Biblia inasema katika kitabu cha Mwanzo.
Mwanzo 4:1 Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa Bwana.
2 Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili. Habili alikuwa mchunga kondoo, na Kaini alikuwa mkulima ardhi”
Mtoto mwingine aliyezaliwa na Adamu na Hawa alikuwa ni Sethi.
Mwanzo 5:1 “Hiki ndicho kitabu cha vizazi vya Adamu. Siku ile Mungu alipoumba mtu, kwa sura ya Mungu alimfanya;
2 mwanamume na mwanamke aliwaumba, akawabariki akawaita jina lao Adamu, siku ile walipoumbwa.
3 Adamu akaishi miaka mia na thelathini, akazaa mwana kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi”
Lakini pia Biblia haiishi hapo, inasema Adamu alizaa watoto wengine wakiume na wakike baada ya kumzaa Sethi.
Mwanzo 5:4 “Siku za Adamu baada ya kumzaa Sethi zilikuwa miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake”.
Na hao watoto wakike waliozaliwa ndio waliokuja kuwa wake wa hao watoto wengine wa kiume wa Adamu.
Hivyo Biblia haitoi idadi kamili ya watoto wa Adamu, pengine walikuwa 5 au 10 au 20 au 30, hatujui lakini zaidi ya Sethi, walikuwapo pia watoto wengine wa Adamu ambao habari zao hazikuandikwa katika biblia.
ADAMU ALIISHI MIAKA MINGAPI?
Jibu tunalipata katika Mstari wa 5
Mwanzo 5:5 “Siku zote za Adamu alizoishi ni miaka mia kenda na thelathini, naye akafa.”
Kwahiyo siku zote za Adamu ilikuwa ni miaka 980, akafa
Mada Nyinginezo:
JE! ADAMU ALIWASALIANA NA MUNGU KWA LUGHA IPI PALE BUSTANINI?
MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA NI UPI?.
About the author