Swali: Je Bwana YESU alikuwa amemfunga shetani wakati wa kuzaliwa kwake Kulingana na Mathayo 12:29?
Jibu: Turejee.
Mathayo 12:29 “Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, ASIPOMFUNGA KWANZA yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake”.
Jibu ni kwamba shetani hakuwa amefungwa wakati wa kuzaliwa Bwana YESU, na hata sasa shetani hajafungwa!, kwani Ingekuwa shetani amefungwa wakati wa kuzaliwa Bwana, basi Herode asingetafuta kumwua mtoto..
Mathayo 2:13 “Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize”.
Tukio hilo linaeleweka vizuri katika Ufunuo 12:1-6.
Vile vile Ibilisi asingesimama kumjaribu Bwana kule jangwani..
Mathayo 4:1 “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ILI AJARIBIWE NA IBILISI. 2 Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa. 3 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate”
Mathayo 4:1 “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ILI AJARIBIWE NA IBILISI.
2 Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa.
3 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate”
Na ikiwa shetani amefungwa leo, maasi yasingeendelea kuwepo na maandiko yasingetuonya kuwa tusimpe nafasi..
Waefeso 4:28 “wala msimpe Ibilisi nafasi. 28 Mwibaji asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akitenda kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe, apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji”.
Waefeso 4:28 “wala msimpe Ibilisi nafasi.
28 Mwibaji asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akitenda kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe, apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji”.
Maandiko yametabiri shetani kuja kufungwa katika ule utawala wa miaka elfu wa Bwana wetu YESU hapa duniani. Na utawala huo utaanza baada ya dhiki kuu kuisha, na hukumu ya Mungu kwa mataifa kupita (Ufunuo 16), hapo ndipo utawala wa miaka elfu moja utakapoanza na shetani (pamoja na majeshi yake) kufungwa kwa kipindi hiko.
Ufunuo 20:1 “Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake. 2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu; 3 akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache”.
Ufunuo 20:1 “Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake.
2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu;
3 akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache”.
Kwahiyo shetani kwasasa yupo na hakuwahi kufungwa wakati wowote huko nyuma, lakini atakuja kufungwa baada ya hukumu ya Mungu kwa mataifa inayotajwa katika Ufunuo 16.
Sasa swali kama ni hivyo je! Maandiko hayo katika Mathayo 12:29 yana maana gani?….
Turejee tena..
Haya ni maneno ambayo Bwana YESU aliyasema, akifundisha nguvu iliyo kuu/kubwa inapoingia mahali basi inateka au inafunga ile nguvu iliyo dhaifu.
Na ukisoma kuanzia juu kidogo utaona ni wakati ambapo Mafarisayo walimwona akitoa pepo kwa uweza wa Mungu, lakini wakasema yeye hatoi kwa uweza wa Mungu bali kwa uwezo wa Pepo mkuu aitwaye Beelzebuli, ambaye ni shetani mwenyewe.
Na Bwana akawahoji, akiwauliza yawezekanaje Shetani amtoe shetani mwenzake?..jambo ambalo haliwezekani!, vinginevyo ufalme wa giza hauwezi kusimama, lakini kama wakiona pepo katolewa maana yake katolewa kwa uweza wa Mungu, kwasababu kamwe shetani hawezi kumtoa shetani mwenzake.
Na ili kulifanya hilo lizidi kueleweka vizuri ndipo akatoa mfano mwingine kwamba… “Awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, ASIPOMFUNGA KWANZA yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake”
Ikifunua kuwa Bwana anapotoa pepo, kwanza anauteka ule ufalme wa giza (maana yake wote unakuwa chini ya amri yake) halafu ndipo anaamrisha pepo zitoke na kwenda atakako yeye soma Mathayo 8:28-32.
Sasa kitendo cha Bwana YESU kusimama na kuamrisha, maana yake mamlaka yake ni KUU inayoteka, na kufunga, na kuhamisha.. Na mamlaka hiyo hajabaki kwake tu peke yake, bali pia amewapa na wale wote wanaomwamini na kufanya mapenzi yake, kwamba kwa jina lake wanateka, na wanafunga na kuhamisha kila falme za giza.
2Wakorintho 10:4 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) 5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; NA TUKITEKA NYARA KILA FIKIRA IPATE KUMTII KRISTO; 6 tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”.
2Wakorintho 10:4 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; NA TUKITEKA NYARA KILA FIKIRA IPATE KUMTII KRISTO;
6 tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”.
