Category Archive Uncategorized @sw-tz

Ndugu Yule anayezungumziwa kwenye 2Wakorintho 8:18 ni nani?

SWALI: Kwenye 2Wakorintho 8:18, Mtume Paulo anamtaja ndugu ambaye jina lake hajaliweka wazi. Ni kwanini afanye hivi tofauti na alivyozoea kufanya katika nyaraka zake nyingine, kuwataja aliowatuma?

 2Wakorintho 8:18 Na pamoja naye tukamtuma ndugu yule ambaye sifa zake katika Injili zimeenea makanisani mwote.19  Wala si hivyo tu, bali alichaguliwa na makanisa asafiri pamoja nasi katika jambo la neema hii, tunayoitumikia, ili Bwana atukuzwe, ukadhihirike utayari wetu.


JIBU: Katika waraka huu, tunaona Paulo akiwaandikia kanisa la Korintho, suala la changizo kwa ajili ya watakatifu maskini waliokuwa Yerusalemu. Hivyo akawatuma pia na watatu ili kulifanikisha jambo hilo. Wa kwanza ni Tito, Ukisoma mstari wa 16-17, katika sura hiyo hiyo ya 8, anatajwa, wa pili ndio huyu ambaye sifa zake za injili zilivuma kwenye makanisa, na watatu ni ndugu mwingine ambaye pia hajatajwa jina, isipokuwa Paulo alimwita kama ‘ndugu yetu’ ambaye tunamsoma kwenye mstari wa 22

2Wakorintho 8:22  Nasi pamoja nao tumemtuma ndugu yetu tuliyemwona mara nyingi katika mambo mengi kuwa ana bidii, na sasa ana bidii zaidi sana kwa sababu ya tumaini kuu alilo nalo kwenu.

Watu hawa watatu ndio waliotumwa kwa ajili ya huduma hiyo ya changizo kwa wakorintho. Lakini swali huulizwa huyu ndugu wa pili ni nani hasaa?

Wengine husema ni Luka, wengine Barnaba, wengine Apolo, wengine Marko, Aristako. Kutokana na kwamba wengi wa hawa walisifika kwa usambazi injili, lakini pia walikuwa na Paulo mara nyingi kwenye huduma.

Lakini Hayo ni makisio tu, anaweza akawa miongoni mwa hawa, lakini pia asilimia kubwa anaonekana sio kabisa miongoni mwao, waliowahi kutajwa na Paulo.

Jambo la muhimu  ambalo, linalengwa hapo, kufichwa kwa jina lake. Sio kwamba Mungu anataka tumchunguze ni nani? Hapana Lakini alipenda kutuonyesha kwamba SIFA, hujitambulisha zaidi kuliko jina.

Ukichunguza hapo, utaona Paulo anasema sifa zake zimeenea kwenye “makanisa yote”. Ikiwa na maana kuanzia huko Akaya mpaka Makedonia. Alijulikana kuwa mhubiri mwenye juhudi na mwenye kuthamini injili. Na si hivyo tu, walimchagua mwenyewe kusafiri pamoja na Paulo. Hivyo Paulo kuandika waraka huo, kwa kueleza sifa zake, aliona hilo latosha tu, kumtambulisha bila hata ya jina. Kwasababu hakuna mwingine zaidi yake. Yaani kwa namna nyingine Paulo anasema, “Mpaka hapo mmeshamtambua ni nani”.

Sikuzote wanaotambulishwa kwa majina huwa ni watu wasiojulikana, au wasio na sifa za kutosha kwenye jamii husika.

Ndivyo ilivyokuwa pia kwa Yule mtu wa tatu ambaye Paulo alimwita kama “NDUGU YETU”. Kulikuwa hakuna haja ya kumtambulisha kwa jina kwasababu walikuwa wanamwona wakati wote akiwa na akina Paulo katika ziara zake na huduma. Hivyo kumtafaja tu ndugu yetu ilitosha, alijua kila mmoja alielewa ni nani aliyekuwa anazungumziwa, kwasababu mitume hawakuwa na ndugu mwingine zaidi ya huyo, aliyekuwa karibu nao.

Hata leo, Bwana anapenda sisi tutambuliwe kwa SIFA zetu, zaidi ya MAJINA yetu. Kiasi kwamba kazi itakayoonekana kwa ajili ya Kristo, itutambulishe sisi, sio sisi tuyatambulishe majina yetu katikati ya watu.

Utaona baadhi ya wahubiri wanachokifanya, ni kutumia nguvu kubwa kutangaza majina yao, na sura zao, ili wajulikane, lakini kazi zao hazitambuliki. Hilo sio lengo la mhubiri, au Mtumishi wa Mungu. Bwana wetu Yesu Kristo alipokuwa duniani, haikuwa na muda wa kujitangaza, wakati mwingine hakutaka mambo yake yadhihirishwe kiwepesi, mpaka atakapomaliza kazi yake, Na sisi pia tupende aina hii ya utumishi.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Epafrodito ni nani kwenye biblia?

Epafra ni nani katika biblia? (Wakolosai 1:7)

Je ni sawa kuukubali udhaifu kama mtume Paulo alivyojisifia kwa huo? (2Wakorintho 12:9-10)

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! Uvimbe unatibika?

Jibu ni ndio.

Lakini sio njia zote zinaweza kutibu ugonjwa huo. Ni kweli madaktari hufanya kwa sehemu yao. Lakini Mungu hufanya zaidi, kwake yote hutibika.

Uvimbe wa aina yoyote ile, uwe ule wa kwenye mfuko wa uzazi, au kibofu, au  kwenye koo, au kichwa, au tumboni. Popote pale, maadamu ni uvimbe, haijalishi ukubwa wake, unaponyeka huo.

Na anayeweza kufanya hivyo ni YESU TU.

Tafsiri ya jina lake ni MWOKOZI. Ndiye aliyetumwa na Mungu mahususi kuwaokoa wanadamu na dhambi zao, pamoja na shida zao na magonjwa yao, alizaliwa kwa kusudi hilo tu moja. Hivyo maadamu yeye yupo huna haja ya kuwa na hofu.

Isaya 53:4 Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.  5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona

Huo ugonjwa alishauchukua zamani sana, kabla ya wewe kuzaliwa.  Alimponya Lazaro aliyekufa na ugonjwa, na kuzikwa na kuoza. Atakuponya na wewe, ambaye hata bado hujafa kwa ugonjwa huo. Ni kumwamini tu, basi,

Lakini hatua ya kwanza ni wewe kumpokea maishani mwako. Kukubali neema yake, kwa kutubu dhambi zako, kwa kumaanisha kabisa kuziacha, kisha yeye mwenyewe atakupa ondoleo la dhambi hizo, na utakuwa umeupokea uzima wa milele, Wala hatazikumbuka tena kuanzia siku hii ya leo na kuendelea.

Ikiwa upo tayari kupokea wokovu huu bure basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Ikiwa sasa tayari umeokoka. Basi unahitaji msaada ya kimaombi.

Piga namba uzionazo chini ya chapisho hili nasi tutakuombea (bure) na kwa imani utapokea uponyaji wako.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KANSA/SARATANI INATIBIKA.

SALA YA UPONYAJI/MAOMBI YA UPONYAJI.

UPONYAJI WA YESU.

JE! UKIMWI UNATIBIKA?

Rudi Nyumbani

Print this post

Kuhisi vitu vinatembea mwilini.

Yapo matatizo ya kimwili ambayo kwa tiba hutatulika, Ukiona unahisi vitu vinatembea mwilini kama vile wadudu, na kukusababishia madhara fulani mwilini lada kuchoka, mwili kuuma, ni vema ukaenda kwanza kuangalia afya yako kwa daktari, utashuariwa na kupewa tiba, Ukiona limetatulika basi ilikuwa ni shida ya kimwili.

Lakini ukiona tiba, haitatui haeleti majibu yoyote. Unahitaji msaada wa kiroho. Mara nyingi wanaokumbana na hali hii ya kuhisi vitu vinatembea mwilini, au sindano zipita zinachoma-choma, au kuhisi kitu kinatembea tumboni, au mgongoni, mikononi na miguuni, huwa ni dalili za mapepo kuwapo ndani yao.

Angalia, je, hali hiyo inapokutokea unakuwa katika mazingira gani? Je, kwenye maombi ndio huzidi? Je! Unapojaribu kusikiliza, au kusoma biblia? Ukiona hiyo hali inakujia halafu inaambatana na mambo kama kupoteza kumbukumbu, au unakuwa na hasira, au hofu, au ufanisi wako unapungua. Hizo ni dalili za mapepo. Hivyo hayana budi kuondolewa ndani yako.

Kumbuka mtu anafunguliwa kwanza kuwa kumkumbali Yule ambaye atamwokoa yaani YESU KRISTO. Hivyo jambo la kwanza ni wewe kumpokea moyoni mwako. Kwa msaada huo waweza fungua hapa, upata wokovu >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Lakini kwa msaada wa ki-maombi (bure), wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini mwa makala hii, na Bwana atakufanya huru kwelikweli.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

DALILI TISA (9) ZA PEPO KUWEPO NDANI YA MTU.

