Title May 2019

BWANA YESU ALIKUWA ANAONYESHA KUWA MUNGU NI MUNGU MWENYE AKILI TIMAMU.

Bwana Yesu mara nyingi alikuwa akiwaaminisha watu kwa mifano, yaani ni jinsi gani Mungu alivyo na akili timamu na alivyo na kumbukumbu nzuri sana katika mambo yake yote, alijaribu kila namna kuwatolea watu ile dhana ya kuwa Mungu ni kiumbe cha ajabu kilicho mbinguni kinahitaji kuabudiwa tu wakati wote, na hakina muda wa kutazama mambo mengine manyonge yawahusuyo wanadamu, nikisema mambo manyonge ninamaanisha mambo yanayozunguka maisha ya mwanadamu ya kila siku, kama vile majukumu, afya, chakula, malazi, matamanio ya maisha bora, raha, sherehe n.k..

Yesu alituhakikishia kuwa Mungu anatuzingatia sana, kwa kutumia mifano mirahisi kabisa iliyo hai ili kutuonyesha sisi ni jinsi gani Mungu alivyo na kumbukumbu ya haraka sana juu ya watu wake na viumbe vyake vyote..Embu chukua muda tafakari huu mfano kama ulivyo, najua unaweza kuwa na tafsiri nyingi unazozifahamu lakini naomba kwa sasa usiongeze chochote utafakari tu kama ulivyo, naamini utajifunza kitu kikubwa sana ndani yake…

Mathayo 6:26 “Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. NINYI JE! SI BORA KUPITA HAO?”.

Nataka nikuambie Mungu hategemei msaada wako wewe ili akutimize mahitaji yako ya riziki, yeye anaweza kufanya hayo yote bila msaada wako na ukaishi vizuri tu,,..Huoni kama hilo linaweza kuwa ni faraja kwako katika kile UNACHOKIFANYA sasahivi, kiwe ni kinakidhi au hakikidhi?, pengine umekata tamaa ya maisha kwa namna moja au nyingine na kuona kama vile Mungu haoni unayopitia, lakini nataka nikumbie kama ndege hawamwongezei chochote na analo jukumu la kuwalisha, wewe hupaswi kuwa na hofu hata kidogo..Kwasababu wewe ni mara nyingi sana zaidi ya wao.

Mfano mwingine ni huu..

Mathayo 6:30 “Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?”.

Nilipokuwa ninautafakari sana huu mstari na kujiuliza ni wapi maua yanamzidi Sulemani kwa kuvikwa vizuri, nikagundua japo kuwa hayajisumbukii kwa chochote yapo pale pale, lakini kumbe rangi za maua huwa hazifubai, lakini mavazi ya Sulemani yalikuwa yanachakaa na kila siku anahitaji yabadilishwe apewe mapya.

Japo Sulemani alikuwa anaoga kila siku lakini aliishia kutoa jasho lakini maua hayana historia ya kuoga lakini yanatoa harufu nzuri miilini mwao, ambazo ndio hizo wanadamu hutumia kujinakshi miili yao na majumba yao na kutengenezea marhamu mbali mbali…Kwa Hapo Sulemani ameachwa mbali sana na maua ya kondeni.

Lakini nataka nikuambie, hata wewe utajiri wako, au mali zako, au UMASKINI wako hauwezi kumsaidia Mungu, kukupendezesha au kukufanya mpya zaidi na kuvutia.. Fahamu tu ukipenda kudumu katika kuutafuta ufalme wake basi, lile Neno “Je! hatazidi sana kuwavika ninyi enyi wa imani haba” litakuwa ni la kwako, iwe ni katika uchache au katika wingi..

Mfano mwingine tena ni huu…

Mathayo 7:11 “Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamwombao?”.

Watoto wetu wakituomba, tuchukulie mfano baiskeli tutafanya juu chini kwenda kuwanunulia…hata kama hakitakuja kwa wakati husika lakini kwa jinsi wanavyoendelea kusumbua tutafanya juu chini tuwanunulie tu hata kwa kukopa au kujichanga…

Sasa kama wewe unaelewa hali ya mwanao, kwanini yeye Mungu wetu wa mbinguni asielewe yako?, mpaka unapaniki na kuogopa na kukosa raha ya maisha kama vile yeye sikio lake ni zito, yupo mbali hakuoni wala hakusikii.. Nataka nikuambie huna haja ya kufunga na kuomba juu ya hilo, Mungu yupo “very sensitive, more than any living creature on Earth or Heaven”..Anao upeo mpana wa kufikiri na kuhisi mambo kuliko wewe unavyodhani, anaweza kuhisi tatizo lako ni lipi kabla hata halijaingia akilini mwako. Biblia inalithibitisha hilo.

Mathayo 6: 7 “Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi.

8 Basi msifanane na hao; MAANA BABA YENU ANAJUA MNAYOHITAJI KABLA NINYI HAMJAMWOMBA”.

Unaona?, Anajua hata unalokwenda kumwomba wiki ijayo,,, ashindweje kujua taabu au shida unayopitia sasa hivi, anajua unaumwa na unateseka katika magonjwa na unahitaji kupona, analijua hilo, anafahamu una haja na kuwa na maisha mazuri anajua, anajua unahitaji kuolewa na umri umeshakwenda, anajua unahitaji pesa uvae nguo nzuri upendeze, anajua unahitaji uishi katika nyumba yako mwenyewe uwe na uhuru wako binafsi, anajua kwasasa ungependa uwe na usafiri wako,,..anafahamu hayo yote…Lakini unajiuliza inakuwaje sasa?

Sasa sikiliza hekima zake zinavyomalizia na kusema..

Mathayo 6:31 “Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33 BALI UTAFUTENI KWANZA UFALME WAKE, NA HAKI YAKE; NA HAYO YOTE MTAZIDISHIWA.

34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”.

Anasema Utafute kwanza ufalme wake…rafiki, tamani kumjua kwanza Mungu maishani mwako, tamani kufahamu hukumu zake na mapenzi yake kwako,..Weka mambo yako ya wokovu wako sawa sasa, uwe unahukika kwamba hata leo ukifa Mbingu ni yako, uwe na uhakika kwanza hata unyakuo ukipita leo usiku wewe utakuwa wa kwanza kuisikia sauti ya Bwana Yesu ikikuita mawinguni…Na kisha hayo mengine mwachie yeye atamalizana nayo.. NA HAYO YOTE MTAZIDISHIWA.

Fahamu kuwa Mungu anazo akili timamu zaidi ya unavyofikiri.

Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

JE! UMEFUNDISHWA?

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

KWA KUVUMILIA AKAIPATA ILE AHADI.

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

WALIO NA HEKIMA NDIO WATAKAOELEWA


Rudi Nyumbani

Print this post

NEHUSHTANI (NYOKA WA SHABA).

Musa alipewa maagizo na Mungu atengeneze nyoka wa shaba, amning’inize ili wale wote waliomuasi Bwana watakapomtazama nyoka Yule wapone saa ile ile.

Hesabu 21: 8 ‘’Bwana akamwambia Musa, Jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti, na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo ataishi.

9 Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti, hata ikiwa nyoka amemwuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya shaba, akaishi’’.

Lakini Mungu hakuwahi kuwaagiza Wana wa Israeli kuwa wakati wowote watakapokutana na madhara au matatizo basi wamsimamishe nyoka wa shaba wamtazame ili wapone, hakuwahi kufanya hivyo, lakini wana wa Israeli walitazama wakagandua SIRI ndani yake, wakasema ni lazima kutakuwa na uponyaji Fulani kwenye nyoka wa shaba kama sivyo Mungu asingemwagiza Musa kuiunda, hivyo ngoja tujijengee utaratibu wetu, wa kuifanyia ibada, na kumwomba Mungu kupitia ile naye Mungu atatusikia dua zetu..

Hivyo hilo jambo lilikuja kuendelea hivyo kwa mamia ya miaka mbeleni, mpaka likajengewa madhabahu kubwa na kuwa jambo maarufu sana Israeli, watu wakawa wanakwenda kuiinamia ile sanamu ya nyoka na kumwomba Mungu wa Israeli kupitia ile awaponye matatizo yao, wakaifukizia uvumba..

Hawakujua hilo lilikuwa ni chukizo kubwa sana kwa Mungu ndilo lililowapelekea hata kukumbana na matatizo yote yale ikiwemo kuchukuliwa utumwani tena.. Ndipo sasa baada ya miaka mingi sana kupita akatokea mfalme mmoja anayeitwa Hezekia yeye ndiye aliyefanikiwa kuliona hilo chukizo mara moja, Tusome:

2 WAFALME: 18:1 ‘’Ikawa katika mwaka wa tatu wa Hoshea, mwana wa Ela, mfalme wa Israeli, Hezekia, mwana wa Ahazi, mfalme wa Yuda, alianza kutawala.

2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na kenda katika Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Abiya, binti Zekaria.

3 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, mfano wa yote aliyoyafanya Daudi, baba yake.

4 Alipaondoa mahali pa juu, akazibomoa nguzo, akaikata hiyo Ashera; akaivunja vipande vipande ILE NYOKA YA SHABA ALIYOIFANYA MUSA; maana hata siku zile wana wa Israeli walikuwa wakiifukizia uvumba; naye akaiita jina lake NEHUSHTANI

5 Alimtumaini Bwana, Mungu wa Israeli; hata baada yake hapakuwa na mfano wake katika wafalme wote wa Yuda, wala katika hao waliomtangulia’’.

Embu jaribu kutafakari kwa utulivu uone kitu hapo! AGIZO lilikuwa ni la Mungu mwenyewe lakini sasa linageuka kuwa kitanzi na kikwazo kikubwa sana kwa watu…Tunaweza kuwalaumu wale tukasema walipungukiwa na akili lakini nataka nikuambie sisi wa kizazi hiki ndio tuliopungukiwa akili zaidi ya wale..Tutaona ni kwa namna gani tunafanya makubwa zaidi ya wao.

Mungu alimwagiza Musa achonge nyoka wa shaba kama ISHARA tu! ya kitu Fulani tu rohoni, nacho ndicho tunakuja kukiona sisi watu wa agano jipya, kuwa tendo lile Mungu aliliruhusu lifanyike vile kumfunua Bwana wetu Yesu Kristo atakapotundikwa msalabani kwamba kila mtu atakayemwamini aokolewe, hilo tunalithibitisha kwa maneno yake mwenyewe..

Yohana 3:14 ‘’Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyohivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa;

15 ili kila mtu aaminiye awe na uzima wa milele katika yeye’’.

… lakini hakukuwa na kitu chochote cha maana ndani ya ile SHABA, uponyaji halisi haukuwa ndani ya shaba ile bali ulitoka kwa Mungu mwenyewe..matokeo yake watu wakaacha kumtazama Mungu ambaye ni mponyaji wao wakaigeukia shaba isiyoweza kusema, wala kunena, wala kuzungumza..

Leo hii tunajua ni kweli Mungu alimwagiza Elisha achukue CHUMVI na kuitia katika chemchemi ya maji iliyokuwa inazaa mapooza..Na baadaye maji yale yakawa matamu,.Lakini kumbuka sio chumvi iliyotibu maji bali ni Mungu ndiye aliyefanya vile, lakini ni kwanini leo hii tunaihusisha chumvi na mambo ya ibada ikiwa hatujaongozwa kuitumia?.Nasi tunasema vile vile kama wana wa Israeli, Mungu kaweka uponyaji wa kiungu ndani ya chumvi,..tunasema kuna nguvu fulani ndani ya chumvi kama sivyo kwanini Mungu alimwagiza Elisha aiweke katika maji?…Tunamtia Mungu wivu pasipo sisi kujijua..

Halikadhalika tunayapa MAJI heshima, na kusema maji yana nguvu ya kusafisha mtu ndani yake, na kumtakasa, Tunamweka nyuma Mungu tunayapa maji heshima, ndugu Huko ni sawa kuiabudu sanamu ya Shaba.

Vivyo hivyo na vitu vingine vyote, tunasema UDONGO unabeba uhai, kwahiyo tukiumwaga kwenye biashara zetu, utazifufua, huku tukishikilia kile Bwana Yesu alichokifanya alipotengeneza TOPE ardhini na kumpaka Yule kipofu machoni, na macho yake kufumbuka, tunasema kama udongo usingekuwa na uponyaji Fulani Yesu asingeagizwa kutengeneza tope na kumpa kipofu..na kibaya zaidi mpaka tumeshavipa majina kama VITENDEA KAZI VYA KIROHO.

Tunahusisha MISALABA katika Ibada zetu. Kama unapenda msalaba wako kwanini usiunig’inize nyumbani kwako kama kumbukumbu lako la Bwana kukufia msalabani, lakini ni kwanini unakwenda kuuinamia, kuomba kupitia huo, unadhani unampa Mungu heshima hujui kuwa ni ASHERA hilo umeiweka moyoni mwako.