Kwahiyo mantiki ya Bwana YESU hapo ya KUFUNGA, haikuwa ya kumfunga shetani asiwepo duniani, bali katika kuzifunga kazi za ibilisi na majeshi yake zisisimame mbele yetu. (lakini shetani yupo, na ataendelea kuwepo na kuwasumbua wale wote wasiomwamini na kumfuata Bwana YESU), lakini walio na Bwana shetani hana nguvu juu yao.
Mathayo 18:18 “Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni”.
Je umeokoka??..Hizi ni siku za hatari na BWANA anarudi. Na shetani anajua wakati wake uliobaki ni mchache sana, hivyo anafanya kazi kwa kasi sana kusudi asiende kwenye lile ziwa la moto peke yake.
Ufunuo 12:12 “Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu”
Je bado wewe ni rafiki wa dunia?, bado ni mshabiki wa mipira, bado unacheza Kamari, bado unavaa kidunia na kuupenda ulimwengu?
1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake. 16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia. 17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”
1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.
16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.
17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je YUDA alikuwa ni shetani kulingana na Yohana 6:70?
NIFANYE NINI NIMSHINDE SHETANI?
Je! Yesu aliwezaje kuchukuliwa na shetani juu ya kinara cha hekalu kujaribiwa?
Nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.
Kusujudu ni nini, na je tuna sharti la kusujudu kwa Mungu?
Rudi Nyumbani
Print this post
Swali: Kitani ni nini, na Bafta ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 19:9?
Isaya 19:9 “Tena wao wafanyao kazi ya kuchana KITANI watafadhaika, na hao pia wafumao BAFTA”.
1.KITANI
“Kitani” ni aina ya mmea unaostawi kwa sana maeneo ya mashariki ya kati, mbegu za mmea huu hutumika kwa matibabu lakini pia nyuzi zake hutumika kati kutengenezea mavazi mbalimbali ikiwemo mavazi ya harusi.
Ufunuo 19:7 “Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari. 8 Naye amepewa kuvikwa KITANI NZURI, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu. 9 Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu”.
Ufunuo 19:7 “Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.
8 Naye amepewa kuvikwa KITANI NZURI, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu.
9 Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu”.
Lakini si tu mavazi ya harusi bali pia ilitumika katika kutengenezea sanda za maziko.
Yohana 19:40 “Basi wakautwaa mwili wake Yesu, wakaufunga sanda ya KITANI pamoja na yale manukato, kama ilivyo desturi ya Wayahudi katika kuzika”
Mistari mingine inayozungumziwa mavazi ya Kitani ni pamoja na Mithali 31:22, Ezekieli 44:17, Danieli 10:4-5,Marko 14:51 na Ufunuo 18:16.
Vazi la kitani kiroho linafunua “Matendo ya Mtu” ikiwa ni kitani safi bali ni matendo safi, (Sawasawa na Ufunuo 19:8) lakini ikiwa ni kitani iliyoharbika, basi maana yake ni matendo yaliyoharibika.
2. BAFTA.
“Bafta” ni Kiswahili kingine cha “Pamba”.. Zao la pamba mbali ni kutumika katika matibabu, linatumika sana pia katika utengenezaji wa mavazi. Nyuzi za kitani zilitumika kutengeneza mavazi magumu nay ale ya nakshi, lakini pamba hutumika kutengenezea mavazi au mapazia yenye nyuzi laini na zenye kuhifadhi joto.
Ezekieli 9:11 “Na tazama, mtu yule aliyevaa bafta, mwenye kidau cha wino kiunoni, akaleta habari, akisema, Nimefanya kama ulivyoniamuru”.
Mistari mingine inayotaja mavazi na mapazia ya Bafta ni pamoja na Esta 1:6, Ezekieli 9:2 na Ezekieli 10:7.
Je unaye YESU maishani mwako?.. ni vazi gani ulilonalo kiroho?.. je ni kitani nyeupe? Au iliyoharibika? Je unayatunza mavazi yako au umeyaacha yaharibike?.. Kwa maarifa Zaidi ya namna ya kutunza mavazi yako kiroho fungua hapa >>
USIYAACHE MAVAZI YAKO NA KWENDA UCHI!
+255789001312/ +255693036618
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?
VAA MAVAZI, USIVALIE MAVAZI.
TUNZA MAVAZI YAKO NA FUA NGUO ZAKO!
KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.
Swali: Je Mungu anaua kama watu wanavyoua?
Jibu: Ndio Mungu pia anaua, maandiko yanasema hivyo..