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Tafsiri ya Wakolosai 2:18 Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu,

SWALI: Nini maana ya vifungu tunavyovisoma katika Wakolosai 2:18,

 ‘Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili;


JIBU: Tukianzia mistari ya juu anasema..

16  Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;

17  mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo. 18 Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili;

Katika vifungu hivyo, Mtume Paulo anaanza kwa kuwaambia ‘mtu asiwanyang’anye thawabu yenu’. Akiwafananisha na wana-michezo ambao wanashiriki katika mashindano Fulani, ambao hujitahidi kwa kila namna kujizuia, na kujichunga ili wafanye vema katika mashindano hayo wachukue tuzo.

Sasa Paulo, anatoa angalizo, akirejea mfano wa washindani hao, yawezekana mwingine akamfanyia hila mwenzake, ili asiwe na ufanisi, kwenye michezo hiyo akashindwa kushiriki vema na kuchukua tuzo, kwamfano anaweza kumpa kinywaji Fulani ambacho kitadhoofisha uchezaji wake, au atamdanganya afanya zoezi Fulani,  ambalo anajua kabisa halina manufaa kwake, kwamfano labda mchezaji ni mwana-riadha, utaona Yule mwingine anamwambia akanyanyue vyuma vizito atakuwa mwepesi kukimbia. Kumbe kukimbia hakuhusiani na misuli mikubwa bali pumzi.

Vivyo hivyo Paulo aliona kuwa kuna waalimu wa uongo, viongozi wa uongo,watakaozuka, kuwadanganya watu waiache njia sahihi, ya kukubaliwa na Mungu. Na ndio hapo anataja  mambo matatu ambayo watakuwa nayo;

Jambo la kwanza,

Watachukua thawabu yao kwa kunyenyekea kwa mapenzi yao wenyewe tu,

Kunyenyekea sio kubaya, ni tunda la Roho Mtakatifu ndani ya mtu, na wakristo wote, tunasukumwa katika unyenyekevu. Lakini angalia hapo anasema kunyenyekea KWA MAPENZI YAKE MWENYEWE. Maana yake, ni kuwa hanyenyekei kwa mapenzi ya Mungu, bali yake. Na hiyo ni mbaya, kwasababu watu wa kidini leo hii ndio kanuni yao, hubuni njia zao za kumwabudu Mungu, na hiyo huwavutia watu wengi, waone kama ni Mungu kweli anaabudiwa, kwa unyenyekevu na heshima, nao wanaingia kwenye mkondo huo. Wanasahau kuwa ibada lazima ifanyike kwanza katika Roho na Kweli.

Mambo kama kusujudia, kuvaa mavazi Fulani meupe, kutawadha mwili, kuvua viatu katika nyumba za ibada, kuomba kwa sauti ya kuvuta sana, ya upole, huku umeinamisha kichwa chini, unaibusu biblia. Hudhanikuwa kuwa ndio hicho Mungu anakitaka,  Lakini ndani, kinywa chake kina matusi, akitoka hapo anakwenda kuishi maisha kishirikina, na ulevi.  Huo ni udanganyifu mkubwa sana.

Ndicho Paulo alichokiona kwa kanisa la Kolosai, kulitokea watu wanawaambia usile kambale ni chukizo kwa Mungu, shika siku  ya sabato, inatosha.. Yote hayo yakifanyika kimwili. Lakini wasifundishe kwamba unyenyekevu wa ki-Mungu hutoka rohoni, ukisukumwa na neema katika  Roho Mtakatifu, Ambapo mtu kupaswa kukubali wokovu kwanza, na kutii kwa kumfuata Kristo anayeweza kumfanya mtu kiumbe kipya, na sio jambo la kufanya kimwili tu, akidhani atampendeza Mungu.

Jambo la pili

 wanaweza kuwanyang’anya thawabu yao kwa mafundisho ya kuabudu malaika.

Tangu zamani, kulikuwa na watu waliowaweka malaika katika nafasi ya Mungu. Na kuvuka ile mipaka ya kutuhudumia tu sisi  (Waebrania 1:14). Hivyo ikiwa mtu alikuwa na karama Fulani ya maono, ambapo mengine huletwa kwa mikono ya malaika, tunaliona hilo mara nyingi tangu Musa, na wana wa Israeli jangwani, pamoja na mitume mpaka Yohana kule Patmo. Mungu aliwatumia malaika kwa sehemu kubwa kutufikishia sisi jumbe zake, kwasababu waliwekwa kutuhudumia sisi.

Lakini dini na imani zikazuka kuanzia hapo, kwa baadhi ya watu wakaanza kuwafanyia ibada, jambo ambalo ni chukizo kwa Bwana. Hata leo utaona zipo sala za malaika na watakatifu kuwataka wawaombee. Au wawasaidie vitani. Ikiwa wewe ni mtoto wa Mungu umeokoka, kuwa makini na ibada hizo, taabu yako kwa Mungu yaweza kuwa bure, kwasababu unamudhi Mungu. Ibada za namna hiyo hazina tofauti na ibada za majini. Usiabudu mwanadamu, wala kiumbe chochote kilicho mbinguni wala duniani.

Jambo la tatu

Na mwisho anasema wakijivuna bure kwa akili zao za mwili.

Kujivuna, maana yake kusifia vitu vya mwilini mfano vipaji vyao, wengine ujuzi wa kuongea vizuri, na kupangalia maneno, werevu, elimu za falsafa, mambo ambayo Paulo aliyaona, yakiwavuta wengi, na kuacha njia kamilifu ya Kristo iliyo katika neema, upendo,  Imani na nguvu za Mungu. (2Wakorintho 11:18-20).

Injili inabadilishwa inakuwa vichekesho, na kanuni za ki-ujasiriamali,

Hata leo mimi na wewe ni kuwa makini, bidii yako katika Kristo isichukuliwe na udini, bali Neno, isichukuliwe na maono na karama, na ibada za malaika bali Mungu, isichukuliwe na falsafa za kibinadamu, na mwonekano, bali, Roho Mtakatifu na kweli, katika neema.

mtu asichukue taji lako

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 2)

Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?

Rudi Nyumbani

Print this post

UFUATILIAJI NI SEHEMU YA HUDUMA MUHIMU KWENYE UINJILISTI

Matendo  11:25

Kisha akatoka akaenda Tarso kumtafuta Sauli;

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, napenda leo tujifunza jambo moja ambalo huwenda linasahaulika miongoni mwetu kama watendakazi shambani mwa Bwana.

Hatuna budi kufahamu ,ufuatiliaji huenda sambamba na uinjilisti. Twaweza hubiria watu wakaokoka, wakamjua Kristo, wakati mwingine wakaweza hata kujisimamia wenyewe, lakini tusipojijengea tabia ya kuwafuatilia na kukaa nao, kuwaimarisha, basi kazi yetu yaweza kuwa bure, au isiwe na matunda mazuri kama ipasavyo.

tunajifunza kwa mtu mmoja aliyeitwa Barnaba, aliyejulikana pia kama mwana wa faraja. Huyu aliithamini huduma hii. Baada ya kusikia kuwa Paulo, amegeuka na kuwa mkristo, lakini akaenda mahali panaitwa Tarso, mbali kidogo na kanisa, Barnaba aliona si vema amwache huko. Ikabidi afunge safari yeye mwenyewe kutoka Antiokia aende kumtafuta.

Hatujui safari yake ilichukua siku ngapi, wiki ngapi, miezi mingapi. Lakini hatimaye akampata ..Alipomwona huwenda hakuridhishwa na mazingira ya kihuduma aliyokuwa nayo, hakuridhishwa na hali ya kiroho aliyokuwa nayo. Kwasababu hata mtume Paulo kuondoka Yerusalemu ilikuwa si kupenda kwake ni kutokana pia na kukataliwa na kanisa, na hatari ya kuuliwa na wayahudi.

Lakini Barnaba alipomuona. Akamchukua amlete mahali bora zaidi, ambapo kanisa lipo hai. Akafika akaendelea na huduma, akaanza kuwa moto tena na kutokea hapo ndipo Mungu alipomfanya mhubiri wa kimataifa.

Leo hii tunasoma ushujaa wa Paulo, lakini kusimama kwake kulichangiwa na nguvu ya kufuatiliwa kwa waliomtangulia kiroho.

Je na sisi tumejiwekea desturi hii? kuwafuatilia mara kwa mara tunaowashuhudia injili?

