JE NI KIKOMBE KIPI UTAKINYWEA SIKU ILE?

JE NI KIKOMBE KIPI UTAKINYWEA SIKU ILE?

Rohoni vipo vikombe viwili ambavyo Mungu ameviandaa kwa wanadamu.

  1. Kikombe Cha kwanza kinajulikana kama kikombe Cha ghadhabu ya Mungu.
  2. Na kikombe Cha pili kama kikombe Cha baraka/ wokovu.

KIKOMBE CHA GHADHABU

Kama hufahamu, Mungu Huwa anajiwekea “akiba” ya hasira yake. Ikiwa na maana si mwepesi kutimiliza hasira yake Kwa haraka, Huwa anaikusanya na siku ikifika kipimo chake Kisha akaimimina hapo huwa hapana Rehema Tena. Ni kilio na kusaga meno!.

Soma

Nahumu 1:2-3

[2]BWANA ni Mungu mwenye wivu, naye hujilipiza kisasi; BWANA hujilipiza kisasi, naye ni mwingi wa hasira; BWANA hujilipiza kisasi juu ya adui zake, huwawekea adui zake akiba ya hasira.

[3]BWANA si mwepesi wa hasira, ana uweza mwingi, wala hatamhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; BWANA ana njia yake katika kisulisuli na tufani, na mawingu ni mavumbi ya miguu yake.

Mifano halisi ya hasira ya Mungu tunaiona kipindi Cha gharika, kipindi Cha sodoma na Gomora. Na ameahidi pia katika siku za mwisho ataleta hukumu hiyo Kwa ulimwengu mzima, na itatimilika yote katika lile ziwa la moto.(2Petro 3:7-5)

Utapata majibu Kwanini Leo,  Mungu anaonekana kama vile yupo kimya Kwanini uovu unaendelea hachukui hatua stahiki duniani, fahamu ni kwamba anangoja kipimo chake kijae, kikombe kijae ili waovu wanywe ghadhabu yake yote. Ndivyo alivyowaambia Ibrahimu kuhusu kuangamia Kwa wakaanani, alikuwa anasubiria uovu wao utumie (Mwanzo 15:16), na siku ilipofika Yoshua aliwaangamiza wote.

Hivyo mtu unapokuwa mwovu unakijaza kikombe Cha ghadhabu ya Mungu, Na kama dhiki kuu itakupita basi utakatana na kikombe hicho siku Ile ya hukumu, utakinywa Kwa kutupwa kwenye lile ziwa la moto.

Ufunuo wa Yohana 14:10

[10]yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo.

KIKOMBE CHA BARAKA.

Lakini pia watakatifu nao Bwana anawawekea akiba ya Baraka na mema. Kwa maisha ya haki wanayoishi sasa hapa duniani, usidhani kuwa hayo mema unayotendewa ndio malipo stahiki Kutoka Kwa Mungu wako,hapana..Bwana anakijaliza kikombe Cha watakatifu na siku Ile tutakinywea na Yesu Kristo kule mbinguni kwenye Karamu ya Mwana kondoo. Haleluya.

Mathayo 26:27-29

[27]Akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, Nyweni nyote katika hiki;

[28]kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.

[29]Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.

Hapo ndipo tutakapoona wema wote wa Mungu maishani mwetu. Tutakinywea kikombe hicho, tutamiminiwa thawabu na Raha isiyo na kifani. Hapo ndipo tutakapojua ni jinsi gani Mungu anavyotujali. Usikose mbingu ndugu, kosa vyote lakini Unyakuo usikupite.

Ndugu ukiona unamtumikia Mungu Leo huoni faida yoyote, kama vile huoni malipo yoyote, ,tambua kuwa Bwana anaona..anaweka tu akiba, utaipokea Raha siku Ile itakapofika.

Unapojitesa kuishi maisha ya haki, halafu unaona kama vile Mungu hakujali..usijidanganye kikombe unakijazilisha tu. Wakati wa kukinywea utafika.

Soma haya maneno ya faraja Mungu aliyoyatamka Kwa watu wake..

Malaki 3:13-18

[13]Maneno yenu yamekuwa magumu juu yangu, asema BWANA. Lakini ninyi mwasema, Tumesema maneno juu yako kwa namna gani?

[14]Mmesema, Kumtumikia Mungu hakuna faida; na, Tumepata faida gani kwa kuyashika maagizo yake, na kwa kwenda kwa huzuni mbele za BWANA wa majeshi?

[15]Na sasa twasema ya kwamba wenye kiburi ndio walio heri; naam, watendao uovu ndio wajengwao; naam, wamjaribuo Mungu ndio waponywao.

[16]Ndipo wale waliomcha BWANA waliposemezana wao kwa wao. Naye BWANA akasikiliza, akasikia; na kitabu cha ukumbusho kikaandikwa mbele zake, kwa ajili ya hao waliomcha BWANA, na kulitafakari jina lake.

[17]Nao watakuwa wangu, asema BWANA wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam, watakuwa hazina yangu hasa; nami nitawaachilia, kama vile mtu amwachiliavyo mwanawe mwenyewe amtumikiaye.

[18]Ndipo mtakaporudi, nanyi mtapambanua kati ya wenye haki na waovu, na kati ya yeye amtumikiaye Mungu na yeye asiyemtumikia.

Bwana atupe macho ya kumwelewa yeye. Kijazilishe kikombe Cha wokovu wako. Ili siku Ile ushiriki mema yote.

Ubarikiwe.

Je umeokoka? Kama bado unasubiri Nini Leo usifanye hivyo. Ikiwa upo tayari kumgeukia Yesu na kumfanya mwokozi wa maisha Yako, akusamehe dhambi zako. Basi ni wewe tu kufungua moyo wako na kuikubali msamaha huo.Ikiwa upo tayari kufanya.hivyo basi fungua hapa Kwa mwongozo huo.

Bwana akubariki..

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

SIKU YA MAONYESHO MAKUU YA BWANA YESU, IPO KARIBU.

NIMEAZIMIA KUWAKUSANYA MATAIFA. NIPATE KUWAMWAGIA GHADHABU YANGU

UUNGU NI NINI? (1Petro 1:3-4)

KIKOMBE CHA GHADHABU YA MUNGU KINAJAA.

Kwanini Mungu aliwaagiza wana wa Israeli wasikisaze chakula?

IEPUKE GHADHABU YA MUNGU.

USIIHARIBU TABIA YAKO KWA MAZUNGUMZO YAKO.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments