Mtu wa Kwanza kufika mwezini

Mtu wa Kwanza kufika mwezini

Hakukuwa na mtu mmoja maalumu aliyefika mwezini, kulingana na Sayansi…Waliofika mwezini ilikuwa ni TEAM ya watu watatu (Neil A. Armstrong, Michael Collins na  Edwin E. Aldrin Jr.) Hao ndio waliokuwa ndani ya chombo cha Kwanza kulichotua mwezini, na wote watatu walikuwa ni wa-Marekani na safari yao iliyojulikana kama Apollo 11. Safari yao ilichukua siku 8 na masaa 3..Kwenda na kurudi, Na hiyo ilikuwa ni Mwaka 1969.

Sasa kumbuka tukio lolote linaloendelea duniani, linafunua tukio fulani linaloendelea katika roho.

Kama wanadamu wamefikia hatua ya kutengeneza chombo ambacho kimewafanya wafike juu zaidi ya mawingu, na kutua Mwezini. Kadhalika kuna kitu pia kinaendelea kutengenezeka  sasa katika roho, ambapo itafikia kipindi kitakamilika, na hicho kitalifanya kanisa kupaa juu sana zaidi ya mawingu na zaidi ya mwezi na kulifanya lifike mahali panapoitwa Mbinguni.

Na kama tunavyoona hiyo safari ya kwenda mwezini ilihusisha watu wachache sana, kadhalika, safari ya kwenda mbinguni itahusisha watu wachache sana, kwasababu biblia inasema mlango ni mwembamba na njia imesonga ielekeayo uzimani..

Hivyo ndugu, huu ni wakati wa kuingia ndani ya Kristo, kwani injili sasa inahubiriwa na teknolojia tunazoziona, Hizi ni zile siku za mwisho ambazo biblia imesema maarifa yataongezeka…Na tunaona jinsi yanavyoongezeka kwa Kasi, na katika roho pia yanaongezeka, watu wa Mungu hivi karibuni watafikia Imani ya kunyakuliwa na hivyo kuondoka kwenda mbinguni kwa Bwana..Je! na wewe utakuwa miongoni mwao?

Jibu unalo, tubu mpe Kristo maisha yako na uishi maisha yanayopatana na Toba yako.

Bwana akuabariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA

NYOTA ZIPOTEAZO.

KUONGEZEKA KWA MAARIFA.

ROHO SABA ZA MUNGU NI ZIPI? NA JE ZINATOFAUTIANA NA ROHO MTAKATIFU?


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments