mwisho..

“1 Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda.

2 Na roho ya Bwana atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana;

3 na furaha yake itakuwa katika kumcha Bwana; wala hatahukumu kwa kuyafuata ayaonayo kwa macho yake, wala hataonya kwa kuyafuata ayasikiayo kwa masikio yake;

4 bali kwa haki atawahukumu maskini, naye atawaonya wanyenyekevu wa dunia kwa adili; naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, na kwa pumzi ya midomo yake atawaua wabaya.

5 Na haki itakuwa mshipi wa viuno vyake, na uaminifu mshipi wa kujifungia.

6 Mbwa-mwitu atakaa pamoja na mwana-kondoo, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwana-simba na kinono watakuwa pamoja, na mtoto mdogo atawaongoza.

7 Ng’ombe na dubu watalisha pamoja; watoto wao watalala pamoja; na simba atakula majani kama ng’ombe.

8 Na mtoto anyonyaye atacheza penye tundu la nyoka, na mtoto aliyeachishwa atatia mkono wake katika pango la fira.

9 Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; maana dunia itajawa na kumjua Bwana, kama vile maji yanavyoifunika bahari.

10 Na itakuwa katika siku hiyo, shina la Yese lisimamalo kuwa ishara kwa kabila za watu, yeye ndiye ambaye mataifa watamtafuta; na mahali pake pa kupumzikia patakuwa na utukufu”.

Ufunuo 3:20 “Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.

21 YEYE ASHINDAYE, NITAMPA KUKETI PAMOJA NAMI KATIKA KITI CHANGU CHA ENZI, KAMA MIMI NILIVYOSHINDA NIKAKETI PAMOJA NA BABA YANGU KATIKA KITI CHAKE CHA ENZI.

22 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”

Na pia alisema..

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.

14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.

15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.

16 Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi.

17 Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”

Kama hujampa Yesu Kristo Maisha yako, jua umechelewa sana, lakini mlango bado hujafungwa ingia kabla mlango hujafungwa..mwisho wa mambo yote umekaribia, na Kristo yupo Mlangoni kurudi, atakaporudi nyakati hii ya mwisho atakuja kama mfalme na mtawala mkuu hatakuja tena kama mwokozi.

Bwana akubariki.

Tafadhali share kwa wengine


Mada Nyinginezo:

MWANA WA MUNGU.

ANGUKO LA UFALME WA SHETANI:

JIWE LA KUSAGIA

HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.

JE! MTU KUSIKIA SAUTI ZA WATU WALIO MBALI, KUNAWEZA TOKANA NA MUNGU?

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “HERI WALIOTASA, NA MATUMBO YASIYOZAA, NA MAZIWA YASIYONYONYESHA”?


Rudi Nyumbani:

Print this post

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, Leo ni siku nyingine Bwana ametupa neema  mimi na wewe kuiona, hivyo ni wajibu wetu kiutimia vizuri siku yetu kwa kujifunza maneno yake ambayo ndio nuru yetu na uzima wetu hapa duniani kila siku.

Leo kwa neema za Bwana tutajifunza juu ya huu mwaka wa Bwana uliokubaliwa ni upi ambao Bwana Yesu aliuzungumzia katika…

Luka 4:18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,

19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa”.

Sasa ni vizuri kufahamu kuwa biblia inaposema mwaka sio kila mahali inamaanisha kuwa ni mwaka Fulani mahususi labda 2018 au 2019 hapana, bali inamaanisha kipindi Fulani cha wakati kilichotengwa mahususi kukamilisha lengo Fulani chenye mwanzo wake na mwisho wake ambacho kimefananishwa na mwaka..

Hivyo hapo ni sawa na kusema “kuutangaza wakati wa Bwana uliokubaliwa”..Ikiwa na maana kuwa kama huo ndio wakati uliokubaliwa, basi pia  zilikuwepo nyakati nyingine ambazo hazikukubaliwa…. Na pia tunapaswa kufahamu ulikubaliwa kwa kusudi lipi?

Katika agano la kale kila mwaka wa 50 uliitwa Yubilee, mwaka huu ulikuwa ni mwaka wa maachilio, haikuruhusiwi kulima wala kupanda, ardhi ilikuwa inastarehe, ni mwaka ulioitwa mwaka wa maachilio ya watumwa, na kusamehe watu madeni yao (Walawi 25:11),

Na ndicho Bwana Yesu alichokuja kukifanya katika agano jipya, kuleta maachilio ya vifungo vyote, vya rohoni na mwilini, vile vile alikuja kuutangaza huo mwaka Bwana uliokubalika, yaani wakati wa Mungu kumkubali mwanadamu, kumwokoa na kumfunulia uso wake na mapenzi yake amjue yeye..Hiyo ililetwa na Bwana YESU tu peke yake, kumbuka  hapo kabla Mungu alikuwa hampokei Mwanadamu yeyote haijalishi ni kuhani au nabii au rabi kiasi gani, hakukuwa na mwanadamu yeyote ambaye aliwahi kumkaribia  Mungu na kutoa hoja zake pasipo kuwa na deni la dhambi ndani yake, na ndio maana ilimpasa kuhani mkuu peke yake aingie patakatifu pa patakatifu mara moja tu kwa mwaka afanye upatanisho wa dhambi za watu, pamoja na dhambi zake mwenyewe ambazo kimsingi zilikuwa haziondolewa bali zinafunikwa, baada ya hapo shughuli imeishia hakuna mashauri wala mahojiano, unaondoka mbele ya madhabahu ya Mungu ambayo ilikuwa duniani na wala sio mbinguni..

Lakini Bwana Yesu alipokuja yeye alisimama kama kuhani mkuu, na hivyo sasahivi sio tu tumepata ondoleo la dhambi na  maombi yetu kusikiwa bali pia tunaketi na kula na kunywa na Mungu katika ulimwengu wa Roho kama vile Baba na mtoto wake wa pekee ampendaye.. Haleluya!.

Kwahiyo tunaishi bado katika kipindi cha Mwaka wa Bwana uliokubalika…Lakini huu wakati hautadumu milele, mwaka Bwana uliokubalika hautadumu milele, kuna wakati Bwana Yesu kama kuhani mkuu atasimama kutoka katika kiti chake cha ukuhani, na kuanzia huo wakati na kuendelea hakutakuwa na rehema tena, na wala Mungu  hatakuwa na nafasi ya kuwatazama waasi, kinachobakia tu ni ghadhabu ya Mungu kumiminwa juu ya waovu wote..Na huo wakati upo karibu sana ndugu, Unyakuo ukishapita tu basi fahamu kuwa kiti cha rehema kilishaondolewa..

Luka 13.24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.

25 Wakati mwenye nyumba ATAKAPOSIMAMA na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;

26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.

28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje”.

Na ndio maana biblia inasema wakati uliokubalika ndio sasa, ndio huu tulionao mimi na wewe,  yaani leo kwasababu kesho hatujui itakuwaje….

2 Wakorintho  6:2 “(Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)”..

Usisubirie wakati ambao haukubaliki ndio umkumbuke Mungu, utakuwa umeshachelewa ndugu. Ikiwa bado upo mbali na Kristo wakati ndio huu wa sasa tubu dhambi zako, jitwike msalaba wako umfuate YESU, atakusamehe dhambi zako, kisha hakikisha baada ya kutubu kwako unabatizwa  kisha yeye mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu bure kama alivyoahidi katika (Matendo 2:38)…

Bwana akubariki sana.


Mada Nyinginezo:

NINI MAANA YA KUISHI KWA KUUKOMBOA WAKATI?

CHANZO CHA MAMBO.

WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA.

JE! TARATIBU ZA KUFUNGA NDOA [YAANI HARUSI] NI AGIZO LA MUNGU AU NI MAPOKEO TU YA KIBINADAMU?

KUNENA KWA LUGHA KUKOJE?


Rudi Nyumbani:

Print this post

UKristo Ni Nini?

Ili kuelewa Nini maana ya Ukristo, tutafakari kwanza maana ya Neno UTAIFA…Neno utaifa limetokana na Nomino Taifa…Kwahiyo kitendo chochote kinachofanyika kinachohusisha mapenzi na Taifa, kitendo hicho kinaitwa Utaifa..

Tukirudi katika UKristo, Neno Ukristo nalo pia limetokana na Nomino Kristo…Na maana ya Kristo ni “Mtiwa Mafuta” au “Masihi” na wala sio Yesu,…Mtu aliyetiwa Mafuta na Mungu zamani hizo aliitwa kristo  na hata sasa kibiblia bado wanajulikana hivyo hivyo kama makristo.. Chimbuko la neno hilo Masihi au kristo Ni lugha ya Kigiriki.

Hivyo walikuwepo makristo wengi, sana zamani..Katika Biblia Daudi alijulikana kama ni kristo (yaani masihi wa Bwana) 1Samweli 16:6, kadhalika Mfalme Sauli (1Samweli 24:6) na wengine wengi, walijulikana kama ni makristo/masihi wa Bwana.

Lakini alipokuja mmoja ambaye alikuwa ni mkuu kuliko hao wote, aliyetiwa mafuta na Mungu mwenyewe kuwa juu ya vitu vyote, huyo naye aliitwa masihi au Kristo, isipokuwa ili kumtofautisha na masihi na makristo wengine, huyu jina lake lilianza kwa Herufi kubwa, yaani aliitwa Kristo badala ya kristo. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU. Ndio maana mahali popote katika biblia panapomtaja Kristo Yesu ni lazima hilo neno Kristo lianze kwa herufi kubwa, kuwatofautisha na makristo wengine.

Kwahiyo tukirudi kwenye swali, U-Kristo ni nini? Jibu ni kuwa U-Kristo ni kitendo mtu anachokifanya kinachohusisha mapenzi yake na mtu mmoja anayeitwa Kristo Yesu, zingatia hilo neno Kristo Yesu na sio “kristo yesu”…kwasababu makristo wapo wengi, na ma-yesu wapo wengi  lakini Kristo yupo mmoja na Yesu yupo Mmoja.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

DINI NI NINI?

JE! UKIMWI UNATIBIKA?

SHETANI NI NANI?

JE! UBATIZO SAHIHI NI UPI?

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Biblia ni nini?

Biblia ni nini?

Ni neno la Kigiriki, lenye maana ya “mkusanyiko wa vitabu vitakatifu”..kikiwa kitabu kimoja kinaitwa Biblion lakini vikiwa vingi vinaitwa Biblia..

Hivyo Biblia ni mkusanyiko wa vitabu 66 vitakatifu..Vitabu hivyo vimeandikwa na wanadamu, lakini kwa Uongozo wa Roho Mtakatifu, kwasababu Mungu anafanya kazi ndani ya watu..(Warumi 8:28), Wanadamu wachache Mungu aliowachagua waliandika habari za Mambo yahusuyo sheria za Mungu, Maneno ya Mungu, Uweza wa Mungu, Upendo wa Mungu, huruma ya Mungu, Utukufu wa Mungu, na Ukuu wa Mungu..

Bwana Mungu aliwachagua waandishi hao kutoka katika makundi yote, kwa nyakati tofauti tofauti..Iliandikwa na Wafalme, Manabii, Matabibu, Wavuvi wa samaki, Wakusanyaji wa kodi n.k

Biblia imegawanyika katika sehemu mbili:  Agano la Kale na Agano Jipya, au Agano la Kwanza na Agano la Pili..

Agano la kale lina jumla ya vitabu 39, na Agano la Jipya lina jumla ya vitabu 27 kufanya jumla ya vitabu 66 vya Biblia Nzima.

Kiini cha Biblia yote ni mtu mmoja tu anayeitwa YESU KRISTO, Kila kitabu katika Biblia Takatifu kimeandika kwa wazi au kwa kinabii, habari za Yesu Kristo. Maonyo na Mafundisho yaliyomo ndani yake ni maonyo ya Yesu Kristo Mwenyewe.

Biblia ndio kitabu pekee, kilichobeba sauti ya Mungu ndani yake..Hakuna kitabu kingine chochote duniani kilichobeba kusudi la Mungu juu ya mwanadamu zaidi ya Biblia Takatifu. Na hakuna njia nyingine yoyote mwanadamu anaweza kumfikia Mungu tofauti na kitabu hicho


Mada Nyinginezo:

SHETANI NI NANI?

SIKU YA HUKUMU ITAKUWAJE?

DINI NI NINI

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE


Rudi Nyumbani:

Print this post

KIFAA BORA CHA MATUMIZI.

Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, maandiko yanasema,

Mhubiri 10:10 “Iwapo chuma hakipati, wala mtu hakinoi; Ndipo hana budi kutumia nguvu zaidi. Walakini yafaa kutumia hekima, na kufanikiwa”.

Katika tafsiri nyingine hilo Neno Chuma limetafsiriwa kama shoka, ikiwa na maana kuwa kama shoka ni butu au halinolewi mara kwa mara basi itampasa mtu kutumia nguvu zaidi katika kukata vitu au kuchonga, au kuchanja kama anakata nyama itampasa atumie nguvu zaidi kuikata nyama ile, kama anakata mti basi itampasa atumie jitihada ya ziada yenye kuchosha kuudondosha mti kwasababu Shoka ni butu haliwezi kupenya kwa haraka ndani ya shina..Tofauti na kama kifaa hicho kingekuwa ni kikali, angetumia nguvu chache tu na matokeo kuwa makubwa ndani ya muda mfupi…

Ni kama tu kisu au kiwembe kikiwa ni kakali basi ukipitisha hata kwenye karatasi ni mara moja tu limegawanyika, lakini kama ni butu basi utakipeleka mbele na nyuma, na utachukua muda, na bado halitachanika vizuri kama lile lililochanwa na kiwembe kikali..

Lakini Mhubiri anaendelea kwa kusema, “walakini yafaa kutumia hekima, na kufanikiwa”,.. Ikiwa na maana usipoweza kutumia hekima, kuamua maisha yako kwa kukifanya kisu chako kuwa kikali basi mambo yako, licha tu ya kuwa magumu lakini pia utatumia nguvu nyingi kuyafikia…

Duniani Vipo visu vingi tofauti tofauti na mashoka tofuati tofauti na kila mtu analo lake, ambalo kwa namna moja au nyingine linamsaidia kufanya mambo yake kuwa mepesi, wengine ni elimu, wengine ni ujuzi, wengine ni fedha n.k..Lakini hasara moja ya vifaa hivyo vyote sio vya kudumu, huwa vinakuwa butu kwa jinsi muda unavyokwenda na kwa jinsi vinavyotumika…. Mtu akiviacha vinachakaa na pia isitoshe havitumiki kila mahali…huwezi kutumia elimu kutibu kifo, vile vile huwezi tumia pesa kununua furaha, au upendo au amani..

Ni kifaa kimoja tu ambacho Mtu mwenye akili na Hekima anaweza kukitumia kwa matumizi yote na kukata kila kitu pasipo kutumia nguvu, na bado kutokupungua ubora wake na makali yake…Nacho ni Neno la Mungu..

Waebrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.

13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu.”

Mtu akiwa na Neno la Mungu peke yake, hiyo ni salaha tosha, ya kurahisisha mambo yako..hili haliwi butu kama vile mengine, linao uwezo sio tu wa kukata kwa ukali zaidi ya upanga wowote, bali pia linaweza kuchoma hata kuzigawanya nafsi na roho, yaani linaingia ndani ya moyo wa mwanadamu na kugawanyisha kila kitu na kutambua mawazo yake, kitu ambacho pesa haiwezi kufanyi, elimu ya dunia hii haiwezi kufanya, ujuzi wowote ule wa mwanadamu hauwezi kufanya..

Ndio maana mtu yeyote aliyejaa Neno la Mungu ndani yake, hakuna jambo lolote linaloweza kumlemea hata liwe gumu kiasi gani kwasababu anafahamu vizuri silaha aliyonayo inaubora kiasi gani..

Mhubiri anatushauri NI HERI KUTUMIA HEKIMA NA KUFANIKIWA, tunapaswa tujue ni kifaa gani kitakachotufaa katika maisha yetu, katika mapori yanayotuzunguza mbele yetu ambayo yanapaswa yafyekwe kweli kweli, kifaa ambacho tunaweza kukabiliana na adui yetu ibilisi na kummaliza haraka sana bila kutumia nguvu nyingi… silaha hiyo si nyingine zaidi ya Neno la Mungu. Waefeso 6: 17 “Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;”

Tunapoliishi Neno la Mungu, maisha yetu hatutayaona ni magumu, hatutasumbuka kama ulimwengu unavyosumbuka, Kwani ni Mungu mwenyewe ndiye atakayekuwa anatupigania,,Lakini tunapoliweka Neno la Mungu kando, tunapolidharau na kuchagua mambo mengine, au kuyaona mambo mengine ni ya muhimu zaidi ya Neno lake, tuwe na uhakika kuwa safari yetu itaishia ukingoni…Ni kutumia kifaa butu, kuufyeka msitu…Mambo yatakuwa magumu tu, huo ndio ukweli, Nira iliyo nyepesi ipo kwa Bwana Yesu tu, pengine kote ni Nzito na mateso yasiyoelezeka..(Mathayo 11:28)

Ndugu/Kaka Ikiwa hujayakabidhi maisha yako kwa BWANA Mlango wa Neema upo wazi, usisubiri baadaye au kesho, muda umekwenda sana kama unyakuo hautakukuta moja ya hizi siku, hujui baadaye yako itakuwa vipi, waliokufa leo asubuhi sio kwamba walikuwa waovu zaidi yako wewe, au walikuwa wameshajiandaa kwa safari ya kwenda huko ng’ambo, hapana lakini kifo kiliwakuta kwa ghafla tu, na ndivyo kitakavyotukuta wote walio haki na wasio haki…Hivyo fanya uamuzi wa busara wakati huu kwa kutubu dhambi zako kama hujatubu na kumgeukia Bwana sasa hivi.. kumgeukia Bwana Yesu sio kuwa vuguvugu, ni kitendo cha kumaanisha kabisa….Kisha utafute mahali wanapobatiza ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi kwa Jina la YESU KRISTO, kama pia bado hujafanya hivyo..Upate ondoleo la dhambi zako, kulingana na (Matendo 2:38) ili Bwana akupe kipawa cha Roho wake Mtakatifu ambaye ndio muhuri wetu, Mungu anaotutia mpaka ile siku wa ukombozi wetu (Waefeso 4:30).

Bwana Azidi kukubariki.

Maran atha! Bwana wetu anakuja.


Mada Nyinginezo:

MUNGU WANGU,MBONA UMENIACHA?

USIWE SABABU YA WATU KUMKUFURU MUNGU.

LAANA YA YERIKO

NINI MAANA YA USIPUNGUZE WALA KUONGEZA NENO LA MUNGU?

JE! NI DHAMBI KUSHEREKEA SIKU YA KUZALIWA? BIRTHDAY!


Rudi Nyumbani

Print this post

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

Jina la Bwana YESU litukuzwe daima. Karibu tujifunze Neno la Mungu, leo kwa neema za Bwana tutajifunza juu ya njia sahihi ya kufunga.

Zipo aina nyingi za kufunga lakini kwa vyovyote vile, hatufungi ili Mungu atusikie au atujibu maombi yetu, Mungu hasubiri kwanza tuteseke ndio atusikie hapana kwani alishaweka wazi katika Neno lake, kuwa yeye anajua tunachohitaji kabla hata hatujamwomba (Mathayo 6:8)…Lakini pamoja na hayo Kufunga kunasaidia kuongeza uwezekano wa wewe kupata majibu ya maombi yako au kupata unachokitafuta kwa haraka tofuati na yule asiyefunga. Ni sawa tu na mwanafunzi anayesomea maktaba na Yule anayesomea nyumbani, anayesomea maktaba anaongeza uwezekano mkubwa wa kufaulu mitihani kuliko Yule anayesomea nyumbani, kwasababu kule maktaba kunakuwa na utulivu mkubwa na mazingira mazuri ya kujisomea kuliko nyumbani..Lakini hiyo haimfanyi afaulu mtihani moja kwa moja Yule wa nyumbani anaweza kufanya vizuri kushinda hata yeye..Lakini itampasa awe mtu wa kujitambua sana.

Vivyo hivyo na katika kufunga, Mtu mwenye desturi ya kuomba kwa kufunga anajijengea daraja zuri la yeye kuwasiliana na Mungu kuliko Yule apelekaye dua zake kwa Mungu bila kufunga, Kwasababu Kufunga kunampa utulivu Fulani wa Roho tofauti na mtu asiyefunga.

Na hiyo yote ni Kutokana na kutokuwa na Mungu katika mwili, au kutokumwona Mungu katika mwili ndio maana inatupelekea tumtafute Mungu kwa umakini zaidi kuliko kama tungekuwa tunamwona kwa macho…Mitume walipokuwa na Bwana duniani hakukuwa na sababu ya kufunga, ufunge ya nini wakati unayemtafuta upo naye hapo? Mpaka watu wengine wakashangaa inakuwaje hawa ni mitume wa Bwana lakini hawafungi, Ndipo Bwana alikawaambia wanachokifanya hawajakosea kwasababu mimi nipo, Siku zitakuja nitakapoondoka ndipo watakapofunga kama wengine…

Marko 2:18 “Nao wanafunzi wake Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga; basi walikuja, wakamwambia, Kwani wanafunzi wa Yohana na wanafunzi wa Mafarisayo hufunga, bali wanafunzi wako hawafungi?

19 Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kufunga maadamu bwana-arusi yupo pamoja nao? Muda wote walipo na bwana-arusi pamoja nao hawawezi kufunga.

20 Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana-arusi, ndipo watakapofunga siku ile.”

Hivyo kitendo cha kufunga hakikwepeki sasa kwa mkristo yeyote. Na zipo aina nyingi za kufunga, lakini aina iliyozoeleka ni ile ya kuacha kula chakula. Lakini mfungo huu unafanywa kimakosa na wengi kwasababu ya kutokufahamu ni kwanini mtu anaacha kula..Na ndio hapo mtu mmoja atafunga vizuri kweli hata wiki tatu au mwezi au siku arobaini, lakini anafanya kama desturi za dini nyingine wanavyofanya, ukiangalia huku nyuma utamwona anaendelea na maisha yake ya kidunia anadhani kusikia kule njaa ndo Mungu anampa thawabu,. Hajui kuwa Mungu hamjibu mtu kwa mateso,(Maombolezo 3:31-35) sasa hapo mtu wa namna hiyo kaamua tu kujitesa bure..Hakuna chochote atakachokipata kutoka kwa Mungu.

Au unakuta mwingine anafunga kwa lengo la kumuomba Mungu mambo ambayo sio sawa na mapenzi yake, mwingine atamwomba Mungu ampe mali, lakini ndani ya moyo wake anawaza aitumie kwa anasa, mwingine atamwomba Mungu ampe hiki au kile, lakini nia yake moyoni ni kutumia kwa mambo maovu.. mtu wa namna hiyo pia asitazamie kupata kitu.

