Category Archive maswali na majibu

Mata ni nini (Mwanzo 27:3).

Mata ni kitu gani na imebeba  ujumbe gani kiroho?


Jibu: Turejee,

Mwanzo 27:2 “Akasema, Tazama, sasa mimi nimekuwa mzee, wala sijui siku ya kufa kwangu.

3 Basi, nakuomba, chukua MATA yako, podo lako na upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo;  4 ukanifanyie chakula kitamu namna ile niipendayo, ukaniletee, ili nile; na roho yangu ikubariki, kabla sijafa”.

“Mata” Ni jina jingine la “Silaha”. Kwahiyo badala ya kutumia neno “silaha” ni sahihi pia kutumia neno “Mata”.

Kwahiyo mstari huo wa tatu (3) ni sahihi kuuweka hivi,… “chukua SILAHA yako, podo lako na upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo ”

Na silaha hiyo inaweza kuwa mkuki, mshale au upanga, lakini katika andiko hilo silaha (Mata), iliyomaanishwa pale ni “Mshale”. Na kwanini ni mshale na si upanga wala mkuki?.. ni kwasababu kuna Podo imetajwa pale na upinde..

Maana yake huwezi kubeba upanga na upinde bila mshale, hivyo ni wazi kuwa Mata iliyomaanishwa pale ni mshale, kwasababu kuna upinde na Podo.

Sasa kwa maarifa kuhusu “Podo” na ufunuo wake kiroho waweza fungua hapa >>> Podo ni nini na umuhimu wake ni upi rohoni?

Sasa hizi zote ni silaha za mwili, lakini biblia inatufundisha kuwa zipo silaha za roho ambazo kila mkristo ni lazima azivae, na silaha hizo tunazisoma katika kitabu cha Waefeso 6:10-18, ambazo ni Chapeo ya Wokovu, Dirii ya Haki, Ngao ya Imani, Kweli, Upanga wa Roho, na Utayari miguuni pamoja na sala na maombi.

Na kwa silaha hizo pekee ndio tutaweza kumshinda adui yetu shetani, kwa mapana kuhusiana na silaha hizi jinsi ya kuvizaa na namna zinavyotenda kazi fungua hapa >>>MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

UTHABITI WA AGANO LA MUNGU KWA MKRISTO.

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.

KWANINI UPIGE MISHALE CHINI?

NDUGU,TUOMBEENI.

Nini maana ya  Mithali 21:1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana;

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya makuhani na walawi ni ipi?

SWALI: Na je! Walawi na makuhani katika kanisa la sasa ni watu wa namna gani?

JIBU: Mungu alilichagua kabila moja kati ya kumi na mbili liwe kabila lake takatifu litakalosimama katika kazi na shughuli zote za kidini na ibada Israeli.

Sasa katikati ya hawa walawi ndipo walipotolewa makuhani ndani yake. Hivyo makuhani wote walikuwa ni walawi lakini walawi wote si makuhani.

Hizi ndizo kazi za walawi.

  1. Walawi wanasimama kama wasaidizi wa makuhani katika shughuli zote za kiibada mbele za Mungu. Hesabu 1:50
  2. Walisimama pia kama waandishi wa torati,  kufundisha na kutafsiri maandiko kum 33:10,
  3. Walisimama kama walinzi wa mazingira yote ya hema/ hekalu hesabu 3:21-26
  4. Walisimama kama wajenzi wa hema, na kulihamisha na kulijenga tena pale walipobadili makazi, Hesabu 1:48-54
  5. Walisimama pia kama waaamuzi, walitoa hukumu ya mambo ya sheria. kumb 17:8-13
  6. Vilevile walisimama kama waimbaji mbele ya hekalu la Mungu daima, 1Nyakati 9:33

Na hizi ndizo kazi za makuhani.

  1. Walifanya kazi za upatanisho wa dhambi na makosa ya watu, kwa sadaka za kuteketezwa na damu ipelekwayo ndani ya hema mbele ya madhabahu.(Waebrania 10:11-18)
  2. Waliwajibika kuwabariki watu. Kumb 10:8
  3. Pia walifanya kazi ya kulibeba sanduku la agano, popote pale walipokwenda. kumb 31:9

Kwasasa, kila mkristo, ni Mlawi. Kwasababu tayari ameshapewa uwezo ndani yake na karama, ya kuifanya kazi ya Mungu pale tu anapookoka. Kila mmoja ni kiungo kwa mwenzake ndani ya kanisa. Lakini mkristo anabadilika kutoka kuwa mlawi mpaka kuwa kuhani pale anaposimama hasaa kwa ajili ya huduma/kazi  ya Mungu kwa watu wake.

Anapobeba maono Fulani, labda  tuseme kulichunga kanisa, huyo ni kuhani wa Mungu, na hivyo anaposimama na kuwabariki watu basi Baraka hizo huwafikia watu moja kwa moja kutoka kwa Mungu, mfano tu wa makuhani wa agano la kale. Au anapotumika katika kuwafundisha, kuwaombea wengine, kuwasimamia wengine, haijalishi ngazi aliyopo, au mahali au jinsia, huyo rohoni ni kuhani wa Mungu.

