Category Archive Mafundisho

BWANA UNIJULISHE MWISHO WANGU.

Karibu tujifunze biblia..

Daudi anasema..

Zaburi 39:4 “Bwana, unijulishe mwisho wangu, Na kiasi cha siku zangu ni kiasi gani……..”

Hapa si kwamba Daudi anataka aijue siku ya kufa kwake!, Hapana!, Mungu hajawahi kumwahidia mwanadamu hayo maarifa..(Hakuna maombi ya mtu kufunuliwa siku yake ya kufa).  Bali hapo Daudi anaomba Mungu ampe KUZIJUA SIKU ZAKE DUNIANI KWAMBA SI NYINGI, Kwamba siku za mwanadamu ni kama maua! Si wa kudumu (Zaburi 103:15).

Hivyo Daudi alijua Mungu akimpa moyo wa kuelewa kuwa “Yeye ni kama mpitaji tu hapa duniani, na siku zake si nyingi”.. basi atakuwa mnyenyekevu zaidi, na ataishi maisha ya kumtafuta Mungu, kumcha Mungu na kuishi kwa hekima duniani..

Zaburi 90:12 “Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima”.

Na sio tu yeye aliyepaswa kuomba maombi kama haya, bali hata sisi pia watu wa siku za Mwisho, ni lazima tumwombe Mungu atujulishe siku zetu! (Yaani atupe mioyo ya hekima kujua kuwa sisi ni wapitaji tu, na siku zetu za kuishi si nyingi).

Faida ya kuomba Moyo huu kutoka kwa Mungu, ni kwamba tutakuwa watu wa kutazama maisha yajayo zaidi kuliko maisha haya ya hapa duniani ya kitambo!.. Kwasababu ndani ya akili zetu tutajua kuwa siku zetu si nyingi!..kwamba siku yoyote safari ya maisha yetu itafikia mwisho.

Watu wengi wenye huu moyo, utaona ndio watu wenye mioyo ya kumtafuta Mungu kwa kujikana nafsi kwelikweli…ndio watu wenye mioyo ya kusaidia wengine, ndio watu wenye mioyo ya kuwahubiria wengine mwisho wa maisha haya.

Na watu kama hawa, hata kama wakiambiwa kuwa watapewa miaka elfu moja ya kuishi duniani, bado tu!, watajiona kuwa siku zao ni chache, kwasababu tayari ndani yao wamepewa mioyo ya “kuzihesabu siku zao na kujijua kuwa wao si kitu, ni kama maua tu, yaliyopo leo na kesho kutupwa kwenye tanuru” hivyo maisha yao yatakuwa ni yale yale siku zote ya kutafuta kutengeneza maisha yajayo ya umilele.

Shetani hapendi watu wawe na moyo huu, anataka watu wawe na moyo wa kufikiri kwamba wataishi milele katika hii dunia, hataki watu wajue kwamba siku yoyote safari ya maisha yao itafikia ukingoni, kwasababu anajua watu wakilijua hilo, basi watatengeneza maisha yao hapa kwaajili ya huko waendako, na hivyo atawapoteza wengi. Na yeye (shetani) hataki kumpoteza mtu hata mmoja, anataka wote waende katika ziwa la moto kama yeye!!.

Kwahiyo kila siku ni muhimu sana kuomba Bwana atupe huu moyo.. “Atujulishe miisho yetu, na siku zetu za kuishi” ili tufahamu kuwa “sisi ni wapitaji tu”.

Moyo huu utaupata kwa kufanya mambo yafuatayo matatu (3)

1.Kwa kuomba

Majibu ya mambo yote tunayapata katika maombi, kama vile Sulemani alivyoomba kwa Mungu apewe moyo wa hekima na Mungu akamsikia, vile vile pia Moyo wa kujua kuwa wewe ni mpitaji tu, unatoka kwa Bwana, ndio maana hata hapo Daudi anaonekana kama anaomba.. “Bwana nijulishe”..Na wewe siku zote sema “Bwana nijulishe”

2. Kwa kutafakari matukio ya vifo yanayotokea.

Unapotenga muda wa kutafakari matukio ya Ajali yanayotokea, au unapotazama wagonjwa mahututi, au unapokwenda kwenye nyumba za misiba..sehemu hizo ni sehemu ambazo Mungu anaitengeneza mioyo ya wengi.. Hivyo na wewe huna budi kuhudhuria misiba, au kufuatilia matukio (Wengi hawapendi kufuatilia haya), kwasababu hawataki kuumia moyo, lakini ndani ya mioyo yao wana viburi vya maisha, wanajiona kama wao wataishi milele.. Biblia inatufundisha pia tuhudhurie sehemu za Misiba, sio kwenye karamu tu, ili tukajifunze huko..

Mhubiri 7:2 “Heri kuiendea nyumba ya matanga, Kuliko kuiendea nyumba ya karamu. Kwa maana huo ndio mwisho wa wanadamu wote, naye aliye hai atautia moyoni mwake. 

3 Huzuni ni afadhali kuliko kicheko, Maana simanzi ya uso ni faida ya moyo”.

3. Kwa kusoma Neno.

Unaposoma Biblia, huko ndiko utakapopata Maarifa kamili ya Neno la Mungu, na maneno ya kuunyenyekeza moyo wako, biblia ndio kioo kamili cha kujijua wewe ni nani?.. ukitaka kujijua wewe ni mtu wa namna gani, basi soma Biblia.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

KWA MIOYO YAO WAKAREJEA MISRI.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

Rudi nyumbani

Print this post

MUNGU HAJARIBIWI NA MAOVU BALI MEMA.

Yakobo 1:13 “Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu”

Hapo Neno linasema kuwa Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, kinyume chake ni kweli kwamba yeye anajaribiwa na MEMA tu!. Maana yake tunapofanya mema hapo tunakuwa tunamweka Mungu kwenye jaribu la kutubariki.. Na hivyo ni lazima aachie baraka kwetu.

Lakini tukienda kinyume na Neno lake na huku tunataka atubariki, hapo maana yake tunamjaribu yeye kwa Maovu.. Mfano wa watu waliomjaribu Mungu kwa maovu ni Wana wa Israeli kipindi wapo jangwani, Walitaka Bwana awashushie chakula kile cha kimiujiza, huku mioyoni mwao wamemwacha Mungu, ni watu wenye viburi, ni watu wa kunung’unika, ni watu wasio na heshima wala staha kwa Mungu na mwishowe wakaangukia hukumu.

Waebrania 3:7 “Kwa hiyo, kama anenavyo Roho Mtakatifu, Leo, kama mtaisikia sauti yake,

8  Msifanye migumu mioyo yenu, Kama wakati wa kukasirisha, Siku ya kujaribiwa katika jangwa,

9  Hapo baba zenu waliponijaribu, wakanipima, Wakaona matendo yangu miaka arobaini.

10  Kwa hiyo nalichukizwa na kizazi hiki, Nikasema, Sikuzote ni watu waliopotoka mioyo hawa; Hawakuzijua njia zangu;

11  Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu”.

Na maandiko yanasema Mungu ni yeye Yule jana na leo na hata milele, alilolikataza miaka elfu 2 iliyopita analitakata hata leo.. Akisema “yeye hajaribiwi na Movu, ni kweli hajaribiwi na hayo”.. Lakini kinyume chake anajaribiwa na Mema yaliyoandikwa katika Neno lake.

Kwamfano unapomtolea Mungu sadaka isiyo na kasoro (Maana yake iliyo sawasawa na Neno lake, na kwa nia njema) Hilo ni jaribu kwa Mungu kukubariki wewe, na hapo utakuwa umemjaribu kwa Mema.

Malaki 3:8 “Je! Mwanadamu atamwibia Mungu? Lakini ninyi mnaniibia mimi. Lakini ninyi mwasema, Tumekuibia kwa namna gani? Mmeniibia zaka na dhabihu.

 9 Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote.

 10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.

11 Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema Bwana wa majeshi”.

Na mambo mengine yote mema, ambayo tunayafanya yaliyo sawasawa na Neno la Mungu, mambo hayo ni TANZI kwa Mungu, kutumwagia Baraka zake, au kuzungumza na sisi.

Lakini kama moyoni mwako umemwacha Bwana, halafu unatafuta kuisikia sauti yake, unaenda kwa nabii ili usikie Mungu anasema nini kuhusu wewe, hapo unamjaribu Mungu kwa mabaya na hivyo unajitafutia laana badala ya Baraka.

Ezekieli 14:4 “Basi sema nao, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Kila mtu wa nyumba ya Israeli atwaaye vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, na kumwendea nabii; mimi, Bwana, nitamjibu neno lake sawasawa na wingi wa sanamu zake;

  5 ili niwakamate nyumba ya Israeli kwa mioyo yao wenyewe, kwa sababu wamefarakana nami kwa vinyago vyao.

  6 Kwa sababu hiyo uwaambie nyumba ya Israeli, Bwana MUNGU asema hivi; Rudini ninyi, mkageuke na kuviacha vinyago vyenu; mkageuze nyuso zenu zisielekee machukizo yenu yote. 

7 Kwa maana kila mtu wa nyumba ya Israeli, au wa wageni wakaao katika Israeli, ajitengaye nami, na kuvitwaa vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, kisha kumwendea nabii, na kuniuliza neno kwa ajili ya nafsi yake; mimi, Bwana, nitamjibu, mimi mwenyewe

8 nami nitaukaza uso wangu juu ya mtu yule, na kumfanya kuwa ajabu, awe ishara na mithali, nami nitamkatilia mbali, asiwe kati ya watu wangu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.”

Bwana Yesu atusaidie.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je Adamu na Hawa, walikuwa hawafanyi mema kabla ya kula tunda?

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?

LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

KWANINI MIMI?

Rudi nyumbani

Print this post

NA TAA YA MUNGU ILIKUWA BADO HAIJAZIMIKA

Jina la Bwana na Mwokozi, Mkuu wa Uzima, Yesu Kristo lihimidiwe!..karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu.

Upo wakati ambao TAA ya Mungu itazima!.. Tuitikie wito wa Mungu, kabla ya huo wakati kufika..

1Samweli 3:2 “Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona), 

3 NA TAA YA MUNGU ILIKUWA HAIJAZIMIKA BADO, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu la Bwana, palipokuwa na sanduku la Mungu;

 4 basi, wakati huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa.”

Sasa ili kuelewa vizuri Taa ya Mungu ni kitu gani, na ilikuwa inazimika wakati gani..hebu turejee ile Hema ambayo Musa aliagizwa aitengeneze, tunasoma Ilikuwa imegawanyika katika Sehemu kuu tatu, Ua wa Ndani, Patakatifu na Patakatifu pa patakatifu.

Na ndani katika Patakatifu, palikuwa na madhabahu ya uvumba, Meza ya mikate ya wonyesho pamoja na KINARA CHA TAA, ambacho kilikuwa na Mirija saba. (Tazama picha juu).

Hiki kinara cha Taa kazi yake ilikuwa ni kutia Nuru ile hema wakati wa USIKU. Kwamba Nyakati zote za usiku ni sharti ndani ya Hema kuwe na Nuru, na amri hiyo ilikuwa ni ya Daima, maana yake ya kila siku!.. haikupaswa hata Usiku mmoja upite bila Kinara hicho kuwashwa ndani ya Hema.

Kutoka 27: 20 “Nawe waamuru wana wa Israeli wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya nuru, ili kufanya ile taa kuwaka daima. 

21 Ndani ya ile hema ya kukutania, nje ya hilo pazia, lililo mbele ya huo ushuhuda, Haruni na wanawe wataitengeza TANGU JIONI HATA ASUBUHI MBELE YA BWANA; itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyao vyote kwa ajili ya wana wa Israel”

Tusome tena..

