Category Archive Home

KUOTA UNA MIMBA.

Usipokuwa na uelewa wa kutosha  juu ya ndoto, unaweza ukajikuta unatoka nje ya kusudi la Mungu ambalo amekukusudia wewe uishi kwalo hapa duniani..

Na hiyo imewafanya watu wengi wazunguke huko na huko, kutafuta tafsiri ya ndoto zao..Lakini jambo la kwanza na la msingi sana kufahamu ni kuwa, tunapaswa kujua kuwa ndoto yoyote ni lazima iwepo katika mojawapo ya  makundi haya matatu:

> Kundi la kwanza ni ndoto zinazotokana na Mungu,

> Kundi la Pili ni ndoto zinazotokana na shetani,

> na kundi la tatu ni ndoto zinazotokana na mtu mwenyewe.

Sasa ndoto hizi zinazotokana na mtu mwenyewe huwa zinaathiriwa sana na mambo mbalimbali aidha kutokana na mazingira ya mtu yanayomzunguka au shughuli anazozifanya mara kwa mara,  au mambo anayoyawaza kila wakati..Na aina hii ya ndoto ndiyo inayochukua asilimia kubwa sana ya ndoto watu tunazoziota kila siku, naweza kusema hata asilimia 95 ya ndoto tunazoziota kila siku na hizi huwa hazina maana sana, lakini watu kwa kukosa ufahamu imefanya wahangaike kutwa kuchwa kutafuta tafsiri ya kila ndoto yanazoziota mpaka inawafanya kuwa watumwa wa ndoto…Kumbe kiuhalisia sio kila ndoto ina ujumbe wa kutufaa..

Hivyo mtu akishakuwa na uelewa wa namna ya kuzigawanya ndoto hizi katika makundi haya hatapata shida kuitafsiri ndoto yake..Hivyo nakuashuri pitia kwanza somo hili kisha ndio tuendelee.  >> NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI? 

Sasa ukiota una mimba: Ikiwa ndoto hiyo haitokani na shughuli zako mwenyewe au mazingira yanayokuzunguka, au mawazo unayoyawaza kila mara, kwasababu kumbuka ndoto kama hizi huwa zinawatokea mara nyingi wanawake, kwahiyo uwezekano wa kuangukia katika  kundi hilo la tatu la ndoto ni mkubwa kwasababu wanawake maisha yao tangu wakiwa watoto wanawaza siku moja ni kuwa na mtoto kwahiyo kuota wamebeba mimba si jambo la kushangaza, au utakuta mwingine maisha yake yote anatamani sana kuwa na mtoto, hana watoto, moja kwa moja mtu kama huyo ni rahisi kuota ni mjamzito au mwingine utakuta anaishi na mwanamke mjamzito  karibu na mazingira yake au jana amemwona mwanamke mmoja barabarani akipita akiwa mjamzito akajikuta usiku anaota kabeba mimba akadhani kuwa ndoto hiyo inamaana sana kwake..,

Ikiwa ni hivyo, basi zipuuzie tu, ni ndoto zinazokuja kutokana na mawazo yako. Hizo hazibebi ujumbe wowote kwako.

Lakini hapa tunadhania kuwa ndoto hiyo haijatoka katika vyanzo vya namna hiyo, 

Sasa fahamu kuwa tendo lolote kuchukua mimba liwe ni jema au liwe ni baya, liwe limekuja kwa  njia ya uzinzi au kwa njia ya haki ni lazima tu kiumbe kipya kije duniani mwisho wa siku hakuna namna!..Na kabla hakijaja lazima dalili Fulani zionekane…Hivyo kama ndoto yako  imekuwa ni ya kujirudia rudia basi itilie maanani zaidi kwasababu inaweza kuwa imebeba ujumbe kutoka kwa Mungu,..

Utakumbuka Farao alipoota ndoto ile ihusuyo miaka saba na njaa na miaka saba ya neema, ilikuja mara mbili, hata kama ilichukua taswira nyingine lakini ujumbe ulikuwa ni mmoja..ndipo akawa na uhakika wa kuwa ndoto ile ni ya kuizingatia..Vivyo hivyo na wewe ikiwa unaota mara kwa mara una mimba, ni mjamzito izingatie sana ndoto hiyo.

Kwahiyo jambo unalopaswa kufanya hapo kwa kuwa wewe ndiye unayeyafahamu maisha yako zaidi kuliko mtu mwingine yeyote , kaa chini kwa utulivu mwingi utafakari maisha yako na njia yako unayoiendea sasa hivi..iwe ni katika huduma yako, iwe ni katika familia yako, iwe ni katika shughuli yako unayoifanya sasa, kuna uamuzi uliuchua, au kuna jambo ulilifanya  ambalo hivi karibuni utakwenda kuona matokeo yake..

Hivyo kama ulimwomba Mungu juu ya kitu Fulani, kwa muda mrefu akupatie basi kaa katika matarijio ya kukipata, au kama ulijitaabisha katika kitu ambacho kwasasa faida yake haionekana kaa katika matarajio ya kukipata muda si mrefu..