Hivyo kila mkristo anaouwezo wa kuwa kuhani wa Mungu, kwasababu lengo la Mungu ni sote tuwe makuhani wake, sio tu walawi, Na Yesu Kristo Bwana wetu akiwa ni kuhani Mkuu.

1Petro 2:9  Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;

Bwana akubariki.

Je! Kristo yupo moyoni mwako?

Kama ni hapana, basi wakati ndio huu, mgeukie, akusamehe dhambi zako, kwa kutubu na kumaanisha kabisa kuziacha, naye atakukomboa. Ikiwa upo tayari kwa ajili ya mwongozo huo, basi waweza fungua hapa kwa mwongozo >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Kwa namna gani tumefanyika Makuhani na Ufalme?.(Ufunuo 1:6)

WALAWI WALIKUWA WENYE MIOYO YA ADILI KWA KUJITAKASA KULIKO MAKUHANI.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Kwanini Yesu aliwaambia wale wakoma wakajionyeshe kwa makuhani?

Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana achukizwe na mtumwa yule aliyeficha talanta yake ardhini? (Mathayo 25:26-30)

Swali: Kwani kulikuwa na ubaya gani, wa bwana yule kurudisha talanta ile moja?, kwani hakupoteza kitu wala hajaleta hasara yoyote?..je kulikuwa na sababu gani ya yeye kuhukumiwa vile?.


Jibu: Ili tuweze kuelewa vizuri sababu ya mtumwa yule kuhukumiwa vile, tuisome habari yenyewe kwa uchache..

Mathayo 25:14  “Maana ni mfano wa mtu atakaye kusafiri, aliwaita WATUMWA WAKE, akaweka kwao MALI ZAKE.

15  Akampa mmoja talanta tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja talanta moja; kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake; akasafiri”.

Nataka tuzingatie hayo maneno mawili “Watumwa wake” na “Mali zake”.

Kwa haraka tukiisoma habari hii tunaweza kutafakari kuwa huyu mtu aliwekeza mali zake kwa “rafiki zake” au “ndugu zake”..

Ingekuwa heri kama ingekuwa ni “rafiki zake” au “ndugu zake” kwani hata wasingeleta faida yoyote angeweza kuwaelewa  lakini aliwekeza mali zake kwa “watumwa wake” ambao ni watu anaowalipa mshahara huenda kila siku au kil amwisho wa mwezi.

Sasa ili tuelewe vizuri, tengeneza picha una biashara yako (labda duka) halafu umeajiri mfanya kazi pale na kukubaliana naye mshahara, na ukaondoka na kurudi jioni na kukuta hajafanya kazi yoyote na Zaidi anakuambia fedha zako za mtaji zipo pale pale hajazigusa.

Bila shaka utachukizwa naye..kwanini?..cha kwanza ulitegemea kupata faida ndio maana wewe ukamweka pale, pili mshahara wake unatokana na faida katika hiyo kazi, kwa utendaji wake..

Kwahiyo kama hatafanya kazi yoyote na mwisho wa mwisho wa siku au mwezi atataka mshahara je utamlipa nini?…maana utakapofika mwisho wa mwezi atakudai mshahara, na wewe umeshaingia naye mkataba wa kumlipa..

Kwahiyo ni wazi kuwa ni lazima utakasirika, kwasababu kutokufanya kwake kazi ni hasara kwako, kwasababu mwisho wa siku ni lazima utamlipa, hivyo anakurudisha nyuma hata kama hajagusa mtaji wako, lakini mwisho wa siku utaathirika wewe katika wakati wa kumlipa mshahara..Hivyo ni hasara!!!

Ndicho kilichowatokea yule mtumwa aliyeficha talanta aliyopewa na bwana wake, maana yake ni kweli kairudisha ile talanta kama ilivyo, lakini mwisho wa mwezi atataka mshara (kwasababu yeye ni mwajiriwa na si ndugu/rafiki).. sasa bosi wake atatolea wapi fedha ya kumlipa ikiwa hajazalisha chochote?..

Ndio maana bwana wake akamwambia ni heri hata angeipeleka kwa watoa riba kuliko kuificha ardhini.

Hili ni fundisho kamili kwa wakristo kwamba vipawa na karama na uwezo tuliojaliwa na Bwana basi tutumie katika kumtumikia Mungu pasipo udhuru, kwasababu sisi ni watumwa wake!, ametuweka kwa faida yake…

Bwana atusaidie tusifiche talanta zetu ardhini bali tuzitendee kazi au tuzipeleke kwa watoa riba.

Mathayo 25:27  “basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake.

28  Basi, mnyang’anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi.

29  Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang’anywa.

30  Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”

Kufahamu kwa mapana maana ya “kupeleka fedha kwa watoa riba”, basi fungua hapa >>>Watoao riba ni akina nani? (Mathayo 25:27)

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

JINSI YA KUISHINDA HALI YA MSONGO WA MAWAZO.

BASI NIKAOGOPA, NIKAENDA NIKAIFICHA TALANTA YAKO.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

Nini maana ya.. “Utoapo sadaka mkono wako wa kuume usijue ufanyalo mkono wako wa kushoto”

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Rudi nyumbani

Print this post

Watoao riba ni akina nani? (Mathayo 25:27)

Swali: Je Bwana alimaanisha nini kusema “ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba” Je alikuwa na maana gani kusema vile?