Walawi 24:1 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, 

2 Waagize wana wa Israeli kwamba wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya ile nuru, ili hiyo taa iwake daima. 

3 Hapo nje ya pazia la ushahidi, ndani ya hema ya kukutania, Haruni ataitengeza TANGU JIONI HATA ASUBUHI MBELE ZA BWANA DAIMA; ni amri ya milele katika vizazi vyenu”

Hapo mstari wa 3, unasema ataitengeneza “tangu jioni hata asubuhi” maana yake wataiwasha tangu jioni mpaka asubuhi, na kukiisha pambazuka basi taa ile inazimwa, kwasababu kulikuwa na Nuru ya mwanga wa Nje wa jua iliyokuwa inaingia ndani ya Hema.

Sasa tukirudi katika habari hiyo ya Samweli,  maandiko yanasema Samweli alikuwa analala katika Hema karibu na sanduku la BWANA, na wakati ambapo Taa ya Mungu bado haijazimika..Maana yake bado hakujapambazuka, (kwasababu kukisha pambazuka tu, tayari ile taa ilikuwa inazimwa).

Wakati huo ndipo Samweli aliisikia Sauti ya Mungu ikimwita mara 4, na Samweli akaitikia wito wa Mungu.

Lakini ni nini tunajifunza katika hiyo habari?

Upo wakati ambao sauti ya Mungu inaita juu ya Mtu..na wakati huo ni wakati wa giza Nene juu ya maisha ya mtu.. Huo ndio wakati ambapo Mungu anamwita mtu, na anamwita kwa sauti ambayo inakuwa inayofanana na ya watu wa Mungu.. kiasi kwamba mtu anaweza kudhani ni mtu anayemwita/kumshawishi kumbe ni Mungu, ndio maana Samweli alipoitwa alikimbilia kwa Eli akidhani ni Eli anayemwita kumbe ni MUNGU.

Vile vile Mungu anawaita leo watu kutoka katika dhambi, na uvuguvugu lakini watu wanadhani ni wachungaji wao ndio wanaowaita, wengine wanadhani ni wahubiri ndio wanaowatafuta wawe washirika wao, pasipo kujua kuwa ni sauti ya Mungu ndio inayowaita na si watu.

Sasa endapo Samweli asingeitikia ule wito wakati ule ambapo TAA BADO HAIJAZIMIKA, huenda ile sauti ya Mungu asingeisikia tena kwa wakati ule mpaka labda kipindi kingine ambapo Taa hiyo itakuwa inawaka.

Ndugu TAA ya Mungu leo ni NEEMA,  Hii Neema kuna wakati itasimama!, na hakutakuwa tena na nafasi ya kumkaribia Mungu, wakati ambao unyakuo wa kanisa utapita, ndio wakati ambao TAA itakuwa imezima, vile vile wakati ambao utaondoka katika haya maisha huo ndio wakati ambao Taa ya Mungu itakuwa imezimika juu yako.

Je umemkabidhi Yesu maisha yako?.. Umebatizwa katika ubatizo sahihi? Umeokoka?.. Kama bado ni vyema ukafanya hivyo sasa kabla Taa haijazimika.

Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo. 

Maran atha!

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

Kiango na Pishi ni nini (Mathayo 5:15)?

NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.

NYAKATI AMBAZO NI LAZIMA TUKUTANE NAZO TU:

Rudi nyumbani

Print this post

Thenashara ni nini? (Marko3:16)

Thenashara ni neno la kiebrania linalomaanisha namba “kumi na mbili” (12). Kwahiyo badala ya kusema watu 12, ni sahihi kabisa kusema “watu Thenashara”, au badala ya kusema “miezi 12” ni sahihi kusema “miezi Thenashara”…badala ya kusema makabila 12 ni sawa na kusema “Makabila thenashara” n.k

Biblia imelitumia Neno hilo Thenashara kuwakilisha wale Wanafunzi 12 wa Bwana Yesu, ambao baadaye waliitwa Mitume.

Marko 3:16  “Akawaweka wale Thenashara; na Simoni akampa jina la Petro;

17  na Yakobo, mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye Yakobo, akawapa jina la Boanerge, maana yake, wana wa ngurumo;

18  na Andrea, na Filipo, na Bartholomayo, na Mathayo, na Tomaso, na Yakobo wa Alfayo, na Thadayo, na Simoni Mkananayo,

19  na Yuda Iskariote, ndiye aliyemsaliti. Kisha akaingia nyumbani”

Na ni kwanini wanafunzi hawa 12, watenganishwe kwa kuitwa hivyo Thenashara?.. Ni kwasababu Bwana Yesu alikuwa anao wanafunzi wengine wengi zaidi ya 70,

Luka 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.”

 hivyo ili kuwatofautisha hawa wanafunzi 70 na wale 12 aliowateua kwanza kndio likatumika hilo neno “Thenashara”

Unaweza kulisoma neno hilo pia katika Mathayo 26:14-16, Marko 4:10, Marko 9:35, na Yohana 20:24

Je umefanyika kuwa Mwanafunzi wa Yesu? kwa kutubu dhambi zako zote, na kumaanisha kuziacha na vile vile kuchukua msalaba wako na kumfuata yeye?

Luka 14:27  “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Wahuni ni watu gani katika biblia?

SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?

Rudi nyumbani

Print this post

Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)

Jibu: Kutoka 40:20 “Akautwaa ule ushuhuda, akautia ndani ya sanduku, akaiweka miti ya kuchukulia juu ya sanduku, akakiweka kiti cha rehema juu ya sanduku”.

Kiti cha Rehema kilichokuwa juu ya Sanduku la Agano hakikuwa “kiti” kama viti hivi tuvijuavyo, vyenye miguu minne, na vyenye nafasi ya Mtu kuketi.. Bali neno “kiti” kama lilivyotumika hapo limemaanisha “Nafasi ya wazi”.

Kwahiyo juu ya sanduku la Agano hakukuwa na Kitu Fulani mfano wa “Stuli” juu yake, hapana! bali palikuwa na nafasi wazi ambayo ndiyo iliyoitwa “kiti cha rehema”. Nafasi hiyo ilikuwa ipo katikati ya wale Makerubi wawili wa dhahabu ambao walikuwa wanatazamana, na mbawa zao kukutana kwa juu na kuifunika hiyo sehemu ya wazi (yaani kiti cha rehema).

Nafasi hiyo haikuwa kubwa sana, na pia ilikuwa ni sehemu ya mfuniko wa Sanduku zima (maana yake wale Makerubi wawili pamoja na kile kiti cha rehema vilikuwa vimeungana, na kwa pamoja kufanya mfuniko wa sanduku), na ndani ya sanduku kulikuwa na Mana, zile Mbao za mawe zenye amri kumi pamoja na ile fimbo ya Haruni iliyochipuka. (Tazama picha juu).

Hivyo ulipofika muda wa Upatanisho, Kuhani Mkuu aliingia na damu Ng’ombe na kwenda kuinyunyiza juu ya kiti cha rehema mara saba, na damu hiyo inakuwa ni upatanisho kwa wana wa Israeli, dhidi ya dhambi zao.

Walawi 16: 14 “Kisha atatwaa baadhi ya damu ya yule ng’ombe, na kuinyunyiza kwa kidole chake juu ya kiti cha rehema upande wa mashariki; na mbele ya kiti cha rehema atainyunyiza ile damu kwa kidole chake mara saba”.

Katika Agano la kale, Israeli walikitazama hicho kiti cha Rehema kama kitovu chao cha kwenda kupata msamaha, kupitia kuhani mkuu wao aliyeteuliwa kwa wakati huo.

Lakini kiti hicho cha rehema kilikuwa na mapungufu yake, kwasababu watu hawakuwa wanapata msamaha wa dhambi, bali dhambi zao zilikuwa zinafunikwa tu!, na kulikuwa na kumbukumbu la dhambi kila mwaka….kwamaana damu za Ng’ombe na Kondoo haziwezi kuondoa dhambi za mtu, vile vile Makuhani wa kibinadamu ambao nao pia wamejaa kasoro hawawezi kuwapatanisha wanadamu na Mungu, kwasababu wao pia ni wakosaji!.. Na pia kiti cha rehema ambacho kipo duniani, kilichotengenezwa na mikono ya wanadamu hakiwezi kufanya utakaso mkamilifu wa dhambi, kwasababu na chenyewe kimetengenezwa na mikono ya watu wenye dhambi..

Hivyo ni lazima kiihitajike kiti kingine cha Rehema kilicho kikamilifu ambacho hakijatengenezwa na mikono ya wanadamu, na vile vile ni lazima ipatikane damu kamilifu ya Mwanadamu asiye na kasoro, na hali kadhalika ni lazima apatikane kuhani Mkuu ambaye hana dhambi..Ndipo UTAKASO na UPATANISHO WA MWANADAMU UWE KAMILI.

Na kiti hicho cha Rehema kipo Mbinguni sasa, na kuhani Mkuu mkamilifu tayari tumepewa, ambaye si mwingine zaidi ya YESU, na damu kamilifu isiyo na kasoro imeshamwagwa kwaajili yetu, na damu hiyo si NYINGINE ZAIDI YA DAMU YA YESU. Hivyo Msamaha mkamilifu unapatikana sasa, na upatanisho mkamilifu unapatikana sasa kupitia Damu ya YESU, kwa kila aaminiye.

Waebrania 9:11  “Lakini Kristo akiisha kuja, ALIYE KUHANI MKUU wa mambo mema yatakayokuwapo, kwa HEMA ILIYO KUBWA NA KAMILIFU ZAIDI, isiyofanyika kwa mikono, maana yake, isiyo ya ulimwengu huu

12  wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali KWA DAMU YAKE MWENYEWE aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele”.

Je umemwamini Yesu na kuoshwa dhambi zako? Na kupata ukombozi mkamilifu?. Kama Bado unasubiri nini? Kiti cha Rehema kipo wazi sasa, lakini hakitakuwa hivyo siku zote, siku si nyingi baada ya unyakuo kupita mlango wa Neema utafungwa.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

INJILI NI UWEZA WA MUNGU, UULETAO WOKOVU.

BABA UWASAMEHE

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Ukuta uliopakwa chokaa (Matendo23:3)?

Jibu: Tusome kuanzia mstari wa kwanza..

Matendo 23:1 “Paulo akawakazia macho watu; wa baraza, akasema, Ndugu zangu, mimi kwa dhamiri safi kabisa nimeishi mbele za Mungu hata leo hivi.

2 Kuhani Mkuu Anania akawaamuru wale waliosimama karibu naye wampige kinywa chake.

3 Ndipo Paulo akamwambia, Mungu atakupiga wewe, UKUTA ULIOPAKWA CHOKAA. Wewe umeketi kunihukumu sawasawa na sheria, nawe unaamuru nipigwe kinyume cha sheria?”

Makaburi ya zamani sio kama ya zama hizi.. Haya ya wakati yanachimbwa kuelekea chini, na mtu anawekwa kwenye jeneza na kisha kufukiwa chini, lakini makaburi ya zamani hayakuwa hivyo.. Bali yalikuwa katika mfumo wa pango, ambayo linafunguliwa na watu wanawekwa ndani ya hayo mapango, na kisha kwa nje yanarembwa kwa kupakwa chokaa au rangi nyingine ya kuvutia.

Sasa Bwana Yesu alitumia mfano wa makaburi hayo yaliyopakwa chokaa, ambayo kwa nje yanaonekana ni mazuri na kuvutia kana kwamba kuna kitu cha thamani ndani, kumbe ndani yake ni mifupa tu imejaa. Alitumia mfano huo kuwalinganisha na watu ambao kwa mwonekano wa nje wanaonekana wanafaa, wanaonekana na wacha Mungu, wanaonekana ni Watumishi wazuri, wanaonekana ni waimbaji wazuri, ni wakristo wa zuri, kumbe ndani yao ni MIFUPA TU!.. Ni wanafiki.. Bwana alisema Ole wa hao!!.