Mathayo 10:28 “Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; AFADHALI MWOGOPENI YULE AWEZAYE KUANGAMIZA MWILI NA ROHO PIA KATIKA JEHANUM”
Sasa anayeweza kuua mwili na kuungamiza kwenye jehanamu ya moto ni MUNGU peke yake, mwanadamu anaweza tu kumuua mtu, lakini asiweze kuiona roho ya mtu wala asijue inakokwenda, lakini Bwana MUNGU anaweza kufanya yote (kuua mwili na kuangamiza roho vile vile)
Na maangamizi ya MUNGU ni makubwa na mabaya sana kwani hasira yake iwakapo haangalii wingi, ndicho kilichotokea wakati wa gharika ya Nuhu, dunia nzima iliuawa isipokuwa watu nane (8) tu ndio waliosalimika, na aliyewaua si shetani bali ni MUNGU mwenyewe.
1Petro 3: 20 “watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji”.
Na Bwana MUNGU anaua mtu/watu pale maovu/maasi yanapozidi sana, kiasi kwamba watu hao hata maonyo hawataki kusikia tena..
Kutoka 22: 22 “Usimtese mjane ye yote aliyefiwa na mumewe, wala mtoto yatima. 23 Ukiwatesa watu hao katika neno lo lote, nao wakanililia mimi, hakika yangu nitasikia kilio chao, 24 na hasira yangu itawaka moto, NAMI NITAWAUA NINYI KWA UPANGA; na wake wenu watakuwa wajane, na watoto wenu mayatima”
Kutoka 22: 22 “Usimtese mjane ye yote aliyefiwa na mumewe, wala mtoto yatima.
23 Ukiwatesa watu hao katika neno lo lote, nao wakanililia mimi, hakika yangu nitasikia kilio chao,
24 na hasira yangu itawaka moto, NAMI NITAWAUA NINYI KWA UPANGA; na wake wenu watakuwa wajane, na watoto wenu mayatima”
Maandiko mengine yanayoonyesha kuwa Mungu anaweza kuua ni pamoja na Amosi 2:3 na Ufunuo 2:23.
Lakini pamoja na kwamba Mungu ni mwingi wa hasira na pia anaua, na maangamizi yake ni makubwa na mabaya kuliko ya wanadamu, lakini bado yeye NI MWINGI WA REHEMA WALA SI MWEPESI WA HASIRA.
Nahumu 1:3 “Bwana si mwepesi wa hasira, ana uweza mwingi,…”
Hasira yake ipo mbali sana, na iko hivyo ili tupate nafasi ya kutubu kabla ya hasira yake kumwagwa.
2Petro 3:9 “Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba. 10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea”
2Petro 3:9 “Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.
10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea”
Je umempokea Bwana YESU au bado unajitumainisha na mambo ya mwilini, yaletayo hasira ya Mungu?..
Warumi 8: 13 “kwa maana kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi”
Bwana atusaidie.
SIKU YA HASIRA YA BWANA.
MWE NA HASIRA, ILA MSITENDE DHAMBI.
NIFANYE NINI NIWEZE KUDHIBITI HASIRA?
Wivu ni nini na kuna aina ngapi za Wivu?
UFANYE MOYO WA MUNGU UWAELEKEE WATU WAKE.
Swali: Je Bwana Mungu anayo jinsia kama wanadamu tulivyo na jinsia?
Jibu: Biblia inasema Mungu alimwumba “MTU” kwa mfano wake, na si “WATU” kwa mfano wake.
Na Mtu wa kwanza kuumbwa alikuwa ni ADAMU mwenye jinsia ya KIUME, na baadaye ndipo Hawa akaumbwa kutoka katika ule ubavu uliotwaliwa kwa Adamu.
Kwahiyo Mtu wa kwanza kuumbwa aliyekamilika ndio TASWIRA kamili ya MUNGU. Na Mtu huyo ni Adamu, aliye na jinsia ya kiume,
Sasa maadamu MUNGU si mwanadamu, hivyo yeye hana jinsia ya kiume, bali anao Utu wa KIUME, Kwasababu jinsia inahusisha mambo mengi ya kibinadamu ikiwemo mifumo ya uzazi. Lakini Mungu yeye sio kama sisi wanadamu, hivyo yeye anao utu wa KIUME na sio wa KIKE, na utu huo wa Kiume alionao ulianza kwake ndipo tukapewa sisi, na haukuanza kwetu kisha yeye akaiga baadae hapana!.
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba utu wa MUNGU ni wa kiume, na ndio sababu anajitambulisha yeye kama BABA kwetu, (Soma Mathayo 6:9) na sehemu nyingine anajitambulisha kama MUME (Soma Isaya 54:5), na hakuna mahali popote katika biblia panapoonyesha Bwana MUNGU akichukua uhusika wa kike, au utu wa kike.
Na la mwisho pia kufahamu ni kuwa, Mungu ni Roho, na tunamwabudu katika Roho na kweli.
Yohana 4:23 “Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu 24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”
Yohana 4:23 “Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu
24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”
Je umeokoka?, kama bado unangoja nini?..Hizi ni siku za mwisho na YESU yupo mlangoni, wakati wowote parapanda ya mwisho italia, je utakuwa wapi?
Anaposema mwanamume mmoja katika elfu nimemwona anamaana gani?
NI KIPI MUNGU ANACHOKITAZAMA ZAIDI, MOYO AU MWILI?
Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?
VIJANA NA MAHUSIANO.
Je suruali ni vazi la kiume tu?
Jibu: Ipo elimu isemayo kuwa “Mtu akiokolewa, ameokolewa na hivyo hawezi kupoteza wokovu”.. (Once saved, always saved).
Ni kweli msemo huo ni kama unataka kuleta maana kwamba mtu akiupokea wokovu hawezi tena kuupoteza…
Lakini maandiko yapo wazi yanayoonyesha kuwa mtu anaweza kuupoteza Wokovu.
Ufunuo 3:11 “Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, ASIJE MTU AKAITWAA TAJI YAKO”
Sasa jiulize, kama mtu hawezi kupoteza wokovu alionao, kwanini Bwana YESU asisitize kushika kile tulicho nacho.
Lakini pia, bado maandiko yanazidi kutufundisha kupitia safari ya wana wa Israeli, kwamba kweli walipata WOKOVU kutoka katika utumwa wa FARAO, lakini walipokuwa katika safari yao ya kuelekea KANAANI njiani waliupoteza ule wokovu, na Mtume Paulo kwa ufunuo wa Roho aliliona hilo pia na kulisema huku akilifananisha na Wokovu tuupatao, kwa njia ya kumwamini Bwana YESU na kuokoka kwamba tusipouthamini basi hatutapona kama wana wa Israeli walivyopotea.
Waebrania 2:1 “Kwa hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa. 2 Kwa maana, ikiwa lile neno lililonenwa na malaika lilikuwa imara, na kila kosa na uasi ulipata ujira wa haki, 3 SISI JE! TUTAPATAJE KUPONA, TUSIPOJALI WOKOVU MKUU NAMNA HII? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia”
Waebrania 2:1 “Kwa hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa.
2 Kwa maana, ikiwa lile neno lililonenwa na malaika lilikuwa imara, na kila kosa na uasi ulipata ujira wa haki,
3 SISI JE! TUTAPATAJE KUPONA, TUSIPOJALI WOKOVU MKUU NAMNA HII? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia”
Sasa kiswahili chepesi cha maandiko hayo ni hiki… “SISI JE TUTASALIMIKAJE TUSIPOUJALI NA KUUSHIKILIA ULE WOKOVU TULIOUPOKEA???” Na kumbuka hapo Mtume Paulo alikuwa haongei na watu ambao hawajaokoka, LA! Bali alikuwa anaongea na watu ambao tayari wanao wokovu, lakini huenda wanasuasua, hivyo anatoa hiyo tahadhari.
Wengi tusomapo mstari huo, tunawalenga wale wanaosikia injili lakini wanaifanya mioyo yao kuwa migumu kutii, lakini andiko hilo, halikuwa kwaajili ya watu walio nje ya Imani, bali kwa watu ambao tayari wanao WOKOVU.
Maana yake ni kwamba wokovu mtu anaweza kuupoteza kabisa kama hatakuwa makini, kama atakuwa sio mtu wa kujali.
Wanaoshikilia kuwa “Mtu akiokolewa ameokolewa hawezi kupoteza tena wokovu” wanasimamia mfano ule wa Baba na mtoto, kwamba mtoto akishazaliwa katika familia, hakuna kitakachoweza kumfanya asiwe mtoto wa baba yake.
Ni kweli kibinadamu hilo haliwezekani, aliyezaliwa katika familia ni lazima damu yake itabaki kuwa ya Baba yake hawezi kamwe kuupoteza ule wana (hiyo ni kweli kabisa)… Lakini kimaandiko sisi hatupokei uwezo wa kuwa wana kibinadamu, bali ni katika roho.. na kama uwezo huo unafanyika katika roho, basi pia katika roho unaweza kutanguka.