Na mambo mengine mengi, tunayafanya hatujui kuwa ndivyo tunavyomtia Mungu wivu. Fumbua macho yako, utoke kwenye uchanga wa kiroho, ikiwa Mungu amekuongoza kutumia mojawapo ya vitu hivyo kama ishara ya kitu Mungu anachokifanya rohoni ni sawa, kama amekuongoza kutumia maji tumia, amekuongoza kutumia mafuta tumia, na uthibitisho wa kuwa umeongozwa na Mungu kufanya hivyo, ni kwamba hakitakuwa unakirudia rudia,….Elisha halikuwa hatumii chumvi kila tatizo linalokuja mbele yake…Wala sio kila mgonjwa aliyekuja mbele yake alikuwa anamwambia akaoge mto Yordani mara saba. Alikuwa anafanya vile pale alipokuwa anaongozwa tu! Na sisi tunapaswa tuwe hivyo hivyo.

lakini kama tunageuza Imani yetu kutoka katika nguvu ya uweza wa DAMU YA YESU inayoweza kufuta na kuondoa kila kitu na kuvipa vitu hivyo visivyo na uhai heshima Fulani ya kiroho kwamba vina nguvu Fulani au uwezo Fulani wa wa kusababisha mambo, basi tujue moja kwa moja tunamfanyia ibada shetani. Na Mungu anachukizwa nazo kupindukia kwa namna ile ile anavyochukizwa na waabudu baali na Jua.

Na madhara yake ni kwamba, Mungu atatupiga kwa kukosa kwetu maarifa, wakati mwingine badala ya tatizo kuisha ndivyo litakavyoongezeka, kwasababu biblia inasema ni heri ungekutana na ghadhabu ya Mungu kuliko WIVU wake, na ibada zote za sanamu zinaleta wivu mbele za Mungu.

Mithali 27:4 ‘Ghadhabu ni kali, na hasira ni gharika; Lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya WIVU’.

Wimbo uliobora 8: 6“………….wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu.”

Huu ni wakati wa kutubu (yaani kugeuka), na kumwabudu yeye katika Roho na Kweli.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo lihimidiwe milele na milele. Amin.

 Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa  Maombezi, Ushauri au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312



Mada Zinazoendana:

FIMBO YA HARUNI!

HISIA YA MUNGU ILIYO MBAYA KULIKO ZOTE.

MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.

FAHAMU ZA WATU HUWA ZINAONDOLEWA NA NINI?


Rudi Nyumbani

Print this post

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.

 Shalom. Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Neno la Kristo linasema:

1 Petro 3:7 “Kadhalika ninyi waume, KAENI NA WAKE ZENU KWA AKILI; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.”

Agizo hilo biblia iliyotoa linawahusu wanaume waliooa , na si kila mwanamume tu!..kwasababu utasikia mtu ambaye anaishi na mwanamke ambaye hawajaoana, au anaishi na mwanamke ambaye si mke wake, bali ni mke wa mtu mwingine…. anakwambia… “Biblia imetuambia tuishi na wake zetu kwa akili”… nataka nikuambia ndugu hapo utakuwa huishi kwa akili, bali kwa kukosa akili…kwasababu mtakuwa mnafanya uzinzi na uasherati! Utasema hilo lipo wapi katika maandiko

Mithali 6: 32 “Mtu aziniye na MWANAMKE HANA AKILI KABISA; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake. 33 Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima; Wala fedheha yake haitafutika”.

Umeona? Akili inayozungumziwa hapo?..sio akili ya kuwa beberu ndani ya nyumba, au kuchepuka.. Ikiwa na maana kuwa moja wapo ya akili anazotakiwa mwanamume awe nazo anapoishi na mke wake ndio hiyo… “ KUWA MWAMINIFU KATIKA NDOA YAKE KWA KUJIEPUSHA NA ZINAA NJE YA NDOA YAKE”.

Kwasababu biblia inasema mtu aziniye na mwanamke atapata jeraha na kujivunjiwa heshima yake..itakufaidia nini unafanya zinaa nje ya ndoa yako halafu siku moja unafumaniwa na watu wanaanza kukunyooshea kidole?..hapo utakuwa umefanya jambo la kipumbavu, na biblia inasema fedheha yako haitafutika..Ni doa la daima.

Na hiyo AKILI ya kushinda, uasherati inakuja kwa kumwamini Yesu Kristo tu!, na kuoshwa dhambi zako kwa damu yake na kufanyika kiumbe kipya…haiji kwa kuongeza mke wa pili au watatu…Yesu pekee ndiye atakayeweza kukuondolea kiu ya mambo yote machafu ya ulimwengu huu.

⏩Maana nyingine ya kuishi na mke kwa akili, ni kumpenda na kumjali, upendo husitiri mambo mengi sana..Na hakuna mtu anayechukia kupendwa, kwahiyo upendo wa kweli na wa dhati ukiwepo hakuna matatizo yoyote yatakayojitokeza katika maisha ya ndoa..kutakuwa siku zote ni furaha, hiyo nayo ni akili.

⏩Maana nyingine ya kuishi na mke kwa akili, ni kugundua kasoro zake, na mapungufu yake, na kujua namna ya kuyatatua hayo ki BIBLIA!..Zingatia hilo neno KI BIBLIA! Sio kwa kutumia hekima za waswahili, au wasanii, au mila, au marafiki hapana! Bali biblia…epuka sana kutafuta suluhisho la “wahenga walisema”..au “wazee wazamani walisema” au “watu wanasemaga”…badala yake ni lazima UJIFUNZE kutafuta suluhisho kutoka kwenye Biblia(Maandiko matakatifu). Hekima za watu wa ulimwengu huu, zinafaa kwa baadhi ya mambo lakini si yote! Asilimia kubwa ya hekima za dunia hii zinazoshauri kuhusu masuala ya ndoa zinapotosha nyingi ni za Yule adui.

Kwahiyo hapo, ni lazima MWANAMUME ulijue NENO LA MUNGU kwa wingi ndani yako, hiyo ndio AKILI ya kuishi na mke wako?.

⏩Na maana ya mwisho ya kuishi kwa akili ni kuishi kwa Malengo Fulani ya kimaisha, ambayo hayakinzani na Neno la Mungu, hapa ndio linakuja suala la kupanga maisha na namna ya kujiongezea kipato kwa kazi zinazompa Mungu utukufu na mambo yote yanayofanana na hayo kwa ajili ya maisha mazuri ya familia.

⏩Lakini pia kumbuka Neno la Mungu halijamzuia pia mwanamke kuishi na mwanamume kwa akili, kwasababu na yeye kapewa akili vile vile, nanapaswa na yeye pia aishi na mume wake kwa akili, Kwa kujiepusha na zinaa na mambo yote tuliyojifunza hapo juu.

Pia wewe kama mwanamke soma vifungu hivi vitakusaidi kujua mwanamke mwenye akili kibiblia ni yupi..si yule wa kukaa vibarazani na kuwasema watu.

Mithali 31: 10 “Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani.

11 Moyo wa mumewe humwamini, Wala hatakosa kupata mapato.

12 Humtendea mema wala si mabaya, Siku zote za maisha yake.

13 Hutafuta sufu na kitani; Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo.

14 Afanana na merikebu za biashara; Huleta chakula chake kutoka mbali.

15 Tena huamka, kabla haujaisha usiku; Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula; Na wajakazi wake sehemu zao.

16 Huangalia shamba, akalinunua; Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.

17 Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi; Hutia mikono yake nguvu.

18 Huona kama bidhaa yake ina faida; Taa yake haizimiki usiku.

19 Hutia mikono yake katika kusokota; Na mikono yake huishika pia.

20 Huwakunjulia maskini mikono yake; Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake.

21 Hawahofii theluji watu wa nyumbani mwake; Maana wote wa nyumbani mwake huvikwa nguo nyekundu.

22 Hujifanyia mazulia ya urembo; Mavazi yake ni kitani safi na urujuani.

23 Mume wake hujulikana malangoni; Aketipo pamoja na wazee wa nchi.

24 Hufanya nguo za kitani na kuziuza; Huwapa wafanya biashara mishipi.

25 Nguvu na hadhi ndiyo mavazi yake; Anaucheka wakati ujao.

26 Hufumbua kinywa chake kwa hekima, Na sheria ya wema i katika ulimi wake.

27 Huangalia sana njia za watu wa nyumbani mwake; Wala hali chakula cha uvivu.

28 Wanawe huondoka na kumwita heri; Mumewe naye humsifu, na kusema,

29 Binti za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe umewapita wote.

30 Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa. 31 Mpe mapato ya mikono yake, Na matendo yake yamsifu malangoni.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa Maombezi, Ushauri au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225683036618/ +225789001312



Mada Zinazoendana:

FAHAMU ZA WATU HUWA ZINAONDOLEWA NA NINI?

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

‘’MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI’’..NA NDIVYO ILIVYO KWA UASHERATI

NINI TOFAUTI KATI YA UZINZI NA UASHERATI ?


Rudi Nyumbani

Print this post

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

Ukisoma vitabu vya Injili utaona mfano wa kwanza kabisa BWANA YESU alioutoa ni ule mfano wa Mpanzi, utaona jinsi mpanzi alivyotoka na kwenda kupanda mbegu zake, ukiendelea kusoma pale utagundua kuwa ule mfano haukueleweka kwa wengi, sio tu kwa makutano bali pia kwa wanafunzi wake..Lakini walipomfuata na kumwomba awafafanulie kuna kauli Bwana Yesu aliitoa pale nataka tuione; nayo ni hii:

Marko 4.13 ‘Akawaambia, Hamjui mfano huu? BASI MIFANO YOTE MTAITAMBUAJE?’.

Tafakari hilo Neno, BASI MIFANO YOTE MTAITAMBUAJE?..Kumbe Mfano huo ni msingi wa kuielewa na mifano mingine yote iliyobakia, kwa watu wanaofahamu somo la Hisabati vizuri wanaelewa kuwa kanuni ya PAI π..Ni kiungo kikuu cha Hisabati, ukitaka kutafuata Eneo la kitu chochote kile iwe ni duara au tufe, pipa, n.k. basi PAI ni lazima itumike.

Vivyo hivyo tukirudi kwenye maandiko ili kuielewa mifano yote Yesu aliyokuwa anaifundisha kuhusiana na ufalme wa mbinguni basi tafsiri ya mfano ule wa Mpanzi ni lazima kuulewa vinginevyo hutaambulia chochote.

Sasa tukirudi katika huo mfano kwa kuwa unajulikana hatutaweza kuuleza wote hapa, lakini mpanzi Yule alipotoka kwenda shambani malengo yake yalikuwa ni mbegu zake zote zimee vizuri na kuzaa nyingine 30, nyingine 60, nyingine 100. Lakini tunasoma zilikumbana na changamoto kadhaa kabla ya kufikia hatua ya kuzaa matunda.

Sasa kabla hatujafika mbali nataka tuone mifano miwili iliyofuata mbele yake baada ya huo..Ili itusaidie kuunga kiini cha somo letu la leo vizuri ..

Tusome..

Marko 4:26 ‘Akasema, Ufalme wa Mungu, mfano wake ni kama mtu aliyemwaga mbegu juu ya nchi;

27 akawa akilala na kuondoka, usiku na mchana, nayo mbegu ikamea na kukua, asivyojua yeye.

28 Maana nchi huzaa yenyewe; kwanza jani, tena suke, kisha ngano pevu katika suke.

29 Hata matunda yakiiva, mara atapeleka mundu, kwa kuwa mavuno yamefika.

30 Akasema, Tuulinganishe na nini ufalme wa Mungu? Au tuutie katika mfano gani?

31 Ni kama punje ya haradali, ambayo ipandwapo katika nchi, ingawa ni ndogo kuliko mbegu zote zilizo katika nchi,

32 lakini ikiisha kupandwa hukua, ikawa kubwa kuliko miti yote ya mboga, ikafanya matawi makubwa; hata ndege wa angani waweza kukaa chini ya uvuli wake.

33 Kwa mifano mingi ya namna hii alikuwa akisema nao neno lake, kwa kadiri walivyoweza kulisikia’.

AMEN.

Sasa Nataka tuichukue kwa pamoja mifano hii mitatu, tuunde kitu ambacho kitatusaidia wote,..Mifano hii, yote inaonyesha historia ya mbegu, jinsi zilipotoka na jinsi zilivyoishia isipokuwa katika TABIA tofauti tofauti na mapito tofauti tofauti.

Kumbuka kule nyumba kabisa kwenye mfano wa mpanzi Bwana Yesu alitoa tafsiri ya Ile mbegu kuwa lile ni NENO LA Mungu (Luka 8:11) lililopandwa ndani ya moyo wa mtu. Hivyo Neno la Mungu linapopandwa katika moyo wa mtu katika hatua za awali penda lisipende litapita katika nyakati TATU kulingana na mifano hiyo mitatu.

1) ⏩Kwanza ni lazima lipitie changamoto: Mtu aliyepandwa atakumbana na udhia, na misongo ya hapa na pale, kulingana na ule mfano wa mpanzi, Hili ni jukumu la mhusika mwenyewe kuhakikisha kuwa haling’olewi na Yule adui, wala halisongwi.

2)⏩ Pili Litakuwa linamea lenyewe: Hili sio jukumu tena la mtu, bali ni jukumu la Mungu mwenyewe, wakati linavumilia vipindi vigumu vya hatihati ya kung’olewa au kusongwa, huku kwa nyuma siku baada ya siku linakuwa lenyewe taratibu.

3) ⏩Na Tatu japo litaanzia katika udogo sana, likishafikia ukomavu litakuwa kubwa kuliko miti mingine yote. Hivyo mwisho wa safari ya utunzaji wa mbegu ile. Basi litakuwa baraka kubwa sana kuliko chochote kile duniani.

Hivyo ndugu, ndio maana sasa baada ya mifano ya namna hiyo kuisha YESU akaanza kuwafundisha watu mifano inayoelezea thamani ya mbegu hiyo akiifananisha na Hazina kubwa sana na lulu za thamani ..utaona anasema, ufalme wa mbinguni umefanana na mfanyabiashara aliyekuwa anatafuta Lulu ya thamani kubwa, na alipoina akaenda kuuza vyote alivyonavyo na kwenda kuinunua lulu ile, anasema tena ni sawa na mtu aliyeona hazina iliyositirika katika shamba, alipoiona akaificha na kwa furaha akaenda kuuza vyote alivyonavyo na kwenda kulinunua shamba lile.

Hiyo yote ni kuonyesha kuwa ana AKILI sana mtu yule anayelisikia Neno la Mungu na kuzingatia kuliweka moyoni mwake, na kwenda kufanyia kazi kile anachofundishwa, anafanya bidii kulifakari Neno la Mungu, analiona kama almasi, anatafuta huku na kule huku akilinganisha na maandiko, akivulimilia dhiki zote zinazokuja kutokana na ukristo wake na itikadi zake kali za kuliishi Neno, na shutuma na kuchekwa, na kudharauliwa, na kutengwa, na kuchukiwa, akivumilia yote bila kuliacha hilo Neno lililopandwa moyoni mwake kudondoka, akihakikisha shughuli za ulimwengu huu hazimsongi mpaka anakosa muda wa kuwa karibu na Mungu wake, akihakikisha anapata muda mrefu wa kulitafakari Neno la Mungu kuliko kuchati..

Sasa Biblia inaeleza mtu huyo kuna faida kubwa inamngoja mbeleni yake.. Yeye kwa wakati huo hatajua chochote, wala hatafahamu kama kuna kitu kinakuwa ndani yake, anaweza kuona kama anafanya kitu ambacho hakimletei faida yoyote katika mwili, hakimwingizii pesa, hakimpi umaarufu, lakini kumbe kidogo kidogo, ile mbegu inamea, kutoka KUWA MBEGU MPAKA JANI MPAKA SUKE.. Na japo ilianza ndogo sana kama chembe ya haradali itakuwa yenyewe, kumbuka haihitaji msaada wowote kukuzwa na mtu, itakuwa na kuwa kubwa kuliko miti yote, na ndipo hapo watu watakuja kushangaa, kumetokea nini kwa mtu huyu tusiyemtazamia amekuwa hivi ghafla…Ndipo kama mfano unavyosema ndege watakuja kukaa chini ya huo mti, ndivyo itakavyokuwa kwa mtu huyo, atakuja kuwa msaada mkubwa kwa watu wengi kwa kila kitu. Kwa vitu vya rohoni na mwilini.

Hiyo ilimtokea kiongozi wetu mkuu YESU KRISTO, Biblia inasema alikuwa ni mtu wa kudharauliwa, wa kutokuaminiwa siku zote, lakini yeye alilitunza Neno la Mungu tangu utoto wake, mpaka utu uzima, mpaka alipofikia kilele sasa cha Neno lenyewe kutaka kuanza kuzaa matunda, ndipo walipomtambua kuwa Yule hakuwa mwanadamu wa kawaida..Utasoma pale walianza kujiuliza huyu sio Yule seremala, na ndugu zake tunao wote hapa? Sasa katolea wapi hekima yote hii ambayo hajasoma, na miujiza yote hii, ulimwengu mzima ulimfuata kumsikiliza, yeye ni nani hasa? Ukisoma biblia utaona kuna watu walitoka mpaka Uyunani huko kuja kutaka kumwona Bwana Yesu…Hayo ndio maajabu ya Neno la Mungu likitunzwa vizuri ndani ya mtu…Linafanya mambo makubwa, na ndio maana shetani katika hatua za kwanza atahakikisha kwa bidii zote analiondoa ndani yako.

Hizi ni siri kutoka kwa MKUU wetu YESU KRISTO, Kwamba kama na sisi tukizitumia, tutafika pale alipo yeye. Leo hii, mbegu nyingi zinatupwa ndani yako, unazidharau, kwasababu labda mtu huyo anayekuhubiria hajulikani, ni mtu tu wa mtaani unayemfahamu, lakini kumbuka ufalme wa Mungu ndani ya mtu unaanza kama chembe ya haradali, ndogo sana, maneno ambayo mtumishi yoyote yule wa kawaida anaweza akayabeba ndani yake, inaanza kwa maneno machache sana ya wokovu, ambayo baadaye yakiisha kukua ndani ya mtu yanaweza kuupindia ulimwengu mzima.. Usipuuzie Neno la Mungu leo unapolisikia, embu chukua hatua ya kuanza kulitunza, anza kulifanyia kazi, hakikisha shetani hakichukui hichi ulichokisia moyoni mwako, na dalili zitakazoonyesha hiyo mbegu inakuwa ni maadui kutokea, shetani atafanya juu chini kuing’oa lakini wewe zingatia kanuni hizo, UVUMILIE yote, iwe ni dhiki, iwe ni misongo ya mambo ya ulimwengu huu..Fanya bidii kulitunza Neno la Mungu, faida yake utaiona baada ya muda Fulani.

Ni matumaini yangu, utatubu leo na kumkabidhi Bwana maisha yako. Huo ndio mwanzo wa kuitunza mbegu yao.

Ubarikiwe sana.

Amen.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa Maombezi, Ushauri, au Ratiba za Ibada wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312


Mada Zinazoendana:

JE! WEWE NI MBEGU HALISI?

USIACHE KUJIFUNZA NENO LA MUNGU

NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.

TUNAPOSEMA TUISHI KWA NENO, INAMAANISHA TUISHI MAISHA YA NAMNA GANI?


Rudi Nyumbani

Print this post

OKOA BADALA YA KUANGAMIZA!

Shalom, Mwana wa Mungu karibu tujifunze maandiko…Leo tutajifunza kwa Neema za Bwana namna ya kuokoa roho.

Bwana Yesu alisema “sikuja kuziangamiza roho bali kuziokoa (Luka 9:56)” sentensi hiyo aliisema baada ya wanafunzi wake kumwomba ashushe moto uwaangamiza wale watu wa Samaria waliokataa kumpokea…Lakini kwanini alisema vile kuwa hakuja kuziangamiza bali kuziokoa?…ni kwasababu alikuwa na uwezo wa kuziangamiza lakini hakutaka kufanya vile..kinyume chake alitafuta namna ya kuwafikishia wokovu na sio kuwaua.

Wakati mwingine tunaweza tukawa na silaha mikononi mwetu au midomoni mwetu tulizopewa na Mungu kihalali kabisa za kujeruhi na kuangusha watu wote wanaokwenda kinyume na sisi..lakini tukikosa hekima kama aliyokuwa nayo Bwana tutajikuta tunaangamiza roho badala ya kuokoa.

Hebu mtafakari Musa, wakati wana wa Israeli wanamkosea Mungu kule jangwani…Mungu alimwambia Musa ajitenge na wale watu ili apate kuwaangamiza…na atamfanya Musa kuwa Taifa kubwa, atampa uzao utakaoirithi nchi….ingekuwa ni mmojawapo wa sisi tungesema asante Mungu, kwa kuwa umeteta nao wanaoteta nami, lakini tunaona Musa, alilipindua wazo la Mungu na kuanza kuwaombea msamaha ndugu zake na kuwatafutia upatanisho na Mungu, na Mungu akalisikiliza ushauri wa Musa na kughairi mawazo yake…

Sasa tuchukulie mfano Musa, angekubali kujitenga nao, unadhani, kulikuwa kuna kosa lolote pale? hapana Mungu kweli angewaangamiza wale watu na angeenda kumfanya Musa kuwa Taifa kubwa kama alivyomwahidia..Lakini Musa angekuwa hajatenda kwa busara mashauri yale yalitoka kweli kwa Mungu, angekuwa hajastahili kuwa kiongozi bora kwasababu hakuizuia ghadhabu ya Mungu juu ya watu wake. Kwahiyo pengine hata Mungu asingemtukuza Musa kwa kiwango hichi alichomtukuza sasa.

Kutoka 32:9 “Tena Bwana akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu

10 basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.

11 Musa akamsihi sana Bwana, Mungu wake, na kusema, Bwana, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu?

12 Kwa nini Wamisri kunena, wakisema, Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi? Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako.

13 Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele.

14 Na Bwana akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake”.

Kwahiyo hiyo inatufundisha kuwa siyo kila fursa au mamlaka tunayopewa na Mungu, tuyatumie tu bila kutafakari vizuri..Mungu wetu hajatuumba kama maroboti kwamba yeye ni wa kusema na sisi ni wakufuata tu pasipo kutafakari..hapana! huo ni utumwa na sisi sio watumwa sisi ni wana, tunazungumza na Baba yetu na kushauriana naye…ametuumba tuzungumze naye, tusemezane naye, tupeane naye mashauri.

Isaya 1: 18 “Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu”.

Ndio maana Musa alisemezana na Bwana na akasafisha dhambi za wana wa Israeli zilizokuwa nyekundu kama bendera, na akazifanya kuwa nyeupe kama sufu. Haleluya!

Mungu anaweza kumweka mtu anayekuchukia, au anayekupiga vita mikononi mwako, au mtu ambaye alikufanyia visa Fulani, ukapata madhara fulani…Mungu anaweza kumweka mikononi mwako kiasi kwamba ukisema tu neno moja umemmaliza, au ukifanya jambo Fulani tu, habari yake imekwisha ikawa ni kweli Mungu kamtia mikononi mwako ili kumlipizia kisasi, kwa ubaya aliokufanyia….kama vile Mungu alivyomtia Sauli mikononi mwa Daudi..akajua kabisa hii ni fursa ya kummaliza lakini hakufanya hivyo…nasi pia huo usiwe wakati wa kummaliza, badala yake uitumie fursa hiyo kumgeuza kwa Kristo, huo ndio wakati wa kusemezana na Bwana juu ya dhambi zake zote, na kumwombea Msamaha…hakika ukifanya hivyo na kuigeuza hasira ya Bwana, Bwana atakupenda zaidi ya anavyokupenda sasa…atakutukuza zaidi ya anavyokutukuza sasa…

Utasema hiyo habari ya Musa na Daudi ilikuwa ni ya agano la kale, vipi kuhusu agano jipya, je! Kuna mtu yeyote alishawahi kufanya hivyo..Jibu ni ndio! Hata katika agano jipya tunayo hiyo mifano.

Tunasoma habari za Paulo na wenzake, wakati mmoja walipokwenda Makedonia kuhubiri, walikutana na mtu mwenye pepo na walipomtoa Yule pepo, ndipo wakuu wa mji wakawakamata na kuwachapa bakora na kisha kuwatupa gerezani.

Sasa lile jambo halikumpendeza sana Mungu, na hivyo Bwana akawatengenezea njia ya kutoka mule gerezani, akamtuma malaika wake usiku ule wakati Paulo na Sila walipokuwa wanamsifu Mungu, ghafla vifungo vikalegea na milango ya gereza ikafunguka…sasa Lengo la Yule malaika kufungua milango ya gereza haikuwa tu kuwafurahisha wale watu , hapana ilikuwa ni ili Paulo na Sila watoke!!, waondoke mule gerezani,..Kama vile Yule malaika alivyomtoa Petro gerezani wakati Fulani alipokuwa amefungwa.

Lakini tunasoma Paulo na Sila walilitengua agizo la Bwana, badala ya kutoka na kwenda zao, waliendelea kukaa mule gerezani japokuwa Mungu aliwafungulia mlango wa kutoka…lakini walitafakari mara mbili mbili, endapo tukitoka na kwenda zetu tutakuwa kweli hatujatenda dhambi lakini tutaacha madhara makubwa huku nyuma, tutasababisha kifo badala ya kuokoa roho, na zamani zile utawala wa Rumi, mfungwa yoyote akitoroka kinachobakia kwake ni kifo tu, na ndio maana Yule askari ilikuwa nusu ajiue, lakini Paulo na Sila wakamzuia.

kwahiyo wakaitumia ile nafasi sio kwa faida yao bali kwa faida ya wengine, ndio tunaona wakaenda kumwuhubiria Yule askari injili pamoja na familia yake wote wakaokoka, na mwisho wa siku kesho yake asubuhi wakatolewa gerezani, kwahiyo ikawa faida kwao mara mbili.

Matendo 16: 22 “Makutano wote wakaondoka wakawaendea, makadhi wakawavua nguo zao kwa nguvu, wakatoa amri wapigwe kwa bakora.

23 Na walipokwisha kuwapiga mapigo mengi, wakawatupa gerezani, wakamwamuru mlinzi wa gereza awalinde sana.

24 Naye akiisha kupata amri hii akawatupa katika chumba cha ndani, akawafunga miguu kwa mkatale.

25 Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.

26 GHAFULA PAKAWA TETEMEKO KUU LA NCHI, HATA MISINGI YA GEREZA IKATIKISIKA, NA MARA HIYO MILANGO IKAFUNGUKA, VIFUNGO VYA WOTE VIKALEGEZWA.

27 Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia

28 Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa.

29 Akataka taa ziletwe, akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila;

30 kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka?

31 Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.

32 Wakamwambia neno la Bwana, yeye na watu wote waliomo nyumbani mwake.

33 Akawakaribisha saa ile ile ya usiku, akawaosha mapigo yao, kisha akabatizwa, yeye na watu wake wote wakati uo huo.

34 Akawaleta juu nyumbani kwake, akawaandalia chakula, akafurahi sana, yeye na nyumba yake yote, maana amekwisha kumwamini Mungu.

35 Kulipopambauka makadhi wakawatuma wakubwa wa askari wakisema, Waacheni watu wale waende zao.

36 Yule mlinzi wa gereza akamwarifu Paulo maneno haya akisema, Makadhi wametuma watu ili mfunguliwe; basi, sasa tokeni nje, enendeni zenu kwa amani”.

Sasa hebu fikiri endapo Paulo na Sila wangeondoka usiku ule mule gerezani, na kusema safi sana! Mungu katupigania! Kawaaibisha maadui zetu!…. ni wazi kuwa wangeshampoteza Askari na kusudi la wao kwenda makedonia lingekuwa ni sifuri kwa maana wenyewe walikwenda kwa nia ya kuhubiri injili, na sasa hapa ni sawa na wamemsababishia wengine mauti.

Kwahiyo ndugu tunajifunza, sio kila fursa ya kumpiga adui yako ni mapenzi kamili ya Mungu, sio kila mlango Mungu anaokufungulia ni wa kuutumia pasipo kutafakari, aliyekutukana, aliyekuaibisha, aliyekupiga, aliyekunyima kazi wakati Fulani tena akakufanyia na visa juu, aliyekurusha, aliyekuharibia mipango yako na maisha yako, sasa Mungu kamleta mikononi mwako..huo sio wakati wa kuitumia hiyo fursa Mungu aliyokuwekea mbele yako pasipo hekima!! Itumie hiyo KUOKOA ROHO, BADALA YA KUANGAMIZA. Hicho ndio kitu Mungu anachotaka kuona kwetu!.

Kuna muhubiri mmoja, ambaye alikuwa ni Nabii, siku moja wakati anahubiri kanisani kwake malaika wa Bwana alimwambia atazame mwisho kabisa wa kanisa, na alipotazama akaona watu wawili kwa mbali mwanamume na mwanamke wanafanya kitendo kichafu cha kunyonyana ndimi na hiyo ilikuwa ni katikati ya ibada…Yule muhubiri akakasirika sana, akawa anawaendea…wakati yupo njiani anawaendea Yule malaika aliyemwambia atazame nyuma ya kanisa, huyo huyo akamwambia sema Neno lolote na mimi nitalitimiza hilo neno saa hivi hivi kama ulivyosema…yaani maana yake angesema “Bwana naomba waanguke sasa hivi wafe, wangekufa saa ile ile”..na alipofika pale Yule muhubiri..kitu fulani kikamwingia ndani yake, kama huruma Fulani hivi… akasema “nimewasamehe”…Baadaye alivyomaliza ibada, sauti ikazungumza ndani ya moyo wake na kumwambia..”hicho ndio nilichokuwa nataka kusikia kutoka kwako”…msamaha…

Ni wazi kuwa hao watu kwa msamaha huo, baadaye walitubu na kumgeukia Mungu kwa kumaanisha.

Umeona? Epuka injili unazohubiriwa kila wakati piga adui yako, usiposamehe kuna wakati nawe utafika utamkosea Mungu, naye Mungu hatakusamehe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa Maombezi, Ushauri, au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Print this post

USILITAJE BURE JINA LA BWANA!

Kutoka 20:7 “Usilitaje bure jina la Bwana, Mungu wako, maana Bwana hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure..”

Hii ni moja ya amri tulioizoea sana, Na tumekuwa tukidhani kulitaja jina la Mungu bure ni pale tu tunapo muhusisha na mambo yasiyo na maana, au pale tunapo apa, lakini hiyo ni sehemu mojawapo ya kulitaja bure jina la Mungu, ipo sehemu nyingine ambayo ni kuu zaidi, na inamuudhi Mungu sana, pengine na wewe ulishawahi kuifanya bila kujua na pengine ndio imekuwa kikwazo kikubwa cha mafanikio ya roho yako.

Pale unaposema leo nimeamua kuwa Mkristo nimeamua kumfuata Mungu kwa moyo wangu wote, pale unaposema maisha yangu ya kale basi, hapo ni sawa na umemwita Mungu aje kuyaongoza maisha yako kuanzia huo wakati na kuendelea, au kwa lugha ki-kibiblia tunasema umeliitia jina la Mungu lije kukuokoa, lakini pale unaposema Nimeokoka, mimi ni mkristo halafu, unaendelea kuyafanya yale yale uliyoyaacha kule nyuma, unaendelea kuiba,unazidi kuzini, unatazama pornography, unasengenya n.k. Hapo ni sawa kabisa na umemdhahaki Mungu kwamba ulimwita akuokoe na kumbe haupo tayari kuokolewa, Hapo umelitaja JINA LA MUNGU wako bure!.. Ni heri usingedhubutu kuujaribu wokovu kabisa maishani mwako ..

Ukisoma katika kitabu cha Mwanzo utaona watu walioanza kumtafuta Mungu, biblia imetafsiri kama “waliliita au wanalitaja Jina la Mungu”

Mwanzo 4: 25 “Adamu akamjua mke wake tena; akazaa mwana mwanamume, akamwita jina lake Sethi; maana alisema, Mungu ameniwekea uzao mwingine mahali pa Habili; kwa sababu Kaini alimwua.

26 Sethi naye akazaa mwana; akamwita jina lake Enoshi. HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA”.

Utaona pia katika maandiko BWANA akitangaza jina lake yeye mwenyewe…utaona halitaji jina lake kama YEHOVA, bali analitaja jina lake kama TABIA..Tunalisoma hilo katika kitabu cha Kutoka.

Kutoka 34: 5 “Bwana akashuka ndani ya lile wingu, akasimama pamoja naye huko, AKALITANGAZA JINA LA BWANA.

6 Bwana akapita mbele yake, AKATANGAZA, BWANA, BWANA, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli;

7 mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; WALA SI MWENYE KUMHESABIA MTU MWOVU KUWA HANA HATIA KAMWE; MWENYE KUWAPATILIZA WATOTO UOVU WA BABA ZAO, NA WANA WA WANA WAO PIA, HATA KIZAZI CHA TATU NA CHA NNE”.

Unaona mstari wa saba hapo?…tafsiri ya jina lake sio tu Mungu mwenye huruma bali pia ni MUNGU asiyeacha kumwesabia mtu mwovu kuwa hana makosa kamwe. Kwahiyo unapompokea Kristo maishani mwako halafu maisha yako yapo vilevile hayabadiliki…Hapo ni sawa na umelitaja jina Bwana Mungu wako Bure na atakuhesabia kuwa na hatia kwa hilo.

Embu tafakari mfano huu halafu wewe uhukumu, ni sawa na leo mtu ameagiza gari nje ya nchi labda tuseme Japan kwa makubaliano ya kuwa siku litakapofika ndipo atalilipa..Lakini siku linafika ili akabidhiwe gari lake afanye malipo biashara iishe, anageuka na kusema mimi sina haja na hilo gari kwanza nilikuwa ninawatania tu, labda siku nyingine nikiwa tayari.

Wewe unadhani, wale watu watamfanyaje?. Ni dhahiri kuwa hawawezi kumwacha hivi hivi waingie hasara kwa ajili ya uzembe wake, hivyo hapo kama hatatozwa faini, basi atafunguliwa mashtaka mahakani, na mwisho wa siku lazima atajikuta analipa mpaka senti ya mwisho kwa njia yoyote ile,…Na ndivyo ilivyo kwa Mungu, tunapolitaja jina lake, (JINA LA YESU ambalo hakuna jingine zaidi ya hilo ambalo litupasalo sisi kuokolewa kwalo. Matendo 4:12) lije lituokoe, tuonyeshe kweli kweli kutaka kuokolewa vinginevyo , Bwana hatutacha hivi hivi bila kutuhesabia kuwa wenye hatia..wakati mwingine mapigo au vifo vinatukuta kwa sababu hiyo.

Na ndio maana mtunzi wa Mithali alisema.. 30:8 “Uniondolee ubatili na uongo; Usinipe umaskini wala utajiri; Unilishe chakula kilicho kadiri yangu. 9 Nisije nikashiba nikakukana, Nikasema, Bwana ni nani? Wala nisiwe maskini sana NIKAIBA, NA KULITAJA BURE JINA LA MUNGU WANGU”.

Unaona huyu mtu alijua kabisa dhambi za wizi ni sawa na kulitaja jina la Mungu wake bure.

Na sisi pia kama tunalitaja jina la YESU mwokozi wetu kuwa ndio jina pekee linalotusababisha kuwa hivi tulivyo leo ndani ya wokovu basi na tuuweke ulimwengu mbali na sisi tumfuate Mungu wetu kweli kweli kwa kumaanisha..ili tujiepushe na laana, Kwasababu maandiko ndivyo yanavyotuonya.

2Timotheo 2:19 “..KILA ALITAJAYE JINA LA BWANA NA AUACHE OUVU”.

Jina la Kristo lisitamkwe kinywani mwako kama haupo tayari kuuacha ouvu..Na unaacha uovu kwa kutubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kutokuzifanya tena, na kisha kubatizwa na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Jina la mwokozi wetu YESU KRISTO na lihimidiwe daima..

Amen.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa Maombezi, Ushauri au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312


Mada Zinazoendana:

JINA LA MUNGU NI LIPI?

JINA LAKO NI LA NANI?

SIKU YA HASIRA YA BWANA.

KANUNI JUU YA KANUNI.


Rudi Nyumbani

Print this post

UTEKA ULIOGEUZWA.

Ukisoma kitabu cha Ayubu utagundua kuwa jaribu kubwa shetani alilomshambulia Ayubu halikuwa Kufiwa na wanawe au kupoteza mali zake zote ndani ya siku moja! Hayo kweli yalimuumiza sana…lakini utaona Ayubu hakuongea lolote kuhusu hayo…Alisema tu BWANA ALITOA na BWANA AMETWAA…Jina la Bwana libarikiwe. Basi akaishia hapo! Ndio maana unaona mpaka sura ya Pili habari ya Ayubu inakuwa imeshaisha…

Lakini kuanzia sura ya 3 hadi ya 42…utaona ni habari nyingine zinaanza kuzungumziwa hapo…utaona ni mazungumzo kati ya watu watatu mpaka wane…Ayubu, Sofari, Bildadi na Elifazi…akitoka huyu anaongea huyu, akitoka huyo sofari anaongea bildadi, akitoka bildadi anaongea Ayubu hivyo hivyo mpaka mpaka sura ya 40.

Sasa wengi wetu tunapenda kusoma tu ile sura ya kwanza na ya Pili tukidhani kuwa ndio lengo la kile kitabu cha Ayubu, lakini hiyo sio kweli..Ufunuo mkubwa wa kitabu cha Ayubu upo kuanzia ile sura ya 3 na kuendelea…kuanzia ile sura ya 3 na kuendelea ndio utaona jinsi gani shetani alivyokuwa anampepete Ayubu kwa kupitia vinywa vya wale marafiki zake watatu.

Utaona jinsi gani wale marafiki zake Ayubu, walivyokuwa wanatumia maandiko kuivunja imani ya Ayubu. Nakushauri ndugu kama hujakipitia kitabu cha Ayubu kuanzia hii sura ya 3 na kuendelea kafanya hivyo leo..Kuna mambo mengi sana Bwana atakuonyesha ambayo ulikuwa huyajui.

Shetani anakawaida ya kuwa..akishindwa kumjaribu mtu kwa njia ya kawaida ya nje! Huwa anabadilisha mbinu na kuja kwa njia nyingine ya kutumia maandiko, atawaingia hata wapendwa au hata wachungaji kukuhakikishia jambo Fulani ambalo sio sahihi, nia na madhumuni ni kukuangusha tu!. Ili kulielewa hili vizuri chukua mfano ufuatao.

Tuseme shetani anataka kumwangusha mtu anayeitwa Amelia aanguke kwenye dhambi ya uasherati. Atakachokifanya kama kawaida atatafuta kwanza kibali kutoka kwa Mungu, akishakipata ataanza kutikisa kwanza uchumi wake..ili amweke katika mazingira ya uhitaji wa fedha, wakati yupo katika hayo mazingira ya kuhitaji fedha anatokea mtu mwenye fedha nyingi kidogo na kumshawishi. Na atakaposhinda vile vishawishi na kumkataa Yule mtu…Shetani atamjaribu kwa njia nyingine, atamletea mpaka magonjwa ilimradi tu! Atafute njia mbadala ya kupata fedha kwa kuutoa mwili wake….Na endapo akimwona bado huyo mwanamke kasimama…atamjaribu kwa njia nyingine mbalimbali..Na mwishowe ataacha na kuingia kwenye mbinu yake ya mwisho na kuu kuliko zote ya kumwangusha.

Katika hiyo mbinu yake ya mwisho hatatumia tena watu wa nje kumshawishi, kwasababu anajua huyu dada Amelia amesimama hawezi kutikiswa na watu wasiomjua Mungu, atakachokifanya atamfuata kule kule kanisani kwasababu imani yake yote ipo katika nyumba ya Mungu na anawaamini watu wa Mungu.

Kwahiyo siku moja ataingia kanisani na kusikia mahubiri yafuatayo…. “kuna watu humu ndani wanachezea bahati, utakuta mtu anashida, Mungu anamfungulia mlango wa fedha anakataa, unakuta mtu ni mgonjwa, hana hela anakuja mtu anataka kumsaidia anakataa, kwa njia hiyo hata kuolewa hutaolewa..dada! na watu wote kanisani wanajibu Ameen!” Na huyo mtumishi atasoma mistari kadha kadhaa kwenye biblia kuthibitisha mahubiri yake.

Sasa kwa mahubiri kama hayo..huyu dada atatoka kanisani huku kuna kitu kinamuhukumu ndani,…anaanza kujitathimini pengine lile Neno lilikuwa linamhusu yeye…Ni watu wangapi wamekuja kumjaribu akawakataa…pengine kweli anachezea bahati! Akijiangalia ni kweli ana matatizo ya fedha, sasa Kidogo kidogo anaanza kushawishika na kuhisi alikuwa anafanya makosa kujiepusha na wale watu waliokuwa wanakuja kumjaribu, anaanza kufikiri pengine hata alikuwa anamkosea Mungu, hivyo baada ya siku kadhaa akitokea mwingine anaanza kumsikiliza na mwishowe kuanguka kwenye dhambi ya uasherati na kushindwa na shetani.

Hizo ndizo njia shetani anazozitumia kuwaangusha wengi waliosimama…Na ndio Ayubu naye yalimkuta hayo hayo…shetani alipoona hatetereki hata kwa msiba wa wanawe..akawaingia marafiki zake Ayubu watatu ambao nao pia walikuwa tunaweza kusema ni watumishi kama Ayubu, walikuwa wanamtafuta Mungu pamoja naye na kusali pamoja naye. Wakaanza kumwambia Ayubu, tatizo haliko kwa Mungu, tatizo lipo kwako, haiwezekani yakupate haya yote wewe tu na si mtu mwingine, lazima utakuwa umetenda dhambi kwahiyo nenda katubu! Ubadilishe na njia zako. Na walitumia maaandiko kumshawishi Ayubu ageuke aiache njia yake. Lakini tunaona Ayubu alisimama thabiti mpaka Mwisho na hatimaye Bwana akageuza uteka wake..

Sasa leo kwa Neema za Bwana hatutazungumzia sana juu ya huduma za hawa rafiki zake watatu Ayubu, kama utahitahi somo kwa urefu kuhusu huduma zao unaweza ukawasiliana na mimi inbox nikutumie somo hilo.

Lakini leo tutazungumzia ni kwa namna gani Bwana alimrejeshea Ayubu mali zake zote maradufu na familia yake. Kwa namna hiyo hiyo na sisi tunaweza kuzipata Baraka zetu maradufu endapo tukifanya kama Ayubu alivyofanya.

Ukisoma Mwishoni mwa kitabu cha Ayubu ile sura ya 42 tunasoma..

Ayubu 42: 7 “Basi ikawa, baada ya Bwana kumwambia Ayubu maneno hayo, Bwana akamwambia huyo Elifazi Mtemani, Hasira zangu zinawaka juu yako, na juu ya hao rafiki zako wawili; kwa kuwa ninyi hamkunena yaliyo sawa katika habari zangu, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu.

8 Basi sasa, jitwalieni ng’ombe waume saba, na kondoo waume saba, mkamwendee mtumishi wangu Ayubu, mjisongezee sadaka ya kuteketezwa; na huyo mtumishi wangu Ayubu atawaombea ninyi; kwa kuwa nitamridhia yeye, nisiwatende sawasawa na upumbavu wenu; kwani ninyi hamkunena maneno yaliyonyoka katika habari zangu, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu.

9 Basi Elifazi, Mtemani, na Bildadi, Mshuhi, na Sofari, Mnaamathi, wakaenda, wakafanya kama vile Bwana alivyowaamuru; naye Bwana akamridhia Ayubu.

10 KISHA BWANA AKAUGEUZA UTEKA WA AYUBU, HAPO ALIPOWAOMBEA RAFIKI ZAKE; BWANA NAYE AKAMPA AYUBU MARA MBILI KULIKO HAYO ALIYOKUWA NAYO KWANZA.

11 Ndipo wakamwendea nduguze wote, waume kwa wake, nao wote waliojuana naye hapo zamani, wakala chakula pamoja naye katika nyumba yake; nao wakamlilia na kumtuza moyo katika habari za huo uovu wote Bwana aliouleta juu yake; kila mtu akampa kipande cha fedha, na pete ya dhahabu kila mmoja.

12 Basi hivyo Bwana akaubarikia huo mwisho wa Ayubu zaidi ya mwanzo wake; naye alikuwa na kondoo kumi na nne elfu, na ngamia elfu sita, na jozi za ng’ombe elfu, na punda wake elfu.

13 Tena alikuwa na wana waume saba, na binti watatu.

14 Akamwita huyo wa kwanza jina lake Yemima; na wa pili akamwita jina lake Kesia; na wa tatu akamwita jina lake Keren-hapuhu.

15 Katika nchi hiyo yote hawakuwapo wanawake waliokuwa wazuri kama hao wana wa Ayubu; na baba yao akawapa urithi kati ya ndugu zao wana waume.

16 Kisha baada ya mambo hayo Ayubu akaishi miaka mia na arobaini, naye akawaona wanawe, na wana wa wanawe, hata vizazi vinne.

17 Basi Ayubu akafa, mzee sana mwenye kujawa na siku”.

Nataka uuone huo mstari wa 10 unaosema.. “ kisha bwana akaugeuza uteka wa ayubu, HAPO ALIPOWAOMBEA RAFIKI ZAKE; Bwana naye akampa ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza”.

HAPO ALIPOWAOMBEA RAFIKI ZAKE”…hilo ndilo Neno la Msingi la leo. Pamoja na kwamba shetani aliwatumia rafiki zake kumjaribu yeye, pamoja na kwamba rafiki zake walimchukiza sana Mungu, mpaka hasira za Bwana zikawaka juu yao, akataka kuwaua…Lakini Ayubu hakuwahukumu wala kuwachukia aliwahurumia…akaenda akapiga magoti akawaombea toba! Na msamaha! Akatubu kwa ajili yao kwa dhabihu na machozi…Akawaombea rafiki zake Baraka badala ya Laana, heri badala ya shari..Na Mungu akawasamehe.. Na Bwana akapendezwa sana na AYUBU kwasababu hiyo ya kuwaombea rafiki zake…ndipo UTEKA WAKE UKAGEUZWA.. Akapewa vile vitu mara mbili..Bwana akamrudishia vyote alivyopoteza HALELUYA!!

Tunajifunza nini hapo?…kuna watu watatumiwa na shetani kutujaribu, hususani wanaotumia biblia..pengine ni marafiki zetu au ndugu zetu, na kwasababu Neno la Mungu linakaa ndani yetu, tunazitambua fikra za shetani ndani yao..Na mambo wanayofanya ukaona kabisa yanamchukiza Mungu na Mungu kawakasirikia, sasa huo sio wakati wa kupiga maadui yako!! Sio wakati kusema walaaniwe maadui zangu, wafe maadui zangu, waanguke!! Hapana! Biblia haitufundishi hivyo hata kidogo…inatufundisha kwenda kwenye magoti kutubu kwa ajili yao, kuwaombea msamaha, kulia hata ikiwezekana kutoa sadaka kwa ajili yao…hivyo ndivyo Bwana naye atakavyogeuza UTEKA WETU! Ndugu jitenge na injili za kupiga maadui si za kimaandiko hata kidogo…ukifanya hivyo Mungu hatageuza uteka wako hata kidogo. Tujifunze kwa Ayubu hakuna mtu aliyeumizwa moyo kama Ayubu, kapata msiba na wakati huo huo rafiki zake wanamwambia ana dhambi nyingi…inaumiza kiasi gani, lakini hakuwalaani bali aliwaombea..

Biblia inasema katika Mithali 24: 17 “Usifurahi, adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;

18 Bwana asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake”.

Unaona! Ndio maana Bwana alisema “ombea adui yako”..kwasababu unavyomwombea ndivyo Bwana anavyogeuza uteka wako.

Bwana akubariki sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa Maombezi, Ushauri au Ratiba za Ibada, Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312


Mada Zinazoendana:

HUDUMA YA (ELIFAZI, BILDADI, NA SOFARI).

MNGOJEE BWANA

AYUBU ALITESEKA KATIKA MAJARIBU KWA MIAKA MINGAPI?.

NINAJUA MAWAZO NIKUWAZIAYO:

AYUBU 28 : HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?


Rudi Nyumbani

Print this post

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

Karibu katika mwendelezo wa kujifunza vitabu vya biblia.

Kwa ufupi tumeshapitia vitabu vinne vya kwanza yaani kitabu cha Mwanzo, kutoka,Mambo ya Walawi na Hesabu na leo Kwa Neema za Bwana tutasogea mbele na vitabu vingine vinne vinavyofuata.

5) KUMBUKUMBU LA TORATI:

Kitabu hichi cha kumbukumbu la torati kiliandikwa na Musa, katika hatua za mwisho kabisa karibia na wana wa Israeli kuingia nchi ya Ahadi, Musa alipewa maagizo na Mungu aandike kitabu hichi kwaajili ya ukumbusho wa Torati..Kama jina lake lilivyo “kumbukumbu la Torati”..kwahiyo ni wazi kuwa kilikuwa ni kitabu cha kumbukumbu ya vitu ambavyo walikuwa tayari walishapewa au kuagizwa.

Mungu aliruhusu kitabu hichi kiandikwe kwaajili ya kizazi kipya cha wana wa Israeli, waliozaliwa katikati ya safari. Kwasababu wengi wa waliotoka nchi ya Misri walikufa njiani, kutokana na manung’uniko yao kwa Mungu ndio wale waliyoyaona matendo yote makuu Mungu aliyowatendea kwa macho yao lakini hawakutaka kumwamini na hiyo ikapelekea Mungu kuchukizwa nao, Mpaka kuwaahidia kuwa hakuna hata mmoja aliyetoka nchi ya Misri atayaeiona nchi ya Ahadi isipokuwa Kalebu na Yoshua tu! Ndivyo ilivyokuja kutimia kama ilivyo, wote walikufa wakabaki watoto wao..na hawa watoto waliozaliwa jangwani walikuwa hawamjui Mungu wa Israeli vizuri, hawakuyaona matendo Mungu aliyoyafanya wakiwa kule Misri,

kwahiyo ililazimika Kitabu kiandikwe ili kuwakumbusha TORATI ya Mungu aliyowapa wakiwa jangwani…ili wasije wakakengeuka na kumkosea Mungu kama baba zao na mama zao walivyofanya.

Kumbukumbu la torati 6: 4 “Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja.

5 Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.

6 Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako;

7 NAWE UWAFUNDISHE WATOTO WAKO KWA BIDII, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo”.

Kwahiyo kwa maagizo ya kitabu hichi cha kumbukumbu la torati, watoto wote waliozaliwa katikati ya safari kiliwasaidia kuwakumbusha matendo ya Mungu yote aliyoyafanya tangu alipowatoa wana wa Israeli katika nyumba ya utumwa, Kwahiyo kilibeba kumbukumbu ya sheria na amri zote za Mungu kuanzia Amri kumi mpaka sheria za Makuhani (Walawi). Kwahiyo kwa ufupi tunaweza kusema ni kama kitabu cha marudio ya sheria, hukumu, na baraka..Mungu alizowawekea wana wa Israeli wakiwa njiani kuelekea Nchi ya Kaanani.(Ndio maana kikaitwa kumbukumbu la Torati)

6) KITABU CHA YOSHUA:

Kitabu cha Yoshua kiliandikwa na Yoshua mwenyewe, baada ya Musa kufa…Yoshua ndiye aliyekabidhiwa gurudumu na Mungu mwenyewe, kuwaongoza wana wa Israeli kuingia nchi ya Kaanani, baada ya kuzunguka miaka 40 jangwani..Kwahiyo Yoshua na Kalebu ndio waliosalia miongoni wa waliotoka Misri, hawa wawili ndio waliobebeshwa jukumu kukiingiza kizazi kipya cha wana wa Israeli katika nchi ya ahadi.

Kusudi kubwa la kuandika hichi kitabu cha Yoshua ni kuonyesha jinsi Wana wa Israeli walivyoshindana katika kutwaa urithi wao walioahidiwa…Hatua kwa hatua, jinsi walivyopigana vita na kuyatoa yale mataifa saba yaliyoshikilia urithi wao..Ni kitabu cha Vita, chini ya amiri jeshi wao Yoshua, Bwana aliyemtia mafuta kwa kuwashindania Israeli.

Yoshua 1: 1 “Ikawa baada ya kufa kwake Musa, mtumishi wa Bwana, Bwana akamwambia Yoshua, mwana wa Nuni, mtumishi wa Musa, akasema,

2 Musa mtumishi wangu amekufa; haya basi, ondoka, vuka mto huu wa Yordani; wewe na watu hawa wote, mkaende hata nchi niwapayo wana wa Israeli.

3 Kila mahali zitakapopakanyaga nyayo za miguu yenu, nimewapa ninyi, kama nilivyomwapia Musa.

4 Tangu jangwa hili na mlima huu, Lebanoni, mpaka mto ule mkubwa, mto wa Frati, nchi yote ya Wahiti, tena mpaka bahari ile kubwa upande wa machweo ya jua, hapo ndipo patakapokuwa mpaka wenu.

5 Hapatakuwa mtu ye yote atakayeweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako; kama nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe; sitakupungukia wala sitakuacha”.

Kwahiyo rekodi yote ya vita, iliandikwa ndani ya hichi kitabu cha yoshua, ni sawa kipindi kile Rais Nyerere amwagize aliyekuwa mkuu wa Majeshi, aandike kitabu cha jinsi walivyovamia majeshi ya Uganda na kuyaangusha, kwenye vita dhidi ya Idd Amin, hatua kwa hatua jinsi walivyoteka jimbo moja baada ya lingine, na hatimaye jinsi walivyofanikiwa kuiteka Uganda yote na kuuangusha utawala wa Idd Amini. Ndivyo kitabu cha Yoshua kilivyo kinaelezea hatua kwa hatua namna Israeli walivyoteka na kuyatwaa maeneo ambayo Mungu aliwaahidia yatakuwa urithi wao katika nchi ya Ahadi.

Na hichi kitabu cha yoshua  pia kiliandikwa kwa dhumuni ya kuonyesha mipaka ya wana wa Israeli katika nchi mpya ya Kaanani waliyoiingia..kwamba kila Kabila liligawiwa sehemu yake..

Kumbuka vitabu hivi pia, havikuandikwa kama hadithi tu, kutufurahisha sisi tunaosoma wa vizazi hivi..hapana bali kila kitabu kina kimebeba maana kubwa sana na ujumbe mzito katika roho. Vitabu hivi vina maudhui makubwa sana katika kutufundisha sisi watu wa siku za mwisho. Hivyo nakushauri unaposoma vitabu hivi, omba Roho wa Mungu akusaidie kupata uelewa ya ujumbe kwa wakati wako husika. Na hakika utafurahia na kujifunza mengi sana.

7) KITABU CHA WAAMUZI:

 Kitabu kinachofuata ni kitabu cha Waamuzi kitabu hichi kiliandikwa na nabii Samweli. Kama jina la kitabu lilivyo “waamuzi” maana yake ni kitabu kinachozungumzia watu fulani ambao wamewekwa kutoa “suluhisho la mwisho la mambo yahusuyo nchi” au kwa lugha rahisi tunaweza kuwaita mahakimu.

Sasa Nabii Samweli ndiye aliyeagizwa na Bwana akiandike hichi kitabu cha Waamuzi, miaka mingi sana baada ya waamuzi wote kupita…aliagizwa aandike mambo waliyoyafanya hawa waamuzi moja baada ya lingine, kwani matendo yao yamebeba ufunuo wa KiMungu mkubwa sana ambao ungekuja kueleweka na vizazi vya mbeleni..ambao ndio sisi tunaosoma sasa.

Waamuzi walikuwa ni watu waliokuwa wanatoa maamuzi ya mwisho katika Israeli, baada tu ya wana wa Israeli kuingia katika nchi ya Kaanani..Mungu hakuwahi kuweka muamuzi katika nchi, lakini kwasababu ya kukengeuka kwa wana wa Israeli na kuiacha sheria na maagizo yake, Ndipo Mungu aliwatupa kwenye mikono ya maadui zao wateswe lakini walipomlilia Mungu, ndipo Mungu akawatumia mwokozi ili awaokoe kutoka kwenye shida zao, na huyo mwokozi Bwana aliyewatumia baada ya kuwaokoa katika shida zao ndio anakuwa kama MWAMUZI wa Taifa hilo kwa wakati huo.

Kitabu cha Waamuzi 2: 8 “Kisha Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Bwana, akafa, naye alipata umri wa miaka mia na kumi.

9 Nao wakamzika katika mpaka wa urithi wake katika Timnath-heresi, katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu, upande wa kaskazini wa mlima wa Gaashi.

10 Tena watu wote wa kizazi hicho nao walikusanywa waende kwa baba zao; kikainuka kizazi kingine nyuma yao, ambacho hakikumjua Bwana, wala hawakuijua hiyo kazi ambayo alikuwa ameitenda kwa ajili ya Israeli.

11 WANA WA ISRAELI WALIFANYA YALIYOKUWA NI MAOVU MBELE ZA MACHO YA BWANA, NAO WAKAWATUMIKIA MABAALI.

12 Wakamwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri, wakafuata miungu mingine, baadhi ya miungu ya watu wale waliokaa karibu nao pande zote, wakajiinamisha mbele yao; wakamkasirisha Bwana, akaghadhibika.

13 Wakamwacha Bwana, wakamtumikia Baali na Maashtorethi.

14 HASIRA YA BWANA IKAWAKA JUU YA ISRAELI, NAYE AKAWATIA KATIKA MIKONO YA WATU WALIOWATEKA NYARA, AKAWAUZA NA KUWATIA KATIKA MIKONO YA ADUI ZAO PANDE ZOTE; HATA WASIWEZE TENA KUSIMAMA MBELE YA ADUI ZAO.

15 Kila walikokwenda mkono wa Bwana ulikuwa juu yao kuwatenda mabaya, kama Bwana alivyosema, na kama Bwana alivyowaapia; nao wakafadhaika sana.

16 KISHA BWANA AKAWAINUA WAAMUZI, waliowaokoa na mikono ya watu hao waliowateka nyara.

17 Lakini hawakuwasikiliza hao waamuzi wao, maana walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine, wakajiinamisha mbele yao; wakageuka upesi, na kuiacha njia ile waliyoiendea baba zao, waliozitii amri za Bwana bali wao hawakufanya hivyo.

18 Na wakati Bwana alipowainulia waamuzi, ndipo Bwana alikuwa pamoja na mwamuzi huyo, akawaokoa na mikono ya adui zao siku zote za mwamuzi huyo; maana Bwana alighairi kwa ajili ya kuugua kwao kwa sababu ya watu wale waliowaonea na kuwasumbua.

19 Lakini ikawa, wakati alipokufa mwamuzi huyo, wakarudi nyuma wakafanya maovu kuliko baba zao, kwa kuifuata miungu mingine ili kuitumikia, na kuinama mbele yao; hawakuacha matendo yao, wala njia zao za ukaidi”.

Katika Israeli walipita waamuzi 16 Samsoni akiwa mmoja wao, na Gideoni na Debora, na Yefta n.k. Hawa wote waliiamua Israeli kwa vipindi tofauti tofauti walikuwa wana madaraka karibia yafanane na ya kifalme lakini hawakuwa wafalme..Na Samweli mwandishi wa kitabu hichi ndiye aliyekuwa mwamuzi wa Mwisho katika Israeli, ni sharti mwamuzi wa Mwisho ndiye awe mwandishi kwasababu yeye ndiye atakayekuwa na rekodi ya matukio yote ya waamuzi waliomtangulia…Mwamuzi wa kwanza haiwezekani apewe jukumu la kuandika historia ya mbeleni, ni lazima yule wa mwisho ndio awe muhasisi….

Kwahiyo hichi kitabu cha WAAMUZI, unapokisoma kimebeba siri nyingi Mungu alizozificha ndani ya hawa waamuzi, ukimsoma Gideoni utaona ufunuo wa ajabu sana, Vivyo hivyo Samsoni, vivyo hivyo Debora, vivyo hivyo Yeftha na wengine wote.

8) KITABU CHA RUTHU:

Hichi kitabu cha Ruthu ni kitabu cha Nane katika Biblia..Kitabu hichi kiliandikwa na Nabii Samweli yule yule aliyekuwa mwamuzi wa Mwisho wa Israeli, na aliyeandika kitabu cha Waamuzi, Bwana alimwongoza Nabii Samweli akiandike kitabu hichi kwani kimebeba maudhui makubwa sana katika mwili na katika Roho kwa kanisa lake..katika siku za mbeleni.

Kama jina la kitabu lilivyo RUTHU, Ikimaanisha kuwa ni kitabu kinachomwelezea mtu anayeitwa Ruthu. 

Kinaelezea maisha ya Ruthu, na kinaelezea jinsi Mungu alivyomlipaji wa thawabu kwa wote wenye haki, jinsi alivyomlipa Ruthu kwa uvumilivu wake na upendo wake..Mpaka kufanyika kuwa mama wa Bibi wa Mfalme Mkuu atakayekuja kutokea miaka michache mbeleni (yaani Mfalme Daudi)…

Mwana wa Mjukuu wa Ruthu ndiye Mfalme Daudi. Yaani katika uzao wa tumbo lake ukawa uzao wa kifalme. Jinsi gani Mungu anawapa thawabu hata watoto wa watoto wetu endapo sisi tukimcha yeye na kumpendeza na kuwa wavumilivu na wenye upendo kama wa Ruthu…Kumbuka Ruthu hakuwa hata mwisraeli alikuwa ni mtu wa mataifa lakini kwa upendo wake na uvumilivu wake…katika uzao wa tumbo lake akatoka Mfalme Mkuu Daudi, aliye Baba yake Suleimani…na katika Mnyororo huo ndio MFALME WA WAFALME, YESU KRISTO KATOKEA!! Ni Baraka kiasi gani…

Kwahiyo  hichi kitabu cha Ruthu kimebeba maudhui makubwa sana ya kutufundisha sisi watu wa siku za mwisho, tukianza kuzungumzia jambo moja baada ya lingine na kulitolea ufafanuzi tutamaliza kurasa na kurasa hapa…lakini wewe mwenyewe chukua nafasi ya kukisoma hichi kitabu cha Ruthu na Bwana atakupa ufunuo wa kipekee..na Pia utahitaji maelezo marefu juu ya kitabu hichi cha Ruthu unaweza kubofya hapa kwa uchambuzi zaidi >>> MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

Bwana akubariki sana..

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

 

Tutaendelea na sura zinazofuata Bofya hapa >>> VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 3


Mada Nyinginezo:

BWANA ALIMPA FARAO MOYO MGUMU, ASIMTII, JE! HAPO BWANA ATAMHUKUMU KAMA MKOSAJI SIKU ILE?

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

RAHABU.

HUYU AZAZELI NI NANI TUNAYEMSOMA KATIKA(WALAWI 16:8)

SANDUKU LA AGANO LILIKUWA LINAWAKILISHA NINI KATIKA AGANO JIPYA?

YATAFUTE YALIYO JUU SIKU ZOTE.


Rudi Nyumbani:

Print this post

ZIFAHAMU KAZI KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

Zaburi 119:105 “Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu…”

Hakika tukilifahamu Neno la Mungu kama mtu mmoja alivyosema, hata tukifungiwa katika chumba chenye giza tukapewa mshumaa na Biblia tu tutaweza kukuleza mambo yote yanayoendelea na kazi zote za shetani azifanyazo duniani bila hata kuhadithiwa na mtu yeyote,..Kumbe hatuhitaji shuhuda kutoka kuzimu ili kutusaidia sisi kufahamu utendaji kazi wa shetani, Biblia imeweka wazi mambo yote, na leo hii tutaziona hizo kazi kubwa shetani anazojishughulisha nazo kwa msaada wa Neno la Mungu:

1) KUSHITAKI WATAKATIFU:

Ufunuo 12:10 “Nikasikia sauti kuu mbinguni,ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, YEYE AWASHITAKIYE mbele za Mungu wetu, mchana na usiku..

11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa”.

Leo umekuwa mtakatifu kwa kumwamini mwana wa Mungu, lakini fahamu kuwa shetani bado hajakata tamaa ya kukufutilia, nyendo zako, na akipata kosa tu kazi yake ni kulipeleka mbele za Mungu ili uhukumiwe, anapeleka mashtaka usiku na mchana, lakini ashukuruwe Mungu sisi tulio ndani ya Kristo, pale anapokwenda kutushitaki, hapo hapo ameketi mwombezi wetu Yesu Kristo, kututetea sisi. Hivyo ni jukumu letu  kuziweka njia zetu katika mstari ulioonyooka ili adui akose la kutushitaki.

2) KUZUIA KAZI YA MUNGU: 1Wathesalonike 2.18 “Kwa hiyo tulitaka kuja kwenu, naam, mimi Paulo, mara ya kwanza, na mara ya pili, na Shetani akatuzuia”.

Ni jambo la kawaida kukutana na shetani uso kwa uso unapojaribu kuieneza kazi ya Mungu, Hiyo ni moja ya huduma yake duniani, Paulo alizuiwa na jeshi la mapepo alipokuwa akienda kuhubiri Injili Thesalonike,.Hata sasa mambo hayo hayo anayafanya,.Hivyo nawe pia ukiwa umevaa zile silaha zote zinazozungumziwa katika Waefeso 6, usiogope, kusimama, kwasababu aliyesimama upande wetu ni mkuu kuliko aliyeupande wao..Utakutana na visa na mawimbi ya ajabu njiani lakini usiogope..Aliyekutuma atakuwa pembeni yako.

3) KULETA MAJARIBU: Hii pia ni kazi anayoifanya shetani kwa maaminio kila siku, ili kuwadondosha , na kuwafanya wauone ukristo kuwa ni mgumu na mwisho wa siku wakate tamaa, na waiache njia ya wokovu,Tunaona yalitokea kwa Ayubu, Yalitokea kwa Bwana wetu Yesu Kristo, yalitokea kwa mitume, na yatatokea na kwetu,

Waebrania 11: 36 “wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani;”

Lakini ashukuriwe Mungu, ambaye anatupa nguvu ya kuyashinda,.kwasababu biblia inaweka wazi kabisa mtu yeyote atakayeingia katika PENDO la Kristo, hakuna kitu chochote kitakachoweza kumtenganisha nalo.

Lakini kumbuka pia mtu yeyote aliye nje ya Kristo hajaribiwi, wala asijidanganye kusema anapitia majaribu, atajaribiwa na nini wakati yupo tayari kwenye dhambi?.kinyume chake yeye ndiye anafanyika chombo cha shetani kuwajaribu watu wa Mungu..

4) KULETA MAGONJWA: Luka 13:16 “Na huyu mwanamke, aliye wa uzao wa Ibrahimu, ambaye Shetani amemfunga miaka kumi na minane hii, haikupasa afunguliwe kifungo hiki siku ya sabato?”

Huyu ni mwanamke aliyefunguliwa na Bwana Yesu ambapo Pepo la udhaifu lilimsababishia ulemavu wa kudumu wa mgongo (yaani kibiongo). Hii ni kutuonyesha kuwa sababu ya magonjwa mengi yanayowapata watu leo hii ni kazi ya shetani. Yeye ndiye anayehusika na magonjwa na matatizo yote, Lakini tumaini lipo na tiba na kinga vile vile ipo kwa yeyote amwaminiye Kristo leo, kwasababu maandiko yanasema (Isaya 53: 4 Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu;..Na kwa kupigwa kwake sisi tulipona)..HALELUYA!!

5) KUUA:

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; ..”

Hii ni kazi nyingine kubwa ya shetani kuangamiza kotekote yaani mwilini na rohoni. Ndugu fahamu kuwa shetani hakupendi hata kidogo, ni Rehema za Mungu tu zinatushikilia wewe na mimi, zinakushikilia wewe ambaye bado upo kwenye dhambi, ungeshakufa siku nyingi biblia inasema shetani asili yake ni uuaji tangu mwanzo alikuwa hivyo, na ndio chanzo cha mauaji unayoyaona yanaendelea sasahivi duniani, na atakuja kutekeleza vizuri katika kipindi cha ile dhiki kuu, lakini yeye aliye ndani ya Kristo, amefichwa ndani ya ule mwamba imara wala mwovu hawezi kumgusa, na hata akimgusa basi ni kwa ajili ya kutimiza kusudi la Mungu kama Ayubu, na sio kuuliwa ovyo ovyo kama tu kuku.

6) KUDANGANYA:

Yohana 8:44“…..wala hakusimama katika kweli [shetani], kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo”.

Unaona?. Kazi ya upotoshaji ni kazi inayomletea shetani matunda makubwa sana, Anachofanya yeye, hakuzuii kumwabudu Mungu wala kwenda kanisani, bali anakuhubiria njia zake za uongo, ili umwabudu yeye pasipo wewe kujua ukidhani unamwabudu Mungu, au anakushawishi ufanye kitu Fulani ukidhani ni chema kumbe unamkosea Mungu, na mwisho wa siku unakufa unajikuta upo kuzimu, mpango wake umekamilika juu yako. Na ndio maana tumeonywa kila siku tuijue kweli ili tuwe huru, na KWELI ni NENO LA MAUNGU, katika zama tulizopo udanganyifu wa ibilisi umezidi kuongezeka, tuombe Mungu atusaidie, huku na sisi wenyewe tukionyesha bidii kumtafuta Mungu.

7) KUPOFUSHA:

2Wakorintho 4:3 “Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea;

4 ambao ndani yao MUNGU WA DUNIA HII AMEPOFUSHA FIKIRA ZAO WASIOAMINI, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.

Leo hii unaweza ukajiuliza ni kwanini watu wengi wanasikia injili, wanaziona kazi za Mungu waziwazi akifanya ishara na miujiza, wanajua kabisa Mungu yupo lakini bado hawataki kubadilika,..ni kwasababu wametaka wenyewe kuwa chini ya shetani, hivyo na shetani naye akatumia fursa hiyo kuwapofusha fikira zao moja kwa moja wasiiamini Injili wakapona.. Na anafanya hayo akishirikiana na wakuu wake wa giza hili pamoja na mapepo yote,.Hivyo ndugu ikiwa wewe ni mmojawapo wa watu wasiosikia injili, jichunguze tena, na uamue kubadilika, Mgeukie Bwana akupake dawa kwenye macho yako upate kuona.

Bwana anasema katika

Ufunuo 3:17-20 “…Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, NA KIPOFU, na uchi.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.

19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.

20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.”

8) KUNYAKUA NENO LA MUNGU:

Mathayo 13:18 “Basi ninyi sikilizeni mfano wa mpanzi.

19 Kila mtu alisikiapo neno la ufalme asielewe nalo, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa karibu na njia.”

Hapa napo shetani amewekeza sana, na amefanikiwa pakubwa..Akishaona mtu Fulani anaonyesha uelekeo wa kutaka kuamini, alipohubiriwa injili, ilipomchoma, sasa yeye anachohakikisha ni kuwa anapambana kwa kila namna kuliondoa lile Neno ndani ya mtu yule, ndio hapo utakuta mtu anakosa Muda wa kutafari lile Neno alilofundishwa, badala yake shetani atamletea vitu mbadala vya kujishuhulisha navyo, kama vile movies, mpira, michezo, tv, kuchati, mihangaiko, miziki n.k..mwisho wa siku anasahau kile alichopandiwa ndani yake, na baadaye anarudia hali yake ya mwanzo na kuwa kama vile mtu ambaye hajawahi kusikia Neno la Mungu kabisa..

Hiyo ni njama kubwa sana shetani anayoitumia kuiondoa mbegu iliyopandwa ndani ya mtu, hata katika mambo ya dunia, mwanafunzi akitaka kuondoa kitu alichokipata darasani, aanze tu kungalia movie muda mrefu, au kuchat au kusikiliza miziki…mwanafunzi wa namna hiyo ndani ya muda mfupi sana, utakuta kashazika kila kitu katika akili yake kuhusu kitu alichojifunza muda mfupi au siku chache nyuma..Na shetani ndio anatumia vitu hivyo hivyo kuiba mbegu iliyopandwa ndani ya mtu.

Embu jiulize injili imehubiriwa kwako mara ngapi, na bado upo vilevile, Neno la Mungu lilivyo na nguvu ilipaswa usikie mara moja tu na kugeuka moja kwa moja, lakini kwasababu shetani umempa nafasi basi amekuwa akiifanya hii kazi ndani yako kila siku pasipo hata wewe kujijua, Hivyo chukua hatua ubadilike mara kwa kuitii Injili inapohubiriwa kwako weka mbali miziki ya kidunia, filamu, tamthilia, novels zisizokuwa na maana na mambo mengine yote yanayofanana na hayo.

9) KUJIGEUZA NA KUWA MFANO WA MALAIKA WA NURU:

2Wakorintho11:13 “Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo.

14 Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.

15 Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.”

Ni tabia ya shetani kujigeuza na kujifanya malaika mtakatifu, hivyo anawarithisha na watoto wake kazi hiyo hiyo, na ndio maana katikati ya kanisa la Mungu leo hii utaona manabii wengi wa uongo na mitume na watumishi wa uongo humo humo. Hiyo ni kazi ya shetani ili kulikoroga kanisa la Mungu lisisimame. Lakini sasa wewe kama mkristo ni jukumu lako kuwatambua, kwasababu biblia inasema mtawatambua kwa matunda yao.. je! Wanayatenda mapenzi ya baba yao aliye mbinguni?..Hilo tu.

Unafundishwa Neno la Mungu na utakatifu? Au mambo mengine, je! Tangu uwepo mahali hapo maisha yako ya kiroho yalishawahi kubadilika au ndio yanazidi kuteterekea?. Unapata matumaini ya utajiri na mali lakini je! Juu ya hayo ulishapata matumaini ya uzima wa milele yanayopatikana kwa kuishi maisha ya utakatifu na kujitenga na dhambi?

10) KUFANYA ISHARA NA MIUJIZA YA UONGO:

Ufunuo 13:13 “Naye afanya ishara kubwa, hata kufanya moto kushuka kutoka mbinguni uje juu ya nchi mbele ya wanadamu.

14 Naye awakosesha wale wakaao juu ya nchi, kwa ishara zile alizopewa kuzifanya mbele ya huyo mnyama, akiwaambia wakaao juu ya nchi kumfanyia sanamu yule mnyama, aliyekuwa na jeraha la upanga naye akaishi.”

Mambo haya haya yalifanyika wakati wa kipindi cha Musa, wakati wale Yane na Yambre, walipokuja na wao kutoa ishara zao mbele za Musa ili kuwachanganya watu wa Mungu,.hata sasa anafanya hayo hayo, kwa kutumia uchawi wake, anaowapa watumishi wake wa uongo.

Tunaweza kuona kulikuwa na mtu mwingine aliyeitwa Simoni kwenye Biblia, naye alikuwa vivyo hivyo.

Matendo 8:9 “Na mtu mmoja, jina lake Simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la Wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa.

10 Wote wakamsikiliza tangu mdogo hata mkubwa, wakisema, Mtu huyu ni uweza wa Mungu, ule Mkuu.

11 Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake”.

Hivyo kwa kuyafahamu hayo tutaweza kujua ni jinsi gani shetani anavyotuwinda kuliko tunavyodhani, hofu ni kwako wewe uliye nje ya wokovu, nje ya YESU KRISTO utawezaji kuviruka viunzi vyote hivyo vya adui?. Upo katika hatari kubwa sana ya kuangamia na kuishia kuzimu. Kinga tulishapewa nayo ni YESU KRISTO, Amwaminiye yeye shetani kwake ni kama KIKARAGOSI!! Kisichoweza kumfanya lolote, wala kumdhuru. Lakini ukiwa nje ya Kristo shetani kwako ni mungu wako, atakufanya anachotaka.

Uamuzi ni wako, TUBU leo ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kimaandiko upate ondoleo la dhambi zako, uingie katika familia ya wana wa Mungu, furahani kwa Bwana, mahali ambapo chemchemi ya maji ya uzima inapobubujika. Mahali ambapo hakuna aliyemfuata akajuta. Tulikuwa na sisi katika dhambi kuliko wewe lakini sasa tunapata raha ndani ya Kristo Yesu, Ingia na wewe ujionee mwenyewe..

Ubarikiwe …

Kwa Maombezi, Ushauri, au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Rudi Nyumbani

Print this post

MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.

1 Timotheo 4 :1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;”

Mwanzoni nilipokuwa ninausoma huu mstari nilidhani kuwa itafikia kipindi watu watauchukia ukristo na kugeukia imani nyingine, labda uislamu au kama sio hivyo basi watageuka na kuwa wapagani moja kwa moja, lakini nilipokuja kuuchunguza tena kwa makini Bwana akanipa kujua kuwa kumbe sio hivyo, badala yake ni kwamba watu wataendelea kubakia katika Ukristo lakini kumbe Imani zao siku nyingi tayari zilishabadilishwa na kuwa kitu kingine,..

Ni sawa na wanafunzi waliosajiliwa shuleni Tanzania lakini mwalimu wao anawafundisha sylabus ya Kenya, unaona haijalishi wataelimika kiasi gani, haijalishi watafahamu mambo mengi kiasi gani, siku ikifika ya mtihani wa mwisho wa taifa wanafunzi wale wote wanauwezekano mkubwa wa kufeli, kwani watakutana na mambo ambayo hawajawahi kufundishwa. Na mwisho wa siku itageuka na kuwa hasara kwao na sio hasara ya mwalimu.

Na ndivyo ilivyo katika siku hizi za mwisho, Biblia inasema wengine watajitenga na Imani, hii ikiwa na maana kuwa watakosa shabaha ya Imani halisi ya kikristo, wakidhani kuwa wapo katika njia sahihi kumbe walishapotea au walishapotezwa siku nyingi. Wameifuata Imani feki isiyotambulika mbinguni.

Ndugu jambo hili sio la kulichukulia juu juu tu, naomba usome mpaka mwisho inawezekana na wewe ulichukuliwa katika wimbi hilo pasipo kujijua, kwani shetani ni mjanja sana, usijione unafahamu kila kitu, wala tusijione kuwa tunafahamu mambo yote, tunakuwa na kujifunza kila siku.

Leo tutaona mambo mawili makuu yatakayopelekea wewe kujitenga na Imani ya kweli mwenyewe. Sasa tukirudi kwenye huo mstari hapo juu, tunaona unasema.. Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, WAKISIKILIZA ROHO ZIDANGANYAZO, na MAFUNDISHO YA MASHETANI;

Umeona sababu zenyewe hapo?, kitakachowasababishia kujitenga na Imani kwanza, ni kusikiliza roho zidanganyazo, na pili ni Kusikiliza mafundisho ya mashetani.

1) KUSIKILIZA ROHO ZIDANGANYAZO: Hizi roho zidanganyazo ni zipi,? biblia imeweka wazi kama tukindelea kusoma vifungu vinavyofuata tutapata picha yote ilivyo…Na roho hizi pia zimetajwa kugawanyika katika mafungu makuu mawili, moja ni Kuzuiwa kuoa, na pili ni kulazimishwa ujiepushe na vyakula…Tusome.

Timotheo 4:1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;

2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;

3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli”.

4 Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa shukrani;

5 kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba”.

Angalia maneno hayo ndugu ukishaona unafika mahali unaambiwa ili ukubaliwe na Mungu au ili uwe mtumishi wa Mungu, ni lazima usioe kama Mtume Paulo alivyokuwa vinginevyo haustahili kuwa askofu, au mchungaji au mtumishi wa kanisa, basi fahamu kuwa hizo ni roho zidanganyazo na zinakutenga na Imani halisi inayotajwa kwenye biblia ya mitume..

Hali kadhalika ukiona, umefika mahali unaanza kuambiwa chakula hichi ule au hichi usile, hiki ni najisi hakifai, ukila hichi ni dhambi, kama vile wafanyavyo baadhi ya dini kama sabato, Ndugu fahamu kuwa upo katikati ya roho zidanganyazo, zitakazokupeleka mbali na Imani, Ni kwanini hayo mambo ni mabaya?…Ni kwasababu yanakutoa katika kuhesabiwa haki kwa Imani na kukuleta katika kuhesabiwa haki kwa vitu vya mwilini kama vyakula, na kuutiisha mwili kwa nguvu.. …Haihitaji ufunuo kuelewa hilo, na ndio maana hapo juu biblia inasema Roho ananewa wazi wazi, unaona ni mambo yaliyowazi kabisa,

Jitenge nazo haraka sana, kwasababu zilishatabiriwa katika siku za mwisho hizo ndizo zitakazowaongoza watu waikose mbingu, watu watakuwa wanakazana kuangalia namna ya kula kama ndio kitu kinachompendeza Mungu, na wanasahau mambo muhimu ya Imani kama upendo, utakatifu, amani n.k

Wakolosai 2:20 “Basi ikiwa mlikufa pamoja na Kristo mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, kwa nini kujitia chini ya amri, kama wenye kuishi duniani,

21 Msishike, msionje, msiguse;

22 (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata maagizo na mafundisho ya wanadamu?

23 Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili”.

2) MAFUNDISHO YA MASHETANI: Haya mafundisho ya mashetani ni yapi?, Biblia nayo imeendelea kuweka wazi katika vifungu vinavyofuata..

(4:7 Bali hadithi za kizee, zisizokuwa za dini, uzikatae; nawe ujizoeze kupata utauwa..)

Unaona biblia inazitaja hadithi za kizee, ambazo hizo hata hazina vimelea vya dini ndani yake, haya ndio mafundisho ya mashetani yaliyobuniwa kuzimu ili kuwafanya watu wasiliamini tena Neno la Mungu hata kidogo na uweza ulio katika Kristo Yesu badala yake kuhamishia imani zao katika vitu visivyo na uhai. Na hapa ndipo wakristo wengi walipokamatiwa hususani wa makanisa ya kiroho,.Hizi zinaitwa hadithi za kizee, ni hadithi ambazo zimetungwa lakini zinahusishwa na imani, kwamfano utafika mahali unafundishwa usipande mti Fulani nyumbani kwako, unasababisha baba wa nyumba kufa, unasababisha mikosi kwenye nyumba, na magombano yasiyoisha, na wewe kama mkristo unakwenda kuung’oa huo mti, wewe hujui kuwa Imani yako imehamishwa kutoka katika kweli ya Mungu na kuamia katika ibada za sanamu, mambo ambayo hayana tofauti na yale yanayofanywa na waganga wa kienyeji.

Utakuta mwingine anakuambia, lipande ua hili au mti huu au fuga mnyama ndani ni viumbe rafiki vinaleta Baraka katika nyumba na kuondoa mikosi, na wewe kama mkristo unamsikiliza mtu huyo ambaye anajiita ni mtumishi wa Mungu bila kuhakiki jambo hilo linatoka wapi katika maandiko wewe unakwenda kufanya hivyo, hujuwi unamtia Mungu wivu kiasi gani unasahau kuwa Baraka za Mungu zinatoka katika chemchemi ya maji ya Uzima ndani Yesu Kristo peke yake,..unasahau kuwa utakatifu ndio nyenzo ya kuishi maisha ya amani hapa duniani lakini wewe unakwenda kutafuta njia mbadala kutoka katika viumbe na mimea, na mchanga, na vyakula, unasikiliza hadithi za kizee sizizo na dini, unajitenga na Imani ya Kristo Yesu wewe mwenyewe bila ya wewe kujijua, unamtia Mungu wivu kwa mambo hayo yasiyotokana na Imani ya Kristo Yesu.

Kaka/ndugu, Hizi ni siku za mwisho Roho amekwisha kunena wazi wazi tena leo hii bila kutuficha, Biblia Inaposema wengi watajitenga na Imani, haimaanishi watahama ukristo na kugeukia dini nyingine, hapana watabaki huku huku lakini kumbe siku nyingi walishahamishwa..Na ndio lengo la shetani hilo…Kudanganya, siku zote kudanganya..Maana ya kudanganya ni kudhani umeambiwa/unafanya kweli kumbe ni uongo.

Na ndio maana Paulo kwa uweza wa Roho alimsisitiza sana Timotheo kwenye vifungu hivyo vya maandiko na kumwambia.

4:6 “Uwakumbushe ndugu mambo hayo, nawe utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, na MZOEVU WA MANENO YA IMANI, na mafundisho mazuri yale uliyoyafuata..”

Unaona, kama mtumishi wa Mungu alionywa kuwakumbusha watu mambo hayo na kufanya vile naye atakuwa “mzoefu wa maneno ya Imani”, hii ikiwa na maana kuwa asipokuwa makini kama mahubiri atakengeuka na kufundisha maneno mengine ambayo sio ya Imani.

Nasi tunakukumbusha leo hii na kukwambia, ONDOKA! Mahali unapozuiwa kuwa mchungaji kisa umeoa mke, kama kanisa Katoliki lifanyavyo, Vile vile mahali ambapo pia wanakuzuia kuwa mhudumu wa Kristo kisa hujaona, ondoka hilo eneo kwasababu katika maandiko hakuna mahali popote pameagiza hivyo.

Ondoka, mahali ambapo unaambiwa ili Mungu akukubali au ili uwe kwenye njia sahihi ni lazima usile kitu Fulani, ni lazima, ushike siku Fulani, ya jumamosi au jumapili, ni lazima ushike sabato, wanasisitiza mambo ya mwilini tu siku zote lakini Utakatifu wa ROHONI haugusiwi ondoka haraka eneo hilo kabla tatizo hilo halijawa donda ndugu kwako lisiloweza kupona tena, usije ukabakia kuwa mfuasi wa dini kushindana na kulumbana na watu kila mahali kama walivyokuwa wanafanya mafasayo na waandishi. Na uthibitisho wa roho hii, huwe inawapeleka watu kwenye malumbano na mashindano ya dini, ambayo biblia imetuonya tukae mbali nayo.

Ondoka pia mahali ambapo wanapenda njia mbadala za kutatua matatizo yako kwa kutegemea vitu vingine nje ya Neno la Mungu na uweza wa damu ya Yesu Kristo. Unaambiwa suluhisho la matatizo yako ni maji Fulani yaliyoombewa, au mafuta, au chumvi au udongo, na huambiwi kwasababu hapana tofauti na kwa mganga wa kienyeji, kwasababu huwezi kwenda kwa mganga wa kienyeji hata siku moja ukakemewa tabia yako, yeye ukifika pale atakupa dawa ya matatizo yako kwa njia nyingine anayoijua yeye, lakini sio kwa kukutathamini tabia yako, hata siku moja hawezi kukwambia wewe ndio mbaya, atakwambia mtu Fulani ambaye ni adui yako ndio mbaya, kwahiyo hata kama wewe ndio mwenye makosa atakupa dawa ya kumshambulia Yule asiye na kosa, vivyo hiyo na mahali popote unapofika ambapo unatabiriwa tu kupigwa kwa maadui zako lakini hujawahi kuambiwa kuwa ile tabia yako ya uasherati ndio adui mkubwa wa maisha yako, ondoka hilo eneo kwa usalama wa maisha yako. Unafika tu na kuambiwa nunua maji haya yaliyoombewa baada ya siku kadhaa matatizo yako yote yataondoka..Ujue hizo ni hadithi za kizee za kujitenga nazo.

Hivyo Kwa kuzingatia vipengele hivyo vikubwa viwili basi utakuwa umenusurika pakubwa na undanganyifu ulipo duniani katika siku hizi za mwisho.

Ni jukumu la Kila mkristo kuilinda Imani yake na kuishindania, biblia inatuagiza hivyo.

Yuda 1:3 “Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba MWISHINDANIE IMANI WALIYOKABIDHIWA WATAKATIFU MARA MOJA TU.

Ikiwa wewe ni mmoja wa waliokombolewa na Yesu basi Nikutakia heri na mafanikio yote katika safari yako njema ya kwenda mbinguni. Bwana akubariki sana.

Kwa Maombezi, Ushauri, au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

HADITHI ZA KIZEE.

MAFUNDISHO YA MASHETANI

BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA!

INARUHUSIWA KULA NYAMA YA NGURUWE KWA MKRISTO WA KWELI?

TUZIJARIBU HIZI ROHO.


Rudi Nyumbani

Print this post