Mathayo 23;27 ‘Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na MAKABURI YALIYOPAKWA CHOKAA, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa MIFUPA YA WAFU, na uchafu wote.

28 Vivyo hivyo ninyi nanyi, kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, bali ndani MMEJAA UNAFIKI NA MAASI’.

Hizo ndizo tabia walizokuwa nazo makuhani na mafarisayo wa wakati huo, walikuwa wamejaa unafiki ndani yao, na wana maasi mengi ingawa kwa nje wanasifiwa na watu wote!!.

Na katika siku hizi zetu tunazoishi, mambo haya haya yanajirudia katikati ya watu wa Mungu.. tunaonekana kwa nje ni wakristo wazuri, ni wahubiri wazuri, ni waimbaji wazuri…lakini ndani tuna unafiki uliopitiliza.. Ndani tumejaa viburi, uongo, kutokusamehe, vinyongo, visasi na kila aina ya uchafu!

Bwana Yesu atusaidie tusiwe kuta zilizopakwa chokaa, bali tuwe wakamilifu nje na ndani..

1Wathesalonike 5:22 “jitengeni na ubaya wa kila namna.

23 Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi NAFSI ZENU NA ROHO ZENU NA MIILI YENU mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo”.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAKABURI YAKAFUNUKA; IKAINUKA MIILI MINGI YA WATAKATIFU WALIOLALA;

HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.

EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.

TIMAZI NI NINI

Na ulimi laini huvunja mfupa (Mithali 25:15)

Rudi nyumbani

Print this post

Nini tofauti ya Majira na Wakati?

Wakati ni “kipindi cha Muda” kwa kusudi Fulani, Kwamfano ukipanga kesho saa 7 mchana uende sokoni kununua bidhaa.. sasa huo muda wa “Saa 7 mchana” ndio unaoitwa “wakati wa kwenda kununua bidhaa”

Lakini “Majira” ni kipindi cha Muda ambacho ni cha “Msimu” Kwamfano Msimu wa mvua za masika hayo ni “majira ya masika”..msimu wa matunda ya maembe “hayo ni majira ya maembe”.. Msimu wa baridi, unaitwa “Majira ya baridi”.. Msimu wa joto huo unaitwa “majira ya joto”.

Mwanzo 8:22 “Muda nchi idumupo, MAJIRA YA KUPANDA, na mavuno, wakati wa baridi na wakati wa hari, wakati wa kaskazi na wakati wa kusi, mchana na usiku, havitakoma”

Sulemani alizidi kuliweka hili vizuri kitabu cha Mhubiri..

Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna MAJIRA YAKE, Na WAKATI kwa kila kusudi chini ya mbingu. 

2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;

3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga; 

4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza”

Unaweza kusoma zaidi juu ya Majira na Nyakati katika Mwanzo 7:21, Zaburi 1:3, Walawi 15:25,  na Ayubu 39:1.

Lakini pia yapo majira na nyakati katika makusudi ya Mungu. Na kusudi kuu ambalo ni muhimu kulijua majira yake ya kurudi kwa BWANA YESU MARA YA PILI!.. Hatuwezi kujua “Wakati” lakini “majira” ya kurudi kwake, tunaweza kuyajua… Ni kama vile hatuwezi kujua siku au wakati mvua itanyesha, lakini tunajua msimu, kuwa tukishaufikia huo msimu basi tunajua  siku yoyote mvua itaanza kunyesha.

Vile vile Bwana Yesu hakutoa wakati wa kurudi kwake, lakini alitoa “MAJIRA” Kwamba tuyafikiapo hayo majira basi tutajua kuwa WAKATI wowote atatokea mawinguni.

Marko 13:32 “Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba.

33  Angalieni, kesheni, [ombeni], kwa kuwa hamjui WAKATI ule utakapokuwapo”

Sasa Majira ya kurudi kwake ni yapi, ambayo tukiyatazama tutajua kuwa yupo mlangoni?.

Si mengine zaidi ya yale tunayoyasoma katika Mathayo 24, Luka 21 na Marko 13... kwamba kutatokea “Tauni” mahali na mahali, kutasikika tetesi za vita mahali na mahali, kutatokea na magonjwa mfano wa Tauni mahali na mahali, vile vile kutatokea na manabii wengi wa uongo ambao watawadanganya wengi na upendo wa wengi utapoa na maasi yataongezeka.

Hivyo tukishaona hizo dalili basi tunajua kuwa tayari tumeingia katika MAJIRA YA KURUDI KWAKE…na kwamba wakati wowote atatokea mawinguni, na hivyo tunapaswa tuchukue tahadhari… Na majira yenyewe ndio haya tuliyopo mimi na wewe..

Ndugu yangu Yesu anarudi wakati wowote!!, na yeye mwenyewe alituonya tuwe macho!, tukeshe katika roho kila siku, ili siku ile isije ikatujia ghafla..

Lakini tukifumba macho yetu na kukataa kuyatazama haya majira na kuchukua tahadhari.. basi tutaangukia katika like kundi la wanafiki Bwana Yesu alilolitaja katika Luka 12:54-56 na siku ile itatujia ghafla na hatutapona.

Luka 12:54  “Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.

55  Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.

56  Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, BASI, KUWA HAMJUI KUTAMBUA MAJIRA HAYA?”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

WAKATI ULIOKUBALIKA NALIKUSIKIA

Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

KUNA NGUVU YA ZIADA KATIKA KULING’ANG’ANIA KUSUDI LA MUNGU.

KUOTA UNAENDESHA GARI.

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

Rudi nyumbani

Print this post

Nzige, Parare, madumadu na tunutu ni wadudu gani? (Yoeli 2:25)?

Swali: Hawa wadudu, tunaowasoma katika Yoeli 2:25  (Nzige,Parare, madumadu na tunutu) ni wadudu gani na wanabeba ujumbe gani kiroho?

Tusome,

Yoeli 2:25 “Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na NZIGE, NA PARARE, NA MADUMADU, NA TUNUTU, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu”.

Hizi ni jamii za wadudu waharibifu wanaokula mazao hususani ya nafaka!.(Tazama picha juu)

1. NZIGE.

Hii ni jamii ya Panzi, ambayo ndio jamii kubwa kimaumbile kuliko jamii zote za panzi, Nzige wanasifa ya kutembea kimakundi na wanahama kutoka ukanda mmoja kwenda mwingine, na wanapotua mahali wanaharibu mazao ndani ya muda mfupi sana. Sifa ya nzige ni kwamba hawana kiongozi kama walivyo wadudu wengine kama Nyuki au Mchwa. (Soma Mithali 30:27).

Mfano wa hao Nzige ni wale Wamisri walioletewa na Mungu, ambapo walitua na kula kila mmea uliopo juu ya uso wa nchi yote ya Misri kasome (Kutoka 10:12-15), Na pia jamii ya mfano wa Nzige ni wale waliotua katika sehemu ya ukanda wa Afrika mashariki, wajulikanao kama Nzige wa Jangwani.

Lakini Nzige wanatabia ya kula Matawi ya Nafaka na kubakisha mapengo mapengo na kisha kuondoka.

2. PARARE.

Parare ni jamii nyingine ya Panzi, ambayo yenyewe inakula sehemu zile Nzige (walizobakisha/walizosaza). Parare kimaumbile ni wadogo kuliko Nzige, na kimwonekano wanayo miiba katika Miguu.. Parare si waharibifu kama Nzige, ingawa kwa nafaka ambazo tayari zimeshaharibika basi wenyewe wanaongezea uharibifu kwa kula vile vilivyosalia.

3. MADUMADU.

Madumadu ni jamii ya Panzi wadogo, wale (wanaokaa katika Nyasi)..Hii ndio jamii ya panzi wadogo kuliko wote, na sifa yao kubwa ni kula sehemu za majani zilizo ndogo sana, ambazo Nzige wala Parare hawawezi kula.

4. TUNUTU.

Tunutu ni vimelea vidogo kabisa vya wadudu, ambavyo vipo kama minyoo. Wadudu wengi warukao kabla ya kufikia hatua ya kukomaa huwa wanapitia hii hatua, ambapo wanakuwa kama viminyoo vidogo ambayo huwa vinakula mabua au sehemu ya majani ambayo Nzige, Parare, au Madumadu hawawezi kula. (Tazama picha chini)

Sasa tukirudi katika hiyo Yoeli 2 kwanini Bwana awataje wadudu hao?

Ili tuelewe vizuri hebu tusome tena kuanzia mstari wa 1.

Yoeli 1:1 “Neno la Bwana lililomjia Yoeli, mwana wa Pethueli.

 2 Sikieni haya, enyi wazee; Sikilizeni, enyi wenyeji wote wa nchi. Je! Mambo haya yamekuwako katika siku zenu, Au katika siku za baba zenu? 

3 Waarifuni watoto wenu habari yake, Watoto wenu wakawaambie watoto wao, Na watoto wao wakakiambie kizazi kingine.

 4 YALIYOSAZWA NA TUNUTU YAMELIWA NA NZIGE; NA YALIYOSAZWA NA NZIGE YAMELIWA NA PARARE; NA YALIYOSAZWA NA PARARE YAMELIWA NA MADUMADU

5 Levukeni, enyi walevi, mkalie; Pigeni yowe, ninyi nyote mnywao divai; Kwa sababu ya divai mpya; Maana umekatiliwa mbali na vinywa vyenu”

Umeona hapo?.. Bwana anamwonesha Yoeli hali ya kimwili ya wana wa Israeli jinsi alivyowapiga kwa Hawa wadudu Nzige, Parare, Madumadu, na Tunutu kutokana na Makosa yao. (Ambapo janga hili lilitokea dhahiri kabisa katika Israeli kwa miaka kadhaa, wakaishiwa chakula mpaka sadaka za unga zikakoma kutolewa katika nyumba ya Mungu kutokana na upungufu wa chakula).

Sasa wadudu hawakuishia kuwa wa kimwili tu, bali waliendelea kuwa hadi wa kiroho.. Maana yake ni kwamba Bwana kawaletea Nzige katika roho, Parare katika roho, Madumadu katika roho, na Tunutu katika roho, na kuyaharibu maisha yao. Na hiyo ikasababisha maisha yao kupukutika hata vile vichache walivyobakiwa navyo pia vikapukutika kama vile madumadu wanavyokula hata vile vidogo kabisa visivyoonekana.

Maana yake ni kwamba Mungu aliyaharibu maisha yao hata hawakubakiwa na kitu.. aliwaletea mikosi, na maafa na hasara, na wakaishiwa kabisa..kwasababu walimwacha!.

Hiyo ikifunua kuwa Na sisi tukimwacha Mungu, basi atalituma jeshi hili kuyaharibu maisha yetu, Utajikuta unafanya kazi kweli unapata pesa nyingi au faida nyingi, lakini itakapoishia hutajua, utajikuta tu hujasalia na chochote, utajikuta mara hili limezuka mara lile.. Ukiona hali kama hiyo basi jua kuwa ni Mungu kalituma jeshi hilo la Nzige, parare, madumadu na tunutu katika roho kula kila kitu ulicho nacho, na hata kukufanya usibakiwe na chochote.

Hagai 1:5 “Basi sasa, Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu.

 6 Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo; mnakula lakini hamshibi; mnakunywa lakini hamkujazwa na vinywaji; mnajivika nguo lakini hapana aonaye moto; na yeye apataye mshahara apata mshahara ili kuutia katika mfuko uliotoboka-toboka.