Ndicho kilichomtokea Esau, ni kweli alikuwa mwana wa kwanza wa Isaka, lakini alipoidharau nafasi yake ile ya uzaliwa wa kwanza ilihamia kwa ndugu yake Yakobo, yeye Esau aliendelea kuwa mzaliwa wa kwanza kwa tarehe za damu na nyama, lakini katika roho tayari ni mzaliwa wa pili, sasa kama mambo hayo yanaweza kubadilika hivyo, kwanini mtu asipoteze UWANA pale ambapo anaupuuzia wokovu wake? (Waebrani 12:16-17).
Ni wazi kuwa atapoteza ile hali ya kuwa Mwana wa Mungu, na atakuwa mwana wa Ibilisi katika roho, endapo asipouthamini wokovu wake.
2Petro 2:20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza. 21 Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa. 22 Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni”
2Petro 2:20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza.
21 Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa.
22 Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni”
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Mtu anaweza kupoteza Wokovu endapo hataushikilia ipasavyo na hataujali, na kumbuka siku hizi za mwisho mafundisho haya yanamea kwa kasi sana, ambayo yanawafundisha watu kuwa ukishamwamini BWANA YESU inatosha, ishi uishivyo, fanya ufanyalo, wewe mbinguni utaenda.
Ndugu usidanganyike, maandiko yameweka wazi kabisa kuwa pasipo Utakatifu! Hakuna mtu atakayemwona MUNGU, iwe Mchungaji, iwe nabii, iwe Raisi wa nchi, iwe Mtume, iwe Papa, iwe mwanaume iwe mwanamke, iwe mtu yoyote ule. PASIPO UTAKATIFU, HAKUNA MBINGU!!!
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, AMBAO HAPANA MTU ATAKAYEMWONA BWANA ASIPOKUWA NAO”
JE! SISI KAMA WAKRISTO NI DHAMBI KUSHEHEREKEA KRISMASI?.
Nini tofauti ya haya maneno. 1) KUOKOKA, 2) WOKOVU, 3) KUONGOKA.?
Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?
DHAMBI YA ULIMWENGU.
ESTA: Mlango wa 4
Swali: Patasi ni nini kama tunavyosoma katika kitabu cha Kutoka 32:4?
Jibu: Turejee..
Kutoka 32:4 “Akaipokea mikononi mwao akaitengeneza kwa PATASI, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa kuiyeyusha; nao wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.”
“Patasi” ni zana inayotumika kuchonga vitu vya jamii ya mbao au chuma. Kifaa hiki mara nyingi kinatumiwa na mafundi seremala, katika kuchonga mbao, na kuzitia urembo mbalimbali, au maandishi (Tazama picha chini).
Katika biblia neno hili limeonekana mara moja tu, pale ambapo wana wa Israeli walipojitengenezea sanamu ya ndama ili iwarudishe Misri walikotoka. Na waliifanya kwa kuyeyusha dhahabu zao na kisha kuzichonga kwa mfano wa ndama kupitia patasi.
Kutoka 32:1 “Hata watu walipoona ya kuwa Musa amekawia kushuka katika mlima, wakakusanyana wakamwendea Haruni, wakamwambia, Haya! Katufanyizie miungu itakayokwenda mbele yetu, kwa maana Musa huyo aliyetutoa katika nchi ya Misri hatujui yaliyompata. 2 Haruni akawaambia, Zivunjeni pete za dhahabu zilizo katika masikio ya wake zenu, na wana wenu, na binti zenu, mkaniletee. 3 Watu wote wakazivunja pete za dhahabu zilizo katika masikio yao, wakamletea Haruni. 4 Akaipokea mikononi mwao akaitengeneza kwa patasi, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa kuiyeyusha; nao wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri. 5 Naye Haruni alipoona jambo hili, akajenga madhabahu mbele yake; Haruni akatangaza akasema, Kesho itakuwa sikukuu kwa Bwana. 6 Wakaondoka asubuhi na mapema, wakatoa dhabihu, wakaleta sadaka za amani, watu wakaketi kula na kunywa, wakaondoka wacheze. 7 Bwana akamwambia Musa, Haya! Shuka; kwa maana watu wako uliowatoa katika nchi ya Misri wamejiharibu nafsi zao”.
Kutoka 32:1 “Hata watu walipoona ya kuwa Musa amekawia kushuka katika mlima, wakakusanyana wakamwendea Haruni, wakamwambia, Haya! Katufanyizie miungu itakayokwenda mbele yetu, kwa maana Musa huyo aliyetutoa katika nchi ya Misri hatujui yaliyompata.
2 Haruni akawaambia, Zivunjeni pete za dhahabu zilizo katika masikio ya wake zenu, na wana wenu, na binti zenu, mkaniletee.