Isaya 58:3 “Husema, Mbona tumefunga, lakini huoni? Mbona tumejitaabisha nafsi zetu, lakini huangalii? Fahamuni, siku ya kufunga kwenu mnatafuta anasa zenu wenyewe, na kuwalemea wote watendao kazi kwenu.

4 Tazama, ninyi mwafunga mpate kushindana na kugombana, na kupiga kwa ngumi ya uovu. Hamfungi siku hii ya leo hata kuisikizisha sauti yenu juu.

5 Je! Kufunga namna hii ni saumu niliyoichagua mimi? Je! Ni siku ya mtu kujitaabisha nafsi yake? Ni kuinama kichwa kama unyasi, na kutanda nguo za magunia na majivu chini yake? Je! Utasema ni siku ya kufunga, na ya kukubaliwa na Bwana?

6 Je! Saumu niliyoichagua, siyo ya namna hii? Kufungua vifungo vya uovu, kuzilegeza kamba za nira, kuwaacha huru walioonewa, na kwamba mvunje kila nira?

7 Je! Siyo kuwagawia wenye njaa chakula chako, na kuwaleta maskini waliotupwa nje nyumbani kwako? Umwonapo mtu aliye uchi, umvike nguo; wala usijifiche na mtu mwenye damu moja nawe?

8 Ndipo nuru yako itakapopambazuka kama asubuhi, na afya yako itatokea mara; na haki yako itakutangulia; utukufu wa Bwana utakufuata nyuma ukulinde.

9 Ndipo utaita, na Bwana ataitika; utalia, naye atasema, Mimi hapa. Kama ukiiondoa nira; isiwepo kati yako, wala kunyosha kidole, wala kunena maovu;

10 na kama ukimkunjulia mtu mwenye njaa nafsi yako, na kuishibisha nafsi iliyoteswa; ndipo nuru yako itakapopambazuka gizani; na kiwi chako kitakuwa kama adhuhuri.”

Unaona? Dhumuni la msingi kabisa la kujizuia kutokula mtu anapaswa afahamu ni kuyaleta mapenzi ya mwili chini na kuruhusu mapenzi ya Mungu yaje juu, ile njaa inakukumbusha kwenda mbele za Mungu kwa unyenyekevu mwingi , sikuzote mtu mwenye njaa anakuwa katika uhitaji sana kuliko mtu aliye shiba, hivyo mtu wa namna hiyo anapokwenda mbele za Mungu kumaanisha kwake kunakuwa kwa kiwango cha juu zaidi kuliko mtu aliyeridhika, hata maombi yake yanakuwa marefu sana, jaribu hata kwako utaligundua hilo..Na hiyo ndio faida kubwa ya kutokula wakati wa maombi. Hivyo inapelekea maombi yako kuwa na nguvu zaidi mbele za kuliko wengine.

Vile vile kuna kufunga ambako sio kwa kula, bali kwa kujizuia na mambo mengine yanayoweza kukusonga usiisikie sauti ya Mungu. Kufunga kwa namna hii kumekuwa kwa kawaida kwa watumishi wengi wa Mungu, Nabii Elisha ilimpasa atumie muda mwingi kujitenga na mazingira ya watu ili kudumisha joto la uhusiano wake na Mungu. Sio kwamba kuna shida kujihusisha na mambo ya kawaida ya kila siku, hapana lakini ni utaratibu wa Mungu kuzungumza katika sauti ya utulivu, na kama ni sauti ya utulivu hivyo naye huwa anahitaji mazingira tulivu ya kumwelewa.

Ufunuo wowote Mungu anaompa mwanadamu, hampi akiwa katika mazingira ya usumbufu wa akili, Usijidanganye kuwa Mungu atakupa ufunuo wowote katika hali ya masumbufu, kama utaisoma biblia na huku unasikiliza miziki ya kidunia, au huku una chat, au huku unafanya mambo mengine, Ni heri uifunge uje usome baadaye usiku peke yako…. inahitaji utulivu wa fikra na mawazo..Na hapo ndipo inakupasa ufunge baadhi ya vitu unavyovifanya, au ulivyozoea kuvifanya..Na kwa jinsi unavyovifunga kwa muda mrefu zaidi ndivyo unavyoongezeka uwezekano wa Mungu kusema na wewe kwa haraka na kwa mara nyingi zaidi.

Kufunga ni kuna faida kwasababu yeye mwenyewe anasema wote wafanyao hivyo huwapa thawabu kama hawatafanya kinafki na kwa nia mbaya..(Mathayo 6:16)

Ni ahadi yake kukulipa, Funga tu kwa kumaanisha kumsogelea Mungu zaidi, utapata zaidi ya kile ulichomwomba. Kuna mtu aliuliza swali je! Maandiko yanasema tunapaswa tufunge kuanzia saa ngapi hadi saa ngapi na ni kwa siku ngapi?..Jibu ni kuwa Biblia haijatoa masharti yoyote juu ya muda wa kufunga au siku za kufunga..Imezoeleka siku 3, siku 21 na siku 40 kwasababu ndio siku ambazo zimeonekana zikifungwa na wengi..Lakini hiyo haimaanishi kuwa nawe ufunge muda huo, ni vile Roho atakavyokuongoza na kulingana na aina ya dua uipelekayo kwa Mungu, unaweza ukafunga, siku moja, au wiki, au mwezi, au mwaka, na Mungu akaridhia, vile vile unaweza ukafunga saa 6 kwa siku, saa 12, au siku tatu bila kula, au siku 40 bila kula , ni vile tu Mungu atakavyokupa neema..Lakini vyovyote vile kufunga ni muhimu kwa kila mkristo. Na kuna manufaa na thawabu nyingi.

Ubarikiwe sana. Tafadhali “Share” Ujumbe huu kwa wengine. Na Bwana atakubariki.


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU

KAZI YA UZURURAJI WA SHETANI.

RUDIA, TENA NA TENA KUMWOMBA MUNGU USIKATE TAMAA.

NINI MAANA YA MSIMWITE MTU BABA DUNIANI?

KAINI ALIPATIA WAPI MKE?


Rudi Nyumbani:

Print this post

IPO NGUVU ITUVUTAYO KWA KRISTO, ITHAMINI!.

Kuna nguvu ya kipekee sana, inayoendelea duniani kote leo, hiyo inawavuta watu kwa Kristo, Nguvu hiyo ni nguvu ya Roho Mtakatifu, inazungumza mioyoni mwa watu, ikiwashawishi kuwavuta kwa Mungu. Nguvu hiyo ndio ile ile nguvu iliyokuwa inawavuta wale Wanyama kipindi cha Nuhu, waielekee Safina.

Kipindi kifupi kabla ya gharika kushuka juu ya nchi, ghafla tu Nuhu alianza kuona Wanyama wanasogea karibu na mahali Safina ilipokuwa inatenengenezwa, pengine kaamka asubuhi ghafla anaona simba wawili wakike na kiume wamelala pembezoni mwa kichaka Fulani kilichopo karibu na Safina ilipokuwepo, na wamekaa kama wanasubiri kuingia mahali Fulani hivi, halafu wamekuwa wapole jambo ambalo si la kawaida.

Mita kadhaa mbele pengine anaona tembo wamesimama kama vile wanahaja na kitu Fulani, nao hawana madhara…baada ya siku moja nyingine au mbili anaona chui, swala…na wote wakiwa na shauku ya kuingia ndani ya Hiyo nyumba yao mpya (safina). Kama vile kuku, au ng’ombe au mbuzi wanavyokuwaga na shauku ya kuingia mabandani mwao kila inapofika jioni..Giza linapoingia utaona kuku wamekusanyika mlangoni mwa banda lao wakingoja mlango ufunguliwe waingie…

Ndivyo ilivyokuwa kipindi kile cha gharika, shauku ya wale Wanyama kuingia ndani ya Safina, ilikuwa ni kubwa mpaka ikazima ukali wao, wote wakawa wapole wakitii na kusubiri amri ya kuingia ndani ya Safina.

Sasa ni nani aliowaongoza hao Wanyama mpaka wafike mlangoni mwa Safina?..je! walihubiriwa na watu kwamba kuna gharika inakuja hivyo wajiepushe?..Jibu ni hapana!…Kuna nguvu Fulani ndani yao iliyokuwa inawasukuma waende mahali ambapo ni salama Zaidi…Kuna mazingira Fulani yaliwafanya wahisi kuwa mwisho umefika na kuna mauti kubwa inakuja mbeleni(hukumu), na Zaidi ya hayo kuna kitu kiliwafanya pia wahisi kuwa kuna Maisha yataendelea baada ya hukumu hiyo, ili kuendelea kuishi hayo Maisha yanayokuja, daraja lake ni kutafuta hifadhi sasa.

Unajua hata watabiri wa vimbunga na matetemeko, wanatumia ishara ya Wanyama kutabiri maafa?..Endapo wakiona kuna tabia ya kipekee ya Wanyama imezuka mahali Fulani, labda ndege wote wameondoka mijini na kukimbilia milimani au mahali pa mbali, na wakati si jambo la kawaida, wanatangaza kuwa kuna janga litatokea siku si nyingi, hivyo watu wachukue tahadhari, na kweli baada ya kipindi Fulani kifupi labda wiki, mwezi au mwaka janga linatokea mahali hapo.

Kama Mungu, aliiachia hii nguvu ya wokovu hata kwa Wanyama (Warumi 8:19-22), si Zaidi wanadamu?…Hata sasa hii nguvu ipo, Wewe mwenyewe unajua ndani yako kuna nguvu Fulani inakushuhudia kwamba tunaishi siku za mwisho! Na kwamba siku moja mwisho wa mambo yote utafika, na ulimwengu utahukumiwa….Na hiyo nguvu haiishii hapo, inazidi kukushuhudia kwamba kutakuwa na maisha baada ya hukumu…Na pia haiishii hapo, inakusukuma kuifuata Safina mahali popote ilipo…Usiipuuzie hiyo sauti!!.

Nuhu wetu wa Sasa ni Yesu Kristo, Safina ni Neno lake, Wote aliopewa Nuhu walikwenda kwake kadhalika wote aliopewa Bwana Yesu na Baba walikwenda kwake na wanakwenda kwake sasa hivi..

Yohana 6:37 “Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe.

38 Kwa kuwa mimi sikushuka kutoka mbinguni ili niyafanye mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenipeleka”.

Yohana 6: 43 “Basi Yesu akajibu, akawaambia, Msinung’unike ninyi kwa ninyi. Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho”.

Muda unakwenda kwa kasi sana! Je! Hii nguvu bado ipo ndani yako? Au umeizimisha? Je! Kama ipo Umeikaribia Safina kiasi gani?..Umemkaribia Nuhu kiasi gani?, Jibu unalo..Fanya maamuzi thabiti kabla hazijafika siku za hatari, ambazo wengi watatamani waingie safinani na watashindwa…

Luka 13:23 “Mtu mmoja akamwuliza, Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache? Akawaambia,

24 Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.

25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;

26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.

28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje”.

Biblia inaposema kama zilivyouwa siku za Nuhu ndivyo itakavyokuwa siku za kuja kwake mwana wa Adamu, tunapaswa tujifunze pia tabia kama hizi, za kuvutwa safinani, vile vile tunapaswa tujue kuwa sio wanyama wote waliingia bali ni wachache..Vivyo hivyo leo hii wanaoitii hiyo sauti ni wachache,..Tujitahidi na sisi tuwe miongoni mwao, kwa kuitikia wito huo wa Mungu uitao mioyoni mwetu kila siku.

Tafadhali share na wengine

Bwana akubariki.


Mada Nyinginezo:

NUHU WA SASA.

FAHAMU KINACHOMGHARIMU MUNGU, KUTOA URITHI WAKE.

JE! MUNGU ATAIANGAMIZA DUNIA TENA BAADA YA GHARIKA YA NUHU?

MANENO HAYA YANA MAANA GANI? “..KWA SABABU HAMTOI ROHO KWA KIPIMO. (YOHANA3:34)

JE! MUNGU ANAUPENDELEO KWA WANAUME ZAIDI YA WANAWAKE?

JE! KUFANYA MASTURBATION (PUNYETO) NI DHAMBI?


Rudi Nyumbani

Print this post

JE! UKIMWI UNATIBIKA?

Kwanza ni vizuri kufahamu kuwa hakuna jambo lolote linaloshindikana hapa duniani,  lakini habari mbaya ni kuwa yapo mambo mengi yanayotushinda sisi wanadamu, na hiyo ni kutokana na kuwa kwa namna moja au nyingine tumekosa kujua njia sahihi ya kutatua matatizo hayo au wakati mwingine kukosa maarifa ya kutosha juu ya tatizo husika, kwa mfano watu wawili wanaweza kuumwa Malaria lakini mmoja akawa na ufahamu kuwa huu ni ugonjwa wa malaria, hivyo akaenda hospitali akapewa dawa akanywa akapona, na mwingine kwa kuwa hajawahi kufahamu au kusikia juu ya ugonjwa huo akadhani amelogwa akaenda kwa mganga, akaambiwa leta unyayo wa jirani yako, lakini mwisho wa siku akajikuta anakufa katika hali ile  ile, hiyo ni kwasababu alikosa maarifa ya kujua chanzo cha tatizo na njia sahihi  ya kulitatua..

Vivyo hivyo na magonjwa mengine yote yasiyotibika, kama vile ukimwi, kansa, Kisukari n.k. sio kwamba hayana tiba, hapana tiba yanayo ukimwi unatibika isipokuwa tu tumekosa maarifa ya kutosha ya kujua mahali pa kuyatatua na njia sahihi,..Na hiyo imetufanya tuhangaike huku na huko na mwisho wa siku tunaangamia…Madaktari wetu wanafanya kazi njema ya Mungu, lakini upo wakati ambao uwezo wao kutibu unafika kikomo, hivyo inahitaji mtu mwingine ambaye mwenye uwezo mkubwa zaidi ya yeye kukusaidia hapo.

Habari  njema ni kuwa yupo anayeweza kuyaondoa yote pasipo gharama yoyote na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO. Zipo shuhuda nyingi, na bado zitaendelea kuwa nyingi za watu wanaoponywa magonjwa hayo kwa damu yake. Anachotaka kwako sio tu kukuponya mwili wako lakini pia kuiponya roho yako, kwasababu hiyo ndiyo ya muhimu zaidi.

Kwani kuna makundi mawili ya watu wanaopatwa na matatizo haya, kundi la kwanza ni wale waliopata kutokana na dhambi zao, kwamfano mtu amekuwa mzinzi na mwasherati matokeo yake akapata Ukimwi, sasa watu wengi wa namna hii wakati mwingine wanataka Mungu awaponye, lakini hawezi kuwaponya kama hawatakuwa tayari kutubu na kuacha dhambi zao, kundi la pili, ni wale wanaopatwa kwa njia za kawaida tu sio kwa dhambi, sasa hawa kama mtu atakuwa bado yupo nje ya Kristo ni vizuri akaokoka na kama yupo ndani ya Kristo asiwe na wasiwasi Bwana atamponya tu.

Jambo ni moja tu ni kumwamini Bwana YESU..Kwasababu ndiye pekee aliyekufa kwa ajili yetu, hakuna kiongozi yoyote, au mtume yeyote, au nabii yeyote ambaye aliyewahi kuyatoa maisha yake makamilifu kwa ajili ya shida za watu wengine, hakuna haijawahi kutokea katika historia na wala haitakaa itokee, Ni mmoja tu ambaye ni YESU KRISTO. Yeye ndiye aliyeyachukua magonjwa yetu yote na madhaifu yetu.

Mathayo 8:16 “Hata kulipokuwa jioni, wakamletea wengi wenye pepo; akawatoa pepo kwa neno lake, akawaponya wote waliokuwa hawawezi,

17 ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu.”

Isaya 53:4 Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.

5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.

Wewe Unajuaje kuwa ni huyo huyo YESU ndiye aliyekupitisha katika ukurasa huu?, Ameona shida zako na magonjwa yako unayopitia kuwa muda mrefu, Hivyo usiogope leo hii ugonjwa huo utaondoka, Jambo la kwanza unalopaswa kufanya kama hajatubu basi tubu leo hapo ulipo kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi zako na kumwishia yeye, kwasababu hapo ulipo anakuona, na anakutazama, anajua kila kitu kilichopo ndani ya moyo wako, hivyo tubu makosa yako yote kwa kumaanisha ikiwa upo nje ya Kristo, na yeye atakusamehe, kisha baada ya maombi ambayo nitaomba na wewe muda si mrefu, ukatafute mahali wanapobatiza ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO ili ukamilishe wokovu wako, na baada ya hapo Mungu mwenyewe atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu.

Sasa nataka ufanya jambo moja hapo ulipo weka mkono wako wa kuume mahali pale unapoumwa,..kama ni mwili mzima au ndani ya damu weka mkono wako katika kifua chako.. Kisha Sema kwa sauti maneno haya kwa IMANI.

BWANA YESU, NAJA KWAKO, NINAKIRI KUWA WEWE NI BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NA TENA WEWE NI MPONYAJI WANGU, WALA SINA MPONYAJI MWINGINE ILA WEWE, UMEWAPONYA WENGI NA SHUHUDA ZAO KILA SIKU NINAZISIKIA NA KUZIONA MBELE YA MACHO YA WATU, NAMI LEO HII NATAKA UNIPONYE NA MIMI EE YESU MPENZI, NIMEONA KUWA HAKUNA MWINGINE ANGEWEZA KUNIPENDA KAMA WEWE ULIVYONIPENDA, KWA KUJITOA NAFSI YAKO, MAISHA YAKO, NA UHAI WAKO ILI MIMI NIPATE UKOMBOZI WA BURE, NA LEO HII NINAKIRI KUWA SITAKUACHA, NITATEMBEA NA WEWE SIKU ZOTE ZA MAISHA YANGU. ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPONYA.

AMEN.

Ikiwa umefuatiliza sala hiyo, sasa hapo ulipo jiangalie mahali ulipokuwa unaumwa, au nenda hospitali kapime, na huo ugonjwa ulionao utakuta umeshaondoka. Hivyo usiache kututumia shuhuda zako kwa namba hizi:

+255789001312

+255654555788,

Au kwa barua pepe hii:

email: watakatifuwasikuzamwisho@gmail.com

Pia unaweza soma shuhuda mbalimbali hapo chini zitakazokusaidia kujenga imani yako kwa Bwana.


 

Mada Nyinginezo:

USHUHUDA WA UPONYAJI WA UKIMWI.

USHUHUDA WA UPONYAJI WA KANSA.

NAMNA GANI NITAPOKEA NGUVU ZA BWANA YESU?

YESU MPONYAJI.

JE! NI KWELI BWANA ALIMAANISHA HATUTAONJA MAUTI KABISA TUKIMWAMINI?(YOHANA 11:25)

UNYAKUO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KAZI YA UZURURAJI WA SHETANI.

Biblia inatuambia tabia mojawapo ya shetani ni “kuzunguka zunguka”, na sikuzote tunajua mzungukaji huwa na tabia Fulani ya udadisi na hiyo inafanya mwisho wa siku kuwa na tabia ya kupenda kuteka pia, kwasababu mahali alipo anaona hapamtoshi na hivyo anaamua kutoka na kwenda kuchunguza chunguza maeneo mengine na huko huko akiona upenyo mdogo tu au fursa fulani huwa anaitumia ipasavyo kutimiza matakwa yake mwenyewe..Na ndio maana jina Mzungu, limetokana na Neno mzungukaji, watu waliotoka bara la ulaya zamani walikuwa wakizunguka zunguka nchi mbalimbali na mabara mbalimbali duniani ili kutafuta rasilimali kwa ajili ya nchi zao, Na walipofika maeneo kama Afrika, na kuona kuna kila kitu na vile vitu walivyokuwa wanavitafuta ndipo wakatua hapo, na kufanya yaliyo yao na hata kutumia fursa hiyo kuteka watu na kuwatawala…

Vivyo hivyo na shetani naye, ni mzungukaji kufanikiwa kwake kunategemea kuzunguka zunguka huku na huko duniani, anajua asipofanya hivyo kabisa hawezi kufanikiwa kuuimarisha ufalme wake, Tukisoma kwenye maandiko katika kitabu cha Ayubu tunaona wakati Fulani malaika wa Bwana walipokwenda kujihudhurisha mbele za Mungu, shetani naye alikwenda katikati yao, ndipo Mungu akamuuliza maneno haya..

Ayubu 1:7 “Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo”.

Unaona hapo, anasema duniani, ikiwa na maana kila kona ya dunia alikuwa anazunguka zunguka, inamaana hata katika kila taasisi, kila shirika, kila dini, na katika kila nchi, na ndio maana hatushangai kumwona shetani yupo hata katikati ya kanisa la Mungu. Na lengo lake kubwa sio kutalii, hapana bali ni kuchukua mateka, na kuharibu kile kinachoonesha dalili ya kuinuka na kufanikiwa kwa ajili ya Bwana..Ukitaka kujua ukali wa shetani na jinsi anavyomchukia mwanadamu kwa namna isiyokuwa ya kawaida angali tu kitu alichomfanyia Ayubu baada ya Mungu kuuondoa ule ulinzi wake kwake..

Utaona bila kupoteza muda alimletea radi, ikawapiga wale kondoo wake wote, akanusurika Yule mtu mmoja aliyemletea taarifa ambaye alimwambia nimeona moto wa Mungu umeshuka, ilikuwa ni radii ile, sio moto tu kama moto, Hata wewe vile vile anaweza kukutengenezea radi ikiwa tu upo nje ya ulinzi wa Mungu, yaani nje ya wokovu, hiyo ndio kazi inayomfanya azungukezunguke duniani.

Utaona tena Muda huo huo akaandaa majeshi ya maadui, yakawavamia wafugaji wake yakawaua wote, halafu yakaondoka na mifugo, vivyo hivyo hata wewe anaweza akakuundia tu kikundi cha vibaka wakati unakatiza usiku umetoka labda kwenye shughuli zako, wakakuvamia na kukuchoma visu wakaondoka na fedha zako na wewe ukafa saa hiyo hiyo ikiwa tu haupo ndani ya wokovu..

Wakati huo huo tena Shetani akamletea upepo wenye nguvu ukaipiga ile nyumba ikawaangukia watoto wake wote wakafa, hashindwi kukuletea kipunga hapo ulipo umekaa kwa amani, au mafuriko, na kukusababishia tu ajali ambayo chanzo chake hakieleweki, hata gesi tu kukulipukia nyumbani, hashindwi kukufanyia hivyo au shoti kutokea nyumbani au kung’atwa na nyoka tu njiani na habari yako ikawa imeishia hapo,..hashindwi kufanya hivyo vyote kwa mtu ambaye ulinzi wa Mungu haupo juu yake.