Sara alikuwa katika matarajio ya kupata mtoto kwa muda mrefu, lakini wakati ulipofika malaika alimjia na kumwambia panapo wakati kama huu mwakani utalea mtoto..VIvyo hivyo na wewe kama upo katika mstari ulionyooka na Mungu wako basi tarajia Mungu kukupa kile ulichokuwa unakitafuta. Kwasababu mimba sikuzote ni matokeo ya ile mbegu iliyoingia ndani yako..Kama ni mbegu njema uliipanda basi utavuna kilicho chema.

Vile vile kama ulikuwa ni mwovu unafanya mambo yasiyompendeza Mungu nawe pia kaa katika matarajio ya kukipata hicho ulichokuwa unakifanya, ikiwa ulikuwa mchawi jiandae kuvuna matunda ya uchawi wako, ikiwa ulikuwa ni tapeli au mla rushwa jiandae kukumbana na ulichokihangaikia, kama ulikuwa ni mrushi vile vile jiandae kukutana na malipo yake hivi karibuni…

Usishangae kukutana na mabaya, kwasababu biblia inasema dhambi nayo huwa inapitia hatua hizo hizo mpaka kufikia mauti.

Yakobo 1:14 “Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.

15 Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.”

Zaburi 8:14 “Tazama, huyu ana utungu wa uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.”

Isaya 59:3 “Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong’ona ubaya.

4 Hapana adaiye kwa haki, wala hapana atetaye kwa kweli; hutumainia ubatili, hunena uongo; hupata mimba ya madhara, na kuzaa uovu.”

Hivyo kama unatenda maovu sasa, acha mara moja, Tubu dhambi zako, umegukie muumba wako YESU KRISTO kabla huo wakati wa mabaya haujafika, lakini kama unajijua upo katika njia iliyonyooka na umekuwa katika dua ya kumwomba Mungu kwa ajili ya kitu Fulani chema..Basi kuwa katika matarajio ya kukipata siku za hivi karibuni.

Ubarikiwe.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

USHUHUDA WA RICKY:

MTETEZI WAKO NI NANI?

KUOTA UNAPEWA PESA.

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Mtakatifu ni Nani?

 JIBU: Tafsiri ya kibiblia ya MTU MTAKATIFU ni tofauti na tafsiri ya kiulimwengu.
 
Ulimwengu unatafsiri Mtu mtakatifu ni mtu yeyote anayetenda matendo mema! mtu asiyetenda dhambi!..mtu anayekubalika na asiye na mawaa,
 
Lakini Biblia haitafsiri hivyo, kwasababu hakuna mwanadamu yeyote anayeweza kusimama mbele za Mungu kwa Matendo yake, na kujigamba mbele zake, wanadamu wote tunatenda dhambi kwa namna moja au nyingine aidha kwa kujua au kwa kutokujua. Na hivyo wakati unapojiona upo sawa, kumbe haupo sawa..wakati unajiona ni msafi kumbe ni mchafu n.k
 
Sasa Biblia inamtaja mmoja tu ambaye hakuwa na dhambi hata moja na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO peke yake! huyo ndiye biblia imemtaja kuwa mtakatifu, kwasababu alizaliwa bila dhambi na aliondoka duniani bila dhambi hata moja. Huyo peke yake ndiye anayeweza kusimama mbele za Mungu kwa matendo yake. Na ndiye pekee Mungu anayemwangalia kuwa ni Mtakatifu. Wengine wote tumetenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
 
Warumi 3: 23 “kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;
24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu”
 
Sasa Kwa kupitia huyo sisi wengine tutakaomwamini yeye ndio tutahesabiwa kuwa ni watakatifu,. Kama mtu yeyote hatakuwa ndani ya YESU hawezi kuonekana mtakatifu mbele za Mungu, hata kama anajiona ni mkamilifu kiasi gani, hata kama atatenda matendo ya haki kiasi gani…mbele za Mungu ni kama Uchafu tu!
 
Yesu ni kama vazi letu la nje sisi tulio wachafu! Ukimvaa Yesu mbele za Mungu hakuoni wewe, bali anamwona Yesu mwanawe ambaye ni Mtakatifu, hivyo na wewe unaonekana mtakatifu kwa ajili yake. Hiyo ndio maana ya NEEMA, Tunahesabiwa HAKI (yaani tunahesabiwa kuwa watakatifu) bure kwa njia tu ya kumwamini YESU KRISTO. Hapo ndipo mtu unaouna umuhimu wa YESU kuja duniani, Kwahiyo watakatifu ni wale walio ndani ya YESU tu!.
 
Hivyo wale wanaosema duniani hakuna watakatifu, ni kweli kwa mtazamo wa kibinadamu, lakini kwa mtazamo wa Mungu duniani wapo watakatifu maandiko yanatumabia hivyo katika:
 
Zaburi 16:3 “Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao”.
 
Na hawa ndio wale wale wote walio ndani ya YESU KRISTO.
Sasa utauliza! Ina maana tukiwa ndani ya Yesu hata kama tukitenda dhambi za makusudi, tutazidi kuonekana NI watakatifu mbele za Mungu? jibu ni la! hakuna mtu yeyote aliye ndani ya Kristo, akawaza tena kutenda dhambi za makusudi, hakuna mtu aliye ndani ya Kristo akafanya uasherati, au akalawiti au akaua..ukiona mtu anatenda dhambi za Makusudi huyo bado hajawa ndani ya YESU, bado ni wa Ulimwengu. (Soma 1Yohana 3:9 na Warumi 6:1-2 )..
 
Kwasababu mtu yeyote aliyempokea YESU huwa anapokea hapo hapo kipawa cha Roho Mtakatifu, ambaye huyo kazi yake ni kumwongoza, kumfundisha na kumpasha habari ya mambo yote..kwahiyo mtu wa namna hiyo moja kwa moja atajikuta anatamani kupiga hatua mbele kila siku kuelekea ukamilifu na sio nyuma…Hata ile tamaa ya kufanya dhambi huwa inakufa yenyewe ndani yake, na hivyo hawezi kutenda dhambi mwenyewe za makusudi.
 
Ubarikiwe.

 


Mada Nyinginezo:

JEHANAMU NI NINI?

MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?

ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU.

USITAFUTE FAIDA YAKO MWENYEWE BALI YA WENGINE.

NJAA ILIYOPO SASA.

JIKANE NAFSI MTEULE WA MUNGU.


Rudi Nyumbani:

Print this post

CHAGUA UPANDE WA UZIMA.

Kama ukichunguza kwa makini, utaona Mungu kaumba kila kitu katika sehemu kuu mbili…Kwamfano utaona mtu katengenezwa kwa vipande viwili, kushoto na kulia, na vipande hivyo vinafanana..kila kimoja ni taswira ya mwenzake….Mkono wa kushoto unafanana na mkono wa kulia..lakini kimaumbile upo kinyume na mwenzake kadhalika mguu wa kushoto kimaumbile ni kinyume cha mguu wa kulia…
 
Na pia ukitazama, kuna pande mbili za mwangaza…Kuna upande wa Nuru, na upande wa Giza, hivi navyo kila kimoja ni kinyume na mwenzake…Ndio maana urefu wa usiku ni sawa na wa mchana.
 
Lakini pia zipo pande mbili nyingine zilizo pacha zenye sehemu kubwa sana katika maisha…ambazo nazo zinafanana isipokuwa kimaumbile ni kinyume na mwenzake…nazo si nyingine Zaidi ya UZIMA na KIFO. Hivi vitu viwili ili Maisha yawe na maana ni lazima viwepo. Wengi hawafahamu kuwa Kifo ni sehemu ya uumbaji wa Mungu…Na kifo Mungu hakukiumba kwa bahati mbaya au kwa makusudi mabaya…Wala giza Mungu hakuliumba kwa madhumuni mabaya…Giza Lilivyoumbwa lilikuwa na kazi yake maalumu ya kiMungu na takatifu….Kadhalika Kifo kilivyoumbwa kilikuwa na kazi yake ya muhimu na takatifu, kifo kisingekuwepo Maisha yasingekamilika hapa duniani…Ni kama tu mkono wa kushoto ulivyoumbwa!…huwezi kusema mkono wa kushoto hauna kazi yeyote katika mwili wako, au mguu wa kushoto! Kadhalika Kifo kiliumbwa kwa kusudi maalumu..
 
Kifo kisingekuwepo, zile mboga na zile mbegu za matunda Adamu na Hawa walizokuwa wanakula pale bustanini zingemea tumboni mwao, kwasababu zingekuwa bado na uzima, hivyo ilimpasa aliue kwanza lile tunda kwa kulichuma kutoka katika shina la mti kisha alile lote…kadhalika Adamu na Hawa wasingeweza kuilima na kuitunza bustani ambayo Mungu aliwaambia waiilime na kuitunza, kwasababu hata nyasi ambazo wangezilima, zingekuwa mbichi vile vile daima, zisingekauka, na kufa na kupotea… hivyo miti na nyasi zingeendelea kuota duniani na dunia nzima ingekuwa ni misitu tu, ambayo inaendelea kuota na kuota, hata maana ya kulima ingekuwa haipo tena…
 
Kwahiyo ili kuweka usawa..dunia iweze kujisafisha na kulimika na kutunzika, Bwana Mungu alikiumba Kifo… kwamba ni lazima vitu vingine vife ili viache nafasi ya vingine vipya kuja lakini kwa utaratibu…kuwe na mzunguko wa namna hiyo…mti atapata uzima, lakini utapata pia kifo pia..n.k
Sasa Mwanadamu hakuumbiwa hicho kifo tangu Edeni, yeye alipoumbwa alipewa zawadi ya upande mmoja tu wa UZIMA. Kwamba ataishi milele…Lakini baada ya anguko Adamu na Mkewe Hawa, kuvunja maagizo ya Mungu…Kifo nao kikawaingia ambacho hakikupasa kiwe kwao, uzio ukaondoka wa wao kutopenya upande wa kifo…jambo ambalo halikuwa mpango wa Mungu…kwamba Mwanadamu aje na kupita…hivyo nao wakawa wanakufa kama mimea.
 
Lakini Yesu Kristo alipokuja, kwa kupitia Msalaba alikikomesha kifo…alisema katika
Yohana 11:25 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; 26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele”.
 
Na Yesu Kristo huyo huyo ndio NJIA YA UZIMA..Hakuna mwanadamu yeyote, wala mungu yeyote anayeweza kutibu kifo! Wala awezaye kumfufua mtu…usidanganyike kwamba kuna mungu wa dini yeyote duniani, ambaye anaweza kutoa tumaini la ufufuo wa wafu! Hakuna! Ni Yesu Kristo pekee, ambaye alikufa na akafufuka! Huyo ndiye anayeweza kufufua wafu na kukikomesha kifo…Yeye peke yake ndiye aliyetabiriwa kuwa atamweka adui wa mwisho chini ya miguu yake, ambaye adui huyo ni mauti. (1 Wakorintho 15:25-26).
 
Na hakuna namna yeyote tunaweza kuishi katika haya Maisha kama hatutakuwa na uhakika wa UZIMA WA MILELE…hivyo huu ni wakati wetu wa chagua uzima au mauti, lakini kumbuka Itatufaidia nini tuwe matajiri wa kupindukia, halafu tujue baada ya miaka 70 tunakufa! Na biashara yetu itakuwa imeishia hapo?…Ni heri kutafuta kwanza uzima wa Milele, na hayo mengine yatakuja…Ni heri sasa kutafuta mabilioni na mabilioni ya miaka isiyoisha ya kuishi…na hayo mengine nitayafanya nikishapata hayo mabilioni ya miaka isiyoisha…ndani ya hayo mabilioni ya mamiaka nitakuwa na muda wa kutosha pengine hata kutafuta hizo mali, kama kutakuwa na kutafuta mali…Lakini kutafuta mali na huku nina miaka 70 tu ya kuishi na baada ya hapo ni ziwa la moto! Hiyo sio akili wala hekima.
 
Tafuta uzima wa milele! Ambao huo unapatikana kwa Yesu Kristo pekee! Baada ya kifo.
 
Bwana akubariki sana.

Mada Nyinginezo:

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

JE, KAMA HAUNA UBATIZO SAHIHI HAUWEZI KUWA NA ROHO MTAKATIFU?

SANDUKU LA AGANO LILIKUWA LINAWAKILISHA NINI KATIKA AGANO JIPYA?

BWANA YESU ALIKUWA NA MAANA GANI KUSEMA CHAKULA CHA WATOTO USIWAPE MBWA KATIKA MATHAYO 15:21-28?


Rudi Nyumbani:

Print this post

ASIYEFANYA KAZI NA ASILE

Biblia ina maanisha nini iliposema “Asiyefanya kazi na asile”?

Maandiko hayo yanapatikana kutoka katika kitabu cha 2 Wathesalonike 3:10 “Kwa kuwa hata wakati ule tulipokuwapo kwenu tuliwaagiza neno hili, kwamba ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula”.

Mstari huo unatafsiriwa isivyopaswa na wengi wanaousoma..

Lakini mstari huo, unawahusu Wakristo! yaani watu wanaokusanyika  pamoja kanisani.

Katika Kanisa la Kwanza ulikuwepo utaratibu wa Waumini wote kufanya vitu kwa shirika,  ikiwemo kila mmoja kutoa sehemu ya mali zake na kuzileta kanisani ili zitumike katika kusaidiana pamoja na kunyanyuana..hususani kwa wale wenye mahitaji…. Hilo tunalisoma katika kitabu cha Matendo ya Mitume 2

Matendo 2:44 “Na wote walioamini walikuwa mahali pamoja, na kuwa na vitu vyote shirika,

45 wakiuza mali zao, na vitu vyao walivyokuwa navyo, na kuwagawia watu wote kama kila mtu alivyokuwa na haja.

46 Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,

47 wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa”.

Sasa kilichokuwa kinatokea ni kwamba, kulikuwepo na watu wachache ambao, walikuwa na uwezo wa kwenda kufanya kazi, lakini kwasababu wanaona kuna ofa hiyo ya kugawiwa baadhi ya vitu bure ikiwemo chakula kanisani, wakawa hawaendi kufanya kazi, na kukaa kusubiria hilo fungu la kanisa lifike wapewe, hivyo hiyo ikawa inasababisha kanisa kulemewa, kwa kuongezeka kwa watu wasio na shughuli zao na huku bado wanataka kupewa fungu kutoka kanisani.

Nakala hii inataja unayopenda kwa bei ya chini sana. Chagua kutoka kwa usafirishaji wa siku hiyo hiyo, https://www.swisswatch.is/product-category/tag-heuer/ uwasilishaji wa gari au kuchukua agizo.

Sasa kulitatua tatizo hilo, Ndipo Mtume Paulo kwa Uwezo wa Roho akaagiza katika makanisa yote kwamba watu wakafanye kazi, wale chakula chao wenyewe ili kanisa lisilemewe…Wabakie tu wale wanaostahili kweli kweli kupata fungu kutoka kanisani…Na wengi wa hao wanaostahili walikuwa ni wajane wenye umri wa miaka 60 na kuendelea, tena wasio na ndugu wa kuwasaidia, wameachwa wenyewe, na pia wana rekodi nzuri ya kuifanya kazi ya Mungu kanisani…hao ndio waliostahili kupokea sehemu ya fungu… na watu wasio na uwezo kabisa..Lakini wengine waliosalia wasipewe kitu chochote hata chakula kutoka kanisani, wakafanye kazi ili kanisa lisilemewe.


Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

TUNAPOSEMA TUISHI KWA NENO, INAMAANISHA TUISHI MAISHA YA NAMNA GANI?

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

JE! KUBET NI DHAMBI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Fahamu Namna ya Kuomba.

Wengi wa wanaompa Yesu Kristo maisha yao kwa mara ya kwanza, ndio maswali ya kwanza kwanza kujiuliza…nitaombaje! namna gani ya kuomba ili Mungu anisikie!

Kiuhalisia hakuna fomula fulani maalumu ya kuomba wala chuo fulani maalumu cha kujifunzia kuomba, Kwasababu Mungu wetu si mwanadamu wala hana udhaifu wa kutuelewa…Sehemu nyingine katika maandiko inasema “Baba yetu wa mbinguni anajua tujayohitaji hata kabla sisi hatujamwomba”

Unaona? kwa sentensi tu hiyo inaonesha kuwa Mungu si dhaifu wa kutuelewa sisi, kiasi kwamba tunahitaji course fulani tukasome ndipo atuelewe au kutusikia. Kitendo cha Kuwa mwanadamu tu! tayari Mungu anakuelewa kuliko unavyojielewa.

Hivyo mbele za Mungu, hatuendi na mpangilio mzuri wa Maneno kama tunavyoandaa hotuba kwenda kuisoma mbele za Mkuu wa Nchi…Isipokuwa tunakwenda na hoja zenye nguvu...Na hoja hizo ndio zile Bwana alizotufundisha wakati wa kuomba..katika Mathayo 6

“9 Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,

10 Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.

11 Utupe leo riziki yetu.

12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.

13 Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina”.

Kwamba tuombapo tuhakikishe tunaomba toba, na pia tuhakikishe tunawasamehe wengine ili na sisi pia tusamehewe…Kadhalika tunapoomba tuhakikishe tunalitukuza jina la Yesu, na pia tunaomba ufalme wake uje…Na pia tusisahau kusema mapenzi yake yatimizwe…kwasababu sio kila kitu tunachokiomba ni mapenzi ya Mungu…Pia tunapaswa tumwombe Mungu atupe riziki zetu za kila siku, kama chakula, mavazi, malazi pamoja na fursa.

Kadhalika tunamwomba asitutie majaribuni hiyo inahusisha kumwomba Bwana atuepushe na yule mwovu katika maisha yetu, imani yetu, familia zetu, kazi zetu, huduma zetu za kila siku za kuwaleta watu kwa Kristo, tunazungukwa na nguvu za yule adui kila mahali, hivyo ni muhimu kumwomba Bwana atuepushe na mitego yake yote.

Na bila kusahau kurudisha utukufu, na kutambua kuwa uweza, nguvu na mamlaka vina yeye milele na milele…Hivyo hakuna kama yeye, na yeye ndiye mwanzo na mwisho.

Hizo ndio hoja zenye nguvu…usitazame ni maneno kiasi gani umekosea kuongea, wala ni lugha gani umezungumza wakati wa kuomba, hakikisha tu maombi yako yanahusisha hivyo vipengele.

Kwa mawasiliano/mafundisho zaidi kwa njia ya whatsapp, tutumie ujumbe kwenye
namba hizi: +255789001312/ +255693036618


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU

FAIDA ZA MAOMBI.

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

TUMEAMBIWA TUNAPOSALI TUSIPAYUKE-PAYUKE, JE! HUKO KUPAYUKA PAYAUKA NDIO KUPI?

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi injili?


Rudi Nyumbani:

Print this post

kanisa la kwanza duniani ni lipi?

Maana ya kanisa ni “walioitwa” kwahiyo watu walioitwa watoke sehemu fulani wanaitwa kanisa…..Hivyo tafsiri ya kanisa sio jengo kama inavyodhaniwa na wengi…

Kwahiyo katika maandiko kanisa la kwanza lilianza siku ile ya PENTEKOSTE. Roho Mtakatifu aliposhuka juu ya watu! Soma Matendo Mlango wa pili yote.

Wale waliomwamini Yesu, na kubatizwa walishukiwa na Roho Mtakatifu, na hivyo Roho huyo huyo aliwaongoza kukusanyika pamoja kwa lengo la kujifunza Neno ambalo Mitume ndio waliokuwa wanalifundisha,  pia walidumu katika kushiriki meza ya Bwana, katika kufanya ushirika na katika  Kusali. Hayo mambo manne ndiyo yaliyokuwa yanafanyika katika kanisa la kwanza.

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.

40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi.

41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu.

42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali”.

(Hilo ndilo kanisa la kwanza)

Kanisa katoliki llinalosemekana kama kanisa la kwanza, hilo ilikuja kuzaliwa mwaka wa 325 Baada ya Kristo. Ambalo hilo lilikuwa kinyume na kanisa la kweli la Kwanza la Pentekoste.

Kanisa katoliki, ni kanisa la uongo kwasababu halikudumu katika hayo mambo manne hapo juu… halidumu katika fundisho la Mitume kama kanisa la Kwanza,  fundisho la Mitume linasema tusiabudu sanamu na pia linasema mpatanishi kati ya  Mungu na mwanadamu ni mmoja tu Yesu Kristo, wakati kanisa katoliki linaamini Mariamu pia ni mpatanishi…..

Pia kanisa katoliki halidumu katika kumega mkate, kwani mwenye ruhusu ya kushiriki ni Padre tu! peke yake jambo ambalo ni kinyume na maandiko, pia halidumu katika kufanya ushirika wala kusali…Sala zinazofanywa ni za desturi za kipagani, kusalia rozari na sanamu jambo ambalo kanisa la kwanza halikufanya. Maombi ya moja kwa moja kwa Mungu hayatiliwi mkazo, na zaidi ya yote maombi ya masafa marefu hayapo kabisa ndani ya kanisa katoliki.


Mada Nyinginezo:

MARIAMU NI NANI?

UHURU WA ROHO.

JE! BIKIRA MARIA NI MALKIA WA MBINGUNI?

JE! NI SAHIHI KUMUITA MARIA MAMA WA MUNGU?


Rudi Nyumbani:

Print this post

YESU NI NANI?

Yesu ni nani? Hili ni swali ambalo sio tu linawachanganya watu wengi wa leo, lakini pia limekuwa ni swali lililowasumbua watu wengi tangu  enzi na enzi vizazi na vizazi huko nyuma, hata tangu wakati Bwana Yesu mwenyewe akiwa hapa duniani utaona siku moja aliwauliza wanafunzi wake nao swali kama hilo,

Mathayo 16:13 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?

14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.

15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

Unaona, hata leo hii tu angekuwepo duniani angetuuliza na sisi swali hilo hilo, tunamnena yeye kama nani, ni wazi utasikia kila mtu anatoa jibu lake wengine utawasikia watasema, ni mjumbe wa Mungu, wengine watasema ni mmojawapo wa mitume wa Mungu, wangine watasema alikuwa ni nabii wa Mungu, wengine watasema ni mkombozi, wengine watasema ni Mungu…nk. N.k

Lakini Je hiyo inamaanisha mitazamo yao wote haipo sawa?, jibu ni hapana, wanaweza wakawa sawa mahali fulani lakini si sawa kulingana na Mungu anavyotaka watu wamjue Yesu kama nani..Ni sawa tu na leo usimame na boss labda tuseme mbele ya watu 1000 tofauti tofauti, na ukasema kila mmoja aanze kumzungumzia , hutashangaa katikati ya huo mkutano wengine wakimwita, mjomba, wengine wakimwita rafiki, wengine wakimwita baba, wengine wakimwita binamu, wengine wakimwita jirani, wengine wakimwita mwenyekiti, wengine wakimwita shemeji, wengine wakimwita mwenetu n.k…

Hapo utaona akiitwa kila aina ya cheo ambacho hujawahi kutazamia kwamba anaweza akawa nacho boss wako, sasa hapo huwezi kusema hawapo sawa kisa tu kwasababu hukumsikia hata mmoja wao akimwita boss, wao kila mmoja alimwita kulingana na mahusiano aliyonayo naye..ikiwa ni mtoto wake alisimama mbele yake hawezi kumwita shemeji au boss ni lazima atamwita Baba tu..

Lakini hata kama wapo sawa kiasi gani, Bado hawapo sawa kulingana na wewe unavyotaka watu wale wamjue kama boss.

Na vivyo hivyo kwa Bwana Yesu, wengi wanamjua kama mtume wa Mungu, na kweli ndivyo alivyo yeye ndiye mtume mkuu, wengi wanamjua kama nabii, na ni kweli ndivyo ilivyo yeye alikuwa ni nabii mkuu, wengine wanamjua kama kiongozi na kweli ndivyo alivyo, vile vile wengine wanamjua kama Mungu mwenyewe aliyeuchua mwili na kuishi na sisi duniani, na kweli ndivyo ilivyo maandiko mengi yanathibitisha hilo kuwa YESU ndiye Mungu mwenyewe katika mwili wa kibinadamu..lakini swali linakuja pale pale Je! Mungu anataka sisi tumjue  YESU  kama nani?.

Sasa tukiendelea kusoma pale chini tunaona Petro anamjibu Bwana maneno haya:

15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

16 Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.

17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.

18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.”

Unaona Ufunuo aliopata Petro juu ya YESU kama KRISTO, aliyekuja kama mwana wa Mungu, ndio aliokuwa anauhitaji na ndio kwa kupitia huo huo YESU amelijengea kanisa lake na milango ya kuzimu haiwezi kulishinda.