 7 Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu”.

Hivyo kama hujaokoka!..Fahamu kuwa maisha yako ya kimwili na kiroho kila siku yatazidi kuharibika, lakini kama leo hii ukiamua kumgeukia Mwokozi Yesu, kwa kutubu na kumaanisha kugeuka na kuacha dhambi kwa matendo, basi Bwana Yesu mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake mtakatifu na zaidi ya yote, atairejesha ile miaka yote ambayo imeliwa na Parare na Nzige, na Madumadu sawasawa na Neno lake katika Yoeli 2:25

Yoeli 2:22 “Msiogope, enyi wanyama wa kondeni; maana malisho ya jangwani yanatoa miche, na huo mti unazaa matunda yake, mtini na mzabibu inatoa nguvu zake.

 23 Furahini, basi, enyi wana wa Sayuni, mkamfurahie Bwana, Mungu wenu; kwa kuwa yeye huwapa ninyi mvua ya masika, kwa kipimo cha haki, naye huwanyeshea mvua, mvua ya masika, na mvua ya vuli, kama kwanza. 

24 Na sakafu za kupepetea zitajaa ngano, na mashinikizo yatafurika kwa divai na mafuta.

25 Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na NZIGE, NA PARARE, NA MADUMADU, NA TUNUTU, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu.

 26 Nanyi mtakula chakula tele na kushiba, na kulihimidi jina la Bwana, Mungu wenu, aliyewatendea mambo ya ajabu; na watu wangu hawatatahayari kamwe”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

kwanini Yakobo amefananishwa na mdudu?(Isa 42:14)

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)

Nini maana ya “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi”?

Ulafi ni nini kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

TUSIIFUATISHE KAWAIDA YA ULIMWENGU HUU.

Bwana Yesu atukuzwe daima. Karibu tena tuyasogelee maneno matukufu ya Mungu wetu Yehova; 

Maandiko yanasema hivi; 

Waefeso 2:1-2

[1]Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;

[2]ambazo mliziendea zamani KWA KUIFUATA KAWAIDA YA ULIMWENGU HUU, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;

Kumbe hii dunia ina “kawaida yake”..yaani kwa ufupi ina desturi yake ambayo imeshajizoesha tangu enzi na enzi, tangu Adamu alipoasi hata sasa, kuendana nayo.

Kwamfano leo ukienda nchi nyingi za magharibi au Asia kama vile Japan na Nepal, utakuta wanaume na wanawake sehemu za umma wanashea vyoo . Tofauti na huku kwetu, jambo hilo halikubaliwi kabisa na ni ajabu sana ukikutwa mtu unatumia choo cha jinsia tofauti.

Hivyo huku kwetu ni jambo lisilo na heshima lakini kwao ni “la kawaida”..ndio desturi yao.

Mataifa mengine kama Jamaika kuvuta bangi, ni haki kisheria lakini kwetu sisi, ni kosa..kwao ni “kawaida” kwetu sisi ni kosa la jinai..

Vivyo hivyo na hii dunia ina kawaida yake ambayo inakinzana na kanuni za ufalme wa mbinguni, Na sisi kama wakristo hatupaswi kuiiga, hata kidogo…japokuwa tutaonekana ni watu wa ajabu sana, kama mtume Petro alivyosema katika;

1 Petro 4:3-5

[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;

[4]MAMBO AMBAYO WAO HUONA KUWA NI AJABU YA NINYI KUTOKWENDA MBIO PAMOJA NAO katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana.

[5]Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa.

Mwanamke mmoja alinifuata na kuniambia mwanaume kama huna mojawapo ya starehe hizi yaani; 1) Ushabiki wa mpira, 2) wanawake,  3) pombe.. Wewe sio mwanaume kamili, una mapungufu. Nikasema ni kweli kwasababu kawaida ya ulimwengu huu, inalazimisha watu wawe na tabia hizo.

Binti unaambiwa usipokuwa na boyfriend, usipotumia kidogo mkorogo, usipovaa visuruali na visketi vifupi vifupi utaitwa mama/mbibi.. Wala usishangae kwasababu kawaida ya ulimwengu huu ni lazima utaonekana hivyo.

Lakini sisi kama wapitaji, makao yetu yaliyo mbinguni wala sio hapa duniani, hatuna ruhusu ya kuifuata, haijalishi itaonekana ni njema mbele ya dunia nzima..Sisi tunaifuata ‘kawaida ya mbinguni’..ambayo inatufundisha kuishi maisha ya utakatifu na usafi, kama Mungu mwenyewe na malaika zake walivyo watakatifu.

Hatuna desturi ya kuzini kabla ya ndoa, hatuna desturi ya kutembea na vimini, na mavazi ya utupu barabarani, hatuna ruhusa ya kuzifurahia anasa za ulimwengu huu, miziki, disco, kamari, pombe.

Warumi 12:2

[2]WALA MSIIFUATISHE NAMNA YA DUNIA HII; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.

Hivyo ndugu uliyeokoka, kamwe usitake kumpendeza mtu, ukafaraka na Mungu. Mambo mengi ya ulimwengu huu yamefaraka na Mungu..Huo ndio ukweli, Ukiupenda ulimwengu ukasema unampenda na Mungu pia hapo unajidanganya.

1 Yohana 2:15-17

[15]Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

[16]Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

[17]Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.

Chagua leo ni kawaida ipi, unasimama nayo..Je! ile ya mbinguni au ya duniani hii. Kamwe usijaribu kuwa hapo katikati, yaani vuguvugu..una hatari kubwa sana ya kutapikwa..kumchanganya Mungu na udunia, ni hatari kubwa sana.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia inamaanisha nini iliposema “wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa;?

KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU.

HAMA KUTOKA GIZANI

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

Vitabu vya Deuterokanoni ni vya kiMungu?

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

Rudi nyumbani

Print this post

USIZISHIRIKI DHAMBI ZA WATU WENGINE.