Jibu: Mathayo 2:27 “basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake.

28  Basi, mnyang’anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi”

Ukisoma habari hiyo kuanzia juu utaona ni mfano uliokuwa unazungumzia watumwa ambao Bwana wao aliwapa talanta, na yule aliyepokea talanta tano, alizalisha nyingine tano, huenda kwa biashara aliyoifungua…na yule aliyepokea talanta mbili naye pia akazalisha nyingine mbili huwenda kutokana biashara aliyoifungua..

Lakini yule aliyepokea Moja, hakuenda kuifanyia kazi badala yake alienda kuificha chini ya ardhi, na siku ya mwisho akamrejeshea Bwana wake talanta ile ile moja aliyoipokea kutoka kwa Bwana wake, Lakini tunasoma Bwana wake akamkemea na kumwambia kuwa ni mtumwa “mbaya na mlegevu”.

Maana yake kama ameshindwa kabisa kwenda kuifanyia kazi basi angalau angeiweka kwa watoao riba, ..maana yake akakopeshe watu ambao wao wataenda kuizungusha ile fedha na hatimaye kumrejeshea iliyo yake na faida yake, lakini huyu mtumwa hakufikiri hata hilo, badala yake alienda kuifukia chini ya ardhi..

Sasa kiroho talanta zinafananishwa na “kipawa au uwezo” wowote ambao mtu kapewa na Mungu, unaomtofautisha yeye na mwingine.

Sasa kama mtu si Mtumishi wa madhabahuni, si mchungaji, si mwalimu, si mwinjilisti wa kwenda huku na kule kuhubiri habari njema… wala haoni kama anaweza kufanya kazi moja wapo ya hizo, lakini Mungu kamjalia kauwezo Fulani cha kifedha,

Basi kuliko kukaa bila kufanya kazi yoyote ya Mungu, ni afadhali fedha zake hizo ziwe chache au nyingi, aziwekeze katika injili (maana yake awape wanaokwenda kuieneza injili huku na kule) ili matunda yatakayopatikana kupitia injili watakaohubiri wengine kwa sapoti yake, basi na yeye awe mshirika wa matunda hayo kwasababu kachangia injili hiyo.. (Hiyo ndio maana ya kuweka fedha kwa watoa riba). Yeye  hajahubiri lakini kapeleka nguvu zake kwa wanaohubiri.

Lakini kama haubiri, haufanyi uinjilisti wowote, si mwalimu, si mchungaji, na hutaji hata moja ya fedha zako kuipeka kwenye injili, mwisho wake utakuwa kama wa huyu aliyeificha talanta yake ardhini.

Luka 16:9  “Nami nawaambia, Jifanyieni rafiki kwa mali ya udhalimu, ili itakapokosekana wawakaribishe katika makao ya milele”.

Bwana atusaidie tutumie talanta zetu vizuri.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

ANGALIA JINSI USIKIAVYO:

talanta ni nini

BASI NIKAOGOPA, NIKAENDA NIKAIFICHA TALANTA YAKO.

TENGENEZA MAMBO YA NYUMBA YAKO.

Azidishaye mali yake kwa riba, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.

Rudi nyumbani

Print this post

Kiti cha Musa ni kipi? (Mathayo 23:2)

Swali: Biblia ina maana gani kusema Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa? Je hiki kiti cha Musa ndio kipi?



Jibu: Turejee,

Mathayo 23:2 “Waandishi na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa”

“Kiti cha Musa” maana yake ni “Nafasi ya Musa”.. Leo hii tukisema mtu kaketi katika kiti cha Uraisi, maana yake ni kuwa “kachukua nafasi ya Uraisi”.

Sasa Musa alikuwa na nafasi gani?

Musa alikuwa na nafasi kuu mbili (2) mbele za wana wa Israeli.

   1) UALIMU.

Mtu wa Kwanza kuwafundisha wana wa Israeli HUKUMU, AMRI NA SHERIA za Mungu alikuwa ni MUSA.

Kumbukumbu 4: 14 “Bwana akaniamuru wakati ule NIWAFUNDISHE maagizo na hukumu, mpate kuzitenda katika nchi ile mtakayoivukia ili kuimiliki.

15 Jihadharini nafsi zenu basi; maana hamkuona umbo la namna yo yote siku ile Bwana aliyosema nanyi kutoka kati ya moto;

16 msije mkajiharibu nafsi zenu, mkajifanyia sanamu ya kuchonga, mfano wa sura yo yote, mfano wa mwanamume au mwanamke”.

Na mahubiri yake yaliendelea kuwa msingi wa marejeo kwa vizazi na vizazi mbeleni.

2) UONGOZI.

Hii ni nafasi ya pili aliyokuwa nayo Musa mbele ya wana wa Israeli:
Maandiko yanasema Mungu alimfanya Musa kuwa “Mkuu sana” mbele ya Misri na mbele ya wana wa Israeli. Kiasi kwamba maamuzi ya mwisho yalikuwa yanatoka kwake, kwa lugha nyepesi alikuwa ni kama Mfalme.

Kutoka 11:3 “…Zaidi ya hayo, huyo Musa ALIKUWA NI MKUU SANA katika nchi ya Misri, machoni pa watumishi wa Farao, na machoni pa watu wake”.

Soma pia Kutoka 18:13-24, utaona nafasi ya Musa katika kuwaamua Israeli.

Sasa baada ya Musa kuondoka (yaani kufa), Mafarisayo na Waandishi wakajiweka katika nafasi yake, maana yake wao ndio wakawa WAALIMU kama alivyokuwa Musa, na pia wakajiweka kuwa VIONGOZI kama alivyoukwa Musa, kiasi kwamba maamuzi ya mwisho yalikuwa yanatoka kwao.

Lakini ni heri kama wangekuwa wameketi kwenye nafasi hiyo ya Musa, na wakawa kama Musa..(yaani wacha Mungu kama Musa, au wapole kama Musa)..

Lakini wao walikuwa ni kinyume chake, walikuwa wanawatawala watu na kuwahukumu kwa sheria ya Musa lakini wao wenyewe ni wanafki mioyoni mwao.. mioyo yao ilikuwa ipo mbali na Mungu ingawa kwa nje wanaonekana ni waamuzi wazuri na viongozi wazuri wenye kusifiwa, lakini ndani yao wamejaa unafiki!.

Na Bwana YESU anatuonya tusiwe kama wao..

Mathayo 23:2 “Waandishi na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa”

3 basi, yo yote watakayowaambia, myashike na kuyatenda; lakini kwa mfano wa matendo yao, msitende; maana wao hunena lakini hawatendi

4 Wao hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole chao.

5 Tena matendo yao yote huyatenda ili kutazamwa na watu; kwa kuwa hupanua hirizi zao, huongeza matamvua yao;

6 hupenda viti vya mbele katika karamu, na kuketi mbele katika masinagogi,

7 na kusalimiwa masokoni, na kuitwa na watu, Rabi.

8 Bali ninyi msiitwe Rabi, maana mwalimu wenu ni mmoja, nanyi nyote ni ndugu.

9 Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni.

10 Wala msiitwe viongozi; maana kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo.

11 NAYE ALIYE MKUBWA WENU ATAKUWA MTUMISHI WENU.

12 Na ye yote atakayejikweza, atadhiliwa; na ye yote atakayejidhili, atakwezwa”.

Je YESU KRISTO ni Bwana na Mwokozi wa maisha yako?..Je una uhakika jina lako lipo katika kitabu cha uzima?.. Kama bado YESU hayupo maishani mwako ni heri ukampokea leo, maana saa ya wokovu na wakati uliokubali ni sasa.
Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NI KIZAZI KIPI WEWE UPO?

Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?

USIWE NA TAMAA YA CHAKULA KINGINE.

Rudi nyumbani

Print this post

Kunyoa denge ni kufanyaje na je ni dhambi? (Walawi 19:27).

Jibu: Tusome,

Walawi 19:27 “Msinyoe denge pembe za vichwani, wala msiharibu pembe za ndevu zenu”.

“Denge” ni mtindo wa kunyoa nywele kwa kuziacha nyingi upande wa juu (katikati) na kuziacha chache au kuzimaliza zote kwa upande wa chini (kuzunguka kichwa), kwa lugha ya sasa ni maarufu kama “Panki”.

Zamani sana nyakati za biblia mtindo huu waliokuwa wananyoa walikuwa ni watu wanaoabudu miungu, (wakiamini kwa kunyoa vile basi watajikinga na madhara Fulani ya kiroho), lakini siku zilivyozidi kwenda mtindo huu ulikuwa unatumiwa na watu wa ulimwengu kama fasheni, kiasi kwamba walionyoa hivyo basi walikuwa wanajulikana kama “wahuni” (wenye lengo la kupalilia zinaa na uasherati)  , lakini zama hizi mtindo huu unatumiwa na watu wote, hadi wachungaji!!, na hauonekani kuwa ni tatizo.

Sasa swali ni je! Ni dhambi kunyoa denge/panki?

Jibu ni Ndio!..na itabaki kuwa ndio pasipo kujalisha ni watu wangapi wanafanya hivyo..

Na kwanini ni kosa?…kwasababu ile ile ya kuchanja chale..

Walawi 19:27 “Msinyoe denge pembe za vichwani, wala msiharibu pembe za ndevu zenu. 

28 MSICHANJE CHALE YO YOTE katika nyama ya miili yenu kwa ajili ya wafu, wala msiandike alama miilini mwenu; mimi ndimi Bwana”.

Mtu anayenyoa denge, na anayechanja chale.. NI MAMOJA! Zote ni alama katika mwili ambazo zilitambulisha ibada Fulani, na mpaka leo zinafanya kazi hiyo hiyo… ni agano kamili katika mwili wa mtu linalohubiri ibada za miungu, haijalishi mtu huyo anajua au hajui..ndio maana kuna umuhimu mkubwa sana wa kufuatilia historia ya kitu kabla ya kukitumia kitu hicho/ mtindo huo…

Kwasababu si kila mtindo unaokubaliwa na wengi ni wa kiMungu, wala si kila desturi inayokubaliwa na kutumiwa na wengi ni ya kiMungu, nyingi ya tamaduni, desturi na mitindo ya kimaisha asili yake ni adui.

Na huwezi kukitumia kidonge chenye lengo la matibabu kama PIPI kwasababu tu kina utamu, halafu kisiwe na madhara kwako, vile vile huwezi kutumia elimu ya shetani au malighafi za shetani na kuzifanya mtindo, au urembo, halafu zisiwe na madhara kwako!..

Chale ni tiba ya shetani, denge ni tiba ya shetani, mitindo hiyo ilibuniwa na yeye kufanya tiba za kishetani… hivyo zinapotumiwa kama urembo! au fasheni! Ni kweli zitaleta mvuto kwa macho ya nje ya kibinadamu lakini zitabaki kubeba madhara yale yale katika kiroho. Ndio maana biblia ikakataza tusinyoe denge!.

Na hii sio sheria, kwamba ni agano la kale..na sasa tupo agano jipya hivyo kila kitu ni ruksa… Suala la ibada kwa miungu migeni litabaki kuwa katazo kwetu kwa nyakati zote.. Na denge, pamoja na chale ni ibada hizo…kama vile unavyoikimbia chale vile vile ikimbie kimbia denge.

Wala usiseme “ni nywele tu hazina maana”…Nywele zako zinamaana sana kiroho, ndio maana Bwana amekukataza usinyoe denge.. Bwana YESU alisema maneno yafuatayo..

Mathayo 10:30  “lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote”

Na tena alisema katika Luka..

Luka 21:18  “Walakini hautapotea hata unywele mmoja wa vichwa vyenu”

Sasa kama nywele za vichwa vyetu Mungu hazitazami wala hashughuliki nazo..basi atakuwa mwongo aliposema hapo kuwa “zimehesabiwa zote na tena hakuna hata moja itakayopotea”.. Lakini kama Mungu ni kweli, basi pia nywele zetu ni lazima tuziweke kama atakavyo..

Ukizipunguza punguza kama unavyotaka wewe unaharibu mahesabu ya kimbingu, ukizisuka suka na kuziongezea marasta unaharibu mahesabu ya kimbingu, na hivyo unajiingiza katika mahesabu ya kishetani.

Hivyo usinyoe denge mtu wa Mungu,  wala usisuke marasta…kama miaka ya zamani (katika biblia)mtu aliyenyoa denge alionekana ni mshirikina, iweje leo dunia ikuhubirie wewe ni mtakatifu?..kama miaka ya nyuma tu mtu aliyenyoa denge(panki) alionekana muhuni, iweje leo hii dunia ikuambie kuwa sio ni urembo?.. Huoni kama kuna udanganyifu mkubwa unaondelea sasa kutoka kwa adui..

Usiangalie ni idadi kubwa kiasi gani ya watu wananyoa denge, au wanasuka rasta na kuamini kuwa ni sawa, wewe liangalie Neno la Mungu..kwani nyakati tunazoishi ni za hatari.

Bwana akubariki.

Ikiwa bado hujaokoka fahamu kuwa Siku ya Wokovu ni leo, wala usingoje kesho.. kwa msaada wa kuongozwa sala ya kumkiri BWANA YESU basi fungua hapa >>>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Je kwa mkristo aliyeokoka, ni dhambi kunyoa ndevu zake?

Je! kuchora tattoo ni dhambi?

UMETEKWA NA UPENDO WA KRISTO?

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

Rudi nyumbani

Print this post

Madirisha ya mbinguni ni nini/yapi?(Mwanzo 7:11)

Ni neno lenye maana zaidi ya moja, kwamfano katika vifungu hivyo, Lilimaanisha chemchemi za maji zilizokuwa juu ya anga, Mungu alizifungua, mvua ikaanza kunyesha bila kipimo au kiasi, usiku na mchana kwa  siku arobaini.

Mwanzo 7:11 Katika mwaka wa mia sita wa maisha ya Nuhu, mwezi wa pili, siku ya kumi na saba ya mwezi, siku ile chemchemi zote za vilindi vikuu zilibubujika kwa nguvu, madirisha ya mbinguni yakafunguka.  12 Mvua ikanyesha juu ya nchi, siku arobaini mchana na usiku

Utakumbuka kuwa katika siku ile ya pili ya uumbaji, Mungu aliyatenga maji ya juu na ya chini (Mwanzo 1:6-7). Sasa yale ya juu, aliyaachia yote, yakawa yanashuka juu ya nchi na matokeo yake yakaifunika tena dunia. Hayo ndio madirisha ya mbinguni yaliyofunguliwa.

Ni neno pia linalomaanisha, Baraka za Mungu nyingi.

Kwamfano katika vifungu hivi, lilimaanisha hivyo;

Wafalme 7:2 Basi yule akida, ambaye mfalme alikuwa akitegemea mkono wake, akamjibu yule mtu wa Mungu, akasema, Tazama, kama Bwana angefanya madirisha mbinguni, je! Jambo hili lingewezekana? Akamwambia, Angalia, wewe utaliona kwa macho yako, lakini hutakula.

Hichi ni kile kipindi, Israeli imepitia njaa kali kiasi cha watu kulana, lakini Elisha akatokea na kumwambia Yule mkuu wa mfalme, kwamba Bwana atawaletea Baraka nyingi siku hiyo, na chakula kitakuwa kama si kitu tena Israeli. Yeye akadhihaki na kusema hata kama Mungu akifungua milango yake yote ya mbinguni  (Baraka) hilo jambo haliwezekani ndani ya siku moja. Elisha akamwambia utaliona kwa macho yako, lakini hutakula chochote katika hivyo.