Hivyo hatupaswi kuhangaika sana, kutafuta kumjua YESU ni nani? Tukianza kumchambua hatutammaliza, lakini biblia imetupa mwongozo mwepesi uliomwelezea yeye kwamba tumjue yeye kama KRISTO, maana ya neno Kristo ni mtiwa mafuta, yaani mtu aliyetiwa mafuta kuwakomboa wanadamu,..hivyo tukishamjua YESU kama mkombozi huo ni ufunguo mkubwa sana uliobeba vyeo vyake vingine vyote vilivyobakia.. Kwamba yeye ndio njia ya kwenda mbinguni, na mtu hawezi kufika kwa Mungu pasipo kupitia yeye.

Hivyo ukiulizwa leo YESU ni nani, jibu tayari lipo yeye ni KRISTO, yaani mkombozi wa ulimwengu, hilo linatosha kumwelezea yeye..Na mtu yeyote akimwelewa kwa namna hiyo hivyo akamruhusu ayakomboe maisha yake basi ajue kuwa shetani atagonga mwamba, tiketi ya kwenda mbinguni ipo mikononi mwake.

Ubarikiwe.

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

UBATILI.

RACA

KWANINI AWE NI PUNDA NA MWANA-PUNDA?

MUNGU MWENYE HAKI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

HERI WAFU WAFAO KATIKA BWANA

Ufunuo 14:13 “Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao”.

Biblia inasema “Heri” heri maana yake “amebarikiwa yeye”…na inasema pia heri wafu wafao katika Bwana, ikiwa na maana kuwa sio kufa tu! bali kufa katika Bwana.. Wafu ambao hawajafa katika Bwana ni kinyume chake, kwamba Ole wao…

Sentensi hizo zinamaanisha kuwa kuna kitu kitafuata baada ya kifo, nacho si kingine zaidi ya hukumu! Na watakaokufa katika Kristo wanatumaini la kufufuliwa tena na kupewa uzima wa milele, na kupata raha isiyoisha..ndio maana wanaambiwa wana heri…. ingekuwa hakuna kitu kinachofuata, isingesema heri wafu! bali ingesema heri walio hai!

Je! maisha yako umeyatengeneza kiasi kwamba, una uhakika, hata leo hii ukiondoka ulimwenguni! utakuwa na heri? Utayatengenezaje?..kwa matendo yako!  kwasababu Matendo ya kila mtu yanamfuata popote aendapo! Majumba tukifa tutayaacha, magari tutayaacha, mali tutaziacha lakini matendo tunakwenda nayo huko ng’ambo ya pili. Hivyo sio kitu cha kukichukulia kiwepesi!

kumbuka hakutakuwa na nafasi ya pili baada ya kifo.

Waebrania 9:27 “Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu”; 

Mgeukie Bwana Yesu kikamilifu. Kimbilio letu na Tumaini letu

Maran atha!


Mada Nyinginezo:

SIKU YA HUKUMU ITAKUWAJE?

NIFANYE NINI ILI NIIKWEPE HUKUMU.

UFUFUO WA UZIMA NA WA HUKUMU.

UMEPATA UHAKIKA WA KUTOKUINGIA HUKUMUNI KATIKA SIKU ILE?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Baraka inatoka wapi

Chanzo cha Baraka zote ni Mungu..Na Mungu anaweza kumbariki mtu moja kwa moja kupitia yeye mwenyewe…na anaweza pia kumbariki mtu kupitia mtu mwingine.

Kwamfano kwenye Biblia Mungu alimbariki Ibrahimu moja kwa moja…akamwambia 

Mwanzo 22:15 “Malaika wa Bwana akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni

16 akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,

17 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;

18 na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu”.  

Na pia Mungu anaweza kumbariki mtu kwa kupitia Mtu mwingine, kwa mfano “Mzazi ana uwezo wa kumbariki mwanawe” na baraka hizo zikamfikia vile vile kama alivyombariki. Mfano katika Biblia tunamwona Yakobo Mwana wa Isaka, aliwabariki wanawe 12, na kila mmoja baraka aliyombarikia ilimfikia.

Hivyo Ili tufanikiwe katika maisha yetu, hatuna budi kutafuta Baraka, na Baraka hizo zinakuja kwa kumpendeza Mungu, pamoja na wanadamu…Kuyashika maagizo ya Mungu, na Kuwaheshimu wazazi pamoja na watu wote. Kinyume na hapo ni kujitafutia Laana.


Mada Nyinginezo:

MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO.

NITAONGEZAJE NGUVU ZANGU ZA ROHONI?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

KWANINI MUNGU HAKUMUUA NYOKA MPAKA AKARUHUSU AJARIBIWE PALE BUSTANI NA EDENI?

JE! MTU ALIYEOKOKA ANARUHUSIWA KUMILIKI GUEST HOUSE AU LODGE AMBAYO INA BAR NDANI YAKE NA KUTOA FUNGU LA KUMI KWA KUPITIA HIYO KAZI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Mbinguni ni sehemu gani?

JIBU: Ili tusichanganyikiwe jambo la muhimu  tulinalopaswa kujua ni kuwa Katika biblia Neno “mbinguni” limetumika kuwakilisha sehemu tofauti tofauti tatu.

Sehemu ya kwanza ni anga hili ambalo lipo juu yetu: Ambalo ndilo hili tunaloliona lenye nyota, mawingu, mwezi jua na sayari, ambalo ndege wote wa angani wanaruka na kufurahia, biblia imelitaja kama mbingu..Tunasoma..