Kamwe usimdharau mwongofu mpya, hata kama atakuwa anasua-sua, au mdhaifu sasa. Fahamu kuwa huyo ndio Paulo wa baadaye. Usihubiri tu ukaacha, ukadhani atajikuza mwenyewe.  Shughulika naye, omba naye, mfuate alipo, mfundishe, ikiwezekana mwamishe eneo alilopo ikiwa linamfanya asisimame kiroho. Na kazi yako itazaa matunda, usichoke.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

MAMBO NANE (8), AMBAYO WEWE KAMA KIONGOZI UTAIGWA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Ijapokuwa amekufa, angali akinena(Waebrania 11:4)

SWALI: Maandiko yanaposema Habili ijapokuwa amekufa angali akinena, je! Ananenaje, wakati yeye ni marehemu. Je! Hiyo inamaana wazee wetu wa zamani wanaweza kunena na sisi?

Waebrani 11:4  Kwa imani Habili alimtolea Mungu dhabihu iliyo bora kuliko Kaini; kwa hiyo alishuhudiwa kuwa ana haki; Mungu akazishuhudia sadaka zake, na kwa hiyo, ijapokuwa amekufa, angali akinena


JIBU: Kibiblia ni kweli kabisa watakatifu waliokufa kale hunena nasi. Lakini kunena kwao ni tofauti na huku kunakodhaniwa, kwamba mzimu unakutokea kwenye ndoto, au unasikia sauti ya petro makaburini ikizungumza na wewe,  Hapana, ukiona hivyo ujue huzungumzi na huyo mtu, bali ni pepo.

Sasa watakatifu waliokufa wanazungumzaje na sisi?

Ni kwa ushuhuda waliouacha. Maisha yao na maagizo yao, ndio huzungumza nasi, sikuzote, kana kwamba tupo nao sasa, kwa mafundisho yao yaliyopo  mpaka sasa kana kwamba tunawaona wenyewe kumbe wamekufa.

Ndio maana ile habari ya Yule tajiri wa Lazaro, tunaambiwa alipofika kule kuzimu akaomba mtu atolewe kwa wafu awahubirie injili, akakataliwa, kuonyesha kuwa hakuna mtu aliyekufa mwenye uwezo wa  kuja tena kuzungumza na sisi, nafasi hiyo haipo kwao. Lakini waliambiwa WANAO MUSA NA MANABII, WAWASIKILIZE.

Luka 16:29  Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.

Maana yake ni kuwa sio kwamba Musa kweli alikuwepo duniani, au manabii wa kale kama Isaya walikuwa duniani kwa wakati huo, anaambiwa hayo maneno. Lakini shuhuda zao na mahubiri yao, huwawakilisha wao. Tunaweza kusema “ijapokuwa wamekufa wangali wakinena”

Ndivyo ilivyo kwa Habili, ijapokuwa aliuliwa na ndugu yake, lakini IMANI yake inasema nasi mpaka leo. Mitume wa Kristo ijapokuwa hawapo duniani lakini sauti zao tunazisikia hadi sasa.

Lakini pia kuna mahali pengine biblia inasema damu ya Yesu hunena mema kuliko ya Habili (Waebrania 12:24). Kufahamu kwa kina damu ya mtakatifu  hunenaje? Pitia somo hili. >>> DAMU YA ZAKARI BIN BARAKIA.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.

ALIPOKUWA ANGALI MBALI, BABA YAKE ALIMWONA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Yakobo alimaanisha nini kusema ‘ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu’ Mwanzo 28:21

Mwanzo 28:21

[21]nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu, ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu.


JIBU:

Sura hiyo inaeleza ugumu wa safari ya Yakobo alipokuwa anamkimbia ndugu Yake Esau kuelekea nchi ya ugenini ya baba zake. 

Hivyo akiwa huko jangwani peke yake, haoni mbele wala nyuma, haoni msaada kwa mtu wala kitu, ndipo akamwekea Mungu nadhiri, na kumwambia maneno hayo. 

‘nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu, ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu’. 

Lakini swali linakuja je hakumwamini Mungu, au kumfanya Mungu wake mpaka hapo ambapo angetimiziwa nadhiri zake? Kwamaana baada ya miaka 20, ndio tunaona yakitimia hayo yote? je hiyo miaka yote ya hapo katikati YEHOVA hakuwa Mungu wake, mpaka wakati ambapo angetimiziwa nadhiri yake?

Jibu: mstari huo haumaanishi kwamba Yakobo alikuwa anamweka kwanza Mungu kwenye majaribio halafu akishamfanikisha ndipo amfanye rasmi kuwa Mungu wake.

Hapana, ingekuwa hivyo tusingeona  katika kipindi hicho chote Yakobo akimtumainia Mungu wa baba zake, angeendelea tu na mambo yake mpaka huo wakati ufike.Lakini tunaona Yakobo hakucha kumwamini Mungu mahali popote.

Katika kauli hiyo hapo Yakobo alikuwa anaongezea tu, kujitoa kwakwe zaidi kwa Mungu, endapo  atarudishwa salama, na ndio maana maana ukiendelea vifungu vinavyofuata..

anasema atamtolea Mungu wake Fungu la kumi kwa kila atakachokipata..

jambo ambalo hapo mwanzo asingeweza kwasababu alikuwa hana chochote.

Mwanzo 28:21-22

[21]nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu, ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu.

[22]Na jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu; na katika kila utakalonipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi. 

Kwa namna nyingine..anamwambia Mungu nitafanya vizuri zaidi kwako, endapo nitarudi salama, kutoka katika nchi ya ugenini.

Au ni sawa na leo mtu aseme Bwana nitakutumikia endapo utaniondolea huu ugonjwa wangu wa kupooza. 

Hiyo haimaanishi kuwa amemwekea Mungu masharti, kwamba sasahivi hataki mtumikia mpaka aponywe hapana, lakini anaeleza kikwazo chake. Na kwamba kikiondolewa ataweza timiza vizuri matakwa yake ya kiutumishi. Ndicho alichokimaanisha Yakobo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

USIMPE NGUVU SHETANI.

Kutoka 21:10 ina maana gani?.

Print this post

Epafrodito ni nani kwenye biblia?

Epafrodito alikuwa ni mmoja wa watendakazi wa makanisa yaliyokuwa Filipi. Anajulikana kama mhudumu wa mahitaji ya mtume Paulo. Tunaona upendo wa Kanisa la Filipi jinsi lilivyomkumbuka Mtume Paulo alipokuwa kifungoni Rumi. Hivyo likaazimu kumtumia mahitaji yake ya kifedha. Ndipo likamchagua huyu Epafrodito. Kusafiri umbali wote huo mrefu na kiasi hicho kingi cha fedha mpaka Rumi.

Wafilipi 4:18  Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vitu vile vilivyotoka kwenu, harufu ya manukato, sadaka yenye kibali, impendezayo Mungu.

Na jambo hili lilikuwa ni desturi yao, kumtimizia Paulo mahitaji yake mara kwa mara (Wafilipi 4:16)

Lakini tunaona mbeleni katika waraka wa Paulo, anaeleza hali ya ndugu huyu ambaye Paulo  alimwita pia mtume,jinsi ilivyobadilika kwa kuugua sana karibu na kufa, akiwa katika kazi hiyo hiyo ya kumuhudumia Paulo. Lakini  Ijapokuwa alikuwa katika hali mbaya bado hakuacha kumuhudumia Paulo,

Tunasoma katika hali yake ngumu ya kuumwa, Mungu alimhurumia akamponya. Hatujui aliugua ugonjwa gani, lakini ni ugonjwa uliomdhoofisha kwelikweli, kiasi cha kudhaniwa ‘huyu ni wa kufa tu’, na bila shaka ulikaa ndani yake muda mrefu.

Lakini alipomaliza huduma yake, Ndio tunaona Paulo anawaandikia wafilipi waraka huo, na kuurejesha kwao kwa mkono wa huyo huyo Epafrodito,na ndani yake akielezea pia, shida zilizomkuta.

Wafilipi 2:25  Lakini naliona imenilazimu kumtuma kwenu Epafrodito, ndugu yangu, mtenda kazi pamoja nami, askari pamoja nami; tena ni mtume wenu na mhudumu wa mahitaji yangu.

26  Kwa kuwa alikuwa na shauku kwenu ninyi nyote, akahuzunika sana, kwa sababu mlisikia ya kwamba alikuwa hawezi.

27  Kwa maana alikuwa hawezi kweli kweli, karibu na kufa; lakini Mungu alimhurumia; wala si yeye peke yake, ila na mimi pia; nisiwe na huzuni juu ya huzuni.

28  Kwa hiyo nimefanya bidii nyingi zaidi kumtuma, ili mtakapomwona tena mpate kufurahi, nami nipunguziwe huzuni yangu.

29  Mpokeeni, basi, katika Bwana, kwa furaha yote, mkawahesabu watu kama huyu kuwa watu wa kuheshimiwa.

30  Maana kwa ajili ya kazi ya Kristo alikaribia kufa akaponza roho yake; ili kusudi ayatimize yaliyopungua katika huduma yenu kwangu.

Ni nini tunajifunza kwa mtumishi wa Mungu huyu?

Upendo wa kujali hali za wengine. 

Biblia inasema upendo hautafuti mambo yake wenyewe (1Wakorintho 13). Alikuwa tayari kufa, ili askari mwenzake asikose mahitaji yake. Si ajabu Paulo alimwita mtume. Mungu anathamini sana, utume wa namna hii.

Lakini Tunajifunza huruma ya Mungu ijapokuwa alikuwa karibu na kufa, bado Mungu aliweza kumponya akawa mzima kabisa. Hata mimi na wewe, je tunaweza kufikia hatua mbaya ambayo hata madaktari wanasema haiwezekani kupona? Kama ndio mkumbuke Epafrodito, una hali ngumu unayoweza kusema hapa sivuki, mwisho umefika? Mkumbuke Epafrodito. Yote yanawezekana kwa Mungu.

Ikiwa ni mtumishi wa Mungu, usiohofu uteterekapo kiafya au kihali, Mungu anakuona, atakutia nguvu, usiache kumwamini.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

USIFE NA DHAMBI ZAKO!

KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.

Rudi Nyumbani

Print this post

Epafra ni nani katika biblia? (Wakolosai 1:7)

Epafra ndiye alikuwa mwangalizi wa kanisa la Kolosai, Paulo alimtambua  kama mhuhudumu mwaminifu wa Kristo. Kiasili naye pia alikuwa mwenyeji wa mji huo huo wa kolosai kufuatana na kauli Paulo aliyoisema katika Wakolosai 4:12, “aliye mtu wa kwenu”

Waraka huu unaonyesha Epafra kama  mhudumu ‘mwaminifu’ wa Kristo. Ikiwa na maana alijitoa kikamilifu kwenye kazi ya Mungu bila kupunguza chochote, mtumwa aliyegawa posho kwa wakati.

Aliyeitwa pia mjoli wa Paulo. Ikimaanisha mtendakazi pamoja na Paulo katika shamba la Bwana.

Lakini pia Paulo alikuwa ni kiongozi na mshauri wake. Tunaona aliwasilisha ripoti zake kwake, za maendeleo ya kanisa. Jinsi upendo wao ulivyokuwa mwingi.

Wakolosai 1:7  kama mlivyofundishwa na Epafra, mjoli wetu mpenzi, aliye mhudumu mwaminifu wa Kristo kwa ajili yenu

8  naye alitueleza upendo wenu katika Roho.

Epafra alikuwa na juhudi sio tu kwa kanisa la Kolosai, bali pia na makanisani mengine ambayo ni  Laodikia na Hierapoli (Wakolosai 4:13).

Tunasoma pia Epafra alikuwa mtu wa bidii  ki-maombi kwa ajili ya kanisa la Kolosai

Wakolosai 4:12  Epafra, aliye mtu wa kwenu, mtumwa wa Yesu Kristo, awasalimu, akifanya bidii siku zote kwa ajili yenu katika maombi yake, ili kwamba msimame wakamilifu na kuthibitika sana katika mapenzi yote ya Mungu.

13  Maana namshuhudia kwamba ana juhudi nyingi kwa ajili yenu, na kwa ajili ya hao walioko Laodikia, na kwa ajili ya hao walioko Hierapoli.

Lakini mbeleni katika waraka wa Paulo kwa Filemoni tunaona alikuja pia kufungwa, pamoja na Paulo kule Rumi.

Filemoni 1:23  Epafra, aliyefungwa pamoja nami katika Kristo Yesu, akusalimu;

Ni nini tunajifunza katika maisha ya Epafra?

Kujitoa kwake kimaombi, kwa kanisa ili lisimame kamilifu na kuthibitika katika mapenzi ya Mungu. Epafra alikuwa na juhudi isiyo ya kawaida katika kuliombea kanisa. Alijua kanisa lisipoombewa haliwezi kusimama vema. Hivyo aliwekeza sana katika maombi na kuwa pia na bidii katika uaminifu kwenye  huduma.

Bidii yake hakika ilizaa matunda, na ndio maana Bwana akaruhusu habari zake ziandikwe, na kusomwa hadi leo.

Je! Na sisi tunathamini maombi katika kuliombea kanisa? Unapoona watu wamepoa kiroho, watu wanaishi kimwili kanisani, wanafanya mambo ya aibu, sio kumnyooshea kidole mchungaji, au shemasi au mzee wa kanisa na kumlaumu. Hapo huwezi tatua tatizo. Shida ipo kwenye kupungukiwa kwa maombi. Chukua muda mwingi kuliombea kanisa kuliko kuzungumza. Bwana atayatenda yote uliyoyatamani.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya kuabudu malaika? (Wakolosai 2:18)

Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,

UAMINIFU NI KIGEZO KIKUBWA CHA KUTUMIWA NA MUNGU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; (Luka 17:10) 

SWALI: Naomba kufahamu maudhui iliyo nyuma ya  Luka 17:10 inayosema..