Utaona tena Shetani akimletea Ayubu mpaka magonjwa ambayo hajawahi kuumwa, Leo hii usijione unayo afya na bado upo nje ya wokovu ukadhani wewe unayo kinga kubwa zaidi ya wengine waliopo mahospitalini ndio maana huugui ugui ovyo, shetani anao uwezo wa kukutupia hapo hata kansa usijue imetokea wapi, au ugonjwa wa ajabu ajabu usiojulikana, na ukafa ndani ya siku tatu tu…

Hayo ndio matunda ya shetani ya kuzunguka zunguka kwake ni ili tu kutafuta mtu wa kummeza basi.. Na kumbuka lengo lake sio kukuangamiza tu halafu basi hapana bali ni anataka ufe haraka katika hiyo hali hiyo hiyo ya dhambi uliyonayo sasa ili uende kuzimu moja kwa moja hilo ndio lengo lake…kwasababu anajua akizidi kuchelewa pengine neema ya Mungu inaweza kukupitia ukatubu siku moja.

Na ndio maana Biblia inazidi kutuhimiza maneno haya..

1Petro 5:8 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.

9 Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.’’

Unaona ni jinsi gani shetani anavyokuchukia wewe uliye kwenye dhambi, kama sio huruma za Mungu tu kumzuia shetani tayari angeshakuangamiza siku nyingi…

Hivyo kama unahitaji kumruhusu leo Bwana aingie maishani mwako, utakuwa umefanya uamuzi wa busara, hapo ulipo tubu kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi zako zote, na kwamba unamaanisha kutokurudia yale yote maovu uliyokuwa unayafanya huko nyuma, Kisha mwambie Bwana Yesu nisamehe na nakukaribisha uje katika maisha yangu….Na ukishamaliza kumweleza mambo hayo yote kwa kumaanisha kabisa, hatua inayofuata tafuta mahali ukabatizwe ili kukamilisha wokovu wako, kumbuka ubatizo ni muhimu, na ni maagizo ya msingi kwa yeyote aliyempokea Bwana, Usipuuzie, ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi ni wa kuzingatia na uwe ni kwa jina la BWANA YESU KRISTO sawasawa na maandiko haya (Matendo 2:38, 8:16, 10:48, 19:5).

Hivyo ukikamilisha hayo, Bwana mwenyewe atakupa Roho wake Mtakatifu, naye atakaa na wewe milele kukulinda dhidi ya Yule adui azururaye huko na huko, mpaka ile siku ya mwisho ya kwenda mbinguni itakapofika.

Bwana akubariki.


Mada Nyinginezo:

ANGUKO LA UFALME WA SHETANI:

ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

UNALITUMIA KWA HALALI NENO LA KWELI?.

NJAA ILIYOPO SASA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU


Rudi Nyumbani:

Print this post

SIKU YA HUKUMU ITAKUWAJE?

Shalom mtu wa Mungu, karibu tujifunze Maandiko..Biblia inatuasa tuwe tunajikumbusha kila siku yale ambayo tumeshajifunza ( 2 Petro 1:12-13, Yuda 1:5), hiyo itatusaidia kutompa nafasi shetani kuziiba zile mbegu ambazo zilishapandwa ndani yetu tayari…Leo kwa Neema za Bwana tutajikumbusha ni kwa jinsi gani Ulimwengu utahukumiwa na watakatifu.

Ni jambo la kufurahisha kuona bado kuna watakatifu ulimwenguni, watu wanaojitunza na kumweshimu Mungu, kwa viwango vya juu…kuona bado kuna watu wanamcha Mungu, kuna wanawake na wanaume wanaojiheshimu, kuona kuwa bado kuna watu ni wapole, ni wasomaji na watendaji wa Neno, ni wavumilivu, wasikivu, wenye huruma, wasiolipiza kisasi, wenye mioyo ya Toba, na wenye kuwahurumia wengine n.k Haijalishi watakuwa ni wachache kiasi gani, lakini uwepo wao tayari ni Tiba kubwa kwa ulimwengu.

Jambo lisilojulikana na wengi ni kuwa Uwepo wa Watakatifu duniani leo hii, ndio unaosababisha ulimwengu usiangamizwe…Bwana akitazama katika mji mmoja na kuona maovu yaliyomo ndani ya huo mji, na akaona huko watakatifu watano, basi huo mji wote unaweza ukasalimika kwasababu tu ya hao watakatifu watano waliopo ndani ya Huo mji. Na siku maangamizi ya Huu ulimwengu yatakapokuja Bwana atakuwa ameshawaondoa watakatifu wake kwa kuwanyakua, haiwezekani kuwaangamiza watakatifu wake pamoja na waovu. Ndio maana utaona Bwana alitamani kuuhurumia mji wa Sodoma na Ghomora endapo tu angekuta huko watu kumi tu walio wakamilifu, lakini hawakuwepo hata hao kumi..Na zaidi ya yote, hata Lutu huyo mmoja aliyesalia walimdharau. Na hivyo kujisababishia maangamizi yao….Hiyo ndiyo Neema wanayoibeba watakatifu waliopo katika ulimwengu sasa…

Lakini katika upande wa pili wa shilingi, Uwepo wa Watakatifu mahali fulani pia ni Ishara mbaya kwa ulimwengu…Kwasababu hao hao watakatifu ambao kwa kupitia wao Mungu anairehemu dunia, hao hao siku ya Hukumu watauhukumu Ulimwengu. Biblia inasema hivyo katika

1 Wakorintho 6:2 “Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu?……”

Sasa utauliza Watakatifu wataihukumu vipi dunia?..Na nafasi ya Bwana Yesu ya kuhukumu itakuwa ni ipi Kama watakatifu wataihukumu dunia?, Na pia inawezekanikaje siku ile mtu amhukumu ndugu yake ambaye alikuwa anamfahamu?.

Kuelewa Hukumu itakuwaje siku ile, hebu tafakari mfano ufuatao.

Mwalimu alikuwa na darasa lake la wanafunzi 10 la wanafunzi wa Bweni, akawafundisha kwa mwaka mzima, kisha mwisho wa mwaka akawapa mtihani, wawili kati ya hao 10 walipata alama ‘A’ na nane kati yao wakapata alama ya mwisho kabisa ‘F’. Mwalimu akafurahi kuona amepata wanafunzi wawili waliofaulu vizuri, lakini akahuzunika kuona Zaidi ya robo tatu wamefeli na kupata alama ya mwisho kabisa ‘F’…tena miongoni mwa hao waliopata F kuna wengine wamepata sifuri kabisa. Akawapatia zawadi wale wawili, kwa kuwapandisha daraja la juu na wale 8 akawapa barua ya kuwafukuza shule.

Lakini wale waliofukuzwa wakaanza kumlalamikia kwanini tumefukuzwa…Mwalimu akawaambia ni kwasababu mmefeli mtihani, wakaanza kila mmoja kulalamika…oo ni kwasababu Umetoa kitu ambacho hujatufundisha, wengine wakasema oo ni kwasababu mazingira ya shule hayakuwa mazuri, wengine wakasema oo ni kwasababu chakula kilikuwa kibovu kila siku mlo ule ule tu! Ndio maana tukashindwa kula vizuri na kupelekea kufeli, wengine wakasema tunaomba utupe nafasi ya pili.

Mwalimu akawauliza swali moja wote! Je! Hao waliopata alama ‘A’ hawakuwa kwenye mazingira kama hayo hayo ya kwenu? Ndio mwalimu akaamua kumuita mmoja wa hao waliopata alama ‘A’ mbele yao na kuanza kumhoji na kumwuliza…

Je! Wewe ulikuwa unakula chakula kizuri sana tofauti na hawa ndio ikakusababishia kufaulu, yule akajibu hapana mwalimu, nilikula chakula kimoja na hao, isipokuwa mimi nilikuwa sio mnung’unikaji kama wao nilijua tu hapa shuleni napita hivyo nilivumilia tu shida za kitambo hizi na nikaweka jitihada yangu yote kwenye masomo…akaulizwa tena je! Ulikuwa unalala kwenye kitanda kizuri Zaidi ya wengine, akasema hapana!..akaulizwa na swali la mwisho je! Katika mtihani uliofanya ulikutana na swali ambalo mimi sikuwahi kuwafundisha darasani?…akasema hapana! Maswali yote uliyoyatoa uliyafundisha darasani ndio maana mimi nimeweza kuyajibu mengi ya hayo kifasaha..

Baada ya mwalimu kumwuliza hayo maswali, akawageukia wale wanafunzi 8 waliofeli akawaambia..mnasikia anachosema mwenzenu?..Huyo ndiye anayewahukumu sio mimi…mlilala wote pamoja, mlikula wote chakula kimoja, wote mlikuwa darasa moja…lakini tofauti yenu ni kwamba ninyi hamkuwa makini na shule, na pia hamkujua kilichowapeleka shuleni ndio maana mkafeli kwahiyo ni haki yenu kufukuzwa shule. Kwasababu mlipitia mazingira sawasawa na ya wenzenu waliofaulu lakini nyinyi hamkuzingatia, mlipaswa mvumilie na kujituma kama wenzenu hata kama chakula kilikuwa ni mlo mmoja kila siku. Wale wanafunzi walikosa cha kujitetea na wakaondoshwa shuleni.

Ndugu yangu ndivyo itakavyokuwa siku ile ya Hukumu, Bwana atawahukumu wenye dhambi wote kulingana na matendo yao mbele ya kile kiti cheupe! Atawaambia wamefeli mtihani wa haya Maisha, na hivyo watashushwa daraja la chini (ambalo ni ziwa la Moto), Majina yao hayataonekana katika Kitabu cha uzima hivyo wataondolewa mbele yake, Kwasababu kila mtu sasahivi anafanya mtihani wake na kuandika kitabu chake…Na wengi watakaosikia hiyo hukumu wataanza kulalamika kuwa wanaonewa, wengine watasema Ulimwengu ulikuwa umejaa vishawishi tungewezaje kushinda! Wakubwa kwa wadogo, matajiri kwa maskini, kila mtu ataanza kutoa malalamiko yake..Ndipo yule aliyeketi katika kile kiti cha hukumu, atawaita watakatifu walioshinda ulimwenguni na kuwahoji mbele yao. Na hao waliohukumiwa watakosa cha kujitetea mbele yao, Kwahiyo wataenda kwenye lile ziwa la moto kwa huzuni na majuto makubwa, wakijua kuwa ni kweli wamestahili.

Ndugu wakati leo hii unaona wapo watakatifu wanaojituma kweli katika Mungu, hao sio ishara nzuri kwako, siku ile ya Hukumu watakuhukumu…Utasema Bwana mbona ilikuwa ni ngumu sana mimi kuacha uasherati kwenye kizazi changu ambacho kila kona ya barabara nilipishana na wanawake wapo nusu uchi? Nikifungua tv, internet, radio nakutana na mambo yavishawishi vya uasherati? Bwana atamleta mmoja ambaye alikuwepo kwenye hicho hicho kizazi chako, ambaye naye pia alikuwa anapitia majaribu kama ya kwako na hata pengine Zaidi hata na hayo yako kama vile Yusufu na akashinda uasherati na wewe utakosa cha kujitetea siku hiyo..

Utasema mbona mimi nilikuwa mzuri sana ningewezaje kushinda vishawishi mahali ambapo kila kona watu walikuwa wananitaka?..simalizi hatua mbili kila mwanamume ananijaribu? Siku ile watasimamishwa waliokuwa wazuri kuliko wewe mfano wa Sara katika kizazi chako, na pamoja na kwamba walikuwa ni wazuri sana, lakini walishinda vishawishi, na kujihadhari na ulimwengu, utakosa cha kujitetea siku ile.

Utasema nitawezaje kutubu na kumgeukia Kristo ninaposikia injili, si kila mtu atanicheka na kuniona mwendawazimu, nitawezaje kuacha Imani yangu na dini yangu, na dhehebu langu nililolizoea? Na kutubu na kumgeukia Kristo kikamilifu?…Biblia inasema katika Mathayo 12: 41 “Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona”

Utasema tena Bwana mimi nilikuwa ni Tajiri sana, nilikuwa ni Mkuu wa Wilaya, ningewezaje kupata muda wa kukutafuta wewe?..Siku ile watasimamishwa waliokuwa matajiri kuliko wewe katika wakati wako na katika utajiri wao wote walimtafuta Mungu na kujiepusha na ulimwengu. Biblia inasema katika..

Mathayo 12: 42 “Malkia wa kusini atasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, naye atawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu yeye alikuja kutoka pande za mwisho za dunia ili asikie hekima ya Sulemani, na hapa yupo aliye mkuu kuliko Sulemani”

..Malkia anasafiri maelfu ya Maili…kwenda kuitafuta Hekima ya Mungu, wewe Balozi wa nyumba kumi huna muda! Siku ile hutakuwa na la kujibu.

Kwahiyo uonapo! Mtu mwema anafanya wema katika mazingira yasiyostahili wema..usiishie kufurahia tu! Bali pia Ujiulize nawe pia unafanya wema kama yeye katika mazingira kama yake?..Kwasababu kama hufanyi hivyo siku ile hutakuwa na cha kujitetea, na wala hutapata mtetezi…Dada uonapo kuna mwanamke mzuri kuliko wewe anavaa kwa kujisitiri pamoja na uzuri wake wote..usifikiri utakuwa na cha kujitetea siku ile ya hukumu mbele za Mungu, utaelekea kwenye Ziwa la Moto, na utasema ni kweli umestahili.

Unapoona kuna watu wanamtafuta Mungu katika kizazi chako cha uovu..Usiishie kufurahia tu! Na kusema nakushukuru Mungu!…Tambua kuwa kitendo wafanyacho huko mbeleni kitakuja kugeuka kuwa mashitaka kwa wasiomtafuta Mungu katika kizazi hicho hicho kigumu.

Bwana akubariki sana. Ni matumaini yangu kuwa umepata kitu, kama hujampa Kristo Maisha yako, mlango wa Neema haujafungwa, lakini siku si nyingi utafungwa, watakatifu wataondolewa duniani na kunyakuliwa juu mbinguni, na dhiki kuu kuanza duniani. Je! Bado ni vuguvugu?..bado unaupenda ulimwengu na anasa zake! Shetani anakudanganya kuwa hakuna watu wanaomcha Mungu duniani leo?…usidanganyike Mungu ana watu wake kila mahali, shetani anachotaka ni wewe uendelee kufikiri hivyo ili siku ile ya hukumu, uhukumiwe vizuri na Maisha ya watakatifu waliopo leo duniani.

Baada ya kutubu kama ulikuwa hujatubu, ni Ubatizo, ubatizo sahihi ni ule wa kuzama mwili wote katika maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu.


Mada Nyinginezo:

KUNA HUKUMU ZA AINA NGAPI?

KUNA UFUFUO WA AINA NGAPI?

UTAWALA WA MIAKA 1000.

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

WAFALME WATOKAO MAWIO YA JUA.

NYOTA ZIPOTEAZO.


Rudi Nyumbani:

Print this post