3 Watu wote wakazivunja pete za dhahabu zilizo katika masikio yao, wakamletea Haruni.
4 Akaipokea mikononi mwao akaitengeneza kwa patasi, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa kuiyeyusha; nao wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.
5 Naye Haruni alipoona jambo hili, akajenga madhabahu mbele yake; Haruni akatangaza akasema, Kesho itakuwa sikukuu kwa Bwana.
6 Wakaondoka asubuhi na mapema, wakatoa dhabihu, wakaleta sadaka za amani, watu wakaketi kula na kunywa, wakaondoka wacheze.
7 Bwana akamwambia Musa, Haya! Shuka; kwa maana watu wako uliowatoa katika nchi ya Misri wamejiharibu nafsi zao”.
Kiroho jambo hili linaendelea hata sasa, sanamu zinaendelea kuchongwa hata sasa,..matendo yasiyofaa tuyafanyayo ndio ibada ya sanamu (soma Wakolosai 3:5) na tamaa zetu ndio “Patasi”.
JINSI WATU WANAVYOIUNDA SANAMU YA NDAMA MIOYONI MWAO.
HARUNI
FIMBO YA HARUNI!
USIABUDU SANAMU.
Kwanini ndugu wanaokaa pamoja wawe kama mafuta ya Haruni?
WhatsApp
Mwanzo 9:27 “Mungu AKAMNAFISISHE Yafethi, Na akae katika hema za Shemu; Na kaanani awe mtumwa wake”
Kunafisisha ni “KUTOA NAFASI au KUTANUA” .. Kwani mzizi wa neno hilo ni “Nafasi”…hivyo andiko hilo tunaweza kuliweka hivi… “Mungu akamtanue Yafethi, Na akae katika hema za Shemu; Na kanaani awe mtumwa wake”
Kwanini Mungu amtanue Yafethi na kumlaani Kanaani?.
Ni kwasababu Hamu alifanya dhambi ya kuutazama uchi wa baba yake.
Mwanzo 9:20 “Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu; 21 akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake. 22 Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje. 23 Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao. 24 Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea. 25 Akasema, Na alaaniwe Kaanani; Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake”.
Mwanzo 9:20 “Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;
21 akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.
22 Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje. 23 Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.
24 Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.
25 Akasema, Na alaaniwe Kaanani; Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake”.
Je umempokea YESU?.. Kama bado basi wakati uliokubalika ni sasa, fanya maamuzi kabla kabla hazijaja siku za hatari.
Kanaani ililaaniwa (Mwanzo 9:20-25,) kwanini Mungu awapeleke wana wa Israeli katika nchi iliyolaaniwa?
Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?
KWANINI NABII ISAYA ALIAGIZWA KUHUBIRI UCHI?
KUOTA UPO UCHI.
Je shauri la kuipepeleza Kanaani lilitoka kwa wana wa Israeli au kwa BWANA?
Jibu: Labda tuanzie mstari ule wa 18, ili tupate kuelewa vizuri.
Isaya 3:18 “Siku hiyo Bwana atawaondolea uzuri wa njuga zao, na kaya zao; 19 na pete za masikio, na vikuku, na taji zao; 20 na dusumali, na mafurungu, na vitambi, na vibweta vya marashi, na matalasimu; 21 na pete, na azama, 22 na mavazi ya sikukuu, na DEBWANI; NA SHALI, NA VIFUKO”
Isaya 3:18 “Siku hiyo Bwana atawaondolea uzuri wa njuga zao, na kaya zao;
19 na pete za masikio, na vikuku, na taji zao;
20 na dusumali, na mafurungu, na vitambi, na vibweta vya marashi, na matalasimu;
21 na pete, na azama,
22 na mavazi ya sikukuu, na DEBWANI; NA SHALI, NA VIFUKO”
Hayo ni aina ya mavazi waliovaa watu wa zamani, na baadhi ya hayo hata sasa yanavaliwa.. Sasa hapo yametajwa mengi, ikiwemo Dusumali, kwa urefu kuhusu Dusumali basi fungua hapa>>Dusumali ni nini katika biblia?
Lakini tutatazama hayo matatu yaliyotajwa katika huo mstari wa 22 ambayo ni “DEBWANI, SHALI, na VIFUKO”.
1. DEBWANI.
Debwani ni vazi refu linaloanzia mabegani mpaka miguuni, vazi hili linavaliwa na wanawake, (Tazama picha chini juu).
2. SHALI.
Shali ni vazi linalofanana na Debwani isipokuwa lenyewe linafunika kuanzia kichwa mpaka miguu, na hili linaweza kuvaliwa na jinsia zote, kwani kazi yake kubwa ni kujikinga na hali ya hewa, (baridi au mvua au upepo mkali), Shali ni Kiswahili cha “Overcoat” (Tazama picha chini).
3. VIFUKO
Vifuko si vazi bali ni mikoba inayobebwa na wanawake katika safari fupi. (Tazama picha chini)
Je umempokea Bwana YESU?
Kama bado ni nini kinachokusubirisha? Fahamu kuwa hizi ni siku za mwisho na Bwana amekaribia sana kurudi, je ni nini kipo katika akili yako wewe kama Baba, au mama au kijana?. Je unawaza nini?.. kujenga maisha ya kimwili, kula, kunywa na kuvaa??..au unawaza nini Zaidi.
Kama unawaza kupendeza na kujifanya mzuri kwa mavazi na mitindo ya kidunia, Neno la Mungu linasema siku inakuja ambayo Mungu atawaondolea watu wote uzuri wa njuga zao watu wote waliomwacha yeye..
Isaya 3:18 “Siku hiyo Bwana atawaondolea uzuri wa njuga zao, na kaya zao; 19 na pete za masikio, na vikuku, na taji zao;”
19 na pete za masikio, na vikuku, na taji zao;”
Achana na mapambo na fasheni za kidunia, mpokee YESU leo ukaoshwe dhambi zako.
TWEKA MPAKA VILINDINI.
MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 12 (Kitabu cha Isaya)
Ni kwa jinsi gani Mungu anapatiliza maovu ya baba zetu sawasawa na Kutoka 20:5-6?
SWALI: Shuleni tumefundishwa sayari zipi Tisa Lakini je maandiko yanasemaje kuhusu hili, je zipo kweli kwa idadi hiyo?
JIBU: Biblia si kitabu cha kisayansi, au cha taaluma yoyote, kwasababu lengo lake sio uvumbuzi na utafiti wa mambo ya ulimwenguni. Bali ni kumrejesha mwanadamu kwa muumba wake. Ni kitabu chenye msingi wa IMANI. Mambo yasiyothibitika kwa macho bali rohoni. Ni kitabu kielezacho njia ya ukombozi wa mwanadamu inayopatikana kupitia YESU KRISTO mwokozi wa ulimwengu.
Ijapokuwa vipo vifungu vichache vichache vinavyoelezea uhalisia wa elimu za duniani, lakini isidhaniwe kuwa lengo lake kuu ni kutoa taarifa za kila kitu kwenye hii dunia, bali mara nyingi huwa ni kuelezea vema habari husika ya rohoni iliyokuwa inazungumziwa hapo.
Tukirudi kwenye swali linalouliza kuhusu sayari, kwamba sayansi inatuambia zipo tisa, je biblia nayo inazitaja ngapi?
Kama tulivyotangulia kusema biblia haielezi kila kitu kuhusu dunia hii, bali inaeleza kila kitu kuhusu wajibu wa mwanadamu kwa muumba wake.
kuhusu Sayari biblia inazitaja bila shaka kwamba yeye ndio aliziumba, na magimba yote angali, ambayo yamejumuishwa katika neno jeshi la mbinguni .
Katika biblia sayari zimejatwa kwenye vifungu hivi;
Ayubu 38:32
[32]Je! Waweza kuziongoza Sayari kwa wakati wake? Au waweza kuongoza Dubu na watoto wake?
2 Wafalme 23:5
[5]Akawaondosha wale makuhuni walioabudu sanamu, ambao wafalme wa Yuda waliwaweka ili kufukiza uvumba katika mahali pa juu, ndani ya miji ya Yuda, na katika kila mahali, pande zote za Yerusalemu; na hao pia waliomfukizia uvumba Baali, na jua, na mwezi, na sayari, na jeshi lote la mbinguni.
Lakini biblia Haijatoa idadi, kama ni tisa, au mia au elfu Mungu alizoziumba, bila shaka ni nyingi, kwani turudipo kwenye sayansi, ndio tunathibitisha kuwa zipo mabilioni kwa mabilioni kwa mabilioni, hizi tisa walizoziona ni ambazo zipo tu kwenye mfumo wa jua letu..lakini huko angani kuna ma-jua mengi yasiyo hesabika na yote hayo yana sayari zake. Hata hivyo husema hizi nyota zote tuzionazo angani ni ma-jua kama hili letu isipokuwa tu yapo mbali sana.
Kwahiyo wanasayansi hututhbitishia zaidi uweza wa ajabu wa Mungu. Mambo yasiyoelezeka kwa ukuu na maarifa. Utukufu una yeye milele na milele. Amina.
Lakini Je! umempokea huyu Mungu aliyeumba mambo haya ya ajabu? kumbuka kumpokea yeye ni kumwamini Yesu. Kuaminije? . Ni kuamini ile kwa ile kazi yake kamilifu ya ukombozi wetu aliyotutenda sisi kwa kifo chake pale msalabani, iletao ondoleo la dhambi.
Ikiwa upo tayari leo kumpokea huyu mwokozi basi bofya hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Mtu wa Kwanza kufika mwezini
Je! dunia Ni duara, tufe au ipo kama sahani?biblia inasemaje?
ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.
SWALI: Naomba kufahamu Je! dunia Ni duara, tufe au ipo kama sahani imefunikwa na glasi kwa juu?.
JIBU: Jambo la msingi kufahamu kuhusu biblia ni kwamba, Biblia si kitabu cha kisayansi, au cha taaluma nyingine yoyote, kana kwamba unaweza vumbua elimu ya kidunia kupitia hicho. ukitegemea biblia ikupe majibu ya kitaaluma, kwa bahati mbaya unaweza usifikie lengo lako, kwasababu hakikuandikwa na Roho Mtakatifu kwa dhumuni hilo.
Biblia ni kitabu kinachoeleza sifa na tabia za Mungu, na jinsi mwanadamu anavyopaswa aoane nazo ili aweze tembea kama Mungu mwenyewe atakavyo. Ni kitabu kinachomrejesha mtu kwa muumba wake. Kwa hiyo mtaala wake ni tofauti kabisa na elimu za ulimwengu huu na mavumbuzi yake.
Ni ajabu kuona mkristo analazimishia kutafuta kanuni za kibiashara kwenye biblia. Huwezi ona huko “demand and supply” au “cash flow” au masoko ya hisa. Nenda tu darasani utafundishwa vema kanuni za uwekezaji na utafanya vema.
Vivyo hivyo na kwenye sayansi, huwezi ona aina za atomu au miamba, au mionzi, au chembe hai nyeupe za seli, au asprin huko . Nenda tu darasani utafundishwa vema yote hayo.
Ndio, hatuwezi kukataa zipo sehemu chache chache sana, zinazozungumzia elimu ya ulimwengu huu, lakini sio kwa lengo la kutufundisha kanuni zake, bali kwa lengo la kuelezea kwa undani jambo la kiroho katika tukio husika.
kwasababu biblia yenyewe inasema, hekima ya huu ilimwengu ni upumbavu mbele za Mungu, vilevile hekima ya Mungu ni upumbavu kwa ulimwengu. haviingiliani
1 Wakorintho 1:20
[20]Yu wapi mwenye hekima? Yu wapi mwandishi? Yu wapi mlete hoja wa zamani hizi? Je! Mungu hakuifanya hekima ya dunia kuwa ni upumbavu?
Kuhusu mapinduzi yote ya kiteknolojia ya wanadamu ambayo tunayaona sasa, na hata yatakayokuja huwezi yapata kwenye biblia, huwezi ona facebook, internet, vikizungumziwa kwenye biblia, sio kwamba Mungu hakuyaona au kuyajua, aliyajua sana, lakini yote hayo yamejumuishwa katika neno moja kuwa “maarifa kuongezeka” (Danieli 12:4)
Sasa tukirudi kwenye swali, ambalo linauliza je dunia ni tufe, duara au kama sahani imefunikwa na glass juu. Jibu ni lile lile hakuna taarifa za kutosha kwenye biblia zinazofafanua juu ya hilo lakini haya ni maandiko machache yanayotuambia kuhusu uhalisia wa dunia..
Isaya 40:22
[22]Yeye ndiye anayeketi juu ya duara ya dunia, na hao wanaokaa ndani yake huwa kama panzi; yeye ndiye azitandazaye mbingu kama pazia na kuzikunjua kama hema ya kukaliwa;
Kwa andiko hili, tunaonyeshwa kuwa dunia ipo katika duara, aidha kama tufe au mpira. lakini ni mzunguko, na sio kama sahani yenye glasi juu.
Hivyo tukirudi katika sayansi, ukisoma huko ndio utaelewa vizuri zaidi kuwa dunia ni mfano wa tufe, na sisi tukiwa tumenata-nata juu yake sio ndani yake.
Lakini tukumbuke kuwa haya ni maarifa ya mwanadamu, aliyopewa na Mungu ya kutafiti, na maarifa yake yanatabia ya kuboreka na kupinduka. Lakini kwa upeo wao wameweza kuthibitisha hilo.
MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!
Heshima ni nini kibiblia?
NYOTA ZIPOTEAZO.