[10]Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya.


JIBU: Kufahamu kwanini Yesu  aliwaambia wanafunzi wake maneno hayo. Ukianzia juu utaona ni kufuatana na swali walilomuuliza kuhusiana na IMANI. Walimfuata na kumwomba awaongezee Imani.

Lakini Yesu aliwajibu na kuwaambia kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali mngeuambia mkuyu huu ng’oka ukapandwe baharini nao ungewatii.

Luka 17:6

[6]Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu huu, Ng’oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii.

Akimaanisha kuwa  sio suala la kuongezewa Imani, ili mweze kufanya makubwa, bali kile kidogo sana kinaweza tenda yote. Na kidogo hicho mitume walikuwa nacho ndani yao, ambacho hata mimi na wewe tunacho. Isipokuwa hawakujua namna ya kukitoa.

Ndipo Yesu akaendelea kuwaambia kwa mifano sasa, ili jambo hilo litokee, kanuni yake ni kuwa wanapaswa wawe kama watumwa wasiokuwa na faida kwa Bwana wao. Sasa kwa namna gani? fuatilia mfano wenyewe…

Luka 17:7-10

[7]Lakini, ni nani kwenu mwenye mtumwa alimaye au achungaye ng’ombe, atakayemwambia mara arudipo kutoka shambani, Njoo upesi, keti, ule chakula?

[8]Je! Hatamwambia, Nifanyie tayari chakula, nile; jifunge unitumikie, hata niishe kula na kunywa, ndipo nawe utakapokula na kunywa?

[9]Je! Atampa asante yule mtumwa, kwa sababu ameyafanya aliyoagizwa?

[10]Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya.

Mfano huo unajieleza, zamani mtumwa aliponunuliwa hakuwa anafanya kazi kama mwajiriwa, bali kama mnyama tu mfano wa punda ambapo kazi yake ilikuwa ni moja tu kumuhudumia Bwana wake, na sio kujitafutia maisha.

Sasa hapo Yesu anatumia mfano wa huyo Bwana mwenye mtumwa wake ambaye amemweka kuwa mkulima wa shamba lake, ambaye asubuhi huondoka jioni hurudi kwa Bwana wake.

Anasema, je atakaporudi atamwambia kaa hapo upumzike? wakati mimi bado sijala? Ni wazi kuwa ataongezewa majukumu, mpaka ahakikishe Bwana wake ameshiba, hana mahitaji tena ndipo sasa na yeye apewe nafasi ya kupumzika na kula.

Hivyo Yesu alitumia mfano huo, kuwaambia wanafunzi wake, jinsi na wenyewe wanavyopaswa kuwa kwa Mungu.

“[10]Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya.”

Akiwa na maana, mkihitaji hilo jambo la IMANI mjaliwe, yawapaswa muwe kama watumwa wasiokuwa na faida. Mtumikieni kwanza Bwana wenu sana, kama watu wasiotazamia malipo yoyote.

Ukihubiri sana miaka ishirini, unatanga na jua huoni faida yoyote iliyoongezeka kwenye maisha yako, huoni maendeleo yoyote. Usimuulize Bwana mbona hujanipa chochote mpaka leo. kuwa kama mtumwa asiye na faida.

Huu ndio utumishi Bwana anaoutaka kwetu, leo hii wahubiri wengi, watumishi wengi, wachungaji wengi wamepoa, wamerudi nyuma kwasababu walitazamia malipo kutoka kwa Bwana katika kwa kile walichokuwa wanakifanya, na waliopoona hawapati, kinyume chake maisha yao ndio yanakuwa magumu, wakaacha utumishi wakaenda kutafuta mambo yao.

Ndugu ni lazima tuelewe kanuni za Mungu wetu. Ikiwa unaenda kuifanya kazi ya Bwana ili ukusanye sadaka, upate unafuu kimaisha..Ni heri ukaacha ukatafute biashara nzuri uwekeze nguvu zako huko. Mungu anaweza asikupe chochote kwa miaka mingi, unataabika tu,  je utaendelea kumtumikia?

tukubali kuwa watumwa wasio na faida. Akitupa sawa, asipotupa sawa. Lakini tujue kuwa sikuzote anatuwazia yaliyo mema.

Ujumbe wa Bwana hapo ni kwamba tukitaka imani itoke tuwe watumwa wa namna hii.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.

Tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu.

Nawiwa na Wayunani na wasio Wayunani.

Rudi Nyumbani

Print this post