Vilevile katika vifungu hivi, utaona vikimaanisha Baraka pia;

Malaki 3:10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.

Bwana anataka tumjaribu kiutoaji, ndipo atafanya muujiza wa kutufungulia Baraka zake nyingi ambazo hazitatosha hata mahali pa kuzihifadhia.

Hivyo Neno hili kibiblia lilimaanisha, hukumu ya Mungu iliyopitiliza, au Baraka za Mungu zilizopitiliza kufuata na tukio lenyewe lililoambatana nalo.

Bwana akubariki.

Je! Unatamani kushiriki Baraka zote za Mungu rohoni? Unatamani madirisha ya mbinguni yafunguliwe juu yako. Kama ni ndio basi sharti uokoke, umkabidhi Kristo maisha yako, kwa kutubu dhambi zako na kuwa tayari kumfuata Kristo, ili upate ondoleo la dhambi zako.

Ikiwa utapenda mwongozo wa sala ya kumpokea Kristo, baada ya toba yako ya kweli. Basi fungua hapa kwa sala hiyo>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NUHU WA SASA.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU BARAKA

Nini maana ya huu mstari; Mithali 10:22 “Baraka ya Bwana hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo”

JE NI KIKOMBE KIPI UTAKINYWEA SIKU ILE?

Rudi nyumbani

Print this post

Kuharimishwa ni nini, na kwanini Paulo aombe hivyo?(Warumi 9:2).

Jibu: Ili tuweze kuelewa vizuri tuanzia ule mstari wa kwanza, na tusome mpaka ule wa 5

Warumi 9:1  “Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu,

2  ya kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu.

3  Kwa maana ningeweza kuomba MIMI MWENYEWE NIHARIMISHWE NA KUTENGWA NA KRISTO KWA AJILI YA NDUGU ZANGU, JAMAA ZANGU KWA JINSI YA MWILI;

4  ambao ni Waisraeli, wenye kule kufanywa wana, na ule utukufu, na maagano, na kupewa torati, na ibada ya Mungu, na ahadi zake;

5  ambao mababu ni wao, na katika hao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili. Ndiye aliye juu ya mambo yote, Mungu, mwenye kuhimidiwa milele. Amina”

“Kuharimishwa” maana yake ni “kutengwa mbali na mtu/kitu (kwa ufupi kufanywa haramu)”.

Paulo aliomba kama ingewezekana Aharamishwe kwaajii ya ndugu zake katika mwili (yaani waisraeli), ili waokolewe.

Sasa kwanini aliomba vile, na je jambo hilo linawezekana?

Awali ya yote ili tuelewe vizuri hebu tuweke msingi kwanza kwa kuelewa agenda ya Wokovu ulioletwa na YESU KRISTO.

Wokovu kwamba ulianzia kwa Wayahudi, (soma Yohana 4:22) na baadaye ukahamia kwa watu wa mataifa.

Na kipindi Wokovu (injili) inahubiriwa kwa wayahudi, sisi watu wa mataifa tulikuwa tumeharimishwa, maana yake tulikuwa tumetengwa mbali na injili/neema, na kufanyika watu tusiostahili..

Waefeso 2:11 “Kwa ajili ya hayo kumbukeni ya kwamba zamani ninyi, mlio watu wa Mataifa kwa jinsi ya mwili, mnaoitwa Wasiotahiriwa na wale wanaoitwa Waliotahiriwa, yaani, tohara ya mwilini iliyofanyika kwa mikono;

12  kwamba zamani zile mlikuwa hamna Kristo, MMEFARAKANA NA JAMII YA ISRAELI, wageni wasio wa maagano ya ahadi ile. MLIKUWA HAMNA TUMAINI, HAMNA MUNGU DUNIANI”

Umeona?..kumbe kuna wakati sisi watu wa mataifa hatukuwa na Mungu (neema),Na wakati ulipofika waisraeli (wayahudi) walipomkataa Masihi YESU KRISTO, na kusema yeye siye yule aliyetabiriwa, Ndipo Ikafanya Neema iondoke kwao na kuja kwetu sisi watu wa mataifa, hivyo nao pia WAKAHARIMISHWA ili sisi tupate Neema..

Sasa Utauliza hilo tunalithibitisha vipi kimaandiko..

Warumi 11:30 “ KWA MAANA KAMA NINYI ZAMANI MLIVYOMWASI MUNGU, LAKINI SASA MMEPATA REHEMA KWA KUASI KWAO”

31  KADHALIKA NA HAO WAMEASI SASA, ILI KWA KUPATA REHEMA KWENU WAO NAO WAPATE REHEMA.

Soma pia  Matendo 28:28 na Matendo 13:46,utaona jambo hilo Zaidi.

Sasa Mtume Paulo kwa kulijua hilo kwamba “Neema imewaondokea Wayahudi wengi” na imeenda kwa watu wa MATAIFA, kwa mantiki hiyo hiyo akatamani kama ingewezekana IONDOKE kwake (yaani aharimishwe), ili irudi tena kwa WAISRAELI ndugu zake wapate kuokolewa.

Na neema ikiondoka juu ya mtu/watu maana yake ile nguvu ya kumwamini KRISTO inakuwa haipo tena!, kila kitu kumhusu YESU ni upumbavu kwa mtu huyo au watu hao, (Mfano wa PAULO alivyokuwa kabla ya kuokoka..alikuwa anaona injili ni upuuzi na Zaidi sana alikuwa anawaua wafuasi wa BWANA YESU). (Hiyo yote ni kutokana na neema kutokuwepo juu yake).

Sasa swali ni je! Jambo hilo aliloliomba Paulo linawezekana?..yaani Mungu anaweza kumharimisha yeye ili ndugu zake wapone?

Jibu ni LA! Ni jambo ambalo haliwezekani,..Paulo alisema vile kutokana na huruma na upendo kwa ndugu zake!..Ni sawa na mtu aliye mzima, aone ndugu yake anateseka na ugonjwa mbaya..na aombe ahamishiwe yale maumivu kwake kutokana na kumhurumia yule mgonjwa, na ndivyo Paulo alichokuwa anakiomba.

Kadhalika Mungu hawezi kuihamisha Neema aliyokupa na kuipeleka kwa mtu mwingine kwa wewe kumwomba...(hawezi kukupokonya uzima wa milele ikiwa umestahili uzima wa milele) Neema huwa inaondoka kutoka kwa mtu kwa njia ya matendo yake(kama matendo yake yakiwa hayafai, lakini si kwa kumwomba Mungu aihamishe kutoka kwako.

Je umeokoka?..kama bado unasubiri nini?

Fahamu kuwa tunaishi siku za mwisho na BWANA YESU yupo mlangoni.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.

JINSI YA KUITUMIA VYEMA NEEMA YA MUNGU ILIYO JUU YANGU.

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

MAMBO YATAKAYOTOKEA ISRAELI SIKU ZA HIVI KARIBUNI.

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

Rudi nyumbani

Print this post

Yahu ni nani? (Wimbo 8:6).

Jibu: Turejee,

Wimbo 8:6 “Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni MIALI YA YAHU”.

“YAHU” ni jina lingine la “YAHWE” ambalo ndilo “YEHOVA”.

Kutoka 6:2 “Kisha Mungu akasema na Musa, akamwambia, Mimi ni YEHOVA; 

3 nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao”.

Kwahiyo YAHU, YAHWE na YEHOVA ni jina Moja!

Lakini hapo katika Wimbo 8:6 maandiko yanasema kuwa “upendo una nguvu kama mauti”.. maana yake kama vile mauti ilivyo na nguvu kiasi kwamba wanaokufa ni ngumu kurudia uzima! Vile vile Upendo wa Mungu kwetu ni mkuu kiasi kwamba akitupenda ametupenda!, hakuna wakati atatuchukia, anaweza asipendezwe na sisi lakini si kutuchukia!.

Warumi 8:35 “Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?………

38  Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,

39  wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Lakini pia anasema wivu ni mkali kuliko Ahera..Ahera ni “Kaburi”, Kwa urefu Zaidi fungua hapa >>>Ahera ni wapi? Kama tunavyosoma katika biblia.

Na miali yake ni miali ya YAHU. Maana yake ni kuwa Mungu ana upendo lakini pia anawivu, huwezi kamwe kutanganisha vitu hivi viwili, UPENDO na WIVU.

Kwahiyo kama Mungu ametupenda, basi hapendi kuona tunaabudu miungu mingine, tukifanya hivyo tunamtia yeye wivu, umbao unaweza kutupeleka kaburini (Ahera).

Kutoka 20:3 “Usiwe na miungu mingine ila mimi.

4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, NI MUNGU MWENYE WIVU; NAWAPATILIZA WANA MAOVU YA BABA ZAO, HATA KIZAZI CHA TATU NA CHA NNE CHA WANICHUKIAO, 

6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.

YAHU atusaidie tusimtie Wivu, lakini tumpende, na vile vile upendo wake utubidiishe katika kuyafanya mapenzi yake.

Maran atha.

Mafundisho Mengine:

Wivu ni nini na kuna aina ngapi za Wivu?

UMETEKWA NA UPENDO WA KRISTO?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

IJUE HEKIMA YA MUNGU KATIKA KUKUINUA KIMAISHA.

WEKA KUMBUKUMBU YA MAMBO BWANA ANAYOKUFANYIA KWASABABU YATAKUFAA MBELENI.

Rudi Nyumbani:

 

Print this post

Falaki ni elimu gani? (Isaya 47:13).

Falaki ni nini katika biblia?

Jibu: Turejee,

Isaya 47:12 “Simama sasa na uganga wako, na wingi wa uchawi wako, uliojitaabisha nao tangu ujana wako; labda utaweza kupata faida, labda utaweza kushinda. 

13 Umechoka kwa wingi wa mashauri yako; basi, na WASIMAME HAO WAJUAO FALAKI, wazitazamao nyota, watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo yatakayokupata”.

“Falaki” ni “elimu ya nyota na sayari na jua”.

Wanaofanya Falaki, wanaamini kuwa  “mpangilio wa nyota, mwezi na jua na sayari angani, unaathiri tabia ya nchi na tabia ya mtu/watu”. Jambo ambalo kwa sehemu moja ni kweli na sehemu nyingine uongo!.

Ni kweli Mpangilio wa Jua na mwezi, unaweza kuathiri tabia ya nchi, kama  vile vipindi vya mvua, kiangazi, au kipupwe….ipo miezi ambayo mvua inanyesha, na miezi ambayo mvua hainyeshi, ipo miezi ya kiangazi na miezi ya kipupwe…Majira ya mwezi wa 6 na 7 ni Kipindi ambacho jua linakuwa mbali na dunia na kweli nchi inaathirika na baridi kali, katika ukanda wa kusini wa dunia.

Vile vile tabia za mimea zinaathiriwa na majira na nyakati, yanayotokana na mpangilio wa mwezi na jua angani, mfano tabia za miembe kuzaa maembe zinaathiriwa na mwezi wa 12, kwamba yanapofika majira ya mwezi huo wa 12 mpaka wa 1 basi miti yote ya miembe inazaa sana, tofauti na kipindi kingine chote (kwahiyo kwa sehemu ni kweli).

Sasa kwa mantiki hiyo wana-falaki wanaamini kuwa kama mpangilio wa jua, mwezi na nyota angani unaweza kuathiri mazingira na hali ya hewa, basi vile vile mpangilio huo huo unaweza kuathiri tabia za watu, na hisia zao, na maamuzi yao na hata hatima yao!.

Kwamba kila tarehe na mwezi unabeba matukio yake kulingana na mtu na mtu, na pia kulingana na tarehe aliyozaliwa, vile vile mpangilio wa nyota na mwezi unaweza kuelezea ni kitu gani mtu atafanya, au atakitenda, au kitampata, vile vile ni bahati gani ipo mbele yake au hatari gani inamkabili.

Kwahiyo wote waliohitaji kujua mambo yatakayowapata mbeleni waliwatafuta hawa wana-Falaki, au kwa lugha nyingine wanajimu kujua hatima zao.

Lakini swali ni je! Elimu hii ina ukweli wowote na je wakristo ni sahihi kuitafuta, ili kujua hatima zetu kupitia falaki?

Jibu ni LA! Elimu hii haina ukweli wowote, mpangilio wa sayari na nyota, na mwezi hauwezi kuelezea tabia, hisia, maamuzi au hatima ya Mwanadamu!…mpangilio huo unaweza kufaa katika utabiri wa hali ya hewa na misimu ya kupanda na kuvuna (tena kwa sehemu ndogo) lakini hauwezi kutabiri maisha ya mtu.

Maisha ya mtu hayatabiriwi wala kusomwa kwa kutazama jua, au mwezi au nyota au sayari, kama ndivyo kulikuwa hakuna haja ya Kristo kuja, au hata kama angekuja basi angetuhubiria sana hiyo elimu, bali maisha ya mtu yanatabiriwa kwa KULITAZAMA NENO LA MUNGU peke yake!.

Ukitaka kujua kesho yako itakuwaje, isome biblia, itakuambia sio tu kesho utakuwa wapi, bali MILELE UTAKUWA WAPI!!!.

Utauliza vipi wale Mamajusi, mbona walioiona nyota ya Bwana YESU kutoka mashariki?.

Mungu alipenda kutumia ishara ya nyota kuelekeza utukufu wa mwanae alipozaliwa, lakini hakuwa anahubiri elimu ya nyota pale!, ni sawa na alivyotumia ishara ya Nguzo ya wingu au nguzo ya moto juu ya wana wa Israeli walipokuwa jangwani,.. ilikuwa ni kwa lengo la kuelekeza utukufu wa wana wake mahali walipo, lakini hakuwa anahubiri elimu za mawingu na moto, kwamba zikasomwe kwa bidii ili kuelezea utukufu juu ya mtu/watu.

Vile vile leo hii shetani anapenyeza elimu hii ya Nyota(Falaki) ndani ya kanisa kwa kasi sana!. Elimu hii inatoka kwa waganga na inahamia kanisani kwa kasi sana..Watu hawasomi tena biblia wanatafuta kusomewa nyota zao! Hawaombi tena kulingana na Neno wanaombea nyota kwa kurejea elimu ya falaki.

Ndugu usidanganyike!..Elimu ya nyota (Falaki) ni elimu ya shetani asilimia mia.

Kama unataka kusafisha hatima yako itii biblia, wala usitafute maombi ya kutakasiwa nyota!, hiyo ni elimu nyingine!… Vile vile ukitaka kujua kesho yako itakuwaje kasome biblia, usitafute utabiri wa kusomewa nyota kutoka kwa yoyote yule iwe mganga au anayejiita mtumishi wa Mungu.. Biblia pekee ndiyo itakayokuonyesha tabia yako na kukupa utabiri sahihi wa maisha yako ya kesho na ya milele.

Je umemwamini Yesu?, je umebatizwa ubatizo sahihi? Je umepokea Roho Mtakatifu?.

Bwana Yesu anarudi.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MSHIKE SANA ELIMU.

NYOTA ZIPOTEAZO.

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

MIEZI 13 YA KIYAHUDI.

Rudi nyumbani

Print this post