1Timotheo 5:22 “Usimwekee mtu mikono kwa haraka, wala usizishiriki dhambi za watu wengine. Ujilinde nafsi yako uwe safi”.

Hapa tunaona mtume Paulo, anampa Timotheo maagizo ya namna ya kuwa kiongozi bora (Askofu bora) wa makanisa la Mungu. Utaona anampa maagizo ya utaratibu wa kuwaandika wajane, kwamba ahakikishe wanaoandikwa ni wale walio wajane kweli kweli. (soma 1Timotheo 5:9-16).

Pia utaona anampa vigezo vya uongozi kwa viongozi wapya wa makanisa mapya, kwamba wanapaswa wawe wameshuhudiwa kuwa na sifa njema…ndipo awawekee Mikono!, lakini asiwe mwepesi wa kuwawekea mikono kwa haraka.

Na pia viongozi wa makanisa (yaani wachungaji, maaskofu na wote wanaosimama kama viongozi wa kanisa) basi wanapaswa wapewe heshima maradufu, maana yake Wakumbukwe katika riziki na mahitaji yao mara dufu zaidi ya wengine, kwasababu wanakesha kwaajili ya roho za watu, kuwaombea na kuwachunga na kufundisha.

1Timotheo 5:17  “Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha.

18  Kwa maana andiko lasema, Usimfunge kinywa ng’ombe apurapo nafaka. Na tena, Mtenda kazi astahili ujira wake”

Na zaidi sana asikubali Mashitaka ya Wazee kwa haraka, (Juu ya wachungaji, au mashemasi)..isipokuwa kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu.. kwamaana ibilisi anapenda kuwatumia watu kuzusha jambo Fulani la uongo juu ya kiongozi wa kanisa, lengo lake likiwa ni kuliharibu kundi hilo..

Kwahiyo hapa Mtume kwa uongozo wa Roho anamwonya Timotheo asiwe mwepesi kusikiliza au kuamini maneno yazungumzwayo au mashitaka yaletwayo dhidi ya viongozi wa makanisa.. Bali alichunguze jambo kwa makini mpaka atakapopata uthibitisho kamilifu kwa vinywa vya mashahidi wengi.

Lakini la mwisho kabisa Paulo anamwambia Timotheo kuwa ASIZISHIRIKI DHAMBI ZA WENGINE!.

1Timotheo 5:22 “Usimwekee mtu mikono kwa haraka, WALA USIZISHIRIKI DHAMBI ZA WATU WENGINE. UJILINDE NAFSI YAKO UWE SAFI”.

SASA NINI MAANA YA KUZISHIRIKI DHAMBI ZA WENGINE?

Kwanza ni muhimu kufahamu hao “wengine” wanaotajwa hapo ni akina nani?.. Wengine wanaotajwa hapo sio watu wa mataifa (yaani ambao hawajaokoka), la! Bali wengine wanaotajwa hapo ni “watu walio ndani ya Kanisa”. Watenda dhambi hawapo tu Bar!, au kwenye madanguro..bali wapo wengi pia kanisani.

Sasa Mtu wa kanisani anapofanya dhambi na wewe ukaiona na kuifanya kama hiyo hiyo? Maana yake na “wewe umeishiriki ile dhambi”, Kwamfano unapomwona mtu kaingia kanisani kavaa Nusu tupu, au kavaa nguzo zinazobana au zisizo na maadili, na wewe ukaona na ukamwiga, siku inayofuata na wewe ukavaa kama yeye..basi hapo kibiblia umeshiriki dhambi za huyo mwingine, hata kama kanisa zima linafanya mambo yasiyofaa sisi tunapaswa kushiriki dhambi zao, Kwasababu kuna madhara makubwa sana ya kushiriki dhambi za wengine.

Vile vile inawezekana wewe ni Mwimbaji ndani ya kanisa, lakini kuna waimbaji wenzako matendo yao ni ya giza, maandiko yanatuonya tusishiriki dhambi zao, maana yake tusiwe kama wao..

Vile vile wewe kama ni kiongozi (Mchungaji, askofu, shemasi)..halafu ukamwona kiongozi mwingine anafanya mambo yaliyo kinyume na maandiko, aidha ni mla rushwa, au ni mwizi, au mzinzi, au mlevi na anafanya mambo mengine mabaya na wewe ukaiga ule ubaya au ukaufumbia macho..kibiblia umeshiriki dhambi zake huyo kiongozi.

Na hapa Mtume Paulo anamwonya Timotheo kuwa ajihadhari asije akashiriki dhambi za wengine, ajilinde nafsi yake awe safi.

SASA MADHARA YA KUSHIRIKI DHAMBI ZA WATU WENGINE NI NINI?

Unaposhiriki dhambi za mwingine, maana yake MAPIGO nayo mnashiriki sawasawa, na LAANA pia mtashiriki sawasawa, maana yake kama Mungu amemkusudia kumwangamiza kabisa mtu huyo kutokana na tabia yake ya wizi anaoufanya kila siku ndani ya Nyumba ya Mungu, na wewe ukamwiga kwakufanya mara moja moja tu.. basi mtashiriki kiwango cha adhabu sawa.. Wewe unayeiba mara moja moja na Yule anayeiba kila siku wote kiwango chenu cha adhabu kitafanana, kwahiyo utajikuta wewe unayefanya kidogo mnapata adhabu sawa na Yule anayefanya sana.

Ndio maana Paulo anamwonya Timotheo asizishiriki dhambi za wengine, bali ajilinde nafsi yake awe safi.. Na sisi hatuna budi kuzilinda nafsi zetu ziwe safi.. Na tujiepushe na dhambi za wengine.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

REKEBISHA YAFUATAYO ILI MAMBO YAENDE SAWA.

Bwana alimaanisha nini kusema “Mwanafunzi hawi mkuu kuliko mwalimu wake”?

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Je ni kweli miaka yetu ya kuishi ni 80 tu (kulingana na Zaburi 90:10).

Rudi nyumbani

Print this post