Isaya 55:10 “Maana kama vile mvua ishukavyo, na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; bali huinywesha ardhi, na kuizalisha na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, na mtu alaye chakula;

11 ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.”

Luka 17:24 “kwa kuwa, kama vile umeme umulikavyo toka upande huu chini ya mbingu hata upande huu chini ya mbingu, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake”.

Sehemu ya Pili ya mbingu ni makao ya Mungu yalipo: Na hii ipo katika Roho, sehemu ambayo Mungu na malaika zake wanaishi, hatuwezi kuiona kwa jicho la kibinadamu wala hatuwezi kufika huko kwa kifaa chochote cha kibinadamu, lakini ni mahali halisi kabisa. Tiketi ya pekee ya kufika huko biblia inatuambia ni Yesu Kristo tu, Na hii mbingu ni pana sana ndio imejumuisha ile mbingu mpya na nchi mpya ambayo itakuja kuwa ni makao ya watakatifu baadaye, pamoja na ile paradiso (peponi) kule ambapo wale wote waliokufa zamani na wanaokufa sasa hivi katika Kristo wanahifadhiwa kwa muda wakisubiria ufufuo siku ile ya Unyakuo ili kwa pamoja waingie katika makao ya Mungu mwenyewe yaliyo juu sana na ndio maana utaona mtume Paulo alinyakuliwa mpaka mbingu ya Tatu, mbingu hii ya tatu ni hiyo ya makao ya Mungu mwenyewe,  akaonyeshwa sehemu ya maono ya huko, na kusema mambo yaliyo huko hayajuzu hata mwanadamu kuyatamka,(2Wakorintho 12:2-4). na ndiko watakatifu waliokombolewa watakapokwenda siku ile ya Unyakuo itakapofika, ni mahali patakatifu na pasafi ambapo mtu yeyote mchafu hataingia..

1Wafalme 8:27 “Lakini Mungu je? Atakaa kweli kweli juu ya nchi? Tazama, mbingu hazikutoshi, wala mbingu za mbingu; sembuse nyumba hii niliyoijenga!”

1Timotheo 6:16 “ambaye yeye peke yake hapatikani na mauti, amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa; wala hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata milele. Amina.”

Na sehemu ya tatu biblia inapataja kama mbinguni ni mahali pa juu sana, makao ya juu sana: Mahali ambapo Mungu pekee ndiye anayestahili kuwepo, jambo ambalo hata hapa duniani linaweza kufikiwa,

Watu walio ndani ya Yesu, ambao wameokoka kikamilifu kwa kumwamini Yesu na kubatizwa, katika ulimwengu wa roho, ni sawa na wameketi pamoja na Kristo mbinguni..

Waefeso 2:5 “hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.

6  Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu;”

Kadhalika pia, Ufalme wowote au mtu yeyote anayetafuta kuinuliwa ziadi ya vitu vingine vyote huyo katika roho anaonekana anakipandia cheo cha Mungu kilipo, na Mungu yupo mbinguni, hivyo anaonekana kama amefika mbinguni.

Danieli 4:19 “Ndipo Danieli, aliyeitwa jina lake Belteshaza, akashangaa kwa muda, na fikira zake zikamfadhaisha. Mfalme akajibu akasema, Ee Belteshaza, ndoto ile isikufadhaishe wala tafsiri yake. Belteshaza akajibu, akasema, Bwana wangu, ndoto hii iwapate wao wakuchukiao, na tafsiri yake iwapate adui zako.

20 Ule mti uliouona, uliokua, ukawa na nguvu, urefu wake ukafika mpaka mbinguni, na kuonekana kwake mpaka dunia yote;

21 ambao majani yake yalikuwa mazuri, na matunda yake mengi, na ndani yake chakula cha kuwatosha wote; ambao chini yake wanyama wa kondeni walikaa, na ndege wa angani walikuwa na makao yao katika matawi yake;

22 ni wewe, Ee mfalme, uliyekua, na kupata nguvu; maana ukuu wako umekua na kufika mpaka mbinguni, na mamlaka yako yamefika mpaka mwisho wa dunia.

Mathayo 11:23 “Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo.”

Isaya 14:12 “Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa!

13 Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini.

14 Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu.

15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo”.

Hivyo kwa vyovyote vile, tunapaswa tujitahidi ili tufike huko, si kwa kujiinua tukiyatumainia haya Maisha, bali kwa kupitia Yesu Kristo, kwasababu biblia inasema mambo tuliyoandaliwa huko, jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia.

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

JE! NI KWELI DUNIA ILIUMBWA TAKRIBANI MIAKA 6000 ILIYOPITA? NA JE! SHETANI ALIKUWEPO DUNIANI WAKATI DUNIA INAUMBWA?

TUMEAMBIWA TUNAPOSALI TUSIPAYUKE-PAYUKE, JE! HUKO KUPAYUKA PAYAUKA NDIO KUPI?

JE! KUNA DHAMBI KUBWA NA NDOGO?

NI NANI ANAYETAWALA DUNIA KATI YA MUNGU NA SHETANI?.


Rudi Nyumbani:

Print this post